Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 3: EPISODE 11
Akiwa amepitiwa na
usingizi sofani,Gosu Gosu
alihisi kama mikono laini
inamgusa shingo
yake.Akajaribu kufumbua
macho kweli kulikuwa na
mtu mbele yake
“Sandra” akasema Gosu
Gosu
“Samahani kwa
kukatisha usingizi
wako”akasema Sandra
“It’s okay” akasema Gosu
Gosu na kunyanyuka haraka
akainyakua bastora yake
“Any danger?akauliza
“Relax Gosu
Gosu.Hakuna hatari
yoyote.Kumekucha tayari.Ni
muda wa kuendelea na kazi”
akasema Sandra na kuelekea
katika kompyuta
“Sikufumba macho toka
nilipoanza uchunguza
kompyuta hizi za Tamar na
nimefanikiwa kupata mambo
kadhaa.Nadhani
tungekutana wote ili
niwaeleze kile
nilichobahatika kukipata”
akasema Sandra.Gosu Gosu
akaenda kuwaamsha Austin
na Agatha wote wakakutana
ofisini
“Kuna mambo kadhaa
nimefanikiwa kuyapata
katika kompyuta hii kubwa
ya Tamar.Kwanza kabisa
Tamar amekuwa akipokea
fedha kutoka katika akaunti
moja kwenye benki ya Autum
iliyoko Ufaransa.Sijaweza
kumpata mmiliki wa akaunti
hiyo kwani amefichwa lakini
inaonyesha ni fedha nyingi
amekuwa akipokea.Akaunti
yake iliyoko katika benki
moja hapa nchini ina shilingi
bilioni mbili na milioni mia
sita sabini na tisa”Sandra
akanyamaza
“Ni fedha nyingi sana”
akasema Austin
“Ndiyo maana hakuona
ugumu kunipatia zaidi ya
milioni moja kila siku”
akasema Agatha
“Tamar ni mtu makini
sana na amekuwa makini
katika kuchunga
mawasiliano yake kama
nilivyowaambia kwamba
nilimtengenezea program
maalum ya kufuta rekodi za
mawasiliano yake yote ya
simu na ndivyo anavyofanya
katika kompyuta yake kila
anapowasiliana na mtu
hufuta kila kitu.Kwa bahati
mbaya kwake na nzuri kwetu
nilikuta kuna barua pepe
ambayo aliisoma na kusahau
kuifuta ambayo iliingia jana
usiku.Imetoka kwa mtu
anaitwa Dinosaur”
“Dinosaur? Akauliza
Gosu Gosu na kutoa kicheko
kidogo
“Wanyama hawa
wamekwisha toweka duniani
miaka mingi.” Akasema
Austin kwa utani
“Mtu huyo anajiita
Dinosaur amemtumia Tamar
ujumbe huu” akasema
Sandra na kuwaonyesha
akina Austin ule ujumbe
uliotumwa na Dinosaur
“Awamu ya kwanza na
ya pili zimemalizika
vyema,jiandae kwa awamu
kubwa ya tatu.Nimetaarifiwa
njiwa anaandaliwa na muda
wowote atatua Dar es
salaam.Maandalizi
yamekamilika?
Hivi ndivyo ulisomeka
ujumbe ule aliotumiwa
Tamar.Ukimya ulitanda pale
sebuleni baada ya muda
Austin akasema
“Kama alivyosema Gosu
Gosu kazi bado tunayo
kubwa.Huyo Dinosaur ni
nani? Umeweza kufuatilia
barua pepe yake na
kumgundua mahala
alipo?akauliza Austin
“Nimejaribu lakini
sijafanikiwa.Ni mtandao wa
watu makini na wenye
utaalamu mkubwa katika
kuficha mambo yao”
akasema Sandra
“Kuna mpango mkubwa
unaandaliwa kati ya Tamar
na huyo Dinosaur.Kuna mtu
anakuja Dar es salaam
ambaye katika maelezo haya
ametajwa kama
njiwa.Dinosaur pia ametaja
kumalizika kwa awamu ya
kwanza na ya pili na sasa
wanaingia katika awamu ya
tatu inaonekana kuna
mpango mkubwa
unaoendelea ambao una
awamu tatu na mbili tayari
zimekamilika na sasa
inafuata awamu ya tatu
ambayo ndiyo hiyo
inamuhusisha huyo njiwa
anayetarajiwa kuingia nchini
hivi karibuni.Tumebaki njia
panda”akasema Austin
“Hili ni fumbo kubwa
tulimuhitaji sana Tamar
aweze kutupa majibu ya
maswali haya”akasema Gosu
Gosu
“Tamar hayupo,hivyo
basi tuna kazi kubwa mbele
yetu.Tayari tuna huyu mtu
anaitwa
Dinosaur.Tunatakiwa
kumfahamu ni nani yuko
wapi na nini mipango yao na
Tamar.Kuna ile akaunti
ambayo imekuwa ikitumika
kumtumia Tamar fedha
katika akaunti yake hiyo
nayo tunapaswa kuifahamu
ni ya nani.Kazi nyingine
kubwa ambayo tunayo ni
kumfahamu mtu ambaye
ametajwa kwa jina la njiwa
ni nani?Hiyo ndiyo kazi
kubwa iliyoko mbele yetu”
akasema Austin
“Bado haikuishia hapo”
akasema Sandra
“Katika kompyuta hii pia
nimegundua kuna faili moja
lilikuwa limefichwa sana lina
video mbili.Katika video hizo
anaonekana Tamar na mtu
ambaye naamini ni Rais Dr
Fabian wakifanya mapenzi
lakini Dr Fabian anaonekana
akimuingilia Tamar kwa
nguvu”akasema Sandra
“What?akauliza Gosu
Gosu na Sandra akacheza
video moja.Katika video hiyo
Tamar anaonekana akiwa
kitandani amejipumzisha
akiwa na nguo ya ndani na
mara akatokea mtu mmoja
ambaye sura yake ilikuwa
inafanana na Dr Fabian
akaenda kulala pembeni
yake na kuanza kumtomasa
Tamar.Kulitokea
kutokuelewana kati yao na
Tamar akamnasa kofi.Dr
Fabian akaonekana
kukasirika akamnasa Tamar
makofi mfululizo Tamar
akajikunja kitandani
akilia,Dr Fabian akachukua
waya akamfunga Tamar
mikono kwa nyuma halafu
akaanza kumuingilia huku
akiwa amemziba
mdomo.Alipomaliza akavaa
nguo zake na kumfungua ule
waya aliomfunga halafu
akaondoka zake akamuacha
Tamar kitandani
akilia.Baada ya muda
akainuka na kwenda kuizima
kamera iliyokuwa ikichukua
video ile.Video ya pili
anaonekana Tamar akitoka
kuwasha kamera na vinywaji
vikaonekana mezani.Baada
ya muda akatokea Fabian
akiwa anafunga vizuri
suruali yake.Alionekana
ametoka maliwato.Akaketi
pembeni ya Tamar wakaanza
kunywa pombe huku
wakivuta sigara.Mara
Fabian akambusu Tamar
shavuni na kutaka kutoa
ulimi wake akaupeleka
katika mdomo wa Tamar
ambaye hakuonekana
kupendezwa na kitendo kile
akamnasa kofi.Fabian
alichukizwa na kitendo cha
Tamar kumnasa kofi
akasimama na kumnasa
Tamar makofi mawili
mfululizo halafu
akamsukumia katika sofa na
kuichana sketi aliyokuwa
ameivaa Tamar halafu
akaivuta nguo ya ndani
akaitupa chini akashusha
suruali yake na kuanza
kumuingilia Tamar huku
akimnasa
makofi.Alipomaliza akavaa
suruali yake na
kuondoka.Tamar akaenda
kuizima kamera.Sebule
ilikuwa kimya kila mmoja
alipatwa na mshangao
mkubwa.
“I can’t believe this !
akasema Gosu Gosu
“Play that again.Nataka
nihakikishe kama kweli
huyu anayeonekana katika
video hii ni Dr Fabian huyu
Rais wetu au ni video ya
kutengeneza.Teknolojia
imekua sana zama hizi na
watu wanaweza kutengeneza
video kwa ajili ya kumchafua
mtu Fulani” akasema Austin
na Sandra akaicheza tena ile
video.
“Play it again ! akasema
Austin ikachezwa tena.
“Sandra unaweza
ukanihakikishia kwamba
anayeonekana katika video
hii ni Rais Dr
Fabian?akauliza Austin
“Kuna progamu ya
utambuzi wa sura ambayo
inaweza kutusaidia kujua
kama kweli huyu
anayeonekana katika video
hii ni Rais Dr Fabian.Tatizo
ni kwamba program hiyo iko
SNSA na ili kuipata lazima
nitumie akaunti yangu.Je
mtakuwa tayari nitumie
akaunti yangu ya
SNSA?akauliza Sandra
“Do it” akasema
Austin.Sandra akaingia
katika akaunti yake ya
SNSA akafungua program
hiyo ya kutambua sura na
kuchukua picha iliyoko
katika ile video akaiingiza
katika program ikaanza
kutafuta.Baada ya sekunde
chache program ikatoa
majibu na ikathibitisha Yule
ni Rais Dr Fabian.
“Oh my God ! akasema
Austin
“Sasa nimeanza kupata
picha kwa nini Dr Fabian
amekuwa mwepesi sana
kumsikiliza Tamar kila
atakachomweleza.Ni kwa
sababu ya video
hizi.Tumejiuliza mimi na
Austin kwa nini Dr Fabian
anampa Tamar kipaumbele
kikubwa namna hii sasa jibu
tumelipata” akasema Gosu
Gosu
“Kuna kitu nimekiona
katika video hizi
mbili.Ukitazama video hizi
mbili utaona kamera
iliyokuwa inachukua videro
hizi ilitegwa mahala ambako
Dr Fabian asingeweza
kuiona wala kujua kama
wanarekodiwa.Tunaona
baada ya matukio yote
mawili kumalizika Tamar
anainuka na kwenda kuzima
kamera.Hii inaonyesha
kwamba alitegemea kitendo
kile kutokea” akasema
Sandra
“Nakubaliana na Sandra”
akasema Austin
“Inaonyesha wazi kabisa
kwamba Tamar alitegemea
matukio yale kutokea na
akatega kamera ili
arekodi.Nini hasa lengo lake
kurekodi akitendewa vile na
Dr Fabian?akauliza Austin
“Nahisi Tamar amekuwa
na mahusiano na Dr Fabian
na inawezekana hii ni tabia
ya Dr Fabian na alikuwa
akimtendea hivi mara kwa
mara ndiyo maana akaamua
kumrekodi.Na mimi narejea
swali lako kwa nini
amrekodi? Gosu Gosu
akauliza
“Nahisi Tamar alitumiwa
na watu ili kurekodi video
zile”akasema Agatha
“Walimtumia kwa
madhumuni yapi? Video hizi
zinaonyesha ni za muda
mrefu kabla ya Dr Fabian
hajawa Rais.Je kama ni watu
walimtumia Tamar kurekodi
ile video walijua kama Dr
Fabiuan atakuwa Rais wa
Tanzania? Akauliza Sandra
“Tuna mengi bado ya
kuyatafutia majawabu”
akasema Austin
“Jamani nina wazo.Tuna
mambo mengi ya kuyatafutia
majawabu kama alivyosema
Austin lakini mikono yetu
imefungwa.Austin
unatafutwa na SNSA,Agatha
anatafutwa na SNSA mimi
pia nitakuwa ninatafutwa
kwa vile ni mtu wa mwisho
kuwasiliana na Tamar
simuni.Kazi yetu itakuwa
ngumu sana hivyo nina
ushauri”
“Go ahead” akasema
Austin
“Tumetoa jasho jingi
kuhakikisha Rais anakuwa
salama.Haikuwa kazi
nyepesi kuzipata rekodi zile
ambazo kama zingetumika
zingemuweka pabaya sana
Rais wetu,maisha ya watu
pia yamepotea katika
kuzitafuta zile video lakini
Rais hajui kitu
kinachoendelea.Kwa kazi hii
kubwa tuliyoifanya we need
something in
return.Tumtake Rais amteue
mmoja wetu hapa awe mkuu
wa SNSA baada ya Tamar
kufariki.Kama tukifanikiwa
kumpata mmoja wetu katika
nafasi hiyo basi tutaweza
kufanikisha mipango yetu
iliyobaki.Pale SNSA kuna
kila kitu tunachokihitaji ili
kutusaidia kufanikisha
mipango yetu”akasema
Sandra
“That’s a good idea.Una
akili sana Sandra”akasema
Austin
“Wazo hili linastahili
tuzo” akasema Gosu Gosu na
wote wakatoaa kicheko
“Ahsante kama nyote
mnakubaliana na wazo
hili.Nani basi kati yetu
ambaye tumpendekeze awe
mkuu wa SNSA endapo Rais
atakubali? Akauliza Sandra
“Austin anafaa sana”
akasema Agatha
“Mimi hapana.Tayari
mimi ni mkuu wa kikosi cha
operesheni maalum hivyo
nafasi yangu naomba ibaki
hivyo hivyo.Kwa nini asiwe
Gosu Gosu?
“Me ?akauliza Gosu Gosu
na kucheka
“I’m a killer.Nikipewa
nafasi hiyo kila siku watu
watakuwa wanakufa”
akasema Gosu Gosu na wote
wakacheka
“Seriously I’m not fit for
that position lakini kuna mtu
ambaye anaweza akafaa
sana katika nafasi hiyo”
akasema na kunyamaza
“Nani ?akauliza Austin
“Ruby”
“Ruby?
“Ndiyo.Anafaa sana kwa
nafasi hii.Tukimuweka pale
SNSA nina uhakika kila kitu
kitakwenda vizuri”
“Whos’s she?akauliza
Sandra
“Ruby ni mchawi wa
kompyuta.Anaijua kompyuta
kuliko aliyeigundua.Kwa
sasa yuko uingereza
anafanya kazi katika
mamlaka kuu ya
mawasiliano ya kiintelijensia
nchini Uingereza GCHQ”
“Wow ! huyo anaonekana
anaweza kuwa chaguo
zuri”akasema Sandra
“She’s more than perfect
for this position” akasema
Gosu Gosu
“Wote tunakubaliana
kwamba Ruby achukue
nafasi hiyo? Akauliza Austin
na wote
wakakubaliana.Austin
akachukua simu yake
akaiwasha na kumpigia Dr
Fabian
“Austin ! Akauliza Dr
Fabian kwa sauti iliyojaa
wasiwasi
“Mheshimiwa Rais
ahsante kwa kupokea simu
yangu.Nahitaji kuonana
nawe”
“After what you’ve done
do you think I’m going to
trust you again?akauliza Dr
Fabian kwa ukali
“I’ve done nothing bad to
you Mr President.Tafadhali
naomba uniruhusu nije
kuonana nawe.Nina jambo la
muhimu sana la
kuzungumza nawe”
“Austin sina muda wa
kuonana nawe!
Naku…………” akasema Dr
Fabian lakini Austin
akamkatisha
“Mheshimiwa Rais kabla
ya alasiri ya leo nchi
itatikiswa kwa rekodi za
mazungumzo yako na Rais
Patrice Eyenga kuhusiana na
mauaji ya Lucy Muganza”
akasema Austin
“Mazungumzo?! Akauliza
DrFabian
“Ndiyo utayafahamu
hapo baadae mheshimiwa
Rais”
“Are you trying to
threaten me young
man?akauliza Dr Fabian
“Hapana mheshimiwa
Rais sina uwezo huo lakini
naomba tusifike huko kwani
madhara yake ni makubwa
hasa kwa upande
wako.Naomba tuonane
mheshimiwa Rais
tuzungumze”akasema
Austin.Dr Fabian akafikiri
kidogo kisha akasema
“Fine.Saa tano za
asubuhi njoo hapa ikulu”
akasema Dr Fabian na
kukata simu
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 3: EPISODE 12
Austin alifika ikulu
lakini Dr Fabian
hakuonyesha uchangamfu
kama ambavyo
huchangamka kila
anapokutana na Austin.Sura
yake ilija hasira.Baada ya
Austin kupokelewa Ikulu
waliingia katika chumba cha
mazungumzo ya faragha
kama wafanyavyo kila
Austin afikapo ikulu kwa
mazungumzo.
“Kabla hujanieleza kile
unachotaka kunieleza
naomba nikufahamishe
kwamba nimepokea taarifa
za kifo cha Tamar kwa
masikitiko makubwa na
nimeapa yeyote Yule
aliyehusika katika kifo hicho
nitamsaka hadi apatikane
awe mzima au
amekufa.Hakuna aliyeshiriki
atakayebaki salama !
akasema Dr Fabian kwa
ukali
“Mheshimiwa Rais
usitumie nguvu kubwa sana
kuongelea suala hilo au
kumtafuta muuaji wa Tamar
Axon wakati unaye mbele
yako”
“You?! Akauliza Dr
Fabian
“Yes me and my friends
we killed her”
“Jesus Chris ! akasema
Dr Fabian
“Dr Fabian naomba
kwanza unisikilize kile
ninachotaka kukwambia
halafu mwisho utaamua
kama unataka kunikamata
na kunifungulia mashtaka
au vinginevyo lakini kwanza
nisikilize” akasema
Austin.Dr Fabian hakujibu
chochote aliendelea
kumtazama kwa hasira
“Mheshimiwa Rais
ulitupa kazi mimi na
wenzangu ya kumuua Lucy
Muganza na tukaitekeleza
kazi hiyo vizuri lakini baadae
likaibuka tena suala la balozi
Benjamin nalo ukatukabidhi
sisi tumchunguze kwa bahati
mbaya akafariki wakati
uchunguzi
unaendelea.Mpaka sasa
hatujui nani walimuua balozi
Benjamin na kwa nini”
“Hamjui nani kamuua
balozi Benjamin?Mnadhani
mimi ni mtoto mdogo ambaye
nitashindwa kugundua
mchezo mlioufanya?Wewe na
wenzako mlimuua balozi
Benjamin” akasema Dr
Fabian
“Kwa nini tumuue mtu
ambaye ulitutuma
tumchunguze?akauliza
Austin na Dr Fabian akawa
kimya
“Mheshimiwa Rais
hatukumuua
Benjamin.Kama kuna mtu
amekueleza kwamba sisi
tulimuua
amekudanganya.Sikiliza
namna
ilivyokuwa.Tuligundua
kwamba balozi Benjamin
amealikwa katika hafla ya
uchangishaji fedha za
mabweni ya watoto waishio
kwenye mazingira magumu
na sisi kwa vile tulikwisha
anza kumfuatilia tulikuwepo
ukumbini.Benjamin alitoka
ukumbini akaenda katika
lifti na akiwa ndani ya lifti
mwanamke mmoja
alimuwekea bahasha katika
mfuko wake wa koti na mtu
wangu aliyekuwamo ndani
ya lifti akimfuatilia
Benjamin alikiona kitendo
hicho.Tulimuandama Yule
mwanamke tumjue ni nani
na amempa nini balozi
Benjamin kwa siri namna
ile.Tulifanikiwa kumpata
mwanamke huyo na baada
ya kumuhoji akadai yeye ni
mfanyakazi wa SNSA.Kazi
yake kubwa ni
mdukuaji.Alitueleza kwamba
kwa muda wa wiki kadhaa
amepewa kazi maalum ya
kudukua simu yako na
kuhifadhi mazungumzo yako
yote ya simu,hivyo
mheshimiwa Rais fahami
kila simu unayopiga au
kupigiwa inasikilizwa na
SNSA”
“Simu yangu
unadukuliwa? Dr Fabian
akahamaki
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Simu yako inadukuliwa
na SNSA”
Dr Fabian akasimama na
kushika kiuno.
“Mheshimiwa Rais
mawasiliano yako yote ya
kila siku hurekodiwa na
kisha huwekwa katika faili
maalum”
“SNSA hawawezi
kudukua simu ya Rais !
That’s a big lie ! akafoka Dr
Fabian
“Nisikilize kwanza
mheshimiwa Rais” akasema
Austin
“Mkurugenzi wa SNSA
Tamar Axon ndiye aliyetoa
maelekezo kwamba simu
yako idukuliwe”
“Tamar ! akazidi
kuhamaki Dr Fabian
“Tamar hawezi kabisa
kufanya kitu kama hicho !
akasema Dr Fabian
“Hiki si kitu cha kubuni
mheshimiwa Rais.Ni kweli
jambo hilo linafanyika na
aliyekuwa akifanya ndiye
aliyetueleza
kinachoendelea.Katika
kukusanya rekodi za
mawasiliano yako Agatha
aligundua uliwasiliana na
Rais Patrice Eyenga wa
Congo na mlikuwa
mnazungumzia kuhusu
mauaji ya Lucy
Muganza.Rekodi zako zote
ulizozungumza kuhusu
mauaji ya Lucy Muganza
Agatha alizificha
hakumuonyesha
Tamar.Agatha alipewa diski
mweko na Tamar ampelekee
balozi Benjamin na
alipokuwa njiani
aliichunguza kujua kuna nini
ndani akakuta kuna rekodi
mbili za mazungumzo yako
na Rais Patrice Eyenga
kuhusu mauaji ya Lucy
Muganza”
“Real?!! Akauliza Dr
Fabian Austin akatikisa
kichwa
“Tamar anaweza kweli
akanifanyia mambo kama
hayo? Dr Fabian akabaki
anashangaa
“Ni kweli mheshimiwa
Rais” akasema Austin
“Ni vigumu kuamini”
Austin akatoa diski
mfukoni akaichomeka katika
kompyuta na Rais akaanza
kusikiliza rekodi za
mazungumzo yake ya
simu.Austin akamchezea
rekodi mbili akizungumza na
Patrice Eyenga.
“Mheshimiwa Rais ziko
nyingi hizi ni mbili tu
nimekuchezea” akasema
Austin.
“A..A..AAAA…Austin I
don’t know what to say !
“Don’t say anything Mr
President.Siku ile
tulipokwenda nyumbani kwa
Tamar kufanya uchunguzi
ukatuzuia tulikuwa
tunatafuta faili lenye rekodi
hizi”
“Austin I’m sorry .I didn’t
know anything.Kwa nini
hukunieleza jambo kubwa
kama hili mapema?
“Nilitaka kukueleza
lakini hukunipa nafasi na
badala yake ukatengeneza
mtego ili nikamatwe na
SNSA”
“Austin…”akasema Dr
Fabian na kushindwa
kuendelea.Alikosa neno la
kusema
“Mheshimiwa Rais,Jana
usiku tumevamia nyumbani
kwa Tamar na kufanikiwa
kulipata faili lenye rekodi
zote tumezifuta na zilizobaki
ni hizi hapa” akasema Austin
na kumpatia Dr Fabian ile
diski mweko.Dr Fabian
akashusha pumzi
“Thank you Lord”
akasema na kuichukua ile
diski
“Una hakika hakuna
sehemu nyingine zilipo
rekodi hizi?
“Hakuna mheshimiwa
Rais.Tulipandikiza kirusi
katika mfumo wa kompyuta
wa SNSA na kuharibu kila
kitu rekodi zilikuwa
zimebaki katika kompyuta
ya Tamar”
“Good job
Austin.Ahsanteni sana wewe
na wenzako kwa kazi hii
kubwa mliyoifanya.Naomba
unisamehe sana kwa yale
niliyokufanyia”
“Mheshimiwa
Rais,Tamar alijiua mwenywe
kwa kujipiga
risasi.Tunaamini alikuwa
anashirikiana na balozi
Benjamin lakini mpaka sasa
hatujui nani waliomuua
balozi Benjamin na kwa
nini.Japokuwa wote wawili
wamefariki dunia lakini
hatari bado haijaisha.Kuna
mambo tumeyagundua
kwanza Tamar alikuwa
anapokea fedha kutoka
katika akaunti iliyoko
Ufarnsa ambayo mmiliki
wake amefichwa.Amekuwa
akipokea fedha nyingi
kupitia akaunti
hiyo.Tunatafuta kujua
mmilikiwa hiyo akaunti na
fedha hizo zote zina malengo
gani.Katika akaunti yake
tumekuta ana zaidi ya bilioni
mbili.Tumegundua pia
mawasiliano yake na mtu
anaoitwa Dinosaur.Bado
hatujafahamu mtu huyu
yuko wapi lakini barua pepe
tuliyoikuta katika kompyuta
ya Tamar inasomeka hivi”
akasema Austin na
kumuonyesha Rais barua
pepe waliyoikuta katika
kompyuta ya Tamar.Dr
Fabian akazidi
kuchanganyikiwa
“Ukisoma barua pepe hii
utagundua Tamar na huyo
Dinosaur wana mipango
mikubwa inayokwenda kwa
awamu na tayari awamu
mbili zimekamilika na sasa
wanaingia awamu ya tatu na
njiwa anayetaja hapa si
njiwa mnyama bali ni mtu
anategemewa kuwasili muda
wowote.Bado hatumjui ni
nani na anakuja kufanya
nini”
“Dah ! siamini macho
yangu.Tamar ?!! akasema Dr
Fabian
“Nilimuamini sana
kumbe ni chui.Umesema
anatumiwa fedha kutoka
akaunti iliyoko
Ufaransa,balozi Benjamin
pia anatokea Ufaransa,Lucy
na Laurent Muganza makazi
yao wote ni Ufaransa,Rais
wa umoja wa Ulaya anatokea
Ufaransa na hata ukiangalia
wale waliotuma jumbe katika
kurasa zao zao za twitter
Benjamin na Rais Michael
wote wanatoka Ufaransa.Leo
nimekuwa na malumbano
makubwa na Rais wa
Ufaransa kuhusu kifo cha
Benjamin.Ukiunganisha
haya yote unapata picha
kwamba mchezo huu
tunacheza na
Ufaransa.Ukijiuliza kwa nini
tucheze na Ufaransa?Jibu ni
rahisi jamhuri ya
kidemokrasia ya
Congo.Baada ya kuingia
madarakani Rais Patrice
Eyenga amekata mirija yote
ya mataifa makubwa
kunufaika kwa kuchota
rasilimali za Congo hasa
madini na sasa wanatafuta
namna ya kurudi.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
inazidi kuimarisha ukuta wa
kuzuia uchotwaji wa
rasilimali zake kwa kujiunga
na jumuiya ya Afrika
mashariki ndiyo maana
mataifa haya ambayo
yanataka kurejea Congo kwa
nguvu wanataka kuanza na
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika Mashariki halafu
waingie Congo.Kama Tamar
alikuwa na mahusiano na
balozi Benjamin basi ni wazi
anashirikiana pia na umoja
wa Ulaya na ndiye aliyekuwa
akimpatia balozi Benjamin
siri za nchi kwani SNSA ina
siri nyingi za nchi.Ukifuatilia
mtiririko wa mambo ulivyo
toka alipouawa Lucy
Muganza utaona kabisa
kwamba balozi Benjamin na
wenzake walihisi serikali ya
Tanzania inahusika na
mauaji yale hivyo wakawa
wanatafuta
ushahidi.Ninamshukuru
sana huyo ambaye alificha
rekodi za mazungumzo
yangu na Patrice
Eyenga.Alifanya jambo
kubwa na la kishujaa”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais hii ni
vita na ulipaswa kutuamini
vijana wako lakini ulituzuia
hatakuendelea na operesheni
yetu.Licha ya kutuzuia lakini
bado tumeendelea kuweka
hatarini maisha yetu na
kupambana hadi
tukafanikiwa kupata rekodi
hizo.You are safe now Mr
President” akasema Austin
“Austin nimeishiwa
maneno ya kusema.Mimi ni
rais wako lakini ninajiona
mjinga sana kwa mambo
niliyoyafanya.Kwa nini
nilishindwa kukuamini
Austin?Nisamehe sana
kijana wangu najua
nilichokif……….”
“Usijali mheshimiwa
Rais” Austin akamkatisha Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais kuna
jambo la mwisho”
“Jambo gani Austin?
“Wakati tunapekua
kompyuta ya Tamar
tumekuta kuna video hizi”
akasema Austin na
kumchezea Dr Fabian video
moja kati ya mbili
walizozikuta katika
kompyuta ya Tamar.
“Stop it ! akafoka Dr
Fabian.Alikuwa anahema
haraka haraka
“Mr President can you
say something about
this?akauliza Austin
Dr Fabian akafikiri kwa
muda halafu akasema
“Kuna mwingine yeyoye
ambaye ameziona video hizi?
“Hapana ni sisi pekee”
akajibu Austin na Dr Fabian
akavuta pumzi ndefu
“Kwa miaka saa
nimekuwa nikiteseka kwa
ajili ya video hizi na nimelipa
gharama kubwa sana mpaka
sasa.Kuna nyakati
nilitamani hata nife
niondokane na adha
nilizokuwa nazipata kutoka
kwa Tamar kwa sababu ya
video hizi” akanyamaza na
kuchukua kitambaa akafuta
jasho usoni akainamisha
kichwa akazama mawazoni
“Mheshimia Rais naomba
unihakikishie je video hizi ni
za kweli na
zimetengenezwa?akauliza
Austin
“Video hizo ni za kweli
kabisa Austin.Unaowaona
ndani ya hiyo video ni mimi
na Tamar.Labda nikupe
picha tu kwamba mimi na
Tamar tulikuwa na
mahusiano ya kimapenzi
lakini yalikuwa ya
siri.Tamar alikuwa ndiye
mwanamke niliyepaswa
kumuoa lakini sikufanya
hivyo kutokana na tabia yake
ya kuwa na wanaume wengi
nikamuoa Millen.Mimi na
Tamar tuna mtoto mmoja wa
kiume anaishi na mama yake
mdogo nchini Hungary,hivyo
Tamar alikuwa sehemu ya
maisha yangu.Nilimjengea
jumba kubwa Afrika kusini
nikampa mahitaji yale yote
aliyohitaji lakini bado Tamar
hakuacha tabia yake ya
kutoka na wanaume wengine
japo kila mwisho wa wiki
nilikuwa nakwenda Afrika
kusini kwa ajili
yake.Niliweka watu wa
kumfuatilia na wakanitumia
picha zake akiwa na
wanaume tofauti ndani ya
nyumba niliyojenga
mimi.Nilikasirishwa na
kitendo hicho ndiyo maana
nikafanya vile
nilivyofanya.Ilikuwa ni
hasira tu” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais mimi
na wenzangu hatuna haja ya
kufahamu chochote wala
kuingilia maisha yako binafsi
lakini kuna kitu tumekiona
katika video hizi.Inaonekana
Tamar alitegemea kitendo
kile kutokea hivyo akatega
kamera mahala ambako
usingeweza kuiona na
akarekodi matukio
yale.Katika video zote mbili
baada ya wewe kuondoka
Tamar anaonekana akiinuka
na kwenda kuzima
kamera”akasema Austin
“Sijawahi kuona kipande
hicho.Mimi alinitumia
kipande kidogo na ndicho
ambacho amekuwa
akikitumia kunitisha
kwamba atakiachia
hadharani watu
wakione.Sikuwa tayari kwa
hilo ndiyo maana
nilimtimizia kila
alichokitaka” akasema Dr
Fabian na Austin
akamuonyesha mwisho wa
video zile Tamar akiinuka na
kwenda kuzima kamera.
“Shetani mkubwa Yule !
akasema kwa hasira
“Mheshimiwa Rais
unaweza kukubaliana nasi
kwamba Tamar alifanya vile
makusudi kabisa kwa
malengo anayoyajua yeye
mwenyewe?akauliza Austin
“Inaweza kuwa kweli
kwani toka alipopata video
hiyo amekuwa akinipa
vitisho vingi na mimi
sikutaka kupoteza heshima
yangu katika jamii ndiyo
maana nikawa tayari
kumtimizia kila
anachokihitaji”
“Uliwahi kumueleza nia
yako ya kuwania urais kabla
ya tukio hili
kutokea?akauliza Austin
“Austin tayari
umekwisha fahamu siri
zangu hivyo siwezi kukificha
kitu.Mimi nilianza
kuandaliwa kuwa Rais
miaka minne kabla ya rais
aliyepita kumaliza muda
wake.Mipango hii ilipoanza
nilimshirikisha pia
Tamar.Kujibu swali lako ni
kweli alifahamu kama
ninaandaliwa kwa nafasi ya
urais.Baada ya mimi kuwa
Rais ndipo alipoanza vituko
vyake kutaka nimtimizie kila
anachokihitaji kwa madai ya
kuachia video ile endapo
nisipomtimizia.Aliyekuwa
mkurugenzi wa SNSA
alifariki dunia nchini Afrika
kusini na Tamar alinitaka
nimteue yeye kuwa
mkurugenzi wa SNSA.Baada
ya kupitia taarifa zake za
kielimu na kuona ana vigezo
nikamteua kuwa mkurugenzi
mkuu wa SNSA” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais
napenda kukutoa hofu
kwamba sasa uko
salama.Kila kitu tunacho
mikononi mwetu na
hakutakuwa tena na kitisho
chochote kwako.Sisi tuko
kwa ajili yako.Tutakulinda
kama tulivyofanya”
“Ahsante sana
Austin.Ninajiona mjinga
sana kwa mambo niliyotaka
kukufanyia kumbe wewe
ndiye mkombozi
wangu.Tamar ndiye
aliyekuwa ananiongoza
kutaka nikupoteze na mimi
kwa ujinga wangu na kwa
kumuogopa nilitekekeleza
kila alichonitaka.Usiku ule
mlipokwenda nyumbani
kwake ni yeye aliyenipigia
simu na kunitaka niwatake
muondoke haraka sana
nyumbani kwake na mimi
nikafanya hivyo japo nilijua
lazima kuna jambo la
muhimu lililowapeleka
pale.Ni yeye aliyetengeneza
ule mtego ili uende pale
Dino’s hotel ukamatwe oh my
God ! akasema Dr Fanian na
kuinama akisikitika
“Mheshimiwa Rais hayo
yote yamebaki historia sasa
tunakwenda kuufungua
ukurasa mpya sisi na wewe”
akasema Austin na
kumtazama Dr Fabian
“Tumefanya kazi kubwa
mheshimiwa Rais
kuhakikisha unakuwa
salama lakini na sisi kuna
kitu tunakihitaji”
“Sema Austin mnahitaji
nini?
“Kwa sasa baada ya
Tamar ambaye ni
mkurugenzi wa SNSA
kufariki idara ile haina
mkurugenzi.Tunataka
umteue mtu kutoka katika
watu wangu kuwa
mkurugenzi wa SNSA”
akasema Austin akimkazia
macho Dr Fabia ambaye
alivuta pumzi ndefu na
ksuema
“Are you blackmailing me
Austin?! Akauliza Dr Fabian
“Hapana mheshimiwa
rais.Bado tuna kazi kubwa
ya kufanya.Bado hatari
haijakwisha.Bado vita
inaendelea .Kuna maswali
mengi ya kuyatafutia
majawabu.Tunahitaji kujua
nani waliomuua balozi
Benjamin?nani anamtumia
fedha Tamar?Dinosar ni
nani?Wana mipango gani
dhidi ya nchi yetu?Mwisho
tunahitaji kujua mtu ambaye
anatarajiwa kuingia nchini
hivi karibuni kutekeleza
awamu ya tatu ya mpango
wa Dinosaur na Tamar ni
nani?Tutaweza kuyapata
majibu hayo kama mmoja wa
watu wangu atakuwa
mkurugenzi wa SNSA.Idara
ile ni nyeti sana na kazi yake
ni kubwa kwa nchi inatakiwa
iongozwe na mtu muadilifu
sana lakini ilikuwa
imeshikwa na madalali wa
mebapari.Tunataka
kuirejesha heshima ya idara
hii” akasema Austin
“Austin sijui niseme nini
kwa hili jambo zito
ulilolizungumza.SNSA ni
idara nyeti kabisa ya
usalama wa nchi lakini
niliiweka mikononi mwa
makuwadi wa
wanyonyaji.Nataka wewe
uwe mkuu wa SNSA kama
itakupendeza” akasema
DrFabian
“Mheshimiwa Rais mimi
ni kiongozi wa kikosi
muhimu kabisa naomba
niendelee kubaki hapohapo
katika nafasi yangu lakini
kuna mtu ninampendekeza
kwako anaitwa Ruby Rafael
Magalla.Huyu ni mtanzania
mwenye uraia wa
Uingereza.Kwa sasa
anafanya kazi katika
mamlaka kuu ya
mawasiliano ya kiintelijensia
Uingereza.Ninamfahamu
Ruby nimewahi kufanya
naye kazi ni mtu mwenye
akili nyingi na ana uwezo
mkubwa sana wa kucheza na
kompyuta.Nina hakika
akiwekwa pale SNSA
atakuwa na msaada mkubwa
sana” akasema Austin
“Austin huna haja ya
kunielezea kwa undani
kuhusu huyo mtu
unayempendekeza.Ninakua
mini.Sina shaka na uzalendo
wako hata kidogo ninaamini
mtu huyo uliyempendekeza
anafaa kabisa.Mimi sina
shida yoyote ya kumteua
kuwa mkurugenzi wa
SNSA.Swali ni je yeye
mwenyewe yuko tayari?
Akauliza Dr Fabian
“Ruby anaipenda sana
Tanzania na si mara moja
amekuwa akija Tanzania
kushiriki katika misheni
mbali mbali toka wakati wa
Rais aliyepita”
“Real?
“Ndiyo mheshimiwa
Rais”
“Basi vizuri.Nipe
mawasiliano yake
nitazungumza naye mimi
mwenyewe na kumuomba aje
Tanzania.Nitamshawishi
kwa kila namna hadi
akubali” akasema Dr Fabian
“Nakushukuru sana
mheshimiwa Rais”
“Kama kuna kitu kingine
chochote nieleze tafadhali”
“Hakuna mheshimiwa
rais kilichonileta hapa kwako
ni hayo niliyokueleza”
“Austin najua
nimekukosea wewe na
wenzako.Najua haitakuwa
rahisi kuniamini tena lakini
naomba tusameheane kwa
yale yaliyotokea na tufungue
ukurasa mpya.Tuna vita
kubwa inatukabili mbele
yetu nahitaji watu kama
ninyi wazalendo wa kweli
kwa nchoi yenu ambao mko
tayari hata kuyatoa maisha
yenu kwa ajili ya Tanzania.”
“Sisi hatuna tatizo lolote
nawe mheshimiwa Rais
kikubwa tunachokitaka toka
kwako tuamini”
“Siwezi kurudia tena
makosa niliyoyafanya
Austin.Lakini nakuomba
hizo rekodi na hizo video
ziharibuni kabisa”
“Usihofu kuhusu hilo
mheshimiwa Rais.Zote
zitaharibiwa na hakutakuwa
na kitisho kingine chochote
dhidi yako” akasema Austin
na kuzifuta rekodi zile na
video mbele ya Rais
Austin na Dr Fabian
walimaliza mazungumzo yao
na kuagana Austin
akaondoka
RAMALLAH – PALESTINA
Mathew Mulumbi
alifumbua macho baada ya
kusikia sauti za watu
wakikimbia karibu na
dirisha la chumba
alimolala.Alitoka kitandani
akajinyoosha halafu akaenda
kufunua pazia akachungulia
nje.Mara mlago wake
ukagongwa akavaa shati na
kwenda kuufungua
akakutana na Ammar
“Abu Al zalawi” akasema
Ammar
“Ammar”
“Unaendeleaje Abu?
“Ninaendelea vizuri sana
Ammar”
“Nafurahi kusikia
hivyo.Abu naomba nikutoe
hofu kwa lile tukio la jana
halitajirudia tena.Wewe ni
mtu wetu wa muhimu sana
hivyo unastahili heshima
kubwa.Naomba utambue
kwamba mimi kama kiongozi
wa kikundi hiki ninakuamini
asilimia mia moja hivyo
usiwe na hofu yoyote”
akasema Ammar
“Ahsante sana Ammar
kwa kuniamini” akasema
Mathew
“Abu nimekuja kukuaga
ninatoka kidogo kuna
sehemu ninakwenda
kuangalia kazi za
zinavyokwenda,wewe
utaendelea kupumzika hapa
ukihudumiwa.Unatakiwa
upone kabisa mjeraha yako
yote na utakapokuwa
umepona kabisa tutaanza
kazi” akasema Ammar
“Ahsante sana
Ammar.Ninahudumiwa
vizuri sana hapa.Ninajihisi
nyumbani” akasema Mathew
na Ammar akatabasamu
“Abu sikufanya makosa
kuamua kuungana
nawe.Ninapata picha ya
kundi letu kuwa kubwa na
hatari baada ya kujiunga
kwetu” akasema Ammar
“Usijali Ammar
tutafanya mambo mengi
sana pamoja.Tuzidi kuomba
uzima” akasema Mathew.
“Majeraha yako
yanaendeleaje?akaliza
Ammar.Mathew akavua
shati na Ammar
akamtazama akasikitika
“Watu wale ni wanyama
sana.Atakuja Nawal
kukuganga,ana taaluma ya
uuguzi na amekuwa
akisaidia sana watu wangu
kila pale wanapopatwa na
majeraha” akasema Ammar
na kuondoka
Kupitia dirishani
Mathew aliweza kuona
msafara wa magari
ukiondoka akarejea
kitandani kukaa.
“Natakiwa kuwajulisha
Mossad kwamba tayari
nimekwisha jiunga na
kikundi cha Ammar brigades
lakini sijui namna ya
kuwasiliana nao” akawaza
Mathew na picha ya Peniela
mke wake ikamjia kichwani
“Peniela na wanangu
ndio wanaonipa nguvu ya
kuendelea kuvumilia mateso
hata pale ninapokuwa
nimekata tamaa
kabisa.Nitahakikisha
ninajitahidi kutoka salama
mahala hapa ili nikaungane
nao tena” akawaza Mathew
na kumkumbuka Ruby
“Sipati picha Ruby
atakuwa alilia machozi kiasi
gani alipopata taarifa
kwamba nimefariki
dunia.Yule mrembo
ananipenda kupindukia na
alikuwa tayari kuacha kila
kitu kwa ajili yangu.Alikuwa
tayari hata kuhama London
na kuishi Tanzania kwa ajili
yangu.Sikuwahi kumpa jibu
kama nimekubali ombi lake
la mimi na yeye kuwa
wapenzi nilitaka kumpa jibu
baada ya kurejea kutoka
kuwakomboa Olivia na
Coletha lakini kwa bahati
mbaya sikurejea.Hii itakuwa
ilimuumiza mno.Je tayari
amekwisha pata mwanaume
mwingine kama Peniela?Ni
miaka mitatu tu lakini tayari
Peniela amekwisha pata
mwanaume.Je alikubaliana
na taarifa kwamba
nimefariki dunia?Alikubali
vipi nimekufa bila kuiona
maiti yangu? Alijaribu hata
kidogo kuutafuta ukweli na
kujiridhisha kweli nimekufa?
Akajiuliza Mathew
“Anyway nisimlamu sana
haya yote yaliyotokea ni kwa
sababu yangu.Kama
ningejiweka mbali na hizi
kazi hivi sasa ningekuwa
nafurahi na familia
yangu.Vipi kuhusu
wenzangu akina Gosu
Gosu?Nao pia wamekubali
kweli nimefariki? Gosu Gosu
sikuwa naye usiku ule
hiv……” Mathew akatolewa
mawazoni baada ya mlango
kugongwa.Akaenda
kuufungua akakutana na
Nawal
“Habari za asubuhi Abu
Al zalawi” akasema Nawal
“Habari nzuri
Nawal,karibu” akasema
Mathew na kumkaribisha
Amar ndani.Alikuwa
amebeba sinia lililokuwa na
kifungua kinywa vile vile
alikuwa ni kikapu ambacho
kilikuwa na dawa
“Abu nimeelekezwa nije
kukuganga majeraha yako”
akasema Nawal.Mathew
akavua shati na Nawal
akastuka baada ya kuyaona
majeraha makubwa
mgongoni mwa Mathew
“Pole sana
Abu.Wamekuumiza sana”
akasema Nawal akaanza
kuyasafisha majeraha yale
“Abu kwa nini uko
hapa?akauliza Nawal wakati
akiendelea kumganga
Mathew
“Kwa nini unauliza hivyo
Nawal?
“Hauonekani kama ni
gaidi.Sura na tabia za
magaidi ninazifahamu lakini
wewe si mmoja
wao.Unatafuta nini
hapa?akauliza Nawal
“Nilimuua mkuu wa
Mossad afrika Mashariki na
majasusi wengine
wawili.Niko hapa
kupambana na Israel”
akasema Mathew
“Jina lako halisi ni
nani?akauliza Nawal
“Naitwa Abu Al zalawi”
akasema Mathew
“Jina lako si Abu Al
Zalawi,wala wewe si gaidi”
akasema Nawal
“Amini utakavyo Nawal
lakini mimi jina langu ni
hilo” akasema Mathew
Nawal akaacha kazi
aliyokuwa anaifanya
akaenda kukaa mbele ya
Mathew.Muda wote
walikuwa wakizungumza
kiarabu lakini mara Nawal
akabadili lugha wakaanza
kuzungumza kiingereza
“Your real name is
Mathew Mulumbi and not
Abu Zalawi.You are from
Tanzania and not from
Kenya.You are an agent and
not a terrorist(jina lako ni
Mathew Mulumbi na si Abu
Zalawi.Unatokea Tanzania
na si Kenya.Wewe ni jasusi
na si gaidi)” akasema
Nawal.Mathew alihisi tumbo
linaanza kuunguruma kwa
mstuko alioupata.Akahisi
kijacho kumtoka
GCHQ
LONDON – UINGEREZA
Ruby akiwa katika ofisi
yake akiendelea na
majukumu simu yake
ikaita.Zilikuwa ni namba
ngeni katika simu yake na
simu ile ilitokea Tanzania
“Ni nani huyu?akajiuliza
Ruby akiwa ameishikilia ile
simu akizitazama zile namba
“Anayefahamu namba hii
kutoka Tanzania ni Gosu
Gosu pekee.Kama ni yeye
kwa nini ananipigia muda
huu wakati
nilikwishamuonya asinipigie
wakati niko kazini?akajiuliza
Ruby akionekana
kukasirika.Simu ilikatika
ikaanza kuita tena akaipokea
“Hallow” akasema
“Hallow” ikasema sauti
ambayo Ruby hakuwa
akiifahamu haikuwa sauti ya
Gosu Gosu aliyokuwa
ameitegemea
“Nazungumza na nani?
Akauliza
“Naongea na Ruby Rafael
Magalla?
Ruby akastuka jina lake
lilipotajwa
“Ndiyo unazungumza na
Ruby.Wewe ni nani?Umepata
wapi namba zangu?akauliza
Ruby kwa sauti ya ukali
kidogo
“Naitwa Dr Fabian
Kelelo Rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania”
akasema Dr Fabian na Ruby
akabaki
anashangaa.Alistuka sana
“Hallow Ruby”
“Nimestuka kidogo
mheshimiwa Rais”
“Ruby samahani kwa
kukupigia simu hii bila
taarifa lakini nimelazimika
kukupigia kwa ajili ya jambo
moja la muhimu sana”
“Nakusikiliza
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby
“Ruby nimeamua
kukupigia simu mimi
mwenyewe kukujulisha
kwamba nimekuteua uwe
mkuu wa idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi
SNSA”
“What? Ruby akashangaa
“Ni kweli Ruby
nimekuchagua kuwa
mkurugenzi mkuu wa idara
ya siri ya usalama wa ndani
ya nchi”
Ruby akacheka kidogo na
kusema
“Mheshimiwa Rais sijui
niseme nini lakini nimestuka
sana.Kwanza sifahamu
umenifahamuje hadi
ukaniona ninafaa?Pili mimi
si raia wa Tanzania japo
wazazi wangu ni watanzania
ambao baadae walichukua
uraia wa Uingereza”
“Ruby tafadhali usiseme
hapana.Nimekuteua kwa
kuwa ninaamini unaweza
ukaiongoza idara hii kwa
ufanisi mkubwa.Sikuwa
ninakufahamu lakini
wenzako akina Austin
wamekupendekeza kwangu
kwamba unafaa kwa nafasi
hii”
“Umesema Austin?! Ruby
akashangaa
“Ndiyo.Ninamuamini
sana Austin.Aliponieleza
kuwa unafaa kuongoza idara
hii sikuwa na shaka nawe
hata kidogo.Ruby nchi yetu
kwa sasa iko katika vita
kubwa ya kiuchumi na
tunaitegemea sana idara hii
ambayo nataka
uiongoze.Ruby nafahamu
nimekustukiza jambo kama
hili ila naomba utafakari na
unipe majibu kama utakuwa
tayari”
“Mheshimiwa Rais
nashukuru.Naomba nipe
muda nitafakari halafu
nitakujibu” akasema Ruby
na kuagana na Rais
“Mstuko kama huu
nilioupata leo niliupata siku
ile nilipoambiwa kwamba
Mathew amefariki
dunia.Japo mstuko huu
hawezi kulingana na ule wa
taarifa ya kifo cha Mathew
lakini nimestuka sana.Rais
anataka niwe mkurugenzi
wa SNSA ! Dah hiki si kitu
kidogo.Idara ile ni kubwa
sana na inahitaji mtu
makini.Ni idara ambayo
aliiongoza Devotha ambaye
alitaka kuniua kwa
risasi.Siwezi kusahau
kitendo kile” akawaza
Ruby.Kazi zake zote
zilisimama alishindwa
kuendelea na kazi
“Lazima iko sababu
kubwa hadi Austin
anipendekeze kwa Rais niwe
mkurugenzi wa SNSA.Huu
ni mtihani mkubwa kwangu
kwani hata hapa
wananitegemea sana lakini
asili yangu ni Tanzania.Toka
ndani ya moyo wangu
ninaipenda Tanzania kwani
ndiko atokako Mathew
Mulumbi mwanaume
nimpendaye kuliko wote
ambaye mpaka leo hii bado
siamini kama kweli
amefariki dunia.Nadhani
nafasi hii imekuja kwa
kusudi maalum kwani
nikiwa mkurugenzi wa idara
ile nitafahamu mambo mengi
ya nchi,siri nyingi za nchi
nitazijua na nitapata nafasi
nzuri ya kuupata ukweli
kuhusu Mathew
Mulumbi.Sina haja ya
kukataa nafasi kama hii
wala kujiuliza mara mbili
kama nikubali au nikatae”
akawaza Ruby na kuchukua
simu akapiga namba zile za
Rais
“Ruby” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais sina
sababu ya kutafakari jambo
kama hili wakati nchi
inanihitaji.Japo kwa sasa ni
raia wa nchi nyingine lakini
Tanzania ni nyumbani na
nina mapenzi makubwa na
nchi yangu hivyo nimekubali
uteuzi”
“Ahsante sana
Ruby.Ahsante
sana.Nimefurahi mno.Nchi
inahitaji vijana kama
wewe.Lini utakuja Tanzania?
“Kwanza itanilazimu
kuanza mchakato wa kuacha
kazi hapa ninapofanya kazi”
akasema Ruby na
kunyamaza kidogo
“Mheshimiwa rais
halitakuwa jambo jepesi na
la haraka kuacha kazi hapa
kwani kazi ninayoifanya ni
nyeti sana lakini kwa namna
yoyote ile lazima nihakikishe
nimefanikiwa kuacha kazi
hapa.Ninachokuomba jambo
hili la uteuzi wangu liwe siri
lisitangazwe” akasema Ruby
“jambo hili ni la siri
kubwa na anayefahamu ni
Austin na wenzake na siwezi
kumweleza mtu yeyote.Ruby
nafasi hii hatapewa mtu
mwingine zaidi yako hivyo
basi kamilisha taratibu zako
uje nyumbani tunakusubiri”
akasema Dr Fabian na
kuagana na Ruby
USIKOSE SEHEMU
IJAYO……………..
 
Aya izo apo 8,9,&10, ivi kumbe kuweka story apa ni kazi kweli kweli, tuwe tunawashukuru sana na kuwavumilia wanaotuleteaga izi mambo asee ile mwanzo mwisho inaitaji moyo laana ukijumlishia na yale malawama yetu, big up to all'ya
Uko vizuri mzee.. sasa tunaomba 2,3,4,5,6 na 7 maana 8 mpaka 10 ushatupa. Tupe hivyo vipande vya nyuma mkuu

BACK TANGANYIKA
 
Aya izo apo 8,9,&10, ivi kumbe kuweka story apa ni kazi kweli kweli, tuwe tunawashukuru sana na kuwavumilia wanaotuleteaga izi mambo asee ile mwanzo mwisho inaitaji moyo laana ukijumlishia na yale malawama yetu, big up to all'ya

Kumbe mkuu Hii simulizi ni ndefu sana. Umetupa seasons 8 to 10. kumbe kuna season 3.4.5.6.7. sasa ndo tupo ya 3 tu. Hatari. Kama itawezekana Tunaomba at least hata 3 na nne. Ili tujivute. Please sir.
 
Kumbe mkuu Hii simulizi ni ndefu sana. Umetupa seasons 8 to 10. kumbe kuna season 3.4.5.6.7. sasa ndo tupo ya 3 tu. Hatari. Kama itawezekana Tunaomba at least hata 3 na nne. Ili tujivute. Please sir.
Kweli aisee nimeshindw hata kusoma maaan nitavurugikiwa
Mkuu tunakuombaa aisee
 
Tupe msaada mkuu wa season 2-3-4-5-6-7
Aya izo apo 8,9,&10, ivi kumbe kuweka story apa ni kazi kweli kweli, tuwe tunawashukuru sana na kuwavumilia wanaotuleteaga izi mambo asee ile mwanzo mwisho inaitaji moyo laana ukijumlishia na yale malawama yetu, big up to all'ya
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 3: EPISODE 12
Austin alifika ikulu
lakini Dr Fabian
hakuonyesha uchangamfu
kama ambavyo
huchangamka kila
anapokutana na Austin.Sura
yake ilija hasira.Baada ya
Austin kupokelewa Ikulu
waliingia katika chumba cha
mazungumzo ya faragha
kama wafanyavyo kila
Austin afikapo ikulu kwa
mazungumzo.
“Kabla hujanieleza kile
unachotaka kunieleza
naomba nikufahamishe
kwamba nimepokea taarifa
za kifo cha Tamar kwa
masikitiko makubwa na
nimeapa yeyote Yule
aliyehusika katika kifo hicho
nitamsaka hadi apatikane
awe mzima au
amekufa.Hakuna aliyeshiriki
atakayebaki salama !
akasema Dr Fabian kwa
ukali
“Mheshimiwa Rais
usitumie nguvu kubwa sana
kuongelea suala hilo au
kumtafuta muuaji wa Tamar
Axon wakati unaye mbele
yako”
“You?! Akauliza Dr
Fabian
“Yes me and my friends
we killed her”
“Jesus Chris ! akasema
Dr Fabian
“Dr Fabian naomba
kwanza unisikilize kile
ninachotaka kukwambia
halafu mwisho utaamua
kama unataka kunikamata
na kunifungulia mashtaka
au vinginevyo lakini kwanza
nisikilize” akasema
Austin.Dr Fabian hakujibu
chochote aliendelea
kumtazama kwa hasira
“Mheshimiwa Rais
ulitupa kazi mimi na
wenzangu ya kumuua Lucy
Muganza na tukaitekeleza
kazi hiyo vizuri lakini baadae
likaibuka tena suala la balozi
Benjamin nalo ukatukabidhi
sisi tumchunguze kwa bahati
mbaya akafariki wakati
uchunguzi
unaendelea.Mpaka sasa
hatujui nani walimuua balozi
Benjamin na kwa nini”
“Hamjui nani kamuua
balozi Benjamin?Mnadhani
mimi ni mtoto mdogo ambaye
nitashindwa kugundua
mchezo mlioufanya?Wewe na
wenzako mlimuua balozi
Benjamin” akasema Dr
Fabian
“Kwa nini tumuue mtu
ambaye ulitutuma
tumchunguze?akauliza
Austin na Dr Fabian akawa
kimya
“Mheshimiwa Rais
hatukumuua
Benjamin.Kama kuna mtu
amekueleza kwamba sisi
tulimuua
amekudanganya.Sikiliza
namna
ilivyokuwa.Tuligundua
kwamba balozi Benjamin
amealikwa katika hafla ya
uchangishaji fedha za
mabweni ya watoto waishio
kwenye mazingira magumu
na sisi kwa vile tulikwisha
anza kumfuatilia tulikuwepo
ukumbini.Benjamin alitoka
ukumbini akaenda katika
lifti na akiwa ndani ya lifti
mwanamke mmoja
alimuwekea bahasha katika
mfuko wake wa koti na mtu
wangu aliyekuwamo ndani
ya lifti akimfuatilia
Benjamin alikiona kitendo
hicho.Tulimuandama Yule
mwanamke tumjue ni nani
na amempa nini balozi
Benjamin kwa siri namna
ile.Tulifanikiwa kumpata
mwanamke huyo na baada
ya kumuhoji akadai yeye ni
mfanyakazi wa SNSA.Kazi
yake kubwa ni
mdukuaji.Alitueleza kwamba
kwa muda wa wiki kadhaa
amepewa kazi maalum ya
kudukua simu yako na
kuhifadhi mazungumzo yako
yote ya simu,hivyo
mheshimiwa Rais fahami
kila simu unayopiga au
kupigiwa inasikilizwa na
SNSA”
“Simu yangu
unadukuliwa? Dr Fabian
akahamaki
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Simu yako inadukuliwa
na SNSA”
Dr Fabian akasimama na
kushika kiuno.
“Mheshimiwa Rais
mawasiliano yako yote ya
kila siku hurekodiwa na
kisha huwekwa katika faili
maalum”
“SNSA hawawezi
kudukua simu ya Rais !
That’s a big lie ! akafoka Dr
Fabian
“Nisikilize kwanza
mheshimiwa Rais” akasema
Austin
“Mkurugenzi wa SNSA
Tamar Axon ndiye aliyetoa
maelekezo kwamba simu
yako idukuliwe”
“Tamar ! akazidi
kuhamaki Dr Fabian
“Tamar hawezi kabisa
kufanya kitu kama hicho !
akasema Dr Fabian
“Hiki si kitu cha kubuni
mheshimiwa Rais.Ni kweli
jambo hilo linafanyika na
aliyekuwa akifanya ndiye
aliyetueleza
kinachoendelea.Katika
kukusanya rekodi za
mawasiliano yako Agatha
aligundua uliwasiliana na
Rais Patrice Eyenga wa
Congo na mlikuwa
mnazungumzia kuhusu
mauaji ya Lucy
Muganza.Rekodi zako zote
ulizozungumza kuhusu
mauaji ya Lucy Muganza
Agatha alizificha
hakumuonyesha
Tamar.Agatha alipewa diski
mweko na Tamar ampelekee
balozi Benjamin na
alipokuwa njiani
aliichunguza kujua kuna nini
ndani akakuta kuna rekodi
mbili za mazungumzo yako
na Rais Patrice Eyenga
kuhusu mauaji ya Lucy
Muganza”
“Real?!! Akauliza Dr
Fabian Austin akatikisa
kichwa
“Tamar anaweza kweli
akanifanyia mambo kama
hayo? Dr Fabian akabaki
anashangaa
“Ni kweli mheshimiwa
Rais” akasema Austin
“Ni vigumu kuamini”
Austin akatoa diski
mfukoni akaichomeka katika
kompyuta na Rais akaanza
kusikiliza rekodi za
mazungumzo yake ya
simu.Austin akamchezea
rekodi mbili akizungumza na
Patrice Eyenga.
“Mheshimiwa Rais ziko
nyingi hizi ni mbili tu
nimekuchezea” akasema
Austin.
“A..A..AAAA…Austin I
don’t know what to say !
“Don’t say anything Mr
President.Siku ile
tulipokwenda nyumbani kwa
Tamar kufanya uchunguzi
ukatuzuia tulikuwa
tunatafuta faili lenye rekodi
hizi”
“Austin I’m sorry .I didn’t
know anything.Kwa nini
hukunieleza jambo kubwa
kama hili mapema?
“Nilitaka kukueleza
lakini hukunipa nafasi na
badala yake ukatengeneza
mtego ili nikamatwe na
SNSA”
“Austin…”akasema Dr
Fabian na kushindwa
kuendelea.Alikosa neno la
kusema
“Mheshimiwa Rais,Jana
usiku tumevamia nyumbani
kwa Tamar na kufanikiwa
kulipata faili lenye rekodi
zote tumezifuta na zilizobaki
ni hizi hapa” akasema Austin
na kumpatia Dr Fabian ile
diski mweko.Dr Fabian
akashusha pumzi
“Thank you Lord”
akasema na kuichukua ile
diski
“Una hakika hakuna
sehemu nyingine zilipo
rekodi hizi?
“Hakuna mheshimiwa
Rais.Tulipandikiza kirusi
katika mfumo wa kompyuta
wa SNSA na kuharibu kila
kitu rekodi zilikuwa
zimebaki katika kompyuta
ya Tamar”
“Good job
Austin.Ahsanteni sana wewe
na wenzako kwa kazi hii
kubwa mliyoifanya.Naomba
unisamehe sana kwa yale
niliyokufanyia”
“Mheshimiwa
Rais,Tamar alijiua mwenywe
kwa kujipiga
risasi.Tunaamini alikuwa
anashirikiana na balozi
Benjamin lakini mpaka sasa
hatujui nani waliomuua
balozi Benjamin na kwa
nini.Japokuwa wote wawili
wamefariki dunia lakini
hatari bado haijaisha.Kuna
mambo tumeyagundua
kwanza Tamar alikuwa
anapokea fedha kutoka
katika akaunti iliyoko
Ufarnsa ambayo mmiliki
wake amefichwa.Amekuwa
akipokea fedha nyingi
kupitia akaunti
hiyo.Tunatafuta kujua
mmilikiwa hiyo akaunti na
fedha hizo zote zina malengo
gani.Katika akaunti yake
tumekuta ana zaidi ya bilioni
mbili.Tumegundua pia
mawasiliano yake na mtu
anaoitwa Dinosaur.Bado
hatujafahamu mtu huyu
yuko wapi lakini barua pepe
tuliyoikuta katika kompyuta
ya Tamar inasomeka hivi”
akasema Austin na
kumuonyesha Rais barua
pepe waliyoikuta katika
kompyuta ya Tamar.Dr
Fabian akazidi
kuchanganyikiwa
“Ukisoma barua pepe hii
utagundua Tamar na huyo
Dinosaur wana mipango
mikubwa inayokwenda kwa
awamu na tayari awamu
mbili zimekamilika na sasa
wanaingia awamu ya tatu na
njiwa anayetaja hapa si
njiwa mnyama bali ni mtu
anategemewa kuwasili muda
wowote.Bado hatumjui ni
nani na anakuja kufanya
nini”
“Dah ! siamini macho
yangu.Tamar ?!! akasema Dr
Fabian
“Nilimuamini sana
kumbe ni chui.Umesema
anatumiwa fedha kutoka
akaunti iliyoko
Ufaransa,balozi Benjamin
pia anatokea Ufaransa,Lucy
na Laurent Muganza makazi
yao wote ni Ufaransa,Rais
wa umoja wa Ulaya anatokea
Ufaransa na hata ukiangalia
wale waliotuma jumbe katika
kurasa zao zao za twitter
Benjamin na Rais Michael
wote wanatoka Ufaransa.Leo
nimekuwa na malumbano
makubwa na Rais wa
Ufaransa kuhusu kifo cha
Benjamin.Ukiunganisha
haya yote unapata picha
kwamba mchezo huu
tunacheza na
Ufaransa.Ukijiuliza kwa nini
tucheze na Ufaransa?Jibu ni
rahisi jamhuri ya
kidemokrasia ya
Congo.Baada ya kuingia
madarakani Rais Patrice
Eyenga amekata mirija yote
ya mataifa makubwa
kunufaika kwa kuchota
rasilimali za Congo hasa
madini na sasa wanatafuta
namna ya kurudi.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
inazidi kuimarisha ukuta wa
kuzuia uchotwaji wa
rasilimali zake kwa kujiunga
na jumuiya ya Afrika
mashariki ndiyo maana
mataifa haya ambayo
yanataka kurejea Congo kwa
nguvu wanataka kuanza na
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika Mashariki halafu
waingie Congo.Kama Tamar
alikuwa na mahusiano na
balozi Benjamin basi ni wazi
anashirikiana pia na umoja
wa Ulaya na ndiye aliyekuwa
akimpatia balozi Benjamin
siri za nchi kwani SNSA ina
siri nyingi za nchi.Ukifuatilia
mtiririko wa mambo ulivyo
toka alipouawa Lucy
Muganza utaona kabisa
kwamba balozi Benjamin na
wenzake walihisi serikali ya
Tanzania inahusika na
mauaji yale hivyo wakawa
wanatafuta
ushahidi.Ninamshukuru
sana huyo ambaye alificha
rekodi za mazungumzo
yangu na Patrice
Eyenga.Alifanya jambo
kubwa na la kishujaa”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais hii ni
vita na ulipaswa kutuamini
vijana wako lakini ulituzuia
hatakuendelea na operesheni
yetu.Licha ya kutuzuia lakini
bado tumeendelea kuweka
hatarini maisha yetu na
kupambana hadi
tukafanikiwa kupata rekodi
hizo.You are safe now Mr
President” akasema Austin
“Austin nimeishiwa
maneno ya kusema.Mimi ni
rais wako lakini ninajiona
mjinga sana kwa mambo
niliyoyafanya.Kwa nini
nilishindwa kukuamini
Austin?Nisamehe sana
kijana wangu najua
nilichokif……….”
“Usijali mheshimiwa
Rais” Austin akamkatisha Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais kuna
jambo la mwisho”
“Jambo gani Austin?
“Wakati tunapekua
kompyuta ya Tamar
tumekuta kuna video hizi”
akasema Austin na
kumchezea Dr Fabian video
moja kati ya mbili
walizozikuta katika
kompyuta ya Tamar.
“Stop it ! akafoka Dr
Fabian.Alikuwa anahema
haraka haraka
“Mr President can you
say something about
this?akauliza Austin
Dr Fabian akafikiri kwa
muda halafu akasema
“Kuna mwingine yeyoye
ambaye ameziona video hizi?
“Hapana ni sisi pekee”
akajibu Austin na Dr Fabian
akavuta pumzi ndefu
“Kwa miaka saa
nimekuwa nikiteseka kwa
ajili ya video hizi na nimelipa
gharama kubwa sana mpaka
sasa.Kuna nyakati
nilitamani hata nife
niondokane na adha
nilizokuwa nazipata kutoka
kwa Tamar kwa sababu ya
video hizi” akanyamaza na
kuchukua kitambaa akafuta
jasho usoni akainamisha
kichwa akazama mawazoni
“Mheshimia Rais naomba
unihakikishie je video hizi ni
za kweli na
zimetengenezwa?akauliza
Austin
“Video hizo ni za kweli
kabisa Austin.Unaowaona
ndani ya hiyo video ni mimi
na Tamar.Labda nikupe
picha tu kwamba mimi na
Tamar tulikuwa na
mahusiano ya kimapenzi
lakini yalikuwa ya
siri.Tamar alikuwa ndiye
mwanamke niliyepaswa
kumuoa lakini sikufanya
hivyo kutokana na tabia yake
ya kuwa na wanaume wengi
nikamuoa Millen.Mimi na
Tamar tuna mtoto mmoja wa
kiume anaishi na mama yake
mdogo nchini Hungary,hivyo
Tamar alikuwa sehemu ya
maisha yangu.Nilimjengea
jumba kubwa Afrika kusini
nikampa mahitaji yale yote
aliyohitaji lakini bado Tamar
hakuacha tabia yake ya
kutoka na wanaume wengine
japo kila mwisho wa wiki
nilikuwa nakwenda Afrika
kusini kwa ajili
yake.Niliweka watu wa
kumfuatilia na wakanitumia
picha zake akiwa na
wanaume tofauti ndani ya
nyumba niliyojenga
mimi.Nilikasirishwa na
kitendo hicho ndiyo maana
nikafanya vile
nilivyofanya.Ilikuwa ni
hasira tu” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais mimi
na wenzangu hatuna haja ya
kufahamu chochote wala
kuingilia maisha yako binafsi
lakini kuna kitu tumekiona
katika video hizi.Inaonekana
Tamar alitegemea kitendo
kile kutokea hivyo akatega
kamera mahala ambako
usingeweza kuiona na
akarekodi matukio
yale.Katika video zote mbili
baada ya wewe kuondoka
Tamar anaonekana akiinuka
na kwenda kuzima
kamera”akasema Austin
“Sijawahi kuona kipande
hicho.Mimi alinitumia
kipande kidogo na ndicho
ambacho amekuwa
akikitumia kunitisha
kwamba atakiachia
hadharani watu
wakione.Sikuwa tayari kwa
hilo ndiyo maana
nilimtimizia kila
alichokitaka” akasema Dr
Fabian na Austin
akamuonyesha mwisho wa
video zile Tamar akiinuka na
kwenda kuzima kamera.
“Shetani mkubwa Yule !
akasema kwa hasira
“Mheshimiwa Rais
unaweza kukubaliana nasi
kwamba Tamar alifanya vile
makusudi kabisa kwa
malengo anayoyajua yeye
mwenyewe?akauliza Austin
“Inaweza kuwa kweli
kwani toka alipopata video
hiyo amekuwa akinipa
vitisho vingi na mimi
sikutaka kupoteza heshima
yangu katika jamii ndiyo
maana nikawa tayari
kumtimizia kila
anachokihitaji”
“Uliwahi kumueleza nia
yako ya kuwania urais kabla
ya tukio hili
kutokea?akauliza Austin
“Austin tayari
umekwisha fahamu siri
zangu hivyo siwezi kukificha
kitu.Mimi nilianza
kuandaliwa kuwa Rais
miaka minne kabla ya rais
aliyepita kumaliza muda
wake.Mipango hii ilipoanza
nilimshirikisha pia
Tamar.Kujibu swali lako ni
kweli alifahamu kama
ninaandaliwa kwa nafasi ya
urais.Baada ya mimi kuwa
Rais ndipo alipoanza vituko
vyake kutaka nimtimizie kila
anachokihitaji kwa madai ya
kuachia video ile endapo
nisipomtimizia.Aliyekuwa
mkurugenzi wa SNSA
alifariki dunia nchini Afrika
kusini na Tamar alinitaka
nimteue yeye kuwa
mkurugenzi wa SNSA.Baada
ya kupitia taarifa zake za
kielimu na kuona ana vigezo
nikamteua kuwa mkurugenzi
mkuu wa SNSA” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais
napenda kukutoa hofu
kwamba sasa uko
salama.Kila kitu tunacho
mikononi mwetu na
hakutakuwa tena na kitisho
chochote kwako.Sisi tuko
kwa ajili yako.Tutakulinda
kama tulivyofanya”
“Ahsante sana
Austin.Ninajiona mjinga
sana kwa mambo niliyotaka
kukufanyia kumbe wewe
ndiye mkombozi
wangu.Tamar ndiye
aliyekuwa ananiongoza
kutaka nikupoteze na mimi
kwa ujinga wangu na kwa
kumuogopa nilitekekeleza
kila alichonitaka.Usiku ule
mlipokwenda nyumbani
kwake ni yeye aliyenipigia
simu na kunitaka niwatake
muondoke haraka sana
nyumbani kwake na mimi
nikafanya hivyo japo nilijua
lazima kuna jambo la
muhimu lililowapeleka
pale.Ni yeye aliyetengeneza
ule mtego ili uende pale
Dino’s hotel ukamatwe oh my
God ! akasema Dr Fanian na
kuinama akisikitika
“Mheshimiwa Rais hayo
yote yamebaki historia sasa
tunakwenda kuufungua
ukurasa mpya sisi na wewe”
akasema Austin na
kumtazama Dr Fabian
“Tumefanya kazi kubwa
mheshimiwa Rais
kuhakikisha unakuwa
salama lakini na sisi kuna
kitu tunakihitaji”
“Sema Austin mnahitaji
nini?
“Kwa sasa baada ya
Tamar ambaye ni
mkurugenzi wa SNSA
kufariki idara ile haina
mkurugenzi.Tunataka
umteue mtu kutoka katika
watu wangu kuwa
mkurugenzi wa SNSA”
akasema Austin akimkazia
macho Dr Fabia ambaye
alivuta pumzi ndefu na
ksuema
“Are you blackmailing me
Austin?! Akauliza Dr Fabian
“Hapana mheshimiwa
rais.Bado tuna kazi kubwa
ya kufanya.Bado hatari
haijakwisha.Bado vita
inaendelea .Kuna maswali
mengi ya kuyatafutia
majawabu.Tunahitaji kujua
nani waliomuua balozi
Benjamin?nani anamtumia
fedha Tamar?Dinosar ni
nani?Wana mipango gani
dhidi ya nchi yetu?Mwisho
tunahitaji kujua mtu ambaye
anatarajiwa kuingia nchini
hivi karibuni kutekeleza
awamu ya tatu ya mpango
wa Dinosaur na Tamar ni
nani?Tutaweza kuyapata
majibu hayo kama mmoja wa
watu wangu atakuwa
mkurugenzi wa SNSA.Idara
ile ni nyeti sana na kazi yake
ni kubwa kwa nchi inatakiwa
iongozwe na mtu muadilifu
sana lakini ilikuwa
imeshikwa na madalali wa
mebapari.Tunataka
kuirejesha heshima ya idara
hii” akasema Austin
“Austin sijui niseme nini
kwa hili jambo zito
ulilolizungumza.SNSA ni
idara nyeti kabisa ya
usalama wa nchi lakini
niliiweka mikononi mwa
makuwadi wa
wanyonyaji.Nataka wewe
uwe mkuu wa SNSA kama
itakupendeza” akasema
DrFabian
“Mheshimiwa Rais mimi
ni kiongozi wa kikosi
muhimu kabisa naomba
niendelee kubaki hapohapo
katika nafasi yangu lakini
kuna mtu ninampendekeza
kwako anaitwa Ruby Rafael
Magalla.Huyu ni mtanzania
mwenye uraia wa
Uingereza.Kwa sasa
anafanya kazi katika
mamlaka kuu ya
mawasiliano ya kiintelijensia
Uingereza.Ninamfahamu
Ruby nimewahi kufanya
naye kazi ni mtu mwenye
akili nyingi na ana uwezo
mkubwa sana wa kucheza na
kompyuta.Nina hakika
akiwekwa pale SNSA
atakuwa na msaada mkubwa
sana” akasema Austin
“Austin huna haja ya
kunielezea kwa undani
kuhusu huyo mtu
unayempendekeza.Ninakua
mini.Sina shaka na uzalendo
wako hata kidogo ninaamini
mtu huyo uliyempendekeza
anafaa kabisa.Mimi sina
shida yoyote ya kumteua
kuwa mkurugenzi wa
SNSA.Swali ni je yeye
mwenyewe yuko tayari?
Akauliza Dr Fabian
“Ruby anaipenda sana
Tanzania na si mara moja
amekuwa akija Tanzania
kushiriki katika misheni
mbali mbali toka wakati wa
Rais aliyepita”
“Real?
“Ndiyo mheshimiwa
Rais”
“Basi vizuri.Nipe
mawasiliano yake
nitazungumza naye mimi
mwenyewe na kumuomba aje
Tanzania.Nitamshawishi
kwa kila namna hadi
akubali” akasema Dr Fabian
“Nakushukuru sana
mheshimiwa Rais”
“Kama kuna kitu kingine
chochote nieleze tafadhali”
“Hakuna mheshimiwa
rais kilichonileta hapa kwako
ni hayo niliyokueleza”
“Austin najua
nimekukosea wewe na
wenzako.Najua haitakuwa
rahisi kuniamini tena lakini
naomba tusameheane kwa
yale yaliyotokea na tufungue
ukurasa mpya.Tuna vita
kubwa inatukabili mbele
yetu nahitaji watu kama
ninyi wazalendo wa kweli
kwa nchoi yenu ambao mko
tayari hata kuyatoa maisha
yenu kwa ajili ya Tanzania.”
“Sisi hatuna tatizo lolote
nawe mheshimiwa Rais
kikubwa tunachokitaka toka
kwako tuamini”
“Siwezi kurudia tena
makosa niliyoyafanya
Austin.Lakini nakuomba
hizo rekodi na hizo video
ziharibuni kabisa”
“Usihofu kuhusu hilo
mheshimiwa Rais.Zote
zitaharibiwa na hakutakuwa
na kitisho kingine chochote
dhidi yako” akasema Austin
na kuzifuta rekodi zile na
video mbele ya Rais
Austin na Dr Fabian
walimaliza mazungumzo yao
na kuagana Austin
akaondoka
RAMALLAH – PALESTINA
Mathew Mulumbi
alifumbua macho baada ya
kusikia sauti za watu
wakikimbia karibu na
dirisha la chumba
alimolala.Alitoka kitandani
akajinyoosha halafu akaenda
kufunua pazia akachungulia
nje.Mara mlago wake
ukagongwa akavaa shati na
kwenda kuufungua
akakutana na Ammar
“Abu Al zalawi” akasema
Ammar
“Ammar”
“Unaendeleaje Abu?
“Ninaendelea vizuri sana
Ammar”
“Nafurahi kusikia
hivyo.Abu naomba nikutoe
hofu kwa lile tukio la jana
halitajirudia tena.Wewe ni
mtu wetu wa muhimu sana
hivyo unastahili heshima
kubwa.Naomba utambue
kwamba mimi kama kiongozi
wa kikundi hiki ninakuamini
asilimia mia moja hivyo
usiwe na hofu yoyote”
akasema Ammar
“Ahsante sana Ammar
kwa kuniamini” akasema
Mathew
“Abu nimekuja kukuaga
ninatoka kidogo kuna
sehemu ninakwenda
kuangalia kazi za
zinavyokwenda,wewe
utaendelea kupumzika hapa
ukihudumiwa.Unatakiwa
upone kabisa mjeraha yako
yote na utakapokuwa
umepona kabisa tutaanza
kazi” akasema Ammar
“Ahsante sana
Ammar.Ninahudumiwa
vizuri sana hapa.Ninajihisi
nyumbani” akasema Mathew
na Ammar akatabasamu
“Abu sikufanya makosa
kuamua kuungana
nawe.Ninapata picha ya
kundi letu kuwa kubwa na
hatari baada ya kujiunga
kwetu” akasema Ammar
“Usijali Ammar
tutafanya mambo mengi
sana pamoja.Tuzidi kuomba
uzima” akasema Mathew.
“Majeraha yako
yanaendeleaje?akaliza
Ammar.Mathew akavua
shati na Ammar
akamtazama akasikitika
“Watu wale ni wanyama
sana.Atakuja Nawal
kukuganga,ana taaluma ya
uuguzi na amekuwa
akisaidia sana watu wangu
kila pale wanapopatwa na
majeraha” akasema Ammar
na kuondoka
Kupitia dirishani
Mathew aliweza kuona
msafara wa magari
ukiondoka akarejea
kitandani kukaa.
“Natakiwa kuwajulisha
Mossad kwamba tayari
nimekwisha jiunga na
kikundi cha Ammar brigades
lakini sijui namna ya
kuwasiliana nao” akawaza
Mathew na picha ya Peniela
mke wake ikamjia kichwani
“Peniela na wanangu
ndio wanaonipa nguvu ya
kuendelea kuvumilia mateso
hata pale ninapokuwa
nimekata tamaa
kabisa.Nitahakikisha
ninajitahidi kutoka salama
mahala hapa ili nikaungane
nao tena” akawaza Mathew
na kumkumbuka Ruby
“Sipati picha Ruby
atakuwa alilia machozi kiasi
gani alipopata taarifa
kwamba nimefariki
dunia.Yule mrembo
ananipenda kupindukia na
alikuwa tayari kuacha kila
kitu kwa ajili yangu.Alikuwa
tayari hata kuhama London
na kuishi Tanzania kwa ajili
yangu.Sikuwahi kumpa jibu
kama nimekubali ombi lake
la mimi na yeye kuwa
wapenzi nilitaka kumpa jibu
baada ya kurejea kutoka
kuwakomboa Olivia na
Coletha lakini kwa bahati
mbaya sikurejea.Hii itakuwa
ilimuumiza mno.Je tayari
amekwisha pata mwanaume
mwingine kama Peniela?Ni
miaka mitatu tu lakini tayari
Peniela amekwisha pata
mwanaume.Je alikubaliana
na taarifa kwamba
nimefariki dunia?Alikubali
vipi nimekufa bila kuiona
maiti yangu? Alijaribu hata
kidogo kuutafuta ukweli na
kujiridhisha kweli nimekufa?
Akajiuliza Mathew
“Anyway nisimlamu sana
haya yote yaliyotokea ni kwa
sababu yangu.Kama
ningejiweka mbali na hizi
kazi hivi sasa ningekuwa
nafurahi na familia
yangu.Vipi kuhusu
wenzangu akina Gosu
Gosu?Nao pia wamekubali
kweli nimefariki? Gosu Gosu
sikuwa naye usiku ule
hiv……” Mathew akatolewa
mawazoni baada ya mlango
kugongwa.Akaenda
kuufungua akakutana na
Nawal
“Habari za asubuhi Abu
Al zalawi” akasema Nawal
“Habari nzuri
Nawal,karibu” akasema
Mathew na kumkaribisha
Amar ndani.Alikuwa
amebeba sinia lililokuwa na
kifungua kinywa vile vile
alikuwa ni kikapu ambacho
kilikuwa na dawa
“Abu nimeelekezwa nije
kukuganga majeraha yako”
akasema Nawal.Mathew
akavua shati na Nawal
akastuka baada ya kuyaona
majeraha makubwa
mgongoni mwa Mathew
“Pole sana
Abu.Wamekuumiza sana”
akasema Nawal akaanza
kuyasafisha majeraha yale
“Abu kwa nini uko
hapa?akauliza Nawal wakati
akiendelea kumganga
Mathew
“Kwa nini unauliza hivyo
Nawal?
“Hauonekani kama ni
gaidi.Sura na tabia za
magaidi ninazifahamu lakini
wewe si mmoja
wao.Unatafuta nini
hapa?akauliza Nawal
“Nilimuua mkuu wa
Mossad afrika Mashariki na
majasusi wengine
wawili.Niko hapa
kupambana na Israel”
akasema Mathew
“Jina lako halisi ni
nani?akauliza Nawal
“Naitwa Abu Al zalawi”
akasema Mathew
“Jina lako si Abu Al
Zalawi,wala wewe si gaidi”
akasema Nawal
“Amini utakavyo Nawal
lakini mimi jina langu ni
hilo” akasema Mathew
Nawal akaacha kazi
aliyokuwa anaifanya
akaenda kukaa mbele ya
Mathew.Muda wote
walikuwa wakizungumza
kiarabu lakini mara Nawal
akabadili lugha wakaanza
kuzungumza kiingereza
“Your real name is
Mathew Mulumbi and not
Abu Zalawi.You are from
Tanzania and not from
Kenya.You are an agent and
not a terrorist(jina lako ni
Mathew Mulumbi na si Abu
Zalawi.Unatokea Tanzania
na si Kenya.Wewe ni jasusi
na si gaidi)” akasema
Nawal.Mathew alihisi tumbo
linaanza kuunguruma kwa
mstuko alioupata.Akahisi
kijacho kumtoka
GCHQ
LONDON – UINGEREZA
Ruby akiwa katika ofisi
yake akiendelea na
majukumu simu yake
ikaita.Zilikuwa ni namba
ngeni katika simu yake na
simu ile ilitokea Tanzania
“Ni nani huyu?akajiuliza
Ruby akiwa ameishikilia ile
simu akizitazama zile namba
“Anayefahamu namba hii
kutoka Tanzania ni Gosu
Gosu pekee.Kama ni yeye
kwa nini ananipigia muda
huu wakati
nilikwishamuonya asinipigie
wakati niko kazini?akajiuliza
Ruby akionekana
kukasirika.Simu ilikatika
ikaanza kuita tena akaipokea
“Hallow” akasema
“Hallow” ikasema sauti
ambayo Ruby hakuwa
akiifahamu haikuwa sauti ya
Gosu Gosu aliyokuwa
ameitegemea
“Nazungumza na nani?
Akauliza
“Naongea na Ruby Rafael
Magalla?
Ruby akastuka jina lake
lilipotajwa
“Ndiyo unazungumza na
Ruby.Wewe ni nani?Umepata
wapi namba zangu?akauliza
Ruby kwa sauti ya ukali
kidogo
“Naitwa Dr Fabian
Kelelo Rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania”
akasema Dr Fabian na Ruby
akabaki
anashangaa.Alistuka sana
“Hallow Ruby”
“Nimestuka kidogo
mheshimiwa Rais”
“Ruby samahani kwa
kukupigia simu hii bila
taarifa lakini nimelazimika
kukupigia kwa ajili ya jambo
moja la muhimu sana”
“Nakusikiliza
mheshimiwa Rais” akasema
Ruby
“Ruby nimeamua
kukupigia simu mimi
mwenyewe kukujulisha
kwamba nimekuteua uwe
mkuu wa idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi
SNSA”
“What? Ruby akashangaa
“Ni kweli Ruby
nimekuchagua kuwa
mkurugenzi mkuu wa idara
ya siri ya usalama wa ndani
ya nchi”
Ruby akacheka kidogo na
kusema
“Mheshimiwa Rais sijui
niseme nini lakini nimestuka
sana.Kwanza sifahamu
umenifahamuje hadi
ukaniona ninafaa?Pili mimi
si raia wa Tanzania japo
wazazi wangu ni watanzania
ambao baadae walichukua
uraia wa Uingereza”
“Ruby tafadhali usiseme
hapana.Nimekuteua kwa
kuwa ninaamini unaweza
ukaiongoza idara hii kwa
ufanisi mkubwa.Sikuwa
ninakufahamu lakini
wenzako akina Austin
wamekupendekeza kwangu
kwamba unafaa kwa nafasi
hii”
“Umesema Austin?! Ruby
akashangaa
“Ndiyo.Ninamuamini
sana Austin.Aliponieleza
kuwa unafaa kuongoza idara
hii sikuwa na shaka nawe
hata kidogo.Ruby nchi yetu
kwa sasa iko katika vita
kubwa ya kiuchumi na
tunaitegemea sana idara hii
ambayo nataka
uiongoze.Ruby nafahamu
nimekustukiza jambo kama
hili ila naomba utafakari na
unipe majibu kama utakuwa
tayari”
“Mheshimiwa Rais
nashukuru.Naomba nipe
muda nitafakari halafu
nitakujibu” akasema Ruby
na kuagana na Rais
“Mstuko kama huu
nilioupata leo niliupata siku
ile nilipoambiwa kwamba
Mathew amefariki
dunia.Japo mstuko huu
hawezi kulingana na ule wa
taarifa ya kifo cha Mathew
lakini nimestuka sana.Rais
anataka niwe mkurugenzi
wa SNSA ! Dah hiki si kitu
kidogo.Idara ile ni kubwa
sana na inahitaji mtu
makini.Ni idara ambayo
aliiongoza Devotha ambaye
alitaka kuniua kwa
risasi.Siwezi kusahau
kitendo kile” akawaza
Ruby.Kazi zake zote
zilisimama alishindwa
kuendelea na kazi
“Lazima iko sababu
kubwa hadi Austin
anipendekeze kwa Rais niwe
mkurugenzi wa SNSA.Huu
ni mtihani mkubwa kwangu
kwani hata hapa
wananitegemea sana lakini
asili yangu ni Tanzania.Toka
ndani ya moyo wangu
ninaipenda Tanzania kwani
ndiko atokako Mathew
Mulumbi mwanaume
nimpendaye kuliko wote
ambaye mpaka leo hii bado
siamini kama kweli
amefariki dunia.Nadhani
nafasi hii imekuja kwa
kusudi maalum kwani
nikiwa mkurugenzi wa idara
ile nitafahamu mambo mengi
ya nchi,siri nyingi za nchi
nitazijua na nitapata nafasi
nzuri ya kuupata ukweli
kuhusu Mathew
Mulumbi.Sina haja ya
kukataa nafasi kama hii
wala kujiuliza mara mbili
kama nikubali au nikatae”
akawaza Ruby na kuchukua
simu akapiga namba zile za
Rais
“Ruby” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais sina
sababu ya kutafakari jambo
kama hili wakati nchi
inanihitaji.Japo kwa sasa ni
raia wa nchi nyingine lakini
Tanzania ni nyumbani na
nina mapenzi makubwa na
nchi yangu hivyo nimekubali
uteuzi”
“Ahsante sana
Ruby.Ahsante
sana.Nimefurahi mno.Nchi
inahitaji vijana kama
wewe.Lini utakuja Tanzania?
“Kwanza itanilazimu
kuanza mchakato wa kuacha
kazi hapa ninapofanya kazi”
akasema Ruby na
kunyamaza kidogo
“Mheshimiwa rais
halitakuwa jambo jepesi na
la haraka kuacha kazi hapa
kwani kazi ninayoifanya ni
nyeti sana lakini kwa namna
yoyote ile lazima nihakikishe
nimefanikiwa kuacha kazi
hapa.Ninachokuomba jambo
hili la uteuzi wangu liwe siri
lisitangazwe” akasema Ruby
“jambo hili ni la siri
kubwa na anayefahamu ni
Austin na wenzake na siwezi
kumweleza mtu yeyote.Ruby
nafasi hii hatapewa mtu
mwingine zaidi yako hivyo
basi kamilisha taratibu zako
uje nyumbani tunakusubiri”
akasema Dr Fabian na
kuagana na Ruby
USIKOSE SEHEMU
IJAYO……………..

Mkombozi wetu ni huyu bwana mbududa. Tunamtakie yote mema
 
Hii kitu ni noma Sana aisee, hutamani kuiacha ukianza kusoma!!!
 
mkuu mbududa asante sana kwa riwaya hii hebu tupia ya weekend hii
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 1
RAMALLAH – PALESTINA
Mathew aliendelea
kumtazama Nawal kwa
mshangao alishindwa
amwambie kitu gani.Maneno
aliyoambiwa yalimstua
sana.Kwa ndani alihisi
kutetema.Nawal alilitambua
hilo
“Usihofu Abu
Zalawi,hakuna
anayelifahamu hilo zaidi
yangu” akasema Nawal huku
akitabasamu
“Kwa nini uko
hapa?akauliza Nawal
“Huyu mwanamke
amenifahamuje.Tayari kila
kitu kimeharibika. ?
Sikutegemea kufahamika
mapema namna hii” akawaza
Mathew
“Mathew nakuuliza kwa
nini uko hapa?Unatafuta
nini?akauliza Nawal
“Nawal naomba iwe
mwanzo na mwisho kuniita
kwa jina hilo mimi si
Mathew Mulumbi bali ni Abu
Al Zalawi” akasema Mathew
kwa sauti ndogo lakini ya
ukali
“Abu usihofu sintakuita
kwa jina hilo lakini
ninafahamu hilo si jina lako
na wewe ni Mathew
Mulumbi jasusi kutoka
Tanzania.Ninataka
kukusaidia hivyo ninataka
kujua nini kimekuleta
hapa?akauliza Nawal
Mathew akawa kimya
“Abu ninakuuliza hivyo
kwa sababu yawezekana
umekuja mahala ambako si
sahihi na unaweza ukapoteza
hata maisha yako.Hii ni
sehemu hatari sana na hawa
jamaa wakigundua kwamba
wewe si mwenzao bali uko
hapa kwa misheni maalum
watakuua.Nataka nikusaidie
ili uweze kufanikisha
misheni yako lakini
nitakusaidia endapo
utanieleza ukweli” akasema
Nawal na kuzidi
kumchanganya Mathew
“Nahisi hawa jamaa
tayari wamekwisha
nifahamu na wanamtumia
Nawal ili kujiridhisha
kwamba kweli mimi ni jasusi
kutoka Tanzania na si gaidi
mwenzao kama
nilivyojitambulisha
kwao.Napaswa kuwa makini
sana na mtego huu
vinginevyo nitaangamia
kabla ya kukamilisha
misheni yangu” akawaza
Mathew
“Mathew mbona
hunijibu?akauliza Nawal
“Nawal najua
wamekutuma uje
kunichunguza kama kweli
mimi ni jasusi lakini
wamekosea sana.Mimi si
huyo mtu unayemtaja
Mathew Mulumbi.Mimi ni
Abu Al Zalawi.Tafuta taarifa
zangu katika mtandao wa
Mossad utazipata” akasema
Mathew
“Mathew oh samahani
Abu” akasema Nawal na
Mathew akakasirika
akamkaba shingo
“Nitakuua Nawal kama
ukiendelea kuniita kwa jina
hilo ! akasema Mathew
akiwa amekasirika Nawal
akaogopa
“Nani amekutuma uje
unichunguze?akauliza
Mathew na kumuachia
Nawal ambaye alianza
kukohoa
“Ammar amekutuma uje
unipeleleze? Akauliza tena
“Hakuna aliyenituma
kwako.Sikiliza nikueleze
ukweli” akasema Nawal na
kukohoa kidogo halafu
akafungua mlango
akachungulia kama kuna
mtu karibu akaenda
kuangalia pia dirishani
halafu akasema
“Mimi ninafanya kazi na
shirika la ujasusi la
Marekani CIA”
“CIA ? Mathew
akashangaa
“Ndiyo.Niko katika
kitengo cha D.U.A”
“D.U.A ni nini”akauliza
Mathew
“Deep undercover agent”
“Oh my God !! akasema
Mathew
“Niko hapa kwa misheni
maalum ya kumtafuta mtu
mmoja anaitwa Abdul Yasin
Al Nasser.Huyu ni gaidi
ambaye anahusika katika
mashambulio manne
makubwa ya kigaidi
yaliyotokea katika miji
miwili nchini Marekani na
kuua watu zaidi ya mia moja
na hamsini.Abdul Yasin ni
ndugu na Ammar ndiyo
maana niko hapa”akasema
Nawal na kumuacha Mathew
katika mshangao .Baada ya
dakika moja akaendelea
“Mimi ndiye
niliyewasaidia Mossad
wakaweza kumpata Ammar
kupitia kwa
CIA.Nilipoelezwa kwamba
wewe ndiye uliyemsaidia
Ammar akaweza kutoka
gerezani sikuamini taarifa
hizo kwani gereza alilokuwa
amefungwa Ammar lina
ulinzi mkali mno na
hajawahi kutoroka mfungwa
yeyote na ndipo nilipoanza
kukuchunguza nikagundua
kwamba wewe si gaidi kama
inavyotajwa bali ni jasusi na
nikajua kwamba kutoroka
gerezani ulikuwa ni mpango
maalum” akasema
Nawal.Akatoka na kwenda
kufungua mlango
akachungulia nje kama kuna
mtu pale karibu
“Lazima nichukue
tahadhari kwani hakuna
anayeifahamu siri hii hadi
sasa.Nimekwambia wewe
kwa sababu ninataka
kukusaidia” akasema Nawal
na kumtazama Mathew
“Baada ya kukueleza siri
yangu kubwa sasa ni zamu
yako.Nataka unieleze kwa
nini uko hapa? Akauliza
Nawal
Mathew akatafakari
kidogo halafu akasema
“Mimi niko hapa kwa
ajili ya kushirikiana na
Ammar kupambana na
Israel”
“Abu unaniudhi sana
unapoukwepa
ukweli.Nimekueleza siri
yangu kubwa kwa nini
hutaki kuniamini?Usihofu
tafadhali hakuna
atakayefahamu siri
hii”akasema Nawal
“Kwa nini unataka
kufahamu kilichonileta
hapa?akauliza Mathew
“Kwa sababu nataka
nikusaidie uweze kumaliza
misheni yako uondoke
.Uwepo wako hapa unaweza
ukasababisha misheni
yangu kuharibika kwani
hawa jamaa wanaweza
wakakugundua kabla
hujatekeleza misheni yako
hivyo lengo langu ni kukupa
msaada “ akasema Nawal
“Huu ni mtihani mgumu
sana.Nashindwa kufanya
maamuzi je huyu mwanamke
anachokiongea ni kitu cha
kweli au ni mtego?Ni vipi
kama nikikubali mimi ni
Mathew Mulumbi halafu
kumbe ametumwa aje
anichunguze?Nitakuwa
nimeharibu kila kitu na
sintatoka hapa
salama.Lakini ni vipi kama
ni kweli haya anayoniambia
halafu nikakataa
kushirikiana naye?Kama ni
kweli huyu mwanamke ni
CIA anaweza akawa na
msaada mkubwa sana
kwangu” akawaza Mathew
na kumtazama Nawal kwa
makini
“Ngoja nicheze kamari
nijaribu kumuamini na kama
kutatokea tatizo lolote
nitakabiliana nalo” akawaza
na kukohoa kidogo akasema
“Ni kweli.Mimi ni
Mathew Mulumbi jasusi
kutoka Tanzania na niko
hapa kwa ajili ya misheni
maalum.Ninamtafuta Habiba
Jawad”
“Habiba Jawad?Nawal
akashangaa
“Ndiyo ninamtafuta
Habiba Jawad na ndiyo
maana niko
hapa.Unamfahamu?
“Kwa nini
unamtafuta.Kwa nini
umetumia njia ya hatari
namna hii hadi ukafika
hapa?akauliza Nawal
“Miaka mitatu iliyopita
kulifanyika shambulio la
kigaidi nchini Tanzania
lililofanywa na kundi la
kigaidi la IS.Wakati wa
kulichunguza suala hilo
tukagundua kwamba kundi
hilo la IS linafadhiliwa na
Habiba Jawad na kwa sasa
kundi hilo limejielekeza
katika kujitanua barani
Afrika.Habiba Jawad
kutokana na utajiri wake
amekuwa ndiye uti wa
mgongo wa makundi mengi
ya kigaidi na hata kundi hili
la Ammar brigades nalo limo
katika orodha ya makundi ya
kigaidi yanayofadhiliwa
naye.Ni hadithi ndefu hadi
nimefika hapa lakini naomba
nikueleze kwa kifupi
tu.Mossad walingia nchini
Tanzania na kumteka mtu
mmoja anaitwa Edger Kaka
aliyekuwa mbunge katika
bunge la jamhuri ya
muungano wa Tanzania
ambaye alikuwa na
mahusiano ya karibu na
Habiba Jawad na
kutengeneza ajali ambayo
ilituaminisha wote kwamba
Edger amekufa lakini baadae
kikundi cha IS wakagundua
kwamba Edger hajafariki na
wakadhani serikali ya
Tanzania ndiyo
iliyotengeneza uongo ule
kwamba Edger amefariki
dunia hivyo wakaandaa
mpango wa kumshinikiza
Rais wa Tanzania kumuachia
huru Edger ambaye
waliamini anashikiliwa na
serikali ya Tanzania.Mpango
yhuo wa kumshinikiza Rais
wa Tanzania amuachie
Edger Kaka uliambatana na
mambo mengi ikiwemo
mauaji na utekaji wa
watu.Katika kulichunguza
tukio moja la utekaji nilibain
kwamba Edger Kaka ambaye
IS walikuwa wanamtafuta
alikuwa ametekwa na
Mossad na alifichwa katika
ubalozi wa Israel jijini
Nairobi.Niliongoza timu
kwenda Nairobi
kumuokoa.Hapo ndipo
ugomvi na Israel ulipoanza
kwani ilinilazimu kuua
mkuu wa Mossad Afrika
Mashariki na majasusi
wengine wawili ili kumpata
Edger ili kumkabidhi kwa IS
abao walikuwa wamemteka
mtoto wa Rais na ili
kuwaachia huru
walimuhitaji Edger
kaka.Wakati tukifanya
mabadilishano ya mateka
likatokea shambulio la
kustukiza” akasema Mathew
na kunyamaza kidogo
“Mlishambuliwa na nani?
Nawal akauliza
“Vikosi vya
Israel.Sifahamu walipataje
taarifa za mabadilishano yale
lakini ndio waliotuvamia
wakaniteka mimi na Edger
Kaka.Nilipelekwa Israel
ambako kwa miaka mitatu
nimekuwa nikiteswa
wakinitaka nikiri na
niwataje wenzangu
niliokuwa nao wakati
ninavamia ubalozi wa Israel
jijini Nairobi na aliyenituma
kufanya hivyo.Kwa miaka
mitatu ya mateso makali
sikuwahi kufumbua mdomo
wangu kuzungumza
chochote na ndipo
walipoamua kumtuma
mmoja wa watu wao kwenda
kuanzisha mahusiano ya
kimapenzi na mke wangu na
wakanionyesha picha za
wawili hao wakiwa katika
mapenzi mazito.Niliumia
sana na ndipo nlipokubali
kuzungumza nikakubaliana
nao kwamba nitawasaidia
kumpata Habiba Jawad ili
niweze kuwa huru.Ninataka
kumpata Habiba Jawad ili
kulifanya kundi la IS na
mengine ya kigaidi
yanayofadhiliwa naye yakose
nguvu ya kiuchumi na
kutoweka taratibu kutokana
na kushindwa
kujiendesha.Ili kupata
sehemu ya kuanzia
ilinilazimu kujenga
mahusiano na mmoja wa
watu ambao Israel walikuwa
wanawashikilia kwa ugaidi
na wakanikutanisha na
Ammar nikajenga mahusiano
naye na kupanga mpango wa
kutoroka.Lengo la
kumtorosha Ammar ni ili
niweze kuingia katika
mtandao wa kigaidi na
hatimaye niweze kumfikia
Habiba Jawad.Nadhani
nimejibu maswali yako
uliyoniuliza kwamba kwa
nini nilimtorosha Ammar
gerezani na kwa nini niko
hapa” akasema Mathew
“Pole sana Abu lakini
njia uliyoipita ni ndefu na ya
hatari kubwa” akasema
Nawal
“Hakukuwa na namna
nyingine ya kuweza kuingia
katika mtandao wa kigaidi
kama nisingetumia njia hii”
“Nalifahamu hilo lakini
hofu yangu hawa jamaa
wakigundua kwamba wewe
ni jasusi na una misheni
yako ya siri watakuua kabla
hujakamilisha misheni
yako.Hapa ni sehemu hatari
sana” akasema Nawal
“Hatari niliyonayo mimi
na wewe unayo vile vile
kwani hawa jamaa
wakikugundua kwamba
wewe unafanya kazi na CIA
watakuua.Hivyo basi
tunatakiwa tusaidiane ili
tukamilishe malengo
yetu.Huyo gaidi
unayemtafuta umekwisha
fanikiwa kujua mahala
alipo?akauliza Mathew
“Hapana bado
sijafanikiwa kujua mahala
alipo. Hawa jamaa
wanajitahidi sana kuficha
mambo yao ndiyo maana
mpaka sasa bado
sijafanikiwa kumpata Yasin
Al Nasser lakini hatua
niliyopiga ni kubwa hadi
sasa.Nimepata mambo mengi
yanayohusiana na mitandao
ya kigaidi.” akasema Nawal
“Katika muda uliokaa
hapa umewahi kumuona au
kumsikia Habiba Jawad?
“Habiba jawad sijawahi
kuonana naye ana kwa ana
lakini nimemsikia akitajwa
sana na Ammar.Kama
ulivyosema ni mfadhili
mkubwa wa makundi haya
ya wanamgambo na magaidi
na kama ukiendelea kuwa na
ukaribu na Ammar unaweza
ukafahamu mahala alipo
lakini naomba uwe makini
sana kwani hawa jamaa
hawapaswi kukutilia shaka
hata kidogo vinginevyo
watakuua.Kwa sasa endelea
kuwa karibu na Ammar
kwani ametokea kukuamini
sana.Usimuulize
maswalimengi kuhusu
kikundi chake nenda naye
taratibu.Watakushirikisha
katika mipango yao
mbalimbali ya kigaidi
wakiamini wewe ni mwenzao
na chochote
watakachokutaka ufanye
usionyeshe wasiwasi wala
kuuliza maswali kwani
wanakutambua kama gaidi
hivyo mipango mingi
watakushirikisha.Hata
wakikutuma uniue mimi
usisite fanya hivyo” akasema
Nawal
“Nitajitahidi kufanya kila
niwezalo kumfanya Ammar
aendelee kuniamini lakini
nina ombi moja
kwako.Nahitaji kuwasiliana
na Mossad kuwajulisha
kwamba tayari niko katika
kundi hili la Ammar
brigades”akasema Mathew
“Siwezi kukusaidia kwa
hilo Abu kwa sababu inaweza
ikaniharibia hata mimi.Niko
hapa kwa siri kubwa hivyo
sitaki Mossad wajue kama
kuna mtu wa CIA ndani ya
kundi hili.Hata hivyo
nitaangalia namna ya
kukusaidia” akasema Nawal
“Sawa nimekuelewa
lakini naomba unisaidie
kufanya uchunguzi kuhusu
mahala alipo Habiba Jawad ”
akasema Mathew
“Si jambo jepesi kama
unavyodhani kwani hawa
jamaa wanamlinda sana kwa
kuwa wanajua anatafutwa
nay eye ndiye muwezeshaji
wao.Hawa jamaa wanajua
sana namna ya kujificha kwa
mfano kwa miaka zaidi ya
mitatu sasa nimekuwa
nikimtafuta Yasin Al Nasser
bila mafanikio ila naamini
niko karibu sana kujua
mahala alipo” akasema
Nawal
“Nawal wewe uko karibu
sana na Ammar hivyo
utakapoona kuna hatari
yoyote inanikabili nijulishe
mara moja” akasema
Mathew
“Nitajitahidi kwa kila
namna usiingie katika hatari
na kama nitagundua hatari
yoyote nitakujulisha haraka
sana”
“Hata hivyo ilikuaje hadi
ukafika mahala hapa na
kuolewa na Ammar?akauliza
Mathew
“Ni hadithji ndefu
nitakusimulia siku nyingine
.Sitaki kutumia muda
mwingi humu ndani ili watu
wasianze kuwa na wasiwasi
kuhusu mimi na
wewe.Nikipata nafasi
nitamuomba Ammar
unisindikize kwenda mjini
siku moja na nitakueleza
mengi huko” akasema Nawal
akamalizia kumganga
Mathew majeraha halafu
akaondoka.
“Daah ! dunia hii imejaa
siri nyingi.Kumbe Nawal ni
CIA !” akawaza Mathew
“Hata hivyo mwanamke
huyu ni jasiri anastahili sifa
kubwa.Kitendo cha kuja
kujipachika kwa watu hatari
kama hawa ni kitendo cha
kishujaa mno.Ameweka
rehani maisha yake kwa ajili
ya nchi yake.Wamarekani
wako salama lakini
yawezekana hawajui kama
kuna watu kama hawa
ambao wameyaweka rehani
maisha yao ili wao wawe
salama.Wakati mwingine
yawezekana hata nchi yako
unayoipigania isikuthamini
kama ilivyonitokea
mimi.Baada ya kutekwa na
Mossad sina hakika kama
kuna juhudi zozote
zilifanyika kunitafuta na
kujua mahala nilipo”
akawaza Mathew na kuanza
kukumbuka usiku ule
waliposhambuliwa na watu
wasiowafahamu na yeye
akajikuta katika mikono ya
Mossad.
“Lilikuwa ni shambulio
la ghafla sana ambalo
hakuna aliyekuwa
amelitegemea.Nakumbuka
tulishambuliwa kutoka kila
upande.Nilipigwa risasi
mbili.Sina hakika kama
Olivia na Coletha
walifanikiwa
kuokolewa.Huwa sipendi
sana kukumbuka kuhusu
usiku ule kwani ni tukio
baya mno katika maisha
yangu.Ni siku ambayo
ilibadili kabisa maisha
yangu.Huwa najiuliza
kuhusu Rais Dr Evans,
nilipambana kumuokoa
mwanae lakini yeye
amefanya juhudi gani za
kunitafuta? Sitaki kuwaza
zaidi jambo hili linaumiza
sana.Yaliyopita yamekwisha
pita na kwa sasa niko hapa
peke yangu sina msaada
wowote nchi yangu
wanaamini nimekwisha
fariki hivyo basi ni juhudi
zangu binafsi ndizo
zitakazoniokoa.Nimeamua
kuja sehemu hatari kama hii
ambako dakika yoyote mtu
unaweza ukjapoteza maisha
lakini sikuwa na namna
nyingine ya kujiokoa zaidi ya
kuamua kuja hapa na lengo
ni kuendelea kupambana
kuhakikisha watu wanakuwa
salama.Mtandao wa IS
umeotesha mizizi pia hata
nyumbani Tanzania hivyo
nikifanikiwa kumuondoa
Habiba nitakuwa nimelea pia
usalama nchini kwangu
hivyo kwa namna yoyote ile
lazima mfadhili huyu wa
ugaidi apatikane” akawaza
Mathew na kwenda
kuchungulia nje kulikuwa
kimya na walinzi wachache
akarudi kitandani
kujipumzisha
PARIS – UFARANSA
Rais Michael Weren wa
Ufaransa alipomaliza kikao
na baadhi ya watendaji wake
akajulishwa kuhusu kuwasili
kwa mgeni muhimu
aliyekuwa na miadi ya
kuonana naye siku
hiyo.Michael akaelekeza
mgeni wake apelekwe katika
chumba maalum cha
mazungumzo ya faragha yeye
akaenda ofisini kwake
akakutana na mshauri wake
mmoja wakajadiliana kuhusu
suala Fulani halafu akatoka
kwenda kuonana na mgeni
wake
“Devotha Adolph.Karibu
sana” akasema Michael
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais.Kuna
taarifa gani
umeniletea?akauliza Michael
“Mheshimiwa Rais
taarifa niliyokuja nayo si
taarifa nzuri” akasema
Devotha na Rais Michael
akastuka kidogo
“Kuna taarifa gani
mbaya?akauliza
“Tamar Axon amefariki
dunia usiku wa kuamkia leo?
“Nini?! Tamar
amefariki?akauliza Michael
kwa mshangao
“Samahani mheshimiwa
Rais kwa kukustua lakini ni
kweli Tamar amefariki dunia
usiku wa kuamkia
leo”akasema Devotha na Rais
Michael akasimama
“Devotha tafadhali
niambie kama jambo hili si la
kweli”
“Ni kweli mheshimiwa
Rais.Tamar amefariki dunia”
akasema Devotha na Michael
akasimama akaenda katika
kabati lake la vitabu
akaegemea na kuinamisha
kichwa halafu akarejea tena
katika kiti alichokuwa
amekaa
“Amepata ajali?akauliza
“Hapana.Ameuawa”
“Ameuawa?
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Kwa taarifa nilizozipata
ni kwamba kuna watu
walimvamia nyumbani
kwake wakamuua kisha
wakaichoma nyumba yake”
akasema Devotha na kimya
kikatawala ndani ya kile
chumba.Rais Michael
alichanganyikiwa
“Kweli hii ni taarifa
mbaya sana
umeniletea.Tamar ni mtu
ambaye tulikuwa
tunategemea mno katika
mipango yetu.Nani
waliomuua?Kuna yeyote
ambaye amekamatwa mpaka
sasa kuhusiana na mauaji
hayo? akauliza
“Mpaka sasa hakuna
aliyekamatwa kuhusiana na
mauaji hayo” akasema
Devotha
Ulipita ukimya wa
dakika mbili halafu Rais
Michael akauliza
“Devotha hili jambo
limetokeaje?
“Kwa mujibu wa taarifa
nilizozipata ni kwamba
Tamar alivamiwa na watu
wasiofahamika wakamuua
wakamtoa ndani
wakamuweka katika gari
lake halafu wakaichoma
nyumba yake na kuharibu
kila kitu.Wauaji walijua
kuna kamera za ulinzi za siri
nyumbani kwa Tamar hivyo
ili kuzuia wasijulikane
wakaichoma nyumba na
kuharibu kila kitu hivyo
hakuna kumbu kumbu
yoyote iliyopatikana”
akasema Devotha
“Devotha
nimechanganyikiwa.Sikutege
mea kabisa jambo kama hili
kutokea hasa kwa wakati
kama huu ambao
tulimuhitaji mno
Tamar.Unadhani waliomuua
Tamar kuna kitu
walikigundua kuhusu
kushirikiana na balozi
Benjamin?
“Kuna kila dalili kwamba
wauaji hao kuna kitu
walikifuata kwa Tamar na
yawezekana baada ya kupata
walichokifuata
wakamuua.Waliomuua si
majambazi bali ni watu
wenye ujuzi mkubwa sana
kwani nyumba ya Tamar ina
mfumo mkubwa wa ulinzi na
majambazi hawawezi kuingia
lazima watakuwa ni watu
hatari sana”
“Unahisi serikali inaweza
kuwa na mkono wake katika
kifo hiki cha Tamar?akauliza
Michael
“Sina uhakika sana wa
hilo lakini inawezekana
pia.Kitu muhimu ni kufanya
uchunguzi na
kujihadhari”akasema
Devotha na ukimya ukapita
kisha Rais Michael akauliza
“Tamar alifahamu nani
waliomuua balozi Benjamin?
“Hapana hafahamu
chochote.Naye kama walivyo
watu wengine anaamini
serikali ya Tanzania
inahusika katika mauaji yale
ya balozi Benjamin.
Niliwatumia vijana wengine
kabisa kama tulivyokuwa
tumekubaliana” akasema
Devotha na ukimya ukapita
halafu Rais Michael akasema
“Devotha sikufichi
nimestushwa mno na taarifa
hii ya kifo cha
Tamar.Mipango yetu yote
kwa kiasi kikubwa
ilimtegemea sana yeye.Kila
kitu kilikuwa kinakwenda
vizuri sana hadi baada ya
kuzipokea taarifa hizi
mbaya.Hivi sasa tulikuwa
tunajiandaa kuingia katika
awamu ya tatu ambapo
Theresia Muganza
anaandaliwa kwa ajili ya
kwenda Tanzania na Tamar
ndiye aliyekuwa anafanya
maandalizi ya jambo
hilo.Kifo chake kitasababisha
mkwamo mkubwa katika
mipango yetu.Kuna nini
Tanzania? Lucy Muganza
ameuawa Tanzania na sasa
Tamar.Kwa nini Tanzania
imekuwa inatukwamisha
katika mipango yetu yote?
Akauliza Rais Michael na
kugonga meza kwa hasira
“Ninaapa nitapambana
na nchi hii ambayo imekuwa
kikwazo kikubwa kwetu.Ni
aibu kukubali kuyumbishwa
na nchi kama Tanzania !
akasema Michael
“Mheshimiwa Rais
naomba nikutoe
wasiwasi.Kifo cha Tamar si
mwisho wa mipango
yetu.Kila tulichokipanga
kitaendelea kama kawaida
na tutafanikiwa” akasema
Devotha
“Tanzania
wameturudisha nyuma kiasi
kikubwa sana !
“Mheshimiwa Rais
nakubali kwamba Tamar
alikuwa ni nguzo yetu na kifo
chake kimeturudisha nyuma
sana hata hivyo bado
tunaweza kuendelea na
mipango yetu”akasema
Devotha
“Ni jinsi gani tutaweza
kuendelea na mipango yetu
bila Tamar? Akauliza Rais
“Mheshimiwa Rais ni
kweli tutapata ugumu
kuendelea na mipango yetu
bila ya Tamar lakini
tunaweza kuendelea na
mipango yetu yote hata bila
ya yeye kuwepo”
“Ni hapo ndipo
ninapotaka kupafahamu
tutaendelea vipi bila Tamar?
Yule alikuwa ndiye jicho letu
katika serikali.Nataka
kusikia mawazo yako
tafadhali”akasema Michael
“Mheshimiwa Rais
pamoja na hili ililotokea la
kuuawa Tamar lakini hatua
tuliyopiga katika mpango
wetu si ndogo.Mpaka sasa
Tanzania imekwisha chafuka
kimataifa.Duniani kote
wanafahamu kwamba
Tanzania hakuna usalama
na tukitaka kuisambaratisha
Afrika Mashariki lazima
tuanze kwanza na Tanzania
kwani ndipo ilipo mizizi ya
jumuia hii.Tanzania
ikidhoofika jumuiya hii
itakosa nguvu.Tanzania
ikichafuka eneo zima la
Afrika Masharikilitachafuka
hivyo hatua tuliyopiga
mpaka sasa si ndogo.Dunia
nzima wanajua Tanzania
inahusika katika mauaji ya
balozi Benjamin Hudson
kufuatia ujumbe alioandika
katika ukurasa wake wa
twitter akiwataka raia wa
kutoka nchi za umoja wa
Ulaya kutotembelea au kuwa
makini wanapokuwa
Tanzania.Nina imani
kufuatia kifo cha balozi
Benjamin Watalii
wanaotembelea Tanzania na
Afrika Mashariki
watapungua kwa hofu ya
usalama wao na hilo ni
jambo kubwa sana
kwetu.Hata hivyo bado
tunayo kazi kubwa ya
kufanya na kwa sasa baada
ya Tamar kuuawa
tunatakiwa kubadili mbinu
za kuendelea na mpango
wetu” akasema Devotha
“Nakusikiliza Devotha
endelea” akasema Rais
Michael
“Kipaumbele kwa sasa ni
kuhakikisha Theresia
Muganza anaingia Tanzania
na ili aweze kufanikisha
vyema kazi yake ya
kusambaratisha Afrika
Mashariki tunahitaji mtu
ndani ya idara ya
SNSA.Kuna mtu ndani ya
idara ya SNSA anaitwa
Edwin mbeko huyu alikuwa
msaidizi wa Tamar na ndiye
niliyemtumia katika mauaji
ya balozi Benjamin.Huyu
anaweza kuwa mbadala wa
Tamar na kuna uwezekano
Rais akamteua kuwa
mkurugenzi wa SNSA
kushika nafasi ya
Tamar.Nashauri tuendelee
kumtumia huyu jamaa
ambaye nilimfundisha kazi
mimi mwenyewe wakati
ninaongoza idara
ile.Sijamueleza chochote kwa
sasa hadi utakaporidhia
kwamba awe ndiye mbadala
wa Tamar” akasema Devotha
na Rais Michael akafikiri na
kusema
“Unamuamini anaweza
akaifanya kazi yake
kikamilifu kama
Tamar?akauliza Rais
Michael
“Ndiyo
ninamuamini.Kama
nilivyokueleza ndiye
niliyemtumia katika mauaji
ya balozi Benjamin
Hudson.Ni mtiifu,msikivu na
anafanya kazi yake kwa
umakini mkubwa sana”
akasema Devotha
“Mimi sina tatizo .Kama
unaamini anaweza akawa
mbadala wa Tamar basi
tumtumie”
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais” akasema
Devotha
“Jambo la pili .Wakati
tukiendelea na mchakato wa
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika Mashariki kwa
kumtumia Theresia Muganza
,kwa upande wa pili lazima
tuendelee na mpango wa
kumuondoa madarakani Rais
Dr Fabian Kelelo.Huyu ni
kikwazo kikubwa sana
katika mipango
yetu.Natakiwa kukalia kiti
chake haraka sana kama
tulivyokuwa tumekubaliana
ili niweze kusaidia katika
mpango huu
mkubwa”Devotha
akanyamaza na Rais Michael
akauliza
“Tukianzia na mpango
wa kwanza wa kumuingiza
Theresa nchini Tanzania
uUnadhani Theresia
ataingiaje chini Tanzania?
Umesema tumtumie msaidizi
wa Tamar ni vipi kama Rais
Dr Fabian hatamteua kuwa
mkurugenzi wa SNSA na
badala yake akateua mtu
mwingine? Nataka nisikie
mpango yako katika
hilo.Kumbuka hiki ni kipimo
kwako kama endapo
tutakusaidia ukachukua
urais utaweza kweli nafasi
hiyo na ukatekeleza mipango
yetu yote? Akasema Rais
Michael
“Baada ya Tamar
kutolewa katika picha ninao
mpango mwingine wa
kumuingiza Theresia nchini
Tanzania na kumuwezesha
kutekekeza mipango yetu
bila matatizo.Hapa Paris
kuna bilionea anaitwa
Peniela.Nadhani umewahi
kumsikia”
“Ndiyo ninamfahamu.Ni
bilionea mkubwa na hakuna
asiyemfahamu”akasema
MIchael
“Japo kwa sasa ana uraia
wa Ufaransa lakini Peniela
anatokea Tanzania” akasema
Devotha
“Nalifahamu hilo”
akasema Rais Michael na
Devotha akaendelea
“Peniela na mume wake
wamewekeza miradi mbali
mbali nchini Tanzania.Mume
wa Peniela aliitwa Mathew
Mulumbi ambaye kwa sasa
ni marehemu.Kutokana na
mumewe kufariki mali za
Peniela ambazo ziko Afrika
Mashariki zinakosa
usimamizi makini kwani
Peniela anaichukia sana
Tanzania”
“Anaichukia Tanzania
nchi yake?akauliza Rais
Michael
“Ndiyo.Kwa sababu ya
kifo cha mumewe.Mathew
alikuwa anafanya kazi ya
ujasusi na hata mimi
nimewahi kufanya naye
kazi.Alifariki akiwa katika
misheni aliyotumwa na Rais
hivyo basi kitendo hicho
kimemuumiza mo Peniela na
kumfanya asitake tena
kurejea Tanzania.Theresa
atakwenda kwa Peniela
akimuomba amuuzie baadhi
ya makampuni yake yaliyoko
Tanzania na ataingia
Tanzania kama muwekezaji”
akasema Devotha.Ulipita
muda kidogo na Rais Michael
akasema
“Huo unaonekana ni
mpango mzuri lakini kama
Peniela tayari ana chuki na
Tanzania kufuatia kifo cha
mumewe,hatuwezi
kumshirikisha katika
mpango wetu huu? Akauliza
Rais Michael
“Hapana.Hatuwezi
kumshirikisha.Si mtu
ambaye tunaweza
kumuamini”
“Sawa.Basi mpango huo
wa kumpeleka Theresia
Tanzania kama muwekezaji
ni mpango mzuri.Unaamini
Peniela atakuwa tayari
kuuza baadhi ya mali zake
nchini Tanzania?
“Nina watu ambao wako
karibu na Peniela ambao
wamenihakikishia kwamba
Peniela ana mpango huo wa
kuuza mali zake zote nchini
Tanzania kwani hana
mpango wa kurudi tena
huko”akasema Devotha
“Sawa endelea
kulishughulikia hilo
suala.Baada ya Theresia
kupona atapelekwa kwanza
mafunzoni kisha mchakato
wa kuelekea Tanzania
utaanza.Hata hivyo nina
ushauri .Naamini mpango
wetu wa kumuandaa Lucy
Muganza kuchukua urais wa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo ulivuja ndiyo maana
akauawa.Kuuawa kwa
Tamar kunadhihirisha
kwamba tayari Tanzania
wanafahamu kila kitu
kuhusu mipango yetu ndiyo
maana wanajaribu kwa kila
wawezavyo kuhakikisha
hatufanikiwi. Ushauri wangu
kwa sasa inatubidi tutulie
kwanza huku tukiendelea
kujipanga kimya kimya kwa
ajili ya operesheni
mpya.Tumfanye Rais Fabian
ajue kwamba baada ya
kumuua Tamar basi mambo
yamekwisha.Nitawashawishi
pia wenzangu wa umoja wa
Ulaya kutulia kimya
wasiongee chochote kuhusu
Tanzania kwa sasa.Katika
mpango huu mpya
tujihadhari sana usije
ukavuja.Unadhani
hawataweza kugundua kama
Tamar alikuwa na
mawasiliano nawe? Akauliza
Rais Michael
“Jina Devotha Adolph
limekwisha sahaulika
Tanzania hakuna anayejua
kama niko hapa
Paris.Kingine kizuri ni
kwamba Tamar alikuwa
anatumia program maalum
katika simu yake ambayo
kila amalizapo kuzungumza
na simu basi kumbu kumbu
zote hufutwa haraka sana
hivyo hakuna rekodi zozote
za mazungumzo ya simu
watakazozipata katika simu
ya Tamar kama wakitaka
kufuatilia kujua alikuwa
anawasiliana na
nani”akasema Devotha
ukapita ukimya kidogo na
Rais Michael akasema
“Devotha ulijunga nasi
katika mpango wetu wa
kutaka kuisambaratisha
jumuiya ya Afrika Mashariki
kwa sharti kwamba unataka
tukusaidie ushike nafasi ya
Urais wa Tanzania .Mimi na
wenzangu wa umoja wa
Ulaya hatuna kipingamizi
katika suala hilo kwani
utakuwa na manufaa
makubwa kwetu.Tanzania ni
kioo cha Afrka Mashariki
hivyo licha ya kwamba
malengo yetu makubwa ya
mpango huu ni jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
lakini Tanzania tunaihitaji
pia hivyo tunahitaji
kumuweka mtu wetu
madarakani.Usiwe na hofu
Devotha fanikisha Theresia
aingie Tanzania,mimi na
wezangu tutakuweka
madarakani kwani uwezo
huo tunao.Kwa sasa twende
kwanza na jambo moja
tukilifanikisha tutaanza
jambo la pili.Narudia tena
kukusisitiza kwamba
hakikisha mpango huu
hauvuji kama ilivyokuwa
kwa mpango ule wa kwanza”
akasema rais Michael
BAADA YA WIKI NNE
PARIS – UFARANSA
Saa kumi na moja za
jioni Rais Michael Weren
aliwasili katika jumba lake
kubwa ambalo huwa
analitumia kwa mapumziko
na familia yake.Katika
jumba hili ndimo anamoishi
Theresia Muganza
akiendelea kupatiwa
matibabu na jopo la
madaktari baada ya
kufanyiwa upasuaji wa
plastiki kubadilisha
muonekano wake.Alifika
hapa kumtazama Theresa
baada ya kutaarifiwa na
madaktari kwamba kwa
asilimia tisini Theresa
alikuwa amepona.
Rais Michael alipokewa
na daktari mkuu wa lile jopo
la madaktari waliopiga
kambi katika jumba lile
kuhakikisha wanaikamilisha
kazi waliyopewa na
Rais,kisha wakaelekea ndani
ambako alisalimiana na
madaktari wengine na kabla
hajaingia katika chumba
alimo Theresa akapewa
taarifa na mkuu wa jopo lile
la madaktari kuhusiana na
kazi
waliyoifanya.Alionyeshwa
picha mbili tofauti.Picha ya
kwanza ilimuonyesha
Theresa Muganza kablaya
upasuaji na ya pili
ilimonyesha baada ya
upasuaji.Zilikuwa ni sura
mbili tofauti zilizomuacha
Rais Michael mdomo wazi
“Haya ni maajabu.Mtu
unaweza ukabadilishwa
kabisa mwonekano wako na
watu wakashindwa
kukutambua” akawaza
Baada ya kupokea taarifa
ile ya madaktari akaingizwa
katika chumba kikubwa
alimokuwamo Theresa
ambaye alikuwa amejilaza
katika sofa.
“Theresa ! akasema Rais
Michael kwa
mshangao.Alipoonyeshwa
zile picha mbili hakuwa bado
akiamini sana akataka
athibitishe mwenyewe kwa
kumtazama.Alichokiona
mbele yake kilimshangaza
sana.Theresa alikuwa
amebadilika.Hakuwa
Theresa Yule wa wiki kadhaa
zilizopita.Huyu wa sasa
alikuwa ni mwanamke
mwenye umbile la aina
yake.Alikuwa na sura nzuri
iliyochongwa na kuvutia
mno.Alipotabasamu uzuri
uliongezeka mara dufu.Rais
Michael akageuka na kumpa
mkono daktari mkuu
akampongeza kwa mara
nyingine tena kwa kazi ile
kubwa.Madaktari wakatoka
wakamuacha Rais na
Theresa.
“Karibu sana
mheshimiwa
Rais.Sikutegemea kama
ungekuja leo” akasema
Theresa huku akitabasamu
“Nilitaarifiwa na
madaktari kwamba
wamekamilisha kazi yao
hivyo nikaona nije niangalie
kile
walichokifanya.Nimeishiwa
maneno ya kusema kwa
namna walivyoifanya kazi
yao kwa umahiri
mkubwa.Hivi ndivyo
nilivyokuwa
nataka.Umekuwa tofauti
kabisa na Theresa Yule wa
mwezi uliopita.Wanastahili
sifa madaktari hawa”
akasema Rais Michael bado
akiendelea kumtazama
Theresa huku akitabasamu
“Unauonaje muonekano
wako
mpya?Unaufurahia?akauliza
“Nimeufurahia sana
mwonekano huu.Nimekuwa
mrembo zaidi ya
nilivyotegemea.Nakushukur
u sana mheshimiwa Rais”
akasema
“Ninapaswa
kukushukuru wewe kwa
kukubali kubadili
mwonekano wako.Si jambo
jepesi hata kidogo”akasema
Rais Michael na kumtazama
Theresa tabasamu
halikukauka usoni kwake.
“Sikuwahi kufikiria
kufanya kitu kama hiki
lakini kwa ajili ya wazazi
wangu waliouawa kinyama
imenilazimu nifanye
hivi.Nataka kufahamu je
mpaka sasa kuna mtu yeyote
amekwisha kamatwa
kuhusiana na mauaji
yale?akauliza Theresa
“Hapana.Hakuna mpaka
sasa mtu aliyekamatwa
kufuatia mauaji yale.Watu
ambao walitajwa kuhusika
katika tukio lile la mauaji
ambao ni majambazi
waliuawa siku ile ile ile ya
tukio hivyo mpaka leo hii
hakuna mtu yeyote
anayeshikiliwa kwa mauaji
yale.Huo ni upande mmoja
wa taarifa iliyotolewa na
serikali.Upande wa pili
tumefanikiwa kupata taarifa
ya daktari aliyefanyia
uchunguzi wa miili ya
marehemu.Taarifa hiyo
inaonyesha risasi
zilizotumika kuwaua
marehemu haziendani na
silaha walizokutwa nazo
wale watu wanaotajwa
kufanya mauaji yale.Aina ya
silaha iliyotumika ni
bunduki zinazotumiwa na
wadunguaji.Ni bunduki nzito
sana na ambazo mara nyingi
huwa zinamilikiwa na
jeshi.Taarifa nyingine
tuliyonayo inatuonyesha
kwamba Tanzania wanazo
bundukiza aina hiyo
walizinunua kutoka
Marekani.Taarifa hizi
zinatufanya tuamini kwamba
serikali ya Tanzania
wanahusika katika mauaji
yale.Tulianza kufanya
uchunguzi wa suala hili
lakini bado hatujapata
majibu kwani aliyekuwa
anatusaidia kufanya
uchunguzi wa suala hili
ameuawa wiki chache
zilizopita na tunaamini haya
yote yanafanywa na serikali
ya Tanzania”
“Nimeishi Tanzania ni
nchi ya amani sana.Kwa nini
waliua wazazi wangu?
Akauliza Theresa na machozi
yakaanza kumtoka
“Usilie Theresa.Muda wa
kulia umekwisha”
“Inaumiza sana
mheshimiwa Rais.Wazazi
wangu waliuawa kikatili
sana na mimi mwenyewe
nilipona kwa bahati tu
mpaka leo ninapojitazama
siamini kama nilinusurika
katika tukio lile.Ninahitaji
kujua kwa nini wazazi
wangu waliuawa? Akasema
Theresa.
“Theresa nitakueleza
ukweli” akasema Rais
Michael na kunyamaza kwa
sekunde kadhaa halafu
akaendelea
“Baada ya uchaguzi
mkuu wa Rais na wabunge
nchini jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
kufanyika,Patrice Eyenga
aliibuka mshindi.Baada ya
kushinda uchaguzi Patrice
Eyenga alikutana na
makundi ya waasi
wakazungumza kuhusu
kumaliza vita vya miaka
mingi vya wenyewe kwa
wenyewe.Katika majadiliano
hayo namna ya kumaliza vita
hivyo walikubaliana
kugawana faida
itakayotokana na rasilimali
za madini yaliyoko nchini
humo.Hiyo ndiyo siri ya
waasi kuweka silaha chini
nchini Congo DRC na amani
kupatikana.Wawekezaji
wengi walifukuzwa nchini
humo na kuleta wawezekaji
wengine ambao waliingia nao
makubaliano.Kwa ufupi
naweza kusema kwamba
wanaofaidika kwa rasilimali
za Congo ni kikundi cha
watu wachache sana.Umoja
wa Ulaya hatukuwa tayari
kukubali kikundi cha watu
wachache waendelee
kufaidika na rasilimali za
Congo na kuwaacha
wananchi wakiendelea
kuogelea katika lindi la
umasikini.Tukaamua
kumuandaa mtu ambaye
atakuja kumaliza udhalimu
huu unaoendelea nchini
Congo na ndipo
tulipomuandaa Lucy
Muganza agombee urais
katika uchaguzi mkuu
utakaofanyika hivi karibuni
na tuliamini angeshinda
uchaguzi lakini kwa bahati
mbaya mpango wetu huo
ulivuja na tunaamini ndiyo
sababu ya wazazi wako
kuuawa kwani mafisadi
hawa walijua kwamba
endapo Lucy angeshinda
uchaguzi basi kiama chao
kingewadia hivyo wakaona
suluhisho ni
kumuua”akasema Rais
Michael
“Serikali ya Congo nao
walishiriki katika mauaji
yale?akauliza Theresa
“Hatuna ushahidi wa
moja kwa moja lakini
tunaamini serikali ya Congo
na Tanzania wameshirikiana
katika mauaji hayo.Tulikuwa
tunadukua mawasiliano ya
Rais wa Tanzania tujue
wanawasiliana nini na Rais
wa Congo lakini
hatukufanikiwa kuna watu
waliingilia zoezi hilo”
akasema Michael
“Roho inaniuma sana
nikiwakumbuka wazazi
wangu.Ninaumia mno”
akasema Theresa.
“Theresa kama
utakumbuka hapo awali
niliwahi kukueleza kwamba
wewe ndiye utakayevaa viatu
vya mama yako”akasema
Michael
“Siipendi kazi ya
siasa.Kama mama yangu
asingejiingiza katika
masuala ya siasa hivi sasa
angekuwa hai.Sitaki kuwa
mwanasiasa wataniua hasa
wakijua mimi ni mtoto wa
Lucy Muganza” akasema
Theresa
“Hautaingia katika
siasa.Licha ya kwamba
tulimuandaa kwa ajili ya
kushika urais wa Congo
lakini Theresa alikuwa na
kazi nyingine mahsusi
ambayo ndiyo utakwenda
kuifanya.Usihofu kuhusu
usalama wako.Kwa nza
kabisa hakuna atakayejua
wewe ni Theresa
Muganza.Kuanzia sasa
hautajulikana tena kama
Theresia Muganza bali
utajulikana kwa jina la
Melanie Davis bilionea na
raia wa Ufaransa” akasema
Rais Michael na kuichukua
bahasha iliyokuwa mezani
akaifungua na kutoa
nyaraka kadhaa
akamkabidhi Theresa
“Kuanzia sasa jina lako
ni Melanie Davis.Jina la
Theresia Muganza tunalizika
rasmi.Hizi hapa ni nyaraka
mbali mbali zinakuonyesha
wewe ni mzaliwa wa
Ufaransa na unayemiliki
utajiri mkubwa uliorithi
kutoka kwa wazazi wako
ambao wote wawili
wamekwisha fariki
dunia.Suala la kubadili
mwonekano wako lilifanyika
kwa siri kubwa na tulifanya
hivi ili kuzuia siri hii
kuvuja” akasema Rais
Michael.Theresa akaendelea
kuzipitia nyaraka zile
alipomaliza akafuta machozi
na kusema
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais kwa
kupambana kuyaokoa
maisha yangu.Naamini kama
ningeendelea kubaki
Tanzania hivi sasa
ningekwisha uawa.Ni
gharama kubwa sana
umeitumia.Naomba
uniambie nini unataka
nikifanye kama malipo ya
haya uliyonifanyia?akauliza
Theresa
“Ninataka ukaifanye kazi
aliyotakiwa kuifanya mama
yako”
“Niko tayari mheshimiwa
Rais kwa kazi hiyo hata
kama ni ya hatari lakini
nitaifanya ”
“Vizuri.Tunataka
uongoze mapambano ya
kuikomboa jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo”
akasema Rais Michael na
ukimya mfupi ukapita
Theresa akasema
“Mheshimiwa Rais
nadhani jukumu hilo
unalonipa ni gumu mno liko
juu ya uwezo wangu.Mimi
nikaikomboe nchi ya
Congo?Siwezi mheshmiwa
Rais nitauawa kabla
sijatekeleza hilo jukumu”
akasema Theresa kwa wasi
wasi
“Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo nchi
uliyozaliwa kwa sasa
imeingia katika jumuiya ya
Afria Mashariki.Rais Patrice
Eyenga amefanya hivi
makusudi ili kuendelea
kujiimarisha kiutawala
.Hatutaweza kuikomboa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo bila kwanza kuiondoa
katika jumiya ya Afrika
Mashariki .Jukumu kubwa la
kwanza unalokwenda
kulifanya ni
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika Mashariki” akasema
Michael na kunyamaza
baada ya sura ya Theresa
kuonyesha mstuko
“Najua nimekustua
Theresa lakini hilo ndilo
jukumu kubwa la kwanza
ambalo alikuwa nalo
marehemu mama yako Lucy
Muganza na sasa wewe ndiye
unayekwenda
kulitekeleza.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
imejiwekea mwavuli baada
ya kujiunga na jumuiya hii
hivyo basi hakuna namna
tunavyoweza kuondoa
unyonyaji unaofanywa na
Patrice Eyenga na genge la
mafisadi wenzake wachache
wanaoendelea kunufaika na
rasilimali za nchi yako huku
mamilioni ya watu
wakiendelea kuogelea katika
umasikini mkubwa.Ni
jukumu kubwa lakini
kumbuka kwamba
waliopanga njama za
kumuua mama yako ni hawa
viongozi wa Afrika Mashariki
hivyo basi pamoja na
kwamba tunapambana
kuikomboa nchi yako ya
Congo lakini vile vile
tunakwenda kulipiza kisasi
kwa wale wote waliowaua
wazazi wako kikatili.Usihofu
hautakuwa mwenyewe bali
sisi tuko nyuma yako na
tutakuwezesha kwa kila
kitu.Kazi yako itakuwa
rahisi sana na wala
hautakuwa katika hatari
yoyote” akasema Rais
Michael na Theresa akafuta
machozi
“Nini hasa ninatakiwa
kukifanya huko mnakotaka
kunituma? akauliza Theresa
“Kabla ya kwenda huko
Afrika Mashariki utapewa
kwanza mafunzo ya nini
unakwenda
kukifanya.Lazima tukuandae
kwa kazi hii.Kesho atakuja
mtu kukuchukua na
kukupeleka mahala
utakapopewa mafunzo na
pale utakapokuwa
umehitimu mafunzo yako
basi utakwenda Afrika
Mashariki”
“Ni mafunzo gani ambayo
ninakwenda kupewa?
Akauliza Theresa
“Ni mafunzo maalum ya
kukuandaa na kukujenga,
kukuondoa kutoka Theresa
Muganza na kuwa Melanie
Davis.Narudia tena kukutoa
hofu kwamba tutakuwa
nyuma yako kukulinda
kuhakikisha huingii katika
hatari yoyote” akasema Rais
Michael
“Kwa ajili ya kulipiza
kisasi kwa wale wote
waliowaua wazazi wangu
kinyama niko tayari
mheshimiwa Rais” akasema
Theresa huku akidondokwa
na machozi
“Usilie Theresa.Muda wa
kulia umekwisha pita hivi
sasa ni muda wa kujiandaa
kulipa kisasi kwa waliowaua
wazazi wako na kikomboa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo.Utaelezwa
mengi,utafundishwa mengi
hivyo nakuomba zingatia
yale yote utakayofundishwa”
akasema Rais Michael na
kuagana na Theresa
akaondoka
“Rais Michale amekuja
kukitonesha kidonda
kilichoanza kunyauka.Nina
hasira sana na wale
waliofanya kitendo kile cha
kinyama.Waliwaua wazazi
wangu kikatili sana.Naamini
yalikuwa ni mapenzi ya
Mungu nibaki hai ili niweze
kuikamilisha kazi ambayo
mama yangu alikuwa
amejitolea kuifanya ya
kuokoa rasilimali za nchi
yangu ya Congo.Damu ya
wazazi wangu haitapotea
bure lazima nihakikishe
ninawalipia kisasi.Hakuna
aliyeshiriki katika mauaji
haya atabaki
salama.Sikuwahi kuwa na
chuki kubwa moyoni
mwangu kama niliyo nayo
sasa.Nilikuwa ninasikia
simulizi za watu ambao
wazazi wao waliuawa
kinyama na sikujua mateso
ya namna gani wanayapitia
hadi na mimi nilipopoteza wa
kwangu.Ni mateso makubwa
mtu kuwakatili uhai wazazi
waliokuleta duniani na
kukulea kwa upendo
mkubwa.Wazazi wangu
hawakuwahi kunifundisha
kumchukia mtu lakini hawa
watu makatili wamenifanya
niwe na roho ya
chuki.Ninawachukia
wanasisasa,ninawachukia
viongozi wa nchi yangu ya
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo na Afrika Mashariki.
Kitu pekee kilichobaki
ambacho naamini kinaweza
kunipa amani ya moyo ni
pale nitakapohakikisha
kwamba wale wote
walioshiriki katika mauaji ya
wazazi wangu wanapata
adhabu inayowastahili”
akawaza Theresa.
LONDON – UINGEREZA
Baada ya Ruby kukubali
uteuzi wa Rais Fabian Kelelo
wa kuwa mkurugenzi mkuu
wa idara ya siri ya usalama
wa ndani wa
nchi,aliwasilisha kwa
uongozi wake wa wajuu wa
mamlaka kuu ya
mawasiliano ya kiintelijensia
ya uingereza maombi ya
kuacha kazi.Ulikuwa ni
mstuko mkubwa kwa
viongozi wa juu wa mamlaka
ile hawakuwa wametegemea
mtu kama Ruby angeweza
kuamua kuacha kazi licha ya
kuwa na mshahara mkubwa
na mnono na alipata kila
alichokihtaji.Ruby aliombwa
awape viongozi wake muda
wa kulijadili ombi lake kabla
ya kutoa maamuzi.
Sababu aliyoitoa Ruby ya
kutaka kuacha kazi
haikuwashawishi viongozi
wake kulikubali ombi lake
hivyo baada ya wiki mbili
akaitwa tena kuzungumza
na jopo la viongozi
wakamjulisha kwamba ombi
lake la kuacha kazi
wamelikataa hivyo basi
wakamtaka Ruby aendelee
na kazi lakini bado
aliendelea kuwa na
msimamo ule wa kutaka
kuacha kazi.Kikao kati yake
na jopo la viongozi
kilifanyika kwa muda wa saa
nne bila maafikiano na
wakaomba wapewe tena
muda wajadiliane.Baada ya
Ruby kutoka katika kikao
hicho viongozi wale
waliendelea na kikao na wote
walionyesha wasi wasi wao
kuhusu nia ya Ruby kuacha
kazi.Waliamua kutumia
idara ya ujasusi ya MI5
kumchunguza Ruby
mienendo yake,mawasiliano
yake ili kuona kama kuna
sababu nyingine
iliyompelekea Ruby kutaka
kuacha kazi.
Saa moja za jioni
alipotoka kazini Ruby na
wafanyakazi wenzake
walifika katika mgahawa
mmoja kupata
chakula.Walikuwa na
kawaida ya kila wamalizapo
majukumu yao ya siku
hukutana katika mgahawa
huo kupata chakula na
kinywaji kabla ya kwenda
majumbani.Wakiwa
wanasubiri chakula huku
wakiendelea na mazungumzo
na kupata kinywaji alifika
muhudumu akiwa na sinia la
chakula akajigonga katika
meza na mchuzi
ukammwagikia Ruby katika
nguo yake.Muhudumu Yule
akamuomba samahani na
kumtaka ampeleke katika
chumba chake akabadili
shati lake jeupe
lililochafuliwa kwa mchuzi ili
lifuliwe.Ruby aliongozana na
yule muhudumu hadi katika
chumba cha kubadili mavazi
cha wahudumu na alipoingia
mle ndani alipatwa na
mshangao mkubwa.
“Joe ?! akauliza kwa
mshangao baada ya kumkuta
mtu anayemfahamu ndani ya
kile chumba
“Ruby usihofu nimetumia
njia hii ili niweze kuonana
nawe bila mtu yeyote kuwa
na wasiwasi nawe” akasema
Joe ambaye ni rafiki mkubwa
wa Ruby na alikuwa ni
mfanyakazi wa idara ya MI5
“Kuna nini Joe?Unajua
namna ya kuwasiliana
name.Unayo namba yangu
ya simu kwa nini
hukunipigia?akauliza
Ruby.Joe akamshika Ruby
bega
“Ruby kuna tatizo ndiyo
maana sikutaka kukupigia
simu”
“Tatizo gani joe?
“MI5 wanakuchunguza”
akasema Joe na sura ya
Ruby ikaonyesha mstuko
mkubwa
“MI5
wananichunguza?akauliza
“Ndiyo wanakuchunguza”
“Nini wanakitafuta
kwangu?
“Wanachunguza kila
kitu.Wanachunguza
mawasiliano yako na kila
unachokifanya.Kuna kamera
za siri zimefungwa nyumbani
kwako hivyo basi kuwa
makini uwapo nyumbani
kwani kila unachokifanya
kinaonekana.Mawasiliano
yako yote yanafuatiliwa.Kila
unayekutana na
kuzungumza naye
anachunguzwa.Wanataka
kujua sababu ya kuacha
kazi” akasema Joe
“Joe ahsante sana kwa
kunipa taarifa hizi
muhimu.Nilitegemea jambo
kama hili kutokea kwani
mpaka leo hii hawajakubali
kuniacha niende ” akasema
Ruby
“Kwa nini umeamua
kuacha kazi Ruby?akauliza
Joe
“Ninataka kupumzika”
akajibu Ruby
“Ni sababu hiyo tu ndiyo
ambayo imekufanya uache
kazi?
“Ndiyo Joe.Ninataka
kupumzika”
“kwa nini usiombe upewe
likizo hata ya muda mrefu
upumzike kuliko kuamua
kuacha kabisa kazi?akauliza
Joe
“Nimechoshwa na kazi
hii Joe hivyo ninataka
nipumzike huku nikitafakari
nini cha kufanya lakini sitaki
tena kufanya kazi GCHQ”
akasema Ruby
“Ruby ninayaheshimu
sana mawazo yako lakini
nakuomba uwe makini sana
kuanzia sasa,kila
unachokifanya fahamu
kwamba kuna watu wako
nyuma yako wanakufuatilia”
akasema Joe
“Joe ninashukuru sana
kwa
kunitahadharisha.Nitakuwa
makini sana kwa kila
nikifanyacho”
“Nitalifuatilia kwa
karibu sana hili jambo na
kama kukiwa na hatari
yoyote nitakujulisha haraka
sana.Sitaki uingie katika
hatari yoyote Ruby” akasema
Joe
“Nashukuru sana
Joe.Kweli wewe ni rafiki wa
kweli.Ninafurahi kuwa na
rafiki kama wewe”akasema
Ruby
“Ruby siwezi kusahau
misaada mbali mbali ambayo
umekuwa
ukinisaidia.Nisingefika hapa
nilipo kama si wewe hivyo
basi siwezi kukubali
ukaingia katika hatari.Sasa
badilisha shati lako urejee
hotelini ukaungane na
wenzako.Hakikisha unakuwa
kawaida na usionyeshe
mabadiliko yoyote
yale.Endelea kutumia simu
yako kama kawaida kwa
mawasiliano ya kawaida na
marafiki zako lakini kwa
mawasiliano yale ya muhimu
ya siri usitumie simu hii
kwani inafuatiliwa” akasema
Joe.Haraka haraka Ruby
akavua lile shati
lililomwagikiwa mchuzi
akavaa shati lingine
alilokuja nalo Joe akatoka
kwenda kuungana na
wenzake wakaendelea
kupata chakula.Baada ya
chakula wakaondoka kila
mmoja akielekea nyumbani
kwake
“Nilijua toka awali
kwamba haitaweza kuwa
rahisi GCHQ kukubali
niache kazi.Nimekuwa mtu
muhimu sana katika
mamlaka hii na tayari
ninazifahamu siri nyingi na
hilo ndilo linalowapa ugumu
wa kukubali niache
kazi.Wana hofu labda
nikiondoka ninaweza kutoa
siri za nchi ninazozifahamu
ndiyo maana
wananichunguza kujua
ninawasiliana na nani na
kuzungumza nini.Kabla hata
Joe hajanieleza
kinachoendelea tayari
nilikwisha anza kuchukua
tahadhari kubwa ndiyo
maana nimekuwa makini
sana ninapowasiliana na
Rais Dr Fabian ili wasijue
kama ninakwenda Tanzania
kuwa mkurugenzi wa
SNSA.Kwa namna yoyote ile
wakatae wasikatae lazima
niondoke hapa Uingereza
niende Tanzania.” akawaza
Ruby.
Alifika nyumbani kwake
na kama alivyokuwa
ameelekezwa na Joe
hakuonyesha mstuko wowote
kama kuna kamera za siri
zimefungwa nyumbani
kwake.Alikwenda chumbani
kwake akavua mavazi yake
akabakiwa na nguo za ndani
halafu akaenda sebuleni
akajilaza sofani akitazama
filamu huku chupa ya
mvinyo laini ikiwa mezani
akiendelea kupiga mafunda
taratibu.Alipitiwa usingizi
sofani na baada ya kustuka
akaenda chumbani kwake
kulala
Saa kumi na mbili za
asubuhi aliamka na kuanza
kujiandaa kwenda
kazini.Wakati akipata
kifungua kinywa akafungua
kompyuta yake ili kutazama
jumbe alizotumiwa na moja
ya ujumbe ulitoka kwa
mkuu wake aliyemtaka
akaonane naye siku
ile.Alipokuwa tayari
akafunga mlango wa nyumba
yake na kuondoka.Kitu cha
kwanza alichokifanya baada
ya kufika ofisini kwake ni
kwenda kuonana na mkuu
wake akamsalimu kisha
mkuu Yule akaongozana
naye wakaenda hadi katika
ofisi ya mkurugenzi mkuu
ambako kulikuwa na jopo la
viongozi wa GCHQ.Hakuwa
ametaarifiwa kuhusiana na
kikao kile.
“Ruby karibu.Habari za
asubuhi” akasema
mkurugenzi mkuu baada ya
Ruby na mkuu wake wa
idara kuingia mle ofisini
“Habari nzuri kabisa
mkurugenzi.Habari zenu
wakuu wangu wengine”
akasema Ruby kwa adabu
wakaitikia wote halafu
akaketi kitini.
“Ruby hatukuwa
tumekujulisha kuhusu kikao
hiki lakini kwa ufupi ni
kwamba kikao hiki ni cha
dharura na mada kuu ni lile
suala lako la kutaka kuacha
kazi” akasema mkurugenzi
mkuu na kumtazama Ruby
“Ruby kwa mara
nyingine tena napenda
kuchukua nafasi hii
kukujulisha kwamba suala
lako limekuwa linatuumiza
vichwa vyetu sana toka
ulipoliwasilisha kwetu.Hiyo
ni kwa sababu wewe ni
muhimu sana kwetu na
umefanya kazi ambayo
naweza kusema ni ya
kutukuka kabisa.Wewe ni
mmoja wa wafanyakazi bora
kabisa hapa.Kinachotuumiza
vichwa vyetu na kutufanya
tuendelee kukutana kila
uchao kujadili jambo hili ni
umuhimu wako kwa
mamlaka hii.Bado
tunakuhitaji sana na hatuoni
sababu ya kukuacha
uende.Tumeichambua
sababu yako ya kutaka
kuacha kazi lakini bado
hatujaona kama ni sababu
yenye mashiko hivyo
napenda kukujulisha
kwamba kwa mara nyingine
tena msimamo wa mamlaka
ni kwamba ombi lako la
kuacha kazi GCHQ
limekataliwa” akasema
mkurugenzi Yule mwenye
umbo kubwa.Ruby akavuta
pumzi ndefu halafu akasema
“Mkurugenzi
ninashukuru sana kwanza
kwa kupokea ombi langu na
kulijadili.Ninashukuru vile
vile kwa maamuzi yenu
ambayo mmefikia.Lakini
kwa bahati mbaya na mimi
pia bado msimamo wangu ni
ule ule kwamba ninataka
niache kazi hapa
GCHQ”akasema Ruby na
ofisi ile ikatawaliwa na
ukimya
“Ruby” akasema
mkurugenzi mkuu na
kumtazama Ruby
“Kama nilivyokueleza
kwamba umuhimu wako ni
mkubwa sana katika
mamlaka yetu hivyo basi
kuna mambo ambayo idara
tumeamua kuyafanya ili
kukushawishi ubadilishe
mawazo yako ya kuacha kazi
katika mamlaka yetu.Sababu
uliyoitoa ya kuacha kazi
haijatushawishi hivyo
kutufanya tuamini kuna
sababu nyingine kubwa
kwani mshahara wako hapa
ni mzuri na unapata kila kitu
hata hivyo tumeamua
kukuongeza mshahara mara
saba ya mshahara unaolipwa
sasa” akasema mkurugenzi
mkuu na sura ya Ruby
ikaonyesha mshangao
.Hakutegemea kulipwa
mshahara mkubwa kiasi
kile.Mshahara wake ulikuwa
mkubwa lakini uliongezwa
mara saba zaidi ili
kumshawishi abaki kazini.
“Haya sasa ni
majaribu.Mshahara mkubwa
sana huu ambao wanataka
kunipa” akawaza Ruby
“Ukiacha mshahara huo
pia tutakupandisha cheo
utakuwa ni mkuu wa
idara.Mkuu wako wa sasa wa
idara atapangiwa kazi
nyingine.Utapewa nyumba
kubwa na nzuri zaidi
.Utapewa walinzi wa
kukulinda kila mahala
uendako.Hayo ni yale
makubwa ambayo
tunatarajia kukufanyia
lakini kuna mengi ambayo
yapo katika makataba huu
tuliouandaa ambao tunataka
ukaupitie na kuona yaliyomo
halafu utatujulisha”akasema
mkurugenzi mkuu wa GCHQ
na kumsogezea Ruby faili
akainuka akaenda
kulichukua.Akapitia haraka
haraka nyaraka zilizomo
“Huu ni mtego mkubwa
wameniwekea.Nikiendelea
kukataa watajua lazima
kuna sababu kubwa na
ninaweza hata kuuawa na
nikashindwa kufikia malengo
yangu ya kwenda
Tanzania.Ninachotakiwa
hapa ni kulegeza msimamo
wangu ili kuwapa moyo”
akawaza Ruby
“Ruby” akaita
mkurugenzi na Ruby
akainua kichwa
“Una maoni gani?
“Mkurugenzi nimeupokea
mkataba huu na ninakwenda
kuupitia nione kilichomo
ndani yake halafu nitakuja
tena kwako tutazungumza
lakini nina ombi moja
kwenu”
“Omba chochote Ruby”
“Nahitaji siku saba za
mapumziko” akasema Ruby
na ofisi ikawa kimya.Baada
ya muda mkurugenzi mkuu
akasema
“Kwa nini unahitaji siku
saba za mapumziko
Ruby?Kwa nini isiwe siku
mbili ?
“Nimekuwa nikifanya
kazi mfululizo bila
kupumzika siku nyingine
kwa saa ishrini na nne
nahitaji siku chache za
kupumzisha mwili na
akili”akajibu Ruby
Mkurugenzi akamtaka
Ruby akaendelee na kazi
atamjulisha baadae kile
watakachokuwa
wamekiamua kuhusu
maombi yake ya likizo fupi
ya siku saba.
Baada ya Ruby
kutoka,mkurugenzi mkuu
akachukua simu na
kupiga.Hazikupita dakika
mbili mtu mmoja akaingia
akiwa na kompyuta
mpakato.
“Tueleze nini
umekigundua kwa
Ruby?akauliza mkurugenzi
mkuu.Yule jamaa
akaifungua kompyuta yake
na kusema
“Nilichokigundua ni
kwamba Ruby ana kitu
anacho hataki kukiweka
wazi.Nadhauri tuendelee
kumchunguza” akasema yue
jamaa ambaye ni mtaalamu
wa kuchunguza watu kupitia
maneno na matendo yao
kujua kama wanasema
ukweli ama
wanadanganya.Baada ya
kuwasilisha taarifa yake
akatoka na wakuu wale
wakaendelea na kikao chao.
“Mmemsikia mtaalamu
wetu alichokisema.Ruby
kuna kitu anakificha na
hataki kuwa muwazi.Pamoja
na taarifa ya mtaalamu
lakini nyote mmeshuhudia
mstuko aliouonyesha Ruby
baada ya kutamkiwa
kwamba ataongezwa
mshahara mara saba zaidi ya
ule anaolipwa sasa.Hakuwa
ametegemea kama
tungeweza kumlipa kiasi
kikubwa namna hii cha fedha
ndiyo maana hata msimamo
wake umelegea hadi
akaamua kuchukua mkataba
ule akaupitie.Hapo ndipo
alipokosea” akasema
mkurugenzi mkuu na
kunyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Sikuwa nimewajulisha
dhumuni la kutaka
kumuongezea Ruby
mshahara mara saba zaidi ya
mshahara wake wa
sasa.Nadhani hata ninyi
nyote mmestuka sana baada
ya kusikia jambo hilo kwani
nililifanya siri.Kama Ruby
akilipwa mshahara mara
saba ya mshahara wake wa
sasa ninyi nyote ambao ni
viongozi wake mtakuwa chini
yake na atakuwa
ananikaribia sana kufikia
mshahara wangu mimi.”
Akanyamaza tena kwa
sekunde chache
“Sikuwa nimedhamiria
kumlipa Ruby kiasi kile
kikubwa cha fedha kama
nilivyomtamkia bali ulikuwa
ni mtego
nimemuwekea.Nilitaka
kumpima msimamo wake
mbele ya fedha.Mtakumbuka
toka alipowasilisha ombi lake
la kuacha kazi tumekuwa
tukikaa naye na
kuzungumza kujaribu
kumshawishi asiache kazi na
kama haitoshi mimi binafsi
nimekuwa nikimpigia hata
simu kumuomba abadili
maamuzi yake lakini
amekuwa na msimamo
usioyumba.Niliwahi
kumgusia kumuongeza
mshahara lakini hakuwa
tayari kubadili msimamo
wake.Leo baada ya
kumtamkia kwamba
ataongezwa mara saba zaidi
ya mshahara wake wa sasa
amelegeza msimamo wake na
amekubali kuchukua
mkataba akaupitie na kuna
kila dalili kwamba anaweza
akakubali na kuendelea na
kazi.Mtego wangu ulikuwa
hapa kutaka kumpima Ruby
msimamo wake mbele ya
fedha.Ameonyesha shida
yake ni fedha kwani kama
shida yake si fedha
asingelegeza msimamo wake
lakini anaonekana shida
yake ni fedha ndiyo maana
amekubali kuchukua
mkataba akaupitie.Wasi wasi
wangu ni kwamba kama
fedha imemfanya akalegeza
msimamo wake ni vipi kama
akitokea mtu au nchi na
wakamlipa fedha mara kumi
ya fedha tunayomlipa sisi
kwa lengo la kutaka kupata
siri Fulani za nchi yetu
hamuoni kama anaweza
akauza siri huyu
mwanamke?akauliza
mkurugenzi mkuu
“Nadhani mmenielewa
ninachokimaanisha.Kama ni
hivyo huyu mwanamke ni
hatari sana
kwetu.Hatupaswi kuendelea
kuwa naye katika mamlaka
yetu.Tunapaswa kumuondoa
haraka.Anafahamu mengi
hadi sasa na madhara yake
yanaweza kuwa makubwa
kama akiamua kuuza kile
anachokifahamu kuhusu nchi
yetu.Sioni sababu ya
kuendelea kumshikilia mtu
mmoja kana kwamba
akiondoka basi mamlaka
haitakuwepo tena.Yeye ni
mfanyakazi wa kawaida tu
kama wengine.Narudia tena
uamuzi wangu ni huo
kwamba mwanamke huyu ni
hatari na lazima tutafute
namna ya kumuondoa hivyo
timu inayoendelea
kumchunguza iwe makini
sana.Nitampigia simu
kumjulisha kwamba
nimekubali ombi lake la
mapumziko ya siku saba na
katika muda huo
tumchunguze anachokifanya
na tutafute namna ya
kumuondoa.Tutumie
utaalamu mkubwa
kumuondoa na ionekane
amejiua kutokana na msongo
wa mawazo.Na sisi
tutalithibitisha hilo kwamba
aliomba mapumziko ya siku
saba na alionekana ana
msongo wa mawazo.Nadhani
mmenielewa” akasema
mkurugenzi mkuu na wote
wakakubaliana naye.
“Ahsanteni sana kwa
kunielewa lakini
nawakumbusha tena
kwamba suala hili ni siri
kubwa.Najua Ruby ni
mwanamke mwenye akili
nyingi na anayeweza
kutambua hatari iliyoko
mbele yake lakini vile vile
ana marafiki wengi katika
mamlaka na katika vyombo
mbali mbali vya kiusalama
hivyo basi suala hili
lihusishe watu wachache
sana ili kuzuia kuvuja”
akaelekeza mkurugenzi
mkuu na majadiliano
yakaendelea kwa nusu saa
kisha wakuu wale wakatoka
kwenda kuendelea na
majukumu yao.Mkurgenzi
mkuu akampigia Ruby na
kumtaka aende ofisini kwake
ambako alimjulisha kwamba
wamekubali aende
mapumziko ya siku saba
kama alivyokuwa ameomba.
Baada ya ombi lake la
mapumziko kukubaliwa
Ruby hakutaka tena
kuendelea kukaa ofisini
akakusanya baadhi ya vitu
vyake vichache vya muhimu
akatoka.Moja kwa moja
akaelekea katika ofisi za
shirika la ndege la Misri
ambako alikata tiketi ya
ndege kwa ajili ya safari ya
kuelekea Misri asubuhi ya
siku inayofuata halafu
akaelekea nyumbani kwake
kupumzika
Taarifa ya Ruby kukata
tiketi ya ndege kwa lengo la
kusafiri kuelekea Misri
zilimfikia mkurugenzi mkuu
wa GCHQ kupitia kwa timu
ya majasusi waliowekwa
kumfuatilia Ruby na mara tu
alipoipata taarifa ile
akaitisha kikao cha dharura.
“Jamani nimewaiteni
tena kwa dharura kufuatia
taarifa niliyoipata kutoka
kwa timu ya watu
wanaoendelea kumfuatilia
Ruby.Nimetaarifiwa kwamba
baada ya kutoka hapa Ruby
alielekea katika ofisi za
shirika la ndege la Misri
akakata tiketi kwa ajili ya
kuelekea Misri kwa ndege ya
shirika hilo itakayoondoka
kesho saa tatu asubuhi. Ruby
anataka kuondoka nchini na
hatujui kwa nini anakwenda
Misri?akasema mkurugenzi
mkuu
“Labda niwakumbushe
viongozi wenzangu kwamba
mwaka 2013 Edward
Snowden wa Marekani
aliomba likizo kwa ajili ya
mapumziko ya kiafya
akaelekea Hong Kong na
huko alivujisha siri za
serikali ya Marekani.Ruby
amekuwa akifanya kazi
katika idara nyeti kabisa na
siri nyingi
anazifahamu.Sitaki
kilichotokea Marekani
kitokee na hapa
kwetu.Nadhani mpaka hpa
tayari mmekwisha pata
picha ya nini kinaendelea”
akasema mkurugenzi na
majadiliano yakaendelea
Ruby akiwa nyumbani
kwake
akipumzika,akapigiwa simu
na mtu aliyejitambulisha
kama muhudumu wa
mgahawa ambao Ruby
amekuwa akienda mara kwa
mara na wenzake kupata
chakula cha usiku baada ya
kumaliza kazi.Muhudumu
Yule akamkumbusha Ruby
kwamba shati lake ambalo
lilichafuliwa na mchuzi kwa
bahati mbaya lipo tayari na
apite kulichukua.Ruby
akamuahidi Yule muhudumu
kwenda kulichukua shati
lake jioni ya siku ile vile vile
akaweka oda ya chakula kwa
ajili yake na wenzake
“Huyu lazima atakuwa ni
Joe anataka nikaonane
naye.Kuna taarifa atakuwa
ameipata anataa kunipa”
akawaza Ruby na kuendelea
kutazama filamu.Alijua
anaangaliwa kupitia kamera
za siri hivyo basi hakutaka
kuoyesha kama ameipania
sana safari ile hivyo
alijitahidi kwa kila namna
aweze kuonyesha kwamba
safari ile ilikuwa ya kawaida
na haikuwa na uzito wowote.
Alipochoka kutazama
filamu akajilaza kitandani
hadi ilipotimu saa kumi na
mbili za jioni.Akaamka
akajiandaa kisha akatoka
kwenda kukutana na
marafiki zake katika
mgahawa wanapokutana kila
mara.Wenzake tayari
walikwisha fika na walikuwa
wanaendelea kupata
kinywaji Ruby akaungana
nao na katika mazungumzo
yao akawajulisha kwamba
siku inayofuata anasafiri
kwenda Cairo Misri.Wenzake
wote walimshangaa kwa
safari ile ya ghafla
“Kwa nini Misri?
Akauliza mmoja wao.
“Ninapenda kusoma
historia za mataifa mbali
mbali na historia ya nchi ya
Misri imenivuia sana.Nataka
nikashuhudie kwa macho
namna walivyokuwa
wakiwazika wafalme wao wa
zamani .Kuna mambo mengi
nataka nikajifunze kule
Misri” akajibu Ruby
.Muhudumu akafika na
kumtaka Ruby akachukue
shati lake akawaomba radhi
wenzake na kuelekea upande
wa ndani katika vyumba vya
wahudumu ambako kama
alivyokuwa ametegemea
akakutana na Joe.
“Habari yako Joe”
akasema Ruby
“Habari nzuri
Ruby.Nimefurahi kukuona”
“Mimi pia nimefurahi
kukuona.Nilipojulishwa na
muhudumu kuhusu shati
moja kwa moja nikajua ni
wewe.Vipi kuna taarifa
gani?akauliza Ruby
“Ruby tayari
wanafahamu kwamba kesho
unasafiri kwenda Misri”
akasema Joe
“Nalitambua
hilo.Wananifuatilia kila kona
hivyo nisingeweza kuficha
kuhusu safari
yangu.Naamini hivi sasa
wako nyumbani kwangu
wakipekua kutafuta kwa nini
ninasafiri kesho” akasema
Ruby
“Ruby uko katika hatari
kubwa sana.GCHQ
wamepanga kukuua”
akasema Joe na Ruby
akastuka
“Wanataka kuniua?
“Ndiyo.Ulifanya kosa
kubwa kukubali kuchukua
ule mkataba
waliokuandalia.Ulikuwa ni
mtego” akasema Joe na Ruby
akavuta pumzi ndefu
“Usijali Ruby tayari
ninafahamu mpango mzima
namna ulivyopangwa na
nitakusaidia.Utafuata kile
nitakachokueleza.Nilijua
toka awali kwamba GCHQ
wasingekuacha salama hivyo
nikaanza kujiandaa kwa ajili
ya kukusaidia.Usiwe na wasi
wasi Ruby.Mimi nipo
nitakusaidia” akasema Joe
na kumuelezea Ruby kwa
ufupi namna
watakavyofanya.
“Ahsante sana
Joe”akasema Ruby na
kumkumbatia Joe.
“Tayari
tumeelewana.Hivyo nenda
sasa ukajumuike na wenzako
ili wale wanaokufuatilia
wasije wakaanza kuwa na
wasiwasi nawe” akasema Joe
na Ruby akatoka akaenda
kuungana na wenzake.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 2
Saa kumi na mbili za
asubuhi tayari Ruby
alikwisha amka akijiandaa
kwa safari ile.Ni vitu
vichache tu aliviweka katika
sanduku lake dogo kwani
alijua anaonekana kupitia
kamera.Katika sanduku lile
aliweka nguo chache na vitu
vingine vidogo vidogo kama
vpodozi.Kompyuta yake
akaifungia katika kabati lake
kwa lengo la kuwatoa wasi
wasi wale waliokuwa
wanamfuatilia.Aliandaa
kifungua kinywa akakaa
mezani na wakati akipata
mlo ule wa asubuhi
akawapigia simu marafiki
zake kadhaa kuwajulisha
kwamba anasafiri asubuhi ile
kueleka Cairo Misri lakini
atarejea baada ya siku nne.
“Sasa muda
umewadia.Today is victory or
death.Lakini namuamini
sana Joe ni mmoja wa
majasusi hatari kabisa ndani
ya MI5.Sijui nitamshukuruje
kwa msaada huu mkubwa
alionisaidia.Bila yeye
nisingefahamu kama kuna
mpango mkubwa
umepangwa wa kuniua.Kwa
hili alilonifanyia Joe hata
yeye mwenyewe
amehatarisha maisha yake
lakini amefanya hivi
kutokana na mapenzi
makubwa aliyonayo
kwangu.Ananipenda mno na
siku zote amekuwa
ananitaka tuwe wapenzi
lakini moyo wangu umekuwa
mgumu kufunguka
kwake.Moyo wangu bado uko
kwa Mathew Mulumbi.Bado
kuna kitu ndani ya nafsi
yangu kinaniambia Mathew
yuko hai lakini kama
amekufa basi nitakutana
naye huko wanakoenda
wafu.Nampenda Mathew
pekee”akawaza Ruby
akijitazama katika kioo
akaridhika na mwonekano
wake halafu akachukua simu
yake na kuita taksi ikafika
na kumpeleka uwanja wa
ndege wa kimataifa wa
heathrow.
Dakika mbili baada ya
Ruby kuondoka nyumbani
kwake gari moja aina ya Van
lenye rangi nyeusi likafika
nyumbani kwa Ruby
wakashuka watu watatu
waliovaa sare maalum za
kazi wakiwa na kofia
vichwani mwao
wakazunguka mlango wa
nyuma kisha wakafunika
nyuso zao na kuacha macho
wakafungua mlango wa
nyuma na kuingia ndani
mwa Ruby.Haraka haraka
wakaenda katika chumba
cha kulala Ruby wakafungua
kabati ambamo Ruby
aliweka kompyuta yake
ndogo wakaichukua halafu
wakatoka haraka sana.
Watu wale wakiwa ndani
ya nyumba ya Ruby waliweza
kuonekana katika kompyuta
za timu ya MI5 waliokuwa
wakimfuatilia Ruby.Wote
walishangazwa sana na
kitendo cha wale jamaa
kuingia na kuchukua
kompyuta ya Ruby na
kuondoka haraka namna
ile.Hakukuwa na timu yoyote
ya MI5 iliyokuwa karibu na
eneo lile la nyumbani kwa
Ruby kwani timu nzima
ilihamishiwa uwanja wa
ndege alikoelekea Ruby.
Ruby akiwa katika
uwanja wa ndege wa
Heathrow hakuonekana
kuwa na wasi wasi
wowote.Alikuwa amekaa na
abiria wengine wakisubiri
ndege huku akichezea simu
yake.Alipokea simu chache
kutoka kwa marafiki zake
wakimtakia safari njema
“Mungu anisaidie Joe
aweze kufanikisha mpango
wake kwani kama si hivyo
leo ninakwenda
kufa.Ninawaona majasusi
kadhaa wa MI5 wako hapa
uwanjani naamini
wananifuatilia.Ninamuamini
Joe lazima mpango wake
utafanikiwa” akawaza Ruby
Hatimaye abiria
waliokuwa wakisubiri ndege
ile aliyokuwa anaisubiri
Ruby wakatangaziwa
kuingia ndani ya ndege.Ruby
akiwa na abiria wengine
wakaingia ndegeni tayari
kwa safari.Ruby
hakuonyesha wasiwasi
wowote lakini kwa ndani
alikuwa na woga
usioelezeka.Aliketi kitini
akiwa na tabasamu usoni.
“Kweli hawa jamaa
wamedhamiria
kunipoteza.Nimewaona
majasusi wawili wa MI5
wakinifuatilia hadi humu ya
ndege kuhakikisha nimeingia
ndegeni halafu wakatoweka
naamini watakuwa
wameshuka” akawaza Ruby
Baada ya dakika kadhaa
akainuka na kuacha mkoba
wake mdogo pamoja na simu
katika kiti chake ili
kumthibitishia mtu yeyote
kuwa angerejea muda
wowote akaelekea chooni
Gari la ngazi
likaondolewa taratibu na
mlango wa ndege ukafungwa
ishara kwamba ndege
ilikuwa tayari
kuondoka.Ndege ilipoanza
kuondoka taratibu
iligundulika kwamba abiria
mmoja hakuwepo katika kiti
chake huyu alikuwa ni
Ruby.Mkoba na simu yake
vilikuwepo katika kiti chake
na hii ikawafanya
wahudumu waamini kwamba
yawezekana amebanwa yuko
chooni na angerejea.
Gari la ngazi liliambaa
taratibu.Ndani ya gari lile
walikuwamo watu watatu
wote wakiwa wamevaa sare
za wafanyakazi wa kampuni
moja ya upakiaji na upakuzi
wa mizigo.Ukiacha dereva
wengine waliokuwamo ndani
ya gari lile ni Joe na Ruby
aliyekuwa amevaa mavazi
yalimyomfanya muonekano
wake ubadilike.Gari lile
lilikwenda hadi mahala
linakoegeshwa gari dogo la
kampuni ile ya upakiaji na
upakuzi wa mizigo ndegeni
“Ahsante sana Bobby”
akasema Joe na kufungua
mlango akaangalia nje kama
kuna hatari yoyote kisha
akamtaka Ruby ashuke
garini wakaingia katika lile
gari dogo na
kuondoka.Wakati
wakiondoka pale uwanjani
ndege ya shirika la ndege la
Misri aliyotakiwa kupanda
Ruby ikapaa
“Joe nakushukuru sana
kwa jambo hili kubwa
ulilolifanya.Umehatarisha
maisha yako kwa sababu
yangu” akasema Ruby
“Usinishukuru Ruby
bado tuna kazi kubwa ya
kufanya.Natakiwa
kuhakikisha nimekuondoa
hapa nchini kabla
hawajagundua kwamba
hauko ndegeni”akasema Joe
huku akiendesha gari kwa
umakini na uangalifu
mkubwa akichunguza mara
kwa mara kama
wanafuatiliwa.Hatimaye
baada ya mizunguko kadhaa
wakaingia katika nyumba
Fulani ambako waliwakuta
watu watatu.Joe
akawasalimu halafu
akampeleka Ruby katika
mojawapo ya chumba mle
ndani akamtaka abadili
mavazi.Alivaa gauni refu
lenye nakshi za
kupendeza,kichwani akavaa
wigi lenye nywele ndefu
akafunika macho kwa
miwani kubwa myeusi na
kisha akajitanda
ushungi.Alipojitazama
katika kioo
akatabasamu.Haikuwa
rahisi kutambulika.
“Itachukua muda kwa
mtu kuweza kukutambua”
akasema Joe aliyekuwa na
Ruby mle chumbani
akimsaidia katika kubadili
mwonekano
“Ahsante sana Joe.Sijui
bila wewe ningefanya nini”
akasema Ruby .Joe akatoka
akaenda sebuleni kukutana
na wale jamaa waliowakuta
mle ndani baada ya muda
akarejea chumbani alimo
Ruby
“Ruby kompyuta yako hii
hapa.Niliwatuma vijana
wangu waende wakaichukue
mara tu ulipoondoka pale
nyumbani kwako kama
tulivyokuwa tumepanga”
“Ahsante sana
Joe”akasema Ruby na Joe
akachukua bahasha nyingine
ndogo akampatia Ruby
“Humo kuna hati ya
kusafiria yenye jina la
Annabel Jones ambalo ndilo
jina utakalolitumia kuanzia
sasa.Humo ndani ya ndege
kuna tiketi ya treni
utakwenda hadi Paris
Ufaransa na pale utakutana
na binamu yangu ambaye
atakusaidia kuweza kupata
usafiri wa kuelekea kokote
unakotaka kwenda duniani
tayari nimekwisha mpa
maelekezo.Nitakupa kijana
mmoja ataongozana nawe
kukulinda endapo kutatokea
hatari yoyote” akasema Joe
Hakukuwa na muda wa
kupoteza wakaingia garini
na kuelekea katika kituo cha
treni ya kuelekea jijini Paris.
“Joe sina neno zuri la
kukushukuru kwa kuyaokoa
maisha yangu.Sintakusahau
katika maisha yangu”
akasema Ruby baada ya
kufika katika kituo cha treni.
“Ruby ingia ndani ya
treni,jitahidi sana kuchukua
kila aina ya
tahadhari”akasema Joe.Ruby
akaingia ndani ya treni huku
machozi yakimtoka.Joe
hakuondoka pale kituoni
hadi alipohakikisha treni
imeondoka kuelekea Paris
SAA MOJA BAADAE
Taarifa za ndege aina ya
Boeing 747 ya shirika la
ndege la Misri iliyokuwa na
abiria wapato 257 ndani yake
ikitokea London kuelekea
Cairo kupoteza mawasiliano
ikiwa angani zilianza
kusambaa na mamlaka
husika zilianza
kuitafuta.Baada ya saa moja
ilitangazwa kwamba ndege
hiyo ilianguka katika kisiwa
cha Sardina na watu wote
257 waliokuwamo ndani ya
ndege hiyo walipoteza
maisha. Ilikuwa ni taarifa
iliyoistua dunia
RAMALLAH – PALESTINA
Maisha katika kambi ya
kikundi cha Ammar Nazari
Brigades kwa upande wa
Mathew Mulumbi
yaliendelea vizuri.Tayari
amekwisha anza
kushirikishwa katika
masuala mbali mbali
yanayohusiana na operesheni
za kikundi hicho.Amekuwa
karibu sana na Ammar na
kwa muda huu wote
amekuwa akijifunza mambo
mambo mbali mbali
yanayohusiana na
mapambano dhidi ya
Israel.Katika kipindi hiki cha
mwezi mmoja maroketi
kadhaa yalirushwa katika
upande wa Israel lakini
hayakusababisha kifo
chochote.
Jioni moja baada ya
kupata chakula cha usiku
Ammar alimtaka Mathew
akapumzike kujiandaa kwa
safari muhimu siku
inayofuata.Mathew
alipoingia chumbani kwake
akajitupa kitandani alihisi
uchovu mwingi kwani siku
ile walikuwa na mizunguko
mingi.
“Umekwisha pita mwezi
sasa nikiwa na hawa
jamaa.Hakuna shaka yoyote
hadi sasa tayari
wananiamini na tayari mimi
ni mwenzao.Licha ya Ammar
kunipa upendeleo mkubwa
lakini hata watu wengine
nao tayari wamekwisha
niamini na wananipenda.Siri
zao nyingi nimezifahamu
namna wanavyoandaa na
kurusha maroketi upande wa
Israel,mahala yalipo
mahandaki yao,namna
wanavyopata silaha na
mambo mengine
kadhaa.Kubwa ninalolilenga
kwa sasa ni kumtafuta
Habiba Jawad.Toka nimefika
hapa sijawahi kumgusia
lolote Ammar kuhusiana na
Habiba Jaw………..”Mlango
wa Mathew ukagongwa na
kumuondoa mawazoni
akainuka kwenda kuufungua
akakutana na Nawal
aliyekuwa amebeba nguo
zilizokuwa zimefuliwa.
“Nawal kwa nini
usingesubiri hadi kesho
ndipo uniletee hizi nguo?
Wewe ni mke wa mtu na
kuonekana huku kwangu
usiku huu haitaleta picha
nzuri wanaweza wakaanza
kuhisi vingine na tukaharibu
kila kitu”akasema Mathew
“Abu unaponitamkia
mimi ni mke wa Ammar
unanikumbusha machungu
ninayopata kwa uwepo
wangu hapa.Nyote hamjui
kile ninachokipitia lakini
ninayavumilia kwa ajili ya
nchi yangu na watu
wangu.Tuachane na hayo
nimekuja kukupa taarifa
muhimu sana”akasema
Nawal
“Taarifa gani Nawal”
akasema Mathew huku
akjiweka sawa kuipokea
taarifa hiyo.
“Kuna shambulio
linaandaliwa kufanyika
kesho jijini Jerusalem na
wewe ndiye unayepangwa
kwenda kufanya shambulio
hilo” akasema Nawal na
Mathew akastuka sana
“Shambulio?
“Ndiyo.Kuna bomu
linaandaliwa kwenda
kulipuliwa kesho wewe ndiye
utakayebeba
kilipuzi.Nimeona nije
kukutaarifu mapema ili
uanze kujiandaa”
“Nawal kwa nini
tusiwataarifu Mossad
kuhusu shambulio hilo ili
waanze kujiandaa?akauliza
Mathew
“Hapana Abu hatupaswi
kuwajulisha
Mossad.Shambulio hilo
lazima lifanyike na
lifanikiwe ili hawa jamaa
waendelee kuwa na imani
nawe.Endapo Mossad
watafahamu kuhusu
shambulio hilo na
likashindwa kufanikiwa
wanaweza watatafuta kwa
nini siri hiyo imevuja kwani
mpango huu wameuandaa
kwa siri kubwa”akasema
Nawal
“Kwa sasa nchini Israel
ninajulikana kama mtu
hatari gaidi niliyetoroka
gerezani nitaingia vipi
Jerusalem?Mathew akauliza
“Hawa jamaa wana
mtandao mrefu hata ndani
ya Israel hivyo usihofu
wamejiandaa vya
kutosha.Ninachokuomba
hakikisha bomu hilo
linalipuka kesho.Maisha ya
watu wasio na hatia
yatapotea lakini hakuna
namna ya kuweza kuwaokoa
lazima bomu lilipuke ”
akasema Nawal na Mathew
akainamisha kichwa
akafikiri kidogo na kusema
“Nawal siko tayari kwa
watu wasio na hatia
kupoteza maisha huku
nikishuhudia.Lazima
tuwajulishe Mossad”
akasema Mathew
“Abu hapana na
ninakuonya ukithubutu
kufanya jambo lolote na
kusababisha bomu hilo
kushindwa kulipuka basi
misheni yako itakuwa
imefika mwisho
hautafanikiwa tena kumpata
Habiba Jawad .Hawa jamaa
watachunguza na
wakikugundua watakuua na
mimi sintakuwa na msaada
wowote kwako hivyo fanya
ninavyokuelekeza.Wakati
mwingine katika misheni
kama hizi lazima tukubali
kushindwa ili kuupata
ushindi.Umenielewa
Abu?akauliza Nawal
“Nimekuelewa” akajibu
Mathew kwa sauti ya chini
“Ahsante.Tafadhali
usionyeshe kama kuna kitu
kinakusumbua wala usihoji
maswali fanya
utakachoelekezwa na
uonyeshe kufurahia bomu
lile kulipuka” akasema
Nawal na kutoka akimuacha
Mathew katika mawazo
mengi.
”Maisha ya watu wasio
na hatia yanakwenda
kupotea hiyo kesho na mimi
ndiye nitakayebeba swichi
itakayolipua hilo bomu.Mimi
ndiye nitakayetoa roho za
watu hao wasio na hatia.Kwa
nini lakini nimefikia hatua
hii? Ni lazima kuwatoa
sadaka watu hao kwa ajili ya
mtu mmoja tu Habiba
jawad?akajiuliza Mathew
“Lakini ngoja nifuate
ushauri wa Nawal kwamba
natakiwa kuendelea
kujiweka karibu zaidi na
hawa watu ili waendelee
kuniamini na kuniona ni
mwenzao.Lazima bomu hilo
lilipuke” akawaza Mathew
“Kwa miaka mingi
nimekuwa nikipambana na
magaidi hawa wanaoua watu
lakini leo hii nimejiunga nao
na kushiriki katika mauaji
ya watu wasio na
hatia.Damu yote
itakayomwagika kesho
haiwezi kupotea bure lazima
Habiba Jawad apatikane na
hapo ndipo vikundi kama
hivi vya akina Ammar
vitajikuta vikifa taratibu
kwani havitakuwa na vyanzo
vingine vya mapato.Wote
hawa wanamtegemea sana
Habiba kuwapa fedha za
kujiendesha” akaendelea
kuwaza Mathew
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 3
Saa tisa za usiku mlango
wa chumba cha Mathew
ukagongwa akaamka na
kuufungua akakutana na
mmoja wa walinzi wa
Ammar ambaye alimjulisha
Mathew kwamba ajiandae
anahitajika katika kikao
“Mambo
yameanza.Nadhani kikao
hicho ni kwa ajili ya kujadili
mauaji ya watu wasio na
hatia yanayokwenda
kufanyika leo” akawaza
Mathew akiwa bafuni
akinawa uso halafu akatoka
na kwenda kuhudhuria
kikao.
“Habari za asubuhi Abu
Zalawi” akasema Ammar
akiwa katika sura yenye
tabasamu
“Ahsante sana
Ammar.Habari zenu nyote”
akasema Mathew
“Abu samahani kwa
kukuamsha mida hii lakini
kama ujuavyo sisi ni jesho
hivyo hufanya kazi muda
wote” akasema Ammar
“Usijali Ammar
ninalifahamu hilo” akasema
Mathew
“Sasa tumekamilika
tunaweza kuendelea”
akasema Ammar
“Kwa muda wote niliokaa
gerezani mashambulio dhidi
ya Israel yalipungua
sana.Mashambulo
yaliyofanyika si mengi na
waisrael waliouawa idadi
yao bado ni ndogo.Israel
imeendelea kupanua makazi
ya wayahudi katika ardhi
yetu.Nimerudi mwenyewe
kamanda wa vita na
mapambano yanaanza upya
na safari hii lazima Israel
watasalimu Amri”akasema
Ammar na kuwatazama
watu wake waliokuwa
makini wakimsikiliza
“Mwezi mmoja sasa
umepita toka nimerejea na
kipindi chote hicho
tumekuwa tukifanya
maandalizi ya kufanya
shambulio kubwa na sasa
wakati umefika.Tunakwenda
kuanzisha tena vita na Israel
na kuwataka wasitishe
mpango wao wa kupanua
makazi ya wayahudi katika
ardhi yetu.Baadae leo
tutafanya shambulio kubwa
la bomu na kumwaga damu
ya waisrael.Abu Al Zalawi
wewe ndiye utakayeongoza
mapambao haya ya leo na hii
itakuwa ni kazi yako ya
kwanza tangu ujiunge nasi”
akasema Ammar na
kumtazama Mathew ambaye
alitabasamu na kusema
“Nakushukuru sana
Ammar kwa kunichagua
mimi niongoze shambulio la
leo.Nimekuwa nikiisubiri
sana siku kama hii ili niweze
kumwaga damu ya
waisrael.Bado nina hasira
nao sana” akasema Mathew
“Abu Zalawi kauli yako
inadhihirisha wewe kweli ni
mpiganaji.Kwa muda wote
ambao nimekuwa katika
mapambano haya sijawahi
kukutana na mtu ambaye
alifurahia alipopewa jukumu
la kwenda kutekeleza
shambulio la bomu.Ni moja
kati ya mashambulio ambayo
wengi wanayaogopa lakini
wewe umelipokea kwa ujasiri
mkubwa” akasema Ammar
“Ammar nina hasira
kubwa sana na Israel ndiyo
maana najisikia fahari
kubwa kumwaga damu
nyingi ya viumbe hawa”
akasema Mathew Mulumbi
“Mungu atanisamehe
kwa maneno haya lakini
ninafanya hivi ili kujenga
imani kwa hawa magaidi
wakati ninatengeneza njia ya
kwenda kwa Habiba
Jawad.Ninaapa siku za hawa
jamaa zinahesabika kwani
damu hii inayokwenda
kumwagika kwa
mashambulizi haya
haitapotea bure” akawaza
Mathew
Ramani kubwa ikaletwa
na kuwekwa mezani.
“Kesho shambulio
linakwenda kufanyika katika
kituo kikuu cha treni.Kwa
kawaida katika kituo hiki
huwa kuna mkusanyiko
mkubwa wa watu hasa
nyakati za asubuhi.Treni
inapofika kunakuwa na idadi
kubwa ya watu wanaoshuka
na wengine wanaoingia na
hapo ndipo tutalilipua bomu
letu.Abu wewe utakuwa
umejificha sehemu Fulani na
utakuwa na kifaa cha
kulipulia bomu hivyo
shughuli hii nzima
inakutegemea sana
wewe.Hakikisha unalilipua
bomu pale tu ambapo utaona
kuna idadi kubwa ya watu
eneo lilipo bomu” akaelekeza
Ammar.
Majadiliano yakaendelea
kwa muda wa saa nzima na
kisha Mathew akaenda
kujiandaa kwa
safari.Alipewa suti nzuri
mpya ili awe katika
muonekano nadhifu.
“Ee Mungu nisamehe
kwa hili ninalokwenda
kulifanya leo” akaomba
Mathew kabla hajatoka
chumbani kwake.
Gari mbili ziliondoka
katika makazi ya Ammar
kuelekea Jerusalem umbali
wa kama kilometa kumi na
sita.Mida hiyo ilikuwa ni saa
kumi na moja za alfajiri.
Walipita njia zilizojificha
ili kukwepa vizuizi vya
askari na walipofika sehemu
Fulani wakakuta kuna gari
moja limeegeshwa chini ya
mti.Ammar na watu wake
wakashuka na kutoka ndani
ya lile gari walilolikuta njiani
akashuka mwanamke mmoja
mwembamba.Ammar na
Yule mwanamke
wakasalimiana halafu
akamtambulisha Mathew
kwa Yule mwanamke
“Huyu ni mwenzangu
anaitwa Abu Al Zalawi na
ndiye atakayesimamia zoezi
la leo” akasema Ammar na
kumgeukia Mathew
“Abu huyu ni mshirika
wetu anaitwa Nadya yeye
anaishi Jerusalem.Yeye
ndiye atakayewapa kila aina
ya msaada mnaouhitaji ili
kufanikisha zoezi la leo”
akasema Ammar. Nadya
akaaga na na Ammar kisha
sanduku lenye bomu
likaingizwa katika gari la
Nadya.Mathew na kijana
ambaye ndiye atakayebeba
sanduku lile lenye bomu
wakaingia katika gari lile la
Nadya na kuondoka.
“Jukumu langu ni
kuhakikisha mnaingia
Jerusalem na kutekeleza
shambulio lenu hivyo
mtafuata maelekezo
nitakayowapa na sitaki
kuulizwa swali
lolote.Tumeelewana?akauliza
Nadya
“Hakuna tatizo Nadya”
akajibu Mathew
Saa kumi na mbili kasoro
waliwasili jijini Jerusalem na
kuelekea katika nyumba
Fulani wakapumzika na
kupitia tena mpango wa
shambulio lile halafu
wakaondoka kuelekea
mahala ambako kulipangwa
kufanyika shambulio.
Nadya aliegesha gari
katika maegesho ya kituo
cha treni.Watu walikuwa
wengi asubuhi hii wengi
wakitaka kupanda treni
kuwahi makazini na katika
shughuli mbalimbali
“Tumefika” akasema
Nadya.Walitumia dakika
kadhaa ndani ya gari
Mathew akijaribu kufanya
uchunguzi kuona kama kuna
hatari yoyote halafu Yule
kijana akachukua sanduku
na kuungana na abiria
wengine waliokuwa
wakiingia ndani ya kituo kile
cha treni.Kwa muonekano
wake kila mmoja aliamini
kijana Yule ni msafiri kama
wengine na haikuwa rahisi
kumuhisi kama amebeba
bomu kwani alionekana ni
kijana nadhifu na mwenye
maisha mazuri.Nadya na
Mathew nao wakashuka
garini kisha wakaelekea
katika sehemu ya kukatia
tiketi wakaingia ndani .Watu
walikuwa ni wengi ndani ya
kituo .
Treni waliyokuwa
wakiisubiri akina Mathew
ilitangazwa kuwa ndiyo
itakayofuata.Mathew
ambaye alikuwa makini sana
aliweza kumuona vyema
kijana wake akiliweka chini
sanduku lililokuwa na
bomu.Treni ile waliyoishubiri
ikafika na milango
ikafunguliwa watu wakaanza
kushuka huku wengine
wakijiandaa kuingia.Watu
walikuwa ni wengi.Mathew
alimuona Yule kijana wake
akiondoka taratibu eneo lile
huku akiliacha sanduku lake
chini. Mwili ulimtetemeka.
“Ee Mungu nisamehe”
akawaza Mathew kisha
akatoka upande ule na
kuiingia upande wa
kusubiria treni ambako
alimuona Nadya akamfanyia
ishara atoke wakaongozana
kuelekea nje
“Muda umefika” akasema
Nadya
Kwa kutumia kidole
gumba cha mkono wa kulia
Mathew akabonyeza kile
kilipuzi kilichokuwa
mfukoni.Kishindo kikubwa
kikasikika kikiambatana na
moto na moshi
mzito.Kishindo cha mlipuko
ule kilikuwa kikubwa na
kulitetemesha eneo
lile.Mathew akawahi
kumdaka Nadya na
kumkinga.Watu waliokuwa
nje ya kituo walianza
kukimbia hovyo kunusuru
maisha yao.Mathew na
Nadya wakainuka na
kuelekea katika gari lao na
kumkuta Yule kijana wao
akiwasubiri.Wakaingia
garini na kuondoka.
“Kazi nzuri sana
Abu.Mapambano haya
yataendelea hadi Israel
watakapoondoka katika
ardhi yetu” akasema Nadya
“Uko sahihi Nadya ni
wakati wa Israel kulipa uovu
wao” akasema Mathew
“Abu wewe unatokea
wapi? NI nadra sana kuona
mtu mweusi katika
mapambano haya ya Israel
na Palestina” akauliza
Nadya
“Asili yangu ni
Misri.Baba yangu alkiuawa
na majeshi ya Israel hivyo
niliweka kiapo cha
kupambana na Israel.Niliishi
Kenya ambako nilimuua
mkuu wa Mossad Afrika
Mashariki na ndipo
nilipokamatwa na Israel
nikafungwa na gerezani
nikakutana na Ammar
tukafanikiwa kutoroka”
akasema Mathew
“Sipendi maswali kama
haya.Sipendi kurudia
kujieleza mimi ni nani!
Akawaza Mathew
“Unafanya kazi gani
hapa Jerusalem?akauliza
Mathew
“Ninasoma” akajibu
Nadya akiwa makini katika
usukani.Ukimya ulitawala
mle garini
TEL AVIV – ISRAEL
MAKAO MAKUU YA
SHIRIKA LA UJASUSI
ISRAEL (MOSSAD)
“Mimi Ammar Al
Nazari,Bin Khalfan bin Said
kiongozi wa kikundi cha
Ammar Nazari brigades
ninayo furaha kubwa
kuitangazia dunia kwamba
shambulio lililotokea leo
katika kituo kikuu cha treni
jijini Jerusalem
limetekelezwa na kikundi
changu.Kikundi changu cha
Ammar Nazari Brigades
kimepanga kufanya
mashambulizi makubwa
katika miji mbali mbali ya
Israel na kumwaga damu
nyingi ya
waisrael.Kilichotokea leo ni
sehemu ndogo tu ya
mashambulizi makubwa
tutakayoyafanya.Tunataka
walowezi wa kiyahudi
waondoke katika ardhi yetu
na mpango wa kupanua
makazi ya wayahudi katika
ardhi ya wapalestina
usitishwe haraka
sana.Kupuuzia kuyafanya
hayo ni kuruhusu damu zaidi
ya waisrael kumwagika kila
uchao kwani sisi na vikundi
vingine vya kupigania haki
za wapalestina tumejipanga
vizuri na kila siku damu
nyingi itamwagika. Vita hii
haitakoma na itaendelea
viazi hata vizazi hadi pale
tutakapoipata ardhi yetu”
Hii ilikuwa ni video
ambayo ilitoka muda mfupi
baada ya shambulio la bomu
kutokea katika kituo kikuu
cha treni jijini Jerusalem
ikimuonyesha Ammar Nazari
kiongozi wa kikundi cha
Ammar Nazari brigades
akijitapa kikundi chake
kufanya shambulio lile
lililoua watu ishirini na moja
na wengine wengi
kujeruhiwa .
Katika chumba cha
mikakati walimokuwamo
viongozi wa Mossad hali
ilikuwa ya ukimya mkubwa
baada ya kuitazama video
ile.
“Tayari wataalamu wetu
wamekwisha tuthibitisha
kwamba anayeonekana
katika video hiyo ni Ammar
Nazari”akasema Moshe
Levine mkurugenzi mkuu wa
Mossad.
“Ilituchukua muda mrefu
kumpata Ammar na
tunawashukuru CIA ambao
ndio walitusaidia tukaweza
kumpata.Alipokuw gerezani
mauaji kama haya
yalipungua .Tulifanya
maamuzi ya kumuachia
Ammar atoroshwe na
Mathew Mulumbi kwa
mategemeo kwamba
tungeweza kumpata Habiba
Jawad lakini mpaka sasa
umepita mwezi mzima
hakuna mafanikio yoyote
wala mawasiliano yoyote
kutoka kwa Mathew.Kundi
la Ammar brigades limepata
nguvu mpya baada ya
kiongozi wao kutoka gerezani
na tayari limeanza kumwaga
damu ya waisrael.Kama
alivyosema katika video hii
kwamba wamejipanga kwa
ajili ya kufanya
mashambulizi mengine zaidi
ndani ya ardhi yetu”
akasema Moshe na
kunyamaza akawatazama
viongozi wale
“Nataka kufahamu kuna
taarifa yoyote kutoka kwa
Mathew Mulumbi?akauliza
Moshe
“Mpaka sasa hakuna
taarifa zozote kutoka kwa
Mathew Mulumbi.Taarifa
yenye uhakika tuliyo nayo ni
kwamba baada ya kutoka
gerezani Mathew Mulumbi
aliambatana na Ammar
Nazari kuelekea k atika
kambi yao na toka wakati
huo hatujawahi kusikia
chochote kutoka kwa
Mathew Mulumbi” akasema
Efraim Dagan
“Mna uhakika Mathew
Mulumbi bado yuko hai?
Nina wasiw asi yawezekana
Ammar amemgundua kuwa
ni pandikizi na
wamemuua.Lazima tukubali
tulifanya kosa kubwa
kumuachia Ammar na sasa
ameanza
kutushambulia.Hatuwezi
tena kuendelea kumsubiri
Mathew Mulumbi.Hatujui
kama yuko hai au ameuawa
hivyo basi lazima tuchukue
hatua za haraka sana
kumdhibiti Ammar.Watu
waliouawa leo ni wengi na
ameahidi kuendelea
kumwaga damu zaidi hivyo
ni jukumu letu sisi
kuhakikisha mipango yake
hiyo haitimii.Waziri mkuu
amekwisha weka vikosi
katika utayari ili viweze
kuvamia makazi ya
wapalestina na kuanza
msako wa nyumba kwa
nyumba hadi wahakikishe
wanampata Ammar.Njia hii
kama mnavyojua ina
madhara makubwa kwani
maisha ya watu wengi wasio
na hatia hupotea.Waziri
mkuu anataka kusikia
Ammar Nazari ameuawa
hivyo basi suala la Mathew
Mulumbi limekwisha rasmi
na mkakati ulioko kwa sasa
ni kuhakikisha Ammar
anauawa.Wazri
mkuuameniagiza
nizungumze na mkurugenzi
mkuu wa CIA ili waweze
kutupatia taarifa zozote
walizonazo kuhusu Ammar
naili vikosi vya jeshi viweze
kumteketeza yeye na kizazi
chake chote.CIA walitusaidia
awali kumpata Ammar na
ninahakika wanaweza kuwa
na taarifa zinazoweza
kutusaidia kumpata Ammar”
akasema Moshe akionekana
kuwa na hasira
“Mkurugenzi” akaita
Efraim
“Unasemaje Efraim?
“Binafsi bado nina imani
kubwa na Mathew
Mulumbi.Ninaamini ….”
Efraim akanyamaza baada
ya Moshe kumkatisha
“Nini kinakupa imani
kuhusu Mathew Mulumbi?
Suala lake tayari
limefungwa.Kama yuko kwa
Ammar naye atateketezwa
kama wengine ! akasema
Moshe
“Nina imani Mathew
Mulumbi hakuwa
akidanganya.Alikuwa na ya
dhati ya kumpata Habiba
Jawad na vile vile anahitaji
sana kuwa huru.Hawezi
kukimbia kwani anaamini
sisi tuko nyuma yake na
akijaribu kufanya kitu
chochote cha kijinga basi
atakuwa anaiweka familia
yake katika hatari”akasema
Efraim
“Efraim naomba usiwe
na mawazo hayo tena.Yule
jamaa alicheza na akili zetu
na sisi tukajikuta tukiingia
katika mtego wake
tukamuamini akatoroka
gerezani na sasa hatutaweza
tena kumpata.Tumempoteza
yeye na mtu hatari sana
Ammar.Tukubali tulifanya
makosa na sasa faili lake
ninalifunga rasmi” akasema
Moshe
“Mkurugenzi naomba
tulipe muda suala hili ili
tuweze kujiridhisha kama
kweli Mathew yuko kwa
Ammar” akasema Efraim
“Utafanikisha vipi suala
hilo?Una mawasiliano
naye?akauliza Moshe na
Efraim Dagan akabaki
kimya.Alikosa jibu
“Hakuna namna yoyote
ile ya kuweza kufahamu
kama kweli Mathew
Mulumbi yuko na Ammar
Nazari.Aligoma tusimuwekee
kifaa cha kutuwezesha
kumfuatilia kwa kuwa
alikuwa na mipango yake ya
kutoweka na sisi
tukakubali.Tunastahili
mzigo wa lawama kwa haya
yote yanayoendelea kutokea
katika ardhi
yetu.Nawahakikishia dam u
hii iliyomwagika leo na
inayoendelea kumwagwa
yote inatulilia sisi kwa kuwa
tulikubali kumuachia muuaji
aende zake.Sitaki tena
mjadala kuhusu jambo hili
ninachokwenda kukifanya ni
kuzungumza na mkurugenzi
wa CIA kumuomba atusaidie
kufahamu mahala alipo
Ammar na kisha tutatoa
taarifa kwa vikosi vya jeshi
ambavyo viko katika utayari
na kumsambaratisha Ammar
na kizazi chake chote.Hiyo
ndiyo adhabu pekee ambayo
Ammar anastahili” akasema
Moshe
“Mkurugenzi
utanisamehe kwa maswali
yangu lakini nataka
ufafanuzi mdogo.Umesema
mpango ulioko mezani kwa
sasa ni kumteketeza Ammar
kwa bomu endapo
tutafanikiwa kufahamu
mahala alipo.Swali langu ni
vipi kama Mathew Mulumbi
atakuwa bado yuko kwa
Ammar?Ninauliza hivyo kwa
sababu naamini haiwezi
kuwa rahisi kwa magaidi
wale kumuamini Mathew
haraka haraka na kuanza
kumshirikisha katika
mipango yao.Kabla ya
kuletwa hapa makao makuu
nimewahi kuwa andakava
kwa miaka mitatu
nikifuatilia mtandao wa
kuuza silaha kwa magaidi na
si kitu chepesi.Unaweza
ukauawa muda
wowote.Sitaki kumtetea
Mathew lakini kuna kitu
kinaniambia ndani yangu
kwamba Mathew bado yuko
upande wetu na tuvute
subira.Nahisi anajitahidi
kujenga mahusiano mazuri
na Ammar na kundi lake na
pale atakapokuwa
amefanikiwa basi
atatufahamisha.Mkumbuke
kwamba dhumuni kubwa la
Mathew ni kumfikia Habiba
Jawad ambaye ndiye uti wa
mgongo wa makundi karibu
yote ya kigaidi yaliyoko
Palestina ambayo
yanaendelea kumwaga damu
ya watu wetu wasio na
hatia.Tukimuua Ammar bila
kumkamata au kumuua
Habiba Jawad bado
hatutakuwa tumetatua
jambo hili kwani kwani
mauaji,mashambulizi ya
mabomu,maroketi na kujitoa
mhanga havitakoma bado
vitaendelea kila uchao.Kama
Mathew Mulumbi bado yuko
hai basi ni msaada mkubwa
kwetu.Yule ni jasusi na
hastahili kuwekwa katika
kundi la magaidi” akasema
Efraim na ukimya ukatawala
mle ndani
“Efraim umejaribu
kuelezea kwa umakini
mkubwa kuhusu umuhimu
wa Mathew na
ninakubaliana nawe kwamba
kama angefanya kwa mujibu
wa makubaliano yetu basi
kusingekuwa na tatizo lakini
shida inakuja kwamba
hatujui mpaka leo kama bado
ni mzima au
ameuawa,hatujui kama yuko
na Ammar au ametokomea
zake anakojua yeye na
kikubwa zaidi ni kwamba
hatuwezi kusubiri zaidi
kwani Ammar anapanga
mashambulizi
mengine.Efraim naomba
ufahamu si kwamba mawazo
yako ninayapuuza lakini hali
halisi ilivyo unaiona.Ammar
anaendelea kumwaga damu
ya waisrael na hatuwezi
kukaa tukimuangalia
tukitegemea tuna mtu
tumempandikiza katika
kundi lake.Katika hili suala
tukubali kwamba tulijaribu
na tumeshindwa hivyo tuje
na mkakati mpya ambao ni
kumteketeza Ammar na uzao
wake wote.Kama vitaendelea
kuibuka vikundi vingine vya
wanamgambo tutakabiliana
navyo pia.Kama Mathew
Mulumbi bado yupo na
Ammar atatusamehe kwani
hatuna jinsi lazima naye
ateketee.Mimi kama
mkurugenzi mkuu wa
Mossad ninasema
tuhitimishe suala hili na
tuanze kushughulikia suala
la kumuua Ammar Nazari”
akasema Moshe na wakuu
wale wa idara mbali mbali
ndaniya Mossad wakatoka
Baada ya wakuu wale wa
idara mbali mbali
kutoka,Moshe akampigia
simu mkurugenzi mkuu wa
shirika la ujasusi la
Marekani (CIA) Jason
Washington.
“Habari yako Bwana
Moshe” akasema Jason
“Bwana
Washington.Habari za huko?
“Huku kwema
kabisa.Poleni sana kwa
shambulio lililotokea”
“Ahsante sana”akajibu
Moshe
“Nimeiona video ya
Ammar Nazari akijitapa
kutekeleza shambulio
lile,imekuaje akawa huru
wakati alikuwa
gerezani?akauliza Jason
“Ni kweli alikuwa
gerezani lakini kuna jambo
lilitokea hivi karibuni na
Ammar akawa huru”
akasema Moshe
“Sihitaji kujua nini
kilitokea lakini Ammar
hakupaswa kuwa huru”
akasema Jason
“Ni kweli Jason ndiyo
maana nimekupigia kuomba
msaada wako”
“Unahitaji msaada gani
Moshe?
“CIA mlitusaidia mara ya
kwanza tukafanikiwa
kumpata Ammar tunaomba
tena safari hii mtusaidie
tuweze kufahamu mahala
alipo.Hatutaki kumkamata
tena tunataka kumteketeza
yeye na kizazi chake chote”
akasema Moshe na ukimya
wa sekunde kadhaa ukapita
halafu Jason Washington
akasema
“Hilo jambo litakuwa na
gumu kwa sasa.Nasikitika
kusema kwamba hatutaweza
kuwasaidia katika hilo”
“Kwa nini Jason?CIA na
Mossad tumekuwa na
mashirikiano ya karibu kwa
muda mrefu na kusaidiana
kila pale
inapolazimika.Shambulio la
leo ni baya na kama
ulivyoona kwenye video ya
Ammar ametishia kufanya
mashambulizi zaidi.Tunajua
kumkamata tena halitakuwa
jambo jepesi hivyo tunataka
kufahamu mahala alipo ili
tumteketeze kwa bomu”
akasema Moshe
“Moshe kama
nilivyokueleza awali ni
kwamba hatutaweza
kuwasaidia kwa sasa katika
jambo hilo” akajibu Jason
“Jason Marekani na
Israel wote tuko kwenye
mapambano dhidi ya
ugaidi.Tumekuwa na
utamaduni wa kubadilishana
taarifa za kiintelijensia
kuhusiana na mitandao ya
kigaidi au watu wanaosakwa
kwa ugaidi.Mfano mzuri ni
miezi minne iliyopita
majasusi wetu wa
wamefanikiwa kuwakamata
wahusika wawili
waliotekeleza shambulio la
kigaidi huko Florida
waliokuwa wamekimbilia
nchini Misri.Ushirikiano wa
namna hii umekuwepo kwa
miaka mingi ndiyo maana
tumekuja tena kwenu
kuwaomba mtusaidie kupata
taarifa za mahala alipo
Ammar Nazari ili
tumteketeze kabla
hajaendelea kutekeleza
mashambulio yake aliyoahidi
kuendelea
kuyatekeleza.Tafadhali
Jason” akasema Moshe
“Moshe nakubali
mashirikiano yetu na ninyi
ni mazuri na tumefanikiwa
mambo mengi katika
ushirikiano huo lakini katika
suala hili kuna ugumu
kidogo”
“Ugumu gani Jason?
“Ugumu uliopo ni
kwamba tuna mtu wetu
ndani ya kikundi cha Ammar
Nazari brigades ambaye
amepandikizwa kwa kazi
maalum ambayo bado
hajaikamilisha.Kitendo
chochote cha kumkamata
Ammar kwa sasa au kumuua
ni hatari kwa mtu wetu
aliyeko huko ambaye jukumu
lake ni kubwa sana.Endapo
Ammar atakamatwa tena
lazima wataanza kuwa na
hisia kwamba kuna mtu
anatoa taarifa za mahala
alipo hivyo wanaweza
wakaanza kufanya
uchunguzi na wakamgundua
huyo mtu wetu na
kumuua.Kuhusu
kumteketeza Ammar nao niI
mpango hatari kwa mtu wetu
ambaye tumetumia gharama
kubwa kumpandikiza hapo
na anafanya kazi nzuri
sana.Kwa sababu hizo
Moshe siwezi kukusaidia
katika mpango huu”
akasema Jason
“Jason umenishangaza
sana.Kwa muda huu wote
una mtu wako ndani ya
kikundi cha Ammar bila
kutujulisha?Ammar ni mtu
muhimu sana kwetu kwa
sasa.Naomba utusaidie
kumpata tafadhali”
“Moshe mtu wangu
aliyemo katika kikundi cha
Ammar Nazari brigades yuko
pale kwa jambo kubwa sana
na la muhimu hivyo kwa
namna yoyote ile siwezi
kukubali akawa katika
hatari hasa kwa wakati huu
ambao amepiga hatua kubwa
katika kazi tuliyomtuma
akaifanye”
“Moshe una maana
kwamba tumuache Ammar
aendelee kutekeleza mipango
yake ya mashambulizi na
kumwaga damu ndani ya
ardhi yetu?akauliza Moshe
“Tafuteni njia mbadala
ya kuweza kudhibiti mipango
yake lakini kuhusu kumuua
au kumkamata kwa sasa hilo
jambo halitawezekana kwani
kwa kufanya hivyo mtakuwa
mmeharibu misheni yetu ya
muda mrefu.Tuliwasaidia
pale mwanzo mkafanikiwa
kumpata Ammar lakini
mkampoteza.Nimeamua
kukueleza siri hii kwa
sababu Ammar hatakiwi
kuguswa kwa namna yoyote
ile”
“Jason tafadhali
nihakikishie kwamba
humaanishi kauli yako hiyo”
akasema Moshe
“Utanisamehe
Moshe.Ninamaanisha kile
ninachokisema.Naomba
Ammar Nazari asiguswe kwa
sasa kwani mkimgusa kwa
namna yoyote ile mtakuwa
mmevuruga misheni kubwa
ya CIA ambayo imeandaliwa
kwa gharama kubwa na kwa
muda mrefu.Hatuko tayari
kwa hilo” akasema Jason
Washington na Moshe Levine
akavuta pumzi ndefu
“Jason kwa mara ya
kwanza leo umenisikitisha
sana.Siamini kama kweli
CIA wako tayari kumuona
Ammar Nazari akiendelea
kufanya mashambulio katika
ardhi ya Israel na kumwaga
damu ya watu wasio na
hatia” akasema Moshe
“Moshe nimejitahidi sana
kukuelewesha kuhusu
umuhimu wa Ammar na
ninaomba uyazingatie yale
niliyokueleza.Tunafuatilia
kwa makini sana jambo hili
hivyo msijaribu kufanya kitu
chochote kwa siri” akasema
Jason na kukata simu.Moshe
akakasirika na kugonga
meza kwa hasira.
“CIA ni washirika wetu
wakubwa sana lakini leo
nimeshangaa kwa matamshi
ya Jason kwamba wako
tayari Ammar aendelee
kumwaga damu ya waisrael
ili kulinda misheni yao.Siko
tayari kwa hilo .Siko tayari
kumuona Ammar akiendelea
kutamba akimwaga damu za
waisrael” akawaza Moshe na
kuinua mkono wa simu
akampigia katibu muhtasi
wake
“Naomba niletee faili la
Mansur Al Mustapha”
akasema Moshe.Baada ya
muda katibu muhtasi
akaingia na kumletea Moshe
faili la Mansur Al
Mustapha.Akalifungua faili
lile akaanza kupitia ukurasa
baada ya ukurasa.Alilifunika
faili lile akaegemea kiti
chake akafikiri kwa muda
halafu akachukua lile faili
akaelekea lilipo gari lake
akampa maelekezo dereva
sehemu wanakoelekea.
Kutoka makao makuu ya
Mossad Moshe alielekea hadi
katika gereza moja kubwa
wanakofungwa watu wenye
makosa makubwa ya mauaji
na magaidi ambako alitumia
kama nusu saa kisha
akatoka na kuelekea katika
ubalozi wa Marekani ulioko
jijini Jerusalem.Balozi wa
Marekani nchini Israel Sarah
Howard akajulishwa ujio ule
wa mkurugenzi wa Mossad
na akaelekeza akaribishwe
ofisini kwake.Moshe
akakaribishwa ofisini kwa
balozi
“Moshe karibu
sana”akasema Sarah
“Ahsante sana
Sarah.Habari za hapa?
“Nzuri
kabisa.Nimestushwa kidogo
na ujio wako huu wa ghafla”
akasema Sarah
“Usihofu mheshimiwa
balozi nimekuja kwa dharura
kuna kitu nataka
kuzungumza nawe” akasema
Moshe
“Moshe unazidi kunipa
hofu na ujio wako huu.Kuna
tatizo gani?akauliza balozi
Sarah
“Miaka mitatu iliyopita
ubalozi wa Marekani hapa
Jerusalem ulilipuliwa kwa
bomu na takribani watu
sabini waliokuwa
wakifanyakazi katika ubalozi
huo waliuawa na mmoja wa
watu waliouawa katika
shambulio lile ni mumeo
Mike Howard” akasema
Moshe na sura ya Sarah
ikabadilika
ghafla.Alikumbushwa mbali
sana kwani wakati
shambulio lile linatokea yeye
ndiye aliyekuwa balozi na
kwa wakati huo hakuwepo
lakini mume wake ambaye
naye alikuwa ni mfanyakazi
wa ubalozi huo aliuawa.
“Moshe sipendi sana
kukumbushwa kuhusu jambo
hilo kwani bado kidonda
chake hakijapona.Nini hasa
kimekuleta hapa
kwangu?Kama kuna kitu
kingine kimekuleta nieleze
tafadhali na tusizungumzie
suala la yale mauaji”
akasema balozi Sarah.
“Mheshimiwa balozi
kilichonileta hapa kwako ni
hicho.Nataka tuzungumzie
tukio lile.Nafahamu
nimekukumbusha mbali
lakini utanisamehe.”
Akasema Moshe na
kunyamaza kimya
“Toka tukio lile
lilipotokea bado mpaka leo
hii muhusika mkuu wa
shambulio lile
hajapatikana.Najua
ungetamani sana kumuona
mtu aliyefanya unyama ule
akipatikana na haki
kutendeka” akasema Moshe
“Ni Mungu pekee
anayejua ni mateso gani
niliyoyapita na ninayoyapitia
kwa kifo cha mpenzi wangu
Mike.Alikuwa ni kila kitu
kwangu na pengo lake
halitazibika.Kingine
kinachoniumiza ni kwamba
kama ningekuwepo ofisini
siku ile na mimi pia
ningekuwa katika orodha ya
waliofariki.Nimekuwa
nikifuatilia mara kwa mara
kujua kama waliotekekelza
shambulio lile
wamekamatwa lakini mpaka
leo hi hawajakamatwa.Hili
linaniumiza sana” akasema
balozi Sarah Howard.Baada
ya muda mfupi Moshe
akasema
“Mossad tunamfahamu
aliyefanya shambulio lile”
“Mnamfahamu?akauliza
Sarah kwa mshangao
“Ndiyo tunamfahamu”
“Mungu wangu ! kwa
muda huu wote tumekuwa
tukimsaka mshambulaji
huyo kwa nini hamjatupa
taarifa?akauliza Sarah
“Muuaji huyo amefungwa
katika gereza moja hapa
Israel kwa makosa hayo hayo
ya mauaji.Ni mtu muhimu
sana kwetu hivyo hatuwezi
kumkabidhi kwa Marekani”
“Marekani na Israel
tumekuwa na mashirikiano
makubwa hasa linapokuja
suala la kupambana na
ugaidi.Moshe tafadhali
naomba mtu huyo
akabidhiwe kwa Marekani ili
aweze kupatiwa adhabu
stahiki kwani mauaji
aliyoyafanya ni ya kinyama
sana” akasema Sarah
“Sarah ni kweli
ulichokisema kwamba
Marekani na Israel
tumekuwa na mashirikiano
makubwa hasa linapokuja
suala la kupambana na
ugaidi.Lakini kuna sababu
kwa nini hatujawajulisha
CIA kuhusu kukamatwa kwa
mtu aliyefanya shambulio
lile baya.Hata hivyo
nimekuja kwako kukupa
taarifa hii kwa kuwa nina
hakika una kisasi na huyo
mtu na ungependa kumuona
akipata adhabu stahiki”
akasema Moshe
“Sijakuelewa Moshe
unamaanisha nini?
“Kuna kitu nakihitaji
hivyo kama ukinisaidia
kukipata basi nitakupatia
huyo muuaji” akasema
Moshe na balozi Sarah
akapiga piga kalamu katika
meza yake
“Unataka nini Moshe?
` “Nataka kupata orodha
ya majasusi wa siri wa
Marekani walioko hapa
Israel na Palestina na
misheni zao” akasema
Moshe.Balozi Sarah alistuka
sana
“Unataka orodha ya
majasusi wa Marekani?
“Ndiyo”
“Kwa nini?
“Sarah sitaki
kuzungumza kwa undani
suala hilo lakini kama
unataka kuiona haki
ikitendeka kwa mtu
aliyemuua mume wako na
watu wengine basi nisaidie
niweze kupata hiyo orodha”
akasema Moshe na Sarah
akasimama
“Moshe hilo nijambo
lisilowezekana.Hayo ni
mambo ya siri kubwa na
mimi sina uwezo wa
kuyapata na hata kama
ningekuwa na orodha hiyo
siwezi kukupatia”
“Sarah naomba nikuweke
wazi kwamba Mossad haina
lengo baya na orodha ya
majasusi hao.Labda
nikueleze japo kidogo kwa
nini ninataka orodha
hiyo.Umesikia shambulio
lililotokea leo asubuhi katika
kituo cha treni na kuua watu
wengi.Aliyetekeleza
shambulio lile anaitwa
Ammar Nazari.CIA wana
taarifa za mahala alipo
Ammar
Nazari.Nimezungumza na
mkurugenzi mkuu wa CIA
nikamuomba anisaidie kujua
mahala alipo Ammar lakini
alikataa kwa madai kwamba
kuna jasusi wa siri wa CIA
yuko katika kundi hilo la
Ammar akitekeleza misheni
maalum.Sisi pia tuna mtu
wetu ndani ya kundi hilo
lakini tumepoteza
mawasiliano naye na hatujui
kama bado yuko hai hivyo
tunataka kumtumia jasusi
huyo wa CIA kuweza kujua
kama mtu wetu huyo yuko
hai.Jambo lingine ni kwamba
jeshi la Israel linajiandaa
kufanya mashambulizi ya
anga katika kambi mbali
mbali za wanamgambo na
kuna hatari mojawapo ya
kambi hizo ni ya Ammar
hivyo basi maisha ya jasusi
wa CIA yako
hatarini.Ninataka kuokoa
maisha yake kabla majeshi
yetu hayajaanza kufanya
mashambulizi” akasema
Moshe.Sarah akafikiri kidogo
na kusema
“Kama mkurugenzi wa
CIA alikataa kukupa orodha
hiyo basi kuna sababu ya
msingi sana halafu mambo
kama haya ni ya siri kubwa”
“Nalifahamu hilo Sarah
ndiyo maana nimekufuata
wewe” akasema Moshe.Sarah
akafikiri na kusema
“Moshe natamani sana
kama ningeweza kuipata
orodha hiyo unayoitaka
lakini sina uwezo wa
kuipata”akasema Sarah
“Unao uwezo wa kuipata
taarifa hiyo Sarah.Naamini
unao watu ndani ya CIA
ambao unaweza ukawatumia
kuipata taarifa hiyo na mimi
nikakubabidhi mtu huyo
ambaye unaweza ukamfanya
unachokitaka” akasema
Moshe na kumfanya balozi
Sarah azame
mawazoni.Moshe akafungua
mkoba wake na kutoa faili
akaliweka mezani
“Huyo ndiye aliyelipua
ubalozi wa Marekani na
ndiye aliyemuua mumeo”
akasema Moshe na Sarah
akalifungua faili lile akaanza
kulipitia.Kila alivyofungua
ukurasa sura yake ilizidi
kubadilika
“Mtu huyu aliwahi
kufanya kazi CIA?akauliza
Sarah kwa mshangao
“Ndiyo alikuwa ni jasusi
wa CIA.Nilifanya naye
mahojiano kabla ya kuja
hapa” akasema Moshe na
kutoa diski mweko(flash disc)
akampa Sarah ambaye
aliichomeka katika
kompyuta yake na kuanza
kuangalia mahojiano ya
Moshe na mtu ambaye
alilipua ubalozi wa Marekani
Video ilianza kwa Moshe
kuonekana peke yake ndani
ya chumba lakini baada ya
dakika chache akaingia mtu
mmoja aliyekuwa
amefungwa pingu miguu na
mikono akaketi kitini na
Moshe akaanza kumuhoji
“Mansur Al Mustapha”
akasema Moshe
“Unaendeleaje?Vipi
maisha ya
gerezani?akauliza.Mansur
akamtazama kwa macho
yaliyojaa hasira kubwa.
“Kitu gani kimekuleta
hapa? Akauliza Mansur
“Mansur nimekuja hapa
kuzungumza nawe jambo
muhimu sana”
“Mimi nawe hatuna cha
kuzungumza”
“Tunacho cha
kuzungumza” akasema
Moshe na kunyamaza
akamtazama Mansur kwa
makini kisha akasema
“Muda mfupi kabla ya
kuja hapa nimetoka
kuzungumza na mkurugenzi
mkuu wa CIA Jason
Washington.Kuna taarifa
nyeti sana nilikuwa
nazihitaji kutoka kwake na
hakuwa tayari kunipatia
taarifa hizo vivyo
nikamuahidi kumpatia kitu
chenye thamani kubwa ili
anipe taarifa hiyo.Bado
sijamwambia kama kitu
hicho ninachotaka kumpatia
ni wewe” akasema Moshe na
kumtazama tena Mansur
kwa sekunde kadhaa
“Marekani wanakutafuta
sana ila hawajui kama
umefungwa hapa.Ninataka
nikukabidhi kwa Marekani
lakini kabla sijafanya hivyo
nimeona nije nizungumze
nawe kwanza” akasema
Moshe
“Unataka nini kutoka
kwangu?akauliza Mansur
“Mansur ulikuwa jasusi
wa Marekani umefanya kazi
CIA kwa muda mrefu
ukitumika katika eneo la
mashariki ya kati lakini ni
wewe ambaye ulilipua
ubalozi wa Marekani jijini
Jerusalem na kuua watu
kadhaa na miononi mwao
wapo waisrael.Nataka kujua
kwa nini ulibadilika na
kushambulia ubalozi wa
Marekani?akauliza Moshe
Mansur akatazama chini
“Najua umeulizwa swali
hili mara nyingi na hujawahi
kunijbu lakini leo nataka
unijibu kwani niko hapa kwa
ajili ya kukusaidia” akasema
Moshe.Mansur alionekana
kukasirishwa na swali lile
akamtazama Moshe kwa
macho makali kisha akasema
“Ndege za marekani
ziliangusha bomu katika
hoteli ambayo familia yangu
walikuwa wamefikia jijini
Damascus.Mke wangu na
watoto wawili wakafariki
dunia.Niliumia mno kwa
kitendo hicho ingawa
waliomba radhi baadae
wakidai ni bahati mbaya
lakini baada ya kufuatilia
nikagundua haikuwa bahati
mbaya kwani kuna mtu
walikuwa wamemlenga
aliyekuwamo ndani ya ile
hoteli ndiyo maana
wakailipua.Hiyo ndiyo
sababu ya kuamua kulipua
ubalozi wa Marekani jijini
Jerusalem” akasema
Mansur.
“Huyo unayemona hapo
ndiye Mansur Al Mustafa
ambaye alilipua ubalozi wa
Marekani na mumeo
akafariki” akasema Moshe
huku Sarah akiirudia
kuitazama video ile
“Moshe namuhitaji huyu
mtu ! akasema Sarah kwa
hasira
“Nisaidie niweze kuipata
orodha hiyo haraka nami
nitakukabidhi mtu huyu”
akasema Moshe.
Sarah alichukua simu
yake akapiga namba Fulani
akazungumza na mtu kwa
takribani dakika kumi halafu
akaombwa asubiri
“Kuna mtu wangu yuko
makao makuu ya CIA
nimezungumza naye
anisaidie niweze kuipata
taarifa hiyo.Ni mtu mzito
hivyo usiwe na wasi
wasi.Tuvute subira” akasema
Sarah na kuendelea
kuitazama video ile ya Moshe
na Mansur
“Nilikuwa naota siku
moja niweze kukutana na
muuaji Yule na leo
amepatikana” akawaza
Sarah akiuma meno kwa
hasira.
Zilipita dakika kumi ofisi
ikiwa kimya simu ya sarah
ikaita akaipokea akapewa
maelekezo Fulani halafu
akafungua katika barua pepe
yake na kukuta kuna ujumbe
katumiwa akaufungua
akausoma.Ilikuwa ni orodha
ya majasusi wa Marekani
walioko katika nchi za
Israel,Palestina,Misri,Iran,Ir
aq,Syria na Jordan.
“Tayari nimeipata orodha
hiyo lakini sintakupatia hadi
pale nitakapokuwa nimemtia
mikononi muuaji wa mume
wangu” akasema Sarah
“Usiwe na
shaka.Nitakupeleka kwenda
kumuona mtu huyo kisha
utaamua mwenyewe
umfanye nini” akasema
Moshe wakatoka na kuingia
katika gari la Moshe
wakaelekea katika gereza
alikofungwa Mansur.
“Tumefika gerezani.Hapa
ndipo alipofingwa mtu huyo”
akasema Moshe.Sarah
akavuta pumzi ndefu halafu
akasema
“Moshe mtu huyo nataka
nimhukumu mimi
mwenyewe” akasema Sarah.
“Usihofu kuhusu hilo”
akasema Moshe.Waliingia
ndani ya gereza
wakasalimiana na mkuu wa
gereza.Moshe akazungumza
naye kwa muda muda na
mkuu wa gereza akatoa
maelekezo.Mansur akatolewa
ndani ya gereza akiwa
amefunikwa mfuko kichwani
akaingizwa katika gari la
Moshe
wakaondoka.Hakukuwa na
mazungumzo garini.Sarah
alikuwa anafuta machozi
mara kwa mara.Kitendo cha
kukutana na mtu aliyemuua
mume wake kilimuumiza
sana.
Walifika katika nyumba
Fulani akapiga honi na geti
likafunguliwa wakaingia
ndani.Moshe akatoa
maelekezo Mansur akatolewa
garini akaingizwa katika
chumba maalum.
“Sarah hapa ni nyumba
yetu ya mahojiano.Ni
sehemu ya mateso.Hapa
ndipo utakapotoa hukumu
yako kwa mtu aliyemuua
mumeo.Kuna mabadiliko
yoyote?akauliza Moshe
“Siwezi kubadilisha
mawazo yangu
Moshe.Ninataka
kumuhukumu kwa mkono
wangu”akasema Sarah na
Moshe akamuongoza hadi
katika chumba maalum
ambacho Mansur alikuwa
amewekwa.Moshe akautoa
ule mfuko kichwani kwa
Mansur kisha akasogea
pembeni akamuacha Sarah
akiwa amesimama karibu na
Mansur.Uso wake ulijaa
hasira
“Mansur Al
Mustafa.Miaka mitatu
iliyopita ulilipua ubalozi wa
Marekani na kuua watu
wengi miongoni mwa watu
waliouawa alikuwepo pia
mume wangu.Baada ya
kukutafuta kwa muda mrefu
hatimaye leo
umepatikana.Sintakupeleka
Marekani nitakuhukumu
hapa hapa kwa mkono
wangu”akasema Sarah huku
akielekea katika meza
iliyokuwa na vifaa vingi vya
kutesea.
“Sarah kabla hujaendelea
na zoezi naiomba kwanza ile
orodha” akasema
Moshe.Sarah akachukua
kompyuta yake na kumtumia
Moshe ile orodha.
“Sasa unaweza
kuendelea” akasema Moshe
baada ya kuhakikisha
ameipata orodha ile na
kuituma kwa katibu wake
muhtasi ili kuipitia
Sarah akachukua kisu
kikali na kumfuata Mansur
akamuamuru asimame lakini
Mansur akagoma.Sara
akainua kiti na kumpiga
nacho kichwani Mansur
akaanguka chini na damu
zikaanza kumtoka kichwani
mahala alikochanika.Moshe
akamfuata akamuinua na
sara kwa kutumia kile kisu
kikali akaichana chana nguo
aliyokuwa ameivaa Mansuri
akabaki mtupu
“Unataka kunifanya nini
kahaba wewe?! Akauliza
Mansur na kumtemea mate
Sarah ambaye alipandwa na
hasira zaidi na kukipisha
kisu kile kikali kwa nguvu
katika uume wa Mansur
ukaanguka chini.Mansur
akapiga kelele kubwa.Sarah
akazidi kupandwa na hasira
akamfuata pale chini
akamkalia kifuani.
“Uliwaua watu bila
huruma na leo ni zamu yako
kupata mateso waliyoyapata
! akasema Sarah na
kukiingiza kisu kile mdomoni
akamkata ulimi.Kama hiyo
haitoshi akaanza kumchoma
choma na kisu kile usoni
akamtoboa ,macho yote
mawili.Ndani ya muda mfupi
Mansur hakuwa
akitazamika.
“Nipe bastora! Akasema
Sarah na Moshe akampa
bastora iliyokuwa na
kiwambo cha sauti akaanza
kummiminia risasi Mansur
hadi zilipokwisha kwenye
bastora.Tayari Mansur
hakuwa na uhai
tena.Akamtazama kwa
hasira
“Natumai umekwisha
kutana na wale wote
uliowakatili uhai kikatili
shetani we! akasema
Sarah.Alikuwa amechafuka
damu mwili mzima
“Moshe ahsante.Huko
aliko mume wangu atafurahi
nimemlipia kisasi.Sasa nina
amani.Nipeleke nyumbani
kwangu” akasema
Sarah.Moshe akamuingiza
katika chumba kingine kwa
ajili ya kunawa kuondoa
damu zilizotapaka kila
sehemu mwilini.Moshe
akatoa maelekezo ya
kufanyiwa usafi mle
chumbani wakaondoka hadi
nyumbani kwa balozi Sarah
wakaagana
“Moshe suala hili ni siri
kubwa kati yetu tafadhali
asifahamu mtu yeyote”
akasema Sarah akashuka
garini na kuingia
ndani.Moshe akaondoka
kurejea makao
makuu.Aliitisha kikao cha
dharura cha wakuu wa idara
ndani ya Mossad na kuwapa
taarifa za kupatikana kwa
orodha ile ya majasusi wa
siri.Bila kupoteza muda
wakaanza kuipitia orodha ile
na kumpata jasusi aitwaye
Nawal Hashim ambaye
alipandikizwa na CIA katika
kikundi cha Ammar
RAMALLAH
Kuonyesha furaha kubwa
aliyokuwa nayo baada ya
shambulio la bomu
kufanikiwa katika jiji la
Jerusalem Ammar Nazari
alichinja ngamia wawili na
kufurahi pamoja na watu
wake.Kilipikwa chakula
kizuri na watu walikula
nyama huku ngoma
zikipigwa na kucheza
kufuraha kitendo kile cha
kinyama ambacho wao
walikiona ni kitendo cha
kishujaa.Mathew Mulumbi
ambaye ndiye aliyelipua lile
bomu alipongezwa sana na
wenzake wakimuita shujaa.
Wakati sherehe
zikiendelea Nawal aliyekuwa
na wanawake wengine
wakipika chakula,simu yake
ikaita akaitoa katika gauni
lake refu alilovaa na
kutazama mpigaji.Zilikuwa
ni namba ngeni.Kutokana na
kuwepo kwa kelele nyingi za
muziki na ngoma akasogea
pembeni akaipokea ile simu
“Hallow nani
mwenzangu?akauliza
“Nawal tafadhali naomba
kama uko karibu na watu
usionyeshe mstuko wowote
sogea pembeni kuna jambo la
muhimu nataka kuzungumza
nawe” ikasema sauti ya
kiume upande wa pili
“Wewe ni nani unataka
nini?
“Naitwa Moshe Levine
mkurugenzi mkuu wa shirika
la ujasusi la Israel Mossad”
“Kwa nini
umenipigia?Umepata wapi
namba yangu ya
simu?akauliza Nawal kwa
wasiwasi.Alishtuka sana
“Nawal tunafahamu
wewe ni jasusi wa CIA na
uko hapo katika kundi la
Ammar Nazari brigades kwa
misheni maalum” akasema
Moshe na kuzidi
kumshangaza Nawal
“Nashindwa
kukuelewa.Tafadhali
umekosea namba”akasema
Nawal
“Usikate simu
tafadhali.Naomba
unisikilize.Asubuhi ya leo
kumefanyika shambulio la
bomu katika kituo kikuu cha
treni na watu wengi
wamepoteza maisha
shambulio ambalo
limetekelezwa na kikundi
cha Ammar Nazari brigades
na Ammar ametishia
kuendeleza mashambulizi
zaidi.Tayari tumekwisha
gundua mahala alipo Ammar
na hivi ninavyozungumza
nawe jeshila anga la Israel
linajiandaa kufanya
shambulio kubwa sana hapo
katika makazi ya
Ammar.Tunafahamu wewe
ni jasusi wa CIA hivyo
tunataka kukuokoa.Hivi sasa
ndege ziko angani na
ninakupa dakika ishirini tu
za kuondoka mahala hapo
kabla ya eneo hilo kugeuzwa
juu chini kwa mabomu
mazito” akasema Moshe na
Nawal akatazama angani
“Kwa nini CIA
wasinipigie wanijulishe
kama kuna jambo
hilo?akauliza Nawal huku
mapigo ya moyo wake
yakimuenda mbio
“CIA hawajui chochote
kuhusu shambulio hilo”
“Kama hujaelezwa na
CIA umefahamuje kuhusu
mimi? Akauliza Nawal
“Nawal hatuna muda wa
kupoteza.Tafadhali fanya
kile
ninachokueleza.Shambulio
kubwa litafanyika hapo
muda si mrefu.Ondoka hapo
haraka sana” akasema
Moshe na kukata
simu.Nawal
alichanganyikiwa.
“Misheni yangu
imeharibika na siwezi tena
kumpata mtu ambaye
nilikuwa nikimsaka kwa
muda huu wote niliokuwa
hapa.Nimeumia sana lakini
ngoja kwanza nifanye
jitihada za kujiokoa kisha
nitajua
kitakachoendelea.Natakiwa
pia kumuokoa Abu siwezi
kumuacha hapa” akawaza
Nawal na kuelekea mahala
ambako wanamgambo
walikuwa wakicheza ngoma
huku Ammar na Mathew
wakishangilia.Nawal
akamfuata Ammar
akamnong’oneza kitu halafu
Ammar akamshika Mathew
bega akamtaka
waondoke.Nawal
aliwaongoza hadi katika
kijichumba kidogo ambacho
Ammar hukitumia kwa
mazungumzo ya faragha
“Nawal kuna nini mbona
umetuleta humu?akauliza
Ammar huku
akitabasamu.Nawal
akaufunga mlango halafu
akamwambia Ammar
ampatie bastora yake.Ammar
huku bado akishangaa
akatoa bastora na kumpatia
Nawal
“Nawal kuna nini?Mbona
sikuelewei?akauliza Ammar
“Ammar nimekuleta
hapa kuna jambo ambalo
nataka ulifahamu”
“Jambo gani
Nawal?akauliza Ammar
“Kuhusu mimi”
“Kuhusu wewe?akauliza
Ammar kwa mshangao
“Huyu Nawal anataka
kufanya kitu gani tena?
Anataka kumweleza Ammar
ukweli yeye ni nani? Mathew
akajiuliza
“Kwa muda wote tuliokaa
wote nikiwa mke wako
hujafanikiwa kunifahamu
lakini mimi ni jasusi wa CIA
na niko hapa kwa misheni
maalum”
“Nawal ! akasema
Mathew
“Abu nyamaza ! akafoka
Nawal.Sura ya Ammar
ilibadilika
“Sijakuelewa Nawal !
akasema Ammar huku sauti
yake ikiwa na kitetemeshi
ndani yake
“Nimekwambia mimi ni
jasusi kutoka shirila la
ujasusi la Marekani CIA na
niko hapa kwa misheni
maalum” akasema Nawal na
Ammar akamtazama kwa
macho makali yaliyoonyesha
ukatili mkubwa.
“Nawal haya
unayonieleza ni ya
kweli?akauliza
“Ndiyo.Mimi ni CIA”
akajibu Nawal na ghafla
Ammar akachomoa kisu na
kutaka kumrushia Nawal
lakini Mathew aliyekuwa
karibu yake akamuwahi
akamrukia na kumuangusha
chini akamtandika ngumi
mfululizo uso wa Ammar
ukaloa damu.
“Abu zalawi kwa nini
unanifanyia hivi?
Unaungana na huyu
shetani?akauliza Ammar na
Mathew akamtandika ngumi
nyingine nzito kisha
akainuka.Nawal
akakichukua kile kisu cha
Ammar
“Shetani ni wewe ambaye
umeua watu wengi bila
huruma na sasa ni zamu
yako” akasema Nawal na
kukizamisha kile kisu
shingoni mwa Ammar
akakichomoa na kukichoma
tena halafu akachoma
kifuani mahala ulipo
moyo.Mathew alikuwa
amesimama akiangalia
“Kwa nini
umemuua?akauliza Mathew
lakini Nawali hakumjibu
akampatia kisu
“Mkate kichwa haraka
sana! Akasema Nawal na
Mathew akafanya kama
alivyoelekezwa akamkata
Ammar kichwa chake
“Huu ndio mwisho wa
Ammar Nazari brigades”
akasema Nawal halafu
akachukua simu yake na
kuupiga picha mwili wa
Ammar
“Sasa ni wakati wa
kuondoka mahala hapa”
“Tunakwenda wapi?
“Abu sitaki maswali
nataka ufuate maelekezo
yangu” akasema Nawal
Mathew akajifuta damu
mikononi halafu wakatoka
hadi chumbani kwa Ammar
na kuchukua simu pamoja na
kitabu chenye jalada gumu
jekundu ambacho Ammar
hukitumia kuhifadhi kumbu
kumbu zake
muhimu.Wakachukua pia
bastora kadhaa
“Tuondoke” akasema
Nawal wakaingia katika gari
dogo la Nawal alilopewa
zawadi na Ammar
wakaondoka.Geti la kuingilia
katika makazi ya Ammar
likafunguliwa na gari la
Nawal likatoka.Hakuna
aliyemuuliza chochote kwani
wanalifahamu gari lile.
“Nawal umenishangaza
sana.Nini kimesababisha
ukafanya vile?Kwa nini
umeamua kumuua
Ammar?Tunaelekea
wapi?akauliza Mathew
wakiwa garini lakini Nawal
hakumjbu kitu akaongeza
mwendo wa gari
Dakika chache baada ya
kuondoka katika makazi yale
ya Ammar simu ya Nawal
ikaita,akaitambua namba ile
ilikuwa ni ya Moshe
Levine,akasimamisha gari na
kuipokea simu
“Nawal tayari
umekwisha ondoka?akauliza
“Ndiyo nimekwisha
ondoka”
“Naomba unithibitishe
kwamba Ammar yuko katika
makazi yake”
“Ndiyo nimemuacha
pale,wanasherehekea
mafanikio ya shambulio lile
walilolifanya leo ” akasema
Nawal
“Nawal nilisahau
kukuuliza pale awali.Kuna
mtu anaitwa Abi Al Zalawi
umewahi kumuona?
Alitoroka gerezani akiwa na
Ammar” akauliza Moshe na
Nawal akageuka kumtazama
Mathew
“Hapana sijawahi
kumuona huyo mtu” akajibu
Nawal
“Ahsante Nawal.Kama
kuna msaada wowote
utauhitaji tafadhali nijulishe
lakini usirejee tena katika
makazi yale ya Ammar
kwani muda mfupi ujao eneo
lote hakutakuwa na makazi
tena” akasema Moshe na
kukata simu.Nawal
akawasha gari safari
ikaendelea
“Ulikuwa unazungumza
na nani?akauliza Mathew
“Nitakueleza kila kitu
lakini kwa sasa kuna kitu
ambacho tunatakiwa
kukishuhudia” akasema
Nawal akazima gari
wakashuka na kupanda
katika kilima kidogo na
kutazama walikotoka
“Tunatazama nini
Nawal?Mathew akauliza
lakini Nawal hakumjibu kitu
Baada ya dakika mbili
moshi mkubwa mweusi
ukaanza kuonekana angani
na kwa mbali kishindo cha
milipuko ya mabomu
kikasikika
“Israel wameshambulia
kambi ya Ammar Nazari
brigades.Huu ndio mwisho
wa kikundi hiki” akasema
Nawal na Mathew
akashangaa
“Israel wamefahamuje
mahala alipo
Ammar?akauliza Mathew
“Niliyekuwa nazungumza
naye simuni ni Moshe Levine
mkurugnzi wa Mossad
ambaye alinipigia simu na
kunitaka niondoke mahala
pale haraka sana kwani
majeshi ya Israel
yanategemea kufanya
shambulio”
“Moshe ndiye
aliyekupigia simu?Mossad
wamefahamuje kuhusu
wewe? Wamejulishwa na
CIA?akauliza Mathew
“Kwa mujibu wa Moshe
Levine CIA hawajui chochote
kuhusiana na hiki
walichokifanya
Israel.Sifahamu wamewezaje
kupata namba yangu ya
simu”akasema Nawal
“Wamekuuliza chochote
kuhusu mimi?
“Ndiyo lakini
nimemdanganya.Nimemwam
bia kwamba sijawahi
kukuona.Mossad hawana
mpango nawe tena na
walitaka ufe katika
mashambulio yale” akasema
Nawal na ukimya mfupi
ukapita
“Kwa sasa tunaelekea
wapi ? Akauliza Mathew
“Misheni yangu ya
kumtafuta Abdul Yasin Al
Nasser tayari
imevurugika.Natakiwa
kuwajulisha CIA kuhusu
kuvurugika kwa misheni
yangu ili wanipe maelekezo
mengine.Kuhusu wewe
nitakusaidia uweze kufika
kwa Habiba Jawad na
ukamilishe misheni yako”
akasema Nawal
“Unafahamu alipo
Habiba Jawad?akauliza
Mathew
“Sifahamu alipo lakini
hapa tunayo simu ya Ammar
na hiki kitabu ambacho
huandika mambo yake ya
muhimu.Naamini tunaweza
kupata taarifa muhimu
kuhusu Habiba Jawad”
akasema Nawal
“Nawal nina
wazo”akasema Mathew na
kunyamaza baada ya
kishindo kikubwa
kusikika.Mashambulizi ya
mabomu yaliendelea katika
kambi ya Ammar
“Una wazo gani
Abu?akauliza Nawal
“Habiba Jawad amekuwa
ndiye mfadhili mkuu wa
makundi haya ya
wanamgambo na magaidi na
ninaamini lazima atakuwa
anamfahamu Abdul Yasin Al
Nasser.Tujitahidi kufanya
kila linalowezekana tuweze
kufika kwa Habiba” akasema
Mathew
“Ni wazo zuri lakini
kabla ya kufanya chochote
lazima kwanza niwajulishe
CIA kile kilichotokea”
akasema Nawal na kupiga
makao makuu ya CIA
akawajulisha
kilichotokea.CIA walimtaka
aende haraka sana katika
ubalozi wa Marekani nchini
Israel ulioko katika jiji la
Jerusalem.
“Jambo hili lililofanywa
na Mossad kumuua Ammar
limewashangaza sana CIA
hawakuwa
wamelitegemea.Hata hivyo
wamenitaka niende katika
ubalozi wa Marekani
Jerusalem lakini sintaenda
huko tunaendelea na
operesheni yetu lazima tufike
kwa Habiba Jawad” akasema
Nawal
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Wakati taarifa ya
kuanguka kwa ndege ya
shirika la ndege la Misri na
kuua abiria wote
waliokuwemo ndani yake
zikiendelea kusambaa kwa
kasi duniani kote,Rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania Dr Fabian Kelelo
alikuwa ofisini kwake
amechanganyikiwa.Kilichom
canganya ni kuliona jina la
Ruby Rafael Magalla katika
orodha ya abiria
waliokuwemo
ndegeni.Alijaribu kumpigia
Austin lakini simu iliita bila
kupokelewa.Akiwa amejawa
na mawazo mengi simu yake
ikaita zilikuwa ni namba
ngeni zilizotoka nje ya nchi
akaipokea
“Hallow” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais
unazungumza na Ruby”
“Ruby?! Akashangaa Dr
Fabian na kusimama.
“Ruby ni wewe kweli?
“Ndiyo mheshimiwa Rais
ni mimi”akasema Ruby na Dr
Fabian akavuta pumzi ndefu
na kuinua mkono juu
“Mungu wangu kweli una
nguvu.Ahsante baba”
akasema kwa sauti ndogo
“Ruby nimeliona jina
lako katika orodha ya abiria
waliokuwamo ndani ya ndege
iliyoanguka ya shirika la
ndege la Misri na kuua watu
wote.Nilikuwa
nimechanganyikiwa sikujua
nifanye nini”
“Mheshimiwa Rais ni
kweli jina langu limo katika
orodha ya watu waliofariki
katika ajali ile lakini
sikuwamo ndani ya
ndege.Mheshimiwa Rais
nimekupigia kukujulisha
kwamba niko salama”
“Uko wapi kwa sasa?
“Mheshimiwa rais kwa
sasa siwezi kukueleza niko
wapi kwa ajili ya usalama
wangu lakini naomba
ufahamu kwamba niko
salama na sijafa.Niko katika
safari yangu ya kuja
huko.Siwezi kukueleza
nitafika lini lakini naomba
uamini nitafika huko”
akasema Ruby
“Ruby tafadhali naomba
unieleze kama kuna kitu
chochote ninaweza
kukusaidia.Ninaweza
kutuma ndege ije ikuchukue
mahala ulipo”
“Ninashukuru sana
mheshimiwa Rais
ninafahamu unaweza
kunisaidia lakini kwa sasa
usihofi nitakuwa
salama.Nitakujulisha pale
nitakapohitaji msaada
wowote.Ninachokuomba
suala hili liwe ni siri yako
kubwa.Usimueleze mtu
yeyote kama nimekupigia
simu niko hai.” akasema
Ruby
“Ruby kwa nini nisitume
ndege ikaja kukuchukua
mahal aulipo? Kama ni
usalama niko tayari kutuma
kikosi maalum kuhakikisha
una kuwa salama”
“Usihofu mheshimiwa
Rais.Hakuna ulazima wa
kutuma kikosi wala
ndege.Ninakuja Tanzania
lakini itanichukua muda
kidogo ila fahamu kwamba
nitafika niko njiani.Kwa heri
kwa sasa mheshimiwa Rais”
akasema Ruby na kukata
simu
Dr Fabian akashusha
pumzi baada ya Ruby kukata
simu
“Nini kimetokea hadi jina
la Ruby likaonekana katika
orodha ya watu waliofariki
katika ajali ya ndege lakini
hajafa? Nahisi Ruby atakuwa
katika hatari lakini kwa nini
hakunipa nafasi nimsaidie?
Ningeweza kumtumia ndege
mahala alipo pamoja na
ulinzi ili kuhakikisha
anakuwa salama lakini vyote
hivyo amevikataa.Ngoja
niendelee kumsubiri hadi
atakapofika kama
alivyoahidi yeye mwenyewe
naamini anayo siri
kubwa.Mungu amlinde
katika safari yake hii ya
hatari” akawaza Dr Fabian
PARIS – UFARANSA
“Ruby uko tayari kwa
safari?akauliza Joseph
ambaye ndiye aliyempokea
Ruby jijini Paris.
“Niko tayari tunaweza
kuondoka” akajibu Ruby
Waliingia katika gari na
kuondoka kuelekea katika
bandari ya Le havre
“Ruby utanisamehe kwa
usafiri huu utakaoutumia
kwani ndio ambao nimeweza
kuupata kwa haraka lakini
ndio usafiri
salama.Itakuchukua muda
mrefu kidogo kufka Tanzania
ila naamini utafika salama
kuliko kama ungetumia
usafiri wa ndege”akasema
Joseph
“Usijali
Joseph.Ninakushukuru sana
kwa msaada huu mkubwa
ulionisaidia.Nimeupenda
usafiri huu kwani ni salama
zaidi kwangu kwa sasa”
akasema Ruby
“Nahodha wa meli
utakayoondoka nayo ni
ndugu yangu hivyo
atahakikisha unakuwa
salama na unafika salama
huko uendako” akasema
Joseph
Iliwachukua saa mbili
kufika katika bandari ya Le
havre.Meli ambayo alitakiwa
kuondoka nayo Ruby tayari
ilikwisha pakia mzigo na
aliyekuwa akisubiriwa ni
Ruby ili waanze safari.
Joseph alimkabidhi Ruby
kwa nahodha wa meli ile
kubwa ya mizigo wakaagana
na Ruby akaingizwa
melini.Safari ya kuelekea
Afrika ikaanza.
“Kwa heri
Ulaya.Ninarejea katika nchi
yangu ambako nitatumia
ujuzi na maarifa yangu yote
kuitumikia kuliko
kuwatumikia watu hawa
ambao nimewafanyia kazi
kwa uaminifu mkubwa kwa
muda mrefu lakini
hawajauthamini mchango
wangu kwao na badala yake
wanataka kuniua.Huko
waliko wanaamini kwamba
tayari nimekwisha kufa na
lengo lao
limetimia.Namshukuru sana
Joe ambaye ndiye
aliyenisaidia hadi nimefika
hapa.Sikujua kama kuna
mpango wowote unaandaliwa
wa kuniua lakini ni yeye
ambaye alinidokeza uwepo
kwa mpango huo na
akajitolea maisha yake
kunisaidia nikaweza
kuukwepa mtego ule na na
endapo wakigundua kwamba
yeye ndiye aliyenisaidia
nikatoroka lazima
watamuua.Namuomba
Mungu amsaidie aweze kuwa
salama.Safari hii ya majini
ni safari ndefu lakini
nitavumilia kwani ndiyo njia
pekee salama kwa mimi
kufika Tanzania kuliko kama
ningetumia
ndege.Nitavumilia” akawaza
Ruby akiwa amepumzika
katika chumba chake
alichopewa ndani ya meli ile
kubwa ya mizigo
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 4
Geti la kuingilia katika
jumba kubwa la bilionea
Peniela lilifunguliwa na gari
moja likaingia.Watu wawili
wakashuka toka ndani ya
gari lile la kifahari
wakapokewa na Dinah
ambaye ndiye mratibu wa
shughuli zote za
Peniela.Aliwakaribisha
katika sebule kubwa na
nzuri ambayo Peniela
huitumia kukutana na
wageni wake wa
muhimu.Muhudumu alifika
haraka na kuwahudumia
wageni vinywaji .Wakati
wageni wale wakiendelea na
mazungumzo na Dinah
akaingia Peniela ambaye
jioni hii alikuwa amevaa
suruali nyeusi na shati laini
rangi nyeusi vile vile.
“Karibuni
wageni”akasema Peniela na
kuwakaribisha wageni wake
“Tunashukuru sana”
wakasema wageni wale
“Jamani wageni wetu
huyu ndiye bilionea Peniela”
akasema Dinah
“Tunafutahi
kukufahamu.Mimi nilizoea
kukuona katika picha
magazetini ni furaha yangu
leo nimekutana nawe ana
kwa ana.U mrembo sana”
akasema mmoja wa wageni
wale na Peniela
akatabasamu
“Peniela hawa ndio wale
wageni wako
niliokueleza.Yule pale
anaitwa Devotha Adolph na
huyu malaika hapa anaitwa
Melanie David” akasema
Dinah
“Nimefurahi sana
kukutana nanyi jamani
karibuni sana.Dinah
aliniambia kwamba mlitaka
kuonana nami wiki iliyopita
lakini niliomba tuvute muda
kidogo kwani nilikuwa na
matatizo.Nilivamiwa na
watu wasiojulikana na
walinzi wangu wakauawa”
“Pole sana” wakasema
Melanie na Devotha
“Ahsanteni sana”
akasema Peniela
“Niliambiwa kuna jambo
la muhimu mnataka
kujadiliana nami” akasema
Peniela
“Ndiyo madam kuna
jambo limetuleta hapa
kwako.Nisiwe mzungumzaji
mkubwa nimuachie
muhusika mkuu ambaye ni
huyu Melanie aweze
kuzungumza nawe”akasema
Devotha
“Naitwa Melanie Davis
kama nilivyojitambulisha.Ni
mtoto wa pekee kwa wazazi
wangu ambao wote
wamekwisha tangulia mbele
za haki”
“Pole sana” akasema
Peniela
“Ahsante sana”
“Wazazi wangu
wanatokea jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo”
“Ouh kumbe wanatokea
Afrika Mashariki” akasema
Peniela huku akitabsamu
“Ndiyo wanatokea Afika
mashariki ndiyo maana
unaniona ninaweza
kuzungumza Kiswahili
vizuri.Walikuwa wafanya
biashara na makazi yao
yalikuwa Ufaransa lakini
mimi nimesoma elimu yangu
ya juu nchini Tanzania
katika chuo kikuu cha Dar es
salaam.Ninaipenda sana
Tanzania” akasema Melanie.
“Nimefurahi kusikia
umesoma Tanzania.Mimi pia
ni mtanzania japo kwa sasa
nina uraia wa Ufaransa na
kama unavyofahamu
kwamba nchi yetu haikubali
uraia wa nchi mbili.Niliamua
kuukana uraia wangu wa
kuzaliwa kwa sababu mbali
mbali za kiuchumi.Devotha
nawe unatokea wapi?Manake
unazungumza Kiswahili safi
kabisa”
“Mimi pia ni mtanzania
lakini nimeishi sana nje ya
nchi na kwa sasa makazi
yangu ni hapa Paris.Bado
sijachukua uraia wa nchi
nyingine kwani nina mpango
wa kurejea nyumbani siku
moja” akasema Devotha na
Melanie akaendelea
“Wazazi wangu walikuwa
wafanya biashara matajiri
kama
nilivyoeleza.Walipouawa
utajiri wote nilirithi
mimi.Kwa sasa baada ya
kumaliza masomo ninataka
kujikita katika kusimamia
biashara walizoacha wazee
na kuongeza nyingine
zaidi.Ninataka kuwekeza
katika eneo la Afrika
Mashariki ambako
nimeziona fursa nyingi za
kibiashara.Ninataka
kuwekeza sehemu mbali
mbali kama vile kwenye
madini,biashara za vyakula
nakadhalika.Wakati
nikifikiria ni wapi
nitawekeza nilipata tetesi
kwamba kuna mtu anaitwa
bilionea Peniela amewekeza
sana Afrika Mashariki lakini
kwa sasa anataka kuuza
baadhi ya mali zake zilizoko
Afrika mashariki nikaona hii
itakuwa ni fursa nzuri ya
kuja kuzungumza nawe
kama jambo hili ni la kweli
ili niweze kununua mali hizo
kuliko kuanza kuwekeza
kutoka chini” akasema
Melanie.Peniela akanywa
funda dogo la kinywaji na
kusema
“Ni kweli nimewekeza
sana Afrika
Mashariki.Niliamua
kuwekeza sana nyumbani
kabla ya kuwekeza nje ya
nchi.Katika kusimamia
biashara zetu mimi na mume
wangu tuligawana yeye
akawa anasimamia miradi
yetu iliyoko Tanzania na
mimi nikawa nasimamia
miradi iliyoko Ulaya na
Asia.Kwa bahati mbaya
mume wangu amefariki
miaka mitatu iliyopita na
kwa sasa biashara zote
zilizoko Tanzania
zinasimamiwa na rafiki wa
mume wangu anaitwa Papii
Gosu Gosu naye ana asili ya
Congo.Ninataka kuuza
makampuni yangu na
biashara zilizoko Tanzania
kwani siwezi kusimamia
miradi hii yote mingi peke
yangu”akasema Peniela
“Pole sana kwa kifo cha
mumeo” Devotha na Melanie
wakasema
“Ahsante nimekwisha
poa” akajibu Peniela
“Kwa hiyo Melanie ni
kweli ninauza mali zangu
zote zilizoko Tanzania kama
utakuwa tayari tunaweza
kufanya mazungumzo na
nitakupa upendeleo mkubwa
wewe kwani kuna wengi
wameonyesha nia ya
kuzinunua” akasema Peniela
“Peniela kama unauza
mali zako Tanzania mimi
nitazinunua zote tafadhali
usimuuzie mtu mwingine
mali hizo” akasema Melanie
Mazungumzo kati ya
Peniela na wageni wake
yalikuwa marefu na walipata
wote chakula cha usiku pale
pale nyumbani.Peniela
alimuomba Melanie ampe
siku mbili ili aweze kumuita
msimamizi mkuu wa mali
zake nchini Tanzania
pamoja na wanasheria ili
waweze kuanza mchakato wa
kuuziana mali zile
“Sina sababu ya
kuendelea kuishi
Tanzania.Ni nchi yangu
lakini baada ya Mathew
kufariki sina hamu tena ya
kutia mguu wangu kule
ndiyo maana ninataka kuuza
biashara zangu zote ili nisiwe
na sababu yoyote ya
kunipeleka huko.Laiti
kungelikuwa na kaburi la
Mathew ningekuwa na
sababu ya kuendelea
kuwekeza lakini hata kaburi
lake halipo waliniambia eti
mume wangu aliliwa na
fisi.Walimuacha akafa kifo
cha kinyama sana ndiyo
maana wamenifanya niwe na
chuki na nchi yangu.Si
kwamba biashara hazifanyi
vyema kwani yupo Gosu
Gosu anasimamia vizuri
lakini kila nikikumbuka
kuhusu Mathew ninapatwa
na hasira nyingi ndiyo
maana nataka niuze kila kitu
nisiwe na sababu yoyote ya
kwenda tena Tanzania”
akawaza Peniela akiwa
chumbani kwake baada ya
akina Melanie kuondoka.
“Nakumbuka siku ile
kabla ya kuuawa Nahum
aliniambia kwamba
nimtafute Mathew Mulumbi
yuko hai lakini siamini
maneno yake.Amefahamu
vipi kama Mathew yuko
hai?Hajawahi kufika
Tanzania na wala
hamfahamu Mathew ndiyo
maana hata maneno yale
nimeyapuuzia.Mathew
amekwisha fariki na hakuna
namna anayoweza kuwa
hai.Nilitumiwa ujumbe na
Rais wa Tanzania
aliyemaliza muda wake na
kujulishwa kwamba Mathew
alifariki katika operesheni ya
kuwakomboa mateka
waliokuwa wametekwa na
kikundi cha kigaidi cha
IS.Ngoja niachane na hili
suala linaweza kuanza
kunitoa machozi muda huu”
akawaza na kuchukua simu
akampigia simu Gosu Gosu
akamtaka afanye kila
awezalo aende Paris haraka
iwezekanavyo
RAMALLAH - PALESTINA
Mathew Mulumbi na
Nawal walikaa chini ya jiwe
Nawal akikipitia kitabu kile
ambacho Ammar huandika
kumbu kumbu zake mbali
mbali.Kwa muda wa saa
moja toka alipoanza
kukipitia kitabu kile hakuwa
amepata kitu chochote
kinachoweza kuwasaidia
kufahamu au kufika kwa
Habiba Jawad.
“Hakuna kitu cha maana
humu.Yote aliyoyaandika
ndani ya hiki kitabu ni
mambo yanayohusiana na
shughuli zinazofanywa na
kikundi chake”akasema
Nawal na kuzama katika
mawazo.Mathew akapanda
juu ya mwamba ule na
kuangalia kama kuna mtu
yeyote anayemfuata na
akiwa kule juu akasikia sauti
ya Nawal akiimuita
akashuka haraka
“Kuna nini
Nawal?akauliza
“Nimekumbuka
kitu.Kuna mwanamama
mmoja anaitwa Fatma huyu
nadhani ni mshirika wa
Ammar.NImewahi kufika
nyumbani kwake mara mbili
nikiwa na Ammar na yeye
mwenyewe Fatma amewahi
kuja kwetu mara
kadhaa.Kila wanapokutana
huwa wanazungumza
pembeni na hakuna anayejua
huwa wanazungumza
nini.Nilihisi labda watu wale
wana mahusiano ya
kimapenzi na Ammar
anataka kuoa mke wa tatu
lakini akanihakikishia
kwamba Fatma ni mshirika
wake na hawana mahusiano
yoyote.Nadhani Fatma
anaweza akatusaidia
kufahamu au kumpata mtu
anayeweza kufahamu alipo
Habiba Jawad” akasema
Nawal
“Ni wazo zuri
sana.Twende tukajaribu”
akasema Mathew wakashuka
katika mwamba na kuingia
ndani ya gari lao safari
ikaanza kuelekea Ramallah
anakoishi Fatma.
“Nawal usijali utampata
Abdul Yasin Al Nasser.Nina
uhakika mkubwa kama
tukifanikiwa kumpata
Habiba tutajua mahala alipo
Abdul Yasin Al Nasser.Hawa
wote mfadhili wao ni mmoja
Habiba Jawad” akasema
Mathew baada ya kumuona
Nawal akiendesha gari lakini
akiwa na mawazo mengi
“Katika mashambulizi ya
mabomu aliyoyafanya Abdul
baba yangu pia ni mmoja wa
waliouawa hivyo siwezi
kuondoka bila kumpata
Abdul.Lazima nihakikishe
anapatikana”akasema Nawal
Safari iliendelea
wakaingia katikati ya jiji la
Ramallah.Nawal
akapunguza mwendo baada
ya kuingia katika mtaa
Fulani wenye maduka
makubwa.Baada ya mwendo
wa dakika mbili akakata
kulia na kufuata ujia ulio
elekea katika geti la rangi ya
bluu.Akamtaka Mathew
abaki garini akafungua
mlango akashuka na kwenda
kuzungumza na jamaa
mmoja aliyekuwa
amesimama
mlangoni.Walizungumza kwa
muda mfupi na Yule jamaa
akachukua simu akapiga
halafu akafungua
geti.Nawal akarejea garini
akaingiza gari ndani.
Mandhari ya ndani ya
jumba lile yalikuwa ya
kuvutia sana.Kulipandwa
maua mazuri na miti ya
kupendeza.Kulikuwa na
nyumba tatu nzuri na
mojawapo kati ya hizo
ilikuwa ya ghorofa.Kulikuwa
na njia nzuri
zimetengenezwa kueleka
katika kila nyumba.Nawal
akafuata njia iliyoelekea
katika nyumba ya ghorofa
akasimamisha gari nje ya
nyumba ile
“Ni hapa tumefika”
akasema Nawal na kufungua
mlango akashuka Mathew
naye
akashuka.Mwanamamama
mmoja mnene aliyevaa gauni
refu na kujitanda mtandio
mwepesi akatokeza katika
mlango mkubwa wa kuingilia
sebuleni
“Nawal ! akasema Yule
mama
“Fatma” akasema Nawal
na kukumbatiana na Yule
mama halafu akasalimiana
na Mathew
“Karibu sana Nawal”
akasema Yule mama na
kuwakaribisha ndani
akamuita muhudumu
akawahudumia wageni chai
“Nashukuru sana Nawal
kwa kunitembelea.Ammar
niliwasiliana naye jana
lakini hakuniambia kama
utakuja mjini leo” akasema
Fatma
“Fatma kuna jambo
limetokea leo” akasema
Nawal
“Kumetokea
nini?akauliza Fatma
akionekana kuwa na
wasiwasi
“Ammar ameuawa”
“Ameuawa?
“Ndiyo.Ameuawa a vikosi
vya Israel.Vimefanya
mashambulizi katika makazi
yetu.Kwa bahati nzuri
wakati mashambulizi
yameanza Ammar alifanya
kila aliloweza kuhakikisha
ananiokoa mimi na
wenzangu lakini aliuawa
wakati akiwa katika
harakati hizo.Wenzangu pia
hawakubahatika kutoka
salama.Mke mkubwa na
familia yake waliokuwa
katika gari lingine
walilipuliwa na
bomu.Ninamshukuru sana
Abu Zalawi ambaye
alipambana kuhakikisha
ninakuwa salama.Huyu ni
mtu wa karibu na Ammar na
ndiye aliyemsaidia hata
kutoroka gerezani” akasema
Nawal
“Nimestuka
sana.Sijazipat a taarifa hizo
bado.Pole sana Nawal”
akasema Fatma akionekana
kustuka
“Israel wamemtafuta
Ammar kwa muda mrefu
sana na hatimaye
wamefanikiwa
kumpata.Imeniumiza mno”
akasema Fatma na kufuta
machozi
“Asubuhi ya leo nimeiona
video ya Ammar akitangaza
kikundi chake kuhusika
katika shambulio la bomu
lililotokea jijini
Jerusalem.Nilifurahi
sana.Kila mmoja alifurahi
mno kwa kile alichokifanya
Ammar na hakuna aliyejua
kama muda mfupi baadae
angefariki dunia.Hata hivyo
Ammar amekufa
kishujaa.Tutaendelea
kumuenzi siku zote kama
mmoja wa mashujaa
waliomwaga damu yao
akilipigania taifa lake”
akasema Fatma na kufuta
machozi
“Ammar alimtuma Abu
Zalawi kutekeleza shambulio
lile” akasema Nawal na
Fatma akastuka
“Kumbe wewe ndiye
uliyetekeleza shambulio
lile?akauliza Fatma
“Ndiyo ni mimi”
“Hongera sana Abu
Zalawi.Wewe u shujaa
mkubwa” akasema Fatma
“Ukiacha shambulio la
leo asubuhi,Abu Zalawi ndiye
aliyemtorosha Ammar
kutoka gerezani”
“Mungu
mkubwa.Nimefurahi
kukutana nawe
Abu.Yawezekana hauna asili
ya eneo hili lakini u mtu
muhimu sana kwetu”
akasema Fatma
“Nilikuwa nimefungwa
gerezani baada ya kumuua
mkurugenzi wa Mossad
Afrika mashariki pamoja na
majasusi wawili wa Israel
nchini Kenya.Nilikamatwa
na kuletwa Israel
nikafungwa na hapo ndipo
ndipo nilipokutana na
Ammar tukapanga mpango
wa kutoroka gerezani
tukafanikiwa” akasema
Mathew
“Poleni sana Nawal na
Abu.Lakini huu si mwisho
wa mapambano.Kumuua
Ammar hakuwezi
kudhoofisha mapambano ya
kudai haki ya maeneo
yetu.Mapambano
yataendelea” akasema Fatma
“Fatma nimekuja kwako
nataka utusaidie tuweze
kufika kwa Habiba Jawad”
“Habiba Jawad?! Fatma
akastuka.
“Ndiyo” akajibu
Nawal.Fatma akashusha
pumzi.Akafikiri kidogo na
kusema
“Kuna chochote Ammar
amewahi kukueleza kuhusu
Habiba Jawad?akauliza
Fatma
“Ammar hakunielekeza
chochote kwa Habiba lakini
aliwahi kunieleza kuwa ni
mtu muhimu sana
kwake.Ninataka kuonana
naye kwa mambo
mawili.Kwanza ni mimi
mwenyewe nahitaji hifadhi
baada ya Ammar
kuuawa.Pili ni Abu
Zalawi.Ana jambo la
kuzungumza na Habiba”
“Abu unamfahamu
Habiba Jawad?akauliza
Fatma
“Nimekuwa nikimsikia
lakini sijawahi kumtia
machoni”
“Una jambo gani
unalotaka kuzungumza
naye?
“Ni kuhusu mtu anaitwa
Edger Kaka”
“Edger Kaka ni
nani?Fatma akauliza
“Huyu aliwahi kuwa
mbunge katika bunge la
jamhuri ya mungano wa
Tanzania na alikuwa mtu wa
karibu sana na Habiba
Jawad” akasema Mathew
“Sijakuelewa bado Abu”
akasema Fatma
“Naomba nikupe maelezo
kidogo.Makazi yangu
yalikuwa Nairobi Kenya na
ndiko nilikomuua
mkurugenzi wa Mossad
Afrika mashariki.Nikiwa
Nairobi nilifahamiana na na
mtu anaitwa Rashid ambaye
huyu alikuwa ni
mwanachama wa kundi la IS
nchini Kenya.Siku moja
aliniomba nikaungane naye
katika mabadilishano ya
mateka.Alikuwa amewateka
watu wawili ambao ni mtoto
wa Rais wa Tanzania pamoja
na mwanamke mwingine na
Tanzania wao walikuwa
wamemteka Edger
Kaka.Nilikubali kwenda
kumsaidia katika
mabadilishano hayo na
wakati tukibadilishana
mateka hao ndipo likatokea
shambulio kubwa na mimi
kutekwa lakini sikuwa peke
yangu nilitekwa pia na Edger
Kaka tukaletwa
Israel.Nilipewa mateso
makali sana na siku moja
nilipoteza fahamu
nikapelekwa katika hospitali
moja ambako nilipozinduka
nilifanikiwa kumuona Edger
kaka ambaye alikuwa katika
hali mbaya.Ninataka
kuonana na Habiba Jawad
kumueleza kuhusu mtu huyo
ambaye nilielezwa na Rashid
kwamba ni mtu muhimu
sana kwake” akasema
Mathew na Fatma
akatafakari kidogo
“Ndugu zangu naomba
niwaweke wazi kwamba
Habiba si mtu ambaye
unaweza ukaonana naye
kirahisi.lakini kwa sababu ya
Nawal ninaweza kuwasaidia
ila mtapitia mlolongo mrefu
kidogo hadi kumfikia.Abu
umesema huyo mtu ambaye
ulielezwa ana ukaribu na
Habiba Jawad anaitwa
nani?akauliza Fatma
“Anaitwa Edger Kaka”
akasema Mathew na Fatma
akatoka akaenda chumbani
kwake akapiga simu
akazungumza na mtu na
baada ya dakika tatu
akarejea
“Abu una uhakika mtu
ambaye ulitekwa naye ni
Edger kaka? Akauliza Fatma
“Ndiyo nina
uhakika.Baada ya kutekwa
katika yale mabadilishano
nilipelekwa sehemu Fulani
kama pango nikaingizwa
humo na kwa kuwa nilikuwa
nimejeruhiwa kwa risasi
nikaanza kupatiwa matibabu
lakini wakati nikipatiwa
matibabu akaletwa mtu
akalazwa katika kitanda cha
pembeni yangu na
nilipotazama alikuwa ni
Edger kaka.Nilipoteza
fahamu na nilipozinduka
nilijikuta nikiwa katika
gereza nchini
Israel.Niliteswa sana na siku
moja baada ya kupatiwa
mateso makali nilipoteza
fahamu nikapelekwa katika
hospitali ya gereza na ndiko
nilikomuona Edger Kaka
akiwa katika hali
mbaya.Alikuwa amewekewa
mipira ya kumsaidia
kupumua.” Akajibu Mathew
na Fatma akarejea tena
chumbani kuzungumza na
simu.
Baada ya dakika chache
akarejea tena na sura yake
ilionyesha mabadiliko
“Inaonekana huyu mtu
unayemsema ni mtu muhimu
sana kwa Habiba
Jawad.Nitalazimika mimi
mwenyewe kusafiri nanyi na
kuhakikisha mnakwenda
kuonana na Habiba
Jawad.Kwanza itawalazimu
kukaa hapa kwa muda wa
siku mbili ili niweze
kushughulikia hati zenu za
kusafiria halafu ndipo safari
ianze” akasema Fatma
BAADA YA SIKU 3
PARIS - UFARANSA
Ni jioni tulivu ndani ya
jiji la Paris katika himaya ya
biliona Peniela,tayari Papii
Gosu Gosu alikwisha wasili
kuitika mwito wa Peniela
aliyemtaka kwenda Paris
mara moja.Kwa muda wa
siku nzima walikuwa
wamejifungia katika ofisi ya
nyumbani ya Peniela na kazi
kubwa waliyokuwa
wakiifanya ni kupitia kwa
uangalifu nyaraka zote za
usajili na umiliki wa
biashara mbali mbali za
Mathew Mulumbi ambazo
Gosu Gosu alikuwa
amezipeleka kwa
Peniela.Vile vile walikuwa na
kazi ya kupitia mahesabu na
mwenendo mzima wa
biashara zote.Baada ya kazi
ile ngumu ya siku nzima
Peniela akamtaka Gosu Gosu
watoke na kwenda
kupumzika bustanini.
“Gosu Gosu
ninakushukuru sana kwa
kazi kubwa uliyoifanya ya
kusimamia miradi hii yote
baada ya Mathew
kuondoka.Miradi ni mingi na
si kazi nyepesi kuisimamia
lakini wewe umeweza
kuifanya kazi hii kwa
uaminifu mkubwa sana na
katika taarifa zote za fedha
hakuna hata mradi mmoja
unaoonyesha kujiendesha
kihasara na vile vile hakuna
upotevu wowote wa
fedha.Umesimamia miradi
hii kama mali yako.U mtu
mwaminifu mno.Endapo
biashara hizi zingekuwa
katika mikono ya mtu
mwingine hivi sasa zingebaki
nyaraka tu za umiliki lakini
kusingekuwa na senti yoyote
inayoingia.Mathew
hakukosea
kukuamini”akasema Peniela
na Gosu Gosu akatabasamu.
“Mathew ni mtu wangu
wa muhimu sana.Ninajua
mwenyewe mahala
alikonitoa na kunifikisha
hapa.Kwangu mimi Mathew
si rafiki bali ni zaidi ya
ndugu” akasema Gosu Gosu
“Ahsante sana kwa mara
nyingine tena” akasema
Peniela na kunyamaza kwa
muda kidogo kisha akasema
“Gosu Gosu pamoja na
usimamizi mkubwa na mzuri
unaoufanya lakini nimeamua
kuuza mali zote” akasema
Peniela na kunyamaza
akatazama angani.Gosu
Gosu akavuta pumzi ndefu
“Unataka kuuza mali
zote? Akauliza Gosu Gosu
“Ndiyo ninataka kuuza
mali zote.Si kwa sababu ya
kushindwa kusimamia au
hasara bali sina mpango
kuendelea kuwekeza
Tanzania.Kifo cha Mathew
kimenifanya nikafikia hatua
hii lakini usiogope
nitakuachia baadhi ya mali
utaendelea kuziendesha
wewe mwenyewe zitakuwa
za kwako.Nitakuachia
nyumba ile unayoishi pamoja
na nyumba nyingine
mbili.Magari yote aliyokuwa
anayatumia Mathew utabaki
nayo.Umefanya kazi kubwa
na kwa uaminifu mkubwa
hivyo basi unastahili kuwa
na maisha mazuri ndiyo
maana nakuomba usistuke
kwa maamuzi haya ya kuuza
mali hizo” akasema Peniela
“Peniela nimekosa neno
la kusema linaloweza
kueleza shukrani zangu
kwako kwa kuniamini na
kunikabidhi mali zenu zote
zilizoko Tanzania
nizisimamie .Wako watu
wengi ambao ungeweza
kuwaamini ukawapa mali
hizo waziendeshe lakini
ukawaacha wote
ukanichagua mimi.Ahsante
sana kwa
kuniamini.Ninashukuru vile
vile kwa mali
ulizonipatia.Ninajiona kama
sistahili kupata mali hizi
nyingi”
“C’mon Gosu Gosu
unastahili kupata mali
hizi.Kazi uliyoifanya ni
kubwa sana.Ningeweza
kukuachia mali zote
uendelee kuziendesha lakini
nataka niitoe Tanzania
katika akili yangu.Kitendo
walichomfanyia Mathew
kimeniumiza sana.Mathew
nimetoka naye mbali na sisiti
kusema kwamba yeye ndiye
sababu ya mimi kufika hapa
nilipofika.Mathew amekuwa
ni kila kitu kwangu.Mathew
aliipenda sana nchi yake na
ndiyo maana hata baada ya
kuachana na shughuli za
ujasusi lakini bado
aliendelea kufanya kazi
mbali mbali za nchi kila
alipotakiwa kufanya hivyo
lakini kupenda huko kazi
yake ndiko kumemsababisha
akafa kifo cha kinyama
sana.Kwa mambo
aliyoyafanya Mathew
alistahili hata kujengewa
mnara wa kumbu kumbu.Ni
mambo makubwa
ameyafanya lakini aliachwa
afe peke yake porini na maiti
yake ikaliwa na fisi.Jambo
hili linaniumiza sana na
ndiyo maana nataka
niisahau Tanzania japo ni
nchi nilikozaliwa” akasema
Peniela.Ukapita ukimya
mfupi halafu Gosu Gosu
akasema
“Madam utaniwia radhi
kwa hiki ninachotaka
kukuuliza”
“Uliza Gosu Gosu usiwe
na hofu yoyote kuwa na
amani” akasema Peniela
“Hujawahi kufikiria
kama yawezekana Mathew
Mulumbi yuko hai
bado?akauliza Gosu Gosu na
maneno ya Nahum yakapita
kichwani kwa Peniela
“Nisikilize
Peniela.Mathew Mulumbi
yuko hai.Tafadhali mtafute”
“Nahum alirudia maneno
haya kwa zaidi ya mara
moja.Alimaanisha kile
alichokuwa anakisema au
alikuwa anaweweseka akijua
atauawa?Natamani
nimweleze Gosu Gosu jambo
hili lakini naona aibu kwani
Mathew ni rafiki yake.Ngoja
niachane na hili suala”
akawaza Peniela na
kumgeukia Gosu Gosu
“Kwa nini umeuliza hivyo
Gosu Gosu?
“Madam kuna hisia huwa
zinakuja kwamba Mathew
hajafa.Sijui kwa nini
ninakuwa na hisia kama
hizo” akasema Gosu
Gosu.Ukimya ukapita tena
halafu Peniela akasema
“Gosu Gosu hizo ni hisia
tu na kila mtu ambaye
alikuwa na ukaribu na
Mathew anazo hisia
hizo.Hata mimi nilikuwa na
hisia kama hizo lakini
kilichonisaidia ni kwamba
ninamfahamu Mathew sana
kama angekuwa hai
angekwisha wasiliana
name.Kifo chake kina utata
mwingi ndiyo maana
unakuwa na hisia hizo lakini
tukubali Mathew amekwisha
fariki dunia.Nikupe mfano
mpaka leo hii bado kuna
idadi kubwa ya watu duniani
wanaoamini kwamba Tupac
Shakur Yule mwanamuziki
wa Marekani hajafa.Hii ni
kwa sababu ya mazingira ya
kifo chake lakini ukweli ni
kwamba alifariki dunia na
hiki ndicho tunachokipitia
kwa Mathew
Mulumbi.Hakuna aliyeuona
mwili wake na hicho
kinatufanya tuamini labda
Mathew bado yuko hai lakini
ukweli ni kwamba Mathew
amekwisha fariki
dunia.Hakuna namna
anayoweza kurejea tena
kwetu.Nakusihi Gosu Gosu
endelea na maisha yako”
akasema Peniela na mara
akakumbuka kitu
“Gosu Gosu una mke?
“Hapana bado sina mke”
“Unasubiri nini kuwa na
mke?Sikiliza Gosu Gosu
maisha haya ni mafupi sana
hivyo tunapaswa kutumia
kikamilifu muda
tunaoupata.Umri unapanda
juu haushuki chini hivyo ni
wakati muafaka wa kufikiria
kuwa na familia.Vipi kuhusu
mchumba unaye?
“Hapana hata mchumba
sina”
“Hata mchumba huna?
Peniela akashangaa
“Ndiyo madam”
“Is everything okay with
you? I mean are you…...”
Kabla Peniela hajamaliza
sentensi yake Gosu Gosu
akamkatisha
“Hapana siko hivyo.Mimi
ni rijali” akasema huku
akicheka
“Kama ni rijali kwa nini
huna mchumba mpaka leo
wakati una
mafanikio.Umekuwa
ukisimamia miradi mingi,you
have money,nice cars and
everything”akasema Peniela
“Mara chache nimekuwa
nikitoka na wanawake just
for one night stand”akasema
Gosu Gosu
“Sikiliza Gosu
Gosu.Wewe ni mtu wa
muhimu sana kwetu hivyo
ninakushauri ni wakati sasa
wa kufikiria kuhusu mke na
kuanzisha familia.Unataka
kuwa na familia ukiwa tayari
na miaka hamsini?
“Madam si kwamba
sipendi kuwa na familia au
kuwa na watoto lakini hofu
yangu ni kwamba sintakuwa
mume au baba mzuri”
“Kwa nini Gosu Gosu?
“Historia yangu si nzuri”
“Mathew aliwahi
kunidokeza kidogo kuhusu
wewe lakini kama hutajali
unaweza ukanieleza kwa
ireful zaidi kuhusu historia
yako”akasema Peniela
“Utanisamehe madam
lakini naomba nisikueleze
kuhusu historia yangu ila
nitaendelea kumshukuru
Mathew kwani ni yeye
aliyenitoa huko nilikokuwa
na akanfikisha hapa”
akasema Gosu Gosu
“Nimekuelewa Gosu
Gosu lakini kuna jambo
naomba tuelewane”
“Nakusikiliza madam”
“Ninataka kukutafutia
mwanamke” akasema
Peniela na GosuGosu
akacheka
“Madam unataka
kunitafutia mwanamke!
Akasema na kuendelea
kucheka
“Ndiyo na ninamaanisha
ninachokisema.Siwezi
kukuacha ukaendelea na
maisha hayo ya kuishi
mwenyewe .Sahau historia
ya nyuma lakini kwa sasa
wewe ni gosu gosu mpya.Una
kila kitu.Wewe ni milionea
hivyo una kila sababu ya
kuwa na mwanamke wa
maana.Kuna mwanamke
mmoja ni binti mwenye uzuri
wa kimalaika.Uzuri wake ni
wa ajabu kabisa huyo ndiye
nitakuunganisha
naye.Naamini atakufaa”
“Yuko wapi huyo malaika
manake umempa sifa kubwa
sana” akasema Gosu Gosu
“Anaitwa Melanie Davis
na huyo ndiye ninayemuuzia
biashara zangu.Bado umri
wake mdogo lakini ni
bilionea.Amerithi utajiri
kutoka kwa wazazi
wake.Huyo naamini
atakufaa” akasema Peniela
“Madam nakushukuru
sana kwa kunijali lakini
mimi ninapendelea
mwanamke wa kawaida
asiye tajiri.Hao wenye uzuri
wa malaika na fedha nyingi
wanasumbua sana na mara
nyingi huwa hawadumu
katika mahusiano.Unadhani
binti mwenye sura ya
kimalaika anaweza
akakubali kuwa na
mwanaume wa aina
yangu?akauliza Gosu Gosu
na Peniela akacheka kidogo
“Si kila mwanamke
mwenye pesa basi anakuwa
mkorofi na hadumu katika
mahusiano.Tazama mimi na
Mathew.Mbona tunaishi
vizuri na kwa kupendana
japo mimi ndiye chanzo cha
utajiri wetu.Siwezi sema
kwamba matatizo hayapo
kwani sisi si malaika lakini
heshima ni kubwa.Gosu
Gosu kinachomvutia
mwanamke si sura bali
upendo wa dhati.Mwanamke
anahitaji kujaliwa,kupendwa
na kutunzwa hata kama ana
pesa kama
mchanga.Ukimfanyia hayo
atakuheshimu.Mwanamke ni
kiumbe laini hivyo
usimpeleke kwa
mabavu,tumia lugha nzuri
unapozungumza naye.Lugha
unayotumia ukiwa na mke
wako iwe tofauti na
unavyozungumza na
wanawake wengine huko
mtaani.Mwanamke anataka
heshima,anahitaji ulinzi.Si
kwamba umlinde kama
mlinzi bali anatakiwa ajisikie
amani na salama akiwa
nawe.Mwisho mwanamke
anahitaji kuridhishwa haja
zake za
mwili.Nakuhakikishia
ukiyafanya hayo mwanamke
uliye naye atakulinda kama
mboni ya jicho ili wale macho
juu wanaopita wakikodolea
waume wa wenzao
wasikuibe” akasema Peniela
na Gosu Gosu
akacheka.Alifurahi sana
“Ahsante sana madam
kwa somo hilo zuri
nitazingatia hayo
uliyoyasema” akasema Gosu
Gosu.
“Vipi kuhusu suala
nililokwambia?Nakuhakikish
ia Gosu Gosu ukimuona huyo
malaika ninayekwambia
wewe mwenyewe moyo
utakuruka” akasema Peniela
“Madam wewe na
Mathew ni walezi wangu
hivyo siwezi kusema
hapana.Niunganishe na huyo
malaika” akasema Gosu
Gosu
“Ahsante sana Gosu
Gosu.Naamini wewe
mwenyewe ukimuona
utakubali haya
ninayokwambia.She’s an
angel”
“Hana mpenzi?akauliza
Gosu Gosu
“Usihofu kuhusu
mpenzi.Hata kama akiwa
naye tunafanya
mapinduzi.Ukimpata mtunze
kama malkia.Mkiwa
kitandani hakikisha
unamfikisha mahala ambako
hakuna mwanaume amewahi
kumfikisha na ninakuapia
hata kama alikuwa
amevishwa pete ya uchumba
ataivua” akasema Peniela
wakaendelea na
mazungumzo kisha
wakaenda kupata chakula
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 5
Siku nyingine jijini
Paris.Siku hii Gosu Gosu
alikuwa amevaa suti kali
iliyompendeza
“Kuanzia sasa huo ndio
muonekanao unaotakiwa
kuendelea nao.Unatakiwa
kuwa mtu wa suti kila
wakati” akasema Peniela
baada ya Gosu Gosu
kumaliza
kujiandaa.Walipata kifungua
kinywa kisha wakaingia
katika gari tayari kwenda
kukutana na ujumbe wa
Melanie Davis.Kikao
kilifanyika katika hoteli moja
kubwa jijini Paris
inayomilikiwa na
Peniela.Peniela na ujumbe
wake ndio waliokuwa wa
kwanza kuwasili hivyo
kuwalazimu kuwasubiri
akina Melanie.
“Are you nervous?Peniela
akamuuliza Gosu Gosu
“Kidogo sana.Hamu
yangu kubwa ni kumuona
uyo malaika ambaye jana
ulimpa sifa lukuki” akasema
Gosu Gosu
“Usijali utamuona
atafikahapa” akasema
Peniela.Waliendelea kusubiri
kwa dakika kama ishirini
hivi kisha msafara wa
magari matano ukawasili
pale hotelini.Melanie na
ujumbe wake wakapokewa
na Peniela wakakaribishwa
ukumbini.Wakati watu
wakijiandaa wakiweka sawa
makabrasha yao Peniela
akamuita pembeni
Melanie.Gosu Gosu jicho
lilimtoka kama fisi
alipomuona Melanie
akitembea.
“Daah ! Peniela
hakukosea kumpa sifa
zile.Huyu kweli ni
malaika.Melanie ana uzuri
wa ajabu sana.Nilipomuona
hadi nimemuogopa.Viumbe
wa namna hii wanaweza
wasiwe binadamu wa
kawaida.Mnaweza mkadhani
ni mwanadamu mwenzenu
kumbe ni kiumbe toka sayari
nyingine manake uzuri huu
si wa kawaida.Kuanzia
kwenye unywele hadi
miguuni mtoto huyu
anavutia.Amekamilika kila
kitu.Sura ina tabasamu
ambalo ni adimu sana
kupatikana mguu wake
daaah nashindwa hata
kumuelezea huyu
mtoto.Nimebahatika
kuzunguka zunguka katika
baaadhi ya nchi nimekutana
na wanawake warembo
lakini huyu ametia fora”
akawaza Gosu Gosu
“Mwanamke mwenye
uzuri kama huu anaweza
akanikubali mtu kama mimi
kweli?I’m so ugly siendani
naye kabisa.Lakini Peniela
alinihakikishia kwamba
ataniunganisha naye.Anajua
mwenyewe namna
atakavyofanya lakini mimi
kumuingia mwenyewe mtoto
kama huyu ni ngumu sijui
nitaanzia wapi halafu sina
ujuzi sana wa kutongoza
wanawake ndiyo maana
hupenda kuchukua wale wa
usiku mmoja ninamlipa pesa
zake tunamalizana.Lakini
endapo mtoto kama huyu
akiingia kwenye anga zangu
naapa hatabanduka.Nitampa
mapenzi hadi atasahau kama
kuna wanaume wengine
ndani ya hii dunia.Ataniona
mimi peke yangu” akawaza
Gosu Gosu
Peniela alitoka ndani ya
ule ukumbi na kusimama na
Melanie katika korido.
“Habari za toka majuzi
Melanie?akauliza Peniela
“Habari nzuri kabisa
Peniela.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vyema sijui
wewe”:
“Mimi niko safi kabisa”
“Naona umejiandaa vya
kutosha.Mimi pia
nimekwisha kamilisha kila
kitu”
“Vizuri sana”
“Melanie kabla ya
kuanza kwa kikao kuna mtu
ambaye ninataka ukutane
naye”
“Nani huyo?akauliza
Melanie
“Nipe dakika mbili”
akasema Peniela na
kufungua mlango wa ukumbi
akamtuma muhudumu
amuite Gosu Gosu.Mapigo ya
moyo yalianza kumwenda
mbio baada ya kusikia mwito
ule wa Peniela.Alijua
anakwenda kukutanishwa na
Melanie.Aliinuka
akatengeneza vizuri tai yake
halafu akaanza kutembea
kutoka nje akaufungua
mlango na kuwaona Peniela
na Melanie wamesimama
wakimuangalia.Akahisi
kama miguu inamtetemeka
baada ya kugonganisha
macho na Melanie.Akajikaza
na kupiga hatua akawafuata
“GosuGosu samahani
kwa kukutoa ukumbini
nimekuita hapa ili
nikukutanishe na mtu
muhimu sana.Huyu anaitwa
Melanie Davis yeye ndiye
ambaye leo hii ninamuuzia
mali zangu .Usimuone mdogo
mdogo lakini ana utajiri wa
kutisha” akasema Peniela na
kutoa kicheko kidogo Gosu
Gosu naye akacheka kidogo
“Melanie huyu anaitwa
Gosu Gosu.Huyu ndiye
ambaye amekuwa
akisimamia biashara zangu
zote Tanzania baada ya
mume wangu kufariki.Ni
mtu maminifu na
mchapakazi.Mambo
aliyonifanyia katika biashara
ni makubwa na nina uhakika
anaweza akawa na msaada
mkubwa sana
kwako”Akasema Peniela na
Melanie akatabasamu kisha
akanyoosha mkono na
kumpa Gosu Gosu
“Gosu Gosu nafurahi
sana kukutana nawe”
Mapigo ya moyo wa Gosu
Gosu yalitaka kusimama
baada ya kuugusa mkono wa
Melanie
“Hata mimi nafurahi
kukutana nawe” akajibu
Gosu Gosu
“Jamani ni hilo tu
ambalo nimewaitia hapa
nadhani baadae jioni ya leo
tutakutana sisi watatu na
tutakuwa na mazungumzo ya
kina zaidi.Kwa sasa
tukaendelee na kikao”
akasema Peniela wakarejea
ndani ya ukumbi.Gosu Gosu
damu ilimchemka hakuweza
kutulia tena.
Peniela alifungua kikao
kile kwa kufanya
utambulisho kwa wajumbe
wa upande wake halafu
Melanie naye akafanya
utambulisho wa wajumbe
aliokuja nao kisha mambo
yakaanza.
********************
Tayari kiza kimekwisha
Melanie Davis aliwasili
katika jumba la Peniela
akapokewa na kukaribishwa
sebuleni.Usiku huu alikuwa
amependeza sana alivaa
gauni fupi jeupe.Alipendeza
mno.Melanie alifika hapa
usiku huu kufuatia mwaliko
wa Peniela aliyemkaribisha
nyumbani kwake kwa
chakula cha usiku.Dakika
chache baadae Peniela
akajitokeza sebuleni akiwa
naye amevaa gauni refu
jeupe kama vile aliambizana
na Melanie wavae wote rangi
moja.
“Melanie karibu
sana.Umependeza sana
usiku huu” akasema Peniela
“Hata wewe umependeza
sana Peniela” akasema
Melanie
“Huyu mtoto ni mzuri
jamani.Kama ningekuwa
mwanaume katu
nisingekubali kumkosa
kimwana huyu.Hata hivyo
lazima nihakikishe
ninamuunganishia Gosu
Gosu” akawaza Peniela
“Ahsante sana kwa
kufika Melanie.Kama
hutajali naomba tuzunguke
kidogo bustanini wakati
wahudumu wanaendelea
kufanya maandalizi”
akasema Peniela na Melanie
akaungana naye wakatoka
kuelekea bustanini.
“Melanie najua huu si
wakati mzuri wa
kuzungumza masuala ya
biashara kwani kutwa nzima
ya leo tumekuwa
tunazungumza masuala hayo
lakini napenda nikushukuru
kwa mchakato kwenda
vizuri”
“Mimi ndiye
ninayepaswa kukushukuru
kwa kukubali kuniuzia
biashara zako.Japo nimetoa
fedha lakini naona kama vile
umenipa bure”akasema
Melanie
“Lini umepanga kwenda
Tanzania?akauliza Peniela
“Mapema
iwezekanavyo.Ndani ya siku
mbili au tatu zijazo nitakuwa
nimefika Tanzania” akajibu
Melanie
“Vizuri sana.Kuna swali
la kizushi nataka kukuuliza
kama hutojali”
“Uliza usihofu” akasema
Melanie
“Una mchumba tayari?
Akauliza Peniela na Melanie
akatabasamu
“Hapana sina mchumba”
akajibu Melanie
“Malaika kama wewe
unakosaje mchumba?Au
wanaume wanakuogopa
kutokana na uzuri wako?
Akauliza Peniela na Melanie
akacheka
“Niliamua mimi
mwenyewe nisiwe katika
mapenzi” akasema Melanie
Peniela alitumia zaidi ya
nusu saa kumchombeza
Melanie aweze kumkubali
Gosu Gosu.Muda wote ambao
Peniela alikuwa akimuelezea
Gosu Gosu Melanie alikuwa
anatabasamu kutokana na
namna alivyomuelezea Gosu
Gosu.Melanie alimueleza
Peniela kwamba angehitaji
kupata nafasi ya
kuzungumza na Gosu
Gosu.Walirejea ndani
ambako walimkuta Gosu
Gosu sebuleni
akiwasubiri.Usiku huu
alikuwa amevaa suti nzuri ya
kijivu.Baada ya kusalimiana
Peniela akawakaribisha
katika chumba cha chakula
kulikoandaliwa chakula
maalum kwa ajili yao.Baada
ya kumaliza kupata chakula
Peniela akawaomba
waelekee katika chumba cha
mapumziko ambamo
kulikuwa na runinga kubwa
.Wakiwa mle Peniela
akatoka na kuwaacha Gosu
Gosu na Melanie.Ukimya
ulikuwa umetawala mle
katika chumba cha
mapumziko hadi pale
Melanie alipoinuka na
kumfuata Gosu Gosu katika
sofa na kukaa pembeni yake.
“Unaonekana una hofu
Gosu Gosu.Nini kinakupa
hofu?akauliza Melanie
“Sina hofu Melanie”
akajibu Gosu Gosu.Baada ya
sekunde kadhaa Melanie
akasema
“Madam Peniela amenipa
ujumbe wako.Kwa nini
hukunieleza wewe
mwenyewe hadi ukamtumia
Peniela?akauliza Melanie
“Naomba niwe muwazi
kwako Melanie.Nilishindwa
namna ya kuzungumza nawe
suala lile”
“Gosu Gosu“ akasema
Melanie kwa sauti laini na
mwili wa Gosu Gosu ukazidi
kusisimka
“Nini kilikupa hofu ya
kuja kunieleza jambo
lile?Melanie akauliza
“U mzuri mno Melanie
hadi nikaogopa.Kwa kawaida
wanawake wazuri kama
wewe si rahisi kuwa na watu
wa aina yangu.Ndiyo maana
nikamuomba Peniela
anisaidie” akasema Gosu
Gosu
“Usiwe mwoga Gosu
Gosu.Ukimtaka mwanamke
usimtumie mtu wa katikati
bali mfuate wewe mwenyewe
mweleze na ataamua
mwenyewe akukubali au vipi
lakini kitendo cha kumtumia
mtu mwingine kinakufanya
uonekane hujiamini”
“Ninajiamini Melanie
lakini kuna utofauti mkubwa
sana kati yangu nawe na hilo
ndilo lililonipa woga”
“Hukupaswa kuogopa.Ni
vipi nikikwambia kwamba
hata mimi nilivutiwa nawe
mara tu
nilipokuona?akasena
Melanie na moyo wa Gosu
Gosu nusura usimame kwa
mstuko alioupata.
“Me?akauliza Gosu Gosu
“Ndiyo Gosu Gosu.Mimi
sioni woga kukutamkia
kwamba nilivutiwa nawe
mara tu nilipokuona ”
“Oh my God ! nini
kimekuvutia kwangu?
“Sikiliza Gosu Gosu mimi
najifahamu ni mzuri.Ni
mzuri sana lakini sipenzi
wanaume wenye sura
nzuri.Mara nyingi ukiwa na
mwanaume mzuri
inakufanya uwe katika
mashindao na wanawake
wengine nje ambao
wanamtolea macho kama
mwewe aliyeona
kifaranga.Nikiwa nawe watu
wanaweza wakanicheka
kwamba imekuwaje
mwanake mzuri kama huyu
akawa na mtu kama
huyu?Simaanishi kwamba
wewe ni mbaya but you are
not handsome.Hakuna
mwanamke ambaye atataka
kushindana nami kukupata
hivyo utakuwa wangu peke
yangu na hicho ndicho
ninachokitaka.Kwa uzuri
huu nilio nao hata wewe
hautasumbuka kutafuta
mwanamke mwingine kwani
nimewazidi wengi
uzuri.Pamoja na hayo…”
akasema Melanie na kuinua
glasi akanywa funda moja
akaendelea
“I have everything in
life.Ninachohitaji mwanaume
nitakayekuwa naye awe na
uwezo wa kunitosheleza
kitandani.Hiyo ndiyo starehe
yangu kubwa Usistuke Gosu
Gosu mimi ni muwazi sana
hivyo napenda kukuweka
wazi kwamba napenda sana
kufanya mapenzi.Mwanaume
ninayemtaka lazima awe na
uwezo wa
kuniridhisha.Nimewahi
kuwa na wanaume kadhaa
lakini walikimbia wenyewe
walishindwa kutimiza
mahitaji.Mimi nataka kama
dozi ya dawa kutwa mara
tatu au nne” akasema
Melanie na wote wakacheka
“Huo ndio ukweli Gosu
Gosu na ndiyo maana
wanaume wale niliowahi
kuwa nao ambao ninaweza
kuwaita wavulana
walishindwa na kuondoka
zao.Nataka mwanaume
anayeiweza shughuli na
sitaki Yule anayetumia dawa
za kuongeza nguvu.Nataka
nguvu za asili.Nilipokuona
wewe Gosu Gosu sijui kwa
nini nilivutiwa nawe lakini
unaonekana uko tofauti
kidogo na wengine.Peniela
aliponipa ujumbe wako
nilihisi kama vile moyo
wangu umepigwa na radi
kwa mstuko.Nilifurahi sana
kwamba hata wewe ulikuwa
umevutiwa nami.Nataka
kukuthibitishia kwamba
ombi lako nimelipokea lakini
kabla ya yote kabla
sijatamka kitu nataka
kuhakikisha kama hisia
zangu kwamba wewe ni
tofauti ni za kweli.Usiku wa
leo nataka tukalale
wote”akasema Melanie na
bado GosuGosu hakuwa
ameamini.TaratibuMelanie
akaupitisha mkono wake
hadi maeneo ya ikulu kwa
Gosu Gosu ambako hali
ilikuwa mbaya .
“Mbona uko kimya Gosu
Gosu?akauliza Melanie huku
akiupitiasha mkono wake
maeneo yale ambako
kulikuwa kumefura vibaya
sana
“Wow it looks so big !
akasema Melanie na kuzidi
kumchanganya Gosu Gosu
“Devotha aliniambia
nifanye juu chini niweze
kumteka huyu jamaa Gosu
Gosu.Aliniambia kwamba ni
mtu ambaye anaweza
akanisaidia sana katika kazi
ninayokwenda kuifanya
Afrika Mashariki kwani ni
muuaji hatari sana.Alinipa
historia ya huyu jamaa
kwamba aliwahi kupigana
vita ya msituni kwa muda
mrefu hivyo ni mwanajeshi
mzuri na mimi nahitaji mtu
kama huyu.Mpaka hapa
tayari nimekwisha mpata na
anaonekana ni mdhaifu sana
kwa wanawake.Mtazame
alivyopoa kama maji ya
mtungi” akawaza Melanie na
kutolewa mawazoni baada ya
Peniela kuingia mle ndani na
kustuka kwa hali aliyoikuta
“Sorry guys” akasema
Peniela
“Usijali madam Peniela
mimi na Gosu Gosu tulikuwa
na mazungumzo kidogo hata
hivyo tulikuwa tunakusubiri
uje ili tukuage leo
ninaondoka na Gosu Gosu
nitamrejesha hapa
kesho.Nataka
nikamuonyeshe uzuri wa jiji
la Paris” akasema Melanie
“Hakuna tatizo lakini
hakikisha Gosu Gosu
anakuwa salama” akasema
Peniela huku akitabasamu
Baada ya mazungumzo
mafupi Gosu Gosu na
Melanie wakaondoka
“Nataka nimchanganye
kwa mapenzi mwanaume
huyu hadi afanye kila
nitakachomuamuru.Hadi
hapa naamini nimekwisha
mpata kwa asilimia sabini”
akawaza Melanie wakiwa
garini
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 6
Mlio wa simu ya mkononi
ulimstua Melanie akaamka
na kutazama mpigaji.Katika
kioo lilitokea jina Dev likiwa
na maana ya Devotha.Tayari
kulikwisha pambazuka.
“Nilikuwa na usingizi
mzito sana sikujua kama
tayari kumepambazuka”
akawaza Melanie na
kuelekea sebuleni akaipokea
ile simu
“Hallow”akasema
“Melanie sauti yako ya
uchovu sana bado
umelala?akauliza Devotha
“Simu yako ndiyo
iliyonitoa usingizini”
“Vipi mipango
ilifanikiwa?
“Kila kitu kilikwenda
vizuri”
“safi sana.Jiandae
baadae leo unakwenda
kukutana na Rais” akasema
Devotha
“Sawa ahsante kwa
taarifa” akasema Melanie na
kukata simu
“Dah ! usiku wa jana
sintausahau.Huyu jamaa
kweli mwanajeshi na
inaonekana ana muda mrefu
hajakutana na mwanamke
kwani mambo aliyonifanyia
jana hadi mimi mwenyewe
nilishindwa kuhimili.Ana
nguvu za
kutosha.Alinipeleka
mizunguko minne hadi
nikaishiwa nguvu kabisa na
kumuomba aniache nilale
ndiyo maana nimelala kama
chatu.Kweli hapa nimepata
mtu ninayemuhitaji”
akawaza na kutabasamu
baada ya matukio ya usiku
ule kumjia kichwani
“Ulikuwa ni usiku mzuri
sana.Sijawahi kupelekeshwa
kama nilivyopelekwa jana”
akaendelea kuwaza halafu
akaingia chumbani na
kumkumbatia Gosu Gosu
“Devotha alinitaka niwe
na mahusiano na huyu
jamaa kwa ajili ya kunisidia
katika mipango yangu lakini
nahisi tayari nimeanza
kumpenda” akawaza Melanie
na kumtazama Gosu Gosu
aliyekuwa
amelala.Akamuamsha kwani
ni muda wa kuondoa kwenda
kuendelea na majukumu
mengine
Saa tano za asubuhi
iliwakuta Devotha na
Melanie Davis katika ikulu
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 4: EPISODE 7
Saa tano za asubuhi
iliwakuta Devotha na
Melanie Davis katika ikulu
ya Ufaransa kwa ajili ya
kukutana na Rais Michael
Weren.
“Devotha na Melanie
karibuni sana.Nimefurahi
kukuona Melanie .Kwa uzuri
huo utaitingisha dunia”
akasema Michael na wote
wakaangua kicheko.
“Melanie nimetaarifiwa
kwamba ulikamilisha
mafunzo na ukafanya vyema
na sasa uko tayari kwa
kazi.Nimejulishwa pia na
Devotha kwamba mipango
yote imekwenda vizuri na
muda wowote utaelekea
Afrika mashariki tayari
kuanza kazi”akanyamaza
kidogo halafu akaendelea
“Tunazo taarifa kwamba
mkutano mkubwa wa wake
za maraisi duniani
unatarajiwa kufanyika jijini
Dar es salaam Tanzania
mwezi ujao.Mkutano huo
umeandaliwa na taasisi ya
mke wa Rais wa Tanzania
Millen Kelelo.JIna lake
linafanana sana na
lako.Mkutano huu unakuja
miezi michache baada ya
mauaji ya wazazi wako na
mauaji ya balozi wa umoja
wa Ulaya nchini
Tanzania.Tunaamini lengo la
mkutano huo ni kwa ajili ya
kuidhihirishia dunia
kwamba Tanzania ni nchi
salama ndiyo maana wake
wa marais wote duniani
wamealikwa.Mkutano huu
ukifanikiwa basi lengo letu la
kuichafua Tanzania na
Afrika Mashariki litakuwa
limefeli.Unakwenda kufanya
kazi ya kuisambaratisha
Afrika mashariki na kazi
yako itaanzia katika
mkutano huo wa wake za
marais.Afrika Mashariki
itaanzia kusambaratika
hapo. Kwa kuanzia nataka
mke wa Rais wa Rwanda
auawe nchini Tanzania na
ionekane nchi ya jamhuri ya
kidemokrasi ya Congo
inahusika katika mauaji
hayo.Nataka mahusiano ya
Rwanda na Congo DRC
yavunjike.Nchi mbili hizi
zikianza malumbano ndani
ya jumuiya ya Afrika
Mashariki zitasababisha
jumuiya kutetereka.Wakati
Rwanda na Congo
zikilumbana nataka uibuke
mgogoro mwingine kati ya
Tanzania na Rwanda.Balozi
wa Rwanda anatakiwa naye
auawe.Tukifanikisha kuibua
migogoro hiyo tayari
tutakuwa tumetoboa tobo na
meli itaanza kuzama
taratibu.Huu ni mpango
mkubwa na Devotha ambaye
ndiye anayeratibu kila kitu
atakupa maelezo mengi zaidi
ya nini unatakiwa ufanye
lakini usiwe na hofu yoyote
kuhusu usalama
wako.Utakuwa salama kwani
kuna majasusi wa siri
wamekwisha andaliwa kwa
ajili ya kukulinda na
hutawaona ila fahamu kila
unapokwenda watakuwepo
na watahakikisha unakuwa
salama.Unapokuwa katika
utekelezaji wa jukumu hili
usisahau kwamba
tunayafanya haya kwa ajili
ya kwanza kulipiza kisasi na
pili kuikomboa
Congo.Umekwisha
fundishwa kila kitu na
ninachokifanya hapa ni
kukukumbusha tu jukumu
lako.Kwa namna yoyote ile
usikubali ukaenda nje ya
lengo.Macho na akili yako
vyote vielekeze katika kazi
uliyopewa.Ukienda tofauti na
kazi uliyopewa hautakuwa
ukiwatendea haki wazazi
wako ambao wameuawa
kikatili na wapinga
maendeleo hivyo basi lengo
letu ni kuhakikisha kwamba
yeyote Yule ambaye ana
mkono wake katika mauaji
ya wazazi wako habaki
salama lakini kubwa zaidi ni
kuhakikisha kwamba Congo
inatoka katika jumuiya ya
Afrika Mashariki na
kuliondoa genge la watu
wachache wanaojinufaisha
na rasilimali za nchi
hiyo.Nadhani umenielewa
Melanie” akasema Michael
Weren
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais.Tayari
nimekwisha pewa mafunzo
ya kutosha na ninaelewa nini
ninakwenda kukifanya
Afrika Mashariki na
ninakuahidi kwamba
nitafanya kwa umakini
mkubwa kazi niliyotumwa na
sintakuangusha” akasema
Melanie
“Nashukuru kwa maneno
hayo yenye kutia moyo.Basi
mimi sina la ziada nakutakia
kila la heri na taarifa za
maendeleo yako nitakuwa
nikizipata kutoka kwa
Devotha” akasema Rais
Michael Weren na kuagana
na akina Melanie
MPENZI MSOMAJI
- BAADA YA
KUNUSURIKA KATIKA
MTEGO WA KUUAWA
RUBY YUKO NJIANI
AKIELEKEA DAR ES
SALAAM.JE ATAFIKA
SALAMA?
- MATHEW MULUMBI
TAYARI YUKO KATIKA
HARAKATI ZA
KUONANA NA HABIBA
JAWAD JE
ATAFANIKIWA?
- THERESA MUGANZA
AMBAYE KWA SASA
ANAJULIKANA KAMA
MELANIE DAVIS
ANAANZA SAFARI YA
KUELEKEA DAR ES
SALAAM KATIKA
MISHENI NZITO YA
KUISAMBARATISHA
JUMUIYA YA AFRIKA
MASHARIKI JE
ATAFANIKIWA?
KWA MAJIBU YA
MASWALI HAYA
MPENZI MSOMAJI
USIKOSE SEHEMU
IJAYO…
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom