Form 4 mwenye ndoto za kusomea IT usipoteze mda wako kwenda form 6, nimekupa ramani nzima hapa

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,026
๐™๐™Š๐™๐™ˆ 4 ๐™ˆ๐™’๐™€๐™‰๐™”๐™€ ๐™‰๐˜ฟ๐™Š๐™๐™Š ๐™•๐˜ผ ๐™†๐™๐™Ž๐™Š๐™ˆ๐™€๐˜ผ ๐™„๐™ ๐™๐™Ž๐™„๐™‹๐™Š๐™๐™€๐™•๐™€ ๐™ˆ๐˜ฟ๐˜ผ ๐™’๐˜ผ๐™†๐™Š ๐™†๐™’๐™€๐™‰๐˜ฟ๐˜ผ ๐™๐™Š๐™๐™ˆ 6, ๐™‰๐™„๐™ˆ๐™€๐™†๐™๐˜พ๐™ƒ๐™Š๐™๐™€๐˜ผ ๐™๐˜ผ๐™ˆ๐˜ผ๐™‰๐™„ ๐™‰๐™•๐™„๐™ˆ๐˜ผ ๐™ƒ๐˜ผ๐™‹๐˜ผ

Muhimu; Kama una changamoto za kiuchumi ni vyema ukasome form 6 kwenye shule ya serikali uliyochaguliwa ili umalize form 6 na ujaribu bahati yako kuomba mkopo wa serikali ili usome chuo, Post hii nawalenga wale ambao wana uwezo wa kulipia ada za chuo ambazo zina range kuanzia laki 9 hadi milioni 1.3, shule nyingi za private ada ni milioni 2 na kitu, kama unaweza lipia hizo shule basi ni wazi unaweza kuchagua kusoma chuo

๐€) ๐‰๐„, ๐ฆ๐ก๐ข๐ญ๐ข๐ฆ๐ฎ ๐ฐ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ’ ๐š๐ง๐š๐š๐ง๐ณ๐ข๐š ๐ฅ๐ž๐ฏ๐ž๐ฅ ๐ข๐ฉ๐ข ๐ง๐š ๐ข๐ง๐š๐œ๐ก๐ฎ๐ค๐ฎ๐š ๐ฆ๐ข๐š๐ค๐š ๐ฆ๐ข๐ง๐ ๐š๐ฉ๐ข ๐ก๐š๐๐ข ๐š๐ฆ๐š๐ฅ๐ข๐ณ๐ž ๐๐ž๐ ๐ซ๐ž๐ž?

Utaanzia certificate, kiingilio ni kuwa na D nne, (D mojawapo iwe angalau ya hesabu)

Cerificate utasoma mwaka 1
Diploma utasoma Miaka 2
Degree utasoma Miaka 3 au 4

Katika kila hatua unapomaliza unapewa cheti cha kungilia hatua inayofata

๐) ๐‰๐„, ๐ฆ๐ญ๐ฎ ๐š๐ฅ๐ข๐ž๐ฆ๐š๐ฅ๐ข๐ณ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ” ๐š๐ง๐š๐š๐ง๐ณ๐ข๐š ๐ฅ๐ž๐ฏ๐ž๐ฅ ๐ข๐ฉ๐ข
Mtu aliemaliza form 6 ataanzia ngazi ya degree na kuisoma kwa miaka 3 au 4, hatapitia certificate na Diploma

๐‚) ๐Š๐ฐ๐š๐ง๐ข๐ง๐ข ๐ฎ๐ž๐ง๐๐ž ๐œ๐ก๐ฎ๐จ ๐›๐š๐š๐๐š ๐ฒ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ’??

- Form 6 hakuna kozi ya iliyojikita kwenye directly kwenye IT ila ukienda chuo utapata nafasi ya kusomea kozi zinazohusu IT, form 6 kuna kombi za pcm, pgm, pcb, cbg n.k hazifikii hata theluthi kwa kinachofundishwa kwenye IT au computer science, kuna kozi mpya imeanzishwa ya phiysics, chemistry na computer lakini kiukweli bado huu sio mbadala, Na ndio maana wenzetu Kenya mtu akimaliza tu form 4 anaenda chuo, Waliifuta form 5 na 6.

- Mtu wa form 6 atasomea elimu ya IT kwa miaka 3 au 4 na atakuwa na cheti cha degree pekee ila Mtu alieunga chuo baada ya form 4 atasomea IT miaka 6 au 7 na atakua na vyeti vya certificate, Diploma na Degree, hivi vyeti vinahusiana moja kwa moja na IT tofauti na vyeti vya form 6 vya pcm, pcb, pgm, n.k.

- Form 6 huwezi kupata ajira ila kwa mtu mwenye diploma anaweza kuajiriwa, ukimaliza diploma yako una sifa za kuajirika tayari, Pia mkikutana huko degree na waliomaliza form 6, yule wa form 6 akishindwa kumaliza chuo basi atabaki na cheti cha form 6 ambacho haajiriki ila mwenye cheti cha diploma hata akishindwa kumaliza degree anaweza kuajirika kwa diploma yake, Licha ya hivyo kuna kazi ambazo zinahitaji mtu awe na diploma na sio degree, Hapa mwenye cheti cha degree pekee hawezi kupewa hii kazi, ila mwenye cheti cha diploma nadegree anaweza kutumia cheti chake cha Diploma kupewa kazi,

- Kwenda field ni kufanya kazi kwa vitendo kwenye mashirika / Taasisi za serikali au private mfano TRA, Halmashauri, Bandarini, Tanroads, n.k hili ni somo la lazima chuoni na linajenga mwanafunzi kupata uzoefu nje ya darasani, Ukianza certificate utafanya field, ukiingia diploma utafanya field na ukiingia degree kuna field, Hii ni advantage kwa mtu aliemaliza form 4 na kwenda chuo, Kwa mtu alieingia degree kwa form 6 ataifanya mara 1 tu huku mwenzake itakuwa ni mara ya 3.

๐ƒ) ๐‰๐„, ๐ง๐ข๐ฌ๐จ๐ฆ๐ž ๐œ๐ก๐ฎ๐จ ๐ ๐š๐ง๐ข?

Kundi A - vyuo vya nje - Wenye uwezo nawasihi sana msipoteze mudahapa nchini, Kama nyumbani mambo yapo vizuri sioni sababu ya wewe kung'ang'ania kusomea hapa nchini, kama hauna uwezo unaweza kupata scholarship kupitia mitihani ya SAT pale ubalozi wa marekani na mimi ni shahidi, kuna dogo namjua anasomeshwa uturuki, Nenda ubalozi wa marekani kaulizie mitihani ya SAT, Kiingilio huwa ni dola 64 ambayo haizidi laki na nusu ya pesa yetu, hapoinabidi uwe tayari umeanza form 5 na ukipata hio scholarship huna haja ya kumaliza form 6, Vito vya mitihani huwa ni International school of Tanganyika, Dar International Academy, n.k Mtihani ujao unafanyika November, Tembelea hapa kujua vituo vya kufanyia pepa na tarehe >> Find SAT Test Centers

Kundi B - UDSM - Kwa upande wa UDSM hakuna mtu asiejua kwamba udsm ndio chuo baba kwa Tanzania, Maprofesa, Viongozi wa taasisi, wakurugenzi, Mawaziri, Researchers, n.k karibu asilimia 90 wamesomea UDSM, pambana kufa kupona usomee hapa, cheti pekee bila hata kujali ufaulu kinaweza kuku boost kupata ajira, cheo, n.k

Kundi C.Vyuo specific kwajili ya IT - Hivi ni vyuo vimejikita zaidi kwenye elimu ya fani flani, kwenye Sayansi na Teknolojia kuna vyuo vyake kama DIT, MUST, Arusha Tech, n.k Ni vyuo vizuri maana vimejikita zaidi kwenye texhnology na ukisomea IT inakuwa relevant, Ila natoa onyo kwamba hivi vyuo wamekaza mno elimu zao, Hesabu ni nyingi, Masomo ni mengi, Ratiba zimebana ile, Yaani inahitaji kujitoa mno!! Wanafunzi wengi wa hivi vyuo huwa wanadanganwa na waalim wao kwamba kwakuwa wanakaziwa sana, wanasoma masomo mengi, mitihani migumu, n.k basi wao ndio cream ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Hizo stori huwa zinaishia huko huko vyuoni, hali ya ajira ni tofauti kabisa, Ajira kinachoangaliwa zaidi ni kwamba una cheti, stori imeisha hapo, Mambo ya ulisoma masomo mangapi, mitihani migumu, n.k yanabaki huko huko vyuoni, wanaotaka kwenda vyuo hivi wawe tayari kujitoa maana ukipata ufaulu mdogo unaweza kushindwa kukosa sifa za kusoma masters au kupata scholarship kufadhiliwa kusoma nje ya nchi.

Kundi D. Vyuo vya serikali General - Hivi vyuo vipo kwajili ya kutoa kozi nyingi kwa usawa,Ukiachana na UDSM ambayo nishaitaja kuna UDOM wana taasisi yao inaitwa college of Informatics, Ukikosa hapo nenda Mzumbe nao ni chuo general

Kundi E. Vyuo vya serikali Specific ila indirect - Havina utofauti na kundi C ila hivi ni kwajili ya mambo mengine Mfano kuna IAA hiki ni chuo kipo Arusha kimelenga uhasibu lakini huku kwenye teknolojia hawapo nyuma wana kozi za cyber security, IT, Computer science, kozi za kutengeneza app, Media, n.k, vyuo vingine kuna IFM, Ardhi, TIA, n.k

Kundi F.Private universities - ukikosa kabisa nenda Private, ila kiukweli vyuo vyao vingi vina skendo za kufungiwa fungiwa, walimu wenye sifa ndogo, n.k pia serikali imeweka kipaumbele kwenye wahitimu wa vyuo vyao vya serikali kundi A hadi C..

MUHIMU: Unapoomba ushauri hakikisha kwanza unamuuliza chuo alichosomea anaekupa ushauri, wengi wana tabia ya kusifia sana vyuo walivyosoma mpaka kuvuka mipaka, Kwahio na wewe hapa usiingie mkenge.
 
Nikweli mkuu ila kinachoniuma hata hiyo D 4 form four sikujariwa kuipata ila IT nimeipiga kimtaa mtaa yaani maswala ya. Haxking, trogan horse Network topology, data base na nyingine nyingi hayanipigi chenga ila shida huja kwenye vyeti inapotokea ajira kwenye shirika
 
kama unataka kusoma IT iliyoshiba nenda India.

usije kupoteza mda na hii bongo kwa elimu,hata ukikosa ajira unaweza kujiajili.

india kuna course ambazo bongo zinakuja nje ya mda kabisa.

miaka ya nyuma mtu unasoma oracle 9 wanaosoma india wapo oracle 12 .

tuje upanda wa kozi cisco kuna baazi hapa bongo itabidi usome vyuo fulani ila india kila kona.

kuna course kama microsoft certified india hipo.

mpaka certified course kama google, gsx, AI(artificial intelligence ),Linux, ethical hacking, server, data, software engineering, programming mathematics na n.k


india wapo vizuri !

angalizo india kama unaenda kilaza kitakacho kutokea bora baki bongo
 
Nikweli mkuu ila kinachoniuma hata hiyo D 4 form four sikujariwa kuipata ila IT nimeipiga kimtaa mtaa yaani maswala ya. Haxking, trogan horse Network topology, data base na nyingine nyingi hayanipigi chenga ila shida huja kwenye vyeti inapotokea ajira kwenye shirika
Tafuta Chet umejaribu kuuliza vyuo mbalimbali ujuzi mwingi hasa IT ukiwa seriously unajifunza online kuna YouTube channel nyingi zinafundisha for free. Ila utayari wakujifunza ndio shida

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
kama unataka kusoma IT iliyoshiba nenda India.

usije kupoteza mda na hii bongo kwa elimu,hata ukikosa ajira unaweza kujiajili.

india kuna course ambazo bongo zinakuja nje ya mda kabisa.

miaka ya nyuma mtu unasoma oracle 9 wanaosoma india wapo oracle 12 .

tuje upanda wa kozi cisco kuna baazi hapa bongo itabidi usome vyuo fulani ila india kila kona.

kuna course kama microsoft certified india hipo.

mpaka certified course kama google, gsx, AI(artificial intelligence ),Linux, ethical hacking, server, data, software engineering, programming mathematics na n.k


india wapo vizuri !

angalizo india kama unaenda kilaza kitakacho kutokea bora baki bongo
Nako huko india kunategemeana na chuo ulichoenda kusoma pamoja na bidii yako, kuna vyuo huko india havitambuliki hata na TCU, ukimaliza huko hicho cheti huwezi tumia huku kuombea ajira
 
kama unataka kusoma IT iliyoshiba nenda India.

usije kupoteza mda na hii bongo kwa elimu,hata ukikosa ajira unaweza kujiajili.

india kuna course ambazo bongo zinakuja nje ya mda kabisa.

miaka ya nyuma mtu unasoma oracle 9 wanaosoma india wapo oracle 12 .

tuje upanda wa kozi cisco kuna baazi hapa bongo itabidi usome vyuo fulani ila india kila kona.

kuna course kama microsoft certified india hipo.

mpaka certified course kama google, gsx, AI(artificial intelligence ),Linux, ethical hacking, server, data, software engineering, programming mathematics na n.k


india wapo vizuri !

angalizo india kama unaenda kilaza kitakacho kutokea bora baki bongo
Kwamba Ku Disco ni saa tatu asubuhi?
 
Hiyo
๐™๐™Š๐™๐™ˆ 4 ๐™ˆ๐™’๐™€๐™‰๐™”๐™€ ๐™‰๐˜ฟ๐™Š๐™๐™Š ๐™•๐˜ผ ๐™†๐™๐™Ž๐™Š๐™ˆ๐™€๐˜ผ ๐™„๐™ ๐™๐™Ž๐™„๐™‹๐™Š๐™๐™€๐™•๐™€ ๐™ˆ๐˜ฟ๐˜ผ ๐™’๐˜ผ๐™†๐™Š ๐™†๐™’๐™€๐™‰๐˜ฟ๐˜ผ ๐™๐™Š๐™๐™ˆ 6, ๐™‰๐™„๐™ˆ๐™€๐™†๐™๐˜พ๐™ƒ๐™Š๐™๐™€๐˜ผ ๐™๐˜ผ๐™ˆ๐˜ผ๐™‰๐™„ ๐™‰๐™•๐™„๐™ˆ๐˜ผ ๐™ƒ๐˜ผ๐™‹๐˜ผ

Muhimu; Kama una changamoto za kiuchumi ni vyema ukasome form 6 kwenye shule ya serikali uliyochaguliwa ili umalize form 6 na ujaribu bahati yako kuomba mkopo wa serikali ili usome chuo, Post hii nawalenga wale ambao wana uwezo wa kulipia ada za chuo ambazo zina range kuanzia laki 9 hadi milioni 1.3, shule nyingi za private ada ni milioni 2 na kitu, kama unaweza lipia hizo shule basi ni wazi unaweza kuchagua kusoma chuo

๐€) ๐‰๐„, ๐ฆ๐ก๐ข๐ญ๐ข๐ฆ๐ฎ ๐ฐ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ’ ๐š๐ง๐š๐š๐ง๐ณ๐ข๐š ๐ฅ๐ž๐ฏ๐ž๐ฅ ๐ข๐ฉ๐ข ๐ง๐š ๐ข๐ง๐š๐œ๐ก๐ฎ๐ค๐ฎ๐š ๐ฆ๐ข๐š๐ค๐š ๐ฆ๐ข๐ง๐ ๐š๐ฉ๐ข ๐ก๐š๐๐ข ๐š๐ฆ๐š๐ฅ๐ข๐ณ๐ž ๐๐ž๐ ๐ซ๐ž๐ž?

Utaanzia certificate, kiingilio ni kuwa na D nne, (D mojawapo iwe angalau ya hesabu)

Cerificate utasoma mwaka 1
Diploma utasoma Miaka 2
Degree utasoma Miaka 3 au 4

Katika kila hatua unapomaliza unapewa cheti cha kungilia hatua inayofata

๐) ๐‰๐„, ๐ฆ๐ญ๐ฎ ๐š๐ฅ๐ข๐ž๐ฆ๐š๐ฅ๐ข๐ณ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ” ๐š๐ง๐š๐š๐ง๐ณ๐ข๐š ๐ฅ๐ž๐ฏ๐ž๐ฅ ๐ข๐ฉ๐ข
Mtu aliemaliza form 6 ataanzia ngazi ya degree na kuisoma kwa miaka 3 au 4, hatapitia certificate na Diploma

๐‚) ๐Š๐ฐ๐š๐ง๐ข๐ง๐ข ๐ฎ๐ž๐ง๐๐ž ๐œ๐ก๐ฎ๐จ ๐›๐š๐š๐๐š ๐ฒ๐š ๐Ÿ๐จ๐ซ๐ฆ ๐Ÿ’??

- Form 6 hakuna kozi ya iliyojikita kwenye directly kwenye IT ila ukienda chuo utapata nafasi ya kusomea kozi zinazohusu IT, form 6 kuna kombi za pcm, pgm, pcb, cbg n.k hazifikii hata theluthi kwa kinachofundishwa kwenye IT au computer science, kuna kozi mpya imeanzishwa ya phiysics, chemistry na computer lakini kiukweli bado huu sio mbadala, Na ndio maana wenzetu Kenya mtu akimaliza tu form 4 anaenda chuo, Waliifuta form 5 na 6.

- Mtu wa form 6 atasomea elimu ya IT kwa miaka 3 au 4 na atakuwa na cheti cha degree pekee ila Mtu alieunga chuo baada ya form 4 atasomea IT miaka 6 au 7 na atakua na vyeti vya certificate, Diploma na Degree, hivi vyeti vinahusiana moja kwa moja na IT tofauti na vyeti vya form 6 vya pcm, pcb, pgm, n.k.

- Form 6 huwezi kupata ajira ila kwa mtu mwenye diploma anaweza kuajiriwa, ukimaliza diploma yako una sifa za kuajirika tayari, Pia mkikutana huko degree na waliomaliza form 6, yule wa form 6 akishindwa kumaliza chuo basi atabaki na cheti cha form 6 ambacho haajiriki ila mwenye cheti cha diploma hata akishindwa kumaliza degree anaweza kuajirika kwa diploma yake, Licha ya hivyo kuna kazi ambazo zinahitaji mtu awe na diploma na sio degree, Hapa mwenye cheti cha degree pekee hawezi kupewa hii kazi, ila mwenye cheti cha diploma nadegree anaweza kutumia cheti chake cha Diploma kupewa kazi,

- Kwenda field ni kufanya kazi kwa vitendo kwenye mashirika / Taasisi za serikali au private mfano TRA, Halmashauri, Bandarini, Tanroads, n.k hili ni somo la lazima chuoni na linajenga mwanafunzi kupata uzoefu nje ya darasani, Ukianza certificate utafanya field, ukiingia diploma utafanya field na ukiingia degree kuna field, Hii ni advantage kwa mtu aliemaliza form 4 na kwenda chuo, Kwa mtu alieingia degree kwa form 6 ataifanya mara 1 tu huku mwenzake itakuwa ni mara ya 3.

๐ƒ) ๐‰๐„, ๐ง๐ข๐ฌ๐จ๐ฆ๐ž ๐œ๐ก๐ฎ๐จ ๐ ๐š๐ง๐ข?

Kundi A - vyuo vya nje - Wenye uwezo nawasihi sana msipoteze mudahapa nchini, Kama nyumbani mambo yapo vizuri sioni sababu ya wewe kung'ang'ania kusomea hapa nchini, kama hauna uwezo unaweza kupata scholarship kupitia mitihani ya SAT pale ubalozi wa marekani na mimi ni shahidi, kuna dogo namjua anasomeshwa uturuki, Nenda ubalozi wa marekani kaulizie mitihani ya SAT, Kiingilio huwa ni dola 64 ambayo haizidi laki na nusu ya pesa yetu, hapoinabidi uwe tayari umeanza form 5 na ukipata hio scholarship huna haja ya kumaliza form 6, Vito vya mitihani huwa ni International school of Tanganyika, Dar International Academy, n.k Mtihani ujao unafanyika November, Tembelea hapa kujua vituo vya kufanyia pepa na tarehe >> Find SAT Test Centers

Kundi B - UDSM - Kwa upande wa UDSM hakuna mtu asiejua kwamba udsm ndio chuo baba kwa Tanzania, Maprofesa, Viongozi wa taasisi, wakurugenzi, Mawaziri, Researchers, n.k karibu asilimia 90 wamesomea UDSM, pambana kufa kupona usomee hapa, cheti pekee bila hata kujali ufaulu kinaweza kuku boost kupata ajira, cheo, n.k

Kundi C.Vyuo specific kwajili ya IT - Hivi ni vyuo vimejikita zaidi kwenye elimu ya fani flani, kwenye Sayansi na Teknolojia kuna vyuo vyake kama DIT, MUST, Arusha Tech, n.k Ni vyuo vizuri maana vimejikita zaidi kwenye texhnology na ukisomea IT inakuwa relevant, Ila natoa onyo kwamba hivi vyuo wamekaza mno elimu zao, Hesabu ni nyingi, Masomo ni mengi, Ratiba zimebana ile, Yaani inahitaji kujitoa mno!! Wanafunzi wengi wa hivi vyuo huwa wanadanganwa na waalim wao kwamba kwakuwa wanakaziwa sana, wanasoma masomo mengi, mitihani migumu, n.k basi wao ndio cream ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Hizo stori huwa zinaishia huko huko vyuoni, hali ya ajira ni tofauti kabisa, Ajira kinachoangaliwa zaidi ni kwamba una cheti, stori imeisha hapo, Mambo ya ulisoma masomo mangapi, mitihani migumu, n.k yanabaki huko huko vyuoni, wanaotaka kwenda vyuo hivi wawe tayari kujitoa maana ukipata ufaulu mdogo unaweza kushindwa kukosa sifa za kusoma masters au kupata scholarship kufadhiliwa kusoma nje ya nchi.

Kundi D. Vyuo vya serikali General - Hivi vyuo vipo kwajili ya kutoa kozi nyingi kwa usawa,Ukiachana na UDSM ambayo nishaitaja kuna UDOM wana taasisi yao inaitwa college of Informatics, Ukikosa hapo nenda Mzumbe nao ni chuo general

Kundi E. Vyuo vya serikali Specific ila indirect - Havina utofauti na kundi C ila hivi ni kwajili ya mambo mengine Mfano kuna IAA hiki ni chuo kipo Arusha kimelenga uhasibu lakini huku kwenye teknolojia hawapo nyuma wana kozi za cyber security, IT, Computer science, kozi za kutengeneza app, Media, n.k, vyuo vingine kuna IFM, Ardhi, TIA, n.k

Kundi F.Private universities - ukikosa kabisa nenda Private, ila kiukweli vyuo vyao vingi vina skendo za kufungiwa fungiwa, walimu wenye sifa ndogo, n.k pia serikali imeweka kipaumbele kwenye wahitimu wa vyuo vyao vya serikali kundi A hadi C..

MUHIMU: Unapoomba ushauri hakikisha kwanza unamuuliza chuo alichosomea anaekupa ushauri, wengi wana tabia ya kusifia sana vyuo walivyosoma mpaka kuvuka mipaka, Kwahio na wewe hapa usiingie mkenge.
SAT unaweza piga ata kama umemaliza form six?
Je pia huwa ni full funded au? sky soldier
Maana kuna dogo apa nimpe fursa
 
Back
Top Bottom