Mkuu mara unasema haina mrejesho mara unasema marejesho wake marahaba,sasa huo si ndio mrejesho ?
NENO Marahaba ni mrejesho wa shikamoo.
Kuhusu maana mkuu maana yake ni hiyo kuwa ni mrejesho wa shikamoo.sijajua unataka kujua nini zaidi.
Sasa mkuu taarifa inayotoa si ni muitikio kuonesha kuwa anaeamkiwa ameitikia.
Kwa sababu ukimuambia mtu shikamoo akikuambia marhaba inakuwa hujaelewa kwamba marhaba ni muitikio mkuu?
Kwa sababu kila sehemu katika sisi waswahili ukisema marahaba tu from no where utaulizwa ama watakushangaa kwani kuna aliyekuamkia hapa ?
Hii kuonesha kuwa marahaba inafahamika maana yake kuwa ni jawabu la shikamoo.
Sijui unataka maana ipi mkuu ?
Kazi ya shikamoo na marahaba sio kujua hali,bali ni kutoa heshima tu.
Na heshima unatakiwa umpe mtu aliyekuzidi haijalishi yupo katika hali gani,kwa hiyo maadamu heshima ni lazima utoe kwa mtu aliyekuzidi bila kujali hali yake,basi hapo ndo shikamoo na marahaba ni PAHALA PAKE.
Ukitaka kujua yanayofuata utaongeza na maongezi mengine kama vile vipi hali,salama,unaendeleajeee ?
Kwa hiyo lazima utambue kwanza kwamba shikamoo/marahaba nii ni kwa ajili ya heshima na sio kwa ajili ya kujua hali.
Ukitaka kujua hali usitumie shikamooa kwa sababu shikamoo hapo sio pahala pake.
Ni kama ambavyo mkionana mnapeana mikono kwa kuonesha mnajaliana na kupendana..
Huwezi kuhoji kuwa kupeana mikono ifutwe ati kwa sababu ukimpa mtu mkono unakuwa hujui hali yake kama anaumwa au ana njaa ?
Au kupungiana mikono mkiwa mbali uone haifai ati kwa sababu ukimsalimia hivyo mtu inakuwa hujui hali yake kama mgonjwa au mzima ?
Kupungiana mikono ni ishara ya kuonana kwa mbali nayo ni salamu na hii salamu kazi yake sio kujua hali ya mtu bali kuonesha mmeonana japo kwa mbali.
Sasa hapa hizi ni salamu za kujua hali na sio salamu za heshima ama kuonana.
Ukitaka kujua hali ya mtu sasa uliza hivyo ulivyoandika.kuuliza hali ya mtu ni kinyume na kumsalimia tu kwa kumpa heshima.
Kama ambavyo neno pole anaambiwa yule ambae anahisiwa kuwa kapata shida ama kusumbuka ndivyo ambavyo shikamoo anaambiwa mtu mkubwa aliekuzidi umri.
Kwa hiyo kujua hali ya mtu ni tofauti na salamu ya heshima.lugha ya kiswahili nayo ni tajiri.sio kwamba ukisema habari ukinibiwa ndo umejumuisha kila kitu hapana.
Hapa ndo pale pale kuwa UNAIJAALIA SHIKAMOO NA MARAHABA KUWA NI SALAMU YA KUJULIANA HALI,HAPANA
sahikamoo marahaba ni salamu ya heshima sio kujuliana hali kabisa,ni heshima ambayo salamu hii ataanza mdogo kusema shikamoo na mkubwa ataitikia marhaba.
Usiifanye kuwa ni salamu ya hali hii ni salamu ya heshima,na heshima unatakiwa umpe mtu skiwa katika hali yeyote,ya uzima,ugonjwa n.k
Kwa hiyo salamu ya jeshima ina mrejesho wa moja kwa moja kuwa shikamoo mrejesho wake marahaba.
Huo ni nrejesho mujarrabu kabisa ambao kila mtu anaufahamu kindakindaki kuwa ukisalimiwa hivi itikia hivi.
Kwa maneno yako haya mkuu [emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516][emoji3516] kumbe unakubali kuwa hata hizo salamu ambazo unazitaka tuzifanye bado zinaweza sizitosheleze kujua hali ya mtu kama ambavyo shikamoo haiwezi kutosheleza kujua hali ya mtu moja ?
Kwa hiyo sio shikamoo tu ndo ambayo haifanyi mtu kujua hali ya mwingine zaidi,bali hata hizo salamu zingine pia zinaweza zisitoe majawabu ya hali ya mtu mpaka maongezi mengine yaendelee kama ulivyosema mkuu.
Kwa hiyo kuibatilisha shikamoo kwa hoja ya kuwa haitoshelezi kujua hali ya mtu manake unazibatilisha hata hizo salamu zingine ulizozionesha huko juu kwa sababu hata hizo pia pekee hazitoshelezi kujua hali ya mtu moja kwa moja.
Ili ujue hali ya mtu itabidi utoke katika salamu uingie katika maongezi,na huku ni kuonesha kuwa SALAMU haileti jawabu la kutosheleza kujua hali ya mtu.
Kwa hivyo mimi SIUNGI MKONO HOJAHII