Salute kwa waliosoma PCB/PCM

o-level nilisoma sayansi matokeo yametoka masomo ya arts yote nina alama D na masomo ya sayansi nikapata F yote!!! nilidata hadi bi mkubwa akawa hana amani kama yeye ndo kafeli
ushauri ukaja nikasome madiploma ya arts kwa D zangu uku wengine wakisema sayansi uwezi hata kidogo, umetuletea miswaki minne... lakini nafsi aikukukubali kabisa. nilikuwa bado najiona mimi ni doctor na moyoni nashudiwa kabisa sayansi naiweza
nilikaachini na almashauri yangu ya kichwa, nikatoa tamko nalisiti masomo manne yote ya sanyansi yani bios, chemia, phys na maths,
nyumbani wakasema wewe huna akili ya kusoma masomo ya sayansi kasome cozi yoyote kwa D zako za arts lakini sio kulisiti, humna uwezo na sayansi na niliambiwa kama utaki kusoma cozi za arts kaa nyumbani saidia kazi na swala la kusoma lifute kwenye maisha yako
niligoma kuchuku ushauri wa cozi za arts hadi bi mkubwa akasema weww utakuwa na maisha ya shida sana, kwa jinsi alivokuwa anaongea nilihisi hii itakuwa ni laana lakini mwisho nikomaa na malengo yangu kulisit
nikaanza halakati za kulisiti msuli mnene nyumbani masomo manne yote ya sayansi nilikuwa nasoma usiku nilisoma kwa interest sana haya masomo na nilikuwa naelewa sana, nasoma mpaka mama alikuwa akanza kuelewa kuwa nipo serious
cha ajabu siku namuomba mama ela ya kulipia masomo ya kulisiti necta akagoma kunipa kabisa yani lakin mimi nilikua naendelea na kusoma tena usiku mnene, zikabaki siku tatu usajili naecta kufungwa na mama ajanipa hela nakumbuka niilingia chumbani kwa mama mw
mweyewe nikachukua kama laki na nusu kwenye mkoba wake nikaenda kulipia kituo cha kufanyia mtihani kimya kimya lisiti nikatulia nazo
mama alikuwa anashangaa tu! hela ajatoa mtu anakomaa kusoma usiku, hadi siku ya mtihani inafika asubuhi sisemi naenda wapi mpaka namaliza mitihani yote mama akujua kitu
wakaiti nasubiri matokeo ya kulisit siku mama akawa analalama kuna mtu kaiba hela yake na mimi nikajitokeza kuw ndo mimi nilichukua nikamuonesha na lisiti za kulipia pepa akagomba lakini mwisho akatulia
matokeo yanatoka nikapiga B B chemia, bios, phys maths nikapiga C
A- level nikachukua PCB, msuli wa PCB si kitoto lakini Mungu hakuniacha nikapiga one ya tisa, sasa nivyoandika hapa mimi ni doctor na mama ananikubali sana jembe lake kwa misimamo yangu
masomo ya sayansi sio magumu kama ukiwa unayasoma kwa kuyakubali kutoka moyoni. wanasema kama unataka kujua kitu kipende kwanza alafu kifanye kwa mapendo yote, lazima ukiweze tu

NOTE: kama unaamini unaweza kufanya jambo lolote ata kama linaonekana ni la kichizi kwa kiasi gani wewe endelea kuamini na onesha juhudi kwenye jambo lako hakika utafanikiwa tu
 

Mkuu yupo na moyo wa kusoma hiyo combination anao lakini itapendeza mbinu ukaziweka hapa ili ziwasaidie na wengine pia.
Natanguliza shukrani
 
Ahsante kw ushuhuda, mkumbuke Mungu wako ndo alokuwezesha yote na akakusamehe ukibaka wa hela za mama, usirudie tena
 
Wewe mchokozi, mfupi anatamani urefu 80/
 
Aisee...kipind nipo o-level nilikuwa na mapenzi na PCM lkn nilibadili gear hewani nikaenda zangu PCB huku basic mathematics naijua ipasavyo.....

Kuifaham basic mathematics kulinisaidia kuweza kusolve maswal ya Physics hakika kwangu physics nilikuwa chai kwangu....pia mapenz yangu ya mathematics kuliniboost kuiweza BAM...

Huyu chemistry tulikuwa tunaita kamastarehe....biology skupata SHIDA kuikariri maana hapo ni mwendo Wa kukariri tu BS....

Kwangu mim niliamin kuwa PCB wengi hawawezi Physics hivyo muda mwingi nilisoma hilo somo.....hakika nilifurahia kusoma physics....

NB: nilikuwa naenda msuli tembo kwenye level zote....mim skuwa na weekend skul....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtabe mmoja wa PCM tulkutana chuo kwenye course ya finance.
Nkawa namuuliza Newton's laws zinakusaidia nini hapa tulipo??

Hadi kesho hajanipa majibu huyu banker wa sasa hivi na pcm wa zamani.
Newton laws hazitokusaidia chochote kama chuo utaenda kusoma coz ambazo hazihusiani na science.

Watu wa engineering wana apply hivi vitu kwenye kazi zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilisoma PCM sababu Kiswahili kilinikataa kabisa hasa fasihi. Na history kuandika mavitu marefu na mimi mwandiko wangu mdogo. Chuo sikusoma engineering japo natamani nirudi nikasome Civil.


Sent using Jamii Forums mobile app
Karibu civil,ukirudi kusoma unitafute nikupige pindi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sifa za kusoma PCB na PCM zinaishia chuoni tu.. Huku mitaani ni habari nyingine kabisa!!!! By the time unaingia mitaani na MD yako au BSc (Mechanical/electrical Eng. etc) unawakuta madogo uliokuwa umewaacha O level na A level na FOUR zao ndio wanaotamba mitaani. Wengine wana biashara kubwa sana na wamejenga na kuendesha magari ya kifahari wakati wewe ndo kwanza unatembea kwa miguu mitaani na bahasha mkononi. Mwanzoni unakuwa smart baadaye u-smart wala hutajua umeudondoshea wapi!!!! Utakuwa unaitwa kwenye interview nafasi moja mnaigombania watu kama mia moja!!! Baadaye hata steam ya kuhudhuria interview inakata!!!! Madokta wengi wananyonywa kwenye hospitali za binafsi kwa ujira kiduchu lakini kwa kazi hatarishi kwa afya zao na masaa mengi ya kazi!!!! Hapo ndo utajua ujanja ni kupata au ujanja ni kutangulia!!!!! ni hayo tu!!!
 
Mida hiyo ya saa 11-12 nilikuwa napumzika kama wewe na pia nilikuwa nautumia muda huu vizuri kuwahi msosi jikoni ili nichukue toplayer..toplayer ni habari nyingine kabisa shuleni..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo unashauri watu wasiende advance au kusoma kabisa??..watu waishie form four then kila mtu afungue biashara??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vip indetermite sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…