Samsung Grand Prime Plus+ Inafaa

Samsung Grand Prime Plus+ Inafaa

mambo madogo tu mkuu, ram yake ni kubwa na cpu yake ni average ila gpu ni ndogo na sababu ni mediatek kuna vitu kama virusi, jiandae. nimeiona madukani 250,000 bei sio mbaya compare na competition zinazopatikana madukani.

ila kama una uwezo ni bora utafute simu za xiaomi mkuu, redmi 3 au redmi 4a ina specs za maana kushinda hadi simu za laki 5 au 4 za samsung na wengine wanaopatikana Tanzania. na bei zake zote ni chini ya dola 100. zipo kenya tu hapo official kama una uwezo jitahidi kutafuta hizo.
Mkuu hii ya Mediatek na virusi imekaje hii? naomba unieleweshe mkuu..
 
Mkuu hii ya Mediatek na virusi imekaje hii? naomba unieleweshe mkuu..
Simu yoyote ya android inaweza ingia hawa malware ila tatizo la mediatek ni kwamba ni rahisi kuiroot, inakuwa na bugs ambazo application inaweza kujipa root.

Application ikishajipa root inajibadili kutoka application ya kawaida hadi system app. Nikisema system app namaanisha application zinazokuja na simu kama vile sms, gallery, calender etc. Hivyo hata ukieka ant virus inakuwa haisaidii sababu ant virus haiwezi kugusa hizo system apps inascan tu app unazodownload, kifupi malware anakuwa na nguvu kushinda hata hio ant virus.

Sababu pia ni system app hata ukifanya hard reset haisaidii sababu system apps hazifutiki ukifanya hard reset.


Ndio maana mtaani simu za mediatek kama huawei za bei rahisi, Tecno, Itel etc zina matatizo sana unaskia mtu analalamika simu yangu inaonyesha video za ngono, mwengine anakwambia nikiwasha data yanakuja matangazo etc.

Kibaya zaidi ni kwamba simu nyingi za mediatek hazipati updates, hasa hasa monthly updates za security toka google, hivyo hata kama kuna patch ya kusolve hivi vitu hizo simu hazipati
 
Simu yoyote ya android inaweza ingia hawa malware ila tatizo la mediatek ni kwamba ni rahisi kuiroot, inakuwa na bugs ambazo application inaweza kujipa root.

Application ikishajipa root inajibadili kutoka application ya kawaida hadi system app. Nikisema system app namaanisha application zinazokuja na simu kama vile sms, gallery, calender etc. Hivyo hata ukieka ant virus inakuwa haisaidii sababu ant virus haiwezi kugusa hizo system apps inascan tu app unazodownload, kifupi malware anakuwa na nguvu kushinda hata hio ant virus.

Sababu pia ni system app hata ukifanya hard reset haisaidii sababu system apps hazifutiki ukifanya hard reset.


Ndio maana mtaani simu za mediatek kama huawei za bei rahisi, Tecno, Itel etc zina matatizo sana unaskia mtu analalamika simu yangu inaonyesha video za ngono, mwengine anakwambia nikiwasha data yanakuja matangazo etc.

Kibaya zaidi ni kwamba simu nyingi za mediatek hazipati updates, hasa hasa monthly updates za security toka google, hivyo hata kama kuna patch ya kusolve hivi vitu hizo simu hazipati

asante sana mkuu, sasa kuna mtu ana budget ya between 250000-350000 unamshauri achukue simu gani ambayo si mediate kwani yeye ni mtumiaji wa kawaida tu..brawsing, emails etc. Msaada pls!
 
asante sana mkuu, sasa kuna mtu ana budget ya between 250000-350000 unamshauri achukue simu gani ambayo si mediate kwani yeye ni mtumiaji wa kawaida tu..brawsing, emails etc. Msaada pls!


kwa samsung budget hio anapata galaxy j5, ila ahakikishe ni version ya 4G maana ipo ya 3G tupu, kwa age hizi 4G ni must. pia hakikisha ina smart care yaani warranty ya samsung

kwa huawei kuna p8 lite nayo imetulia japo battery ni average.

kuna thread ya oppo icheki hapa nayo ni simu nzuri kwa 250,000

Nimeamua kubadili brand ya simu rasmi
 
Mkuu Chief-Mkwawa heshima kwako:

Naomba msaada hapa... Nataka nijilipue kwa SG J7 prime ambayo ina 3gb ram na 16gb rom ila kwenye pitapita zangu mtandaoni nikaona kuwa hazitapata updates za Nougat!!
Pili kuna prime za 32gb rom ila wadau wanazoziuza wanadai hazina warrant... Ebu naomba mtizamo wako hapo kuhusu huyu prime.
 
Mkuu Chief-Mkwawa heshima kwako:

Naomba msaada hapa... Nataka nijilipue kwa SG J7 prime ambayo ina 3gb ram na 16gb rom ila kwenye pitapita zangu mtandaoni nikaona kuwa hazitapata updates za Nougat!!
Pili kuna prime za 32gb rom ila wadau wanazoziuza wanadai hazina warrant... Ebu naomba mtizamo wako hapo kuhusu huyu prime.

mkuu kama una uwezo subiria j7 ya 2017 itakuwa na mambo yote hayo pamoja na full hd super amoled na processor inayotunza chaji.

kuhusu hio nougat update nafkiri itakuja ila itachelewa tu, wapi umeona haitapata updates?

na ni vyema iwe na warranty, hizo ambazo hazina nyingi ni vimeo wanatafuta refurbished phone na kuja kuzidump huku kwetu.
 
mkuu kama una uwezo subiria j7 ya 2017 itakuwa na mambo yote hayo pamoja na full hd super amoled na processor inayotunza chaji.

kuhusu hio nougat update nafkiri itakuja ila itachelewa tu, wapi umeona haitapata updates?

na ni vyema iwe na warranty, hizo ambazo hazina nyingi ni vimeo wanatafuta refurbished phone na kuja kuzidump huku kwetu.
Kudos mkuu..
Kwenye reviews za watu kule phonearena.
 
Naomba mniambie ubora wa infinix note 3 maana mimi naitumia nimeapgrade kwenda kwenye android 7.01 naona kila kitu kipo sawa je na miss nini?
 
mkuu kama una uwezo subiria j7 ya 2017 itakuwa na mambo yote hayo pamoja na full hd super amoled na processor inayotunza chaji.

kuhusu hio nougat update nafkiri itakuja ila itachelewa tu, wapi umeona haitapata updates?

na ni vyema iwe na warranty, hizo ambazo hazina nyingi ni vimeo wanatafuta refurbished phone na kuja kuzidump huku kwetu.

Unanishaurije J3 2017 imeishatoka bado haijafika?
 
yap ni majanga, simu ya mediatek nunua ikiwa inakupa perfomance kubwa kuliko competition, mfano kuna simu za mediatek helio x20 chini ya laki 4 hilo ni deal nzuri lakini hawa kina samsung, Tecno, Htc, huawei, Lg etc sio tu kwamba wanaeka mediatek, wanaeka mediatek zile ndogo kabisa ambazo hata perfomance nzuri ya kila siku hutaipata
Brand sells.
 
Ha ha ha sema kenya sasa kupata mtu wa kukununulia ni ishu kenya hadi vyombo bya muziki ni nusu ya bei ya Tz ila sasa namna ya kuvinunua ndio ishu. Kuna jamaa waliniambia wanatuma nikaona nitapigwa hapa
Inategemea ila wapo roho safi pia watanzania wenzako
 
Unanishaurije J3 2017 imeishatoka bado haijafika?
mkuu hio camera yake subiria reviews kwanza maana inatia mashaka, na pia hio cpu kwa simu itakayozidi laki 3 naona kama ni ya kawaida sana. pia kioo na battery naona kama hakuna upgrade ya maana.

kama bei yake itakuwa ni zaidi ya laki 3 ni simu isio na maana sababu j5 za 2015 now unazipata mpya kwa hio bei, nafkiri hata ya 2016 imeshadrop hadi around 350,000.

j5 ina camera nzuri, ram kubwa, software version yake (touchwiz mpya) inashare na wakubwa na inakubali vitu kama themes, cpu nzuri, probably gpu nzuri etc
 
mkuu hio camera yake subiria reviews kwanza maana inatia mashaka, na pia hio cpu kwa simu itakayozidi laki 3 naona kama ni ya kawaida sana. pia kioo na battery naona kama hakuna upgrade ya maana.

kama bei yake itakuwa ni zaidi ya laki 3 ni simu isio na maana sababu j5 za 2015 now unazipata mpya kwa hio bei, nafkiri hata ya 2016 imeshadrop hadi around 350,000.

j5 ina camera nzuri, ram kubwa, software version yake (touchwiz mpya) inashare na wakubwa na inakubali vitu kama themes, cpu nzuri, probably gpu nzuri etc

Nimekuelewa
 
mkuu kama una uwezo subiria j7 ya 2017 itakuwa na mambo yote hayo pamoja na full hd super amoled na processor inayotunza chaji.

kuhusu hio nougat update nafkiri itakuja ila itachelewa tu, wapi umeona haitapata updates?

na ni vyema iwe na warranty, hizo ambazo hazina nyingi ni vimeo wanatafuta refurbished phone na kuja kuzidump huku kwetu.
DUH HIVI KWELI HAMNA PRIME 32GB AMBAYO IKO POA
 
Mkuu Chief-Mkwawa heshima kwako:

Naomba msaada hapa... Nataka nijilipue kwa SG J7 prime ambayo ina 3gb ram na 16gb rom ila kwenye pitapita zangu mtandaoni nikaona kuwa hazitapata updates za Nougat!!
Pili kuna prime za 32gb rom ila wadau wanazoziuza wanadai hazina warrant... Ebu naomba mtizamo wako hapo kuhusu huyu prime.
Mkuu hebu niweke sawa hapo wanaposema kwamba haina warrant maana yake nini yaan wao hawakupi warrant au?
 
Mkuu hebu niweke sawa hapo wanaposema kwamba haina warrant maana yake nini yaan wao hawakupi warrant au?
ukweli ni kwamba warranty haitolewi na mwenye duka, bali hutolewa na mtengeneza simu, kwa case hio ni samsung, simu yako inapoharibika ukiirudisha ulipoinunua ataipeleka samsung au akuelekeze uipeleke.

hivyo samsung wenyewe kuna simu hawataki zije huku kwetu, zinakuwa ni kwa ajili ya masoko fulani tu, lakini wafanya biashara wanazileta tu kwa njia zao wanaojua wao hivyo zikija zinakuwa hazina warranty, na kama ikiharibika ni juu yako, samsung hawatahusika.
 
DUH HIVI KWELI HAMNA PRIME 32GB AMBAYO IKO POA
zipo mkuu prime za 32Gb na specs ni hizo hizo, na j7 prime ipo poa compare na j7 ya 2015 na 2016 ila ikitoka hii ya 2017 ni vyema ukatafuta ya 2017. ila kama unayo tayari prime haina neno bado ni simu nzuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom