Ukarabati wa Miradi ya Maji Vijijini
42. Mheshimiwa Spika, kama nilivyolieleza Bunge lako Tukufu mwaka jana, Wizara yangu, kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za Wilaya, ilifanya utambuzi wa miradi ambayo haijakamilika na haifanyi kazi. Jumla ya miradi 794 yenye kuhitaji shilingi bilioni 43 kuikamilisha, ilitambuliwa. Katika mwaka 2003/2004, Wizara ilitenga jumla ya shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kukarabati miradi 31. Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ilifanya ukarabati wa miradi ya maji ya Migori na Kiponzelo (Iringa Vijijini), Lumeya (Sengerema), Misasi (Misungwi), Malya (Kwimba), Mugango-Kiabakari (Musoma Vijijini) Bunda mjini, Gabimori (Tarime), Hedaru (Same), Lotima (Rombo), Biharamulo na Chunya. Aidha, miradi mingine iliyofanyiwa ukarabati ni Mwamapuli/Bulenya (Igunga), Singida Vijijini, Mahenge Mjini, Shinyanga Vijijini, Kilulu (Bariadi), Magugu (Babati), Korogwe mjini, Nassa (Magu), Kitomondo (Lindi), Urambo mjini, Ndea (Mwanga), Majengo/Eslalei, Elerai/Longido na Mto wa Mbu (Monduli).
Bwana kaka siyo kila kinachofanyika jimboni kina mkono wa mbunge.
Angalia majukumu ya wote hapa chini, unadhani bila mbunge hakuna kinachofanyika cha maendeleo?
Pia ukiangalia vizuri, utagundua mbunge ana majukumu ya kuishauri serikali pale anapoona inapotoka kulingana na matakwa ya waliompa kura, kwani yeye ndo sauti yao bungeni.
Narudia tena, bila kuongea leo ungejua ya Buzwagi?
Bunge likiwa na jukumu la kutunga sheria, utazitunga huku umeuchapa usingizi bungeni?
Kuna haja gani ya kuhudhuria vikao vya bunge kama huna na wala hutarajii kuleta mchango wowote? Au unafata posho tu!
check out below!
.......................................................
c) Mheshimiwa Spika, kazi za Mbunge ni pamoja na uhamasishaji wa maendelo ya wananchi na uwakilishi wa wananchi Bungeni. Masharti ya kazi ya Mbunge kupitia Bunge yameelekezwa katika Ibara ya 63(2) kwamba Bunge litakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake na huo ndio uhusiano wa msingi kati ya Mbunge na kazi za Serikali.
Kwa mujibu wa Sheria Na. 19 ya mwaka 1997 baadhi ya majukumu ya Mkuu wa Wilaya, ni pamoja na kuwa mwakilishi mkuu wa Serikali Kuu Wilayani, msimamizi wa Ulinzi na Usalama, Miongozo na Kanuni za Maendeleo. Jukumu la kusimamia miongozo na Kanuni za Maendeleo linaendana na majukumu ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Mji, Manispaa au Jiji ambaye anayo majukumu ya kisheria na kiutawala katika Halmashauri na pia ni Katibu wa vikao vya Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, Mbunge, Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wote wanatumikia umma na wanatekeleza majukumu yao kwa lengo la kuleta maendeleo ya wananchi. Tofauti waliyonayo ni utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia tofauti za masharti ya kazi na mgawanyo wa madaraka uliozingatia mihimili ya dola.