da
dada ee jifunze kwa mtini,nakupa mf,na ukuongoze utoe maamuzi,kuna dada mmoja huku iringa aliolewa na mwanamume akakaa miaka kama 5au 6 hivi bila mtoto,basi mumewe akawa anampiga sana na ndugu wanamtukana na kumdhalilisha sana ,ati hazai,hatimaye wakamfukuza aende kwao,kumbe tatizo la uzazi lilikuwa ni la mwanaume,lakini yule bidada alikuwa mwaminifu sana,hakuwa anasema lolote anapotukanwa na kupigwa kisa ati hazai,
sikumoja akaja mzungu mmoja toka Denimak,siku moja katika pitapita yule mzungu alimuona yule bidada akauliza wenyeji wake ati huyu mwanamke ameolewa?wenyeji wake wakamwambia aliachika,kisa aliambiwa hana uzazi,yule mzungu aksema mimi nampenda nahitaji nimuoe niende naye Denimaki,je unaweza nisaidia kuongea naye,maana yeye mzungu alikuwa hajui kiswahili,mwenyeji wake akasema bila shaka nitaongea naye,basi mwenyeji wa yule mdenishi alipoongea na yule bidada ,bidada alikubali kuolewa na yule mzungu,basi wakafunga ndoa,baada ya ndoa wakaondoka kwenda denimaki,na yule bidada alifanikiwa kuzaa watoto wa tatu na mzungu,na walirudi Tanzania wakajenga nyumba ya wazazi wake,
yule bwana aliyemtesa ni masikini,hana nyumba,hana hata mtoto
Sasa wewe uliteswa kwavile ulipoteza opportunity ya masomo,akakudharau kwavile hukuwa nakitu,unajuwaje ukirudiana
afu uje uwe hunakitu tena mfano,atakujali,au na hizo ulizotafuta unajuwaje kama atakuwa anhonga wanawake wengine?
kwahiyo ni juu yako kujiongeza upstair yako,okay