GE2025 Salum Mwalimu apinga madai CHAUMMA kutoshiriki uchaguzi, ashangaa CHADEMA kususa ikiwa wananchi wanahitaji mabadiliko

GE2025 Salum Mwalimu apinga madai CHAUMMA kutoshiriki uchaguzi, ashangaa CHADEMA kususa ikiwa wananchi wanahitaji mabadiliko

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amepinga vikali madai kuwa CHADEMA, wanachama na viongozi wake waliafikiana kususia uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, akisema hakuna kikao rasmi kilichopitisha uamuzi huo, na kuitaka CHADEMA kuweka wazi nyaraka za maamuzi hayo endapo zipo

Akihutubia wananchi wa kata ya Kwediboma wilayani Kilindi mkoani Tanga siku ya Jumapili, Salum Mwalimu amesema kuwa Watanzania wamechoka na utawala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hatua ya kuwaambia wananchi wasishiriki uchaguzi ni sawa na kukabidhi ushindi kwa CCM kwa hiari

Soma Pia: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Salum Mwalimu, ambaye zamani alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Zanzibar), alikosoa vikali msimamo wa CHADEMA wa kupinga ushiriki kwenye uchaguzi, akisema hatua hiyo ni kutokuwa na imani na wananchi wanaotaka mabadiliko kupitia sanduku la kura

Amesema CHAUMMA itaendelea kushiriki uchaguzi kwa nguvu zote kwa kuwa ndiyo njia pekee ya kidemokrasia ya kuleta mabadiliko


 
Kila wasimamapo jukwaani hoja zao ni CDM mara kurusha chopper ajabu sana hiki chama cha sera za ubwabwa
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amepinga vikali madai kuwa CHADEMA, wanachama na viongozi wake waliafikiana kususia uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, akisema hakuna kikao rasmi kilichopitisha uamuzi huo, na kuitaka CHADEMA kuweka wazi nyaraka za maamuzi hayo endapo zipo

Akihutubia wananchi wa kata ya Kwediboma wilayani Kilindi mkoani Tanga siku ya Jumapili, Salum Mwalimu amesema kuwa Watanzania wamechoka na utawala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hatua ya kuwaambia wananchi wasishiriki uchaguzi ni sawa na kukabidhi ushindi kwa CCM kwa hiari

Salum Mwalimu, ambaye zamani alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Zanzibar), alikosoa vikali msimamo wa CHADEMA wa kupinga ushiriki kwenye uchaguzi, akisema hatua hiyo ni kutokuwa na imani na wananchi wanaotaka mabadiliko kupitia sanduku la kura

Amesema CHAUMMA itaendelea kushiriki uchaguzi kwa nguvu zote kwa kuwa ndiyo njia pekee ya kidemokrasia ya kuleta mabadiliko


Huyu mpumbavu kweli kweli badala ya kuikabili CCM yeye kila siku anapambana na Chadema.
 
CHAUMMA ipambane na CCM. Salum Mwalimu auze na kunadi sera za chama chake aachane na CHADEMA.
 
Aache kupambana na CDM, apambanie chama chake CHAUMMA na vita yakuitoa CCM madaraka pamoja na kunadi sera zao vs chama tawala kilichotawala zaidi ya miaka 50 na kushindwa kutokomeza umasikini ndani ya jamii.

Uelekeo Fallujah - Iraq.
 
Salum, huenda anaumwa. Ndiyo maana haelewi hata anashindana na nani. Na baada ya huo ushetani, atakapoona hajapata hata alichoahidiwa na CCM ataenda kuilaumu CDM kuwa ndiyo imesababisha!!
 
Hivi mlitaka asijibu uongo na uzushi wa CDM ambao ulirudiwa na aliyemhoji? Kama kulikuwa na makubaliano ya kutoshiriki si wamuumbue tu kwa kujaweka hadharani?

Amandla...
 
katumia neno "chama kikubwa"
 
IMG_20250714_235942.jpg
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amepinga vikali madai kuwa CHADEMA, wanachama na viongozi wake waliafikiana kususia uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, akisema hakuna kikao rasmi kilichopitisha uamuzi huo, na kuitaka CHADEMA kuweka wazi nyaraka za maamuzi hayo endapo zipo

Akihutubia wananchi wa kata ya Kwediboma wilayani Kilindi mkoani Tanga siku ya Jumapili, Salum Mwalimu amesema kuwa Watanzania wamechoka na utawala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hatua ya kuwaambia wananchi wasishiriki uchaguzi ni sawa na kukabidhi ushindi kwa CCM kwa hiari

Soma Pia: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Salum Mwalimu, ambaye zamani alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Zanzibar), alikosoa vikali msimamo wa CHADEMA wa kupinga ushiriki kwenye uchaguzi, akisema hatua hiyo ni kutokuwa na imani na wananchi wanaotaka mabadiliko kupitia sanduku la kura

Amesema CHAUMMA itaendelea kushiriki uchaguzi kwa nguvu zote kwa kuwa ndiyo njia pekee ya kidemokrasia ya kuleta mabadiliko


Unaipigia promo maiti.
 
Back
Top Bottom