Rostam (Mbunge) anawahadaa wananchi wa Igunga

Rostam (Mbunge) anawahadaa wananchi wa Igunga

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
Mpaka Kieleweke,

Umeibua hoja ya msingi kabisa, ikiwa mahudhurio yake bungeni ni kama ulivyobainisha basi si ajabu hajachangia wala kuuliza lolote bungeni kama data alizoleta FD zinavyoashiria.

Hapo awali nilinukuu kipengele kimoja ambapo alikuwa anazungumza kumbe ilikuwa ni semina siyo session ya kawaida ya bajeti bungeni, hivyo ukweli unabaki palepale hajachangia bungeni toka aingie.

Nadhani wapo wabunge wengine ambao wana hatia hiyohiyo, ingelikuwa vema wakaanikwa nao vilevile aidha wananchi waamshwe waanze kuwabana wabunge wao kisawasawa.
 
Duh!?

Mtu mpya, unamtuhumu mtu kwa kosa ambalo so far halijatajwa kisha unamuomba mtetezi aelezee/atetee makosa hayo! Kaazi kweli kweli.

Nikumbushe ndugu yangu Rostam Abdulrasul Azizi Abdulrasul aligombea na nani kiti cha ubunge Igunga?, nani alisimama naye kutoka upinzani au CCM?

Ninachoweza kukusaidia ni kukujulisha namna ya kujenga hoja kwanza, ukishaelewa nitakwambia namna ya kupata ushaidi kuthibitisha madai yako.

Imeandikwa humu RA ajiuzulu wananchi hawamhitaji. Kwanini hwamhitaji? ikasemwa hajazungumza Bungeni, tukasema mbona hilo sio tatizo? wapo wengi tu wa aina hiyo, ila jamaa amefanya mengi, na hayo mmeyajata wenyewe.

Ukaja na ELIMU. Ukajibiwa. Ukasema RA akaseme hayo bungeni. Ninkujibu kuwa, suala la Mishahara ya waalimu ni la kitaifa sio la IGUNGA pekee, ni suala la SERIKALI, na pia suala la mishahara serikalini ni tatizo la kudmu, sio la LEO.

Ukaja na lowest point ya kuwa kama ana hela basi aongezee waalimu mishahara. Hilo unajua for sure haliwezekani. Kama hujui basi hatuna haja ya kujadiliana humu.

So far mjadala mzuri ndugu yangu. Tuendelee
 
Kama hawwzi kuhudhuria vikao vya bunge ana faida gani ya kuwasemea wananchi waliomtuma?

Hajawahi hata kuzungumza zaidi ya kuwahonga wabunge wa ccm ili wamchague kiongozi wa bunge na aliwapa kiasi cha shilingi laki tano kila mbunge wa ccm , ......

Natoa hoja kuwa huyu yafaa asimamishwe na sio kumsimamisha zitto anayelizungumzia taifa.

Igunga hayo maendeleo yako wapi ?
Ni shule ngapi za sekondari zilizopo jimboni mwake ?
Kuna waaalimu kwenye shule hizo?
Zahanati ngapi zipo jimboni mwake? kuna wahudumu?
Wananchi wake wanatumia maji ya visima je?hayo ndio maendeleo?
 
Kama hawwzi kuhudhuria vikao vya bunge ana faida gani ya kuwasemea wananchi waliomtuma?

Hajawahi hata kuzungumza zaidi ya kuwahonga wabunge wa ccm ili wamchague kiongozi wa bunge na aliwapa kiasi cha shilingi laki tano kila mbunge wa ccm , ......

Natoa hoja kuwa huyu yafaa asimamishwe na sio kumsimamisha zitto anayelizungumzia taifa.

Igunga hayo maendeleo yako wapi ?
Ni shule ngapi za sekondari zilizopo jimboni mwake ?
Kuna waaalimu kwenye shule hizo?
Zahanati ngapi zipo jimboni mwake? kuna wahudumu?
Wananchi wake wanatumia maji ya visima je?hayo ndio maendeleo?

Wala akiwezi kueleweka kwa stahili hiyo.

Mshitaki ndio anatakiwa kutoa takwimu. Takwimu hamna YET mnamuhukumu!

Wala hakitaeleweka kwa stahili hiyo ndugu yangu!
 
Tuanze hivi:
Igunga is one of the six districts of the Tabora Region of Tanzania. It is bordered to the north by the Shinyanga Region, to the east by the Singida Region, to the south by the Uyui District and to the west by the Nzega District.

According to the 2002 Tanzania National Census, the population of the Igunga District was 325,547. [1]


[edit] Wards
Igunga District is administratively divided into 26 wards:

Bukoko
Chabutwa
Choma
Igoweko
Igunga
Igurubi
Isakamaliwa
Itumba
Itunduru
Kining'inila
Kinungu
Mbutu
Mwamashiga
Mwamashimba
Mwashiku
Mwisi
Naga
Ndembezi
Ngulu
Nguvumoja (English meaning: one strength)
Nkinga
Ntobo
Nyandekwa
Simbo
Sungwizi
Ziba (English meaning: block)
 
laikini matatizo kama njaa yeye huwa haombi serikali isaide,hutia mkono mfukoni mwake na kusaidia,sasa tena hapo wananchi wanataka nini?
 
Igunga kuna MAJI:

BUNGE::Kitakuwa ni kitu cha kushangaza sana, kama maji yatashindwa kuja Bukombe, ambayo ni Wilaya Ndogo ya Kahama, yaende Nzega mpaka Igunga, yanaelekea kuja Dar ...

parliament.go.tz/bunge/ContrLst.asp?Menu=Contr&PTerm=2005-2010&vpkey=1437&page=19
 
Naendelea.........

Ukarabati wa Miradi ya Maji Vijijini



42. Mheshimiwa Spika, kama nilivyolieleza Bunge lako Tukufu mwaka jana, Wizara yangu, kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za Wilaya, ilifanya utambuzi wa miradi ambayo haijakamilika na haifanyi kazi. Jumla ya miradi 794 yenye kuhitaji shilingi bilioni 43 kuikamilisha, ilitambuliwa. Katika mwaka 2003/2004, Wizara ilitenga jumla ya shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kukarabati miradi 31. Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ilifanya ukarabati wa miradi ya maji ya Migori na Kiponzelo (Iringa Vijijini), Lumeya (Sengerema), Misasi (Misungwi), Malya (Kwimba), Mugango-Kiabakari (Musoma Vijijini) Bunda mjini, Gabimori (Tarime), Hedaru (Same), Lotima (Rombo), Biharamulo na Chunya. Aidha, miradi mingine iliyofanyiwa ukarabati ni Mwamapuli/Bulenya (Igunga), Singida Vijijini, Mahenge Mjini, Shinyanga Vijijini, Kilulu (Bariadi), Magugu (Babati), Korogwe mjini, Nassa (Magu), Kitomondo (Lindi), Urambo mjini, Ndea (Mwanga), Majengo/Eslalei, Elerai/Longido na Mto wa Mbu (Monduli).

Source: http://www.tanzania.go.tz/budgetspeech/2004/mifugo040726.htm

Igunga mambo safi toka 2004... Tutaendelea
 
Upanuzi wa Miradi ya Maji Vijijini



44. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu, kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, Wahisani na Taasisi za ndani na nje, imeendelea kuimarisha na kuboresha huduma ya maji vijijini kwa kupanua na kujenga miradi mipya ya maji katika maeneo mbalimbali nchini. Katika mwaka 2003/2004, Wizara yangu iliendelea kujenga na kupanua miradi ya maji ya Nachingwea Mjini, Maswa, Rondo, Singida Vijijini, Manyoni Vijijini, Nanganga, Kitomanga, Kazilankanda (Ukerewe), Nyakagomba, Losinyai, Hai na bwawa la Mugumu. Aidha, uchimbaji wa visima (2) vya Serengeti na Dang'aida (Hanang') uliokuwa kwenye mpango wa mwaka 2003/2004 utakamilika katika kipindi cha mwaka 2004/2005.



45. Mheshimiwa Spika, baadhi ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka uliopita ni ukamilishwaji wa mradi mkubwa wa maji wa Chalinze. Mradi huo uliogharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali yetu na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, kwa jumla ya shilingi bilioni 23.65, ulizinduliwa na Mhe. Benjamin William Mkapa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwezi Mei 2004. Mradi huo wenye mabomba yenye urefu wa kilometa 160, vituo vya kuchotea maji 332, matanki 10, kwa sasa unahudumia wananchi 70,000 katika vijiji 18 wilayani Bagamoyo.



Mafanikio mengine ni ukamilishaji wa awamu ya pili ya mradi wa Hanang', Singida Vijijini, Manyoni na Igunga uliotekelezwa kwa kushirikiana na Serikali ya Japan na kugharimu shilingi bilioni 3.9. Mradi huo ulizinduliwa na Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwezi Machi 2004 katika wilaya ya Manyoni.

Wapiga kelele mpo wapi!!!!?
 
Programu ya Kitaifa ya Maji na Usafi wa Mazingira



50. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inasimamia Mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini ambao unagharamiwa kwa mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia. Mradi ulianza kutekelezwa katika wilaya tatu (3) za Rufiji, Kilosa na Mpwapwa ambapo jumla ya vijiji 29 vyenye watu 134,000 vinapata huduma ya maji hadi sasa. Mafanikio hayo yametokana na uchimbaji wa visima vifupi na virefu, pamoja na ujenzi wa miradi ya maji ya mtiririko. Katika mwaka 2002/2003, mradi ulipanuliwa na kufikia wilaya 12 na mwaka 2003/2004 wilaya nyingine 38 ziliongezwa hivyo kufikia Wilaya 50 (Kiambatanisho 5a na 5b). Aidha, Wizara ilifanya warsha za uhamasishaji kuhusu maandalizi ya mradi huo katika wilaya zote nchini. Lengo la warsha hizi lilikuwa ni kujadili na watendaji katika ngazi za wilaya na mkoa kuhusu taratibu na maandalizi ya utekelezaji wa mradi katika wilaya husika.



Katika mwaka 2004/2005, Wizara yangu imetenga shillingi bilioni 9.9 kwa ajili ya maandalizi ya mradi huo kwenye wilaya 38 zilizoongezwa pamoja na ujenzi wa miradi katika wilaya 12 za awamu ya kwanza. Pia, maandalizi ya kupanua mradi huu yamekamilika ili kuwa na Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini itakayotekelezwa katika wilaya zote nchini kuanzia Julai mwaka 2005. Maandalizi ya utekelezaji wa Programu hii yanahusisha wadau mbalimbali wa Sekta ya Maji na kuzingatia uzoefu uliopatikana katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi. Aidha, upanuzi wa miradi ya maji katika miji ya Igunga, Kiomboi, Manyoni, Kondoa, Kongwa na Kibaya ulifanyika.
 
Ukarabati wa Miradi ya Maji Vijijini



42. Mheshimiwa Spika, kama nilivyolieleza Bunge lako Tukufu mwaka jana, Wizara yangu, kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za Wilaya, ilifanya utambuzi wa miradi ambayo haijakamilika na haifanyi kazi. Jumla ya miradi 794 yenye kuhitaji shilingi bilioni 43 kuikamilisha, ilitambuliwa. Katika mwaka 2003/2004, Wizara ilitenga jumla ya shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kukarabati miradi 31. Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ilifanya ukarabati wa miradi ya maji ya Migori na Kiponzelo (Iringa Vijijini), Lumeya (Sengerema), Misasi (Misungwi), Malya (Kwimba), Mugango-Kiabakari (Musoma Vijijini) Bunda mjini, Gabimori (Tarime), Hedaru (Same), Lotima (Rombo), Biharamulo na Chunya. Aidha, miradi mingine iliyofanyiwa ukarabati ni Mwamapuli/Bulenya (Igunga), Singida Vijijini, Mahenge Mjini, Shinyanga Vijijini, Kilulu (Bariadi), Magugu (Babati), Korogwe mjini, Nassa (Magu), Kitomondo (Lindi), Urambo mjini, Ndea (Mwanga), Majengo/Eslalei, Elerai/Longido na Mto wa Mbu (Monduli).
 
HOTUBA YA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, MHESHIMIWA OMAR RAMADHAN MAPURI (MB.) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA

KWA MWAKA 2004/05



Malengo ya Huduma za Magereza kwa Mwaka 2004/2005.

55. Mheshimiwa Spika, Jeshi la Magereza katika mwaka ujao wa fedha wa 2004/05 litatekeleza miradi ifuatayo ya maendeleo:



(i) Kukamilisha baadhi ya viporo vya miradi ya mabweni ya wafungwa na mahabusu.

(ii) Kuanza ujenzi wa Gereza la Igunga.
 
HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA

MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE, KUHUSU MAKADIRIO YA

MATUMIZI YA FEDHA

KWA MWAKA 2005/2006
Ununuzi na usambazaji wa dawa za uzazi wa mpango nchi nzima ulifanyika. Pia huduma za mama wajawazito ziliendelea kuboreshwa kwa kutoa vifaa vya kujifungulia. Aidha Halmashauri 9 zenye kiwango cha juu cha vifo vya akina mama vinavyotokana na uzazi walipewa magari ya kubebea wagonjwa ili kupunguza tatizo hilo. Halmashauri hizo ni Bariadi, Maswa, Kahama, Kasulu, Ngara, Karagwe, Manyoni, Igunga na Tarime. Ninazipongeza Halmashauri nyingine zilizoamua kununua magari ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya kupunguza tatizo la akina mama wajawazito na wagonjwa wengine wanaohitaji rufaa. Halmashauri hizo ni Geita, Urambo, Korogwe, Lushoto, Manispaa za Iringa, Tanga, Ilala, Temeke na Kinondoni. Aidha, simu za upepo (redio call) 20 zimenunuliwa na kusambazwa katika Wilaya za Bariadi, Kahama na Maswa ili kurahisisha mawasiliano.
 
AFYA...

Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho



162. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2005/2006, Wizara yangu inatarajia kuongeza wilaya 10 zaidi katika mpango wa kudhibiti ugonjwa wa vikope nchini kwa kutumia mtindo mpya wa "District Wide-Approach". Wilaya 8 kati ya hizo zinatarajiwa kutoa dawa ya Zithromax kwa wananchi. Wilaya zitakazojumuishwa katika mpango huo ni Kongwa, Kilosa, Meatu, Iramba, Singida vijijini, Igunga, Simanjiro, na Mkuranga. Wananchi wapatao 2,300,000 wanatarajiwa kupata matibabu na kinga ya ugonjwa wa vikope.
 
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA CHAKULA, MHESHIMIWA CHARLES N. KEENJA (MB.), KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO NA CHAKULA KWA MWAKA WA 2004/2005



IV. HUDUMA ZA USHAURI WA KITAALAM

51. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo na Chakula kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, imeendelea kuwapatia wakulima teknolojia bora za uzalishaji ili kuwawezesha kuongeza uzalishaji na tija. Katika mwaka wa 2003/2004, mkazo uliwekwa katika matumizi ya mbinu shirikishi jamii ili kuibua matatizo na kuainisha mikakati ya kuongeza tija na uzalishaji. Jumla ya shilingi milioni 167 zilitolewa na kutumika kuanzisha mashamba darasa 267 katika wilaya 41 ambazo ni Iringa, Arumeru, Mbulu, Babati, Kibaha, Bagamoyo, Temeke, Dodoma, Njombe, Bukoba, Ngara, Kasulu, Hai, Kilwa, Musoma, Serengeti, Bunda, Rungwe, Mbeya, Ulanga, Singida, Mtwara, Ukerewe, Sengerema, Magu, Mpanda, Songea, Mbinga, Shinyanga, Kahama, Igunga, Urambo, Korogwe, Lushoto, Sumbawanga, Morogoro, Kongwa, Tabora, Mpwapwa, Arusha Mjini, na Muheza. Wataalam 121, pamoja na wakuu wa wilaya 24 kutoka wilaya za mikoa ya Mara, Kigoma, Tabora, Morogoro, Pwani na Dodoma walifanya ziara za mafunzo ya wiki moja moja mkoani Singida kujifunza mbinu shirikishi jamii. Aidha, vipindi 52 vya mafunzo ya kilimo bora cha mazao na matokeo ya utafiti wa kilimo na ufugaji bora viliandaliwa na kutangazwa na Redio Tanzania. Wizara pia iliandaa mada tatu za video kuhusu kilimo cha paprika na vanila.
 
Jamani,

Ngoja niachie hapa, mwishoni itakuwa kama na SPAM. Ila lengo ni kuwaonyesha watu wanaodai kuwa RA hashughulikii wananyichi wake kuwa ni uongo!

Naomba mkija tena mje na Data, haya ndio mambo yanayofanya CCM iendelee kukaa madarakani milele. Unatoa tuhuma ukiulizwa data zipo wapi unasema lete wewe!!!! KHAA!! nani KATUHUMU?

Tutaendelea kumkoma nyani giladi kwa kuangalia pande zote hapa!
 
Swali kwako wewe mtetezi wa Rostam Azizi,je?huwa hayo matatizo yeye anayasilisha wapi?
Wabunge ambao ni mawaziri najua kuwa wao wanajadili kwenye cabinet mambo ya majimboni mwao je? huyu yeye anajadili wakati gani na wapi?

Ama ndio kusema kaiweka serikali yetu mfukoni ?kuwa yeye kila waziri anampa miradi hata kama hajaomba ama kushawishi ndani ya bunge?

Aangekuwa anazungumza si ajabu kuwa tungeshapata maji kule Igunga walau awe anaandika kama kuzungumza hawezi .

Kuna siku kitaeleweka na kikieleweka ni kuwa ole wao wanaoitia serikali yetu mifukoni mwao maanaa.........watalia na kusaga meno.
 
Aangekuwa anazungumza si ajabu kuwa tungeshapata maji kule Igunga walau awe anaandika kama kuzungumza hawezi .
.

Mzee kuwa makini, Hakuna matatizo makubwa ya maji IGUNGA soma hapo juu toka 2004 Maji yameshafika Igunga.

Umakini ni muhimu. Kama haUpo makini ktk kilichoandikwa AWALI na unacho discuss SASA inakuwa KAMA tunaenda hatua 10 mbele kisha tunarudi hatua 12 nyuma na kuanza kujipongeza. Hakitaeleweka kamwe kwa stahili hiyo!

Wananchi wa Igunga wanataka maendeleo, nimetaja ushaidi wa MAJI na AFYA kwa leo. Anazungumza, anaandika, anasema, anafoka sio jukumu langu mwananchi. NINACHOTAKA NI MAENDELEO. NA YAPO UKILINGANISHA NA SEHEMU NYINGINE NCHINI.

FD
 
Jamani,

Ngoja niachie hapa, mwishoni itakuwa kama na SPAM. Ila lengo ni kuwaonyesha watu wanaodai kuwa RA hashughulikii wananyichi wake kuwa ni uongo!

Naomba mkija tena mje na Data, haya ndio mambo yanayofanya CCM iendelee kukaa madarakani milele. Unatoa tuhuma ukiulizwa data zipo wapi unasema lete wewe!!!! KHAA!! nani KATUHUMU?

Tutaendelea kumkoma nyani giladi kwa kuangalia pande zote hapa!

Kama hali ndio hii kwamba mtu hawezi hata kutofautisha mgawanyo wa kazi kati ya nguzo tatu za utawala, Tanzania itachukua muda mrefu kuendelea.

Uliyoonyesha hapo ni taarifa za serikali kupitia wizara zinasomwa bungeni, aliyeandaa taarifa hizo ni serikali siyo mbunge, na inafanya hivyo kwa nchi nzima!!! lakini tulichokuwa tunasema, baada ya serikali kuja na taarifa za jinsi hiyo ni kazi ya mbunge kwanza kutoa tathmini ya hayo yaliyosemwa kama yapo na yaefanikiwa kwa kiwango kipi, lakini kuishauri serikali kama inaweza kufanya hayo hata katika sehemu nyingine za jimbo lake!! pengine zipo sehemu ambazo tatizo ni kubwa zaidi kupita hata hiyo sehemu iliyotajwa na serikali!!!!

Kwa mfano, katika suala la maji kimetajwa kijiji cha bulenya, wilaya ya igunga ina vijiji zaidi ya 136 na vyote vina matatizo ya uhaba wa huduma za maji, vijiji kama buchenjegere,mwabalatulu, kinin'ginila,imalilo nk watu wanachangia maji na mifugo!!! na hali ni mbaya sana wakati wa kiangazi, shida ya maji ni kubwa kuliko hata bulenya.

Kwa vile utatuzi wa matatizo ya huduma za jamii unaotekelezwa na serikali ni wa pole pole sana, ni kazi ya mbunge kuwa na ubunifu juu ya njia zingine kutatuzi matatizo ya wananchi, katika kuisaidia serikali!!akishirikisha wananchi wenyewe!!

Kinachoulizwa hapa ni juhudi zipi shirikishi, yeye kama mbunge anasaidiana na serikali kutatua matatizo ya igunga! na wala hizo taarifa hazina maana kwamba tayari maendeleo yameshapatikana!!! kama unabisha, kaulize huko bulenya kulikosemwa ka maji wameshapata!!hizo zinabaki kuwa taarifa tu, lakini uhalisi wake haupo!haina maana hata kuleta hizo taarifa hapa.

Lakini ukweli unabaki pale pale, kwamba mbunge ndiye sauti ya matatizo ya watu jimboni kwa kuiambia au kuikumbusha serikali, kitu ambacho rostam hafanyi!!!
 
Back
Top Bottom