SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 3: EPISODE 3
“Gosu Gosu” Sauti laini
ya mwanamke ilimstua Gosu
Gos kutoka katika usingizi
mzito.Alifumbua macho na
kujikuta akiwa amelala
sofani.Mezani kulikuwa na
chupa kadhaa za
bia.Akafikicha macho na
kuinuka akakaa
“Agatha” akasema
“Mlirudi saa ngapi
kutoka kwa Tamar?akauliza
Agatha
“Ahsante kwa
kuniamsha.Ninahisi kichwa
kizito sana.I need to take a
bath” akasema Gosu Gosu na
kuchukua bastora yake
akaelekea chumbani kwake
akajimwagia maji baridi
“Nimelala usingizi mzito
sana halafu mbaya zaidi
niliweka bastora mezani.Hii
ni hatari,angeweza kuingia
mtu mbaya na kunimaliza”
akawaza Gosu Gosu
“Lakini usingizi huu
umesababishwa na bia
nilizokunywa jana.Si
kawaida yangu kulala
namna hii” akaendelea
kuwaza
“Sitaki kushiriki tena
kazi yoyote ile
atakayoniomba Austin.Jana
Rais ametufanyia kitu kibaya
sana na mpaka sasa bado
sifahamu kwa nini alifanya
vile.Kwa nini hakutuacha
tukaendelea na zoezi letu na
badala yake akaamuru
tuondoke haraka nyumbani
kwa Tamar tulikofuata
jambo muhimu tena kwa
faida yake yeye mwenyewe?
Anyway, I’m done.Sitaki tena
kushiriki katika operesheni
yoyote ya serikali.Toka
wakati wa Mathew mambo
kama haya yalikuwa
yanatokea.Viongozi ndani ya
serikali hawaeleweki na
hawaaminiki.Ninaweka
nukta katika mambo haya na
ninataka kujikita zaidi
katika kusimamia biashara
za Mathew” akawaza Gosu
Gosu na kuitazama picha
kubwa ya Mathew ukutani
“What happened to you
Mathew Mulumbi? Are you
real dead ?If not where are
you brother?akajiuliza Gosu
Gosu na mlango wake
ukagongwa akaufungua
alikuwa ni mtumishi wake
wa ndani aliyemjulisha
kwamba kifungua kinywa
tayari.Kabla ya kwenda
katika chumba cha chakula
Gosu Gosu akaenda katika
chumba cha wageni
walimolala akina
Agatha.Mlango
ukafunguliwa akatoka
Agatha
“Gosu Gosu” akasema
Agatha
“Watoto
wanaendeleaje?akauliza
“Bado wako katika
mstuko.Bado wanaogopa”
akajibu Agatha
“Ni kweli lilikuwa tukio
baya.Itachukua muda tukio
lile kuwatoka vichwani
mwao” akasema Gosu Gosu
“It’s breakfast time”
akasema Gosu Gosu
“Sina hakika kama
watakubali kutoka humu
chumbani.Bado wanaogopa
sana”
“It’s okay.Mtumishi
atawaandalia kifungua
kinywa humo humo
chumbani” akasema Gosu
Gosu na kuelekea katika
chumba cha chakula kupata
kifungua kinywa.
“Lazima nitafute namna
ya kuwasaidia Agatha na
familia yake waweze kuwa
salama.Nina uhakika
mkubwa lazima Tamar na
idara yake wataelekeza
nguvu zao nyingi kumsaka
na kuhakikisha
anapatikana” akawaza akiwa
mezani.Alipomaliza akaenda
tena katika chumba cha
Agatha akagonga mlango na
kumtaka Agatha
wazungumze wakaelekea
katika bwawa kubwa la
kuogelea
“Usiwe na hofu Agatha
hapa uko sehemu salama na
nitahakikisha wewe na
familia yako mnakuwa
salama,naomba uniamini”
“Ahsante nashukuru”
“Kwa sasa mtaendelea
kukaa hapa kwangu hadi
pale tutakapopata sehemu
salama zaidi mtakapoishi
kwa amani bila
bughudha.Kitu chochote
mtakachokihitaji usisite
kunijulisha”
“Nakushukuru sana
Gosu Gosu kwanza kwa
kutuokoa jana na pili kwa
kuhakikisha tunaendelea
kuwa salama.Bila wewe hivi
sasa mimi na familia yangu
tungekwisha
uawa.Nashukuru vile vile
kwa huduma nzuri
tunazopatiwa hapa.Ukiacha
mstuko ambao bado watoto
wanao lakini tunajihisi tuko
nyumbani”akasema Agatha
huku akitabasamu
“Msiwe na hofu jisikieni
nyumbani.Jumba hili ni
kubwa na mko huru
kuzunguka sehemu mbali
mbali.Kuna bustani nzuri na
sehemu za michezo ya
watoto.Unaweza ukawatoa
ndani ukawaleta hapa kuja
kupumzika” akasema Gosu
Gosu
“Hujanieleza kuhusu
jana.Mlifanikiwa kupata
chochote nyumbani kwa
Tamar?akauliza Agatha.
“It was complicated”
“Complicated?
How?akauliza Agatha
“Tulifanikiwa kuingia
nyumbani kwa Tamar na
wakati tukielekea katika
chumba chake cha kulala
Austin akapigiwa simu na
Rais akamtaka tuondoke
haraka sana mahala pale”
“Rais? Akauliza Agatha
“Ndiyo.Rais alipiga simu
na kututaka tuachane na
zoezi lile na tuondoke haraka
sana mahala pale”
“Kwa nini akafanya vile?
Si yeye aliyewapa kazi hii
kwa nini basi awazuie
msitekeleze kazi
aliyowapa?akauliza Agatha
akionyesha mshangao
mkubwa
“Hilo ndilo swali ambalo
hata sisi tumekuwa
tunajiuliza.Imetokea nini
hadi Rais akafanya maamuzi
kama haya?Tulikwenda pale
kwa nia ya kumsaidia yeye
mwenyewe ili rekodi za
mawasiliano yake zisiwafikie
wabaya wake lakini dah !
Gosu Gosu akashindwa
kuendelea akainamisha
kichwa
“Alifahamuje kama mko
pale?akauliza Agatha
“Agatha sisi hatufahamu
chochote.Anyway naomba
tuachane na suala hilo kwani
hata sisi tumeamua
kuachana nalo.Kwa vile
aliyetupa kazi ambaye ni
Rais ameamua kutuingilia
katika kazi aliyotupa hatuna
haja ya kuendelea na hili
jambo.Kipaumbele changu
kwa sasa ni kuhakikisha
wewe na familia yako
mnakuwa salama” akasema
Gosu Gosu na ukmya
ukatanda mahala pale.Baada
ya kama dakika tano hivi
Agatha akasema
“Gosu Gosu hampaswi
kuliacha jambo hili
hewani.Rais yuko katika
hatari kubwa.Zile rekodi
kama zikitoka katika
kompyuta ya Tamar basi
Rais atakuwa katika hatari
kubwa.Je mlijaribu
kumweleza jambo hilo na
hatari inayomkabili?akauliza
Agatha
“Hapana hatujamweleza
bado.Tulitaka tuipate
kwanza kompyuta ya Tamar
tuhakikishe tunazo rekodi
ndipo tumueleze Rais
kilichokuwa kinaendelea”
“That’s a mistake.Rais
anapaswa kuambiwa nini
kinaendelea.Yawezekana
hajui kuna bomu
linalokaribia kumlipukia”
akasema Agatha
“Agatha tuachane na
hayo mambo.Wanasiasa wa
aina yake ambao ni vigeu geu
dawa yao ni kuwaacha wafe
na misalaba yao.Hakuna
haja ya kupoteza muda na
kuhatarisha maisha
kumsaidia mtu ambaye
haoni thamani ya msaada
wetu.Let him be.Hilo bomu
likimlipukia atajua
mwenyewe” akasema Gosu
Gosu.
Ukimya ukapita tena
halafu Agatha akasema
“Gosu Gosu nafahamu
umeshafanya mengi kwangu
lakini kuna msaada nina
uhitaji”
“Sema unahitaji nini
Agatha?
“Nahitaji kuzungumza na
Samson”
“I’m sorry Agatha
hutakiwi kuzungumza na
mtu yeyote kwa sasa.Watu
wako wanaweza wakafuatilia
simu na kujua mahala ulipo”
“Nalifahamu hilo ndiyo
maana nataka tukawasiliane
naye mbali kidogo na hapa ili
hata kama wakinifuatilia
wasigundue kwamba niko
hapa.Nakuomba sana Gosu
Gosu nisaidie kwa hilo”
akasema Agatha
“Sauti yako ina
ushawishi mkubwa na
hakuna anayeweza kusema
hapana.Jiandae twende
ukawasiliane na huyo mtu
wako” akasema Gosu Gosu
na Agatha akainuka
kuelekea chumbani kwake
kujiandaa.Gosu Gosu
akabaki kwenye kiti
akimtazama
“Mtoto ameumbwa
kiafrika haswaa.Sura yake
nzuri ya upole,sauti yake
tamu laini,macho yake
malegevu dah naona taratibu
anaanza kuingia katika
ubongo wangu” akawaza
Gosu Gosu huku
akitabasamu naye akainuka
na kuelekea chumbani
kwake kuchukua bastora
Agatha alivaa suruali ya
jeans rangi ya bluu na shati
jeusi kichwani akavaa kofia
na miwani mikubwa myeusi
ili isiwe rahisi
kutambulika.Wakaingia
garini na kuondoka
“Do you mind if I
ask?akauliza Gosu Gosu
“Uliza chochote Gosu
Gosu”
“Mumeo yuko
wapi?akauliza
“Alikwisha fariki kwa
ajali.Alifariki wakati
mwanangu akiwa na mwaka
mmoja”
“Pole sana.Nini kilifuata
baada ya hapo?
“Una maanisha
nini?Agatha akauliza
“Uliolewa tena au bado
uko peke yako?
“Sikutaka kuolewa tena
kwani uwezo wa kumtunza
mwanangu ninao hivyo
sikuona sababu ya kutafuta
mwanaume
mwingine”akasema Agatha
na Gosu Gosu akatoa kicheko
“Nini
kimekufurahisha?akauliza
Agatha
“Wanawake
mnanifurahisha
sana.Hukutaka kuolewa kwa
vile uwezo wa kumsomesha
mwanao unao.Lakini kama
usingekuwa nao
ungeolewa?Why you always
thinking of ..” akanyamaza
“Say it” akasema Agatha
“Tuachane na hilo
jambo”akasema GosuGosu
“Sema tu we always
thinking of money?
“I didn’t mean that.But
isn’t it true? akasema Gosu
Gosu
“Umewaza nini hadi
ukauliza hivyo? Agatha
akauliza
“Zama hivi fedha na mali
vimepewa kipambele sana
katika mahusiano kuliko
upendo alio nao mtu na hii
iko sana kwa upande wa
wanawake.Wengi
wanamkubali mtu kutokana
na uwezo wake wa kifedha
bila kujali kama mtu huyo
ana mapenzi ya kweli kwake
au hapana.Ninazungumza
kitu ambacho nina uzoefu
nacho.Hapo kabla sikuwa
hivi nilivyo,sikuwa na fedha
wala mali,I was no
body.Ilikuwa kazi ngumu
sana kumtongoza
mwanamke akanikubali
kutokana na hali yangu ya
wakati huo lakini kwa sasa
baada ya kuwa mtu
ninauona usumbufu mwingi
sana kutoka kwa
wanawake.They call me
handsome,baby na majina
yote ya kimahaba.Wengine
kwa sura hii hii
wananiambia eti nimefanana
na P didy.Nyie wanawake
Mungu anawaona” akasema
Gosu Gosu na wote
wakaangua kicheko
“Mkeo yuko
wapi?akauliza Agatha
“Sina mke”
“Kwa nini mtu mwenye
mafanikio makubwa kama
haya usiwe na mke mpaka
leo?Utaruka ruka hadi lini?
Au unasubiri ufungue shirika
la ndege ndipo uamue kuwa
na familia?akauliza Agatha
“Ngoja nikueleze ukweli
Agatha mali hizi
unazoziona,jumba lile
kubwa,magari si
vyangu.Mimi ni msimamizi
tu.Mali hii ina mwenyewe
hivyo usione kama
nimefanikiwa” akasema
Gosu Gosu na sura ya
Agatha ikaonyesha
mshangao kidogo
“Nimeona nikwambie
ukweli mapema ujue kwani
wanaume wengi hawapendi
kusema ukweli.Sipendi
kumdanganya malaika kama
wewe kwamba mali hizi ni
zangu.Mimi ni msimamizi tu
yupo mwenyewe” akasema
Gosu Gosu na Agatha
akacheka
“Nimekuwa malaika
tena”
“Hujioni katika kioo
ulivyo Agatha?Mungu
amekupendelea na kukupa
ile sura ya
kimalaika.Wanawake
wachache sana waliojaliwa
uzuri wa aina yako” akasema
GosuGosu na Agatha
akatabasamu
“Una maneno mengi sana
Gosu Gosu.By the way what’s
your real name?akauliza
Agatha
“Jina langu mimi ni hilo
hilo Gosu Gosu sina jina
lingine”
“Una lafudhi ya
kikongo.Umewahi kuishi
kule?
“Ndiyo mimi asili yangu
ni jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo lakini kwa sasa ni
mtanzania.Ninafurahi sana
kuwa mtanzania” akasema
Gosu Gosu
Walifika kati kati ya jiji
Gosu Gosu akaegesha gari
katika mgahawa Fulani
wakashuka na kuingia ndani
wakaagiza supu.Agatha
akaiwasha simu yake na
kumpigia Samson.
Katika idara ya siri ya
usalama wa ndani wa
nchi,simu ya Samson ilikuwa
imewekwa katika kifaa
maalum na mara tu ilipoita
jina la Agatha
likaonekana.Lucas ambaye
alikuwa amekabidhiwa
jukumu la kuifuatilia simu
ile haraka haraka akainua
simu na kumpigia Tamar
akamjulisha kwamba Agatha
anapiga.Haraka haraka
Tamar akatoka ofisini kwake
na kumfuata Lucas katika
meza yake.
“Umefuatilia kujua
anapiga kutokea
wapi?akauliza Tamar.Lucas
akabonyeza kompyuta yake
kisha ramani ikatokea katika
runinga kubwa.
“Yuko mtaa wa Ali
Mzawa”
“Good job.Alex chukua
kikosi cha watu watano
mumfuate Agatha haraka
sana.Yuko mtaa wa Ali
Mzawa tutakuwa tunawapa
maelekezo kila mahala
atakakoenda” akasema
Tamar
“Nitakupata
Agatha.Hutaweza
kunikimbia.Huna sehemu ya
kujificha kahaba wewe nchi
hii yote ninaiona katika
kiganja changu!
Nitakapokutia mikononi
nitakuonyesha raha ya
usaliti” akawaza Tamar na
kurejea ofisini kwake
Agatha alipiga simu
mara ya kwanza lakini
haikupokelewa,akapiga mara
ya pili lakini haikupokelewa.
“Something is not
right.Samson huwa ana kifaa
cha kupokelea simu sikioni
na haijawahi kutokea hata
mara moja nikapiga simu
mara mbili bila
kupokelewa”akasema Agatha
na kunyamaza kidogo
wakatazamana
“He must be in trouble”
akasema Akasema Agatha na
kuizima simu yake
akachomoa betri.
“Twende tuondoke hapa
haraka sana.Lazima
watakuwa wanaifuatilia
simu yangu na watajua niko
hapa” akasema Agatha
GosuGosu akamrushia
muhudumu noti mbili za elfu
kumi kumi kulipia supu ile
ambayo ilikwisha letwa
mezani wakaondoka
“Tunaelekea wapi?
Akauliza Gosu Gosu
“Nataka twende
nyumbani kwake tukajue
kama ana tatizo lolote.Nina
wasi wasi yawezekana
wakawa wamegundua
kwamba kirusi kile
nilichokipandikiza katika
mfumo wao kilipitia katika
akaunti yake.Kama
wakiligundua hilo nitakuwa
nimemuweka katika wakati
mgumu sana” akasema
Agatha na kumuelekeza
GosuGosu anakoishi Samson
Iliwachukua zaidi ya
dakika hamsini kuwasili
katika mtaa anakoishi
Samson.Mara tu
walipokaribia katika nyumba
ya Samson walikutana na
umati mkubwa wa watu na
magari ya polisi.
“Nini kimetokea pale?Ni
karibu sana na nyumbani
kwa Samson” akasema
Agatha kwa woga.Gosu Gosu
akaegesha gari pembeni
“Stay in the
car.Ninakwenda kuangalia
nini kimetokea”akasema
Gosu Gosu na kushuka
garini akaenda kuungana na
umati ule mkubwa wa watu
“Kuna nini hapa”
akamuuliza kijana mmoja
aliyekuwa karibu yake
“Kuna kijana mmoja
amejipiga risasi asubuhi ya
leo”
“Unamfahamu kijana
huyo?
“Ndiyo ninamfahamu
kwa sura lakini nimesikia
watu wanaomfahamu vyema
wanamuita Samson”
“Wanadai nini sababu ya
kujipiga risasi?akauliza
GosuGosu
“Hakuna anayefahamu
hadi sasa chanzo cha
kujipiga risasi lakini wengine
wanadai ni sababu za
kimapenzi ila hakuna
mwenye uhakika” akajibu
Yule kijana.Gosu Gosu
hakutaka kuendelea
kupoteza muda akarejea
garini
“He’s dead.Samson is
dead.Amejiua kwa kujipiga
risasi leo asubuhi” akasema
Gosu Gosu.Agatha akainama
na kuangua kilio.Gosu Gosu
akawasha gari wakaondoka
“Agatha usilie tafadhali
huu ni wakati wa kuwa
imara sana.Mambo ndiyo
kwanza yameanza” akasema
Gosu Gosu
“Samson asingeweza
kujiua na hakuwa na sababu
ya kujiua lazima watakuwa
wamegundua kile
nilichokifanya kupita
akaunti yake na ili
kujiepusha na matatizo
akaamua kujiua.Moyo
unaniuma sana ni mimi
ambaye nimesababisha kifo
chake”akasema Agatha
akiendelea kulia
“Agatha usijilaumu
tafadhali kwa kile
ulichokifanya”
“I did that to protect
President but…….” Agatha
akanyamaza na kufuta
machozi
“Inauma kwani juhudi
zote hizi za kumsaidia Rais
lakini yeye ndiye amekuwa
mstari wa mbele kuturudisha
nyuma.Gosu Gosu please
help me to get out of the
country.Kama nikiendelea
kukaa hapa Tanzania mimi
na familia yangu
tutauawa.Hakuna mahala
ndani ya Tanzania ambako
tunaweza kujificha na
kuamini tuko salama”
akasema Agatha
“Agatha
usihofu.Nitakulinda na
utakuwa salama”
“Gosu Gosu you don’t
know these people they’re
powerfull.Wana uwezo wa
kufika kokote kule” akasema
Agatha
“Naomba uniamini
tafadhali.Nitakulinda kama
nilivyokuahidi” akasema
Gosu Gosu na mara ukaingia
ujumbe katika simu
yake.Mwendo wa gari
ulikuwa wa taratibu sana
kutokana na
foleni.Akaufungua ujumbe
ujumbe ule akausoma
“Tukutane sasa hivi
Msanzi hotel.Kuna jambo la
muhimu sana.Austin”
Ndivyo ulivyosomeka
ujumbe ule
“Austin kwa nini
ameamua kutumia namba
nyingine kunitumia
ujumbe?Kwa nini hajatumia
namba yake ya
kawaida?akajiuliza Gosu
Gosu na kuamua kumpigia
kupitia namba ile
aliyotumiwa ujumbe.
“Hallow”akasema Gosu
Gosu
“Papaa najua
umeshangaa lakini hiyo ni
namba yangu nyingine
ambayo huwa ninaitumia
kwa dharura.Naomba
tafadhali tukutane mahala
nilipokuelekeza”akasema
Austin
“Kuna nini
Austin?akauliza Gosu Gosu
“Nitakueleza utakapofika
Papaa lakini ni jambo la
muhimu sana” akasema
Austin
“Sawa ninampeleka
Agatha nyumbani halafu
nitakuja hapo”akajibu Gosu
Gosu