Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 18...
Catherine alishangaa lakini ndiyo ulikuwa msimamo wa msichana huyo, hakutaka kutoa mimba na alikuwa tayari kuona akizaa na kumtunza mtoto wake. Wakaondoka na kurudi chuo, huko, maisha yaliendelea, hakuacha kumpigia simu David, mwanaume huyo hakuwa akipokea na wakati mwingine alihisi kama anasumbuliwa na hivyo kuizima simu hiyo.
Sarafina aliendelea kuumia moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi. Alipokuwa akimuona Richard alijishtukia, wakati mwingine alikuwa akijificha kwani mwanaume huyo ndiye aliyeonyesha kuwa na shida naye kwa hali na mali japokuwa alionekana kuwa masikini wa kutupwa.
Baada ya miezi kadhaa, kila mtu akajua kwamba alikuwa na mimba, muonekano wake ukawatia hofu wanachuo wote. Uongozi ukamuita na kuzungumza naye, hakubisha, akawaambia kwamba kweli alikuwa na mimba hivyo kufukuzwa chuoni.
Hakuwa na pa kwenda zaidi ya nyumbani kwao. Ingekuwa rahisi kwenda nyumbani kwa kina David kama tu wangekuwa pamoja lakini kwa kuwa alikuwa amekataliwa na mwanaume huyo, hakuwa na jinsi zaidi ya kujipanga kurudi jijini Mwanza.
Ndani ya basi mawazo yake yalikuwa kwa wazazi wake, hakujua wangemfanya nini baada ya kugundua kwamba alikuwa mjauzito. Walitumia kiasi cha fedha kwa ajili yake, walikopa kuhakikisha anapata elimu bora lakini mwisho wa siku alikuwa akiwapelekea mimba nyumbani.
Alipofika Mwanza, kabla ya kwenda nyumbani akatafuta saluni, akatoa blichi na kiduku kisha kujiweka kama msichana wa kawaida asiyekuwa na tatizo lolote lile. Alipofika nyumbani, wazazi wake walishangaa, hakikuwa kipindi cha likizo lakini alikuwa amerudi, alirudi kufanya nini?
“Una mimba?” aliuliza mama yake huku akimwangalia kwa mshtuko, aliligundua hilo baada ya kuona mabadiliko makubwa.
“Ndiyo mama! Naomba unisamehe!” alisema mama yake.
“Yeleuwiiiiiiii….una mimba!” alisema mama yake kwa kupayuka.
Hakuzungumza kitu zaidi ya kupiga kelele, akamwambia kwamba hiyo ilikuwa kesi kubwa na alitakiwa kumsubiri baba yake. Sarafina akabaki akitetemeka, alimfahamu baba yake, alikuwa mwanaume mkorofi ambaye hakuwa na masihara hata kidogo.
Je, nini kitaendelea?
Catherine alishangaa lakini ndiyo ulikuwa msimamo wa msichana huyo, hakutaka kutoa mimba na alikuwa tayari kuona akizaa na kumtunza mtoto wake. Wakaondoka na kurudi chuo, huko, maisha yaliendelea, hakuacha kumpigia simu David, mwanaume huyo hakuwa akipokea na wakati mwingine alihisi kama anasumbuliwa na hivyo kuizima simu hiyo.
Sarafina aliendelea kuumia moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi. Alipokuwa akimuona Richard alijishtukia, wakati mwingine alikuwa akijificha kwani mwanaume huyo ndiye aliyeonyesha kuwa na shida naye kwa hali na mali japokuwa alionekana kuwa masikini wa kutupwa.
Baada ya miezi kadhaa, kila mtu akajua kwamba alikuwa na mimba, muonekano wake ukawatia hofu wanachuo wote. Uongozi ukamuita na kuzungumza naye, hakubisha, akawaambia kwamba kweli alikuwa na mimba hivyo kufukuzwa chuoni.
Hakuwa na pa kwenda zaidi ya nyumbani kwao. Ingekuwa rahisi kwenda nyumbani kwa kina David kama tu wangekuwa pamoja lakini kwa kuwa alikuwa amekataliwa na mwanaume huyo, hakuwa na jinsi zaidi ya kujipanga kurudi jijini Mwanza.
Ndani ya basi mawazo yake yalikuwa kwa wazazi wake, hakujua wangemfanya nini baada ya kugundua kwamba alikuwa mjauzito. Walitumia kiasi cha fedha kwa ajili yake, walikopa kuhakikisha anapata elimu bora lakini mwisho wa siku alikuwa akiwapelekea mimba nyumbani.
Alipofika Mwanza, kabla ya kwenda nyumbani akatafuta saluni, akatoa blichi na kiduku kisha kujiweka kama msichana wa kawaida asiyekuwa na tatizo lolote lile. Alipofika nyumbani, wazazi wake walishangaa, hakikuwa kipindi cha likizo lakini alikuwa amerudi, alirudi kufanya nini?
“Una mimba?” aliuliza mama yake huku akimwangalia kwa mshtuko, aliligundua hilo baada ya kuona mabadiliko makubwa.
“Ndiyo mama! Naomba unisamehe!” alisema mama yake.
“Yeleuwiiiiiiii….una mimba!” alisema mama yake kwa kupayuka.
Hakuzungumza kitu zaidi ya kupiga kelele, akamwambia kwamba hiyo ilikuwa kesi kubwa na alitakiwa kumsubiri baba yake. Sarafina akabaki akitetemeka, alimfahamu baba yake, alikuwa mwanaume mkorofi ambaye hakuwa na masihara hata kidogo.
Je, nini kitaendelea?