Saga la Makonda: My Take

Saga la Makonda: My Take

Naamini wengi wenu humu ndani leo mlitegemea mkuu wa mkoa wa Dar kutumbuliwa na mheshimiwa mtukufu rais wa JMT.

Imani hiyo naamini iliongezwa na utolewaji wa video ya usalama ya kituo cha habari na burudani cha Clouds ambapo mkuu wa mkoa alionekana akiingia na askari wenye bunduki kwenye ofisi za kituo hicho majira ya usiku.

Hilo la kutumbuliwa halijatokea na kusema ukweli mimi sikuwa nategemea litokee hapo Ubungo mbele ya kadamnasi [ingawa Magu na huyo Makonda wake wameshawahi kumtumbua mtu hadharani]. Sikutegema wao kwa wao watumbuane hadharani.

Kwa jinsi rais Magufuli alivyo na kwa jinsi suala zima la vita dhidi ya Makonda linavyoendeshwa hivi sasa [kiudaku udaku hususan huku mitandaoni] mimi sitegemei kuona wala kusikia kuwa Makonda atatumbuliwa hivi karibuni. Uwezekano wa kutumbuliwa upo ila uelekeo wake mimi siuoni.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu nadhani Magufuli akifanya hivyo atakuwa kama kasalimu amri ya shinikizo linalotoka huku kwenye mitandao na sidhani yuko tayari aonekane kasalimu amri.

Naamini kabisa Magufuli naye anayaona makosa ya Makonda. Ila sidhani kama 'ego' yake itamruhusu kufanya vile ambavyo wengi, hususan huku kwenye mitandao, wanataka afanye. Akifanya hivyo itakuwa ni kama kawapa ushindi wapinzani wake.

Baada ya muda suala hili la Makonda litapoa tu. Sina hakika itachukua muda gani lakini naamini litapoa tu.

Likishapoa ni imani yangu pia kuwa hapo ndo utakuwa mwanya wa Magufuli 'kumpangia' Makonda shughuli nyingine.

Lakini kwa sasa jinsi mazingira yalivyo [mipasho madhabahuni, matusi mitandaoni, drama magazetini, n.k.] sidhani kama yanampa rais nafasi nzuri ya kufanya kile ambacho wapinzani wake wanamtaka afanye.

Naona labda hataki kuweka precedent ya kuyumbishwa na kelele za watu. Tena watu wanaomtukana hadi matusi ya nguoni. Watu wanaomzushia kila aina ya uzushi. Watu wamefikia hadi hatua ya kudokeza kwamba Makonda na Magufuli ni wapenzi....seriously?

Mtu mnamtukana hivyo halafu bado mnategemea afanye jambo la kuwasuuza nyoyo zenu? Acheni masikhara bana.

Ila muda utatuonyesha tu....tusubiri tuone.

NYONGEZA YA NUKUU

"Mimi huyu uniingilie..ukiniingilia ushapoteza kabisa"

"Mimi huwa sipangiwi mambo"

"Mimi ni rais ninayejiamini"

"Siwezi nikapangiwa mtu"

"Ninapanga mimi"

Video hii hapa chini.



Hizo nukuu za rais zinaipa nguvu hoja ya kwamba kwa sasa hizi kelele za watu kupitia mitandao ya kijamii hazitamfanya achukue uamuzi wa kumtumbua Makonda.

Ego tripping on steroids.

Umeongea jambo la msingi sana. lakini haya yote ameyatengeneza JPM mwenyewe maana tabia za huyu kijana alizijua fika so hakustahili kumtegemea kwenye mambo nyeti na serious ya kitaifa kwa namna ya juu kiasi hicho??!! Makonda hakustahili kuwa hata mjumbe wa nyumba 10....hana maadili ya uongozi yule mtoto?!! ukiangalia hata marafiki zake wa karibu utajua tu tabia zake.huyu kijana bado hajakuwa kiakili
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Kwani alivyomtumbua mama Malechela nani alimshinikiza Rais, alivyomtumbua Kitwanga ishu ya ulevi nani alimshinikiza Rais, alipomtoa Katibu mkuu wizara ya fedha, Likwelile nani alimshinikiza Rais.. Alipomuondoa mkurugenzi wa Mkinga, nani alimshinikiza Rais.. Wengi waliotumbuliwa hakuna alimshinikiza..
Ofcoz ila ya kitwanga lilikuwa chezo baada ya shinikizo kubwa
 
Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?
Duh! Kwa akili yako ni wapinzani ndiyo wanadai hayo. Kumbuka kuna watu ndani ya chama, wasio na chama wanadai hayo hayo. Enzi za Nyerere ilikuwa hivi hivi n a nakumbuka kuna mkuu wa mkoa aliwahi kuondolewa kwa kelele za watu bahada ya kuvunja miiko ya uongozi. Kiongozi mwenye busara hatendi kwa kiburi ati hasionekane dhaifu bali upima yanayosemwa na utoa maamuzi. Mbona Rais wetu amewahi kufanya hayo hayo kwa kusikia kelele za watu na kuwafuta watu kazi. Kiongozi mwenye hekima utenda kwa haki hat kama mhusika ni kipenzi chako. Kinyume chake unawapa watu ajenda. Kwa hiyo usifikiri watu hawana akili - la sivyo ni wewe ndiyo unakosa hekima kwa kuwaita watu hivyo.
 
Wewe ke.nge kuwa na adabu, LB7 ni bibi yako na waliokuzaa, mimi sio hao mbuzi unaotaja na kama hujui kusoma nenda jukwaa la watoto, hebu soma tena halafu shika adabu yako, kwanza huu ni muda wa kufanya kazi mlizopewa na walimu wenu huko shule
Ukisikia PAAA,jua imempata huyo
 
Wewe ndiyo tumia akili achana na ubashite wa kutetea yale ambayo hayastahili kutetea. Sasa unataka kumpinga hata Ruge! Halafu unajiona eti una akili!

Akili ni nywele, mtu kama hajui tofauti ya kuvamia na kuingia na silaha, ni vigumu sana kumwelimisha sababu akili yake tayari imefungwa ndani ya chupa.
 
mjinga gan tena? huyu aliyewabwaga katka uchaguzi? huyu anayeogoza nchi kwa weledi na kusifiwa duniani kote kama ujinga upo hivi hata mm niwe mjinga tu
 
FB_IMG_1490115392757.jpg
1. Amechelewa kuwapa ushindi wauza dawa za kulevya.Hakuna atayekataa kuwa habari ya Makonda kuandamwa imeanza mara tu baada ya kushughulika na wauza unga. Huu ndio ukweli . Hata Gwajima ameibuka baada ya kutajwa.

Wauza unga wamekuwa wakitamba kuwa hakuna aliyewagusa wao akabaki salama. Ni atakufa kimwili au kisiasa. Kauli hii imekuwa ikiaminiwa si kwa wauza unga tu bali hata wananchi wa kawaida wasio wauza unga.

Mifano ya akina Amina Chifupa na mmewe Mpakanjia Mohd imekuwa ikitolewa. Kauli ni moja tu kuwa ukiwagusa umekwisha.

Kama rais angetengua uteuzi wa mkuu wa mkoa kwasababu yoyote ile, tuhuma yoyote ile, iwe kweli au urongo bila shaka angekuwa ameendelea kutimiliza UNABII HUU( prophecy).

Ungekuwa ni ushindi kwao hata km sababu ya kutengua uteuzi ni tofauti.Huu ndio ukweli na ukweli sharti usemwe.

Rais hakupenda kabisa kuwapa ushindi watu hawa na hilo lazima tulielewe.

2. Rais angetengua uteuzi wa Makonda basi nusu au nusu na robo ya vita ya dawa za kulevya ingekuwa imekufa. Isingekufa kwasababu iliendeshwa na Makonda laa, bali wote waliomstari wa mbele katika hii vita wangerudi nyuma.Wangeanza kuifanya kwa kuchelea.

Hii ni kwasababu kila mtu anayo mapungufu yake hapo alipo au huko alikotokea. Khofu ya kusakamwa kwa mapungufu hayo na baadae kupoteza nafasi yao Kama ambavyo ingekuwa kwa Makonda ndiyo ingewarudisha nyuma walio mstari wa mbele.

Aliyetumbuliwa baada ya kusakamwa angekuwa mfano kwao. Watendaji hawa wangekosa kujiamin katika kazi hiyo kwasababu hakuna anayependa kibarua chake kiharibiwe. Na hapo bila shaka vita ya dawa za kulevya ingekuwa kwaheri. Huu ndio ukweli na ukweli sharti usemwe.

3. Tuhuma za Makonda ziwe kweli au uongo bado walioziibua hata rais mwenyewe wameshamzulia si Mara moja au Mara mbili . Kila mtu anajua Gwajima alisema mangapi dhidi ya rais kipindi cha kampeni. Sitaki kusema kuhusu huyo Mange Kimambi ameandika mangap dhidi ya rais hapo kabla na sasa.

Huwezi kuwa we ni adui yangu halafu ukawa wewe ndio wa kunionesha adui mwingine aliye kwenye himaya yangu. Sio rahisi , tangu hapo hunitakii mema leo imekuwaje. Rais naye ni binadamu na hivyo hawa wawili hawakuwa watu sahihi wa kuibua haya. Huu ndio ukweli na ukweli sharti usemwe.

4. Rais naye ni Mtanzania kama walivyo wengine.Anao uhuru wa kuwa na mtazamo, maono na maoni kama walivyo wengine. Ni haki yake kikatiba na Uikulu hauiondoi.

Basi kwa maoni yake ameona Makonda hafai kuwajibishwa. Huwez kulazimisha maoni yako yawe yake halikadhalika yeye alazimishe yake yawe yako.

Kama maoni yako yalivyoona ni lazima awajibishwe ndivyo maoni ya rais yalivyoona hafai kuwajibishwa. Yote ni maoni na kila mtu ana yake. Sasa iweje ulazimishe afuate ya kwako.

Kwa haraka rais amefanya maamuzi bora katika wakati husika.
 

Attachments

  • FB_IMG_1490115392757.jpg
    FB_IMG_1490115392757.jpg
    55.3 KB · Views: 35
Tatizo ni mitandao au impact ya habari? Je, tatizo ni mitandao au umeielewaje habari? Tatizo ni habari kutoka mitandaoni au ukweli wa habari kutoka mitandaoni.
 
Inawezekana hii ni series, kila mwaka wanatoa episode moja!

I sure hope not!

Makonda kavumiliwa vya kutosha. Kupita kiasi.

Safari hii asipotumbuliwa, Magufuli atapoteza kabisa credibility yoyote aliyonayo.
 
I sure hope not!

Makonda kavumiliwa vya kutosha. Kupita kiasi.

Safari hii asipotumbuliwa, Magufuli atapoteza kabisa credibility yoyote aliyonayo.
Yetu macho, ila huyo nduguyo hachelewi kusema msimpangie cha kufanya!
 
Approach nzima inayotumika dhidi ya Makonda si nzuri maana imekaa kiudaku udaki na kulipiza kisasi.

Halafu watu wanapoanza kudokeza kuwa Magufuli na Makonda ni mashoga...halafu hapo hapo wanamtegemea Magufuli eti amtumbue Makonda!

Mtu mnamtukana halafu hapo hapo mnamtegemea afanye jambo la kuwafurahisha...come on now.

Wrong approach.
Basi nenda kampe taarifa abaki nae

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom