Samwel Sitta ashangiliwa sana UDSM

kama waziri sitta ana uwezo wa kumshauri au kumshawishi rais kuwa dowans isilipwe,je amewahi kumuandikia barua jk kuhusu dowans?je amewahi kupeleka hoja binafsi kuhusu dowans ijadiliwe kwenye baraza la mawaziri?

Kweli wewe mstaafu mawazo ya kizamani sana, your ideas are not workable in the closed and corrupt system like Tanzania.
 
Wanafiki ni wale viongozi ndani ya serikali wanaolalamika chini kwa chini. SAMUEL SITTA ni mtu aliye straightfoward -- haogopi mtu, na daima anasema ukweli kila wakati bila kujali vitisho. Tanzania inahitaji sana viongozi kama yeye.
 
Hivi neno mnafiki maana yake nini hasa? Kwa bahati mbaya sana, maadui wa Samuel Sitta, ambao ni mafisadi wa Richmonduli, rada, Kagoda, TICTS na wengineo, ndio . wamekuwa wakitumia neno hili ndani ya CCM na nje kujaribu kumpiga vita na kumchafua kiongozi huyu.

Kwa nyie msiojua, Samuel Sitta ni kiongozi shupavu, msema kweli, anayethubutu, mchapa kazi na kiboko wa mafisadi. Tanzania ingempata mtu kama huyu kuwa Rais nchi hii ingeondokana na umasikini katika kipindi chake cha kwanza tu cha miaka mitano! Msiwe wavivu wa kufikiri na kuburuzwa na mafisadi kumuita eti Sitta ni mnafiki, kwa lipi wakati yeye kila siku ameonesha uongozi na ushupavu wa kusema ukweli? -- eg kupinga hadharani malipo ya Dowans, kusema serikali iombe radhi kwa mgao wa umeme, na mengine mengi.

Kwa msiojua, hata CHADEMA wanamfahamu sana Sitta kuwa ni kiongozi makini ndio maana mwaka 2010 walimuomba agombee Urais kupitia chama hicho. Sitta alipokataa ndio ilibidi CHADEMA wambembeleze Dr. WILLIBROD SLAA agombee Urais wakati alikuwa anataka kutetea kiti chake cha ubunge wa Karatu.

Na kama CCM ikimsimamisha Sitta kuwa mgombea Urais wa 2015, basi CHADEMA watapata taabu sana kupambana naye jukwaani. Huu ndio ukweli, acheni uvivu nyie kwa kulishwa maneno na propaganda za mafisadi.

Ndugu yangu Fareed umesema ukweli kabisa, huyu kiongozi ana msimamo sana hata mafisadi wanamuogopa sana. Ni hawa mafisadi wenyewe baafa ya kukosa kashfa yoyote dhidi yake wakaanza kueneza propaganda hasa ndani ya CCM kuwa Sitta ni MNAFIKI, ndio maana neno hili mmeona limejirudia rudia sana humu JF.

Pia wametumia baadhi ya wana usalama walionunuliwa, vyombo vya habari kama magazeti ya Tanzania Daima, Mtanzania na mengineo, kujaribu kueneza hii sumu dhidi ya Sitta. Lakini jitihada zao zimegonga mwamba kwani SAMUEL SITTA anakubalika sana na mamilioni ya Watanzania. Huyu ni mtaji mkubwa sana wa Urais wa 2015 kupitia chama chochote!
 
Hiyo ndo Tanzania huwa tunashindwa kuchambua ni kipi cha maana na kipi si cha maana, tukumbuke wakati Baba Riz anaingia madarakani alishangiliwa na kila mmoja na kuamini ni chaguo la Mungu leo sijui ni changuo la SHETANI? Kiongozi bora anapimwa kwa matendo yake na si kushangiliwa na kundi fulani la watu
 
Hivi neno mnafiki maana yake nini hasa? Kwa bahati mbaya sana, maadui wa Samuel Sitta, ambao ni mafisadi wa Richmonduli, rada, Kagoda, TICTS na wengineo, ndio . wamekuwa wakitumia neno hili ndani ya CCM na nje kujaribu kumpiga vita na kumchafua kiongozi huyu.

