SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 10
Ruby alifika nyumbani
kwa Mathew saa kumi na mbili
na nusu za jioni
“Samahani Mathew
nimechelewa sana nilikuwa
nafuatilia maandalizi ya zoezi
la jioni ya leo.Kila kitu
kimekwisha andaliwa”
akasema Ruby wakaelekea
katika ofisi ya Mathew na
Ruby akajiunga na ofisi yao na
picha kutoka katika kamera
mbali mbali katika uwanja wa
ndege wa Julius Nyerere
zikaanza kuonekana.
“Tayari vijana
wamejipanga vizuri.Wapo
walioko ndani kabisa ya
uwanja na katika sehemu
mbali mbali za uwanja na
Khalid atafuatiliwa toka
atakaposhuka uwanjani hadi
atakapoingia ndani ya gari na
watu wetu wengine
wamejipanga sehemu mbali
mbali.Kwa ujumla maandalizi
yote yamekamilika” akasema
Ruby
Saa moja na dakika tano za
jioni ndege ya shirika la ndege
la Ethiopia ilitua katika uwanja
wa ndege wa Julius Nyerere
jijini Dar es salaam.Lango la
ndege likafunguliwa abiria
wakaanza kushuka.Edwin
Mbeko ambaye ndiye
aliyekuwa akiongoza
operesheni ile kutoka ofisi kuu
ya SNSA akawataka watu wake
wakae makini.Hatimaye Yule
aliyekuwa akisubiriwa
akatokeza katika mlango wa
ndege.Alikuwa amevaa suti ya
rangi ya bluu
“Khalid Sultan anashuka
ndegeni.Narudia Khalid Sultan
anashuka ndegeni” mmoja wa
watu wa SNSA aliyekuwa
ndani ya uwanja akawajulisha
ofisi kuu
“Tumekupata namba
3.Endelea kumfuatilia.Namba
5 jiandae Khalid anaelekea
upande wako” akaelekeza
Edwin Mbeko.
Khalid Sultan aliingia
ndani ya jengo la uwanja wa
ndege kwa ajili ya kukamilisha
taratibu za kuingia
nchini.Baada ya kukamilisha
taratibu Khalid akaruhusiwa
kuingia Tanzania.
“Khalid tayari
ameruhusiwa kuinga nchini
anaelekea sehemu ya abiria
wanaowasili” akasema jamaa
mwingine aliyekuwamo ndani
ya jengo la uwanja.
Kamera za ndani ya
sehemu ya abiria wanaowasili
ilimuonyesha Khalid akiingia
kisha akapokewa na vijana
wawili wadogo waliokuwa
wameshika bango lenye jina la
KSK.Wakasalimiana na
kumsaidia kuyabeba
masanduku yake kuelekea
katika maegesho.
“Khalid anatoka nje ya
uwanja anaelekea eneo la
maegesho ya magari” akaripoti
jamaa mwingine
“Endeleeni kumfuatilia”
akaelekeza Edwin
“Kwa nini Khalid
amepokewa na vijana wale
wadogo?Nilitegemea
angepokewa na watu wazima”
akasema Ruby kwa mshangao
lakini Mathew hakumjibu kitu
Vijana wale wawili
walimuongoza Khalid hadi
katika gari moja aina ya Prado
rangi nyeupe wakaingia na
kuondoka pale uwanjani.
“Khalid anaondoka hapa
uwanjani” jamaa aliyekuwa nje
eneo la maegesho ya magari
akaripoti
“Namba nane na timu
yako kazi kwenu anzeni
kumfuatilia.Mtu huyu ni
makini sana hivyo mjitahidi
kuweka umbali kati yenu ili
asijue kama
anafuatiliwa.Mtamfuatilia kwa
msaada wa Satelaiti”
akaelekeza Edwin
Wakati zoezi la
kumfuatilia Khalid likianza
Ruby alikuwa anashughulikia
kuzitambua picha za wale
vijana wawili waliompokea
Khalid uwanja wa ndege na
baada ya muda akaguna.
