Rose Muhando: Safari ya mateso, huzuni, furaha hatimae ushindi

Just Distinctions

JF-Expert Member
May 5, 2016
2,696
5,324
Katika mmoja ya wasanii ambao Tanzania imebarikiwa kuwa nao na wana vipaji vya ajabu ni Rose Muhando hakika hakuna atakaepinga hilo na nyimbo zake kwa miaka mingi zimetubariki na kutusogeza karibu na muumba kwa namna ya pekee kabisa, Mungu aendelee kumbariki.

Wengi wasichokijua ni kuwa Rose Muhando alizaliwa katika familia ya kiislamu na akapewa jina la Shadya Muhando na akapata makuzi ya dini hiyo akiimba kaswida na kujifunza Quran ambapo alimudu kuhifadhi juzuu zote 30 na anasema alikuwa na bidii kubwa sana Madrasa.

Baba yake alikuwa ni Sheikh mkubwa tu huko Dumila Morogoro na ndio alimpa muongozo ya dini hiyo.

Alipokuwa mdogo aliugua na kukonda sana kitu kilichomsumbua kwa muda mrefu na afya yake ilikuwa dhoofu kisa hayo maradhi

Ilifikia kipindi anasema alikonda sana kiasi akilalia mkeka ngozi inashikana na kubaki kwenye mkeka

Familia ilijaribu kumpa matibabu mpaka kwa waganga mbalimbali lakini hakufanikiwa kupata tiba hivyo familia ikaacha tu liwalo na liwe kwani imeshindikana

Wakati akiwa bado mahututi kitandani anajiuguza na hajajiweza kwa muda wa mwaka mmoja siku moja usiku mwangaza mkubwa ulitokea nyumbani kwao ambapo yeye, Baba yake na Mama yake waliuona

Ndani ya ule mwangaza alimuona mtu mweupe ambaye alijitambulisha kama masihi akimwambia inuka nimekuponya ili uje unitumikie

Baada ya mwanga kupotea alipiga yowe akihisi ni ndoto kuwa amepona na kweli akaweza kusimama, Baba na Mama yake walipigwa na butwaa wasijue cha kusema kwani waliuona mwangaza japo yale maneno aliyoyasikia Rose hawakusikia

Kesho yake ilikuwa gumzo kubwa mtaani kwao iweje mtu aliye lala takribani mwaka mzima mahututi ndani kuweza kunyanyuka ndani ya usiku mmoja tu kufumba na kufumbua

Baada ya hapo alijiuliza sana yule mtu ni nani, asipate majibu wakati huo alikuwa na miaka 9 na sauti hiyo ilikuwa ikiendelea kujirudia mara kwa mara

Kuna jirani yao walimmegea shamba ili awe analima alikuwa ni mlokole na alikuwa anataja mara kwa mara jina la mtu huyo

Ndipo Rose alipomfata na kumwambia amwambie habari za mtu huyo ni nani na ikibidi ampeleke kwake maana alisikia sauti yake akijitambulisha kwa jina ila hamjui

Yule Mama Mlokole akamjulisha kuwa huyo unaemsema ni YESU na hayupo hapa duniani bali mbinguni, ila akamshauri akitaka kumjua zaidi hana budi kuokoka na kukubali kubatizwa

Alipofika miaka kumi na miwili akarudisha juzuu madrasa na akamwambia Baba yake anaenda kubatizwa, hii ilizua tafrani nyumbani na kwa nduguze

Siku ya kubatizwa wengi walijaa kanisani kuona kwani alikuwa anafahamika na wengi hapo Dumila

Akabatizwa katika kanisa la Anglikana hapo Dumila, na kupewa Jina Rose lakini uamuzi huo haukupokelewa vyema na nduguze hatimae akafukuzwa kwao na kuhangaika mitaani mpaka watu wa kanisani walipomchukua na kumuhifadhi

Akaanza kuimba kwaya, alipoiva zaidi akaanza kufundisha yeye kutokana na kutokea katika dini isiyo ya ukristo akashauriwa kujifunza masomo ya biblia ambapo aliisoma kwa muda wa miaka miwili huko Morogoro

Akaenda Arusha kufundisha kwaya, kisha akarejea Dodoma ambapo alifanya kazi ngumu ili aishi, mwaka 1997 akataka kurekodi nyimbo zake mwenyewe alipomshirikisha mmoja ya watu kanisani akamshauri wafunge na kuomba ili wapate jibu

Jibu lilikuja asubiri miaka saba ndipo arekodi, akakata tamaa juu ya muziki hasa kurekodi nyimbo zake mwenyewe akaendelea tu na maisha

Baadae sana, alimwomba mchungaji mmoja amsaidie kurekodi baada ya kuulizwa angependa afanye nini, akaenda Dar kwa Master Jay ambapo alitunga albamu nzima kwa siku tatu na kufanya mazoezi ndani ya siku tatu peke yake

Kisha alirekodi nyimbo zote ndani ya siku moja tena one take bila kukosea mpaka studio wakashangaa, hakujua afanye nini baada ya kurekodi kwani yeye kiu yake ilikuwa kurekodi tu basi

Prodyuza akamshauri apeleke albamu kwa wahindi kwani wengine wanapeleka huko, basi akaipeleka albamu na ikatokea kupendwa sana ndipo akakumbuka kuwa nyuma alipata ufunuo kuwa asubiri mpaka baada ya miaka 7 ili arekodi na mwaka huo wa saba ndio 2004 albamu ya mteule uwe macho inaingia sokoni

Ndipo alipostaajabu juu ya kufunuliwa kule na jinsi ilivyokuja kuwa kweli

Tokea hapo kilichofuatia ni historia wote mnakijua, na hiyo ndio historia fupi ya huyu Mama mwenye sauti ya kipekee

(nimeiandika kwa upendo tu kama kuna mahali nimekosea mniwie radhi)

SOURCE : ushuhuda alioutoa kanisani inapatikana pia Youtube pia na mahojiano na vituo mbalimbali vya habari ikiwemo Clouds Media.
 
rose ana sauti ya ajabu sana.napenda nyimbo alizoimba akiwa ametulia sio zile za mchakamchaka.
zipo clip anaimba live kabisani dodoma wanakwaya wenzake,hata studio wanakiri ni kazi nyepesi sana kurekodi wimbo na rose.

bahati mbaya baada ya kuanguka watanzania tulimtosa,mpaka wakenya wakaiona fulsa na kumfanya anyanyuke tena.

Mungu aendelee kumtumia.
 
rose ana sauti ya ajabu sana.napenda nyimbo alizoimba akiwa ametulia sio zile za mchakamchaka.
zipo clip anaimba live kabisani dodoma wanakwaya wenzake,hata studio wanakiri ni kazi nyepesi sana kurekodi wimbo na rose.

bahati mbaya baada ya kuanguka watanzania tulimtosa,mpaka wakenya wakaiona fulsa na kumfanya anyanyuke tena.

Mungu aendelee kumtumia.
Amina hakika ana sauti ya kipekee sana, na kupitia sauti yake tunapata mibaraka ya kipekee, hakika Mungu aendelee kumtumia ili awarudishe walio kizani mwangani
 
Kwani hao 1.8 unaosema wote walimuona Mohammed?? Usiwe na mawazo hasi kana kwamba tunashindana tumia hata akili ya kuvukia barabara kufikiri sahihi
Kama ukristo ndo dini sahihi kwanini Yahweh anaruhusu uwepo wa waislamu?

Hivi rose ukimuangalia haraka haraka yupo sawa kichwani?

Anatunga visa tu
 
Katika mmoja ya wasanii ambao Tanzania imebarikiwa kuwa nao na wana vipaji vya ajabu ni Rose Muhando hakika hakuna atakaepinga hilo na nyimbo zake kwa miaka mingi zimetubariki na kutusogeza karibu na muumba kwa namna ya pekee kabisa, Mungu aendelee kumbariki.

Wengi wasichokijua ni kuwa Rose Muhando alizaliwa katika familia ya kiislamu na akapewa jina la Shadya Muhando na akapata makuzi ya dini hiyo akiimba kaswida na kujifunza Quran ambapo alimudu kuhifadhi juzuu zote 30 na anasema alikuwa na bidii kubwa sana Madrasa.

Baba yake alikuwa ni Sheikh mkubwa tu huko Dumila Morogoro na ndio alimpa muongozo ya dini hiyo.

Alipokuwa mdogo aliugua na kukonda sana kitu kilichomsumbua kwa muda mrefu na afya yake ilikuwa dhoofu kisa hayo maradhi

Ilifikia kipindi anasema alikonda sana kiasi akilalia mkeka nyama inashikana na kubaki kwenye mkeka

Familia ilijaribu kumpa matibabu mpaka kwa waganga mbalimbali lakini hakufanikiwa kupata tiba hivyo familia ikaacha tu liwalo na liwe kwani imeshindikana

Wakati akiwa bado mahututi kitandani anajiuguza na hajajiweza kwa muda wa mwaka mmoja siku moja usiku mwangaza mkubwa ulitokea nyumbani kwao ambapo yeye, Baba yake na Mama yake waliuona

Ndani ya ule mwangaza alimuona mtu mweupe ambaye alijitambulisha kama masihi akimwambia inuka nimekuponya ili uje unitumikie

Baada ya mwanga kupotea alipiga yowe akihisi ni ndoto kuwa amepona na kweli akaweza kusimama, Baba na Mama yake walipigwa na butwaa wasijue cha kusema kwani waliuona mwangaza japo yale maneno aliyoyasikia Rose hawakusikia

Kesho yake ilikuwa gumzo kubwa mtaani kwao iweje mtu aliye lala takribani mwaka mzima mahututi ndani kuweza kunyanyuka ndani ya usiku mmoja tu kufumba na kufumbua

Baada ya hapo alijiuliza sana yule mtu ni nani, asipate majibu wakati huo alikuwa na miaka 9 na sauti hiyo ilikuwa ikiendelea kujirudia mara kwa mara

Kuna jirani yao walimmegea shamba ili awe analima alikuwa ni mlokole na alikuwa anataja mara kwa mara jina la mtu huyo

Ndipo Rose alipomfata na kumwambia amwambie habari za mtu huyo ni nani na ikibidi ampeleke kwake maana alisikia sauti yake akijitambulisha kwa jina ila hamjui

Yule Mama Mlokole akamjulisha kuwa huyo unaemsema ni YESU na hayupo hapa duniani bali mbinguni, ila akamshauri akitaka kumjua zaidi hana budi kuokoka na kukubali kubatizwa

Alipofika miaka kumi na miwili akarudisha juzuu madrasa na akamwambia Baba yake anaenda kubatizwa, hii ilizua tafrani nyumbani na kwa nduguze

Siku ya kubatizwa wengi walijaa kanisani kuona kwani alikuwa anafahamika na wengi hapo Dumila

Akabatizwa katika kanisa la Anglikana hapo Dumila, na kupewa Jina Rose lakini uamuzi huo haukupokelewa vyema na nduguze hatimae akafukuzwa kwao na kuhangaika mitaani mpaka watu wa kanisani walipomchukua na kumuhifadhi

Akaanza kuimba kwaya, alipoiva zaidi akaanza kufundisha yeye kutokana na kutokea katika dini isiyo ya ukristo akashauriwa kujifunza masomo ya biblia ambapo aliisoma kwa muda wa miaka miwili huko Morogoro

Akaenda Arusha kufundisha kwaya, kisha akarejea Dodoma ambapo alifanya kazi ngumu ili aishi, mwaka 1997 akataka kurekodi nyimbo zake mwenyewe alipomshirikisha mmoja ya watu kanisani akamshauri wafunge na kuomba ili wapate jibu

Jibu lilikuja asubiri miaka saba ndipo arekodi, akakata tamaa juu ya muziki hasa kurekodi nyimbo zake mwenyewe akaendelea tu na maisha

Baadae sana, alimwomba mchungaji mmoja amsaidie kurekodi baada ya kuulizwa angependa afanye nini, akaenda Dar kwa Master Jay ambapo alitunga albamu nzima kwa siku tatu na kufanya mazoezi ndani ya siku tatu peke yake

Kisha alirekodi nyimbo zote ndani ya siku moja tena one take bila kukosea mpaka studio wakashangaa, hakujua afanye nini baada ya kurekodi kwani yeye kiu yake ilikuwa kurekodi tu basi

Prodyuza akamshauri apeleke albamu kwa wahindi kwani wengine wanapeleka huko, basi akaipeleka albamu na ikatokea kupendwa sana ndipo akakumbuka kuwa nyuma alipata ufunuo kuwa asubiri mpaka baada ya miaka 7 ili arekodi na mwaka huo wa saba ndio 2004 albamu ya mteule uwe macho inaingia sokoni

Ndipo alipostaajabu juu ya kufunuliwa kule na jinsi ilivyokuja kuwa kweli

Tokea hapo kilichofuatia ni historia wote mnakijua, na hiyo ndio historia fupi ya huyu Mama mwenye sauti ya kipekee

(nimeiandika kwa upendo tu kama kuna mahali nimekosea mniwie radhi)

SOURCE : ushuhuda alioutoa kanisani inapatikana pia Youtube pia na mahojiano na vituo mbalimbali vya habari ikiwemo Clouds Media.
Wasanii wenye mafanikio wengi ni WAKOROFI.
 
Back
Top Bottom