Kwani vyombo vya habari, TLS, Askofu Gwajima na etc ndiyo wenye mamlaka ya kuhakiki vyeti vya watu? Sasa awapelekee vyeti vyake wao kama nani? Umeambiwa cheo cha RC kina rank sawa na Minister. Haingii akilini waziri au mkuu wa mkoa anachukua vyeti vyake anaenda navyo kuhakikiwa na chombo cha habari kinachomilikiwa na Kubenea, Mbowe na etc!! Wapi duniani ilikwisha tokea kitu cha namna hii.
Tuhuma nzito ya Makonda ilikuwa ni ya uvamizi wa kituo Clouds TV. Leo ameielezea vizuri sana. Ni dhahiri kabisa tuhuma hii ni ya kughushi kwa maslahi wanayoyajua wenyewe. Na kuna uwezekano wahusika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa kosa la dedefamation na kudhalilisha ofisi ya mkuu wa mkoa.
Hilo la kubadili jina toka D.A. Bashite na kuwa P.C. Makonda kwa kusudio la kutumia vyeti vya P.C. kujiendeleza kielimu nalo kalikanusha katu katu. Kwamba majina anayotumia ndiyo aliyopewa na wazazi wake. Hakukuwa na haja kuwaonyesha birth certificate kwani wao si mamlaka ya uhakiki. Ni dhahili kuwa hadithi hii ni ya kutungwa pia. Na watungaji ni baadhi ya waliotajwa kwenye orodha ya madawa. Si ajabu watu hawa wakafikishwa mahakamani muda si murefu kwa kosa la defamation na kudhalilisha ofisi ya mkuu wa mkoa. Tumesikia PCCB wanamalizia upelelezi wa kesi hii huko Tabora ambako kuna huyo name mate wa Makonda.
Mkondo wa sheria lazima utachukuwa mkondo wake dhidi ya watunzi hao wa hadithi za uongo ili iwe fundisho pia kwa wengine wenye tabia kama hizi.