Nnauye anasema mambo mazito mahala pasipo! Namhurumia kwamba kwa kauli zake hizi, na kwa kawaida ya CCM, tayari ameshakwama.
Ila madai yake mengine pia ni mepesi kidogo; kusema kwamba Lowasa amefanya ufisadi kwenye hilo jengo kwa kuwa tu ni mwenyekiti wa bodi ya udhamini kunatia shaka umakini wake huyu bwana mdogo. It is very easy these days to make sweeping statements so that you are also seen to be hating or even fighting ufisadi. But such statements, as much as they may boost our politicians' popularity, they don't add any value to the real war against ufisadi!
Mimi tangu mwanzo mara baada ya kusoma habari ya shutuma alizozitoa Bwana Nape Mnauye(MNEC),nilijawa na mshangao mkubwa. Nikajaribu kuweka bayana baadhi ya madukukuduku yaliyokuwa kichwa changu kufuatia hatua hiyo. Sasa kuna watu humu wameshabikia sana na kungana mkono hatua hiyo ya bwana Nape kumwaga radhi hadharani lakini bila ya kutafakari kwa kina athari zake baadaye pindi ikithibitika kwamba tuhuma hizo si za kweli.
Sasa,hilo halikunisumbua sana maana nafahamu kwamba kwa kawaida kila ngoma ina wafuasi wake.Na ndio maana wala sikuhangaika kuanza kupoteza muda kujibishana na watu ambao ama ni kwa hulka ya kupenda ubishi na kupenda malumbano am ni kwa ufinyu wa upeo wa kuweza kutafakari mambo kwa umakini.
Sasa mkuu umeonesha hofu yako kwamba, kwa kawaida ya CCM tayari kijana ameshakwama. Lakini mimi naomba niseme, hapa wala sio suala la kawaida ya CCM.Unajua binadamu yeyote anapenda heshima na kuthaminiwa utu wake. Sasa inapokea kwamba unataka kumshambualia binadamu mwenzio na hivyo kupelekea kuudhalilisha utu na heshima yake,basi ni lazima uwe umejiridhisha na madai yako.La sivyo,unaweza kujikuta unaishia mahali pabaya.Tukumbuke,sheria ni msumemo pindi ikichukua mkondo wake.Haingalii upande mmoja.Sheria inatenda haki.
Baada ya kusikia majibu ya uongozi wa UVCCM na CCM kufuatia madai mazito ya bwana mdogo Nape,kwa ufahamu wangu nimegundua kamba bwana Mnauye hakuwa amejiridhisha vya kutosha kiasi cha kuamua kuvurumusha makombora yake hadharani. Inaonekana wazi kwamba hakuwa anajua undani hasa wa mchakato wa mkataba wa mradi zaidi ya kujua mchanganuo wa mradi/mpango wa biashara pekee. Matokeo yake sasa inaonekana dhahiri kwamba Nape alikurupuka kwenda mbele ya waandishi wa habari kushusha tuhuma ambazo kimsingi anaonekana kuwa hana ushahidi wa kutosha kufikia kuwaita viongozi hao ni mafisadi na kuwataka kuwajibika.
Sasa hii ni hatari sana kwa mustakabali wake wa kisiasa,kijamii na kimaisha pia.
Majibu ya UVCCM na CCM yanaeleza kuwa mkataba haujasainiwa.Ni kwamba upo kwenye mchakato tu mpaka Kamati Kuu ya CCM itakapoubariki.Kwa maana nyingine ni kwamba,kama Kamati Kuu haitajiridhisha na mkataba huo (pengine kwa mtazamo sawa na wa bwana Nape),ni wazi kwamba itausitisha ama kutoa agizo ufanyiwe marekebisho.
Sasa swali kubwa hapa, je pupa gani zilizomfanya bwana Nape kwenda kutoa hukumu mbele ya umma ili hali kumbe hata mkataba wenyewe haujasainiwa na zaidi ni kwamba hata Kamati Kuu haijatoa baraka zake kwa mradi husika?.Mimi hapa kwa kweli ninapata wasiwasi juu ya umakini wa bwana mdogo huyu. Kama Mkuu pia ulivyoonesha wasiwasi wako juu ya umakini wake.Ninatilia shaka pia ukomavu wake kisiasa.
Ninakumbuka sana kuwa mwaka 2002 pale Chimwaga, Nape alipata kura, tena nyingi tu za kumuwezesha kuwa na mjumbe wa NEC kupitia vijana kwa sababu tu ya huruma ya wajumbe Mkutano Mkuu. Huruma ambayo ililenga kumuenzi marehemu baba yake Mzee Moses Mnauye. Nilikuwapo ukumbini siku akiomba kura. Hakuwa na rekodi yoyote ya uzoefu wa uongozi ndani ya UVCCM na CCM. Hata wakati wa kuomba kura kwa wajumbe ,Nape hakuwa na hoja ya ushawishi zaidi ya kusema kwamba kalelewa ndani ya chama.
Hilo halikuwa tatizo sana,maana naelewa kuwa kila mtu anahitaji mahali pa kuanzia ili kuweza kijifunza na kupata uwezo wa jambo husika.Lakini inasikitisha kwamba kwa kipindi chote ambacho amekuwa kwenye siasa,hajaweza kukomaa kisiasa.Sifahamu ni hoja gani alizojenga kuwashawishi wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka jana pale Kizota kuweza kumchangua kwa mara nyingine kuwa MNEC maana sikuwepo kwenye mkutano huo.
Na kama anatumiwa na watu fulani kuwa mkodo wa kupitishia hoja zao kwa malengo na maslahi yao binafsi kwa sababu fulani fulani,basi hiyo inakuwa ni bahati mbaya sana kwake.Hakika hao watu watakuwa hawamtakii mema. Anahitaji ushauri nasaha wa kisiasa.
Sasa hatari ninayoiona mbele ya bwana mdogo Nape ni kwamba, kwanza kabisa ajiandae kifikishwa mahakamani. Nina hofu kuwa bila shaka yoyote aliowatuhumu mbele ya waandishi wa habari,hawatamuacha hivi hivi. Amefanya kosa kubwa sana na la mwaka kujitumbukiza kwenye mdomo wa mamba. Na bahati mbaya ni kwamba,kwa namna suala lenyewe lilivyo,sioni namna yoyote kwa Nape kushinda kesi hiyo pindi ikifunguliwa na wahusika. Wanaweza kuja na madai ya kutaka kulipwa mabilioni ya pesa kwa kuwachufulia majina yao.Na yeye hana uwezo huo,je hatma yake itakuwaje? Namsikitikia sana!
Lakini pia nina mashaka kama azma yake ya kugombea nafasi aliyoomba itatamia.Nahisi haitamia si tu kwa kuwa katoa shutuma nzito kwa uongozi wa UVCCM na CCM bila kuwa na ushahidi wa kutoshawa kuwaita watuhumiwa ni mafisadi, bali ni kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za UVCCM na CCM kwa ujumla. Katika kanuni za uchaguzi kuna kipengere kinachomzuia mwanachama ambaye ana kesi mahakamani kugombea nafasi yoyote ya uongozi. Sasa kama nalivyosema awali, endapo kesi itafunguliwa dhidi yake, basi moja kwa moja ni wazi kwamba hataruhusiwa kugombea kwa mjibu wa kanuni.
Sasa najua kama kawaida wako watakaosema,hata asipogombea kama kulipua bomu keshalipua. Ni sawa kabisa. Maana katika maisha si kila anayekuchekea nakupenda. Lakini hata vitani upaporipua bomu nia ni kumdhuru adui yako.Sasa kama bomu ulilolipua linakudhuru mwenyewe, sioni kama hiyo ni akili, hasa kwa binadamu ambaye akili zake ziko sawasawa.
Vita dhidi ya ufisadi ni muhimu sana kwa maslahi ya taifa. Na ni lazima ipiganwe kwa nguvu zote. Lakini kama zilivyo vita zingine. Ungalifu na umakini katika mapambano ndio silaha bora sana. Mnaweza kuwa na silaha nzito nzito ,lakini kama hamkuwa waangalifu na makini katika kupanga mashambulizi mnaweza kabisa kushindwa kufikia malengo ya vita husika, ambayo ni ushindi dhidi ya adui.