Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Yale yaleeeeeeeeeeee
Hivi vyama vya upinzani vya Tanzania vinachangia tuchelewe kurudi nyumbani...muda huu CCM inalega lega baada ya kujiimarisha ndo kwanza fimbo mkononi,tutafika kweli?
 
Chama chochote lazima kiwe na nidhamu, kama hawatang'oa magugu leo, hakika yanayotokea CCM yatawafika, hakuna haja ya kulindana, ukimiss discipline lazima uadhibiwe.
 
Jasusi,

Sijazumgumzia mafisadi, hoja yangu ni kwenye kuvumiliana kwenye kutofautiana kimawazo kwenye chama.
 
Anastahili kufukuzwa! Yeyote anayejaribu kuleta vurugu kwenye chama chochote dawa ni kufukuzwa tu. Chama hakiendeshwi na watu wakorofi wenye kutaka kuleta migogoro isiyokuwa na sababu? Chama kinaendeshwa kwa maelewano na makubaliano na si kwa migogoro!
 
Enzi za mwalimu, mtu kama Sophia Simba mpaka sasa hivi angekuwa amemwagwa zamani! Ukiwa kiongozi lazima uzijue principles na vision ya chama kiasi mtu anayeonekana ni myumbishaji (kama hawa/huyu wa Chadema walio/aliyetimuliwa) anawekwa kando haraka halafu watu mnasonga mbele. Huyu ni Slaa ambaye kwangu ndiye one of the very few genuine leaders katika siasa za Tanzania
 
Anastahili kufukuzwa! Yeyote anayejaribu kuleta vurugu kwenye chama chochote dawa ni kufukuzwa tu. Chama hakiendeshwi na watu wakorofi wenye kutaka kuleta migogoro isiyokuwa na sababu? Chama kinaendeshwa kwa maelewano na makubaliano na si kwa migogoro!
Alifukuzwa CHACHA, mwacheni aende , kama hakuna maridhiano wanini Chamani
 
Kama kweli kuna watu wanaokiuka maadili ya chama kwa nini wendelee kulea uozo ndani ya chama? Hujui kuwa chachu kidogo huchachua donge zima? Ni afadhali kuvumilia maumivu ya kujisafisha kuliko kufunikia uchafu ambao utakuja kuibuka baadae na uvundo wake utakua mbaya zaidi.

Mnataka Chadema iwe lesser fair kama Chechem inayomwacha kila mtu afanye atakavyo? Nadhani Chadema ni chama Makini na hawawezi kuvumilia ujinga kama huu. Huu ni Msimamo mzuri.
 
Kama ni kufukuzani, fine, lakini kutumia taratibu, sheria na kanuni walizo jipangia, sababu zisiwe chuki binafsi, makundi, au kutofautiana kambi, hali ilivyo CCM kwa sasa ingetakiwa iwe ndio oportunity kwa Chadema ku-seize, lakini nanyi ndio mnaanza...!?
 
tena kama kweli kafukuzwa bora....huyu jamaa alikuwa na timu yake na baada ya kukosa uenyekiti wa bavicha amenazisha tabia ya kutoa siri za chama kwa CCM. Afukuzwe tu!!!!!!!!
 
Huyu kijana inaonekana nidhamu yake imeshuka tangu kipindi kile cha Uchaguzi wa viongozi ndani ya CHADEMA. Na nasikia huyu kijana ni kundi la Zito, kwa hiyo asimdharau mkuu akidhani Zito atamtetea na nina muomba Zito kama kweli ana mapenzi na CHADEMA aache kuingilia na kijana aadhibiwe kama kakosa nidhamu.
 
Zitto alisema humu hakuna atakayefukuzwa.

Mimi nasisitiza kuwa kufukuza mwanachama sio sahii ila kumuondoa kwenye uongozi ni sahihi especially tatizo ikiwa ni kutofautiana misimamo au mtazamo. Ila kama ana makosa kama ya kuvujisha siri basi VIKAO HALALI VIKAE NA KUONYWA, akizidi wamfukuze.

Ila Chadema mmmhhhh!
 
Huyu kijana inaonekana nidhamu yake imeshuka tangu kipindi kile cha Uchaguzi wa viongozi ndani ya CHADEMA. Na nasikia huyu kijana ni kundi la Zito, kwa hiyo asimdharau mkuu akidhani Zito atamtetea na nina muomba Zito kama kweli ana mapenzi na CHADEMA aache kuingilia na kijana aadhibiwe kama kakosa nidhamu.


Sawa kabisa, ila je alishaonywa na kupewa muda ajirekebishe?, kumbuka hakuna binadamu aliye sawa!
 
wakati wa kubembelezana na wahalifu kama CCM wanavyofanya umekwisha. Kama kweli katoa siri za chama nje afukuzwe tu hakuna huruma.......ukitaka kuwa mwana siasa lazima ukubali siasa ichukue mkondo wake, kama haupendi madhara ya siasa hasa za afrika basi kaa kando.
 
Zitto alisema humu hakuna atakayefukuzwa.

Mimi nasisitiza kuwa kufukuza mwanachama sio sahii ila kumuondoa kwenye uongozi ni sahihi especially tatizo ikiwa ni kutofautiana misimamo au mtazamo. Ila kama ana makosa kama ya kuvujisha siri basi VIKAO HALALI VIKAE NA KUONYWA, akizidi wamfukuze.

Ila Chadema mmmhhhh!

Politics ngumu sana, you either get it right and win or you loose and wait for 5 years. Kama kuna mtu anakosa adabu ndani ya chama na kuvujisha siri za chama kwanini aonewe haya?
 
Mimi nadhani na ninaomba aadhibie kama ushahidi upo afukuzwe au anyanganywe nyazifa zote kwa muda abaki kama mwanachama.
 

Nani hapa ana uthibitisho kuwa Kafulila anatoa siri za chama, zipi hizo alizowahi kutoa?

Pili what if anayosimamia Kafulila yapo sahihi na Mbowe yuko wrong, kumbukeni Chacha He was innocent!

Inakuwaje katibu msaidizi wa Chama (Zitto Kabwe ) asijue hii ishu?

Jamani mpaka saa hizi mnakubali kuwa mna chama???

Mnapokuja na hoja dhaifu za 'aende' jamani kumbukeni kila siku mnapiga kelele kuhusu CCM!, nyie wana CHADEMA pona yenu ni kuweka uthibitisho wa ubaya wa Kafulila! otherwise soon hiki chama kitabaki historia, ilikuwepo NCCR jamani!

Kwa nini HAMCHUKUI JAPO DAKIKA KUFIKIRI KABLA YA KUWEKA USHABIKI NA UTETEZI MBELE?? mtaja ubuka jamani, post hizi zitabaki ushahidi siku zote

Mbowe amekaa chni na Kafulila mara ngapi,lini amepewa barua za onyo, lini kaonywa na kamati ya maadili ya chama, JE Kafulila amejieleza na kujitetea kwa madai yaliyoelekezwa kwake??

Mswali haya yasipoulizwa na kujibiwa something wrong, naanza kupata wasiwasi washabiki na wapenzi wengi wa Mbowe ni wadumavu wa akili, na wameweka maslahi mbele kuliko ya taifa, kwani ni tusibaki na CCM angalau basi hakuna ufamilia wala

mmefulia

To hell Chadema!!!!!!!!!
 
Kinacho nishangaza mimi ni vijana wetu wanaojiunga ktk vyama vya siasa hapa TZ. Hawa vijana wenzangu kama kweli wana nia ya dhati ni kukaa kama kikundi na kuanzisha chama chini ya mwembe, hapo watakuwa na sauti moja lakini kukuta Mzee mtei na wenzake wamewekeza ktk chama chao na wewe wanakukaribisha alafu baada ya muda unataka uwe na sauti eti kuwazidi walio kukaribisha ktk chama chao? hilo haliwezekani.

Nashauri vijana kama akina zitto, kafulila, nape na wengine, kama kweli tunataka tuwe na chama chetu ni kuanzisha chama cha vijana wa Tanzania bila kuegemea chama cho chote kilichopo na tukisajiri, hapo tutaweza kuwa na sauti na mapambano ya kweli.
 
Back
Top Bottom