Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

UKiabiwa intelijensia ya chadema ni zaidi ya IKulu wanagwaya gwaya, Gazeti la Mtanzania jana wamesema nusu ya usalama wa taifa wameasi sasa sijui ndio wamehamia chadema kuimarisha kitengo ha ha ha nayaonaje MACCM na master minder uchwara,Mwigulu,Ridhiwani na NAPE nyie mnapasya kuswekwa ndani hima maana munavuruga amani ya nchi
 
[h=5]Tundu Lissu amefanya Press muda mfupi uliopita. Anasema
1. Anafungua kesi Mahakama kuu kuiomba iiamuru Mahakama ya Kisutu kuendelea kusikiliza kesi ya awali iliyofutwa na DPP katika kesi inayomhusu Lwakatare kwani DPP amevuka mipaka yake inayomruhusu kufuta kesi na isitoshe kesi aliyofungua ni ile ile hivyo Mahakama iamuru shauri la awali liendelee.

2. Kuhusu video iliyoonyeshwa kwenye mitandao Lissu anasema kuna mashaka makubwa sana kuhusiana na video ile na kisheria kesi hiyo ikifika mahakamani haitachukua hata nusu saa ataibuka mshindi.

Lissu anasema
- Hakuna mtu anayepanga mauaji katika hadhara mahali ambapo watu wanapitapita kama inavyoonekana kwenye video ile.
-Lwakatare kama alirekodiwa basi lazima ielezwe je ilikuwa ni kwa hiari yake kama si hivyo ni makosa
-Issa Michuzi Mpiga picha wa Rais alikuwa akipongezana na watu wa Ikulu wenzake kuwa TISS (Usalama wa Taifa) wamefanya kazi nzuri kwa kurekodi ile video. Kisheria usalama wa taifa hawatakiwi wala hawaruhusiwi kurekodi au kuvifanyia ushushu vyama vya siasa kwa maslahi ya Chama tawala.
-Ludovick baada ya kukutana na Rwakatale tarehe 28Dec saa 5 muda mfupi baadae yaani saa 5:59 alimpigia simu Mwigulu Nchemba kwa kutumia namba ya simu ya Mwigulu ambayo ameiandikisha kwenye kumbukumbu na vitabu vya Bunge Lissu anadai wana rekodi ya mazungumzo yao.
-Siku iliyofuata tarehe 29Dec akiwa kwenye kipindi cha Tuongee asubuhi cha Star TV alidai ana mkanda wa video unaowaonyesha CHADEMA wakipanga mauaji.
-Pia amedai itabidi waambiwe video hiyo imerekodiwa studio gani, maneno gani yameondolewa na yapi yameongezwa.
Anamalizia kwa kusema walianza kwa kusema CHADEMA ni chama cha familia wakashindwa, wakasema ni chama cha wachaga wakashindwa, wakesema ni chama cha wakatoliki wakashindwa, wakasema ni chama cha wakristo wakashindwa, wakasema ni chama cha ukanda wakashindwa leo wanasema ni chama cha kigaidi WATASHINDWA. Press nzima itakuwa www.chadema.tv muda mfupi ujao
[/h]
 
mwigilu na nape wametuharibia ccm yetu; we want our CCM back the one under Mkapa regime.
 
Kwa vile mambo bado ni mabichi tusubiri , jambo la maana hapa ni kuendelea kufwatilia kwa karibu mambo yanavyoenda.. Maana baadhi ya kauli zinachekesha, kwann kama serikali kupitia jeshi la polisi hawakufwatilia mambo haya mapema.???? Mim nashawishika kuamin kuwa serikali yetu bado ina vigogo ambavyo havifai hata kuwashia moto.. Wee usikie kuwa kuna watu wamekaana kupanga mauaji au ugaidi kama inavyotamkwa na ushahidi upo then mkae kimya .!!!!!!!!!!!! Jaman hapa hakuna watoto wadogo huo mchezo wenu ni makaa ya moto mnajichochea..YETU MACHO
 
Kumbe ya Lwakatare ni ya kweli!. Daa kweli cdm ni disaster!
 
Hata capitalism walitumia mbinu hizo kuangusha socialism ila walichukua mda. Ukombozi wa mara ya pili lazima ufanikiwe baada ya mkoloni 1960s
 
Sasa naona watu wanaanza kufunguka. Kweli mwisho wa ubaya ni Aibu. Kumbe Lodovick alikuwa ni kibaraka aliyenunuliwa na CCM? Nijuzeni mie!!!

Halafu umeshtukia dili? Jana polisi walitaka abaki mahabusu ya polisi ili aendelee ''kuhojiwa'' ila ikakataliwa na akapelkwa magereza.
 
Mbona wanasheria hawasemi ile video ni fake?

Kama ule mkanda nk genuine basi huo ni ugaidi.
Soma vizuri kasema ile video ya U tube ni tofauti sana na video waliyonayo polisi, it means iliyowekwa u tube imechezewa na kulishwa maneno kwa kutumia sura ya Lwakatare..
 
"Kiongozi anayetafuta urais kwa kutumia vyombo vya habari, akipata madaraka ataongoza kwa risasi" By. Frederick Sumaye (Retired PM), 2005.
 
haka ka kajamaa ka Ludovick inawezekana ka mesheni town - mjini hapa hakuna majembe.
 
Clouds wanalazimisha kujitumikisha...siyo tatizo. Lakini wajitahidi kuwa smart!

Wakipatikana safari hii wasiachiwe, ili siku nyingine washike adabu kutorukia mambo kichwa kichwa.

Ruge na Kibonde wataiponza CLOUDS siku si nyingi , mimi ni shahidi , nilisikia kwa Masikio yangu Radio Clouds fm 88 . 5 ikirusha hewani sauti kutokana na hiyo Video ya kutengezwa na Mwigulu , Kisa ! tenda za kufunga spika Chimwaga ! Njaa ya wiki moja italeta dhiki ya Milele ! Shame !
 
Tundu Lissu siku ile alijidhalilisha sana pale mahakamani mpaka akachekwa na umati wa watu!!!

How? alisema nini? na unahisi umati ulicheka kwasababu gani? umati ulimcheka Lisu au ulichekeshwa kwa jambo lingine? ZeMarcopolo ni miongoni mwa watu wachache sana nisiowaelewa kabisa hapa Jamvini!!!!
 
Last edited by a moderator:
kesi ya kisiasa! ati ni kete ya kuimaliza chadema...!!! nadhani bado hawatafanikiwa kwa hili...
 
Inshalah mwenzi mungu yuko na cdm ccm na makafiri. Cdm ndo mkombozi wa watanzania. Hiz ni dalili njema tusife moyo.
 
Narudia tena kwamba hakuna mahali popote kwenye Dunia hii ambapo Dhuluma iliwahi kushinda haki , ni suala la muda tu !
 
Back
Top Bottom