Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 38...
Uzuri wa Gloria ulikuwa balaa, David alikuwa na mawazo tele, kila alipokaa alimfikiria msichana huyo mrembo. Alikuwa mtoto wa kishua, baba yake, Mzee Mpobela alikuwa mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania, alikuwa na makampuni mengi, maduka makubwa, migodi ya dhahabu na vitu vingine vingi.
David alilijua hilo, alihakikisha kwamba anamchukua msichana huyo ili maisha yake yawe laini, apate afueni ya maisha kwani kama kuchunwa na wanawake, alichunwa vilivyo na aliona huo ndiyo muda wa yeye kula pesa za msichana.
Walikuwa wakiwasiliana kama marafiki, David hakutaka kukaa sana kwenye mawasiliano ya kirafiki kitu kilichomfanya kuanza kumchombeza msichana huyo kwa maneno matamu, kwamba alikuwa mzuri kiasi kwamba hata Mungu alikuwa akijivunia kumuumba msichana mzuri kama yeye.
“Hukutakiwa kuwa binadamu, wewe ulitakiwa kuwa malaika,” alisema David, alikuwa akizungumza na msichana huyo ana kwa ana.
“Kweli?”
“Ndiyo! Gloria, nimeona warembo wengi, weupe, weusi, warefu na wafupi, ila kwako! Huna kasoro, wewe ni mrembo uliyekamilika,” alisema David huku akimwangalia Gloria machoni.
Alizaliwa kwenye familia ya kitajiri, alipata kila kitu alichokihitaji ila katika maisha yake alikosa kitu kimoja tu, kusifiwa na mwanaume. Kila mtu aliyemtaka, hasa watoto wa mabilionea wengine, walimfuata, walimpeleka klabu na baada ya kutoka huko wakawa wanafanya mapenzi bila kutongozwa.
Hayo yalikuwa maisha yake, hakuwahi kuambiwa kwamba alikuwa mrembo, hakuwahi kuambiwa kwamba alikuwa na tabasamu pana. Maneno yote hayo aliambiwa na David, ndiyo maneno yaliyomfanya kujisikia kwamba alikuwa mwanamke mrembo, mwenye sifa za kimalaika.
Gloria akajiweka mikononi mwa David, akatokea kumpenda mwanaume huyo kiasi kwamba kwake alikuwa haoni hasikii, haambiwi chochote kile. Hakutaka kujificha, kwa jinsi alivyokuwa akimwangalia David alionekana kuwa kijana muoaji hivyo kumwambia baba yake na ndugu zake kwamba alipata mwanaume ambaye alistahili kuwa mume wake wa ndoa.
“Una uhakika anakupenda kweli?” aliuliza Mzee Mpobela huku akimwangalia Gloria.
“Ndiyo baba!”
“Narudia tena! Una uhakika anakupenda kweli?” aliuliza mzee huyo.
Itaendelea.
Uzuri wa Gloria ulikuwa balaa, David alikuwa na mawazo tele, kila alipokaa alimfikiria msichana huyo mrembo. Alikuwa mtoto wa kishua, baba yake, Mzee Mpobela alikuwa mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania, alikuwa na makampuni mengi, maduka makubwa, migodi ya dhahabu na vitu vingine vingi.
David alilijua hilo, alihakikisha kwamba anamchukua msichana huyo ili maisha yake yawe laini, apate afueni ya maisha kwani kama kuchunwa na wanawake, alichunwa vilivyo na aliona huo ndiyo muda wa yeye kula pesa za msichana.
Walikuwa wakiwasiliana kama marafiki, David hakutaka kukaa sana kwenye mawasiliano ya kirafiki kitu kilichomfanya kuanza kumchombeza msichana huyo kwa maneno matamu, kwamba alikuwa mzuri kiasi kwamba hata Mungu alikuwa akijivunia kumuumba msichana mzuri kama yeye.
“Hukutakiwa kuwa binadamu, wewe ulitakiwa kuwa malaika,” alisema David, alikuwa akizungumza na msichana huyo ana kwa ana.
“Kweli?”
“Ndiyo! Gloria, nimeona warembo wengi, weupe, weusi, warefu na wafupi, ila kwako! Huna kasoro, wewe ni mrembo uliyekamilika,” alisema David huku akimwangalia Gloria machoni.
Alizaliwa kwenye familia ya kitajiri, alipata kila kitu alichokihitaji ila katika maisha yake alikosa kitu kimoja tu, kusifiwa na mwanaume. Kila mtu aliyemtaka, hasa watoto wa mabilionea wengine, walimfuata, walimpeleka klabu na baada ya kutoka huko wakawa wanafanya mapenzi bila kutongozwa.
Hayo yalikuwa maisha yake, hakuwahi kuambiwa kwamba alikuwa mrembo, hakuwahi kuambiwa kwamba alikuwa na tabasamu pana. Maneno yote hayo aliambiwa na David, ndiyo maneno yaliyomfanya kujisikia kwamba alikuwa mwanamke mrembo, mwenye sifa za kimalaika.
Gloria akajiweka mikononi mwa David, akatokea kumpenda mwanaume huyo kiasi kwamba kwake alikuwa haoni hasikii, haambiwi chochote kile. Hakutaka kujificha, kwa jinsi alivyokuwa akimwangalia David alionekana kuwa kijana muoaji hivyo kumwambia baba yake na ndugu zake kwamba alipata mwanaume ambaye alistahili kuwa mume wake wa ndoa.
“Una uhakika anakupenda kweli?” aliuliza Mzee Mpobela huku akimwangalia Gloria.
“Ndiyo baba!”
“Narudia tena! Una uhakika anakupenda kweli?” aliuliza mzee huyo.
Itaendelea.