Rostam (Mbunge) anawahadaa wananchi wa Igunga

Rostam (Mbunge) anawahadaa wananchi wa Igunga

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
uwa na mbunge mwarabu toka 1994
kupaa t shirt na kofia za bure kila baada ya miiaka mitano na mambo mengine kama hayo
 
Pita ukiwa unaend mza hutamini kama ndio jimbo na huyu jamaa,stand vumbi 2pu,na ipo porini hakuna rami kabisa..si mahala pazuri sana.
 
Pita ukiwa unaend mza hutamini kama ndio jimbo na huyu jamaa,stand vumbi 2pu,na ipo porini hakuna rami kabisa..si mahala pazuri sana.
nina uhakika waliozimia sio wananchi ni makada wagawa kofia ,t-shirt na takrima .. Wanajua ndio hivyo syystema ishakufa.. Toka mwana 1994 hadi 2011 sio mchezo . Mtu kakaa kwenye systema ya kugawa kofia kwa mda wote huo thena anaambiwa kuwa bwana wao anaachia ngazi unafikir ataacha kuzimika?
 
nimecheka mpaka machoz yamenitoka
asee huyu jamaa amefanya ufisadi
wooote hata stand hawez weka?
kama ipo maporini si unaweza liwa na simba?
ama ukamezwa na chatu loool
siendi huko mie mpaka stendi
iwe town



Pita ukiwa unaend mza hutamini kama ndio jimbo na huyu jamaa,stand vumbi 2pu,na ipo porini hakuna rami kabisa..si mahala pazuri sana.
 
nasikia kuna mto ukiuvuka ndipo huenda watu wakizikwa. Alipanga kuwajengea labda ndio maana watu wamezimia!
Mbona nae anaishi nao huko huko!
 
nimecheka mpaka machoz yamenitokaasee huyu jamaa amefanya ufisadi wooote hata stand hawez weka?kama ipo maporini si unaweza liwa na simba?ama ukamezwa na chatu looolsiendi huko mie mpaka stendiiwe town
Si unajua nwdays bus lazma lipite stand kila wilaya,igunga stand utadhan ushaacha mji kumbe ndio stand..kiukweli pamechoka,afu wanalialia hovyo.
 
Wanasikitika kwa kumkosa mbunge wao kipenzi 'semi-mzungu'!
 
Pita ukiwa unaend mza hutamini kama ndio jimbo na huyu jamaa,stand vumbi 2pu,na ipo porini hakuna rami kabisa..si mahala pazuri sana.

Mi nilipita hiyo njia 2009, nika icheki ile stand nikajiuliza kama stand tu pako hivi huko vijijini kukoje? Baada ya kusoma maelezo ya Rostam jana, nikabaki najiuliza huko Igunga kulikuwaje kabla ya 1994?? Mana kwa maelezo yake anasema tangu amekua mbunge wa hilo jimbo kumekuwa na maendeleo makubwa sana...Jamani huyu jamaa mbona anataka kutufunga kamba hivi? Anyway labda tathmini yangu haikuwa nzuri.
 
Mi nilipita hiyo njia 2009, nika icheki ile stand nikajiuliza kama stand tu pako hivi huko vijijini kukoje? Baada ya kusoma maelezo ya Rostam jana, nikabaki najiuliza huko Igunga kulikuwaje kabla ya 1994?? Mana kwa maelezo yake anasema tangu amekua mbunge wa hilo jimbo kumekuwa na maendeleo makubwa sana...Jamani huyu jamaa mbona anataka kutufunga kamba hivi? Anyway labda tathmini yangu haikuwa nzuri.
wananchi wapo ndani ya chupa wamefungwa masikio ..laboda hilo vumbi na barabara kuchongwa ndio wanafikiri kuwa hayo ni maendeleo.. hivi watu wangapi wa igunga wapo hapa JF???
 
Habari za leo wana jf
napenda kuongelea suala la ubunge igunga. Wilaya ya igunga imerudi nyuma kimaendeleo kielimu,kiuchumi na hata kifikira tangu alipofariki kabeho. Baada ya rostam kuachia ngazi sasa wanaigunga wanapumua vizuri. Imefika wakati sasa wa wananchi wa igunga kuchagua mtu makini sana ambaye atasimama kidete kwa maendeleo ya igunga. Igunga kwa taarifa ina wasomi kadhaa ambao wakao ndani na nje ya nchi. Kuna watu kama dr. Kafumu kamishna wa madini,inishati na madini, mboje ambaye anataaluma ya masuala ya uvuvi, wizara ya mifugo na uvuvi nasikia yuko marekani kimasomo,malembela shile ambaye yuko kigoma mkuu wa shule,jafary omary sukari kilimanjaro ,hamis mapinda mkonge tanga na wengine wengi wenye uhusiano mzuri na mataifa ya nje wanaweza wakawa viongozi wazuri sana katika jimbo la igunga na likawa mfano wa kuigwa. Watu wa igunga msiletewe watu ambao hawatakuwa na maana katika maendeleo ya jimbo lenu.chagueni mtu ambaye atasikiliza na kutafuta ufumbuzi wa matatizo yenu, asiyepokea wa kutoa rushwa, mtu ambaye atatatua matatizo ya maji, madaraja, kilimo, elimu afya na mengine mengi. Anatakiwa mtu makini ambaye ataona mbali na kufanya vitu vya ukweli.
Hao watu niliowataja chama chochote kiangalie namna yakuwatumia kwa manufaa ya wanaigunga na nchi kwa ujumla.
Hawa ni wasomi wakubwa na viongozi wenye dira. Wajaribuni kwenye tanuru ya moto muone kama wanafaa kwa uongozi thabiti.

Ituganhila mashi
igunga
 
Wewe unasema Igunga imerudi nyuma hukuwaona wenzako juzi wanamlilia Rostum? Wanasema amewaletea maendeleo. Wewe unazungumzia Igunga ipi? Sikonge, naomba msaada wako tafadhali.
 
Bora rostam anaeliliwa na wananchi wake,maana baniani mbaya kiatu chake dawa. Serikali inashindwa kuwahudumia wananchi. fisadi anaweza.bora nani?mkono anaeabudiwa na wananchi wake au ****** anaesafiri kila kukicha?au muongeaji sana asiye na msaada?mnyonge mnyongeni.. Rostam aziz tunamuomba aendelee kutusaidia hususan huduma za afya hapa igunga..
 
Bora rostam anaeliliwa na wananchi wake,maana baniani mbaya kiatu chake dawa. Serikali inashindwa kuwahudumia wananchi. fisadi anaweza.bora nani?mkono anaeabudiwa na wananchi wake au ****** anaesafiri kila kukicha?au muongeaji sana asiye na msaada?mnyonge mnyongeni.. Rostam aziz tunamuomba aendelee kutusaidia hususan huduma za afya hapa igunga..

Hiki ndo viongozi wengi wa CCM wanachotaka na ndipo walipowafikisha wananchi wa kawaida. Wakiingia serikalini kazi yao ni kuendeleza ufisadi na kuua uwezo wa serikali kuwahudumia wananchi ili hatimaye wao ndo waonekane wanatatua matatizo ya wananchi. Huwezi kusema serikali inashindwa halafu fisadi (kiongozi wa serikali) anaweza; anawezaje na lengo lake ni nini? Lengo lake ni kuwatia wananchi utumwani ili yeye abaki ndo bwana wao. Viongozi wote wa namna hii ni viongozi wa hatari sana na hawafai kabisa, yaani viongozi wanaoshangiliwa wao wakati taasisi wanazoziongoza zikizomewa, mfano;
  • Mkuu wa kituo anasifiwa na kupendwa wakati maaskari wote anaowaongoza wakilalamikiwa kuwa hawafai
  • Mwalimu mkuu wa shule anayesifiwa kuwa ni bora huku shule anayoongoza ikiwa mbovu na hovyo
  • Rais wa nchi anayeshangiliwa huku mawaziri wake wakizomewa
  • N.K.
Ubora wa kiongozi lazima uonekane katika kile anachokiongoza. Ubora wa mbunge lazima uonekane kwa jinsi serikali anayoisimamia inavyofanya kazi vizuri. Wananchi wengi wameshaaminishwa kuwa wabunge ni wawakilishi wao, ila hawajui ni wawakilishi wao katika nini?? Kwa hiyo wengi hufikiria kuwa wabunge wao wanapolipwa maposho makubwa bungeni ni haki yao kwani wanakula kwa niaba yao!! Hawajui kuwa kazi ya kwanza ya mbunge ni kuisimamia serikali na kuhakikisha kuwa inafanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu walizozitunga ili zitoe huduma bora kwa wananchi.

Kwa hiyo huwezi kumsifia mbunge anayewajengea wananchi shule wakati serikali anayoisimamia imeshindwa! Ana lengo lake huyo, na lengo lake ni kuwafanya wananchi wamuone yeye badala ya kuiona serikali. Matokeo yake mbunge anaitia serikali mfukoni kwake halafu wananchi badala ya kwenda serikalini kutafuta huduma anawaambia waje kwake!! Huyo ni wa kuogopwa kama ukoma!
 
Back
Top Bottom