Salamu za wiki kwa ZITTO NA LEMA

Nimependa sana hiki kipande,kina mengi ndani yake.
Lakini, nafsi pia inaweza
kukutuma kuchanganya
mazuri na mabaya.
Ukapokea posho ukakataa
rushwa. Au ukakataa
posho ukapokea rushwa.
Ni nafsi yako.
Cc:mad:Zito

Mwandishi yuko vizuri sana na kauli hii ndo tofauti kati ya Lema na Zitto. Mmoja anatudanganya.
 
Tatizo ni kuwa watu wamesahau umuhimu wa Mh Zitto ktk mageuzi Tanzania,Kabla zitto hajaingia Bungeni Mwaka 2005 chadema kilikuwa na wabunge wachache sana pamoja na kuwa Slaa alikuwepepo tangu mwaka 2000.
Hoja madhubuti za kitaifa zilizoibuliwa na kijana huyu,zilimfanya kuonekana shujaa mbele ya macho ya watanzania,ilipofika mwaka 2010 Zitto tulimtumia kama mtaji kwa chama alitembea nchi nzima kukinadi chama na kwakuwa jamaa alikuwa na mvuto aliweza kuwashawishi vijana wengi kupenda siasa na kuona kuwa kumbe vijana wanaweza,amesababisha kamii yetu kituamini vijana tofauti na zamani ambapo vijana tulionekana wahuni na hivyo hatustahili kuingka Bungeni.
Amewanadi vijana wengi bila hata kinyongo,na inasemekana alitumia muda mwingi kuwanadi wanachadema wenzie na akafanikiwa kuwashawishi vijana kuwaunga mkono vijana wenzao,
Sasa kazi nzuri aliyofanya Zitto imeanza kunajisiwa na vijana wasiojitambua kwa kuanza kuturudisha huko tulikotoka. vitendo vya kihuni vinavyofanywa na baadhi ya wabunge ni kuwaharibia vijana wasiaminiwe tena na jamii kama ilivyokuwa zamani.na haya yanafanyika huenda kwa kutokujua,
Matarajio ya vijana wengi ilikuwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha zitto anafunikwa ili na wao waonekane mashujaa mbele ya macho ya watanzania.sasa wanatumia njia haramu kumpoteza zitto. hawa vijana wamesahau kuwa Zitto nsio chachu ya wao kuaminiwa na mwisho kuchaguliwa na jamii.hawapendi wanapoona Zitto akiendelea kufanya mambo yanayo mpatia umaarufu na kumfanya aendelee kuwa kuwa mwanasiasa bora ambae ni kijana,kiukweli Zitto bado ni kijana lkn namsifu kwa ubunifu wake anapojenga hoja,zitto amekuwa na vyanzo vingi vya taarifa nyeti za kitaifa ikiwemo baadhi ya maafisa wa serikali,Wenzake wanapomuona yuko karibu na nao huzusha kuwa wanamtumia wakati watu hao hawamsaidii zitto peke yake,Slaa amekuwa akipata nyaraka nyingi za siri toka serikalini ,hii ni ktk utaratibu kama wa zitto,vihana wenzake ktk chama na hata viongozi wa juu ktk chama wanamchukia kwakuwa anaonekana mtu muhimu sana kiasi cha kutishia nyadhifa zao ktk chama.
Tumwache zitto awatumikie watanzani kama wengi tunavyoamini,Zitto atafika mbali sana kutokana na kujiwekea malengo makubwa kisiasa,tusimkatishe tamaa kwa kengo la kumvunja nguvu.
Mwisho nawaomba wanachadema mkumbuke na kufuatilia historia ya lema ktk siasa kahama vyama vingapi na nini kilimfanya ahame,kwa kumbukumbu zangu ni kuwa lema alianzia ccm,akakimbilia Nccr mageuzi,kisha akakimbilia TLP na sasa yupo chadema, huyu lema hana tofauti Mlema ambae anatumika kama kibaraka wa ccm.tumtazame Lema kwa jicho la tatu,ni mtu hatari kwa ukombozi wa kweli wa Taifa letu.
nawasilisha.
Niko against na CHADEMA kwa mambo mengi kwa hili nakubali ya kuwa Zitto ndio alibadili sana upepo na sura kwa vijana wengi kujiunga na kuisupport CHADEMA,si Mbowe wala Slaa walio fanyayote haya au kuleta huu ushawishi,nivigumu kuamini mtu kama huyu kuweza kutumiwa na baadhi ya watu kukivuruga CDM bado na mashaka sana na baadhi ya viongozi wa cdm kuleta ugomvi binafsi na kuungiza kwenye chama
 
Msando kwenye hiyo post yake anasema Lema ni mnafiki.

Ndio maana anasema tatizo sio posho, wakati Lema anataka kuaminisha watu tatizo ni posho.
 
Albert siyo mwanasheria nguli... May be Zitto na Lema nao ni wanasiasa nguli! S0B
 
ben haya mambo ya kujibishana kwenye social media kwa viongozi wetu ni sawa? naomba mtazamo wako mkuu@ben saanane

Acha watu wajadili wewe, mmekalili kila jambo la siasa lazima likajadiriwe kwenye vikao vya chama? kuna siasa gani katika hilio? Wakajidiri kwenye vikao vya chama, hizo posho wanalipwa na CHADEMA?
 
Albert,

I concur with you....Very good!

Ben, Lema analeta evidence lini? sababu ndio tunachosubili ili tuingie hatua ingine, Zitto kaishasema atajiwajibisha ikithibitishwa kwamba anachukua posho kwenye vikao vya PAC.
 
Lema jeuri-Zitto dharau! And the result is???????? Hakuna mshindi,wote bure tu,kama hakuna kati yao atakayeamua kugeuza shingo yake kuangalia maslahi mapana ya taifa na chama,kama wataamua kubiringishana tu kama mad wrestlers,mwisho wataungana kuulizana waliko,walikotokea,na waanze vipi upya ili jamii iwaelewe,wote watatumbukia kwenye shimo moja la aibu,hivi kama ikitokea upuzi wao huu ukapelekea kukisambaratisha chama tulichokipigania kwa jasho na damu yetu,wanadhani wao watabaki salama mitaani mwetu,tutawadai jasho letu lililopotea,tutawadai damu zetu na ndugu zetu!!!
 
Alberto Msando kaongea vema sana,
"mmoja atatwaliwa mmoja atàchwa"
*mmoja ataleta historia kufundishia*
THEN WOTE wàache kujidanganya kuwa ni màarufu kwani WANAJULIKANA TÛU!
Namwona Zitto huyôoôoôo! kwenye vitabù vya historia asipochukua hatua mathubuti
 
Lema jeuri-Zitto dharau! And the result is???????? Hakuna mshindi,wote bure tu,kama hakuna kati yao atakayeamua kugeuza shingo yake kuangalia maslahi mapana ya taifa na chama,kama wataamua kubiringishana tu kama mad wrestlers,mwisho wataungana kuulizana waliko,walikotokea,na waanze vipi upya ili jamii iwaelewe,wote watatumbukia kwenye shimo moja la aibu,hivi kama ikitokea upuzi wao huu ukapelekea kukisambaratisha chama tulichokipigania kwa jasho na damu yetu,wanadhani wao watabaki salama mitaani mwetu,tutawadai jasho letu lililopotea,tutawadai damu zetu na ndugu zetu!!!


nachojua mpk sasa uongozi wa juu ushafanya kazi yake ndiyo maana kwa sasa wameanza kujitokeza washauri wa karibu kama akina albert
 
Unamuuliza Ben mambo yanayomuhusu Zitto hiyo akili? Kesi ya mbuzi unaopeleka kwa fisi? Unategemea nini?

Wee hujuwi msimamo wa Ben juu ya Zitto? Hata mtoto aliyetumboni anajua Hilo tena lipo wazi kabisa!

Wee kweli hujuwi siasa pole sana!
 
naombeni link ya SIRI ZA ZITO IWEKWE HAPA jamani nawaombeni ili tumalize hiyo cd hii ya posho mnatuhamisha tushike lipi HATA ikae hapa siku 3 tuitadhimini kama kweli au sio kweli hata walio copy pasten jaman
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom