Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe Jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? Au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way he is and we have to live with it.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mimi nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa nitakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo.

So im just keeping it real.
Hasira zako kwa JPM unazihamishia kwa Mungu? pole sana Mungu hajaribiwi wala hadhihakiwi subiri majibu ndani ya siku 7.
 
we umechafukwa wewe si bure! ninachofanya nakuombea Mungu akupe wepesi, kwa post kama yako Mungu asingekuwa ni upendo angeshamtuma Israel atoe roho yako hiyo nyeusi tii isiyo na shukrani, unavuta pumzi bure bado huna shukrani?! KUMBAFU!!!
 
Wewe bado mungu wako si MUNGU, mungu wako atakuwa shetani ukimjua MUNGU wa kweli utapata majibu ya maswali yako yote bila shida kabisa
 
balehe na ubarobaro vnakutesa na sina shina umiongoni mwa wahanga wa vyeti bandia,ila kumbuka kama umetumia simu au kompyuta kuandika haya mataputapu jua kuwa wapo wenzako mungu hakuwapa hio neema,na wengi hawajui kusoma wala kuandika kama wewe,acha kupoteza mda jiondoe kazini au utashtakiwa
 
Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

Mkuu, wala huna haja ya kumchukia Mungu. Ngoja nijaribu kujibu hoja zako kulingana na mie nilivyoelekezwa. Angalia kama ninachosema kina make sense.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe Jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

Si kweli kwamba Mungu ameandaa jehanamu. Jehanamu ni sehemu ya fundisho la kidini la uongo sana. Kwenye Biblia ukweli uko wazi, kwamba Mungu atahukumu kwa kifo watu wanaotenda dhambi - kama alivyofanya wakati wa Sodoma na Ghomora na ghalika. Kwani waliohukumiwa wakati huo wako sehemu fulani jehanamu? Yeye amesema wazi - mshahara wa dhambi ni mauti. Hajawahi kusema mshahara wa dhambi ni moto wa milele. Kwanza unawezaje kumchoma mtu kwa umilele? Yaani aungue milele asife - labda huo moto hauunguzi basi. Lakini hakuna kitu kama hicho.

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

Kitendo cha shetani Mungu hakukipanga wala kuruhusu. Japo Mungu aliweka mti wa matunda kwa ajili ya kujaribu utii wa Adamu, hakutarajia kwamba Adamu angekula lile tunda kupitia kushawishiwa na Ibilisi. Na pia jambo la msingi sana wewe kuelewa, ni kwamba Mungu ana uwezo wa kuelewa kila kitu hata kitakachotokea kesho au muda mrefu ujao - lakini mara nyingine anaamua kutoangalia nini kitatokea mbele ili aone mambo yanavyotokea katika "real time".

Kumbuka pia Mungu alimuuliza Adamu - "nani amekuambia uko uchi, umekula tunda nililosema usile?" Ndipo Adam na Eva wakampa taarifa ya kilichotokea. Asingewauliza yale maswali kama alijua kimefanyika kitu alichopanga. Na hakujua kwamba Adam na Eva wangeshindwa jaribu dogo la tunda - kwa sababu hakutaka kuangalia matokeo yatakuwaje, kama watakula au la. Ukweli ni kwamba alikuwa amewapa jaribu dogo sana ili kupima uaminifu wao kwake. Adamu na Eva walikuwa na maelfu ya matunda na vyakula vingine, sio kuwa walikula kwa sababu ya njaa ya kukosa kitu cha kula. Waliamua kutokutii amri ya Mungu kwa utashi, wakitaka kuwa sawa na Mungu, kama Ibilisi alivyowadanganya.

Matokeo ya sisi kuteseka kutokana na dhambi ya Adamu ni kweli yapo. Lakini hiyo ni sehemu ya shutuma ya Ibilisi kwamba sisi binadamu tunamwabudu pale tu anapokuwa ametupa raha na starehe - kama kusema anatuhonga ili tumtii. Kwa hiyo Mungu ameachia mambo yalivyo sasa ili kujibu shutuma za shetani - kama ilivyokuwa katika episode ya Ayubu. Ila alisema wazi, muda wa kutosha utakapopita kumwonyesha Ibilisi kwamba wanadamu wapo watakaomtii Mungu katika generation zote na hali zote, basi ataleta hukumu. Suala ni sisi kuvumilia hadi siku atakaposema sasa inatosha!


3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? Au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

Hata siku moja Mungu hajasema tusipomtii atatuchoma moto. Kumbuka Ibilisi alimwambia Mungu tunamtii kwa kuwa anatuhonga na hali nzuri, na Mungu akaonyesha si kweli. Sasa unafikiri ingekuwa kweli Mungu anatishia kutuchoma moto ili tumwabudu - si ndio shetani angetoa shutuma mbaya hata zaidi dhidi ya Mungu kwamba watu hawa wanakutii kwa sababu umetishia kuwachoma moto? Kumbuka mshahara wa dhambi ni mauti - na wa utii kwa Mungu unaleta uzima wa milele. Hivyo maandiko yanasema wazi - mbele yetu tuna uchaguzi - uzima wa milele au mauti. Usipotii Mungu ni kwamba utakufa, period. Eidha ukifa sasa hutafufuliwa tena (unakuwa umeshapata mshahara wako) au ukiwa hai siku ya kiama utakufa siku hiyo, Period.

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way he is and we have to live with it.

Bado jibu ni lile lile - Mungu hana mpango wa kuchoma moto wa milele watu wasiomtii. Atawaangamiza kwa kifo kama alivyofanya wakati wa Sodoma na Gomora na Gharika, watakufa wasiwepo tena.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

Kweli, Mungu ana hekima sana kuliko wanadamu. Hatuwezi hata kujilinganisha naye kwa mbali sana. Kwa hiyo una mwanzo mzuri, unaonyesha unyenyekevu tayari. Basi jaribu kuwa mnyenyekevu hata zaidi, na utaona ni jinsi gani kwa maelezo yaliyopo chini.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mimi nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Ni baraka kuzaliwa - kumbuka maandiko yanasema watoto ni zawadi toka kwa Mungu. Sasa je, unalaani zawadi ambayo Mungu aliwapa wazazi wako na huenda wakaifurahia sana? Na kumbuka Mungu ana kusudi moja kwa kila mwanadamu anaezaliwa - kwamba maisha yake yatumike kujibu shutuma za shetani kwamba wanadamu hawawezi kuwa watiifu kwa Mungu, na kwamba Shetani ana uwezo wa kumfanya kila mwanadamu anaezaliwa amtukane Mungu, kwa matendo au maneno. Sasa suala ni wewe unataka usimamie wapi katika hili suala - je utakuwa kati ya watu wachache ambao watamjibu shetani kwamba wapo watu kama wewe ambao come rain come sunshine watakuwa upande wa Mungu? Kumbuka Mungu anataka kumjibu Ibilisi kwamba katika kila generation ya wanadamu, watakuwapo ambao wataonyesha wako upande wa Mungu, hata kama ni angalau mmoja tu. Haitatokea wasiwepo kabisa, Labda wewe pia ulizaliwa kwa ajili ya hilo - uweze kuonyesha kwamba tuhuma za shetani dhidi ya Mungu ni za uongo kwa kuwa wewe pamoja na kuzaliwa katika generation iliyojaa maovu na mateso, bado unasimama upande wa Mungu.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa nitakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo.

Mkuu, nimejifunza mambo mengi sana kwa sababu niliamua kuwa open minded na kufanya discussion nyingi sana na Mashahidi wa Yehova. Hayo mambo niliyokutajia hapo juu wao watakuonyesha hata maandiko ili kukuthibitishia. Ushauri wangu kwako ni kwamba watafute ufanye nao discussion. Wala hawatakutoza fedha. Fanya hivyo, ukiona wanakupa majibu ya kuridhisha, japo siku ya kwanza tu, basi kubali kufanya discussion zaidi pamoja nao. Huenda ukapata majibu kwa maswali yote yanayokusumbua.

Wengi wanawadharau na kuwakebehi Mashahidi wa Yehova bila kujua wana ufahamu wa juu sana juu ya mambo ya Biblia. Ila inahitaji unyenyekevu sana kuwa tayari kuwasikiliza na kujadiliana nao haya mambo. Mkumbuke Naamani. Unyenyekevu ulimsaidia sana.

Kuna uzi humu ndani juu yao hata ilibidi nitoe post kuwaeleza watu ukweli. Angalia

Mahakama Urusi yapiga marufuku Mashahidi wa Yehova


 
Mungu wetu ni mwenye upendo sana, hata baada ya kuwaza hayo bado anakupenda
 
Nilijua nitakutana na mambo yale yale ya kila siku. Mkuu haya mambo uliyosema yako deep sana!
 
@okoyoyo

Amani ya Bwana iwe nawe.
Nitumie fursa hii kukujuza kiwa Dini ni Imani,Muhimu sana,Dini ni Imani na wewe hauna imani.
Unajaribu kutumia akili ya ki binadam kutaka kupata majawabu ya Maswali Magumu ambayo kamwe hutoyapata.
Mungu ni wa Kipekee na ana huruma sana,Kimsingi amesononeshwa sana juu ya allegations zako kwake na anakupenda na kukuhurumia mno.
Kaa Chini,ongea na Mungu na Majibu ya maswali yako yote utayapata kutoka kwake.
Unaweza kuyapata kwa njia ya Matukio katika Maisha yako na kama una Neema yake utajua tu.
It happened to me,Mungu ameshawahi kuongea na mimi kwa kufanya muujiza Mkubwa kabisa,Nilipiga goti na kumshukuru,Nakumbuka niliomba kwa imani kubwa kabisa na ya ajabu kuwa kufanya.
Watu wengi wanakuwaga na ile imani wakiwa na Matatizo,ila wakiwa sawa husahau (Nature.ya Binadamu)

Nakushauri kitu kimoja.
Kila ikifika Saa nne usiku,tenga japo dakika 10,Mshukuru Mungu kwa kila jema alilokufanyia.
Mshukuru kwa Zawadi ya uhai,Afya,watoto (Kama unao),Mali,Rafiki etc halafu.
Mshukuru kwa kukuokoa dhidi ya Mambo ambayo hata huyajui.
Muombe Mungu akusamehe dhambi zako ulizotenda ama kwa Maneno,kwa kuwaza,kwa matendo etc.
Fanya hii kwa Siku 3 Mfululizo ukiwa na utulivu wa akili na Nafsi na kwa imani Kuu kabisa.
Baada ya siku tatu njoo hapa ukipenda kutoa ushuhuda kuwa Mungu hajakupa Mwanga katika Maswali yako.
Hauwezi kujua kuwa Mungu amenitumia mimi kukufikishia huu ujumbe.
Nami ntakuwema kwenye Sala zangu.
Mungu akubariki sana
 
When u pass through the waters, I will be with you; and when you pass through the rivers, they will not sweep over you. When you walk through the fire, you will not be burned; the flames will not set you ablaze............

Okoyoko
note that *The name of the LORD is a fortified tower; the righteous run to it and are safe*

Akuna kulalamika jua yote ni darasa unapitia.......jua wakati wako upo usiogope
Na mapito[emoji470][emoji470][emoji470]
 
Mpaka sasa.

1. Hakuna aliyeweza kuthibisha Mungu yupo.

2. Hakuna aliyejibu swali, kama Mungu yupo, naye ni muumba wa yote, muweza wa yote, mwenye upendo wote na ujuzi wote, aliweza kuuumba ulimwengu huu vyovyote alivyotaka, kwa nini kauumba ukiwa unaruhusu mabaya kuwezekana wakati aliweza kuuumba ukiwa hauruhusu mabaya kuwezekana ?
 
So you do believe in science? Good.

Ulichokisema hapo sijui self motion is just plain BS and means nothing, don't put god into this. The existence of these galaxies that you mentioned definitely prove the absence of god not his presence. I'll explain to you why, take it or leave it.

The farthest galaxy we have observed to date is approximately 13.3 billion light-years (4 billion parsecs). Which I believe is an accurate number unless huamini the method used in measuring the distance, I on the other hand do because I know exactly how it works.

Sasa kama the farthest galaxy is 13.3 billion light years which is approximately the time the big bang happened, hii biblia yenu inayosema the universe is about 6,000 years old huoni inatudanganya? Kama ni 6,000K that light that travelled 13.3 billion years from that galaxy kufika kwenye telescope zetu ulitoka wapi?

Unasema I can't understand the intelligence that created me, lol! could be true, I might as well be a computer simulation running on someone or something's machine, that still doesn't prove your god's existence, kama kweli he does exist then we are doomed maana anatetea slavery infact ana-encourage slaves kuwatii slave masters, ananyima wanawake haki zao, au hujui its written mwanamke hatakiwi ku-lead?, anatetea ukatili. He even knew what would happen to this world yet still put a test to see if it will happen. Lol! what a joke. Sorry aisee there's no way you'll convince me to go back and believe that BS. Miungu zaidi ya 3000 we una uhakika wa kwako ndiye wa kweli? Zunguka dunia uone. Najua there's no way I will convince you kua unachoamini is total bs, its something you'll have to find it in yourself ku-question kama you really think ungezaliwa ufike hata 15 then uanze kufundishwa kama ungekubali, you accepted everything as a kid ukameza now you are what we call brainwashed. Its a very hard prison to break, nilikua kama wewe for 20 years, na nilikua nabishana na atheists humu JF balaa kuliko hata wewe, kutetea uwepo wa god.
So You telling me about your past arguments with atheists about God is supposed to threaten me?

Nshakwambia sio kila kitu tutaweza kuelewa either viko beyond our intelligence au technology.Na pia perception yako a science na ya kwangu Ni tofauti mkuu.

Hiyo furthest galaxy uliyoitaja Ni farthest according to our current technology.Miaka Mia ijayo haitakuwa the furthest galaxy anymore.New things are discovered every single year.Science and technology keep evolving.

Nidharau all you want but it does not affect what I believe.I believe in science as much as as I believe in God.Of course I choose what to believe.I'm not sure about history but I'm sure about my belief on the existence of God.That's faith,which you don't have. And I'm not forcing you to believe.

And sije ukajiona wewe ndo umefanya the wisest decision ever ya kutoamini uwepo wa Mungu.Ukaanza eti kusema you were here.You might have been here but we have different perceptions of things.You might have chosen to be an atheist and I chose to remain a believer.

I'm impressed by the big atheists who gave their faith a second chance Kama Mark Zuckerberg(owner wa FB) ambaye amebadili mawazo na saivi anaamini uwepo wa Mungu.
Albert Einstein mwanasayansi mkubwa aliamini uwepo wa Mungu sembuse leo wewe uje kunihubiria eti Mungu hayupo.Its hilarious.I'm sorry.Stakaa nkafika ulipo wewe,My God lives! Then,now and forever!And nothing will change that belief in me in this world.
 
Labda unamzungumzia mungu na si Mwenyezi Mungu muumba!! Mwenyezi Mungu hana muda na kiumbe maana yeye si mhitaji bali viumbe ndio wanaomuhitaji. Suala la adhabu ya milele hakika lipo wala halina shaka kwa wenye kufikiri na kufahamu. Pepo ipo na Jehannamu ipo. Ni jukumu letu sisi wanadamu aidha kushukuru ama kukufuru. Suala la kuumbwa na kuzaliwa ni hiyari yetu wenyewe kabla hatujazaliwa. ukichagua kuzaliwa na kuishi duniani unapaswa kutii mkataba uliokubaliana sio kulalamika baada ya kushindwa kuutimiza! mfano: hii ni sawa na ule mrabaha wa asilimia tatu ambao leo umekuwa janga kuu kuuvunja wote wanaupita mbali!!
 
Mpaka sasa.

1. Hakuna aliyeweza kuthibisha Mungu yupo.

2. Hakuna aliyejibu swali, kama Mungu yupo, naye ni muumba wa yote, muweza wa yote, mwenye upendo wote na ujuzi wote, aliweza kuuumba ulimwengu huu vyovyote alivyotaka, kwa nini kauumba ukiwa unaruhusu mabaya kuwezekana wakati aliweza kuuumba ukiwa hauruhusu mabaya kuwezekana ?
Uthibitisho wa uwepo wa Muumba ni mpangilio wa maisha na maumbile, nyumba haiwezi kuwepo bila mjenzi. Wale walioamini vitu vimezuka 'Darwinism' leo uongo wao umethibitika kwamba nadharia yao haina mashiko tena. Ila inawezekana kung'ang'ania jambo kiubishi-ubishi!
 
Ukisoma kwenye Bible kitabu cha Ayubu.....utajifunza kitu kama binadam ulivo mbele za Mungu......hiyo hali yako ni ya kawaida hata mimi niliipitia
 
Uthibitisho wa uwepo wa Muumba ni mpangilio wa maisha na maumbile, nyumba haiwezi kuwepo bila mjenzi. Wale walioamini vitu vimezuka 'Darwinism' leo uongo wao umethibitika kwamba nadharia yao haina mashiko tena. Ila inawezekana kung'ang'ania jambo kiubishi-ubishi!
Kama nyumba haiwezikuwepo bila mjenzi, hilo linaonyesha Mungu hayupo.

Kwa sababu hata Mungu naye atahitaji muumba wake.

Point yako haina maana hapa.
 
So You telling me about your past arguments with atheists about God is supposed to threaten me?

Nshakwambia sio kila kitu tutaweza kuelewa either viko beyond our intelligence au technology.Na pia perception yako a science na ya kwangu Ni tofauti mkuu.

Hiyo furthest galaxy uliyoitaja Ni farthest according to our current technology.Miaka Mia ijayo haitakuwa the furthest galaxy anymore.New things are discovered every single year.Science and technology keep evolving.

Nidharau all you want but it does not affect what I believe.I believe in science as much as as I believe in God.Of course I choose what to believe.I'm not sure about history but I'm sure about my belief on the existence of God.That's faith,which you don't have. And I'm not forcing you to believe.

And sije ukajiona wewe ndo umefanya the wisest decision ever ya kutoamini uwepo wa Mungu.Ukaanza eti kusema you were here.You might have been here but we have different perceptions of things.You might have chosen to be an atheist and I chose to remain a believer.

I'm impressed by the big atheists who gave their faith a second chance Kama Mark Zuckerberg(owner wa FB) ambaye amebadili mawazo na saivi anaamini uwepo wa Mungu.
Albert Einstein mwanasayansi mkubwa aliamini uwepo wa Mungu sembuse leo wewe uje kunihubiria eti Mungu hayupo.Its hilarious.I'm sorry.Stakaa nkafika ulipo wewe,My God lives! Then,now and forever!And nothing will change that belief in me in this world.

Lol! Hehe this discussion won't go anywhere, I see you've started calling out Mark Zuckberg and Einstein as if you know the guys. I respect your decision, you tried to force it on me first.

You could be right even though I think you are wrong, who am I to say, I could also be right and you wrong, so don't go there acting like you know shit when the reality is you have no idea what you are saying.
 
Kama nyumba haiwezikuwepo bila mjenzi, hilo linaonyesha Mungu hayupo.

Kwa sababu hata Mungu naye atahitaji muumba wake.

Point yako haina maana hapa.
Hapo ndipo uliposhindwa kuiona point ilipo ndio maana nikasema utakaobakia ni ubishi tu ambao hauna mashiko!!
Ukweli unao moyoni mwako lakini ni vigumu kuukiri kwa sababu ya kuona haya 😀😀😀
 
kwa asiyetaka kuelewa hawezi kuwa na muda wa kufikiria kwanini tuna vidole gumba vikubwa mikononi na miguuni kwanini havikuwa vidole vidogo kama vya chanda? Si rahisi kwa asiyetaka kuelewa kujiuliza kwanini shingo ya mwanadamu haizunguuki kama ya bundi!! Kwanini faida za mbu ni nyingi kuliko hasara zake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom