Robert Kisena atangaza kufilisika kwa UDA

Robert Kisena atangaza kufilisika kwa UDA

Huu ni usanii mwingine katika harakati za kukwepa rungu la JPM.Achekiwe kuhakikisha kama alilipa kodi zetu ipasavyo vinginevyo mali zake zikamatwe,tena fast kwa kuwa anaweza kuanza kuziuza..
Habari wadau,

Mmiliki wa UDA Ndugu Robert Kisena atangaza kufilisika kwa UDA kutokana na Madeni makubwa anayodaiwa ambayo inazidi fedha zilizomo kwenye account ya UDA.

Kampuni hiyo ambayo amesema ina magari kwa sasa 50 ambayo ni spana mkononi.

Madeni hayo ni bilioni 2 alizokwepa mwaka 2012 alipoingiza mabasi nchini na kutopeleka Michango ya NSSF na PAYE za wafanyakazi.

Chanzo: Dira
 
Hawa ndio wale waliopewa BRT... mradi wa mabasi yaendayo kasi.Naona wanafilisika kwa kasi.
 
Nayakumbuka maneno ya Membe kuwa hawa wafanyabiashara ni wa kwenda nao taratibu. Bila ya kuwa waanagalifu, wengi watafunga biashara zao na kusababisha matatizo mengine kama vile ukosefu wa ajira na upungufu wa makusanyo ya serikali.

Wabanwe ili waweze kulipa kodi lakini kwa werevu badala ya kuwaendea kama maadui wa Taifa. Wengi wao hawana shida kama wengi tunavyofikiria, na wanaweza kwenda mahali pengine popote na mitaji yao.
Hawawezi kwenda kokote wamezoea kuiba wakienda china watanyongwa. Wakienda nchi zilizoendelea watafungwa magerezani ni bora wabaki bongo wajifunze umuhimu wa kulipa kodi .
 
Swali rahisi kwa wana bodi!!!!
Hivi Procedure za kutangaza kuwa kampuni imefilisika hapa Tanzania ni rahisi kiasi hicho? Je kwa kampuni yenye assets na liabilities kubwa kama UDA ni nani anayetakiwa kutangaza kwamba kampuni mefilisika? Hivi si mpaka itafutwe kampuni ya ukaguzi ambayo intergrity yake haina wasiwasi wakague mali na madeni, wakishamaliza wawasilishe hesabu hizo kwenye bodi na bodi iridhike kisha mwanasheria wa kampuni atangazie uma kwa utaratibu uliowekwa?

Mkuu hizo ndizo kanuni sahihi za kufuata kabla kampuni haijaji tangaza mufilisi, huwezi ukahamuka asubuhi moja na ku declare kampuni kufilisika kabla wahusika hawajapitia/kagua vitabu vyako vya mahesabu kujua what a hell was going ON?
 
Kama ni kweli Bwana Kisena ametangaza kufilisika, na kwa kuwa serikali nayo ina hisa zake kweye kampuni hio na kwa kuwa UDA iliendeshwa kwa ubia kati yake Bwana Kisena na Serikali basi walitaka kuendelea kuchota fedha kutoka hazina ili ziendelee kufidia gharama za uendeshaji.

Kwa kuwa alikwenda benki kuomba mkopo zaidi na kwa kuwa benki wameona hawawezi kuendelea kutoa fedha Zaidi ya mkopo kwa vile kampuni ya bwana Kisena ina deni kubwa kuliko mali halisi inayomiliki, basi benki wamekataa kutoa mkopo zaidi.

Yaani benki wamemfanyia bwana Kisena "risk assessment" na credit rating yake hairidhishi.

Kwa kuwa bwana Kisena alikwenda kuwaataarifu wahusika wakuu wa huo UFISADI wa kutumia UDA kuhujumu uchumi wa nchi, wahusika wamesita kuendeleza ushirikiano wa kuendelea kuiibia nchi kupitia huo Mradi.

Kwa kifupi ni kwamba pesa ya walipa kodi ndio ingeendelea kutumia kufadhili haya makampuni ya aina ya UDA na mengine.

Kikwazo ni raisi wetu mpya JPM na serikali yake ya awamu ya tano.

Ewe Mungu mlinde raisi wetu JPM aendelee kutumbua haya majipu hata kwa kutumia king'amuzi au "remote control" maana majipu mengine yashaanza kujitumbua yenyewe.

Mungu Ibariki Tanzania.
Ndugu yangu

Huko Benki hawa UDA walikuwa ni matapeli

wanakopa alafu hawalipi...Deni linakuwa non performing

Kwenye mabenki yote walikokopa wanasumbuana mahakamani sasahivi

Kitakachofuatia ni kuziuza mali zao na kulipa madeni kwanza
 
Swali rahisi kwa wana bodi!!!!
Hivi Procedure za kutangaza kuwa kampuni imefilisika hapa Tanzania ni rahisi kiasi hicho? Je kwa kampuni yenye assets na liabilities kubwa kama UDA ni nani anayetakiwa kutangaza kwamba kampuni mefilisika? Hivi si mpaka itafutwe kampuni ya ukaguzi ambayo intergrity yake haina wasiwasi wakague mali na madeni, wakishamaliza wawasilishe hesabu hizo kwenye bodi na bodi iridhike kisha mwanasheria wa kampuni atangazie uma kwa utaratibu uliowekwa?

Ikumbukwe kwamba kila (LTD) kampuni inatakiwa kuwasilisha mahesabu yake yaliyokaguliwa na mkaguzi wa nje kila mwisho wa mwaka wa kampuni kwa TRA na mamlaka za leseni. Hatutegemei kazi kubwa sana hapo kama hayo yalikuwa yanafanyika, otherwise hawa na wale wa HSC hawana namna ya kukimbia sheria hapa, ni lazima mamlaka zipewe mahesabu yaliyokaguliwa kupona namna gani "going concern" ilivyokuwa ikihakikishwa. The funny thing is, utakuta wamehakikisha going concern vizuri sana kwa sababu waklihitaji mikopo na ni mwaka jana tu hawa Simons walikuwa wanasaka mikopo ambayo hawawezi kupewa bila kuhakikisha uwezo wao wa kulipa madeni ya muda mrefu na kutimiza mahitaji ya kila siku kwa wadau wake (waajiriwa, suppliers etc).

Nakuhakikishia, kwa mahesabu ya kitaalam ni kwamba hawa wawili hawawezi kutudanganya ati kwamba wamefilisika wakati waliomba mikopo mikubwa.
 
Hawa ndio wale waliopewa BRT... mradi wa mabasi yaendayo kasi.Naona wanafilisika kwa kasi.
Madai yao wanataka waonewe huruma waruhusiwe kuchaji bei kubwa ili wasifilisike
 
walipiga sana hawa walikataza mabasi mengine yasifanye kazi ruti ya mnazi mmoja to kivukon wakabaki wenyewe tu na wakawa nachaj premium imagine licence gan ya ruti ya kivukoni mpaka mnazi mmoja? biashara gan haina ushindan? au kwa vile walikua wanakaa ikulu jion anachukua hesabu pale pale anakaa anahesabu ruti zake tuu
 
Mambo haya yanatokea hapa Tanzania tu,ingekuwa CHINA tungeishia kusoma historia zao tu!!!!!!

HIVI TUMELOGWA???????????????????????????????????AAAAAAAAAAGGGGGGGHHHHHH!!!!
 
Hawa ndio wale waliopewa BRT... mradi wa mabasi yaendayo kasi.Naona wanafilisika kwa kasi.

Hahaha hapo wamesoma alama za nyakati wakajua in future UDA ni msala usio poneka kabisa the best way ni kujitangaza mufilisi hahahah, Nji hii ni uwanja wa BIBI kweli.

Viongozi walipo baada ya kujitakasa ndio kabisaa wanajichafua Moja haikai wa Mbili haisimami


My Take;
JPM usipo weka mbele masalahi ya nchi yako vyema na watu wako ulio wateua hapo IKULU nchi itawashinda tuuu piga ua galagaza
 
Kazi na ianze sasa wametutesa tunapanda gari kutoka gongo la mboto linaishia mnazi mmoja wao wanakula kilaini hadi ferry
 
HAHAHA HIVI KUNA TOFAUTI YA UDA NA U DART MAANA NIMESIKIA ZOTE MBILI ZIKITAJWA ASUBUHI KWENYE MAGAZETI
UDA na DART ni watu wawili tofauti, UDA walipewa tender ya kuendesha mradi wa DART kwa sabb wana uzoefu wa kusimamia na kuendesha route nyingi Dsm,
Yale mabasi mengi tulioyaona UDA walijisikia nayo ni ya DART na sio UDA
 
Ikumbukwe kwamba kila (LTD) kampuni inatakiwa kuwasilisha mahesabu yake yaliyokaguliwa na mkaguzi wa nje kila mwisho wa mwaka wa kampuni kwa TRA na mamlaka za leseni. Hatutegemei kazi kubwa sana hapo kama hayo yalikuwa yanafanyika, otherwise hawa na wale wa HSC hawana namna ya kukimbia sheria hapa, ni lazima mamlaka zipewe mahesabu yaliyokaguliwa kupona namna gani "going concern" ilivyokuwa ikihakikishwa. The funny thing is, utakuta wamehakikisha going concern vizuri sana kwa sababu waklihitaji mikopo na ni mwaka jana tu hawa Simons walikuwa wanasaka mikopo ambayo hawawezi kupewa bila kuhakikisha uwezo wao wa kulipa madeni ya muda mrefu na kutimiza mahitaji ya kila siku kwa wadau wake (waajiriwa, suppliers etc).

Nakuhakikishia, kwa mahesabu ya kitaalam ni kwamba hawa wawili hawawezi kutudanganya ati kwamba wamefilisika wakati waliomba mikopo mikubwa.
Hii kwa Tanzania ya zamani ilikuwa ndoto, wafanya biashara wamezifilisi bank nyingi tuu kwa kuchukua mikopo bila mpangilio, fanya research kidogo utaona wengi wanafilisi kampuni ili kukwepa mikopo halafu wanaenda anzisha kampuni nyingine
 
Pamoja na harufu kali ya ufisadi biashara ya mabasi ya abiria Ni. Kichaa
Angalia Kamata,Uda original,Salama buses,Buffalo,Mtei trans,Mohamed trans na kubwa lao Scandinavia express na kampuni nyingi za mabasi yote yamekufa ama Yana hali mbaya
Exception ni yule mwenye ma DCM ya Gongo la Mboto
 
Back
Top Bottom