Mi naomba kujibiwa: Why now? kwa nini Suala la Salva lizuke sasa hivi baada ya kupata appointment ya muungwana????????? Kwani kabla ya hapo alikuwa anaishi sayari ya mars au pluto? I can see immense level of hatred and character assasin, maana huyu Salva, mpaka wengine wamesema ndo aliharibu ndoto ya SAS kuwa rais. Granted. Mbona hawakumreport Immigration????? Kama kweli hakuwa raia? au kwa vile alikuwa inconsequential? hakuwa na madaraka? (lakini mtu anayeweza kuinfluence kiongozi wa nchi awe nani, nadhani ni heavy weight)
Kwa nini humu JF thread za uraia wa watu zinazuka pale tuu wanapokuwa wamepata either appointment au fame fulani kwenye nchi yetu? mfano Richa Miss TZ (of all people), Salva, Ikulu, Bandora Ubalozi nk????? Hapana mi naona kuna unafiki na double standards humu kwa walio wengi. Mbona sijawahi kusikia mwenyekiti wakijiji au mtu yeyote asiye na madaraka akifuatiliwa uraia wake? atleast hata humu JF? Mi nina walakini na ndo maana naamini kwamba, TANZANIA IMEJAA WASANII KUANZIA KWA WANANCHI MPAKA VIONGOZI WETU. Ni wachache saaaana walio sincere katika wayafanyayo. TUNAPENDA SANA SHORTCUT katika maisha yetu.
Ni dhambi kubwa kumhukumu au kuhoji uraia wa mtu kisa anatokea, Mbinga, Rukwa, Tarime, Kasulu, Ngara au Karagwe kwa sababu hizi sehemu ziko mipakani. Siamini kwamba mtu ni mtz halisi kwa vile anatokea Singida, Pwani na Tabora. This is pure nonsense Na hapa ndo tutamalizana kwa sababu tunapenda siasa za victimization. Wonder what happened to the politics of hope za watu fulani humu JF! Sikatai kuhoji na kushughulikia illigal immigrants, ila zoezi liwe fair and balanced lisitarget watu solely kwa kuangalia wanakotoka au pua zao.
Hili la Salva lisingezuka kama jamaa angekuwa anatokea Singida au kwingeneko. We jiulize leo Mungai anaitwa Mkikuyu, ila kwa vile anatokea Iringa no body has ever questioned that, Iam sure ingekuwa tofauti kama huyu Mungai angekuwa anatokea Kagera, Kigoma au Mara. Huu ni upuuzi na hapa ndo wengi hatutakubaliana na hizi sisa za opportunism katika nchi yetu. Au jiuliuze kama Burundi na Rwanda zingekuwa prosperous countries, nani angeuliza uraia wa watz wa mipakani huko kaskazini? lakini kwa sababu wana shida, vita nk. wanaoishi karibu ya nchi hizi wanaonekana kuwa wale wale. Sasa baadhi yenu mkijidai kwamba mnaheshimu na kudumisha fikra za mwalimu naona ni UNAFIKI, Nyerere couldnt be privy to these kind of stupid assumptions and politics za kuvictimize watu kwa kuangalia pua au sura ya mtu. Na ndo maana tumeweza kuwa taifa huru na la amani. The old man knew what he was doing.
selfishness and love can never go together. Kama kweli tumeamua kufanya hili zoezi, basi tulifanye kwa maslahi ya nchi na siyo kwa maslahi ya kuumizana na wivu kwa baadhi ya wenzetu. Na wote tujue, unaweza kumchagua rafiki, ila hutamchagua jirani, wote duniania hakuna aliyechagua azaliwe wapi na kwa nani, it was geographical accident, sasa kwa nini Byamungu, Mugisha, Saitoti au Odinga au Mwanawasa waumizwe kisa wana majina yanayofanana na raia wa nchi jirani? Its all nonsense na kwa hili we are going no where.