Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Tokea Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ujitokeze kujibu kejeli zilizotolewa na Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wake, Seif Sharrif Hamad dhidi ya Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, waandishi mbalimbali wa makala magazetini wamekuwa akionyeshana ujuzi na wendawazimu wa kufikiri.

Wengine wanadai UVCCM ilikurupuka, imepoteza mwelekeo, inaelekea kubaya, imekosa hoja na baadhi yao wanafikia mpaka hatua ya kupotosha kuwa tamko lililotolewa na jumuiya hiyo ya CCM kupitia kwa Kaimu Katibu Mkuu wake, Francis Isaack Mtinga lilisheheni matusi dhidi ya Lipumba na Seif.

Wapo wanaofikia hatua ya kumsifu Seif kuwa ni msomi aliyeweka rekodi ya kufaulu vizuri wakati akisoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwanzoni mwa miaka ya 1970, hivyo kwao ni kutukanwa anapokosolewa kuhusu msimamo wake wa kutotaka kura za maoni zitumike kuamua suala la kuwa na Serikali ya Mseto Zanzibar na kung’ang’ania vinginevyo.

Hata Lipumba, profesa wa uchumi naye eti anatukanwa kuambiwa kuwa anaburuzwa na Seif katika uongozi wa CUF huku wakijua ni kweli.

Wanasema Lipumba wala Seif hawawezi kuwa na akili za kuku, lakini hawasemi kwa nini wasiwe hivyo kama wanasahau kwa urahisi misimamo yao ya kila mara ya kutamba kwamba CUF inaweza kufanya lolote kwa vile ina nguvu za umma.

Ni akili za kuku pekee ndizo zinaweza kumfanya mtu atambe hivi leo, lakini kesho akiambiwa tekeleza suala hili kwa kutumia tambo zako anageuka ghafla na kusema “haiwezekani”, ndivyo ilivyo kwa Lipumba na Seif.

Wanasahau mithili ya kuku kwamba siku zote walikuwa wakitangaza dunia nzima kuwa chama chao kina nguvu nyingi Visiwani kuliko CCM, lakini leo wanaoogopa kuingia kwenye kura za maoni ili umma unaowaunga mkono kwa kiasi kikubwa utumike kubariki Serikali ya Mseto, ileile ambayo wamekuwa wakiing’ang’ania siku nyingi na tayari Seif alishatangaza kuwa ikiundwa yeye ndiye atakuwa Waziri Kiongozi.

Kuweka rekodi ya kufaulu Chuo Kikuu zaidi ya miaka 30 iliyopita siyo kigezo cha akili wala ubora kisiasa wala katika uongozi wa umma kwa vile hayo ni mambo mawili yanayotofautiana kwa kiasi kikubwa.

Inawezekana alifaulu na kuweka rekodi hiyo kwa sababu alikuwa bingwa wa kukariri kwa ajili ya mitihani badala ya kujifunza ili kujua, ama aliweka rekodi hiyo kwa vile alishirikiana na aliyekuwa mhadhiri wake kuonyeshwa mitihani na kuifanya kabla ya siku kufika tofauti na wenzake.

Inawezekana aliweka rekodi hiyo kwa vile siku hizo alikuwa na akili timamu, lakini sasa akili zake zimeathiriwa na kuukosa urais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar alioanza kuufukuzia kwa miaka 23 iliyopita.

Wanaodhani kwamba kuweka rekodi ya kufaulu vizuri mitihani ya chuo kikuu ni kipimo cha ubora katika uongozi wa kisiasa au kijamii wanakosea sana.

Unaweza kufaulu vizuri mitihani shuleni au chuoni, lakini ukawa “bomu” katika uongozi wa umma kutokana na sababu mbalimbali, moja kati yake ikiwa ni ubinafsi kama alionao Seif anayedhani ni haramu kwake kutokuwa Rais wa Zanzibar angalau kwa siku moja tu.

Kama ana akili sana nawaomba wanaomtetea katika hilo waongee naye, wamwelimishe kwamba kwa vile CUF ina nguvu sana Visiwani Zanzibar kama anavyosema mara nyingi na kibaraka wake Lipumba basi wasiogope kura za maoni.

Wawaambie Wazanzibari kuwa msimamo wa CUF ni kutaka iundwe Serikali ya Mseto, hivyo kwa vile wanaiunga mkono kwa wingi wapige kura kubariki matakwa hayo na hakika watakubali kwa vile ndiyo msimamo wa chama wakipendacho kama madai hayo yana ukweli.

Wamwambie atumie akili alizokuwa nazo darasani wakati akisoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa uamuzi mzito kama wa kuwa na Serikali ya Mseto kati ya vyama tofauti wakati Katiba inasema chama kinachoshinda uchaguzi mkuu ndicho kinaunda serikali, hivyo wakaichagua CCM na mgombea wake wa urais ni suala linalopaswa kuamuliwa na Wazanzibari wote na si kikundi kidogo cha kina Seif, Ismail Jussa Ladhu, Machano Khamis Bakari au Juma Duni Haji.

Wamwambie asiwe na hofu, aende kila kijiji Unguja na Pemba akanadi msimamo wa chama chake na kwa sababu anasema kina nguvu hakika katika kura za maoni za kutaka iundwe Serikali ya Mseto wapiga kura wataipa ushindi mkubwa CUF dhidi ya CCM.

Kung’ang’ania tu eti rasimu ya mazungumzo ya muafaka baina ya CCM na CUF ilipendekeza kuwe na Serikali ya Mseto wakati ukijua tafsiri halisi ya neon “rasimu” kuwa siyo mkataba wa kisheria wala makubaliano ya mwisho ni upofu wa fikra, uduni wa kufikiri na ndiyo maana wote wanaozungumza vinginevyo dhidi ya tamko la UVCCM ni vizuri waelewe kuwa chombo hicho cha vijana wa CCM hakitabomolewa kwa makala za magazeti.

UVCCM itabaki ileile ikiwa na nguvu na ushawishi uleule katika jamii.
 
Wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM Tayari Wako katika Harakati za Kusaka nafasi ya uenyakiti wa jumuiya hiyo itakayoachwa wazi baadae mwaka huu na Emmanueli Nchimbi ,Joto limepanda na wengi wamedaiwa kuanza kujipanga kusaka kiti hicho miongoni mwa waliokuwa wanatajwa kuwania nafasi hiyo ni katibu mkuu umoja wa vijana CCM taifa (Francis Isack) lakini amejitoa baada ya kuteuliwa kwa wadhifa huo mpya.

Kutangaza kwake Hadharani kuwa alikusudia kugombea uenyekiti Taifa , lakini baada ya kupata majukumu sasa ameicha ni Uwazi unaomyesha kuwa ni kiongozi aliyejipanga kusaidia jumuia yetu.

Natumia fursa hii kumpongaza na kumtaka ahamasishe viongozi wengine wenye nyadhifa kufahamu ya kuwa wana majukumu ya kufanya na hivyo basi wasiwe na tamaa ya madaraka makubwa wakati waliyonayo bado hawajayafanikisha vema .

Sisi vijana tumekuwa na maswali mengi sana juu ya watu wenye nyadhifa tayari kwenye jumuia lakini bado wanautaka uenyekiti ,Tutajiuliza ni kipi mnachokitaka kutufanyia kwenye nafasi ya mwenyekiti ambacho hamuwezi kufanya katika nafasi mlizonazo?

Vijana wa nchi hii wanataka kuona maendeleo yao na pia katika chama wanataka kuona jumuiya ikifanya kazi vema wanataka kuona mabadiliko katika uchumi na ajira ili waweze kuendana na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila Mtanzania.

Nakumbuka Historia ya 2003 tulipokwenda kumchagua Nchimbi pale Dodoma ambae wakubwa hawakumtaka Bali sisi wana UVCCM ndie aliekua chaguo letu, Tunaamini ili kujenga na kuendeleza msingi huu hatutegemei kukuona wewe na wenzio mkituletea wa kutuchaguliwa sisi Mwenyekiti ,tunataka tumchague tunayemtaka ili msingi wetu wa kupata kiongozi wetu vijana uendelee

Kupitia kwako ningependa kutoa rai na kuhamasisha vijana wenye uwezo na nia njema bila kujali wao ni kina nani au nani anamuandaa nani,wajitokeze kwani tunahitaji kiongozi wa vijana na si wa kundi la watu fulani.

Pia wajumbe wa halimashauri kuu ya Taifa NEC Kupitia Vijana hatutegemei kuwaona katika kinyang'anyiro cha uenyekiti ,waachiwe ambao sio waNEC ili tuongeze wigo wa nafasi za vijana katika ngazi za maamuzi.

Pilikapilika zimeanza ,vikao vinafanyika ,watoto wa vigogo wanatishia makatibu wa UVCCM wa mikoa na wilaya ingawa ni haki yao kushiriki wajue tuu kuwa busara ni muhimu zaidi na ustaarabu wa kuridhika kwanza na walichopata, Hatutegemei kuwaona katika kinyang'anyiro cha mwenyekiti ni muhimu wakumbuke kuwa tulimpa Nchimbi kwa kuwa hakuwa mjumbe wa NEC .

Rushwa ya vitisho tumeanza kuiona kauli kama huyu ndiye anayetakiwa ,huyu hatakiwi,huyu mwenzetu ,huyu simwenzetu Vijana huchagua ambaye hashinikizwi kwani tunaamini kuwa ndiye atakuwa wetu, wa kushushwa na watoto wa vigogo atakuwa wa watoto wa vigogo.

TUNASUBIRI KWA HAMU KAULI YA BENNO MALISA KUWEKA HADHARANI KUWA ALIKUSUDIA KUGOMBEA UENYEKITI UVCCM TAIFA LAKINI BAADA YA KUPATA MAJUKUMU YA NAIBU KATIBU MKUU UMOJA WA VIJANA TAIFA UVCCM SASA AMEACHA KUGOMBEA ,Ili kuongeza wigo wa uwakilishi wa Vijana Katika Vikao Vya maamuzi
 
Unazungumzia Fransis aliyemwaga matusi hadharani mbele yetu kwenye press conference pale makao makuu ya UVCCM au mtu mwingine? Huyu aliabisha CCM inayosifika kwa malezi ya vijana.

PM
 
Mimi nafikiri umesahau kuwataja majina wa kwanza ni RIDHIWANI KIKWETE,Wa pili ni MWAMVITA MAKAMBA,Wa tatu VIOLET MZINDAKAYA ambaye inasemekana ni mpenzi wa Benno Malisa....!!! Ndugu wana JF kuhusu niliowataja nitatoa ushahidi endapo utahitajika
 
Mimi nafikiri umesahau kuwataja majina wa kwanza ni RIDHIWANI KIKWETE,Wa pili ni MWAMVITA MAKAMBA,Wa tatu VIOLET MZINDAKAYA ambaye inasemekana ni mpenzi wa Benno Malisa....!!! Ndugu wana JF kuhusu niliowataja nitatoa ushahidi endapo utahitajika

Kwa hiyo unataka kusema kwamba Kikwete, Makamba na Mzindakaya wamewatuma watoto wao ili wamweke mtu wao kwenye Uenyekiti wa Vijana wa CCM au? Huyu Mwamvita ni yule wa Vodacom au kuna mwingine? Hebu tueleze ukweli isije ikawa unasingizia

PM
 
Ndg paparazi Muwazi
Hapana naamini hawajatumwa na Baba zao ila ni watoto wakorofi,watukutu, wanaotumia Majina ya Baba zao..!! wakidhani ndiyo strategy nzuri yakuhadaa wahusika ..kama alivyoeleza ogwalumapesa..!!!
 
hivi hiki chama nyie vijana walala hoi bado mnaffikiri mna hisa kule? kwa nini mnahangaika bure kutafuta hisa katika kampuni iliyokwisha uza hisa zake zote?

mnasahau kuwa ccm ina wenyewe na wenyewe ndo hao mnaowalalamikia? kwa nini msiwaachie chama chao wakaendelea kupigana vikumbo wenyewe?
mna option mbili
1. kujiunga na vyama ambavyo tayari vipo na muwaachie hawo wazee mafisadi na watoto wao wazame na jahazi lao

2 au kama mnaona vyama vilivyopo havifai, mnaweza kuhama kama kundi zima na mkaanzisha chama chenu na siye tutawaunga mkono
 
aAAAAAAH hiki chama hivi nawashangaa hawa wajukuu wa ccm hawajui kama si chama chao? ni chama kilicho na wenyewe. Na wao wanajaribu tu kuweka vichwa vyao humo. Shauri yao watavitoa vikiwa havina kichwa. Eeeee tokeni huko mapema acha kupiga kelele zisizo na msaada. Hakuna wa kukusikiliza kule
 
Tuna nini na watoto wa vigogo?? kuna wavivu wa kufikiri watajitokeza kuwatetea...
Lakini CCM imekwisha hivyo kimebakia kama daraja. Wahuni wanakitumia kupata wanachotaka. Endapo Mkapa angelijua kabla angewashinikiza wanae wawe ktk nafasi nyeti za chama ila ndo ivo tena. Naona Muungwana anajua kucheza turufu
 
Hivi bado kuna watu wanategemea mazuri kutoka kwenye UVCCM, maana inaonekana kana kwamba ni genge la watoto wa wakubwa kujifunzia ufisadi waje waibie nchi.
 
"Mwambi aliigeukia Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na kuituhumu kuwa sasa imekuwa tofauti na ya zamani. Alidai kuwa jumuiya hiyo imekuwa chafu, hivyo inapaswa kujisafisha kwa kuchagua viongozi safi, watakaoifufua"(Jaka Mwambi,2007)

UVCCM imeshakufa kwa hiyo ukiwa na hela wewe nenda kagombee maana ni NGO.
 
Wazo zuri ! Ujumbe Mzuri ! naomba niwahakikishie wahusika enzi za zidumu fikra sahihi za mtu mmoja zimeshapita, wanaoandaa na waandae tu ila wasijerogwa kufikiri kuwa wanaotaka kwa mashinikizo watapata kura vinginevyo tutaandika historia mpya kabisa katika siasa za Bongo ! anaebisha amuulize mtu anaeitwa Nape Moses Nauye kilimpata nini Dom 2003 licha ya kuwa vigogo wote wa Chama walijipanga kumtetea.

Who is Ridhiwani by the way? Ridhiwani ana ubavu kumshinda mzee wa Mtera mbona walichemsha 2003 na Nape wao kwi kwi kwiii

pigeni sana kelele twawasubiri Dom patakuwa hapatoshi
 
Are you all who are talking ill of UVCCM members of UVCCM or CCM? if not why worry about who they choose to elect?

If you belong to CHADEMA, CUF, NCCR and other factions, your focus should be on what your party wants and strategies for your party and its special groups youth, women and others.

Bickering about UVCCM while you are not even part of UVCCM or CCM will not resolve or solve anything. MOstly you are giving UVCCM and CCM a cheap and free publicity.
 
Wazo zuri ! Ujumbe Mzuri ! naomba niwahakikishie wahusika enzi za zidumu fikra sahihi za mtu mmoja zimeshapita, wanaoandaa na waandae tu ila wasijerogwa kufikiri kuwa wanaotaka kwa mashinikizo watapata kura vinginevyo tutaandika historia mpya kabisa katika siasa za Bongo ! anaebisha amuulize mtu anaeitwa Nape Moses Nauye kilimpata nini Dom 2003 licha ya kuwa vigogo wote wa Chama walijipanga kumtetea.

Who is Ridhiwani by the way? Ridhiwani ana ubavu kumshinda mzee wa Mtera mbona walichemsha 2003 na Nape wao kwi kwi kwiii

pigeni sana kelele twawasubiri Dom patakuwa hapatoshi

Mbogo heshima kwako,
Wakati mwingine huwa najiuliza haya ya Nape na kuungwa mkono na vigogo huwa unayasema sana kila ukichangia mada zihusuzo uvccm na uchaguzi,ukweli wake ni nini?Maana nijuavyo wakati huo kulikuwa na politics za 2005,mchakato wa kupata mgombea urais ccm, but Nape mwenyewe alishawahi kukana kusupportmtu katika hili,hebu tupe ushahidi wa hiyo habari ya mtera na Nape,au mnatumia ukaribu wake na wazee vibayaaa?

Katika yote inaonekana mnamwogopa Nape hasa mafisadi kwa uwazi na msimamo wake hasa kwa mtandao maana najua alikuwa mwiba mchungu kwao,nadhani mwaga ushahidi wa uhusiano wake naho wazee tujadili.....
 
Topic hii inanikumbusha mengiiii mabaya ambayo yaliwahi kuandikwa kuhusu Mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa vijana dhidi ya wagombea wenziwe.

Naunga mkono hoja kwamba Umoja wa Vijana CCM ilishachafuka kupindukia kwa hiyo hata wanaojitosa kutaka kuwania kwa migongo ya majina na wazazi wao wanayo haki ya kufanya hivyo kutokana na hali halisi ya uongozi ndani ya Umoja huo.

Huu si ule Umoja wa Vijana wa enzi za akina Joseph Nyerere na Chris Liundi na wazee wengine wa leo waliokuwa viongozi wa kweli wa Umoja huo! Bado tuna imani kwamba iko siku Tanzania itajengwa na Vijana wenye Moyo na mapenzi ya dhati kwa nchi yao!
 
Kimsingi nataka kupingana na mtoa hoja juu ya kuwazuia wanachama wa UVCCM ambao pia ni wajumbe wa NEC ya CCM,kundi la Vijana kuomba kugombea.

Sababu ya kwanza inahusiana moja kwa moja na haki yao ya kuchagua na kuchaguliwa kama ilivyoanishwa kwenye kanuni ya UVCCM.Sasa tukisema wasigombee kwa sababu zozote zile itakuwa ni kutowatendea haki.Na ndivyo ilivyokuwa hata kwa uchaguzi chaguzi za 1998 na 2003.

Mtoa hoja nadhani kumbukumbu zako haziko sahihi.Nakumbuka uchaguzi wa mwaka 1998 mimi nikiwa Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya moja nyeti sana,tulimchagua Mh.Dr.Emanuel Nchimbi(MB) akiwa tayari ni mjumbe wa NEC wa kuchaguliwa.Alichaguliwa katika uchaguzi mkuu wa 1997 pale Chimwaga sambamba na akina Mh.Christopher Ole Sendeka(MB),Mh.Dr Mathayo Msuya(MB),na wengineo.Uchaguzi UVCCM wa mwaka 2003,wagombea wote watatu,Mh.Dr.Nchimbi,Jane Mihanji,na Nape Mnauye,walikuwa ni wajumbe wa NEC.Tofauti ya hapa ni Kwamba Mh.Nchimbi,alikuwa ni mjumbe wa NEC na CC kutokana na wadhifa wake kqmq M/kiti wa taifa wa UVCCM.Jambo la muhimu hapa ni kwamba,ni jambo la busara kwa wale wanachama wa UVCCM ambao ni wajume wa NEC, kuwa na moyo wa kuwashirikisha vijana wengine kwenye ngazi za juu za maamuzi pindi wanaposhinda nafasi ya M/Kiti wa taifa.Hili ndilo alilolifanya Mh.Dr.Nchimbi. Baada ya kukwaa wadhifa huo aliachia nafasi ya ujumbe wa NEC wa kuchaguliwa ili kupisha vijana wengine wagombee na hivyo kuongeza nafasi za uwakilishi wa vijana kwenye kikao muhimu kabisa kulingana na muundo wa chama chetu,NEC.Vijana tulimpongeza sana Mh.Nchimbi kwa uamuzi wake huo ulioonesha kukomaa kisiasa.

Mimi mwenyewe nakumbuka nilikuwa miongoni mwa vijana 19 tuliopitishwa na kamati kuu ya chama kujaza nafasi ya Mh.Nchimbi,na mwanachama mwenzetu Frank Uhaula akatupiga bao katika uchaguzi uliofanywa na NEC,pale Dodoma,mwaka 2004.Kwa hiyo,ninachotaka kusema ni kwamba,sioni tatizo kwa vijana ambao ni waNEC kuomba kugombea.

Ila muhimu ni vema wasukumwe na dhamira ya kutoa nafasi kwa vijana wengine pindi wanaposhinda wadhifa wa M/Kiti.Nasikitika kwamba makamu M/Kiti wa UVCCM Amina Mabrouk hakuwa na moyo huo kwani aliendelea kushikilia nafasi ya ujumbe wa NEC wa kuchaguliwa ili hali kwa nafasi yake ya umakamu aliingia moja kwa moja kwenye NEC. Sasa, hapa ndipo linapokuja tatizo, dhamira!

Kimsingi suala la ndugu Beno Malisa lina utata kidogo endapo kweli ana mpango wa kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa katika jumuiya hii ya CCM. Utata wake hautokani na yeye kuwa mjumbe wa NEC. Utata ninaouona mimi ni kuhusu kanuni za kiutumishi.

Ninavyofahamu, haingii akilini kwa mtumishi wa ngazi ya juu kama ya unaibu katibu mkuu kugombea nafasi ya M/Kiti. Cheo cha M/kiti si cheo cha mshahara.Kwa lugha nyepesi kazi ya mwenyekiti si kazi ya kukaa ofisini. Kazi za mwenyekiti kama zilivyoanishwa na kanuni ya UVCCM ni kuongoza vikao husika. Na ndio maana inapendekezwa mwenyekiti ni vema akawa na shughuli halali itakayomuingizia kipato.

Sasa napata tabu kujua kwamba, je bwana Malisa itabidi aache kazi yake ya mshahara na kuamua kuishi kwa posho za vikao kama mwenyekiti? Ama ana mpango wa kutafuta kazi nyingine? Ukweli ni kwamba,hawezi kuwa naibu katibu mkuu na wakati huo huo awe m/kiti. Kanuni hazikubali.

Hapa nitaomba ufafanuzi kidogo.

Hili la watoto wa vigogo kushiriki katika kampeni za kuwandaa watu wao mimi nadhani ni hofu tu zisikowa na msingi wowote. Tukumbuke Mwenyekiti anachaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu kutoka kila pembe ya nchi. Sasa siamini kama hao watoto wa vigogo watakuwa na uwezo wa kubadili maamuzi na misimamo ya wajumbe.

Ninachoamini mimi ni kwamba,wajumbe watamchagua kijana ambae kwa uwezo, sifa, umakini, maadili, elimu na msimamo wake utawakuwa kwa maslahi ya jumuiya,na sio vinginevyo.Wajumbe watazingatia hoja zinazojengwa na kambi husika kwamba kwanini wanadhani mtu wao ni bora zaidi ya wengine.Na hapa haijalishi nani yuko nyuma ya mgombea.

Awe ni mtoto wa kigogo au mtoto wa mchoma mkaa. Hilo sio muhimu. Muhimu ni hoja za ushawishi. Sasa kama ni Ridhiwani, Mwamvita au Violeth (narejea majina ya mtoa hoja), wajumbe watasikiliza hoja zao,na wala sio kwa sababu eti ni watoto wa vigogo.Hamna haja ya kujenga hofu juu yao.
 
Hivi hawa watoto wa vigogo ni wale waliozaliwa na magogo au vipi? Eti wazaliwa bila ya kukatiwa? Ni nini hasa maana ya gogo kukufanya ukose usingizi na kuanza kulia na magogo yasio katika? enewei shreeeK Mie nauliza tu?
 
Mrithi wa Nchimbi mwenyekiti UVCCM (umoja wa vijana Taifa) Taifa, RIdhwan kikwete katangaza leo kupitia gazeti la Tanzania daima kuwa ana mtu wake anayemtaka awe mwenyekiti wa umoja wa vijana Taifa, Zainabu Kawawa (mtoto wa kawawa Rashid) anagombea uenyekiti taifa, Violet Mzindakaya (mtoto wa Mzindakaya Mbunge wa Sumbawanga, na mtuhumiwa wa ufisadi wa sh bilioni 10 kutoka B.O.T) anagombea ijapokuwa kuna minongono kuwa mwishoni atamuunga mkono kipenzi cha Ridhwan ,Mwamvita Makamba(mtoto wa makamba katibu mkuu wa CCM) nae ana mtu wake.

Wana JF nauliza sisi wototo wa wakulima nafasi yetu ipo wapi? katika jumuia kama watoto wa Nyerere, Makongoro, Madaraka, Ana na watoto wa mzee Ruksa Mwinyi Husein, na Abas wangetaka kuwaweka marafiki zao waliosoma nao (kwa maana na wao wanesoma)jumuia ya vijana(UVCCM) igekuwa wap?
 
Ndio Chukua Chako Mapema hiyo mkuu wewe mkulima katafute shamba bado mapori yamejaa hayana watu..
 
wana JF nauliza sisi wototo wa wakulima nafasi yetu ipo wapi?

Na mimi nakuulizeni nyie watoto wenzetu wa wakulima, kwani kuna mtu kawalazimisha muwe CCM? Kwa nini msiende chama kingine kama umeona hicho chama kimegeuka kuwa cha ukoo wa mabwenyenye?

Matatizo mengine ni ya kujitakia na inakuwa vigumu sana sisi kuwahurumia. Madamu hao uliowataja ni wanachama halali wa chama chenu basi wana haki zote za kugombea nafasi wanazogombea. Na nyie jitupeni humohumo mkiona huku sio kwenu tafuteni chama kingine. Huu ndio ushauri rahisi kabisa na hauna gharama yeyote kuutekeleza.
 
Back
Top Bottom