Salamu ya shikamoo ifutwe rasmi na Serikali

Salamu ya shikamoo ifutwe rasmi na Serikali

Huwezi kupima umri wa mtu kwa macho.

Shikamo haina heshima ila ni salamu kwa ajili ya watu waliokuzidi umri.

Maana ya neno shikamoo na marhaba ni nini?
 
St. Kayumba kilasiku asubuhi watoto ni shkaaaamooooo mwaaalim.
Ni sehemu ya asili ya utanzania wetu.

wakubwa huwa nawaambia" heshma yako mzee/mama"
akisema niamkie basi namuamkia tu wala akuna shida.
 
Mkuu mara unasema haina mrejesho mara unasema marejesho wake marahaba,sasa huo si ndio mrejesho ?

NENO Marahaba ni mrejesho wa shikamoo.

Kuhusu maana mkuu maana yake ni hiyo kuwa ni mrejesho wa shikamoo.sijajua unataka kujua nini zaidi.


Sasa mkuu taarifa inayotoa si ni muitikio kuonesha kuwa anaeamkiwa ameitikia.
Kwa sababu ukimuambia mtu shikamoo akikuambia marhaba inakuwa hujaelewa kwamba marhaba ni muitikio mkuu?

Kwa sababu kila sehemu katika sisi waswahili ukisema marahaba tu from no where utaulizwa ama watakushangaa kwani kuna aliyekuamkia hapa ?

Hii kuonesha kuwa marahaba inafahamika maana yake kuwa ni jawabu la shikamoo.

Sijui unataka maana ipi mkuu ?
Kazi ya shikamoo na marahaba sio kujua hali,bali ni kutoa heshima tu.

Na heshima unatakiwa umpe mtu aliyekuzidi haijalishi yupo katika hali gani,kwa hiyo maadamu heshima ni lazima utoe kwa mtu aliyekuzidi bila kujali hali yake,basi hapo ndo shikamoo na marahaba ni PAHALA PAKE.

Ukitaka kujua yanayofuata utaongeza na maongezi mengine kama vile vipi hali,salama,unaendeleajeee ?

Kwa hiyo lazima utambue kwanza kwamba shikamoo/marahaba nii ni kwa ajili ya heshima na sio kwa ajili ya kujua hali.

Ukitaka kujua hali usitumie shikamooa kwa sababu shikamoo hapo sio pahala pake.
Ni kama ambavyo mkionana mnapeana mikono kwa kuonesha mnajaliana na kupendana..

Huwezi kuhoji kuwa kupeana mikono ifutwe ati kwa sababu ukimpa mtu mkono unakuwa hujui hali yake kama anaumwa au ana njaa ?

Au kupungiana mikono mkiwa mbali uone haifai ati kwa sababu ukimsalimia hivyo mtu inakuwa hujui hali yake kama mgonjwa au mzima ?

Kupungiana mikono ni ishara ya kuonana kwa mbali nayo ni salamu na hii salamu kazi yake sio kujua hali ya mtu bali kuonesha mmeonana japo kwa mbali.
Sasa hapa hizi ni salamu za kujua hali na sio salamu za heshima ama kuonana.

Ukitaka kujua hali ya mtu sasa uliza hivyo ulivyoandika.kuuliza hali ya mtu ni kinyume na kumsalimia tu kwa kumpa heshima.

Kama ambavyo neno pole anaambiwa yule ambae anahisiwa kuwa kapata shida ama kusumbuka ndivyo ambavyo shikamoo anaambiwa mtu mkubwa aliekuzidi umri.

Kwa hiyo kujua hali ya mtu ni tofauti na salamu ya heshima.lugha ya kiswahili nayo ni tajiri.sio kwamba ukisema habari ukinibiwa ndo umejumuisha kila kitu hapana.
Hapa ndo pale pale kuwa UNAIJAALIA SHIKAMOO NA MARAHABA KUWA NI SALAMU YA KUJULIANA HALI,HAPANA

sahikamoo marahaba ni salamu ya heshima sio kujuliana hali kabisa,ni heshima ambayo salamu hii ataanza mdogo kusema shikamoo na mkubwa ataitikia marhaba.

Usiifanye kuwa ni salamu ya hali hii ni salamu ya heshima,na heshima unatakiwa umpe mtu skiwa katika hali yeyote,ya uzima,ugonjwa n.k

Kwa hiyo salamu ya jeshima ina mrejesho wa moja kwa moja kuwa shikamoo mrejesho wake marahaba.

Huo ni nrejesho mujarrabu kabisa ambao kila mtu anaufahamu kindakindaki kuwa ukisalimiwa hivi itikia hivi.
Kwa maneno yako haya mkuu ☝☝☝☝☝ kumbe unakubali kuwa hata hizo salamu ambazo unazitaka tuzifanye bado zinaweza sizitosheleze kujua hali ya mtu kama ambavyo shikamoo haiwezi kutosheleza kujua hali ya mtu moja ?

Kwa hiyo sio shikamoo tu ndo ambayo haifanyi mtu kujua hali ya mwingine zaidi,bali hata hizo salamu zingine pia zinaweza zisitoe majawabu ya hali ya mtu mpaka maongezi mengine yaendelee kama ulivyosema mkuu.

Kwa hiyo kuibatilisha shikamoo kwa hoja ya kuwa haitoshelezi kujua hali ya mtu manake unazibatilisha hata hizo salamu zingine ulizozionesha huko juu kwa sababu hata hizo pia pekee hazitoshelezi kujua hali ya mtu moja kwa moja.

Ili ujue hali ya mtu itabidi utoke katika salamu uingie katika maongezi,na huku ni kuonesha kuwa SALAMU haileti jawabu la kutosheleza kujua hali ya mtu.

Kwa hivyo mimi SIUNGI MKONO HOJAHII
Shikamoo ni salamu ya kifoo dingi.
 
Huwezi kupima umri wa mtu kwa macho.
Umri ni namba tu mzee.

Kama huwezi kupima umri basi angalia muonekano wa mtu,kama kakuzidi utamuamkia.

Wewe kijana mtu aliyekuzidi miaka nabakawa mtu mzima utamjua tu.

Ukikutana na mtu ambae una mashaka kwamba mnaendana umri basi usimuamkie utampa salamu zingine za heshima kama vile habari za asubuhi,habari za mda huu n.k

Kwa sababu shikamoo sio lazima kama ambavyo salamu zingine pia sio lazima bali ni uungwana tu.

Na bila shaka hapa hatuzungumzii ulazima tunazungumzia uungwana tu wa
Shikamo haina heshima ila ni salamu kwa ajili ya watu waliokuzidi umri.
Shikamoo ina heshima kwa sababu ndio inavyotumika kwa muktadhwa huo,huwezi kusema haina heshima.

Ukimuambia baba yako shikamoo alafu umuambie baba mpuuzi wewe bila shaka utapata jibu kuwa heshima ni ipi inatambulika hapo.

Shikamoo ni heshima kwa sababu haitumiki popote isipokuwa katika mazingira ya heshima.

Ukikusudia kumtukana mtu huwezi kumuambia shikamoo kwa sababu hiyo ni heshima bali utamuambia wewe mjinga,mpuuzi n.k

Sasa unaposema sio heshima kwa hoja gani mkuu ?

Maana ya neno shikamoo na marhaba ni nini?
Maana yake inapatikana kwa mujibu wa vile inavyotumika.

Shikamoo ni moja salamu ya kutoa heshima kwa aliekuzidi wewe kiumri ama kimajukumu(sio rasmi sana).

Na marhaba ni kupokea heshima uliyopewa.

Hizo ndo maana zake.

Ukikataa kuwa hizi sio maana zake basi niambie kuwa ili kitu kiwe na maana hiyo maana inatakiwa iwe na sifa ipi ?

Kwa sababu neno "SAMAHANI " ukiulizwa maana yake utasema ni kujishusha pengine unapokosea n.k

Hii inaelezea maana ya neno hilo kwa mujibu wa muktadhwa wake vile inavyotumika.

Kwa hiyo ukija kukataa maana ya shikamoo na marhaba itabidi ulete hoja ambazo zitaonesha kwamba ili kitu kiwe na maana fulani basi kikidhi vigezo hivi na hivi.

Maana za shikamoo na marahaba ndio hizo nilizokupa.

Napengine zipo maana nyingine nyingi tu.
 
Kuna baadhi ya wazee usipo waamkia utasikia hawa vijana wanajifanya wamesoma soma ona sasa hawataki kuamkia wazee

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
St. Kayumba kilasiku asubuhi watoto ni shkaaaamooooo mwaaalim.
Ni sehemu ya asili ya utanzania wetu.

wakubwa huwa nawaambia" heshma yako mzee/mama"
akisema niamkie basi namuamkia tu wala akuna shida.



Shikamoo mwalimu!
 
Kwakweli inatatiza kwa mfano kijana ni tajiri kwenye jamii anasaidia matatizo mbalimbali kwa kipato chake lakini ni kijana mdogo labda 25years alafu yupo mtu wa makamo labda tuseme 45 years uyu yeye hali yake kimaisha ipo chini mala nyingi anamtegemea uyo dogo ..hasa apo wakikutana nani anampa mwenzake shikamoo..??
 
Mambo mengine yabaki hivyo kama utamaduni, kama ni kudhalilishana basi kufuta shikamoo inatakiwa pia na mwanamke kumpigia magoti mwanaume nayo ifutwe. maana ni yale yale
 
Serikali ingefuta hii salaam inadhalilisha sana.Unakuta binti mrembo hata age haujamzidi kihivyo lkn anakupa shikamooo hadi hamu ya kumtokea inakwama.
 
Huwezi kupima umri wa mtu kwa macho.

Shikamo haina heshima ila ni salamu kwa ajili ya watu waliokuzidi umri.

Maana ya neno shikamoo na marhaba ni nini?
Ni ya kitumwa. Mtumwa kumsalimia Mmiliki wa Mtumwa. Sio habari Za kuzidi umri. Sema wazee wa zamani waliopenda Umungu mtu ndio wakaibeba baada ya utumwa ilhali walijua haikuwa Ina maana nzuri.
Unaemwambia shikamoo "niko chini ya miguu yako" unampa cheo cha KiMungu mtu kwamba hata life yako Yeye ndio anayeweza kuamua uwe hai au ufe kama kipindi cha utumwa.
Mimi home tangu wadogo tunasalimia wazazi kwa kilugha tu. Napataga shida Sana kumwambia mtu shikamoo. Siipendi kabisa hii salamu. Ukiwa huru hutakiwi kuwa na minyororo ya kitumwa na ndo maana hata America wamelifuta neno NIGER kulitamka sababu ya historia yake kwa watu weusi kipindi cha utumwa.
 
Naunga mkono hoja, unakuta upo ofisini afu anakuja mtu anaona kabisa unamzidi na ni mzee ila anasalimia shikamoo😅, kweli huu ni utumwa..
 
Pia maofisini wazee wengi tu ukifanya nao kazi sana mkiwa na urafiki hawapendi uwape shikamoo hata kama amekuzidi sana.
Ni salamu iliyojengwa na misingi ya woga sio heshima.
Naunga mkono hoja, unakuta upo ofisini afu anakuja mtu anaona kabisa unamzidi na ni mzee ila anasalimia shikamoo[emoji28], kweli huu ni utumwa..
 
Back
Top Bottom