Riwaya: Ufukwe wa Madagascar

Riwaya: Ufukwe wa Madagascar

Huyu vero lazima atakuwa mtego tu huyu.
Jamaa kajiingiza kijinga kweli yani.
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 49

Japokuwa nilikuwa jasusi hatari wa kuogopwa lakini mbele ya mlimbwende yule nilikuwa kama mbwa muoga mbele ya chatu mwenye njaa kali. Veronica akavuta kamba nyembamba ya kivazi chake kiunoni na hapo kivazi kile kikaanguka chini na kumuacha na nguo yake nyekundu nzuri ya ndani huku harufu nzuri ya manukato yake ikinishawishi kuendelea na hatua inayofuata.
Sikuwa na ujasiri wa kupingana zaidi na hizia zangu hivyo taratibu nikaupeleka mkono wangu ndani ya nguo ya ndani ya Veronica na kuanza kuyatomasa makalio yake laini yaliyoshiba minofu. Veronica akashtuka kidogo na kuachia mguno hafifu wakati mkono wangu mwingine ulipokuwa ukiyatomasa matiti yake taratibu. Ndimi zetu zilipoachana ulimi wangu chakaramu nikautembeza taratibu shingoni na hatimaye sikioni mwake na hapo nikasikia sauti yake hafifu mguno wa mahaba. Veronica hakuweza kuvumilia tena hivyo haraka akaishusha chini nguo yangu ya ndani na kuupeleka mkono wake akizichezea malighafi zangu na kunipelekea nianze kuhema ovyo.
Muda mfupi uliofuata tulikuwa kwenye kochi kubwa la sofa lililokuwa pale sebuleni huku kila mmoja akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi. Veronica alikuwa msichana mtundu sana aliyeyamudu vyema mapenzi kiasi cha kunipelekea nijihisi kama mvulana wa sekondari. Pamoja na ufundi wangu wote wa mapenzi lakini kwake bado sikuweza kufua dafu kwani alinidhibiti vyema pale kwenye kochi mimi chini yeye juu huku nikiitazama mijongeo hafifu ya kiuno chake wakati alipokuwa akipanda juu na kushuka chini taratibu.
Tulikuwa kwenye ulimwengu mzito wa mapenzi na dunia ilikuwa kama kisiwa cha raha kwa ajili yetu. Veronica alikuwa amezitendea vyema hisia zangu na raha niliyoipata macho yangu hayakuweza tena kumtazama usoni.
_____
Kwa mara kwa kwanza tangu nitoke jijini Dar es Salaam nilikuwa nimelala usingizi mtamu wa kueleweka. Ilikuwa tayari imetimia saa kumi na moja na robo alfajiri wakati niliposhtuka kutoka usingizi. Veronica alikuwa bado yupo usingizini huku kichwa chake amekilaza kifuani kwangu pale kwenye kochi. Mguu wake mmoja ulikuwa katikati ya mapaja yangu huku mkono wake mmoja ameuzungusha shingoni mwangu na kwa mbali niliweza kusikia sauti hafifu ya mkoromo wake wa uchovu. Penzi zito la Veronica lilikuwa limeamsha ari mpya nafsini mwangu na kupitia ukaribu ule kitu fulani kilikuwa kimeanza kujengeka moyoni mwangu. Kwa namna moja au nyingine Veronica alikuwa ameuteka moyo wangu na sasa nilianza kuona ugumu wa kuwa mbali naye katika harakati zangu.
Taratibu nikayatembeza macho yangu kuipeleleza vizuri sebule ile. Ilikuwa sebule ndogo yenye samani za kawaida kama seti moja ya makochi ya sofa na meza ndogo ya chakula iliyozungukwa na viti vinne iliyokuwa upande wa kushoto kwenye sebule ile. Katikati ya sebule ile kulikuwa na meza nyingine fupi na nzuri ya mbao ya mti wa msonobari iliyofunikwa kwa kitambaa cheupe kizuri chenye maua mekundu ya kufuma kwa mkono. Juu ya meza ile kulikuwa na ua zuri ndani chungu cha udongo mfano wa kibuyu cha asili kilichofinyangwa kwa mkono. Sakafu ya mle ndani ilifunikwa kwa zulia maridadi la rangi za kupendeza na katika kuta safi nyeupe za sebule ile niliziona picha mbili kubwa za kuchora za wanyama wa mwituni na kalenda nzuri zikiwa zimetundikwa. Kupitia zile samani za pale sebuleni haraka nikatambua kuwa kipato cha Veronica kilikuwa cha chini sana ingawa alionekana kuishi maisha ya daraja la kati kwa kadiri alivyoweza.
Upande wa kulia wa ile sebule nikauona mlango uliofunikwa kwa pazia jepesi. Hisia zangu zikanitanabaisha kuwa ule huwenda ulikuwa mlango wa kuelekea chumbani.
Nilipokumbuka kazi ngumu iliyokuwa mbele yangu sikuona sababu ya kuendelea kulala pale sebuleni hivyo taratibu nikamsogeza Veronica pembeni yangu na kisha kuketi na wakati nikifanya vile maumivu makali ya majeraha yangu yakapenya mwilini
Mara moja nilipoyatazama yale majeraha ya mbwa mikononi mwangu nikaanza kuingiwa na wasiwasi wa kuugua maradhi mabaya ya kichaa cha mbwa kwa vile sikuwa na hakika yoyote juu ya afya ya wale mbwa walionishambulia usiku wa jana kule Le Tulip Hôtel Africaine. Tumbo langu lilikuwa dhaifu sana kwa vile usiku wa jana sikuwa nimetia kitu chochote tumboni. Penzi zito la msichana Veronica usiku uliopita lilikuwa limenipelekea nisahau njaa kali iliyokuwa ikinitafuna tumboni. Haraka nikasimama pale kwenye kochi na kuanza kuichunguza ile nyumba kwa utulivu. Nilipomaliza nikagundua kuwa ile nyumba ilikuwa na chumba kimoja cha kulala, sebule, jiko, choo na bafu.
Nililikuta begi langu la mgongoni nililomuachia Veronica asubuhi ya jana kule Havana Club likiwa juu ya meza ndogo iliyokuwa kando ya kitanda chumbani kwake. Haraka nikaingia bafuni kuoga nilipotoka mwili ulikuwa tayari umepata nguvu mpya ambapo nilijiandaa vizuri na kubadili nguo. Kulikuwa na vifaa muhimu vya huduma ya kwanza kwenye begi langu hivyo nilijifanyia tiba muhimu dhidi ya yale majeraha kwa kujichoma sindano ya kuzuia maradhi ya kichaa cha mbwa. Nilipomaliza nikaelekea sebuleni ambapo nilimkuta Veronica akiendelea kuuponda usingizi pale kwenye kochi. Sikumuamsha badala nikaliokota koti langu na kofia na kisha kuelekea bafuni ambapo nilivisafisha vizuri na kuvitia mwilini. Sasa nilikuwa katika muonekano mpya wa suruali nyeusi ya jeans, fulana ya rangi ya kijivu, kofia nyeusi ya kapero, koti jeusi la mvua na buti ngumu za ngozi miguuni.
Nilipotoka bafuni nikaelekea jikoni na baada ya pekuapekua ya hapa na pale nikakuta hotpot yenye chakula kizuri cha ndizi za matoke zilizopikwa kwa ufundi wa hali ya juu huku zikiwa zimechanganywa vizuri na samaki wa ziwa Tanganyika waitwao Mukake. Sikuwa na shaka yoyote kuwa chakula kile kilikuwa kimeandaliwa na Veronica kwa ajili yangu usiku wa jana. Pembeni ya hotpot ile kulikuwa na chupa ya chai ambapo nilipoifungua ndani yake nikaona maziwa fresh. Kile chakula kilikuwa kingi hivyo tungeweza kula mimi na Veronica na kushiba vizuri kabla kila mmoja hajaelekea kwenye harakati zake. Hivyo haraka nikapasha moto kile chakula kwa jiko la gesi na kuchemsha yale maziwa.
Ni wakati nilipokuwa mbioni kumaliza zoezi lile la kuandaa chakula pale niliposhtushwa na mkono laini ukinishika begani. Mara moja nikashtuka na kugeuka nyuma huku moyo wangu ukianza kupoteza utulivu lakini kitendo cha kumuona Veronica kikauyeyusha haraka mshtuko wangu na kusababisha tabasamu jepesi lichomoze usoni mwangu. Veronica alikuwa amenyata taratibu kutoka sebuleni kwenye kochi na hatimaye kusimama nyuma yangu. Ingawa macho yake yalikuwa na kila dalili za uchovu lakini tabasamu lake maridhawa lilirudisha uhai mpya usoni mwake na kumpelekea aonekane mwanamke mzuri na mrembo sana kupita wote niliowahi kuwaona duniani.
Mwanga hafifu wa pambazuko la alfajiri uliokuwa ukipenya taratibu mle ndani ukaniwezesha kuiona hazina matata iliyojificha katika umbo la mlimbwende yule. Veronica alikuwa amesimama nyuma yangu kama alivyozaliwa bila nguo yoyote ya kujisitiri mwilini mwake. Loh! nywele zangu zikasimama wima, moyo wangu ukacheza kidogo kisha mdomo wangu ukaachama huku nikimkodolea macho ya uchu kama fisi aliyeona mfupa.
“Mbona umeamka mapema mpenzi?”. Sauti nyororo ya Veronica ikaziachia huru fikra zangu na kuzirudisha kwenye ufikirivu wa kawaida na hapo nikaunyanyua mkono na kuitazama saa yangu ya mkononi.
“Sasa hivi ni saa kumi na mbili kasoro mpenzi”. Nikaongea kwa sauti hafifu ya kirafiki na hapo nikamuona Veronica akishikwa na mshangao.
“Khe! kumbe kumeshapambazuka!”
“Kazini unaingia saa ngapi?”. Nikamuuliza.
“Saa moja na nusu asubuhi”. Veronica akanijibu kwa sauti hafifu huku akionesha kukerwa na ratiba ile.
“Hata leo Jumapili?”
“Kila siku mpenzi”. Mara moja nikamtazama Veronica na kumhurumia hata hivyo sikuwa na namna na hatimaye nikavunja ukimya.
“Nenda kaanze kujiandaa utakapomaliza chakula kitakuwa tayari mezani”. Maneno yangu yakampelekea Veronica atabasamu kidogo kisha akanitupia macho usoni na macho yetu yalipokutana hisia za mapenzi zikafufuka upya nafsini mwetu.
“Gilbert…”
“Naam Veronica”
“Je tʾaime a la folʾie”. Nakupenda hadi najihisi kuchanganyikiwa.
“Moi aussi”. Mimi pia.
“Sʾil vous plaît, ne me quitte pas mon amour”. Tafadhali usiniache mpenzi wangu.
“Jusquʾ à ce que la mort nous sèpare”. Hadi kifo kitakapotutenganisha. Nikaongea kwa utulivu huku nikiruhusu tabasamu langu kuchanua usoni. Veronica akanisogelea na kunibusu mdomoni kisha taratibu akageuka na kuondoka na hapo nikapata kuona vizuri mtikisiko maridhawa wa umbo lake chakaramu. Kwa mara ya kwanza nikahisi nafsi yangu ilikuwa imepata utajiri mkubwa wa furaha isiyoelezeka.

Ilipofika saa kumi na mbili na nusu Veronica alikuwa tayari amekwishamaliza kujiandaa. Alipotoka chumbani akanikuta nikiwa nimeketi tayari kwenye ile meza ya chakula sebuleni huku taratibu nikipekua kurasa moja baada ya nyingine ya kile kitabu kidogo cha sala nilichokipata kwa yule padri wa kizungu aliyenyongwa kule kwenye kile chumba 403 cha Le Tulip Hôtel Africaine nikijaribu kuchunguza kama ningeweza kuvumbua kitu chochote cha kunisaidia katika harakati zangu. Kurasa ya mwisho ya kitabu kile haikuongeza ziada yoyote katika kile nilichokuwa nikikifahamu hapo awali hivyo nikafunika kile kitabu na kukitia mfukoni huku macho yangu yakiwa kwa Veronica nikijidai kuwa nilikuwa katika harakati za kuombea chakula.
Asubuhi hii Veronica alikuwa amependeza zaidi katika muonekano wa vazi la kitenge cha wax na kilemba kilichofungwa kwa ufundi wa hali ya juu kichwani mwake. Kama ningekuwa promota wa mitindo ya mavazi ya kiafrika sikuwa na shaka yoyote kuwa Veronica angeweza kuniletea ushindi wa kuaminika. Nilipomuuliza juu ya sare zake za kazi akaniambia kuwa angebadili mavazi baada ya kufika kazini kwake.
Wakati tukipata mlo pale mezani kila mmoja akawa amejikita katika kumdadisi mwenzake na hapo nikapata nafasi ya kujua mambo machache kuhusu Veronica ingawa kwa upande wangu aliambulia uongo katika kila swali aliloniuliza.
Saa moja asubuhi kasoro dakika tano tulimaliza kupata kifungua kinywa na kisha kushushia na mvinyo mtamu wa Chateau Lascombes nilioupata kwenye kile chumba cha ofisi ya meneja wa New Paradol Residence usiku wa jana kutoka kwa yule mtu wa mwisho niliyepambana naye. Mvinyo ule ulikuwa umeamsha ari mpya katika miili yetu na kutuchangamsha vizuri kasi cha kupunguza nishai machoni. Veronica akaondoa vyombo na kwenda kuvisuuza jikoni, aliporudi akachukuwa pochi yake ya begani na hapo tukatoka nje ya nyumba ile na kufunga mlango.

Asubuhi ile hali ya hewa ya jiji la Bujumbura ilikuwa imepoa zaidi, manyunyu hafifu ya mvua yalikuwa yakianguka kutoka angani kulikotanda wingu zito la mvua kiasi cha kuweza kuizuia miale ya jua la asubuhi kutua vizuri ardhini. Kufuatia lile jaribio la mapinduzi ya kijeshi jiji la Bujumbura ni kama lilikuwa limelala kwani wakazi wake hawakuwa huru sana kurandaranda mitaani kama ilivyokuwa desturi yao badala yake hofu ilikuwa imetanda kila kona.
Mara baada ya kuyaacha maskani ya Veronica tulishuka kwenye jengo lile la ghorofa la shirika la nyumba la taifa na kushika uelekeo wa ilipo barabara ya Boulevard de Independence. Wakati tukitembea macho yangu yalikuwa makini kutazama kila mahali katika namna ya kuchunguza kuwa hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa akitufuatilia nyendo zetu.
Tulipoyafikia makutano ya barabara ya Boulevard de Independence na barabara ya Avenue de Litalie, Veronica akanishawishi kuwa tuvuke makutano yale na kuendelea kutembea kidogo kwa kuifuata barabara Boulevard de Iʾindependence kwani mbele kidogo tungekuja kukutana na kituo cha maegesho ya teksi nje ya kiwanda cha kuchapisha magazeti. Lilikuwa wazo zuri hivyo nilikubaliana na Veronica bila ubishi wowote kwa vile niliona kuwa kutembea kwa...ITAENDELEA
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 50

...miguu umbali mrefu ingekuwa ni hatari zaidi kwetu sote kwa vile nilivyokuwa nikisakwa na wale watu hatari. Veronica alitaka kujua kuwa nilikuwa nikielekea wapi, nikamdanganya kuwa nilikuwa nikielekea katikati ya jiji kukutana na mfanyabiasha mmoja mkubwa wa pale jijini Bujumbura na bila shaka jibu langu lilikuwa na ushawishi mkubwa kwani hakudiriki kuniuliza tena. Aliponiuliza juu ya yale majeraha ya usiku wa jana mwilini mwangu jibu tayari nilikuwa nalo mdomoni kuwa nilikuwa nimepata ajali ya bodaboda baada ya dereva kukosa umakini barabarani na kwa kumthibitishia nikaapa mbele yake kuwa kamwe sitatumia tena usafiri wa bodaboda hata kama nina haraka ya namna gani.
Nje ya kiwanda cha kuchapa magazeti kando ya barabara ya Boulevard de Iʾindependence tukakuta maegesho ya teksi. Kitu cha ajabu ni kwamba madereva wa teksi wa eneo lile hawakujisumbua kutugombea badala yake nilimuona dereva mmoja wa teksi kijana wa makamo akiangua tabasamu la kibiashara pindi alipomuona Veronica na hapo nikajua kuwa Veronica alikuwa ni mteja wake wa kuaminika. Hatukupoteza muda hivyo tukafungua milango ya nyuma ya teksi ile na kuzama ndani. Muda uleule ile teksi ikaacha maegesho na kuingia barabara huku yule kijana dereva wa teksi akijitia uchangamfu wa kila namna katika kuhakikisha kuwa ananizoea, nafasi ambayo kamwe hakuipata. Kwa kukwepa mizunguko isiyo na ulazima dereva wa teksi akaifuata barabara ya Boulevard de Iʾindependence akiendesha kwa mwendo wa haraka.
Safari ilipoanza tu nikaanza kuchunguza kama tungefungiwa mkia na gari nyingine nyuma yetu lakini hilo halikujitokeza. Baada ya mwendo mrefu wa safari yetu hatimaye tukayafikia makutano ya barabara ya Boulevard de Iʾindependence na barabara ya Boulevard de Iʾuprona. Tulipoyafikia makutano yale dereva akaingia upande wa kushoto akiifuata barabara ya Boulevard de Iʾuprona na hapo kumbukumbu nzuri ya mandhari yale ikanijia akilini mara tu baada ya kuzipata ofisi za ubalozi wa Ufaransa mbele kidogo upande wa kushoto. Haraka nikagundua kuwa tulikuwa tumeingia kwenye ile barabara iliyokuwa ikipakana na Havana Club.
Kulikuwa na magari machache katika barabara ile hivyo mwendo wetu uliongezeka na baada ya muda mfupi wa safari ile teksi ikasimama nje ya Havana Club. Veronica akashuka haraka na kuniaga kwa vile muda wa kuingia kazini kwake ulikuwa tayari umefika. Alipotaka kumlipa dereva wa teksi nikamsihi aache na kumuahidi kuwa ni mimi ndiyo ningemlipa. Hivyo tukaagana na Veronica kwa makubaliano kuwa tungeonana usiku kule nyumbani kama ilivyo ada na hapo dereva wa ile teksi akatia moto gari tukielekea katikati ya jiji la Bujumbura. Hakukuwa na gari lililokuwa likitufungia mkia nyuma yetu hivyo bado mambo yalikuwa shwari.
_____
“Un lideur de Coup d'état militaire du pay de Burundi géneral Godfroid Niyombare et ses compagno is sont arrêtés”. Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi nchini Burundi generali Godfroid Niyombare na washirika wake wakamatwa.
Zilikuwa habari za kushtua zilizoamsha hisia mpya moyoni mwangu. Mtangazaji wa kituo kimoja maarufu cha redio cha jijini Bujumbura alikuwa akimalizia kutangaza taarifa ile wakati dereva wa teksi alipovunja ukimya ulioshamiri mle ndani ya teksi tangu kuanza kwa safari yetu kwa kuwasha redio ya gari. Mara moja nilipomtazama dereva yule nikagundua kuwa alikuwa hajafurahishwa kabisa na taarifa ile kwa namna uso wake ulivyobadilika na hapo nikajifunza kuwa raia wengi wa nchini Burundi huwenda walikuwa wamefurahishwa na mapinduzi yale ya kijeshi hivyo kukamatwa kwa wahaini wale wa jaribio la mapinduzi ya kijeshi kulikuwa kumewavunja moyo sana wa kusimikwa kwa utawara mpya kama dereva yule alivyoonesha hisia zake za waziwazi.
Kwa kukwepa kutengeneza vielelezo rahisi kwa mtu yeyote aliyekuwa akinipeleleza nyendo zangu nilikuwa nimeamua kukodi teksi nyingine mara baada ya yule dereva wa teksi wa Veronica kumtaka anishushie katikati ya jiji la Bujumbura nje ya ofisi kuu za shirika la posta. Dereva wa ile teksi alipotokomea nikavuka barabara na kutembea hadi mtaa wa tatu ambapo nilikodi teksi nyingine na kumtaka dereva wa teksi ile mwanaume mrefu wa asili ya kitutsi mwenye umri kati ya miaka thelathini na tano hadi arobaini anipeleke eneo linaloitwa Bubanza.
Wakati nilipoinua mkono na kuitazama saa yangu ya mkononi nikagundua kuwa muda wa saa moja tayari ulikwishapita tangu kuanza kwa safari yetu ya kuelekea eneo la kaskazini ya jiji la Bujumbura. Sehemu kubwa ya nchi ya Burundi ilikuwa imemezwa na ukimya wa hofu. Wanajeshi watiifu wa serikali ya Rais Pierre Nkurunziza sasa walikuwa wametanda kila kona kuanzia mitaa ya jiji la Bujumbura hadi kwenye barabara zinazokwenda mbali na miji. Vizuizi vya askari wa barabarani vilikuwa vimeongezwa na upekuzi wa magari na watu waliokuwa wakitoka na kuingia mijini ulikuwa ukifanyika.
Mazingira hayakuwa rafiki kwa mtu yeyote mgeni wa nchi ya Burundi hivyo kwa kukwepa kusababisha migogoro hatari yenye upotevu wa muda wenye kugharimu uhai wangu kwenye vizuizi vya barabarani nikaamua kutumia kitambulisho changu bandia kinachonitambulisha kwa jina Céléstine Desire Bizimana kama kada mwandamizi wa chama kilichopo madarakani nchini Burundi cha CNDD-FDD-Conseil National pour la Défense de la Démocratié-Forces de Defense de la Démocratié. Hivyo katika kila kizuizi tulichosimamishwa askari walipoona kitambulisho changu hawakunitilia mashaka yoyote badala yake walituruhusu tuendelee na safari katika nyuso za kiungwana.
Barabara ya kuelekea eneo la Bubanza lililopo maili nyingi kaskazini mwa jiji la Bujumbura ilikuwa mbaya mno isiyokuwa na lami yenye mashimo na makorongo karibu kila mahali. Kufuatia mvua za masika zilizokuwa zikiendelea kunyesha baadhi ya madaraja madogo madogo yalikuwa yamesombwa na mafuriko. Hivyo dereva yule wa teksi alijikuta akitumia akili na nguvu za ziada katika kufanikisha safari ile kwenye barabara mbovu ya kidongo chekundu iliyokuwa ikikatisha katikati ya misitu mizito. Njiani katika baadhi ya maeneo tulikutana na makundi ya raia wa Burundi wengi wao wakiwa wanawake na watoto wakiwa na mizigo yao vichwani huku wakitembea kwa hofu kandokando ya barabara ile kukimbia mapigano katika miji yao na kwenda kutafuta hifadhi ya kikimbizi katika maeneo yenye usalama nafuu mashariki mwa D.R. Congo.
Niliwatazama watu wale na kujikuta nikiwaonea huruma sana kwa namna walivyokuwa wakitaabika kwa kuisaka amani kwa udi na uvumba. Ilikuwa taswira ya kusononesha mno kiasi cha kushawishika kutaka kumwambia dereva wa ile teksi asimamishe gari ili tumchukue mama mmoja mwenye watoto sita wadogo waliodhoofika afya baada ya safari ndefu ya kutembea kwa miguu bila chakula wala maji. Hata hivyo niliachana na mpango ule baada ya kuhisi kuwa mara baada ya kumuona mama yule na watoto wake tukiwasaidia wakimbizi wengine wangetaka nao wasaidiwe jambo ambalo lisingewezekana na huwenda lingeamsha chuki na hasira dhidi yetu.
_____

Baada ya kitambo kirefu cha safari hatimaye tukafika sehemu yenye njia panda. Mara moja tulipoanza kukaribia eneo lilie dereva wa ile teksi akaanza kupunguza mwendo na hapo nikayahamisha macho yangu kutoka dirishani na kutazama kule mbele ya gari. Nilichokiona kwenye ile njia panda kikapelekea baridi nyepesi isambae moyoni mwangu. Maiti nyingi za watu waliouwawa muda mfupi uliopita zilikuwa zimezagaa eneo lile huku wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto. Taratibu nikashusha kioo cha dirishani na kuchungulia nje na hapo simanzi na hasira vikanishika.
Ulikuwa ni ukatili wa aina yake kuwahi kufanyiwa binadamu. Watu wale walikuwa wameuwawa kwa kupigwa mapanga kichwani. Maiti za wanawake zilikuwa uchi wa mnyama katika namna ya kuaminika kuwa walikuwa wamebakwa na wavamizi kabla ya kuuwawa. Baadhi ya zile maiti zilikuwa zimezagaa barabarani. Dereva wa ile teksi akawa kama anayepunguza mwendo ili asimame kisha tushuke tukasaidiane kuziondoa zile maiti na kuziweka kando ili tuweze kupita.
Lilikuwa wazo zuri kwa vile hatukuwa na sehemu nyingine ya kupita lakini moyo wangu ukasita kidogo baada ya kulichunguza vizuri lile eneo. Nafsi yangu ikanitanabaisha kuwa hatukuwa sehemu salama. Mbele yetu kulikuwa na barabara nyingine iliyokuwa ikikatisha na eneo lile lilikuwa limepakana na msitu mzito wenye miti mirefu iliyozingirwa na vichaka vinavyotisha. Nilipotazama vizuri kule mbele kwenye makutano ya zile barabara nikaona bango dogo jeupe lenye mshale mweusi unaoelekeza upande wa kulia juu yake kumeandikwa Bubanza 20KM Est.
Dereva wa ile teksi akionekana dhahiri kuingiwa na hofu akageuka na kunitazama kama anayetaka nimruhusu asimame hata hivyo nikakataa kwa kutingisha kichwa hali iliyosababisha mshangao usioelezeka usoni mwake. Nilifahamu kuwa lile lilikuwa jambo gumu kwake kwani kwa vyovyote vile ili kupita eneo lile yule dereva angelazimika kuzikanyaga zile maiti kwa magurudumu ya gari katika baadhi ya sehemu. Hata hivyo hapakuwa na namna nyingine kwani wale watu tayari walikuwa wafu hivyo usalama wetu ulikuwa muhimu zaidi kwa kuzingatia kuwa wafu hawakuwa na cha kupoteza.
Huku jasho likianza kumtoka dereva wa ile teksi akatia gari moto na kuanza kuzikanyaga zile maiti za wafu mbele yetu na wakati akifanya vile mimi nikawa makini kulichunguza lile eneo. Lilikuwa eneo linalotisha na hapakuwa na dalili zozote za makazi ya watu.
Tulikuwa mbioni kabisa kuifikia ile njia panda wakati nilipogeuka nyuma na kuona kikundi cha wanaume kikichomoza kutoka msituni kando ya ile barabara na kuanza kutufuata huku mikononi wakiwa na silaha za jadi na bunduki. Muda uleule mara tukaanza kushambuliwa kwa risasi. Kuona vile nikamuhimiza yule dereva wa teksi aongeze mwendo na hapo nikachomoa bastola yangu kutoka kwenye mfuko wa koti na kuanza kujibu mashambulizi baada ya kufungua mlango wa nyuma na kujilaza chini.
Ingawa watu wale walijitahidi kwa kila namna kutuzuia huku wakilishambulia gari letu lakini hawakufanikiwa kwani niliwadondosha mmoja baada ya mwingine kwa risasi zangu zenye shabaha makini huku yule dereva wa teksi akizidi kutia moto gari. Muda mfupi tukawa tumeyafikia yale makutano ya barabarana hapo yule dereva wa teksi akaingia upande wa kulia akitimua mbio zisizo za kawaida. Nikaendelea kuwatazama wale watu waliosalia nyuma yetu wakiendelea kutufukuza hata hivyo tuliendelea kuwaacha kwa umbali mrefu na hatimaye tukawapotea kabisa tukiendelea kuchanja mbuga kwenye barabara nyembamba ya vumbi iliyokuwa ikikatisha katikati ya misitu minene.
Kulikuwa na matundu machache ya risasi nyuma ya gari na kwenye kioo cha nyuma dirishani zaidi ya pale hapakuwa na athari nyingine katika uvamizi ule. Wakati tukiendelea na safari mara kwa mara nilimtazama yule dereva wa teksi na kumuona ni kama aliyekuwa akijuta kuambatana na mimi. Sasa alikuwa akinitazama kwa woga wa hali ya juu kupitia kioo cha mbele cha ndani ya gari na macho yetu yalipokutana niliona namna hofu ilivyolipuka usoni mwake. Bila shaka alikuwa ameshtushwa na kitendo cha mimi kumiliki silaha na kuitumia kwa ufundi wa hali ya juu.
_____

Mara baada ya kuvuka daraja la mto mkubwa uliokatisha katikati ya msitu mkubwa tukaingia upande wa kushoto. Hatukufika mbali sana mara nikamuona dereva wa ile teksi akipunguza mwendo na kabla sijamuuliza kuwa alikuwa akifanya vile kwa sababu gani akawahi kugeuka nyuma na kuniambia.
“Puis je aller pour un court appel sʾil vous plait”. Naomba niende nikajisaidie kidogo tafadhali.
“D'accord”. Sawa. Nikamruhusu huku nikimtazama yule dereva kwa mashaka kidogo. Yule Dereva wa teksi akaegesha gari kando ya ile barabara na kushuka. Mara tu aliposhuka akageuka na kunikata jicho na namna ya utazamaji wake ukanitia mashaka kidogo. Waswahili husema moyo wa binadamu ni kama kichaka kizito kwani nilipenda kufahamu kuwa mtu yule alikuwa akiniwazia nini kichwani mwake na kama alikuwa amabanwa kweli na haja au alikuwa akifanya hila. Majibu sikuyapata kwa vile Mungu alikuwa ameninyima binadamu uwezo huo hivyo nafsi yangu ikabaki imetawaliwa na hisia tu na hapo nikabaki nimeketi nyuma ya ile teksi huku nikimtazama yule dereva wa teksi namna alivyokuwa akizitupa hatua zake kwa utulivu kuelekea kichakani kando ya ile barabara huku mara kwa mara akigeuka nyuma na kunitazama. Hatiamye yule dereva wa teksi akapotelea kwenye kichaka kikubwa kilichokuwa kando ya ile barabara na hapo nikahisi kuwa huwenda alikuwa ameshikwa na tumbo la kuhara kwa namna alivyokuwa akizidi kuharakisha na kuzipangua nyasi ndefu akizidi kutokomea ndani ya kile kichaka. Ingawa sikupenda tusimame barabarani sehemu ya wazi kama ile lakini niliheshimu vizuri matatizo ya binadamu hivyo nikabaki garini nimeegemea siti huku nikiendelea kutazama nyuma ya ile barabara kupitia kioo cha ndani cha mbele kwa dereva huku mawazo mengi yakipita kichwani mwangu.
_____

Kama siyo tabia mbaya ya kupenda kula ovyo vyakula vya barabarani pasipo kuzingatia usafi wa upishi basi maradhi ya tumbo la kuhara huweza pia kusababishwa na hofu ambayo binadamu hukutana nayo. Dereva wa teksi huwenda alikuwa ameshikwa na hofu baada ya yale mapambano dhidi ya wale wavamizi wa kule barabarani tulipotoka. Nikajikuta nikiwaza hivyo baada ya kuyatuliza tena mawazo yangu mle ndani ya gari.
Lakini sasa wasiwasi tayari ulikuwa umeanza kuniingia baada ya kuitazama saa yangu ya mkononi na kugundua kuwa dakika chache zilikuwa zimesalia kabla ya muda wa nusu saa kutimia tangu yule dereva wa teksi alipoingia kule kichakani. Muda wa nusu saa kwa mtu aliyechafukwa na tumbo la kuhara kichakani nikaanza kuuona kuwa ulikuwa ni mwingi sana hivyo nikaanza kuingiwa na hofu kiasi cha kuanza kushawishika kuwa nishuke kwenye ile teksi na kuelekekea kwenye kile kichaka ili nikamsihi yule dereva wa teksi aharakishe haja yake ili tuendelee na safari kwa vile nilianza kuhisi kuwa nilikuwa nikielekea kuchelewa kule niendako. Hata hivyo baada ya kujishauri sana hatimaye nikaamua kutoa msamaha wa dakika tano za nyongeza huku nikiamini kuwa muda wowote kuanzia pale yule dereva wa teksi angejitokeza kichakani huku uso wake ukiwa na faraja baada ya kuutua mzigo mzito.
Hata hivyo wakati nikiendelea kusubiri mle ndani ya teksi nikaona kuwa siyo vibaya kulichunguza lile gari kwa kuyatembeza macho yangu hapa na pale. Kwa kufanya vile mara moja nikagundua kuwa funguo za gari hazikuwepo kwenye swichi yake chini ya usukani. Hivyo kwa tafsiri nyingine ni kuwa dereva wa ile teksi alikuwa amendoka na funguo za gari wakati ule aliposhuka na kwenda kujisaidia kichakani. Dereva wa ile teksi alikuwa na maana gani kuondoka na funguo za gari wakati alikusudia kutumia muda mfupi tu kamaliza haja yake kichakani?. Au huwenda alikuwa amehofia kuwa kuacha funguo za gari mle ndani kungeweza kunipa fursa nzuri ya kutokomea na gari lake wakati yeye akiwa kichakani anapambana na haja yake?. Majibu sikuyapata hivyo wasiwasi sasa ulikuwa dhihiri nafsini mwangu.
Hatimaye sikuona sababu ya kuendelea kusubiri zaidi mle ndani ya ile teksi hivyo nikafungua mlango na kushuka huku mkono wangu wa kushoto ukiwa umeikamata vyema bastola ndani ya mfuko wa koti langu. Kwa sekunde kadhaa nikasimama pembezoni ya ile barabara nikifanya tathmini dhidi ya mazingira yale na kwa kufanya vile hisia zangu zikanitanabaisha kuwa tulikuwa kwenye eneo la msitu mzito wenye miti mirefu na mikubwa iliyokula chumvi nyingi katika sehemu isiyokuwa na makazi ya watu. Nilipoyatega kwa makini masikio yangu kwa mbali niliweza kuzisikia sauti za tetere zikihanikiza juu ya miti iliyokuwa eneo lile.
Hatimaye nikaanza kutembea taratibu kukifuata kile kichaka kilichokuwa kando ya ile barabara alichokuwa amepotelea yule dereva wa teksi. Mara tu nilipoingia kwenye kile kichaka mashaka yakazidi kuniingia baada ya kutomuona yule dereva na badala yake nikauona uchochoro mwembamba wa nyasi zilizolala chini muda mfupi uliopita baada ya mtu kupita eneo lile. Sikuwa na shaka yoyote kuwa yule dereva wa teksi ndiye ambaye angekuwa amepita eneo lile na kuendelea kule mbele. Kwanini yule dereva wa teksi aliamua kwenda mbali zaidi na eneo lile kama kweli alikuwa ameshikwa na haja ya ghafla?. Nikajiuliza tena bila kupata majibu.
Hata hivyo nikaamua kuanza kuufuata ule uchochoro wa nyasi zilizokanyagwa chini ya miti mikubwa na mirefu ya mivule huku nikilichunguza lile eneo kwa makini na tayari kukabiliana na hatari yoyote ambayo ingejitokeza mbeleni. Bado sikuona dalili za uwepo wa mtu yeyote eneo lile.
Umbali niliotembea kwa miguu nikiufuata ule uchochoro wa nyasi zilizolala kwa kukanyagwa ulikuwa zaidi ya mita mia mbili na ule uchochoro ulionekana kuzidi kusonga mbele zaidi hali iliyonitia mashaka. Nilipozidi kuwaza sikuona sababu yoyote ya mtu aliyebanwa na haja ya ghafla iwe ndogo au kubwa kutembea umbali wa zaidi ya mita mia mbili msituni eti kutafuta sehemu nzuri ya kujisaidia. Hivyo haraka nikaanza kuhisi hatari ingawa niliendelea kujipa moyo kwa kumuita yule dereva wa teksi pasipo mafanikio yoyote. Mwishowe nikakata tamaa lakini kabla sijaamua kurudi kule barabarani ilipoegeshwa ile teksi nikataka kujipa hakika zaidi na uchunguzi wangu. Hivyo nikachagua mti mmoja mrefu wenye ukubwa wa wastani na kuanza kuukwea.
Muda mfupi baadaye nikawa nimemaliza kukwea na kufika juu ya ule mti na hapo nikapata nafasi nzuri ya kuona mandhari ya eneo lile. Kwa mbali niliweza kuona milima na mabonde, vichuguu, misitu na nyasi ndefu zinazoweza kuwaficha wanyama hatari wa porini kama simba, mbwa mwitu, chui au fisi. Lakini bado hapakuwa na dalili zozote za uwepo wa binadamu eneo lile na jambo lile lilinishangaza sana. Nikiwa bado pale juu ya mti nikaendelea kulichunguza lile eneo la msitu kwa utulivu huku nikitarajia kumuona yule dereva wa teksi katikati ya kichaka au nyasi ndefu akimalizia haja yake lakini hilo halikutokea badala yake nikaishia kumuita yule dereva kwa kila namna hali iliyowapelekea ndege wa porini wanisikilize kwa makini na hatimaye kunicheka. Mwishowe nikaona kuwa nilikuwa nikipoteza muda wangu bure hivyo taratibu na kwa tahadhari ya hali juu nikashuka chini ya ule mti na kurudi kule barabarani ilipoegeshwa ile teksi.
Majira ya saa yangu ya mkononi yakanitahadharisha kuwa muda haukuwa rafiki sana kwangu hivyo nilipoifikia ile teksi nikafungua mlango wa dereva na kuingia ndani. Funguo za gari hazikuwepo mahala pake lakini kwa kuwa nilikuwa na weledi mzuri katika ufundi wa magari nikabomoa swichi ya gari na kutafuta nyaya fulani mbili ambapo nilipozigusanisha kidogo mchuma ukatoa majibu chanya. Kwa dakika chache nikaiacha injini ya ile gari ikiunguruma kwa hasira huku nikipiga honi mfululizo ambazo zingeweza kumshtua yule dereva wa teksi kokote alikokuwa karibu na eneo lile kichakani. Yule dereva wa teksi hakujitokeza na jambo lile likazidi kunichanganya akilini. Mwishowe sikuona sababu ya kuendelea kusubiri zaidi hivyo nikatia moto gari na kuingia barabarani nikitoweka mbali na eneo lile katikati ya barabara iliyopakana na misitu mizito yenye milima na mabonde huku mawazo mengi yakipita kichwani mwangu...ITAENDELEA
 
RIWAYA: UFUKWE WA MADAGASCAR
SEHEMU: 51
_____

Kanisa la Katoliki la Diocèse de Bubanza lilikuwa kando kidogo ya mji mdogo wa Bubanza kaskazini mwa jiji la Bujumbura, kilometa chache upande wa kulia baada ya kuachana na barabara ya vumbi inayoelekea mto Ruzizi ulipo mpaka wa nchi ya Burundi na D.R.Congo upande wa magharibi. Tofauti na jiji la Bujumbura mji mdogo wa Bubanza haukuwa na pilika nyingi za watu magari na shughuli nyingi za binadamu. Barabara zake zilikuwa duni sana, huduma za kijamii kama maji safi, hospitali za kisasa, shule zilikuwa zinahesabika. Sikuwa na shaka yoyote kuwa taarifa za jaribio la mapinduzi ya kijeshi nchini Burundi zilikuwa tayari zimewafikia wakazi wa mji ule na kupelekea mashaka dhidi ya usalama wao.
Baada ya ulizauliza ya hapa na pale kwa wenyeji wa mji ule hatimaye nikalifikia kanisa la katoliki jibo la Bubanza kando kidogo ya mji ule. Nikafurahi kukuta misa ilikuwa ikiendelea. Nje ya kanisa lile kulikuwa na magari machache ambayo nilipoyachunguza vizuri nikagundua kuwa yalikuwa ni mali ya kanisa lile kutokana na maelezo yaliyokuwa yameandikwa ubavuni. Miongoni mwa magari yale nikaliona gari la Askofu mkuu wa jimbo, gari la padri na lori moja la hospitali ya Catholic Mission de Bubanza. Magari yale yakiwa yameegeshwa katika sehemu maalumu ya kuegesha magari mbele ya minara mikubwa ya masanamu.
Taratibu nikaegesha ile teksi na kushuka huku nikiyatembeza macho yangu kulichunguza vizuri eneo lile. Ukubwa wa kanisa ungeweza kumeza watu elfu moja bila usumbufu wowote. Upande wa kushoto nilipochunguza nikaona kuwa lile kanisa lilikuwa limepakana na hospitali ndogo ya mission ya kikatoliki ambayo bila shaka ndiyo ilikuwa tegemeo kubwa la wakazi wa kitongoji kile. Upande wa kulia kanisa lile lilipakana na ofisi za makasisi na watawa wa kikatoliki pamoja na jengo la kituo kidogo cha kanisa cha kulelea watoto yatima. Upande wa nyuma ya kanisa nisingeweza kuona chochote ingawa mandhari yake yalipambwa kwa miti ya kupandwa. Kwa kuwa misa ilikuwa ikiendelea sikumuona mtu yeyote nje ya kanisa lile hivyo taratibu nikaanza kuzitupa hatua zangu kuelekea ndani ya kanisa lile huku macho yangu yakijitahidi kusoma maelezo yalikuwa sehemu ya juu ya mlango wa kuingilia kanisani yanayosomeka Cathédrale Christ Roi Diocèse de Bubanza, yaani Kanisa la Kristo Mfalme Dayosisi ya Bubanza.

Nilipofika karibu na mlango wa kuingilia mle kanisani taratibu nikaanza kupanda ngazi kuelekea kwenye baraza kubwa ya lile kanisa. Muda mfupi uliofuata nikawa nimemaliza kupanda zile ngazi huku nikizipita nguzo mbili za sanamu za mitume wa Kristo na bikira Maria huku nikiutathmini muonekano wangu kama ungeshabihiana na baadhi ya waumini waliokuwa mle ndani ya kanisa. Anga lilikuwa limeshaanza kufunikwa tena na wingu zito kuashiria kuwa mvua ingenyesha.
Hatua zangu madhubuti wakati nikiingia mle kanisani zikatengeneza kishindo hafifu na hapo nyuso za waumini waoga zikageuka na kunitazama kwa woga kama shetani aliyeingia kanisani kuungama dhambi zake. Sikupenda kuvuta macho ya watu wala kuonekana kivutio hivyo mara moja nikapunguza mwendo nikitembea taratibu huku nikiyatembeza macho yangu huku na kule kuzitazama nyuso za watu wa mle ndani na vilevile nikitafuta sehemu nzuri ya kukaa mle ndani ambapo macho yangu yangeweza kufanya tathmini vizuri.
Hatimaye nikaenda kuketi mwisho wa benchi la tatu kutoka nyuma ya kanisa sehemu walipokuwa wameketi wanaume wawili wazee na kijana mdogo wa shule ya msingi. Wakati nikiketi baadhi ya watu wakageuka nyuma na kunitazama kidogo kisha wakayarudisha macho yao kutazama mbele kwa muhubiri ingawa wapo baadhi ya watu waliendelea kunitazama bila haya yoyote. Sikumbuki mara ya mwisho kuingia kanisani ilikuwa ni lini ingawa tathmini yangu ilinitanabaisha kuwa huwenda misa ile ilikuwa na waumini wengi zaidi kushinda misa nyingine zilizotangulia asubuhi.
Lilikuwa kanisa kubwa lenye paa refu na imara. Ukutani kulikuwa na madirisha makubwa marefu ya vioo vyenye mchanganyiko wa rangi ya njano, nyeupe na kijani na katikati ya madirisha yale kulichorwa picha ya bikira Maria akiwa amempakata mtoto Yesu. Labda niseme zilikuwa ni picha za kufikirika kwani teknolojia ya upigaji na utengenezaji wa picha ni dhahiri haikuwepo nyakati za Yesu alipokuwa hapa duniani. Kila baada ya madirisha mawili ya kanisa lile kulikuwa na nguzo ndefu zilizotoka chini hadi juu kushikilia paa la kanisa lile na nguzo zile zilikuwa zimechongwa kwa ustadi sanamu za mfano wa wanafunzi kumi na wawili wa Yesu huku wakiwa wamemwinamia Yesu miguuni kama ishara ya utukufu. Juu ya sanamu zile kulikuwa na msalaba mkubwa wa kuchongwa uliotiwa nakshi za kupendeza. Mbele ya kanisa lile ilipo altale upande wa kushoto na kulia kulikuwa na vyumba vya kuungama dhambi na juu ya vyumba vile kulikuwa na ngazi ndefu za kuelekea sehemu ya juu ya kanisa lile zilikofungwa kengele kubwa mbili za kanisa.
Macho yangu yakatulia kutazama mishumaa mikubwa iliyowekwa kwenye vikombe maalum vya shaba vilivyokuwa ukutani ikiendelea kuangaza mle kanisani. Nilipochunguza vizuri mle ndani nikagundua kuwa idadi ya watoto ilikuwa ndogo sana ukilinganisha na idadi ya wanaume na wanawake, wazee kwa vijana.
Askofu wa jimbo alikuwa mbele ya kanisa na wasaidizi wake wakishirikiana kikamilifu kuendesha misa ile na wote walikuwa katika mavazi ya kanzu nyeupe zenye misalaba myekundu katikati huku baadhi ya wale wasaidizi wakiwa wameshika chetezo kufukiza ubani. Lugha kuu iliyokuwa ikitumika kuendesha ibada ile ilikuwa ni lugha ya kirundi kilichochanganyika na kifaransa na hapo nikafanikiwa kuokota neno moja moja la kifaransa ambapo nilipoyaunganisha nikapata maana iliyozifungua kidogo fikra zangu. Mahubiri yale yalikuwa yamelenga katika kutilia mkazo suala la amani nchini Burundi huku mhubiri akionekana kukemea vitendo vya uvunjifu wa amani na machafuko ya kisiasa yaliyokuwa yakiendelea nchini mle huku akitumia mifano mingi kutoka kwenye kitabu chake cha kuongozea misa. Waumini walionekana kumkodolea macho mhubiri yule huku wakimsikiliza kwa makini na kutafakari.
Mimi sikuwa miongoni mwa watu waliofika pale kanisani kushiriki misa ingawa suala la kumuabudu na kumcha Mungu ni jukumu la kila mwanadamu. Hivyo wakati misa ile ikiendelea fikra nyingi zikawa zikipita kichwani mwangu nikiwaza juu ya Padri Aloysius Kanyameza ambaye kupitia kile kitabu kidogo cha sala nilichokikuta mfukoni mwake nilikuwa na kila sababu ya kuamini kuwa alikuwa miongoni mwa makasisi wa kanisa lile. Niliamini kuwa kuonana na Padri Aloysius Kunyameza kungeweza kunifungulia njia katika upelelezi wangu na hatimaye kumfikia mtu aliyefahamika kama Pierre Okongo ambaye ni yeye ndiye angeweza kutegua kitendawili cha nani aliyehusika na kifo cha yule Padri wa kizungu aliyenyongwa ndani ya kile chumba 403 cha Le Tulip Hôtel Africaine.
Kulikuwa na watu wachache waliokuwa wakiendelea kunitazama mle kanisani na kwa kuwa sikupendezwa na tukio lile nikayapeleka macho yangu kuwatazama watu wale na macho yetu yalipokutana wakaona aibu na kutazama kwingine huku dhahiri wakionekana kusubiri kwa hamu misa ile ifike ukingoni ili wakaendelee na shughuli zao. Kwa kufanya vile nikafanikiwa kuyafukuza macho ya watu wengi na wale wachache waliokomaa kunikodolea macho nikawapuuza kwa kutoa kile kitabu kidogo cha sala na kuanza kukipitia ingawa fikra zangu kamwe hazikuwa pale kitabuni. Mawazo juu ya yule dereva wa teksi aliyetoweka katika mazingira ya kutatanisha kule msituni njiani bado yalikuwa yakiitafuna nafsi yangu.

_____

Sikuwa na shaka yoyote kuwa misa ile ilikuwa ikielekea ukingoni na wakati yule askofu akiendelea kuhubiri mimi macho yangu yalikuwa kitabuni kuununua muda huku nikijiuliza kama kweli nasaha zile zilikuwa zikiwaingia vizuri wale waumini akilini mwao au lah!. Hatimaye mawazo yangu yakahamia kwa Hidaya huku nikijaribu kufikiria namna atakavyosumbuliwa na maafisa usalama wa nchini Burundi mara baada ya lile gari nililokuwa nikilitumia la ubalozi wa Tanzania kuonekana katika maegesho ya viunga vya Le Tulip Hôtel Africaine.
Sauti ya muungurumo wa gari lililokuja ghafla na kuegesha nje ya lile kanisa ikazirudisha fikra zangu mle ndani ya kanisa na hapo taratibu nikafunika kile kitabu kidogo cha sala mikononi mwangu na kugeuka nyuma nikitazama pale mlangoni. Kitambo kifupi cha ukimya kikapita na wakati huo nikashtukia kuwa watu wengi mle kanisani nao walikuwa wamegeuka nyuma kama mimi na kutazama kwenye ule mlango wa kuingilia mle kanisani huku wakionesha hamasa ya kutaka kufahamu ni nani ambaye angeingia mle kanisani baada ya muungurumo wa lile gari nje kufika ukomo.
Muda mfupi uliofuata mara watu watatu wakaingia mle kanisani na muonekana wao ukanipelekea nishikwe kidogo na mduwao. Wanaume wale watatu walikuwa wamevaa suti nadhifu nyeusi na miwani myeusi machoni mwao. Miili yao ilikuwa imejengekea vyema kwa mazoezi ya nguvu na lishe ya uhakika. Urefu wao ulishabihiana na walikuwa weusi mno labda ningeweza kuwaita wajaluo kama siyo wenye asili ya Sudani ya kusini. Askofu wa kanisa lile akasita kidogo kuendelea na mahubiri baada ya kuwaona wale watu wakiingia mle ndani tukio lile likapelekea kanisa zima ligeuke na kutazama nyuma pale mlangoni kabla ya askofu yule kuendelea.
Umahiri wangu wa kuzisoma vizuri sura za watu na tabia zao ukanitanabaisha kuwa wale watu hawakuwa waumini wa kawaida kwani kwa sekunde kadhaa wakasimama pale mlangoni wakiyatembeza macho mle ndani kisha nikamuona mmoja wao akitembea kwa utulivu katikati ya kanisa kuelekea mbele ambapo alitafuta sehemu na kuketi upande wa kulia. Mtu wa pili akatembea kwa utulivu huku akitafuta sehemu ya kuketi upande wa kushoto katikati ya lile kanisa. Yule mtu mmoja aliyesalia akayatembeza macho yake kutazama pale nyuma nilipoketi kabla ya kuanza kupiga hatua zake taratibu na hatimaye kuja kuketi nyuma yangu hali iliyonishawishi nitake kugeuka nyuma na kumtazama ingawa sikuthubutu kufanya hivyo. Sasa macho yangu yalikuwa makini kuwatazama wale wanaume wawili walioketi kule mbele ya kanisa na mara moja nikatambua kuwa kila mmoja alikuwa akijishughulisha katika kuzikagua kwa siri nyuso za watu waliokuwa mle ndani.
Nilipoendelea kuwachunguza vizuri wale watu taratibu kumbukumbu zikanijia akilini na kupelekea kijasho chepesi kuanza kunitoka maungoni. Haraka nikawa nimemkumbuka mtu mmoja miongoni mwao kuwa alikuwa miongoni mwa wale watu wawili niliopishana nao wakati nikitoka kule Le Tulip Hôtel Africaine. Loh! harufu ya matata ikaanza kunijia akilini kuwa huwenda mlengwa wa ziara ile ya kushtukiza nilikuwa mimi na hapo nikaanza kujiuliza kuwa kama mimi ndiyo ningekuwa mlengwa wa ziara ile wale watu walijuaje kuwa mimi niko pale tena nikiwa ndiyo kwanza nimefika pale kanisani muda mfupi tu uliyopita?. Jibu sikulipata ingawa sasa nilikuwa makini zaidi na nyendo zangu. Hata hivyo bado nikahisi kuwa wale watu hawakuwa wameniona.
Wakati nikiwa katika harakati za kuamua nini cha kufanya mara misa ile ikafikia ukomo na hapo tukaingia kwenye kipindi cha matoleo baada ya sala fupi kufanyika. Utaratibu wa matoleo ya sadaka ukatulazimu sote mle ndani tusimame na kuanza kupanga mistari miwili minyoofu katikati ya kanisa kuelekea mbele vilipokuwa vyombo vya matoleo. Nikasubiri watu wote wanyanyuke kwenye lile benchi nililoketi kisha nikaunga mstari huku yule mtu nyuma yangu akionesha kunitegea kwa hila ili nitangulie.
Baada ya mgogoro mfupi wa nafsi yangu hatimaye nikaona kuwa nisingefanikiwa kufanya hila kwa kuwa foleni ile ilifuata utaratibu maalum kuwa watu wa benchi la mbele wangesimama na kuelekea mbele kutoa sadaka zao na kufuatiwa na watu benchi la nyuma. Hivyo kabla ya yule mtu nyuma yangu mimi ndiyo ningestahili kutangulia vinginevyo ningeonekana mtu wa ajabu. Bila kusita nikasimama na kuunga mstari huku macho yangu yakiwa makini kuwatazama wale watu kule mbele. Wale watu hawakuunga mstari kwenda kule mbele kutoa sadaka kama waumini wengine walivyofanya badala yake wakasimama wakitazamana kama wanaopeana ishara fulani kisha nikaona wakigeuka na kutazama pale nilipokuwa na tukio lile likanipelekea nishtukie kuwa wale watu walikuwa wameniona kwani haraka macho yetu yalipogongana wakayakwepesha macho yao pembeni na kutazamana huku wakijitia kuzirekebisha vizuri tai zao shingoni.
Wakati nikifika katikati ya kanisa na kuunga ule mstari wa matoleo taratibu nikauingiza mkono kuipapasa bastola yangu kwenye mfuko wa koti langu na kitendo cha kuikuta bastola yangu ikiwa imetulia vyema mahala pake kikanifurahisha. Nilipogeuka kutazama nyuma macho yangu yakakutana na macho ya yule mtu aliyekuwa ameketi nyuma yangu muda mfupi uliopita yakiwa yamejificha nyuma ya vioo vyeusi vya miwani yake. Yule mtu akatabasamu kinafiki huku mkono wake mmoja tayari ukiwa umezama kwenye mfuko wa koti lake la suti na hapo nikajua nini maana ya tukio lile. Sikuwa na shaka kuwa yule mtu nyuma yangu alikuwa akinionya kuwa hila yoyote ambayo ningeileta alikuwa tayari kunichapa risasi. Hata hivyo yule mtu alionekana kucheza vizuri na akili yangu kwani hakutoa bastola kutoka kwenye mfuko wa koti lake la suti badala yake akatoa noti moja ya faranga ya kirundi huku akitabasamu na kuyapelekea meno yake meupe yaonekane bila kificho.
Pasipo kuonesha tashwishwi yoyote nikageuka na kutazama mbele huku nikitembea taratibu katika ule mstari kwenda kutoa sadaka. Wakati nikiendelea kutembea kwenye ule mstari mara nikawaona wale watu wengine wawili wakisogea taratibu kutoka sehemu zao walizokuwa na kunikaribia pale kwenye mstari huku kila mmoja akiwa ameutia mkono wake ndani ya mfuko wa koti lake la suti. Hisia zangu zikanitanabaisha kuwa nilikuwa nikiandaliwa mtego wa kukamatwa mzimamzima. Nikiwa tayari nimeishtukia hila ile nikajikuta nikitabasamu moyoni huku akili yangu ikifanya kazi ya ziada. Wale watu waliponifikia mmoja akatangulia na kujichomeka kwenye ule mstari mbele yangu huku yule mwenzake akitembea kando sambamba na mimi ingawa hakuingia kwenye ule mstari kupanga foleni.
Taratibu nikageuka na kuyatembeza macho yangu mle ndani ya kanisani na umati ule wa watu ukanitanabaisha kuwa wale watu wasingeweza kuzitumia bastola zao katika mazingira yale hivyo nafsi yangu ikaniambia kuwa nilipaswa kurelax. Wakati tukilifikia kapu moja la sadaka mara nikamuona yule askofu aliyekuwa akiongoza misa akifunga vitabu vyake vya kuongozea misa kisha wasaidizi wake wawili wakasogea kwa unyenyekevu na kuvichukua vile vitabu na msalaba mkubwa kisha wakaanza kuondoka taratibu pale madhabahuni wakielekea kwenye mlango uliokuwa upande wa kushoto mbele ya lile kanisa. Walipoufikia ule mlango wakaufungua na kuingia mle ndani kisha ule mlango ukafungwa nyuma yao. Pale madhabahuni akabakia mtawa mmoja na watumishi wengine wa kanisa ambao bila shaka walikuwa wameachiwa jukumu la kufunga misa.
Wale watu sasa walikuwa wamenikaribia zaidi mmoja mbele, mwingine nyuma na yule mwingine akiwa kando yangu. Sikupenda kuzongwa namna ile hivyo kwa kuwa pale mbele kulikuwa na vyombo vingi vya kutoa sadaka mara nilipofika pale mbele nikachepuka kando kukifuata chombo cha mbali zaidi cha kutolea sadaka. Wale watu kuona vile wakashtuka na kuanza kunifuata hata hivyo wakati wakinifikia tayari nilikuwa nimeshatia sadaka yangu kwenye kapu na kurudi haraka kwenye ule mstari hivyo wale watu wakapishana na mimi wakati nikirudi. Bila kupoteza muda nikaharakisha na kuunga mstari wa matolea kwa mbele huku nikiuchunguza ule mlango wa ofisi ya askofu. Kwa kufanya vile nikaona kuwa upande wa kushoto pale mbele madhabahuni kulikuwa na nguzo na kando ya nguzo ile kulikuwa na ngazi. Nilipozichunguza zile ngazi nikagundua kuwa zilikuwa zikielekea kwenye ule mlango wa ile ofisi ya askofu.
Haraka nikageuka kuwatazama wale watu kule nyuma na hapo nikagundua kuwa walikuwa wakishangaa shangaa kwa kutoniona baada ya kutoka kutoa sadaka. Nafasi nzuri ambayo kamwe nisingeiacha iende hivihivi hivyo nilipoifikia ile nguzo ya kanisa nikachepuka kidogo na kuanza kupanda zile ngazi za kuelekea ofisi ya askofu. Watu wachache wakageuka na kunitazama kwa mshangao hata hivyo sikuwatilia maanani. Mara tu nilipoingia kwenye ile korido nikawaona wale wasaidizi wa askofu wakitoka kwenye kile chumba cha ofisi ya askofu kisha wakaelekea mbele hadi sehemu kulipokuwa na mlango mwingine ambapo waliufungua na kuingia mle ndani. Nikaendelea kutembea kwa tahadhari kwenye ile korido huku mara kwa mara nikigeuka nyuma kutazama. Sikuwaona wale watu hatari niliyowatoroka hivyo nikajua kuwa bado walikuwa wakinitafuta.
Nilipoufikia ule mlango wa ofisi ya askofu sikubisha hodi badala yake nikaufungua ule mlango na kuingia ndani. Macho ya mwanaume mwenye umri wa miaka hamsini na ushei yakanipokea kwa chuki isiyoelezeka kana kwamba tulikuwa tukifahamiana hapo kabla. Mwanaume yule akiwa katika mavazi yake ya kitumishi nyuma ya meza kubwa yenye lukuki ya vitabu vya kiroho, majarida na maandalio ya masomo ya kanisa. Askofu yule akanitazama kwa hadhari huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi.
Ile ofisi ilikuwa kubwa na ya kisasa. Upande wa kulia kulikuwa na kabati moja la mbao na makabati mawili mengine ya chuma na pembeni ya makabati yale kulikuwa na sanamu kubwa ya bikira Maria chini ya kalenda kubwa ya kirumi. Sakafuni kulikuwa zulia zuri la rangi nyekundu. Upande wa kushoto ukutani kulikuwa na rafu ya mbao iliyopangwa vitabu vya dini na juu ya rafu ile kulikuwa na mishumaa. Pembeni ya rafu ile ukutani kulikuwa na runinga kubwa iliyounganishwa na chaneli nyingi za dini. Mara moja tu nilipoingia mle ndani hali ya hewa nyepesi ikanifanya niyatembeze macho yangu mle ndani na hapo nikakiona kiyoyozi kimoja ukutani...ITAENDELEA
 
sijui kwann waleta hadithi jfnakuwaga ivi asee
Lakini yule jamaa wa Peni na Moni kazidi ndio maana mie namchanaga alafu watu wananiona mbaya, hauwezi kuwapa watu lifti kwa kuwatoa ubungo kisha ukawaacha magomeni, badala ya kuwafikisha kariakoo, then ukasema si lift bhana kwani mlilazimishwa kupanda? (kwani na wewe ulilazimishwa kusimamisha gari na kuwaambia watu wapande)
Ndio jamaa yule alieLEGEa anavyowatesa watu, si bora angekaa na hadithi yake tu hukohuko, miezi miwili unasubiria hadithi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom