Hata watoto zake IS wameshinda,sababu yule kamanda alikuwa kikwazo kwa IS.Sasa hapa ndio ujiulize hivi US anapinga ugaidi au ana support magaidi kwa ajili ya kulinda maslahi yake.
Mauaji ya Jenerali wa Iran ni mwanzo wa maafa, asema Jeremy Bowen.
www.bbc.com
US,Saudi Arabia na Iran ndio vinara wa kutengeneza magaidi mashariki ya kati.US inatumia ugaidi kudestabilize nchi tishio kwake na marafiki zake pale middle east.Taifa lolote linaloibuka na kuwa tishio kwa Israel na Saudi Arabia lazima US adeal nalo.Proxy wars imekuwa mbinu adhimu kufanya hujuma kwa maadui zake.Na lengo kubwa ni kuweaken wanaopinga sera zake ili yeye US aendelee kupata faida za kiuchumi na utajiri wa middle east.
Chain ya ugaidi inatoka from Western intelligence organizations via Saudi Arabian government and economic tycoons na kwenda down into different areas za middle east kuunda militias.Miaka ya 90 hadi early 2000's hii mbinu iliipa US power kubwa pale,lakini baada ya kuisambaratisha Iraq na Afghanistan,na kuanza kuichokonoa Syria,Iran na Russia zikaona maslahi yao middle east yako hatarini na Syria ingeanguka basi anayefuatia angekuwa Iran.Hivyo wakaamua kupambana kuhakikisha Syria haianguki na juhudi za US kugain influence middle east inadidimizwa.Iran wana kitu wanaita "forward defence" (kama nakumbuka vizuri),kwamba wanahakikisha ulinzi wao wa taifa na maslahi yake unaanzia nje ya Iran,na wana kitengo cha makomando wa jeshi lao kinahusika na ujasusi na hujuma za kigaidi nje ya nchi,(IRGC quds force)ndicho hicho cha akina marehemu Soleimani,kikiripoti direct kwa Ayatollah mwenyewe.Kinalinda mfumo wa utawala wa Caliphate wa kishia "velayat e faqih"( mfumo unaompa kiongozi wa kidini wa uislam wa kishia mamlaka juu ya serikali)nje na ndani ya Iran(dhidi ya wasioaminika katika mfumo rasmi wa serikali).Asili ya mbinu hii ya kujihami ilianzia kwenye mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 79.Baada ya kumuondoa Mfalme Shah na kuanzisha serikali ya Uislamu wa kishia,ikawa inasumbuliwa sana na upinzani toka mataifa ya magharibi yaliyopinga uenezi wa serikali za aina hii middle east,pamoja na hujuma za Israel na Saudia ya wasunni.Saudi,US na Israel zimekuwa zikitumia proxy wars kuua influence ya Iran middle east.Na Iran nayo inataka kukuza ustaarabu wake wa kishia eneo hilo.Iran nayo kwa msaada mkubwa wa Russia,wakaamua kuanzisha na wenyewe vikundi vya kigaidi ili kugain influence eneo la middle east na kuvuruga mtandao wa kigaidi wa US,na kuhakikisha vurugu zinaishia nje ya nchi yao,huko huko Iraq,Syria,Yemen,Afghanistan etc.
Hata muundo wa security organs za Iran unaonyesha jinsi walivyoupa umuhimu ujasusi na proxy wars nje ya nchi.
Irgc quds force ina vitengo vya askari maalum kwa maeneo ya middle east,kama vile Rasulullah(Arabian peninsula),Ansar corps(Afghanistan),Ramazan corps(Iraq) etc.
Wana kikosi cha wanamgambo wa kujitolea kinaitwa Basij,kilicho chini ya IRGC,chenye kazi za kimkakati za mobilization,ulinzi wa ndani,kupandikiza na kusimamia mawazo mikakati ya viongozi kwa jamii,kuandaa mikutano ya kidini,etc.Humu ndimo vijana wengi huwa drilled elimu ya awali ya kijeshi na huchukuliwa na kuingizwa jeshini rasmi baadae,na kurecruit militias.
Emergency ya ISIS ilisababisha balaa kwa US,kwani Iran ilitumia gia kubwa kuunda vikundi powerful vya kupambana na Isis,wakaingiza hadi askari wao rasmi kuongoza front operations huko Syria na maeneo mengi ya Levant,wakitumia ushia kupata sapoti ya vijana wengi wa kiarabu kama vile Houthis kule Yemen,mbinu zao zikawa effective zaidi kuishinda Isisi,na hivyo kuanguka kwa Isis ukawa ushindi mkubwa zaidi kwa Iran kuliko US,mtandao wa militias wa Iran na marafiki zake ukawa superior kuliko ule wa US.Marekani ikaiona hatari hii,kwamba Iran inachukua advantage kwa mbinu ambayo US ndio iliyoanzisha.Iran ikaanza kugain popularity hadi ndani ya mioyo ya vijana wa kishia wa Iraq.Ndipo uhatari wa akina Soleimani kwa maslahi ya US ulipoanzia hapo.Sasa US wanataka kusambaratisha mtandao mbadala ulioanzishwa na Iran.Na wameanza vizuri kweli!Kumuua baba wa mikakati ya hujuma za waajemi Commando General Soleimani,ni pigo kuu kwa Iran.The guy was oustanding soldier,very brave,experienced na eneo lile,na pia mbinu za wamarekani alizijua.No wonder Iran ilimlilia kweli,hujawahi kuona mamilioni ya watu wakizika kama alivyozikwa muajemi Soleimani!Nasikia ndiye alikuwa anaandaliwa kuwa Rais ajaye wa Iran.Pia alikufa pamoja na makamanda wake walioshiba falsafa zake za mapigano ambao wangeweza kutumika baadae.Na tukio hili la kulipua ndege ya abiria,ukabisha hujafanya halafu baadae unakubali,ndio limezidi kuivurugia Iran kabisa mbele ya jicho la watu,maana psychological warfare ni tool muhimu sana kwenye mpambano huu.Vikwazo alivyowekewa zamani vilishamuathiri kiuchumi Iran,sasa hivi alivyosema Trump anaviongeza juzi ndio vinakwenda kumalizia kile kilichobaki kwa uchumi wa Iran.Vita zake za proxy zinahitaji fedha,maana ni hujuma za taratibu kwa muda mrefu.Ataweza kuendelea nazo?Nadhani hapo ataomba kudra za mrusi zimuokoe na zengwe la Syria na Iraq(current proxy wars battlefields) lisiishe to american dream!