Sasa mbona ananisumbua?

thatsit

JF-Expert Member
Mar 12, 2017
1,870
2,913
Mm Ni kijana mwenzenu, Nina utata kidogo ktk maisha yangu naomba mawazo yenu.

Nilipata kuwa na mahusiano na kijana mwenzangu wakat tukiwa chuo. Mapenz yetu yalikuwa matam tu tulipendana sana, mpk ilipofika hatua ya kumaliza chuo yule kijana akaenda kwao na mm nikawa nipo tu home.

Kwa vile kila mmoja alikua anakaa mbali na mwenzie na mm nilikuwa cwez kukaa mbali nae nikaamua kumshauri aje nyumbn kuniposa anioe. Yaani kumuambia suala la ndoa tu akawa km nimemfukuza.

Nikafanya jitihada nikamtafuta nikamuambia lazima anioe Mana alishakula tunda langu, ikawa ugomvi hataki mpk wakaingia wazee akalazimishwa akalazimishwa ndo akakubali kunioa.

Baada ya kunioa nilijuta Bora ningekaa nyumbani nikatafuta issue nikafanya , yn mume alikuwa ananipiga, ananisimbulia, ananisimanga kila baya ananifanyia. Huduma Hana ukimuambia anasema kachukue kwenu me sikutak.

Dah nikastahmili nikapata mimba, nilipopata tu mimba mume wangu alizid vituko harud kabisa cjui analala wap. Siku Moja akaniambia nenda kwenu me nataka kusafr, apo nilikuwa na mimba 6 months.

Kumbe yule bwana hakusafr Wala nn anaonekana mjini anadunda nikaja kusikia keshaoa mke mwengine kwangu hapiti kabisa. Nikimpgia cm hapokei Hana mawasiliano na mm iliniuma sana. Kwa uchungu na hacra nikazaa nikiwa na mimba miez Saba.

Baada ya kujifungua niliumwa sana na mtoto pia alikua mgonjwa, babaake alibadlisha namba na tulipokuwa tunakaa akahama.

Ndipo nilipoenda kwao kumuulizia lkn nashangaa ndugu zake walinidharau na kunicheka Kisha wakanipa waliosema mzigo Wangu ambayo ilikua Ni talaka.
Mume wangu aliniacha ktk Hali hii ngumu mm naumwa na mtt anaumwa kwa kweli nilikua namuhitaji nikaondoka nikashukuru mungu.

Kwa kwel nilipoteza muelekeo nikakosa dira nikijiangalia baba yangu alishakufa, mama nae mtu mzima Hana kitu. Nilisomeshwa kwa msaada wa jumuia fulan lkn nilishindwa kufanya vizur kutokana na mapenz nilijuta na kulia sana.

Sikua na msaada nikawa nauza maandazi kwa ajili ya kujikimu mm na mtoto na mama pia.

Siku Moja katika pita pita zangu nikakutana na rafiki yangu wa zamani alinishangaa kuona nilivyochoka akaniuliza yamenikuta yepi? Nikamuhadithia akanihurumia sana nilishaanza kukonga wakati nilikuwa na 23 years old.

Rafiki yangu akaniuliza unataka kufanya kaz za ndani Oman nikamuambia ndio, akanipeleka kwa mtu fulan hivi akaniambia yy atanifanyia Safari. Bac nikaondoka Tanzania nikaenda Oman mwanangu akiwa na miaka 3 na alikua anaendelea vizur japo alikua mwembamba sana.

Nashkuru mungu kumbe hii ilikua ndio njia yangu ya kunifungulia milango ya kheri na barka, nikawa napata pesa Sasa natuma nyumbani. Niliporud nikakuta nyumba yetu ishajengwa vizur na milango ya maduka miwili. Sikutosheka nikarud Tena Oman tukafungua biashara pale home duka Moja la vyakula na Moja stationaries Kuna ndugu zangu wanauza pamoja na mama. Niliporud Tena nikajenga nyumba yangu na biashara ikakua nimekod mlango mjini nikaweka nguo za kike. Huu mwaka wa tano nipo Oman nataka nikirud next year iwe ndo mwisho sirud ntakuwa na kila kitu nilichokuwa nahitaji.

Tatizo Sasa yule kijana aliyeniacha kwa dharau akanifanya nichukie wanaume wote amepata habari zangu na mtoto kampa namba yangu ananipigia kila sekunde ananiambia mke wangu turudiane tulee mtoto wetu. Jaman na mtoto nae anasema nirud kwa babaake km sitak nikiolewa na mtu mwengine atamuua.

Nipo njia panda nampenda sana mwanangu Ila siko tayar kurudiana na yule babaake nifanyeje jamani!!
 
Mm Ni kijana mwenzenu, Nina utata kidogo ktk maisha yangu naomba mawazo yenu.

Nilipata kuwa na mahusiano na kijana mwenzangu wakat tukiwa chuo. Mapenz yetu yalikuwa matam tu tulipendana sana, mpk ilipofika hatua ya kumaliza chuo yule kijana akaenda kwao na mm nikawa nipo tu home.

Kwa vile kila mmoja alikua anakaa mbali na mwenzie na mm nilikuwa cwez kukaa mbali nae nikaamua kumshauri aje nyumbn kuniposa anioe. Yaani kumuambia suala la ndoa tu akawa km nimemfukuza.

Nikafanya jitihada nikamtafuta nikamuambia lazima anioe Mana alishakula tunda langu, ikawa ugomvi hataki mpk wakaingia wazee akalazimishwa akalazimishwa ndo akakubali kunioa.

Baada ya kunioa nilijuta Bora ningekaa nyumbani nikatafuta issue nikafanya , yn mume alikuwa ananipiga, ananisimbulia, ananisimanga kila baya ananifanyia. Huduma Hana ukimuambia anasema kachukue kwenu me sikutak.

Dah nikastahmili nikapata mimba, nilipopata tu mimba mume wangu alizid vituko harud kabisa cjui analala wap. Siku Moja akaniambia nenda kwenu me nataka kusafr, apo nilikuwa na mimba 6 months.

Kumbe yule bwana hakusafr Wala nn anaonekana mjini anadunda nikaja kusikia keshaoa mke mwengine kwangu hapiti kabisa. Nikimpgia cm hapokei Hana mawasiliano na mm iliniuma sana. Kwa uchungu na hacra nikazaa nikiwa na mimba miez Saba.

Baada ya kujifungua niliumwa sana na mtoto pia alikua mgonjwa, babaake alibadlisha namba na tulipokuwa tunakaa akahama.

Ndipo nilipoenda kwao kumuulizia lkn nashangaa ndugu zake walinidharau na kunicheka Kisha wakanipa waliosema mzigo Wangu ambayo ilikua Ni talaka.
Mume wangu aliniacha ktk Hali hii ngumu mm naumwa na mtt anaumwa kwa kweli nilikua namuhitaji nikaondoka nikashukuru mungu.

Kwa kwel nilipoteza muelekeo nikakosa dira nikijiangalia baba yangu alishakufa, mama nae mtu mzima Hana kitu. Nilisomeshwa kwa msaada wa jumuia fulan lkn nilishindwa kufanya vizur kutokana na mapenz nilijuta na kulia sana.

Sikua na msaada nikawa nauza maandazi kwa ajili ya kujikimu mm na mtoto na mama pia.

Siku Moja katika pita pita zangu nikakutana na rafiki yangu wa zamani alinishangaa kuona nilivyochoka akaniuliza yamenikuta yepi? Nikamuhadithia akanihurumia sana nilishaanza kukonga wakati nilikuwa na 23 years old.

Rafiki yangu akaniuliza unataka kufanya kaz za ndani Oman nikamuambia ndio, akanipeleka kwa mtu fulan hivi akaniambia yy atanifanyia Safari. Bac nikaondoka Tanzania nikaenda Oman mwanangu akiwa na miaka 3 na alikua anaendelea vizur japo alikua mwembamba sana.

Nashkuru mungu kumbe hii ilikua ndio njia yangu ya kunifungulia milango ya kheri na barka, nikawa napata pesa Sasa natuma nyumbani. Niliporud nikakuta nyumba yetu ishajengwa vizur na milango ya maduka miwili. Sikutosheka nikarud Tena Oman tukafungua biashara pale home duka Moja la vyakula na Moja stationaries Kuna ndugu zangu wanauza pamoja na mama. Niliporud Tena nikajenga nyumba yangu na biashara ikakua nimekod mlango mjini nikaweka nguo za kike. Huu mwaka wa tano nipo Oman nataka nikirud next year iwe ndo mwisho sirud ntakuwa na kila kitu nilichokuwa nahitaji.

Tatizo Sasa yule kijana aliyeniacha kwa dharau akanifanya nichukie wanaume wote amepata habari zangu na mtoto kampa namba yangu ananipigia kila sekunde ananiambia mke wangu turudiane tulee mtoto wetu. Jaman na mtoto nae anasema nirud kwa babaake km sitak nikiolewa na mtu mwengine atamuua.

