Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Hivi sasa nchi imefika pabaya, Chama Tawala nacho kimefika pabaya kiasi kwamba kinaonyesha wazi-wazi kukumbatia maovu! Wanatakiwa watu jasiri kuweza kuonyesha kidole bila woga. Wazee wa CCM wamekaa kimya labda nguvu za ujasiri zimewaishia. Vijana wa CCM ambao wana uchungu wa dhati na wanalitakia mema taifa lao na Chama chao wanapaswa kusimama imara na kuunga mkono mwenzao anayeonyesha ujasiri wa kupambana na uovu uliopo. Hata kama Nape anafanya kampeni za kuutaka uenyekiti wa UVCCM, ameonyesha ujasiri mkubwa. Nape ni jasiri. Anastahili pongezi maana ni wachache wanaoweza kujitokeza na kuwanyooshea vidole watu 'wanaoogopwa' kwa mengi!
 
Mkataba haujapitishwa lakini njemba imeshaleta vifaa vya ujenzi!!! Kishahakikishiwa na Makamba na mafisadi wenzake usiwe na wasiwasi tutasaini tu mkataba huu na si ajabu kishachukuwa mshiko wake wa kifisadi!!! Nape kama unasoma hapa kaza uzi wa kupambana na mafisadi ndani ya CCM usiogope lakini uwe mwangalifu maana hawatasita hata kidogo kukutoa roho ili watimize ufisadi wao.
 
Vijana wa CCM ambao wana uchungu wa dhati na wanalitakia mema taifa lao na Chama chao wanapaswa kusimama imara na kuunga mkono mwenzao anayeonyesha ujasiri wa kupambana na uovu uliopo. Hata kama Nape anafanya kampeni za kuutaka uenyekiti wa UVCCM, ameonyesha ujasiri mkubwa. Nape ni jasiri. Anastahili pongezi maana ni wachache wanaoweza kujitokeza na kuwanyooshea vidole watu 'wanaoogopwa' kwa mengi

Hapa tupo ukurasa mmoja, bravo mkuu!
 
Nape kama unasoma hapa kaza uzi wa kupambana na mafisadi ndani ya CCM usiogope lakini uwe mwangalifu maana hawatasita hata kidogo kukutoa roho ili watimize ufisadi wao.

Bwana Mdogo nafikiri anakagua sana mitandao akiwa huko shuleni kwake India. Ndio maana kupambana na ufisadi akakuweka mbele mbele kama agenda yake kwenye uchaguzi. Bila shaka atashinda kiulaini kama hawatamtoa roho.
 
TATIZO NDANI YA UVCCM NI NCHIMBI: elimu ndogo (kazi kununua digrii za Ph.D wakati ana Diploma tu ya Mzumbe), ushamba (kipofu kaona mwezi!), ufisadi (ni errand boy wa Rostam, Lowassa na Karamagi na usanii wa kuact as if ni msomi kumbe hata kuandika jina lake ni taabu.
 
Unajua kila ninapsoma post zako ninasikia kutapika, mtu mzima unapokuwa kama mtoto mdogo, hivi unachohangaikia ni nini hasa? Hivi huoni aibu?

Exactly unachoweza kufanya ni nini? Nape ni mjumbe wa NEC, hivi kweli wewe una ndoto hata siku moja kufikia huko? Yaani wewe unayehangaika kutoka majuu lkumfuata Malecela Dodoma, wakati hata kwenu hujaenda kuona ndugu zako leo una ubavu wa kusema haya?

Mijitu mingine bwana yaani hovyo! Nape anaondoka huyo, hakuna cha nani wala nani, kuna watu wengi tu tunaomuunga mkono, sasa tumesubiri aguswe tu na mafisadi uone mtoto utakaowaka, unafikiri amemka tu na kusema?

Subiri uone, ila next time usiniingize kwenye maneno yako ya choooni, nilishakuambia siku nyingi sana kuwa nilishakudharau siku nyingi sana, sasa nashangaa kwamba bado tu jina langu, la Malecela, na mama kilango hayakutoki mdomoni vipi mkuu?

Mkuu Kitila,

tunahitaji vijana imara kama huyu bwana mdogo, it is about time ukampa nafasi na yeye aonyeshe vitu vyake kwa taifa letu.

Ahsante mkuu!
Sijapata kumuongelea mama yenu mpendwa ana kilango,kwa kuwa siongeleagi watu wajinga....Wewe ni kati ya wanaomdanganya Nape kuwa alipuke nao watamsaidia.nilipata kusema hapo nyuma kuwa ata kwa muujiza Nape hawezi jina lake kurudi kwa uenyekiti wa uvccm...leo narudia tena kwa faida yako na wengine wote wasio na jazba kama wewe....jina la nape haliwezi kurudi ata iweje...why?kwanza amekosea sana kutukana wenzie kuwa ni mafisadi ata kama ana hoja,kila kitu kina wakati wake wa kusema,kuwahi kwake kutamzuia kufika popote....pili ni wazi kuwa kanuni inasema mgombea uenyekiti ni lazima awe chini ya miaka 35 anapomaliza muhula wake.Nape kazaliwa mwaka wa 1977.leo ni 2008.ata mtoto wangu nikimpa hesabu hio nyepesi ni wazi kuwa Nape kavuka umri.....mimi nasema jina la Nape likipitishwa na kamati kuu ya m naenda mahakamani kuusimimisha.maana watakuwa wamevunja kanuni iliotuzuia wengi kuchukua form.na nitawashinda na atazuiwa kugombea.
 
TATIZO NDANI YA UVCCM NI NCHIMBI: elimu ndogo (kazi kununua digrii za Ph.D wakati ana Diploma tu ya Mzumbe), ushamba (kipofu kaona mwezi!), ufisadi (ni errand boy wa Rostam, Lowassa na Karamagi na usanii wa kuact as if ni msomi kumbe hata kuandika jina lake ni taabu.
Nashauri jina lako umalizie na herufi "o" mwishoni ndio litatoa maana yako halisi.....tumuongelee Nhimbi kama Nchimbi maana tukianza kuongelea kuwa ana Diploma tu au la sio issue hapa kwa kuwa tuna wachangiaje wengi hapa watajiona wamekuwa offended kwa kuwa wao pia hawana....Nchimbi siyo mshamba,vigezo gani umetumia wewe wa mjini,ni mwanasisa mjanja ambaye hajapata kukosea karata zake,ameutawala uvcmm kwa miaka kumi sasa.nani aliweza?walishindwa wengi sana.Anaweza kampeni za wananhi na za ndani ya chama pia na ndio maana alishinda kwa kishindo ubunge wa songea mjini.na wala msiombe afanye maamuzi ya kumpinga Nape kwa kuwa kitakuwa ni kimbunga ambacho Nape kamwe hatokimudu.
 
Unajua kuna vitoto vinajaribisha viatu vya baba zao! nepi hata akiroga kama ac hawezichaguliwa, kwanza kijeba anataka kupitia mlango wa jikoni! na uchaguzi ujao anatupwa nje ya nec.
 
au mafisadi ndani ya Chama Cha Mafisadi wataulazimisha uendelee pamoja na kuwa hauna maslahi kwa UVCCM?

Date::7/21/2008
Hatima ya jengo la vijana CCM yasubiri Kamati Kuu
Na Kizitto Noya
Mwananchi

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hatma ya mgogoro wa jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) itajulikana baada ya mkutano wa Kamati Kuu utakaofanyika Julai 29 na 30, mwaka huu.

Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hiza, alisema jana kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, atawasilisha nyaraka za Baraza Kuu la UVCCM zilizoridhia mkataba wa jengo hilo ingawa baadhi ya wajumbe wa baraza hilo wamekana kupitisha mkataba huo.

"Makamba ametoka na hatarajii kurudi, lakini kama shida yako ni hiyo, hatma ya mgogoro huo itajulikana wakati wa mkutano wa Kamati Kuu ambako Makamba atawasilisha nyaraka za mkutano wa Baraza Kuu ulioridhia mkataba huo," alisema Tabwe.

Kuhusu uwezekano wa Makamba kuacha mpango wa kuwasilisha suala hilo kwenye kikao hicho kwa sababu limeingia dosari, Tambwe alisema kwa utaratibu Katibu Mkuu hawezi kuacha kufanya hivyo ni kuzuia mchakato mzima.

Alisema kimsingi suala hilo lazima litajadiliwa katika kikao hicho na iwapo kuna utata kama inavyojitokeza sasa, utajulikana na uamuzi mbadala kutolewa.

Kauli ya Tambwe imefuatia kauli ya baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu la UVCCM kwamba Makamba amedanganywa kuhusu suala zima la ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Jumuiya hiyo unaoendelea jijini Dar es Salaam.

Wajumbe hao ambao pia ni wenyeviti wa vijana wa mikoa ya Tanzania bara na visiwani, walisema Baraza la Wadhamini limemdanganya Makamba kwamba limefikisha suala hilo Baraza Kuu na kujadiliwa.

Wakizungumza siku chache baada ya Makamba kutoa tamko la suala hilo na kulitetea, wajumbe hao walisema hakuna kikao chochote cha Bazara Kuu la UVCCM kilichokaa kulijadili na kufikia muafaka.
 
Ikiabainika viongozi hasa watendaji wa jumuiya kwa maana ya katibu mkuu na naibu kwa kushirikiana na mwenyekiti wamelidanganya body ya wadhamini mana yake hatua za kinidhamu zitafuata na mkataba ni lazima utasitishwa kwani utakuwa haukufuata taratibu za jumuiya na ni kosa kwa viongozi watendaji kugushi muhtasari au kuleta taarifa za uongo kukidanganya kikao cha juu ili ku- ifluence maamuzi. Kwa ufupi kibainika mkataba au makubaliano hayana budi kutenguliwa na process zianze upya kwenye vikao vyote.

Aidha mze makamba yeye amelazimika kutumia taarifa ya body ya wadhamini ila sasa itabidi awe makini kuelewa nani anasema kweli viongozi watendaji wa vijana au baraz kuu la vijana na pia kuona nani mwenye mamlaka kati ya baraza kuu la vijana na body ya wadhamni kwa mujbu wakanuni ambayo huidhinishwa na baraza kuu la vijana na inafanya kazi kwa maslahi ya jumuiya
 
It's nice of you to join ufisadi fight, its a long battle which we as Tanzanians have to win, its a very tough fight but we ave to fight and fight to win not just a fight.

be brave and smart enough not to loose truck, election should make you come closer and not otherwise.
but corruption must be fought at all cost.

Wazee wansema usijaribu kuua tembo kwa ubua.
 
Ridhiwani hafai, atapeleka chama pabaya, hivi akikosea mwenyekiti wa chama ccm (rais kikwete) na ambaye ni baba yake ataweza kumwajibisha? Tusipeleke nchi pabaya, hapa pabaya tulipo panatosha.
 
hilo jengo la uvccm na mengine ni mali ya watanzania wote, tulichangia kabla ya kuanza kwa vyama vingi. jambo la maana yangerudishwa serikalini kwanza. ndo tuanze na akina lowasa na wengine
 
Bwn Tom,

..........sitaki kuamini kuwa ndio wewe mbunge wa kuteuliwa, kwani maneno yako hapo juu yametulia na yako deep....anyway..........well said Tom.......kijana Nape anahitaji ushauri.

.....sasa mkuu Tom hebu tueleze....inakuwaje mradi umeanza kabla ya kupata baraka za CC?........kwanini mradi uanze wakati vijana wanaupinga??...........na pengine hapo ndipo kijana Nape anazo inside information zote.........

.
 
Leo mchana aliyekuwa Waziri Mkuu akalazimika kujiuzulu kutokana na UFISADI wa Richmond ametoa waraka ama notisi ya kudhamiria kulipeleka Mwanahalisi Mahakamani ,kutokana na makala yake ya leo pamoja na habari za leo kuhusiana na UFISADI wa jengo la UVCCM.

Ntawapa litakalojiri punde kwani kuna efforts zinafanywa huko Dodoma ili kumhoji ntawaeleza kama atapatikana huko usiku huu.

Mwanahalisi limekubwa na misukosuko mingi sana ,sasa sijui kama litaendelea ama laa kwani limekuwa na kesi nyingi.

Miongoni mwa kesi zake ni pamoja na ile ya Mtikila anadai 3 bilion, Rostam na sasa Lowassa.
 
hapa ndop mafisadi watazidi kujulikana, kadri effort za mafisadi kujilinda zinapombamba moto ndipo tunapowachora na kuwawekea alama X
 
Kuna taarifa kuwa mambo sio sawa ndani ya CCM kutokana na jambo hili kwani limekuwa likiwaumiza vichwa viongozi wakuu wa chama hicho pamoja na wengine kuamua kujitetea.
 
Ni wazi lazima apelekwe mahakamani...jamaa ni muongo sana.anasma kuwa mkataba ulisainiwa usiku,wakati hakuna mkataba uliosainiwa kwa kweli.na hata makala yenyewe hakuna mahali walipofafanua zaidi kuwa kusaini usiku maana yake ni nini...pia si kweli mkataba umesainiwa bali ni ujinga wa kulewa wa Kubena.kwani kilichosainiwa ni memorundum of understanding.Kesi zote zinaendelea vema na muda si mrefu Kubenea atajua hayuko above the law.
 
Ni wazi lazima apelekwe mahakamani...jamaa ni muongo sana.anasma kuwa mkataba ulisainiwa usiku,wakati hakuna mkataba uliosainiwa kwa kweli.na hata makala yenyewe hakuna mahali walipofafanua zaidi kuwa kusaini usiku maana yake ni nini...pia si kweli mkataba umesainiwa bali ni ujinga wa kulewa wa Kubena.kwani kilichosainiwa ni memorundum of understanding.Kesi zote zinaendelea vema na muda si mrefu Kubenea atajua hayuko above the law.

Ni hekima, hata kama haina manufaa kwa jamii, kwa mtoto kumtetea baba yake.
 
Ni wazi lazima apelekwe mahakamani...jamaa ni muongo sana.anasma kuwa mkataba ulisainiwa usiku,wakati hakuna mkataba uliosainiwa kwa kweli.na hata makala yenyewe hakuna mahali walipofafanua zaidi kuwa kusaini usiku maana yake ni nini...pia si kweli mkataba umesainiwa bali ni ujinga wa kulewa wa Kubena.kwani kilichosainiwa ni memorundum of understanding.Kesi zote zinaendelea vema na muda si mrefu Kubenea atajua hayuko above the law.

Tazama inawezekana kabisa hapo imetumika lugha na usiku iliwakilisha hali ,kama unavyojua Usiku ni unawakilishwa na kiza totoro sasa kama mkataba haukujulikana wapi ulisainiwa ,majukumu hayakufuatwa watu wamesitukia tu asubuhi jamaa wanachimba hazina,huoni kama mipango ilikuwa haikuonekana kila watu wakitafuta wanaona kiza tu.
 
Back
Top Bottom