Salamu za wiki kwa ZITTO NA LEMA

Salamu za wiki kwa ZITTO NA LEMA

Kwenye hili Lema alipaswa kuambiwa kweli, kwamba yeye ni mtu mzima awe anatafakari kabla ya kulopoka hovyo, huwezi kumlipua Zitto, Mbowe au Dr Slaa bila kuiathiri Chadema. Lema amejisahau sana anaendesha siasa za kupumbaza vijana aonekane ana hoja za msingi wakati kiukweli anataka maslahi binafsi, Lema usidhani kila mtu ni kijana wako wengine tumeanza mbali nahiki chama ukikivuruga na tukajua source ni wewe utatafuta namna ya kutujibu

unajua kuna watu wanafikiri kwenye hili kutakuwa na mshindi kumbe wana sahau kujiuliza atakaye shindwa atashindwa vipi/

LEMA ANA HITAJI KUAMBIWA UKWELI.
NA KUNBUKA KUNA KIPINDI MBOWE ALIMKEMEA NASSARY LAKINI NA SHANGAA ANA SHINDWA KUMWANBIA LEMA APUNGUZE NIHEMKO YA KISIASA.

NA HIKI NI KIPIMO CHA MBOWE? LEMA NI NANI ASIAMBIWE

LEMA ANAHITAJI KUKEMEWA TUU.

MBOWE NA KUSUBIRI KWENYE HILI.
 
CDM inamadaraja,watu wa kanda yao ya kaskazini wanathamani zaidi ya kanda nyingine.
 
Albert ana wambia wenzie wajiulize kuwa ni watanzania wangapi wanatumia fb?

Anaendelea kuwauliza ni watanzania wangapi watajua ukweli na uongo wao?

Hapo albert kaonesha dharau kwa mitandao na pengine alitamani lema aitishe vyombo vya habari.

Albert anakubaliana na alicho fanya lema kakini alitamani atumie njia itakayo wezesha watanzania wote kujua tuhuma za lema dhidi ya naibu katibu mkuu.

Albert ni mnafiki kajificha kwenye maneno lakini anaumbuka kuwa ni mnafiki ana mlinda lema.

Albert bado anataka lema aendelee kubandika humu makala akiamini kuna mshindi ndio maana amesema lazima muongo na mkweli ajulukane, kifupi amependezwa na reaction ya lema.

Albert anatakiwa kufahamu katika haya malumbano hakutakuwa na mshindi bali ni kurudisha nyuma chama.

Albert acha unafiki ni heri unge kaa kimya.
hapo nilipo bold na wewe umeshaonyesha unafiki wako kabisa kuwa tangu mwanzo wa hili swaga upo upande gani, wewe ni zittofobia, kwa hiyo wewe hupendi ukweli na uongo ujulikane? mkuu jitafakari....
 
Nimemwelewa mtoa hoja,anaonyesha jinsi lema anavyoongozwa na jazba ktk kufanya mambo.na hii ni kitokana na historia yake,
Lema hana tofauti na mlema Augostino.ni mtu wa kuhamahama vyama na kila chama anaacha amenyea kambi. CCM,NCCR,TLP,na sasa CHADEMA. naamini anauzoefu wa usaliti katika vyama.endeleeni kumshangilia msubiri matokeo yake.
 
Albert Msando

Wewe ni rafiki yangu tunafahamiana muda sasa umenistua uliposema tatizo siyo posho kuna kitu nyuma.

Mkuu kama umeamua kufunguka tuambie tatizo ni nini.

Kumbe kelele za posho ni uongo.

Majanga.
 
Last edited by a moderator:
ASANTE KWA KUWEKA WAZI KUWA LEMA KAPOTOKA JAPO MWANZO ULIJICHANGANYA.

KAMA HUWEZI ZUNGUMZIA SWALA LA MWIGAMBA UNAZUNGUMZIAJE SWALA LA LEMA?

KWANINI USISEME WAZI MWIGAMBA ALIKOSEA AU ALIONEWA?UONI UNAJICHANGANYA TENA?

INA MAANA UNAJARIBU KUSEMA UJUI KANUNI ZA CHAMA?HEBU TWAMBIE KANUNI ZINA SEMAJE KWENYE HILI SWALA?

KAMA NJIA ILIYOTUMIWA NA LEMA SI SAHIHI KWA NINI UNAKOSA MSIMAMO KWENYE SWALA LA MWIGAMBA?

UNAJUA HAPA UWEZI KUWA HAKIMU MZURI MAANA UJUI LIPI NI KOSA NA LIPI SI KOSA.

MsandoAlberto unajichanganya jaribu kupitia bandiko lako na maswali yangu uone ulivyo kosa msimamo thabiti.
hapo umemuwekea MsandoAlberto maneno mdomoni, ni wapi kasema Lema kapotoka?
 
Last edited by a moderator:
Ni mtu mpuuzi pekee atakae endelea kumtetea mtu anaepigania posho wakati mwanzo alijifanya kuwa yeye ni mtetezi wa wanyonge.tumwache mtu anaefanya mambo kwa vitendo ,mzalendo wa kweli na mfano bora wakuigwa kwa maslahi ya taifa.
 
ASANTE KWA KUWEKA WAZI KUWA LEMA KAPOTOKA JAPO MWANZO ULIJICHANGANYA.

KAMA HUWEZI ZUNGUMZIA SWALA LA MWIGAMBA UNAZUNGUMZIAJE SWALA LA LEMA?

KWANINI USISEME WAZI MWIGAMBA ALIKOSEA AU ALIONEWA?UONI UNAJICHANGANYA TENA?

INA MAANA UNAJARIBU KUSEMA UJUI KANUNI ZA CHAMA?HEBU TWAMBIE KANUNI ZINA SEMAJE KWENYE HILI SWALA?

KAMA NJIA ILIYOTUMIWA NA LEMA SI SAHIHI KWA NINI UNAKOSA MSIMAMO KWENYE SWALA LA MWIGAMBA?

UNAJUA HAPA UWEZI KUWA HAKIMU MZURI MAANA UJUI LIPI NI KOSA NA LIPI SI KOSA.

MsandoAlberto unajichanganya jaribu kupitia bandiko lako na maswali yangu uone ulivyo kosa msimamo thabiti.

tatizo lako sijui kuna vita ya kimaslahi kati yako na Albert ndiyo maana ukakurupuka na maneno makali.

Elewa point ya hakuna uwoga, bali kinachotakiwa hapa ni Mnafiki ni nani na Mwongo ni nani, na point ya kusema watu wajue ulielewa watajulia wapi?

Acha ushabiki wa u-ccm mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Salaam Zitto na Lema...

Tatizo lenu sio posho. Si vyema kuwadanganya watu au kuwaaminisha kwamba tofauti iliyopo kati yenu ni mawazo au misimamo tofauti kuhusu Posho.

Kama ingekuwa hivyo basi isingekuwa tatizo. Kuwa na mawazo au misimamo tofauti sio tatizo hata siku moja.

Mtu hauhitaji rocket science kuona kwamba kuna zaidi nyuma ya pazia.

Ila kabla sijasema sana niweke mambo machache wazi.

1. Zitto na Lema ni marafiki zangu. Nawafahamu wote kiasi cha kuweza kusema kwamba najua uwezo wa kila mmoja wenu.

2. Sioni tatizo kutumia socia media kugombana au kukosoana. Najua wapo ambao wanasema vikao vitumike. Lakini vikao hivyo wengi wetu hatuhudhurii kwa sababu sio wajumbe. Yatokanayo na vikao hivyo hubaki siri na tunayoletewa ni muhtasari wa vikao. Hatupati nafasi ya kujua nani kasema nini na kwa nini na amesemaje.

3. Chama lazima kikue. Na kukua lazima mambo fulani fulani yatokee. Najua yanaweza yakapitiliza na kuathiri chama ila ni bora yatokee na kuathiri chama kuliko yaje yatokee na kuathiri NCHI. Kama tutavurugana na kugombana chama kikasambaratika basi ni kheri kuliko tuje kufarakana, kuvurugana na kugombana wakati tumepewa madaraka kuongoza watanzania.

Baada ya kuweka hayo mambo matatu wazi niseme kwamba suala la kupokea au kutopokea posho ni suala binafsi sana. Ni suala la NAFSI.

Kama nafsi yako inakutuma upokee posho basi ndio ulivyo. Nafsi hiyo hiyo itakutuma upokee rushwa, useme uongo, ukose maadili nk.

Kama nafsi yako inakutuma ukatae posho basi ndio ulivyo. Nafsi hiyo hiyo itakutuma usipokee rushwa, usiseme uongo, uwe na maadili nk.

Lakini, nafsi pia inaweza kukutuma kuchanganya mazuri na mabaya. Ukapokea posho ukakataa rushwa. Au ukakataa posho ukapokea rushwa. Ni nafsi yako.

Zitto na Lema mjipime kwa kile kilicho ndani ya nafsi zenu. Uzuri ni kwamba mwanadamu huwezi kuidanganya nafsi yako.

Ila kumbukeni yafuatayo;

1. Nyinyi ni vijana ambao mmepewa nafasi za kuongoza wananchi ambao wanawaamini.

2. Nchi yetu inahitaji viongozi ambao ni WAKWELI na WASIO NA TAMAA.

3. Lazima mtofautishe KUJULIKANA na KUWA MAARUFU. Nyie wote mnajulikana. Hamna umaarufu wowote. Sidhani kama mmekuwa viongozi ili muwe maarufu.

4. Mna nafasi kubwa sana kwa vijana kwa sababu ya kujulikana kwenu. Nchi hii itasonga mbele tu kama vijana wataamua kushiriki kikamilifu kwenye siasa. Lakini vijana hawatashiriki ipasavyo kama tutawavuruga na kuwachanganya.

5. Wananchi watapima uongozi wenu sio kwa idadi ya mabandiko FB, tweets au articles. Wananchi hawakuchagua bloggers au waandishi wa articles. Walichagua viongozi wa kuwawakilisha.

Jiulizeni ni watanzania wangapi wako FB na Jamii Forum? Kwa nini idadi yao ni hiyo!? Ukweli wenu au uongo wenu unawafikia?!

Nimesoma andiko la Lema. Limejaa hasira, jazba na kiasi fulani chuki. Nimesoma majibu ya Zitto. Yamejaa kujiamini, kupuuzia na kiasi fulani dharau. Nawajua jinsi mlivyo kwa hiyo sishangai na wala hainikeri.

Lakini mwisho wa siku najua itakavyokuwa. Ukweli utajulikana. Kuna mmoja atabaki mwingine atatwaliwa. Kuna mmoja historia yake itakuwa ni kufundishia mwingine itakuwa kwa ajili ya kukemea. Kwa mlipofikia sasa lazima tujue nani Muongo nani Mkweli.

Kwa sababu mmeamua kufulia nguo kisimani basi zianikeni tuone madoa na usafi wake. Hatutarajii mrudishe kwenye tenga mkaanikie nyumbani.

NB:

Kila mmoja wenu kwa nafasi yake awajulishe watanzania amefanya nini kama Mbunge na Kiongozi wa chama. Kwenye mambo haya;

1. Elimu

2. Afya

3. Ajira

4. Uwajibikaji.

Hayo tu manne. Sitegemei mtatuangusha katika hili. Mkishatoa taarifa zenu basi tutaamua kama mpokee au msipokee posho. Tutatoa msimamo wetu pia.


Tatizo la Zitto ni unafiki, hauhitaji hata kuakaaanae, huyu jamaa ni mnafiki tena sana. Huwa anaangaika sana kujenga hoja ili apate kundi la kumsapoti yeye na nafsi yake, sio wewe Msando.

Nenda kasikie speech zote na hoja zote za Zitto, sikia hoja zote za Lema, alafu utafakari.

Zitto ana madharau, ana makidai, anajifanya mjuaji kuliko mtu yeyote ndani ya cdm. Huyu dawa yake ni hiyo Lema aliyo mpatia. Akiropoka tu, anapewa dozi nyingi.

Wewe Msando, do you find anything novel or any new idea ambayo ni practical from Zitto? He is an economist, physicist, physician, mathematician, politician, everything etc. The guy think he knows everything na degree yake ya political science!! Bull shit!! Kumbe ndo kiongozi wa wasaliti. Na mkiendelea kumwendekeza, nina wahakikishia, cdm itakufa. Unajua itakufaje? Haitakufa kwa kupoteza wanachama au washabiki. Itakufa kwa kupoteza Wafadhili.
 
Huwezi kuwa Chadema kaskazini ukatamka hadharani kuwa Lema anafanya makosa,MsandoAlberto anajaribu kujitutumua lakini anashindwa kuweka bayana tatizo.
 
Rutta, Mwigamba alifanya nini kati ya haya?
1. Kuandika habari JF bila kuwaambia wengine

2. Kutokutumia vikao kusema yale anayoona ni matatizo chamani?

Kumbuka yeye ni mjumbe wa vikao vya chama kaka. Sio kama mimi na wewe ambao ni wajumbe wa JF. Labda ndio maana akahukumiwa haraka haraka. Ila kama alisema ukweli kuhusu Mbowe au mtu mwingine yeyote basi yuko sahihi. Na asipewe adhabu kwa kusema ukweli hata kama unauma na unawagusa wale tunaowapenda.

Kuna kitu kimoja kwenye Sheria, ushahidi ni ushahidi hata kama umepatikana katika mazingira vunjifu ya Sheria. Nasema ukweli ni ukweli hata kama umetolewa katika njia ambayo sio sahihi.

Mwigamba kakosea njia ya kusema kile anachoamini ni ukweli lakini hajakosea kukisema. Sasa tunakijua na hilo ndilo la msingi. Waliosemwa watoe maelezo tofauti na kumpinga kwamba kasemea nje ya vikao lakini hatua pia zichukuliwe kwa yeye kukiuka utaratibu kama upo. Ni rahisi sana mbona?

Zitto na Lema wamesemana na sasa tunajua walichokisema. Njia ya kusemea sio sahihi kwa madai ya baadhi ya watu. Sawa. Lakini tumeshasikia watueleze tatizo ni nini.

Pia Nakubali kujadiliwa. Na kama nimekosea nikishajadiliwa basi nipuuzwe kama nilichosema sio sahihi au kina mapungufu. Hiyo ndio maana ya majadiliano.
 
Rutta, Mwigamba alifanya nini kati ya haya?
1. Kuandika habari JF bila kuwaambia wengine

2. Kutokutumia vikao kusema yale anayoona ni matatizo chamani?

Kumbuka yeye ni mjumbe wa vikao vya chama kaka. Sio kama mimi na wewe ambao ni wajumbe wa JF. Labda ndio maana akahukumiwa haraka haraka. Ila kama alisema ukweli kuhusu Mbowe au mtu mwingine yeyote basi yuko sahihi. Na asipewe adhabu kwa kusema ukweli hata kama unauma na unawagusa wale tunaowapenda.

Kuna kitu kimoja kwenye Sheria, ushahidi ni ushahidi hata kama umepatikana katika mazingira vunjifu ya Sheria. Nasema ukweli ni ukweli hata kama umetolewa katika njia ambayo sio sahihi.

Mwigamba kakosea njia ya kusema kile anachoamini ni ukweli lakini hajakosea kukisema. Sasa tunakijua na hilo ndilo la msingi. Waliosemwa watoe maelezo tofauti na kumpinga kwamba kasemea nje ya vikao lakini hatua pia zichukuliwe kwa yeye kukiuka utaratibu kama upo. Ni rahisi sana mbona?

Zitto na Lema wamesemana na sasa tunajua walichokisema. Njia ya kusemea sio sahihi kwa madai ya baadhi ya watu. Sawa. Lakini tumeshasikia watueleze tatizo ni nini. Bado sijabariki njia aliyotumia ila sina tatizo na yeye kusema kisa tu kitaathiri chama Rutta. Chama ni zaidi ya Zitto na Lema. Trust me.

Pia Nakubali kujadiliwa. Na kama nimekosea nikishajadiliwa basi nipuuzwe kama nilichosema sio sahihi au kina mapungufu. Hiyo ndio maana ya majadiliano.
 
Japokuwa hayo na mengine mengi yameshasemwa hapa, lakini nikupongeze bwana Msando kwa ushauri huu
 
Binafsi natokea jimboni kwa Zitto kabwe,kafanya mengi katika nyanja hizo.
Elimu,kajituma sana katika nyanja hii ,kajenga Mabweni shule ya sekondari Mwamgongo,mkongoro na madarasa ns madawati ktk shule ya sekondari Mungonya. Pia anawasomesha vijana zaidi ya 250.kati ya hao wapo walio vyuo vikuu zaidi ya ishirini na tano.binafsi mdogo wangu ni miongoni na wanaonufaika na mfuko wa Zitto kabwe ktk elimu.
Ujenzi wa Bandari Kagunga ni ahadi iliyotolewa na zitto ktk kampeni zake na sasa bandari inaendelea kujengwa,pia aliahidi kujengwa kwa soko kubwa la ujirani mwema Kagunga na sas soko linajengwa.
Zitto aliingia madarakani kigoma ikiwa haina barabara ya lami hata moj na barabara ya vumbi ya uvinza kuelekea Tabora ilikuwa haipitiki masika kutokana na mafuriko ya mto Maragarasi. Lakini zitto alipoingia si tu aliwapigania wananchi wa jimbo lake bali aliupigania mkoa mzima wa kigoma.leo ukienda kasulu ,kibondo,na kigoma manispaa mtetezi wao ni zitto kabwe.leo tumemwona zitto akija na Rais wa nchi kuzindua ujenzi wa barabara ya mwandiga manyovu,mwandiga kidahwe,na sasa kidahwe malagarasi mpaka tabora ni zao la Juhudi za Mh.zitto ktk kutupigania watu wa kigoma.
Kuhusu maji kajitahidi kutumia pesa ya mfuko wa jimbo kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya kukarabati chanzo cha maji mkongoro ilo kuwa na uhakika wa maji katika vijiji vya Bitale,kiganza mpaka nyumbani Mwandiga.sasa maji yanapatikana.
Uwajibokaji wa viongozi wa halmashauri ,leo manispaa imefanikiwa kuubadili mji wa kigoma.kiukweli zitto si mbunge wa kigoma kaskazini tuu bali ni mbunge wa kifoma nzima,ni mbunge pekee ambae anaweza kugombea jimbo lolote mkoa wa kifoma na kushinda kwa kishindo.
Sasa kunataarifa hapa mjini katika vijiwe marufu vya kisiasa mjoni kigoma vya Urusi na meza ya duara kuwa Zitto atagombea kigoma mjini 2015 na sasa Selukamba kisha kimbilia kaskazini kujipanga maana anajua nguvu za zitto unapopambana nae.
Kiukweli zitto ni zaidi ya mbunge,hiyo ni robo tu ya mengi yaliyofanywa na zitto Mkoa wa kigoma ila mi nimekumbuka hayo.
 
Salaam Zitto na Lema...

Tatizo lenu sio posho. Si vyema kuwadanganya watu au kuwaaminisha kwamba tofauti iliyopo kati yenu ni mawazo au misimamo tofauti kuhusu Posho.

Kama ingekuwa hivyo basi isingekuwa tatizo. Kuwa na mawazo au misimamo tofauti sio tatizo hata siku moja.

Mtu hauhitaji rocket science kuona kwamba kuna zaidi nyuma ya pazia.

Ila kabla sijasema sana niweke mambo machache wazi.

1. Zitto na Lema ni marafiki zangu. Nawafahamu wote kiasi cha kuweza kusema kwamba najua uwezo wa kila mmoja wenu.

2. Sioni tatizo kutumia socia media kugombana au kukosoana. Najua wapo ambao wanasema vikao vitumike. Lakini vikao hivyo wengi wetu hatuhudhurii kwa sababu sio wajumbe. Yatokanayo na vikao hivyo hubaki siri na tunayoletewa ni muhtasari wa vikao. Hatupati nafasi ya kujua nani kasema nini na kwa nini na amesemaje.

3. Chama lazima kikue. Na kukua lazima mambo fulani fulani yatokee. Najua yanaweza yakapitiliza na kuathiri chama ila ni bora yatokee na kuathiri chama kuliko yaje yatokee na kuathiri NCHI. Kama tutavurugana na kugombana chama kikasambaratika basi ni kheri kuliko tuje kufarakana, kuvurugana na kugombana wakati tumepewa madaraka kuongoza watanzania.

Baada ya kuweka hayo mambo matatu wazi niseme kwamba suala la kupokea au kutopokea posho ni suala binafsi sana. Ni suala la NAFSI.

Kama nafsi yako inakutuma upokee posho basi ndio ulivyo. Nafsi hiyo hiyo itakutuma upokee rushwa, useme uongo, ukose maadili nk.

Kama nafsi yako inakutuma ukatae posho basi ndio ulivyo. Nafsi hiyo hiyo itakutuma usipokee rushwa, usiseme uongo, uwe na maadili nk.

Lakini, nafsi pia inaweza kukutuma kuchanganya mazuri na mabaya. Ukapokea posho ukakataa rushwa. Au ukakataa posho ukapokea rushwa. Ni nafsi yako.

Zitto na Lema mjipime kwa kile kilicho ndani ya nafsi zenu. Uzuri ni kwamba mwanadamu huwezi kuidanganya nafsi yako.

Ila kumbukeni yafuatayo;

1. Nyinyi ni vijana ambao mmepewa nafasi za kuongoza wananchi ambao wanawaamini.

2. Nchi yetu inahitaji viongozi ambao ni WAKWELI na WASIO NA TAMAA.

3. Lazima mtofautishe KUJULIKANA na KUWA MAARUFU. Nyie wote mnajulikana. Hamna umaarufu wowote. Sidhani kama mmekuwa viongozi ili muwe maarufu.

4. Mna nafasi kubwa sana kwa vijana kwa sababu ya kujulikana kwenu. Nchi hii itasonga mbele tu kama vijana wataamua kushiriki kikamilifu kwenye siasa. Lakini vijana hawatashiriki ipasavyo kama tutawavuruga na kuwachanganya.

5. Wananchi watapima uongozi wenu sio kwa idadi ya mabandiko FB, tweets au articles. Wananchi hawakuchagua bloggers au waandishi wa articles. Walichagua viongozi wa kuwawakilisha.

Jiulizeni ni watanzania wangapi wako FB na Jamii Forum? Kwa nini idadi yao ni hiyo!? Ukweli wenu au uongo wenu unawafikia?!

Nimesoma andiko la Lema. Limejaa hasira, jazba na kiasi fulani chuki. Nimesoma majibu ya Zitto. Yamejaa kujiamini, kupuuzia na kiasi fulani dharau. Nawajua jinsi mlivyo kwa hiyo sishangai na wala hainikeri.

Lakini mwisho wa siku najua itakavyokuwa. Ukweli utajulikana. Kuna mmoja atabaki mwingine atatwaliwa. Kuna mmoja historia yake itakuwa ni kufundishia mwingine itakuwa kwa ajili ya kukemea. Kwa mlipofikia sasa lazima tujue nani Muongo nani Mkweli.

Kwa sababu mmeamua kufulia nguo kisimani basi zianikeni tuone madoa na usafi wake. Hatutarajii mrudishe kwenye tenga mkaanikie nyumbani.

NB:

Kila mmoja wenu kwa nafasi yake awajulishe watanzania amefanya nini kama Mbunge na Kiongozi wa chama. Kwenye mambo haya;

1. Elimu

2. Afya

3. Ajira

4. Uwajibikaji.

Hayo tu manne. Sitegemei mtatuangusha katika hili. Mkishatoa taarifa zenu basi tutaamua kama mpokee au msipokee posho. Tutatoa msimamo wetu pia.

You nailed it! Wajipime kwa kazi walizofanya, siyo kwa kupokea au kutokupokea posho! Hahahaaaaa
 
Unamuuliza Ben mambo yanayomuhusu Zitto hiyo akili? Kesi ya mbuzi unaopeleka kwa fisi? Unategemea nini?

Wee hujuwi msimamo wa Ben juu ya Zitto? Hata mtoto aliyetumboni anajua Hilo tena lipo wazi kabisa!

Wee kweli hujuwi siasa pole sana!

Ni kweli Mkuu!
 
Back
Top Bottom