Nipo njia panda nampenda sana mwanangu Ila siko tayar kurudiana na yule babaake nifanyeje jamani!!
ameshaona umewin life hapo,anataka slope hujaelewa tu....
na ukimrudia leo na kesho mambo yako yakaenda vibaya(though sikuombei hivyo) atakukimbia tena...
achana nae,move on....
usitumie moyo hapo,tumia akili zaidi...
swala la kuua huo ni mkwara tu...
 
duuuuh pole sana sitaki kukuhukumu ila dada angu achana na huyo mbuzi kaa nae mbali ajakupenda wewe kapenda mali izo sasa kama unataka rudi nyuma mrudie uyo funza maana ni funza hana utu kabisa mwambie mwanao ajue ukweli kuhusu baba ake iyo itasaidia

ila nyie wanawake sijui kunamdudu gani anaingiaga kichwani mwenu kama wewe dada unaweza shangaa anamrudia uyo mwanaume utasikia mapenzi kukohozi babuuu.........
 
Huyo mtoto wako naye ana akili za kibashite?

Haiwezekani uhangaike hivyo alafu aje alete madoido eti atamuua mtu. Muache aende kwa baba yake siku akijisikia aje kwako. Si lazima uishi naye.
Ahsante sana
 
  • Thanks
Reactions: BAK
duuuuh pole sana sitaki kukuhukumu ila dada angu achana na huyo mbuzi kaa nae mbali ajakupenda wewe kapenda mali izo sasa kama unataka rudi nyuma mrudie uyo funza maana ni funza hana utu kabisa mwambie mwanao ajue ukweli kuhusu baba ake iyo itasaidia

ila nyie wanawake sijui kunamdudu gani anaingiaga kichwani mwenu kama wewe dada unaweza shangaa anamrudia uyo mwanaume utasikia mapenzi kukohozi babuuu.........
Siwez kurud mkuu tatizo mtt nitakaa hivi mpk ln na yy hataki niolewe na mwanaume mwengne nampenda sana mwanangu
 
Siwez kurud mkuu tatizo mtt nitakaa hivi mpk ln na yy hataki niolewe na mwanaume mwengne nampenda sana mwanangu
Sidhan kma ataweza fanya ivyo kama ataweza ni hatar apo la muhimu ni kukata mawasiliano kati ya mtoto na baba

All in all nadhan wadau wengn watachangia ila ushauri wangu ni achana na huyo mwanaume thats it
 
ila dada yote aliyokufanyia huyo mwanaume kweli una hamu ata ya kuja kumwanzishia thread uombe ushauri ww bado unampenda huyo jamaa kazi kwako
Mkuuu duh....umesema kweli lakini. Hapa tutahangaika tu, moyoni mwake yupo.
 
Wewe ndio unaweza kuamua, kama humtaki kaa mbali naye. ukitaka mrudiane ili mlee mtoto sawa, na kama bado unampenda ni vizuri urudiane
May be kabadilika.
 
Sidhan kma ataweza fanya ivyo kama ataweza ni hatar apo la muhimu ni kukata mawasiliano kati ya mtoto na baba

All in all nadhan wadau wengn watachangia ila ushauri wangu ni achana na huyo mwanaume thats it
Yy ndio anaemtafuta mtoto anaenda hadi shule na kwa Bibi yake pia anaenda kumtia maneno mpk yameshamjaa ukizingatia jamaaa Mambo yamemchachia sa iv Ni fundi cm
 
Dada yangu tabia ya mtu huwa haibadiliki ukikubali tu kuwa naye Fanya vyovyote usiishie vijiset maana huyo yupo kwako kwa kipato ila mapenzi ya dhati sidhani. Hujabadilika kitu ndo yuleyule wa zamani sasa anataka nini zaidi ya pesa zao.achananae kabisa kwanza alishatoa talaka.
 
Huyo mtoto ana haki ya kumsalimia babake lakini isiwe ndo gia ya wewe kutaka kurudiana na mtalaka wako. Alikuacha mwenyewe, hivyo vitisho ni vya nini. Alikuwa hakupendi na hatokaa akupende milele, anatumua udhaifu wako aje afaidi ulivyonavyo. Wala usimtie maanani
 
ila dada yote aliyokufanyia huyo mwanaume kweli una hamu ata ya kuja kumwanzishia thread uombe ushauri ww bado unampenda huyo jamaa kazi kwako
Hivi hii busara umeitoa wap shunie Jaman khaa mbna sio wa hvyo wewe.
Back to the topic kama unaomba ushaur means bado unampenda other wise usingejisumbua nae.
So kama unamtaka mrudie otherwise usje ukaanzisha thread nyengne
 
Back
Top Bottom