“Vijana wale ni wadogo na
inaonekana hawajafikia umri
wa kusajiliwa katika sehemu
mbali mbali za usajili kwa ajili
ya kupata vitambulisho vya
taifa leseni nk.” Akasema
Ruby.Bado Mathew hakumjibu
kitu alikuwa kimya kabisa
Katika runinga mchoro
mwekundu na wakijani
iliendelea kuonekana
ikijongea.Mchoro mwekundu
ukiwa ni wa gari alilopanda
Khalid na mchoro wa kijani
ukiwa ni wa gari la SNSA
linalomfuatilia Khalid.
“Mmelikaribia sana gari la
Khalid tafadhali acheni umbali
kidogo” Edwin Mbeko akatoa
maelekezo.
Gari lile alilopanda Khalid
lilipita barabara kadhaa na
halafu likafika katika
mzunguko wa chama.Ghalfa
mawasiliano yakakatika.
“Nini kimetokea?Mathew
akamuuliza Ruby
“Sifahamu.Mawasiliano
yamekata ghafla” akasema
Ruby na kuchukua simu yake
akampigia Edwin
“Edwin kompyuta yangu
imekata mawasiliano
ghafla.Kuna tatizo lolote
huko?akauliza Ruby
“Madam Annabel kuna
tatizo limetokea si kwako tu
bali hata huku.Kuna matatizo
katika satelaiti tunayotumia na
timu imeanza kulishughulikia
hilo tatizo” akasema Edwin
“Kuna tatizo limetokea
katika satelaiti na
wanalishughulikia” Ruby
akamwambia Mathew ambaye
alipiga meza kwa hasira
“Usikasirike
Mathew.Wanashughulikia
suala hili na muda si mrefu
litakuwa tayari” akasema Ruby
“Ofisi kuu kuna tatizo
gani?Mawasiliano yamekatika
ghafla hatulioni tena gari la
Khalid” akasema kiongozi wa
timu iliyokuwa ikimfuatilia
Khalid.
“Kuna tatizo limetokea
lakini linashughulikiwa na
muda si mrefu mawasiliano
yatarejea tena” akasema Edwin
Baada ya dakika mbili
mawasiliano yakarejea lakini
mduara uliokuwa ukionekana
ni mmoja tu wa kijani ambao
ni gari la SNSA, gari
alilopanda Khalid halikuwa
likionekana
“We’ve lost him !
Tumempoteza Khalid.How
could they let this happen?!
Mathew akafoka
“I don’t know Mathew”
akajibu Ruby kwa uoga kisha
akampigia simu Edwin
hakupokea.Akampigia tena
simu mtu mwingine akapokea
na kumjulisha kwamba Edwin
alikuwa na timu ya ufundi
wakijaribu kujua nini kilitokea
“Ruby do something !
akasema Mathew
“Nadhani natakiwa niende
ofisini nikajue nini hasa
kilitokea”
“Hata kama ukienda bado
haitasaidia kitu.Khalid
tumekwisha mpoteza.Dakika
mbili ni nyingi sana kwa
gari.Hatutaweza kumpata
mida hii.Kwa nini tatizo hili
limejitokeza sasa wakati wa
zoezi muhimu kama hili?
Akauliza Mathew
“Mathew matatizo kama
haya ya kukatika mawasiliano
hutokea mara nyingi” akasema
Ruby
“Nafahamu Ruby
lakini..oh my God ! akasema
Mathew na kushika kiuno
“Jaribu kufuatilia zile
namba za gari alilopanda
Khalid” akasema Mathew na
Ruby akacheza na kompyuata
yake baada ya muda akasema
“Namba zile ni bandia
hazipo hazijulikani katka
mfumo wa usajili wa namba za
magari” akasema Ruby
“Dah ! Mathew akasema
na kukaa juu ya meza.Akafikiri
halafu akasema
“Ruby nisikilize”
“Hili suala lililotokea
halikutokea kwa bahati
mbaya.Huu ni mchezo
umechezwa”
“Mathew tusifike huko
kwanza.Hii yaweza kuwa ni
hitilafu ya kiufundi
imetokea.Tusubiri timu ya
ufundi ifanye uchunguzi wake
na tutagundua nini hasa
kilitokea” akasema Ruby
“Ruby nafahamu hitilafu
kama hizi huwa zinatokea
lakini hiki kilichotokea usiku
huu na tukampoteza Khalid si
bahati mbaya.Hiki ni kitu
kilichopangwa” akasema
Mathew
“Nani anaweza akafanya
kitu kama hiki?akauliza Ruby
“Hebu jiulize kwa nini
wametumwa watoto wadogo
kwenda kumpokea Khalid? Ni
kwa sababu walifahamu kuwa
Khalid anafuatiliwa na mtu
ambaye angeenda kumpokea
angechunguzwa yeye ni nani
ndiyo maana wakawatumia
wale watoto kwenda
kumpokea ambao hatuwezi
kuwatambua.Khalid ni mtu
mkubwa na hawezi kupokewa
na wale watoto wadogo.Kama
haitoshi namba za gari lile
alilopanda Khalid ni za bandia
na waliweka namba hizo
bandia ili tusiweze kumtambua
mmiliki wa gari hilo.Walijua
tunamfuatilia na ndiyo maana
wakajiandaa namna hii.Huu ni
mtandao mkubwa Ruby una
watu makini na wanajua
wanachokifanya.Walifahamu
tunamfuatilia Khalid ndiyo
maana mawasiliano
yakakatika na hilo lilifanyika
ili kulipoteza gari la Khalid
kwani mawasiliano yaliporejea
gari lile halikuonekana
tena.Tunachotakiwa kujiuliza
ni je wamefahamuje kama
tunamfuatilia Khalid?
Wamefahamuje mipango yetu?
Wamewezaje kukata
mawasiliano kati ya ofisi kuu
na timu iliyokuwa inamfuatlia
Khalid? Akauliza Mathew na
baada ya kufikiri kidogo Ruby
akasema
“Nadhani tuanze
kulitafutia majibu hili swali la
mwisho ulilouliza kwamba
mawasiliano yamekatikaje?
Akasema Ruby
“Kwa ninavyofahamu
mimi mfumo wa mawasiliano
wa idara kama hii umejengwa
katika mfumo ambao si rahisi
kwa mtu wa nje kuuingilia na
kufanya chochote
anachokitaka.Imetumika
teknolojia ya hali ya juu sana”
“Unataka kuniambia
kwamba mtu wa nje hawezi
kuingia katika mfumo na
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi? Akauliza Mathew
“Hapana haiwezekani.Ili
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi lazima kwanza mfumo
ukutambue hapa ninamaana
ya kwamba lazima uwe ndani
ya mfumo wetu ndipo unaweza
ukafanya kitu kama hiki
kilichofanyika” akasema Ruby
“Kwa maana hiyo kama
mawasiliano yalikatwa
makusudi mtu aliyefanya hivyo
lazima atakuwa anatoka ndani
ya SNSA” akasema Mathew
“Ndiyo” akasema Ruby
“Mathew nina….” Akasema
Ruby na kunyamaza baada ya
simu yake kuita alikuwa ni
Edwin
“Edwin ! akasema Ruby
“Madam Annabel
samahani nilishindwa kupokea
simu yako
uliponipigia.Nilikuwa na timu
ya wataalamu tukifuatilia
kujua nini hasa kilichotokea na
kusababisha mawasiliano
kukatika.Kwa mujibu wa
wataalamu wetu ni kwamba
lilikuwa ni tatizo la kawaida
ambalo linaweza kutokea
kufuatia hali mbaya ya hewa
na hakukuwa na makosa
yoyote ya kibinadamu”
akasema Edwin
“Sawa Edwin hakikisha
jambo kama hili halitokei tena
siku nyingine hasa
tunapokuwa katika operesheni
kubwa kama hizi.Mmefikia
wapi katika kumsaka
Khalid?Kuna mafanikio
yoyote?
“Mpaka sasa hakuna
madam na hatujui mahala
alikoelekea kwa sababu
mahala pale ambako
mawasiliano yalikatikia pana
njia nne hivyo hatujui njia ipi
gari lile lilielekea.Tunaendelea
na uchunguzi madam kujua
mahala alikoelekea.Ninaamini
tutalipata tu lile gari” akajibu
Edwin
“Edwin hakikisha ndani ya
muda mfupi tunfahamu
mahala aliko Khalid”
“Usijali madam
tunaendelea na zoezi hilo”
akajibu Edwin na Ruby
akakata simu akamueleza
Mathew kile alichoambiwa na
Edwin.
“Ruby ninaamini mno
utaalamu wako katika masuala
haya ya kompyuta na
mawasiliano kuliko mtu
mwingine yeyote na ndiyo
maana hata kule Uingereza
ulikokuwa unafanya kazi
hawakutaka kukuacha
uende.Sina hakika kama ndani
ya idara ya SNSA kuna mtu
mwenye utaalamu mkubwa wa
kompyuta kama ulio nao
wewe.Nataka ulifanyie
uchunguzi suala hili ili tujue
kama kweli ni tatizo la
kukatika kwa mawasiliano
kama inavyodaiwa?akasema
Mathew
“Ushauri wako ni mzuri
Mathew.Itanilazimu sasa
nielekee ofisini na uchunguzi
huo nikaufanyie nikiwa pale
ndipo nitakapoweza kujua nini
hasa kimetokea.Ninakuomba
twende wote” akasema Ruby
“Mimi si mfanyakazi wa
SNSA hivyo nikionekana pale
haitaleta picha nzuri kwako
utaonekana unaleta ndani ya
idara watu wasiohusika”
akasema Mathew.
“Mimi ndiye mkuu wa
idara hivyo usiwe na wasiwasi
wowote”akasema
Ruby.Hawakupoteza muda
wakaingia katika gari la Ruby
wakaondoka kuelekea ofisi kuu
ya SNSA.
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 10
Ruby alifika nyumbani
kwa Mathew saa kumi na mbili
na nusu za jioni
“Samahani Mathew
nimechelewa sana nilikuwa
nafuatilia maandalizi ya zoezi
la jioni ya leo.Kila kitu
kimekwisha andaliwa”
akasema Ruby wakaelekea
katika ofisi ya Mathew na
Ruby akajiunga na ofisi yao na
picha kutoka katika kamera
mbali mbali katika uwanja wa
ndege wa Julius Nyerere
zikaanza kuonekana.
“Tayari vijana
wamejipanga vizuri.Wapo
walioko ndani kabisa ya
uwanja na katika sehemu
mbali mbali za uwanja na
Khalid atafuatiliwa toka
atakaposhuka uwanjani hadi
atakapoingia ndani ya gari na
watu wetu wengine
wamejipanga sehemu mbali
mbali.Kwa ujumla maandalizi
yote yamekamilika” akasema
Ruby
Saa moja na dakika tano za
jioni ndege ya shirika la ndege
la Ethiopia ilitua katika uwanja
wa ndege wa Julius Nyerere
jijini Dar es salaam.Lango la
ndege likafunguliwa abiria
wakaanza kushuka.Edwin
Mbeko ambaye ndiye
aliyekuwa akiongoza
operesheni ile kutoka ofisi kuu
ya SNSA akawataka watu wake
wakae makini.Hatimaye Yule
aliyekuwa akisubiriwa
akatokeza katika mlango wa
ndege.Alikuwa amevaa suti ya
rangi ya bluu
“Khalid Sultan anashuka
ndegeni.Narudia Khalid Sultan
anashuka ndegeni” mmoja wa
watu wa SNSA aliyekuwa
ndani ya uwanja akawajulisha
ofisi kuu
“Tumekupata namba
3.Endelea kumfuatilia.Namba
5 jiandae Khalid anaelekea
upande wako” akaelekeza
Edwin Mbeko.
Khalid Sultan aliingia
ndani ya jengo la uwanja wa
ndege kwa ajili ya kukamilisha
taratibu za kuingia
nchini.Baada ya kukamilisha
taratibu Khalid akaruhusiwa
kuingia Tanzania.
“Khalid tayari
ameruhusiwa kuinga nchini
anaelekea sehemu ya abiria
wanaowasili” akasema jamaa
mwingine aliyekuwamo ndani
ya jengo la uwanja.
Kamera za ndani ya
sehemu ya abiria wanaowasili
ilimuonyesha Khalid akiingia
kisha akapokewa na vijana
wawili wadogo waliokuwa
wameshika bango lenye jina la
KSK.Wakasalimiana na
kumsaidia kuyabeba
masanduku yake kuelekea
katika maegesho.
“Khalid anatoka nje ya
uwanja anaelekea eneo la
maegesho ya magari” akaripoti
jamaa mwingine
“Endeleeni kumfuatilia”
akaelekeza Edwin
“Kwa nini Khalid
amepokewa na vijana wale
wadogo?Nilitegemea
angepokewa na watu wazima”
akasema Ruby kwa mshangao
lakini Mathew hakumjibu kitu
Vijana wale wawili
walimuongoza Khalid hadi
katika gari moja aina ya Prado
rangi nyeupe wakaingia na
kuondoka pale uwanjani.
“Khalid anaondoka hapa
uwanjani” jamaa aliyekuwa nje
eneo la maegesho ya magari
akaripoti
“Namba nane na timu
yako kazi kwenu anzeni
kumfuatilia.Mtu huyu ni
makini sana hivyo mjitahidi
kuweka umbali kati yenu ili
asijue kama
anafuatiliwa.Mtamfuatilia kwa
msaada wa Satelaiti”
akaelekeza Edwin
Wakati zoezi la
kumfuatilia Khalid likianza
Ruby alikuwa anashughulikia
kuzitambua picha za wale
vijana wawili waliompokea
Khalid uwanja wa ndege na
baada ya muda akaguna.
“Vijana wale ni wadogo na
inaonekana hawajafikia umri
wa kusajiliwa katika sehemu
mbali mbali za usajili kwa ajili
ya kupata vitambulisho vya
taifa leseni nk.” Akasema
Ruby.Bado Mathew hakumjibu
kitu alikuwa kimya kabisa
Katika runinga mchoro
mwekundu na wakijani
iliendelea kuonekana
ikijongea.Mchoro mwekundu
ukiwa ni wa gari alilopanda
Khalid na mchoro wa kijani
ukiwa ni wa gari la SNSA
linalomfuatilia Khalid.
“Mmelikaribia sana gari la
Khalid tafadhali acheni umbali
kidogo” Edwin Mbeko akatoa
maelekezo.
Gari lile alilopanda Khalid
lilipita barabara kadhaa na
halafu likafika katika
mzunguko wa chama.Ghalfa
mawasiliano yakakatika.
“Nini kimetokea?Mathew
akamuuliza Ruby
“Sifahamu.Mawasiliano
yamekata ghafla” akasema
Ruby na kuchukua simu yake
akampigia Edwin
“Edwin kompyuta yangu
imekata mawasiliano
ghafla.Kuna tatizo lolote
huko?akauliza Ruby
“Madam Annabel kuna
tatizo limetokea si kwako tu
bali hata huku.Kuna matatizo
katika satelaiti tunayotumia na
timu imeanza kulishughulikia
hilo tatizo” akasema Edwin
“Kuna tatizo limetokea
katika satelaiti na
wanalishughulikia” Ruby
akamwambia Mathew ambaye
alipiga meza kwa hasira
“Usikasirike
Mathew.Wanashughulikia
suala hili na muda si mrefu
litakuwa tayari” akasema Ruby
“Ofisi kuu kuna tatizo
gani?Mawasiliano yamekatika
ghafla hatulioni tena gari la
Khalid” akasema kiongozi wa
timu iliyokuwa ikimfuatilia
Khalid.
“Kuna tatizo limetokea
lakini linashughulikiwa na
muda si mrefu mawasiliano
yatarejea tena” akasema Edwin
Baada ya dakika mbili
mawasiliano yakarejea lakini
mduara uliokuwa ukionekana
ni mmoja tu wa kijani ambao
ni gari la SNSA, gari
alilopanda Khalid halikuwa
likionekana
“We’ve lost him !
Tumempoteza Khalid.How
could they let this happen?!
Mathew akafoka
“I don’t know Mathew”
akajibu Ruby kwa uoga kisha
akampigia simu Edwin
hakupokea.Akampigia tena
simu mtu mwingine akapokea
na kumjulisha kwamba Edwin
alikuwa na timu ya ufundi
wakijaribu kujua nini kilitokea
“Ruby do something !
akasema Mathew
“Nadhani natakiwa niende
ofisini nikajue nini hasa
kilitokea”
“Hata kama ukienda bado
haitasaidia kitu.Khalid
tumekwisha mpoteza.Dakika
mbili ni nyingi sana kwa
gari.Hatutaweza kumpata
mida hii.Kwa nini tatizo hili
limejitokeza sasa wakati wa
zoezi muhimu kama hili?
Akauliza Mathew
“Mathew matatizo kama
haya ya kukatika mawasiliano
hutokea mara nyingi” akasema
Ruby
“Nafahamu Ruby
lakini..oh my God ! akasema
Mathew na kushika kiuno
“Jaribu kufuatilia zile
namba za gari alilopanda
Khalid” akasema Mathew na
Ruby akacheza na kompyuata
yake baada ya muda akasema
“Namba zile ni bandia
hazipo hazijulikani katka
mfumo wa usajili wa namba za
magari” akasema Ruby
“Dah ! Mathew akasema
na kukaa juu ya meza.Akafikiri
halafu akasema
“Ruby nisikilize”
“Hili suala lililotokea
halikutokea kwa bahati
mbaya.Huu ni mchezo
umechezwa”
“Mathew tusifike huko
kwanza.Hii yaweza kuwa ni
hitilafu ya kiufundi
imetokea.Tusubiri timu ya
ufundi ifanye uchunguzi wake
na tutagundua nini hasa
kilitokea” akasema Ruby
“Ruby nafahamu hitilafu
kama hizi huwa zinatokea
lakini hiki kilichotokea usiku
huu na tukampoteza Khalid si
bahati mbaya.Hiki ni kitu
kilichopangwa” akasema
Mathew
“Nani anaweza akafanya
kitu kama hiki?akauliza Ruby
“Hebu jiulize kwa nini
wametumwa watoto wadogo
kwenda kumpokea Khalid? Ni
kwa sababu walifahamu kuwa
Khalid anafuatiliwa na mtu
ambaye angeenda kumpokea
angechunguzwa yeye ni nani
ndiyo maana wakawatumia
wale watoto kwenda
kumpokea ambao hatuwezi
kuwatambua.Khalid ni mtu
mkubwa na hawezi kupokewa
na wale watoto wadogo.Kama
haitoshi namba za gari lile
alilopanda Khalid ni za bandia
na waliweka namba hizo
bandia ili tusiweze kumtambua
mmiliki wa gari hilo.Walijua
tunamfuatilia na ndiyo maana
wakajiandaa namna hii.Huu ni
mtandao mkubwa Ruby una
watu makini na wanajua
wanachokifanya.Walifahamu
tunamfuatilia Khalid ndiyo
maana mawasiliano
yakakatika na hilo lilifanyika
ili kulipoteza gari la Khalid
kwani mawasiliano yaliporejea
gari lile halikuonekana
tena.Tunachotakiwa kujiuliza
ni je wamefahamuje kama
tunamfuatilia Khalid?
Wamefahamuje mipango yetu?
Wamewezaje kukata
mawasiliano kati ya ofisi kuu
na timu iliyokuwa inamfuatlia
Khalid? Akauliza Mathew na
baada ya kufikiri kidogo Ruby
akasema
“Nadhani tuanze
kulitafutia majibu hili swali la
mwisho ulilouliza kwamba
mawasiliano yamekatikaje?
Akasema Ruby
“Kwa ninavyofahamu
mimi mfumo wa mawasiliano
wa idara kama hii umejengwa
katika mfumo ambao si rahisi
kwa mtu wa nje kuuingilia na
kufanya chochote
anachokitaka.Imetumika
teknolojia ya hali ya juu sana”
“Unataka kuniambia
kwamba mtu wa nje hawezi
kuingia katika mfumo na
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi? Akauliza Mathew
“Hapana haiwezekani.Ili
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi lazima kwanza mfumo
ukutambue hapa ninamaana
ya kwamba lazima uwe ndani
ya mfumo wetu ndipo unaweza
ukafanya kitu kama hiki
kilichofanyika” akasema Ruby
“Kwa maana hiyo kama
mawasiliano yalikatwa
makusudi mtu aliyefanya hivyo
lazima atakuwa anatoka ndani
ya SNSA” akasema Mathew
“Ndiyo” akasema Ruby
“Mathew nina….” Akasema
Ruby na kunyamaza baada ya
simu yake kuita alikuwa ni
Edwin
“Edwin ! akasema Ruby
“Madam Annabel
samahani nilishindwa kupokea
simu yako
uliponipigia.Nilikuwa na timu
ya wataalamu tukifuatilia
kujua nini hasa kilichotokea na
kusababisha mawasiliano
kukatika.Kwa mujibu wa
wataalamu wetu ni kwamba
lilikuwa ni tatizo la kawaida
ambalo linaweza kutokea
kufuatia hali mbaya ya hewa
na hakukuwa na makosa
yoyote ya kibinadamu”
akasema Edwin
“Sawa Edwin hakikisha
jambo kama hili halitokei tena
siku nyingine hasa
tunapokuwa katika operesheni
kubwa kama hizi.Mmefikia
wapi katika kumsaka
Khalid?Kuna mafanikio
yoyote?
“Mpaka sasa hakuna
madam na hatujui mahala
alikoelekea kwa sababu
mahala pale ambako
mawasiliano yalikatikia pana
njia nne hivyo hatujui njia ipi
gari lile lilielekea.Tunaendelea
na uchunguzi madam kujua
mahala alikoelekea.Ninaamini
tutalipata tu lile gari” akajibu
Edwin
“Edwin hakikisha ndani ya
muda mfupi tunfahamu
mahala aliko Khalid”
“Usijali madam
tunaendelea na zoezi hilo”
akajibu Edwin na Ruby
akakata simu akamueleza
Mathew kile alichoambiwa na
Edwin.
“Ruby ninaamini mno
utaalamu wako katika masuala
haya ya kompyuta na
mawasiliano kuliko mtu
mwingine yeyote na ndiyo
maana hata kule Uingereza
ulikokuwa unafanya kazi
hawakutaka kukuacha
uende.Sina hakika kama ndani
ya idara ya SNSA kuna mtu
mwenye utaalamu mkubwa wa
kompyuta kama ulio nao
wewe.Nataka ulifanyie
uchunguzi suala hili ili tujue
kama kweli ni tatizo la
kukatika kwa mawasiliano
kama inavyodaiwa?akasema
Mathew
“Ushauri wako ni mzuri
Mathew.Itanilazimu sasa
nielekee ofisini na uchunguzi
huo nikaufanyie nikiwa pale
ndipo nitakapoweza kujua nini
hasa kimetokea.Ninakuomba
twende wote” akasema Ruby
“Mimi si mfanyakazi wa
SNSA hivyo nikionekana pale
haitaleta picha nzuri kwako
utaonekana unaleta ndani ya
idara watu wasiohusika”
akasema Mathew.
“Mimi ndiye mkuu wa
idara hivyo usiwe na wasiwasi
wowote”akasema
Ruby.Hawakupoteza muda
wakaingia katika gari la Ruby
wakaondoka kuelekea ofisi kuu
ya SNSA.