Huna kitu....empty shellukikuwa ukiacha utoto njoo tuzungumze
Huna kitu....empty shellukikuwa ukiacha utoto njoo tuzungumze
Naamini wengi wenu humu ndani leo mlitegemea mkuu wa mkoa wa Dar kutumbuliwa na mheshimiwa mtukufu rais wa JMT.
Imani hiyo naamini iliongezwa na utolewaji wa video ya usalama ya kituo cha habari na burudani cha Clouds ambapo mkuu wa mkoa alionekana akiingia na askari wenye bunduki kwenye ofisi za kituo hicho majira ya usiku.
Hilo la kutumbuliwa halijatokea na kusema ukweli mimi sikuwa nategemea litokee hapo Ubungo mbele ya kadamnasi [ingawa Magu na huyo Makonda wake wameshawahi kumtumbua mtu hadharani]. Sikutegema wao kwa wao watumbuane hadharani.
Kwa jinsi rais Magufuli alivyo na kwa jinsi suala zima la vita dhidi ya Makonda linavyoendeshwa hivi sasa [kiudaku udaku hususan huku mitandaoni] mimi sitegemei kuona wala kusikia kuwa Makonda atatumbuliwa hivi karibuni. Uwezekano wa kutumbuliwa upo ila uelekeo wake mimi siuoni.
Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu nadhani Magufuli akifanya hivyo atakuwa kama kasalimu amri ya shinikizo linalotoka huku kwenye mitandao na sidhani yuko tayari aonekane kasalimu amri.
Naamini kabisa Magufuli naye anayaona makosa ya Makonda. Ila sidhani kama 'ego' yake itamruhusu kufanya vile ambavyo wengi, hususan huku kwenye mitandao, wanataka afanye. Akifanya hivyo itakuwa ni kama kawapa ushindi wapinzani wake.
Baada ya muda suala hili la Makonda litapoa tu. Sina hakika itachukua muda gani lakini naamini litapoa tu.
Likishapoa ni imani yangu pia kuwa hapo ndo utakuwa mwanya wa Magufuli 'kumpangia' Makonda shughuli nyingine.
Lakini kwa sasa jinsi mazingira yalivyo [mipasho madhabahuni, matusi mitandaoni, drama magazetini, n.k.] sidhani kama yanampa rais nafasi nzuri ya kufanya kile ambacho wapinzani wake wanamtaka afanye.
Naona labda hataki kuweka precedent ya kuyumbishwa na kelele za watu. Tena watu wanaomtukana hadi matusi ya nguoni. Watu wanaomzushia kila aina ya uzushi. Watu wamefikia hadi hatua ya kudokeza kwamba Makonda na Magufuli ni wapenzi....seriously?
Mtu mnamtukana hivyo halafu bado mnategemea afanye jambo la kuwasuuza nyoyo zenu? Acheni masikhara bana.
Ila muda utatuonyesha tu....tusubiri tuone.
NYONGEZA YA NUKUU
"Mimi huyu uniingilie..ukiniingilia ushapoteza kabisa"
"Mimi huwa sipangiwi mambo"
"Mimi ni rais ninayejiamini"
"Siwezi nikapangiwa mtu"
"Ninapanga mimi"
Video hii hapa chini.
Hizo nukuu za rais zinaipa nguvu hoja ya kwamba kwa sasa hizi kelele za watu kupitia mitandao ya kijamii hazitamfanya achukue uamuzi wa kumtumbua Makonda.
Ego tripping on steroids.
Ofcoz ila ya kitwanga lilikuwa chezo baada ya shinikizo kubwaKwani alivyomtumbua mama Malechela nani alimshinikiza Rais, alivyomtumbua Kitwanga ishu ya ulevi nani alimshinikiza Rais, alipomtoa Katibu mkuu wizara ya fedha, Likwelile nani alimshinikiza Rais.. Alipomuondoa mkurugenzi wa Mkinga, nani alimshinikiza Rais.. Wengi waliotumbuliwa hakuna alimshinikiza..
Duh! Kwa akili yako ni wapinzani ndiyo wanadai hayo. Kumbuka kuna watu ndani ya chama, wasio na chama wanadai hayo hayo. Enzi za Nyerere ilikuwa hivi hivi n a nakumbuka kuna mkuu wa mkoa aliwahi kuondolewa kwa kelele za watu bahada ya kuvunja miiko ya uongozi. Kiongozi mwenye busara hatendi kwa kiburi ati hasionekane dhaifu bali upima yanayosemwa na utoa maamuzi. Mbona Rais wetu amewahi kufanya hayo hayo kwa kusikia kelele za watu na kuwafuta watu kazi. Kiongozi mwenye hekima utenda kwa haki hat kama mhusika ni kipenzi chako. Kinyume chake unawapa watu ajenda. Kwa hiyo usifikiri watu hawana akili - la sivyo ni wewe ndiyo unakosa hekima kwa kuwaita watu hivyo.Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?
Ukisikia PAAA,jua imempata huyoWewe ke.nge kuwa na adabu, LB7 ni bibi yako na waliokuzaa, mimi sio hao mbuzi unaotaja na kama hujui kusoma nenda jukwaa la watoto, hebu soma tena halafu shika adabu yako, kwanza huu ni muda wa kufanya kazi mlizopewa na walimu wenu huko shule
Wewe ndiyo tumia akili achana na ubashite wa kutetea yale ambayo hayastahili kutetea. Sasa unataka kumpinga hata Ruge! Halafu unajiona eti una akili!
Asimtumbue tu ili azidi kututia hasira na tuzidi kuzijua zaidi tabia zao.
Mjinga mpe sifa.
Ndo hivyo meno ya mbwa hayaumani!!!Bashite alipewa go ahead na mamlaka ya juu, Siyo kwamba alikurupuka tu.Ngosha hawezi kumtumbua ngosha mwenzie.
You know how to read trends...Flashback Friday....
You know how to read trends...
Inawezekana hii ni series, kila mwaka wanatoa episode moja!Flashback Friday....



I hope he will survive this too....reading from the public reaction, if I were president I would know how to dispose of him safely.Hahahaaa thanks my guy.
Makonda boy is in some deep doo-doo.
Inawezekana hii ni series, kila mwaka wanatoa episode moja!![]()
I hope he will survive this too....reading from the public reaction, if I were president I would know how to dispose of him safely.
Yetu macho, ila huyo nduguyo hachelewi kusema msimpangie cha kufanya!I sure hope not!
Makonda kavumiliwa vya kutosha. Kupita kiasi.
Safari hii asipotumbuliwa, Magufuli atapoteza kabisa credibility yoyote aliyonayo.
Basi nenda kampe taarifa abaki naeApproach nzima inayotumika dhidi ya Makonda si nzuri maana imekaa kiudaku udaki na kulipiza kisasi.
Halafu watu wanapoanza kudokeza kuwa Magufuli na Makonda ni mashoga...halafu hapo hapo wanamtegemea Magufuli eti amtumbue Makonda!
Mtu mnamtukana halafu hapo hapo mnamtegemea afanye jambo la kuwafurahisha...come on now.
Wrong approach.