Saga la Makonda: My Take

Saga la Makonda: My Take

Kama ni hivyo angemwambia aandike barua ya kajiuzulu! Mitandao ni sauti ya watu, sio wote wana access ya kutoa maoni yao kwenye radio na TV. Hata yeye hufuatilia sana social media ndo maana amekuwa na maneno ya udaku na hekima pia.

Kama hataki kuonekana anayumbishwa na sauti za watu, amwambie ajiuzulu au ampe likizo kupisha uchunguzi. Kwa maneno yale ni dalili ya kiburi na dharau kwa sauti ya umma
 
Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?

Kwani wanaoupinga upuuzi wa Bashite ni upinzani tuu..? Sijui ni kwanini lakini kila unapoamua kutumia vdole vyako kufikisha ujumbe, unakuwa unafikisha ujinga na upuuzi zaidi.. Wako wana ccm wenye akili mara mia zaidi yako na wanausemea huu upuuzi..
 
You have said it all mkuu,

Huwezi kumtukana Rais halaf utegemee akusikilize interests zako

Approach nzima inayotumika dhidi ya Makonda si nzuri maana imekaa kiudaku udaki na kulipiza kisasi.

Halafu watu wanapoanza kudokeza kuwa Magufuli na Makonda ni mashoga...halafu hapo hapo wanamtegemea Magufuli eti amtumbue Makonda!

Mtu mnamtukana halafu hapo hapo mnamtegemea afanye jambo la kuwafurahisha...come on now.

Wrong approach.
 
Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?

Nape ni upinzani?
 
Binafsi nakubaliana na hoja yako.... Hii vita dhidi ya Makonda imekaa kidaku mno (Wauza unga+media+Vyama vya upinzani+Wasaka uraisi ndani ya CCM)Magufuli kwasasa hawezi kumtumbua Makonda kupitia shinikizo la watu hata siku moja binafsi napenda hii hoja ya Makonda ife kabisaa tufocus kwenye maendeleo inatupotezea muda tu aliyemteuwa anajua ukweli zaidi kuliko sisi wapiga kelele.
 
Awe na ego au la amecheza move ambayo ita mbana pande zote hata ikifika muda habari za makonda zikipoa. For now ana underestimate nguvu za sauti za watu mitandaoni akisahau kuwa wenye sauti hizo ni wale wale wananchi wake and they exist in both worlds za mitandaoni na in real life. Time is the best teacher
 
Hivi kabisa walitegemea atumbuliwe?hahahaha Magufuli hatumbui kwa shinikizo hata mara moja na hata wabunge wote wakitishia kujiuzulu hatomtumbua....Kosa walilofanya toka mwanzo ni kumuandama muda mrefu...
 
Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?
Wewe kuna ccm gani zaidi yako ambao watasapoti alichofanya clouds?
achilia mbali vyeti feki!

Ila amwache tu tuendelee kupata zile za moto moto kutoka magogoni!
kwasababu mule mule ndani kuna wengine hawapendi ujinga huu
 
Upinzani wa Tanzania hawana Akili na ni wote, kudili na Raisi Magufuli ni rahisi sana kama mtu una uwezo wa kumsoma mtu na kumuelewa, kwenye hii ishu wao wangekaa kimya tu na kuacha na nina uhakika wangefika mbali zaidi kuliko kushinda siku nzima kumtukana, kumkejeli, kumchora katuni halafu hapo mnategema afanye mnavyotaka? Hata yeye Raisi Magufuli ni Binadamu pia na anaumia kwa matusi yenu/yao!
Yaani kwa akili yao walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?
Kwanza niondoa hizi ''akili ukoko'' zilizoganda kwenye kichwa chako na kukariri kila mtu anayeyeonyesha maovu/upungufu wa serikali hususani Magufuli kuwa ni ''Upinzani''. Hizi ni akili za kukariri na hazina nafasi kwenye jumuia ya watu wenye akili. Hivyo nasema kuna wengi wameona upungufu, usanii na makosa ya mkuu huyo wa mkoa na wanataka kuonyesha uchapakazi sio huo!
 
Naamini wengi wenu humu ndani leo mlitegemea mkuu wa mkoa wa Dar kutumbuliwa na mheshimiwa mtukufu rais wa JMT.

Imani hiyo naamini iliongezwa na utolewaji wa video ya usalama ya kituo cha habari na burudani cha Clouds ambapo mkuu wa mkoa alionekana akiingia na askari wenye bunduki kwenye ofisi za kituo hicho majira ya usiku.

Hilo la kutumbuliwa halijatokea na kusema ukweli mimi sikuwa nategemea litokee hapo Ubungo mbele ya kadamnasi [ingawa Magu na huyo Makonda wake wameshawahi kumtumbua mtu hadharani]. Sikutegema wao kwa wao watumbuane hadharani.

Kwa jinsi rais Magufuli alivyo na kwa jinsi suala zima la vita dhidi ya Makonda linavyoendeshwa hivi sasa [kiudaku udaku hususan huku mitandaoni] mimi sitegemei kuona wala kusikia kuwa Makonda atatumbuliwa hivi karibuni. Uwezekano wa kutumbuliwa upo ila uelekeo wake mimi siuoni.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu nadhani Magufuli akifanya hivyo atakuwa kama kasalimu amri ya shinikizo linalotoka huku kwenye mitandao na sidhani yuko tayari aonekane kasalimu amri.

Naamini kabisa Magufuli naye anayaona makosa ya Makonda. Ila sidhani kama 'ego' yake itamruhusu kufanya vile ambavyo wengi, hususan huku kwenye mitandao, wanataka afanye. Akifanya hivyo itakuwa ni kama kawapa ushindi wapinzani wake.

Baada ya muda suala hili la Makonda litapoa tu. Sina hakika itachukua muda gani lakini naamini litapoa tu.

Likishapoa ni imani yangu pia kuwa hapo ndo utakuwa mwanya wa Magufuli 'kumpangia' Makonda shughuli nyingine.

Lakini kwa sasa jinsi mazingira yalivyo [mipasho madhabahuni, matusi mitandaoni, drama magazetini, n.k.] sidhani kama yanampa rais nafasi nzuri ya kufanya kile ambacho wapinzani wake wanamtaka afanye.

Naona labda hataki kuweka precedent ya kuyumbishwa na kelele za watu. Tena watu wanaomtukana hadi matusi ya nguoni. Watu wanaomzushia kila aina ya uzushi. Watu wamefikia hadi hatua ya kudokeza kwamba Makonda na Magufuli ni wapenzi....seriously?

Mtu mnamtukana hivyo halafu bado mnategemea afanye jambo la kuwasuuza nyonyo zenu? Acheni masikhara bana.

Ila muda utatuonyesha tu....tusubiri tuone.
Nyani,,,,tambua kila jambo lenye faida lina hasara zake.

Mchana mwema
 
Back
Top Bottom