Riwaya ya Kijasusi: "Msako wa Mwehu"

Riwaya ya Kijasusi: "Msako wa Mwehu"

mpasta shusha vitu kande zinoge
- 19 -

Riwaya: MSAKO
Mtunzi: Japhet Nyang’oro

Saa tisa na robo alasiri, wakati Jacob Matata anakata shauri kuanzia Upanga NHC nyumba namba 41A, Poka Kingu na yeye alikuwa kwenye hesabu zake.
“Wapelelezi ni kama Inzi tu, wanapoona kinyesi hawaachi kuzungukia hapo. Nina hakika atarudi tena kwa Nana, hivyo watatu mtakwenda nyumbani kwa marehemu Lucas Mwenda kumngoja Jacob Matata. Nina hakika baada ya kuona kile kifaa tulichomwachia Nanalungu kwa vyovyote atataka kwenda ili asubiri yeyote atakeyekwenda akabiliane nae na kuweza kutufikia. Hakuna anayeweza kukabiliana na Jacob Matata hapa kati yenu, hivyo mtakachofanya mkimuona tu ni kumfuatilia kila anapokwenda na kunipa taarifa. Nataka kujua ameweka kambi wapi. Maana sasa anatafutwa sana na vyombo vya usalama hivyo najua kuna sehemu amejizika ili isijulikane alipo.” Poka Kingu alisema kwa vijana wake ambao alikuwa amewakusanya wamsaidie kufanya kazi ya kukusanya taarifa na kufuatilia watu huku yeye akiwa amejiwekea kazi ya kung’oa visiki.

Wakati Poka Kingu akiwa anatoa maelezo hayo, Luteni Frank Misanya na Nanalungu Bin Muhusin walikuwa wanaanza maongezi yao kwa njia ya simu.
“Naona mambo yanatunyookea!’’ Nana alisema.
“Haswa, wale vijana tuliokuwa nao siku ile tunamhoji Sabodo Sumari wote wameuawa leo!’’ Frank alisema.
“Oooh! maskini, wanaoneka walikuwa vijana wakakamvu sana. Imekuwaje, vifo vyao ni sehemu ya mkakati au janga limewafika?’’ Nana alihoji.
“Sehemu ya mkakati, Mzee aliwakabidhi kwa Jacob Matata, Jamaa kawaswaga wote!’’ Frank alisema kwa sauti baridi.
“Miye nilijua Jacob kawekewa watu makini baada ya kuwataarifu kufika pale msibani. Nilifanikiwa kumfanya ajue kuwa niko upande wake. Halafu niliona jinsi alivyonitamani. Jacob mgonjwa wa wanawake aisee, yaani katika mazingira kama yale ya msiba bado akawa ananimezea mate! Ila ni bonge la mkaka, bsi tu! Sasa mkakati hapo ni upi?’’ Nanalungu ambaye ni mke wa Inspekta Mwenda alisema.
“Ni sehemu ya kukulinda wewe Nana. Tungekosea Jacob angewahi kujua kuwa wewe ulitupa taarifa zake. Ila kwa hivi tulivyofanya Jacob Matata ataendelea kukuamini. Lakini nahisi kama Mzee hatuamini kuwa tunaweza kukabiliana na Jacob au kuna namna anataka asife sasa.” Frank Misanya alisema.
“Halafu nina ujumbe wako toka kwa mzee” Frank Misanya alisema
“Nini tena, niko msibani jamani au hamjui? Nana alisema kwa mshituko.
“Anasema umeshamaliza kazi ngumu, baada ya kuwaua Inspekta Menda na Sabodo unatakiwa upumzike. Hivyo kasema nenda kajichimbie kule Masaki kwenye nyumba uliyojengewa na Sabodo Sumari, hadi hapo utakapopewa maelekezo mengine.” Misanya aliongeza.

********

ILIPOFIKA saa kumi kasoro dakika kumi na tano alasiri wakati ambao msako dhidi yake ulikuwa umepamba moto, Jacob Matata aliingia mtaani nia yake sasa ikiwa ni kwenda Upanga NHC nyumba namba 41A. Hatimaye alifika Mzumbe University Cumpas ya Dar es salaam, akiwa katika mavazi yenye utata, ambayo si rahisi mtu kumtambua. Kwa vile alijua kuwa alikuwa anatafutwa, aliamua kubadili sana uvaaji na mwoneka wake. Kufanya isiwe rahisi kujulikana hadi atakapofikia hatma ya kisa hiki. Japo hakuwa na hakika ya kumaliza akiwa hai au la.
Alitembea taratibu, ungedhani anaelekea Regent. Lakini akaiacha hiyo barabara na kuchukua ile ya vumbi. Hapo alitembea taratiibu, hadi kwa mbali aliweza kuiona ile nyumba na 41A ya shirika la nyumba.

Alipapasa bastola yake kiunoni, huku akiendelea kutembea taratibu hadi alipokuwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia ndani upande wa uani. Eneo la nje lilimwashiria wazi kuwa hakukuwa na mtu aliyekuwa akiishi eneo hilo. Hata hivyo sheria mojawapo ya upelelezi ni kutokuamua mambo kwa kudhani. Mara nyingi ukionacho ni tofauti na uhalisia wake, usione ukadhani.

Hivyo dakika chache baadae alikuwa ameshaingia ndani, alizunguka maeneo yote bila kuona dalili yoyote ya kuwa na mtu anaishi ndani. Alikagua sehemu ya chini kabla ya kupanda ngazi kwenda upande wa juu, maana nyumba hiyo ilikuwa na ghorofa moja. Alipanda kwa hadhari kubwa. Alifika kwenye kibaraza cha sehemu ya juu. Alianza kuangalia chumba kimoja baada ya kingine hadi alipofungua malango wa chumba cha tatu taratibu huku mapigo yake ya moyo yakienda kasi. Bastola ikiwa imara mkono wake wa kulia. Taratibu aliingia ndani. Chumba kilikuwa ukiwa huku kukiwa na mifupa ya mtu iliyokuwa imelala chini. Inaonyesha mtu huyo alikufa siku nyingi, akaoza na sasa mifupa ikawa pale chini kama mti. Jacob Matata alishangaa sana.
Kama mtu alikufa, akaoza, mwili ukaliwa na wadudu hadi sasa amebakia mifupa inamaana hakuna mpangaji mwingine kwenye ile nyumba kwa muda mrefu sana?
Ina maana hata majirani hawakutambua kuwa jirani yao alitoweka?
Ina maana majirani hao hawakusikia hata harufu ya ule mwili?
Kama hakuna mpangaji shirika limechukua hatua gani?
Kama kuna mpangaji, huyo mpangaji ni nani?

Maswali yote hayakuwa na majibu.

Tofauti na alivyopanga, saa kumi na robo jioni, Jacob Matata alikuwa amesimama nyuma ya mlango wa Afisa Mahusiano ya wateja wa Shirika la Nyumba Makao Makuu.

Alikaribishwa na mama mmoja wa makamo. Baada ya kujitambulisha mahojiano yalianza.
"Kama nilivyokutaarifu kwenye simu, kazi yangu imenifikisha nyumba namba 41A. Ningependa kujua nini unajua kuhusiana na nyumba hii hasa ukizingatia kuwa ni mali yenu. Nani mpangaji wake kwa sasa?’’ Jacob Alisema huku macho yake yakiwa katikati ya uso wa huyo mama. "

Asante, mara baada ya kunipigia nimeitisha faili linalohusiana na hiyo nyumba. Nyumba hiyo ina mpangaji wa muda mrefu sana." Aliongea yule mama huku akiwa anapekuapekua lile faili.
"Okay, je, ni nani huyo mpangaji wa muda mrefu?’’ Jacob Alihoji.
"Si utamaduni wetu kutaja majina ya wateja wetu kwa mamlaka zisizo rasmi......" Yule Afisa alisema na kukatishwa na Jacob.
"Kujua siri ndiyo kazi yangu, hivyo usijali hapa ndiyo nyumbani kwake na Mr. Siri." Jacob alisema.

“Hiyo haitowezekana kaka yangu.” Mama aliweka ngumu. “Sawa mama, nakutakia kazi njema.” Jacob Matata alisimama na kuondoka.
 
MSAKO WA MWEHU
SEHEMU YA KUMI NA TATU


SURA YA NANE
Kisengerenyuma hadi 23/09/2014
Masoud Masoud alikuwa ndio anaripoti chuo kikuu cha "Stanford University" akiwa kama mwanafunzi wa kitivo cha Uhandisi wa Mitambo "Mechanical Engineering". Kukanyaga kwake Ulaya kwa Masoud Masoud akitokea mitaa ya uswahilini Sinza ilikuwa ni kama ndoto ya alinacha tena ya mchana wa saa sita, jua limesimama dede, alikuwa haamini kabisa.
Majumba ya kifahari, magari ya kisasa, mabasi ya mwendokasi na treni za umeme aliyokuwa anayashuhudia tu kwenye filamu na televisheni sasa alikuwa anayaona mubashara kwa mboni za macho yake. Wiki ya kwanza ya mwelekeo "Orientational Course", haikuwa na durusu za darasani. Ilikuwa ni wiki ya kufanya usajili wa chuo, kuonyeshwa benki ilipo ili kufungua akaunti, kuelekezwa maduka ya kununua bidhaa, na sehemu zote muhimu kwa mahitaji ya mwanadamu.
Ilipoanza wiki ya pili, ndio masomo yakaanza rasmi. Shule ilikuwa ngumu kama ilivyo kawaida ya shule ya uhandisi, haitopata kuwa rahisi hata siku moja mpaka dunia itakavyotoweka. Ndio maana wahandisi wanapenda sana watambulike kama Injinia fulani ili kujimwambafai kidogo kufidia machungu ya ugumu wa shule.
Masoud Masoud licha ya ugumu wa masomo alikuwa anaweza kwenda nayo sambamba, huku akiwagaragaza vibaya watoto wa kizungu. Baadhi ya wanafunzi wenzake wakampachika jina "Maso Square The Duduman" kuonyesha kukubali utabe wake katika masomo. Lakini baada ya masomo kwisha darasani alijikuta yupo mpweke kupitiliza hana sehemu ya kwenda, hana mtu wa kumtembelea wala kumjulia hali. Vyakula vya nyumbani kama ugali, wali wa nazi, mihogo ya kuchemsha, magimbi na mengineyo mengi akawa anayakosa. Akaanza kutamani kurejea nyumbani, Tanzania, Waingereza wanasema alipatwa na "Home Sickness".
Mwanachuo mwenzake aliyekuwa mkubwa kwake kiumri, kijana wa kutoka Sudani, kwa jina anaitwa Mudrah Mudriki, aliyekuwa anasomea Shahada ya Sheria. Ambaye ni chotara wa baba Msudani na mama Mzanzibari akatumia hiyo fursa ya upweke wa "Maso Square The Duduman" kumzoea kwa haraka sana, na akafanikiwa.
"Kwanza rafiki yangu Masoud tuanze kwa kuwekana wazi usione matreni ya umeme, ukaona majumba mazuri ukaona Mahoteli na Mikahawa mikubwa mikubwa au ukaona mabenki makubwa huku Ulaya ukadhani Waafrika kwa Wazungu wote wanaishi kwa raha. La hasha ni wachache sana, maisha ya Ulaya yamejaa msongo wa mawazo ambao siyo wa kawaida na kuna wakati hasa wageni wanaingia katika majaribu mbalimbali hata ya kutaka kujinyonga. Ndio maana kama umefuatilia vyombo vya habari jana Waziri Mkuu wa Uingereza kamchagua Waziri wa Upweke. Miongoni mwa malengo ya kuwekwa Wizara ya Upweke ni kukabiliana na upweke unaowakabili watu wazima, wale waliopoteza wapendwa wao, wale wasio na watu wa kuzungumza nao ama hata kugawana fikra na uzoefu" yalikuwa ni maneno ya nasaha ya Mudrah kwa rafiki yake Masoud ya kumfanya asijisikie mpweke. "Sawa nakuelewa rafiki yangu, lakini lakini kwanini sasa kule nyumbani Tanzania hata kwenu Sudani watu wanatamani kuzamia Ulaya kuja kutafuta maisha bora, wakati huku hamna starehe yoyote ya maisha?" aliuliza "Maso Square The Duduman" kwa rafiki yake aliyemsafishia nia na kumuamini.
"Tatizo nadhani ni lile lile tu la kuzuzuka na maroshani wanayoyaona yameota kama uyoga, na vitu vya anasa wanavyoviona. Laiti wangefahamu haya yanayotukuta, Balozi zao za nchi za Ulaya kule nyumbani Afrika wangefugia kuku kwa kukosa watu wanaokimbilia kuomba visa", alijibu kwa umakini Mudrah swali aliloulizwa na rafiki yake Masoud.
Kutokea hapo wakawa wapo kama mapacha, utasema ni "Sunche" na "Kapeto" unapomuona Mudrah ndio umemuona Maso, ukimuona Maso basi ndio umemdiriki Mudrah.
Kidogo kidogo "Maso Square The Duduman" akaanza kuizoea hali ya Uingereza. Wakawa sasa wapo bega kwa bega kila mahali, mambo yao wanayafanya kwa mkono mmoja, sio kwenye kuangalia mechi za kandanda ligi ya Uingereza, sio kwenda muziki, na kwenye kila aina ya starehe.
"Maso Square The Duduman" alimuona rafiki wa kweli ni Mudrah kwa sababu alijitoa wakati yupo kwenye taklifu ya kuyazoea maisha ya Ulaya. Wakawa kama kijibwa na mwanawe, lakini kwa kiasi kikubwa "Maso Maso" alikuwa ameshajenga utegemezi mkubwa kwa Mudrah, na hilo ndio jambo Mudrah alikuwa analitaka, na kulitamani litokee nalo likajipa.
Ikajitokeza ghafla tu Mudrah kakata mguu kwa rafikiye Maso bila taarifa yoyote. Akawa sio wa kumpigia wala kupokea simu ya swahiba wake Maso, wala si wa kujibu barua pepe anayotumiwa na rafiki yake. Hiyo hali ilidumu kwa muda wa si chini ya wiki mbili.
Mbaya hata akienda chumbani kwa Mudrah hapatikani, mlango umefungwa. Na akiwaulizia sanjali wenzake wa kozi ya sheria nao wanasema hawamuoni daima dawamu darasani. Maso akaanza kupata upweke wa mwanzoni, ukamrudia kwa kasi. Akapatwa na daka la roho kwa kumkosa bila taarifa rafiki yake kipenzi walioshibana. Akaanza kupatwa na msongo wa mawazo, na kuanza kupoteza hamu ya kula mpaka akaanza kuwa gofu la mtu mithili ya mgonjwa UKIMWI.
Mwaka wa masomo kuhitimisha muhula wa pili ulikuwa ndio unakaribia kwisha, akawa anajifikiria ndio kwanza anamaliza mwaka mmoja na bado miaka mitatu mbele yake. Masharti ya mfadhili wake ni kubakia Ulaya mpaka amalize Chuo ndio atarudi nyumbani Tanzania. Mbaya zaidi huku nyumbani kwao mama yake alipigwa mkwara na mfadhili kuwa asimsumbue kabisa mtoto wake masomo ni magumu, mtoto wake akifeli hata somo moja tu hatomlipia tena gharama za masomo na maisha.
Ikabidi Bi. Mwantumu awe anawasiliana kwa nadra sana na mtoto wake, jambo ambalo lilizidi kumuongezea upweke kipindi ambacho alikuwa anahitaji mfariji. Ghafla bin vuu, siku moja usiku akiwa amekaa nje ya bustani za hosteli maalumu kwa Wanachuo, akiwa ameshakata tamaa ya kuishi Ulaya, anatafakari kitu cha kufanya. Akajitokeza rafiki yake Mudrah Mudriki katika uoni wa macho yake kama mzuka vile.

Maso akiwa amepigwa na butwaa na kushikwa na gagaziko la ulimi, hayaamini macho yake "Assalaamu Aleikum rafiki yangu kipenzi wa moyoni" aliwahiwa kusalimiwa na Mudrah huku wakikumbatiana. Badala ya kujibu salamu, Maso haraka haraka akamtupia swali, "ulipotelea wapi ulinipa wahaka wa moyo usiomithilika kubeba nisiyoyaweza kifuani mwangu, kitu gani nilikukera uniambie kabla wakati haujazidi kwenda matiti nikuombe radhi tusameheane turudi kuwa washirika wa chanda na pete kama zamani". "Maso Square The Duduman" alikuwa anaongea kwa hisia za ndani ya moyo mpaka machozi yalikuwa yanamlengalenga.
Alikuwa ndio kwanza anatimiza miaka 21 bado anahitaji muongozo na faraja ya watu wa karibu. Mudrah Mudriki rafiki mkia wa fisi ukimshiriki atakufilisi alikuwa anafurahi kimoyomoyo kuwa lengo lake linakaribia kutimia muda sio mrefu la kumtumbukiza Maso kwenye shimo refu ambalo kuchomoka kwake itahitajika kudra za Rabana tu.
Kiuhalisia Mudrah Mudriki alikuwa Mwanachuo feki, alitumwa kazi maalumu ya kumuingiza "Maso square The Duduman" kwenye kundi la kigaidi la "Al-shabaab". Mchongo wote ulichongwa na mwarabu mmoja Mfanyabiashara na Mkandarasi maarufu nchini Tanzania 'Hafeedh Abdullah', ambaye ndio aliyemrubuni Bi.Mwantumu kuwa anataka kumsaidia kumsomesha mtotowe Uhandisi huko Ughaibuni ili aje kumuajiri kwenye kampuni zake zilizosambaa Arabuni na Afrika. Akamzuga ameamua kumsomeshea mwanawe kwa sababu yeye ni mwanamke mjane na pia kutokana na mtoto wake kufanya vizuri kwenye mitihani yake ya Kitaifa. Akamuingiza kingi kuwa Mwenyezi Mungu katika vitabu vya dini amesisitiza sana kuwajali wajane na mayatima kama Maso. Mfanyabiashara huyo Hafeedh Ibn Abdullah alikuwa ana ushirika na kampuni za Ukandarasi wa majengo nchini Sudani tokea mwaka 1989.
Hivyo Osama Bin Laden alivyokuja kuishi nchini Sudani kuanzia mwaka 1991-1996 alivyotafuta washirika wake wa kufanikisha ajenda zake za kigaidi siku za usoni akamsajili kibopa Hafeedh Ibn Abdullah kuwa ndio msimamizi mkuu wa shughuli za "Al-qaeda", Ukanda wa Afrika Mashariki. Chambo chao cha udaga kilikuwa kinakaribia kumnasa samaki muhimu kwao katika karata ya ugaidi.
Walitambua kabisa ugaidi katika karne ya 21 unahitaji watu wenye ubongo unaochemka sana kama "Maso Maso" ambaye alikuwa amemaliza shule katika sekondari ya watoto wenye vipaji maalumu vya kiakili, Mzumbe Sekondari. Mapambo yoyote dhidi ya adui yako katika zama za sayansi na teknolojia zilikuwa zinahitaji akili nyingi kuliko nguvu nyingi.
"Rafiki yangu samahani sana nimeipata njia ya kunikurubisha kwa Mola wangu. Mie nimeamua kujitenga na wewe kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qur'an Surat Mujaadalah, surah ya 58 aya namba 22; "Hutokuta watu wanaomuamini Allaah na Siku ya Mwisho kuwa wanafanya urafiki na kuwapenda wanaompinga Allaah na Rasuli Wake, japo wakiwa ni baba zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao (Allaah) Amewaandikia katika nyoyo zao iymaan, na Akawatia nguvu kwa Ruwh (Wahyi) kutoka Kwake, na Atawaingiza Jannaat zipitazo chini yake mito ni wenye kudumu humo. Allaah Ameridhika nao, nao wameridhika Naye. Hao ndio kundi la Allaah. Tanabahi! Hakika kundi la Allaah ndio lenye kufaulu". Akapumzika kuongea baada ya kumaliza kusoma aya. Akachomoa hanchifu yake mfukoni, akaanza kufuta machozi yake yaliyokuwa yanabubujika kama maji, kujionyesha amejawa na mapenzi ya Allah moyoni mwake kumbe bosheni tu, kisha akaendelea na mahubiri yake.
"Sasa kwa msingi huo mie nakuacha rasmi kwenye maisha yako ya kumtumikia Shetani, mimi sasa nimempokea Allah na kumfanya kuwa taa ya maisha yangu. Sasa wewe bado unahudhuria muziki, bado unaangalia kandanda wakati wachezaji wake wamevaa nusu uchi na dhunubu kibao ambazo zinamchukiza Allah na Mtume wake, hivyo nakuaga rasmi urafiki mimi na wewe basi, kwaheri" akaaga, akageuka akawa anajifanya anaondoka.
"Maso Square The Duduman" akawa anaona sasa anaachwa solemba moja kwa moja, hata onana tena na swahibu wake. Kuachana kwao urafiki inamaanisha hana nguzo tena ya kujishikia atakapopatwa na shida ugenini. Ndugu yake mwenye asili ya nyumbani Zanzibari, Tanzania aliyemtegemea sasa anamuacha kwenye mataa. "Mudraaaaah Mudraaaaaah....pliiiiiiz my friend don't leave me, let's talk pliiiz..!! " ilikuwa ni sauti ya kubembeleza ya Maso ikimtaka rafiki yake Mudrah arejee wayajenge. Furaha ya Mudrah moyoni mwake ilikuwa kama amepaa yupo juu ya mwezi, ndio kitu alichokuwa anakitarajia. Alikuwa tayari ameshakaribia kutaka kupotea kwenye upeo wa Maso ndio akasikia sauti inayomuita kwa nguvu zote.
Akajifanya anatikisa kiberiti kwa kujichelewesha kidogo, akasikia tena sauti ya Maso inamuita. Kiunyonge akajifanya anarudi alipo Maso. Alipofika wakakumbatiana na rafiki yake, huku anajifanya kulia kifaurongo. "Sasa inabidi nikupeleke msikitini ukatubu dhambi zako usilimu upya"
Wakakubaliana wapitiane saa kumi na nusu usiku kuelekea msikitini kwa shekhe Dawoud El-jabeer. Shekhe ambaye durusu zake za masomo ya dini baada ya sala ya alfajiri zilikuwa zinavutia vijana wengi wa Ulaya hususani nchini Uingereza. Huyo Shekhe ndio alikuwa bomu maalumu lililotegwa na Al-qaeda kuwapika magaidi wapya kwa kutumia kasumba ya Uislamu wa itikadi kali. "Maso Square The Duduman" alikuwa anaenda kulishwa itikadi kali ya kiislamu iliyopotoshwa makusudi ili kuwapotosha vijana wasio na hatia wajitoe muhanga kwa kujivika mabomu.

[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
"Maso Square The Duduman" amesajiliwa rasmi kuwa gaidi.
Ulikuwa ni usiku wa giza nene lililoenea kila mahali. Nuru pekee iliyoangaza nchi ilikuwa ni ya nyota tu zilizoko angani ambazo zilimeremeta kwa utulivu. Watu wengi walikwisha jilalia zao usingizi wa pono kutokana na uchovu wa mihangaiko ya kimaisha ya mchana kutwa. Wakati fulani sauti za wazururaji wa usiku na walevi wenye kupenda ugomvi ilisikika mbali kabisa na karibu na kambi ya siri ya magaidi wa "Al-shabaab" iliyopo katika Milima inayoitwa 'Jabar Marrah', Magharibi mwa Jimbo la Darfur, nchini Sudani. Walevi hao walikuwa wanajiiba tu kutimiza hawaa za nafsi zao kwa kunywa pombe katika nchi ambayo inafuata utawala wa Sharia za Kiislamu, ambapo ukikamatwa umekunywa pombe unapigwa mboko hadharani.
"Maso Square The Duduman" usiku huo alikuwa amejisokota kwenye kichaka kilichopo kwenye Milima hiyo akiwa amevaa sare maalumu za "Al-shabaab", kombati za rangi ya kijani mpauko. Ghafla bin vuu bila kutegemea, katika mazingira ya ukame wa jangwani, mvua ya kidindia ikaanza kunyesha mfululizo. akaanza kulowana na akatota chapachapa mwili mzima.
Hakuwa na jinsi bali kuendelea kubakia pale pale alipohitajiwa kuwepo na wakufunzi wake. Alikuwa yupo doria ya kambi katika siku yake ya mwanzo kabisa akiwa kambini hapo kwa ajili ya mafunzo ya muda mrefu yatakayompika aje kuwa gaidi mahiri duniani. Alishakacha masomo kitambo na kutorokea nchini Sudani bila familia kung'amua. Siku ambazo ilikuwa hamna kulala mchana na usiku kwa muda wa miezi miwili mtawalia. Ilikuwa ni mwendo wa kunyanyua vitu vizito na kutembea navyo umbali kadhaa, kubiringika, kupiga pushapu, skwashi, kutambaa na kifua, kukimbia na kunyoosha viungo. Kambi ya 'Jabbar Marrah' ilikuwa ni pacha wa kambi kuu ya kigaidi ya "Al-qaeda" iliyopo katika mashamba ya 'Tarnak' huko 'Kandahar', Afghanistani. Hiyo ndio kambi aliyokuwa anaishi gaidi mkuu Osama Bin Laden, enzi za uhai wake wakati amejichimbia nchini Afghanistani.
Wakufunzi wake wote kijana "Maso Maso" walitokea huko 'Tarnak' wakitumia mitaala ya huko huko Kandahar iliyoachwa na muasisi wa Al-qaeda, Osama Bin Laden. Wakufunzi wa "Maso Maso" walikuwa ndio wale wale wakufunzi mahiri waliowafunza vijana hatari kwa ugaidi duniani, "Mohammed Atta" na "Ziad Jarrah". "Mohammed Atta" raia wa Misri na "Ziad Jarrah" raia wa Lebanoni wakiwa wamemaliza elimu yao ya Chuo Kikuu jijini Hamburg, nchini Ujerumani, hawa ndio walioshiriki mashambulizi ya kujitoa mhanga kwa kutumia ndege ya tarehe 11/09/2001, maarufu kwa "September 11" yaliyotokea nchini Marekani.
ITAENDELEA
IMG_20200609_163242_928.jpg
 
SITOENDELEA NA RIWAYA YA MSAKO WA MWEHU BAADA YA KUHARIBIWA MUENDELEZO WAKE KWA KUCHANGANYWA NA RIWAYA NYINGINE TOFAUTI.

SAMAHANI SIO KUSUDIO LANGU HALI HALISI NDIO HIVYO
 
SITOENDELEA NA RIWAYA YA MSAKO WA MWEHU BAADA YA KUHARIBIWA MUENDELEZO WAKE KWA KUCHANGANYWA NA RIWAYA NYINGINE TOFAUTI.

SAMAHANI SIO KUSUDIO LANGU HALI HALISI NDIO HIVYO
Aiyaaaa ushatubwenga rungu la kichwa sijui itakuwaje sasa?
Utamu umeishia njiani yaani
aisee!!!
ADK ukije huku Naash Nash haipo tena
 
  • Thanks
Reactions: ADK
Aiyaaaa ushatubwenga rungu la kichwa sijui itakuwaje sasa?
Utamu umeishia njiani yaani
aisee!!!
ADK ukije huku Naash Nash haipo tena
MODERATOR MODERATOR
BILA NIANZISHE HADITHI MPYA TU
 
RIWAYA: MSAKO WA MWEHU

SEHEMU YA NANE

Wakazunguka nyuma ya kibanda kwenye maboksi na uchafu wa dukani na kilipo kifurushi cha mwehu "Maso Maso". Kachero Manu akakalia kiti cha mbao kichakavu huku Soni akikalia juu ya dumu tupu, lenye rangi ya manjano la lita 20 la mafuta ya kula. Mahojiano yakaanza kama ifuatavyo;
Kachero Manu: "Unamfahamu vipi Maso Maso?"
Soni: "Kumfahamu kivipi ningeomba ufafanuzi "
Kachero Manu: "Hivyo hivyo unavyomjua" alijibu Kachero Manu kwa sauti yenye hasira ila hakutaka kujijulisha.
Soni: "Maso Maso", ni mwehu ambaye amezoea kukaa hapa dukani kwangu, pembeni hapo ulipokaa ndio kikazi chake. Iwe mvua iwe jua hapo ndio maskani yake, wanasema watu kapigwa kipapai"
Kachero Manu: "Ana muda gani tokea awe anakita kambi dukani kwako hapa?"
Soni:"Sikumbuki vizuri sana ila haizidi miezi sita"
Kachero Manu: "Kuna vitu labda alikuwa anaongea ongea na wewe? "
Soni: "Hapana, mara nyingi alikuwa anautumia kuimbaimba nyimbo zake na kuandika andika kwenye kidaftari chake, mara chache ndio alikuwa anaongea lakini maongezi yasiyo na mtiririko maalumu ya kiwehuwehu"
Kachero Manu: "Unaweza kunionyesha hilo furushi lake nione hicho anachokiandika!". Soni akajibu swali kwa vitendo kwa kwenda kubeba fuko lenye vitu vya chizi "Maso Maso" akalibwaga mbele ya Kachero Manu. Kachero Manu akasitisha mahojiano kwa muda akaanza kazi ya kuchakurachakura kwenye lile fuko la mwehu. "Kweli hili fuko la chizi, mpaka chupa za mikojo zimo! " alijisemea kimoyomoyo Kachero Manu. Kulikuwa na vikorokoro vya simu mbovu, taa mbovu za kuchaji za Mchina, karatasi zilizochanika za aya za Qu'ran, viwembe vilivyotumika, mabakuli na vikombe na kila aina ya takataka zinazostahili kuwemo kwenye furushi la chizi.
Alipokuwa anakaribia kukata tamaa akashika kitu kigumu, alipokivuta akakuta ni daftari. Akashikwa na tashiwishi ya kulifungua na kujua kilichoandikwa. Ikadondoka kikaratasi chakavu cha maandishi ya Kiarabu, akakihifadhi sehemu salama. Kisha alipozidi kulifungua daftari hakuona chochote cha kumsaidia zaidi ya namba za simu kochokocho.
Kachero Manu: "Je siku ya mlipuko, Maso Maso alikuwepo au hakufika kabisa?". Akaendeleza mahojiano yake baada ya kulifunga furushi vizuri.
Soni: "Ndio alikuwepo alikaa hapo hapo, ila siku hiyo alikuwa kama mgonjwa hakuwa mchangamfu na hakula chochote tokea asubuhi, ulipotokea ule mlipuko, taharuki iliyokuwepo siku hiyo kila mtu aliingilia upande wake, na hajaonekana tena eneo hili mpaka tuna wasiwasi kama amesalimika na kifo"
Kachero Manu: "Ahsante sana kwa ushirikiano wako, nikikuhitaji tena nitakuja na samahani kwa kukuchelewesha na biashara yako"
Soni: "Hamna shida karibu tena, ngoja nifungue duka langu sitaki kula mate " aliongea kwa sauti ya hasira huku uso wake umebeba mawimbi ya ndita kuonyesha kuchukizwa kwa kuhojiwa muda wa biashara. Kachero Manu hakujali akaondoka zake huku akiwa amechukua kila kiratasi na kile kidaftari cha "Maso Maso" huku akishukuru kwa kupata majibu yaliyomkifu kifaya.
Muda sasa ulikuwa umeenda harijojo, ilikuwa imeshafika saa moja kasorobo magharibi. Akapitiliza moja kwa moja mpaka kwenye geti la Wizara ya Mambo ya Ndani kwenda kukagua namba za hiyo gari v8 PT3001 aliyotajiwa na Soni kuwa kigogo anayeitumia hiyo gari anamsaka .
Kachero Manu alikuwa tayari kasharuhusiwa na walinzi wa eneo hilo kufanya ukaguzi wake wa gari anayoitafuta. Alikuta v8 zaidi ya 18 rangi ya buluu zimejipanga. Hayo yote yalikuwa ni magari yanayotumiwa na Vigogo wa Wizara na Polisi Makao Makuu. Akaanza kufanya spenkesheni yake kwenye yale magari. Alirudia zaidi ya mara tatu halikuona lile gari alilotajiwa jina namba zake na Soni, PT3001.
Kijasho chembamba kikaanza kumvuja mpaka kwenye meno. Uso wake ukala debe akaanza kukata tamaa ya kuikosa gari hiyo. Akaamua awashe na mwangaza wa tochi ya simu yake ya mkononi kusaidia mwangaza wa eneo lile. Alipofika kwenye gari lenye namba 'PT1003' akasimama kwa muda akiikagua. "Namba hili zinafanana na zilizotajwa PT3001 tofauti ni mpangilio wa namba tu, labda zinachezewa" aliwaza Kachero Manu.
Akaanza kuchezea kile kibao namba za gari, akakikuta kibao kimeungwaungwa kiufundi mkubwa huwezi kugundua kwa haraka. Katika kupekenyua akakuta kuna nyaya zimepita kwenye namba tatu na moja. "Shabaaaashiii......kuna mchezo mchafu unafanyika, inaelekea gari ikitoka geti kuna kitufe kinabinywa kuzichezea namba za mwishoni zinapishana ndio maana mtaani linasoma PT3001, lakini humu ndani linasoma PT1003, kwisha kazi ujanja wake upo uchi" alijisemeza yeye mwenyewe.
Haraka haraka akawa anarudi pale getini kuulizia jina la kigogo anayetumia lile gari lenye namba za utata.
Alipofika wakati anaandikiwa jina la kigogo anayeitumia hiyo gari, tahamaki mtaani karibia na getini ikasikika milio ya risasi mbili zilizopigwa mtawalia, na kufuatiwa na risasi moja iliyobutuliwa juu, halafu ikasikika mseleleko mkali wa gari lenye kwenda kwa mchepuo wa kasi. Akajua mambo yameshaenda segemnege huko nje. Akafanya haraka kuchukua ile karatasi aliyopewa na kukimbilia nje ya geti huku mkononi tayari kachomoa bastola yake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
"Muuza duka Soni ameuliwa kinyama kibandani kwake"
Mamia ya watu walikuwa wamekusanyika karibia na kiduka cha Soni, huku giza lilikuwa tayari limeanza kushitadi angani katika usiku huo mbichi. Kila mmoja akijiuliza kulikoni mpaka muuza duka Soni ameuliwa kikatili namna ile. Hali ya hewa ilishachafuka kifo cha Soni kilizua tenge tahanani eneo hilo jirani na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Maiti ya Soni ilikuwa imelala chali, damu zinamtiririka huku matundu ya risasi yakionekana dhahiri shahiri kwenye paji lake la uso na shingoni.
"Mie nimeshuhudia kila hatua ya tukio hili, walikuja watu wawili kwenye gari rangi ya kijivu aina ya "Brevis", mtu mmoja mrefu amevaa koti la kujikinga na mvua na kofia akashuka akaenda mubashara kwenye kiduka. Sikumfuatilia nikajua ni mteja wake tu anahitaji vitu vya dukani. Baadae nikaona kama kuna furushi kalibeba tokea kule anakohifadhia marehemu Soni takataka zake akalirusha ndani ya gari. Nae akaingia ndani ya gari kwa kuharakisha, lakini hawakuliondoa gari. Halafu baada ya kupita kitambo kama cha dakika 10 akashuka mmoja akakaribia tena kama meta 3 akanyanyua bastola yake na kumfyatulia risasi mbili za kichwani, ikabidi nijifiche nyuma ya kabati la fundi viatu jirani pale. Mpigaji akakimbilia kwenye gari kwa haraka. Alivyoona tumeanza kujikusanya wakadhani tunataka kuwapiga kipopo, mmoja wao akapiga risasi moja hewani, kisha wakatimka na gari lao wakala matu kwa umahiri mkubwa. Wakaingilia hiyo barabara ya mtaa wa Ohio na gari lao na kutokomea kusikojulikana" alielezea tukio hilo kwa ufasaha mkubwa mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Kachero Manu alivyoona umati wa watu umejikusanya akaamua kuirudisha silaha yake kwenye ala yake, akasogea karibu na eneo la tukio. Alikuwa ni mmoja wa wale waliosikiliza kwa umakini kabisa maelezo ya yule shuhuda. Baada ya hapo akaisogelea maiti ya Soni, akaona tayari kashaaga dunia, ameshaelekea jongomeo zamani.
Akajiona ni mtu mwenye bahati ya mtende kuwahi kuzungumza nae Soni muda mchache kabla hajapoteza maisha yake na kupata maelezo yaliyompa mwangaza wa upelelezi wake. Akatumia fursa ya watu kushuhudia mwili wa marehemu kuzunguka kule nyuma ya kiduka kwenye matakataka kuangalia kama furushi la chizi "Maso Maso" lipo au ndio limebebwa na wauaji!. Alipopiga jicho, akaona hamna kitu limepotea. "Kumbe furushi la mwehu, ni dili kama dhahabu linasakwa kwa udi na uvumba" alijiwazia peke yake Kachero Manu huku anatabasamu. Alishaanza kuunganisha matukio mbalimbali yatakayofanikisha upelelezi wake na hatimaye kuwatia mbaroni wahusika wa matukio ya ugaidi uliotekelezwa kwenye jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani, Ijumaa iliyopita.
Askari kanzu wakawa wameshafika na kuanza kutawanya watu huku wakizungushia uzio eneo la tukio. Kachero Manu akaona isiwe tabu akaanza kuondoka mdogo mdogo kwa miguu kurejea ofisini, kufungasha vitu vyake arejee nyumbani kwake, tayari kwa safari ya Dodoma kesho kutwa yake.
Alipanga kwenda kumuongezea nguvu Kachero Yasmine. Lakini tukio la kuuliwa kwa kijana Soni kulimpa msongo wa mawazo wa kutaka kufahamu "je kuna uhusiano kati ya mauaji ya Soni na msako wa walipuaji wa jengo la Wizara? "
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
ITAENDELEA
KUPATA HARDCOPY NICHEKI
0625920847

Soft copy bei gani?
 
Mods kwa mara ya kwanza mmenikwaza sana kuunganisha vitu. Hili ni jukwaa huru kila mtu anaweza anzisha chochote ili mradi asivunje tuu kanuni na taratibu. Kuunganisha hizo threads mbili hamjatutendea haki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mods kwa mara ya kwanza mmenikwaza sana kuunganisha vitu. Hili ni jukwaa huru kila mtu anaweza anzisha chochote ili mradi asivunje tuu kanuni na taratibu. Kuunganisha hizo threads mbili hamjatutendea haki

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata mimi nimekereka....wastage of energy bila sababu
 
Invisible kama bado moderator please tunaomba fikisho ombi letu watutenganishie hizi Riwaya ili tuendelee kuburudika baada ya kazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom