Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

nadhani hii shuruba(uoga wa kutoa maamuzi makubwa) anayoipata jakaya ndio itakuwa fundisho kwa wote wenye nia ya kugombea URAIS......URAIS si RAHISI
 
kuna watu watavuliwa uanachama kama the real first strike ya JK... hapo ndipo maandamano yataanza kuzizima!

Mkuu sidhani kama JK anaweza kufanya maamuzi yoyote mazito.Tusitarajie kuona lolote kutoka kwa huyu mkwere.Butiama ilikuwa hivi hivi tukaishia patupu! ikaja ya Dodoma nayo ni ileile patupu na wananchi wakaandamishwa! na sasa hili la Nape nalo si JK labda cheche za wengine lakini siyeye.JK anachotaka ni kumaliza muda wake bila ya kuwa na adui yoyote yule ili aje aishi maisha ya raha na starehe baada ya uraisi.
 
Mkuu sidhani kama JK anaweza kufanya maamuzi yoyote mazito.Tusitarajie kuona lolote kutoka kwa huyu mkwere.Butiama ilikuwa hivi hivi tukaishia patupu! ikaja ya Dodoma nayo ni ileile patupu na wananchi wakaandamishwa! na sasa hili la Nape nalo si JK labda cheche za wengine lakini siyeye.JK anachotaka ni kumaliza muda wake bila ya kuwa na adui yoyote yule ili aje aishi maisha ya raha na starehe baada ya uraisi.

kaka Wembemkali unamjua vizuri Mkwere xxxxx Jamaa hapendi kunyooshewa kidole xxxx mara nyingi hupenda lawama ziwaendee wengine lakini sio yeye xxxxx Nakumbuka alivyoonyeshwa Ripoti ya Mwakyembe,alitoa Go ahead,Lakini baadaye alijifanya kuwa nae alisikia Ripoti ile siku iliposomwa Bungeni xxxxx Tatizo la Mkwere pamoja na Urais wake,lakini wapo wengi anaowaheshimu na kuwaogopa xxxxxxx Kwa kuwa issue hii ya Nape inamuhusisha Lowassa, nawahakikishieni hakutokuwa na jipya......
 
kaka Wembemkali unamjua vizuri Mkwere xxxxx Jamaa hapendi kunyooshewa kidole xxxx mara nyingi hupenda lawama ziwaendee wengine lakini sio yeye xxxxx Nakumbuka alivyoonyeshwa Ripoti ya Mwakyembe,alitoa Go ahead,Lakini baadaye alijifanya kuwa nae alisikia Ripoti ile siku iliposomwa Bungeni xxxxx Tatizo la Mkwere pamoja na Urais wake,lakini wapo wengi anaowaheshimu na kuwaogopa xxxxxxx Kwa kuwa issue hii ya Nape inamuhusisha Lowassa, nawahakikishieni hakutokuwa na jipya......


ya nape inamuhusu lowassa na yeye kwa kuwa these are partners...na anayejenga ni business partner wao....so likely wana share kwenye hilo jengo......

umesema vema kikwete hapendi kuonekana mbaya ...anataka lawama ziwaendee wengine tu!!!
 
Baraza kuu la UVCCM halina ubavu wa kumvua Uanachama wa CCM, nadhani aende mahakamani apiganie haki yake ya kuwa mwanachama. Na Pia nadhani kama kusingekuwa na makaburu waliokuwa wamechoka na ubaguzi ndani ya serikali ya kikaburu mabadiliko huko SA yangekuja kwa kuchelewa sana na watu wengi wangepoteza maisha kwa ajili ya hiyo, vivyo hivyo kwa uhuru wa Tanganyika, haki za wamarekani weusi. Kwa hiyo tunahitaji watu kama akina Nape kubaki Ndani ya Mfumo wa Chukua Chako Mapema ili walete mapinduzi, ndio watakao uangusha huu mfumo unaodondoka.
 
FMES,Kichuguu,....

..hivi msiba wa Mzee Moses Nnauye[r.i.p] ni ulikuwa nyumbani kwa Mzee Makamba?..nilidhani hizi familia mbili zipo karibu sana. ..nilitegemea Mzee Makamba atakuwa ndiye mlezi wa Nape Nnauye katika siasa na CCM.

Mkuu Joka,

Makamba ni mtoto wa mjini, alilikoroga kwenye ujumbe wa NEC, alipojaribu kumtoa Kigoda, kwa njia za kichini chini akitumia jina la Rais, kitendo hicho kilimuudhi sana muungwana, kwa sababu anao maadui wa kutosha hataki kuongeza wengine, na ilikuwa ampuzishe na kumpa Kinana,

Makamba, akaponea chupu chupu baada ya kina Lowassa na Kingunge, na Ra, kumuombea sana kwa muungwana, since then amekuwa under the mercy ya mafisadi, kwa hiyo hapa hata undugu wake na Marehemu Mnauye, hauna nguvu tena maana anajaribu ku-survive kwenye power na wanaoweza kumlinda so far ni kina Lowassa,

Majuzi kwenye CC, Makamba aliingia na hoja ya kutaka wabunge wote wanaokikosoa CCM wachukuliwe hatua, akanyamazishwa kama mbwa na muungwana, lakini bado hasikii tu, sasa ngoja usikie yatakayomkuta tena huko CC!
 
Matamshi ya wajumbe hao yanathibitisha kuwa Lowassa huenda akawekwa kiti moto na kujikuta kwenye wakati mgumu kunusuru nafasi yake kisiasa ambayo tangu mwaka 2008 uanze amekuwa akiporomoka toka nafasi ya uwaziri mkuu hadi Mbunge baada ya kuwajibika kutokana na makosa ya baadhi wa maofisa serikalini juu ya mkataba wa ufuaji wa umeme wa dharura wa kampuni ya Richmond. [/B]


1. Makamba majuzi kwenye CC alitaka wabunge wanaokosoa CCM waadhibiwe, akatukanwa kama mbwa na muungwana.

2. Nipashe wakasema Nape amekaangwa na mkataba wa jengo umepita, muungwana akamtwangia waya mengi kutaka kujua nani aliyewapa hizo habari wanazoziiita za CC,

-Muungwana akawalazimisha kuzifuta na kuomba masamaha na pia kumtaja aliyewapa hizo habari, they did kwamba ni Nchimbi anayewapa habari.

3. Muungwana akawapandisha kuwa mawaziri kamili washikaji wote wa Nchimbi kasoro Nchimbi tu!

4. Muungwana akairukia ishu ya jengo, hata kabla haijapitia vikao vyake kikatiba na kutafuta mawakili wa kuuchunguza mkataba, ambao taayari wameifahamisha CC majuzi kwa maandishi kuwa mkataba ni ufisadi! Na kila mjumbe anayo nakala!

5. Muungwana akamuamuru Nchimbi kwenda Dodoma, haraka kukutana UV-CCM ili waamue kuhusu jina la Nape! Yeye akaenda kupendekeza Nape afukuzwe uanachama!

Now ni vipi mafisadi wanaweza ku-pull this one up mbele ya macho yetu wote wananchi, my reading ni kwamba hakuna mtandao tena ila kuna kundi jipya la mafisadi likiongozwa na Lowassa, yeye mwenyewe ana wasi wasi mkubwa sana mpaka ameshatayarisha alternative ya mtu kuchukua nafasi yake kuliongoza hilo kundi incase something happens to him, swali kama what? Na Kwa nini ana wasi wasi hivi?

Mara ya mwisho muungwana alikuwa Lusaka, akaambiwa kuhusu kusimamishwa kwa Zitto bungeni na matokeo yake jinsi Zitto alivyojengeka kisiasa in one night, alipouliza nani anahusika akaambiwa Lowassa, kwa hasira tena akifoka sana alisema this should be an end to mtandao, the next step mamvi akapandsihwa ndege ya uchumi, waliomuona muungwana kwenye kikao cha CC majuzi wanasema hakuwa yeye wa kawaida,

Hivi karibu nimekuwa nikitumiwa ujumbe mwingi sana in private mzito kuhusiana na thread ya Nape na UV-CCM, tumetumia kila njia kuzi-trace hizo message zinakotoka, mpaka kwenye makampuni ya simu bongo, lakini ni dead end,

Mkuu Mamamia, ninajaribu kuamini kuwa muungwana anwaogopa mafisadi na haweiz fanya kitu, lakini my instinct inakataa kabisaa kwa hiyo nimeamua kuyaaminia maneno yako kuwa kuna moto utawaka huko.... lakini..... I do not know nina feeling kuwa uzi wa mwisho wa mtandao huenda ukakatwa this time, ikawa kila mtu na lwake!

Mtandao uliisha siku nyingi, ilichobaki ni official announcement na ninaamini inakuja this time, I mean mafisadi wakiweza ku-pull this one basi 2010 wametinga, maana huu ndio mtihani wa mwisho kwa muungwana, na believe me analijua hilo, tena sana.
 
Nape Nnauye: Nchi yasubiri maamuzi mazito CCM-NEC Dodoma

Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
Date::9/9/2008


HATIMA ya mwanasiasa kijana, Nape Nnauye na jina la mgombea wa ubunge ya jimbo la Tarime Mjini ndio mambo yanayotarajiwa kukuna vichwa vya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) baada ya vichwa 39 vya Kamati Kuu kujadili jana hadi usiku wa manane.

Hakuna uamuzi uliotangazwa jana baada ya Kamati Kuu, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kujadili masuala hayo, pamoja na agenda nyingine za NEC kwa vipindi viwili, cha kwanza kikianza saa 9.00 alasiri na kingine saa kikianza saa 3:00 usiku.

"Wameamua kupumzika kwa ajili ya futari na tumeambiwa kuwa watakutana tena saa 3:00 usiku kuendelea na kikao cha maandalizi ya NEC," alisema mmoja wa wafanyakazi kwenye jengo la CCM Makao Makuu mjini Dodoma.

Rais Jakaya Kikwete aliwasili Dodoma jana mchana na aliingia kwenye chumba cha mkutano, akiwa na lundo la nyaraka, hali iliyoonyesha kuwa kikao hicho kilikuwa na shughuli kubwa ya kujadili kabla ya kuyasukumia masuala hayo moto kwenye kikao cha leo.

Katika kile kinachoonekana kuwa ni kumalizana na ajenda nyepesi, awamu ya kwanza ilijadili hali ya kisiasa na uteuzi wa mgombea wa kiti cha ubunge cha Tarime Mjini, kwa mujibu wa taarifa toka CCM.

Waandishi waliruhusiwa kuchukua picha za ufunguzi wa kikao hicho na baadaye kutolewa nje, kabla ya kikao hicho, ambacho maamuzi yake yanasubiriwa kwa hamu, kuanza.

Kamati Kuu, ambayo kwa kawaida hupanga ajenda za NEC na kuwasilisha mapendekezo, hoja na hatua mbalimbali ambazo huamuliwa na halmashauri hiyo yenye wajumbe zaidi ya 130, ilitarajiwa kujikita zaidi katika suala la Nape, ambaye anagombea uenyekiti wa UVCCM, lakini akakumbana na kikwazo kikubwa toka Baraza Kuu.

Nape, mtoto wa mwanasiasa wa zamani wa CCM, Moses Nnauye, ndiye anayevuta hisia za wengi baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), kupendekeza kijana huyo avuliwe nyadhifa zote ndani ya chama, akidaiwa kukiuka kanuni za umoja huo kwa kukikosoa chama hadharani.

Nape anadaiwa kusema uongo na kutoa siri za vikao vya chama baada ya kuweka hadharani utata katika mkataba wa uwekezaji katika Jengo la Makao Makuu ya umoja huo na kumtuhumu mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini, Edward Lowassa, mwenyekiti wa UVCCM, Dk Emmanuel Nchimbi na aliyekuwa katibu mkuu wa umoja huo Amosi Makala, ambaye sasa ni mweka hazina wa CCM.

Ingawa uamuzi wa kumsimamisha Nape katika umoja huo umepingwa na kulaaniwa na watu wa kada mbalimbali wakiwemo wasomi, wanasiasa na baadhi ya wanachama wa UVCCM, wachambuzi wa mambo wanasema kunusurika kwake litakuwa jambo gumu ‘mithili ya ngamia kupita kwenye tundu la sindano'.

Wachunguzi hao wanasema msimamo wa baadhi ya wazee wa chama hicho kupitia kauli zao za hivi karibuni na ile ya Dk Nchimbi aliyeongoza vikao vya awali vya UVCCM vilivyotoa maamuzi dhidi ya Nnauye, na Makamba, ambaye ndiye mtendaji Mkuu wa chama hicho, unaashiria kuwa uwezekano wa Nape kuendelea na harakati zake ndani ya umoja huo mdogo mno, ingawa bado bado kuna nguvu ya Mwenyekiti Kikwete.

"Baraza Kuu halina ubavu wa kunitimua," alisema Nape juzi baada ya uamuzi huo uliofanywa mwishoni mwa wiki. "Nina imani na vikao vya juu vya maamuzi na nina imani na chama. Nina imani kuwa vikao vya juu vitafanya maamuzi na kunirudishia haki yangu."

Imani ya Nape kwa NEC ilithibitishwa na mjumbe wa halmashauri hiyo, Cleopa Msuya, ambaye ni waziri mkuu wa zamani, aliyekaririwa jana akisema kuwa uamuzi wa Baraza Kuu la UVCCM ulikuwa wa jazba na hivyo anasubiri aone nini kilifanyika.

Hata hivyo, wachambuzi wa siasa za CCM wanasema kwa jinsi wajumbe walinaompinga Nape walivyojipanga, inaonekana kuwa nguvu ya ushawishi ya wajumbe wanaomuunga mkono inaweza kuwa ndogo na hivyo kuwa katika uwezekano wa kuadhibiwa vikali na NEC.
 
1. Makamba majuzi kwenye CC alitaka wabunge wanaokosoa CCM waadhibiwe, akatukanwa kama mbwa na muungwana.

2. Nipashe wakasema Nape amekaangwa na mkataba wa jengo umepita, muungwana akamtwangia waya mengi kutaka kujua nani aliyewapa hizo habari wanazoziiita za CC,

-Muungwana akawalazimisha kuzifuta na kuomba masamaha na pia kumtaja aliyewapa hizo habari, they did kwamba ni Nchimbi anayewapa habari.

3. Muungwana akawapandisha kuwa mawaziri kamili washikaji wote wa Nchimbi kasoro Nchimbi tu!

4. Muungwana akairukia ishu ya jengo, hata kabla haijapitia vikao vyake kikatiba na kutafuta mawakili wa kuuchunguza mkataba, ambao taayari wameifahamisha CC majuzi kwa maandishi kuwa mkataba ni ufisadi! Na kila mjumbe anayo nakala!

5. Muungwana akamuamuru Nchimbi kwenda Dodoma, haraka kukutana UV-CCM ili waamue kuhusu jina la Nape! Yeye akaenda kupendekeza Nape afukuzwe uanachama!

Now ni vipi mafisadi wanaweza ku-pull this one up mbele ya macho yetu wote wananchi, my reading ni kwamba hakuna mtandao tena ila kuna kundi jipya la mafisadi likiongozwa na Lowassa, yeye mwenyewe ana wasi wasi mkubwa sana mpaka ameshatayarisha alternative ya mtu kuchukua nafasi yake kuliongoza hilo kundi incase something happens to him, swali kama what? Na Kwa nini ana wasi wasi hivi?

Mara ya mwisho muungwana alikuwa Lusaka, akaambiwa kuhusu kusimamishwa kwa Zitto bungeni na matokeo yake jinsi Zitto alivyojengeka kisiasa in one night, alipouliza nani anahusika akaambiwa Lowassa, kwa hasira tena akifoka sana alisema this should be an end to mtandao, the next step mamvi akapandsihwa ndege ya uchumi, waliomuona muungwana kwenye kikao cha CC majuzi wanasema hakuwa yeye wa kawaida,

Hivi karibu nimekuwa nikitumiwa ujumbe mwingi sana in private mzito kuhusiana na thread ya Nape na UV-CCM, tumetumia kila njia kuzi-trace hizo message zinakotoka, mpaka kwenye makampuni ya simu bongo, lakini ni dead end,

Mkuu Mamamia, ninajaribu kuamini kuwa muungwana anwaogopa mafisadi na haweiz fanya kitu, lakini my instinct inakataa kabisaa kwa hiyo nimeamua kuyaaminia maneno yako kuwa kuna moto utawaka huko.... lakini..... I do not know nina feeling kuwa uzi wa mwisho wa mtandao huenda ukakatwa this time, ikawa kila mtu na lwake!

Mtandao uliisha siku nyingi, ilichobaki ni official announcement na ninaamini inakuja this time, I mean mafisadi wakiweza ku-pull this one basi 2010 wametinga, maana huu ndio mtihani wa mwisho kwa muungwana, na believe me analijua hilo, tena sana.

Je, haya yote uliyoandika hapa ni kweli ndugu yangu?

Mbona yanatia raha ingawa raha yenyewe inakuwa way too late.
 
kaka Wembemkali unamjua vizuri Mkwere xxxxx Jamaa hapendi kunyooshewa kidole xxxx mara nyingi hupenda lawama ziwaendee wengine lakini sio yeye xxxxx Nakumbuka alivyoonyeshwa Ripoti ya Mwakyembe,alitoa Go ahead,Lakini baadaye alijifanya kuwa nae alisikia Ripoti ile siku iliposomwa Bungeni xxxxx Tatizo la Mkwere pamoja na Urais wake,lakini wapo wengi anaowaheshimu na kuwaogopa xxxxxxx Kwa kuwa issue hii ya Nape inamuhusisha Lowassa, nawahakikishieni hakutokuwa na jipya......


Mwawado, unataka kusema kuwa JK anamwogopa sana Lowasa? Mbona alimtapisha uwaziri mkuu kiulaini tu?
 
Jamani hakuna mwenye taarifa za CC ya CCM?

JF vipi wakuu mliopo jikoni tupeni taarifa
 
Jamani hata breakfast sijapata.niko jamvini nasuburi taarifa ya CC huko dodoma.vp wakuu bado tu?Maana uamuzi wa hapa ndo kioo cha either nchi hii ni kwa ajili ya wazalendo WATANZANIA au kwa ajili ya MAFISADI.
 
Amekwisha na Lowassa amepanda na sasa anafaa kuwa RAIS WETU na Nape akamatwe na kuswekwa ndani huku wafadhili wetu kina Jeetu Patel, Yussuf Manji, Johnson Lukaza na wenzao watuchangie kufanya maandamano ya kuipongeza kwa uamuzi wa kishujaa na kihistoria kumteua Zuma wetu Lowassa



mh!!! naona wale wale .....hii ni udaku tu.
Ni jambo la kufikilika..........
 
Mwawado, unataka kusema kuwa JK anamwogopa sana Lowasa? Mbona alimtapisha uwaziri mkuu kiulaini tu?

Mwalimu Kichuguu,Ukweli wa mambo ni kwamba Mh.Lowassa alikosea hesabu mwenyewe alipotamka Bungeni kuwa "Nimegundua kuwa kuna watu wananionea wivu kwa sababu ya huu Uwaziri Mkuu,kama sababu ni huu uwaziri Mkuu,basi Mheshimiwa Spika na Wabunge,Leo natangaza rasmi naachia ngazi".Mwisho wa kunukuu..

Mheshimiwa Lowassa aliyasema maneno haya kwa Hasira,na alijua wazi kuwa Mh.Jakaya atakataa ombi lake la kujiuzulu Uwaziri Mkuu.Pamoja na ujanja wake wote alishindwa kujua kuwa Mh.Rais alikuwa anamtafutia sababu ya kumuondoa kwenye nafasi ya Uwaziri Mkuu,kwa sababu kuna Taarifa nyingi zilikuwa zinamueleza Kikwete kwamba, Lowassa anautumia uzembe/uzubavu wa Kikwete kutafuta umaarufu kisiasa.

Kwa maelezo hayo nafikiri utaona kuwa EL alibugi step mwenyewe,kwani Kikwete hakuzungumza nae,bali alitumia presidential pen kuweka saini kwenye Taarifa ya EL kuhusu kujiuzulu .Maelezo ya Rais yalikuwa kama ifuatavyo "Kwa masikitiko makubwa nakubali Waraka wako wa kujiuzulu,JK".
 
Jamani hata breakfast sijapata.niko jamvini nasuburi taarifa ya CC huko dodoma.vp wakuu bado tu?Maana uamuzi wa hapa ndo kioo cha either nchi hii ni kwa ajili ya wazalendo WATANZANIA au kwa ajili ya MAFISADI.
Ni kweli tulichelewa kupata taarifa kamili ya kilichijiri jana kwenye kamati kuu kwa kuwa kikao kilianza muda wa saa tisa mchana na kuendelea mpaka muda wa kufturu.then kikaahilishwa na kuendelea tena saa tatu usiku.ajenda zilizokuwepo ni pamoja na ubunge tarime,nafasi 30 za udiwani,taarifa za kazi,na jengo la umoja wa vijana...kama nilivyosema awali na kupingwa vikali na FMES ajenda ya Nape kwakweli haikuwepo kabisa na ila watu kama wawili walichangia hoja hio kwenye mengineo.....ajenda ya jengo la uvcm ilipitishwa na wajumbe wameafiki kuwa mkataba uendelee bila kipingamizi chochote kile.
 
Sasa kumbe na wewe unachukua taarifa kutoka mtaani,mbona ulijifanya uko jikoni?
 
Kwa hiyo wamebariki ujenzi wa jengo la UVCCM? Maana yake ni Lowassa kapeta na Nape hana chake tena!!?
 
Sasa kumbe na wewe unachukua taarifa kutoka mtaani,mbona ulijifanya uko jikoni?

ata kama niko jikoni haimanishi naweza kupata taarifa ata kabla hazijazungumzwa kwanza.utakuwa ni uzushi....ajenda iliongelewa saa tano usiku.
 
Kwa hiyo wamebariki ujenzi wa jengo la UVCCM? Maana yake ni Lowassa kapeta na Nape hana chake tena!!?


Sasa JK naye sijui nimfikirie vipi huyu mkuu,au nae alipokiri kuna utata aliropoka? Si na yeye atimuliwe basi?
 
Back
Top Bottom