Kwa nyie msiojua, Samuel Sitta ni kiongozi shupavu, msema kweli, anayethubutu, mchapa kazi na kiboko wa mafisadi. Tanzania ingempata mtu kama huyu kuwa Rais nchi hii ingeondokana na umasikini katika kipindi chake cha kwanza tu cha miaka mitano! Msiwe wavivu wa kufikiri na kuburuzwa na mafisadi kumuita eti Sitta ni mnafiki, kwa lipi wakati yeye kila siku ameonesha uongozi na ushupavu wa kusema ukweli? -- eg kupinga hadharani malipo ya Dowans, kusema serikali iombe radhi kwa mgao wa umeme, na mengine mengi.

Kwa msiojua, hata CHADEMA wanamfahamu sana Sitta kuwa ni kiongozi makini ndio maana mwaka 2010 walimuomba agombee Urais kupitia chama hicho. Sitta alipokataa ndio ilibidi CHADEMA wambembeleze Dr. WILLIBROD SLAA agombee Urais wakati alikuwa anataka kutetea kiti chake cha ubunge wa Karatu.

Na kama CCM ikimsimamisha Sitta kuwa mgombea Urais wa 2015, basi CHADEMA watapata taabu sana kupambana naye jukwaani. Huu ndio ukweli, acheni uvivu nyie kwa kulishwa maneno na propaganda za mafisadi.

Waache waendelee tu kuimbaimba Mnafiki...Mnafiki...Mnafiki kama mazuzu, wameshakaririshwa so usitegemee jambo tofauti.

Watanzania ni watu rahisi sana kuwatawala, and they doomed kutawaliwa kijingajinga milele na wanastahili hilo...
 
Well said, nimegundua wanajamvi wengi humu JF aidha wanafaidi na mfumo uliopo wa kifisadi indirectly au wao ni mafisadi in the making. Haiwezekani mtu anayepinga ufisadi anaitwa mnafiki kwa sababu tu record imekuwa tainted na jambo fulani. Hii siyo haki kabisa

hivi unaweza kumfananisha sitta na slaa katika kupinga ufisadi?mshaurini sitta atulie aendelee kutetea posho bungeni na sio kuuza sura magazetini.
 
Hiyo ndo Tanzania huwa tunashindwa kuchambua ni kipi cha maana na kipi si cha maana, tukumbuke wakati Baba Riz anaingia madarakani alishangiliwa na kila mmoja na kuamini ni chaguo la Mungu leo sijui ni changuo la SHETANI? Kiongozi bora anapimwa kwa matendo yake na si kushangiliwa na kundi fulani la watu

Hata Slaa alishangiliwa sana, hiyo maana yake ni kuwa akiingia madarakani atakuwa kiongozi mbovu kama JK? Acheni kupindisha maneno, Sitta ni jembe na wote wanajua hilo. Wanafunzi wamemshangilia kwa kuwa wanakubali yeye ni shujaa ambaye daima anasema ukweli na hayuko tayari kuwa MNAFIKI!
 
Ndugu yangu Fareed umesema ukweli kabisa, huyu kiongozi ana msimamo sana hata mafisadi wanamuogopa sana. Ni hawa mafisadi wenyewe baafa ya kukosa kashfa yoyote dhidi yake wakaanza kueneza propaganda hasa ndani ya CCM kuwa Sitta ni MNAFIKI, ndio maana neno hili mmeona limejirudia rudia sana humu JF.

Pia wametumia baadhi ya wana usalama walionunuliwa, vyombo vya habari kama magazeti ya Tanzania Daima, Mtanzania na mengineo, kujaribu kueneza hii sumu dhidi ya Sitta. Lakini jitihada zao zimegonga mwamba kwani SAMUEL SITTA anakubalika sana na mamilioni ya Watanzania. Huyu ni mtaji mkubwa sana wa Urais wa 2015 kupitia chama chochote!

Umesahau Bungeni juzi aliwaita Wapinzani wanafiki juu ya posho na yeye akasema posho ? Unakumbuka aliliia na maandamano baada ya siku chache akaaandamana Mbeya ? Kwa matukio machache unaonaje si mnafiki huyu ?
 
Umesahau Bungeni juzi aliwaita Wapinzani wanafiki juu ya posho na yeye akasema posho ? Unakumbuka aliliia na maandamano baada ya siku chache akaaandamana Mbeya ? Kwa matukio machache unaonaje si mnafiki huyu ?

nashukuru kwa kutukumbusha matukio muhimu
 
Umesahau Bungeni juzi aliwaita Wapinzani wanafiki juu ya posho na yeye akasema posho ? Unakumbuka aliliia na maandamano baada ya siku chache akaaandamana Mbeya ? Kwa matukio machache unaonaje si mnafiki huyu ?

Hizi ni siasa za ushindani tu, sioni tatizo kwa Sitta kupingana na upinzani na kuitetea serikali kwa yale ambayo anayaunga mkono. Posho ni mjadala mwingine, ki msingi hata Nyerere alilipa posho kwenye serikali yake, kinachotakiwa ni usimamizi mzuri wa malipo hayo kuangalia kama viwango kweli vinaendana na uchumi wa nchi na pesa hizi hazifujwi.

Tanzania inahitaji viongozi wasema kweli na shupavu kama Sitta na si watawala wanafiki!
 
Kumbe kuna wasomi wanaomshangilia huyu mnafiki?..
Ana mazuri na mabaya ake, but for now, he is a lesser devil if you compare him with a couple of other government leaders. Hata ndani ya kundi la wasomi kuna wanafiki, vibaraka, wenye dhamira ya kweli ya kuikomboa nchi, wenye uroho wa pesa na wengine wengi utakaoweza kuwataja. So, as a citizen, Samwel Sitta has a liberty to advocate whatever he believes in.
 
Hizi ni siasa za ushindani tu, sioni tatizo kwa Sitta kupingana na upinzani na kuitetea serikali kwa yale ambayo anayaunga mkono. Posho ni mjadala mwingine, ki msingi hata Nyerere alilipa posho kwenye serikali yake, kinachotakiwa ni usimamizi mzuri wa malipo hayo kuangalia kama viwango kweli vinaendana na uchumi wa nchi na pesa hizi hazifujwi.

Tanzania inahitaji viongozi wasema kweli na shupavu kama Sitta na si watawala wanafiki!
vipi kuhusu maandamano
 
Umesahau Bungeni juzi aliwaita Wapinzani wanafiki juu ya posho na yeye akasema posho ? Unakumbuka aliliia na maandamano baada ya siku chache akaaandamana Mbeya ? Kwa matukio machache unaonaje si mnafiki huyu ?

Hivi mtu ambaye hadharani anasema posho ni wizi wa fedha za umma na wakati huohuo sirini anazipokea kwa furaha, kuna jina gani la kumuita zaidi ya mnafiki? Mh. Sitta alikuwa sahihi katika hilo.

Katika Wabunge woote walioziita posho kuwa ni wizi, ni Mh. Zitto peke yake aliyeweza kuwa na ujasiri wa kuzikataa posho kwa vitendo, hilo ndilo tunalolihitaji kwa viongozi wetu, uongozi sio kupiga domo tu bali ni kuwa na uwezo pia wa kutembea kwenye maneno yako.
 
Katika kamusi, neno ‘Mnafiki' maana yake ni mtu mwenye kigeugeu au mwenye kuwa na sura mbali mbali: Leo hivi kesho vile. Nyie mnaosema eti Sitta ni mnafiki, je ni kwa lipi? Huyu kiongozi Watanzania wengi wanamkubali kwa kuwa amekuwa na msimamo usiotetereka. Mfano ni kupinga malipo ya kifisadi kwa Dowans, Sitta amesimama kidete na hata kusema hadharani kila mara kuwa anapinga malipo haya ya kifisadi na yuko tayari kwa lolote.

If anything, Sitta is the complete opposite of unafiki, kwani amekuwa daima akisimamia anachoamini bila kutetereka. Hata walipomtishia kumfukuza kazi serikalini au kwenye CCM kwa kupingana na msimamo wa serikali juu ya Dowans na ufisadi mwingine alisimama kidete na kukataa kuwa kigeugeu kwenye msimamo wake. Huyu ndiye aina ya kiongozi ambaye Tanzania inamhitaji.

Mafisadi ndiyo wamejaribu kumchafua Sitta kuwa eti ni "mnafiki" kwa kuwa amekuwa ni mwiba mkali sana asiyetetereka ndani na CCM na serikali kupinga ufisadi. Ni aibu kubwa na jambo la kusikitisha kuona baadhi ya The so-called Great Thinkers wa JF nao wameingia kwenye mkumbo wa mafisadi...
 
Well said, nimegundua wanajamvi wengi humu JF aidha wanafaidi na mfumo uliopo wa kifisadi indirectly au wao ni mafisadi in the making. Haiwezekani mtu anayepinga ufisadi anaitwa mnafiki kwa sababu tu record imekuwa tainted na jambo fulani. Hii siyo haki kabisa

Wallahi vile, hakuna cha Great Thinkers au lolote. Wengine humu wana tabia ya kupenda kukaririshwa maneneno halafu wao kazi yao ni kuyaimba tuuu kama majuha. Ukiliangalia neno "mnafiki", ukaangalia na vitendo vya Samuel Sitta ni vitu viwili tofauti! Tena wanaotumia neno hili eti kujaribu kumchafua ndio wanamjenga bila kujua kwani Sitta ni kinyume kabisa cha mnafiki. Wanafiki ni wale viongozi ambao wanakaa kimya wakiona maovu serikalini, kama malipo kwa DOWANS, halafu wanabaki kulalamika tu pembeni.

Sitta amekataa kwa vitendo kuwa mnafiki na amekuwa kila mara akisema ukweli kuwa nchi hii imeshikwa na mafisadi wachache ambao wanautafuna uchumi wa taifa kama mchwa, amesimama hadharani na kukiri kuwa rushwa imekithiri serikalini, amesimama hadharani na kukiri kuwa mgao wa umeme ni aibu kwa taifa na serikali lazima iombe radhi, amesimama hadharani kusema kuwa viongozi wengi wamekosa maadili na wanatafuta mali tu serikalini, amesimama hadharani na kusema umasikini wa Tanzania haukubaliki na unaweza kutokomezwa kama serikali ikiwa makini, amesimama hadharani na kusema atapinga milele malipo ya kifisadi ya DOWANS licha ya serikali kukubali kulipa.

Sitta ni kiongozi pekee ndani ya serikali ya CCM aliyeonesha USHUPAVU, UZALENDO, MSIMAMO, na KUTOTETEREKA.
 
Ni kweli kashangiliwa lkn ni kati ya watu hawana msimamo anauchu na ikulu pia ni kati ya watu wanafiki ambao wanatoa hoja nzito lkn kuitetea hawawezi kumbukeni Bunge lililopita na akiwa anamsidia waziri mkuu kujibu maswali alivyokuwa anajaribu kuzizima hoja za msingi kwa taifa letu kweli mgema akisifiwa Tembo hulitia maji
 
Ni kweli kashangiliwa lkn ni kati ya watu hawana msimamo anauchu na ikulu pia ni kati ya watu wanafiki ambao wanatoa hoja nzito lkn kuitetea hawawezi kumbukeni Bunge lililopita na akiwa anamsidia waziri mkuu kujibu maswali alivyokuwa anajaribu kuzizima hoja za msingi kwa taifa letu kweli mgema akisifiwa Tembo hulitia maji

Hatudanganyikiiiiii! Sitta ni kiongozi mwenye msimamo, kuisadia serikali na waziri mkuu kwa mambo anyoamini ni sawa kwani ikumbukwe kuwa yeye ni mwana CCM na ni waziri. Tunamwamini na kumhitaji SAMUEL SITTA kutokana na kukataa kuwa kigeugeu na mnafiki katika kupinga ufisadi na siku zote amekuwa msema kweli na kiongozi shupavu.

Wenye uchu wa kwenda Ikulu wanajulikana, kinara wao ni waziri mkuu wa zamani aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond.
 
Independent Thinkers ni watu wachache sana. Watanzania wengi ni wavivu wa kuamini, wanasubiri wasome vitu kwenye vyombo vya habari, eg makala za Absalom Kibanda wa Tanzania Daima zinazofadhiliwa na Edward Lowassa na Rostam Aziz dhidi ya Samuel Sitta, au waone post humu JF basi na wao kuunga tela kama ng'ombe wakimfuata mchungaji. Zindukeni Watanzania! Tumieni akili zenu kufikiria wenyewe si kukaririshwa maneno!

Iweje kamanda mpambanaji wa ufisadi, tena anayethubutu kusimama hadharani na kupingana na maamuzi ya kifisadi ya serikali, kama kuilipa Dowans akaitwa mnafiki? Msikubali kupakatwa na mafisadi!
 
Laiti wangelijua kuwa huyo ni Mbwa mwitu mkali!! ndani ya ngozi ya kondoo.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom