Samwel Sitta ashangiliwa sana UDSM

Wewe usiseme kuhusu cda, hapo ndiyo aliharibu kabisa na aliemuokoa ni mwalimu nyerere! Aliwaajiri ndugu zake akina ismael rage wakafanya ufisadi wa ajabu! Jamani kama mmezaliwa majuzi tafuteni historia ya nchi hii kwanza ndiyo mposti habari zenu! Leo ukitaja cda enzi ya sitta kuna watu watakutafuna!
 
Tatizo hapa ni kuwa watu wamelishwa maneno na hawajui hata maana yake halisi. Samuel Sitta angekuwa mnafiki basi angepinga posho ili kupata umaarufu wa bure kumbe kwa undani anaunga mkono. Kwa kuwa Sitta si mnafiki hata kidogo, akasema kweli Bungeni kuwa yeye anaunga mkono posho. Sitta akiwa Spika alisimama kidete na kuruhusu mjadala na uchunguzi huru wa Richmond mpaka waziri mkuu mpenda mali na mawaziri wake wakalazimika kujiuzulu. Utekelezaji wa maazimio ya ripoti ya Richmond umeharibiwa na serikali, Sitta hahusiki hapo. Ndio maana kasimama kidetete bila kutetereka na kusema hadharani kuwa DOWANS WASILIPWE!!
Mkuu Sitta ndiye aliyezima ule mjadala kwasababu zake,kama aliweza kusimamia mpaka eddo akajiuzulu kwanini akaizima hoja bila sababu tena kwa ukali kabisa.kama wabunge akina Dr slaa wangepewa nafasi ya kuendelea kuibana tume na ukweli kuwa wazi sheria ingechukua mkondo.mjadala aliuzima kihuni mwenyewe alafu leo analalama nini? Tena mbaya zaidi akijitamba kuwa atasema mengi wakati hata kumtaja mmiliki wa Richmond anaogopa anaishia kusema tunawajua!
 
ok kumbe utajiri wa lowassa ndiyo chuki yako? Sasa ukae ukijua utajiri wake ni wa halali, yeye ndiyo rais mtarajiwa, hakuna wa kumzuia na hao unaowataja hawana watu kwani wanachotegemea ni ukabila. Hakuna wa kumzuia lowassa kuwa rais wa nchi hii kwa njia yoyote ile, fedha, umma au kisiasa, hakuna! ni swala la muda tu sasa.
 
Wewe usiseme kuhusu cda, hapo ndiyo aliharibu kabisa na aliemuokoa ni mwalimu nyerere! Aliwaajiri ndugu zake akina ismael rage wakafanya ufisadi wa ajabu! Jamani kama mmezaliwa majuzi tafuteni historia ya nchi hii kwanza ndiyo mposti habari zenu! Leo ukitaja cda enzi ya sitta kuna watu watakutafuna!

Acha porojo wewe, Nyerere hakuwa na upuuzi wa kuokoa viongozi wanaoharibu kazi. Ukiharibu kazi Nyerere anakufukuza tu, hakuwa na kubebana. Umekosa hoja kabisa, yaani unamwaga pumba kama mtambo wa kutengeneza GONGO!

Watanzania wanajua kuwa SAMUEL SITTA ni kiongozi makini, mchapa kazi, kamanda anayepambana na ufisadi, msema kweli, mzalendo halisi, shupavu na mtu mwenye maadili. Ndio maana wanafunzi wa UDSM walimshangilia na Watanzania popote aendapo nchini wanamshangilia na kumuunga mkono. The truth will set you free!
 
Hata ukitumia maandishi makubwa na bold ukweli utabaki palepale, Edward Lowassa hafai kuwa kiongozi Tanzania. Ni mpenda mali, ana utajiri mkubwa wa mashaka, amehusika na kashfa ya ufisadi ya Richmond ndio maana akalazimika kujiuzulu na ni kibaraka wa Rostam Aziz.

Samuel Sitta na Harrison Mwakyembe ni viongozi makini wanaopinga ufisadi na ni mtaji mkubwa kwenye uchaguzi wa 2015. Watanzania tunatambua hilo.
Aaaah wapi!
 
ni kweli mkuu kama asingeuzima haya niliyoyaeleza kuhsu unafiki wake yeye na karamagi na msabaha yangekuwa wazi mapema ile, chuki yake ni kukosa kazi iliyochukuliwa na dowans, mbona imechukuliwa na simbion kwa njia ile ile ya dowans watu hawasemi? Tuache unafiki watanzania.
 
ok kumbe utajiri wa lowassa ndiyo chuki yako? Sasa ukae ukijua utajiri wake ni wa halali, yeye ndiyo rais mtarajiwa, hakuna wa kumzuia na hao unaowataja hawana watu kwani wanachotegemea ni ukabila. Hakuna wa kumzuia lowassa kuwa rais wa nchi hii kwa njia yoyote ile, fedha, umma au kisiasa, hakuna! ni swala la muda tu sasa.

Sawa Frederick Lowassa endelea kumtetea baba yako. Watanzania wanajua kuwa kiongozi wa umma kama Lowassa anatoa wapi utajiri wa kununua hekaru London la thamani ya shilingi bilioni 1 (soma Rai Mwema), kumiliki majumba, majengo, biashara lukuki, akaunti zenye mabilioni ndani na nje ya nchi?! Ni ufisadi tu hapa. Labda awe Rais wa familia yenu, si taifa la Tanzania.

Hata mzimu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, utasimama kupinga Tanzania isiende kwa mbwa.
 
ni kweli mkuu kama asingeuzima haya niliyoyaeleza kuhsu unafiki wake yeye na karamagi na msabaha yangekuwa wazi mapema ile, chuki yake ni kukosa kazi iliyochukuliwa na dowans, mbona imechukuliwa na simbion kwa njia ile ile ya dowans watu hawasemi? Tuache unafiki watanzania.

Crap, crap, crap!!!
 
Jina la Samwel Sitta lilipotajwa ili apokee recognition pale udsm kama Spika aliyesoma kitivo cha sheria alishangiliwa sana. Ukumbi ulilipuka kwa shangwe. Kushangiliwa kwake tena na wasomi inaonyesha watanzania wana imani kubwa nae. CCM wakifanya mizengwe namshauri ajiunge Chadema, atapata nafasi nzuri, watanzania wanamhitaji sana.
Aje ajiunge kama mwanachama wa kawaida si kutaka kugombea uongozi, huku watu wamejipanga!!!!!!!!!!
 
Jina la Samwel Sitta lilipotajwa ili apokee recognition pale udsm kama Spika aliyesoma kitivo cha sheria alishangiliwa sana. Ukumbi ulilipuka kwa shangwe. Kushangiliwa kwake tena na wasomi inaonyesha watanzania wana imani kubwa nae. CCM wakifanya mizengwe namshauri ajiunge Chadema, atapata nafasi nzuri, watanzania wanamhitaji sana.

Nakubaliana na wewe.

SS bado watu wana mwamini kwa vile anasimamia ukweli na hayumbi. Kwa vile HUWEZI KULISUKUMA GARI UKIWA NDANI YAKE, basi tunamshauri ahamie haraka sana CHADEMA kabla ya 2015 kwa vile CCJ ilishindikana kwasababu ya mizengwe ya kina Nnauye.i
 
du naona kama wanafanana kwa kila kitu mkuu! unafiki wao ni wa kihistoria na mbaya zaidi ni marafiki
Waberoya umeibuka kumbe bado upo, hee umeona watu wako wanavyopambana?????????? Chomoka huko uje CDM tupiganie kukomboa nchi mikononi mwa maghamba's wacha kuishabikia uozo unaouona!!!!!!
 
unafiki wa sitta ni huu.

richmond ilipofutwa, sitta aliamua kuanzisha kampuni yao yeye, karamagi na msabaha lakini wakachelewa kwenda brela wakazidiwa ujanja na dowans, kuona wamezidiwa ujanja na dowans sitta akamshawishi waziri wa nishati afute mkataba na dowans. Pamoja na kwamba dk. Rashid alielezea athari zake na ambazo ni hizi za sasa kuilipa dowans mabilioni ya shilingi hawakusikia. Kisha akamteua dk. Mwakyembe kuongoza tume kwa kushirikiana na wabunge wa chadema wakati anajua mwakyembe, (waziri mkuu wa sitaa ikiwa atapata urais), ana interests zake za umeme wa upepo singida! Huo ndiyo unafiki mkubwa wa samuel sitta. Mgombea urais kwa tiketi ya chadema 2015! Sasa watanzania ukweli wameujua, icc imeeleza ukweli wote, lowasa hajaonekana mahali ametajwa, walioshirikishwa kwenye unafiki wa sitta na wenzake wakiwemo chadema kumdhalilisha mpiganaji lowassa sasa wanahaha wengine wameanza kujikomba kwa lowassa! Jamani watanzania tutafuteni ukweli kwanza kabla ya kujigongagonga. Huu ndiyo ukweli na wananchi wameanza kuujua na ndiyo maana pale udsm juzi alipoingia akiwa na rais, wasomi wa kweli walimshangilia.


umelipwa bei gani ndugu yetu? hizo ulizolipwa zinaweza kubadilisha maisha au basi tu? kujifanya mjinga ni kitu kibaya sana kama huyu hapa yaani umezaliwa na akili kutoka kwa wazazi wawili halafu unadiriki kutumiwa kwa kupumbuza akili yako. hii damej inaweza kua irivesabo shauri yako utashindwa hata kukaa na mke ndugu yangu. kua na akili kidogo,u shauri wa bure
 
Samuel Sitta ni kiongozi shupavu pekee kwenye serikali ya Jakaya Kikwete, kwani amekuwa na guts za kusimama hadharani na kusema ukweli kupingana na ufisadi wa Dowans, mgao wa umeme, kukosekana kwa maadili ya uongozo na mwingineo. Wanafiki ni wale viongozi waliopo serikalini halafu wanalalamika chini kwa chini.

Long live Samuel Sitta, una maadui wengi sana mafisadi, but God and the people of Tanzania are with you all the way!!!

Fareed: Hivi neno mnafiki maana yake nini hasa? Kwa bahati mbaya sana, maadui wa Samuel Sitta, ambao ni mafisadi wa Richmonduli, rada, Kagoda, TICTS na wengineo, ndio . wamekuwa wakitumia neno hili ndani ya CCM na nje kujaribu kumpiga vita na kumchafua kiongozi huyu.

Kwa nyie msiojua, Samuel Sitta ni kiongozi shupavu, msema kweli, anayethubutu, mchapa kazi na kiboko wa mafisadi. Tanzania ingempata mtu kama huyu kuwa Rais nchi hii ingeondokana na umasikini katika kipindi chake cha kwanza tu cha miaka mitano! Msiwe wavivu wa kufikiri na kuburuzwa na mafisadi kumuita eti Sitta ni mnafiki, kwa lipi wakati yeye kila siku ameonesha uongozi na ushupavu wa kusema ukweli? -- eg kupinga hadharani malipo ya Dowans, kusema serikali iombe radhi kwa mgao wa umeme, na mengine mengi.

Kwa msiojua, hata CHADEMA wanamfahamu sana Sitta kuwa ni kiongozi makini ndio maana mwaka 2010 walimuomba agombee Urais kupitia chama hicho. Sitta alipokataa ndio ilibidi CHADEMA wambembeleze Dr. WILLIBROD SLAA agombee Urais wakati alikuwa anataka kutetea kiti chake cha ubunge wa Karatu.

Na kama CCM ikimsimamisha Sitta kuwa mgombea Urais wa 2015, basi CHADEMA watapata taabu sana kupambana naye jukwaani. Huu ndio ukweli, acheni uvivu nyie kwa kulishwa maneno na propaganda za mafisadi.



Nyie mnaomtetea Sitta wenu mnafuata mkumbo. Vita yake na EL ndio kilichompelekea akajiita Mpinga mafisadi ili kulipa kisasi kwa wana mtandao kwa kutopewa u-PM alioahidiwa 2005 wakiwa kwenye harakati za kuelekea uchaguzi mkuu. Bungeni ilikuwa ni platform yake pekee ya kumrudi EL. Kwanza Sitta atuambie alipokuwa TIC ndio kipindi Richmond ilisajiliwa, kama alijua ni kampuni feki mbona hakusema? Msishabikie vita - maslahi. Sitta huwezi kumtenga na mafisadi wengine.

Muulizeni huyo Sitta wenu ofisi yake aliyojenga Urambo iliyotumia zaidi ya sh. 470m halafu anamdanganya hadi Rais kuwa imetumia only 170m. Kama si ufisadi ni nini? Sitta alipoona CCM wanataka kumtema yeye na akina Mwakyembe, Mwambalaswa, Nape, Mpendazoe and others wakaanzisha CCJ iliyokuja hujumiwa baadaye na kukosa usajili wa kudumu, vinginevyo wengi wenu ndio mngejua true colours za Sitta!

Kuna kundi lao wakati huo walipokuwa mjengoni wakijiita wabunge wapinga mafisadi wakiwemo hao niliowataja hapo juu na akina Anne Kilango, Stella Manyanya, Lembeli, Selelii na wengineo waliweza kuwadanganya Watz kuwa wao ni tofauti na magamba wengine, kitu ambacho si cha kweli. Wanatumia umbumbumbu wa Wananchi wasiojua kupembua mbivu na mbichi kujijengea umaarufu. Wote ni wanafiki, yote hayo ni mbio za kuelekea ikulu 2015. Msituzingue!
 
Heshima kwenu wanaukumbi.

Wakuu waTanzania ni watu wa ajabu sana hata uwafanyie nini hawana shukrani naweza kuwalinganisha watanzania na wananchi wa Libya ambao Gaddaf aliwafanyia mambo mengi mazuri lakini shukrani waliomrejeshea ni kumtoa uhai wake na kuufanyia dhihaka mwili wake.

Mheshimiwa Sitta ana mapungufu mengi kama walivyo binadamu wote lakini yapo baadhi ya mambo kayafanya kwa kweli lazima tuyatambue na kuyaenzi.Tatizo la waTanzania wengi hasa hapa ukumbini tunapenda kutoa sifa kwa wanasiasa kwa kuangalia wanawakilisha chama gani,nina hakika Sitta angekuwa mwaCDM ukumbi huu ungerindima kwa shangwe na vifijo,sifa zake zingeelezwa bila hiyana yoyote bahati mbaya Sitta ni mwanaCCM.

Mheshimiwa Sitta kajitahidi sana kwa nafasi yake ya Uspika kubadili kanuni na uendeshaji wa bunge na ndiyo maana leo hii bunge letu linafuatiliwa na wananchi wengi wa kawaida.
Kama si Mheshimiwa Sitta bunge lingebaki uchuro na kichekesho mbele ya jamii ya kitanzania.Ni Mheshimiwa Sitta aliyeahakikisha kama za Kamati ya Hesabu za Serikali,Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa,Kamati ya hesabu za mashirika ya umma zinaongozwa na wabunge wa upinzani.Bunge la Tanzania limewahi kuongozwa na maspika wengi ambao hawakuwa na jambo jipya zaidi ya kusinzia na kuvaa majohoo.
 
Kweli wewe mstaafu mawazo ya kizamani sana, your ideas are not workable in the closed and corrupt system like Tanzania.
kwa hiyo unaniambia sitta anatumia mawazo ya kisasa kulikabili suala la dowans?basi badala ya kumuita manafiki tutamuita mchochezi na muhuni!
 
Katika kamusi, neno ‘Mnafiki’ maana yake ni mtu mwenye kigeugeu au mwenye kuwa na sura mbali mbali: Leo hivi kesho vile. Nyie mnaosema eti Sitta ni mnafiki, je ni kwa lipi? Huyu kiongozi Watanzania wengi wanamkubali kwa kuwa amekuwa na msimamo usiotetereka. Mfano ni kupinga malipo ya kifisadi kwa Dowans, Sitta amesimama kidete na hata kusema hadharani kila mara kuwa anapinga malipo haya ya kifisadi na yuko tayari kwa lolote.

If anything, Sitta is the complete opposite of unafiki, kwani amekuwa daima akisimamia anachoamini bila kutetereka. Hata walipomtishia kumfukuza kazi serikalini au kwenye CCM kwa kupingana na msimamo wa serikali juu ya Dowans na ufisadi mwingine alisimama kidete na kukataa kuwa kigeugeu kwenye msimamo wake. Huyu ndiye aina ya kiongozi ambaye Tanzania inamhitaji.

Mafisadi ndiyo wamejaribu kumchafua Sitta kuwa eti ni "mnafiki" kwa kuwa amekuwa ni mwiba mkali sana asiyetetereka ndani na CCM na serikali kupinga ufisadi. Ni aibu kubwa na jambo la kusikitisha kuona baadhi ya The so-called Great Thinkers wa JF nao wameingia kwenye mkumbo wa mafisadi...

Mdau, Sitta ana nafasi kubwa ya kumuona Rais privately na kumshauri, bado ana nafasi ktk BLM kutofautiana na wenzie lkn hafanyi hivyo na anakimbilia kwenye vyombo vya habari na kueleza misimamo yake tofauti na wenzie, collective responsibility iko wapi kwa Sitta. Amini nakuambia mtu wa namna hii is not reliable, hata wewe mkikubaliana kitu anaweza kukugeuka kesho yake na hiyo ndio character ya Sitta haikuanza jana wala leo. Sitta amefanikiwa kuwavuta watu kama akina Fareed na wewe the Informer kumuamini. Zindukeni hakuna msafi wa kihivyo mnavyodhani!
 
Mnaodai kuwa sita ahamie chadema,mnainadhifu chadema bure 2.hata huko hakuna wasafi.chadema imejaa udini{ukristo} ukabila na ukanda.kina zito wamewekwa km babaisha ***** 2. Fahamuni kuwa HAKUNA MTETEZI WA MNYONGE ZAIDI YA MNYONGE MWENYEWE.si chama cha siasa wala mwanasiasa atakaeweza kumkomboa mtanzania maskini zaid ya mtanzania mwenyewe.ACHENI SIASA ZA NJOZ,KUWENI WAHALISIA!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom