Samsung Grand Prime Plus+ Inafaa

Samsung Grand Prime Plus+ Inafaa

ukweli ni kwamba warranty haitolewi na mwenye duka, bali hutolewa na mtengeneza simu, kwa case hio ni samsung, simu yako inapoharibika ukiirudisha ulipoinunua ataipeleka samsung au akuelekeze uipeleke.

hivyo samsung wenyewe kuna simu hawataki zije huku kwetu, zinakuwa ni kwa ajili ya masoko fulani tu, lakini wafanya biashara wanazileta tu kwa njia zao wanaojua wao hivyo zikija zinakuwa hazina warranty, na kama ikiharibika ni juu yako, samsung hawatahusika.
Ahaaa sasa mkuu naweza kujuaje kama sim ina warrant au la?
 
zipo mkuu prime za 32Gb na specs ni hizo hizo, na j7 prime ipo poa compare na j7 ya 2015 na 2016 ila ikitoka hii ya 2017 ni vyema ukatafuta ya 2017. ila kama unayo tayari prime haina neno bado ni simu nzuri.
Shukran mie wasiwasi wangu ulikuwa hapo kwenye rom ya 32gb uliposema wanazidump basi mie nikajua hizo za 32gb si special kwa ajili yetu labda
 
xiaomi-redmi-note-3-phone-14.jpg


specification hizi hapa
Xiaomi Redmi Note 3 - Full phone specifications

specs zinazoifanya iwe ni simu ya kipekee ni
-battery kubwa 4050mah
-ina core mbili za cortex a72
Zinavutia
 
Mimi ninayo hii simu na nazijua..kuijua ya Snapdragon nenda settings then about phone finally angalia kipengele cha CPU,kama ni Snapdragon imeandikwa "Hexacore" ila kama ni Mediatek utakuta octacore.
Hii simu nikiitaka naipataje?
Na bei yake ipoje sokoni kwa sasa mkuu!
 
Simu yoyote ya android inaweza ingia hawa malware ila tatizo la mediatek ni kwamba ni rahisi kuiroot, inakuwa na bugs ambazo application inaweza kujipa root.

Application ikishajipa root inajibadili kutoka application ya kawaida hadi system app. Nikisema system app namaanisha application zinazokuja na simu kama vile sms, gallery, calender etc. Hivyo hata ukieka ant virus inakuwa haisaidii sababu ant virus haiwezi kugusa hizo system apps inascan tu app unazodownload, kifupi malware anakuwa na nguvu kushinda hata hio ant virus.

Sababu pia ni system app hata ukifanya hard reset haisaidii sababu system apps hazifutiki ukifanya hard reset.


Ndio maana mtaani simu za mediatek kama huawei za bei rahisi, Tecno, Itel etc zina matatizo sana unaskia mtu analalamika simu yangu inaonyesha video za ngono, mwengine anakwambia nikiwasha data yanakuja matangazo etc.

Kibaya zaidi ni kwamba simu nyingi za mediatek hazipati updates, hasa hasa monthly updates za security toka google, hivyo hata kama kuna patch ya kusolve hivi vitu hizo simu hazipati
Asante mkuu kwa kutupa elimu kwa sisi tusio wakali wa IT,
Vipi na TECNO phamtom 6 nayo ni mediatek?
 
Asante mkuu kwa kutupa elimu kwa sisi tusio wakali wa IT,
Vipi na TECNO phamtom 6 nayo ni mediatek?
Mkuu nasubiria sana jibu ya hili swal
Phantom 6 plus inanishwaishi ila ngoja wataalam waje
 
kwa samsung budget hio anapata galaxy j5, ila ahakikishe ni version ya 4G maana ipo ya 3G tupu, kwa age hizi 4G ni must. pia hakikisha ina smart care yaani warranty ya samsung

kwa huawei kuna p8 lite nayo imetulia japo battery ni average.

kuna thread ya oppo icheki hapa nayo ni simu nzuri kwa 250,000

Nimeamua kubadili brand ya simu rasmi
Mkuu Chief, oppo ni nzuri kwa bei tuu! Vipi kuhusu ufanyaji kazi wake kwa ujumla?
Mi nipo njiani kununua phamtom 6 ndio naona inanifaa kwa sasa,
 
Mkuu Chief, oppo ni nzuri kwa bei tuu! Vipi kuhusu ufanyaji kazi wake kwa ujumla?
Mi nipo njiani kununua phamtom 6 ndio naona inanifaa kwa sasa,
inategemea mkuu unanunua ipi, mfano kama hii alioileta jamaa kwenye thread hii
Karibuni tuichambue simu ya Oppo f3 Plus

ni nzuri kushinda phantom 6/6 plus.

4gb ram, 64gb memory, dual selfie camera, sd 653, sensor ya kisasa ya camera ya IMX 398, battery kubwa la 4000mah etc
 
Tofauti ni hipi na hiz mediatk zingine.mana naona hizo phantom bei iko juu.
mediatek ni jina tu, zipo mediatek nyingi kuanzia za bei rahisi hadi ghali kuna helio x10, x20, x25, helio p10, p20 etc kila moja ina bei yake. unapotumia soc ya bei ghali ndio simu inavyokuwa ghali, pia kuna mambo mengine kama display, camera, material ya nje, speaker, mic etc navyo pia vina gharama, simu za bei kubwa hivyo vitu huwa ni vizuri zaidi.
 
Wakuu nipo china kwa sasa.....Anayehitaji simu ya brand za China niWhatsapp nikupe bei...0684366488
Narudi tar 30
 
mediatek ni jina tu, zipo mediatek nyingi kuanzia za bei rahisi hadi ghali kuna helio x10, x20, x25, helio p10, p20 etc kila moja ina bei yake. unapotumia soc ya bei ghali ndio simu inavyokuwa ghali, pia kuna mambo mengine kama display, camera, material ya nje, speaker, mic etc navyo pia vina gharama, simu za bei kubwa hivyo vitu huwa ni vizuri zaidi.
Thanks chief nmekupata barabara
 
Chief Mkwawa naomba msaada.

Kati ya TECNO PHANTOM 6, 6+ na LG G5 ipi simu bora zaidi.

Na Bei ya LG G5 mpya inaweza kuwa kiasi gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom