Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Six Man

JF-Expert Member
Dec 19, 2017
254
892
Matairi meusi ya ndege ya shirika la ndege la kimataifa la Kenya (Kenya airways) yaligusa taratibu katika ardhi ya uwanja wa kimataifa wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar es salaam. Abiria wengi walianza kushuka katika ndege hiyo kwa kutumia ngazi ndefu nyeupe iliyotokea baada ya ndege hiyo kutua. Baada ya abiria wote kushuka ndani ya ndege na kumaliza taratibu zote za uwanja wa ndege, walianza kutoka nje ya uwanja huo mkubwa zaidi nchini Tanzania.

Katika eneo la kupokea wageni kulikuwa na umati mkubwa sana wa madereva teksi na watu mbalimbali waliokuwa wakisubiri wageni wao. Wengi wao walikuwa na vibao vyenye majina ya ndugu zao walivyovinyoosha juu. Miongoni mwa washika vibao hao alikuwemo Joyce.

Joyce alikuwa amevaa suti nyeusi ya kike iliyombana vyema hasa katika maeneo ya mapaja, huku kwa chini akiwa amevaa viatu virefu vya rangi nyeusi pia. Mkono wake wa kulia alishika kibao kidogo chenye maandishi meusi alichokinyoosha juu, kilikuwa kimeandikwa maneno sita...

'Karibu sana Tanzania Bwana Alexander Helb'.

Macho ya Joyce yalikuwa hayatulii sehemu moja. Mara kwa mara yalikuwa katika ziara isiyo rasmi ya kuangalia huku na kule, yakimtafuta huyo mgeni wake. Kama ungelikuwa umekaa pembeni na kumtazama kwa 'makini' Joyce, kitu ambacho ungegundua kuwa alikuwa ni mtu aliyekuwa amejawa na wasiwasi na uwoga.

Kwa mbali, mita kama ishirini hivi mbele yake alimwona kijana mmoja wa kizungu. Kijana alikuwa amevaa fulana ya rangi nyeupe ambayo kwa mbele ilikuwa na picha ya mbwa mdogo mweusi, huku chini akiwa amevaa suruali nyeusi ya kitambaa na raba nyeupe zenye mchoro wa mbwa mdogo mweusi pia. Mgongoni kwake alikuwa amebeba begi kubwa kiasi lenye rangi nyeusi lenye mchoro wa nyota tatu nyeupe.
Kwa tahadhari kubwa, Joyce alimsogelea yule mzungu.

"Ni mwenyewe niliyemuona kwenye picha.." Joyce alijisemea kimoyomoyo huku akimsogelea kwa tahadhari kubwa.

"Karibu sana Tanzania, Mr Alexander Helb" Joyce alisema kwa Kingereza huku akimpa mkono yule mzungu.

"Ahsante sana binti" Alexander alijibu huku akimpa naye mkono wake.

"Kumbe unajua kiswahili?' Joyce aliuliza kwa mshangao.

"Nafahamu lugha kumi na tatu za mataifa mbalimbali hapa duniani, kiswahili ikiwa ni lugha mojawapo" Alexander alijibu kwa kiswahili safi.

"Safi sana, ni fahari sana kwetu kuona lugha yetu imefika mbali kiasi hicho, mimi ninaitwa Joyce , nimetumwa na Mzee nije kukupokea" Joyce alisema huku akitabasamu.

"Ahsante sana Joyce. Mimi ninaitwa Thamani." . Alexander alisema huku akisugua pua mara tatu kwa mkono wake wa kushoto. Hapo ndipo Joyce alipoamini kwamba huyu ndiye aliyepaswa kumpokea.

Huyu ndiye Alexander Helb...

Joyce na Alexander waliongozana hadi katika gari la Joyce alililokuwa amelipaki pembezoni mwa uwanja wa ndege.
Wakaingia.
Joyce akiwa kaingilia upande wa kulia, wakati Alexander aliingilia upande wa kushoto. Joyce alishika usukani kwa mkono wa kushoto na kutia gari moto kwa mkono wake wa kulia, wakaanza kutoka taratibu katika eneo la uwanja wa ndege.

"Karibu sana kazini.." Joyce alimwambia Alexander.

Alexander alimwangalia tu, akatabasamu.

"Ni yeye" Joyce alisema kwa sauti ndogo.

***

Mita kama mia mbili, kutoka katika gari waliloingia wakina Joyce, kulikuwa na gari nyingine ndogo nyeusi ikiwatazama. Ndani ya gari hiyo kulikuwemo na watu wawili.

Upande wa kulia wa gari hiyo alikuwemo kijana mmoja mtanashati. Kiumri alikuwa na miaka ishirini na tisa. Pamoja na kuwa alikuwa amekalia anayeitwa Daniel Mwaseba. Daniel alikuwa ni mpelelezi katika idara ya usalama wa Taifa. Pembeni yake, alikuwemo Martin Hisia. Martin alikuwa ni mpelelezi wa kujitegemea.

"Hatimaye hisia za Hannan zimekuwa kweli. Alexander Helb ameingia Tanzania akitokea nchini Kenya. Nampongeza sana Hannan. Alifanya jambo la maana sana kudukua simu ya balozi Rwekaza. Hatimaye sasa tunaenda kugundua mpango wa watu hawa..." Daniel alisema huku akiliangalia gari walilopanda wakina Joyce likiondoka.

"Upo sahihi Daniel, Hannan amefanya jambo kubwa sana kwa nchi yake. Alexander Helb, mgeni akiyemuongelea balozi Rwekaza sasa yupo mbele yetu. Sasa, lazima tuhakikishe tunamtia mikononi mwetu kabla hajafika katika milki yao!" Martin alisema.

"Alexander inaonesha ni mtu hatari sana, ndio maana wametumia gharama kubwa sana kumtoa nchi za mbali ili aje kuwasaidia katika mpango wao, yatupasa tuwe makini sana ili kumnasa" Martin alisema tena.

"Jinsi ya kumpata hakuna tatizo. Ni uharaka wetu tu, nimekata breki waya wa breki wa gari yao, sio muda tutaishuhudia ajali ambayo itatupa urahisi kumnasa Alexander Helb" Daniel alisema kwa uhakika.

"Daniel!! Umeifanya saa ngapi hiyo kazi ya kwenda kukata breki? Tumekuja wote hapa, tumekaa wote hapa na hujatoka ndani ya gari hata dakika moja?" Martin aliuliza kwa mshangao.

"Kazi hizi hufanywa kwa ushirikiano Martin, nina vijana wangu hapa uwanja wa ndege ambao ninawatumia katika mambo kama haya mara kadhaa. Kuna kijana wangu mmoja nimemtumia meseji na ameitekeleza hiyo kazi kikamilifu. Kazi hii..." Daniel hakumalizia alichotaka kusema, mbele yao waliishuhudia ajari mbaya sana ya gari. Gari aliyopanda Alexander na yule mwanamke ilikuwa nyang'anyang'a!!!

"Twende fasta tukamchukue kabla watu hawajajaa na kupata nafasi ya kutafakari.." Daniel alisema.

Mkukumkuku walitoka kwenye gari yao na kuelekea kule ilikotokea ajari. Kwa haraka walimbeba yule mzungu aliyekuwa hajitambui na kumkimbiza katika gari yao, wakawasha na kutimka zao. Kilikuwa ni kitendo cha muda mfupi sana ambacho hakikuwapa watu nafasi ya kutafakari..

"Safi sana, tumempata kirahisi sana huyu mtu, sasa ataenda kufunguka kila kitu anachokijua" Martin alisema kwa furaha.

"Ni kweli, ingawa haitakuwa kazi rahisi kumfungua. Bila shaka ni jasusi huyu, na majasusi wote wapo tayari wafe kuliko kuzianika siri zao" Daniel alisema.

"Mbele ya Daniel Mwaseba, atasema tu!" Martin alisema kwa kujiamini.

***

Taarifa ya ajari ya gari iliyotokea katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere ilivuma mithili ya upepo wa kusi. Vyombo vya habari vikisindikizwa na mitandao ya kijamii iliipeperusha habari hiyo kila kona ya nchi. Kutoka Kipawa ulipo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, taarifa za ajari zikafika hadi Sinza, nyumbani kwa balozi Rwekaza.

"Haiwezekani! Haiwezekani! Joyce na Alex wapate ajari? Hiyo haiwezi kuwa ajari ya kawaida! Kwanini iwe leo?" Balozi Rwekaza alisema peke yake huku akizunguka kitanda chake. Moja ilikuwa haikai, mbili ilikuwa haikai.

Akiwa katikati ya mzunguko wa kitanda, simu yake ya mkononi ilipata uhai.

"Haloo balozi Rwekaza"

"Haloo mheshimiwa Donald Tengo"

"Balozi Rwekaza umesikia kwamba gari yetu imepata ajari uwanja wa ndege?"

"Ndio nimesikia. Ni kwa bahati mbaya sana gari ya watu wetu muhimu sana ndio iliyopata ajari, hapa nipo katika harakati za kuelekea eneo la ajari"

"Sawa Balozi Rwekaza, fanya hivyo haraka sana, Joyce na Alexander ni watu muhimu sana katika mpango wetu. Wakipotea tutakuwa tumerudi nyuma kwa hatua nyingi sana" Donald alisisitiza.

"Naelewa Donald. Na ninakuahidi kila kitu kitakuwa sawa" Balozi Rwekaza alisema.

Baada ya kukata simu ya Donald Tengo, balozi Rwekaza alitoka nje na kuingia katika gari yake.

"Tunaelekea uwanja wa ndege" Alimwambia dereva wake aliyekuwa amekaa kitini.
Gari yake ilivyotoka, gari nyingine ilifata nyuma, ilikuwa ni gari ya walinzi wake.

Saa moja na nusu baadae walifika uwanja wa ndege. Hali ilikuwa shwari na harakati zilikuwa zinaendelea kama kawaida. Ilikuwa ni kama hapajatokea ajari mbaya saa moja na nusu iliyopita.

Balozi Rwekaza alishuka garini, huku walinzi wake wanne wakiwa nyuma yake, wakifuata hatua zake. Alielekea katika duka moja ambalo lilikuwa linauza vinyago na maua ambalo lilikuwa jirani tu na mahali ilipotokea ajari.

"Habari yako kaka?" Mzee Rwekaza alisalimu.

"Mzuri mzee, shikamoo. Karibu sana dukani kwetu"

"Ahsante sana kijana. Samahani naomba nikuulize vitu, nimetanguliza samahani kwakuwa vipo nje ya biashara"

"Haina shida mzee"

Mzee Rwekaza alimwangalia yule kijana muuza duka kisha akasema.

"Ulikuwepo hapa asubuhi wakati ajari ya gari lililogongwa na gari la majitaka ikitokea?"

"Ndio, nilikuwa hapa wakati ajari ile inatokea"

"Kama hutojari kijana, naomba uniambie nini kilitokea?"

"....ile gari nahisi ilikatika breki! Nililiona likiserereka kwa kasi na kwenda kujibamiza vibaya katika gari la majitaka lililokuwa linatokea katika vyoo vya uwanja wa ndege"

"Halafu?"

"Watu walianza kujaa na baadae gari ya wagonjwa ikaja na kuondoka na majeruhi"

"Unahisi wamepelekwa hospitali gani majeruhi?"

"Mimi sifahamu kwakweli"

"Hukuona jambo lengine lolote la ajabu?"

Muuza duka alifikiria kidogo. Hofu ilionesha katika sura yake. Balozi Rwekaza alitoa pochi yake, akatoa shilingi laki mbili. Akampa huku akimuuliza.

" Uliona tukio gani la ajabu"

"Nilionaaa....."

"Jambo gani hilo uliloliona?" Balozi Rwekaza aliuliza akiwa na wahka mkubwa.

"Kuna tukio la kushangaza kidogo lilitokea baada ya ajari kutokea. Kwa wakati ule nililichukulia ni tukio la kawaida tu, nikihisi labda ni wasamaria wema, lakini baadae nilijiuliza mwenyewe, kwanini wamchukue majeruhi mmoja tu na mwengine wamuache?" Muuza duka alisema huku akimwangalia balozi Rwekaza aliyekuwa katika hamu kubwa ya kusikia...

"Sijakuelewa kijana.."

"Ni hivi, kwenye gari kulikuwa na watu wawili, lakini mmoja alichukuliwa na vijana wawili kabla gari ya wagonjwa haijafika"

"Unasema?"

"Baada tu ya kutokea ile ajari kuna watu wawili walikimbilia, wakavunja kioo cha mbele na kukimbia na majeruhi mmoja. Kilikuwa ni kitendo kilichofanyika kwa haraka sana, ni watu wachache sana waliokishuhudia"

"Ooh Mungu wangu!, Itakuwa wameondoka na Alexander Helb!! Ni watu gani hao? Walifahamu vipi ujio wa Alexander?" Balozi Rwekaza alijiuliza mwenyewe, lakini hakukuwa na wa kumjibu.

Kijana muuza duka alibaki akimshangaa.

Je Alexander Helb ni nani? Wakina Daniel watapata kitu gani kutoka kwa Alexander Helb? Je wakina Donald Tengo wana mpango gani?
Hii ni sehemu ya kwanza ya mtoto wa rais..
Tuwe wote katika sehemu ijayo...
 
***

Safari ya kina Daniel Mwaseba iliwafikisha katika nyumba yake mpya iliyopo maeneo ya Tabata. Alipaki gari na kwa kusaidiana na Martin walimtoa Alexander Helb. Alexander alikuwa anavuja damu vibaya sana baada ya kukatwa na vioo vya gari. Shati lake jeupe lilikuwa limebadilika rangi na kuwa jekundu.
Bila kujari chochote Daniel na Martin walimbeba hadi ndani.

"Tumpeleke kile chumba cha mwisho. Nitampigia simu daktari wangu aje kumtibu hapahapa" Daniel alisema walipofika ukumbini.

Walimbeba tena na moja kwa moja walimpeleka Alexander katika chumba cha mwisho. Kisha wakarejea ukumbini.
Daniel alimpigia simu Dokta Viran.

"Hallo Dokta Viran" Daniel alisema baada ya simu yake kupokelewa.

"Hallo Daniel, naona umekuwa kimya kwa muda sasa, vipi upo salama?"

"Nipo salama Dokta Viran. Nina tatizo kidogo, ninaomba uje hapa nyumbani kwangu"

"Nikipokea simu yako tu najua kuna tatizo. Eeeh niambie nije na vifaa gani?"

"Njoo wewe tu, vifaa vyote vya tiba vipo hapa nyumbani"

"Sawa Daniel, baada ya nusu saa nitakuwa hapo"

Baada ya simu kukatwa Daniel na Martin walikaa sofani.

"Daniel, hivi unafikiri hawa watu watakuwa wana mpango gani haswa?"

"Hadi sasa hata mimi sijaelewa kwakweli. Lakini kwakuwa tuna huyu mzungu ndani angalau tutapata mwanga juu ya mpango wa hawa watu"

"Ni kweli Daniel, je Dokta Viran atachukua muda gani kufika hapa?"

"Hawezi kuchukua muda mrefu, amenambia ndani ya nusu saa. Hebu kampekua yule mzungu kabla Dokta Viran hajaja tuone kuna kitu gani kutoka kwake kinachoweza kutusaidia"

Martin alienda tena katika chumba cha mwisho. Akampekua Alexander, akaipata simu yake ya mkononi, pesa na tiketi ya ndege, vyote alivipeleka kwa Daniel. Daniel aliviangalia vile vitu, akaisoma ile tiketi ya ndege. Tiketi ilisoma kwamba yule mtu anaitwa Alexander Helb kutoka Uholanzi. Akaiangalia ile simu, simu ilikuwa na nywila ambayo si rahisi kuingilika.

"Tunamhitaji Hannan aje kutufungulia hii simu. Nenda kamwamshe Hannan chumbani kwake, lazima tujue ndani ya hii simu kuna nini cha kuweza kutusaidia"

"Sawa Daniel" Martin alisema huku akielekea chumbani kwa Hannan, akamwamsha na kurejea nae sebuleni.

"Kumbe mmerudi, nilikuwa nimelala. Nilichoka sana kwa kubaki mpweke humu ndani"

"Pole sana Hannan.." Daniel alisema.

"Ahsante sana, je mmempata huyo mtu aliyekuwa anamuongelea balozi Rwekaza jana?"

"Ndio tumempata, yupo katika chumba cha matibabu. Tulimsababishia ajari hivyo tunamsubiri Dokta Viran aje amtibu ili tuweze kuongea nae" Daniel alisema.

"Kazi nzuri sana Daniel"

Baada kama ya dakika kumi, alamu ya geti la nje iliita.

"Atakuwa Dokta Viran huyo, kamfungulie Martin" Daniel alisema.

Martin alitoka nje, baada ya kama dakika mbili alirudi akiwa ameongozana na Dokta Viran.

"Karibu sana Dokta Viran, tuna majeruhi muhimu sana. Tunahitaji taarifa kutoka kwake. Naomba umtibu vizuri kuhakikisha hafi. Martin mpeleke Dokta chumba cha mwisho akamuhudumie yule mzungu"

Martin alinyanyuka, akampeleka Dokta Viran katika chumba cha matibabu alipokuwa amewekwa Alexander.

"Daah jamaa ameumia sana, vipi alikutana na mkono wa Daniel nini?" Dokta Viran alisema akiwa katika mshangao mkubwa.

"Hapana, jamaa amepata ajari huyu uwanja wa ndege" Martin akajibu.

"Ahaa nilisikia hiyo ajari. Msinambie kama ni ninyi"

Martin alimwangalia tu.

"Basi, nioneshe vifaa vya tiba nianze kazi, jamaa amemwaga damu nyingi sana" Dokta Viran alisema.

Martin alifungua kabati moja la rangi ya kahawia. Kabati lilikuwa limejaa vifaa tiba kwa majeruhi.

"Duh, katika nyumba hii Daniel amejikamilisha sana. Tofauti na ile ya kule Mikocheni" Dokta Viran alisema baada ya kuona vifaa vilivyojaa kabatini.

"Mimi ninatoka nje. Ukimaliza au ukihitaji chochote utabonyaza pale. Kazi njema Dokta" Martin alisema na kutoka nje.

***

Kule ukumbini Daniel alimpa Hannan simu ya Alexander.

"Cheza nayo hiyo simu yake, pengine tutapata taarifa muhimu"

"Sawa, ngoja nikachukue laptop yangu ya kazi"

Baada ya dakika tatu, Hannan alikuwa na tarakilishi mpakato mkononi, wakati huo Martin alikuwa amesharejea ukumbini. Hannan akaanza kucheza na tarakilishi mpakato yake baada ya kuunganisha waya mwembamba kutoka katika ile simu ya Alexander. Baada ya kama dakika tatu uso wa Hannan ulijaa tabasamu.

"Yes, nimefanikiwa. Nimehamisha mafaili yote ya simu katika tarakilishi yangu. Na pia nimeiunganisha simu yake na tarakilishi yangu. Tutaona kila simu atakayopigiwa Ingawa atakayepiga ataambiwa haipatikani, na atakayejaribu kuidukua haitamuonesha sehemu sahihi alipo.." Hannan alisema.

"Kazi nzuri sana Hannan, anza kuyapitia hayo mafaili. Tuone kuna jambo gani tutalipata" Daniel alisema.

Hannan alianza kuyapitia mafaili kutoka katika simu ya mzungu, Alexander Helb.

Je watakutana na nini katika simu ya Alexander?

Itaendelea Kesho Mungu akipenda..
 
***

Safari ya kina Daniel Mwaseba iliwafikisha katika nyumba yake mpya iliyopo maeneo ya Tabata. Alipaki gari na kwa kusaidiana na Martin walimtoa Alexander Helb. Alexander alikuwa anavuja damu vibaya sana baada ya kukatwa na vioo vya gari. Shati lake jeupe lilikuwa limebadilika rangi na kuwa jekundu.
Bila kujari chochote Daniel na Martin walimbeba hadi ndani.

"Tumpeleke kile chumba cha mwisho. Nitampigia simu daktari wangu aje kumtibu hapahapa" Daniel alisema walipofika ukumbini.

Walimbeba tena na moja kwa moja walimpeleka Alexander katika chumba cha mwisho. Kisha wakarejea ukumbini.
Daniel alimpigia simu Dokta Viran.

"Hallo Dokta Viran" Daniel alisema baada ya simu yake kupokelewa.

"Hallo Daniel, naona umekuwa kimya kwa muda sasa, vipi upo salama?"

"Nipo salama Dokta Viran. Nina tatizo kidogo, ninaomba uje hapa nyumbani kwangu"

"Nikipokea simu yako tu najua kuna tatizo. Eeeh niambie nije na vifaa gani?"

"Njoo wewe tu, vifaa vyote vya tiba vipo hapa nyumbani"

"Sawa Daniel, baada ya nusu saa nitakuwa hapo"

Baada ya simu kukatwa Daniel na Martin walikaa sofani.

"Daniel, hivi unafikiri hawa watu watakuwa wana mpango gani haswa?"

"Hadi sasa hata mimi sijaelewa kwakweli. Lakini kwakuwa tuna huyu mzungu ndani angalau tutapata mwanga juu ya mpango wa hawa watu"

"Ni kweli Daniel, je Dokta Viran atachukua muda gani kufika hapa?"

"Hawezi kuchukua muda mrefu, amenambia ndani ya nusu saa. Hebu kampekua yule mzungu kabla Dokta Viran hajaja tuone kuna kitu gani kutoka kwake kinachoweza kutusaidia"

Martin alienda tena katika chumba cha mwisho. Akampekua Alexander, akaipata simu yake ya mkononi, pesa na tiketi ya ndege, vyote alivipeleka kwa Daniel. Daniel aliviangalia vile vitu, akaisoma ile tiketi ya ndege. Tiketi ilisoma kwamba yule mtu anaitwa Alexander Helb kutoka Uholanzi. Akaiangalia ile simu, simu ilikuwa na nywila ambayo si rahisi kuingilika.

"Tunamhitaji Hannan aje kutufungulia hii simu. Nenda kamwamshe Hannan chumbani kwake, lazima tujue ndani ya hii simu kuna nini cha kuweza kutusaidia"

"Sawa Daniel" Martin alisema huku akielekea chumbani kwa Hannan, akamwamsha na kurejea nae sebuleni.

"Kumbe mmerudi, nilikuwa nimelala. Nilichoka sana kwa kubaki mpweke humu ndani"

"Pole sana Hannan.." Daniel alisema.

"Ahsante sana, je mmempata huyo mtu aliyekuwa anamuongelea balozi Rwekaza jana?"

"Ndio tumempata, yupo katika chumba cha matibabu. Tulimsababishia ajari hivyo tunamsubiri Dokta Viran aje amtibu ili tuweze kuongea nae" Daniel alisema.

"Kazi nzuri sana Daniel"

Baada kama ya dakika kumi, alamu ya geti la nje iliita.

"Atakuwa Dokta Viran huyo, kamfungulie Martin" Daniel alisema.

Martin alitoka nje, baada ya kama dakika mbili alirudi akiwa ameongozana na Dokta Viran.

"Karibu sana Dokta Viran, tuna majeruhi muhimu sana. Tunahitaji taarifa kutoka kwake. Naomba umtibu vizuri kuhakikisha hafi. Martin mpeleke Dokta chumba cha mwisho akamuhudumie yule mzungu"

Martin alinyanyuka, akampeleka Dokta Viran katika chumba cha matibabu alipokuwa amewekwa Alexander.

"Daah jamaa ameumia sana, vipi alikutana na mkono wa Daniel nini?" Dokta Viran alisema akiwa katika mshangao mkubwa.

"Hapana, jamaa amepata ajari huyu uwanja wa ndege" Martin akajibu.

"Ahaa nilisikia hiyo ajari. Msinambie kama ni ninyi"

Martin alimwangalia tu.

"Basi, nioneshe vifaa vya tiba nianze kazi, jamaa amemwaga damu nyingi sana" Dokta Viran alisema.

Martin alifungua kabati moja la rangi ya kahawia. Kabati lilikuwa limejaa vifaa tiba kwa majeruhi.

"Duh, katika nyumba hii Daniel amejikamilisha sana. Tofauti na ile ya kule Mikocheni" Dokta Viran alisema baada ya kuona vifaa vilivyojaa kabatini.

"Mimi ninatoka nje. Ukimaliza au ukihitaji chochote utabonyaza pale. Kazi njema Dokta" Martin alisema na kutoka nje.

***

Kule ukumbini Daniel alimpa Hannan simu ya Alexander.

"Cheza nayo hiyo simu yake, pengine tutapata taarifa muhimu"

"Sawa, ngoja nikachukue laptop yangu ya kazi"

Baada ya dakika tatu, Hannan alikuwa na tarakilishi mpakato mkononi, wakati huo Martin alikuwa amesharejea ukumbini. Hannan akaanza kucheza na tarakilishi mpakato yake baada ya kuunganisha waya mwembamba kutoka katika ile simu ya Alexander. Baada ya kama dakika tatu uso wa Hannan ulijaa tabasamu.

"Yes, nimefanikiwa. Nimehamisha mafaili yote ya simu katika tarakilishi yangu. Na pia nimeiunganisha simu yake na tarakilishi yangu. Tutaona kila simu atakayopigiwa Ingawa atakayepiga ataambiwa haipatikani, na atakayejaribu kuidukua haitamuonesha sehemu sahihi alipo.." Hannan alisema.

"Kazi nzuri sana Hannan, anza kuyapitia hayo mafaili. Tuone kuna jambo gani tutalipata" Daniel alisema.

Hannan alianza kuyapitia mafaili kutoka katika simu ya mzungu, Alexander Helb.

Je watakutana na nini katika simu ya Alexander?

Itaendelea Kesho Mungu akipenda..
Sawa mkuu
 
"Njooni muone!" Hannan akasema kwa nguvu baada ya kuchezea tarakilishi mpakato yake kwa zaidi ya dakika kumi. Kwa haraka Martin na Daniel wakasogelea katika tarakilishi ya Hannan.

"Kumbe huyo jamaa haitwi Alexander Helb kama hati yake ya kusafiria na tiketi ilivyoandikwa. Jina lake halisi ni Robin. Si unaona katika ujumbe huu, ametambulishwa kama Robin.." Hannan alisema kwa uhakika.

"Safi Hannan, hebu mpekue kuhusu huyohuyo Robin, ni nani haswa?" Martin alisema.

Hannan akaanza kusaka taarifa za Robin. Akazipata, wakati anasoma taarifa za Robin jasho lilikuwa linamtoka. Wakina Daniel nao walikuwa wanasoma lakini Hannan aliwashinda kasi katika usomaji.

"Kumbe jamaa ni jasusi kutoka Marekani!" Hannan akasema kwa nguvu.

"Umejuaje Hannan?" Daniel alishangaa.

"Nimemtafuta kutoka katika mtandao wa siri wa majasusi, nimetumia mfumo wa siri sana inayoweza kupata taarifa za majasusi kutoka katika mashirika mbalimbali ya majasusi duniani. Humo ndio nimelikuta jina la Robin katika orodha ya majasusi wa CIA, si unaona na sura yake hii?" Hannan alisema huku akikionesha kidole kioo cha tarakilishi.

"Daah Hannan umegundua kitu kikubwa sana. Bado nakusifu kwa kumtilia shaka Balozi Rwekaza na kuamua kumfatilia. Endelea kufukua mashimo tuone kuna kitu gani kingine kinaweza kutusaidia" Daniel alisema.

Hannan alikuwa kimya, makini akipekua mafaili kutoka katika simu ya Robin. Lakini, hawakupata kingine chochote kile zaidi ya jina halisi la Alexander na kazi yake ya ujasusi aliyoipata katika mtandao wa majasusi.

"Humu kuna meseji za kawaida tu. Hazihusiani na kazi, hazihusiani na kilichomtoa Marekani na kumleta Tanzania. Inaonesha kuna njia nyingine anayowasiliana na kina Balozi Rwekaza tofauti na hii" Hannan alisema.

"Vipi? Hatuwezi kuzipata baruapepe zake?" Martin aliuliza.

"Ngoja Martin, ngoja nichomeke tena hapa nijaribu kunyonya barua pepe zake" Hannan alisema.

Akachomeka tena ule waya katika simu ya Robin, na kuunganisha katika tarakilishi yake. Akacheza nayo kama muda wa nusu saa. Ukumbi ulikuwa kimya. Mlio wa te te te kutoka katika saa ya ukutani ndio uliokuwa unasikika. Zilikuwa ni dakika chache sana lakini zenye mhemuko mkubwa. Wote walijua kwamba barua pepe ndio kitu pekee kitakachowapa kitu cha kwenda kumuhoji Robin. Bila hivyo hawakuwa na kitu kingine cha kwenda kumuhoji Robin. Hadi sasa walikuwa hawajui nini hasa wanachunguza, walikuwa wanazifuata hisia tu za Hannan baada ya kukutana na Balozi Rwekaza katika sherehe ya kuzaliwa ya rais Profesa Mark ikulu.

Siku chache nyuma

Ilikuwa ni siku ya jumapili jioni. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Profesa Mark alikuwa anatimiza miaka hamsini na tatu ya kuzaliwa. Na sherehe yake ilifanyika katika viunga vya Ikulu jijini Dar es salaam.

Wageni mbalimbali walikuwa wamealikwa. Viongozi wa kiserikali, viongozi wa chama, dini, wasanii na raia wa kawaida. Ilikuwa ni sherehe iliyofana sana. Sherehe iliyoandaliwa na kituo cha redio cha Ocafona.

Hannan Halfani naye alikuwemo katika hafla hiyo. Alikuwa ni mmoja wa maaskari wachache waliokuwa wameandamana na mkuu wa Polisi nchini, IGP John Zotta.
Hannan, wakati akiwa katika majukumu yake alipatwa na haja ndogo. Ilimpasa kwenda maliwatoni. Wakati akiwa maliwatoni ndipo aliposikia mtu akiongea kwa simu katika choo cha kiume vilivyokuwa vinapakana tu. Aliyasikiliza mazungumzo ya simu ya mtu huyo, na hayo ndio yaliyomtilia shaka.

"Nakuahidi Mzee, hili jengo linaenda kuwa letu, pale mpango wetu utakapokamilika..."

Kukawa kimya kidogo, kisha akasema tena.

"Sawa Mzee, nitakuja makao tuongee"

Simu ikakatwa.

Hisia za kipelelezi za Hannan zikataka kujua ni mpango gani huo unaokuja kuongelewa chooni? Na huyo Mzee ni nani? Kauli ya kusema hili 'jengo litakuwa letu' aliamini kuwa jengo linalongelewa ni Ikulu. Ndio jengo walilokuwemo. Je wanataka kumpindua rais?. Maswali mengi magumu na yasiyo na majibu yalishonana kichwani mwake.

Aliposikia mlango wa choo cha kiume unafunguliwa naye akafungua wake. Wakakutana uso kwa uso mtu aliyekuwa anazungumza chooni.

Alikuwa ni Balozi Rwekaza.

Balozi alionesha hali ya wasiwasi sana. Yeye alidhani sehemu ile yuko peke yake. Hiyo ilikuwa dhana lakini sio ukweli. Ukweli ni kwamba kulikuwa na mtu, alikuwepo Hannan.

Sherehe iliisha bila ya tukio lolote lile la ajabu. Hannan alirejea nyumbani kwake. Lakini aliondoka akiwa na kazi ya ziada ya kuifanya, kazi yakudukua simu ya Balozi Rwekaza. Ilikuwa ni kazi ya ziada kwake lakini haikuwa kazi ngumu kwake.

Alifanikiwa kuidukua.

Ndani ya siku tatu hakupata lolote la maana katika simu hiyo, akaanza kuzidharau hisia zake. Labda pengine alimwelewa vibaya balozi Rwekaza. Siku ya nne nayo ikatembea zake. Siku ya tano na sita nazo zikakimbia mbio. Akaanza kusahau kuhusu Balozi Rwekaza na simu zake za ajabu za kuongelea chooni..

Ilikuwa ni wakati wa jioni. Hannan alikuwa ametoka kuoga, akasogea mbele ya kabati lake yenye vipodozi na urembo mbalimbali. Alikuwa anajiangalia kwenye kioo huku akijipodoa kikike. Hapo ndipo simu yake iliingia ujumbe, ujumbe ambao alijua unachomaanisha. Balozi Rwekaza alikuwa anaongea na mtu, akabonyazabonyaza simu yake, maongezi ya mzee Rwekaza yalikuwa hadharani. Aliyasikiliza kwa muda wa dakika kumi na saba. Neno moja lilitawala sana katika simu hiyo 'Mpango'. Akahisi ni ule mpango aliousikia chooni ikulu, katika sherehe ya kuzaliwa ya rais. Mpango ambao ukikamilika jengo la ikulu litakuwa lao. Hamu ya kuujua kwa undani mpango huo ikapanda maradufu.

"Alexander Helb atakuja keshokutwa na ndege ya Kenya airways. Akija yeye nd'o atakuja kumalizia hatua ya mwisho ya mpango wetu."

Maneno hayo ya mwisho yalimfanya Hannan atake kuujua zaidi huo mpango. Akawasiliana na Daniel Mwaseba na kumueleza kila kitu. Ndipo Daniel na Martin walienda uwanja wa ndege kumpokea huyo Alexander, ikiwezakana awaambie kuhusu huo mpango wao wa kuimiliki ikulu.

***

"Ona hii, ona Daniel!" Hannan alisema kwa nguvu huku akionesha kidole kioo cha tarakilishi yake.

"Alexander au Robin alipokea baruapepe jana jioni kutoka kwa waziri wa ulinzi wa Marekani. Barua pepe ina maneno mafupi tu,

'Kuwa makini Robin'.

Inaonesha serikali ya Marekani inajua nini amekuja kufanya Robin hapa nchini" Hannan alisema kwa fadhaa.

"Na sisi tunaenda kuujua hivi punde" Daniel alisema kwa kujiamini.
 
"Alexander au Robin alipokea baruapepe jana kutoka kwa waziri wa ulinzi wa Marekani. Barua pepe ina maneno mafupi tu,

'Kuwa makini Robin'.

Inaonesha serikali ya Marekani inajua nini amekuja kufanya Robin hapa nchini" Hannan alisema kwa fadhaa.

"Na sisi tutajua hivi punde" Daniel alisema kwa kujiamini.

"Ni kweli Daniel, hatuna haja ya kutafakari sana wakati mtu mwenye majibu yote tunaye hapa. Tukimbana Robin tutajua tu nini hasa kimemleta Tanzania" Martin alisema.

"Na je ukiwa mpango nzuri?" Hannan aliuliza.

"Hakuna mpango nzuri unaoongelewa chooni. Mpango wa kumiliki lile jengo jeupe katu hauwezi kuwa mzuri" Daniel alijibu.

Mara simu ya Hannan ilitoa mlio, kuashiria balozi Rwekaza alikuwa anaongea na mtu. Hannan akaibonyazabonyaza simu yake, simu ya mzee Rwekaza ikawa inasikika kwa wote.

"Ni wakina nani hao waliyemchukua Alexander? Ina maana mipango yetu imevuja?"
Ikawa kimya akisikiliza.

Kisha akaongea "Ongea na vijana wa Bahari nyekundu ili kuhakikisha kwa namna yoyote ile Alexander anapatikana leoleo!"

Akasikiliza tena, ndipo akaongea. "Sawa mkuu, nimekuelewa. Nitafanya kama ulivyoagiza. Ninaelewa mpango wetu utakuwa ngumu sana kukamilika bila uwepo wa Alexander"

Baadae wakaongea kama dakika kumi hivi na kukata simu.

"Hannan, unaweza kuipata namba ya huyo akiyeongea na balozi Rwekaza?" Daniel alisema.

"Ni kazi ndogo sana hiyo, ngoja niifanye" Hannan alisema.

Hannan alianza kuchezea tarakilishi mpakato yake, akaipata.

"Namba yake ni hii hapa ngoja tuangalie usajiri wake" Hannan alisema huku akibonyaza simu kwa kufanya kama anataka kuitumia pesa.

"Ni namba ya Donald Tengo!" Hannan alisema.

"Waziri wa fedha?" Daniel alishangaa.

"Bila shaka" Martin alimalizia.

"Hannan angalia taarifa za Donald Tengo" Daniel alisema.

Hannan alianza kuchezea tarakilishi yake tena. Baada ya dakika saba alisema.

"Anaitwa Donald Richardson Tengo. Ni mbunge kutoka jimbo la Muheza Tanga. Alichaguliwa kuwa waziri wa fedha katika serikali ya mheshimiwa Profesa Mark mara tu alipoapishwa. Kitaaluma Donald ni mchumi. Ana mke na watoto wawili wa kike, Candy na Cindy.."

"Hapohapo panatosha Hannan. Lazima tuipate familia ya Donald Tengo hapa. Tutaitumia pia familia yake kujua kuwa wana Mpango watu hawa?" Daniel alisema.

***

Katika chumba cha matibabu, ndani ya nyumba ya Daniel Mwaseba.. Dokta Viran alikuwa anaendelea kumtibu Robin. Robin alijifanya yupo katika hali mbaya sana. Hii ilimpa nafasi Dokta Viran kumhudumia bila wasiwasi wowote ule. Dokta Viran hakujua kwamba Robin Johnson sio mtu wa kawaida.

"Sijaelewa nini kimetokea pale uwanja wa ndege. Bila shaka ile haikuwa ajari ya kawaida. Ilipangwa. Na baada ya ajari tu nahisi kama nilichukuliwa msobemsobe, na nimeletwa hapa. Bila shaka yoyote waliosababisha ajari ndio walioniteka. Ni kina nani hawa? Nitaendelea kujifanya nipo hoi ili niendelee kuwasoma na kujipanga pia. Je wamenusa chochote kutoka kwangu juu ya lengo la ujio wangu? Naona ufinyu wa kumpata ZAK.." Robin aliwaza huku akiiangalia dripu ya damu ikizama katika mishipa yake. Mara Daniel aliingia, Robin aliyaona yote hayo kwa jicho lake moja akiloangalia kwa siri.

"Vipi anaendeleaje?" Daniel alimuuliza Dokta Viran.

"Anaendelea vizuri, alimwaga damu nyingi lakini nashukuru mlikuwa na akiba ya damu ya kutosha humu ndani, nimeipata damu inayofanana nae na kumwekea. Majeraha yake yote tumeyatibu kama unavyoona. Anahitaji muda mdogo tu wa kupumzika ili arejewe na nguvu.."

"Hatuna huo muda mdogo wa kupumzika Dokta Viran. Ninahitaji taarifa muhimu sana kutoka kwake na ninazitaka taarifa hizo sasahivi!" Daniel alisema.

"Sawa Daniel, ngoja nikupishe uendelee na majukumu yako"

Dokta Viran alitoka nje, akimwachia uwanja Daniel. Alimjua Daniel jinsi asivyopenda mas'hala katika kazi.

"Pole sana Mr Robin Johnson" Daniel alisema huku akikifata kitanda alicholala Robin.

Robin alistuka kidogo. Yeye alijua kwamba kama watu wale watamwita kwa jina basi litakuwa Alexander Helb Lililopo katika tiketi yake ya kusafiri, na sio kumwita jina lake halisi.

"Robin nina muda mfupi sana wa kukaa hapa kuongea na wewe. Najua hali yako si nzuri, unahitaji matibabu. Basi nijibu maswali yangu mafupi kisha nimwache Dokta Viran aendelee kukutibu" Daniel alisema kwa upole.

Robin alifungua macho yote mawili kumwangalia mtu anayemuongelesha. Alikutana na mtu aliyevaa fulana nyeupe, jinzi ya bluu na viatu vyeupe vyenye nembo ya adidas pembeni. Kwa macho yake ya harakaharaka hakujua amekutana na mtu wa aina gani?

"Umekosea jina, naitwa Alexander Helb.." Robin alisema akiwa katika hali ya maumivu..

"Sipo hapa kwa ajili ya utani Robin. Nina swali moja tu, ni mpango gani uliokuleta hapa nchini?"

Robin alimwangalia Daniel juu-chini kisha akasema, " nimekwambia ninaitwa Alexander Helb kutoka Uholanzi. Nimekuja hapa kama mtalii, nina mpango wa kwenda Serengeti, Ngorongoro na mlima Kilimanjaro...." Robin alijibu bila wasiwasi.

"Ngoja nikuoneshe unaongea na mtu wa namna gani?" Daniel alisema kwa sauti ndogo.

Akaenda kwenye kabati jeusi lilikuwa mle ndani. Akafungua. Akachukua mkasi mkubwa na burungutu la pamba. Akafungua droo lilikokuwa pembeni ya kabati hilo na kuchukua chupa ndogo ya dawa, dawa ilikuwa na rangi nyekundu.

"Nakukata kidole kimoja baada ya kingine mpaka pale utakapoamua kuniambia ukweli!" Daniel alisema akimaanisha.

Alimsogelea Robin pale kitandani. Akaushika kwa nguvu mkono wake wa kushoto. Akakishika kidole cha mwisho cha Robin. Akaupitisha ule mkasi mkubwa wenye makali maradufu. Akagusanisha kwa nguvu ili mishikio ya mkasi.
Ulisika milio wa kaaaa!!

Daniel, akakita kidole kidogo na kudondoka chini!!!

Robin alipiga ukelele mkubwa sana, wakati huo damu zikibubujika isivyo kifano!
Fulana nyeupe ya Daniel ilikuwa imetapakaa damu!

"Nakukata kidole kingine!" Daniel alisema wakati akiwa ameshika kidole cha kati cha Robin.

Robin alilia sana lakini Daniel hakujari. Aliupitisha tena ule mkasi wa kukatia vidole.

"Nita..sem..aa, nitak..wambia uk..weli wote" Robin alisema huku akilia kwa maumivu.

"Nakusikiliza..." Daniel alisema akikiachia kile kidole.

"Ninaomba unitibie kidole changu kwanza, nitakwambia kila kitu" Robin alisema akiwa katika hali ya maumivu.

Daniel akatoka nje, baada ya dakika chache akaingia Dokta Viran. Akaanza kumtibia Robin kile kidole.

" Kijana nakushauri kama kuna kitu Daniel anakitaka kutoka kwako mpe. Yule kiumbe hana huruma hata kidogo. Kwanza una bahati sana wewe, kuna watu wakiingia katika hiki chumba anawachakaza haswa. Nikifika mimi nawakuta hawana macho, hawana sehemu za siri, hawana vidole, hawana maini na wengi hawana vichwa! Yaani hawatamaniki, na hilo nilitegemea pia kutoka kwako, lakini wewe kakupendelea sana, kakukata kidole kimoja tu" Dokta Viran alisema.

Robin akiwa anagugumia kwa maumivu alishangaa sana. Alishangaa mwonekano wa Daniel na sifa zake. Daniel hakuwa na sura ya kikatili hata kidogo.

Dokta Viran alidhibiti damu isitoke pale kidoleni na kulifunga lile jeraha. Kisha akaenda kumwita Daniel.
Daniel aliingia ndani.

"Nimerudi tena Rafiki. Tutaendelea tulipoishia. Naomba sasa unijibu, ni mpango gani uliokuleta hapa nchini?"

"Kwakweli mimi sifahamu nimekuja Tanzania kwa ajili ya mpango gani? Ilinipasa nije hapa nionane na mtu anayeitwa Donald Tengo ndipo ningepewa majukumu yangu" Robin alisema.

"Ungekutana wapi na Donald Tengo?" Daniel akauliza.

"Alimtuma katibu wake anayeitwa Joyce, yeye ndo angenipeleka kukutana na Donald Tengo" Robin alisema.

"Wewe ni wakala wa C.I.A?" Daniel aliuliza.

Uso wa Robin ulisawajika kwa swali hilo. Katika maswali yote aliyokuwa anayawaza hili hakulitegemea. Akabaki amekaa kimya.

"Unatokea C.I.A?" Daniel alirudia swali.

Robin alibaki kimya.

"Usinilazimishe kufanya ninachofikiria kukufanya!" Daniel alisema huku akielekea katika kabati jeusi.

"Hata anitese vipi hilo sipaswi kukubali. Nimeapa kutosema siri hata siku moja kwa ajili ya maslahi ya nchi yangu. Mbona imekuwa mapema sana na wamejua mengi kuhusu mimi" Robin aliwaza.

Daniel alifungua kabati. Akatoa bomba la sindano. Akaelekea pale kitandani na kuichukua ile chupa ya dawa nyekundu aliyoitoa awali. Akaivuta ile dawa. Akaididimiza kwa nguvu kwenye paja la Robin! Akabonyaza kwa juu kuruhusu ile dawa imwingie...

Robin alilia kwa nguvu sana. Maumivu aliyokuwa anayasikia yalikuwa makali sana! Alilia na kulia wakati Daniel akiruhusu ile dawa iingie taratibu. Maumivu aliyokuwa anayapata ilikuwa ni kama mtu anamchuna ngozi akiwa hai! Mwili unamuwaka moto! Mwili una maumivu yasiyo mfano!

"Unaniuaaaaaa...!"

"Hautakufa Robin, ila nitakachokufanya ni bora ungekufa tu...."

Aliliacha lile bomba la sindano likiwa linaning'inia pajani, akaenda tena katika kabati jeusi, akabeba viwembe vinavyotumika katika upasuaji!.

"Nakutoa jicho moja! Na nitakutoa lingine, nitaacha kukuadhibu pale utakapoamua kusema ukweli.." Daniel alisema akimaanisha.

Robin alikuwa analia, akitetemeka. Hofu kuu ikimtawala usoni mwake.
Leo hii, Jasusi alikuwa amepatikana. Jasusi alikuwa ameingia kwenye anga sio. Ameingia katika anga ya wenyewe.
Anga ya wenye kazi hii.
Anga ya kichaa.
Anga ya mwanaume.
Anga ya Daniel Mwaseba!

Daniel kama Daniel.....

Mikono ya Daniel ilikuwa inamaanisha inaenda kutekeleza ilichoamrishwa na moyo wake. Anaenda kumtoa jicho Robin Johnson ili apate taarifa!!!

Robin kabananishwa konani.
Je atasema asichotaka kusema mbele ya Daniel Mwaseba?
Huu ni mwanzo, usiache kuifatilia kalamu ya Halfani Sudy katika safari ndefu ya simulizi hii yenye visa vya ajabu.

Mtoto wa Rais.

Kwanini mtoto wa rais?
 
"Ninaomba unitibie kidole changu kwanza, nitakwambia kila kitu" Robin alisema akiwa katika hali ya maumivu.

Daniel akatoka nje, baada ya dakika chache akaingia Dokta Viran. Akaanza kumtibia Robin kile kidole.

" Kijana nakushauri kama kuna kitu Daniel anakitaka kutoka kwako mpe. Yule kiumbe hana huruma hata kidogo. Kwanza una bahati sana wewe, kuna watu wakiingia katika hiki chumba anawachakaza haswa. Nikifika mimi nawakuta hawana macho, hawana sehemu za siri, hawana vidole, hawana maini na wengi hawana vichwa! Yaani hawatamaniki, na hilo nilitegemea pia kutoka kwako, lakini wewe kakupendelea sana, kakukata kidole kimoja tu" Dokta Viran alisema.

Robin akiwa anagugumia kwa maumivu alishangaa sana. Alishangaa mwonekano wa Daniel na sifa zake. Daniel hakuwa na sura ya kikatili hata kidogo.

Dokta Viran alidhibiti damu isitoke pale kidoleni na kulifunga lile jeraha. Kisha akaenda kumwita Daniel.
Daniel aliingia ndani.

"Nimerudi tena Rafiki. Tutaendelea tulipoishia. Naomba sasa unijibu, ni mpango gani uliokuleta hapa nchini?"

"Kwakweli mimi sifahamu nimekuja Tanzania kwa ajili ya mpango gani? Ilinipasa nije hapa nionane na Donald Tengo ndipo ningepewa majukumu yangu" Robin alisema.

"Ungekutana wapi na Donald Tengo?" Daniel akauliza.

"Alimtuma katibu wake anayeitwa Joyce, yeye ndo angenipeleka kukutana na Donald Tengo" Robin alisema.

"Unatoka C.I.A?" Daniel aliuliza.

Uso wa Robin ulisawajika kwa swali hilo. Katika maswali yote aliyokuwa anayawaza hili hakulitegemea. Akabaki amekaa kimya.

"Unatoka C.I.A?" Daniel alirudia swali.

Robin alibaki kimya.

"Usinilazimishe kufanya ninachofikiria kukufanya!" Daniel alisema huku akielekea katika kabati jeusi.

"Hata anitese vipi hilo sipaswi kukubali. Nimeapa kutosema siri hata siku moja kwa ajili ya maslahi ya nchi yangu. Mbona imekuwa mapema sana na wamejua mengi kuhusu mimi" Robin aliwaza.

Daniel alifungua kabati. Akatoa bomba la sindano. Akaelekea pale kitandani na kuichukua ile chupa ya dawa nyekundu aliyoitoa awali. Akaivuta ile dawa. Akaididimiza kwa nguvu kwenye paja la Robin! Akabonyaza kwa juu kuruhusu ile dawa imwingie...

Robin alilia kwa nguvu sana. Maumivu aliyokuwa anayasikia yalikuwa makali sana! Alilia na kulia wakati Daniel akiruhusu ile dawa iingie taratibu. Maumivu aliyokuwa anayapata ilikuwa ni kama mtu anamchuna ngozi akiwa hai! Mwili unamuwaka moto! Mwili una maumivu yasiyo mfano!

"Unaniuaaaaaa...!"

"Hautakufa Robin, ila nitakachokufanya ni bora ungekufa tu...."

Aliliacha lile bomba la sindano likiwa linaning'inia pajani, akaenda tena katika kabati jeusi, akabeba viwembe vinavyotumika katika upasuaji!.

"Nakutoa jicho moja!" Daniel alisema akimaanisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom