RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 49
Japokuwa nilikuwa jasusi hatari wa kuogopwa lakini mbele ya mlimbwende yule nilikuwa kama mbwa muoga mbele ya chatu mwenye njaa kali. Veronica akavuta kamba nyembamba ya kivazi chake kiunoni na hapo kivazi kile kikaanguka chini na kumuacha na nguo yake nyekundu nzuri ya ndani huku harufu nzuri ya manukato yake ikinishawishi kuendelea na hatua inayofuata.
Sikuwa na ujasiri wa kupingana zaidi na hizia zangu hivyo taratibu nikaupeleka mkono wangu ndani ya nguo ya ndani ya Veronica na kuanza kuyatomasa makalio yake laini yaliyoshiba minofu. Veronica akashtuka kidogo na kuachia mguno hafifu wakati mkono wangu mwingine ulipokuwa ukiyatomasa matiti yake taratibu. Ndimi zetu zilipoachana ulimi wangu chakaramu nikautembeza taratibu shingoni na hatimaye sikioni mwake na hapo nikasikia sauti yake hafifu mguno wa mahaba. Veronica hakuweza kuvumilia tena hivyo haraka akaishusha chini nguo yangu ya ndani na kuupeleka mkono wake akizichezea malighafi zangu na kunipelekea nianze kuhema ovyo.
Muda mfupi uliofuata tulikuwa kwenye kochi kubwa la sofa lililokuwa pale sebuleni huku kila mmoja akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi. Veronica alikuwa msichana mtundu sana aliyeyamudu vyema mapenzi kiasi cha kunipelekea nijihisi kama mvulana wa sekondari. Pamoja na ufundi wangu wote wa mapenzi lakini kwake bado sikuweza kufua dafu kwani alinidhibiti vyema pale kwenye kochi mimi chini yeye juu huku nikiitazama mijongeo hafifu ya kiuno chake wakati alipokuwa akipanda juu na kushuka chini taratibu.
Tulikuwa kwenye ulimwengu mzito wa mapenzi na dunia ilikuwa kama kisiwa cha raha kwa ajili yetu. Veronica alikuwa amezitendea vyema hisia zangu na raha niliyoipata macho yangu hayakuweza tena kumtazama usoni.
_____
Kwa mara kwa kwanza tangu nitoke jijini Dar es Salaam nilikuwa nimelala usingizi mtamu wa kueleweka. Ilikuwa tayari imetimia saa kumi na moja na robo alfajiri wakati niliposhtuka kutoka usingizi. Veronica alikuwa bado yupo usingizini huku kichwa chake amekilaza kifuani kwangu pale kwenye kochi. Mguu wake mmoja ulikuwa katikati ya mapaja yangu huku mkono wake mmoja ameuzungusha shingoni mwangu na kwa mbali niliweza kusikia sauti hafifu ya mkoromo wake wa uchovu. Penzi zito la Veronica lilikuwa limeamsha ari mpya nafsini mwangu na kupitia ukaribu ule kitu fulani kilikuwa kimeanza kujengeka moyoni mwangu. Kwa namna moja au nyingine Veronica alikuwa ameuteka moyo wangu na sasa nilianza kuona ugumu wa kuwa mbali naye katika harakati zangu.
Taratibu nikayatembeza macho yangu kuipeleleza vizuri sebule ile. Ilikuwa sebule ndogo yenye samani za kawaida kama seti moja ya makochi ya sofa na meza ndogo ya chakula iliyozungukwa na viti vinne iliyokuwa upande wa kushoto kwenye sebule ile. Katikati ya sebule ile kulikuwa na meza nyingine fupi na nzuri ya mbao ya mti wa msonobari iliyofunikwa kwa kitambaa cheupe kizuri chenye maua mekundu ya kufuma kwa mkono. Juu ya meza ile kulikuwa na ua zuri ndani chungu cha udongo mfano wa kibuyu cha asili kilichofinyangwa kwa mkono. Sakafu ya mle ndani ilifunikwa kwa zulia maridadi la rangi za kupendeza na katika kuta safi nyeupe za sebule ile niliziona picha mbili kubwa za kuchora za wanyama wa mwituni na kalenda nzuri zikiwa zimetundikwa. Kupitia zile samani za pale sebuleni haraka nikatambua kuwa kipato cha Veronica kilikuwa cha chini sana ingawa alionekana kuishi maisha ya daraja la kati kwa kadiri alivyoweza.
Upande wa kulia wa ile sebule nikauona mlango uliofunikwa kwa pazia jepesi. Hisia zangu zikanitanabaisha kuwa ule huwenda ulikuwa mlango wa kuelekea chumbani.
Nilipokumbuka kazi ngumu iliyokuwa mbele yangu sikuona sababu ya kuendelea kulala pale sebuleni hivyo taratibu nikamsogeza Veronica pembeni yangu na kisha kuketi na wakati nikifanya vile maumivu makali ya majeraha yangu yakapenya mwilini
Mara moja nilipoyatazama yale majeraha ya mbwa mikononi mwangu nikaanza kuingiwa na wasiwasi wa kuugua maradhi mabaya ya kichaa cha mbwa kwa vile sikuwa na hakika yoyote juu ya afya ya wale mbwa walionishambulia usiku wa jana kule Le Tulip Hôtel Africaine. Tumbo langu lilikuwa dhaifu sana kwa vile usiku wa jana sikuwa nimetia kitu chochote tumboni. Penzi zito la msichana Veronica usiku uliopita lilikuwa limenipelekea nisahau njaa kali iliyokuwa ikinitafuna tumboni. Haraka nikasimama pale kwenye kochi na kuanza kuichunguza ile nyumba kwa utulivu. Nilipomaliza nikagundua kuwa ile nyumba ilikuwa na chumba kimoja cha kulala, sebule, jiko, choo na bafu.
Nililikuta begi langu la mgongoni nililomuachia Veronica asubuhi ya jana kule Havana Club likiwa juu ya meza ndogo iliyokuwa kando ya kitanda chumbani kwake. Haraka nikaingia bafuni kuoga nilipotoka mwili ulikuwa tayari umepata nguvu mpya ambapo nilijiandaa vizuri na kubadili nguo. Kulikuwa na vifaa muhimu vya huduma ya kwanza kwenye begi langu hivyo nilijifanyia tiba muhimu dhidi ya yale majeraha kwa kujichoma sindano ya kuzuia maradhi ya kichaa cha mbwa. Nilipomaliza nikaelekea sebuleni ambapo nilimkuta Veronica akiendelea kuuponda usingizi pale kwenye kochi. Sikumuamsha badala nikaliokota koti langu na kofia na kisha kuelekea bafuni ambapo nilivisafisha vizuri na kuvitia mwilini. Sasa nilikuwa katika muonekano mpya wa suruali nyeusi ya jeans, fulana ya rangi ya kijivu, kofia nyeusi ya kapero, koti jeusi la mvua na buti ngumu za ngozi miguuni.
Nilipotoka bafuni nikaelekea jikoni na baada ya pekuapekua ya hapa na pale nikakuta hotpot yenye chakula kizuri cha ndizi za matoke zilizopikwa kwa ufundi wa hali ya juu huku zikiwa zimechanganywa vizuri na samaki wa ziwa Tanganyika waitwao Mukake. Sikuwa na shaka yoyote kuwa chakula kile kilikuwa kimeandaliwa na Veronica kwa ajili yangu usiku wa jana. Pembeni ya hotpot ile kulikuwa na chupa ya chai ambapo nilipoifungua ndani yake nikaona maziwa fresh. Kile chakula kilikuwa kingi hivyo tungeweza kula mimi na Veronica na kushiba vizuri kabla kila mmoja hajaelekea kwenye harakati zake. Hivyo haraka nikapasha moto kile chakula kwa jiko la gesi na kuchemsha yale maziwa.
Ni wakati nilipokuwa mbioni kumaliza zoezi lile la kuandaa chakula pale niliposhtushwa na mkono laini ukinishika begani. Mara moja nikashtuka na kugeuka nyuma huku moyo wangu ukianza kupoteza utulivu lakini kitendo cha kumuona Veronica kikauyeyusha haraka mshtuko wangu na kusababisha tabasamu jepesi lichomoze usoni mwangu. Veronica alikuwa amenyata taratibu kutoka sebuleni kwenye kochi na hatimaye kusimama nyuma yangu. Ingawa macho yake yalikuwa na kila dalili za uchovu lakini tabasamu lake maridhawa lilirudisha uhai mpya usoni mwake na kumpelekea aonekane mwanamke mzuri na mrembo sana kupita wote niliowahi kuwaona duniani.
Mwanga hafifu wa pambazuko la alfajiri uliokuwa ukipenya taratibu mle ndani ukaniwezesha kuiona hazina matata iliyojificha katika umbo la mlimbwende yule. Veronica alikuwa amesimama nyuma yangu kama alivyozaliwa bila nguo yoyote ya kujisitiri mwilini mwake. Loh! nywele zangu zikasimama wima, moyo wangu ukacheza kidogo kisha mdomo wangu ukaachama huku nikimkodolea macho ya uchu kama fisi aliyeona mfupa.
“Mbona umeamka mapema mpenzi?”. Sauti nyororo ya Veronica ikaziachia huru fikra zangu na kuzirudisha kwenye ufikirivu wa kawaida na hapo nikaunyanyua mkono na kuitazama saa yangu ya mkononi.
“Sasa hivi ni saa kumi na mbili kasoro mpenzi”. Nikaongea kwa sauti hafifu ya kirafiki na hapo nikamuona Veronica akishikwa na mshangao.
“Khe! kumbe kumeshapambazuka!”
“Kazini unaingia saa ngapi?”. Nikamuuliza.
“Saa moja na nusu asubuhi”. Veronica akanijibu kwa sauti hafifu huku akionesha kukerwa na ratiba ile.
“Hata leo Jumapili?”
“Kila siku mpenzi”. Mara moja nikamtazama Veronica na kumhurumia hata hivyo sikuwa na namna na hatimaye nikavunja ukimya.
“Nenda kaanze kujiandaa utakapomaliza chakula kitakuwa tayari mezani”. Maneno yangu yakampelekea Veronica atabasamu kidogo kisha akanitupia macho usoni na macho yetu yalipokutana hisia za mapenzi zikafufuka upya nafsini mwetu.
“Gilbert…”
“Naam Veronica”
“Je tʾaime a la folʾie”. Nakupenda hadi najihisi kuchanganyikiwa.
“Moi aussi”. Mimi pia.
“Sʾil vous plaît, ne me quitte pas mon amour”. Tafadhali usiniache mpenzi wangu.
“Jusquʾ à ce que la mort nous sèpare”. Hadi kifo kitakapotutenganisha. Nikaongea kwa utulivu huku nikiruhusu tabasamu langu kuchanua usoni. Veronica akanisogelea na kunibusu mdomoni kisha taratibu akageuka na kuondoka na hapo nikapata kuona vizuri mtikisiko maridhawa wa umbo lake chakaramu. Kwa mara ya kwanza nikahisi nafsi yangu ilikuwa imepata utajiri mkubwa wa furaha isiyoelezeka.
Ilipofika saa kumi na mbili na nusu Veronica alikuwa tayari amekwishamaliza kujiandaa. Alipotoka chumbani akanikuta nikiwa nimeketi tayari kwenye ile meza ya chakula sebuleni huku taratibu nikipekua kurasa moja baada ya nyingine ya kile kitabu kidogo cha sala nilichokipata kwa yule padri wa kizungu aliyenyongwa kule kwenye kile chumba 403 cha Le Tulip Hôtel Africaine nikijaribu kuchunguza kama ningeweza kuvumbua kitu chochote cha kunisaidia katika harakati zangu. Kurasa ya mwisho ya kitabu kile haikuongeza ziada yoyote katika kile nilichokuwa nikikifahamu hapo awali hivyo nikafunika kile kitabu na kukitia mfukoni huku macho yangu yakiwa kwa Veronica nikijidai kuwa nilikuwa katika harakati za kuombea chakula.
Asubuhi hii Veronica alikuwa amependeza zaidi katika muonekano wa vazi la kitenge cha wax na kilemba kilichofungwa kwa ufundi wa hali ya juu kichwani mwake. Kama ningekuwa promota wa mitindo ya mavazi ya kiafrika sikuwa na shaka yoyote kuwa Veronica angeweza kuniletea ushindi wa kuaminika. Nilipomuuliza juu ya sare zake za kazi akaniambia kuwa angebadili mavazi baada ya kufika kazini kwake.
Wakati tukipata mlo pale mezani kila mmoja akawa amejikita katika kumdadisi mwenzake na hapo nikapata nafasi ya kujua mambo machache kuhusu Veronica ingawa kwa upande wangu aliambulia uongo katika kila swali aliloniuliza.
Saa moja asubuhi kasoro dakika tano tulimaliza kupata kifungua kinywa na kisha kushushia na mvinyo mtamu wa Chateau Lascombes nilioupata kwenye kile chumba cha ofisi ya meneja wa New Paradol Residence usiku wa jana kutoka kwa yule mtu wa mwisho niliyepambana naye. Mvinyo ule ulikuwa umeamsha ari mpya katika miili yetu na kutuchangamsha vizuri kasi cha kupunguza nishai machoni. Veronica akaondoa vyombo na kwenda kuvisuuza jikoni, aliporudi akachukuwa pochi yake ya begani na hapo tukatoka nje ya nyumba ile na kufunga mlango.
Asubuhi ile hali ya hewa ya jiji la Bujumbura ilikuwa imepoa zaidi, manyunyu hafifu ya mvua yalikuwa yakianguka kutoka angani kulikotanda wingu zito la mvua kiasi cha kuweza kuizuia miale ya jua la asubuhi kutua vizuri ardhini. Kufuatia lile jaribio la mapinduzi ya kijeshi jiji la Bujumbura ni kama lilikuwa limelala kwani wakazi wake hawakuwa huru sana kurandaranda mitaani kama ilivyokuwa desturi yao badala yake hofu ilikuwa imetanda kila kona.
Mara baada ya kuyaacha maskani ya Veronica tulishuka kwenye jengo lile la ghorofa la shirika la nyumba la taifa na kushika uelekeo wa ilipo barabara ya Boulevard de Independence. Wakati tukitembea macho yangu yalikuwa makini kutazama kila mahali katika namna ya kuchunguza kuwa hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa akitufuatilia nyendo zetu.
Tulipoyafikia makutano ya barabara ya Boulevard de Independence na barabara ya Avenue de Litalie, Veronica akanishawishi kuwa tuvuke makutano yale na kuendelea kutembea kidogo kwa kuifuata barabara Boulevard de Iʾindependence kwani mbele kidogo tungekuja kukutana na kituo cha maegesho ya teksi nje ya kiwanda cha kuchapisha magazeti. Lilikuwa wazo zuri hivyo nilikubaliana na Veronica bila ubishi wowote kwa vile niliona kuwa kutembea kwa...ITAENDELEA