mkuu froida, yes kesi hiyo iko vile vile ila kunatofauti kwenye filing, jinsi walivyo file mwanzo, sivyo walivyo file mara ya pili!.
Ni kama mgeni ameleta barua nyumbani na kukukabidhi kwa kukuambie mpe baba, alipokupa mara ya kwanza, hakuifunga ile bahasha, mara baada ya kukukabidhi, akakumbuka hajafunga bahasha, hivyo baada tuu ya kuondoka, mara akarudi na kukuomba ile barua, hakuambii sababu, akaondoka nayo kidogo tuu mara akarudi nayo, ila this time ameifunga ile bahasha!. Barua ni ile ile, na bahasha ni ile ile ila mwanzo ilikuwa wazi, sasa imefungwa!.
Vivyo hivyo, serikali ilipopeleka ile kesi mwanzo, iliifile kikawaida, hivyo mahakama ya kisutu ilikuwa na mamlaka ya kutoa dhamana. Walipo file tena, sasa kisutu wamefungwa mikono, they've nothing to do with this kesi ya ku mention tuu, ngoma yote sasa itachezwa mahakama kuu!.
Dpp akileta nolle, the case is dead, huwezi kuifufua, wala hakuna yoyote mwenye mamlaka kumuuliza dpp chochote, wala lolote, uamuzi wake ni final, finale!.
Pasco.