The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,801
Baraza Kuu la Mitume na Manabii Tanzania limekanusha kuhusika na barua ambayo imesambaa mtandaoni ikieleza kinachodaiwa kuwa ni tamko la baraza hilo kuhusu sakata linaloendelea la Mkataba wa Bandari.
Akieleza katika video aliyoiposti kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Itifaki wa baraza hilo, Dkt. Peter Rashid Abubakar amesema kuwa barua hiyo haijatoka katika ofisi yake na pia haina vielelezo vyovyote vinavyothibitisha kuwa ni nyaraka rasmi ya taasisi hiyo.
Dkt. Abubakari pia ameeleza kuwa hajui ni nani aliyeiandika na kuisambaza.
Akieleza katika video aliyoiposti kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Itifaki wa baraza hilo, Dkt. Peter Rashid Abubakar amesema kuwa barua hiyo haijatoka katika ofisi yake na pia haina vielelezo vyovyote vinavyothibitisha kuwa ni nyaraka rasmi ya taasisi hiyo.
Dkt. Abubakari pia ameeleza kuwa hajui ni nani aliyeiandika na kuisambaza.