Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Leo asubuhi nimesikia radioni kuwa nape ataingia kwenye kikao cha neki kama kawaida na kama mjumbe halali, kunamtu anaweza kunitafsiria
 
Leo asubuhi nimesikia radioni kuwa nape ataingia kwenye kikao cha neki kama kawaida na kama mjumbe halali, kunamtu anaweza kunitafsiria

Maana yake hajavuliwa uanachama wa UVCCM, maana anaingia NEC kama mjumbe toka UVCCM. Au ndio atakuwa amerudishiwa uanachama wa UVCCM na CC-CCM.
 
Leo asubuhi nimesikia radioni kuwa nape ataingia kwenye kikao cha neki kama kawaida na kama mjumbe halali, kunamtu anaweza kunitafsiria
Nape hajafutwa ujumbe wa nec wala uanachama wa ccm bali kavuliwa uanachama wa uvccm na kuombewa ndani ya chama pia avuliwe nafasi zake za uongozi...hivyo yeye kapoteza nafasi zake za uongozi za uvccm lakini za chama bado anaendelea nazo mpaka hatima yake itakapojulikana baada ya kumjadili kwenye chama.
 
Nape hajafutwa ujumbe wa nec wala uanachama wa ccm bali kavuliwa uanachama wa uvccm na kuombewa ndani ya chama pia avuliwe nafasi zake za uongozi...hivyo yeye kapoteza nafasi zake za uongozi za uvccm lakini za chama bado anaendelea nazo mpaka hatima yake itakapojulikana baada ya kumjadili kwenye chama.

Lakini NAPE si ni mjumbe wa NEC kupitia UVCCM? Kama kavuliwa uanchama wa UVCCM maana yake hata nafasi yake ya ujumbe wa NEC kupitia UVCCM si imefutwa!? More clarification please...
 
Lakini NAPE si ni mjumbe wa NEC kupitia UVCCM? Kama kavuliwa uanchama wa UVCCM maana yake hata nafasi yake ya ujumbe wa NEC kupitia UVCCM si imefutwa!? More clarification please...



Kwani wataliona hilo? Ngoja uone atakavyoingia mtini
 
lakini nape si ni mjumbe wa nec kupitia uvccm? Kama kavuliwa uanchama wa uvccm maana yake hata nafasi yake ya ujumbe wa nec kupitia uvccm si imefutwa!? More clarification please...

hakika hapa ni usanii mtupu, kwani hili halihitaji elimu kujua nini kinaendelea. Yeye nape ni mwakilishi wa uvccm kwenye kikao husika yaani nec, leo kama kweli kavuliwa uanachama wa uvccm inakuaje anakwenda kuwawakilisha hao hao kwenye kikao cha nec????????? Kama mwakilishi wao na wao wamemkataa uwakilishi wake pia ungekuwa batili hapa ni mchezo unachezwa na lengo ni kumzuia mwana mapinduzi wa kweli nape, ambaye ameweka wazi msimamo wake kuwa nchi kwanza chama next, hatma ya mafisadi hakika i ukingoni.....................................
 
hakika hapa ni usanii mtupu, kwani hili halihitaji elimu kujua nini kinaendelea. Yeye nape ni mwakilishi wa uvccm kwenye kikao husika yaani nec, leo kama kweli kavuliwa uanachama wa uvccm inakuaje anakwenda kuwawakilisha hao hao kwenye kikao cha nec????????? Kama mwakilishi wao na wao wamemkataa uwakilishi wake pia ungekuwa batili hapa ni mchezo unachezwa na lengo ni kumzuia mwana mapinduzi wa kweli nape, ambaye ameweka wazi msimamo wake kuwa nchi kwanza chama next, hatma ya mafisadi hakika i ukingoni.....................................



Kama hawajagundua hilo utashangaa mtu anaibia hapa JF anaenda kujifanya yeye ndiye kaliona hilo,hasa kwa watu wa kujipendekeza mpaka wanajiita majina ya Kifisadi.


Hebu tuone kama watamzuia kuwa mjumbe wa NEC. Maamuzi ya kukurupuka na ya Jazba lazima yawe incomplete hivyo.Ubongo haukushirikishwa vya kutosha
 
Lakini NAPE si ni mjumbe wa NEC kupitia UVCCM? Kama kavuliwa uanchama wa UVCCM maana yake hata nafasi yake ya ujumbe wa NEC kupitia UVCCM si imefutwa!? More clarification please...
hio sasa itahitaji marekebisho ya kanuni na katiba ya uvccm.kwa sasa katiba ya ccm inaelekeza sababu za kumvua unec mtu haziusiani na kuondolewa uanachama wa jumuhia....zaidi ya yote kumbuka Nape hakupigiwa kura na umoja wa vijana kuwa mjumbe wa nec bali ni mkutano mkuu wa ccm.
 
hio sasa itahitaji marekebisho ya kanuni na katiba ya uvccm.kwa sasa katiba ya ccm inaelekeza sababu za kumvua unec mtu haziusiani na kuondolewa uanachama wa jumuhia....zaidi ya yote kumbuka Nape hakupigiwa kura na umoja wa vijana kuwa mjumbe wa nec bali ni mkutano mkuu wa ccm.

Alipita kupitia tiketi gani hasa? Naona na wewe akili zimekaa kushoto
 
Fisadi Mtoto,

Asante kwa taarifa. Kweli upo karibu na jiko.

Inamaanisha NAPE basi tena au NEC itaamua?
 
Sumaye amtetea Nape

na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ameeleza kushangazwa na kushtushwa na uamuzi wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana la Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wa kumpokonya uanachama wake, Nape Nnauye.

Sumaye amesema anakusudia kueleza dukuduku lake hilo kuhusu uamuzi huo wa UVCCM wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) inayokutana mjini Dodoma leo.


Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka mjini Dodoma anakohudhuria kikao hicho cha NEC, Sumaye alisema uamuzi wa kumwadhibu Nape wakati akiwa mgombea wa uenyekiti wa UVCCM unaweza kutafsiriwa kuwa ni jitihada za makusudi zilizofanywa na maadui zake kisiasa.


Alisema Baraza Kuu la UVCCM liliingia kwenye kikao hicho likiwa na mambo mawili, mosi kupitisha majina ya wagombea walioomba uteuzi wa nafasi za juu za uongozi wa jumuiya, Nape akiwa mmoja wao, na pili, kushughulikia kauli ya Nape dhidi ya tuhuma alizozitoa kuhusiana na mradi wa ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya UVCCM, kwamba ulikuwa na harufu ya ufisadi.


"Mimi sina hakika sana na haya ninayoyasoma kwenye vyombo vya habari, lakini kama baraza lingeamua kujadili majina, basi lingeshughulika na majina ya wagombea tu, na kama lingetaka kujadili kauli ya Nape kuhusu tuhuma alizotoa, basi lingefanya hivyo, kwani unapozichanganya hoja zote kwa wakati mmoja, lazima watu watahoji, kama ilivyo sasa," alisema Sumaye.


Alisema baraza lilikuwa na uwezo wa kuijadili kauli ya Nape kuhusu ufisadi na kumwita ajieleze, lakini lilisubiri kwa makusudi kuileta hoja hiyo wakati wa kujadili majina, huku likijua fika kuwa yeye ni mmoja wa wagombea.


Akifafanua, alisema ni makosa kwa baraza kumshughulikia kwa tuhuma alizozitoa wakati anagombea, kwani uamuzi huo unaweza kutafsiriwa kuwa umefanywa kwa makusudi na wabaya wake kisiasa.


Alisema hata Mwalimu Nyerere wakati wa utawala wake, mara nyingi alisisitiza kuwa kama kuna mwanachama ana makosa, ni bora ahojiwe na kuadhibiwa na vikao husika, lakini si busara kusubiri wakati wa uchaguzi, ndipo madhambi yake yaibuliwe.


"Ninavyoongea na wewe hapa, ndivyo nitakavyoongea ndani ya kikao cha NEC leo kwa masilahi ya chama chetu, kwani tuna dhamana ya kukilinda na kukitetea," alisema Sumaye kwa kujiamini.


Mbali ya kubeza hatua zilizochukuliwa na UVCCM dhidi ya Nape, Sumaye ambaye ndiye waziri mkuu pekee aliyedumu kwa vipindi viwili mfululizo vya miaka 10, alieleza kusikitishwa kwake na kauli zinazotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba kuhusiana na uamuzi huo.


"Kama kweli Makamba amesema yanayosemwa kwenye vyombo vya habari, maana wakati mwingine magazeti yetu yanaongeza chumvi, lakini kama ni kweli, nadhani hizo si kauli za mtu anayepaswa kuwa kiongozi wa chama chetu," alisema Sumaye bila kutaka kuingia kwa undani juu ya suala hilo.


Vyombo kadhaa vya habari vimemkariri Makamba akisema kwamba, uamuzi wa UVCCM wa kumfuta uanachama wake Nape, hauwezi kuhojiwa na mamlaka yoyote nyingine nje ya jumuiya hiyo ya CCM.


Kauli hiyo ya Sumaye inakuja ikiwa ni siku moja tu baada ya waziri mkuu mwingine mstaafu, Cleopa Msuya, kukaririwa akieleza kushangazwa na uamuzi huo wa UVCCM kumvua uanachama Nape.


Msuya ambaye naye ni mjumbe wa NEC alikaririwa akisema kwamba, uamuzi wa Baraza Kuu la UVCCM kumvua uanachama wake Nape ulifanywa katika mazingira ya jazba.


Kwa mujibu wa Msuya, hakutegemea kabisa kusikia kwamba uamuzi wa namna hiyo ungechukuliwa na vikao vya CCM ya sasa yenye dhamira ya dhati ya kujenga demokrasia ya mtu kutoa maoni.


Kwa maoni yake, Msuya alisema sababu zilizoelezwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Francis Isaac, kuhusu kupokonywa uanachama kwa Nape akidaiwa kusema uongo, ni nyepesi na hazina uzito unaostahili.


Msuya alieleza kushangazwa kwake na uamuzi wa UVCCM kumpokonya uanachama badala ya kumsimamisha uanachama na kutoa fursa kwa vikao vya juu viamue kuhusu majaliwa ya kijana huyo.


Malumbano hayo yanakuja siku takriban nne sasa tangu Nape alipovuliwa uanachama akituhumiwa kusema uongo wakati alipopinga mkataba wa ujenzi wa jengo la UVCCM na hivyo kwenda kinyume cha Kanuni za 17 (C) na18 (B) za jumuiya hiyo ya CCM.


Isaac aliyataja makosa hayo kuwa ni pamoja na kutoa tuhuma nzito kwa viongozi wa juu wa UVCCM, akiwamo Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la UVCCM, Edward Lowassa, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Emmanuel Nchimbi, Isaac mwenyewe na aliyekuwa Katibu Mkuu wa taasisi hiyo, Amos Makala, wote akiwahusisha katika kashfa ya mradi huo.


Isaac alisema licha ya adhabu hiyo, baraza limependekeza kwa chama chao kumvua nyadhifa zote za uongozi alizonazo Nape katika ofisi ndogo ya makao makuu ya chama hicho, Dar es Salaam, uamuzi ambao una nafasi ndogo ya kupata baraka za vikao vya juu vya chama hicho.


Kwa sababu hiyo, iwapo uamuzi wa kumvua Nape uanachama utabakia pasipo kutenguliwa, basi anaweza akajikuta akipoteza sifa za kuendelea kuwa mjumbe wa NEC ya CCM, ingawa nafasi zake nyingine za kimamlaka ndani ya chama hicho hazitokani moja kwa moja na kuwa mwanachama wa UVCCM.


Hata hivyo habari zaidi kutoka mjini Dodoma zinasema kuwa, hoja ya Nape, inaweza kuigawa NEC leo kutokana na misimamo tofauti ya wajumbe.


Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima mjini Dodoma, unaonyesha kuwa kuna wajumbe wanaounga mkono uamuzi wa baraza na kumwona kama Nape amekiuka maadili ya chama kwa kutoa siri za vikao na maoni nje, badala ya kufanya hivyo ndani ya vikao vya chama.


Pia wapo wajumbe waliobeba misimamo kuwa Nape ameonewa na hata kuishawishi NEC kwa hoja ili iweze kutengua baadhi ya maamuzi ya UVCCM.


Jana jioni Kamati Kuu (CC) ambayo pamoja na mambo mengine ilitarajia kuijadili hoja ya Nape, ilikuwa ikiendelea na kikao chake kilichoanza saa 10 jioni, chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete.


Nape amekuwa katika mjadala mzito katika uchaguzi wa UVCCM, kutokana na hatua yake ya kulipua kile kinachoonekana kuwa bomu la ufisadi linalohusu mradi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya umoja huo.


Kwa mara ya kwanza, Nape alitoa hoja yake hiyo saa chache tu baada ya kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo inayompa fursa mshindi kuwa mjumbe wa vikao vya kimaamuzi vyenye nguvu kubwa ndani ya chama hicho tawala, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
 
hio sasa itahitaji marekebisho ya kanuni na katiba ya uvccm.kwa sasa katiba ya ccm inaelekeza sababu za kumvua unec mtu haziusiani na kuondolewa uanachama wa jumuhia....zaidi ya yote kumbuka Nape hakupigiwa kura na umoja wa vijana kuwa mjumbe wa nec bali ni mkutano mkuu wa ccm.


Kwa maana hii basi, mamlaka ya kumwadhibu Nape inabidi itoke kwa wale wale waliomweka pale alipokuwa, kwa maana ya mkutano mkuu!
Kama kuna ufafanuzi naomba nipewe!
 
Nape hajafutwa ujumbe wa nec wala uanachama wa ccm bali kavuliwa uanachama wa uvccm na kuombewa ndani ya chama pia avuliwe nafasi zake za uongozi...hivyo yeye kapoteza nafasi zake za uongozi za uvccm lakini za chama bado anaendelea nazo mpaka hatima yake itakapojulikana baada ya kumjadili kwenye chama.

Nape hajavuliwa anything, isipokuwa UV-CCM wamependekeza kwa CC kuwa avuliwe unachama wa UV-CCM, iwapo CC itakubali basi wao wataipeleka NEC ambao ndio wenye uamuzi wa mwisho kama Nap eavuliwe au hapana, Nchimbi na UV-CCM, hawana hiyo powe rya kumvua Nape anything, ila wana power ya kupendekeza tu ndichi walichofanya so far, Nap ebado ni mjumbe wa NEC na ni mwanachama wa CCM,

- Ila kwa sasa hawezi hudhuria vikao vya UV-CCM, mpaka fate yake itakapoamuliwa na NEC kwa ushauri toka CC, kwa kifupi ni kwamba amesimamishwa kuingia kwenye mikutnao ya UV-CCM tu mpaka umauzi utakapotolea na CC, ambao bado haujatolewa.
 
Mkuu FMES,

Hebu tupe dataz mkuu,Sasa kama Sumaye nae kaamua kusimama na Nape,leo moto utawaka huko ndani.Naona kamlima hata huyo mzee mropokaji Makamba.

Pia inabidi hata Nchimbi nae apigwe biti na kauli zake hizo za 'kiuendawazimu'
 
Mimi nasubiri nione actual action kabla ya kufurahia, maana Nape amenisikitisha kwani imeshadhibitishwa kuwa hule mkataba una matatizo hakusitahili kufukuzwa wakati mkataba una matatizo kweli.

Maana yao ni kwamba hata mwanachama akipata ukweli wa wizi wowote asiseme maana watamfukuza uanachama.
 
Hivi huyu NNAPE hana blog?

Sina hakika na Blog kama anayo lakini ni mmoja wa wasomaji na wachangiaji hapa JF kwani nilibahatika kukutana naye Mwanza wakati tukijadiliana kuhusiana na Kijarida cha Cheche za Fikra alinieleza kuwa naye ni Member hapa.
Ila iwapo utapenda kuwasiliana naye + 255 (0) 786 131977
 
Kutoka Dom; CC imeunda tume kuchunguza mradi wa jengo la vijana, Dk. Kigoda amepewa kazi ya kuongoza tume hiyo, baada ya matokeo yake ndio mbivu na mbichi zitajulikana. CC imekubali kuwa Nape bado ni mjumbe halali wa NEC. Ni kweli kuwa Lowassa na Nchimbi waliwekwa kitimoto katika kikao hicho jana
 
Nape hajafutwa ujumbe wa nec wala uanachama wa ccm bali kavuliwa uanachama wa uvccm na kuombewa ndani ya chama pia avuliwe nafasi zake za uongozi...hivyo yeye kapoteza nafasi zake za uongozi za uvccm lakini za chama bado anaendelea nazo mpaka hatima yake itakapojulikana baada ya kumjadili kwenye chama.

Fisadi Mtoto:Hapa naomba niweke sawa kwa upeo wangu na kwa jinsi ninavyojua NAPE ni mjumbe wa NEC kupitia UVCCM, hivyo kwa mantiki hiyo baada ya kuvuliwa uanachama UVCCM alipaswa kupoteza sifa ya kuwa mjumbe wa NEC, lakini kwa sababu ya umbumbumbu wa Makamba ametangaza kuwa atahudhuria NEC ama ndiko wanakusudia kumfuta na uanachama CCM hivyo ameamua kupindisha kanuni za Chma achake ili wakamchinjie mbali na huko au JK ameamuru aitwe huko ili naye atangaze kumrejesha UVCCM.
 
Fisadi Mtoto:Hapa naomba niweke sawa kwa upeo wangu na kwa jinsi ninavyojua NAPE ni mjumbe wa NEC kupitia UVCCM, hivyo kwa mantiki hiyo baada ya kuvuliwa uanachama UVCCM alipaswa kupoteza sifa ya kuwa mjumbe wa NEC, lakini kwa sababu ya umbumbumbu wa Makamba ametangaza kuwa atahudhuria NEC ama ndiko wanakusudia kumfuta na uanachama CCM hivyo ameamua kupindisha kanuni za Chma achake ili wakamchinjie mbali na huko au JK ameamuru aitwe huko ili naye atangaze kumrejesha UVCCM.

Mongo,

Hapana, maelezo ya FMES ni sahihi, kilichofanyika ni UVCCM wamependekeza kwa CC Nape avuliwe uanachama wa vijana na nyadhifa zake nyingine ikiwemo U_NEC vijana. Mpaka hapo kamati kuu itakapo bariki mapendezo ya UVCCM ndipo atakuwa amevuliwa rasmi uanachama wa UVCCM. In the mean time he still M-NEC vijana. If that make a sense....
 
Back
Top Bottom