Rose Muhando: Safari ya mateso, huzuni, furaha hatimae ushindi

Pamoja na kwamba mimi ni Muislam, nampenda sana Rose Muhando. Yani nampenda kuliko ninavyoweza kuelezea.
Hakuna album wala wimbo wake ambao haupo katika simu yangu.

Hizi ni nyimbo zangu bora zaidi kutoka kwake...
1. Mteule uwe macho: Huu wimbo nahisi alisaidiwa na malaika kuuandika, ujumbe na vingi alivyoimba vinatokea hii leo!
Yalikuwa maono. Huu ndio wimbo wangu bora wa muda wote wa injili.

2. Kumbe ndivyo ulivyo: Huu wimbo nikiusikiliza huwa hadi nalia, aliimba kwa hisia kali na ni wimbo wa faraja. Nyakati
zangu za huzuni huwa nausikiliza sana.

3. Akina mama: Huku wanawake tumechambwaaaa, ila una mafunzo na nitayazingatia. Lol

4. Nakaza mwendo: Ni wimbo uliojaa matumaini na kutokujali sana ya dunia, naupenda.

5. Nibebe: Nafikiri huu ndio wimbo mkubwa zaidi kutoka kwake, ulikuwa ufunguo wake kimataifa. Ujumbe wake
sidhani kama nahitaji kuuelezea. Una majonzi ya uchungu wa usaliti kutoka kwa watu wa kuaminika.

6. Ee Mungu nitakushukuru: Huu wimbo huwa nausikiliza kila ninapohitaji kujikumbusha ukubwa wa Mungu na kuomba
kwake busara na hekima.
Nafikiri uko kwenye evolution stage.unatoka kwenye dini unaelekea kwenye IMANI ambayo ndiyo msingi wa mahusiano.
Watu wanadhani katika dini tunapata imani,ila kumbe katika IMANI ndo tunapata dini.
 
Pamoja na kwamba mimi ni Muislam, nampenda sana Rose Muhando. Yani nampenda kuliko ninavyoweza kuelezea.
Hakuna album wala wimbo wake ambao haupo katika simu yangu.

Hizi ni nyimbo zangu bora zaidi kutoka kwake...
1. Mteule uwe macho: Huu wimbo nahisi alisaidiwa na malaika kuuandika, ujumbe na vingi alivyoimba vinatokea hii leo!
Yalikuwa maono. Huu ndio wimbo wangu bora wa muda wote wa injili.

2. Kumbe ndivyo ulivyo: Huu wimbo nikiusikiliza huwa hadi nalia, aliimba kwa hisia kali na ni wimbo wa faraja. Nyakati
zangu za huzuni huwa nausikiliza sana.

3. Akina mama: Huku wanawake tumechambwaaaa, ila una mafunzo na nitayazingatia. Lol

4. Nakaza mwendo: Ni wimbo uliojaa matumaini na kutokujali sana ya dunia, naupenda.

5. Nibebe: Nafikiri huu ndio wimbo mkubwa zaidi kutoka kwake, ulikuwa ufunguo wake kimataifa. Ujumbe wake
sidhani kama nahitaji kuuelezea. Una majonzi ya uchungu wa usaliti kutoka kwa watu wa kuaminika.

6. Ee Mungu nitakushukuru: Huu wimbo huwa nausikiliza kila ninapohitaji kujikumbusha ukubwa wa Mungu na kuomba
kwake busara na hekima.
Dah unazikumbuka vizuri nyimbo zake. We itakua sio muislamu kiviiile.
 
Huyu mama ana balaa.....
Ni aibu wabongo tulifurahia anguko lake, i dont care anachoimba ni gospel au lah but ana balaa.
 
Back
Top Bottom