Riwaya: Siri

SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 10
Ruby alifika nyumbani
kwa Mathew saa kumi na mbili
na nusu za jioni
“Samahani Mathew
nimechelewa sana nilikuwa
nafuatilia maandalizi ya zoezi
la jioni ya leo.Kila kitu
kimekwisha andaliwa”
akasema Ruby wakaelekea
katika ofisi ya Mathew na
Ruby akajiunga na ofisi yao na
picha kutoka katika kamera
mbali mbali katika uwanja wa
ndege wa Julius Nyerere
zikaanza kuonekana.
“Tayari vijana
wamejipanga vizuri.Wapo
walioko ndani kabisa ya
uwanja na katika sehemu
mbali mbali za uwanja na
Khalid atafuatiliwa toka
atakaposhuka uwanjani hadi
atakapoingia ndani ya gari na
watu wetu wengine
wamejipanga sehemu mbali
mbali.Kwa ujumla maandalizi
yote yamekamilika” akasema
Ruby
Saa moja na dakika tano za
jioni ndege ya shirika la ndege
la Ethiopia ilitua katika uwanja
wa ndege wa Julius Nyerere
jijini Dar es salaam.Lango la
ndege likafunguliwa abiria
wakaanza kushuka.Edwin
Mbeko ambaye ndiye
aliyekuwa akiongoza
operesheni ile kutoka ofisi kuu
ya SNSA akawataka watu wake
wakae makini.Hatimaye Yule
aliyekuwa akisubiriwa
akatokeza katika mlango wa
ndege.Alikuwa amevaa suti ya
rangi ya bluu
“Khalid Sultan anashuka
ndegeni.Narudia Khalid Sultan
anashuka ndegeni” mmoja wa
watu wa SNSA aliyekuwa
ndani ya uwanja akawajulisha
ofisi kuu
“Tumekupata namba
3.Endelea kumfuatilia.Namba
5 jiandae Khalid anaelekea
upande wako” akaelekeza
Edwin Mbeko.
Khalid Sultan aliingia
ndani ya jengo la uwanja wa
ndege kwa ajili ya kukamilisha
taratibu za kuingia
nchini.Baada ya kukamilisha
taratibu Khalid akaruhusiwa
kuingia Tanzania.
“Khalid tayari
ameruhusiwa kuinga nchini
anaelekea sehemu ya abiria
wanaowasili” akasema jamaa
mwingine aliyekuwamo ndani
ya jengo la uwanja.
Kamera za ndani ya
sehemu ya abiria wanaowasili
ilimuonyesha Khalid akiingia
kisha akapokewa na vijana
wawili wadogo waliokuwa
wameshika bango lenye jina la
KSK.Wakasalimiana na
kumsaidia kuyabeba
masanduku yake kuelekea
katika maegesho.
“Khalid anatoka nje ya
uwanja anaelekea eneo la
maegesho ya magari” akaripoti
jamaa mwingine
“Endeleeni kumfuatilia”
akaelekeza Edwin
“Kwa nini Khalid
amepokewa na vijana wale
wadogo?Nilitegemea
angepokewa na watu wazima”
akasema Ruby kwa mshangao
lakini Mathew hakumjibu kitu
Vijana wale wawili
walimuongoza Khalid hadi
katika gari moja aina ya Prado
rangi nyeupe wakaingia na
kuondoka pale uwanjani.
“Khalid anaondoka hapa
uwanjani” jamaa aliyekuwa nje
eneo la maegesho ya magari
akaripoti
“Namba nane na timu
yako kazi kwenu anzeni
kumfuatilia.Mtu huyu ni
makini sana hivyo mjitahidi
kuweka umbali kati yenu ili
asijue kama
anafuatiliwa.Mtamfuatilia kwa
msaada wa Satelaiti”
akaelekeza Edwin
Wakati zoezi la
kumfuatilia Khalid likianza
Ruby alikuwa anashughulikia
kuzitambua picha za wale
vijana wawili waliompokea
Khalid uwanja wa ndege na
baada ya muda akaguna.
“Vijana wale ni wadogo na
inaonekana hawajafikia umri
wa kusajiliwa katika sehemu
mbali mbali za usajili kwa ajili
ya kupata vitambulisho vya
taifa leseni nk.” Akasema
Ruby.Bado Mathew hakumjibu
kitu alikuwa kimya kabisa
Katika runinga mchoro
mwekundu na wakijani
iliendelea kuonekana
ikijongea.Mchoro mwekundu
ukiwa ni wa gari alilopanda
Khalid na mchoro wa kijani
ukiwa ni wa gari la SNSA
linalomfuatilia Khalid.
“Mmelikaribia sana gari la
Khalid tafadhali acheni umbali
kidogo” Edwin Mbeko akatoa
maelekezo.
Gari lile alilopanda Khalid
lilipita barabara kadhaa na
halafu likafika katika
mzunguko wa chama.Ghalfa
mawasiliano yakakatika.
“Nini kimetokea?Mathew
akamuuliza Ruby
“Sifahamu.Mawasiliano
yamekata ghafla” akasema
Ruby na kuchukua simu yake
akampigia Edwin
“Edwin kompyuta yangu
imekata mawasiliano
ghafla.Kuna tatizo lolote
huko?akauliza Ruby
“Madam Annabel kuna
tatizo limetokea si kwako tu
bali hata huku.Kuna matatizo
katika satelaiti tunayotumia na
timu imeanza kulishughulikia
hilo tatizo” akasema Edwin
“Kuna tatizo limetokea
katika satelaiti na
wanalishughulikia” Ruby
akamwambia Mathew ambaye
alipiga meza kwa hasira
“Usikasirike
Mathew.Wanashughulikia
suala hili na muda si mrefu
litakuwa tayari” akasema Ruby
“Ofisi kuu kuna tatizo
gani?Mawasiliano yamekatika
ghafla hatulioni tena gari la
Khalid” akasema kiongozi wa
timu iliyokuwa ikimfuatilia
Khalid.
“Kuna tatizo limetokea
lakini linashughulikiwa na
muda si mrefu mawasiliano
yatarejea tena” akasema Edwin
Baada ya dakika mbili
mawasiliano yakarejea lakini
mduara uliokuwa ukionekana
ni mmoja tu wa kijani ambao
ni gari la SNSA, gari
alilopanda Khalid halikuwa
likionekana
“We’ve lost him !
Tumempoteza Khalid.How
could they let this happen?!
Mathew akafoka
“I don’t know Mathew”
akajibu Ruby kwa uoga kisha
akampigia simu Edwin
hakupokea.Akampigia tena
simu mtu mwingine akapokea
na kumjulisha kwamba Edwin
alikuwa na timu ya ufundi
wakijaribu kujua nini kilitokea
“Ruby do something !
akasema Mathew
“Nadhani natakiwa niende
ofisini nikajue nini hasa
kilitokea”
“Hata kama ukienda bado
haitasaidia kitu.Khalid
tumekwisha mpoteza.Dakika
mbili ni nyingi sana kwa
gari.Hatutaweza kumpata
mida hii.Kwa nini tatizo hili
limejitokeza sasa wakati wa
zoezi muhimu kama hili?
Akauliza Mathew
“Mathew matatizo kama
haya ya kukatika mawasiliano
hutokea mara nyingi” akasema
Ruby
“Nafahamu Ruby
lakini..oh my God ! akasema
Mathew na kushika kiuno
“Jaribu kufuatilia zile
namba za gari alilopanda
Khalid” akasema Mathew na
Ruby akacheza na kompyuata
yake baada ya muda akasema
“Namba zile ni bandia
hazipo hazijulikani katka
mfumo wa usajili wa namba za
magari” akasema Ruby
“Dah ! Mathew akasema
na kukaa juu ya meza.Akafikiri
halafu akasema
“Ruby nisikilize”
“Hili suala lililotokea
halikutokea kwa bahati
mbaya.Huu ni mchezo
umechezwa”
“Mathew tusifike huko
kwanza.Hii yaweza kuwa ni
hitilafu ya kiufundi
imetokea.Tusubiri timu ya
ufundi ifanye uchunguzi wake
na tutagundua nini hasa
kilitokea” akasema Ruby
“Ruby nafahamu hitilafu
kama hizi huwa zinatokea
lakini hiki kilichotokea usiku
huu na tukampoteza Khalid si
bahati mbaya.Hiki ni kitu
kilichopangwa” akasema
Mathew
“Nani anaweza akafanya
kitu kama hiki?akauliza Ruby
“Hebu jiulize kwa nini
wametumwa watoto wadogo
kwenda kumpokea Khalid? Ni
kwa sababu walifahamu kuwa
Khalid anafuatiliwa na mtu
ambaye angeenda kumpokea
angechunguzwa yeye ni nani
ndiyo maana wakawatumia
wale watoto kwenda
kumpokea ambao hatuwezi
kuwatambua.Khalid ni mtu
mkubwa na hawezi kupokewa
na wale watoto wadogo.Kama
haitoshi namba za gari lile
alilopanda Khalid ni za bandia
na waliweka namba hizo
bandia ili tusiweze kumtambua
mmiliki wa gari hilo.Walijua
tunamfuatilia na ndiyo maana
wakajiandaa namna hii.Huu ni
mtandao mkubwa Ruby una
watu makini na wanajua
wanachokifanya.Walifahamu
tunamfuatilia Khalid ndiyo
maana mawasiliano
yakakatika na hilo lilifanyika
ili kulipoteza gari la Khalid
kwani mawasiliano yaliporejea
gari lile halikuonekana
tena.Tunachotakiwa kujiuliza
ni je wamefahamuje kama
tunamfuatilia Khalid?
Wamefahamuje mipango yetu?
Wamewezaje kukata
mawasiliano kati ya ofisi kuu
na timu iliyokuwa inamfuatlia
Khalid? Akauliza Mathew na
baada ya kufikiri kidogo Ruby
akasema
“Nadhani tuanze
kulitafutia majibu hili swali la
mwisho ulilouliza kwamba
mawasiliano yamekatikaje?
Akasema Ruby
“Kwa ninavyofahamu
mimi mfumo wa mawasiliano
wa idara kama hii umejengwa
katika mfumo ambao si rahisi
kwa mtu wa nje kuuingilia na
kufanya chochote
anachokitaka.Imetumika
teknolojia ya hali ya juu sana”
“Unataka kuniambia
kwamba mtu wa nje hawezi
kuingia katika mfumo na
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi? Akauliza Mathew
“Hapana haiwezekani.Ili
kukata mawasiliano kati ya
ofisi kuu na watu walioko nje
ya ofisi lazima kwanza mfumo
ukutambue hapa ninamaana
ya kwamba lazima uwe ndani
ya mfumo wetu ndipo unaweza
ukafanya kitu kama hiki
kilichofanyika” akasema Ruby
“Kwa maana hiyo kama
mawasiliano yalikatwa
makusudi mtu aliyefanya hivyo
lazima atakuwa anatoka ndani
ya SNSA” akasema Mathew
“Ndiyo” akasema Ruby
“Mathew nina….” Akasema
Ruby na kunyamaza baada ya
simu yake kuita alikuwa ni
Edwin
“Edwin ! akasema Ruby
“Madam Annabel
samahani nilishindwa kupokea
simu yako
uliponipigia.Nilikuwa na timu
ya wataalamu tukifuatilia
kujua nini hasa kilichotokea na
kusababisha mawasiliano
kukatika.Kwa mujibu wa
wataalamu wetu ni kwamba
lilikuwa ni tatizo la kawaida
ambalo linaweza kutokea
kufuatia hali mbaya ya hewa
na hakukuwa na makosa
yoyote ya kibinadamu”
akasema Edwin
“Sawa Edwin hakikisha
jambo kama hili halitokei tena
siku nyingine hasa
tunapokuwa katika operesheni
kubwa kama hizi.Mmefikia
wapi katika kumsaka
Khalid?Kuna mafanikio
yoyote?
“Mpaka sasa hakuna
madam na hatujui mahala
alikoelekea kwa sababu
mahala pale ambako
mawasiliano yalikatikia pana
njia nne hivyo hatujui njia ipi
gari lile lilielekea.Tunaendelea
na uchunguzi madam kujua
mahala alikoelekea.Ninaamini
tutalipata tu lile gari” akajibu
Edwin
“Edwin hakikisha ndani ya
muda mfupi tunfahamu
mahala aliko Khalid”
“Usijali madam
tunaendelea na zoezi hilo”
akajibu Edwin na Ruby
akakata simu akamueleza
Mathew kile alichoambiwa na
Edwin.
“Ruby ninaamini mno
utaalamu wako katika masuala
haya ya kompyuta na
mawasiliano kuliko mtu
mwingine yeyote na ndiyo
maana hata kule Uingereza
ulikokuwa unafanya kazi
hawakutaka kukuacha
uende.Sina hakika kama ndani
ya idara ya SNSA kuna mtu
mwenye utaalamu mkubwa wa
kompyuta kama ulio nao
wewe.Nataka ulifanyie
uchunguzi suala hili ili tujue
kama kweli ni tatizo la
kukatika kwa mawasiliano
kama inavyodaiwa?akasema
Mathew
“Ushauri wako ni mzuri
Mathew.Itanilazimu sasa
nielekee ofisini na uchunguzi
huo nikaufanyie nikiwa pale
ndipo nitakapoweza kujua nini
hasa kimetokea.Ninakuomba
twende wote” akasema Ruby
“Mimi si mfanyakazi wa
SNSA hivyo nikionekana pale
haitaleta picha nzuri kwako
utaonekana unaleta ndani ya
idara watu wasiohusika”
akasema Mathew.
“Mimi ndiye mkuu wa
idara hivyo usiwe na wasiwasi
wowote”akasema
Ruby.Hawakupoteza muda
wakaingia katika gari la Ruby
wakaondoka kuelekea ofisi kuu
ya SNSA.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 11
Baada ya mawasiliano
kukatika kati ya ofisi kuu ya
SNSA na timu iliyokuwa
ikimfuatilia Khalid
Sultan,jamaa aliyekuwa katika
usukani wa gari lile alilopanda
Khalid ambaye aliweka kifaa
Fulani sikioni kwa ajili ya
mawasiliano akaelekezwa
kuendelea na mpango kama
ulivyokuwa
umepangwa.Dereva Yule
akaelekea katika barabara ya
Arusha halafu akakata kulia
akaingia mtaa wa Mtepa
akaingia katika shule moja ya
watoto wadogo.Khalid na watu
wengine wawili wakashuka na
kuingia katika gari lingine
lenye rangi nyeusi,likatoka
ndani ya ile shule na kuelekea
Kisulo Car wash Khalid na
watu wale wawili wakashuka
na kuingia katika gari ambalo
kulikuwa na dereva
mwanamke ambaye aliliondoa
lile gari mahala pale.Safari
ilikuwa ya kimya kimya hadi
walipofika katika makazi ya
Melanie Davis geti likafunguka
gari likaingia ndani.Khalid na
wale jamaa wawili wakashuka
garini wakapokewa na Melanie
Davis akawakaribisha ndani.
“Khalid karibu sana
Tanzania,karibu sana Dar es
salaam.Utatusamehe kwa
mzunguko mrefu hii ni kwa
sababu za kiusalama”akasema
Melanie
“Ninawapongezeni kwa
tahadhari kubwa
mlizozichukua.Ninyi ni watu
makini sana nimefurahishwa
na umahiri wenu katika
kuhakikisha ninakuwa salama”
akasema Khalid wakitumia
lugha ya kiingereza
“Khalid kwa kuwa umefika
salama nadhani ningekupeleka
chumbani kwako ukaoge kisha
tupate chakula halafu
mazungumzo yataanza”
“James Kasai amekwisha
fika?akauliza Khalid
“James Kasai amekwisha
wasili yuko chumbani kwake
akipumzika.Utaonana naye
baadae” akasema Melanie na
kumpeleka Khalid katika
chumba alichoandaliwa kisha
akarejea sebuleni walikokuwa
wale watu wawili waliokuja na
Khalid.
“Madam sisi tumemaliza
kazi yetu tuliyopewa ambayo
ilikuwa ni kuhakikisha mgeni
anafika hapa salama na sasa
tunaweza kuondoka”akasema
mmoja wa wale jamaa.
“Ahsanteni sana kwa
kumfikisha mgeni
salama.”akasema Melanie na
kumtaka Joyce dereva wake
awapeleke wale wageni.
Baada ya Khalid kuoga
akaelekea sebuleni ambako
alikutana na James
Kasai.Wakasalimiana kwa
furaha
“Nimefurahi sana
kukutana nawe
James”akasema Khalid
“Mimi pia” akasema James
Melanie akawapeleka
katika chumba cha chakula
wakapata chakula cha usiku
pamoja.Wakati wakipata
chakula Edwin Mbeko
akawasili na kujumuika na
akina Melanie mezani kwa
chakula.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 12
Ruby na Mathew
waliwasili ofisi kuu ya SNSA
wakashuka garini na kuelekea
moja kwa moja katika ofisi ya
Ruby ambako Mathew
alikaribishwa kisha Ruby
akatoka na kumfuata Edwin
ofisini kwake.
“Karibu madam” akasema
Edwin
“Edwin nataka kufahamu
mahala mlikofikia hadi sasa
katika kumtafuta Khalid”
akasema Ruby
“Madam mpaka sasa bado
hatujafanikiwa na mimi
ninajiandaa kwenda kuungana
na timu ya nje kuendelea na
zoezi la kumsaka
Khalid.Hatutalala leo hadi
tuhakikishe Khalid
amepatikana”
“Nataka nipate taarifa ya
wataalamu wetu kuhusiana na
namna tukio lile la kukatika
mawasiliano lilivyotokea”
akasema Ruby
“Madam awali tulidhani
labda kuna mkono wa mtu
katika tukio lile lakini baada ya
wataalamu wetu kufanya
uchunguzi wao wanasema
kwamba ni hali mbaya ya hewa
ndiyo iliyopelekea tukio lile
kutokea” akasema Edwin
“Sawa Edwin.Namtaka
mkuu wa idara ya ufundi
ofisini kwangu mara moja”
akasema Ruby na kuelekea
katika ukumbi mkubwa
ambako kazi zilikuwa
zinaendelea.
“Naomba mnisikilize
tafadhali” akasema Ruby na
watu wote wakaacha shughuli
zao na kumgeukia Ruby.
“Asubuhi niliwaeleza
kuhusiana na ujio wa Khalid
Sultan Khalid na namna gani
mtu huyo alivyo hatari kwa
nchi yetu.Niliwaeleza kwamba
mtu huyu anatoka IS na ni
mtaalamu wa milipuko
mikubwa na niliweka wazi
hofu yangu kwamba kuna
uwezekano mkubwa IS
wanaandaa tena shambulio
lingine kubwa hapa nchini
ndiyo maana Khalid amekuja
nchini.Pamoja na kujipanga
vizuri sana kumfuatilia Khalid
lakini teknolojia imetuangusha
na tumejikuta tukimpoteza
Khalid bila kutarajia na sasa
tuna kazi nyingine kubwa ya
kumsaka Khalid na kujua
mahala alipo.Lazima tufanye
kila tuwezalo kuhakikisha
tunampata Khalid.Uwezo huo
tunao kwani tunao uwezo wa
kuona asilimia tisini ya kamera
zote za usalama zilizoko
barabarani,tunao uwezo wa
kudukua mitandao yote ya
simu hapa nchini hivyo hatuna
sababu yoyote ya kutufanya
tushindwe kufahamu mahala
alipo Khalid.Tumieni kila
tulichonacho katika idara yetu
kuhakikisha Khalid
anapatikana.Edwin
anakwenda kuungana na timu
ya nje kuendelea na zoezi la
kutafuta mahala aliko Khalid
na sisi tulioko hapa tuendelee
pia na zoezi hilo.Tunakesha
hapa usiku wa leo hakuna mtu
atakayeondoka kwenda
nyumbani hadi tuhakikishe
Khalid anapatikana” akasema
Ruby kisha akaelekea ofisini
kwake.Mara tu alipoingia
ofisini Fidelis mkuu wa idara
ya ufundi akaingia Ruby
akamchukua wakaelekea
katika chumba kidogo cha
mazungumzo kilichokuwa
pembeni ya ofisi ile ya Ruby.
“Fidelis wewe ndiye mkuu
wa idara ya ufundi nataka
uniambie nini hasa
kilichotokea na kusababisha
mawasiliano yakakatika hadi
tukampoteza mtu muhimu
kabisa?akauliza Ruby na Fideli
akaanza kumuelezea kile
alichokigundua katika
uchunguzi wake.Wakati
wakiendelea na mazungumzo
akaingia Edwin na kumkuta
Mathew akiwa ameketi sofani
akamsalimu halafu akafungua
mlango wa kioo wa chumba
walichokuwamo Ruby na
Fidelis wakizungumza.
“Madam ninaondoka
ninakwenda kuonana na vijana
kuendelea na lile zoezi”
akasema Edwin
“Sawa Edwin .Nataka
mawasiliano ya mara kwa
mara tafadhali”akasema Ruby
na Edwin akatoka. Baada ya
takribani dakika ishirini za
mazungumzo Fidelis akatoa
ofisini kwa Ruby.
“Watu wa idara hii
hawajanifahamu vyema mimi
ni nani”Ruby akamwambia
Mathew baada ya kutoka
kuzungumza na Fidelis
“Huyu jamaa aliyetoka
hapa muda mfupi uliopita
anaitwa Fidelis ni mkuu wa
idara ya ufundi.Baada ya tukio
lile kutokea huyu jamaa na
timu yake ndio waliochunguza
kujua kilichotokea.Nilimuita
hapa ili anieleze kwa kina nini
hasa kilichotokea lakini
maelezo anayonipa hayaingii
akilini ni kama vile anampa
maelezo mtu ambaye hana
ujuzi wowote wa
kompyuta.Kwa bahati nzuri
hapa idarani hakuna anayejua
uwezo wangu katika mambo
haya ya teknolojia ya
kompyuta” akasema Ruby
“It’s time to show them
who you real are.Mimi bado
naamini kabisa kwamba kuna
kitu hapa katika lile tukio”
akasema Mathew
“Mathew ninataka
kulishughulikia suala hili na
nitakuomba univumilie hadi
pale nitakapomaliza kazi
yangu”
“Usijali Ruby endelea na
kazi yako.Tunahitaji sana
kuufahamu ukweli” akasema
Mathew
“Thank you my love”
akasema Ruby huku
akitabasamu kisha akaanza
kazi katika kompyuta yake.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 13
Baada ya kupata chakula
Melanie akawaongoza akina
Khalid katika chumba cha
mazungumzo.
“Khalid na James Kasai
karibuni sana Tanzania
karibuni sana Dar es salaam”
akasema Melanie
“Melanie ninashukuru
sana kwa mapokezi mazuri
sana hadi mkanifikisha
hapa.Nilisema pale awali na
ninarudia tena kwamba ninyi
ni mahiri sana katika mipango
yenu.Mnastahili pongezi
kubwa.Ni mara yangu ya
kwanza kufika Tanzania na
sikutegemea kukutana na watu
wenye ujuzi mkubwa namna
hii kama ninyi.Kingine
ambacho kilinipa mawazo
mengi sana ni kama James
Kasai angeweza kuingia hapa
nchini kufuatia kutafutwa sana
na nchi za Afrika mashariki
kutokana na lile shambulio la
hivi majuzi.Nilipoambiwa
kwamba tayari yuko hapa
nchini sikuamini hadi pale
nilipomtia machoni.Ninajisikia
fahari kufanya kazi na watu
kama ninyi.Kama mmeweza
kufanikisha kumuingiza James
Kasai nchini Tanzania licha ya
ulinzi mkali ulioko mipakani
na kila sehemu basi mnaweza
kufanya kitu chochote hapa
nchini” akasema Khalid
“Ahsante sana kwa
pongezi Khalid.Tunao uwezo
wa kufanya chochote hapa
nchini lakini haya yote
yanawezekana kwa sababu ya
huyu mtu hapa” akasema
Melanie na kumshika bega
Edwin
“Anaitwa Edwin
Mbeko.Huyu ni mkurugenzi
wa idara ya siri ya usalama wa
ndani ya nchi.Yeye ndiye
anayechukua nafasi kubwa
katika haya yote
yanayoendelea hivi sasa.Hata
katika mipango yetu yote
tutakayoipanga huyu ndiye
hasa ambaye ataitekeleza”
akasema Melanie
“Hongera sana Edwin.Kazi
yako tumeiona.Ni kazi nzuri
sana” akasema Khalid.
“Nadhani sasa tuendelee
na mazungumzo” akasema
Melanie
“Nmeelekezwa nije
Tanzania na wakuu wangu
kwamba kuna kazi ya kufanya
lakini sijui ni kazi gani kwa
hiyo ninyi ndio mnaotakiwa
mnipe taarifa ni kitu gani hasa
nimekuja kukifanya huku
Tanzania” akasema Khalid na
Melanie akampa ishara James
Kasai aendelee.
“Jambo kubwa ambalo
limetukutanisha hapa ni
kujadiliana kuhusu mpango
wa kuwaua marais wa
Tanzania na Congo kwa bomu
la kujitoa mhanga” akasema
James
Wakati mazungumzo ya
kuhusu mpango wa kuwaua
marais Dar Fabian Kelelo na
Patrice Eyenga yakiendelea
nyumbani kwa Melanie Davis,
katika ofisi kuu ya SNSA Ruby
aliendelea na zoezi la kujaribu
kutafuta chanzo cha
mawasiliano kukatika ghafla
na kupelekea Khalid
kupotea.Dakika arobaini
zimekwisha pita toka
alipoanza zoezi hilo.Mathew
Mulumbi badi alikuwa ofisini
kwa Ruby akisubiri zoezi lile
limalizike.Mawazo yake
yalikuwa mbali sana.Kichwa
chake kilijaa mawazo ya
namna walivyoachana na
Peniela.Alikumbuka historia
yao walikotoka mambo
waliyopitia na hadi
walivyoachana.
“Mambo yanayokuja
kichwani kwangu kuhusu
mimi na Peniela ni kama
ninatazama filamu lakini hii si
filamu bali ni kitu cha kweli
kabisa.Ni maisha halisi
ambayo mimi na Peniela
tumeyaishi.Tulikuwa na
mipango mingi sana ya siku za
usoni lakini yote hatawezekana
tena” akawazaMathew
“Sasa niko huru wa kuwa
na mwanamke mwingine na
kama nikiambiwa nichague
basi Ruby anafaa sana
kuchukua nafasi ya Peniela
lakini je ni vipi kama
yatamkuta kama yale ya
Peniela je ataweza kuvumilia
au nitakuwa ninamuumiza
huyu binti malaika?Kila
ninapomtazama Ruby
ninapata mawazo mengi
sana.Najua ananipenda na
mimi pia ninampenda
lakini…....”
“Mathew ulikuwa
sahihi”akasema Ruby na
kumtoa Mathew mawazoni
akasimama
“Unasemaje
Ruby?akauliza
“Ulikuwa
sahihi.Mawasiliano kukatika
hakukusababishwa na hali ya
hewa kama inavyodaiwa bali ni
kitendo kilichofanywa na mtu
kwa makusudi”
“Oh my God ! Unaweza
ukafahamu nani aliyefanya
hivyo?akauliza Mathew.Ruby
akaendelea kubonyeza
kompyuta yake na baada ya
dakika tatu akasema
“Tatizo hilo lilitokea katika
stesheni 5” akasema Ruby na
kufungua faili Fulani
“Stesheni 5 ni ya mtu
anaitwa Edina Mkwena”
“Ruby are you sure?
Mathew akauliza
“I’m sure”akasema Ruby
“Jambo hili lilifanywa
kitaalamu sana lakini kwa
bahati mbaya hawakujua kama
mimi ni mtaalamu zaidi
yao.Hawafahamu kama
nimeanza kucheza na
kompyuta toka nikiwa na
miaka minne na kwa maisha
yangu yote ndicho kitu
ambacho nimekuwa
ninakifanya.Nilifanya vyema
kutojitambulisha kwao uwezo
wangu na sasa tumeanza
kupata picha ya namna
mambo yanavyokwenda katika
idara hii” akasema Ruby
“Nilijua tu kwamba lazima
jambo lile limefanyika kwa
makusudi kabisa hasa
ukiangalia mahala ambako
mawasiliano yalikatikia
kwenye mzunguko wenye
barabara nne na baada ya
mawasiliano kurejea hatujui
gari lile lilifuata barabara
ipi.Mpaka hapa tayari
tumeanza kupata mwanga
kwamba kuna mtu ndani ya
idara hii anahusika katika lile
tukio.Yawezekana huyu
amepandikizwa maalum kwa
ajili ya kufuatilia kila
kinachoendelea ndani ya hii
idara na kuwapa taarifa hao
waliomtuma.Yuko hapa kwa
malengo maalum na
inawezekana huyo ndiye
aliyewapa taarifa kwamba
Khalid anafuatiliwa na
wakapanga wafanye vile
walivyofanya.Hawa watu kama
nilivyokwambia kwamba ni
watu makini sana na wanajua
wanachokifanya.Wameotesha
mizizi yao karibu kila sehemu
muhimu ya serikali” akasema
Mathew
“What are we going to do?
Akauliza Ruby
“Tayari tumepata chanzo
hivyo hatupaswi kwenda naye
haraka.Tunachotakiwa
kufanya ni kumchunguza kwa
siri sana kila
anachokifanya.Tufuatilie
mawasiliano yake tujue
anaowasiliana nao na
wanawasiliana nini,tufunge
kamera za siri nyumbani
kwake na kufuatiliakila
kinachoendelea hapo
kwake.Huyu ndiye
atakayetuongoza kuelekea
mahala walipo
waliomtuma.Anza kwa kujenga
naye urafiki.Muweke karibu
yako ili iwe rahisi kumfuatilia”
akasema Mathew na Ruby
akainua simu akapiga stesheni
5 ambayo ni ofisi ya Edina
lakini simu ikaita bila
kupokelewa.Akapiga tena simu
ikaita haikupokelewa.
“Hapokei simu” akasema
Ruby na kumpigia mtu
mwingine akamtaka
akamuangalie Edina ofisini
kwake.Baada ya dakika mbili
simu ikaita Ruby akaipokea
akajulishwa kwamba Edina
hakuwepo ofisini kwake.Ruby
akampigia simu mtu mwingine
akamuita ofisini kwake
akamtaka akamtafute Edina
“Nina wasiwasi kama
atakuwepo bado mahala hapa”
akasema Mathew
“Nilitoa maelekezo
asiondoke mtu yeyote leo
kwenda nyumbani hadi
tuhakikishe tumempata Khalid
hivyo lazima atakuwepo hapa
hapa ndani” akasema Ruby.
“Kwa mujibu wa taarifa
nilizonazo ni kwamba Khalid
anakuja nchini kuonana na
James Kasai.Nashawishika
kuamini kwamba mtandao
huu ambao umemleta nchini
Khalid ndio ambao unamleta
na James Kasai hapa Dar es
salaam.Huyu Edina ni
muhimu sana kwetu kwa sasa
kutusaidia kuufahamu
mtandao huu” akasema
Mathew
“Kwa nini tusimkamate
tukamuweka ndani na
kumfanyia mahojiano ya kina
akateswa na akaeleza kila kitu
anachokifahamu kuhusiana na
mtandao wao na watu
waliomtuma?akauliza Ruby
“Tungeweza kufanya hivyo
lakini tutawastua na
kuwapeleka
mafichoni.Tumfuatilie taratibu
na kwa karibu sana tutafika
hadi kwa watu waliomtuma”
akasema Mathew
Wakati wakiendelea na
mazungumzo mlango wa ofisi
ya Ruby ukafunguliwa
akaingia Yule jamaa ambaye
alitumwa kwenda kumtafuta
Edina.
“Madam nimezunguka kila
kona Edina hayupo” akasema
Yule jamaa
“Una hakika hayumo
humu ndani?Ruby akauliza
“Hayupo.Nimetafuta kila
sehemu hayupo” akajibu Yule
jamaa na kutoka.
“Hayuko hapa.Tayari
amekwisha ondoka” akasema
Mathew
“Ameondokaje?akauliza
Ruby na kuinua simu akapiga
geti kuu akawauliza kama
Edina amepita pale getini
usiku ule na kwenda nje
akajibiwa kwamba hajapita
pale kwani kila anayetoka
lazima apitishe kadi yake ya
ufunguo katika mashine
iliyoko getini.
“Hata geti kuu wanasema
hawajamuona akitoka”
akasema Ruby
“Kuna mageti mangapi
hapa ya kuingia na kutoka?
“Geti lililopo ni moja tu na
ambalo kila mfanyakazi lazima
apite ili ajulikane kama
hayupo au yupo ndani.Kama
hajaonekana getini basi lazima
atakuwa yuko humu humu
ndani’
“Kama yuko humu ndani
yuko wapi?akauliza Mathew
“Hapo ndipo ninapokosa
majibu.Naomba unipe dakika
mbili” akasema Ruby na
kushuka hadi katika ukumbi
ule mkubwa
“Samahani jamani naomba
tusikilizane” akasema Ruby na
watu wote wakaacha kazi
wakamgeukia kumsikiliza
“Kuna mwenzetu mmoja
ambaye haonekani humu
ndani na taarifa ya geti kuu
inaonyesha kwamba hajatoka
anaitwa Edina.Kuna yeyote
anaweza akasaidia kujua
mahala alipo?Kuna yeyote
ambaye amemuona sehemu
yoyote humu ndani?akauliza
Ruby
‘Tafadhali kama kuna
yeyote amemuoa au anajua
mahala alipo anieleze
ninamuhtaji sana kuna kazi ya
muhimu nahitaji kumpatia
sasa hivi” akasema Ruby na
watu wakaanza kuulizana
lakini hakuna aliyefahamu
mahala alipo.
“Kuna yeyote
anayefahamu nyumbani
kwake?akauliza Ruby na watu
zaidi ya watano wakanyoosha
mikono
“Naomba mmoja wenu
anielekeze nyumbani
kwake.Namuhitaji sana”
akasema Ruby na dada mmoja
akamuelekeza mahala
anakoishi Ruby
“Ahsanteni sana.Endeleeni
na kazi zenu.Kumbukeni kabla
ya mapambazuko lazima tuwe
tumempata Khalid Sultan”
akasema Ruby na kurejea
ofisini kwake.
“Mathew uko sahihi.Huyu
Edina hayuko humu
ndani.Tayari amekwisha
ondoka lakini sifahamu
ameondokaje” akasema Ruby
“Yawezekana amekwenda
mahala na atarejea
tena”akasema Mathew
“Nimeelekezwa mahala
anakoishi.Twende tumfuate
nyumbani kwake yawezekana
tukapata kitu muhimu cha
kuweza kutusadia kumfahamu
vyema huyu mtu” akasema
Ruby wakaondoka kuelekea
katika gari lake
SAA MOJA ILIYOPITA
Ofisi kuu ya SNSA ilikuwa
katika heka heka kubwa kila
idara ndani ya ofisi hiyo
wakijaribu kutafuta sababu ya
mawasiliano kukatika ghafla
na kukwamisha zoezi la
kumfuatilia Khalid Sultan
Khalid.Wakati watu
wanaohusika na masuala ya
ufundi wakijitahidi kurejesha
mawasiliano,Edwin akaingia
katika chumba kilichojulikana
kama chumba cha seva
ambamo kulikuwa na
kompyuta nyingi
kubwa.Hakuna aliyemjali kila
mmoja alikuwa anashughulika
akamfuata Edina aliyekuwa
amesimama akiangalia kile
kilichokuwa kinaendelea
akamshika mkono na kumpa
kijikaratasi.Edina akatoka mle
ndani akaenda maliwato
akakikunjua kile kikaratasi na
kukisoma
“Baada ya mawasiliano
kurejea nataka nikupeleke
nyumbani ukahifadhi fedha
zako wakiziona hapa
wataanza kuulizana
ulikozitoa.Jitahidi utokapo
asikuone mtu nenda hadi
katika gari langu fungua
mlango jifiche kiti cha nyuma
halafu utanitumia ujumbe
nitakupeleka nyumbani
ukahifadhi mzigo wako na
kukurudisha” ndivyo
ulivyosomeka ule ujumbe
Mawasilinao yalirejea na
kazi zikaendelea kama kawaida
na baada ya muda mkurugenzi
akawasili na kuzungumza na
wafanyakazi na kisha likaanza
zoezi la kumsaka Khalid
Sultan.Wakati zoezi likindelea
Edina akachukua bahasha
yake iliyokuwa na fedha
akatoka kama vile anaelekea
maliwato na kuelekea moja
kwa moja katika maegesho ya
magari ya wakuu wa
idara,analifahamu gari la
Edwin akafanya kama
alivyoelekezwa akaingia katika
kiti cha nyuma halafu
akamtumia ujumbe Edwin
kumjulisha kwamba tayari
amekwisha ingia garini.Edwin
akamuaga Ruby kisha akatoka
akaingia garini na
kutoka.Baada ya kutoka katika
geti kuu Edina aliyekuwa
amejificha kiti cha nyuma
akaibuka na kukaa
“Ahsante sana Edwin kwa
msaada huu mkubwa”
akasema Edina
“Usijali Dina” akasema
Edwin ambaye alionekana
kutohitaji maongezi akafungua
mziki kwa sauti ya juu
Walifika nyumbani kwa
Edina wakashuka garini,Edna
akamkaribisha ndani
“Edwin karibu ndani
kutana na mdogo wangu
anaitwa Stella.Huyu ndiye
anayesoma chuo kikuu na ile
fedha ni kwa ajili yake”
akasema Edina.Edwin na
Stella wakasalimiana.Dina
akamuandalia Edwin juisi ya
matunda kisha akaelekea
chumbani kuhifadhi zile fedha
“Nimefurahi kuonana
nawe Stella.Dada yako
amekuwa anatueleza sana sifa
zako na bidii yako kubwa
katika masomo” akasema
Edwin
“Nashukuru sana”
akasema Stella.
“Stella naomba maji ya
kunywa tafadhali” akasema
Edwin na Stella akainuka
kwenda kumchukulia Edwin
maji ya kunywa katika friji
mara Edwin akaingiza mkono
katika mfuko wa koti na kutoa
bastora iliyofungwa kiwambo
cha kuzuia sauti na mara tu
Stella alipogeuka akaizinga
bastora na kuachia risasi
iliyompata Stella kati kati ya
paji la uso akaanguka.Sauti ya
glasi kuvunjika ikamstua
Edina aliyekuwa chumbani.
“Stella ! akaita Edina lakini
hakujibiwa akafungua mlango
wa chumba akatoka ili
kuangalia kuna nini akakutana
na risasi mbili zilizompata
katikati ya paji la uso
akaanguka chini.Edwin
akawaongeza tena risasi ili
kuhakikisha hakuna anayebaki
hai kisha akaingia ndani ya
chumba alimotoka Edina
akavaa glovu mikononi
akafungua kabati kubwa la
nguo akafungua droo ndogo
akazikuta fedha ambazo Edina
alikuwa amezihifadhi
akazichukua na kutoka
“I’m sorry Dina” akasema
Edwin na kuchukua simu za
Edina na mdogo wake
akachukua ufunguo akafunga
mlango kwa nje akaondoka.
“Sasa nielekee kwa
Melanie” akawaza Edwin
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 14
Mathew na Ruby
waliwasili katika nyumba
anayoishi Edina.Waliegesha
gari mbele ya nyumba ile
ambayo haikuwa na uzio
wakaelekea mlangoni.Taa ya
nje ilikuwa inawaka Mathew
akagonga mlango lakini
hakujibiwa.Akagonga tena
lakini hakujibiwa.
“Inawezekana hayupo
nyumbani’ akasema Ruby
“Kama hayupo itakuwa
vizuri kwetu,tuingie ndani
pengine tunaweza kupata kitu
cha kutusaidia” akasema
Mathew na kuchukua vifaa
vyake ambavyo humuwezesha
kufungua kitasa au kufuli la
aina yoyote ile kisha
akaufungua ule mlango wa
nyumba ya Edina.
“Jesus Christ ! akasema
Mathew kwa mstuko na kwa
haraka akatoa bastora yake
“Kuna nini
Mathew?akauliza Ruby naye
akaingia ndani
“Edina ?!! akasema Ruby
kwa mstuko.Mathew akaingia
kwa tahadhari katika vyumba
vyote lakini hakukuwa na mtu
yeyote akarejea sebuleni
akaigeuza miili ile ya Edina na
mdogo wake
“Wameuawa usiku huu”
akasema kisha wakaingia
chumbani wakaanza kukagua
kama wangeweza kupata kitu
chochote cha kuwasaidia lakini
hawakupata chochote
wakatoka na kuondoka
“Hawa watu ni wakatili
wakubwa sana.Baada ya
kumtumia Edina wameamua
kumuua kwani waliohofia
labda angeweza
kugundulika.Ni watu wenye
kuchukua tahadhari kubwa
kila wakati.Ruby unapaswa
uwe makini sana kwani watu
hawa wana mtandao mkubwa
na hata idara yako tayari
wameotesha mizizi
yao.Naamini Edina hayuko
peke yale lazima kuna watu
ambao bado wapo ndani ya
idara”
“Mathew nimejikuta
nikiingiwa na woga wa ghafla”
“Usiogope Ruby niko
nyuma yako hakuna yeyote
ambaye atathubutu kucheza na
maisha yako” akasema
Mathew.
“Tunaelekea wapi hivi
sasa? Akauliza Ruby
“Turejee SNSA.Nahitaji
kumuhoji Yule mkuu wa idara
ya ufundi”
“Unadhani kuna kitu
anakifahamu?akauliza Ruby
“Naamini hivyo.Kuna kitu
anakifahamu kuhusu jambo
hili” akasema Mathew
“Itanilazimu kutumia
madaraka yangu ili ukamuhoji
Fidelis kwani wewe si
mfanyakazi wa SNSA lakini ni
vipi endapo hatakuwa
anafahamu chochote? Akauliza
Ruby
“SNSA iko chini ya Rais na
anafahamu hiki
tunachokifanya hivyo hakuna
yeyote atakayekuuliza kitu
chochote.Umepewa madaraka
hivyo lazima uyatumie.Usijali
kuvunja taratibu katika
kutafuta taarifa za muhimu”
akasema Mathew
“Ruby umepewa idara
nyeti sana uiongoze hivyo
jifunze kufanya maamuzi
magumu pale
inapohitajika.Nina uhakika
mkubwa kwamba huyu jamaa
Fidelis kuna kitu anakifahamu
kuhusu hiki kilichotokea.Ruby
idara yako imeingiliwa na
kirusi kibaya sana.Una kazi
kubwa ya kukiondoa kirusi
hicho.Inaonekana tayari
mabeberu hawa wamekwisha
otesha mizizi katika idara yako
na wanaitumia katika
kufanikisha mipango yao na
hii inakuweka katika hatari
kubwa sana lakini usihofu
nitakulinda” akasema Mathew
“Kwa hiki kilichotokea leo
ninaamini hicho
ukisemacho.Idara hii
ilianzishwa kwa ajili ya
usalama wa ndani wa nchi
lakini naweza sema kwamba
bado haijafanya kazi yake ile
inayotakiwa.Imekuwa
ikitumiwa katika kufanikisha
mipango mbali mbali miovu
dhidi ya nchi yetu na mkosi
ulianzia kwa Devotha.Kama
utakumbuka huyu alikuwa ni
wakala wa Mossad hapa nchini
na ikaendelea hivyo hadi kwa
aliyefuata aliitwa Tamar.Kuna
kazi kubwa ya kuisafisha idara
hii ili ifanye kazi
iliyokususdiwa”akasema Ruby
“Umemtaja Devotha
umenikumbusha mbali
sana.Yuko wapi Yule
mwanamke?akauliza Mathew
“Sifahamu yuko wapi
labda wale walioko hapa
nchini Gosu Gosu na Austin
wanaweza wakafahamu
mahala alipo.Sitaki kabisa
kufahamu chochote kuhusu
Yule mwanamke ninamchukia
sana alitaka kuniua pasi na
kosa” akasema Ruby na
ukimya ukapita
“Najaribu kujiuliza Edina
ametokaje pale ofisini wakati
kuna geti moja tu? Nani
kamuua? Akasema Ruby
“Usiumize sana kichwa
Ruby niachie jambo hilo
tutapata majibu yake”
akasema Mathew
“Tumekuwa na mambo
mengi sana hata nimesahau
kuuliza kuhusu Peniela.Nini
kilitokea?Alikueleza chochote
kuhusu Melanie Davis? Halafu
mbona kaondoka haraka
namna hiyo?Nilitegemea
angelala hapa Dar es salaam
kwa mume wake” akasema
Ruby
“Peniela alikuja kwa jambo
moja tu” akasema Mathew na
kunyamaza kidogo
“Alikuja kuhitimisha ndoa
yetu.Mimi naye basi tena”
“Mmeachana?! Ruby
akashangaa
“Ndiyo” akajibu Mathew
na kumsimulia Ruby kila kitu
kilichotokea kati yake na
Peniela
“Mathew I’m so sorry.I
don’t know what to say”
akasema Ruby
“Usijali Ruby haya ni
mapito katika maisha”
“Sikutegemea kama
mambo yangekuwa namna
hii.Lakini Peniela amechukua
maamuzi ya haraka sana”
akasema Ruby
“Simlaumu Peniela kwa
maamuzi aliyoyachukua kwani
yote haya nimeyataka mimi
mwenyewe.Nilichagua kazi
badala ya
familia.Nimewaumiza sana
ana haki ya kuendelea na
maisha yake bila
mimi.Anahitaji mtu ambaye
atampa furaha katika maisha
yake jambo ambalo mimi
nimeshindwa.Haya ndiyo
maisha yangu na lazima
niyakubali” akasema Mathew
“Kikubwa ambacho
ninashukuru ameahidi
kunisaidia kutafuta taarifa za
Melanie Davis.Kama
akilifanikisha hilo atakuwa
ametusaidia jambo kubwa
sana” akasema Mathew
“Mathew you are mine
now.Hakuna yeyote au
chochote cha kunitenganisha
nawe.Mimi ndiye hasa
ninayestahili kuwa nawe.Mimi
ndiye Yule ambaye niliumbwa
kwa ajli yako.Ninakupenda
zaidi ya ninavyojipenda
mwenyewe.Ahsante Peniela
kwa maamuzi haya
uliyoyachukua ambayo
yameniachia mimi uwanja wa
kutawala.Sasa mpira uko
kwangu na katu siwezi
kushindwa kufunga” akawaza
Ruby
Walifika ofisi kuu ya SNSA
wakaelekea ofisini kwa Ruby
ambaye bila kuchelewa
akapiga simu idara ya usalama
ndani ya SNSA akawataka
wamchukue Fidelis wampeleke
katika chumba cha mahojiano
namba 2 halafu akaelekeza
kamera zote katika chumba
hicho cha mahojiano namba
mbili zizimwe.Baada ya dakika
chache akataarifiwa kwamba
Fidelis tayari amepelekwa
katika chumba cha mahojiano
“Mathew mtu
unayemuhitaji tayari
amekwisha pelekwa katika
chumba cha mahojiano”
akasema Ruby na kumuongoza
Mathew hadi katika chumba
alimowekwa Fidelis.Mlinzi
aliyekuwa mlangoni
akaufungua mlango Ruby na
Mathew wakaingia. Ruby
akachomoa nyaya zote
zilizounganishwa na kamera
kwa tahadhari kwani
hakuwaamini wafanyakazi wa
idara ile.
“Mathew he’s all yours”
akasema Ruby.Mathew
akavuta kiti na kuketi.
“Madam what’s going on?
Who is this guy? akauliza
Fidelis
“My name is Mathew
Mulumbi.Nitakuuliza maswali
naomba unijibu kwa usahihi”
akasema Mathew
“Huwezi ukaniuliza
chochote.Wewe si mfanyakazi
wa hapa na siwezi kukujibu
chochote.Madam nini
kinaendelea hapa?Kwa nini
umenileta hapa?akauliza
Fidelis na kutaka kunyanyuka.
“Sit down ! akasema
Mathew kwa ukali
“I’m not going to sit
down.Wewe ni nani wa kunipa
amri…aaaagghhhh !!!.” Fidelis
hakumaliza sentensi yake
akajikuta chini baada ya
kupigwa kofi zito.Mathew
akamfuata pale chini
alipoanguka na kumtaka
ainuke aketi kitini.Bila ubishi
Fidelis akainuka na kuinua kiti
ambacho nacho kilikuwa
kimeanguka akaketi
“Jina lako nani?akauliza
Mathew
“Fidelis Makweba”
“Unashughulika na nini
hapa SNSA?akauliza Mathew
“Mimi ni mkuuwa idara ya
ufundi ambayo kazi yetu ni
kuhakikisha mifumo yetu yote
inakuwa salama muda wote na
kompyuta zote zinakuwa
katika hali nzuri” akajibu
Fidelis.
“Usiku wa leo wakati wa
zoezi la kumfuatilia Khalid
likiendelea mawasiliano
yalikatika kati ya ofisi kuu na
watu wetu waliokuwa
barabarani.Nini kilisababisha
hali ile kutokea?akauliza
Mathew na Fidelis akaanza
kuelezea kiufundi tatizo
lililotokea
“Hata mkurugenzi aliniita
akaniuliza nikamueleza kila
kitu kuhusiana na hiki
kilichotokea” akasema Fidelis
na Mathew akamgeukia Ruby
“Fidelis maelezo uliyonipa
hayana ukweli
wowote”akasema Ruby na
Fidelis akaonyesha mstuko
mkubwa.Ruby akaanza kumpa
maelezo kuhusiana na kile
kilichotokea.Matone ya jasho
yakaonekana usoni kwa Fidelis
“Wewe kama fundi mkuu
lazima ufahamu kitu hiki”
akasema Ruby na kuhitimisha
maelezo yake
“Umesikia alichokisema
mkurugenzi
wako.Unakubaliana na
maelezo yake?akauliza
Mathew na Fidelis akawa
kimya.Alijaribu kufungua
midomo ikabaki inamcheza
“Ukimya wako ni jibu
kwamba alichokisema
mkurugenzi wako ni kitu cha
kweli kabisa” akasema Mathew
na kumtazama Fidelis
“Khalid Sultan Khalid ni
mtu hatari sana ambaye
amekuja nchini kwa lengo la
kupanga shambulio
kubwa.Idara yenu imefahamu
kuhusu ujio wake na kuweka
mikakati ya kumfuatilia kujua
alichokuja kukifanya hapa
nchini vile vile kuwafahamu
washirika wake.IS wana mzizi
wao hapa nchini na sasa
wanataka kusambaa katika
bara zima la Afrika.Operesheni
ile ya kumfuatilia Khalid
ingetuwezesha kuwafahamu
washirika wake na mtandao
mzima wa IS hapa nchini
lakini kwa makusudi kabisa
umeshiriki katika kukwamisha
zoezi lile la kumfuatilia Khalid
na sasa hatujui yuko wapi wala
washirika wake ni akina
nani.Kwa hiki ulichokifanya
umeiweka nchi katika hatari
kubwa na unajua adhabu
wanayopewa watu kama wewe
ambao wanahatarisha usalama
wa nchi.Fidelis ninataka
nikusaidie kukuondoa katika
kitanzi hiki ulichojivisha lakini
hadi pale utakaponieleza
ukweli wote.Kwa nini ulisema
uongo kuhusu tukio lile?Kwa
nini ulimdanganya mkurugezi
wako? Tuanzie hapo” akasema
Mathew.Fidelis hakujibu kitu
alibaki kimya
“Fidelis muda unakwenda
naomba tafadhali unijibu
maswali niliyokuuliza”
akasema Mathew Fidelis
hakujibu kitu
“Fidelis nafahamu hauko
peke yako katika jambo
hili.Nani wengine ulishirikiana
nao?akauliza Mathew lakini
bado Fidelis aliendelea kuwa
kimya
“Fidelis unapokaa kimya
unazidi kupoteza nafasi ya
kusaidiawa” akasema Mathew
“Labda ngoja
nikufahamishe kitu
Fidelis.Tatizo hili lilianzia
stesheni 5 ambayo ni ya
Edina.Naamini jambo hii
ulilifahamu vizuri lakini
ukakubali kupindisha
ukweli.Kwa taarifa yako ni
kwamba baada ya kugundua
kwamba ni Edina ambaye
alifanya kitendo kile nilianza
kumtafuta bila mafanikio
nikaamua kumfuata nyumbani
kwake nimekuta
ameuawa”akasema Ruby na
sura ya Fidelis ikaonyesha
mstuko mkubwa
“Watu waliomtumia Edina
wamemuua kikatili.wewe
unayo nafasi nzuri ya
kusaidiwa yasikukute kama
yaliyomkuta Edina lakini
tutakusaidia tu pale ambapo
utatueleza ukweli nani
alikutuma useme uongo
kuhusiana na tukio
lile?akauliza Mathew na
Fidelis alionyesha uoga
mkubwa
“Fidelis hii ni nafasi pekee
ya kukuokoa umeipata na
kama ukishindwa kuitumia
basi tutakukabidhi kwa
vyombo vya dola ufunguliwe
mashtaka ya kuhatarisha
usalama wa taifa.Naomba
ufunguke tafadhali” akasema
Mathew lakini Fideli bado
alikuwa kimya
“Fidelis una
watoto?akauliza Mathew na
swali lile likaonekana kumstua
Fidelis na akaikumbuka sauti
ya Edwin masikioni
“Endapo ukithubutu
kufunguka na kusema ukweli
kuhusiana na tukio hili
hutaiona tena familia yako !
Fidelis aliyakumbuka
maneno haya aliyoambiwa na
Edwin akahisi baridi
“Fedha alizonipa Edwin
zimeniponza natamani
niwaeleze ukweli hawa watu
lakini nahofia familia yangu
kwani Edwin alinionya
nisithubutu kusema ukweli
kuhusu jambo lile kwani ama
sivyo nitaikosa familia yangu.
Natakiwa kuendelea na
msimamo wangu wa
kutokusema chochote.Mambo
tayari yameshaharibika”
akawaza Fidelis
“Fidelis ninaanza
kuchoshwa na tabia yako ya
kujifanya bubu.Hii ni mara ya
mwisho ninakuuliza nani
waliokutuma useme uongo
kuhusu kukatika kwa
mawasiliano katika zoezi
muhimu? akauliza Mathew
bado Fidelis alikuwa kimya
“Hujanifahamu vyema
kijana, mimi huwa sipendi
mzaha ninapokuwa kazini”
akasema Mathew na
kunyanyuka akamfuata Fidelis
akamuinua akampeleka katika
nguzo akachukua kamba
akamfunga mikono nyuma ya
nguzo na miguu akaikaza
barabara kwa kamba.
“Kwa kuwa umekataa
kufunguka kwa njia ya amani
sasa tunaingia katika njia ya
pili ya kutumia nguvu.Kabla
sijaanza zoezi langu ninakupa
nafasi ya mwisho ya kunieleza
ukweli” akasema
Mathew.Fidelis alikuwa
anatetemeka mwili lakini
hakusema chochote.Bado
aliendelea na msimamo wake
wa kukaa kimya.Mathew
akachukua kopo dogo la gesi
akaliwasha kisha akaanza
kuunguza vidole vya mikono
“Aaaaaaghhhh !! Fidelis
akapiga ukulele mkubwa
“Nani alikutuma?akauliza
Mathew lakini Fideli hakujibu
kitu aliendelea kulia huku
akihisi maumivu
makali.Mathew akamchoma
tena na gesi lakini bado Fidelis
aliendelea kugugumia
maumivu makali bila kusema
chochote
”This isn’t working”
akasema Mathew na kuchukua
mashine ndogo ya umeme.
“Fidelis mimi ni mtu
mbaya sana kama ukinifanyia
mchezo.Unaonekana
kunichezea na mimi sitaki
mchezo” akasema Mathew na
kuiwasha mashine ile
akamchoma Fidelis kwa
umeme akaanza kutetemeka
Mathew akaizima
“Uko tayari kuzungumza?
akauliza Mathew lakini Fidelis
aliendelea kuwa kimya
“Huyu bazazi anacheza na
mimi” akawaza Mathew na
kuitupa ile mashine ya umeme
“C’mon Fidelis tell me the
truth !! akasema
Mathew.Fidelis hakufumbua
mdomo wake kutamka
chochote.Mathew akazidi
kukasirika akaanza
kumporomoshea Fidelis
magumi mazito sehemu mbali
mbali za mwili wake.Ndani ya
muda mfupi uso wa Fidelis
haukuwa ukitazamika ulikuwa
umeloa damu.Ruby akamfuata
na kumzuia Mathew
asiendelee kumpiga
“Mathew
imetosha.Umekwisha
muumiza sana.Bado
tunamuhitaji atupe taarifa
muhimu” akasema Ruby.Bado
Mathew aliendelea kumtazama
Fidelis kwa hasira.
“Fidelis ! Fidelis ! akaita
Ruby lakini Fidelis hakuitika
alikuwa anamwagika damu
mdomoni na alionekana hana
fahamu.Haraka haraka Ruby
akafungua mlango na kumtaka
Yule mlinzi aliyekuwa
mlangoni akawaite watu wa
afya haraka sana.
“Mathew ulitaka kumuua
kabisa huyu mtu” akasema
Ruby
“Bado nina hasira
naye.Hawajui nimepitia
mambo gani hadi kufanikiwa
kuipata taarifa ile muhimu ya
Khalid lakini kwa fedha chache
wanazopewa wanadiriki
kuvuruga misheni yetu na
kuhatarisha usalama wa
nchi.Watu kama hawa si wa
kuwavumilia hata kidogo !
akafoka Mathew
Mlango ulifunguliwa na
watu wanne wakaingia wakiwa
na machela.Wakamfungua
Fidelis wakampakia katika
machela na kuondoka naye.
“Mathew nafahamu una
hasira sana na watu hawa
lakini nakuomba jitahidi
kujizuia kutumia nguvu
kupitiliza kwani ugeweza
kumuua Fidelis na ungeniweka
mimi katika matatizo”
akasema Ruby
“I’m sorry.Ni kweli
nilikuwa na hasira naye
sana.Huyu jamaa anafahamu
kila kitu lakini anaogopa
kusema.Yuko tayari kuvumilia
mateso makali kwa ajili ya
kuwaficha watu hao
waliomtuma” akasema
Mathew
“Baada ya kushindwa
kupata taarifa kutoka kwa
Fidelis nini
kinaendelea?akauliza Ruby
“Tayari tunaye mtu
ambaye anahusika katika
mpango ule wa kuvuruga zoezi
la kumfuatilia Khalid.Fidelis
anafahamu nani aliyemtuma
lakini anamficha.Kwa sasa
yeye ndiye pekee anayeweza
kutueleza ukweli.Tumsubiri
atakapozinduka tutaendelea
naye lazima atueleze kila kitu
anachokifahamu” akasema
Mathew
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 15
Mishale ya saa ilizidi
kuyoyoma na nyumbani kwa
Melanie Davis bado kikao
kiliendelea.Melanie na James
Kasai walimueleza Khalid
Sultan Khalid mpango wao wa
kuwaua marais wawili kwa
kutumia bomu.Khalid baada
ya kuyasikia mawazo yao
aliyakubali na kukubaliana na
pendekezo lao kwamba bomu
litakalotumiwa kuwaua marais
hao wawili liwe la kujitoa
mhanga.Alieleza aina ya bomu
linalohitajika,namna
atakavyolitengeneza na
madhara yakayoweza kuletwa
na hilo bomu.Baada ya watu
wote kuzungumza juu ya
nafasi zao katika mpango ule
ikafuata zamu ya Edwin
Mbeko.Huyu ndiye ambaye
alitegemewa kumaliza mchezo
wote .Mpango ule wote
ulimtegemea yeye ili ukamilike
“Katika kuukamilisha
mpango huu nitafanya
hivi.Nitahitaji mtu kwa ajili ya
kujitoa mhanga.Mtu huyo
ataingizwa uwanja wa ndege
akiwa amevaa mavazi ya askari
wa kutuliza ghasia.Mara nyingi
askari hawa huvaa fulana nene
za kujikinga na risasi lakini
huyu wa kwetu fulana yake
haitakuwa kwa ajili ya
kujikinga na risasi bali
litakuwa ni bomu.Hakuna
ambaye atamtilia shaka mtu
huyo kuwa si askari hivyo
atajitahidi kuwasogelea marais
na akiwakaribia umbali Fulani
atajilipua” akasema Edwin na
kufafanua namna
atakavyomuingiza ndani ya
uwanja mtu huyo atakayevaa
mavazi ya askari polisi na
kubeba bomu.Kila mmoja
akatoa mawazo yake
kuhusiana na wazo lile la
Edwin na baada ya
majadiliano wakafikia
makubaliano.Khalid aliahidi
kumleta haraka sana nchini
mtu ambaye angeweza kubeba
bomu hilo na kujitoa
mhanga.Baada ya kufikia
makubaliano Edwin Mbeko
akaondoka kurejea ofisi kuu ya
SNSA.
Mara tu alipoingia ndani
ya ofisi zao akakutana na hali
isiyo ya kawaida.
“Kuna nini hapa?Mbona
watu wako namna hii?akauliza
Edwin na kuelezwa kile
kilichomtokea Fidelis.Edwin
akahisi miguu ikimtetemeka
kwa mstuko
alioupata.Hakutegemea kama
Fidelis angeweza
kugundulika.Akaelekea ofsini
kwake na kukaa juu ya meza
“Huyu mwanamke
amegunduaje kama Fidelis
anafahamu kilichotokea?Kama
ameweza kugundua
mawasiliano yalikatwa
makusudi basi lazima atakuwa
amefahamu nani aliyefanya
hicho kitendo.Nilifanya jambo
zuri sana kumuua Edina.Kwa
sasa natakiwa kumuondoa
Fidelis pia halafu nianze
kushughulika na huyu
mwanamke kwani
nisipomshughulikia mapema
anaweza akaharibu mipango
yetu yote” akawaza Edwin na
kuelekea sehemu ya afya
alikokuwa amelazwa
Fidelis.Tayari alikwisha pata
fahamu na Edwin alipoingia
akamtambua mara moja
“Fidelis ! akasema Edwin
“Edwin ! akasema Fidelis
kwa sauti dhaifu.
“Nini kimetokea
Fidelis?akauliza Edwin
“Annabel anafahamu..aagh
! akasema huku akigugumia
kwa maumivu
“Anafa…fahamu kila kitu”
akasema Fidelis
“Umemueleza chochote?
Akauliza Edwin na Fidelis
akatingisha kichwa kukataa
“Vizuri sana.Nimekwisha
ita gari la wagonjwa linakuja
tunakupeleka hospitali kuu ya
Mtodora ukapate matibabu
makubwa” akasema Edwin
kisha akafungua mlango
akachungulia nje kama kuna
mtu halafu akarejea ndani
akachukua mto
akamgandamiza Fidelis kwa
nguvu pale kitandani.Fidelis
alianza kuhangaika kutafuta
hewa lakini tayari mwili wake
ulikwisha kuwa dhaifu hivyo
hakuweza kushindana na
Edwin.Baada ya muda Fidelis
akatulia Edwin akatoa ule mto
na kumtazama tayari Fidelis
hakuwa na uhai.
“I’m sorry Fidelis”
akasema Edwin na kuweka
kitanda vizuri halafu
akafungua mlango na kutoka
mbio akiita madaktari ambao
walifika kwa haraka sana
kuangalia kuna nini.Haraka
haraka wakampima lakini
tayari Fidelis alikwisha
fariki.Edwin akionekana kuwa
na hasira akaelekea katika
ukumbi ambako kazi zilikuwa
zinaendelea.
“Naombeni mnisikilize
ndugu zangu ! akasema Edwin
na watu wote wakamgeukia.
“Kuna taarifa mbaya
nimewaleteeni.Mwenzetu,ndu
gu yetu Fidelis amefariki dunia
muda mfupi uliopita ! Sura
zote zikaonyesha mstuko
mkubwa kwa taarifa ile
“Nimejulishwa kwamba
mkurugenzi wetu mpya akiwa
na mtu ambaye ameambatana
naye ambaye si mfanyakazi wa
idara yetu walimuita Fidelis
katika chumba cha mahojiano
na kisha wakamlazimisha
aseme tukio lile la kukatika
kwa mawasiliano lilifanywa
makusudi.Fidelis alikataa na
ndipo alipoanza kupigwa.Huu
ni unyama mkubwa
amefanyiwa Fidelis.Mkurugezi
amevunja kanuni za idara
kwanza kwa kumuingiza
ofisini mtu ambaye si
mfanyakazi wa idara hii ya siri
ya serikali lakini pili mtu huyo
ambaye hatumfahamu ni nani
amesababisha kifo cha
mwenzetu.Hatuwezi kulikubali
jambo hili.Mkurugenzi huyu
ana siku ya pili katika ofisi na
tayari ameanza kuleta humu
ndani watu wasiohusika nina
mashaka naye sana kama
anaweza akaongoza idara hii
nyeti kabisa kwa nchi.Ndugu
zangu nchi kwa sasa
inatutegemea sana sisi hivyo
hatuwezi kuongozwa na mtu
kama huyu katika wakati
huu.Kanuni zetu ziko wazi
kwamba wafanyakazi wa idara
wanao uwezo wa kumuondoa
katika ofisi kwa muda wa siku
saba mkuu wa idara endapo
ataonekana kushindwa
kumudu majukumu yake
vyema au kuvunja kanuni na
taratibu za idara au kuwa
kikwazo katika kufanikisha
mambo muhimu kwa usalama
wa nchi.Katika siku saba hizo
suala la kuondolewa ofisini
mkuu wa idara litafikishwa
kwa Rais kujadiliwa na kisha
kutolewa maamuzi.Nyote
mnazo kanuni na
mnazifahamu hivyo basi kwa
kitendo alichokifanya
mkurugenzi leo amevunja
kanuni na kukwamisha zoezi la
kumtafuta Khalid Sultan kwani
Fidelis ni mmoja wa watu
ambao tunawategemea sana
hapa katika idara.Hata
lilipotokea lile tatizo la
kukatika kwa mawasiliano
yeye ndiye aliyeshughulika na
timu yake na wakafanikiwa
kurejesha tena
mawasiliano.Ninawaomba
mniunge mkono tumuondoe
mkurugenzi katika nafasi yake
mara moja ili zoezi la
kumtafuta Khalid liendelee
usiku huu” akasema Edwin na
watu wote wakaonekana
kukubaliana naye.
“Ahsanteni sana kwa
kuniunga mkono.Sasa
ninakwenda kumuondoa
mkurugenzi ili asiendelee
kutuvuruga” akasema Edwin
na kuelekea katika ofisi ya
Ruby
Ruby akiwa katika ofisi
yake na Mathew alijulishwa na
daktari mkuu wa idara
kwamba Fidelis amefariki
dunia.Ilikuwa ni taarifa
iliyomstua sana Ruby na
kumfanya aweke mezani
mkono wa simu
“Kuna nini Ruby mbona
umestuka sana?
“Nimetaarifiwa na daktari
mkuu kwamba Fidelis
amefariki dunia”
“That’s not true !
“Ni kweli Mathew.Fidelis
amefariki dunia” akasema
Ruby
“Imetokeaje?Nini
kimesababisha kifo
chake?akauliza Mathew na
kabla Ruby hajajibu mlango
ukafunguliwa akaingia Edwin
Mbeko akiwa ameongozana na
watu wanne wenye silaha
“Edwin umerejea.Mambo
yamekwendaje huko?Kuna
mafanikio yoyote?akauliza
Ruby
“Madam Annabel sijaja
hapa kwa ajili ya jambo hilo”
akasema Edwin na Ruby
akaonekana kukasirika
“Nini kimekuleta hapa
basi?
“Madam naamini umepata
taarifa za kifo cha ghafla cha
Fidelis mmoja wa wataalamu
wetu mahiri kabisa ambaye
amekuwa na mchango
mkubwa mno katika
kufanikisha shughuli zetu
mbali mbali”
“Ndiyo nimejulishwa”
“Nimejulishwa kwamba
kifo cha Fidelis
kimesababishwa na kipigo
ambacho wewe na huyu mtu
wako mmempiga” akasema
“Edwin hukuwepo ofisini
wakati jambo hilo linatokea
hivyo basi unatakiwa utulie
uulize na ueleweshwe nini
kimetokea?akasema Ruby
“Madam sina muda wa
kuuliza wakati kila kitu kiko
wazi nimekuja hapa kwa
jambo moja tu.Kwa niaba ya
wafanyakazi wengine wa idara
hii nimetumwa kukujulisha
kwamba kwa kitendo hiki
ulichokifanya leo umevunja
kanuni kwanza kwa
kumuingiza ndani ya ofisi hii
nyeti mtu ambaye si
mfanyakazi wa idara.Hilo ni
moja ya jambo lisiloruhusiwa
kabisa kwani ofisi hii ina siri
nyingi za nchi.Pili kwa
kusababisha kifo cha
mfanyakazi wa idara.Kwa
mujibu wa kanuni zetu
wafanyakazi wanayo madaraka
ya kumuondoa mkurugenzi
katika ofisi yake kwa siku saba
hivyo kwa kutumia kanuni
zetu kwa niaba ya wafanyakazi
wote ninakuondoa katika
nafasi yako na suala lako
linapelekwa kwa Rais kwa ajili
ya maamuzi.Kuanzia sasa
kabidhi kila kitu cha idara na
hutakiwi kuonekana hapa
katika idara kwa muda wa siku
saba na utarejea hapa pale
Rais atakapokwambia hivyo”
akasema Edwin na Ruby
akacheka kidogo
“You can’t be serious
Edwin”
“I’m very serious madam”
akasema Edwin
“Aliyeniweka katika nafasi
hii ni Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania wewe
huna mamlaka yoyote ya
kuniondoa mimi katika nafasi
yangu ! akasema Ruby
“Ni kweli madam sina
uwezo huo lakini kanuni
ambazo zimetiwa saini na Rais
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania ndizo
zinazokuondoa”
“No I won’t leave !
akasema Ruby kwa ukali
“Madam tafadhali
usisababishe nguvu ikatumika
kwani kanuni zinaelekeza
nguvu inaweza ikatumika vile
vile kukuondoa.Tafadhali
kabidhi kila kifaa cha idara
sasa hivi” akasema Edwin
“Just do it ! Mathew
akamwambia Ruby
“No I can’t ! akasema Ruby
“Wape kila kitu chao
tuondoke hapa kwa amani”
akasema Mathew na Ruby
akatoa kadi yake ya ufunguo
bastora na vifaa vingine
akaviweka mezani
“Ahsante sana madam
Annabel” akasema Edwin
huku akikusanya vifaa
vile.Ruby akaichukua
kompyuta yake na kuiweka
katika mkoba.
“Madam kopyuta hiyo
huwezi ukaichukua hadi
ikaguliwe tujiridhishe kama
haina siri za idara” akasema
Edwin
“Nimekuwa hapa siku
mbili tu sina siri zozote za
idara” akasema Ruby kwa
ukali
“Huo ni utaratibu madam”
akasema Edwin
“Ruby pakia kompyuta
yako na vifaa vyako vingine
tuondoke ! akasema Mathew
“And you,who are you?
Akauliza Edwin huku
akimtazama Mathew kwa
hasira
“Mimi ni mtu ambaye
hupaswi kumfahamu ! akajibu
Mathew
“Usijibu kwa dharau
ndugu ninao uwezo wa
kuamrisha ukawekwa ndani
sasa hivi.Wewe si mfanyakazi
wa hapa na huruhusiwi
kuwepo katika ofisi hii !
akafoka Edwin
“Bwana mdogo
usinijaribu.Sipendi kujaribiwa
! akasema Mathew kwa ukali
huku akimsogelea Edwin
“Okay guys tusilifanye
suala hili likawa kubwa.Edwin
the office is yours now.Please
make sure you find Khalid
Sultan” akasema Ruby
“Yes madam we will find
him” akajibu Edwin
“Thank you for
everything.I hope we’ll meet
again soon” akasema Ruby na
kumshika Mathew mkono
wakatoka.Hakumuaga
mfanyakazi yoyote wa idara ile
wakaelekea hadi katika gari
lake wakaingia na kuondoka.
“Mathew mimi sijaelewa
hiki kilichotokea ! Bila wewe
kunilazimisha nikubali kamwe
sikuwa tayari kutoka mle
ofisini.Nimepewa ofisi na Rais
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania nawezaje
kuondolewa kienyeji namna
hii na mtu asiye na hadhi
yoyote?akauliza Ruby akiwa
amekasirika.
“Ruby ni kweli umepewa
ofisi na Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania lakini
idara hii ya SNSA tayari
imekwisha ota mzizi mkubwa
wa mabeberu na umeondolewa
makusudi kabisa kwani tayari
umeanza kuonekana kikwazo
kwao.Zoezi la kumfuatilia
Khalid limekwamishwa
makusudi kabisa na aliyefanya
kitendo kile ameuawa.Pili ni
kifo cha Fidelis.Nina mashaka
sana kama kipigo kile
nilichompiga ndicho
kimesababisha kifo chake”
“Unadhani Fideli
ameuawa?akauliza Ruby
“Ndiyo.Yeye pia
aliufahamu ukweli kuhusiana
na kukatika kwa mawasiliano
wakati wa lile zoezi la
kumfuatiliaKhalid na kama
ilivyokuwa kwa Edina naye pia
ilibidi aondolewe haraka.Nina
uhakika mkubwa
ameuawa.Ninayafahamu haya
mambo” akasema Mathew
“Wameamua kutumia
kanuni ili kukuondoa na
mipango yao
iendelee.Nilikwisha liona hilo
na ndiyo maana nikakutaka
ukabidhi kila kitu chao na
tuondoke kwani bila kufanya
hivyo yangeweza kuibuka
mambo mengine makubwa
zaidi.SNSA ya sasa si ile
ambayo ilianzishwa kwa
malengo ya kulinda usalama
wa nchi.Imekuwa ni sehemu
ya kuhatarisha usalama wa
nchi na hilo limedhihirika
usiku wa leo.Zoezi muhimu
sana la kumfuatilia Khalid
limeshindwa kufanikiwa.Edina
na Fidelis hawako peke yao
ndani ya SNSA lazima upo
mtandao mkubwa”
“Sasa tutafanye nini
Mathew? Rais atanielewaje
akisikia hiki kilichotokea?
“Rais anakuamini sana
lakini kwa misheni hii
tutaiendesha sisi wenyewe bila
kutegemea SNSA.Tutamsaka
Khalid na kuhakikisha
tunampata vile vile James
Kasai.Nina uhakika mkubwa
tutawapata naomba uniamini”
“Mathew ninakuamini
sana lakini hapa tulipo
tumekwama.Tutawezaje
kujikwamua kutoka katika
mkwamo huu?akauliza Ruby
“Ahsante kwa
kuniamini.Endelea kuniamini
na tutalimaliza suala hili”
akasema Mathew
Mara tu baada ya Mathew
na Ruby kuondoka,Edwin
akampigia simu Dr Fabian
Kelelo akamjulisha kile
kilichotokea na hatua
walizozichukua kuhusu Ruby
lakini hakumueleza kitu
chochote kuhusu Khalid.
“Edwin kwa nini
ukachukua maamuzi kama
hayo bila kunishirikisha
kwanza mimi?akauliza kwa
ukali Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
nililazimika kufanya vile kwa
sababu tayari wafanyakazi
walikwisha goma kuendelea
kufanya kazi na madam
Annabel.Hata kanuni zinaeleza
hivyo mheshimiwa rais”
akasema Edwin na Dr Fabian
akashusha pumzi
“Sawa niachie suala hili
nitalishughulikia kama kanuni
zinavyoelekeza” akasema Dr
Fabian na kukata simu
akampigia Ruby
“Rais anapiga simu” Ruby
akamwambia Mathew
“Tayari amekwisha elezwa
kila kitu na Edwin” akasema
Mathew na kumtaka Ruby
apokee ile simu
“Mheshimiwa Rais”
akasema Ruby
“Ruby nimepokea simu
kutoka kwa Edwin muda
mfupi uliopta amenipa
maelezo ambayo yamenistua
sana.Nini hasa kimetokea?
“Mheshimiwa Rais kwa
sasa siwezi kukueleza chochote
naomba unipe muda ili
nikutane nawe tuzungumze
kuhusiana na suala hili”
“Alichokisema Edwin
kwamba umesababisha kifo
cha mfanyakazi wa SNSA
ukishirikiana na mtu ambaye
si mfanyakazi wa idara ni
kweli?
“Ni kweli mheshimiwa
Rais” akasema Ruby
“Kwa nini Ruby?Kwa nini
ukafanya hivyo?Alichokifanya
Edwin ni kitu sahihi
kabisa.Ulivunja kanuni na
wakalazimika kukuondoa
kwani wafanyakazi wote
hawakuwa tayari kuendelea
kufanya kazi nawe.Hata hivyo
niachie suala hili
nitalishughulikia.Kanuni
zinasema ni siku saba utakaa
nje ya ofisi na baada ya hapo
utarejea kazini”
“Sawa mheshimiwa Rais
nitasubiri kwa siku hizo saba”
“Ni nani uliyekuwa naye
ofisini ambaye anatajwa
kushiriki kumuua mfanyakazi?
“Ni Mathew Mulumbi
mheshimiwa Rais?
“Mathew Mulumbi !! Dr
Fabian akashangaa
“Ndiyo mheshimiwa Rais
nilikuwa na Mathew”
“Huyu mtu ametokea wapi
na kuja kuleta matatizo
makubwa namna hii?Kila
sehemu alipo huyu jamaa ni
matatizo matupu ! I’m sorry to
say this but I don’t like that
guy ! akasema Dr Fabian kwa
ukali na ukapita ukimya kisha
akasema
“Nenda kapumzike Ruby
tutazungumza zaidi
kesho.Nitahitaji nisikie pia
upande wako kujua nini hasa
kilitokea”akasema Dr Fabian
na kuagana na Ruby
Mathew na Ruby walifika
nyumbani tayari ilikwisha
kuwa usiku mwingi.Wakati
Ruby akiwa bafuni anaoga
Mathew akaenda ofisini kwake
akafungua kasiki akatoa
kompyuta yake na kumpigia
simu Habiba Jawad
“Mathew habari
yako.Unaonekana umechoka
sana leo” akasema Habia
“Ni kweli mama siku
imekuwa ndefu sana na
mambo yaliyojitokeza ni mengi
pia”
“Naamini umefanikiwa
kumuona Khalid na
kumfuatilia” akasema Habiba
“Kuna tatizo limejitokeza
mama wakati wa kumfuatilia
Khalid” akasema Mathew na
kumsimulia Habiba
kilichotokea
“Mathew usalama wa nchi
yako uko hatarini hivi sasa.IS
wanapanga kufanya shambulio
kubwa lakini bado sijajua ni
shambulio gani na wapi lakini
fahamu kuna shambulio
kubwa linaandaliwa.Misheni
hiyo niliyokutuma ni mtihani
kwako kwani ukifaulu basi
utakuwa umefuzu kwenda
kufanya misheni nyingine
kubwa zaidi.Endapo
utashindwa na IS
wakishirikiana na James Kasai
wakafanikiwa kutekeleza
shambulio lao utanipa
mashaka kama utaweza
misheni nyingine kubwa
inayokusubiri.Hawa jamaa
wana mtandao mkubwa sana
usimuamini mtu yeyoe
kuanzia sasa.Fanya wewe
mwenyewe kila
kitu.Umenielewa Mathew?
“Nimekuelewa mama”
“Vizuri.Nategemea kesho
utakaponipigia simu uwe na
majibu mazuri ya
kunipa.Ninataka uonyeshe
umahiri wako na usitegemee
mimi kukupa kila taarifa”
“Nimekuelewa mama”
akasema Mathew na kuagana
na Habiba
“Habiba Jawad yuko
sahihi.Nimetetereka
sana.Natakiwa kurudi kuwa
Mathew Mulumbi wa kipindi
kile.Mambo yaliyotokea leo
hayakupaswa
kutokea.Nilipaswa hadi muda
huu niwe tayari na taarifa za
mahala alipoKhalid na kama
James Kasai amekwisha ingia
nchini lakini mpaka sasa sina
taarifa zozote .Sifahamu alipo
Khalid wala James”akawaza
Mathew na kugonga meza
“Kuanzia kesho jiji hili
halitakalika.Mathew Mulumbi
will be back.Siwezi kuchezewa
na magaidi kiasi hiki” akawaza
Mathew na kurejea chumbani
kupumzika
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 16
Saa kumi na mbili za
asubuhi simu ya rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania Dr Fabian Kelelo
iliita akaunyoosha mkono na
kuichukua akatazama mpigaji
sura ikabadilika
“Jenerali Akiki ! akasema
kwa sauti ndogo akiwa
amekunja ndita
“Anataka nini huyu jamaa
asubuhi yote hii?Huyu ni mtu
ambaye sitaki kabisa hata
kuisikia sauti yake ! akawaza
Dr Fabian akiitazama simu ile
ikiita na kukatika ikaanza
kuita tena
“Ngoja nimsikilize
anachotaka
kuniambia.Akiniletea dharau
zake leo hii hii nitapelekea
majeshi Uganda nikamchakaze
vibaya sana ! akawaza Dr
Fabian na kuipokea simu ile ya
Jenerali Akiki.
“Mheshimiwa Akiki habari
za asubuhi” akasema Dr
Fabian
“Dr Fabian samahani sana
kwa simu hii ya asubuhi
ambayo hukuwa umeitarajia”
“Ni kweli sikutarajia
kabisa kupokea simu
yako.Unasemaje Jenerali
Akiki?
“Dr Fabian nimekupigia
tuzungumze kidogo mambo ya
msingi.Nafahamu hasira ulizo
nazo juu yangu na ndiyo
maana hata mara ya mwisho
tulipozungumza simuni
mazungumzo yetu hayakuisha
vizuri.Dr Fabian Uganda na
Tanzania hatupaswi kufikia
hatua hii tuliyofika.Sisi si
majirani tu bali ni
ndugu.Uganda tunapolia wa
kwanza kusikia kilio chetu ni
Tanzania na Tanzania inapolia
wa kwanza kusikia kilio chao
ni Uganda.Mheshimiwa rais
naomba hiki kilichotokea siku
chache zilizopita kisivuruge
mahusiano mazuri ya kindugu
kati ya nchi zetu hizi mbili”
“Jenerali Akiki sina imani
kama hayo unayoyasema
yanatoka moyoni.Kama
ungetambua Tanzania na
Uganda ni ndugu
usingethubutu kumuacha
James Kasai akaishi Uganda !
Yote haya yanatokea kwa
sababu serikali yako
inamuhifadhi James Kasai na
sasa anajulikana kama gaidi
James Kasai ! akasema Dr
Fabian kwa sauti ya ukali
“Mheshimiwa Rais ni suala
hilo ambalo limenifanya
nikupigie simu asubuhi hii”
“Nini unataka
kuniambia?akauliza Dr Fabian
“Ninataka suala hili
limalizike hivyo nataka tuwe
na kikao cha pamoja kati yako
na Rais wa jamhuri ya
kidemokerasia ya Congo
bwana Patrice Eyenga mapema
sana ikiwezekana hata kesho
.Nataka tukae tuzungumze na
tumalize suala hili
kindugu.Katika kikao hicho
tutazungumza mengi na
kubwa ni kuhusu James Kasai”
akasema Jenerali Akiki
“Jenerali Akiki kwa muda
mrefu umekuwa ukipigiwa
kelele sana na nchi za Rwanda
na Congo kuhusu James Kasai
lakini wewe na serikali yako
mmekuwa mkikana kabisa
James kuwepo nchini Uganda
na matokeo yake ndiyo haya
yaliyotokea hivi
majuzi.Unasema unataka
kukaa nasi tuzungumze kitu
gani kipya unataka kutueleza
ambacho hujawahi kutueleza?
Akauliza Dr Fabian
“Dr Fabian ninataka
tulimalize hili suala ili
kuepusha nchi zetu kuingia
katika machafuko ambayo
wanayoathiriwa nayo ni raia
wetu”
“ Jeneral Akiki kitu pekee
ambacho tunakihitaji kwa sasa
na ambacho kinaweza kutuleta
mezani kwa mazungumzo ni
kujua mahala alipo James
Kasai” akasema Dr Fabian
“Hicho ndicho kikubwa
ambacho ninataka kuzunguza
nanyi.Najua James ndiye
aliyechafua amani ya Afrika
Mashariki na ninataka
kumaliza sintofahamu
hii.Naomba uandae kikao
hicho cha siri baina yetu ili
tuzungumze kama ndugu”
akasema Jenerali Akiki
“Umeelekeza kwamba
unataka kuzungumza na mimi
na Patrice Eyenga,vipi kuhusu
Rwanda?Nao pia ni waathirika
wa James Kasai” akasema Dr
Fabian
“Suala la Uganda na
Rwanda halijatokana na James
Kasai mheshimiwa Rais.Kuna
matatizo yetu ya muda mrefu
na sitaki kukaa meza moja na
Rwanda”
“Jenerali Akiki
nitawasiliana na rais Patrice na
kumshawishi akubali tukae na
tuzungumze lakini naomba
tafadhali mazugumzo hayo
yawe na tija”
“Nakuhakikishia
mheshimiwa Rais kwamba
sintawapotezea muda wenu
nina nia ya dhati ya kulimaliza
suala hili.Ninaomba sana iwe
mapema zaidi hata kesho
kama ikiwezekana”akasema
Jenerali Akiki
“Sawa nitawasiliana na
Rais Patrice halafu tutaona
kama tukutane kesho au siku
nyingine.Nitakujulisha”akase
ma Dr Fabian
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais.Nategemea
sana jibu lako” akasema
Jenerali Akiki.
Mara tu alipomaliza
kuzungumza na Dr
Fabian,jenerali Akiki
akampigia simu Melanie Davis
“Mheshimiwa rais”
akasema Melanie
“Melani habari yako
mpenzi wangu”
“Nzuri kabisa mheshimiwa
Rais.Nimekuwa nakuwaza
sana usiku wa leo.Tayari
nimeanza kukumbuka
Uganda” akasema Melanie na
wote wakacheka
“Melanie hata mimi
nitafurahi sana kama
nitakuona tena
Uganda.Nategemea utapanga
tena safari hivi karibuni”
akasema Rais Akiki
“Usihofu mheshmiwa
Rais.Nitakuja Uganda tena na
tena” akasema Melanie
“Melanie nimekupigia
kukujulia hali lakini vile vile
kukujulisha kwamba nimetoka
kuzungumza na Rais Dr
Fabian nimemtaka aandae
kikao cha pamoja na Rais
Patrice Eyenga”
“Amekubali?!akauliza
Melanie
“Ndiyo
amekubali.Nimetaka kikao
hicho kiwe kesho lakini
amesema atanipa jibu baadae
baada ya kuwasiliana kwanza
na Rais Patrice na kila mmoja
kuangalia ratiba yake.Natumai
kwa upande wenu mnaendelea
kujiandaa vizuri”
“Ndiyo mzee kwa upande
wetu hakuna tatizo,tunasubiri
upande wako”
“Msiwe na wasiwasi kila
kitu kitakwenda vizuri kama
kilivyopangwa
ninachowasisitiza ni umakini
mkubwa kwani hii ni misheni
kubwa.Endapo mtakosea hata
kidogo tu basi misheni hii
itashindwa kufanikiwa na sisi
sote tutakuwa katika matatizo
hivyo kumbukeni hakuna
kufanya kosa hata dogo.Kila
kitu kipangwe kwa umakini
mkubwa sana” akasema
Jenerali Akiki na kuagana na
Melanie.
PARIS – UFARANSA
Kengele ya mlangoni kwa
Peniela ikalia akainuka
akafikicha macho kisha
akachukua kitanza mbali
akabonyeza kitufe na mtu
aliyekuwa mlangoni
akaonekana katika runinga
iliyokuwa ukutani
“Maggie
unasemaje?akauliza Peniela
kwa sauti ya uchovu
“Kuna mgeni wako
amefika anasema ana miadi
nawe anaitwa Peterson”
“Sawa ninakuja sasa hivi”
akasema Peniela akainuka
akavaa vizuri kisha akatoka
akaelekea sebuleni
“Peterson” akasema
Peniela
“Peniela samahani sana
kwa kukusumbua lakini
nilikuahidi saa kumi na mbili
za asubuhi nitafika hapa”
“Karibu sana
Peterson.Uliifanya ile kazi
niliyokutuma?
“Ndiyo
madam.Nimeifanya”akasema
Peterson na kufungua mkoba
wake akatoa bahasha
akampatia Peniela akaifungua
akatoa makaratasi
yaliyokuwamo ndani.
“Ni ripoti ndefu hii
nitapata muda baadae wa
kuipitia naomba unieleze kwa
mdomo kile ambacho
mmekigundua kuhusu Melanie
Davis” akasema Peniela
“Tulichokigundua ni
kwamba Melanie Davis ni rais
wa Ufaransa lakini hakuna
taarifa zake za
kueleweka.Watu wanaotajwa
kuwa ni wazazi wake na
kwamba walifariki dunia
hakuna taarifa zozote za
kuwahusu,hakuna mahala
wamewahi kusajiliwa kama
wafanya biashara na
hawajulikani walikuwa
wanaishi wapi.Melanie Davis
hana makazi hapa Paris wala
hakuna biashara yoyote
iliyosajiliwa kwa jina lake hapa
Ufaransa.Akaunti yake ya
benki ina shilingi trilioni tano
ambazo hatujui zimetokana na
biashara gani.Kwa sasa
Melanie anaishi Tanzania
ambako amewekeza katika
biashara.Ulielekeza
tuchunguze pia na watu wake
wa karibu tumegundua
kwamba Melanie Davis hana
marafiki hapa Paris ila ana
mtu mmoja tu ambaye ndiye
amekuwa akiwasiliana naye
mara kwa mara anayeitwa
Devotha
Adolph.Tumemchunguza huyo
Devotha Adolph tukagundua
kwamba huyu Devotha
amewahi kuwa wakala wa
Mossad”
“Amewahi kuwa wakala wa
Mossad?
“Ndiyo.Alikuwa wakala wa
Mossad toka akiwa nchini
Marekani na hata alipohamia
Tanzania bado aliendelea
kuwa wakala wa Mossad”
“Bado anaendelea hadi
sasa na kazi hiyo ya
uwakala?akauliza Peniela
“Hapana kwa sasa si
wakala wa Mossad
tena.Ukisoma katika ripoti
inaonyesha anaishi kifahari
sana hapa Paris anatumia
magari ya kifahari ana walinzi
wanaomlinda lakini hajulikani
anafanya kazi gani ila
tumegundua ana ukaribu
mkubwa sana na Rais wa
Ufaransa ambaye
wanawasiliana karibu kila
siku”
“Wana mahusiano gani?
“Uchunguzi unanyesha
ukaribu wao ni wa masuala
mengine na si mapenzi na
tunahisi labda ukaribu huo na
Rais ndio unaomfanya aishi
maisha ya kifahari” akasema
Peterson
“Huyu Devotha ameingia
lini Ufaransa?
“Miaka mitatu iliyopita”
akajibu Peterson na Peniela
akazama mawazoni hakafu
akasema.
“Peterson nakushukuru
sana kwa kazi hii kubwa
mliyoifanya ndani ya kipindi
kifupi.Hata hivyo kuna kazi
nataka ifanyike leo.Huyu
Devotha ninamfahamu na
nitahitaji kumfanyia
mahojiano leo.Nitampigia
simu na kumtaka aje hapa
nyumbani kwangu leo hii kwa
mazungumzo na atakapotoka
Hapa nataka atekwe apelekwe
sehemu mnayotumia kwa
mahojiano halafu
mtanijulisha” akasema
Peniela.
“Sawa madam
Peniela.Ahsante kwa kutupa
kazi kwani hatukuwa na kazi
ya kufanya leo.Utanijulisha
mara tu atakapokuwa amefika
ili zoezi lifanyike
haraka”akasema Peterson
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Mathew na Ruby
waliwasili hospitali kuwajulia
hali Austin na Gosu Gosu.Siku
hii ilianza kwa tabasamu
kwani taarifa waliyoipata
kutoka kwa daktari ni kwamba
tayari Gosu Gosu alikwisha
fumbua macho na hali yake
ilikuwa inaendelea vizuri.Hii
ilikuwa ni taarifa njema sana
kwa akina Mathew.Asubuhi ile
hawakuruhusiwa kuingia
kumuona ili kumpa nafasi ya
kuendelea kupumzika zaidi
wakaelekea katika chumba
alikolazwa Austin ambaye naye
alikuwa anaendelea
vizuri.Austin alifurahi sana
kusikia kuhusu maendeleo
mazuri ya Gosu Gosu.
Baada ya kutoka
kumtazama Austin Mathew na
Ruby wakaelekea katika
nyumba Fulani.
“Hii ni moja ya nyumba
zangu ambazo Peniela
haifahamu hivyo nina uhakika
haijauzwa.Anayeifahamu ni
Gosu Gosu peke yake.Nafikiria
kumuhamisha Gosu Gopsu
kutoka hospitali na kumleta
hapa kwa ajili ya usalama.Pale
hospitali hayuko salama hata
kidogo” Mathew akamwambia
Ruby
“Ni wazo zuri lakini
itategemea na madaktari kama
watakubali mgonjwa ahame”
akasema Ruby
“Watake wasitake lazima
Gosu Gosu ahame.Nitaigeuza
nyumba hii hospitali kwa ajili
ya Gosu Gosu.Kuendelea
kuwepo pale hospitali kwa sasa
wakati hali yake imenza
kuimarika ni kuendelea
kuhatarisha maisha yake.Watu
wanaotaka kumuua lazima
watajaribu tena na tena hadi
pale watakapofanikisha lengo
lao” akasema Mathew na
kushuka garini akaelekea
katika geti ambako kulikuwa
na kisanduku kidogo cheupe
chenye vitufe viwili vya rangi
ya kijani na
nyekundu.Akaweka dole
gumba katika kitufe cha kijani
na mwanga ukatokea halafu
zikatokea namba akatabasamu
na kubonyeza namba Fulani
kisha geti likaanza kufunguka
wakaingia ndani.
“Nyumba nzuri lakini
inaonekana ina muda mrefu
haijakaliwa na mtu
yeyote”akasema Ruby
“Ni kweli ina muda mrefu
haijakaliwa na mtu.Niliijenga
nyumba hii kwa ajili ya
kuipangisha lakini baadae
niliamua kuifanya kuwa ya
mapumziko binafsi.Kila
nilipohitaji kupumzisha akili
yangu huja hapa.Nashukuru
Gosu Gosu kwa kuendelea
kuifanyia usafi na
kuiboresha.Naamini hata
kama nikifa leo bado
watakuwepo watu
watakaonienzi na mmoja wao
ni Gosu Gosu.Japokuwa
iliaminika nimekufa lakini
bado vile vitu ambavyo
vilinihusu sana amekuwa
akivitunza kama vile aliamini
siku moja nitarejea” akasema
Mathew na kufungua sehemu
akatoa funguo akafungua
mlango wa sebuleni wakaingia
ndani.Wakazungukia nyumba
yote wakaikagua ili kuwa
vizuri.
“Nitamleta Lucy kufanya
usafi wakati maandalizi
mengine ya kuigeuza nyumba
hii hospitali kwa ajili ya Gosu
Gosu yakiendelea” akasema
Mathew kisha wakaondoka
kurejea hospitali ambako
Mathew alitaka kuzungumza
na madaktari kuhusu suala la
kumuhamisha Gosu Gosu.
PARIS – UFARANSA
Ni saa tatu za asubuhi
jijini Paris gari moja lenye
rangi nyeusi liliwasili katika
makazi ya bilionea
Peniela.Mlango wa mbele
ukafunguliwa akashuka jamaa
mmoja aliyevaa suti nzuri
nyeusi akatazama kila upande
kuhakiki usalama halafu
akaufungua mlango wa nyuma
na mwanadada mmoja
akashuka akaelekea katika
mlango mkubwa wa kuingilia
ndani ambako alipokewa na
mwanadada aliyevalia sketi
nyeusi na shati jepesi jeupe
akamuongoza kuelekea ndani
ya jumba kubwa la Peniela
akamkaribisha sebuleni.Baada
ya dakika chache akatokea
Peniela akiwa amevaa suruali
nyeupe,shati jekundu
lililokatwa mikono na kofia
nyeupe ya mduara.
“Devotha ! akasema
Peniela na kukumbatiana na
Devotha
“Karibu sana
Devotha”akasema Peniela
“Nashukuru sana Peniela
kwa kunikaribisha tena katika
makazi yako.Nilifurahi sana
uliponipigia simu na kunitaka
nifike hapa kwako.Nilikuwa
natafuta sana nafasi ya kuja
kuonana nawe kuzungumza
masuala Fulani muhimu
nadhani hii ni fursa
nzuri.Ningependa kwanza
kusikia kile ulichoniitia kabla
sijakueleza ya kwangu”
akasema Devotha
“Ahsante sana” akasema
Peniela
“Kikubwa nilichokuitia
hapa ni masuala ya
biashara.Nilitaka kuzungumza
na Melanie lakini nikaona
nizungumze kwanza
nawe.Kama unavyofahamu
mimi ni mfanya biashara
mkubwa.Nina makampuni
mengi na biashara
nyingi.Nilimuuzia Melanie
baadhi ya bisahara zangu
zilizokoTanzania lakini bado
ninazo biashara nyingine
barani Afrika.Nina kampuni
ziko Afrika Kusini,Misri
,Zimbabwe n.k.Ninataka
kuyauza makampuni hayo
yote.Sitaki kuendelea na
uwekezaji wowote barani
Afrika.I’m done with
Africa.Ninataka kumpa
Melanie nafasi ya kwanza
katika wale ninaofikiria
kuwauzia biashara zangu
lakini kabla ya kufanya hivyo
ninataka kufahamu uwezo
wake wa kifedha je unadhani
anaweza akamudu gharama za
kununua makampuni hayo?
Wewe ni mtu wake wa karibu
unamfahamu vyema.Naomba
uniweke wazi kama anaweza
akamudu basi nizungumze
naye” akasema Peniela na
Devotha akatasamu.
“Melanie ni tajiri sana
sidhani kama anaweza
akashindwa kununua
makampuni hayo.Ana fedha za
kutosha ndiyo maana hata
ulipomtajia bei ya makampuni
yale ya Dar es salaam hakusita
wala hakuomba
kupunguziwa.Uwezo anao wa
kununua makampuni zaidi
kama utapenda kumuuzia”
akasema Devotha
“Nimefurahi sana kusikia
hivyo.Ninataka kuyaacha
makampuni hayo kwa mtu
ambaye atakuwa na uwezo wa
kuyaendeleza sitaki nimuuzie
mtu makampuni halafu nisikie
baada ya mwaka mmoja
kumebaki magofu”
“Nakuhakikishia Peniela
,Melanie anao uwezo mkubwa
wa kununua makampunio
hayo” akasema Devotha na
Peniela akapokea simu
akazungumza kwa muda kisha
wakaendelea na maongezi
“Ukiacha biashara zile
nilizomuuzia Melanie kule
Tanzania,ni biashara zipi
nyingine anamiliki?akauliza
Peniela na swali lile
likaonekana kumbabaisha
kidogo Devotha
“Melanie utajiri wake ni
wa kurithi.Wazazi wake
walikuwa matajiri wakubwa
sana na walipofariki katika
ajali ya gari Melanie
akaendeleza utajiri wa wazazi
wake” akasema Devotha
“Wazazi wake walimiliki
biashara zipi hapa
Ufaransa?akauliza Melanie
“Sifahamu sana mambo ya
Melanie.Nimekutana naye
hapa hapa Ufaransa tukawa
marafiki hivyo mambo mengi
kuhusiana na biashara zake
siyajui bado”Devotha
akaonekana kukwepa
kuzungumzia kuhusu biashara
za Melanie
“Peniela kwa nini unataka
kuuza mali zako zote
Afrika?akauliza Devotha
“Kama nilivyosema I’m
done with Afrika.Sitaki tena
kuwekeza kule”akasema
Peniela
“Ni kwa sababu ya kifo cha
mumeo?
“Ndiyo.Hiyo ni sababu
kubwa iliyonifanya niichukie
Afrika na ndiyo maana nataka
kuuza kila kitu sitaki kurejea
tena kule”akasema
Peniela.Waliendelea na
maongezi mengine na baada ya
muda Peniela akasema
“Devotha ulisema kuna
kitu ulitaka kunieleza
tukionana ni kitu gani hicho?
Devotha akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Nina mpango wa kuwania
urais wa Tanzania” akasema
Devotha na Peniela akastuka
“Unataka kuwania urais?
“Ndiyo.Ninataka kuingia
katika mbio za kuwania urais
wa Tanzania”
“Umenistua.Hadi kupata
nafasi ya kuingia katika
kinyang’anyiro cha kuwania
urais si jambo dogo”
“Ni kweli hicho
unachokisema Peniela lakini
ninao mtandao ambao ndio
unaonitengenezea mambo
hivyo ninahitaji sana pale
muda utakapofika ninyi
watanzania wenzangu
mniunge mkono ili niweze
kufanikisha ndoto yangu hiyo”
“Dah ! hongera sana kwa
kuwa na ndoto kubwa namna
hiyo.Uongozi wa nchi si jambo
dogo Devotha inahitaji uzoefu
mkubwa”
“Ninao uzoefu wa
kutosha.Ninayafahamu
majukumu ya Rais na ndiyo
maana ninaamni nitaweza”
“Umewahi kufanya kazi
kulu?
“Nilikuwa mkurugenzi wa
SNSA.Secret National security
Agency.Hii ni idara nyeti sana
ambayo inashughulika na
usalama wa ndani ya nchi na
kwa kuwa kiongozi wa idara hii
ambayo iko chini ya Rais ikulu
kulikuwa ni kama
nyumbani.Hapo ndipo
nilipopata nafasi ya kufahamu
mambo mengi kuhusiana na
kazi ya urais na ndiyo maana
nikasema kwamba ninaweza
kuongoza nchi” akasema
Devotha
Mara tu Devotha
alipotamka SNSA Peniela
akastuka
“Mathew alitamka hii
idara wakati ananieleza kile
kilichomtokea hadi
akapotea.Kumbe huyu
amewahi kufanya kazi katika
idara hiyo.Vile vile Mathew
aliniambia kwamba alitekwa
na watu wa Mossad wakati wa
operesheni ya kubadilishana
mateka kati yao na magaidi wa
IS lakini mpaka leo hii hata
yeye hajui Mossad
walifahamuje kuhusu
mabadilishano yale.Sasa
nimepata picha.Huyu alikuwa
mkurugenzi wa SNSA na vile
vile akawa ni wakala wa
Mossad.Kama anamfahamu
Mathew basi huyu ndiye
atakuwa alimuuza Mathew
kwa Mossad.Nitafahamu kila
kitu leo mimi na
yeye.”akawaza Peniela
“Kwa nini uliacha kazi hiyo
ya ukurugenzi katika idara ya
SNSA?akauliza Peniela
“Niliacha kazi ili nianze
mchakato wa urais”
“Kwani hapa Ufaransa
umekaa kwa muda gani?
“Nina miaka mitatu sasa”
akajibu Devotha
“Devotha mimi nimefurahi
sana kusikia una ndoto kubwa
namna hiyo.Nitakuunga
mkono lakini pale
utakapokuwa umechaguliwa
na chama chako
kugombea.Gharama zote za
kampeni ni juu yangu
mimi.Nitatoa ndege,helkopta
na magari kwa ajili ya
kukusaidia katika kampeni
zako” akasema Peniela
“Peniela ninakushukuru
mno kwa kunielewa na kuahidi
kunisaidia.Sijui
nikushukuruje”
“Usijali.Ni lazima
nikuunge mkono mwanamke
mwenzangu” akasema Peniela
akazungumza kidogo na simu
halafu akasema
“Samahani Devotha
unajua ninapokea simu nyingi
za biashara hivyo univumilie”
“Ninaelewa Peniela usijali”
“Ulisema uliongoza idara
ya SNSA ulimfahamu mume
wangu Mathew
Mulumbi?Huyo naye alikuwa
anashughulika na masuala
hayo hayo ya usalama”akauliza
Peniela na Devotha akaoyesha
mstuko kidogo
“Mathew Mulumbi?!
Akauliza Devotha
“Ndiyo aliwahi kufanya
kazi na idara yenu?
“Hapana hajawahi kufanya
kazi na idara yetu” akajibu
Devotha.Waliendelea na
mazugumzo halafu Peniela
akamtaka radhi Devotha
akaelekea chumbani kwake
akachukua simu na kumpigia
Peterson Lebrave mkurugenzi
wa kampuni ya wapelelezi wa
kujitegemea
“Madam Peniela” akasema
Peterson
“Peterson mtu Yule tayari
ninaye hapa ndani vijana wako
tayari wamejipanga?akauliza
Penila
“Vijana wangu wako
tayari.Atakapotoka hapo
kwako utanijulisha” akasema
Peterson
kisha Peniela akarejea sebuleni
alikomuacha Devotha
wakaendelea na maongezi
kuhusu mambo mbali mbali ya
maisha na kubwa likiwa ni
suala la Devotha kuwania
urais.Dakika arobaini baada ya
Peniela kuzungumza na
Peterson simuni Peniela
akamuomba radhi Devotha
kwamba anahitajika
ofisini.Wakaagana kwa miadi
ya kukutana tena kwa
mazungumzo zaidi.Peniela
akamsindikiza Devotha hadi
katika gari lake wakaagana
akaondoka.Peniela akamtumia
ujumbe Peterson kumjulisha
kwamba Devotha anatoka
getini.
Eneo la makazi ya Peniela
lilizungukwa na miti mingi na
kutoka katika makazi hayo
hadi kukuta barabara kuu ni
umbali wa kilometa moja na
nusu ukipita katika
msitu.Walipokaribia daraja
katika mto unaopita katika
msitu ule wakayakuta magari
mawili yameegeshwa.Dereva
wa gari la Devotha akapunguza
mwendo.Alipotazama katika
kioo cha pembeni akaona kuna
gari nyingine mbili zinakuja
nyuma yao pamoja na piki piki
mbili.
“Kuna nini kinaendelea
pale darajani?akauliza mlinzi
wa Devotha aliyekuwa amekaa
kiti cha mbele
“Nashangaa kwa nini zile
gari mbili zimeegeshwa pale
darajani” akajibu
dereva.Waliyakaribia yale
magari mawili yaliyokuwa
yameegeshwa darajani na
kusimama dereva akapiga honi
na mara pikipiki mbili
zilizokuwa zikija nyuma yao
zikafika na wale jamaa wawili
wakachomoa silaha na kuanza
kumiminia risasi dereva na
mlinzi wa Devotha wote
wakafa pale pale.Devotha
alikuwa anatetemeka mwili
kwa woga.Haraka sana watu
wengine sita wakashuka
kutoka katika magari mlango
gari la Devotha ukafunguliwa
akashushwa na kufunikwa
mfuko kichwani akaingizwa
katika mojawapo ya gari
lililokuwa limeegeshwa
darajani kisha likaondoka kwa
kasi.Maiti za dereva na mlinzi
wa Devotha zikaingizwa katika
gari lingine na kuondolewa
pale kisha usafi ukafanyika
eneo lile kuhakikisha kwamba
hakuna hata kioo
kitakachoonekana.Mkoba wa
Devotha ukachukuliwa simu
yake ikazimwa,gari lake
likapekuliwa kisha
likasukumwa likaangukia
mtoni.Baada ya kuhakikisha
kila kitu kimekwenda vizuri
wale jamaa wakaondoka zao.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 9 : EPISODE 17
Peniela akiwa nyumbani
kwake akajulishwa kwamba
kila kitu kimekwenda vizuri na
akaelekezwa mahala
alikopelekwa Devotha
“Ni wakati wa kwenda
kutafuta majibu.Yule
mwanamke anamfahamu
vyema Melanie na leo
atanieleza Melanie ni nani
hasa? Nilimuahidi Mathew
kumtafutia majibu kuhusu
Melanie na sasa ninakwenda
kuupata ukweli” akawaza
Peniela na kuvua mavazi
aliyokuwa amevaa akavaa
suruali ya jeans na fulana
vyote rangi yeusi akavaa na
kofia nyeusi akaondoka bila
dereva wala mlinzi akaelekea
mahala alikoelekezwa na
Peterson kwamba ndiko
anakoshikiliwa Devotha.
“Kabla ya kukutana na
Mathew Mulumbi niliwahi
kufanya kazi na Team SC41.Ni
kazi ya hatari sana nilikuwa
naifanya lakini ni Mathew
ndiye aliyeniondoa katika
maisha yale na nikawa hivi
nilivyo leo.Kila nikiyakumbuka
maneno yale niliyomtakia jana
roho yangu inaumia
mno.Sikupaswa kumtamkia
maneno kama yale.Sijui
nitafanya nini kuyafuta
maneno yale katika akili
yake.Lakini kwa nini
niliaamua kuchukua maamuzi
kama yale?Je yalikuwa ni
maamuzi sahihi?Toka ndani
kabisa mwa moyo wangu
ninampenda sana Mathew na
hatatokea mwanaume ambaye
nitampenda kama yeye”
akawaza Peniela
Peniela alifika mahala
alikopelekwa Devotha.Ilikuwa
ni katika bohari moja kuu kuu
lililoonekana
kutelekezwa.Aliingiza gari
ndani ya bohari lile akashuka
na kupokewa na Peterson
“Ahsante sana Peterson
kwa kuifanikisha kazi hii kwa
haraka na kwa ufanisi
mkubwa” akasema Peniela
wakati wakielekea katika ofisi
ya Peterson
“Madam Peniela kama
nilivyokueleza kwamba vijana
wangu hawakuwa na kazi ya
kufanya leo ndiyo maana
wakaifanya kazi ile kwa haraka
sana” akasema Peterson
wakaelekea katika ofisi yake
akamweleza Peniela namna
zoezi la kumteka Devotha
lilivyofanyika na kila hatua
waliyochukua kuhakikisha
wanaondoa kila ambacho
kingeweza kuleta matatizo
endapo uchunguzi wa
kutoweka kwa Devotha
ungefanyika.Peniela akafurahi
na kuahidi kuwalipa mara
mbili ya kiasi walichokuwa
wamehitaji.
“Huyu mtu unataka
tumfanye nini?akauliza
Peterson
“Huyu nataka mniachie
mimi mwenyewe
nitashuhulika naye.Kuna
taarifa muhimu sana nazihitaji
kutoka kwake” akasema
Peniela na kupelekwa katika
chumba kilichokuwa na kioo
kikubwa akamtazama Devotha
akiwa ndani ya chumba
kingine amefungwa katika kiti.
“Hatujampa mateso yoyote
tulikuwa tunakusubiri kwanza
ufike” akasema Peterson
“Ahsante Peterson
nifungulieni mlango
nizungumze naye” akasema
Peniela na kufunguliwa
mlango akaingizwa ndani ya
kile chumba alimo Devotha.
“Hallo Devotha ! akasema
Peniela huku akitabasamu
akavuta kiti akaketi akatoa
kofia na miwani.Mstuko
alioupata Devotha ulikuwa
mkubwa.Alihisi yuko njozini
na si kitu cha kweli
anachokishuhudia
“No ! This is not true !
akasema Devotha
“It’s true
Devotha.Unachokiona si njozi
ni kitu cha kweli
kabisa.Aliyeko mbele yako ni
mimi Peniela” akasema
Peniela na Devotha
akamtazama kwa hasira
“Wewe ndiye uliyenifanyia
hivi?! Akauliza kwa ukali
“Ndiyo Devotha ni mimi!
“Kwa nini
Penielea?Nimekukosea nini
hadi unifanyie hivi?akauliza
Devotha
“Devotha nimekuleta hapa
kwa mahojiano na
ninakuomba unijibu kwa
ufasaha maswali
nitakayokuuliza na endapo
utaleta mzaha au kiburi this
will be the end of the road for
you” akasema Peniela
“Don’t threaten me
Peniela.Hunifahamu mimi ni
nani na huna uwezo wa
kuniamuru chochote.Kwa
taarifa yako mambo kama
haya nimeyapitia ninafahamu
kila kitu na huwezi ukanitishia
kunitesa.Peniela nakushauri
usitake kungia katika matatizo
makubwa.Mimi si mtu wa
kutaka kuingia naye katika
matatizo.Nakushauri tulia na
maisha yako mazuri haya
mengne yaache kabisa!
akasema Devotha
“Devotha ninakufahamu
vizuri wewe ni
nani.Ninaifahamu historia
yako umetoka wapi na hadi
umefika hapa na
ninakuhakikishia kwamba
bado hujawahi kupitia
mateso.Bado hujawahi kuaona
mateso na leo utayashuhudia
labda ukubali kutoa
ushirikiano ndipo utajiokoa
lakini kama ukiwa kiburi basi
utazungumza lugha zote
unazozifahamu leo ! akasema
Peniela
“Peniela nani wanataka
kukuingiza katika matatizo
haya makubwa?akauliza
Devotha
“Devotha ninataka
unieleze kuhusu Melanie
Davis.Nimegundua kwamba
anashrikiana na kikundi cha
kigaidi cha IS na wewe kama
mtu wake wa karibu lazima
jambo hili unalifahamu
vizuri.Nataka unieleze ukweli
Melanie Davis ni nani ?
Akauliza Peniela
“You go to hell shetani wa
kike wewe ! akasema Devotha
kwa ukali
“Huwezi ukaniweka hapa
na kunihoji maswali.Wewe ni
mtu mdogo sana wa kunihoji
mimi ! akaendelea kufoka
“Devotha nimekuuliza
swali naomba unijibu.Melanie
Davis ni nani?Peniela akauliza
“Siulizwi maswali na
panya mchafu kama wewe !
akasema Devotha.
“Devotha nimekuuliza
Melanie Davis ni nani?akauliza
Peniela
“We kahaba siwezi
kukujibu swali lako
lolote.Please go to hell !
akasema Devotha
“Sawa Devotha tutaona
mimi na wewe nani
atakayetangulia kwenda huko
unakosema niende ! akasema
Peniela na kubonyeza kitufe na
Peterson akaingia
“Naomba niandaliwe vifaa
! akasema Peniela na Peterson
akafungua kabati la chuma
akatoa vifaa mbalimbali
akaviweka mezani
“Unahitaji msaada wowote
Peniela? Akauliza Peterson
“Huyu nitashughulika
naye mimi
mwenyewe.Ninahitaji watu
wawili kwa ajili ya
kumshika.Nataka
nimuonyeshe kweli mimi ni
shetani wa kike ! akasema
Peniela.Peterson akawaita
jamaa wawili wakaingia mle
ndani Peniela akaenda mezani
akachukua mkasi wa kukatia
vitu vigumu
“Devotha hii ni mara ya
mwisho nitakuuliza.Melanie
Davis ni nani? Akauliza
Peniela
“Peniela narudia kukuonya
kwamba usiendelee na mchezo
huu utajuta sana baadae”
akasema Devotha na Peniela
akawaelekeza wale jamaa
wawili waliojazia miili
wamkamate Devotha
wamfunge katika kitanda cha
chuma kilichokuwamo mle
ndani.Devotha akanyanyuliwa
na kufungwa katika kitanda
kile
“Melanie Davis ni
nani?akauliza Peniela Devotha
akamtemea mate usoni.Peniela
akakishika kiganja cha mkono
mmoja wa Peniela uliokuwa na
vidole vitatu na kwa kutumia
mkasi akakikata kidole cha
mwisho
“Aaaaaaaaghhh !! Devotha
akatoa ukelele
“Melanie Davis ni
nani?akauliza Peniela
“Nitakuua Peniela !
akasema kwa hasira Devotha
.Peniela akakishika kidole
kingine na kukikata Devotha
akaendelea kupiga kelele.
“Who is Melanie
Davis?akauliza
Peniela.Devotha aliendelea
kupiga kelele kubwa kwa
maumivu makali aliyoyapata.
“Devotha
nilikutahadharisha toka awali
kwamba huu unaweza ukawa
ni mwisho wako kama
hautakuwa makini na
ninarudia tena
kukutahadharisha kwamba
endapo hautakuwa makini huu
utakuwa mwisho wako.Sina
utani na Mungu atanisamehe
kwani nitakufanyia kitu kibaya
sana ! akasema Peniela kwa
ukali lakini bado Devotha
alikuwa anatetemeka na kulia
kwa maumivu makali.Peterson
akamsogelea Peniela
akamnong’oneza kitu halafu
akafungua droo na kutoa
chupa yenye dawa ya chumvi
chumvi akaenda kupaka
mahala Peniela alipokata
vidole.Devotha alitoa kelele
kubwa akijaribu kujitoa katika
kamba zile lakini alifungwa
barabara.Aliweweseka
akizungumza maneno kama
mwenda wazimu.
“Ulisema huogopi mateso
na huu ni mwanzo
Devotha.Nitakuharibu haribu
leo.Naomba tafadhali unieleze
Melanie Davis ni nani?
Akauliza Peniela lakini
Devotha hakujibu kitu
aliendelea kulia huku
akiweweseka kwa maumivu
makali.
“Devotha nitamaliza vidole
vyote vya mikono na utabaki
huna hata kidole
kimoja.Malengo yako ya kuwa
Rais yanakwenda kupotea
.Tafadhali nijibu ili tuyamalize
haya mambo ! akasema
Peniela ambaye alikuwa na
hasira kama Mbogo.Devotha
aliendelea kulia Peniela
akaushika tena mkasi
akakimalizia kidole
kilichokuwa
kimebakia.Devotha aliendelea
kupiga kelele kubwa hadi sauti
ikaanza kukwama.
“Devotha nimemaliza
kiganja cha kwanza ninahamia
kiganja cha pili.Nimekwambia
leo nitakufanyia ukatili ambao
haujawahi kuushuhudia”
akasema Peniela na kukishika
kidole cha mwisho cha mkono
mwingine akakikata.
“Peniela please !! Niko
chini ya miguu yako tafadhali
usiendelee kunitesa nama
hii.Nimekukosea nini hadi
unifanyie hivi?akauliza
Devotha akiwa katika
maumivu makali
“Melanie Davis ni
nani?akauliza Peniela
“Nitakwambia Peniela
tafadhali usiendelee kunitesa
namna hii ! akasema Devotha
“Nataka unieleze kila kitu
kuhusu Melanie Davis!
Akasema Peniela
“Melanie Davis….
“Ndiyo nataka unieleze ni
nani?Ana mipango gani nchini
Tanzania? Akauliza
Peniela.Devotha akavuta
pumzi ndefu kisha akasema
“Melanie ..aaahg…..ni
mfanya biashara….Aaagh
Peniela umeniharibu kwa nini
lakini? Akaendelea kulia
“Melanie anashirikiana na
magaidi wa IS wana mipango
gani nchini Tanzania?akauliza
Peniela Devotha hakujibu
akaendelea kugugumia kwa
maumivu
“Devotha naomba jibu
haraka sana kabla sijaendelea
kukuharibu ! akasema Peniela
“Nitakueleza ukweli
Peniela” akasema Devotha na
kuvuta pumzi ndefu mara tatu
halafu akasema
“Melanie nimekutana
naye…aaaghh ! akanyamaza na
kufumba macho kwa maumivu
makali halafu akaendelea
“Nimekutana naye hapa
Paris na tukawa
marafiki.Akanieleza anataka
kuwekeza Afrika nikamshauri
akawekeze Tanzania na ndipo
nilipoambatana naye kuja
kwako kutaka kununua
makampuni yako.Simfahamu
kwa undani na wala sifahamu
kama anashirikiana na
magaidi ! akasema Devotha
“Devotha unanidanganya !
akasema Peniela na kukibana
kidole kwa mkasi
“Peniela usinikate kidole
tafadhali ninachokueleza ni
kitu cha kweli
kabisa.Simfahamu vizuri
Melanie ! akalia Devotha.
“Peniela nionee huruma
unaniumiza bure sifahamu
chochote kuhusu mambo
anayoyafanya
Melanie.Nilimsaidia kumleta
kwako na sifahamu mambo
yake mengine ! akaendelea
kuomba Devotha
“Unafanya kazi gani hapa
Paris? Akauliza
Peniela,Devotha akawa kimya
“Unaishi maisha ya
kifahari hapa Ufaransa
unafanya kazi gani?akauliza
tena Peniela na kukibana
kidole
“Usikate Peniela
nitakwambia.Nina gharamiwa
na Rais wa
Ufaransa.Ninamshauri kuhusu
masuala ya Afrika” akasema
Devotha
“Ulinieleza kwamba
uliwahi kufanya kazi SNSA
nikakuuliza kama
unamfahamu Mathew
Mulumbi ukakana
kutomfahamu.Nakuuliza tena
kwa mara nyingine tena
unamfahamuMathew
Mulumbi? Akauliza Peniela
“Devotha nakuuliza kwa
mara ya mwisho unamfahamu
Mathew Mulumbi? Akauliza
Peniela na kuendelea kukibana
kidole
“Peniela utaniua jamani
usinikate tena vidole
vyangu.Nitaishi vipi
mimi?akalia Devotha
“Nitakuua kweli kama
hautanieleza ukweli”akasema
Peniela
“Ninamfahamu Mathew
Mulumbi”
“Mathew alishirikiana na
idara uliyokuwa unaiongoza
kuwakomboa mateka
waliotekwa na IS lakini
alitekwa na Mossad na
hajulikani alipo.Nataka
unieleze ukweli nani aliyewapa
taarifa Mossad kuhusu
operesheni ile aliyokwenda
kuifanya Mathew? Akauliza
Peniela
“Sifahamu chochote
Peniela” akasema Devotha
“Devotha nafahamu wewe
ulikuwa wakala wa
Mossad.Niambie ukweli kama
ni wewe uliyewapa taarifa za
Mathew Mulumbi na
wakamteka?akauliza Peniela
Devotha alishindwa
kujibu.Peniela akakibana
kidole na kukikata
kikaruka.Devotha akalia kwa
uchungu lakini sauti ilikwama
kutoka
“Devotha niambie ukweli
ama sivyo huu utakuwa ni
mwisho wako ! akasema
Peniela kwa hasira lakini
Devotha hakujibu alifumba
macho akigugumia kwa
maumivu huku akizungumza
maneno yasiyoeleweka.
Peniela akatupa ule mkasi
akaenda kuchukua shoka dogo
na kuwataka wale jamaa
waufungue mkono mmoja wa
Devotha na kuuweka katika
meza
“Devotha ni wazi wew
e ndiye uliyemuuza Mathew
kwa Mossad.Ninakusamehe
kwa hilo lakini nataka unieleze
nini mipango ya Melanie Davis
na IS nchini Tanzania !
akasema Peniela Devotha bado
aliendelea kumwaga
machozi.Peniela akainua
shoka juu kwa ajili ya kukata
kiganja cha mkono Devotha
akapiga kelele akimtaka
asimkate
“Nitakueleza
Peniela.Nitakueleza kila kitu
tafadhali usinikate mkono”
akasema Devotah
“Nieleze haraka sana
mipango ya Melanie na IS !
akafoka Peniela
“Sifahamu mpango
wowote wa Melanie na IS !
akasema Devotha na bila
kuuliza mara ya pili Peniela
akainua shoka juu na
kulishusha kwa nguvu katika
kiganja cha mkono kikaruka
chini.Devotha alishindwa
kupiga kelele kwani sauti
haikutoka tena
“Devotha kinachofuata
nitaukata mkono mzima.Leo
nitakuondoa kiungo kimoja
kimoja kama hautanieleza
ukweli.Nataka uniambie
mipango ya Melanie na IS !
akasema Peniela Devotha
aliendelea kukoroma sauti
haikuwa inatoka.Peniela
akakasirika na kuukata mkono
katika bega
“Devotha nieleze ukweli!
Akasema Peniela.Peterson
akamsogelea akamnong’oneza
sikioni
“Peniela huyu hataweza
kusema chochote
tena.Kiwango cha mateso
alichokipata ni kikubwa sana!
Kwa hatua hii aliyofikia kuna
kitu kimoja tu cha kufanya ni
kumuua”Akasema Peterson
“Devotha nina hasira sana
nawe kwani umeyavuruga
maisha yangu. Kitendo chako
cha kumuuza Mathew kwa
Mossad kimesababisha hadi
sasa maisha yangu yakose
furaha kwani siwezi tena kuwa
na mtu niliyempenda katika
maisha yangu! Mathew
ameteswa na kumizwa mno na
kwa ajili yako leo nitamlipia
kisasi ! akasema Peniela huku
akimtazama Devotha kwa
hasira
“Naomba
u…u.uuusi….niue ! akaomba
Devotha macho lakini Peniela
aliyekuwa na hasira kama
Mbogo akalishusha kwa nguvu
shoka likatua katika goti na
kuutenganisha mguu.
“Hii ni kwa ajili ya Mathew
na mateso yote aliyoyapitia
kwa sababu ya tamaa zako !
akasema kwa hasira na
kuukata mguu wa pili.
“Nilikwambia nitakufanyia
unyama mkubwa sana leo !
akasema Peniela na
kumtazama Devotha
“Kwa heri Devotha !
akasema Peniela na kushusha
shoka kwa nguvu katika shingo
ya Devotha na kuhitimisha
safari yake ya maisha hapa
duniani.Peniela akaenda
katika chumba kilichokuwa na
tanuru kubwa kwa ajili ya
kuchomea miili akavua zile
nguo zilizokuwa zimetapakaa
damu akavaa nguo nyingine
alizokuwa amekwenda nazo
halafu akarejea ndani ya kile
chumba Peterson akampa
karatasi
“Hii ni orodha ya namba
za simu ambazo Devotha
amekuwa akiwasiliana nazo
mara kwa mara” akasema
Peterson.Peniela akaipitia ile
orodhana kukuta kuna namba
nne kutoka Tanzania ambazo
Devotha alikuwa anawasiliana
nazo.
“Ahsante Peterson”
akasema peniela na kuchukua
simu yake akampigia Mathew
kwa njia ya video
“Hallow Peniela” akasema
Mathew baada ya kupokea
simu
“Mathew kabla ya
kukueleza chochote kuna kitu
nataka ukitazame” akasema
Peniela na kuisogeza kamera
ya simu karibu na mwili
uliokatwa katwa wa Devotha
“Unaweza ukaitambua
sura hii” akauliza Peniela
“Oh my God that’s
Devotha ! akasema Mathew
kwa mshangao
“I killed this devil !
“You what ?! Mathew
akauliza
“Nimemuua.Huyu ndiye
aliyekuuza kwa
Mossad.Alikuwa wakala wa
Mossad wakati ule na ndiye
aliyewapa taarifa zako
wakakuteka”
“Jesus ! akasema Mathew
“Huyu ndiye mshirika
mkubwa wa Melanie
Davis.Mathew hawa watu
watakuwa na mipango
mikubwa sana kwani Devotha
amekuwa tayari kufa kuliko
kueleza kile ambacho
MelanieDavis anapanga
kukifanya”
“Melanie na Devotha
wanafahamiana?
“Ndiyo wanafahamiana na
Devotha ndiye aliyemleta
kwangu Melanie” akasema
Peniela
“Sijapata kitu chochote cha
maana kutoka kwake kuhusu
Melanie lakini nimepata
namba nne ambazo amekuwa
akiwasiliana nazo mara kwa
mara nchini
Tanzania.Mtazifuatilia
kuwafahamu watu ambao
amekuwa akiwasiliana nao.”
akasema Peniela
“Peniela sijui
nikushukuruje kwa hiki
ulichokifanya”
“Mathew hawa ndo
waliosababisha mimi nawe
tukatengana hivyo nina hasira
nao sana.Nimefanya hivi kwa
ajili yako.Tafadhali hakikisha
unampata Melanie
Davis.Nimetumia wapelekezi
wa kujitegemea kutafuta
taarifa za Melanie lakini
walichokipata
kinashangaza.Hakuna
biashara zozote zilizosajiliwa
kwa jina lake hapa
Ufaransa,hajulikani mahala
anakoishi hapa Paris,hakuna
taarifa zozote za kueleweka
kuhusu wazazi wake lakini
akaunti yake ina kiasi kikubwa
cha fedha karibu trilioni
tano.Ninaweza kusema
kwamba huyu Melanie Davis
amevaa uhusika bandia kwani
taarifa zake zote zilizopo
zinaonekana ni za
kutengenezwa kwa
madhumuni Fulani na ninahisi
hata wakubwa wa serikalini
hapa Ufaransa wanalifahamu
hilo jambo kwani Devotha
ambaye nimemuua ana ukarbu
mkubwa sana na Rais wa
Ufaransa ambaye tunahisi
ndiye anayemfanya aishi
maisha ya kifahari hapa
Paris.Hicho ndicho
nilichoweza kukipata Mathew”
akasema Peniela
“Peniela nimekosa neno
zuri la kukushukuru kwa hiki
ulichokifanya” akasema
Mathew
“Usinishukuru Mathew.Ni
wajibu wangu
kukusaidia.Kama kuna kitu
chochote kingine ambacho
unataka nikusaidie usisite
kuwasiliana nami.Mwisho
kabisa Mathew I’m very sorry
for what I said
yesterday.Sikupaswa
kukutamkia maneno kama
yale.Ni wewe uliyenifikisha
hapa nilipo leo.Nisamehe sana
zilikuwa ni hasira tu” akasema
Peniela
“Usihofu Peniela yale
yamekwisha pita” akasema
Mathew na kuagana na Peniela
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Mathew Mulumbi akavuta
pumzi ndefu baada kumaliza
kuzungumza na Peniela.Kwa
sekunde kadhaa alifumba
macho yake halafu
akayafumbua akamgeukia
Devotha aliyekuwa pembeni
yake.Walikuwa wameegesha
gari pembeni ya barabara
wakati Mathew akizungumza
na Peniela
“Hatimaye shetani
amepatikana na kuuawa !
akasema Mathew na ujumbe
ukaingia katika simu yake
ukitoka kwa Peniela.Alikuwa
amemtumia namba za simu za
watu walioko Tanzania ambao
wamekuwa wakiwasiliana na
Devotha pamoja na picha za
mwili wa Devotha baada ya
kuuawa.Mathew
akamuonyesha Ruby picha
alizotumiwa na Peniela.Ruby
alijikuta akibubujikwa machozi
“Nimeshindwa kuvumilia
Mathew kwa furaha niliyonayo
kwa huyu mwanamke
kuuawa.Nilichungulia kaburi
kwa sababu yake.Siku nyingine
ukiwasiliana na Peniela
naomba umpe shukrani zangu
kwa hiki alichokifanya kumuua
Devotha” akasema Ruby huku
akifuta machozi
“Kwa mujibu wa Peniela
huyu ndiye aliyewapa Mossad
taarifa za operesheni ile na
wakaniteka.Nashukuru Peniela
amenilipia kisasi kwa mateso
niliyoyapitia”
“Hukuwahi kuniambia
kama ulitekwa na Mossad
lakini Peniela ulimweleza !
akasema Ruby
“Muda utafika nitakueleza
kila kitu.Lakini huyu
mwanamke ndiye chanzo cha
mateso yote niliyoyapata.
Anastahili kufa kifo cha namna
hii” akasema Mathew
“Peniela ametuma namba
hizi za watu ambao wamekuwa
wakiwasiliana na
Devotha,tuanze kuzifuatilia
kuwafahamu wenye namba
hizi.” akasema Mathew kisha
Ruby akaichukua kompyuta
yake akaweka sawa program
zake na kuanza kupiga zile
namba.Namba tatu hazikuwa
zinapatikana na alipoingiza
namba ya nne kwa ajili ya
kupiga akastuka kwani alikuwa
nayo ile namba tikana.
“Edwin Mbeko ! akasema
Ruby
“Edwin Mbeko?Mathew
naye akauliza
“Ndiyo hii ni namba yake”
akasema Ruby
“Sasa picha imeanza
kujitengeneza Ruby.Hebu
tazama huu mtiririko.Devotha
ambaye ni mtu wa karibu na
Melanie amekuwa na
mawasiliano na Edwin Mbeko
wa SNSA.Jana tumempoteza
Khalid Sultan kwa kitendo
kilichofanywa kwa makusudi
na watu ndani ya SNSA aliko
Edwin.Kwa Edwin kuwa na
mawasiliano na Devotha
ambaye ni mtu wa karibu na
Melanie nalazimika kuamini
kwamba lazima Edwin
atakuwa katika mtandao wa
akina Melanie na ndiye
anayewezesha mambo ya yote
ya matandao huo kufanikiwa”
akasema Mathew
“Mathew hapa nilipo
ninahisi mwili wote
unanitetemeka kwa
woga.Sikutegemea kabisa
kama Edwin angeweza kuwepo
katika mtandao huu” akasema
Ruby na Mathew akamtaka
awashe gari
“Tunaelekea wapi?
“Tunakwenda nyumbani
nikachukue silaha kisha
tunamfuata Edwin ofisini
kwake SNSA”
“Hawataturuhusu kuingia
pale kwani mimi si
mkurugenzi kwa sasa hadi
suala langu litakapotatuliwa”
“Ndiyo maana ninakwenda
kuchukua silaha
zitakazotuwezesha kungia pale
SNSA”
“Mathew huo ni mpango
wa hatari kubwa.Ofisi ile ina
ulinzi mkali na si rahisi
kuivamia” akasema Ruby
“Tutaingia pale ndani na
lazima tumpate Edwin.Usihofu
Ruby uko na Mathew Mulumbi
the unstoppable! akasema
Mathew
“Mathew naomba
nikushauri mpenzi wangu.Kwa
mchana huu tulikuwa na
mpango wa kumshughulikia
Gosu Gosu.Tumuhamishe
Gosu Gosu na kuhakikisha
anakuwa sehemu salama
halafu usiku wa leo ndipo
tukavamie SNSA na
kumchukua Edwin.Naamini
mpaka muda huo hatakuwa
anafahamu kama Devotha
ameuawa na wala hatakuwa
akijua kama tumefahamu ana
mawasiliano na Devotha”
akashauri Ruby.Mathew
akafikiri kisha akasema
“Ushauri
mzuri.Tumuhamishe kwanza
Gosu Gosu na kumpeleka
sehemu salama halafu
nitamonyesha Yule Edwin na
mtandao wake mimi ni nani”
akasema Mathew
MPENZI MSOMAJI
TUNAPOKARIBIA
KUMALIZA SIMULIZI HII
YA MAISHA NA KIFO CHA
MELANIE CHUMA KAA
TAYARI KWA AJILI YA
SEHEMU YA TATU NA YA
MWISHO YA SIMULIZI YA
SIRI ITAKAYOJULIKANA
KAMA
JASUSI/GAIDI.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 1
Geti la nyumba anayoishi
Melanie Davis lilifunguliwa na
gari la Edwin Mbeko
likaingia.Akashuka garini na
kufungua buti akatoa maboksi
matano watumishi wa ndani
wa Melanie wakatoka na
kumsaidia kubeba maboksi
yale wakayaingiza ndani.
Mtumishi akamuongoza
Edwin kwenda bustanini
walikokuwa wamekaa
Melanie.James Kasai na
Khalid Khalid.
“ Nimefurahi sana
kuwaoneni tena mkifurahia
hali ya hewa safi ya Dar es
salaam” akasema Edwin
baada ya kusalimiana na akina
Melanie
“Dar es salaam ni jiji
zuri.Nitakuja tena kutembea
siku nyingine.Nitakapokuja
wakati mwingine Melanie
naomba unitafutie mtoto
mzuri wa kitanzania wa
kustarehe naye.Nimepapenda
sana Tanzania” akasema
James Kasai huku akivuta
sigara na mezani kukiwa na
chupa kubwa ya pombe kali
akinywa taratibu.
“Umekuja na vifaa vyote
nilivyoelekeza?akauliza Khalid
“Ndiyo nimefanikiwa
kupata kila kitu” akajibu
Edwin
“Edwin ninafurahi sana
kufanya kazi nawe.Nimependa
namna ulivyo makini katika
kazi yako natumai huko siku za
usoni tutashirikiana katika
kazi nyingi zaidi za hapa
Tanzania” akasema Khalid
“Usijali Khalid
mashirikiano haya
yataendelea” akasema Edwin
“Kwa kuwa kila kitu tayari
mimi ninakwenda kuanza
kutengeneza bomu” akasema
Khalid na wote wakainuka
wakaelekea ndani.Maboksi
yale aliyokuja nayo Edwin
yakaingizwa katika chumba
maalum ambacho kiliandaliwa
kwa ajili ya kutengenezea
bomu vifaa vikatolewa katika
maboksi,Khalid akavikagua
kama vimetimia na bila
kupoteza muda kazi ikaanza.
Wakati Khalid akianza
kutengeneza bomu Edwin
akamuomba Melanie watoke
wakazungumze nje.
“Melanie kuna kitu
kimetokea jana usiku
sikukujulisha nilitaka
nikifanyie kazi kwanza ndipo
nikujulishe” akasema Edwin.
“Nini kimetokea Edwin?
Akauliza Melanie macho yake
yakionyesha wasiwasi.
“Jana usiku baada ya
kutoka huku nilirejea tena
ofisini nikakuta kuna kitu
kimetokea.Mkurugenzi wetu
mpya alifahamu kwamba kuna
mchezo ulifanyika wakati wa
zoezi la kumfuatilia Khalid”
“Amegundua?akauliza
Melanie
“Ndiyo amegundua”
“Amegundua vip?akauliza
Melanie
“Kuna watu ndani ya idara
ambao niliwatumia katika
kuvuruga zoezi lile kwa
kuwapa fedha kidogo.Baada ya
zoezi kumalizika nilimuondoa
mmoja na kwenda kumuua
kwa ajili ya usalama wetu Yule
mwingine nilitegemea baada
ya kutoka huku ndipo
ningeenda kummaliza lakini
niliporejea ofisini nikakutana
na taarifa kwamba mkurugenzi
akishirikiana na mtu mwingine
ambaye si mfanyakazi wa idara
yetu walimpeleka huyo jamaa
katika chumba cha mahojiano
wakamuhoji kisha wakaanza
kumtesa hadi akapoteza
fahamu.Nilipofika nilimkuta
akiwa tayari amepata fahamu
nikamuuliza nini sababu ya
kuteswa vile akanieleza
kwamba tayari Annabel
anafahamu kuhusu kile
kilichofanyika na alimtesa ili
amueleze ukweli..”
“Alimueleza chochote
?akauliza Melanie kwa wasi
wasi
“Hapana hakumueleza
chochote” akajibu Edwin
“Ahsante.Tayari nilikwisha
anza kuwa na wasi wasi
kwamba mpango wetu
umeingia kirusi” akasema
Melanie
“Nilikuwa nimempa onyo
kwamba akithubutu kusema
chochote ataikosa familia yake
ndiyo maana hakusema
chochote kwa ajili ya familia
yake.Hata hivyo nililazimika
kumuua pale pale katika
chumba alichokuwa
amelazwa”
“Ulifanya jambo zuri
sana.Vipi kuhusu huyo
mkurugenzi?Naye pia
anatakiwa ashughulikiwe
haraka sana kwani kuna kitu
amekwisha anza kukihisi.Huyu
ni hatari mno kwetu” akasema
Melanie
“Tayari nilikwisha anza
kumshughulikia.Jana hiyo
hiyo nililazimika kutumia
kanuni zetu kumuondoa katika
nafasi yake ya ukurugenzi.Pale
idarani tunazo kanuni ambazo
zinatuwezesha wafanyakazi
kumuondoa kiongozi na
niliwashawishi wenzangu
tukazitumia kanuni hizo
kumuondoa Annabel katika
nafasi yake.Atakaa nje ya ofisi
kwa muda wa siku
saba.Nilifanya hivi kwa lengo
la kumuweka nje ya ofisi ili
tuendelee na mipango
yetu.Kwa sasa hakuna wasi
wasi na kila kitu kitaendelea
kama kawida” akasema Edwin
“Ahsante Edwin kwa hicho
ulichokifanya hata hivyo bado
haitoshi.Huyu mwanamke
kama amefanikiwa kugundua
jambo hilo hatakaa kimya
lazima ataendelea kuchunguza
hadi aufahamu ukweli.Kwanza
amefahamuje jambo hilo?Au
watu uliowatumia hawakuwa
makini na wakasababisha
akagundua
walichokifanya?akauliza
Melanie
“Niliowatumia ni watu
makini sana na wanajua
wanachokifanya.Niliyemtumia
kuvuruga mawasiliano anaitwa
Dina ndiye ambaye
tunamtegemea sana katika
masuala yote ya satelaiti.Kwa
ujumla wote hawa wawili
niliowatumia wametekeleza
nilivyowaambia hata mimi
nashindwa kuelewa imetokeaje
hadi Annabel akagundua
kuhusu mchezo
ule.Nitaendelea kuchunguza
kujua namna alivyofahamu”
akasema Edwin
“Sawa Edwin lakini huyu
mwanamke ni kama fisi.Tayari
amenusa harufu ya nyama na
ataendelea kuifuatilia kujua
mahala alipo .Huyu Annabel
tayari amekwisha hisi kuna
kitu kinaendelea na hata kama
akiwa nje ya ofisi ataendelea
kufuatilia hadi aufahamu
ukweli. Huyu ni mdudu
ambaye anatakiwa
kufinyangwa haraka .Nataka
auawe haraka sana kabla
hajaleta madhara” akasema
Melanie
“Huo ndio mpango wangu
lakini kwanza nilitaka
nimuondoe ofisini ili atupe
nafasi ya kutekeleza mipango
yetu na baada ya kutoka ofisini
sasa ninaanza kuandaa
mpango wa kumuua
kumuondoa kabisa ili kuwa na
uhakika kwamba hakuna
kiumbe yeyote ambaye
anaweza kuwa hatari
kwetu”akasema Edwin
“Vipi kuhusu Gosu Gosu ?
Kuna taarifa zozote umepata
kutoka hospitali?akauliza
Melanie
“Gosu Gosu sijapata bado
taarifa zake zozote”
“Kill him today ! akasema
Melanie
“Nataka hadi jua
litakapochwea Gosu Gosu awe
tayari ameuawa.Kwa namna
yoyote ile hakikisha siku ya leo
haipiti bila Gosu Gosu
kuuawa.Yule ni mtu hatari
sana kwani mipango yangu
mingi anaifahamu na kwa
mujibu wa Devotha,Gosu Gosu
ana ukaribu na watu ambao
wanaweza kuwa hatari
kwetu.Endapo akifumbua
macho anaweza akawaeleza
watu hao kuhusu mimi na
mambo yakaharibika.Make
sure you kill him today.Sitaki
kuwe na uchafu wowote njiani
tunamopita” akasema Melanie
“Usijali Melanie
nitakapotoka hapa
ninakwenda kushughulikia
suala hilo.Devotha
umewasiliana naye
leo?akauliza Edwin
“Nilijaribu kumtafuta
lakini hapatikani
simuni.Nitamtafuta tena
baadae” akasema Melanie
“Jenerali Akiki alinipigia
simu asubuhi akanijulisha
kwamba alizungumza na Dr
Fabian kuhusu kuandaa
mkutano na amekubali”
“That’s good” akasema
Edwin huku akitabasamu
“Lini wanakutana kwa
mazungumzo?akauliza Edwin
“Jenerali Akiki alitaka iwe
kesho lakini Dr Fabian
ameahidi kumjulisha hapo
baadae baada ya kuwasiliana
kwanza na Rais Patrice
Eyenga”
“Kama Dr Fabian
amekubali basi hata Patrice
hawezi kukataa na kama
Jenerali Akiki ametaka kikao
kifanyike kesho basi
kitafanyika hiyo kesho.Hii ni
fursa ambayo wanaitafuta sana
kukaa meza moja na Jenerali
Akiki kuzungumza na
hawataweza kuipuuzia hata
kidogo.Melanie ninakusifu
sana kwa uwezo mkubwa ulio
nao hadi ukaweza
kumshawishi Jenerali Akiki
akakubaliana nawe”
“Kila penye nia pana njia
Edwin.Ninataka kulipiza kisasi
na lazima nifanye kila
linalowezekana kuhakikisha
mipango yangu inakamilika”
“Khalid amekwisha fanya
mawasiliano na mtu aliyeahidi
kumleta kwa ajili ya kutekeleza
shambulio la kujitoa
mhanga?akauliza Edwin
“Ndiyo.Tayari amekwisha
fanya mawasiliano na hivi
tuzungumzavyo tayari mtu
huyo amekwisha anza safari.Ni
mtu kutoka katika kundi la
Alshabaab la nchini Somalia
ambaye makazi yake ni nchini
Kenya.Tayari amekwisha vuka
mpaka wa Namanga hivi sasa
anaelekea Arusha.Kesho
asubuhi tutampokea hapa Dar
es salaam” akasema Melanie
“Huyu anatakiwa kufika
Dar es salaam leo hii hii ili
tuwe na uhakika mkubwa
kwamba tunaye mtu wa
kutekeleza shambulio hilo.Hivi
sasa bomu linatengenezwa na
alitakiwa awepo hapa tayari
kwa kazi hiyo.Khalid
anatakiwa kuwasiliana na
huyo mtu na kumtaka akifika
Arusha asiendelee tena na
safari.Mimi nitaruka na
helkopta kwenda
kumchukua.Kila kitu lazima
kikamilike leo hii hii” akasema
Edwin
“Hilo ni wazo zuri sana
Edwin” akasema Melanie
wakaelekea ndani ambako
Khalid alikuwa anaendelea na
maandalizi ya kuunda bomu.
Wakamueleza mapendekezo ya
Edwin akakubaliana nayo
kisha kwa kutumia simu ya
Melanie akawasiliana na huyo
mtu aliyekuwa njiani akielekea
Dar es salaam kwenda
kutekeleza shambulio la
kujitoa mhanga akampa
maelekezo ya kutoendelea na
safari atakapofika Arusha na
asubiri maelekezo mengine
“Kwa kuwa limejitokeza
suala hili la huyu mtu
nalazimika kuahirisha baadhi
ya mambo ili nielekee Arusha
kumchukua kisha nirejee
mapema Dar es salaam
kuendelea na masuala
mengine” akasema Edwin
“Sawa Edwin lakini
hakikisha unapoondoka
umeacha watu
watakaolishughulikia suala la
Gosu Gosu pamoja na
mkurugenzi wako Annabel”
akasema Melanie
“Sawa Melanie nitatoa
maelekezo kwa vijana wafanye
uchunguzi namna
tukavyoweza kumuua Gosu
Gosu.Lazima kwanza tufanye
uchunguzi kwa kuwa naamini
umakini utakuwa mkubwa
sana baada ya jaribio lile la
kwanza la kumuua kushindwa
kufanikiwa.Vijana wataniletea
mapendekezo ya namna
tutakavyoweza kutekeleza
mpango huo wa kumuua Gosu
Gosu halafu tutajipanga kwa
usiku wa leo tuweze
kumuonda.Kuhusu Annabel
nitalazimika kumfanyia
uchunguzi kwa kuwa mpaka
sasa sifahamu mahala
anakoishi.Kwa Rais kumpa
nafasi kama ile ya ukurugenzi
wa idara nyeti lazima
amejiridhisha kuwa ana
sifa.Lazima atakuwa ni mtu
mwenye mafunzo ya ujasusi na
anafahamu mbinu nyingi hivyo
kumuua inahitaji umakini
mkubwa.Nitalishughulikia
suala lake nitakaporejea
kutoka Arusha.Msiwe na
wasiwasi wowote kila kitu
kitakwenda vizuri.” akasema
Edwin kisha akaagana na
Melanie akaondoka
“Melanie yuko sahihi
kbaisa.Annabel anastahili
kuuawa lakini kuuawa kwake
kunapaswa kufanywa
kiutaalamu
mno.Nitalishughulikia hili
baada ya kurejea kutoka
Arusha” akawaza Edwin akiwa
garini baada ya kuondoka
nyumbani kwa Melanie
PARIS – UFARANSA
Mlinzi aliyesimama katika
mlano wa ofisi ya Rais wa
Ufaransa aliufungua mlango
watu wawili wakaingia na Rais
Michael Weren akasimama
akawakaribisha watu wale
wakasalimiana kisha
akawaelekeza waketi sofani.
“Nilitegemea Devotha awe
amekwisha fika hapa hadi
mida hii lakini bado hajafika
naomba dakika chache
tumsubiri kwani yeye ni
muhimu sana katika
mazungumzo haya” akasema
Michael Weren na kwenda
mezani kwake akachukua simu
akampigia Devotha lakini simu
yake haikuwa inapatikana
“Simu ya Devotha
haipatikani nadhani tuendelee
na mazungumzo atakuta
tukiendelea” akasema Michael
Weren
“Mheshimiwa Rais kubwa
ambalo limetuleta hapa ni
kutaka kupata mrejesho
kuhusiana na ule mpango wetu
wa Afrika.Nini kinaendelea
hadi hivi sasa?akauliza mmoja
wa wale jamaa aliyekuwa na
suti ya rangi ya kijivu
“Kwa ujumla mpango wetu
unakwenda vizuri sana mpaka
sasa.Kama mnavyosikia katika
vyombo vya habari ni kwamba
hali ya kiusalama katika eneo
la Afrika mashariki ni
tete.Kumetokea mvurugano
mkubwa sana na jumuiya kwa
sasa iko hatarini
kuvunjika.Rwanda na Uganda
zinashambuliana
mpakani.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo nayo
imepeleka vikosi vyake katika
mpaka wake na Uganda.Nchi
tatu za Tanzania,Rwanda na
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo zinaandaa kikosi cha
pamoja kwa ajili ya kuvamia
nchini Uganda kumsaka James
Kasai ambaye alitekeleza
shambulio lililopelekea
mvurugano huu
ukatokea.Tayari Uganda
imetoa onyo kwamba endapo
kikosi hicho kitathubutu kutia
mguu wake nchini Uganda
basi itatumia nguvu kubwa
kukisambaza.Haya yoteni
matokeo ya mipango yetu na
hakuna ubishi kwamba jumuia
ya Afrika mashariki inakwenda
kusambaratika” akasema
Michale Weren
“Tunafuatilia sana hali ya
mambo inavyokwenda Afrika
mashariki na zipo dalili
kwamba jumuiya hiyo inaweza
ikasambaratika na sisi
tukapata njia ya kupita
kuelekea Congo lakini kuna
jambo ambalo linaleta ukakasi
kidogo njia iliyotumika katika
kusababisha hali hii
ikatokea.James Kasai
anayeongoza kikundi cha
waasi pamoja na kikundi cha
kigaidi cha IS walishirikishwa
katika mpango huu.Hii imetia
doa mpango
wetu.Hatukupanga kuwatumia
magaidi au James Kasai
ambaye amekwisha ua mamia
ya watu na anatafutwa na
mahakama ya kimataifa ya
uhalifu wa kivita kutokana na
mauaji aliyoyafanya.Mtu kama
James Kasai au kikundi cha IS
kufahamu mipango yetu ni
hatari kubwa sana kwetu”
akasema Yule mzee
“Hata mimi nilipoelezwa
mara ya kwanza kwamba
James Kasai na kikundi cha
kigaidi cha IS
wameshirikishwa katika
mpango huu nilistuka na
kutaka mpango huo wa
kuwatumia watu hao usitishwe
mara moja lakini nikapewa
ufafanuzi na faida za
kuwatumia James na IS
nikaona ni mpango mzuri
nikatoa maelekezo kwamba
waendelee kushirikiana nao”
akasema Michael
“Unaweza ukatueleza
mheshimiwa Rais faida za
kuwatumia hawa magaidi na
James Kasai?
“Faida kubwa ni kwamba
mpango huu hautajulikana
kama sisi tunahusika
utaonekana ni mpango wa IS
na James Kasai.Mpaka sasa
nchi za Afrika mashariki
zinamsaka James kwa udi na
uvumba na hii inatupa sisi
nafasi ya kuendelea na
mipango yetu bila ya
kutambulika”akasema Rais
Michael na kuwaeleza
kuhusiana na mpango
unaoendelea wa kuwaua
marais wa Tanzania na Congo
kuwafafanulia faida zake
“Kama mpango huo
utafanikiwa basi itakuwa ni
chanzo cha vita kati ya majeshi
ya serikali ya Congo na kikundi
cha James Kasai na vikundi
vingine pia vitaibuka nchi ya
Congo itarejea kuwa kama
ilivyokuwa zamani.Patrice
Eyenga amekuwa ni kikwazo
kikubwa kwetu lakini kama
jumuiya ya Afrika mashariki
ikisambaratika na
tukafanikiwa kumuua Patrice
Eyenga basi njia itakuwa
nyeupe ya kuingia
Congo”akasema Michael
“Ni mpango mzuri sana
huo lakini nina mapendekezo
kwamba huyu mtu ambaye
ametumwa kwenda
kufanikisha mpango huu
auawe mara tu
atakapokamilisha mpango
huo.Mtu huyo kuendelea kuwa
hai ni hatari sana kwetu.Ni
vipi kama siku moja James
Kasai akakamatwa na kumtaja
kuwa anashirikiana naye?
Itakua ni aibu kubwa kwetu
hivyo napendekeza mara tu
atakapokuwa amemaliza kazi
yake auawe mara moja na sisi
tuendelee na mipango
mingine” akatoa ushauri
mmoja wa wale jamaa
“Ushauri wako ni mzuri na
nitauzingatia.Ni kweli huyu
mtu akiendelea kuwepo hai
itakuwa ni hatari kubwa
kwetu.Wazo la kumuua ni
zuri” akasema Rais Michael
Weren na baada ya
mazungumzo ya takribani saa
mbili akaagana na wageni
wake wakaondoka.Mara tu
wageni wake walipoondoka
Rais Michael akachukua tena
simu na kumpigia Devotha
lakini bado simu yake
haikupatikana
“Devotha uko wapi?
Ninahitaji sana kujua taarifa za
kinachoendelea Tanzania”
akawaza Michael na kuketi
katika kiti chake akaweka
miguu juu ya meza
“Kwa nini Melanie
akaanzisha mashirikiano na
magaidi wa IS? Naamini
lazima atakuwa amewaeleza
kuhusiana na mipango yetu na
hiki ni kitu kibaya sana.Jambo
hili si la kuchukulia kirahisi
kwani magaidi hawa wanaweza
wakatugeuka siku za usoni na
kutuchafua.Nadhani
pendekezo la kumuua Melanie
ni zuri.Mara tu atakapomaliza
mpango wa kuwaua marais wa
Tanzania na Congo lazima
naye auawe.Nitajadiliana na
Devotha kwa kina suala hili”
akawaza Michael.
TANZANIA
Saa kumi bna mbili za
jioni helkopta ya idara ya
SNSA ilitua katika bohari kuu
la idara hiyo.Edwin Mbeko
alikuwa ametoka jijini Arusha
kumchukua mtu ambaye
angetekeleza shambulio la
kujitoa mhanga lililolenga
kuwaua marais Dr Fabian na
Patrice Eyenga.Tayari gari lake
lilikwisha fika mahala pale
akashuka katika helkopta
pamoja na mtu wake
aliyekwenda kumchukua
Arusha wakaingia garini na
kuondoka kuelekea nyumbani
kwa Melanie Davis.
“Abdi karibu sana Dar es
salaam” akasema Edwin lakini
Abdi hakujibu kitu alikuwa
ameelekeza macho yake nje
akitazama pilika pilika za jioni
za wakazi wa jiji la Dar es
salaam.
Safari iliendelea kimya
kimya hadi walipowasili
nyumbani kwa Melanie
akafunguliwa geti na kuingia
ndani.Melanie aliwapokea na
kuwakaribisha sebuleni
ambako James Kasai alikuwa
ametulia sofani akiwa na
chupa kubwa ya mvinyo.
“Karibu sana Abdi.Huyu ni
James Kasai naamini
umewahbi kusikia taarifa zake”
Melanie akafanya utambulisho
na Abdi alionekana kustuka
kidogo kumfahamu James
Kasai. Melanie akamchukua na
kumpeleka katika chumba
alichoandaliwa ili apumzike
kabla ya mazungumzo hapo
baadae.
“Mambo yanakwendaje
hapa?akauliza Edwin
“Mambo yanakwenda
vizuri.Khalid anaendelea na
uundaji wa bomu na kwa
maelezo yake anaelekea katika
hatua za mwisho
kulikamlisha”akajibu Melanie
“Vizuri sana.Mpaka hapa
tuna uhakika kwamba bomu
linaelekea kukamilika na mtu
wa kulilipua tunaye.Umepata
mrejesho wowote kutoka kwa
Jenerali Akiki?Edwin akauliza
“Ndiyo.Amenipigia simu
akanijulisha kwamba marais
Dr Fabian na Patrice Eyenga
wamekubali kukutana naye
kesho jijini Dar es
salaam.Mipango yetu yote
inakwenda vizuri”
“Safi sana.Nitarejea hapa
baadae natakiwa kurejea
ofisini nikashughulikie suala la
Gosu Gosu kwani niliwachia
kazi vijana wachunguze namna
tutakavyoweza kumuua.Kabla
ya mapambazuko ya lazima
Gosu Gosu awe
ameuawa.Devotha
umewasiliana naye? Akauliza
Edwin
“Hapana hajanipigia
simu.Mara nyingi yeye
hunitafuta kutaka kujua kila
kinachoendelea huku lakini
nashangaa mpaka muda huu
hajanitafuta na siyo kawaida
yake” akasema Melanie
“Sawa nitamtafuta
nimjulishe kile
kinachoendelea” akasema
Edwin akaagana na Melanie
akaingia garini na kabla ya
kuondoka akachukua simu
akazitafuta namba za Devotha
akampigia lakini simu yake
haikupatikana.
“Where are you
Devotha?Kwa nini leo
hupatikani?akajiuliza Edwin
akawasha gari na kuondoka
“Kila kitu kimekamilika
kwa ajili ya tukio la kesho.Dr
Fabian kama angejua kwamba
kesho atakufa angeanza
kutubu kuanzia sasa
kumuomba Mumgu amsamehe
makosa yake kwani sku ya
kesho hataimaliza atakuwa
amekufa.Nina hasira naye
sana Yule jamaa ameniweka
kukaimu nafasi kwa miaka
mitatu halafu anakuja kumpa
ukurugenzi mtu mwingine
kabisa na kuniacha mimi
ambaye nimefanya kazi kwa
ufanisi mkubwa kwa miaka
mitatu.Baada ya kufariki mimi
nitaendelea kuwa mkurugenzi
kwani Annabel hatarejea
tena.Hakuna wa kumrejesha”
akawaza na kutabasamu
“Usiku huu nitamuondoa
Gosu Gosu na baada ya hapo
nitaanza kumsaka
Annabel.Lazima naye
afe.Kama alivyosema Melanie
kwamba Annabel ni mdudu
anayetakiwa kufinyangwa
haraka sana kabla hajaleta
madhara makubwa”
Edwin aliendelea kuwaza
mambo mengi hadi alipofika
katika jengo la makao makuu
ya SNSA akashuka garini na
kuelekea ofisini kwake ambako
alipewa taarifa kuhusiana na
maandalizi ya mazishi ya
Fidelis na vile vile akajulishwa
kuhusu kifo cha Edina .Edwin
akaonyesha masikitiko
makubwa kwa taarifa ile
mbaya.Hakupoteza muda
akaenda kuzungumza na
wafanyakazi
“Ndugu zangu habari za
muda huu.Awali ya yote
ninapenda kuwashukuru sana
kwa ushirikiano mkubwa
mliouonyesha jana hadi
tukafanikiwa kumuondoa
Annabel ambaye alionekana
kushindwa kumudu vyema
majukumu yake na hata
kupelekea kifo cha mwenzetu
Fideli.Tayari suala lake liko
kwa Rais analishughulikia na
tunasubiri maamuzi
yake.Nimetaarifiwa pia
kwamba maandalizi ya mazishi
ya Fidelis yanaendelea vizuri
na kwa mujibu wa wanafamilia
atazikwa kesho kutwa na sisi
tutashiriki kikamilifu.
Tukiachana na taarifa hizo
za Fidelis,nimepewa tena
taarifa nyingine mbaya za
kuhuzunisha kwamba
mwenzetu,kipenzi
chetu,mdogo wetu dada yetu
Edina amefariki
dunia.Nimestushwa sana na
taarifa hizo.Taarifa zinadai
amepigwa risasi yeye na
mdogo wake.Huu ni ukatili
mkubwa sana amefanyiwa
huyu mwenzetu.Japokuwa
tayari jeshi la polisi linaendela
na uchunguzi wa suala hili sisi
pia tunapaswa kufanya
uchunguzi kujua nani hasa
aliyemuua Edina? Binafsi
ninaunganisha kifo cha Edina
na kifo cha Fidelis.Nina
uhakika vina muunganiko na
aliyesababisha kifo cha Fidelis
ndiye aliyemuua
Edina.Tutaandaa timu ya
kufanya uchunguzi wa kina
kuhusu jambo hili.Hili ni pigo
lingine kubwa tunalipata ndani
ya kindi kifupi hta hivyo
hatupaswi kukata
tamaa.Tutaendelea na jukumu
letu la ulinzi wa nchi na wale
wote wenye lengo la
kutukwamisha
hawatafanikiwa”Edwin
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Jambo la tatu ninalotaka
kuwajulisheni ni kwamba
ninaliondoa rasmi mezani
suala la Khalid Sultan Khalid
lililoletwa na Annabel.Mpaka
sasa hatuna ushahidi wowote
wa kutosha kuhusiana na huyu
mtu ambaye tuliagizwa
kumfuatilia.Annabel akipaswa
kutupa uthibitsho usio na
shaka kuhusiana na uhatari wa
huyu mtu kwa nchi
yetu.Hatutaendelea tena
kupoteza muda kumtafuta
Khalid ambaye hatuna uhakika
kama ni gaidi hadi hapo
Annabel kama atabahatika
kurejea atupe uthibitisho
kwamba kweli mtu huyu ni
gaidi kutoka IS hivyo kuanzia
sasa hakuna mtu yeyote
kuendelea na suala lile
nimeliondoa rasmi” akasema
Edwin na kutoa maelekezo
kadhaa akarejea ofisini kwake
ambako vijana wawili ambao
aliwatuma kufanya uchunguzi
hospitali kutafuta namna ya
kumuua Gosu Gosu
wakamfuata
“Victor naamini kazi
niliyowatuma mmeikamilisha”
akasema Edwin
“Mkuu ile kazi
haijakamilika kw……..
“Kwa nini haijakamilika
wakati niliwaambia kwamba ni
kazi ya muhimu? Akauliza
Edwin kwa ukali
“Mkuu kuna jambo
limejitokeza ndiyo maana
tulishindwa kuikamilisha kazi
uliyotutuma” akasema Victor
“Nini kimetokea?akauliza
Edwin
“Gosu Gosu hayupo
hospitali amehamishwa”
“Amehamishwa?! Edwin
akashangaa
“Ndiyo mkuu
amehamishwa.Hayupo pale
hospitali”
Edwin akavuta pumzi
ndefu na kuwatazama vijana
wake akauliza
“Amehamishiwa
wapi?akauliza
“Hatujui mkuu”
Edwin akagonga meza kwa
hasira
“Kwa nini msijue
amehamishiwa wapi?
“Mkuu hilo jambo
limefanywa kwa siri kubwa na
hata wafanyakazi wa hospitali
hawajui mahala
alikohamishiwa Gosu
Gosu.Kwa mujibu wa watu
tuliowahoji ni kwamba lilifika
gari la wagonjwa ambalo si la
hospitali ile na Gosu Gosu
akatolewa katika wodi
akaingiwa garini likaondoka
bila taarifa kwamba linaelekea
wapi lakini tulipata maelezo
kwamba kabla ya kuondolewa
hospitali daktari anayejulikana
kama Dr Masawe alikuwa na
mazungumzo na watu Fulani
wawili ofisini kwake halafu
baada ya muda likafika hilo
gari Gosu Gosu akahamishwa
na huyo daktari na wengine
wawili pamoja na wauguzi
wawili waliondoka na gari
lingine na tunadhani
walilifuata lile gari lililombeba
Gosu Gosu.Tumefuatilia
hospitali mbali mbali kubwa
lakini hajapelekwa huko”
akasema Victor na Edwin
akashika kichwa .
“Walifahamu Gosu Gosu
yuko hatarini kuuawa ndiyo
maana wameamua kumtoa
pale hospitali na kumpeleka
mafichoni.Wamempeleka
wapi? Akajiuliza Edwin
“Mkuu kutokana na
uchunguzi wetu inaonekana
huyo Dr Masawe kuna kitu
anakifahamu kuhusu
kuhamishwa kwa Gosu Gosu
na kama tukimpata tunaweza
kufahamu alikopelekwa
mgonjwa.Tulikwenda mbali
zaidi na kufahamu hadi
mahala anakoishi huyo Dr
Masawe lakini hatukuweza
kufanya chochote tukisubiri
maelekezo yako”akasema
Victor
“Good.Kazi nzuri sana
mmeifanya.Kama tayari
mmefanikiwa kufahamu
mahala anakosihi Dr Masawe
itakuwa rahisi sana kwetu
kufahamu mahala alipo Gosu
Gosu” akasema Edwin na
kuwaelekeza wale vijana
kwenda kujiandaa
“Kwa namna yoyote ile
lazima Gosu Gosu apatikane
na auawe.Lile tayari ni bomu
na linaweza kulipuka muda
wowote hivyo lazima tulitegue
haraka sana.Melanie alifanya
kosa kubwa kuanzisha
mahusiano na mtu kama Yule
na sasa inatugharimu kuanza
kumuwinda” akawaza Edwin
na kumuita dereva wake
ambaye alifika mara moja
“Jackson kuna kazi
ambayo nataka nikupe
ikaisimamie na kuhakikisha
inakamilika” akasema Edwin
na kumuelekeza Jackson
kuhusiana na zoezi lile la
kumuua Gosu Gosu na
akamtaka ahakikishe anaipata
familia nzima ya Dr
Masawe.Baada ya maelekezo
yale Jackson na vijana wengine
watatu wakaondoka kuelekea
nyumbani kwa Dr Masawe.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 2
Tangu alipotolewa
hospitali na kuletwa katika
nyumba ambayo Mathew
aliiandaa,hali ya Gosu Gosu
bado iliendelea kuwa
mbaya.Alipoteza fahamu
wakati wa zoezi la
kumuhamisha kumtoa
hospitali na hadi giza linangia
hakuwa amerejewa na fahamu.
“Mathew lengo lako la
kumtoa Gosu Gosu kule
hospitali na kumleta hapa ni
zuri sana kwa ajili ya usalama
wake lakini kwa hali hii
aliyonayo nasikitika kusema
kwamba tutalazimika
kumrejesha tena hospitali
akafanyiwe uchunguzi
zaidi.Hapa hatuna vifaa vya
kuweza kumfanyia uchunguzi
kufahamu nini hasa tatizo
lake” Dr Masawe akamueleza
Mathew.
“Dr Masawe naomba
unieleze ukweli kuhusu Gosu
Gosu.Is he going to make
it?akauliza Mathew
“I don’t know Mathew.Hali
ya Gosu Gosu inatuchanganya
sana ndiyo maana ninashauri
tumrejeshe tena hospitali kwa
ajili ya uchunguzi zaidi.Kwa
hali yake ilivyokuwa
hakupaswa kuhamishwa
kuletwa hapa.Kama ni usalama
wake tutatumia walinzi au
tutaomba msaada wa jeshi la
polisi kumlinda isitoshe ana
mahusiano na Rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania
tukimueleza hali halisi
anaweza akatupa
msaada.Kuendelea kumuweka
hapa Gosu Gosu ni
kuhatarisha maisha yake”
akasema Dr Masawe.Mathew
akainamisha kichwa akazama
mawazoni.
“Mathew umejitahidi sana
kuhakikisha mwenzako
anakuwa salama lakini kwa
hapa ilipofika hakuna namna
lazima arudi hospitali”
akaendelea kusisitiza Dr
Masawe.
“Ahsante kwa ushauri
wako Dr Masawe lakini
hapana.Gosu Gosu ataendelea
kukaa hapa hapa.Hatarejea
tena hospitali.Endeleeni
kumuhudumia hapa hapa na
kama ni kupoteza maisha
apoteze maisha akiwa hapa
ndani kwa amri ya Mungu na
si binadamu mwingine kuitoa
roho yake” akasema Mathew
“Mathew mimi ni daktari
na ninashauri Gosu Gosu
arejeshwe hospitali ili tuweze
kuokao maisha yake.Tafadhali
sana” akasema Dr Masawe
“Dr Masawe nimeigeuza
nyumba hii hospitali kwa ajili
ya Gosu Gosu.Nimenunua kila
kifaa ulichokiorodhesha kwa
ajili ya kumsaidia Gosu Gosu
akiwa hapa hivyo ataendelea
kupatiwa matibabu hapa hapa
na hatakwenda tena sehemu
yoyote.Endeleeni
kumuhudumia kwa kila uwezo
mlio nao na kama akipoteza
maisha itakuwa ni amri ya
Mungu.Hakuna tena mjadala
katika hilo Dr Masawe !
akasema Mathew
“Mathew nafahamu
umetumia gharama kubwa
sana kununua mashine na
vifaa mbali mbali kwa ajili ya
kumsaidia Gosu Gosu lakini
bado ushauri wangu uko pale
pale kwamba tunatakiwa
kumrejesha
hospitali.Yawezekana
waliokuwa wanataka kumuua
wamekwisha fika hospitali na
kugundua amehamishwa na
hawajui mahala alipo hivyo
wataachana na zoezi hilo”
“You don’t know anything
Dr Masawe” akasema Mathew
na kutoka sebuleni akaenda
katika chumba alimokuwa
amelazwa Gosu Gosu
akawakuta madaktari wengine
wawili na wauguzi wakiwa
wamesimama wanamtazama
Gosu Gosu.Akamsogelea
karibu
“Gosu Gosu nimefanya
maamuzi magumu
kukuhamisha kutoka hospitali
kukuleta hapa ambako
naamini ni sehemu
salama.Siogopi kutumia hadi
shilingi ya mwisho
kuhakikisha unakuwa salama.I
hope you are going to wake up
soon brother ” akawaza
Mathew huku akimtazama
GosuGosu halafu akatoka mle
chumbani akaenda katika
chumba alimolazwa Austin
ambaye naye alihamishwa
hospitali na hali yake ilikuwa
inaendelea vizuri akamueleza
kile kinachoendelea
“It’s a taugh call Mathew
but it’s the right one.Mathew
ahsante sana kwa maamuzi
haya uliyoyafanya ya
kuhakikisha tunakuwa salama
kwa kutuleta hapa.Pale
hospitali chochote kingeweza
kutokea.Hawa watu lazima
wangefanya kila juhudi
kuhakikisha
tunauawa.Mathew wewe ni
kaka yet…….” Austin
akanyamaza baada ya Ruby
kuingia mle ndani kwa kasi na
kuwastua sana
“Kuna nini Ruby?akauliza
Mathew
“Dr Masawe” akasema
Ruby
“Kafanya nini?Mathew
akauliza
“Wakati tunaendelea na
maongezi amepigiwa simu na
mtu halafua kafungua kitu
kama video katika simu yake
na sura yake ikabadilika ghafla
kisha akanitaka nikamfungulie
geti kuna mahala
anaelekea.Ameondoka kwa
kasi ya ajabu” akasema
Melanie
“What’s going
on?Hajakueleza
chochote?akauliza Mathew
“Hapana hajaniuliza
chochote” akajibu
Ruby.Mathew akajaribu
kumpigia lakini hakupokea
simu.
“Hapokei simu
yawezekana amepata taarifa
mbaya za mgonjwa na
anamuwahi” akasema Mathew
“Kwa mstuko alioupata
baada ya kutazama ile video
katika simu yake pokea ile
simu na kwa namna
alivyoondoka sina hakika
kama anamuwahi
mgonjwa.Halafu hata kama
angekuwa anamuwahi
mgonjwa lazima angetueleza
lakini ameondoka kimya
kimya bila kusema
chochote.Something is not
right” akasema Ruby
“Usihofu Ruby kama kuna
kitu kibaya Dr Masawe
atatueleza” akasema Mathew
huku akitazama saa yake
“Austin sisi
tunaondoka.Usiku wa leo
tunavamia ofisi za
SNSA.Ninahitaji kumpata
Edwin Mbeko usiku wa
leo.Madaktari wako hapa na
wauguzi wanaendelea
kumtazama Gosu
Gosu.Natamani tungekuwepo
na sisi pamoja nanyi lakini
tuna kazi nyingine kubwa ya
kufanya.Ni kazi ngumu na ya
hatari kutokana na ulinzi
mkali uliopo SNSA lakini
nakuahidi tutarejea salama”
akasema Mathew
“Ninaelewa
Mathew.Ninawatakia kila la
heri.Hakikisheni mnampata
huyo Edwin” akasema
Austin.Mathew akachomoa
bastora na kumpa.
“Kama likitokea tatizo
lolote kabla hatujarejea please
save yourself and Gosu Gosu
too” akasema Mathew kisha
wakatoka na kwenda kuwaaga
wale madaktari
wanaomuhudumia Gosu Gosu
na kuwakuta wakijadiliana
kuhusiana na namna Dr
Masawe alivyoondoka.Mathew
akawaaga kwamba
wanaondoka na watarejea
baadae wakaingia garini na
kuondoka.
“Mathew I’m
scared.Tunaondoka wakati hali
ya Gosu Gosu ni
mbaya”akasema Ruby
“Tunahitaji kuwa majasiri
sana wakati huu.Kama hali ya
Gosu Gosu ingekuwa
inaruhusu kusafirishwa
kwenda nje ya nchi tungefanya
hivyo lakini kwa hali yake
hatuwezi kumsafirisha na kule
hospitali hatuwezi kumrejesha
tena kwa sababu za
kiusalama.Kilichobaki hapa ni
kumkabidhi Mungu suala hili
yeye ndiye mwamuzi wa yote
akiamua kumchukua Gosu
Gosu sisi hatupaswi
kulalamika.Naamini Mungu
anaona mawazo yetu na
anasikia maombi yetu hivyo
atamponya Gosu Gosu”
akasema Mathew
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 3
“Ruby hii ni misheni ya
hatari sana hivyo
hatutaongozana
wote.Nitakwenda peke yangu
wewe utabaki hapa
ukiniongoza” akasema Mathew
wakiwa katika ofisi ya
nyumbani kwake
“Sawa Mathew nitajiunga
na SNSA nitakuongoza hadi
kufika katika ofisi ya
Edwin.Hata kama hatakuwepo
ofisini lakini unaweza
ukafanikiwa kupata kitu
ambacho kinaweza kutusaidia
kufahamu kwa kina
mahusiano yake na Devotha na
vile vile tujue kama ana
mahusiano na Melanie Davis”
akasema Ruby
“Kitu cha kwanza
ninachokitaka baada ya
kuvuka geti kuu ni kuzima
umeme.Kukiwa giza nitaweza
kuingia kwa urahisi zaidi
ndani”
“Kuna chumba maalum
ambacho kina kila kitu
kinachohusiana na umeme wa
jengo lile na ndani ya chumba
hicho kuna jenereta la dharura
pindi umeme
ukikatika.Unapoingia katika
maegesho ya viongozi mkono
wako wa kulia utaiona nyumba
ina madirisha makubwa na
nyumba hiyo ndiyo ina
jenereta na vifaa vyote vya
umeme wa jengo” akasema
Ruby huku akiendelea kubofya
kompyuta yake
“I’m in” akasema Ruby
kisha ramani ya jengo la
makao makuu ya SNSA
ikaonekana katika kompyuta
yake akaihamishia katika
runinga kubwa ukutani
“Hii ndiyo ramani ya jengo
la makao makuu ya SNSA.Ile
nyumba ninayokwambia ilimo
jenereta ya umeme haiko
katika ramani hii kwa sababu
haina muda mrefu toka
imejengwa.Utakapozima
umeme utaelekea katika
maegesho ya viongozi na
utatumia mlango huu wa
maegesho ya viongozi kuingia
ndani ya jengo. Umeme
unapokatika jenereta huwaka
baada ya dakika moja lakini
nitabadilisha katika mfumo ili
liwake baada ya dakika
tatu.Nitafanya hivi ili uweze
kutumia muda huo kuufungua
mlango wa kuingilia ndani
kupitia maegesho ambao
hufunguliwa kwa kadi maalum
lakini wewe utatumia vifaa
vyako kuufungua mlango huo .
Ukishaingia ndani ya jengo
hilo umeme utawaka na
utapita njia hii hapa ambayo ni
njia ya dharura ya kupita
viongozi endapo kutatokea
dharura yoyote aidha ya moto
au kitu chochote cha
hatari.Utakutana na mlango
ambao namba zake za
kufungulia ni
KW23T860.Ukifungua huo
mlango itaonekana katika
mfumo wao hivyo ukiufungua
na kuingia ndani utabonyeza
namba TTY79 na itajulikana ni
mmoja wa watu wa idara ya
SNSA.Utaelekea hadi ghorofa
ya tano ambako ndiko ziliko
ofisi zetu.Nitakuunganisha na
kompyuta hii ili niwe nakuona
na kukupa maelekezo njia ya
kupita kuelekea katika ofisi ya
Edwin” akasema Ruby.
Mathew akatoka na
kuelekea katika chumba chake
ambacho kulikuwa na silaha
na vifaa vingine mbali mbali
akaanza kujiandaa.Alipokuwa
tayari akarejea ofisini
alikomuacha Ruby.
“Mathew umevaa
kikomando hasa” akasema
Ruby
“Ni kutokana na ulinzi
uliopo mahala hapo
ninakoelekea ndiyo maana
nimejiandaa kiasi
hiki”akasema Mathew na
kuweka mezani kifaa Fulani
kama boksi akakifungua na
kukiwasha halafu akachukua
kidude kidogo na kukiweka
sikioni
“Huu ni mtambo mdogo
kwa ajili ya mawasiliano.Kuna
dishi kubwa la satelaiti liko nje
ya nyumba ambalo ni maalum
kwa ajili ya kifaa hiki ambacho
ndicho tutatumia kwa
mawasiliano.” akasema
Mathew na kufanya majaribio
na kifaa kile kilifanya kazi
vizuri
“Mathew hakikisha
unafanikiwa kumpata
Edwin.Ni mtu ambaye
tunamuhitaji sana”akasema
Ruby
“Usijali Ruby nitatumia
kila uwezo nilio nao
kuhakikisha Edwin
anapatikana usiku huu”
akasema Mathew
wakakumbatiana
“Mathew please be safe !
akasema Ruby na Mathew
akachukua begi lake akalivaa
mgongoni akaelekea katika
gari na kuondoka.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 4
“Ee Mungu naomba
usimame na familia yangu ili
hao waliowateka wasiwafanyie
kitu chochote kibaya” Dr
Godwin Masawe alimuomba
Mungu.
Alipokuwa nyumbani kwa
Mathew akizungumza na Ruby
alipigiwa simu na mtu
asiyemfahamu akamtaka
atazame video atakayomtumia
na alipoitazama video
aliyotumiwa aliwaona mke na
watoto wake wakiwa
wamefungwa mikono huku
wamepigishwa magoti na watu
wawili waliofunika nyuso zao
wakiwa na bunduki
wakiwalinda.Mtu Yule
aliyempigia simu alimtaka
awashe gari na aondoke
mahala alipo aende nyumbani
kwake na asithubutu
kuwajulisha polisi au mtu
yeyote kuhusu tukio lile.Hii
ndiyo sababu iliyomfanya Dr
Masawe kuondoka kimya
kimya nyumbani kwa Mathew
bila kuaga mtu yeyote.
“Nani hawa walioteka
familia yangu? Nini
wanakitaka hadi wakafanya
hivi?akajiuliza maswali mengi
Dr Masawe alifika
nyumbani kwake akapiga honi
lakini hakuna aliyetoka
kumfungulia geti akalazimka
kushuka garini akaenda
taratibu na kulisukuma geti
halikuwa limefungwa
akaingiza gari ndani.Akashuka
kwa tahadhari na kuingia
ndani akamuita mke wake
lakini hakukuwa na dalili
zozote za kuwepo mtu mle
ndani.Ni sauti ya runinga
ndiyo iliyosikika
sebuleni.Akaizima na kisha
akaanza kuingia chumba
kimoja baada ya kingine lakini
hakukuwa na mtu yeyote mle
ndani.Dr Masawe
akachanganyikiwa.
“Hawa watu wanataka nini
kwangu?Wamewapeleka wapi
familia yangu? Akajuliza akiwa
amesimama ameegemea
mlango wa chumba chake cha
kulala
“Natamani niwajulishe
polisi lakini naogopa wale
jamaa wanaweza wakaidhuru
familia yangu kwani
walinionya nisithubutu
kuwaambia chochote polisi”
akawaza na kuelekea
chumbani kwake akafungua
kasiki lake akaanza kuhesabu
fedha zilizopo.
“Nahisi hawa jamaa
wanahitaji fedha ndiyo maana
wakateka familia yangu.Hapa
nina jumla ya shilingi milioni
thelathini na saba na kama
wakihitaji zaidi nitajitahidi
kukopa sehemu yoyote kwa
ajili ya kuikomboa familia
yangu” akawaza Dr Masawe na
mara simu yake
ikaita.Akatazama mpigaji
akahisi mwili unamtetemeka
kwani zilikuwa ni namba za
Yule jamaa mtekaji
“Hallow” akasema kwa
woga
“Dr masawe kuna mtu
anakuja hapo nyumbani kwako
kukuchukua. Ndani ya dakika
tano mtu huyo atakuwa
amefika. Ninapokata simu hii
zima simu yako tafadhali.”
akasema Yule jamaa
“Nini unakitak…..”
akasema Dr Masawe lakini
Yule mtekaji alikata
simu.Kijasho kilimtoka Dr
Masawe usoni.Akaizima simu
yake kama alivyoelekezwa
akaelekea sebuleni.Baada ya
dakika tano kama alivyokuwa
ameelekezwa mlango wa
sebuleni ukagongwa
“Nahisi huyo ndiye mtu
aliyetumwa kuja kunichukua”
akawaza na kutoka akakutana
na mtu mmoja aliyevaa suti
nyeusi na mkononi akiwa na
bastora .Dr Masawe
akatetemeka
“Funga nyumba yako !
akaelekeza Yule jamaa na Dr
Masawe akafunga nyumba
Yule jamaa akamtaka amfuate
wakatoka nje ya geti ambako
Yule jamaa alikuwa ameegesha
gari lake.Akamfungulia
mlango Dr Masawe akaingia
garini halafu akamfunga
kitambaa usoni na safari
ikaanza
Dr Masawe hakujua
mahala anakopelekwa.Baada
ya mzunguko wa dakika
kadhaa gari lile likasimama na
mlango ukafunguliwa Dr
Masawe akashushwa garini
akashikwa mkono akaongozwa
kuelekea ndani ya jengo kisha
wakaingia katika lifti baada ya
muda milango ya lifti
ikafunguka wakatoka
wakatembea kwa muda mfupi
mlango wa chumba
ukafunguliwa Dr Masawe
akaingizwa ndani akakalishwa
katika kiti akafungwa mikono
kwa pingu zilizokuwa katika
meza halafu mlango
ukafungwa akabaki peke yake
“Ee Mungu naomba
unisaidie mimi na familia
yangu tuwe salama.Watu hawa
hawaonekani kuwa watu
wazuri na wana lengo baya
nasi” akaomba Dr Masawe
Zilipita dakika kadhaa
mlango ukafunguliwa tena na
watu wakaingia ndani ya kile
chumba Dr Masawe akavuliwa
kitambaa usoni .Mle ndani ya
chumba kulikuwa na watu
wanne mmoja ndiye aliyekuwa
amekaa kitini wengine
wamesimama.
“Hallow Dr Masawe pole
sana kwa mstuko
ulioupata.Mimi naitwa Edwin
Mbeko ni mkurugenzi wa idara
ya SNSA yaani idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi”
akasema Yule jamaa aliyekuwa
amekaa kitini.DrMasawe
hakuweza kujibu chochote
alikuwa anatetemeka
“Relax Dr Masawe.Take a
deep breath” akasema Edwin
kisha akaamuru Dr Masawe
afunguliwe zile pingu
mikononi.
“Usiogope Dr Masawe uko
hapa kwa jambo dogo tu kisha
utaondoka na familia yako”
akasema Edwin
“Familia yangu wako
wapi? Akauliza Dr Masawe
“Usihofu Dr
Masawe.Familia yako iko
salama ! akasema Edwin
akachukua kitanza mbali
akakielekeza katika ukuta wa
kioo akakibonyeza na rangi ya
kioo ikabadilika na upande wa
pili familia ya Dr Masawe
wakaonekana wakiwa
wamekaa sofani.Mke wake
akiwa amewakumbatia watoto
wake.Yule jamaa akabonyeza
tena kitanza mbali na rangi ya
kioo ikabadilika na kuzuia
watu waliokuwa upande wa
pili kuonekana.
“Ahsante Mungu familia
yangu wako salama” Dr
Masawe akashukuru kimya
kimya
“Tayari umewaona familia
yako wote wako salama na
muda mfupi ujao utaondoka
nao” akasema Edwin
“Nini mnakitaka kutoka
kwangu?akauliza Dr Masawe
“Kuna kitu kidogo sana Dr
Masawe ninachokihitaji
kutoka kwako.Ni taarifa ndogo
tu na ukinipatia hiyo basi
familia yako watakuwa salama
na utaondoka nao sasa hivi”
akasema Edwin
“Niambieni tafadhali
mnachokihitaji niwapatie
kama ni fedha niko tayari
kuwapa kiasi chochote kile
mnachokihitaji ili mradi
msiidhuru familia yangu”
akaomba Dr Masawe.
“Kuna mgonjwa mmoja
anaitwa Papi Gosu Gosu
alikuwa amelazwa katika
hospitali ya Mtodora akipatiwa
matibabu baada ya
kushambuliwa kwa risasi na
watu wasiojulikana.Mgonjwa
huyo amehamishwa leo kutoka
hospitalini hapo na kupelekwa
kusikojulikana.Ninachokihaji
kutoka kwako ni kunieleza
mahala aliko Gosu
Gosu.Ukijibu hilo
ninakuhakikishia wewe na
familia yako mtaondoka hapa
salama” Edwin akanyamaza na
kumtazama Dr Masawe
“Wapi alipo Gosu
Gosu?akauliza Edwin
“Hili ni jaribu kubwa
sana.Yawezekana hawa jamaa
ndio wanaotaka kumuua Gosu
Gosu” akawaza Dr Masawe
“Dr Masawe wapi alipo
Gosu Gosu?Nieleze tafadhali ili
tuokoe muda na uondoke hapa
na familia yako”
“Sifahamu mahala aliko
huyo mgonjwa” akajibu Dr
Masawe na Edwin
akamtazama halafu
akatabasamu
“Una uhakika Dr Masawe
hufahamu mahala alipo Gosu
Gosu?akauliza Edwin
“Ni kweli sifahamu mahala
alipo Gosu Gosu.Kama
ningejua mahala alipo
ningewaeleza” akajibu Dr
Masawe
“Dr Masawe tunafahamu
Gosu Gosu amehamishwa leo
kutoka hospitali ya Mtodora na
wewe ukiwa na madaktari
wengine wawili na wauguzi
wawili mliongozana naye
kwenda mahala
alikohamishiwa ili kuendelea
kumpatia matibabu.Nataka
unieleze mahala alikopelekwa
Gosu Gosu.Yule mtu ni hatari
sana kwa usalama wa nchi”
“Sifahamu alikohamishiwa
Gosu Gosu na wala
sikuongozana na
waliomuhamisha” akasema Dr
Masawe
“Dr Masawe
ninakuheshimu sana mzee
wangu na sitaki kukufanyia
jambo lolote baya.Ninakuuliza
kwa upole kabisa wapi alipo
Gosu Gosu?Nieleze tafadhali
uondoke haraka na familia
yako”
“Sifahamu kwa kweli alipo
huyo Gosu Gosu” akajibu Dr
Masawe.Edwin akamtazama
kisha akawasha sigara akavuta
na kupuliza moshi halafu
akasema
“Kwa nini unaficha mahala
alipo Gosu Gosu.Ana
umuhimu gani kwako?
“Simfichi ila sifahamu
mahala alipo.Mnataka kumuua
amewakosea nini? Akauliza Dr
Masawe na kwa kasi ya umeme
Edwin akainuka na kumlamba
kofi zito Dr Masawe
“Huna ruhusa ya kuuliza
swali lolote hapa.Nimekuuliza
swali jibu haraka sana na si
kuniuliza swali.Nakuuliza kwa
mara ya mwisho wapi alipo
Gosu Gosu? Ukishindwa
kunijibu nitaanza kuitesa
familia yako huku ukishuhudia
! akasema kwa ukali Edwin
ambaye sura yake ilikuwa
imebadilika na kuonyesha
ukatili mkubwa
“Wapi alipo Gosu
Gosu?akauliza lakini Dr
Masawe hakujibu kitu.Edwin
akasimama
“Dr Masawe hujanifahamu
vyema mimi ni nani.Sasa
umenilazimisha nifanye kitu
ambacho sikuwa nimetarajia
kukifanya ! akasema na
kuelekeza kitanza mbali katika
kioo akabonyeza na familia ya
Dr Masawe ikaonekana.
“Binti yako ana umri wa
miaka mingapi? Akauliza
“Tafadhali naomba
msiwaguse familia yangu !
Kama ni kunitesa niteseni
mimi ! akasema Dr Masawe na
kulambwa tena kofi zito
“Niambie binti yako ana
miaka mingapi? Akauliza
“Ana miaka kumi na mbili”
“Sawa.Leo hii tunampatia
mchumba hapa na kwa mara
ya kwanza ataingiliwa kimwili
huku ukishuhudia” akasema
Edwin na Dr Masawe
akasimama
“Nasema msimguse binti
yangu tafadh…” hakumaliza
sentensi yake akapigwa ngumi
iliyompeleka chini.Damu
zilianza kumtoka
mdomoni.Akainuliwa
akatolewa mle ndani na
kuingizwa katika chumba
walichokuwamo familia yake
ambao waliangua kilio
walipomuona baba yao.Edwin
akawanyamazisha halafu
akamfuata binti wa Dr Masawe
“Binti unaitwa
nani?akauliza Edwin
“Naitwa Paulina” akajibu
Yule binti huku
akitetemeka.Edwin akamshika
mkono na kumtaka ainuke
akampeleka katika kiti
akamtaka aketi
“DrMasawe hii ni mara ya
mwisho ninakuuliza wapi alipo
Gosu Gosu?
“Tafadhalini jamani
naomba binti yangu
mumuache kwani hahusiki
kwa namna yoyote na suala
hili.Nitawasaidia kutafuta
taarifa za mahala aliko huyo
mtu mnayemtafuta lakini
nawaomba msimguse binti
yangu ! akasema Dr Masawe
“Dr Masawe wapi alipo
Gosu Gosu? Akauliza Edwin
“Naombeni mniamini
vijana wagu sifahamu mahala
alipo Gosu Gosu.Kama
ningefahamu ningewaeleza
lakini sijui chochote ! akasema
Dr Masawe
“Unatulazimisha tufanye
ukatili ambao hatukuwa
tumetegemea kuufanya !
akasema Edwin na kuwapa
ishara watu wake.Jamaa
wawili waliojazia miili yao
wakamshika Paulina binti wa
Dr Masawe na kumpandisha
juu ya meza.Alikuwa analia.
“Dr Masawe fursa ya
mwisho wapi alipo Gosu Gosu?
“Naombeni jamani
muacheni binti yangu hana
mahusiano yoyote na suala
hili.Ninawaahidi nitawasaidia
kutafuta mahala alipo Gosu
Gosu ! akasema Masawe
aliyekuwa amefungwa pingu
mikononi
“Mume wangu kama
unafahamu hicho
wanachokuuliza wajibu
tafadhali ili kumuepusha binti
yetu na ukatili ambao
anakwenda kufanyiwa na hawa
watu! akasema mke wa Dr
Masawe huku akitokwa na
machozi
“Sifahamu mke wangu
mahala alipo huyo mtu
wanayemtaka.Kama ningejua
mahala alipo ningewaeleza !
akasema Dr Masawe.Edwin
akawaelekeza watu wake
kuendelea na zoezi.Kwa
kutumia nguvu Paulina
akavuliwa gauni alilokuwa
amevaa akabaki
mtupu.Alikuwa anapiga kelele
kubwa.Dr Masawe na mke
wake walikuwa wamedhibitiwa
na watu wenye silaha ili
wasiweze kufanya
chochote.Mmoja wa wale
jamaa waliojazia miili yao
akavua suruali yake bila aibu
na kuutoa uume wake
uliosimama.
“Nitawaeleza ! Nitawaeleza
! Nitawaeleza ! akasema Dr
Masawe
“Unasemaje Dr Masawe ?
akauliza Edwin
“Nitawaeleza mahala alipo
Gosu Gosu.Tafadhali
naombeni msimfanye
chochote binti yangu” akasema
Dr Masawe na Edwin
akaelekeza wale jamaa
wamuache Paulina kisha Dr
Masawe akatolewa ndani ya
kile chumba akarejeshwa
katika chumba alichokuwamo
awali.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 5
Mathew Mulumbi
alikaribia kufika katika geti
kuu la kuingilia ofisi za SNSA.
“Ruby tayari ninalitazama
geti kuu la SNSA” Mathew
akamwambia Ruby
“Good.Ninakuona na
tayari nimekwisha cheza na
kamera zote zilizoelekezwa
eneo la geti kuu.You have two
minutes to finish the main
gate” akasema Ruby
“Thank you Ruby” akajibu
Mathew na kupunguza
mwendo baada ya kukutana na
kibao kilichomuelekeza afanye
hivyo.Alipolikaribia geti kuu
akakutana na kibao kingine
kilichomtaka asimame kwa
ajili ya ukaguzi.Jamaa mmoja
aliyevaa sare za ulinzi za rangi
nyeusi akasogelea kioo
Mathew akakishusha
“Habari yako ndugu”
akasalimu Yule mlinzi
“Nzuri ndugu yangu”
“Nikusaidie nini?
“Mimi ni mgeni wa Edwin
Mbeko yuko ndani? Akauliza
Mathew
“Mathew kuna walinzi
wengine watatu wako hapo
getini” Ruby akamwambia
Mathew kupitia kile kifaa
alichokiweka sikioni
Yule mlinzi akamtaka
Mathew asubiri kidogo ili
akawasiliane na Edwin Mbeko
alipogeuka tu mkono wa
Mathew ulikuwa mwepesi
ukanyanyuka kwa kasi ya aina
yake na kwa kutumia bastora
yenye kiwambo cha sauti
akamlenga Yule jamaa risasi
akaanguka chini kisha kama
nyani akashuka kutoka ndani
ya gari lile na kuelekea katika
nyumba ya walinzi na kama
alivyoelekezwa na Ruby
kulikuwa na walinzi
watatu.Mathew alicheza na
bastora yake kama vile ana
mikono minne na ndani ya
sekunde chache wale walinzi
wote wakawa sakafuni
wakivuja damu
“I’m sorry guys wakubwa
wenu ambao wanashirikiana
na magaidi wamesababisha
mkafikwa na masahibu haya”
akasema Mathew huku
akiwavuta walinzi wale na
kuwaingiza katika chumba
kidogo cha mapumziko
“Mathew you have 10
seconds to get out of there !
Ruby akamuelekeza Mathew
ambaye aliingia katika gari
lake na kutoka mahala alipo
Ruby akalifungua geti na
Mathew akapita.Moja kwa
moja akaelekea sehemu ya
maegesho ya viongozi wa
idara.Kabla hajashuka garini
akalitazama eneo lile kama
lina mlinzi yeyote halafu
akawasiliana na Ruby
“Tayari niko eneo la
maegesho ninataka kutoka
garini”
“Sawa Mathew unaweza
kutoka.Hakuna hatari yoyote
eneo hilo” akasema Ruby na
Mathew akafungua mlango wa
gari akashuka akachukua begi
lake akalivaa mgongoni bila
kusahau kofia yake ngumu
ambayo ilifungwa miwani ya
kumuwezesha kuona sehemu
yenye giza.Moja kwa moja
akaelekea katika jengo ambalo
ndimo mna vifaa vyote vya
umeme pamoja na jenereta la
dharura pale umeme
unapokatika.Akalizunguka
kwa nyuma jengo lile halafu
akatoa mkasi mgumu akakata
kipande cha wavu akapenya na
kuingia ndani.Akaelekea moja
kwa moja katika sehemu ya
kukatia umeme akachukua
kifaa Fulani kutoka katika begi
lake akakiweka katika sanduku
kubwa la umeme na baada ya
sekunde chache kukatokea
cheche kubwa na jengo zima
umeme ukakatika kisha
akatoka kwa kasi kupitia
mahala alikoingilia akaelekea
upande ule wa maegesho ya
magari akachomoa vifaa
kutoka mfukoni na
kuuchokonoa mlango
ukafunguka akaingia
ndani.Kulikuwa na giza lakini
aliweza kuona kutokana na ile
miwani ya kuonea usiku.
“I’m in”Mathew
akamwambia Ruby
“Good.Sekunde ishirini na
nne umeme utawaka hivyo
elekea njia ya kushoto kwako
yenye kibao emergency exit.”
Akaelekeza Ruby na Mathew
akaanza kupanda ngazi
taratibu na kwa tahadhari
kubwa.Alisikia kwa mbali watu
wakizungumza kutokea nje
Ndani ya chumba
alichokuwa anahojiwa Dr
Masawe mahojiano
yalisimama baada ya umeme
kukatika na umeme uliporejea
Edwin akatoa simu yake
akapiga kwa fundi mkuu
“Masoud kuna nini
kimetokea hadi umeme
ukakatika na kuchelewa
kuwaka?
“Mkuu imetokea hitilafu
katika boksi kubwa na
kutulazimu kuchepua umeme
katika njia nyingine hadi hapo
tutakapofahamu chanzo cha
hitilafu iliyojitokeza”
“Nakuhitaji ofisini kwangu
haraka sana unieleze kwa kina
kilichotokea kwani jengo hili
halipaswi kukosa umeme zaidi
ya dakika mbili kutokana na
unyeti wake lakini imechukua
zaidi ya dakika tano umeme
kurejea” akasema Edwin na
kuwaelekeza vijana wake
waendelee kumchunga Dr
Masawe ili akafahamu
kilichokuwa kimetokea na
kusababisha hitilafu ile
Mathew aliufikia mlango
alioelekezwa na Ruby
akabonyeza namba huku
akielekezwa na Ruby lakini
zikagoma
“Yawezekana wamebadili
namba ! akasema Ruby
“Ruby find me another
way ! akasema Mathew
“Nipe sekunde chache
Mathew nione kitu cha
kufanya” akasema Ruby na
kushusha pumzi akaanza
kubofya kompyuta yake haraka
haraka na mara simu yake
ikaita alikuwa ni Rais
“Oh no ! kwa nini anapiga
wakati huu?akasema Ruby
kisha akaichukua ile simu na
kutoka nje ya kile chumba
akaipokea
“Hallo mheshimiwa Rais”
akasema Ruby
“Ruby uko wapi ninahitaji
kuzungumza nawe usiku wa
leo kuhusiana na kile
kilichotokea jana kule
SNSA.Nielekeze mahala ulipo
tafadhali ili nitume watu
wangu waje kukuchukua”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
utanisamehe kwani kwa usiku
huu haitawezekana.Naomba
kama itawezekana tuonane
kesho”
“Kesho haitakuwa rahisi
kwa upande wangu kwani
nitakuwa na kikao muhimu
sana na marais
wenzangu.Naomba tafadhali
tuzungumze usiku huu ili
niweze kulimaliza hili swala
nahitaji urejee haraka sana
SNSA kabla ya hizo siku saba”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais kwa
usiku huu haitawezekana kwa
sababu ninamsaidia Mathew
Mulumbi kufanikisha misheni
ya muhimu sana” akasema
Ruby
“Misheni ipi? Naomba
unieleze tafadhali.Nataka
kufahamu anachokifanya
Mathew” akasema Dr Fabian
“Kuna uchunguzi
anakwenda kuufanya ndani ya
SNSA na mimi ndiye
ninayemsaidia ili aweze
kufanikisha hilo jambo”
“Umesema Mathew
anakwenda kufanya uchunguzi
SNSA?
“Ndiyo mheshimiwa
Rais”akajibu Ruby
“Anakwenda kuchunguza
nini?akauliza Dr Fabian
“Kwa sasa naomba
nisikueleze mheshimiwa Rais
lakini pale uchunguzi
utakapokamilika
tutakujulisha” akasema Ruby
“Ruby you have to tell me
everything.SNSA ni ofisi iliyo
chini yangu natakiwa kujua
kila kinachoendelea
pale.Nataka kufahamu kitu
gani anachokwenda
kukichunguza Mathew?Mle
kuna siri nyingi za usalama wa
nchi ambazo mtu kama
Mathew ambaye si mfanyakazi
hapaswi kuzifahamu.Ruby nini
kinaendelea?Mara ya kwanza
umemuingiza ndani ya SNSA
na akashiriki katika tukio la
kusababisha kifo cha mmoja
wa wafanyakazi na leo
anarejea tena kufanya
uchunguzi ..!
“Mheshimiwa Rais
tafadhali naomba umuamini
Mathew.Kuna jambo kubwa
linaendelea hapa nchini hivi
sasa na pale tukikamilisha
uchunguzi tutakujulisha”
“So you are with him !
“Yes Mr President.I’m with
him” akajibu Ruby na Dr
Fabian akavuta pumzi ndefu
“Ruby ninakuamini sana
na ndiyo maana nikakuomba
uje uongoze idara nyeti kama
ile lakini kwa mambo haya
unayoyafanya unanipa
wasiwasi wa kuendelea
kukuamini.Mathew Mulumbi
si mtu wa kumuamini hata
kidogo.Hakuna anayejua
alikuwa wapi na kwa nini
ametokea katika wakati
huu.Huyu ni mtu wa
kuogopwa sana na kwa namna
yoyote ile hukupaswa
kumsaidia kuingia ndani ya
ofisi nyeti kama SNSA!
“Mheshimiwa Rais
nitazungumza nawe
kesho.Sorry ! akasema Ruby
na kukata simu akakimbilia
ndani akavaa spika za
masikioni na kumuita Mathew
“Mathew
unanisoma?akauliza Ruby
“Ulikuwa wapi Ruby?!
Tayari nimekwisha anza
kuingiwa na wasi wasi labda
kuna kitu kimekutokea”
akasema Mathew
“I’m sorry” akasema Ruby
na kuendelea kubonyeza
kompyuta yake kwa kasi
kubwa
“Umefikia wapi kunitafutia
njia nyingine?
“I’m changing the
codes.Ndani ya sekunde
chache nitakupa namba mpya
za kufungulia huo mlango”
akasema Ruby
“Fanya haraka Ruby !
akasema Mathew
Mara tu baada ya Ruby
kukata simu Dr Fabian
akampigia Edwin Mbeko
“Mheshimiwa Rais !
akasema Edwin
“Edwin uko wapi?akauliza
Dr Faban
“Niko ofisini mheshimiwa
Rais”
“Kila kitu kiko sawa hapo
ofisini?
“Ndiyo mheshimiwa Rais
kila kitu kiko sawa kabisa”
“Are you sure?
“Ndiyo mheshimiwa Rais
kila kitu kiko sawa kabisa
ukiacha yale matukio mawili
ya kuwapoteza wafanyakazi
wetu ambayo nimekwisha
kufahamisha lakini hakuna
tena tatizo lingine lolote”
akasema Edwin
“Hakuna tukio lolote
limetokea hapo ofisini ambalo
si la kawaida usiku
huu?akauliza Dr Fabian
‘Kilichotokea muda mfupi
uliopita ni umeme kukatika na
niko hapa na mhandisi wetu
wa umeme akinieleza namna
tukio lilivyotokea”
“Oh my God ! akasema Dr
Fabian
“Kuna nini mheshimiwa
Rais?akauliza Edwin
“Edwin kuna mtu tayari
yuko ndani ya jengo
lenu.Amesaidiwa kuuingia
ndani na mtu aliyeko nje
anayelifahamu vizuri jengo
hilo na mifumo yake.Sifahamu
mtu huyo anakuja kutafuta
nini lakini nahisi kuna siri
anazitafuta.Tafadhali zima
kabisa kila kitu ili mtu huyo
asifanikiwe lengo lake na
hakikisha anatiwa mikononi
na ahojiwe kitu anachokuja
kukifanya hapo SNSA”
akasema Dr Fabian na Edwin
akaonyesha mstuko mkubwa
“Edwin umenisikia?
“Nimekusikia mheshimiwa
Rais” akasema Edwin na Rais
akakata simu.Edwin akatoka
mbio na kuelekea ghorofa ya
tatu ambako kulikuwa na watu
wakiendelea na kazi akawataka
wazime kila kitu kwa haraka
pamoja na kufunga milango
yote ya usalama.
Ruby aliyaelekeza macho
katika kompyuta yake ambayo
iliendelea kuzunguka
ikionyesha asilimia themanini
na nane ili namba mpya
alizoziweka ziweze
kutambuliwa na mfumo wa
SNSA na Mathew aweze
kuufungua mlango.Ilipofika
asilimia tisini na saba mara
mawasiliano yakakatika
ghafla.Ruby akapiga meza kwa
hasira akaendelea kubonyeza
kompyuta yake haraka haraka
lakini hakuweza kujiunganisha
na mfumo wa SNSA
“Bastard ! akasema kwa
hasira kisha akavaa spika zake
za masikioni
“Mathew we have a
problem” akasema
“Nini kimetokea tena
Ruby?akauliza Mathew
“Mawasiliano yamekatika
ghafla inaonekana wamezima
kila kitu.I can’t access
anything ! akasema Ruby
“They know I’m here !
akasema Mathew
“Mathew please get out of
there ! akasema Ruby
“Hapana Ruby siwezi
kurudi.Lazima nimpate Edwin
Mbeko.Ninayo ile ramani ya
jengo zima uliyonitumia katika
simu yangu.I have to do it on
my own.Usiendelee
kuwasiliana nami kwani
wanaweza wakafuatilia
mawimbi na wakagundua
mahala ulipo ukawa katika
hatari.Thank you Ruby let me
do this on my own” akasema
Mathew na kuchomoa kifaa
kile alichokuwa amekivaa
sikioni akakikanyaga kanyaga
na kukata kabisa mawasiliano
na Ruby
“Wamegunduaje kama
niko hapa? Nitafahamu baadae
kwa sasa natakiwa kuhakikisha
ninafika katika ofisi ya Edwin
Mbeko kwa namna yoyote ile”
akawaza Mathew na kutoa
bomu dogo katika begi lake
akaenda kuliweka katika kitasa
cha mlango halafu akarudi
nyuma hatua tano na kulilenga
bomu lile kwa kutumia bastora
yake yenye kiwambo cha sauti
ukatokea mlipuko na mlango
ukasambaratika.Akajibanza
katika kona kusikilizia kama
kuna mtu yeyote atajitokeza
lakini hakukuwa na mtu yeyote
akaanza kupanda ngazi haraka
haraka kwa tahadhari kubwa.
Milango yote ya kuingia na
kutoka ndani ya jengo la SNSA
ilikuwa imezingirwa na walinzi
wenye silaha ili kuzuia Mathew
asiweze kutoka nje na
kutoroka. Wafanyakazi wote
wakakusanywa katika chumba
kilichotengenezwa maalum
kwa nyakati kama hizi kama
kutatoea hatari yoyote ya
kushambuliwa.Ni chumba
kilichotengenewa maalum
ambacho kina milango
isiyopenya risasi na kina
uwezo wa kuwakinga
wafanyakazi dhidi ya
shambulio lolote la kibaolojia.
Edwin Mbeko akiwa
ameongozana na walinzi
wawili wakainga katika
chumba kile ambacho
wafanyakazi wote walikuwa
wamekusanywa.Mara tu
alipoingia wafanyakazi
wakataka kufahamishwa kile
kinachoendelea
“Poleni sana ndugu zangu
kwa mstuko
mlioupata.Halijawahi kutokea
tukio kama hili hapa katika
idara yetu.Kilichotokea ni
kwamba nimepokea taarifa
muda mfupi uliopita kwamba
ndani ya jengo letu kuna mtu
amevamia na lengo lake ni
kutafuta siri za usalama wa
nchi.Baada ya kupata taarifa
hiyo ya kustusha hatua ya
kwanza ilikuwa ni kuzima kila
kitu ili lengo la mtu au watu
hao lisifanikiwe.Kama
mnavyofahamu humu ndani
kuna siri nyingi kuhusiana na
usalama wa nchi hivyo basi
hatuwezi kuwapa nafasi watu
hao ya kufanikisha mipango
yao.Ninachowaomba kwa sasa
tuendelee kutulia humu ndani
wakati suala hili
linashughulikiwa.Tayari kikosi
cha makomando wa idara yetu
kiko njiani kutoka katika
kambi yao wanakuja hapa kwa
ajili ya kuhakikisha mtu au
watu hao wanadhibitiwa
haraka sana” akasema Edwin
na simu yake ikaita akaipokea
akazungumza na aliyempigia
halafu akasema
“Nimetaarifiwa kwamba
walinzi wote waliokuwa geti
kuu usikuhuu wameuawa na
hao watu ndipo wakapata
nafasi ya kupita kuingia ndani
ya jengo.Milango yote kwa
sasa imefungwa na kuna ulinzi
hivyo hawawezi kutoka
nje.Ninawahakikishia kwamba
tutawapata wote” akasema
Edwin
“Mkuu inawezekanaje mtu
au watu hao wakaweza
kuvamia ofisi zetu bila
kujulikana?Kuna kamera kila
mahala na kila mtu au gari
linalokaribia eneo hili
linaonekana na kukaguliwa
imezekanaje mtu au watu hao
wakaweza kufika hadi geti kuu
bila kujulikana? Mmoja wa
wafanyakazi akauliza
“Tutalifanyia uchunguzi
suala hilo kujua namna mtu
huyo alivyoweza kufika hadi
geti kuu akaua walinzi na
kuingia ndani bila kunaswa na
kamera zetu.Tuna mfumo wa
kisasa mno na hata mimi
ninashangaa kwa nini kamera
zetu zimeshindwa kunasa
tukio hilo .Tutafanya
uchunguzi na kuufahamu
ukweli na wote walioshiriki
katika suala hili watajulikana
na kuchukuliwa hatua kali
lakini kwa muda huu
kipaumbele kikubwa ni
kuhakisha mvamizi au
wavamizi hao wanakamatwa”
akasema Edwin
“Mkuu taarifa hii ya
kuwapo kwa mvamizi
umeipata wapi? Mtu huyo
aliyekupa taarifa hii amejuaje
kama kuna mtu kavamia jengo
letu wakati sisi tuliopo ndani
hatufahamu chochote?akauliza
mfanyakazi mwingine.
“Si jambo zuri kuweka
wazi chanzo cha taarifa lakini
katika hili napenda kuweka
wazi kuwa taarifa hii
nimeipata kutoka wa
mheshimiwa Rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania
ambaye ofisi hii iko chini yake”
akasema Edwin na wote
wakabaki na mshangao
minong’ono ikaanza kusikika
“Mingong’ono hiyo ni ya
kujiuliza Rais amefahamuje
kama kuna mtu katuvamia
kabla yetu sisi? Hata mimi
sifahamu Rais amejuaje lakini
baada ya kumtia nguvuni huyo
mvamizi wetu nitazungumza
na Rais naamini atanipa
taarifa kamili ya namna
alivyoweza kupata taarifa za
huyo mtu” akasema Edwin na
ujumbe ukaingia katika simu
yake akausoma halafu
akasema
“Ndugu zangu
nimetaarifiwa kwamba kikosi
cha makomando wetu
kinakaribia
kufika.Ninakwenda
kuwapokea .Kila
kitakachoendelea
mtajulishwa” akasema Edwin
na kutoka mle ndani
akawakuta watu wanne nje ya
kile chumba wakimsubiri
“Mkuu kumegundulika
uwazi mkubwa katika nyumba
ya jenereta tunaamini huyo
mvamizi alikata wavu na
kuingia ndani kisha akakata
umeme.Vile vile tumekuta gari
katika maegesho ya wakuu wa
idara na tunahisi ni gari lake”
akasema mmoja wa wale
jamaa.
“Kama gari lake
limeonekana upande huo
yawezekana ameingia ndani
kupitia njia ya dharura ya
vongozi wa idara ambayo watu
wengi hata walio ndani ya
idara hawaifahamu.Huyu mtu
anaonekana kulifahamu sana
jengo hili ama kuna mtu
ambaye anashirikiana naye”
akasema Edwin na mlio wa
helkopta ukasikika
“Makomando wamefika
nahitaji kuwapokea” akasema
Edwin kisha akaongozana na
walinzi wawili wakaelekea
ghorofani kwa ajili ya
kuwapokea makomando hao
ambao hutumiwa na SNSA
katika operesheni kubwa na za
hatari kwa usalama wa nchi.
“Ni nani huyu mtu
aliyethubutu kuvamia ofisi
zetu.Kitu gani
anakitafuta?Halafu
anaonekana kulifahamu vyema
jengo hili je kuna watu wa
humu ndani ya idara
anashirikiana nao? Akajiuliza
Edwin huku wakipanda ngazi
haraka haraka kuelekea juu ya
jengo.
Helkopta iliyowaleta
makomando ilisimama juu ya
jengo la SNSA makomando
wakaanza kushuka kwa
kutumia kamba.Jumla ya
makomando nane waliojihami
vilivyo wakashuka kiongozi
wao akasalimiana na Edwin
kisha wakaelekea katika ofisi
na Edwin akawaeleza kile
kilichotokea na kupelekea
kuwaita pale.Akawafahamisha
kwamba wanahisi mvamizi
huyo anaweza kuwa amejificha
katika njia ya dharura
Makomando
waligawanyika katika vikosi
viwili vya watu wanne kikosi
kimoja kikashuka chini katika
mlango wa kuingilia wakuu wa
idara ambako ndiko gari la
Mathew lilikoonekana kikosi
cha pili kikaenda ghorofa ya
tano ambako ndiko njia ile
ilikuwa inaelekea zilipo ofisi za
wakuu wa idara.Kikosi cha
makomando wanne
walioshuka chini wakiwa na
mbwa mkubwa kiliingia katika
njia ile ya dharura na kuanza
kupanda juu kwa tahadhari
kubwa.Walikuta mlango
mkubwa ukiwa umefumuliwa
kwa bomu wakawasiliana na
wenzao wakawajulisha kisha
wakaendelea kupandisha
taratibu huku mbwa mkubwa
wa kijeshi waliyekuwa naye
akiwaongoza kuelekea katika
mlango mmoja uliokuwa
umefungwa.Kulionekana
mchirizi wa damu chini ya
mlango.Mbwa Yule
akawaongoza kuelekea katika
mlango ule ulikotokea mchirizi
ule wa damu.Kiongozi wa kile
kikosi akawataka wasimame
kisha akatangulia mbele
taratibu akiwa katika
tahadhari kubwa.Ghafla mbwa
akaruka juu na mkanda
ukamponyoka yule jamaa
aliyekuwa amemshika
akakimbia mbio akaurukia
mlango ambao haukuwa
umefungwa na mara tu mlango
ule ulipofunguliwa kukatokea
kishindo kidogo na wale
makomando wakalala
chini.Ndani ya sekunde chache
eneo lote likajaa moshi mzito
na wale makomando wakaanza
kuhisi kuishiwa nguvu na
kushindwa kupumua.Wakati
wakihangaika kuvuta pumzi
Mathew Mulumbi akajitokeza
akiwa amevaa maski usoni ya
kumkinga dhidi ya hewa chafu.
Mkono wake wa kulia alikuwa
ameshika bunduki ndogo na
mkono wa kushoto alikuwa na
kopo.Alibonyeza lile kopo na
kupulizia hewa eneo lile moshi
ukatoweka na hewa safi
ikapatikana akavua maski yake
na akaweza kuwaona vizuri
wale makomando waliokuwa
wakihangaika kutafuta hewa
huku wakiwa hawana
nguvu.Haraka haraka
akazikusanya bunduki zao na
kuziweka sehemu moja halafu
akachukua pingu za plastiki
akawafunga kisha akatoa kitu
Fulani katika begi lake akaanza
kuwapulizia puani na baada ya
muda mfupi wakaanza kujihisi
vizuri na ndipo walipojikuta
wakitazamana na mtu
aliyekuwa amewaelekezea
bunduki.
“Poleni sana ndugu zangu”
akasema Mathew
“Aaaaghh ! akatoa ukelele
kiongozi wa kikosi kile akitaka
kukata pingu zile za plastiki
walizokuwa wamefungwa
“Please don’t do that or I’ll
shoot you ! akasema Mathew
kwa sauti isiyo na masihara
Yule komandoo akamtazama
kwa dharau na kutunisha
misuli akitaka kukata ile pingu
mara risasi mbili zikapita
pembeni ya kichwa chake na
kupiga ukuta.
“Next time nitakifumua
kichwa chako kama utaendelea
kuwa mkaidi ! akasema
Mathew na Yule jamaa akawa
mpole.Mathew akawatazama
kwa muda halafu akasema
“Listen to me brothers !
akanyamaza na kuwatazama
tena wale jamaa
“Mimi ndiye
mnayenitafuta.Naitwa Mathew
Mulumbi ni…”
“Mathew Mulumbi ?!
Kiongozi wa kile kikosi
akastuka
“Ndiyo mimi ni Mathew
Mulumbi”
“Unafanya nini hapa
Mathew?akauliza Yule jamaa
“Unanifahamu? Mathew
akauliza
“Nimezisikia sana habari
zako.Ninaye ndugu yangu
anafanya kazi katika idara ya
ujasusi ndiye ambaye
amenieleza mambo yako
mengi.Sikujua kama ni wewe
ambaye tumekuja kukutafuta”
akasema Yule jamaa huku
wenzake wakimshangaa.
“Huyu anaitwa Mathew
Mulumbi amewahi kufanya
kazi katika idara ya ujasusi
Tanzania na mambo
aliyoyafanya ni makubwa
sana.Ni mmoja kati ya manguli
wa ujasusi hapa nchini” Yule
kiongozi wa makomando
akawafahamisha wenzake
“Aliyosema mwenzenu ni
kweli kabisa” Mathew
akaongeza
“Kwa nini umevamia jengo
hili na kuua watu?Hujui
kwamba hilo ni kosa?
Tumeambiwa kwamba umeua
walinzi wa geti kuu huo tayari
ni uhalifu ! akasema mwingine
“Ni kweli niliwaua wale
walinzi geti kuu ili nipate
nafasi ya kuingia humu ndani
kwani bila kufanya vile
nisingeweza kuingia
humu.Hata ninyi ningeweza
kuwamaliza lakini sikufanya
hivyo kwa kuwa ninyi ni
wenzangu na mnaweza
mkanielewa nikiwaeleza kile
kilichonileta hapa”akasema
Mathew
“Nini kimekuleta hapa?
Unatafuta siri za serikali?
akauliza komando mwingine
“Sijaja hapa kuiba siri za
serikali na siwezi kufanya
hivyo.Niko hapa kwa sababu
nyingine ya usalama wa
nchi”akasema Mathew
“Usalama wa nchi ndio
uvamie ofisi ya serikali na
kuua watu?
“Labda niwaeleze kwa
ufupi tu pengine mnaweza
mkanielewa.Si muda mrefu
sana IS walifanya shambulio
hapa Dar es salaam ambalo
liliua wake za marais na mpaka
sasa watu waliohusika katika
shambulio hilo
hawajakamatwa.Nilipata
taarifa kutoka katika vyanzo
vyangu vya habari kwamba
kuna mtu anaitwa Khalid
Sultan Khalid kutoka katika
kundi la kigaidi al IS anakuja
hapa nchini.Huyu ni mtu
anayejishughulisha na
milipuko
mikubwa.Mkurugenzi mpya
wa idara hii anaitwa Annabel
ni rafiki yangu na nilimuomba
tuitumie idara yake
kumfuatilia Khalid na
kufahamu kile alichokuja
kukifanya hapa Tanzania
pamoja na washirika
wake.Zoezi lilifanyika vizuri
lakini katikati ya zoezi hilo
mawasiliano yakakatika na
timu iliyokuwa ikimfuatilia
Khalid ikashindwa kufanya
kazi yake na Khalid akapotea
hadi sasa hatujui mahala
alipo.Baada ya kufanya
uchunguzi tukagundua
kwamba mawasiliano hayo
yalikatwa kwa makusudi na
mfanyakazi anaitwa Edina
.Tulimfuatilia huyo Edina na
kukuta ameuawa nyumbani
kwake.Baada ya Edina kuuawa
tukalazimika kumuhoji
mhandisi mkuu ambaye
alisema uongo kwamba
mawasiliano yale yalikatika
kutokana na hali ya
hewa.Ilitumika nguvu kidogo
kumuhoji kwani aligoma
kusema chochote na
alipelekwa katika chumba cha
matibabu baada ya kupoteza
fahamu.Baadae tukaambiwa
amefariki dunia na kitu cha
kushangaza ni kwamba
mkurugenzi huyo mpya
ambaye aligundua kuhusiana
na sababu ya kukatika kwa
mawasiliano yale akaondolewa
katika nafasi yake kwa
kutumia kanuni za idara na
aliyeongoza zoezi hilo ni
Edwin Mbeko.Huo ni upande
mmoja.Upande wa pili kuna
mtu anaitwa Melanie Davis
huyu anaishi hapa nchini na
anashirikiana na James Kasai
ambaye kwa kushirikiana na IS
walitekeleza shambulio lile
lililoua wake za marais.Huyu
Melanie mpaka sasa
tunamsaka na hatujafanikiwa
kumpata lakini kuna mtu wa
karibu na Melanie ambaye
anaishi Ufaransa na baada ya
kumchunguza huyo mtu
tukagundua ana mawasiliano
ya karibu na Edwin Mbeko na
hiyo ndiyo sababu niko
hapa.I’m here for
EdwinMbeko.Nimekuja
kumchunguza kwani ninahisi
anaweza kuwa na mahusiano
na Melanie Davis ambaye
anashirikiana na magaidi wa
IS.Nina uhakika hata tukio lile
la kumpoteza Khalid Sultan
Khalid anahusika.Hivyo ndugu
zangu nadhani kwa hayo
machache mmenielewa”
akasema Mathew
“Kama unamtafuta Edwin
kwa nini ukamfuata hapa?Kwa
usingemtafuta sehemu
nyingine nje ya hapa?
“Edwin Mbeko anatumia
ofisi hii kama mwavuli wa
kufichia mambo yake na ndiyo
maana nimekuja hapa kufanya
uchunguzi katika ofisi
yake.Ndugu zangu nisingeweza
kuja sehemu hii ya hatari kama
nisingekuwa na sababu ya
msingi niliyowaeleza.Kuna
hatari kubwa ya kufanyika kwa
shambulio lingine kubwa hapa
nchini hivyo kila juhudi lazima
zifanyike kuhakikisha
tunalizuia hilo
lisitokee”akasema Mathew
“Kwa nini usiwasilishe
suala hili katika vyombo
husika vilishughulikie?
“Nisingeshindwa kufanya
hivyo lakini hawa jamaa wana
mizizi mirefu hadi katika
taasisi za serikali kama
hii.Ninawaomba ndugu zangu
mnisaidie ili niweze
kufanikisha jukumu lililonileta
hapa.Kama msiponisaidia
nikafanikisha kile kilichonileta
hapa hamtakuwa mnatekeleza
wajibu wenu wa ulinzi wa nchi
na nina uhakika mtaona aibu
pale mtakaposikia magaidi
wametekeleza shambulio
lingine hapa nchini” akasema
Mathew kisha akachukua kisu
na kukata zile pingu za plastiki
halafu akawarejeshea silaha
zao.
“The choice is yours.Take
me down or save the country !
akasema Mathew.Kiongozi wa
kikosi kile akawatazama
wenzake halafu akauliza
“What do you
want?akamuuliza Mathew
“Nataka nifike katika ofisi
ya Edwin.I need your help”
akasema Mathew
“Kama nisingekuwa
nimesikia habari zako
nisingekuamini lakini
nimesikia mambo makubwa
uliyoyafanya kwa ajili ya nchi
hii na ninakuamini.Mimi na
wenzangu tutakusaidia
kufanikisha kile kilichokuleta
hapa japokuwa ni hatari kwetu
lakini ni jambo sahihi
kulifanya kwa ajili ya ulinzi wa
nchi”
“Ahsanteni sana ndugu
zangu” akasema Mathew
“Kwa sasa wafanyakazi
wote walioko ndani ya jengo
hili wamekusanywa ndani ya
chumba maalum na kila kitu
kimezimwa.Milango yote ya
kuingiana kutoka imewekwa
walinzi hivyo si rahisi kwa
wewe kuweza kufika huko
unakotaka kwenda.Sisi
tumekuja jumla nane na
tumegawanyika makundi
mawili.Kundi moja ni sisi
tuliokuja huku chini na kundi
la pili liko
juu.Tutakachokifanya utavaa
mavazi ya mmoja wetu ili
uonekane kama mwenzetu
kisha utaongozana na mmoja
wetu kuelekea katika ofisi ya
Edwin na wakati huo sisi
tutaendelea kuwepo huku
tutawaeleza wenzetu kwamba
tunaendelea
kukutafuta.Naomba ndani ya
dakika kumi uwe umemaliza
kazi yako katika ofisi hiyo
kwani walioko juu wanaweza
wakaingiwa na wasiwasi
tumechukua muda mrefu huku
chini” akasema Yule mkuu wa
ile timu
“Ahsante sana nashukuru
kwa msaada wenu.You are
doing the right thing for the
country” akasema Mathew
huku akianza kuvua mavazi
yake na kubadilishana mavazi
na mmoja wa makomando
wale kisha akaongozana na
komando mwingine
wakashuka ili kwenda kupita
katika mlango mkubwa.
Katika sehemu ya juu ya
njia ile ya
dharura,makomando wanne
wakiwa na Edwin Mbeko na
walinzi wengine wawili
waliendelea kusubiri taarifa
kutoka kwa wenzao waliokuwa
wamepita chini.
“Hakuna njia nyingine
ambayo huyo mvamizi
anaweza akapita na
kutokomea zake?akauliza
mkuu wa kikosi kile.
“Hakuna sehemu
anayoweza kutoka.Ukiacha
mlango huu hapa juu,upo
mlango mwingine ghorofa ya
pili ambao hufunguliwa kwa
namba maalum ambazo walizo
nazo ni viongozi pekee hakuna
tena mlango mwingine zaidi ya
hii miwili” akajibu Edwin
“C2 nini kinaendelea huko
chini?Mmechukua muda
mrefu mko kimya.Tujulisheni
kinachoendelea ova ! akasema
Yule mkuu akiwasiliana na
kikosi kilichokwenda chini
akajulishwa kwamba
wanaendelea na upekuzi wa
kina
Mathew akiwa katika
mavazi waliyovaa wale
makomando akiwa
ameongozana na komando
mwingine wakaelekea upande
wa ofisi za wakuu wa
idara.Anaifahamu ofisi ya
Edwin Mbeko akausogelea
mlango haukuwa umefungwa
kwani Edwin alitoka kwa
haraka na kusahau kufunga
ofisi yake.Mathew akamtaka
Yule komando kumsubiri nje
akausukuma mlango akaingia
ndani moja kwa moja
akaelekea katika meza ya
Edwin.Makaratasi mengi
yalikuwepo mezani na hakujua
aanzie wapi mara akauona
mkoba wa kompyuta ukiwa
pembeni akaushika kwa
umakini huku mkononi akiwa
amevaa glovu akaufungua na
kutoa kompyuta ndogo na
makaratasi kadhaa akayapitia
na kustuka baada ya kuiona
karatasi moja ikiwa
imeandikwa kwa mkono ikiwa
na orodha ya vitu mbali mbali
“Hivi ni vifaa vya
kutengeneza mlipuko.Ahsante
Mungu” akawaza Mathew
kisha akapiga picha karatasi
zile kwa kutumia simu yake
“Ningeondoka na
kompyuta ya Edwin lakini
akiikosa atajua nimefika ofisini
kwake.Ngoja nimpigie Ruby
anipe maelekezo
kuhus…………”akawaza
Mathew na kutolewa
mawazoni na Yule komando
aliyekuwa nje ya mlango
aliyemjulisha kwamba anasikia
vishindo vya watu
wanakuja.Haraka haraka
Mathew akarudisha kila kitu
katika mkoba namna
kilivyokuwa akatoka
wakaondoka eneo lile
wakarejea kule walikowaacha
wenzao.
“Umefanikiwa kupata kile
ulichokuwa
unakitafuta?akauliza kiongozi
wa ile timu ya chini
“Nimepata kitu kidogo
lakini naamini kitakuwa na
msaada mkubwa.Please help
me get out of here” akasema
Mathew
“Kila kitu kimezimwa sasa
hivi hakuna kamera yoyote
inayofanya kazi.Utatokea
upande wa magharibi kwani
geti kuu kuna
walinzi.Utapanda ukuta
utaruka nje kisha utawasiliana
na wenzako watakufuata”
“Ninashukuru sana ndugu
zangu kwa msaada huu
mkubwa mlionisaidia.Mungu
atawajalia kwa hili mlilolifanya
kwa nchi yenu” akasema
Mathew kisha akavaa mavazi
yake akaongozana na
makomando wawili wakatoka
mle ndani.Kulikuwa na walinzi
katika mlango wa kutokea nje
lakini hawakuwauliza
chochote.Mathew na wale
makomando wakaelekea
upande wa magharibi na
Mathew akapanda ukuta
akaruka nje wale makomando
wakarejea ndani kisha
wakawajulisha wenzao
kwamba wametafuta kila
sehemu Mathew hakuwepo.
“Haiwezekani ! akasema
Edwin kwa hasira
“Mtu huyo alikuwemo
humu ndani.Ametoka vipi?
“Yawezekana aliwahi
kutoka kabla hatujafika”
akajibu mkuu wa kile kikosi
cha makomando na Edwin
akawataka waiingie wote kwa
mara nyingine kupekua ili
kujiridhisha kwamba kweli
hakukuwa na mtu.Baada ya
kupekua kona zote
hakuonekana mvamizi
yeyote.Edwin akaelekeza
makomando wale kupekua
sehemu nyingine zote za jengo
lakini Mathew hakuonekana .
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 5
Ruby akiwa katika ofisi ya
Mathew alihisi
kuchanganyikiwa.Alikuwa
akiingia na kutoka ndani ya
ofisi ile huku akizungumza
mwenyewe
“What am I going to do to
save Mathew?akajiuliza
“Ee Mungu naomba
umsaidie Mathew aweze
kutoka salama ndani ya lile
jengo.Maisha yake yako
hatarini.Endapo akikamatwa
mambo yote yataharibika”
akaomba Ruby na kukaa juu ya
meza akiwaza
“Ngoja nipigie simu Austin
yawezekana akawa na msaada
japo anaumwa” akawaza Ruby
na kumpigia simu mmoja wa
madaktari anayewauguza
Austin na Gosu Gosu na
kumuomba azungumze na
Austin
“Hallow Ruby ! Sauti ya
Austin ikasikika baada ya
muda mfupi.
“Austin samahani kwa
usumbufu najua una umwa
lakini sina mwingine
ninayeweza kumkimbilia
kuomba msaada” akasema
Ruby
“Kuna nini Ruby?akauliza
Austin na Ruby akamueleza
kile kilichotokea
“We need to save
Mathew.Please help me”
akasema Ruby
“Ruby please relax ! Nipe
dakika tano nipige simu
niombe msaada wa vijana
wangu waende wakamkomboe
Mathew” akasema Autin
“Thank you Austin”
akasema Ruby
Dakika mbili toka
awasiliane na Austin simu
yake ikaita akaitoa mfukoni
haraka haraka na kustuka
baada ya kukuta mpigaji ni
Mathew hakupoteza hata
sekunde akaipokea
“Mathew are you
okay?akauliza Ruby
“Niko salama Ruby.Tayari
nimetoka ndani ya jengo”
“Ouh thank you
Lord.Umewezaje kutoka?
“Ruby tutazungumza
baadae lakini kwa sasa nahitaji
msaada.Nataka uje unichukue
hapa mahala nilipo.Gari langu
nimeliacha SNSA” akasema
Mathew na kumuelekeza Ruby
mahala alipokuwa.Ruby
akakimbia nje akaingia garini
na kuondoka kwa kasi.Mara tu
alipotoka getini akampigia
simu Austin na kumjulisha
kwamba tayari amewasiliana
na Mathew amekwisha toka
ndani ya lile jengo la SNSA.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 6
Upekuzi katika jengo la
SNSA ulikamilika bila ya
kumpata mvamizi aliyetajwa
kuvamia jengo lile.Kikosi cha
makomando wa SNSA
kilichokuja kupambana na
wavamizi kikaondoka kurejea
katika kambi yao.Edwin
Mbeko akaamuru shughuli
ziendelee kama kawaida huku
ulinzi ukiimarishwa kila kona
ya jengo lile.
“Rais hawezi
akanidanganya lazima
mvamizi alikuwemo humu
ndani.Amewezaje kutoka
ndani wakati milango yote
ilikuwa na
walinzi?Inanishangaza
sana.Au yawezekana wakati
Rais ananipa taarifa tayari
huyo mvamizi alikwisha
toka.Nitazungumza na Rais na
kumfahamisha kila kitu,kwa
sasa ni wakati wa kulimaliza
lile suala la Gosu Gosu kisha
nitakuja kuendelea na hili
suala la huyu mvamizi”
akawaza Edwin na kuelekea
katika chumba alichokuwamo
Dr Masawe
“Dr Masawe nimerejea
tena.Safari hii sitaki mzaha
nataka unieleze mahala
alikopelekwa Gosu Gosu
.Nakuhakikishia ukinieleza
ukweli utaondoka salama na
familia yako” akasema Edwin
“Nitakueleza ukweli lakini
naomba familia yangu
wasiguswe” akasema Dr
Masawe
“Nimekwisha kwambia
kwamba utakaponieleza ukweli
familia yako itakuwa salama
na utaondoka nao” akasema
Edwin na Dr Masawe akavuta
pumzi ndefu halafu
akamueleza Edwin mahala
alipo Gosu Gosu.
“Ahsante kwa kunieleza
ukweli lakini utaondoka hapa
na familia yako baada ya
kujiridhisha kwamba
ulichoniambia ni cha kweli”
akasema Edwin na kutoka
akarejea ofisini kwake
akawaita vijana wake wanne
wakiongozwa na dereva wake
Jackson akawapa maelekezo
ya kwenda mahala aliko Gosu
Gosu kumuua.
“Hakikisheni hakuna mtu
mnayemuacha hai mahala
hapo ! akasisitiza Edwin na
wale vijana wakaondoka kisha
akampigia simu Rais
“Edwin mmempata
Mathew Mulumbi? Akauliza
Dr Fabian
“Mathew Mulumbi ni nani
mheshimiwa Rais?akauliza
Edwin
“Ndiye aliyevamia hapo”
“Mheshimiwa Rais
hatujafanikiwa kumpata huyo
mtu”
“Hamjampata?! Dr Fabian
akashangaa
“Ndiyo mheshimiwa Rais
hatujampata”
“That’s impossible”
“Kweli mheshimiwa Rais”
“Amewezaje kutoka humo
ndani bila kukamatwa?
“Mheshimiw Rais mara tu
uliponipa taarifa ile kila kitu
hapa kilisimama na tukaanza
msako haraka sana na pia
makomando wa idara yetu
walifika wakaendelea na zoezi
la kumtafuta bila mafanikio”
“This man is not a real
human.He’s a ghost ! akasema
Dr Fabian
“Mheshimiwa rais huyu
Mathew Mulumbi ni
nani?Edwin akauliza
“I don’t know much about
him.Inasemekana alifariki
miaka mitatu iliyopita lakini
ameibuka hivi karibuni kutoka
mahala kusikojulikana na
ameanza kuleta matatizo.Sina
hakika kama ni binadamu wa
kawaida.Hakuna chochote
ambacho amechukua hapo?
“Hakuna mheshimiwa
Rais tuliwahi kuzima kila kitu
isipokuwa ameua walinzi wetu
watatu waliokuwa geti kuu”
“Dah ! akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais huyuo
mtu ni nani tuweze
kumfuatilia?akauliza Edwin
“Nitakutafuta baadae
Edwin lakini kwa sasa
hakikisheni ulinzi
unaimarishwa sana hapo
katika idara” akasema Dr
Fabian na kukata simu
“Mathew Mulumbi ni
nani?akajiuliza Edwin baada
ya Rais kukata simu
“Rais amefahamuje kama
kuna mtu amevamia idara
yetu? Akaendelea kujiuliza
Edwin
“Ngoja nimsubiri
yawezekana akanieleza baadae
alikopata taarifa za mtu huyo
kuvamia idara yetu.Kwa sasa
ngoja nijielekeze zaidi katika
mipango yetu” akawaza Edwin
na kuchukua simu akamtafuta
Devotha lakini bado simu yake
haikupatikana
“Devotha amekwenda
wapi?Kwa nini hapatikani
simuni ? Yeye ndiye kiongozi
wa mipango yote hatakiwi
kukosekana simuni lakini
tumekuwa tunamtafuta toka
asubuhi hapatikani na hajatoa
maelezo yoyote ya mahala
alipo.Anatupa wakati mgumu
wa kufanikisha m ipango yetu”
akawaza Edwin
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 7
Mathew alitoka mafichoni
baada ya Ruby kuwasili
mahala alikokuwa amejficha
akaingia garini na Ruby
akaliondoa kwa kasi
“Thank you Ruby”
akasema Mathew
“Mimi ndiye ninayepaswa
kumshukuru Mungu kwa
kukuwezesha kutoka salama
ndani ya lile jengo.Niliogopa
sana nikalazimika kumpigia
simu Austin kumuomba
msaada na muda mfupi baadae
ukapiga simu” akasema Ruby
“Ahsante sana Ruby kwa
kufanya kila jitihada za
kuniokoa.Walifahamuje kama
nimeingia mle ndani? Akauliza
Mathew
“Hata mimi bado
ninajiuliza wamefahamuje”
akasema Ruby na mara
akakumbuka kitu
“Rais alinipigia simu
akanitaka niende ikulu usiku
huu tukazungumze kuhusiana
na lile suala langu la
kuondolewa SNSA
nikamwambia haitawezekana
kwani tuko katika operesheni
muhimu.Akaniuliza ni
operesheni gani inaendelea
nikamueleza kwamba
umekwenda SNSA kuna jambo
unakwenda kulichunguza.Rais
hakuonekana kufurahi”
akasema Ruby
“Ulimueleza Rais kuhusu
operesheni hii?akauliza
Mathew
“Nilimueleza kwamba
kuna jambo unakwenda
kulichunguza SNSA lakini
sikumueleza unachokwenda
kukifanya pale”
“Basi ni yeye aliyewapa
taarifa SNSA ! akasema
Mathew kwa hasira
“Hukupaswa kumueleza
chochote.Ameharibu sana
misheni yetu.Mida hii
tulipaswa kuwa na Edwin
Mbeko tunamuhoji lakini
tumeshindwa kwa sababu
yake.From now on hakuna
kupokea simu yake yoyote hadi
hapo tutakapomaliza
operesheni yetu.Forget about
SNSA ! akasema Mathew kwa
ukali
“Kwa nini lakini afanye
hivi?Kwa nini awaeleze SNSA
huku akijua kwamba kwa
kufanya hivyo anavuruga
misheni yako? Akauliza Ruby
“Rais haniamini hata
kidogo.Toka nilipokwenda
kuonana naye kumueleza suala
la James Kasai hakuonekana
kuniamini” akasema Mathew
“Uliwezeje kutoka mle
ndani? Ruby akauliza na
Mathew akamueleza kila kitu
kilichotokea hadi
alivyofankiwa kutoka nje ya
jengo lile.
“Ahsante Mungu kwa
kumtoa salama huyu
mwanaume ninayempenda
kuliko wote ndani ya hatari
kubwa” akawaza Ruby
“Katika mkoba wa Edwin
nimekuta kuna kompyuta
lakini sikuweza kuifungua
badala yake nikabandika kadi
ndogo chini ya kompyuta
ambayo itatuwezesha
kumfuatilia.Vile vile katika
mkoba huo nimekuta
makaratasi kadhaa na
nilipoyapitia kwa haraka
haraka nilikuta kuna karatasi
moja limeandikwa kwa kalamu
ya wino ina orodha ya vitu
mbali mbali na nilipoipitia
haraka haraka nikagundua
katika orodha hiyo kuna vitu
vinavyotumika katika
kutengeneza
mlipuko.Nimezipiga picha
karatasi zote ili tuweze
kuzifanyia uchunguzi”
akasema Mathew
“Good Job
Mathew.Ilikuwa ni kazi ya
hatari sana lakini kwa hiki
kdogo ulichokipata ni
mafanikio makubwa
kwetu”akasema Ruby
“Sikufanikiwa kumpata
Edwin usiku wa leo lakini
tayari amekwisha ingia katika
rada zetu na saa zake
zinahesabika.Hana muda
mrefu kabla ya kutua katika
mikono yetu” akasema
Mathew alipomtazama Ruby
michiziri ya machozi
ikaonekana machoni pake.
“Ruby let me drive”
akasema Mathew na Ruby
akasimamisha gari pembeni ya
barabara Mathew akashika
usukani.
“Nini kinakutoa machozi
Ruby?akauliza Mathew
“Najiuliza kama hao
makomando wangekataa
kukusaidia ungekuwa wapi
mida hii? Kinachoniumiza
zaidi ni mimi ndiye ambaye
ningekuwa nimesababaisha
misheni ile kuharibika kwa
kumueleza rais” akasema Ruby
na kuinamisha kichwa
“Ningeweza kuwaua
makomando wale lakini
niliwaacha hai kwa kujua
lazima wangenisaidia.Endapo
wangekataa kushirikiana nami
nisingekuwa na kitu kingine
cha kuwafanya zaidi ya
kuwaua.Mimi ninapokuwa
katika kazi yangu huwa sina
huruma hata kdogo.Kikwazo
chochote kinachokuja mbele
yangu lazima nikiondoe ili
niweze kufanikisha misheni
yangu.Bahati yao walikubali
kushirikiana nami.Niliwaweka
katika hatari lakini walifanya
kitu sahihi kwa ajili ya nchi
yao.Kuhusu Rais usijilaumu
kwani hukujua kama
angewezakufanya kitu kama
kile.Kuanzia sasa kata kabisa
mawasiliano naye.Amekwisha
onyesha si mtu tunayeweza
kumuamini” akasema Mathew
Safari iliendelea
wakielekea katika nyumba
waliko akina Gosu Gosu.Mita
kadhaa kabla ya kuifikia
nyumba waliyokuwamo akina
Gosu Gosu likaonekana gari
nje ya geti.Mathew
akapunguza mwendo wa gari.
“Kuna gari pale nje ya
geti.Dr Masawe amerudi na
kushindwa kuingia
ndani?akauliza Mathew
“Kama angekuwa amerudi
na kushindwa kuingia ndani
lazima angekupigia simu
halafu ile si gari ya Dr
Masawe” akasema
Ruby.Mathew akasimamisha
gari
“Something is not
right.Nimepata wasiwasi
kuhusiana na gari lile.Tushuke
hapa hapa tutembee kwa
miguu” akasema Mathew kisha
akavua koti alilokuwa amevaa
akampatia Ruby bastora moja
kisha wakashuka na kuanza
kutembea kwa miguu
kuliendea geti la ile
nyumba.Walilikaribia lile gari
na kulichunguza hakukuwa na
mtu yeyote ndani yake.
“Wenye hili gari wako
wapi? Akauliza Ruby
Mathew akauparamia
ukuta na kuchungulia ndani
akastuka baada ya kumuona
mtu mmoja akiwa na bunduki
amesimama mlangoni huku
akivuta sigara akarudi chini
bila kutoa ukelele.
“Ruby they’re here !
akasema Mathew
“Akina nani? Akauliza
Ruby
“Wale watu wanaotaka
kumuua Gosu Gosu” akasema
Mathew
“Wamefahamuje kama
amehamishiwa hapa? Akauliza
Ruby
“Let’s find out.Follow me”
akasema Mathew
wakazunguka nyuma ya
nyumba Mathew akapanda
ukuta na kurukia ndani bila
kishindo.Bastora ikiwa
mkononi akanyata kuelekea
upande wa mbele ya nyumba
kwenye mlango mkubwa wa
kuingilia sebuleni.Yule jamaa
mwenye bunduki bado
aliendelea kuzunguka zunguka
pale mlangoni.Mathew
akautikisa mti wa maua na
Yule jamaa akastuka akageuka
kutazama kuna nini hakuona
kitu,akaanza kutembea kwa
tahadhari kuelekea ulipo ule
mti ili kujiridhisha kama kweli
hakuna kitu Mathew akajiweka
tayari.Mara tu Yule jamaa
alipokaribia ule mti Mathew
akaruka kama kima
akamvamia Yule jamaa na
kumpiga kichwa kizito
kilichompeleka chini
akapoteza fahamu.Mathew
akachukua pingu ya plastiki
akamfunga mikono na kujaza
tambara mdomoni kisha
akamtupa pembeni sehemu
yenye mwanga hafifu akaenda
mlangoni akachungulia ndani
kupitia dirisha lililokuwa
pembeni ya mlango lakini
hakukuwa na mtu yeyote
sebuleni akakiminya kitasa cha
mlango akaufungua taratibu
sana akaingia sebuleni
akanyata hadi katika korido
akachungulia na kumuona mtu
mmoja akiwa amesimama nje
ya chumba alimolazwa Gosu
Gosu akiwa na
bunduki.Mathew akaenda
katika runinga akaongeza
sauti.Yule jamaa aliposikia
sauti imeongezeka akaanza
kupiga hatua kuelekea
sebuleni kutazama nani
ameongeza sauti ya
runinga.Mathew akajiweka
tayari na Yule jamaa
alipojitokeza akakutana na
ngumi nzito iliyompeleka
ukutani,kabla hajakaa sawa
akavutwa na kupigwa kichwa
kizito akaanguka chini.Mathew
hakutaka kumtazama tena
kwani kwa kichwa kile tayari
hakuwa na fahamu.Mathew
akapiga hatua ndefu za
tahadhari kuelekea katika
chumba cha Gosu
Gosu.Mlango haukuwa
umefungwa akachungulia
ndani akawaona madaktari na
wauguzi waliokuwa
wanamuhudumia Gosu Gosu
wakiwa wamepigishwa magoti
chini huku jamaa wawili
wakiwaelekezea bunduki
“Natoa nafasi ya
mwisho.Nataka mniambie
nani aliyewatuma mumtoe
huyu mgonjwa hospitali?
Akauliza mmoja wa wale
jamaa kwa ukali.Mmoja wa
wauguzi alikuwa analia na
kuwaomba wale jamaa
wawasamehe
“Nitahesabu hadi tatu
kama hamtanieleza nitawapiga
wote risasi ! akasema Yule
jamaa mwenye macho ya
kikatili akaanza kuhesabu
kuanzia tatu.Kabla hajamaliza
kuitamka moja Mathew
akaizinga bastora yake na
kumpiga risasi Yule jamaa
katika kiganja cha mkono
bunduki ikaanguka chini.Yule
mwenzake aliyekuwa naye
alistuka baada ya kumuona
mwenzake ametoa mguno
baada ya risasi kumpiga
kiganja cha mkono.Kabla
hajajua risasi ile ilikotoka
tayari Mathew alikwisha ingia
me chumbani akamtandika tee
zito la mbavu Yule jamaa
aliyempiga risasi ya mkono
akaenda kujibamiza ukutani
halafu akamuelekezea bastora
Yule jamaa mwingine mwenye
bunduki
“Weka silaha yako chini
taratibu ! akasema Mathew
kwa ukali akimuelekezea Yule
jamaa bastora.Taratibu Yule
jamaa akaiweka chini bunduki
yake.Mathew akampa mmoja
wa wale madaktari pingu ya
plastiki na kumtaka amfunge
Yule jamaa mikono kwa
nyuma halafu akawataka
wamsaidie Yule jamaa
aliyepigwa risasi kiganja cha
mkono kuzuia damu
kuendelea kumwagika
“Kuna yeyote
ameumizwa?akauliza Mathew
“Hakuna aliyeumizwa
wote tuko salama.Umetokea
kwa wakati muafaka kabisa
kwani ungechelewa kidogo
sote tungeuawa.Ahsante sana
Mathew kwa kutuokoa bado
siamini kama tumenusurika
kifo ! akasema mmoja wa wale
madaktari huku akilia.
“Wagonjwa wote
wanaendeleaje?
“Wote wanaendelea
vizuri.Hawa watu ni akina
nani?akauliza daktari
mwingine
“Hata mimi siwafahamu
lakini muda si mrefu
tutawafahamu wote” akasema
Mathew kisha akawaelekeza
madaktari wawakusanye wale
jamaa waliopoteza fahamu
wawaweke sebuleni akampigia
simu Ruby na kumtaka aingie
ndani kwani hatari imekwisha
na wale jamaa
wamedhibitiwa.Yule jamaa
aliyepigwa kiganja cha mkono
akapatiwa matibabu halafu
naye akafungwa mikono kwa
waya na wote wakachukuliwa
wakapelekwa sebuleni
wakaungana na wenzao wawili
ambao hawakuwa na fahamu.
Ruby alikwenda kuchukua
gari mahali walikoliacha
akafungua geti akaingia
ndani.Aliposhuka garini
akaingia sebuleni na kupatwa
na mstuko mkubwa
alipowaona wale jamaa
waliokuwa wamedhibitiwa na
Mathew
“You ?! akasema Ruby
akimshangaa mmoja wa wale
jamaa ambaye naye alistuka
mno alipomuona Ruby
akiingia mle ndani
“Unawafahamu?akauliza
Mathew
“Ndiyo.Huyu mmoja
ninamfahamu anafanya kazi
SNSA ni dereva wa Edwin
Mbeko”
“Dereva wa Edwin?!
Akauliza Mathew naye
akishangaa na kuwatazama
wale jamaa kwa hasira
“Ahsante sana Ruby kwa
kunijulisha wanakotoka watu
hawa”
“Watu wote humu wako
salama? Akauliza Ruby
“Wote wako
salama.Niliwahi kabla
hawajawaumiza” akasema
Mathew kisha akawageukia
wale jamaa
“Wakati tunawasubiri
wenzenu wazinduke nataka
mfahamu kwamba hapa
mlipoingia ni katika tanuru la
moto.Uhakika wa kutoka hai
hapa ni mdogo sana labda
kama mtakuwa tayari
kunieleza ukweli lakini endapo
mtakuwa kiburi huu ndio
mwisho wenu ! akasema
Mathew na kuwatazama kwa
hasira kisha akamnyooshea
bastora Yule jamaa
aliyetambuliwa na Ruby
“Jina lako nani? Akaulia
Mathew Yule jamaa akawa
kimya
“Nakuuliza jina lako nani?
Akauliza tena
“Tafadhali sema ukweli
ukijifanya kiburi utapata taabu
sana ! Ruby akamweleza Yule
jamaa
“Jina lako nani?akauliza
Mathew Yule jamaa bado
akawa kimya na kuzidi
kumpandisha Mathew
hasira.Akamfuata Yule jamaa
mwingine aliyepigwa risasi ya
kiganja cha mkono akamuinua
kisha akachukua kisu na
kuzichana chana nguzo zake
akabaki mtupu halafu
akamgeukia Yule dereva wa
Edwin
“Jina lako nani?akauliza
Mathew Yule dereva bado
akawa kimya.Mathew
akageuka kwa kasi na ghafla
Yule jamaa aliyepigwa risasi ya
kiganja akatoa ukelele
mkubwa wa maumivu
makali.Alikuwa amekatwa
uume wake.Aligalagala chini
kwenye damu.Mathew
hakumjali akamfuata Yule
dereva na kumchana chana
nguo zake kwa kisu naye
akabaki mtupu
“Umeona kilichomtokea
mwenzako.Nakuuliza kwa
mara ya mwisho jina lako
nani? Akauliza Mathew
“Naitwa Jackson Kandala”
akasema Yule jamaa huku
akitetemeka kwa woga.
“Nani kawatuma hapa?
“Tumetumwa na mkuu
wetu”
“Mkuu wenu nani?
“Edwin Mbeko ! akasema
Jackson halafu Mathew
akamgeukia Ruby akamtaka
awaite madaktari waje
wamshughulikie Yule jamaa
aliyekatwa uume
wake.Madaktari wakafika na
kumchukua Yule jamaa
wakampeleka katika chumba
kitupu wakaanza
kumuhudumia ili kuzuia damu
kuendelea kumwagika
“Umeona kilichomtokea
mwenzako nawe pia
kitakutokea kama hiki endapo
utaendelea kuwa kiburi.Nataka
unieleze ukweli Edwin Mbeko
amekutuma nini
hapa?akauliza Mathew
Jackson akawa kimya.Mathew
akaushika uume wa Yule
jamaa na kuuvuta akainua
mkono wenye kisu juu
“Usinikate tafadhali
nitakueleza! akasema Jackson
“Edwin amekutuma nini?
“Ametutuma kuja kumuua
mgonjwa ambaye
amehamishwa kutoka hospitali
na kuletwa hapa anaitwa Gosu
Gosu”
“Amewaeleza sababu za
kutaka kumuua Gosu Gosu?
“Hapana hajatueleza
chochote.Katutuma tuje hapa
kufanya kazi moja tu ya
kuwaua watu wote
tutakaowakuta humu ndani”
akasema Jackson
“Amefahamuje kama Gosu
Gosu yuko hapa?akauliza
Mathew Jackson akasita
kujibu
“Jackson nitakuharibu
sasa hivi kama Yule mwenzako
naomba unijibu tafadhali !
akasema Mathew.Jackson
akaingiwa hofu baada ya
kuona macho ya Mathew
yaliyoonyesha alikuwa tayari
kumfanyia ukatili mkubwa.
“Anamshikilia daktari
mmoja anaitwa Dr Masawe na
familia yake na ndiye
aliyemuelekeza mahala
alipohamishiwa Gosu Gosu”
“Edwin anamshikilia Dr
Masawe?
“Ndiyo.Aliiteka kwanza
familia yake kisha akampigia
simu na kumpa maelekezo na
huyo daktari ndiye
aliyemuelekeza Edwin mahala
alipo GosuGosu” akasema
Jackson.Mathew na Ruby
wakatazamana.
“Dr Masawe yuko wapi
hivi sasa?akauliza Mathew
“Yuko SNSA yeye na
familia yake.Edwin
atamuachia pale tu Gosu Gosu
atakapokuwa ameuawa.”
akajibu Jackson.Mathew
akamtaka Jackson avae suruali
yake wakaenda nje sehemu ya
kupumzikia kulikokuwa na
sofa nzuri akamtaka achukue
simu yake
“Mpigie simu Edwin
mwambie kwamba tayari
mmeimaliza kazi
aliyowatuma.Gosu Gosu na
wote mliowakuta hapa
mmewaua” akasema
Mathew.Jackson akazitafuta
namba za simu za Edwin
akampigia huku akiguswa na
mdomo wa bastora kichwani.
“Jackson” akasema Edwin
baada ya kupokea simu
“Edwin kazi
tumeimaliza.Gosu Gosu
tumemuua pamoja na wote
tuliowakuta humu
ndani.Tumeua madaktari
wawili,wauguzi wawili na
wagonjwa wawili Gosu Gosu
na mwenzake”
“Good job
Jackson.Mmenifurahisha
sana.Kabla ya kuwaua
mliwahoji madaktari
wakasema nani aliyewatuma
kumuhamisha Gosu
Gosu?akauliza Edwin
“Tuliwahoji lakini
hawafahamu chochote
tukawaua”akajibu Jackson
“Ahsante
Jackson.Rejesheni silaha kisha
mkapumzike” akasema Edwin
“Ahsante sana mkuu”
akajibu Jackson.Mathew
akaichukua simu ile na
kuizima kabisa.
“Umefanya vizuri
Jackson.Bado kuna mambo
ambayo nataka kuendelea
kukuuliza kuhusu Edwin
Mbeko”akasema Mathew
“Wewe umekuwa ni dereva
wa Edwin Mbeko.Unaweza
ukaniambia sehemu
ulikompeleka kwa siku mbili
jana na leo?Wapi ulimpeleka
nje ya ofisi?akauliza Mathew
“Kwa wiki nzima
sijampeleka Edwin sehemu
yoyote.Amekuwa akiendesha
gari lake yeye mwenyewe”
“Jackson mimi ni mtu
mbaya sana pale mtu
anaponidanganya au
kunionyesha kiburi.Umeona
nilichomfanyia Yule
mwenzako.Nimetoa uanaume
wake na hata wewe ninaweza
kukufanyia vile vile
nilivyomfanya
mwenzako.Yawezekana jua la
kesho msilione tena kama
mtaendelea kunifanyia
kiburi.Nieleze ukweli uokoe
maisha yako na wenzako !
akasema Mathew
“Nitakueleza ukweli kaka
naomba uniamini”
“Nieleze haraka ! akasema
Mathew
“Nimekwambia ukweli
kwamba kwa wiki nzima
sijamuendesha Edwin
amekuwa akiendesha gari lake
yeye mwenyewe lakini
alinituma mara mbili
nimpelekee gari lake katika
bohari kuu la idara”
“Yeye alikuwa wapi hadi
akakutuma umpelekee gari
lake huko katika bohari?
akauliza Mathew
“Mara ya kwanza alikuwa
safarini Kagera akanipigia
simu na kunielekeza
nimpeleke gari lake
bohari.Aliposhuka katika
helkopta akaingia ndani ya
gari na kuondoka na wageni
wake”
“Alikuwa na wageni?
“Ndiyo alikuwa na wageni”
“Uliwaona wageni hao?
“Ndiyo alikuwa na wageni
wawili mwanaume na
mwanamke” akasema Jackson
Mathew akamgeukia Ruby
“Ulikuwa mkuu wa
Edwin.Alikujulisha kuhusu
safari hiyo ya Kagera?
“Hakunijulisha chochote
kama anasafiri.Nakumbuka
kuna siku nilimtafuta
nikamkosa na kesho yake
akaniambia kwamba alikuwa
safari nje ya mkoa nadhani
ndiyo safari hiyo aliyokwenda
Kagera”akajibu Ruby
“Jackson mara ya pili
alipokuelekeza umpelekee gari
katika bohari ilikuwa
lini?akauliza Mathew
“Ni leo jioni.Alikwenda
Arusha na akanitaka
nimpelekee gari bohari.Alikuja
na mgeni mmoja mwanaume
akaingia garini na
kuondoka”akajibu Jackson
“Wageni ambao alikuja
nao mara ya kwanza unaweza
ukawafahamu ukiwaona?
Mathew akauliza
“Ilikuwa jioni na kiza
kilianza kuingia walipotua
hivyo siwezi kuzikumbuka
vyema sura zao.Mwanamke
aliingia haraka haraka ndani
ya gari sikumuona vizuri lakini
Yule mwanaume ninaweza
kumkumbuka alikuwa mrefu
alivaa suti ya bluu na kofia ya
mduara kichwani.Alivaa
miwani mikubwa kuficha
macho yake na kidevu chake
chote kilijaa ndevu
Maelezo yale yakamstua
Mathew.Akamtaka Ruby
akalete picha ya James
Kasai.Ruby akaenda katika
gari na kurejea na kompyuta
yake akaifungua picha ya
James Kasai
“Jackson tazama vizuri
picha hii” akasema Mathew na
Jackson akayaelekeza macho
yake katika ile picha ya James
Kasai
“Mtu huyo uliyemuona
akishuka katika helkopta na
Edwin anafanana na huyu
katika picha?akauliza Mathew
na Edwin akaikazia macho
picha ile na kusema
“Huyu jamaa pichani
anafanana na Yule
niliyemuona lakini kidogo sana
hasa maeneo ya kidevuni”
akasema Jackson.Ruby
akaichukua kompyuta yake na
kuuliza
“Uliyemuona alikuwa
amevaa kofia ya namna gani?
Jackson akamuelekeza
kofia aliyokuwa amevaa Yule
jamaa na Ruby akacheza na
kompyuta yake akaivisha kofia
ile picha ya James Kasai.
“Miwani ya namna gani
alikuwa amevaa?akauliza
James,Jackson akamuelekeza
kila kitu alichokuwa amekivaa
Yule mtu na Ruby akakiweka
katika ile picha halafu
akamuonyesha Jackson
akabaki anashangaa
“Yule mtu alikuwa hivi hivi
isipokuwa ndevu zake
zimekuwa nyingi kidogo tofaui
na hizi katika hii picha”
akasema Jackson.Mathew
akamtazama kwa makini na
kuuliza
“Jackson are you sure?
“Yes I’m sure” akajibu
Jackson
“Jackson ahsante sana kwa
maelezo haya
uliyotupa.Twende ndani”
akasema Mathew na
kumchukua Jackson
akampeleka katika chumba
kitupu akamfunga mikono kwa
pingu za plastiki halafu
akaenda kuwachukua na wale
jamaa wengine wawili ambao
bado hawakuwa wamezinduka
akawapekua na kuchukua
simu zao kisha akawapeleka
katika chumba kidogo cha stoo
akawafungia humo kisha
akamfuata Ruby
“Ruby sina shaka na
maelezo ya Jackson kwamba
mtu huyo ambaye aliongozana
na Edwin Mbeko katika
helkopta kutoka Kagera ni
James Kasai” akasema
Mathew
“Ninataka sana
kumuamini Jackson lakini
ninasita” akasema Ruby
“He’s telling the truth !
akasema Mathew
“Edwin Mbeko alikwenda
Kagera na helkopta ya idara ya
SNSA na akaenda kumchukua
James Kasai.Tulifahamu
James anakuja nchini lakini
hatukujua ataingia vipi.Kila
sehemu kulikuwa na picha
yake na hakukuwa na sehemu
ambayo angeweza kupita bila
kujulikana.Ilihitajika mtandao
mkubwa wenye nguvu kuweza
kumuingiza James Kasai hapa
nchini na SNSA ndio
waliotumika.James Kasai
alivuka mpaka akaingia Kagera
Edwin Mbeko akaruka na
helkopta hadi Kagera akaenda
kumchukua James Kasai na
kumleta hapa Dare s
salaam.Mpaka hapa tuna
uhakika mkubwa kwamba
Edwin Mbeko,Devotha na
Melanie Davis ni kitu kimoja
na Edwin Mbeko kwa kutumia
idara ya SNSA hufanikisha
mipango ya mtandao
huu.Mfano mzuri ni namna
zoezi la kumfuatilia Khalid
Sultan lilivyoshindwa
kufanikiwa na jambo hilo
lilifanywa ndani ya SNSA.
Edwin Mbeko alifahamu
jambo hili na ndiye
aliyefanikisha huo
mpango.Kama haitoshi
akamuua pia Yule mwanadada
Edina ambaye uligundua
kwamba ndiye aliyekata
mawasiliano.Naamini Edina
alifanya vile kwa maelekezo ya
Edwin ndiyo maana
akamuua.Hata Yule jamaa
tuliyemuhoji Fidelis naamini
aliuawa ili kuendelea kuficha
siri.Edwin Mbeko ni shetani
wa mguu mmoja ! akasema
Mathew kwa hasira
“Dr Fabian alifahamu hiki
kinachoendelea katika idara ya
SNSA ndiyo maana akanitaka
nije kuiongoza? Akauliza Ruby
“Inaumiza sana kwa idara
nyeti ya serikali kutumika
katika kufanikisha mipango
miovu ya magaidi”
“Dah ! akasema Mathew
“Baada ya kufahamu
kuhusu Edwin Mbeko nini
kinafuata? Ruby akauliza
“Kwanza Edwin hatakiwi
kujua kama tumekwisha
mgundua lakini tuendelee
kumfuatilia kwa karibu sana
na ndiye ambaye atatuongoza
mahala alipo James
Kasai.Alipo James ndipo alipo
Melanie Davis na ndipo alipo
Khalid.Edwin ni mtu muhimu
sana kwa sasa” akasema
Mathew
“Kwa nini tusimjulishe
Rais kuhusu Edwin itakuwa
rahisi kumkamata kumuhoji
na kisha kujua mahala alipo
James Kasai?akauliza Ruby
“Rais hatakiwi kufahamu
chochote kuhusu suala hili kwa
sasa.Edwin akikamatwa
tutashindwa kuwapata akina
James na watu wengine
wanaohusiana na mtandao
wao hivyo tutamfuatilia kwa
siri sana na tutafahamu kila
kitu” akasema Mathew na
kukumbuka kitu
“Katika zile karatasi
nilizozipata katika mkoba
wake kuna orodha ya vifaa vya
kutengenezea mlipuko.Khalid
Sultan ni mtaalamu wa
milipuko na ambaye zoezi la
kumfuatilia lilivurugwa na
SNSA.Nashawishika kuamini
kwamba Khalid akishirikiana
na washirika wake ambao ni
akina Melanie na James Kasai
wanatengeneza mlipuko na
wanapanga kufanya shambulio
lingine hapa nchini.Ili
tufahamu lini na wapi
shambulio hilo litafanyika
lazima tuendelee kumfuatilia
Edwin Mbeko kwa karibu
sana” akasema Mathew
“Mathew I’m so
scared.Kwa nini tusimjulishe
Rais jambo hili mapema ili
hatua zianze kuchukuliwa?
Tukichelewa hawa jamaa
wanaweza wakatekeleza
shambulio lao na watu wengi
wakapoteza maisha lakini
tukimjulisha angali mapema
vyombo vyote vya usalama
vitaanza kuchukua tahadhari”
“Hatuwezi kumjulisha Rais
kwa sasa kuhusiana na suala
hili kwani jamaa wakifahamu
tayari wamegundulika
wanaweza wakajificha na
tukashindwa kuufahamu
mtandao wao
wote.Tunachopaswa kukifanya
ni kuhakikisha tunawatafuta
watu hawa na tufahamu kama
wanatengeneza bomu na wapi
wamepanga kulitumia hilo
bomu.Taarifa ikianza
kusambaa sasa hivi itavuruga
kila kitu.Hawa jamaa wana
mtandao mrefu na
wamejipachika katika idara
mbali mbali za serikali na
wanaweza wakapata taarifa
haraka kama wanatafutwa”
akasema Mathew na
kumtazama Ruby akamshika
bega
“Ruby we can do
this.We’re going to end them
and save our country.Have
faith in me” akasema Mathew
“I believe you Mathew”
“Thank you” akasema
Mathew
“Niliweka kadi nyuma ya
kompyuta ya Edwin.Activate
that card now.Tunatakiwa
kuanza kumfuatilia kujua
anakoelekea” akasema Mathew
na kumpa Ruby namba za ile
kadi aliyoiweka nyuma ya
kompyuta ya Edwin na Ruby
akaanza kucheza na kompyuta
yake.Baada ya dakika mbili
akasema
“Kadi tayari inafanya kazi
na mpaka sasa inaonekana
kompyuta iko katika jengo la
SNSA.Edwin Mbeko bado yuko
pale”akasema Ruby
“Good.Tutaanza
kumfuatilia bila yeye
kufahamu na kujua kila
sehemu anakoelekea na
tutafahamu mengi kuhusu
mtandao wao.Lakini hata
hivyo nina swali najiuliza.Ni
vipi kama ataiacha kompyuta
yake ofisini? Kama ikiwa hivyo
hatutakuwa tumefanya
chochote. EdwinMbeko ndiye
pekee ambaye tunategemea
atuongoze katika kuifanikisha
misheni hii hivyo lazima
tumchunguze kwa kutumia
kila mbinu.” akasema Mathew
“Mathew umesema kitu
kizuri.Anaweza akaiacha
kompyuta yake ofisini na sisi
tukaendelea kudhani kwamba
yuko ofisini kumbe hayupo”
“Kuna kitu nakifikiria.Yule
dereva wake anaweza akawa
na msaada kwetu.Tunaweza
tukamtumia” akasema Mathew
“Unataka kumtumia Yule
jamaa?akauliza Ruby
“Ndiyo nataka
kuzungumza naye ili aweze
kushirikiana nasi”
“Nadhani hilo si wazo zuri
Mathew.Yule jamaa ni mtiifu
kwa Edwin na anaweza
akamueleza kila kitu kuhusu
sisi” akasema Ruby
“Yule jamaa ndiye
anayemfahamu zaidi Edwin
kuliko sisi na vile vile Edwin
anamuamini sana hivyo
tukiweza kumtumia anaweza
akawa na msaada mkubwa
sana kwetu.Let’s try talk to
him” akasema Mathew na
kwenda kumchukua Jackson
“Jackson nimekuleta tena
hapa tunataka kuzungumza
nawe.Kuwa huru usiogope.Sisi
siyo watu wabaya hadi pale
tunapolazimishwa kuwa
hivyo.Nataka tuzungumze
kirafiki sisi na wewe” akasema
Mathew na kumtazama
Jackson
“Una watoto wangapi
Jackson?
“Nina watoto wawili”
“Wanasoma?
“Ndiyo wanasoma”
“Good.Mimi pia ni baba
nina watoto wanne.Nadhani
unafahamu majukumu ya baba
ni kuhakikisha anailinda
familia yake dhidi ya hatari
yoyote ile na siku zote baba
atafanya kila lililo ndani ya
uwezo wake kuhakikisha
familia yake wanakuwa
salama.Nasema
uongo?akauliza Mathew
“Ni kweli kabisa”akajibu
Jackson
“Vizuri sana.Kama ilivyo
kwa baba kuhakikisha familia
inakuwa salama ndivyo ilivyo
serikali ambayo ina jukumu la
kuhakikisha wananchi wake
wanakuwa salama ndiyo
maana kuna majeshi na idara
mbalimbali za ulinzi yote hii ni
katika kuhakikisha wananchi
wanaishi kwa amani na
salama.Serikali ilianzisha idara
ya SNSA kwa lengo la kupanua
zaidi wigo wa ulinzi na
usalama wa nchi.Kwa bahati
mbaya idara hii nyeti na
muhimu sana kwa nchi
imeyumba na haitekelezi tena
majukumu yake.Mabeberu
tayari wamekwisha otesha
mizizi yao katika idara hii na
sasa wanaitumia kwa malengo
yao.SNSA haifanyitena kazi ya
kulinda nchi bali imekuwa ni
hatari kwa nchi” akasema
Mathew na kunyamaza
akaichukua komputa ya Ruby
akafungua sehemu ya
kuhifadhi picha akaifungua
picha ya Melanie Davis
akamuonyesha Jackson
“Huyu mwanamke anaitwa
Melanie Davis.Ni mshirika wa
James Kasai ambaye
alitekeleza shambulio la hivi
majuzi na kuua wake za
marais.James Kasai ana
mashirikiano na kikundi cha
kigaidi cha IS na anapokea
fedha na silaha kutoka kwa
kikundi cha IS ambazo
zinapita katika mikono ya
huyu mwanamke ambaye ni
tajiri hivyo moja kwa moja
mwanamke huyu ana
mashirikiano na IS.James
Kasai na IS wanapanga
kufanya shambulio lingine
hapa nchini na kwa bahati
mbaya idara ya SNSA
inatumika katika kufanikisha
mipango hiyo.Bosi wako
Edwin Mbeko anashirikiana na
mtandao huu hatari na
anaitumia idara anayoiongoza
kufanikisha mipango ya
mtandao huu” akasema
Mathew na Jackson ambaye
alionyesha kustuka kidogo
akasema
“Hii picha ya huyu
mwanamke uliyenionyesha
amefanana na Yule
mwanamke niliyemuona siku
ile jioni Edwin aliporejea
kutoka Kagera” akasema
Jackson
“Una hakika ulimuona
mwanamke kama
huyu?akauliza Mathew
“Ninakumbuka alifanana
na huyu japo alikuwa amevaa
miwani lakini anafanana sana
na huyu”
“Kama una hakika
mwanamke uliyemuona
anafanana na huyu hakuna
shaka mwanamke huyo ni
Melanie Davis na hii inazidi
kuonyesha ukaribu wa Edwin
Mbeko na mtandao huu.Yule
mwanaume uliyemuona jioni
ile ni James Kasai ambaye kwa
sasa anashirikiana na kundi la
kigaidi la IS.Baada ya James
kuingia nchini tulipata taarifa
nyingine kwamba kuna mtu
anaitwa Khalid Sultan Khalid
anatokea kundi la IS anakuja
hapa nchini.Huyu ni
mtaalamu wa
milipuko.Tuliomba idara ya
SNSA isaidie katika
kumfuatilia Khalid
atakapoingia hapa nchini na
ikaandaliwa timu maalum
ikaanza kumfuatilia lakini
wakati zoezi la kumfuatilia
likiendelea mawasiliano kati ya
timu hiyo na ofisi kuu
yakakatika na tukampoteza
Khalid na hadi sasa hatujui
mahala alipo.Baada ya kufanya
uchunguzi tukagundua
kwamba mawasiliano
yalikatwa makusudi na mmoja
wa wafanyakazi ndani ya SNSA
anaitwa Edina na
tulipomfuatilia tukakuta
ameuawa kwa kupigwa risasi”
Akasema Mathew na
kunyamaza akamtazama
Jackson
“Jackson nimekupa
maelezo haya marefu kidogo
kwa lengo la kukupa picha ya
kile kinachoendelea hapa
nchini na katika idara ya
SNSA.Edwin Mbeko mkuu wa
idara yenu anashirikiana na
magaidi ambao wanapanga
kufanya shambulio lingine
kubwa hapa nchini.Mimi na
wenzangu tunapambana katika
kuhakikisha tunazuia
shambulio hilo lisitokee
pamoja na kuwatia nguvuni
wahusika wote wa mtandao wa
kigaidi hapa
nchini.Tukishindwa kuzuia
shambulio hilo damu nyingine
itamwagika na utakuwa ni
ushindi kwa
magaidi.Hatupaswi kuwaacha
wakafanikisha mipango yao
miovu.Hakuna anayejua
shambulio hilo limepangwa
kufanywa wapi na
lini.Yawezekana ikawa ni
kanisani,shuleni au sehemu
zenye mikusanyiko mikubwa
ya watu na huwezi ukajua
yawezekana mwanao akawepo
eneo la shambulio na
akapoteza maisha.Kama si
mwanao basi ni mtoto wa mtu
mwingine ambaye ni sawa na
mwanao.Hatupaswi kuacha
hilo likatokea na uwezo wa
kuwadhibiti watu hao waovu
tunao na ndiyo maana
tunakuomba ushirikiane nasi
katika harakati zetu za
kuwazuia watu hawa wabaya
kwa nchi yetu.Hatukulazimishi
kwani ni misheni ya hatari
sana lakini sisi sote unaotuona
hapa tumeyatoa maisha yetu
kwa ajili ya nchi na hatuogopi
kufa.Ukiwa kama mwajiriwa
wa idara ya SNSA ambayo
malengo yake ni kuhakikisha
nchi inakuwa salama hivyo
kushiriki katika misheni hii ni
moja ya wajibu wako.Baada ya
haya niliyokueleza nini
maamuzi yako?akauliza
Mathew
“Kaka samahani naomba
niwafahamu ninyi ni akina
nani? Akauliza Jackson
“Mimi naitwa Mathew
Mulumbi na mwenzanu
anaitwa Ruby.Sisi hatufanyi
kazi katika idara yoyote ya
serikali lakini tumeyatoa
maisha yetu kwa ajili ya
kuisaidia nchi kupambana na
wale wote wanaohatarisha
usalama wa nchi” akasema
Mathew
“Kaka Mathew naomba
nikiri kwamba sijawahi kupata
mstuko mkubwa kama
nilioupata leo kwa maneno
uliyonieleza.Sikujua kama
kuna hatari kubwa kiasi hiki
hapa nchini.Nimekuwa SNSA
toka wakati wa Tamar na sasa
Edwin na nimekuwa dereva
wake kwa miaka mitatu lakini
sikuwahi hata mara moja
kufahamu siri zake kama ni
mtu mbaya namna
hii.Aliponielekeza nipeleke
gari lake bohari kuu nilijua
kuna jambo linaendelea lakini
kwa kuwa nilikuwa mtiifu
kwake sikuweza kuhoji
chochote kumbe ni mtu
mkatili asiye na huruma hata
chembe.Umeniambia
silazimishwi kujiunga nanyi
lakini kwa hiari yangu
mwenyewe nataka kujiunga
nanyi kuwadhibiti hawa watu
wasifanikishe mipango yao”
akasema Jackson
“Tutakuamini vipi kama
una nia ya dhati ya kujiunga
nasi na si kugeuka
msaliti?akauliza Ruby
“Kaka hapa amenipa
maelezo marefu kidogo na
nimeyaelewa ndiyo maana kwa
hiari yangu mwenyewe
ninataka kushirikiana
nanyi.Kuhusu kuniamini hilo
litakuwa ni juu yenu lakini
mimi niko tayari kushirikiana
nanyi katika jambo hili.Nipeni
kazi yoyote nitaifanya.Nini
mnataka niwasaidie?akauliza
Jackson
“Nataka usiku huu
uchukue silaha zenu zote
mlizokuja nazo na uzirejeshe
ofisini kwenu ili wasiwe na
wasiwasi kuhusu ninyi
wakikuuliza kuhusu wenzako
waeleze kwamba wamekwenda
makwao kupumzika.Kesho
asubuhi utawahi kazini na
Edwin atakapofika utaweka
kifaa tutakachokupa chini ya
gari lake na kazi yako itakuwa
imekwisha.Endapo itajitokeza
tena kazi nyingine basi
tutawasiliana lakini utaendelea
kuchunguza nyendo za Edwin
hapo ofisini na tutakuwa
tunakupa maelekezo nini cha
kufanya.Unaweza ukalifanya
hilo?akauliza Mathgew
“Ndiyo ninaweza kulifanya
hilo”
“Good” akasema Mathew
“Vipi kuhusu wenzangu?
Nao mtawaachia?
“Hapana tutaendelea
kuwashikilia hadi pale
tutakapokuwa tumekamilisha
misheni yetu na wahusika
wote kutiwa nguvuni ndipo
tutawaachia.Yule mmoja
mgonjwa ataendelea
kuhudumiwa hapa hapa na
madaktari”akasema Mathew
na kumtazama Jackson
“Jackson niangalie vizuri
usoni mimi huwa ni mtu
mbaya mno pale ambapo
utajaribu kutuchezea na
kugeuka msaliti.Ninaapa
nitakusaka na nitakuua kwa
mateso makali
sana.Umenielewa Jackson?
Mathew akauliza
“Nimekuelewa
kaka.Ninaelewa ninachotakiwa
kufanya na sintajaribu
kuwasaliti kwani hii ni kwa
faida ya nchi yetu.Nitafuata
maelekezo yako” akasema
Jackson
“Good” akasema Mathew
na kwenda ndani akamletea
Jackson nguo za kuvaa halafu
akamtaka akachukue silaha za
wenzake akapewa kifaa
ambacho alielekezwa kukiweka
chini ya gari la Edwin
wakaagana akaondoka.
“Mathew do you trust that
guy?Ruby akauliza
“Yes I do.Ruby hatuna
namna lazima
tumuamini.Atafanya kama
tulivyomuelekeza.Kama
akifanya tofauti tutatafuta
namna nyingine lakini kwa
sasa tuendelee kumuamini”
akasema Mathew
“What’s next? Akauliza
Ruby
“Umekuwa ni usiku mrefu
wenye hatari nyingi na
mafanikio pia.Kwa sasa
tupumzike hadi kesho
asubuhi” akasema Mathew
wakaenda kuwatazama
madaktari wakawatoa hofu
kuhusu usalama wao
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 8
Saa kumi na mbili za
asubuhi ilimkuta Edwin
Mbeko amekwisha wasili
nyumbani kwa Melanie Davis.
“Karibu sana
Edwin.Habari za huko
utokako?
“Habari ni njema lakini
jana kuna tukio lilitokea katika
idara yetu kuna mtu alivamia
kwa lengo la kuiba siri za
usalama wa nchi”akasema
Edwin na kumsimulia Melanie
kila kitu kilichotokea usiku
“Poleni sana kwa tukio
hilo.Unahisi huyo mtu kitu
gani alikuwa anakitafuta hapo
katika ofisi zenu?
“Hakuna anayejua lakini
itakuwa ni siri za usalama wa
nchi.Nitazungumza na Rais
baadae leo ili anieleze kwa
kina kuhusiana na huyo mtu ni
nani na namna alivyoweza
kupata taarifa za ofisi zetu
kuvamiwa.Kwa maelezo ya
Rais anaonekana kumfahamu
huyo mtu kwani alimtaja kwa
jina lake la Mathew Mulumbi
na akadai kwamba huyo mtu
alikuwa amefariki na
ameibuka hivi karibuni kutoka
kusikojulikana.Asubuhi ya leo
ninakwenda kuonana na Rais
amenitaka niende nadhani ni
kwa ajili ya kuzungumza suala
hilo hilo” akasema Edwin
“Edwin umesema huyo
mtu aliyejaribu kuvamia ofisi
zenu anaitwa Mathew
Mulumbi?akauliza Melania
“Ndiyo.Unamfahamu?
“Hapana simfahamu lakini
nimewahi kulisikia jina hilo.Si
jina geni kwangu” akasema
Melanie na kukumbuka kitu
“Devotha ! akasema na
kuchukua simu yake akajaribu
kumtafuta Devotha lakini
hakupatikana
“Kwa nini Devotha
hapatikani toka jana?
Nakumbuka ni yeye aliyewahi
kunitamkia hilo jina.Ndiyo
nakumbuka hivyo Devotha
amewahi kulitamka hilo
jina.Tukimpata yeye anaweza
akatupa maelezo kuhusiana na
huyo Mathew Mulumbi ni
nani” akasema Melanie
“Tuachane na hilo suala
Melanie tutapata majibu yake
baadae tuzungumze kuhusu
mipango yetu.Mambo
yanakwendaje hapa? Edwin
akauliza
“Mambo yanakwenda
vizuri.Usiku kucha Khalid
ameendelea na kazi ya kuunda
bomu na ilipofika saa kumi za
alfajiri amemaliza kazi na sasa
bomu liko tayari” akasema
Melanie na kutabasamu
“Edwin leo ni siku kubwa
sana kwetu.Ni siku ya
kuandika historia katika nchi
hii.Ni mara ya kwanza Rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania anakwenda
kuuawa.Binafsi nina furaha
kubwa kwani ninakwenda
kulipiza kisasi kwa watu wawili
ambao kwa pamoja
walishirikiana katika kuwaua
wazazi wangu kikatili.Mimi
mwenyewe nilinusurika kifo
kwa namna ya ajabu lakini
malengo yao yalikuwa ni kuua
familia nzima.Kama wao
walivyotaka kuimaliza familia
yangu yote ndivyo
itakavyokuwa kwao.Nilianza
na wake zao leo ni zamu yao na
baadae watafuata watoto
wao.Nitahakikisha
ninazisafisha kabisa familia
hizi mbili na kusibaki hata na
kumbu kumbu yao.Ahsante
sana Edwin kwa kunisaidia
hadi tumefikia hatua
hii.Tusingeweza kufika hatua
hii kama si kwa msaada
wako.Nakuahidi baada ya
tukio la leo utaishi maisha
mazuri kama uko peponi.Yale
yote tuliyokuahidi utayapata
kweli na hata zaidi” akasema
Melanie
“Melanie mimi
nakushukuru sana kwa kuwa
msikivu na kufuata maelekezo
japokuwa mwanzo kulikuwa
na kutoelewana kati yetu lakini
yale yamekwisha
pita.Nashukuru kwa mipango
kwenda vizuri.Ninakwenda
ikulu asubuhi hii na nitapata
ratiba kamili.Nitakapotoka
huko nitakuja hapa na sare za
jeshi la polisi ambazo ndizo
mtu wetu atakayejitoa mhanga
atavaa ili aweze kuingiaa ndani
ya uwanja wa ndege.Ninao
watu wangu ndani ya jeshi la
polisi hivyo hakutakuwa na
wasiwasi wowote wa jambo hili
kufanikiwa” akasema Edwin
“Edwin tafadhali hakikisha
hakuna kitu chochote
kitakachoingilia na kuharibu
siku ya leo.Huu ni mpango
mkubwa sana ambao kwa
namna yoyote ile lazima
ufanikiwe” akasisitiza Melanie
“Melanie nakuhakikishia
kwamba kila kitu kitakwenda
kama kilivyopangwa.Hakuna
kitakachoweza kuvuruga
mipango yetu.Andaa shampeni
nzuri kwa ajili ya kujipongeza
jioni ya leo wakati nchi nzima
wanalia” akasema Edwin na
kuagana na Melanie alikuwa
anakwenda kujiandaa kwenda
ikulu kuonana na Rais.
“Mathew Mulumbi !
akawaza Melanie baada ya
Edwin kuondoka
“Hili si jina geni
kulisikia.Devotha aliwahi
kulitamka siku moja na
sikumbuki alikuwa
anazungumza kuhusu nini”
akawaza Melanie
“Hili jina la Mathew
Mulumbi halina mahusiano na
Gosu Gosu au
Penielea?akajiuliza
“Nakumbuka kama
Devotha alilitaja jina hili
wakati tukizungumza kuhusu
aidha Peniela au GosuGosu”
akawaza Melanie na kuchukua
simu tena akampigia Devotha
lakini simu yake
haikupatikana.
“Where are you
Devotha?Kuanzia jana
haupatikani simuni
umekwenda wapi?Kwa nini
hujatupa taarifa? Akajiuliza
Melanie
“Nimepata wazo ngoja
nimpigie simu Peniela
nimuulize kama anaweza
kumfahamu huyu Mathew
Mulumbi.Sifahamu kwa nini
nimestuka baada ya kulisikia
jina hili” akawaza Melanie na
kufungua katika kitabu chake
cha kumbukumbu akaziandika
namna za simu za Peniela
katika simu yake akampigia
“Hallow” ikasema sauti ya
upande wa pili
“Hallow Peniela” akasema
Melanie
“Nani
mwenzangu?akauliza Peniela
“Ni mimi Melanie Davis”
“Oh Melanie habari za Dar
es salaam?
“Nzuri kabisa
Peniela.Habari za Paris?
“Huku kwema pia.Ni mara
ya kanza tunawasiliana toka
umefika Dar es salaam”
“Ndiyo Peniela
hatujawasiliana tangu
nimeondoka Paris”
“Melanie nina hamu sana
ya kuzungumza nawe mambo
mengi lakini naomba nikupigie
baada ya dakika kumi na tano
kuna mgeni muhimu niko naye
tuna mazungumzo ya
kibiashara.Usiende mbali
tafadhali” akasema Peniela
“Ahsante Peniela
samahani kwa usumbufu”
“Hakuna usumbufu
wowote Melanie hata mimi
nimefurahi sana kwa
kunipigia.Nitakupigia ili
tuzungumze mambo
mengi.Kuna makampuni
mengine ambayo nataka
kuyauza.Nisubiri kwa dakika
ishirini” akasema Peniela
“Sawa Peniela ukiwa tayari
nipigie simu” akasema Melanie
na kukata simu
“Shetani jike wewe leo
umejileta mwenyewe
.Umekwisha ! akasema Peniela
baada ya kukata simu na bila
kupoteza muda akampigia
simu Peterson ambaye
anamiliki kampuni ya
wapelelezi wa kujitegema.
“Peniela habari za
asubuhi” akasema Peterson
“Peterson habari ni
nzuri.Samahani kwa usumbufu
wa asubuhi hii”
“Usijali Peniela tayari niko
kazini”
“Kuna simu nataka
kuifuatilia nchini Tanzania na
kujua mtu huyo yuko sehemu
gani.Nakuhitaji hapa mara
moja uje na vifaa vyako kwa
ajili ya kuifuatilia simu hiyo”
akasema Peniela
“Sawa Peniela ninakuja
hapo nyumbani kwako”
“Hautaweza kuwahi kwa
muda ninaoutaka.Ninatuma
helkopta ije ikuchukue”
akasema Peniela na
kumuelekeza Peterson sehemu
ya kwenda kupanda helkopta
itakayompeleka nyumbani kwa
Peniela.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 8
Peterson alishuka katika
helkopta iliyokwenda
kumchukua akiwa na sanduku
jeusi na kuelekea katika jumba
la Peniela.
“Karibu sana Peterson”
akasema Peniela wakaelekea
katika ofisi yake ya nyumbani
“Kama nilivyokueleza
simuni kuna mtu nataka
kumfuatilia kujua mahala alipo
nchini Tanzania”
“Hiyo ni kazi
ndogoPeniela” akasema
Peterson huku akifungua
sanduku lake akatoa kompyuta
ndogo na kuweka sawa
program zake akaweka kifaa
kingine mezani na kumtaka
Peniela ampigie simu mtu
anayemfuatilia
“Jitahidi kumuweka kwa
muda mrefu katika laini ya
simu” akaelekeza Peterson na
Peniela akampigia simu
Melanie
“Hallo Peniela” akasema
Melanie
“Melanie samahani kwa
kukukatisha wakati ule”
“Usijali Peniela.Ahsante
kwa kupiga”
“Sasa niko huru unaweza
ukanieleza kile ulichotaka
kunieleza”
“Umewasiliana na Devotha
kuanzia jana?akauliza Melanie
“Devotha?! Peniela
akauliza
“Ndiyo.Umewasiliana naye
?
“Hapana sijawasiliana
naye.Kuna nini?
“Nimejaribu kumtafuta
kuanzia jana na hapatikani
simuni”
“Nitajaribu kumtafuta
nikimpata nitamjulisha kuwa
unamtafuta”
“Ahsante sana
Peniela.Jambo lingine kuna
kitu nataka kuuliza”
“Uliza Melanie usihofu”
“Kuna mtu anaitwa
Mathew Mulumbi
unamfahamu?
“Mathew Mulumbi?
“Ndiyo unamfahamu?
“Hapana simfahamu huyo
mtu.Ni nani ?akauliza Peniela
“Hata mimi simfahamu
lakini nimewahi kulisikia
mahali hilo jina likitamkwa
ndiyo maana nikaona
nikuulize kama unamfahamu”
“Hapana simfahamu huyo
mtu lakini kama unamuhitaji
sana ninaweza kukusaidia
kumtafuta.Ni mfanya
biashara? Akauliza Peniela
“Hata mimi sifahamu
Peniela kuhusu huyo
mtu.Simfahamu na sina taarifa
zake”
“Sasa imekuaje
ukamuulizia wakati
humfahamu? Akauliza Peniela
“Nimesikia watu
wakizungumza kama alifariki
na ameonekana hai.Niliposikia
jina hilo nikakumbuka
nimewahi kulisikia mahali
lakini sikumbuki wapi ndiyo
maana nikakuuliza”
“Jaribu kumuuliza Gosu
Gosu yeye anaweza kuwa na
taarifa nyingi za watu mbali
mbali hapo Dar es salaam”
“Gosu Gosu am…….”
Akasema Melanie na kusita
“Amefanya nini Gosu
Gosu? Akauliza Peniela
“Alivamiwa na majambazi
akapigwa risasi”
“Mungu wangu ! Peniela
akaonyesha mstuko kama vile
hafahamu chochote
“Vipi hali yake?akauliza
“Hali yake si nzuri
nitaendelea kukujulisha
maendeleo yake” akasema
Melanie
Peterson akamfanyia
ishara Peniela kwamba tayari
amekamilisha zoezi
“Melanie taarifa hizi za
Gosu Gosu zimenistua
sana.Naomba endelea
kufuatilia kwa karibu hali yake
utanijulisha.Nitakuwa na
safari ya Tanzania wiki ijayo
tutazungumza masuala ya
biashara kuna makampuni
yangu mengine nataka
kuyauza.Tutazungumza
nitakapokuja” akasema Peniela
“Sawa Peniela.Nitafurahi
sana kuonana nawe
tena.Utakapokuja tafadhali
usiondoke bila kuonana nami”
akasema Melanie na Peniela
akakata simu
“Umepata mahala alipo
huyu niliyekuwa nazungumza
naye simuni?akauliza Peniela
“Ndiyo tayari nimepata
mahala alipo nchini Tanzania”
akasema Peterson na
kumuonyesha Peniela ramani
katika kompyuta yake
“Yuko katika jiji la Dar es
salaam mahala hapa kwenye
mduara mwekundu” akasema
Peterson
“Ahsante sana
Peterson.Naomba unitumie
picha hiyo katika simu yangu”
akasema Peniela kisha
akaagana na Peterson
akapanda helkopta
kurudishwa mahala
alikochukuliwa.Mara tu
Peterson alipoondoka Peniela
akampigia simu Mathew
Mulumbi.
“Peniela” akasema Mathew
“Mathew habari za Dar es
salaam?
“Huku
kwema.Unaendeleaje na
watoto?
“Sisi tuko vizuri.Mathew
uko katika nafasi nzuri
tuzungumze?
“Ndiyo Peniela”
“Ninakutumia ramani
katika simu yako sasa
hivi.Ukitazama katika mduara
mwekundu ni mahala alipo
Melanie Davis” akasema
Peniela na kumueleza Mathew
kila kitu kilichotokea hadi
akafahamu mahala alipo
Melanie
“Peniela nakushukuru
mno.Sipati maneno mazuri ya
kueleza shukrani zangu kwa
haya uliyonifanyia” akasema
Mathew
“Mathew ni mimi ambaye
nina deni kubwa kwako la
kulipa kwa mambo
uliyonifanyia hivyo kila pale
utakapohitaji msaada wangu
usisite kunijulisha” akasema
Peniela na kuagana na Mathew
“Sikutegemea kama
Peniela anaweza akawa na
msaada mkubwa namna hii”
akawaza Mathew na kuifungua
picha aliyotumiwa na Peniela
ilikuwa ni ramani ya jiji la Dar
es salaam.
“Melanie Davis ! Hatimaye
umeingia katika mikono yangu
! akasema Mathew huku
akiuma meno kwa
hasira.Akamfuata Ruby
chumbani alikokuwa anaoga
akafunga maji
“Kuna nini Mathew?
“Ruby tumepata mahala
alipo Melanie Davis”akasema
Mathew na kumueleza namna
Peniela alivyoweza kugundua
mahala alipo Melanie.
“Siku njema huonekana
asubuhi.Itakuwa siku ndefu na
ngumu sana”akasema Ruby
“Kweli ni siku ngumu
sana.Leo ni sisi au wao.Mbio
zao zimefika ukingoni”
“Nini tunakifanya baada
ya kujua mahala alipo Melanie
Davis?Ruby akauliza
“Kwanza ni kuchunguza na
kujiridhisha kama kweli
Melanie Davis anaishi mahala
hapo.Tukisha kuwa na uhakika
kwamba Melanie Davis Yuko
ndani ya nyumba hiyo
tutaingia katika hatua ya pili
lakini kwanza lazima
tujiridhishe.We’re going
there.Tutaweka kambi karibu
na nyumba hiyo na kufuatilia
kila kinachoendelea ndani ya
nyumba hiyo.Ninayo kamera
ya siri yenye muundo wa
ndege ambayo tutairusha
ndani ya nyumba na itatupa
picha ya kila kinachoendelea
humo ndani.Si rahisi
kugundulika kama ni kamera
kwani inafanana sana na
ndege wa kawaida anayeruka
angani” akasema Mathew
“SNSA wana drone kubwa
ambazo hurushwa angani kila
asubuhi na kuzunguka sehemu
mbali mbali za jiji na
huwasaidia kupata picha mbali
mbali.I can hack one
drone”akasema Ruby
“We’re done with
SNSA.Wanaweza wakagundua
kwamba tunatumia drone yao
na wakavuruga misheni
yetu.Hatuhitaji drone ya
SNSA.Ninayo pia kamera
nyingine ndogo ambayo
tutaitumia.Ni aina mpya ya
kamera za kijasusi ambayo
inafanana sana na
nyuki.Kamera hii inaweza
ikaingia hadi ndani ya nyumba
na kutupa picha nzuri”
akasema Mathew
“Kwa kamera hizo mbili
hatuna haja ya kutumia drone
ya SNSA” akasema Ruby huku
akifuta maji na kutoka bafuni
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 9
“Jackson jiandae nataka
unipeleke ikulu ninakwenda
kuonana na Rais” Edwin
Mbeko akamwambia Jackson
dereva wake mara tu
alipowasili katika ofisi za
SNSA akitokea nyumbani kwa
Melanie Davis.
Jackson akaenda katika
gari la Edwin akaanza kulifuta
vumbi.Akatazama pande zote
hakukuwa na mtu katika
maegesho yale ya viongozi
akachukua kile kifaa
alichopewa na Mathew
akakibandika chini ya gari
halafu akampigia simu
Mathew
“Kaka tayari
nimekibandika kile kifaa
katika gari la Edwin” akasema
Jackson
“Good job Jack.Nini
kinaendelea hapo SNSA kwa
sasa?
“Edwin anataka nimpeleke
ikulu asubuhi hii”
“Sawa Jack endelea
kutujulisha kila mahala
anakoelekea na sisi
tutaendelea kufuatilia kupitia
hicho kifaa ulichokiweka
katika gari lake” akasema
Mathew na kukata simu
“Jackson tayari ameweka
kile kifaa katika gari la Edwin”
Mathew akamwambia Ruby
wakati wakijiandaa kuondoka
nyumbani kwao kwenda kwa
Melanie.Ruby aliyekuwa
pembeni ya Mathew akiwa na
kompyuta yake akakiona kile
kifaa alichokiweka Jackson
“Tayari
nimekiona.Sikutegemea kama
angeweza kufanya
tulivyomuelekeza”
“Unatakiwa kujifunza
kuwaamini
watu.Nitakufundisha namna
ya kumtambua mtu ambaye
anasema ukweli” akasema
Mathew na ujumbe ukaingia
katika simu yake akausoma
ulitoka kwa Dr Masawe
“Please stop calling
me.I’m done with you !
“Dr Masawe hatarejea
tena.Kitendo cha jana kutekwa
na Edwin tayari kimempa uoga
mkubwa kuendelea
kushirikiana nasi.Hakuna
tatizo tutaendelea kuwatumia
wale madaktari waliobaki
ambao wamekubali kuendelea
kumuhudumia Gosu
Gosu.Nitawalipa mara mbili
zaidi ya tulivyokubaliana”
akasema Mathew
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom