Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 1
ARUSHA
Kikao cha wakuu wa nchi
za jumuiya ya Afrika
Mashariki kilichofanyika
katika makao makuu ya
jumuiya hiyo yaliyopo
Arusha Tanzania
kilimalizika kwa mafanikio
makubwa.Kikao hicho cha
kawaida kilichohudhuliwa na
marais kutoka nchi zote sita
zinazounda jumuiya ya
Afrika Mashariki,kilipokea
na kujadili taarifa mbali
mbali zinazohusu jumuia
hiyo ikiwamo taarifa
kuhusiana na mchakato wa
uanzishwaji wa sarafu moja
ya Afrika Mashariki
ulikofikia.Kikao hicho pia
kilijadili ombi la nchi ya
jamhuri ya kidemokrasi ya
Congo kujiunga na jumuiya
hiyo na kuikubali kuwa
mwanachama wa saba wa
jumuiya hiyo.Jambo lingine
lililofanyika katika kikao
hicho ni nchi ya Tanzania
kuchukua nafasi ya uenyekiti
wa jumuiya kwa muda wa
mwaka mmoja.
Baada ya kikao
kumalizika na wakuu wa
nchi kuzungumza na wana
habari kuhusu yale yaliyojiri
katika kikao hicho,wakuu
wote wa nchi walielekea
katika hoteli ya Kobe Village
kwa ajili ya kupata chakula
cha mchana na baada ya
chakula baadhi ya wakuu wa
nchi waliondoka na walibaki
wachache waliokuwa na
mazungumzo binafsi na Rais
wa Tanzania na baada ya
kumaliza mazungumzo yao
marais wa Kenya na Burundi
wakaondoka akabaki Rais
Patrice Eyenga wa jamhuri
ya kidemokrasia ya Congo
ambaye alikuwa na
mazungumzo binafsi na
mwenyekiti wa jumuiya ya
Afrika mashariki rais wa
Tanzania Dr Fabian Kelelo.
Dr Fabian alimkaribisha
Rais Patrice katika chumba
chake kwenye hoteli kubwa
jijini Arusha Kobe village
kwa ajili ya mazungumzo
maalum.Walinzi wote wa
marais hawa wawili
wakabaki nje na kuwapa
nafasi wakuu wao
wazungumze faragha.
“Karibu sana ndugu
Patrice” akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais Dr
Fabian kwanza
ninakushukuru sana kwa
namna ulivyojitahidi katika
kikao kuwashawishi marais
wakubali ombi la nchi yangu
kujiunga na jumuiya hii.Ni
muda mrefu tumekuwa
tukiitafuta nafasi ya
kujiunga na jumuiya ya
Afrika mashariki lakini
migogoro na mapigano
yasiyokwisha nchini kwetu
ndivyo
vimetuchelewesha.Ninashuk
uru sana kwa kutukubali na
sisi tuingie katik ajumuiya
hii.Ni furaha kubwa kwa
wananchi wa Congo kujiunga
na wenzao ” akasema Rais
Patrice Eyenga
“Mheshimiwa Patrice
ninakupongeza sana kwa
maamuzi haya makubwa ya
kuiunganisha nchi yako na
jumuiya ya Afrika
mashariki.Ninaamini nchi
yako itanufaika sana na
fursa zilizomo katika
jumuiya hii.Kuna maombi
mengi ya nchi zinazotaka
kujiunga na jumuiya hii
lakini tumeyachambua na
baaadhi ya nchi
zimekataliwa nyingine
tunaendelea kuzijadili lakini
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo tumewakubali kwa
kuwa ninyi ni ndugu zetu
tunafanya biashara pamoja
na kushirikiana katika
mambo mbali mbali ya
kiuchumi hivyo mnastahili
kabisa kujiunga na jumuiya
ya Afrika Mashariki”
akasema Dr Fabian
“Kwa niaba ya wananchi
wa Congo ninashukuru sana”
akasema Patrice na ukimya
ukapita mle ndani
“Karibu sana tuijenge
afrika Mashariki” akasema
Dr Fabian na ukimya mfupi
ukapita kisha Patrice
akasema
“Dr Fabian tukiachana
na hilo la kukubaliwa
uanachama kuna jambo
lingine kubwa ambalo
nataka kuzungumza nawe ili
kwa pamoja tuone namna ya
kulitatua” akasema Rais
Patrice
“Karibu” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa
Rais,Tanzania na Congo
tumekuwa marafiki na
ndugu kwa miaka
mingi.Tanzania imekuwa ni
nyumbani kwa watu wa
Congo.Kila pale
kulipokosekana amani nchini
kwetu wengi wa watu wa
Congo walikimbilia
huku.Watu wetu wameishi
hapa kwa amani miaka
nenda rudi na kwa sasa
baada ya machafuko vita na
mauaji kumalizika,raia wote
wa Congo waliokuwa
wakiishi katika nchi
mbalimbali kama wakimbizi
wameanza kurejea nyumbani
na kwa pamoja tunaijenga
Congo mpya.Uchumi wetu
umeanza kukua,viwanda
vingi vinajengwa,miundo
mbinu inaboreshwa na kwa
nafasi hii tuliyoipata ya
kujiunga na jumuiya ya
Afrika mashariki nina imani
tutapiga hatua kubwa sana
na ndani ya miaka michache
ijayo nchi ya Congo uchumi
wake utapaa kwa kasi ya
kushangaza kwani ni nchi
tajiri imejaa
rasilimali.Tunataka raia wa
Congo wafaidike na
rasilimali ambazo Mungu
amewajalia.Kwa ujumla
tunakwenda vizuri” akasema
Patrice na kunyamaza kidogo
“Patrice binafsi
ninapenda sana
kukupongeza kwa namna
ulivyofanikiwa kuirejesha
amani ya Congo.Wamepita
maraisi wengi na wamefanya
mengi lakini katika suala la
amani wamejaribu
wakashindwa.Umetokea
wewe na kuishangaza dunia
kwa kuirejesha amani
Congo.Nakushauri Patrice
hakikisha hakutokei tena
chokochoko zozote za kuweza
kuvuruga amani hii
mliyoipata baada ya kuikosa
kwa miaka mingi na amabyo
mmeipata k3a gharama
kubwa.Damu nyingi
imemwagika katikakuipata
amani hii hivyo dhibiti
viashiria vyovyote vile
ambavyo vinaweza
kusababisha mkarejea
mahala mlikotoka katika
mapigano.Nchi ya Congo
mlipaswa kuwa nchi
inayoongoza kwa uchumi
mkubwa barani Afrika lakini
mmecheleweshwa kwa
sababu ya migogoro
isiyokwisha.Narudia tena
kukupongeza wewe kwa
juhudi zako na watu wako
kuamua kuweka silaha chini
na kuijenga nchi.Bado mnayo
safari ndefu na wewe kama
kiongozi wa safari hiyo
simama imara nina uhakika
mkubwa mtafika mahala
ambako mnataka
kufika”akasema Dr Fabian
“Dr Fabian hicho ndicho
hasa kilichonileta hapa
kwako.Tunakaribia kuingia
katika uchaguzi mkuu wa
rais na wabunge.Hivi sasa ni
mchakato wa teuzi ndani ya
vyama unaendelea na chama
changu tayari kimekwisha
niteua mimi niwanie tena
urais kwa muhula
mwingine.Chama cha CDP
ambacho ndicho chama
kikuu cha upinzani wao
wamemteua Lucy Muganza
kuwa mgombea wao.Lucy
Muganza ni mwanamama
bilionea,ana viwanda vingi
vikubwa na amewekeza sana
katika sekta ya madini.Huyu
mwanamama ana ushawishi
mkubwa katika siasa za
Congo na ni mmoja wa watu
anayependwa sana.Kwa
miaka mingi amekuwa
akisaidia walemavu,akina
mama na vijana.Ana taasisi
zake zinazosaidia watu
masikini na watu wengi
wamefanikiwa kujikwamua
katika umasikini kupitia
yeye na ndiyo CDP
walipomtangaza kuwa
mgombea wao,kulikuwa na
shangwe karibu kila kona ya
Congo kuonyesha
kufurushishwa na nia yake
ya kutaka kuwania
urais.Binafsi najiamini
nimefanya mambo makubwa
na ninanguvu kubwa katika
uchaguzi ujao lakini
kuchaguliwa kwa Lucy
Muganza kumebadili upepo
wa uchaguzi na nina hakika
nitakutana na wakati
mgumu sana.Pamoja na
mengi mazuri aliyoyafanya
pamoja na kukubalika kwake
lakini watu wa Congo
hawamfahamu Lucy
Muganza ni nani.Naamini
kama wangemfahamu
wasingeingia mitaani
kushangilia uteuzi wake”
Patrice akanyamaza kidogo
halafu akaendelea
“Tetesi za Lucy
kuteuliwa kugombea urais
na chama cha CDP nilizipata
muda mrefu na kama
kawaida yetu wanasiasa
nilijua lazima kutatokea
mchuano mkali kati yangu
naye na nikaweka timu
maalum ya majasusi ambao
wamekuwa wakimchunguza
kwa siri nyendo zake ndipo
nikagundua kuwa Lucy ni
hatari sana kwa usalama wa
Congo” akanyamaza tena
kwa sekunde chache na
kuendelea
“Tulichogundua ni
kwamba,Lucy anatumiwa na
mataifa ya magharibi kutaka
kuivuruga Congo na hata
kugombea urais si utashi
wake bali amesukumwa na
nchi za Magharibi afanye
hivyo.Utajiuliza nini sababu
ya Lucy kutumiwa na nchi
tajiri kutaka kuiharibu
Congo? Sababu kubwa ni
hii.Nilipoingia madarakani
nchi ya Congo bado ilikuwa
katika vita na mauaji.Bado
rasilimali zetu za madini
zilikuwa zinatoroshwa na
kuzifaidisha nchi
tajiri.Tulichokifanya mimi na
serikali yangu ni kwanza
kurejesha amani Congo na
tukafanikiwa.Baada ya
mapigano kumalizika
kilichofuta kilikuwa ni
kukata mirija yote ya
wanyonyaji wa rasilimali
zetu na hili halikuwapendeza
wakubwa wa huko nje
waliokuwa wakifaidika kwa
kiasi kikubwa na rasilimali
za madini kutoka Congo
ndiyo maana wanataka
kutumia uchaguzi huu
kikamilifu kuhakikisha mtu
wao ambaye atawarejesha
katika kuendelea kuchota
rasilimali za Congo
anashinda uchaguzi.Taarifa
nilizonazo ni kwamba Lucy
ambaye yuko ufaransa kwa
sasa,ameendelea kufanya
vikao vya siri na watu hao
wanaomtaka awe rais wa
Congo wakijadili mikakati
mbali mbali ya kupata
ushindi.Ninakiri Lucy ana
nguvu kubwa sana nchini
Congo na kuna nyakati
ninakuwa na hofu kwamba
ninaweza nikashindwa na
yeye akaibuka mshindi
katika uchaguzi mkuu
ujao.Endapo Lucy atashinda
uchaguzi basi lengo la watu
walio nyuma yake ni
kuirejesha nchi ya Congo
kule ilikotoka katika
machafuko na kuwapa
mabeberu nafasi ya
kuendelea kunyonya
rasilimali zetu wakati sisi
tukipigana kwani ili
watunyonye lazima kwanza
watuvuruge tushindwe
kuelewana wenyewe kwa
wenyewe na hapo wanapata
nafasi nzuri ya kuchota
madini yetu na rasilimali
nyingine bila huruma”
akanyamaza na kunywa
funda la maji halafu
akaendelea
“Lucy Muganza si hatari
kwa Congo pekee bali kwa
jumuiya nzima ya Afrika
Mashariki.Kitendo cha
Congo kujiunga na jumuiya
ya Afrika Mashariki
hakijawafurahisha hawa
wakubwa hivyo wanao
mkakati wa kuisambaratisha
jumuiya hii ambayo uwepo
wake ni kikwazo kikubwa
kwao katika kuendeleza
unyonyaji wa rasilimali za
nchi wanachama kwani nchi
zote ndani ya jumuiya
zinasimama pamoja na
kuzungumza lugha moja
hasa linapokuja suala la
kulinda rasilimali zilizopo
katika nchi zetu.Jumuiya ya
Afrika Mashariki imestawi
sana na kuwa mfano barani
Afrika kiasi cha kuvutia nchi
nyingi kutaka kujiunga
itasambaratika endapo Lucy
Muganza atafanikiwa
kushinda uchaguzi na
kuingia madarakani”
akasema Patrice na
kunyamaza.Dr Fabian bado
alikuwa kimya akisikiliza
“Ipi mikakati yao
kuihujumu jumuiya ya
Afrika Mashariki?akauliza
Dr Fabian
“Dr Fabian unajua ni
kwa nini sikutaka
kulizungumza jambo hili
mbele ya maraisi wengine?
Ni kwa sababu kuna baadhi
ya maraisi tayari wana
mahusiano ya karibu na ya
siri sana na Lucy
Muganza.Hata kabla ya
kushinda uchaguzi tayari
amekwisha anza mikakati ya
kuisambaratisa jumuiya.Upo
mpango wa siri unaandaliwa
wa kuunda jumuiya nyingine
ndogo ya nchi tatu pale
jumuiya hii ya nchi saba
itakapokuwa
imesambaratishwa.Mwanam
ke huyu ni nyoka mkubwa na
anapaswa kukanyagwa
kichwa haraka sana kabla
hajaleta madhara” akasema
Patrice
“Hilo ni suala zito sana
Patrice.Sikuwahi kufikiri
kama ndani ya jumuiya hii
kunaweza kutokea jambo la
namna hiyo.Hili unalonieleza
kuhusu baadhi ya marais
kutaka kujiunga na Lucy
kuanzisha jumuiya yao ndogo
una uhakika nalo?akauliza
Dr Fabian
“Ndiyo Dr Fabian.Ninao
uhakika mkubwa kwamba
kuna jumuiya mpya ya nchi
tatu inataka kuanzisha
baada ya jumuiya hii kubwa
kusambaratishwa”akajibu
Patrice
“Ni marais gani ambao
tayari Lucy ameanza
kuzungumza nao juu ya
jambo hilo?akauliza Dr
Fabian.Patrice akaufungua
mkoba wake akatoa faili na
kumpatia DrFabian.
“What is this?akauliza Dr
Fabian
“Tumekuwa tukifuatilia
mawasiliano yote ya Lucy na
ndani ya faili hilo kua
mawasiliano yake yote
anayoyafanya na marais hao
wawili na kupanga mipango
yao ya kuanzisha jumuiya
mpya ya nchi tatu” akasema
Patrice na Dr Fabian
akaanza kufungua kurasa
moja moja
“Nitakuachia faili hilo
utaendelea kulipitia
taratibu.Kila kitu kiko humo
kuanzia mawasiliano ya
simu,barua pepe na katika
hiyo diski kuna kuna rekodi
za mazungumzo yao ya simu”
akasema Patrice.Dr Fabian
akalifunika lile faili halafu
akasimama akazunguka mle
chumbani huku akitazama
juu halafu akajiegemeza
katika meza na kusema
“Wakoloni hawa
wametutawala tukawa
watumwa wao,wamechukua
rasilimali zetu na kutajirisha
nchi zao huku wakituachia
umasikini
mkubwa.Tunapofanya juhudi
za kujikomboa wao
wanatumia uwezo walio nao
kuhakikisha hatusongi mbele
tunabaki pale pale tulipo na
kama haitoshi bado
wanaendelea na mipango ya
kutaka kuendelea
kutuibia.Ni kwa sababu yao
mifarakano katika bara la
Afrika haiishi.Kila mahala ni
vurugu na ukichunguza
chanzo chake utakuta kuna
mkono wa mataifa
makubwa.Wanasema Afrika
imelaaniwa,ninakataa Afrika
hatujalaaniwa bali wao
wanaokuja kutuibia
rasilimali zetu tulizopewa na
Mungu ndio
waliolaaniwa.Inashangaza
sana kuona mpaka sasa bado
kuna watu tena viongozi
wakubwa wanaendelea
kuwaabudu hawa mabeberu
na wako tayari kufanya
jambo lolote kwa ajili yao
hata kumwaga damu za
ndugu zao ili mradi
kuwafurahisha
mabeberu.Patrice
tunatakiwa kusimama na
kusema hapana kwa
unyonyaji huu.Wazee wetu
akina mzee
Nyerere,Lumumba na
wengineo walijioa
kupambana kuhakikisha
tunajikomboa kutoa katika
makucha ya wanyonyaji ni
jukumu letu na sisi
kusimama imara
kuhakikisha unyonyaji huu
hauendelei.Jumuiya ya
Afrika mashariki kweli ni
mwiba kwao kwani tumekata
mirija ya wanyonyaji na sasa
wanahangaika kutaka
kuivunja” akasema Dr
Fabian
“Ahsante kwa kunielewa
Dr Fabian sasa
tunazungumza lugha
moja.Tanzania imechukua
uongozi wa jumuiya hii sitaki
isambaratikie mikononi
mwako ndiyo maana
ninataka tufanye kila
linalowezekana kuhakikisha
kwamba lengo la mabeberu
hawa halitimii.Tupambane
tuiokoe Congo na tuiokoe
jumuiya ya Afrika mashariki
ambayo wenzetu wanafikiria
kuivunja.Binasi siko tayari
nchi yangu irejee kama
ilivyokuwa zamani Congo ya
vita na mauaji
yasiyokwisha.Imetugharimu
miaka mingi na gharama
kubwa kuipata amani hii
tuliyonayo sasa.Siko tayari
kuipoteza na kuwaacha
mabeberu wakiendelea
kufaidika na rasilimali
zetu,nitapambana hadi tone
la mwisho la damu kuifia
nchi yangu.Hata kama ni
kutawala kwa lazima
nitafanya hivyo kuilinda
amani ya Congo na kuzuia
mabeberu wasithubutu tena
kukanyaga katika ardhi yetu
ndiyo maana nimekuja
kwako rafiki yangu na ndugu
yangu kuomba msaada
wako.Tanzania mmekuwa
nasi wakati wote wa
machafuko na hamjawahi
kutuacha hata mara moja na
ninaamini hamtatuacha hata
sasa tunapohitaji kuilinda
amani yetu kwa gharama
zozote”akasema Patrice.Dr
Fabian akamtazama kwa
makini halafu akauliza
“Nini ushauri wako
katika hili Patrice? Akauliza
Dr Fabian.Ilipita dakika
moja Patrice akasema
“Ni kumuua Lucy
Muganza” akasema na
kunyamaza kwanza ili kile
alichokitamka kimuingie Dr
Fabian halafu akaendelea
“Hiyo ndiyo njia pekee
iliyobaki ya kuliepusha taifa
la Congo kurejea kule
lilikotoka,kuikoa jumuiya ya
Afrika mashariki na kuzima
kabisa ndoto za mabeberu za
kutaka kuendelea kunyonya
nchi zetu.Ni uamuzi mgumu
lakini ndiyo njia pekee ya
kulimaliza hili suala.Binafsi
nimeishi katika shida
kubwa,nimesoma kwa taabu
ninafahamu mateso
waliyokuwa wakiyapata
watu wa Congo ndiyo maana
yeyote anayecheza na amani
ya Congo ni adui yangu
mkubwa.Lucy Muganza ni
hatari sana kwa amani yetu
ndiyo maana ninashauri
tumuondoe” akasema Patrice
na ukimya ukatawala mle
ndani halafu Dr Fabian
akasema
“Patrice sina kipingamizi
chochote na hicho
unachokisema lakini nina
maswali machache.Huyu
mama kama ulivyosema ni
maarufu sana nchini Congo
na ana wafuasi wengi,kama
tukimuua hudhani wafuasi
wake wanaweza wakahisi ni
serikali ndiyo waliofanya
mpango huo wa mauaji na
vurugu kubwa
zikaanza?Jambo lingine hata
kama akiuawa Lucy hawa
wakubwa walioko nyuma
yake hawataweza kutafuta
mtu mwingine ambaye
atachukua nafasi ya Lucy na
kuendeleza mikakati
yao?Kama wakifanya hivyo
tutaendelea kuua kila
atakayeteuliwa?
“Mtu mwingine
wanaweza wakampata ili
kuendelea na mipango yao
lakini hatakuwa na
umaarufu mkubwa kama
Lucy.Huyu mama licha ya
kuungwa mkono na nchi za
Magharibi lakini hata yeye
binafsi nguvu yake ya
ushawishi ni
kubwa.Angeweza hata
kusimama peke yake bila ya
kuungwa mkono na nchi za
magharibi na akashinda
uchaguzi.Tukimuondoa huyu
mama itawapa hata wao
wakati mgumu wa kutafuta
mtu ambaye ana uwezo
kama Lucy na hii
itanihakikishia mimi
ushindi.Kuhusu vurugu
haitakuwa rahisi kutokea
kwani Lucy hatauawa akiwa
Congo.Atauawa akiwa hapa
Tanzania”
“Tanzania?! Dr Fabian
akashangaa
“Ndiyo.Akiuliwa hapa
Tanzania haitakuwa rahisi
mtu yeyote kuhisi kama
serikalio ya Congo inahusika
na mauaji hayo”akasema
Patrice na Dr Fabian
akavuta pumzi ndefu
“Ni vipi kama ukifanyika
uchunguzi na ikagundulika
kwamba sisi ndio
tuliotekeleza mauaji
hayo,huoni kwamba
Tanzania itachafuka
kimataifa jambo ambalo
sitaki litokee.Tunasifika
duniani kote kwa amani
sitaki sifa hii nzuri iharibike
kwa kufanya mauaji hayo
katika ardhi ya
Tanzania”akasema Dr
Fabian
“Dr Fabian nadhani
umewahi kusikia kuhusu
kufanya maamuzi magumu
na katika mambo kama haya
ndipo maamuzi magumu
hufanyika.Usiwe na hofu
nitatuma kikosi changu kuja
kumuua Lucy ili kuiepusha
nchi yao na lawama.Dr
Fabian ninakuomba tufanye
hivi kwa maslahi ya Congo
na jumuiya yetu ya Afrika
Mashariki.”akasema Patrice
“Tatizo si kumuua Lucy
bali ni kumuua katika ardhi
ya Tanzania.Unafahamu
namna nchi hii
inavyoheshimika
kimataifa,sitaki nchi yangu
ichafuke kama ambavyo
wewe hutaki nchi yako
ichafuke”akasema Dr Fabian
“Dr Fabian wewe ni
mgeni katika uongozi una
mwaka mmoja tu sasa na
humfahamu vyema Lucy
Muganza na inawezekana
hujawahi hata kumtia
machoni lakini ni mwanamke
mwenye nguvu kubwa na
ndiyo maana hata mimi
binafsi ninamuogopa
kwamba akiachwa anaweza
akachukua nchi na
ninavyomfahamu akichukua
nchi atairudisha ilivyokuwa
awali.Ataleta machafuko
katika nchi za maziwa
makuu.Nchi na nchi
hazitaelewana,ule umoja
wetu utatoweka na kila nchi
itasimama yenyewe.Hilondilo
wanalitaka hawa wakubwa
ili waweze kuingia na
kutuibia mali zetu.Ni sisi
wawilitu ambao tunaweza
kuzia hayoyasitokee na njia
pekee ya kuzuia yasitokee ni
kwa kumuua Lucy Muganza”
akasema Patrice.Dr Fabina
alikaa kimya kwa muda
halafu akauliza
“Umekwisha andaa
mpango wa kumuua Lucy?
“Kama nilivyosema
kwamba kuna timu ya
majasusi ambayo
inamfuatilia Lucy kwa siri
kubwa sana.Kwa sasa Lucy
yuko Ufaransa ambako
amekuwa na mfululizo wa
vikao na hao wakubwa
wakifanya mikakati ya
kuhakikisha Lucy anashinda
uchaguzi mkuu
ujao.Jumamosi ya wiki hii
atarejea nyumbani lakini
kabla ya kuelekea Kinshasa
atakuja kwanza
Tanzania.Hapa ana mtoto
wake anayesoma katika chuo
kikuu cha Dar es salaam
anaitwa Theresia
Muganza.Katika safari hiyo
Lucy pia atakuwa ameongoza
na mume wake Laurent na
lengo la kuja Tanzania ni
kumchukua binti yao
Theresia ili waelekee
Kinshasa kama familia
ambako mapokezi makubwa
yanamsubiri Lucy kutoka
kwa malefu ya wafuasi wa
chama cha CDP.Nataka
atakapotia mguu hapa
Tanzania asiondoke hai bali
jeneza lake ndilo lirejeshwe
Congo.Ninacho kikosi
nimekiandaa kwa ajili ya
kazi hiyo ambacho kama
ukiniruhusu nitakituma kuja
kumuondoa Lucy hapa
Tanzania” akasema Patrice
Dr Fabian akawaza kidogo
na kusema
“Patrice wewe ni rafiki
yangu mkubwa,tumekutana
masomoni nje ya nchi na
sasa wote tumeshika nafasi
za urais na siwezi
kukukatalia ombi lako kwa
ajili ya kulinda Afrika
Mashariki na kuilinda amani
ya Congo.Lucy atauawa hapa
Tanzania lakini na watu
wangu.Sitaki watu wa nje
waje kufanya mauaji katika
ardhi yetu.Ninao vijana
mahiri wanaoweza kuifanya
hiyo kazi.Nitakachohitaji
kutoka kwako ni
mawasiliano kati ya timu
yako inayomchunguza Lucy
na timu yangu
nitakayoiandaa kwa ajili ya
kumuondoa” akasema Dr
Fabian.Maongezi yaliendelea
kwa takribani nusu saa
kisha wakaagana Patrice
akaondoka kuelekea
Kinshasa.Kiongozi wa
mwisho kuondoka Arusha
alikuwa ni rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania
Dr Fabian Kelelo.Akiwa
ndani ya ndege alikuwa
kimya akilipitia faili lile
alilopewa na
Patrice.Akaichomeka diski
aliyopewa na Patrice katika
kompyuta na kuanza
kusikiliza mazungumzo
yaliyorekodiwa ya Lucy
Muganza na baadhi ya
viongozi wa nchi zilizo katika
jumuiya ya Afrika Mashariki
“Patrice yuko sahihi
mwanamke huyu ni hatari
sana kwa uhai wa jumuiya
yetu ya Afrika mashariki na
anapaswa kuondolewa
haraka sana kabla hajaleta
madhara.Kinachonishangaza
marais hawa ambao Lucy
amekuwa akiwasiliana nao
wakipanga mikakati ya
kuanzisha jumuiya yao ndogo
ni watu walio mstari wa
mbele sana katika kuhimiza
mshikamano madhubuti
miongoni mwa wanachama
wa jumuiya hii kumbe wana
siri kubwa wanatembea
nayo.Nitapambana
kuhakikisha jumuiya hii
haivunjikii mikononi
mwangu.Nitailinda jumuiya
hii kwa gharama zozote
katika wakati wangu kama
mwenyekiti japo wapo
viongozi ambao wako tayari
ivunjike lakini watasubiri
hadi pale nitakapokuwa
nimemaliza muda wangu wa
uongozi lakini nina hakika
kama tukimuondoa Lucy na
mipango yao yote ya
kuanzisha jumuiya yao ndogo
nayo itayeyuka” akawaza na
kulifunika lile faili
“Lakini bado kuna kitu
kinanipa ukakasi katika akili
yangu.Lucy Muganza ni
tegemeo la mataifa ya
magharibi katika
kufanikisha mipango yao ya
unyonyaji wa rasilimali zetu
ni vipi kama walio nyuma
yake wakiamua kufanya
uchunguzi wa kifo chake na
wakabaini kwamba
ninahusika?Nitakuwa
nimeingia katika mgogoro
mwingine mkubwa na nchi
za magharibi.Nifanye
nini?Nijitoe katika mpango
huu wa kumuua Lucy
Muganza?akajiuliza
“Hapana siwezi kujitoa
katika mpango huu.Tayari
nimekwisha muhakikishia
Patrice kwamba niko pamoja
naye katika suala hili.Hata
mimi siko tayari kuona
machafuko yakirejea tena
Congo kama ilivyokuwa
zamani.Watu wa Congo
wameitafuta amani kwa
miaka mingi na wametumia
gharama kubwa hadi
kuipata.Ni jukumu letu sisi
majirani zao kuhakikisha
amani waliyo nayo haipotei
tena.Kibaya zaidi ni mipango
yao ya kuisambaratisha
jumuiya ya Afrika
Mashariki.Nadhani kumuua
Lucy ndiyo njia pekee ya
kulitatua hili jambo hata
hivyo umakini mkubwa sana
unatakiwa.Ni suala ambalo
linapaswa kupangwa
kitaalamu mno” akawaza Dr
Fabian Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
ambaye katika historia ya
marais waliowahi kuingia
madarakani yeye ndiye
anayetajwa kuwa kijana
kuliko wote na mwenye sura
ya kuvutia.
DAR ES SALAAM
Ni saa saba na dakika
ishirini na moja za usiku
lakini bado Dr Fabian
hakuonekana kuwa na
usingizi.Alikuwa ameketi
sofani akiwa na lundo la
vitabu pembeni yake.Millen
mke wake alimfuata pale
sofani na kukaa karibu yake
akakifunika kitabu
alichokuwa anakisoma mume
wake na kumbusu
“What’s wrong
darling.Uliondoka hapa
kuelekea Arusha ukiwa na
furaha kubwa lakini
umerejea ukiwa katika hali
ya mawazo mengi na
haujazungumza nami kitu
chochote kuhusiana na safari
ya Arusha.Nini kimetokea
huko?akauliza Millen
mwanamke mwenye weupe
wa kung’aa na sura ya upole
yenye tabasamu muda
wote.Dr Fabian akamtazama
mke wake halafu
akatabasamu na kusema
“Usijali Millen.Kila kitu
kiko sawa”
“Hapana.Ninakufahamu
vyema Fabian hauko
sawa.Something is wrong
with you.Nini kimetokea
Arusha? Niambie tafadhali
kama kuna tatizo lolote
nijue”akasema Millen
“Fine” akasema Dr
Fabian na kuvuta pumzi
ndefu
“Arusha mambo
yamekwenda vizuri
hakukuwa na tatizo
lolote.Tumechukua uenyekiti
wa jumuiya ya Afrika
Mashariki kwa muda wa
mwaka mmoja.Kwa ujumla
kila kitu kilikwenda vizuri
kabisa”
“Kama kila kitu
kilikwenda vizuri nini hasa
kinakusumbua kichwa chako
mpenzi wangu?Si kawaida
yako kukaa hapa hadi muda
huu.Nini kinakusumbua?
“Ni kweli Millen nina
tatizo lakini naomba
nisikwambie kwa sasa ni
tatizo gani”
“Hapana nieleze
Fabian.Hakuna tatizo lako
ambalo haujawahi kunieleza”
akasema Millen.Dr Fabian
akamtazama mkewe halafu
akasema
“Toka nimeingia
madarakani nimekutana na
mtihani wangu wa kwanza
mkubwa ambao lazima
niushinde”
“Mtihani upi? Akauliza
Millen na Dr Fabian akavuta
pumzi ndefu
“I need to silence
someone very dangerous”
akasema na kukaa kimya
baada ya kuuona mstuko
katika uso wa mke wake
“You mean killing
somebody?akauliza Millen na
Dr Fabian akatikisa kichwa
kukubali
“Kuna mataifa makubwa
ambayo hayapendi kuona
jumuiya ya Afrika mashariki
inastawi na wanajaribu
kutumia kila njia
kuisambaratisha.Kuna mtu
ambaye wanamtumia katika
kulifanikisha hilo.Njia pekee
ya kumaliza mipango na
njama zao ovu ni kwa
kumuondoa huyo ambaye
wanataka kumtumia lakini
jambo hilo linatakiwa
lifanywe kitaalamu sana
ndiyo maana ninasoma
vitabu hapa kuhusu vifo
mbali mbali vya watu
maarufu vilivyowahi kutokea
duniani na ambavyo mpaka
leo hii havijawahi kupatiwa
ufumbuzi.I want this one to
be unsolved murder”
“Fabian hakuna namna
nyingine ya kuweza
kulishughulikia suala hilo
zaidi ya kuua?I’m scared”
akasema Millen
“Millen nimekushirikisha
jambo hili la siri kubwa
ambalo sikupaswa
kukueleza.Natamani
ningekuwa na njia nyingine
ya kuweza kuliondoa tatizo
hilo zaidi ya hii ninayotaka
kuifanya lakini hakunanjia
nyingine.It’s hard even for
me but I have to do it.Mtu
huyo ni hatari na si kwa
jumuiya ya Afrika mashariki
pekee bali ni hatari pia kwa
amani ya Congo.Umewahi
kufanya kazi katika shirika
la umoja wa mataifa la
kuhudumia wakimbizi
unafahamu mateso na taabu
wanazopitia wakimbizi,mtu
huyo anataka kutumiwa
kuirejesha Congo katika
machafuko ili mabeberu
waweze kurejea tena na
kuendelea kuchota rasilimali
za nchi hiyo.I won’t let that
happen ! akasema Dr Fabian
“Hofu yangu Dr Fabian
ni vipi kama ukifanyika
uchunguzi na ikabainika
kwamba unahusika na
mauaji hayo?akauliza Millen
“That won’t happen.Ni
jambo ambalo litafanywa
kitaalamu mno ndiyo maana
nikakwambia kwamba
nataka jambo hili lisiweze
kupatiwa ufumbuzi hata
kama wataamua
kulichunguza” akasema Dr
Fabian.Mke wake
hakuzungumza tena kitu
kingine akamshika mkono
mumewe na kumuongoza
kwenda chumbani
kupumzika kwani muda
ulikuwa umekwenda sana.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 1
ARUSHA
Kikao cha wakuu wa nchi
za jumuiya ya Afrika
Mashariki kilichofanyika
katika makao makuu ya
jumuiya hiyo yaliyopo
Arusha Tanzania
kilimalizika kwa mafanikio
makubwa.Kikao hicho cha
kawaida kilichohudhuliwa na
marais kutoka nchi zote sita
zinazounda jumuiya ya
Afrika Mashariki,kilipokea
na kujadili taarifa mbali
mbali zinazohusu jumuia
hiyo ikiwamo taarifa
kuhusiana na mchakato wa
uanzishwaji wa sarafu moja
ya Afrika Mashariki
ulikofikia.Kikao hicho pia
kilijadili ombi la nchi ya
jamhuri ya kidemokrasi ya
Congo kujiunga na jumuiya
hiyo na kuikubali kuwa
mwanachama wa saba wa
jumuiya hiyo.Jambo lingine
lililofanyika katika kikao
hicho ni nchi ya Tanzania
kuchukua nafasi ya uenyekiti
wa jumuiya kwa muda wa
mwaka mmoja.
Baada ya kikao
kumalizika na wakuu wa
nchi kuzungumza na wana
habari kuhusu yale yaliyojiri
katika kikao hicho,wakuu
wote wa nchi walielekea
katika hoteli ya Kobe Village
kwa ajili ya kupata chakula
cha mchana na baada ya
chakula baadhi ya wakuu wa
nchi waliondoka na walibaki
wachache waliokuwa na
mazungumzo binafsi na Rais
wa Tanzania na baada ya
kumaliza mazungumzo yao
marais wa Kenya na Burundi
wakaondoka akabaki Rais
Patrice Eyenga wa jamhuri
ya kidemokrasia ya Congo
ambaye alikuwa na
mazungumzo binafsi na
mwenyekiti wa jumuiya ya
Afrika mashariki rais wa
Tanzania Dr Fabian Kelelo.
Dr Fabian alimkaribisha
Rais Patrice katika chumba
chake kwenye hoteli kubwa
jijini Arusha Kobe village
kwa ajili ya mazungumzo
maalum.Walinzi wote wa
marais hawa wawili
wakabaki nje na kuwapa
nafasi wakuu wao
wazungumze faragha.
“Karibu sana ndugu
Patrice” akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais Dr
Fabian kwanza
ninakushukuru sana kwa
namna ulivyojitahidi katika
kikao kuwashawishi marais
wakubali ombi la nchi yangu
kujiunga na jumuiya hii.Ni
muda mrefu tumekuwa
tukiitafuta nafasi ya
kujiunga na jumuiya ya
Afrika mashariki lakini
migogoro na mapigano
yasiyokwisha nchini kwetu
ndivyo
vimetuchelewesha.Ninashuk
uru sana kwa kutukubali na
sisi tuingie katik ajumuiya
hii.Ni furaha kubwa kwa
wananchi wa Congo kujiunga
na wenzao ” akasema Rais
Patrice Eyenga
“Mheshimiwa Patrice
ninakupongeza sana kwa
maamuzi haya makubwa ya
kuiunganisha nchi yako na
jumuiya ya Afrika
mashariki.Ninaamini nchi
yako itanufaika sana na
fursa zilizomo katika
jumuiya hii.Kuna maombi
mengi ya nchi zinazotaka
kujiunga na jumuiya hii
lakini tumeyachambua na
baaadhi ya nchi
zimekataliwa nyingine
tunaendelea kuzijadili lakini
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo tumewakubali kwa
kuwa ninyi ni ndugu zetu
tunafanya biashara pamoja
na kushirikiana katika
mambo mbali mbali ya
kiuchumi hivyo mnastahili
kabisa kujiunga na jumuiya
ya Afrika Mashariki”
akasema Dr Fabian
“Kwa niaba ya wananchi
wa Congo ninashukuru sana”
akasema Patrice na ukimya
ukapita mle ndani
“Karibu sana tuijenge
afrika Mashariki” akasema
Dr Fabian na ukimya mfupi
ukapita kisha Patrice
akasema
“Dr Fabian tukiachana
na hilo la kukubaliwa
uanachama kuna jambo
lingine kubwa ambalo
nataka kuzungumza nawe ili
kwa pamoja tuone namna ya
kulitatua” akasema Rais
Patrice
“Karibu” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa
Rais,Tanzania na Congo
tumekuwa marafiki na
ndugu kwa miaka
mingi.Tanzania imekuwa ni
nyumbani kwa watu wa
Congo.Kila pale
kulipokosekana amani nchini
kwetu wengi wa watu wa
Congo walikimbilia
huku.Watu wetu wameishi
hapa kwa amani miaka
nenda rudi na kwa sasa
baada ya machafuko vita na
mauaji kumalizika,raia wote
wa Congo waliokuwa
wakiishi katika nchi
mbalimbali kama wakimbizi
wameanza kurejea nyumbani
na kwa pamoja tunaijenga
Congo mpya.Uchumi wetu
umeanza kukua,viwanda
vingi vinajengwa,miundo
mbinu inaboreshwa na kwa
nafasi hii tuliyoipata ya
kujiunga na jumuiya ya
Afrika mashariki nina imani
tutapiga hatua kubwa sana
na ndani ya miaka michache
ijayo nchi ya Congo uchumi
wake utapaa kwa kasi ya
kushangaza kwani ni nchi
tajiri imejaa
rasilimali.Tunataka raia wa
Congo wafaidike na
rasilimali ambazo Mungu
amewajalia.Kwa ujumla
tunakwenda vizuri” akasema
Patrice na kunyamaza kidogo
“Patrice binafsi
ninapenda sana
kukupongeza kwa namna
ulivyofanikiwa kuirejesha
amani ya Congo.Wamepita
maraisi wengi na wamefanya
mengi lakini katika suala la
amani wamejaribu
wakashindwa.Umetokea
wewe na kuishangaza dunia
kwa kuirejesha amani
Congo.Nakushauri Patrice
hakikisha hakutokei tena
chokochoko zozote za kuweza
kuvuruga amani hii
mliyoipata baada ya kuikosa
kwa miaka mingi na amabyo
mmeipata k3a gharama
kubwa.Damu nyingi
imemwagika katikakuipata
amani hii hivyo dhibiti
viashiria vyovyote vile
ambavyo vinaweza
kusababisha mkarejea
mahala mlikotoka katika
mapigano.Nchi ya Congo
mlipaswa kuwa nchi
inayoongoza kwa uchumi
mkubwa barani Afrika lakini
mmecheleweshwa kwa
sababu ya migogoro
isiyokwisha.Narudia tena
kukupongeza wewe kwa
juhudi zako na watu wako
kuamua kuweka silaha chini
na kuijenga nchi.Bado mnayo
safari ndefu na wewe kama
kiongozi wa safari hiyo
simama imara nina uhakika
mkubwa mtafika mahala
ambako mnataka
kufika”akasema Dr Fabian
“Dr Fabian hicho ndicho
hasa kilichonileta hapa
kwako.Tunakaribia kuingia
katika uchaguzi mkuu wa
rais na wabunge.Hivi sasa ni
mchakato wa teuzi ndani ya
vyama unaendelea na chama
changu tayari kimekwisha
niteua mimi niwanie tena
urais kwa muhula
mwingine.Chama cha CDP
ambacho ndicho chama
kikuu cha upinzani wao
wamemteua Lucy Muganza
kuwa mgombea wao.Lucy
Muganza ni mwanamama
bilionea,ana viwanda vingi
vikubwa na amewekeza sana
katika sekta ya madini.Huyu
mwanamama ana ushawishi
mkubwa katika siasa za
Congo na ni mmoja wa watu
anayependwa sana.Kwa
miaka mingi amekuwa
akisaidia walemavu,akina
mama na vijana.Ana taasisi
zake zinazosaidia watu
masikini na watu wengi
wamefanikiwa kujikwamua
katika umasikini kupitia
yeye na ndiyo CDP
walipomtangaza kuwa
mgombea wao,kulikuwa na
shangwe karibu kila kona ya
Congo kuonyesha
kufurushishwa na nia yake
ya kutaka kuwania
urais.Binafsi najiamini
nimefanya mambo makubwa
na ninanguvu kubwa katika
uchaguzi ujao lakini
kuchaguliwa kwa Lucy
Muganza kumebadili upepo
wa uchaguzi na nina hakika
nitakutana na wakati
mgumu sana.Pamoja na
mengi mazuri aliyoyafanya
pamoja na kukubalika kwake
lakini watu wa Congo
hawamfahamu Lucy
Muganza ni nani.Naamini
kama wangemfahamu
wasingeingia mitaani
kushangilia uteuzi wake”
Patrice akanyamaza kidogo
halafu akaendelea
“Tetesi za Lucy
kuteuliwa kugombea urais
na chama cha CDP nilizipata
muda mrefu na kama
kawaida yetu wanasiasa
nilijua lazima kutatokea
mchuano mkali kati yangu
naye na nikaweka timu
maalum ya majasusi ambao
wamekuwa wakimchunguza
kwa siri nyendo zake ndipo
nikagundua kuwa Lucy ni
hatari sana kwa usalama wa
Congo” akanyamaza tena
kwa sekunde chache na
kuendelea
“Tulichogundua ni
kwamba,Lucy anatumiwa na
mataifa ya magharibi kutaka
kuivuruga Congo na hata
kugombea urais si utashi
wake bali amesukumwa na
nchi za Magharibi afanye
hivyo.Utajiuliza nini sababu
ya Lucy kutumiwa na nchi
tajiri kutaka kuiharibu
Congo? Sababu kubwa ni
hii.Nilipoingia madarakani
nchi ya Congo bado ilikuwa
katika vita na mauaji.Bado
rasilimali zetu za madini
zilikuwa zinatoroshwa na
kuzifaidisha nchi
tajiri.Tulichokifanya mimi na
serikali yangu ni kwanza
kurejesha amani Congo na
tukafanikiwa.Baada ya
mapigano kumalizika
kilichofuta kilikuwa ni
kukata mirija yote ya
wanyonyaji wa rasilimali
zetu na hili halikuwapendeza
wakubwa wa huko nje
waliokuwa wakifaidika kwa
kiasi kikubwa na rasilimali
za madini kutoka Congo
ndiyo maana wanataka
kutumia uchaguzi huu
kikamilifu kuhakikisha mtu
wao ambaye atawarejesha
katika kuendelea kuchota
rasilimali za Congo
anashinda uchaguzi.Taarifa
nilizonazo ni kwamba Lucy
ambaye yuko ufaransa kwa
sasa,ameendelea kufanya
vikao vya siri na watu hao
wanaomtaka awe rais wa
Congo wakijadili mikakati
mbali mbali ya kupata
ushindi.Ninakiri Lucy ana
nguvu kubwa sana nchini
Congo na kuna nyakati
ninakuwa na hofu kwamba
ninaweza nikashindwa na
yeye akaibuka mshindi
katika uchaguzi mkuu
ujao.Endapo Lucy atashinda
uchaguzi basi lengo la watu
walio nyuma yake ni
kuirejesha nchi ya Congo
kule ilikotoka katika
machafuko na kuwapa
mabeberu nafasi ya
kuendelea kunyonya
rasilimali zetu wakati sisi
tukipigana kwani ili
watunyonye lazima kwanza
watuvuruge tushindwe
kuelewana wenyewe kwa
wenyewe na hapo wanapata
nafasi nzuri ya kuchota
madini yetu na rasilimali
nyingine bila huruma”
akanyamaza na kunywa
funda la maji halafu
akaendelea
“Lucy Muganza si hatari
kwa Congo pekee bali kwa
jumuiya nzima ya Afrika
Mashariki.Kitendo cha
Congo kujiunga na jumuiya
ya Afrika Mashariki
hakijawafurahisha hawa
wakubwa hivyo wanao
mkakati wa kuisambaratisha
jumuiya hii ambayo uwepo
wake ni kikwazo kikubwa
kwao katika kuendeleza
unyonyaji wa rasilimali za
nchi wanachama kwani nchi
zote ndani ya jumuiya
zinasimama pamoja na
kuzungumza lugha moja
hasa linapokuja suala la
kulinda rasilimali zilizopo
katika nchi zetu.Jumuiya ya
Afrika Mashariki imestawi
sana na kuwa mfano barani
Afrika kiasi cha kuvutia nchi
nyingi kutaka kujiunga
itasambaratika endapo Lucy
Muganza atafanikiwa
kushinda uchaguzi na
kuingia madarakani”
akasema Patrice na
kunyamaza.Dr Fabian bado
alikuwa kimya akisikiliza
“Ipi mikakati yao
kuihujumu jumuiya ya
Afrika Mashariki?akauliza
Dr Fabian
“Dr Fabian unajua ni
kwa nini sikutaka
kulizungumza jambo hili
mbele ya maraisi wengine?
Ni kwa sababu kuna baadhi
ya maraisi tayari wana
mahusiano ya karibu na ya
siri sana na Lucy
Muganza.Hata kabla ya
kushinda uchaguzi tayari
amekwisha anza mikakati ya
kuisambaratisa jumuiya.Upo
mpango wa siri unaandaliwa
wa kuunda jumuiya nyingine
ndogo ya nchi tatu pale
jumuiya hii ya nchi saba
itakapokuwa
imesambaratishwa.Mwanam
ke huyu ni nyoka mkubwa na
anapaswa kukanyagwa
kichwa haraka sana kabla
hajaleta madhara” akasema
Patrice
“Hilo ni suala zito sana
Patrice.Sikuwahi kufikiri
kama ndani ya jumuiya hii
kunaweza kutokea jambo la
namna hiyo.Hili unalonieleza
kuhusu baadhi ya marais
kutaka kujiunga na Lucy
kuanzisha jumuiya yao ndogo
una uhakika nalo?akauliza
Dr Fabian
“Ndiyo Dr Fabian.Ninao
uhakika mkubwa kwamba
kuna jumuiya mpya ya nchi
tatu inataka kuanzisha
baada ya jumuiya hii kubwa
kusambaratishwa”akajibu
Patrice
“Ni marais gani ambao
tayari Lucy ameanza
kuzungumza nao juu ya
jambo hilo?akauliza Dr
Fabian.Patrice akaufungua
mkoba wake akatoa faili na
kumpatia DrFabian.
“What is this?akauliza Dr
Fabian
“Tumekuwa tukifuatilia
mawasiliano yote ya Lucy na
ndani ya faili hilo kua
mawasiliano yake yote
anayoyafanya na marais hao
wawili na kupanga mipango
yao ya kuanzisha jumuiya
mpya ya nchi tatu” akasema
Patrice na Dr Fabian
akaanza kufungua kurasa
moja moja
“Nitakuachia faili hilo
utaendelea kulipitia
taratibu.Kila kitu kiko humo
kuanzia mawasiliano ya
simu,barua pepe na katika
hiyo diski kuna kuna rekodi
za mazungumzo yao ya simu”
akasema Patrice.Dr Fabian
akalifunika lile faili halafu
akasimama akazunguka mle
chumbani huku akitazama
juu halafu akajiegemeza
katika meza na kusema
“Wakoloni hawa
wametutawala tukawa
watumwa wao,wamechukua
rasilimali zetu na kutajirisha
nchi zao huku wakituachia
umasikini
mkubwa.Tunapofanya juhudi
za kujikomboa wao
wanatumia uwezo walio nao
kuhakikisha hatusongi mbele
tunabaki pale pale tulipo na
kama haitoshi bado
wanaendelea na mipango ya
kutaka kuendelea
kutuibia.Ni kwa sababu yao
mifarakano katika bara la
Afrika haiishi.Kila mahala ni
vurugu na ukichunguza
chanzo chake utakuta kuna
mkono wa mataifa
makubwa.Wanasema Afrika
imelaaniwa,ninakataa Afrika
hatujalaaniwa bali wao
wanaokuja kutuibia
rasilimali zetu tulizopewa na
Mungu ndio
waliolaaniwa.Inashangaza
sana kuona mpaka sasa bado
kuna watu tena viongozi
wakubwa wanaendelea
kuwaabudu hawa mabeberu
na wako tayari kufanya
jambo lolote kwa ajili yao
hata kumwaga damu za
ndugu zao ili mradi
kuwafurahisha
mabeberu.Patrice
tunatakiwa kusimama na
kusema hapana kwa
unyonyaji huu.Wazee wetu
akina mzee
Nyerere,Lumumba na
wengineo walijioa
kupambana kuhakikisha
tunajikomboa kutoa katika
makucha ya wanyonyaji ni
jukumu letu na sisi
kusimama imara
kuhakikisha unyonyaji huu
hauendelei.Jumuiya ya
Afrika mashariki kweli ni
mwiba kwao kwani tumekata
mirija ya wanyonyaji na sasa
wanahangaika kutaka
kuivunja” akasema Dr
Fabian
“Ahsante kwa kunielewa
Dr Fabian sasa
tunazungumza lugha
moja.Tanzania imechukua
uongozi wa jumuiya hii sitaki
isambaratikie mikononi
mwako ndiyo maana
ninataka tufanye kila
linalowezekana kuhakikisha
kwamba lengo la mabeberu
hawa halitimii.Tupambane
tuiokoe Congo na tuiokoe
jumuiya ya Afrika mashariki
ambayo wenzetu wanafikiria
kuivunja.Binasi siko tayari
nchi yangu irejee kama
ilivyokuwa zamani Congo ya
vita na mauaji
yasiyokwisha.Imetugharimu
miaka mingi na gharama
kubwa kuipata amani hii
tuliyonayo sasa.Siko tayari
kuipoteza na kuwaacha
mabeberu wakiendelea
kufaidika na rasilimali
zetu,nitapambana hadi tone
la mwisho la damu kuifia
nchi yangu.Hata kama ni
kutawala kwa lazima
nitafanya hivyo kuilinda
amani ya Congo na kuzuia
mabeberu wasithubutu tena
kukanyaga katika ardhi yetu
ndiyo maana nimekuja
kwako rafiki yangu na ndugu
yangu kuomba msaada
wako.Tanzania mmekuwa
nasi wakati wote wa
machafuko na hamjawahi
kutuacha hata mara moja na
ninaamini hamtatuacha hata
sasa tunapohitaji kuilinda
amani yetu kwa gharama
zozote”akasema Patrice.Dr
Fabian akamtazama kwa
makini halafu akauliza
“Nini ushauri wako
katika hili Patrice? Akauliza
Dr Fabian.Ilipita dakika
moja Patrice akasema
“Ni kumuua Lucy
Muganza” akasema na
kunyamaza kwanza ili kile
alichokitamka kimuingie Dr
Fabian halafu akaendelea
“Hiyo ndiyo njia pekee
iliyobaki ya kuliepusha taifa
la Congo kurejea kule
lilikotoka,kuikoa jumuiya ya
Afrika mashariki na kuzima
kabisa ndoto za mabeberu za
kutaka kuendelea kunyonya
nchi zetu.Ni uamuzi mgumu
lakini ndiyo njia pekee ya
kulimaliza hili suala.Binafsi
nimeishi katika shida
kubwa,nimesoma kwa taabu
ninafahamu mateso
waliyokuwa wakiyapata
watu wa Congo ndiyo maana
yeyote anayecheza na amani
ya Congo ni adui yangu
mkubwa.Lucy Muganza ni
hatari sana kwa amani yetu
ndiyo maana ninashauri
tumuondoe” akasema Patrice
na ukimya ukatawala mle
ndani halafu Dr Fabian
akasema
“Patrice sina kipingamizi
chochote na hicho
unachokisema lakini nina
maswali machache.Huyu
mama kama ulivyosema ni
maarufu sana nchini Congo
na ana wafuasi wengi,kama
tukimuua hudhani wafuasi
wake wanaweza wakahisi ni
serikali ndiyo waliofanya
mpango huo wa mauaji na
vurugu kubwa
zikaanza?Jambo lingine hata
kama akiuawa Lucy hawa
wakubwa walioko nyuma
yake hawataweza kutafuta
mtu mwingine ambaye
atachukua nafasi ya Lucy na
kuendeleza mikakati
yao?Kama wakifanya hivyo
tutaendelea kuua kila
atakayeteuliwa?
“Mtu mwingine
wanaweza wakampata ili
kuendelea na mipango yao
lakini hatakuwa na
umaarufu mkubwa kama
Lucy.Huyu mama licha ya
kuungwa mkono na nchi za
Magharibi lakini hata yeye
binafsi nguvu yake ya
ushawishi ni
kubwa.Angeweza hata
kusimama peke yake bila ya
kuungwa mkono na nchi za
magharibi na akashinda
uchaguzi.Tukimuondoa huyu
mama itawapa hata wao
wakati mgumu wa kutafuta
mtu ambaye ana uwezo
kama Lucy na hii
itanihakikishia mimi
ushindi.Kuhusu vurugu
haitakuwa rahisi kutokea
kwani Lucy hatauawa akiwa
Congo.Atauawa akiwa hapa
Tanzania”
“Tanzania?! Dr Fabian
akashangaa
“Ndiyo.Akiuliwa hapa
Tanzania haitakuwa rahisi
mtu yeyote kuhisi kama
serikalio ya Congo inahusika
na mauaji hayo”akasema
Patrice na Dr Fabian
akavuta pumzi ndefu
“Ni vipi kama ukifanyika
uchunguzi na ikagundulika
kwamba sisi ndio
tuliotekeleza mauaji
hayo,huoni kwamba
Tanzania itachafuka
kimataifa jambo ambalo
sitaki litokee.Tunasifika
duniani kote kwa amani
sitaki sifa hii nzuri iharibike
kwa kufanya mauaji hayo
katika ardhi ya
Tanzania”akasema Dr
Fabian
“Dr Fabian nadhani
umewahi kusikia kuhusu
kufanya maamuzi magumu
na katika mambo kama haya
ndipo maamuzi magumu
hufanyika.Usiwe na hofu
nitatuma kikosi changu kuja
kumuua Lucy ili kuiepusha
nchi yao na lawama.Dr
Fabian ninakuomba tufanye
hivi kwa maslahi ya Congo
na jumuiya yetu ya Afrika
Mashariki.”akasema Patrice
“Tatizo si kumuua Lucy
bali ni kumuua katika ardhi
ya Tanzania.Unafahamu
namna nchi hii
inavyoheshimika
kimataifa,sitaki nchi yangu
ichafuke kama ambavyo
wewe hutaki nchi yako
ichafuke”akasema Dr Fabian
“Dr Fabian wewe ni
mgeni katika uongozi una
mwaka mmoja tu sasa na
humfahamu vyema Lucy
Muganza na inawezekana
hujawahi hata kumtia
machoni lakini ni mwanamke
mwenye nguvu kubwa na
ndiyo maana hata mimi
binafsi ninamuogopa
kwamba akiachwa anaweza
akachukua nchi na
ninavyomfahamu akichukua
nchi atairudisha ilivyokuwa
awali.Ataleta machafuko
katika nchi za maziwa
makuu.Nchi na nchi
hazitaelewana,ule umoja
wetu utatoweka na kila nchi
itasimama yenyewe.Hilondilo
wanalitaka hawa wakubwa
ili waweze kuingia na
kutuibia mali zetu.Ni sisi
wawilitu ambao tunaweza
kuzia hayoyasitokee na njia
pekee ya kuzuia yasitokee ni
kwa kumuua Lucy Muganza”
akasema Patrice.Dr Fabina
alikaa kimya kwa muda
halafu akauliza
“Umekwisha andaa
mpango wa kumuua Lucy?
“Kama nilivyosema
kwamba kuna timu ya
majasusi ambayo
inamfuatilia Lucy kwa siri
kubwa sana.Kwa sasa Lucy
yuko Ufaransa ambako
amekuwa na mfululizo wa
vikao na hao wakubwa
wakifanya mikakati ya
kuhakikisha Lucy anashinda
uchaguzi mkuu
ujao.Jumamosi ya wiki hii
atarejea nyumbani lakini
kabla ya kuelekea Kinshasa
atakuja kwanza
Tanzania.Hapa ana mtoto
wake anayesoma katika chuo
kikuu cha Dar es salaam
anaitwa Theresia
Muganza.Katika safari hiyo
Lucy pia atakuwa ameongoza
na mume wake Laurent na
lengo la kuja Tanzania ni
kumchukua binti yao
Theresia ili waelekee
Kinshasa kama familia
ambako mapokezi makubwa
yanamsubiri Lucy kutoka
kwa malefu ya wafuasi wa
chama cha CDP.Nataka
atakapotia mguu hapa
Tanzania asiondoke hai bali
jeneza lake ndilo lirejeshwe
Congo.Ninacho kikosi
nimekiandaa kwa ajili ya
kazi hiyo ambacho kama
ukiniruhusu nitakituma kuja
kumuondoa Lucy hapa
Tanzania” akasema Patrice
Dr Fabian akawaza kidogo
na kusema
“Patrice wewe ni rafiki
yangu mkubwa,tumekutana
masomoni nje ya nchi na
sasa wote tumeshika nafasi
za urais na siwezi
kukukatalia ombi lako kwa
ajili ya kulinda Afrika
Mashariki na kuilinda amani
ya Congo.Lucy atauawa hapa
Tanzania lakini na watu
wangu.Sitaki watu wa nje
waje kufanya mauaji katika
ardhi yetu.Ninao vijana
mahiri wanaoweza kuifanya
hiyo kazi.Nitakachohitaji
kutoka kwako ni
mawasiliano kati ya timu
yako inayomchunguza Lucy
na timu yangu
nitakayoiandaa kwa ajili ya
kumuondoa” akasema Dr
Fabian.Maongezi yaliendelea
kwa takribani nusu saa
kisha wakaagana Patrice
akaondoka kuelekea
Kinshasa.Kiongozi wa
mwisho kuondoka Arusha
alikuwa ni rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania
Dr Fabian Kelelo.Akiwa
ndani ya ndege alikuwa
kimya akilipitia faili lile
alilopewa na
Patrice.Akaichomeka diski
aliyopewa na Patrice katika
kompyuta na kuanza
kusikiliza mazungumzo
yaliyorekodiwa ya Lucy
Muganza na baadhi ya
viongozi wa nchi zilizo katika
jumuiya ya Afrika Mashariki
“Patrice yuko sahihi
mwanamke huyu ni hatari
sana kwa uhai wa jumuiya
yetu ya Afrika mashariki na
anapaswa kuondolewa
haraka sana kabla hajaleta
madhara.Kinachonishangaza
marais hawa ambao Lucy
amekuwa akiwasiliana nao
wakipanga mikakati ya
kuanzisha jumuiya yao ndogo
ni watu walio mstari wa
mbele sana katika kuhimiza
mshikamano madhubuti
miongoni mwa wanachama
wa jumuiya hii kumbe wana
siri kubwa wanatembea
nayo.Nitapambana
kuhakikisha jumuiya hii
haivunjikii mikononi
mwangu.Nitailinda jumuiya
hii kwa gharama zozote
katika wakati wangu kama
mwenyekiti japo wapo
viongozi ambao wako tayari
ivunjike lakini watasubiri
hadi pale nitakapokuwa
nimemaliza muda wangu wa
uongozi lakini nina hakika
kama tukimuondoa Lucy na
mipango yao yote ya
kuanzisha jumuiya yao ndogo
nayo itayeyuka” akawaza na
kulifunika lile faili
“Lakini bado kuna kitu
kinanipa ukakasi katika akili
yangu.Lucy Muganza ni
tegemeo la mataifa ya
magharibi katika
kufanikisha mipango yao ya
unyonyaji wa rasilimali zetu
ni vipi kama walio nyuma
yake wakiamua kufanya
uchunguzi wa kifo chake na
wakabaini kwamba
ninahusika?Nitakuwa
nimeingia katika mgogoro
mwingine mkubwa na nchi
za magharibi.Nifanye
nini?Nijitoe katika mpango
huu wa kumuua Lucy
Muganza?akajiuliza
“Hapana siwezi kujitoa
katika mpango huu.Tayari
nimekwisha muhakikishia
Patrice kwamba niko pamoja
naye katika suala hili.Hata
mimi siko tayari kuona
machafuko yakirejea tena
Congo kama ilivyokuwa
zamani.Watu wa Congo
wameitafuta amani kwa
miaka mingi na wametumia
gharama kubwa hadi
kuipata.Ni jukumu letu sisi
majirani zao kuhakikisha
amani waliyo nayo haipotei
tena.Kibaya zaidi ni mipango
yao ya kuisambaratisha
jumuiya ya Afrika
Mashariki.Nadhani kumuua
Lucy ndiyo njia pekee ya
kulitatua hili jambo hata
hivyo umakini mkubwa sana
unatakiwa.Ni suala ambalo
linapaswa kupangwa
kitaalamu mno” akawaza Dr
Fabian Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
ambaye katika historia ya
marais waliowahi kuingia
madarakani yeye ndiye
anayetajwa kuwa kijana
kuliko wote na mwenye sura
ya kuvutia.
DAR ES SALAAM
Ni saa saba na dakika
ishirini na moja za usiku
lakini bado Dr Fabian
hakuonekana kuwa na
usingizi.Alikuwa ameketi
sofani akiwa na lundo la
vitabu pembeni yake.Millen
mke wake alimfuata pale
sofani na kukaa karibu yake
akakifunika kitabu
alichokuwa anakisoma mume
wake na kumbusu
“What’s wrong
darling.Uliondoka hapa
kuelekea Arusha ukiwa na
furaha kubwa lakini
umerejea ukiwa katika hali
ya mawazo mengi na
haujazungumza nami kitu
chochote kuhusiana na safari
ya Arusha.Nini kimetokea
huko?akauliza Millen
mwanamke mwenye weupe
wa kung’aa na sura ya upole
yenye tabasamu muda
wote.Dr Fabian akamtazama
mke wake halafu
akatabasamu na kusema
“Usijali Millen.Kila kitu
kiko sawa”
“Hapana.Ninakufahamu
vyema Fabian hauko
sawa.Something is wrong
with you.Nini kimetokea
Arusha? Niambie tafadhali
kama kuna tatizo lolote
nijue”akasema Millen
“Fine” akasema Dr
Fabian na kuvuta pumzi
ndefu
“Arusha mambo
yamekwenda vizuri
hakukuwa na tatizo
lolote.Tumechukua uenyekiti
wa jumuiya ya Afrika
Mashariki kwa muda wa
mwaka mmoja.Kwa ujumla
kila kitu kilikwenda vizuri
kabisa”
“Kama kila kitu
kilikwenda vizuri nini hasa
kinakusumbua kichwa chako
mpenzi wangu?Si kawaida
yako kukaa hapa hadi muda
huu.Nini kinakusumbua?
“Ni kweli Millen nina
tatizo lakini naomba
nisikwambie kwa sasa ni
tatizo gani”
“Hapana nieleze
Fabian.Hakuna tatizo lako
ambalo haujawahi kunieleza”
akasema Millen.Dr Fabian
akamtazama mkewe halafu
akasema
“Toka nimeingia
madarakani nimekutana na
mtihani wangu wa kwanza
mkubwa ambao lazima
niushinde”
“Mtihani upi? Akauliza
Millen na Dr Fabian akavuta
pumzi ndefu
“I need to silence
someone very dangerous”
akasema na kukaa kimya
baada ya kuuona mstuko
katika uso wa mke wake
“You mean killing
somebody?akauliza Millen na
Dr Fabian akatikisa kichwa
kukubali
“Kuna mataifa makubwa
ambayo hayapendi kuona
jumuiya ya Afrika mashariki
inastawi na wanajaribu
kutumia kila njia
kuisambaratisha.Kuna mtu
ambaye wanamtumia katika
kulifanikisha hilo.Njia pekee
ya kumaliza mipango na
njama zao ovu ni kwa
kumuondoa huyo ambaye
wanataka kumtumia lakini
jambo hilo linatakiwa
lifanywe kitaalamu sana
ndiyo maana ninasoma
vitabu hapa kuhusu vifo
mbali mbali vya watu
maarufu vilivyowahi kutokea
duniani na ambavyo mpaka
leo hii havijawahi kupatiwa
ufumbuzi.I want this one to
be unsolved murder”
“Fabian hakuna namna
nyingine ya kuweza
kulishughulikia suala hilo
zaidi ya kuua?I’m scared”
akasema Millen
“Millen nimekushirikisha
jambo hili la siri kubwa
ambalo sikupaswa
kukueleza.Natamani
ningekuwa na njia nyingine
ya kuweza kuliondoa tatizo
hilo zaidi ya hii ninayotaka
kuifanya lakini hakunanjia
nyingine.It’s hard even for
me but I have to do it.Mtu
huyo ni hatari na si kwa
jumuiya ya Afrika mashariki
pekee bali ni hatari pia kwa
amani ya Congo.Umewahi
kufanya kazi katika shirika
la umoja wa mataifa la
kuhudumia wakimbizi
unafahamu mateso na taabu
wanazopitia wakimbizi,mtu
huyo anataka kutumiwa
kuirejesha Congo katika
machafuko ili mabeberu
waweze kurejea tena na
kuendelea kuchota rasilimali
za nchi hiyo.I won’t let that
happen ! akasema Dr Fabian
“Hofu yangu Dr Fabian
ni vipi kama ukifanyika
uchunguzi na ikabainika
kwamba unahusika na
mauaji hayo?akauliza Millen
“That won’t happen.Ni
jambo ambalo litafanywa
kitaalamu mno ndiyo maana
nikakwambia kwamba
nataka jambo hili lisiweze
kupatiwa ufumbuzi hata
kama wataamua
kulichunguza” akasema Dr
Fabian.Mke wake
hakuzungumza tena kitu
kingine akamshika mkono
mumewe na kumuongoza
kwenda chumbani
kupumzika kwani muda
ulikuwa umekwenda sana.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 2
Saa tatu na nusu za
asubuhi gari tatu ziliwasili
ikulu jijiji Dar es
salaam.Kutoka katika
mojawapo ya gari akashuka
Rais mstaafu wa jamhuri ya
muungao wa Tanzania Dr
Evans ambaye alipokewa na
Rais Dr Fabian akamuongoza
ndani.Moja kwa moja
wakaelekea sehemu ya
mazungumzo ya faragha.
“Mambo yanakwenda
vipi hapa mheshimiwa
Rais?akauliza Dr Evans
“Mambo yanakwenda
vyema mzee,tunaendelea
vizuri” akajibu Dr Fabian
“Hongera sana
mheshimiwa Rais.Ni kweli
mambo yanakwenda vizuri
hata sisi tulio huko nje
tunaona.Kila kitu ni
kizuri.Ongeza juhudi zaidi”
“Nashukuru sana mzee”
“Hongera pia kwa
kuchukua uenyekiti wa
jumuiya ya Afrika Mashariki
kwa mara ya kwanza”
“Ahsante mzee
ninashukuru sana.Vipi
maisha ya ustaafu?
“Maisha yanakwenda
vizuri.Ninapumzika vya
kutosha sasa na hata mwili
wangu umeanza kunawiri”
akasema Dr Evans na wote
wakacheka
“Mzee nimekuita hapa
kwa mazungumzo ya faragha
ningeweza kukufuata kwako
mimi mwenyewe lakini kama
unavyojua taratibu za hapa
ni ngumu kidogo”
“Hakijaharibika kitu
mheshimiwa Rais
ninafahamu kila kitu hivyo
usihofu”
“Ahsante
mzee.Nimekuita hapa
ninahitaji sana msaada wako
wa mawazo”
“Ndiyo nakusikiliza”
“Jana tumeipokea rasmi
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo katika jumuiya ya
Afrika mashariki na kufanya
jumla ya nchi wanachama
kuwa saba katika jumuiya
hiyo”
“Hilo ni jambo jema
sana.Jumuiya inazidi
kupanuka na kuimarika
zaidi.Kwa miaka michache
ijayo jumuiya hii itakuwa ni
moja kati ya jumuiya kubwa
kabisa zenye nguvu barani
Afrika”akasema Dr Evans
“Ni kweli mzee hayo
unayoyasema.Jumuiya ya
Afrika Mashariki imestawi
sana na kuzifanya nchi
nyingi kutaka kujiunga
lakini nyingine kama
Somalia zimekataliwa kwa
sasa hadi
baadae”akanyamaza kidogo
na kuendelea
“Baada ya mkutano
kumalizika nilikuwa na
mazungumzo marefu ya
faragha na Rais Patrice
Eyenga wa jamhuri ya
kidemokrasia ya
Congo.Patrice alinieleza
kuhusiana na mchakato wa
uchaguzi mkuu wa rais na
wabunge unavyoendelea
nchini Congo lakini hapo
hapo likaibuka tatizo.Chama
cha upinzani cha CDP
kimemteua mwanamama
Lucy Muganza kupeperusha
bendera yake katika
uchaguzi mkuu ujao”
“Nilisikia taarifa
hizo.Lucy Muganza
nimewahi kumsikia.Ni
mwanamama bilionea nchini
Congo”Akasema Dr Evans
“Ndiye huyo.Ni
mwanamama mwenye nguvu
sana nchini Congo na ni
mpinzani mkubwa wa Rais
Patrice.Pamoja na nguvu
yake kubwa ya ushawishi
aliyonayo mwanamama huyo
lakini kuna jambo kubwa
nyuma yake.Anatumiwa na
mataifa ya magharibi
ambayo hayajafurahishwa na
utawala wa Rais Patrice
ambaye amekata mirija ya
unyonyaji na anataka Congo
inufaike na rasilimali ilizo
nazo.Kwa miaka mingi nchi
ya Congo imekuwa katika
machafuko lakini baada ya
kuingia madarakani Rais
Patrice amefanya kazi kubwa
na hatimaye amani
imepatikana Congo.Mambo
aliyoyafanya Patrice
hayajawafurahisha mataifa
yaliyokuwa yakinufaika na
rasilimali za Congo hivyo
basi wanataka kuweka mtu
wao katika madaraka
ambaye atairejesha tena
Congo katika machafuko ili
wao warejee tena kuendelea
kuchota rasilimali.Mtu huyo
ambaye wanataka kumtumia
ni Lucy Muganza.Kama
haitoshi wana mpango pia
wa kuivuruga jumuiya ya
Afrika Mashariki.Kutokana
na uimara wake jumuiya hii
imekuwa ni mwiba kwa
mabeberu waliozoea kuchota
rasilimali zetu na kufaidisha
nchi zao.Kitendo cha jamhuri
ya kidemokrasia kukubaliwa
kujiunga na jumuiya ya
Afrika mashariki
kinawanyima usingizi kwani
wanaamini itakuwa vigumu
tena kwao kuendeleza
unyonyaji wao kutokana na
uimara wake hivyo kwa
gharama zozote wanataka
kuhakikisha jumuiya hii
inasambaratika.Lucy
Muganza amekwisha anza
mipango hiyo na tayari
amefanya mawasiliano na
baadhi ya wakuu wa nchi
zilizo katika jumuiya ya
Afrika Mashariki na tayari
viongozi wa nchi mbili
wamekwisha kubaliana
kwamba mara tu uchaguzi
utakapofanyika na yeye
akawa mshindi basin chi hizo
zitajiondoa kutoka katika
jumuiya ya Afrika Mashariki
na kuunda jumuiya yao
ndogo ya nchi tatu”
akanyamaza kidogo kwa
muda halafu akaendelea
“Baada ya majadiliano na
Rais Patrice tumeona
hakuna njia nyingine ya
kupambana na mabeberu
hawa na kuififisha mipango
yao miovu zaidi ya
kumuondoa Lucy Muganza”
akanyamaza
“Unaonekana unaogopa
Dr Fabian” akasema Dr
Evans huku akitabasamu
“Mzee napenda nikiri ni
kweli ninaogopa.Ni mara
yangu ya kwanza toka
nimekalia kiti hiki kukutana
na mtihani mgumu kama
huu ambao unanilazimu
nitoe uhai wa mtu”
“Karibu Dr Fabian katika
ulimwengu wa mitihani ya
urais.Mambo ndiyo kwanza
yameanza.Mitihani kama hii
itakuja mingi na unatakiwa
kuishinda.Unachotakiwa ni
kufanya maamuzi ya
haraka,sahihi na kwa wakati
muafaka.Usiwe mwoga
katika kufanya maamuzi
wewe ni rais na watu zaidi ya
milioni hamsini
wanakutegemea wewe kwa
usalama wa maisha yao,afya
zao na mustakabali mzima
wa maisha yao hivyo kama
kuna kitisho chochote kwa
nchi kiondoe haraka mno
kabla hakijaleta madhara
makubwa bila kujali
gharama.Nadhani
umenielewa” akasema Dr
Fabian
“Nimekuelewa mzee
ndiyo maana mimi na Rais
Patrice tumeamua kwa
pamoja kumuondoa Lucy
Muganza.Ambacho kinanipa
wasi wasi ni how to do
it?Kwa usiku mzima
nimekuwa nikitafakari sana
namna ya kulifanya tukio
hilo kuwa unsolved nimekosa
jibu ndiyo maana nimekuita
hapa unisaidie mawazo mzee
wangu.Wewe umekuwepo
madarakani kwa miaka kumi
umepitia mengi na
ninaamini unazo mbinu
nyingi za kuweza
kulishughulikia suala hili”
akasema Dr Fabian na Dr
Evans akamtazama na
kuinuka akaanza kuzunguka
mle ndani
“How to do it” akasema
kwa sauti ndogo
“Fabian my president you
don’t know how to do
it?Please don’t let me
down.Nilikupendekeza,nikak
upigania kwenye chama na
hata katika kampeni because
I saw something special in
you.Nilimuona Rais ambaye
ataipeleka Tanzania mbali
zaidi ya hapa tulipoifikisha
mimi na wengine wote
waliopita.Rais mwenye
nguvu ambaye ataogopwa
ndani na nje.Imekuaje leo
unaniita na kutaka
nikufudishe namna ya
kutatua tatizo dogo kama
hili?akauliza Dr Evans kwa
ukali
“Mzee ninahitaji ushauri
na namna bora ya kuweza
kulitatua suala hili.Wewe
unao uzoefu mkubwa sana
zaidi yangu mimi”
“C’mon Dr Fabian you
are a president ! You have
everything in your
power.Kwa nini unakuja
kwangu?Tafadhali Fabian
usiniangushe mimi ambaye
nilipambana kuhakikisha
unaingia madarakani.Make
me proud.Tumia nguvu uliyo
nayo dhidi ya mtu yeyote wa
ndani au wa nje ya nchi
ambaye anatishia amani
yetu.Usisite kuchukua hatua
haraka kila pale
linapojitokeza suala lolote la
hatari.Usitegemee watu
wengine wafikiri badala yako
watakupoteza.Nimekuwa
nakuelekeza mambo haya
kila wakati” akasema Dr
Evans na kumtazama Dr
Fabian ambaye alikuwa
ameinamisha
kichwa.Maneno yale ya Dr
Evans yalimuingia
“What do you
need?akauliza Dr Evans
“Kwa kuwa Lucy
Muganza ni tegemeo kubwa
kwa nchi za Magharibi nina
uhakika mkubwa baada ya
kumuua watakuja kufanya
uchuguzi.I want it to be
unsolved” akasema Dr
Fabian
“Unataka tukio lifanyike
hapa Tanzania?
“Ndiyo mzee.Likifanyika
Congo watajua ni mpango
umesukwa wa kumuua ndiyo
maana tunataka tukio hilo
lifanyike hapa Tanzania”
“Una ila kitu Dr Fabian
cha kukusaidia.Idara ya siri
ya usalama wa ndani wa nchi
ipo chini yako kwa nini
unashindwa kuitumia wakati
ina watu wenye ujuzi
mkubwa wa kuweza
kulifanya jambo
hilo?akauliza Dr Evans
“Mzee ni kweli
unalolisema lakini suala hili
ni la siri kubwa ndiyo maana
sitaki lijulikane.Zaidi ya yote
bado sina mtandao wa watu
ninao waamini
kuwashirikisha katika
mambo makubwa na ya siri
kama haya”
“That’s the problem Dr
Fabian.Huwezi kuwa peke
yako bila kuwa na watu
unaowaamini.Huwezi
kufanya kila jambo siri
lazima uwe na watu ambao
unawaamini na
unawashirikisha mambo
makubwa kama haya japo
unapaswa uwe makini sana
si kila mtu anapaswa
kuaminiwa”akasema
DrEvans
“Mheshimiwa Rais
ulisalitiwa na waziri mkuu
wako mtu ambaye
ulimuamini sana na kitendo
hicho kinanipa woga hata
mimi kuwaamini watu walio
karibu yangu na
kuwashirikisha mambo
makubwa kama haya”
“Unalolisema ni la kweli
Dr Fabian.Katika mambo
haya ya uongozi umakini
mkubwa unatakiwa kujua
nani unamshirikisha nini na
kwa nini.Si kila mtu
anapenda wewe uwepo
mahali hapa.Wapo watu
ambao wanawaza
kukushusha kutoka mahali
hapa ulipofika lakini
hawataweza.Hata hivyo
unatakiwa uwe na watu
wachache ambao
unawaamini na
watakusaidia sana katika
mambo yako.Kuna mtu
mmoja ambaye wakati
wangu nilimuamini sana na
alikuwa na msaada
mkubwa.Ni mkuu wa kikosi
cha jeshi cha operesheni
maalum anaitwa Austin
January.Ni mtu
makini,mtiifu na mtunza
siri.You can trust him”
akasema Dr Evans
“Austin January”
akasema Dr Fabian
“Ni kijana kama wewe
japo umemzidi kidogo lakini
mnaweza mkaelewana
sana.Binafsi ni mtu ambaye
nilimtumia sana katika
mambo yangu mbali mbali
na amenisaidia mno japo
kuna wakati tulitofautiana
lakini niliyekuwa mkorofi ni
mimi.Nakushauri mtumie
sana huyu mtu”akasema Dr
Evans
“Ahsante sana mzee kwa
ushauri wako huu.Vipi
kuhusu idara ya siri ya
mambo ya ndani?Ninaweza
kuwaamini kuwashirikisha
katika mambo makubwa ya
siri?
“Ni idara yenye msaada
mkubwa kwa Rais lakini
nakushauri kwa mambo
makubwa kama haya
usiwashirikishe.Watumie
kwa mambo mengine ya
kawaida ya usalama wa
ndani ya nchi”
“Mzee ninakushukuru
sana kwa ujio wako huu
ambao umenipa nguvu
mpya”akasema Dr Fabian
“Ninashukuru kwa
kuniita.Kwa kuongezea
kabla sijaondoka,tukio hilo
lifanye lionekane ni tukio la
ujambazi.Austin anafahamu
mambo yote haya na
atakuelekeza nini cha
kufanya” akasema Dr Evans
“Mzee nakushukuru kwa
mara nyingine tena kwa ujio
wako huu ambao umekuwa
na msaada mkubwa
kwangu.Usinichoke pale
nitakapokuita tena
kukuomba msaada.Mimi
bado ni kijana wako
ninaendelea kujifunza
mambo na bado
ninakutegemea”akasema Dr
Fabian
“Mr president please
don’t call me again to come
here labda iwe ni kwa
sherehe.Sifanyi hivi kwa nia
mbaya bali kukupa wewe
uwanja mpana wa kufanya
mambo yako.Huu ni wakati
wako,sisi tumekwisha maliza
muda wetu na tunakupa na
wewe nafasi ya kuongoza
nchi kwa
uhuru.Usitutegemee sana
sisi” akasema Dr Evans
wakaagana akaondoka ikulu.
“Dr Evans ameongea
maneno mazito lakini yenye
maana kubwa.Mimi ni Rais
nina kila kitu ninapaswa
kusimama kama Rais na si
kuonyesha woga wa aina
yoyote.Natakiwa kuilinda
nchi yangu kwa gharama
zozote zile hicho ndicho kiapo
nilichokula” akawaza
DrFabian na kuinua mkono
wa simu akampigia katibu
muhtasi wake na kumtaka
atume ujumbe kwa Austin
January mkuu wa kumtaka
afike ikulu jioni ya siku ile
kwa ajili ya kupata chakula
cha usiku na Rais
*****************
Saa moja na nusu za jioni
Austin January akiwa na
dereva wake aliwasili ikulu
akapokewa na mwenyeji
wake ambaye ni Rais Dr
Fabian.Usiku huu Austin
alivaa suti nzuri ya rangi
nyeusi iliyomkaa
vyema.Ilikuwa ni mara ya
kwanza kufika ikulu tangu
Rais Dr Fabian alipochukua
madaraka.
“Austin January karibu
sana ikulu.Nimefurahi leo
kuonana nawe ana kwa
ana”akasema Dr Fabina
akimkaribisha Austin
“Nshukuru sana
mheshimiwa Rais hata mimi
nimefurahi kukutana
nawe.Ahsante sana kwa
kunikaribisha”akasema
Austin
“Utanisamahe hata hivyo
kwa kuchelewa kukutana na
mtu kama wewe.Mambo ni
mengi ndiyo maana kuna
vitu vingine kama kukutana
na watu muhimu kama ninyi
ninasahau lakini
hakijaharibika kitu.Leo
tumekutana na utakuwa ni
mwanzo wetu mzuri wa
kujenga mahusiano mazuri
na kuendelea kukutana mara
kwa mara”akasema Dr
Fabian
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais.Ni
heshima kubwa kwangu
kukutana nawe kwa mara ya
kwanza toka umeingia
madarakani” akasema
Austin.
Chakula maalum
kiliandaliwa na Austin
akakaribishwa.Alihisi furaha
kubwa kukaribishwa ikulu
na kupewa heshima ya
namna ile.Baada ya chakula
Dr Fabian akamtaka Austin
waelekee katika chumba cha
mapumziko.
“Austin kwa mara
nyingine tena
ninakushukuru kwa kuitika
wito na kuja kunitembelea”
Dr Fabian akaanzisha
maongezi
“Hata mimi
ninakushukuru mheshimiwa
Rais kwa kunialika”
“Austin pamoja na
kutaka kufahamiana na
kujenga mahusiano mazuri
na watu kama wewe,kuna
jambo ambalo ninahitaji
msaada wako.Kama
unavyojua mimi nina mwaka
mmoja tu tangu nichukue
nafasi hii ya urais bado kuna
mambo mengi naendelea
kujifunza ikiwamo kutafuta
watu wa karibu ambao
nitawaamini na
kuwashirikisha kati9ka
mamo mazito ya nchi.Wewe
ni mmoja wa watu ambao
ninategemea kufanya naye
kazi kwa ukaribu sana.”
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais kwa
kuniamini”akasema Austin
“Nimejifunza mengi
kutoka kwa watangulizi
wangu hasa Dr Evans na
kubwa zaidi ni kuwa na
watu wachache
ninaowaamini ambao
nitawaeleza zile siri ambazo
watakwenda nazo
kaburini.Ni Dr Evans ndiye
aliyenifumbua macho kuhusu
wewe.Amekumwagia sifa
lukuki namna ulivyomsaidia
wakati alipokuwa
madarakani.Huko aliko
hatasahau uaminifu wako
mkubwa kwake ndiyo maana
akanishauri uwe mmoja wa
watu nitakaowaamini na
mimi ninamuamini sana
Yule mzee neno lake ni kama
amri kwangu hivyo
nimekuita hapa
kukufahamisha kwamba
kuanzia sasa wewe ni mmoja
wa watu wangu wachache
ambao nitakuwa nao karibu
sana”
“Ahsante mheshimiwa
Rais kwa heshima hii kubwa
uliyonipa.Nakuahidi
uaminifu mkubwa na
utendaji uliotukuka”
akasema Austin
“Austin kuna jambo
ambalo nataka kujadiliana
nawe ili tushauriane njia
bora zaidi ya kulimaliza.Ni
jambo ambalo tunatakiwa
kulimaliza kwa haraka lakini
kimya kimya na kwa usiri
mkubwa” akasema Dr Evans
na kunyamaza kidogo halafu
akasema
“Wewe si mwanasiasa
hivyo sintajikita sana katika
masuala ya kisiasa lakini
kwa ufupi ni kwamba
nimepata taarifa kuna watu
wanapanga mipango ya
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika mashariki.Zipo nchi
kubwa na tajiri ambazo
zilizoea kunufaika na
rasilimali zilizoko katika
nchi wanachama wa jumuiya
hii lakini kutokana na
uimara wa jumuiya na nchi
zote wanachama kuweka
msimamo mmoja katika
kusimamia rasilimali zake
imekuwa vigumu sana kwa
nchi hizo kubwa kuendelea
na unyonyaji wao wa
rasilimali zetu.Jana katika
mkutano wa jumuiya ya
Afrika Mashariki tumeipokea
jamhuri ya kidemokrasi ya
Congo kama mwanachama
mpya na kufanya jumla ya
nchi wanachama kuwa
saba.Kama unavyofahamu
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo wamekuwa katika
machafuko ya muda mrefu
jambo lililopelekea rasilimali
zake nyingi ziibwe kwa muda
mrefu.Baada ya kuingia
madarakani Rais Patrice
Eyenga amejitahidi
kuirejesha amani ya Congo
na sasa nchi imetulia na
Congo imeanza kupiga hatua
kimaendeleo.Patrice na
serikali yake wamekata
mirija yote ya wanyonyaji na
kutaka rasilimali za Congo
ziwanufaishe watu wa
Congo.Kitendo cha serikali
ya Congo kufanya mageuzi
makubwa ya kiuchumi na
kuziba mianya yote ya wizi
wa rasilimali zake na
kujiunga na jumuiya ya
Afrika
Mashariki,havijawafurahish
a nchi za Magharibi hasa zile
ambazo kwa miaka mingi
zimekuwa zikinufaika
kupitia mwanya wa migogoro
isiyokwisha.Kwa sasa nchi
ya Congo na jumuiya nzima
ya Afrika Mashariki tupo
katika vita kubwa ya
kiuchumi na nchi kubwa”
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Ili kukwamisha juhudi
zote zilizofanywa na serikali
ya Congo katika kuikwamua
nchi hiyo kiuchumi,nchi hizo
kubwa wameamua kuutumia
uchaguzi mkuu wa Rais
utakaofanyika hapo baadae
kumuweka madarakani mtu
wao wanayemtaka ambaye
wana uhakika atakuwa na
msaada mkubwa kwao
katika kuendelea kuchota
madini na mali nyingine za
Congo.Jambo lingine
wanalopanga kulifanya
wakubwa hao ni
kuisambaratoisha jumuiya
ya Afrika Mashariki ambayo
imekuwa ni kikwazo
kikubwa kwao katika
uchotaji wa rasilimali kwa
nchi za Afrika
Mashariki.Mtu ambaye
anatumiwa na mabeberu hao
ambaye wanataka
kumuingiza katika ikulu ya
Congo ni mwanamama Lucy
Muganza.Huyu ni
mwanamama bilionea ana
biashara kubwa kubwa
nchini Congo na anatajwa
kuwa ni mtu mwenye nguvu
sana kisiasa na ambaye
wengi wanatarajia anaweza
akamshinda Rais wa sasa
Patrice Eyenga.Kama huyu
mama akifanikiwa kushinda
uchaguzi basi Congo itarejea
kule illikotoka na vile vile
jumuiya yetu ya Afrika
Mashariki
itasambaratika.Tumenasa
mawasilianyo ambayo Lucy
amekuwa akiyafanya na
maraisi wa nchi mbili
wanachama wa Afrika
Mashariki na kuwashawishi
wakubali kujiunga pamoja
kama nchi tatu na
kutengeneza jumuiya yao
ndogo.Mwanamama huyu ni
hatari sana” akanyamaza Dr
Fabian akasimama
“Mazungumzo haya ni
mazito Austin I think we
need a drink” akasema na
kuindea simu iliyokuwemo
mle chumbani akapiga na
kuomba waletewe
mvinyo.Baada ya muda
mfupi akafika mtumishi
akiwa na sinia lenye chupa
ya mvinyo na glasi mbili
akawamiminia wakaendelea
na maongezi yao.
“Jumamosi wiki hii Lucy
Muganza atafika hapa nchini
kwa ndege yake binafsi
akitokea Ufaransa akiwa na
mumewe.Hapa Tanzania
yupo mwanae anasoma
katika chuo kikuu cha Dar es
salaam na lengo la kutua
hapa ni kumpitia mwanae ili
kwa pamoja kama familia
waelekee Congo kwani siku
hiyo ndipo
atakapotambulishwa rasmi
kama mgombea urais kupitia
chama cha CDP na
kumeandaliwa mapokezi
makubwa sana.Atakapoingia
hapa Tanzania sitaki atoke
hai.Nataka jeneza lake ndilo
lirudi Congo.I want her dead”
akasema Dr Fabian na
kuchukua glasi lake
akanywa funda la kinywaji
“Are you with me
Austin?akauliza
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais
unachokimaanisha”
“Good.Nina uhakika
mkubwa kifo chake
kitawastua sana wale ambao
wanamtumia na watataka
kufanya uchunguzi wa kna
kubaini sababu za kifo chake
hivyo nataka tukio hilo
lionekane kama ni tukio la
uporaji.Ionekane kama vile
ameuawa na majambazi
ambao walitaka kumpora
fedha. Nadhani umenielewa
Austin”
“Nimekuelewa
mheshimiwa rais na
ninakuhakikishia kwamba
suala hilo
litakwisha.Umeniambia
kwamba anapokuja hapa
Tanzania atakuwa
ameongoza na mumewe na
anakuja
kumchukuamwanae,vipi
kuhusu hao wawili mumewe
na mwanae?Wao
wanaachwa?
“Hapana.Kill them all !
akasema Dr Fabian
“Sawa mheshimiwa
Rais.Nitakachohitaji ni
kupata taarifa zote za
kuhusiana na huyo
mwanamama ili mimi na
watu wangu tuweze
kujipanga vizuri” akasema
Austin
“Kesho nitakuunganisha
na timu ya majasusi ambao
wanaendelea kumfuatilia
huyo mwanamama kwa siri
na watakupa taarifa zake
zote.Austin nakukumbusha
kwamba suala hili ni
muhimu mno na linatakiwa
kuandaliwa kitaalamu
sana.Lingine nataka
nikukumbushe kuhusu
usiri.Tunapanga kumuondoa
mtu ambaye anaungwa
mkono na mataifa makubwa
yenye nguvu hivyo basi usiri
mkubwa
unatakiwa”akasisitiza
“Nafahamu
ninachotakiwa kukifanya
mheshimiwa Rais na
ninakuahidi kulishughulikia
suala hiki kwa umakini
mkubwa na usihofu kuhusu
siri.Mimi na wenzangu
ambao tutafanya hii kazi siri
hii tutakwenda nayo
kaburini”akasema Austin
“Utii wako ndiyo sababu
ambayo imemfanya Dr Evans
aendelee kukukumbuka kila
wakati.Austin nakuahidi
kama tukiendelea na
mashirikiano mazuri namna
hii utakuwa na nafasi nzuri
sana katika uongozi wangu”
akasema Dr Fabian na
maongezi yakaendelea.Saa
tatu kamili Austin
akaondoka katika makazi
yale ya Rais
“Nimefurahi kukutana
na Rais Fabian.Sikuwa na
mategemeo ya kuonana naye
au kuwa karibu naye kama
nilivyokuwa na Dr Evans
lakini namshukuru mzee
Yule amenisemea vizuri kwa
Rais mpya na sasa
nimekuwa na ukaribu pia na
Rais Fabian.Ni Rais kijana
bado na anayeweza
kushaurika.Pamoja na
furaha niliyo nayo ya
kukutana naye lakini
amenitwisha jukumu zito la
kumuondoa Lucy
Muganza.Hili ni jukumu
kubwa kumuua kipenzi cha
wengi.Ni jukumu langu la
kwanza kupewa na Rais
huyu hivyo lazima
nihakikishe ninalifanikisha
kama alivyotaka ili kujenga
uaminifu kwake” akawaza
Austin
“Hata hivyo kazi hii
haitakuwa kazi ya kikosi
change bali nitaifanya na
watu wangu ninaowaamini
walio nje ya kikosi.Mtu wa
kwanza ambaye
ninamuhitaji ni Papaa Gosu
Gosu.” akawaza Austin na
kuchukua simu yake
akazitafuta namba za Gosu
Gosu akampigia na simu
ikapokelewa
“Kamanda Austin”
akasema Gosu Gosu
“Papaa uko wapi?
“Niko hapa Rombo hotel
nimekuja kupumzisha akili
kuna burudani nzuri ya
muziki”akajibu Gosu Gosu
“Nahitaji kukuona Papaa
ninakuja hapo sasa hivi.Wait
for me” akasema Austin na
kukata simu
“Gosu Gosu ni mpiganaji
mzuri na ndiyo maana
aliaminiwa mno na Mathew
Mulumbi” Austin akahisi
mwili unamsisimka
alipomkumbuka Mathew
Mulumbi
“It’s been three years
hakuna taarifa zozote
kuhusu Mathew
Mulumbi.Bado kuna
mkanganyiko mkubwa sana
kuhusu suala hili kama
Mathew yuko hai au
amekufa.Picha ya
kilichotokea usiku ule
tulipokwenda kuwakomboa
Olivia na Coletha bado
haijatoka kichwani
mwangu.Nimejaribu kuwaza
na kuwazua ilitokeaje
Mathew akapotea mpaka
sasa sijapata majibu.Kwa
wengine tayari wamekata
tamaa lakini mimi bado
sijakata tamaa.Kuna kitu
kinanifanya niamini kwamba
kuna uwezekano mkubwa
Mathew yuko hai.Japo
iliundwa timu ambayo
ilifanya uchunguzi kuhusu
Mathew na ikaja na majibu
kwamba alifariki na
wanahisi aliliwa na fisi lakini
kwangu mimi ninakataa
kabisa.Naamini Mathew
yuko hai.Yuko wapi
anafanya nini na kwa nini
hataki kujitokeza kama yuko
hai ni maswali ambayo
yanaendelea kunitesa mno
na nitaendelea kuteseka
katika maisha yangu yote
kwa kuwa kwa mara ya
kwanza niliondoka na
kumuacha mtu muhimu sana
kwa nchi nyuma.Kwa hili
sintajisamehe”
Sura ya Austin
ilibadilika na kujaa mawazo
baada ya kumkumbuka
Mathew Mulumbi
Walifika Rombo hotel
akamuacha dereva wake
akimsubiri garini akaingia
ndani kumtafuta Gosu Gosu
na kumkuta amekaa katika
meza peke yake akifuatilia
muziki wa bendi iliyokuwa
inatumbuiza katika hoteli
ile.Mara tu Gosu Gosu
alipomuona Austin namna
alivyopendeza akainuka na
kumpa mkono huku
akitabasamu
“Austin kulikoni leo
umependeza kiasi hicho?
Akauliza Gosu Gosu na
Austin akavuta kiti akaketi.
“Habari za siku
Papaa?akauliza Austin
“Inakaribia miezi mitano
hatujaonana”
“Ni kubanwa na
majukumu Papaa.Si unajua
hizi kazi zetu.Vipi
unaendeleaje na
maisha?akauliza Austin
“Ninaendelea vyema.Kila
kitu kinakwenda vizuri”
akasema Gosu Gosu
muhudumu akafika na
kuagizwa kinywaji
“Umetoka kutoa posa
leo?akauliza Gosu Gosu
“Papaa nimetoka ikulu
niliitwa na Rais”
“Uliitwa na Rais?
“Ndiyo alikuwa na
mazungumzo na mimi”
“Una bahati sana
Austin.Kuitwa na Rais ikulu
si jambo dogo” akasema Gosu
Gosu
“Kikubwa ilikuwa ni
kufahamiana.Alipata taarifa
zangu kutoka kwa Dr Evans
na akataka kuniona hivyo
akaniomba tuonane jioni ya
leo kwa chakula cha usiku
ndiyo maana umenioa
nimevaa namna hii.”
akasema Austin
“How’s the new
president? Akauliza Gosu
Gosu huku akiinua glasi
yake na kunywa funda moja
“Ni kijana bado, si
mwongeaji sana anaongea
kwa vituo na yuko makini
sana katika kuchagua kipi
cha kuongea wapi na muda
gani.Kwa ujumla naweza
kusema ni mtu mwelewa
sana na anapokea ushauri
kuliko Yule mzee wetu Dr
Evans” akasema Austin na
Gosu Gosu akacheka
“Umenikumbusha mbali
sana mzee Yule namna
alivyokuwa akibadilika
badilika.Hakuwa na
msimamo” akasema Gosu
Gosu na wote wakacheka
“Papaa pamoja na
kufahamiana lakini Rais
aliniita na kunipa kazi”
“Kazi?! Gosu Gosu
akashangaa
“Ndiyo.” Akasema Austin
na kumueleza Papii kila kitu
kuhusiana na kazi ile
aliyopewa na Rais
“Dah ! si kazi nyepesi hii
Austin”akasema Gosu Gosu
“Ndiyo maana nimekuja
kwako Papaa.Nataka
tushirikiane katika hii kazi”
“Me?akauliza Gosu Gosu
“Ndiyo
Papaa.Nimekutafuta kwa
ajili ya kazi hii”
“Hapana umekosea
Austin kutaka kunijumuisha
katika kazi hii.Mimi tayari
nimekwisha achana na hayo
mambo toka tulipompoteza
Mathew”
“Papaa kupotea kwa
Mathew ni jambo ambalo
linatuumiza sote.He was our
friends lakini pamoja na
kupotea kwake bado mambo
mengine yanapaswa
kuendelea.Huyu
mwanamama Lucy Muganza
ni hatari sana kwa usalama
wa nchi yetu,jumuiya ya
Afrika Mashariki na zaidi
sana nchi yako ya kuzaliwa
Congo.Siwezi kuifanya kazi
hii peke yangu ndiyo maana
nimekuja kwako Papaa
kuomba msaada”
“Austin wewe ni kongozi
wa kikosi una watu wengi
kwa nini usitumie watu wako
kuifanya kazi hiyo hadi
unifuate mimi.Mimi siko
tena katika hayo
mambo.Kwa sasa ni
mfanyabiashara.Ninayo
miradi kadhaa mikubwa
hapa nchini ninaisimamia
hivyo sitaki kujiingiza katika
masuala mengine.Siwezi
kufanya kazi yoyote ya
serikali tena.What they did
to Mathew was unfair”
akasema Gosu Gosu
“I know that and I agree
with you.It was unfair lakini
yalikuwa ni maamuzi ya
kijasiri ya Rais”akasema
Austin na sura ya Gosu Gosu
ikabadilika
“Maamuzi ya
kijasiri?Unayaita maamuzi
yale ya kijasiri?Ule si
ujasiri.Ni uoga na ujinga!
Akafoka Gosu Gosu
“Papaa natamani
ungekuwepo ili ushuhudie
kilichotokea.Hayakuwa
maamuzi mepesi kwa Rais
kuamuru tuondoke na
tumuache Mathew.Lengo la
operesheni ile lilikuwa ni
kuwakomboa mateka
waliokuwa wanashikiliwa na
IS na tayari tulifanikiwa
kuwaokoa hivyo kuendelea
kukaa mahala pale ni
ilikuwa ni kuendelea
kuhatarisha usalama wetu
na wa watu tuliowakomboa
ndiyo maana Rais akafanya
maamuzi yale
magumu.Inaumiza sana
kumpoteza rafiki yetu lakini
haikuwa rahisi hat akwa
Rais mwenyewe naamini
hata wewe ungekuwa
mahala pa Rais ungefanya
vile alivyofanya.It was a
tough call”
“Tough call? Akauliza
Gosu Gosu
“You can’t be serious
Austin.Rais aliamuru mrejee
nyumbani na kumuacha
nyuma Mathew ili
kumuondoa mwanae katika
hatari lakini alisahau kama
mtu aliyeachwa nyuma ndiye
aliyefanikisha kupatikana
kwa mwanae.It hurt
Austin.Inaumiza
sana.Najaribu sana kutaka
kulisahau jambo hili lakini
ninashindwa.Kinachoniumiz
a sikuwepo karibu
nisingekubali ujinga kama
huu kufanyika.Ningebaki
naye porini”akasema Gosu
Gosu
“Papaa,Mathew alikuwa
rafiki yetu na sote
tunaumizwa na kilichotokea
lakini ile ni vita na katika
vita hata watu wema huwa
wanapotea.Wewe I mpiganaji
unalifahamu hilo” akasema
Austin
“You call him your
friend? You left him behind
and you call him your
friend?Austin ujio wako hapa
umekuja kutonesha kidonda
nilichonacho.Hakuna siku
ambayo sijaangusha chozi
nikimlilia
Mathew.Hufahamu chochote
kuhusu Mathew.Sisi ambao
tuko naye karibu ndio
tunaoumia.I was a criminal,a
killer lakini amenitoa kule
nilikokuwa na amenirejesha
katika ubinadamu.Kwangu
mimi unapomzungumzia
Mathew Mulumbi
unamzungumzia mtu
muhimu mno”akasema Gosu
Gosu
“Papaa uko sahihi
kwamba yawezekana
simfahamu vizuri Mathew
kama vile unavyomfahamu
wewe lakini hata mimi
kitendo cha kuondoka na
kumuacha Mathew nyuma
kinaniumiza mno na
sintajisamehe kwa kile
kilichotokea lakini mimi ni
mwanajeshi wewe pia
umekuwa mwanajeshi na
unafahamu kitu kikubwa
tunachofundishwa jeshini ni
utii hasa kwa viongozi.Amri
ilitolewa na amiri jeshi mkuu
na mimi nisingeweza
kuipinga kwa namna yoyote
ile.Papii suala la Mathew
naomba lisitufanye
tukashindwa kufanya
majukumu mengine.We can’t
cry for him forever.We have
to stop ! akasema Austin kwa
sauti yenye amri na
kumtazama Gosu Gosu
“Nimekuja hapa kuomba
msaada wako.Let’s do this for
the our countries and
Mathew either he’s dead or
still alive will be proud of
us.Kumuenzi Mathew ni
kufuata nyayo zake.He was a
super billionaire lakini
linapokuja suala la ulinzi wa
taifa Mathew aliweka utajiri
wake kando akaingia katika
mapambano na hivyo ndivyo
anavyotaka sisi pia
tufanye.Muda wowote tuwe
tayari kukubali kufanya kazi
yoyote kwa ajili ya taifa
letu.Our countries needs us”
akasema Austin na Gosu
Gosu akainamisha kichwa
chini.
“Papaa inua kichwa
nitazame” akasema Austin
na Gosu Gosu akainua
kichwa akamtazama
“Tazama watu wote hawa
humu ukumbini they’re all
happy lakini wapo watu
ambao hawalali kuhakikisha
kwamba watu hawa
wanakuwa salama siku zote
na sisi ni miongoni mwa
watu hao ambao
tumechaguliwa kuifanya kazi
hiyo.Hatuwezi kuikimbia
kazi yetu tunatakiwa kuitika
ndiyo kila pale tunapoitwa
kwa ajili ya taifa letu.Taifa
linatuita na tuitike
ndiyo.Hivyo ndivyo Mathew
angefanya hajawahi kuitika
hapana.Kila pale alipoitwa
aliitika ndiyo.Mimi tayari
nimeitika ndiyo nataka
kusikia kutoka kwako ndiyo
au hapana.If it’s yes I’ll stay
but if it’s no I’ll go away and
I’ll never come bother you
again” akasema Austin.Gosu
Gosu akabaki kimya
akitafakari
“Papaa I need the
answer” akasema Austin
“Yes”akajibu Gosu Gosu
“Good.Let’s do this for
Mathew,for Tanzania,for
Congo and for East Africa
Community” akasema
Austin.Gosu Gosu
akachukua glasi yake ya
kinywaji
“I’m doing this for
Mathew” akasema Gosu
Gosu.Austin naye akainua
glasi
“Fo Mathew” akasema
wakagonganisha glasi na
wote wakanywa halafu Gosu
Gosu akauliza
“What’s the plan?
“Plani ni hii.Tukio hilo
linatakiwa lionekane ni tukio
la kihalifu.Kazi yetu sisi ni
kumuua Lucy,mume
wake,mtoto na
walinzi.Upande wa pili
tutatafuta majambazi ambao
tutawapa taarifa kwamba
ndani ya gari lile la Lucy
kuna fedha nyingi ili
wapange mipango ya
kumvamia.Wakati huo huo
tutakuwa tumewajulisha
polisi kuhusu uwepo wa
mpango wa majambazi hayo
kufanya uporaji ila
hatutawaeleza wanataka
kumpora nani na tutawapa
namba za gari ambalo
majambazi hao
watalitumia.Sisi tukifanya
mauaji hayo polisi kwa kuwa
wanafahamu mpango wa
majambazi na wanalifahamu
gari lao wataamini kwamba
mauaji hayo yamefanywa na
majambazi na hapo itaibuka
vita mpyakati ya polisi na
majambazi hao na sisi
tutakuwa tumemaliza zoezi
tutaondoka
kimyakimya.Dunia nzima
watajua kwamba Lucy
Muganza ameuawa na
majambazi.Unaonaje mpango
huo? Akauliza Austin na kwa
mbali sura ya Gosu Gosu
ikajenga tabasamu
“It’s one of the best plan”
“Thank you.Tatizo ni
namna ya kuweza kuwapata
hao majambazi” akasema
Austin
“I know someone who can
help us.Tutakwenda
kuonana naye kesho hapendi
kutembelewa usiku.Ni
Mathew pekee aliyekuwa na
uwezo wa kumfuata
usiku.Kitu kingine tunahitaji
kupata taarifa za huyo mama
ambaye kama anakuja siku
ya jumamosi ni siku mbili tu
kutoka leo hivyo maandalizi
yanatakiwa yafanywe
haraka” akasema Gosu Gosu.
“Taarifa nitaanza
kuzipata kesho kutoka kwa
majasusi ambao
wanamfuatilia Lucy
Muganza” akasema Austin
na kuagiza tena kinywaji
“By the way where is
Devotha? Have you heard
from her?akauliza Austin
“I don’t know where she
is.Nimejitahidi kumtafuta
bila mafanikio.Austin do you
mind if I ask a question?
“Just ask” akasema
Austin na kunywa bia kidogo
“I know I’ve asked you a
hundred times but I’m going
to ask you again.What real
happened that night?
Akauliza Gosu Gosu.Austin
akachukua kinywaji chake
akanywa halafu akashusha
pumzi na kusema
“Umeniuliza swali hili
mara nyingi lakini bado jibu
nililonalo ni lile lile ambalo
nimekuwa nikikupa siku
zote.Kila unapouliza huwa
ninakueleza kile
nilichokishuhudia mimi kwa
macho yangu usiku
ule.Tulivamiwa wakati
mabadilishano
yakiendelea.Sisi tulimuachia
Edger Kaka aende kwa watu
wa IS na wao waliwaachia
Olivia na Coletha.Mimi na
kikosi change tulikuwa
tumejibanza tukisubiri kama
kungetokea tatizo lolote na
lengo letu lilikuwa baada ya
kuwapata akina Olivia basi
tumuue Edger Kaka lakini
ghafla tulianza
kushambuliwa kwa silaha
kali kutoka kila
upande.Lilikuwa ni
shambulio ambalo hatukuwa
tumelitegemea.Tulipotezana
na kila mmoja alifanya
juhudi binafsi za
kujikomboa.Baada ya hali
kutulia tukajikusanya na
kugundua timu yote ya
Mathew walikuwa
wameuawa lakini Mathew
hakuwepo.Magaidi wote
tuliwaua lakini Edger Kaka
hakuwepo.Hicho ndicho
ninachokumbuka” akasema
Austin na kunywa tena glasi
yake ya kinywa ukimya wa
dakika tatu ukapita Gosu
Gosu akasema
“Austin kufuatia hicho
ulichonieleza kuna swali
ambalo nataka kukuuliza
and please be honest with
me”
“Uliza chochote usihofu
papaa” akasema Austin.Gosu
Gosu akamtazama usoni kwa
muda wa dakika moja halafu
akauliza
“Do you believe Mathew
is dead?
Austin akashusha pumzi
akaegemea kiti akazama
katika tafakari kisha akajibu
“No I don’t.Kuna sauti
ninaisikia ndani yangu
ikiniambia Mathew
hajafa.Hisia hizo ninazo kwa
muda mrefu na siamini kama
kweli Mathew
amekufa”akajibu Austin
“Ni hilo tu nililotaka
kulisikia kutoka kwako.Hata
mimi nina mawazo kama
yako.Siamini kabisa kama
Mathew amefariki
dunia.Austin nadhani
umefika wakati wa
kuutafuta ukweli kuhusu
Mathew”
“Hata mimi nilikuwa na
mawazo hayo ya kulichimba
suala hili la Mathew lakini
kwanza tumalize hii kazi ya
Rais ndipo tuingie katika
mambo mengine kwani
tukitaka kuanza kumtafuta
Mathew tunahitaji kujipanga
kisawa sawa” akasema
Austin wakaendelea na
maongezi kuhusiana na
mpango wao wa mauaji ya
Lucy Eyenga na saa sita za
usiku Austin aliachana na
Gosu Gosu akarejea kambini
kupumzika.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 3
Saa nne za asubuhi siku
iliyofuata Austin aliwasili
katika makazi ya Mathew
Mulumbi ambako kwa sasa
anaishi Gosu Gosu.Siku hii
Austin hakuwa katika sare
za kijeshi alikuwa amevaa
suruali ya jeans rangi ya
bluu na fulana
nyeupe.Alikaribishwa ndani
na Gosu Gosu wakawa na
mazungumzo kidogo kabla
hawajaendelea na kile
walichopanga kukifanya siku
ile
“Any word from
president?akauliza Gosu
Gosu
“Amenipigia simu
asubuhi ya leo akaniambia
kwamba atanipigia baadae
kuniunganisha na timu ya
majasusi ambao
wanamfuatilia Lucy
Muganza”
“Good.Tunakwenda
kuonana na Tino”akasema
Gosu Gosu
“Tino? Austin
akashangaa
“Ndiyo.Tulikuwa naye
Nairobi katika operesheni ya
kumchukua Edger kaka”
“Nimemkumbuka
Tino.Where is he now?
“Tino ni rafiki mkubwa
wa Mathew
Mulumbi.Biashara yake
kubwa ni silaha na
anafahamiana na majambazi
wengi wa Afrika Mashariki
kwani wengi hununua silaha
kutoka kwake.Huyu ndiye
atakayetuunganisha na
majambazi tunaowahitaji
katika misheni
hii.Nimekwisha zungumza
naye simuni nikamueleza
nitakwenda kwake kumuona
nina shida naye akaniahidi
kunisubiri saa tano za
asubuhi hivyo hatuna muda
wa kuoteza twende
tumfuate” akasema Gosu
Gosu wakaingia katika gari
la Mathew na kuondoka.
Walifika nyumbani kwa
Tino ambaye alikuwa
anawasubiri akawakaribisha
ndani
“Gosu Gosu kwa nini
hukuniambia kama
unakuja na kamanda
Austin?akaulizaTino
“Sikutaka kukupa hofu”
“Karibuni sana jamani.Ni
muda umepita
hatujaonana”akasema
Tino
“Kweli zimepita siku
nyingi hatujaonana”
akajibu Gosu Gosu
“Save yourself a drink”
akasema Tino akiwaelekeza
akina Austin kujihudumia
vinywaji.
“So guys tell why you are
here?Najua hamko hapa kwa
ajili ya kunijulia hali”
akasema Tino
“Ni kweli Tino.Tuko hapa
kwa sababu maalum.We
need you and we need your
help” akasema Austin na
Tino akaonekana kustuka
kidogo akaweka chini glasi
ya kinywaji aliyokuwa
ameshika
“You need me and you
need my help” akasema
Tino
“Yes” akajibu Austin na
Tino akatabasamu kidogo
“You guys you are just
like Mathew.You look for me
only whe you have
problems.So what is it this
time? Akauliza Tino
Austin akamuelezea kila
kitu kuhusu Lucy
Muganza.Tino akanywa
kinywaji kidogo na kusema
“Aren’t you guys tired of
being used everytime? These
people they use you for
nothing.Bado sijasahau
kuhusu Mathew.Moyo wangu
unaniuma mpaka leo hii
kumpoteza na alipotea
katika mambo kama haya
mnayotaka niwasaidie.Guys
I’m done.Nimekwisha achana
na hayo mambo na kwa sasa
nina biashara nyingine
zinazoniingizia fedha sitaki
tena kuhatarisha maisha
yangu” akasema Tino
“Tino suala la Mathew
Mulumbi linatuumiza
sote.He was our
friend.Inaniuma zaidi hasa
mimi ambaye nilikuwa naye
hadi dakika za mwisho.Guys
wote hapa ni wanajeshi.Wote
tumekwisha wapoteza
wenzetu muhimu sana
katika mapambano na
Mathew si mtu wa
kwanza.Look at me
nimepoteza familia yangu
yote.Walichomwa moto na
kuungua mpaka kuwa mkaa
but here I am I’m still
fighting.Ninachowaomba
ndugu zangu suala la
Mathew lisitufanye
tushindwe kutimiza
majukumu yetu mengine
kwa taifa.Huyu mama ni
hatari kwa usalama wa nchi
yetu.Kama akifanikiwa
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika mashariki
hatashindwa kuvuruga
muungano wetu.Naamini
hakuna ambaye yuko tayari
kuona hilo likitokea.Papaa
hapa amepigana vita msituni
kwa miaka mingi wakiitafuta
amani na leo nchi alikotoka
kuna amani na taratibu watu
wameanza kusahau kule
walikotoka lakini huyu
mama anakuja kutumiwa
kuleta mgawanyiko tena
nchini Congo ili mabeberu
waweze kuendelea na
mchezo wao wa kuchota
rasilimali.Hakuna kati yetu
anayetaka hilo litokee.Kama
Mathew angekuwepo hapa
asingejiuliza mara mbili
angevaa silaha na kuingia
katika mapambano.Ndugu
zangu tuna majonzi kuhusu
Mathew lakini njia pekee ya
kumuenzi ni kwa kushika
silaha na kupambana dhidi
ya yeyote Yule anayeonekana
kitisho kwa usalama wa nchi
yetu.Rais anatutegemea
sana” akasema Austin
“Rais ana vyombo vingi
vinavyoweza kulifanya hili
jambo kwa nini sisi?akauliza
Tino
“Kuna mambo mengine
ambayo ni ya siri kubwa na
huwezi ukamshirikisha kila
mtu bali watu wachache tu
unaowamini”
“He knows us?He knows
me?akauliza Tino
“He knows and trust me
and I trust you guys.Misheni
hii ni ya siri mno na Rais
ameamua iwe hivyo kwa
sababu lazima uchunguzi
utafanyika hivyo hataki
serikali ya Tanzania au
Congo zionekane zinahusika
katika kifo hicho” akasema
Austin na baada ya ukimya
fupi Tino akauliza
“Mnataka mimi nifanye
nini?Niwasaidie kitu gani
katika misheni hii?
“Misheni hii haitakiwi
kuonekana kama ni tukio la
mauaji ya kupangwa bali
lionekane kama ni tukio la
ujambazi.Tunataka kutafuta
kikundi cha majambazi
ambao tutawapa taarifa
kwamba gari atakalopanda
Lucy Muganza litakuwa na
mamilioni ya fedha ndani
yake hivyo basi watapanga
mipango ya kulivamia na
wakati huo huo
tutawajulisha jeshi la polisi
na kuwapa taarifa zote za
mipango ya majambazi hao
na wataanza kuwafuatilia
watu hao kwa
karibu.Wakifika mahala
ambako tutakuwa
tumepanga kutekeleza
mpango wetu tutawaondoa
Muganza na wengine kwa
haraka na kazi itabaki kwa
polisi na wale
majambazi.Tutawamaliza
Muganza na familia yake
tukiwa mbali hivyo polisi
wataamini kwamba
majambazi ndiyo
waliotekeleza mauaji hayo
katika kufanikisha mpango
wao wa kupora hivyo
watajihami na kutaka
kuwadhibiti.Majambazi
wakiona polisi wanawafuata
wataanza kuwarushia risasi
na hapo utatokea mvurugano
na kwa umahiri wa askari
wetu naamini watawamaliza
majambazi hao ndani ya
muda mfupi hivyo basi moja
kwa moja tukio hili
litaonekana ni tukio la
ujambazi na hakuna ambaye
ataingiza hisia kwamba
serikali inahusika na tukio
hilo.Wewe unawafahamu
watu wanaojihusisha na
hayo masuala ya ujambazi
hivyo utatusaidia kuandaa
mpango huo na wao.Baadae
leo nitaanza kuwasiliana na
kiongozi wa kikundi cha
majasusi wanaomfuatilia
Lucy na watatupa taarifa
zote za kuhusiana na Lucy
na tutazitumia taarifa hizo
kutengeneza mpango wetu
wa kumuondoa”akasema
Austin
“Sawa.Kwangu hilo ni
suala dogo sana” akasema
Tino kisha wakapanga
wakutane jioni ya siku hiyo
kwa ajili ya mikakati zaidi
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 4
Saa mbili za usiku
iliwakuta,Austin na Tino
tayari wamekwisha fika
nyumbani kwa Mathew
Mulumbi ambako Gosu Gosu
alikuwa akiwasubiri kwa
ajili ya kuendelea na
mipango yao.Baada ya
kupata chakula cha usiku
wakaelekea katika chumba
maalum ambacho Mathew
hukitumia kama ofisi yake
“Guys bila kupoteza
muda tuendelee na
majadiliano pale tulipokuwa
tumeishia mchana.Austin
what have you got for
us?akauliza Gosu Gosu
“Tayari nimekwisha pata
mawasiliano na mkuu cha
kikosi cha majasusi ambao
wanaendelea kumfuatilia
Lucy nchini Ufaransa.Kwa
taarifa walizonazo ni
kwamba Lucy atawasili hapa
Tanzania kesho kutwa
Jumamosi saa nne za
asubuhi.Lengo la kuja Dar es
salaam ni kumchukua
mwanae anayesoma katika
chuo kikuu cha Dar es
salaam anaitwa Theresia
Muganza kisha wataelekea
nchini Congo ambako
kumeandaliwa mapokezi
makubwa ambapo Lucy
atatambulishwa rasmi na
chama cha CDP kama
mgombea urais kupitia
chama hicho.Majasusi hao
wanaomfuatilia Lucy
wataendelea kumfuatilia
hadi pale Lucy
atakapoondoka Paris na
baada ya hapo she’ll be ours
hivyo mipango yote ya
kumuondoa ni juu
yetu.Tunatakiwa kuifahamu
ratiba yake atakapokuwa
hapa Tanzania.Tujue
akishuka uwanja wa ndege
ataelekea wapi,atatumia
usafiri upi na bila kusahau
ulinzi.Kwa kuwa ni mtu
ambaye anatumiwa na nchi
kubwa hawawezi kumuacha
hivi hivi lazima
watamuwekea ulinzi
mkubwa wa kutosha hivyo
lazima tujiandae kwa hilo”
akasema Austin
“Nadhani taarifa za
kutosha kuhusu ratiba nzima
ya Lucy Mganza hapa
Tanzania tutaipata kwa
mwanae Theresia.Lazima
watakuwa wanawasiliana na
atakuwa anafahamu kila
kitu.Kuna yeyote amewahi
kumuona au kumsikia huyo
Theresia au kujua mahala
anakoishi?akauliza Tino
lakini wote hawakumfahamu
Theresia Muganza.
“Wote hatumfahamu na
hatujawahi kumuona
Theresia.Nashauri tuanze
kwa kumfuatilia na
kumfahamu halafu tudukue
mawasiliano yake na tujue
wanaongea nini na mama
yake.”akashauri Tino
“Wazo zuri sana hilo
Tino.Hiyo itakuwa ni ratiba
yetu ya kwanza asubuhi ya
kesho.Vipi kuhusu wale
jamaa ambao tulikupa kazi
ya kuwatafuta? Austin
akauliza
“Tayari nimekwisha
fanya mawasiliano na kundi
Fulani nikawaambia
wajiandae nitawaletea
taarifa za kazi ya mamilioni
ya fedha na kwa kuwa
wananiamini
wamekubali.Kwa upande huo
hakuna wasi wasi
kabisa.Ninachohitaji
kufahamu tumejipangaje
kumuondoa Lucy?
“Mpango ninaofukiria
mimi uko hivi.Mpaka Lucy
atakapokuwa ametua hapa
nchini tayari tutakuwa
tumekwisha pata taarifa za
ratiba yake yote.Tutaanza
kumfuatilia kuanzia
atakaposhuka ndegeni hadi
sehemu ambako tutakuwa
tumepanga kufanya misheni
yetu.Ninaamini lazima
Theresia atakuwepo
uwanjani kuwapokea wazazi
wake kisha wataelekea
mahali aidha hoteli au kama
ana nyumba hapa Tanzania
wataelekea huko.Mchezo
wote tutaumalizia
barabarani” akasema Austin
na kuufungua mkoba wake
akatoa karatasi kubwa
ilikuwa ni ramani ya jiji la
Dar es salaam akaiweka
mezani
“Hii ni barabara ya
Serengeti ambayo inatoka
uwanja wa ndege hadi katika
mzunguko wa sanamu ya
kifaru.Pale kuna barabara
tatu.Ipo barabara ya
Arusha,barabara ya Fidel na
barabara ya Twiga.Hapa
ndipo misheni yetu
itakapofanyika.Eneo hili ni
eneo ambalo lina biashara na
shughuli nyingi.Tunatakiwa
kujipanga vizuri
hapa.Ukitoka barabara ya
Serengeti kama ukielekea
barabara ya Arusha pale
kuna hoteli Jacombo.Gosu
Gosu na Tino mtakuwa
hapa.Ni hoteli ambayo iko
pembezoni mwa
barabara.Mtachukua chumba
na kujiweka tayari.Ng’ambo
ya barabara kwa upande wa
Mashariki kuna hoteli 442
hapa nitakuwepo mimi na
mtu mwingine
nitakayemuongeza katika
timu yetu.Lucy atakapofika
katika mzunguko kama
ataelekea barabara ya
Arusha basi Gosu Gosu na
Tino mtafanya kazi ya
kumuondoa lakini endapo
ataelekea barabara ya Twiga
basi Mimi na huyo
nitakayekuwa naye
tutamaliza mchezo.Nina
imani wote ni wataalamu
katika kulenga shabaha na
tutatumia bunduki za hali ya
juu za masafaa marefu aina
ya Barret M82” akasema
Austin
“Mpango huu ni mzuri
lakini nina waza.Hatujui
Lucy anaweza kutumia gari
la aina gani.Kama
ulivyosema kwamba Lucy
anatumiwa na mataifa
makubwa hivyo lazima
wahakikishe wanamlinda na
yawezekana labda gari lake
likawa halipenyi
risasi.Jambo la pili
yawezekana gari lake likawa
na vioo vyeusi na kutupa
ugumu wa kuona
ndani.Tutafanikishaje
mpango wetu?akauliza Tino
“Ahsante kwa wazo
hilo.Ili kufanikisha mpango
wetu lazima tuwaone vyema
watu tunaotaka kuwaua
hivyo basi tunahitaji kufanya
kitu ambacho kitawafanya
waliomo ndani ya gari la
Lucy kufungua vioo vya gari
kama vitakuwa vimefungwa
watakapofika katika
mzunguko wa Kifaru ili
kutupa sisi nafasi ya kuweza
kuwaona vyema namna
walivyokaa ndani na
kuwaondoa”akasema Austin
“Tutengeneze ajali”
akashauri Gosu Gosu.
“Tuligonge kwa nyuma
au ubavuni gari hilo la Lucy
Muganza na watalazimika
kusimama na kushuka
kuangalia kitakachokuwa
kimetokea” akasema Gosu
Gosu
“Wazo la kutengeneza
ajali ni wazo zuri lakini ni
vipi kama ajali hiyo
itasababisha watu wajae
eneo hilo kwa haraka na
tukashindwa kutekeleza
misheni yetu? Kama
unavyojua hapa Dar es
salaam ajali ndogo hujaza
watu ndani ya sekunde
chache”Akasema Austin
“Mara tu milango
itakapofunguliwa tutaweza
kuona ndani na kuwaondoa
Lucy na familia yake haraka
sana kabla watu hawajajaa
eneo hilo la ajali” akasema
Gosu Gosu
“Ni vipi kama atakuwa
na msafara wa gari zaidi ya
moja? Ninahisi yawezekana
kukawa na gari la walinzi
wake au gari la ndugu zake
bila kusahau wapo wakongo
waishio hapa nchini ambao
wapo wanaomuunga mkono
na wanaweza wakajitokeza
pia kumpokea” akasema Tino
“ I have an idea.Dhumuni
letu sisi ni kumfanya Lucy
Muganza aidha afungue
madirisha atakapofika eneo
la mzunguko wa Kifaru au
ashuke kabisa ili tuweze
kupata nafasi nzuri ya
kumdungua.Nashauri tutege
bomu kwenye gari”akasema
Gosu Gosu
“That’s a
terrorism.Tunaweza kuua na
watu wasio na hatia.Tunaye
muhitaji ni Lucy na familia
yake pekee hivyo tujielekeze
hapo na tusifikirie kumwaga
damu za watu wasio na
hata.Ni magaidi pekee
wanaofanya hivyo” akasema
Austin
“Listen guys.Lucy
tunahitaji kumuondoa Lucy
kwa gharama zozote
zile.Endapo ikitokea
tukashindwa kumuua na
akafanikiwa kuondoka
salama hapa nchini madhara
yake ni makubwa tofauti na
kama wangekufa watu
wawili au watatu.Tutatafuta
gari kuukuu na kuliweka
pembeni ya barabara.Mara
tu gari la Lucy litakapofika
katika mzunguko lazima
watasubiri kidogo kuingia
katika mzunguko na
tutaitumia nafasi hiyo
kulipua bomu hilo.Ninaamini
kutakuwa na taharuki
kubwa sana na lazima
atatolewa katika gari ili
kuondolewa katika hatari na
hapo ndipo tutakapoanza
kuwadondosha mmoja baada
ya mwingine” akasema Gosu
Gosu
“Sasa nimekuelewa
Papaa
unachokimaanisha.Kwa
kuitazama ni plani nzuri
lakini tukio letu tunataka
kulifanya lionekane ni tukio
la kijambazi hivyo tukitumia
mlipuko kwanza linaweza
kuonekana kama shambulio
la kigaidi na vile vile
linaweza kuvuruga kabisa
mpango wetu kwani bomu
litakapolipuka itaibuka
taharuki kubwa sana eneo
lile na watu
watasambaratika.Mpango
wetu utakuwa umevurugika”
akasema Austin.
“Wazo lingine” akasema
Tino
“Tutaanza kumfuatilia
Lucy toka atakaposhuka
ndani ya ndege hadi
atakapoingia
barabarani.Wazo langu ni
atakapofika katika
mzunguko wa Kifaru kabla
hajaingia mzungukoni
tutayapiga risasi matairi
yaliyo upande wetu na
wakati huo huo ninyi Austin
na mwenzako mtayadungua
matairi ya upande wenu gari
halitaweza tena
kutembea.Wote walio ndani
ya gari watalazimika
kushuka baada ya gari
kushindwa kutembea ili
kuangalia kilichotokea na
hapo ndipo tutakapoitumia
nafasi hiyo kumuondoa Lucy”
“That’s a good
plan.Nadhani tukubaliane na
wazo hili la Tino” akasema
Austin na wote
wakakubaliana na wazo lile
“Jambo la mwisho
nadhani upo ulazima wa
kuongeza pia watu wachache
katika mpango
huu.Nitawashirikisha watu
wachache kutoka katika
kikosi changu ili kuongeza
nguvu” akasema Austin
JUMAMOSI – DAR ES
SALAAM
Ndege aina ya
Gulfstream III iliwasili
katika uwanja wa ndege wa
Julius Nyerere jijini Dar es
salaam.Ndege hii ya kifahari
ilimilikiwa na mwanamama
bilionea Lucy Muganza
“Ndege imetua
tayari.Narudia tena ndege
imetua” Mtu aliyewekwa
ndani ya uwanja wa ndege
wa Julius Nyerere
kumfuatilia Lucy Muganza
akawajulisha wenzake akina
Austin.Wote walikuwa na
vifaa vya mawasiliano
masikioni mwao hivyo basi
taarifa ile iliwafikia wote.
“Lucy amekwisha shuka
ndegeni?akauliza Austin
“Ndege imetua muda si
mrefu sana na mlango bado
haujafunguliwa” akasema
Yule jamaa
“Endelea kufuatilia
kutujulisha atakayeshuka
ndani ya hiyo ndege pale
mlango utakapokuwa
umefunguliwa” akasema
Austin
“Osmund nini
kinaendelea hapo nje ya
uwanja?akauliza Austin
“Theresia Muganza yuko
hapa sehemu ya kupokelea
abiria wanaowasili.Yuko na
watu kadhaa na wote
wanaonekana wanamsubiri
Lucy”
“Good.Endelea
kutujulisha kile
kinachoendelea upande
huo.Tino na Papaa
tafadhalini nijulisheni kama
mko tayari katika sehemu
zenu” akasema Austin
“Tuko tayari katika
sehemu nzuri tunaweza
kuyaona kwa urahisi magari
yote ambayo yanatokea
barabara ya Serengeti”
akasema Gosu Gosu
“Good.Sisi pia tko vizuri
hapa” akasema Austin.
Mlango wa ndege ya
bilionea Lucy Muganza
ulifunguliwa na baada ya
dakika mbili wakashuka
wasichana wawili halafu
baada ya muda mfupi
akajitokeza mwanamama
akiwa ameongozana na mtu
mmoja mrefu mwembamba
aliyevaa suti nzuri iliyomkaa
vyema.Mwanamama Yule
alikuwa amevaa gauni zuri
lililompendeza sana bila
kuisahau vito vya thamani
alivyovaa shingoni.Nyuma
yao kulikuwa na watu wanne
watatu wakiwa wazungu na
mmoja mwafrika.
“Lucy ameshuka ndegeni
akiwa na mumewe na
walinzi wanne.Narudia tena
Lucy ameshuka ndegeni
akiwa na mume wake na
walinzi wanne” akasema
Barack aliyekuwa ndani ya
uwanja wa ndege
akimfuatilia Lucy
“Barack are you sure?
“100%.Hivi sasa
anaelekea katika jengo la
uwanja”akajibu Barack
“Osmund standby.Lucy
ameingia katika jengo la
uwanja na muda si mrefu
atatoka” akasema Austin
Lucy Muganza akiwa na
mume wake Laurent
Muganza na walinzi wao
wanne walikamilisha
taratibu za uhamiaji
wakaruhusiwa kuingia
nchini. Mara tu walipotokea
katika sehemu ya abiria
wanaowasili Theresia aliruka
kwa furaha na kwenda
kuwakumbatia wazazi
wake.Ulikuwa ni wakati wa
furaha kubwa kwa familia hii
kukutana pamoja.
“Karibuni sana Dar es
salaam” akasema Theresia
“Ahsante sana
Theresia.Vipi maendeleo
yako?akauliza Lucy
“Ninaendelea vyema
kabisa.Nimewakumbuka
mno” akasema Theresia
“Maam we need to
go”mmoja wa walinzi
akamwambia Lucy kisha
wakasalimiana na marafiki
kadhaa wa Theresia
waliofika pale uwanjani
kumpokea na kutoka nje
“Austin this is
Osmund.Lucy tayari
ametoka nje anaelekea
kwenye gari”akasema
Osmund aliyekuwa nje ya
uwanja
“Good Osmund endelea
kufuatilia kila hatua”
akaelekeza Austin.
Gari tatu zilijipanga
tayari kabisa kwa kuondoka
pale uwanjani.Gari la
kwanza lilikuwa ni
Mercedece benz rangi nyeusi
na gari la kati kati lilikuwa
ni aina ya Limuosine nalo
likiwa na rangi nyeusi na
gari la tatu likiwa ni
Mercedece benz.Lucy mume
wake na Theresia wakaingia
katika gari la kati kati aina
ya Limousine na safari
ikaanza
“Lucy anaondoka hapa
uwanjani” akasema Osmund
“Zimeongozana gari tatu
lakini Lucy na familia yake
wamepanda gari la kati kati
aina ya Limousine.Mlinzi
mmoja amepanda mbele
katika Limousine na walinzi
waliobakia wamepanda gari
la nyuma.Hapa uwanjani
kazi imekamilika sisi
tunawafuata kwa nyuma”
akasema Osmund
“Good job
Osmund.Endeleeni
kuwafuatilia na kutujuza
kama kutakuwa na
mabadiliko yoyote” akasema
Austin
“Tino na Papaa jiwekeni
tayari Lucy amekwisha
ondoka uwanja wa ndege na
si muda mrefu sana atafika
mahala hapa.Kila kitu
kiende kama kilivyopangwa
tafadhali” akasema Austin
akiwaweka wenzake katika
utayari halafu akachukua
simu yake na kupiga namba
Fulani
“Christopher tayari
mmejipanga?akauliza
“Tumekwisha jipanga
kuanzia saa mbili za asubuhi
tunakusubiri wewe utupe
maelekezo kaka”
“Safi sana.Tayari Yule
mama amekwisha shuka
uwanja wa ndege hivi sasa
ameingia katika gari na
kuondoka kuelekea
mjini.Sanduku lenye madini
limeingizwa kwenye gari
aina ya Limousine.Mbele ya
hiyo Limo kuna mercedece
benz na nyuma yake kuna
mercedece nyingine jumla
kuna walinzi wanne ambao
nina hakika mnaweza
kuwaondoa bila matatizo”
“Ahsante sana Austin
kwa taarifa
hizo.Tumekwisha jipanga
vizuri na madini hayo
tutayachukua” akasema
jamaa aliyekuwa
akizungumza na Austin
simuni.
“Chris kwa
kuwakumbusha tu
mnatakiwa kutumia gari
yenye nguvu na uwezo
mkubwa wa kukimbia pale
mtakapokuwa mmeyapata
madini.Mnatumia gari gani?
“Tunatumia gari langu
lile Prado lakini nimebadili
namba na kuweka za
bandia.”
“Ok good.Kila la heri”
“Austin ahsante sana
kwa kutupa taarifa
hizi.Nakuahidi kama
tukifanikiwa basi mgawo
utakuwa sawa kwa sawa”
akasema Chris
“Shukran sana
Chris.Tutawasiliana tena
baadae pale kazi
itakapokuwa imekamilika”
akasema Austin na kukata
simu halafu akampigia simu
kamanda wa polisi
akamjulisha kuwa wale
jamaa aliomueleza kuwa
wanajiandaa kufanya tukio
la ujambazi tayari
wamekwisha jiandaa hivyo
polisi wawe tayari kwani
uporaji huo unapangwa
kufanyika katika mzunguko
wa kifaru.Alimueleza kila
kitu kuhusu gari
wanalotumia waporaji.Polisi
nao wakaanza kujipanga
vizuri ili kukabiliana na
majambazi hao.
Gari aina ya Limousine
alilopanda Lucy Muganza
liliwapita akina Chris
mahala walipokuwa
wameegesha gari lao nao
wakaingia barabarani
wakiwa nyuma yao kwa
magari mawili.Ndani ya gari
lile la kifahari maongezi na
vicheko vilitawala Lucy na
familia yae hawakujua kama
kuna jambo kubwa
linakwenda kutokea muda
mfupi baadae
Mwendo wa gari ulianza
kupungua baada ya kuanza
kuongezeka magari hasa yale
yaliyokuwa yakitokea
barabara ya umoja wa wa
Afrika kuingia katika
barabara ya Serengeti.
“Austin,Lucy amekaribia
sana kufika katika
mzunguko wa sanamu ya
Kifaru.Get ready” akasema
Osmund.
“Tino,Jose na Papaa
nadhani mmemsikia
Osmund.Tujipange tayari”
akasema Austin
Magari matatu ya
msafara wa Lucy Muganza
yalifika katika mzunguko wa
Kifaru.Tayari akina Austin
walikwisha liona gari
alilopanda Lucy
“Tino and Papaa please
confirm if you have a clear
shot ! akasema Austin na
akina Tino wakathibitisha
kuwa wameliona gari na
wako katika nafasi nzuri.
“It’s show time” akasema
Austin na ndani ya sekunde
chache wote kwa pamoja
wakaachia risasi
wakiyalenga matairi ya lile
gari la kifahari alimopanda
Lucy Muganza.
Dereva wa gari lile
alistuka baada ya kuhisi
kuna kitu kisicho cha
kawaida katika
gari.Lilibonyea chini ghafla
akafungua dirisha na
kuchungulia nje akastuka
baada ya kuona tairi zote
hazina upepo akapiga
usukani kwa hasira.Haraka
haraka akashuka pamoja na
mlinzi aliyekuwemo ndani ya
ile gari na kukagua tairi zote
hazikuwa na upepo
akawasiliana na wenzake
haraka haraka.Magari
yalikuwa yamesimama
yakipiga honi wakimtaka
dereva alisogeze gari lile
pembeni kwani lilisababisha
msongamano.Walinzi
wengine nao wakashuka kwa
haraka kutoka katika gari
walimokuwemo kwenda
kushuhudia kilichotokea na
wakafanya maamuzi ya
haraka baada ya kugundua
matairi yale yalitobolewa na
risasi
“Madam kuna
tatizo.Shukeni haraka sana
muingie katika gari lingine”
akasema mmoja wa
walinzi.Mlango wa
Limosuine ukafunguliwa
huku walinzi wa Lucy
wakiwa makini sana
wakiangaza huko na huko
kama kuna hatari
yoyote.Askari polisi nao
baada ya kuliona tukio lile
wakaanza kujiweka tayari
wakajua wale majambazi
wanajiandaa kufanya
ujambazi.Lucy,mumewe na
Theresia wakashuka garini
na walinzi wale wakaanza
kuwaongoza kwa haraka
kuelekea katika gari lingine
lakini kabla mlango wa lile
gari haujafunguliwa
kikatokea kitendo cha ghafla
ambacho hawakuwa
wamekitarajia.Ndani ya
sekunde chache walinzi wote
wanne walikuwa
chini.Lucy,mumewe na
Theresia wakabaki peke yao
wamesimama wakishangaa
kilichotokea mara Lucy
akatoa mguno na damu
zikaruka akaanguka chini
alikuwa amepigwa risasi ya
kichwa
“Luc………” Laurent
hakumaliza kulitaja jina la
mke wake naye akapigwa
risasi akaaguka chini.
“Theresia kimbia !!
akapiga kelele dereva wake
laini Theresa aliponyanyua
tu mguu akapigwa risasi ya
kifua akaanguka chini.
Kitendo kile cha akina
Lucy kupigwa risasi
kiliwastua polisi ambao
waliamini majambazi wale
wameanza kufanya kazi yao
hivyo kwa haraka wakaanza
kuwasogelea.Majambazi wale
walistuka kuona askari polisi
wakijipanga na kuelekea
katka gari lao wakajua tayari
wamegundulika wakaanza
kujihami kwa kuwarushia
risasi polisi.Eneo lile lilibaki
tupu baada ya mvua ya risasi
kuanza kunyesha watu wote
walikimbia na kuacha
magari.Mapambano ya
askari na majambazi
yalidumu kwa dakika tano
na askari wakafanikiwa
kuwaua majambazi wote
waliokuwemo ndani ya ile
gari.Baada kuwamaliza wale
majambazi wakaenda
kuwatazama wale watu
waliopigwa risasi ni mmoja
tu Theresia aliyepigwa risasi
kifuani upande wa kulia
ndiye alionekana akiwa hai
lakini wengine wote
hawakuwa na uhai.Haraka
haraka polisi wakataka
kwanza kuokoa maisha ya
Yule aliyekuwa
hai.Wakampakia Theresa
katika gari lao na kuondoka
kwa kasi kubwa
kumuwahisha hospitali.
“Good job guys.Now let’s
go home.Our country is safe”
akasema Austin na wote
wakaanza kufungua silaha
zao na kuziweka katika
mabegi yao kisha
wakaondoka eneo lile ambalo
tayari lilijaa askari.
****************
Hospitali ya mtendeni
ndiyo ilikuwa hospitali ya
karibu na mahala pale tukio
lilipotokea.Gari la polisi
likaingia hospitali hapo na
haraka haraka Theresia
akashushwa akaingizwa
ndani.
“Amepigwa risasi katika
tukio la ujambazi.Tafadhali
okoeni uhai wake” akasema
mmoja wa askari.Haraka
haraka Theresia akaingizwa
katika chumba cha upasuaji
akageuzwa ili kuangalia
kama risasi imetokea upande
wa pili lakini haikutoka
hivyo ilikuwa ndani,ikaletwa
mashine ya mionzi na kupiga
picha kifuani wakaiona risasi
moja
“Anahitaji kufanyiowa
upasuaji mkubwa kuondoa
risasi hii na hapa hospitalini
kwetu hatuna uwezo wa
kufanya upasuaji mkubwa
kama huo.Tutakachokifanya
ni kuzuia damu kuendelea
kuvuja halafu atakimbizwa
katika hospitali kuu ambako
atafanyiwa upasuaji mkubwa
wa kuondoa risasi ambayo
iko sehemu mbaya” akasema
daktari Yule na kwa haraka
likafanyika zoezi la kuzuia
damu kuendelea kuvuja
katika jeraha halafu
akapakiwa katika gari la
wagonjwa na kukimbizwa
katika hospitali kuu ya
Mtodora kwa ajili ya
upasuaji.
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 5
Taarifa za kuuawa Lucy
Muganza na mumewe
Laurent zilisambaa kwa
haraka na kumfikia balozi
wa Ufaransa nchini Tanzania
Rafael Berger ambaye alifika
haraka sana hospitali kuu ya
Mtodora ambako miili
ilipelekwa.Alionyeshwa miili
ya Lucy na mumewe
akajiridhisha kuwa ni
wenyewe.Wakati balozi
Rafael akiwa katika chumba
cha maiti ndani ya chumba
cha upasuaji madaktari
walikuwa katika heka heka
za kuokoa maisha ya
Theresia aliyekuwa
amepigwa risasi
kifuani.Upasuaji mkubwa
ulikuwa unafanyika kuondoa
risasi aliyokuwa amepigwa
kifuani
Balozi Rafael akiwa
ameongozana na daktari
mkuu alipelekwa katika
chumba cha upasuaji akiwa
amevaa mavazi maalum
kushuhudia madaktari
wakiendelea na heka heka za
kuokoa maisha ya
Theresia.Aliridhika na kazi
iliyokuwa ikifanyika akatoka
nje akaagana na daktari
akaelekea katika gari lake
akaondoka pale
hospitali.Akiwa ndani ya gari
balozi Rafael akampigia simu
Rais wa Ufaransa Michael
Weren
“Nipe taarifa Rafael
kuhusu taarifa hizi za
kuuawa Lucy Muganza”
akasema Michael na Rafael
akavuta pumzi ndefu na
kusema
“Ni kweli mheshimiwa
Rais Lucy na Laurent
wameuawa.Nimeiona miili
na nimethibitisha ni
wenyewe.Binti yao Theresa
yeye amenusurika.Amepigwa
risasi ya kifua na hivi sasa
yuko katika chumba cha
upasuaji madaktari
wakiendelea na jitihada za
kuokoa maisha
yake.Nimeingia hadi ndani
ya chumba cha upasuaji
nikajiridhisha na namna
madaktari wanavyofanya
kazi yao” akasema balozi
Rafael na ukimya mfupi
ukapita halafu Rais Michael
akauliza
“Tukio hilo limetokea
katika mazingira gani?
“Mara tu baada ya
kupokea taarifa hizo
niliwasiliana na mkuu wa
jeshi la polisi Tanzania
ambaye ni rafiki yangu na
akaniambia kwamba hata
yeye amepokea taarifa hizo
lakini hakuwa na taarifa
kamili za nini kilichotokea
ameahidikunipa taarifa
baadae atakapokuwa
amepata taarifa kamili lakini
taarifa ya awali inasema
kwamba lilikuwa ni
tukio la ujambazi na watu
watano wameuawa katika
tukio hilo.Inasemekana
walitaka kumvamia Lucy na
kumpora wakiamini anazo
fedha nyingi ndani ya gari
lake” akasema Rafael na
ukimya ukapita tena kisha
Rais Michael akasema
“Rafael tukio hili ni
kubwa na limenistua sana
hata hivyo kuna jambo
ambalo tunatakiwa tulifanye
kwa haraka nalo ni
kumuondoa Theresa hapo
Tanzania na kumleta
Ufaransa kwa matibabu na
usalama zaidi.Hatuna
uhakika bado kama Lucy
ameuawa kweli na hao
majambazi kama
inavyodaiwa au vinginevyo
hadi pale tutakapofanya
uchunguzi wetu hivyo basi
kumuacha Theresia hapo
Tanzania ni kuendelea
kuhatarisha maisha
yake.Nitaelekeza ndege ya
jeshi kutoka katika kambi
yetu ya kijeshi iliyoko
Djibouti ije haraka Tanzania
kumchukua
Theresia.Tafadhali hakikisha
hadi muda huo ndege
itakapowasili hapo Tanzania
Theresa anakuwa salama”
akasema Michael Weren Rais
wa Ufaransa
“Mheshimiwa Rais
unahisi kwamba yawezekana
hili ni tukio la kupangwa na
si la ujambazi kama
inavyodaiwa? Akauliza
Rafael
“Toka alipotangaza nia
ya kugombea urais Lucy
amekuwa na maadui wengi
hasa kutoka nchini mwake
ndiyo maana
tumemuongezea ulinzi lakini
nashangaa kusikia leo
ameuawa.Tukio hilo
linaonekana limepangwa
kitaalamu sana lakini
tutachunguza na kupata
majibu lakini kwa sasa
lazima tumuhamishe kwanza
Theresia yeye atatusaidia
sana kufahamu kile
kilichotokea” akasema Rais
Michael
“Sawa mheshimiwa Rais
nitaomba ulinzi kutoka
vyombo vya ulinzi hapa
Tanzania wamlinde Theresia
wakati tukisubiri ndege hiyo
ifike” akasema balozi Rafael
“Hapana usifanye
hivyo,hatujui nani
wanahusika katika suala hili
hivyo basi suala la
kumuondoa Theresia hapo
Tanzania ni suala la siri na
halitakiwi
kujulikana.Endelea kubaki
hapo hapo hospitali
usibanduke hadi pale ndege
itakapofika na
kumuhamisha” akasema
Rais Michael
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 6
Baada ya kumaliza
kazi,Austin na timu yake
walikutana nyumbani kwa
Mathew Mulumbi ambako
anaishi Gosu Gosu
“Misheni imekwenda
vizuri kama tulivyokuwa
tumepanga.Ninawashukuru
sana jamani kwa kazi hii
kubwa.” akasema Austin
“Baada ya kuimaliza kazi
hii sasa nataka tulijadili
suala la Mathew Mulumbi
kama tulivyokuwa
tumekubaliana” akasema
GosuGosu
“Kuna nini cha kujadili
kuhusu Mathew
Mulumbi?akauliza Tino
“Mimi na Austin
tulifanya majadiliano awali
na tukajikuta mawazo yetu
yanafanana kwamba Mathew
bado yuko hai” akasema
Gosu Gosu
“Nini kimewafanya
muamini hivyo kwamba
Mathew yuko hai?akauliza
Tino
“Ni kutokana na
mazingira ya tukio la
kupotea kwake ndiyo maana
tunahisi yawezekana
Mathew yuko hai” akasema
Gosu Gosu.Tino akavuta
pumzi ndefu na kusema
“Imepita miaka mitatu
sasa toka Mathew alipopotea
na mpaka sasa hakuna
taarifa zozote zilizowahi
kupatikana kama yuko
hai.Limekuwa ni kama
fumbo kubwa na hakuna wa
kulifumbua” akasema Tino
“Ni kweli ni fumbo
kubwa lakini tunataka
kulifumbua.Binafsi na hata
Austin tunaamini kwamba
Mathew bado yuko hai”
“Kama yuko hai where is
he?akauliza Tino
“Hapo ndipo mahala pa
kuanzia” akasema Gosu Gosu
Tino akamgeukia Austin
“Austin ulikuwepo katika
operesheni hiyo ya kwenda
kuwakomboa mtoto wa rais
na Olivia hebu tueleze nini
hasa kilitokea?Kwa nini
unaamini Mathew yuko
hai?akauliza Tino.Austin
akaonekana kuzama
mawazoni halafu akasema
“Guys I real don’t know
what real happened.Kwa
muda wa miaka mitatu sasa
kila siku usiku ninapofumba
macho hujaribu kuvuta picha
ya usiku ule ili walau niweze
kukumbuka kilichotokea na
kupata picha kama Mathew
yu mzima au alikufa lakini
kwa muda wote huu picha
ninayoipata ni ile ile.Olivia
anadai kwamba Mathew
alipigwa risasi akaanguka
chini na akawataka yeye na
Coletha
wakimbie.Hakumbuki nini
kiliendelea lakini kwa kauli
ile ya Olivia inaonyesha wazi
kwamba upo uwezekano
labda Mathew alifariki
dunia.Baada ya shambulio
kukoma mimi na vijana
wangu tulizunguka eneo lote
tukimsaka Mathew bila
mafanikio.Hapo ndipo
kichwa kinapoanza kuniuma
na maswali mengi yalianzia
hapo je kama alijeruhiwa
alitoroka eneo lile na kwenda
kujificha?Kama alitoroka je
yu mzima au alifariki dunia?
Kikosi kilichotumwa kwenda
kufanya uchunguzi na
kumtafuta siku iliyofuata
baada ya lile tukio kilitoa
taarifa yake kwamba
hawakufanikiwa kumpata
Mathew na walihisi
yawezekana aliliwa na fisi
kwani eneo lile lilikuwa na
fisi wengi.Hapo ndipo
mjadala ulipoishia kwamba
Mathew amekufa” akasema
Austin na ukimya ukatawala
mle ndani.
“Kitu gani mlikuwa
mmepanga kukifanya
kuhusu suala hili?akauliza
Tino
“Tulianza kwa kujenga
wazo hilo kwamba Mathew
yuko hai lakini bado
hatujajua wapi tuanzie
kulifanyia kazi hilo wazo”
akasema Gosu Gosu
“Guys mimi nadhani
tuliweke pembeni suala hili
kwa muda.Give me time to
think.Nikipata chochote
ambacho kitatusaidia katika
uchunguzi wetu
nitawaeleza”akasema Austin
“Nadhani Austin yuko
sahihi.Suala hili ni gumu
sana.Kama Mathew yuko hai
yuko wapi?Kwa nini kwa
muda huu wote hajataka
tujue mahala alipo?Nadhani
tuachane na hili jambo na
kama Mathew yuko hai basi
siku moja atarejea” akasema
Tino
“We have to fight for
him.He’s our friend and we
don’t have to stop searching
for him.Tutatulia pale
tutakapothibitisha kweli
amekufa lakini mpaka sasa
hivi hakuna ushahidi wowote
wa kutuonyesha Mathew
amekufa” akasema Gosu
Gosu
“Nakubali Papaa,Mathew
ni mwenzetu na lazima
tuupate ukweli kama kweli
amekufa au ni mzima.Give
me a little time and I’ll come
to you” akasema Austin na
kuchukua simu akampigia
Dr Fabian
“Hallo Austin” akasema
Dr Fabia
“Mheshimiwa Rais
nimekupigia kukujulisha
kwamaba ile kazi
tumeimaliza”
“Ahsante sana Austin
kwa kazi nzuri.Nimekwisha
pata taarifa tayari
kuhusiana na
kilichotokea.Mmetumia akili
nyingi sana kwani hivi sasa
kila mtu anaamini kwamba
tukio lile lilikuwa ni la
kijambazi.Nifikishie salamu
kwa vijana wote
mlioshirikiana katika
kutekeleza jukumu hili
waambie nitapanga nafasi ya
kukutana nao kuwashukuru
kwa kazi hii kubwa kwa taifa
lao”akasema Dr Fabian
“Kwa niaba yao
mheshimiwa Rais nashukuru
sana kwa kutuamini na
kutupatia jukumu hili kubwa
kwa nchi yetu”
“Pamoja na hayo”
akasema Dr Fabian na
kunyamaza kwa muda halafu
akasema
“Kuna jambo dogo
halikwenda sawa lakini si
tatizo.Nimepokea taarifa
kwamba Theresia mtoto wa
Lucy amenusurika yeye
alipigwa risasi ya kifua na
hivi sasa yuko mahututi na
madaktari wanaendelea na
jitihada za kuokoa maisha
yake.Lakini hili si tatizo
kwani mlengwa mkuu
alikuwa ni Lucy
Muganza.Huyu Theresia
hana hatari yoyote kwetu.”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
tunashukuru sana.Imekuwa
heshima kwetu kuaminiwa
nawe”akasema Austin
“Nitafurahi kukutana
nanyi wote na kujenga timu
imara na nitapenda
kuwatumia katika
operesheni zangu mbali
mbali za siri” akasema Dr
Fabian wakaagana na
kukata simu.
TEL AVIV – ISRAEL
Mlipuko mkubwa wa
bomu la kujitoa mhanga
ulitokea katika bustani ya
watoto wadogo katika jiji la
Tel Aviv.Mwanamke mmoja
aliyejitanda vazi refu jeusi
alifika katika bustani hiyo
akiwa na mwanae pamoja na
kikapu kilichojaa pipi
akaingia ndani ya bustani
hiyo akawakusanya watoto
na kuanza kuwagawia pipi
na dakika tano baadae
akajilipua.Watoto kumi na
sita walifariki pale pale
akiwemo mlipuaji na mtoto
aliyekuwa ameongozana
naye.Vikosi vya uokozi
vilifika haraka sana eneo hilo
la bustani na kuanza kazi
haraka ya kuokoa manusura
wa tukio lile.Wakati vikosi
vikiendelea na zoezi la uokozi
katika bustani ya watoto
bomu lingine kubwa
lililotegwa katika gari
lililipuka katika kituo cha
kulelea wazee na
kusababisha vifo vya wazee
tisa.
Muda mfupi baada ya
matukio yale ya milipuko ile
ya mabomu
kutokea,iliwekwa video
mtandaoni ikimuonyesha
Ibrahim Seif Al Nasir mmoja
wa viongozi wa juu wa
kikundi cha IS akijigamba
kwamba kikundi chao ndicho
kilichotekeleza mashambulio
yale mawili na akaendelea
kuonya kwamba
wamejipanga vyema na
kwamba mashambulio zaidi
yataendelea bila kukoma
hadi pale ardhi ya
wapalestina
itakaporejeshwa.Alitoa
angalizo kwa waisrael
wajiandae kwani damu
nyingi zaidi inakwenda
kumwagika.
Video ile ya kikundi cha
IS ilimpelekea waziri mkuu
kuitisha kikao cha dharura
cha wakuu wa vyombo vyote
vya ulinzi na usalama nchini
Israel
IDF,AMAN,AFI,BP,NI,GSS,
RPPC na MOSSAD.Kikao
hicho kizito kilichukua zaidi
ya saa sita kikijadili kwa
kina mashambulio yale
mawili ya mabomu,hali ya
usalama ya Israel na namna
ya kupambana na kikundi
cha IS ambacho kilitishia
kuendelea kufanya
mashambulio zaidi katika
ardhi ya Israel hadi pale
maeneo ya wapalestina
ambayo yanakaliwa
kimabavu na Israel
yatakaporejeshwa.Baada ya
kikao hicho kilichoongozwa
na waziri mkuu wa Israel
kumalizika,mkuu wa shirika
la ujasusi la Israel Moshe
Levine akarejea ofisini
kwake na kuitisha kikao cha
dharura na watendaji wakuu
wa shirika hilo pamoja na
wakuu wa idara zote zilizo
ndani ya Mossad ambao
walifika kwa haraka sana na
kikao kuanza
“Nimetoka katika kikao
kizito na waziri
mkuu.Agenda kuu ya kikao
hicho ni usalama wa Israel
hasa kufuatia milipuko
miwili ya mabomu iliyoua
watu ishirini na tisa.Kama
haitoshi kikundi cha IS
ambao wametekeleza
mashambulizo hayo
wameendelea kutishia
kumwaga damu zaidi katika
ardhi yetu.Israel hatuko
tayari kwa vitisho vya
namna hii na lazima
tuwaonyeshe kwamba
ukimwaga damu ya muisrael
mmoja malipo yake ni
makubwa.Huu ni mwisho wa
kuvumilia na sasa
tunakwenda kulimaliza
kundi hili la kigaidi na
kulinda maisha ya watu
wetu” akasema Moshe na
kunyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Nimeulizwa maswali
katika kikao ambayo sikutoa
majibu ya
kuridhisha.Nimeulizwa kwa
nini hadi leo hii
tumeshindwa kuwakamata
au hata kufahamu waliko
wafadhli wakuu wa kikundi
cha IS na vikundi vingine
vinavyofanya mauaji katika
ardhi yetu? Mossad ni
chombo kikubwa kina
majasusi wenye uwezo
mkubwa mno kuliko vyombo
vingi vya kijasusi
duniani,tumefanikiwa
operesheni nyingi sana
duniani lakini kwa nini
mpaka leo hatujui alipo
Habiba Jawad na wenzake
wanaovifadhili vikundi hivi
vya kigaidi?Vyombo vyote
vya ulinzi hapa Israel
vinatutegemea sisi kupata
taarifa za mahala walipo
watu hao ambao ni wafadhili
wakuu wa vikundi hivi lakini
toka tulipoanza kumtafuta
Habiba Jawad mpaka leo hii
ni miaka kadhaa imepita na
hakuna majibu yopote ya
kuridhisha kuhusu mahala
alipo Habiba na
wenzake.Jibu nililowapa ni
kwamba tayari tuna mipango
tunaendelea nayo katika
suala hilo na nikaomba
tupewe muda kidogo.Waziri
mkuu ametupa muda wa
wiki mbili tuwe tumepata
majibu kutoka katika hiyo
mipango yetu.Waziri mkuu
yuko sahihi kabisa kuwa
mkali kwani suala hili
limechukua miaka mingi kitu
ambacho hakijawahi kutokea
katika shirika letu.Jambo
hili linakaribia miaka kumi
sasa na hatuwezi kuendelea
kumfuatilia mtu mmoja kwa
miaka hiyo yote lazima
jambo hili lifike mwisho na
tufahamu mahala alipo
Habiba na tumtie nguvuni na
kuhitimisha ugaidi katika
ardhi yetu.Nataka leo nipate
taarifa za mipango yetu
inakwendaje.Tuanze na Dr
Daniel.Nimekuita hapa ili
utupe taarifa kuhusiana na
Edger Kaka.Kuna
matumaini yoyote unayaona
kwake?Kuna mabadiliko
yoyote unayategemea?
Akauliza Moshe na Dr Daniel
akajibu
“Kama nilivyoeleza
katika taarifa yangu ya mara
ya kwanza baada ya
kumpima Edger Kaka mara
tu alipoletwa kutoka Kenya
na kwa mujibu wa vipimo
ambavyo nimeendelea
kumpima mara kwa mara
hakuna tena mabadiliko
yoyote yaliyotokea wala
yanayotegemewa
kutokea.Edger hataamka
tena.Ubongo wake umekufa
na hakuna namna ya kuweza
kumuamsha.Kinachomfanya
aonekane yuko hai ni
mashine zile alizofungiwa
lakini kiuhalisia Edger
amekwisha fariki
kitambo”akasema Dr Daniel
“Dr Daniel ahsante kwa
taarifa hiyo.Uliwahi
kutueleza mapema jambo hili
lakini tulikuomba uendelee
kumuweka katika mashine
ya kumsaidia kuishi
tukitegemea labda kutakuwa
na mabadiliko mbeleni lakini
imepita miaka mitatu sasa
na hakuna mabadiliko yoyote
na kwa mujibu wa taarifa
yako ya leo ni kwamba Edger
tayari amefariki dunia hivyo
basi hakuna haja ya
kuendelea naye.Ni wakati wa
kuzima mashine zote na
kumuacha apumzike”
akasema Moshe na chumba
chote kikawa kimya
“Edger Kaka
tunamuondoa rasmi katika
mipango yetu na sasa
tunabaki na mtu mmoja
ambaye tunaamini anaweza
akawa na msaada kwetu
ambaye ni Mathew
Mulumbi.Huyu aliwahi kuwa
jasusi nchini Tanzania na
ndiye aliyeongoza kikosi
kilichovamia ubalozi wetu
Nairobi wakaua watu na
kumchuua Edger Kaka
kutoka mafichoni
tulikomficha.Kwa mujibu wa
taarifa tulizozipata kutoka
kwa aliyekuwa wakala wetu
nchini Tanzania,Mathew na
wenzake ndio waliowaua Avi
Abramson dereva na mlinzi
wake.Wakala wetu huyo
aliyetupa taarifa zote anadai
baada ya kumchukua Edger
Kaka kutoka Nairobi
Mathew alifanya
mawasiliano na Habiba kwa
ajili ya kufanya
mabadilishano ya mateka
yaani yeye awape Edger
Kaka na wao IS waachie
huru rafiki yake anaitwa
Olivia na mtoto wa Rais wa
wakati huo ambao walikuwa
wametekwa na magaidi wa
IS.Ni kwa sababu hiyo
Mathew anakuwa ni mtu
muhimu sana kwetu kwa
sasa.Tunataka kujua namna
alivyoweza kuwasiliana na
habiba Jawad.Kwa bahati
mbaya toka ameletwa hapa
Israel Mathew Mulumbi
hajawahi kufungua mdomo
wake kulia au kutamka
chochote.Ni binadamu wa
ajabu sana.Niliagiza kiwango
cha mateso kipande hadi
kufikia daraja la kwanza
lakini pamoja na mateso
hayo yote bado huyu jamaa
hajathubutu kusema
chochote.Nimevutiwa sana
na aina ya majasusi wa aina
hii ambaye yuko tayari kufa
kuliko kutoa siri.Amekubuhu
vilivyo katika ujasusi”
akasema Moshe na
kunyamaza kwa sekunde
chache
“Njia ya mateso
haikuonekana kuzaa
matunda hivyo tukaamua
kubadili mbinu.Katika
taarifa tulizopewa na huyo
wakala wetu ni kwamba
Mathew ni mtu tajiri
sana.Yeye na mke wake
wanamiliki makampuni na
biashara kubwa kubwa
sehemu mbali mbali
duniani.Mke wake na watoto
wao wawili wanaishi Paris
Ufaransa.Tumeamua
kuitumia familia yake
kumfungua mdomo wake na
nina uhakika safari hii
lazima atafunguka kwani
takwimu zinaonyesha njia hii
imekuwa na mafanikio
makubwa kila pale
inapotumiwa.Efraim Dagan
wewe ndiye msimamizi wa
operesheni hii hebu tupe
mrejesho nini kinaendelea
hivi sasa katika mpango
wetu wa kuitumia familia ya
Mathew? Akauliza Moshe
Levine
“Tayari tumemtuma
mmoja wa watu wetu Nahum
Yatom kwenda jijini
Paris.Akiwa pale Nahum
atakutana na Peniela na
kujenga naye mahusino ya
kibiashara kwani anakwenda
pale kama mfanya bisahara
tajiri.Nahum ni kijana
mtanashati sana mwenye
umbo na sura nzuri yenye
kuvutia wanawake wengi na
yeye ni maalum kabisa kwa
misheni kama hizi za
kujenga mahusiano na
wanawake ambao
tumewalenga.Ni mtaalamu
sana katika upande huo na
anajua nini cha
kufanya.Hajawahi
kushindwa.Anazo mbinu zote
za kuweza kumteka
mwanamke.Baada ya
kuanzisha mahusiano ya
kibiashara na Peniela
jukumu lake la pili ni
kuanzisha mahusiano naye
ya kimapenzi na tayari
amekwisha fanikiwa kwa
hilo.Amekutana na kufanya
mapenzi na Peniela mara
mbili katika hoteli alikofikia
na sasa Peniela amemualika
nyumbani kwake.Nahum
hataki kufanya haraka
kwenda nyumbani kwa
Peniela ili kumfanya
asistuke
chochote.Atakapokwenda
nyumbani kwa Peniela
atafunga kamera za siri
ambazo zitatuwezesha
kumuona yeye na Peniela
katika mahaba mazito na
hapo ndipo tutamuonyesha
Mathew Mulumbi picha hizo
ambazo tunaamini
zitamuumiza sana na
atafunguka.” akasema
Efraim na kwa mbali Moshe
akatabasamu
“Huu ni mpango mzuri
sana.Linapokuja suala la
familia watu wengi hata
wawe wagumu kiasi gani
hushindwa kuvumilia na
kufunguka.Nina uhakika
mkubwa kwa mpango huu
Mathew Mulumbi
atakapomuona mke wake
akiwa na mwanaume
mwingine katika mahaba
lazima atafunguka kila kitu
anachokifahamu kuhusu
Habiba Jawad.Hata hivyo
nataka Nahum asiendelee
kuvuta muda mwingi kufika
nyumbani kwa Peniela.Kama
tayari amekwisha muweka
Peniela kiganjani hakuna
kuchelewa.Afanye haraka
kazi aliyotumwa
huko.Mwambie kwamba
nataka baada ya siku tatu
awe amekamilisha kila kitu
na zoezi lifanyike ili Mathew
ashuhudie.Hatuwezi kusubiri
zaidi ya hapo” akaelekeza
Moshe
BAADA YA SIKU 3
FACILITY 1391 TEL AVIV
Mlango mzito wa chumba
uliafunguliwa wakaingia
watu sita watatu kati yao
akiwa na silaha.Taa
ikawashwa na watu wale
wakaonekana wakiwa
wamezifunika nyuso zao
zisionekane.
“Mathew Mulumbi muda
wa safari” akasema mmoja
wao na kumsogelea Mathew
ambaye alikuwa
amejikunyata katika godoro
akiwa amevalishwa mavazi
meusi akitetemeka kwa
baridi.Mkono wake mmoja
ulikuwa umefungwa pingu
na mnyororo mrefu
ukaunganisha pingu ile na
chuma kizito kilichofukiwa
katika sakafu yenye zege
zito.Mathew Mulumbi
ambaye alikuwa na ndevu
nyingi na nywele ndefu
akafunguliwa pingu ile ndefu
akafungwa nyingine mikono
yote halafu akafunikwa
mfuko mweusi kichwani na
kutolewa ndani ya kile
chumba akaingizwa katika
gari maalum ambalo
liliondoka katika jela hii ya
siri ambamo hufungwa
magaidi na watu hatari kwa
usalama wa Israel.
Baada ya dakika arobaini
gari likasimama mlango
ukafunguliwa na Mathew
Mulumbi akashushwa garini
bado akiwa na mfuko
kichwani.Watu wale
waliomuongoza hawakuwa
wakizungumza.Mathew
alihisi wakipanda lifti na
baada ya muda mfupi
milango ya lifti ikafunguliwa
wakatembea kidogo na
mlango wa chumba
ukafunguliwa akaingizwa
ndani na kukalishwa sofani
halafu mfuko ule mweusi
ukatolewa kichwani
akajikuta katika chumba
kimoja kikubwa kizuri
chenye samani za
kupendeza.Alishangaa kwani
kwa muda wa miaka mitatu
Mathew alikuwa analala
katika godoro kuu kuu ndani
ya chumba chenye baridi
kali.Akiwa bado katika
kukishangaa chumba kile
kizuri mmoja wa wale jamaa
akamwambia
“Ingia bafuni uoge”
akasema Yule jamaa na
kumfugua pingu
akamuonyesha Mathew
mlango wa bafu.Taratibu
Mathew akainuka na
kuufungua mlango wa bafu
akaingia.Lilikuwa ni bafu
zuri sana lakini kabla
hajafanya chochote akapatwa
na mshangao mkubwa baada
ya kujitazama katika kioo
“Nimekuwa
hivi?Nyumbani wakiniona
katika hali hii watadhani
mimi ni
msukule.Ninatisha.Sijawahi
kujitazama kwenye kioo toka
nilipotekwa na hawa
jamaa.Uso wangu
umeharibika ninaonekana
kama shetani” akawaza
Mathew akiendelea
kujitazama katika
kioo.Pembeni akaiona
mashine ya kunyolea pamoja
na dawa mbalimbali
akaishika mashine ile
akaitazama.
“Sijui hata nianzie wapi
kwa namna ninavyotisha.Ni
muda mrefu sijatia maji
mwilini mwangu.Nini hasa
wanataka kunifanyia hawa
jamaa? Akajiuliza
“Hii ni moja ya njia za
majasusi kutaka kupata
taarifa kutoka kwa mtu
wanayemshikilia kwa
kujifanya wanakutendea
wema baada ya njia ya
mateso kushindikana.Lakini
hapa wamefika hata kama
wakitumia njia hii
hawatapata kitu kutoka
kwangu.Niko tayari kufa
kuliko kuwaeleza kitu
chochote hawa jamaa”
akawaza na kuanza kuvua
ile nguo nyeusi aliyokuwa
amevaa na akagundua
kwamba nguo ile ilikuwa
imeshikana na mwili
kufuatia vidonda alivyokuwa
navyo mwilini.Akaitoa kwa
nguvu na kuhisi maumimu
makali kwani alitonesha
baadhi ya vidonda.Akafumba
macho na kusikilizia
maumivu yale.
“Kwa muda mrefu hawa
jamaa wamekuwa
wananitesa wanataka nikiri
kwamba nilihusika katika
uvamizi wa ubalozi wao
Nairobi na papo hapo
niwataje watu nilioshirikiana
nao. Katu siwezi kuwaeleza
chochote.Niko tayari kufa
lakini si kusema chochote
kwa hawa jamaa” akawaza
na kuvua suruali
akajitazama katika kioo
namna mwili wake
ulivyoharibka.Mwili wote
ulijaa vidonda.Taratibu
Mathew akaingia katika
beseni kubwa la kuogea
akafumba macho na
kukukumbuka maisha yale
aliyokuwa akiishi
“Nilikuwa na maisha
kama haya kabla sijatekwa
nyara.Masikini familia
yangu sijui watakuwa katika
hali gani hadi muda huu
sijatokea.Peniela atakuwa
Amelia mn😵h my God
Ruby,sipati picha namna
atakavyokuwa
akihuzunika.Kila
ninapowawaza hawa watu
wangu wa karibu,familia
yangu ,Ruby,Gosu Gosu
ninapatwa na nguvu ya
kuendelea kuvumilia mateso
makali ninayoyapata
hapa.Naamini iko siku
nitatoka katika mateso
haya,iko siku nitarejea
nyumbani kuungana nao
tena” akawaza Mathew
akiwa ndani ya beseni lile la
kuogea
“Kila ninapofumba
macho picha ya usiku ule
hunijia.Nakumbuka namna
tulivyovamiwa na kuanza
kushambuliwa.Nilipigwa
risasi kadhaa na
wakanichukua.Kwa
inavyoonekana wale jamaa
walinilenga zaidi mimi na
Edger Kaka kwani baada ya
kutupata mapambano
yalikoma.Waliotushambulia
kilikuwa ni kikosi cha
Israel.Kitu ambacho
nimekuwa ninajiuliza kwa
muda mrefu walifahamuje
kama tunafanya mabadiliano
ya mateka na IS?Mpango ule
ulikuwa wa siri na ninahisi
kwamba lazima kuna mtu
ambaye aliwapa Israel
taarifa za kuwepo kwa
mpango ule wa
mabadilishano.Akilini
mwangu anakuja Devotha
lakini kuna wakati
ninakataa kwamba Devotha
hawezi akafanya
hivyo.Tumekuwa naye katika
operesheni nzima hadi
mwisho na ameshiriki
kikamilifu katika kuvamia
ubalozi wa Israel
Nairobi.Lakini swali lingine
linalokuja kama si yeye ni
nani basi anaweza akafanya
hivyo? Waliofahamu kuhusu
mabadilishano yale ni Gosu
Gosu na Devotha na kati ya
hao ni Devotha ambaye
alikuwa na mahusiano na
Mossad.Sitaki kuamini moja
kwa moja kama kweli ni yeye
aliyeuza taarifa zetu kwa
Mossad kwani nilimuamini
sana lakini endapo
nikifanikiwa kutoka hapa
nitafanya uchunguzi na
kumbaini mtu aliyesababisha
ninateseka namna hii”
akawaza na kuendelea
kuoga halafu akatoka ndani
ya beseni lile la kuogea
akaenda katika kioo
akachukua mashine na
kunyoa ndevu zote na nywele
“Afadhali hapa kidogo
ninaonekana
binadamu.Mungu
atawabariki kwa wema huu
mdogo walionitendea lakini
naamini kuna kitu
wanakitafuta ndiyo maana
wamefanya hivi”
akawaza.Alipomaliza
akatoka bafuni na kukuta
nguo zikiwa zimewekwa
kitandani.
“Vaa hizo” akasema
mlinzi aliyekuwemo mle
chumbani.Mathew akavaa
nguo zile alizoletewa
akajitazama katika kioo
“Kidogo kwa sasa
ninaonekana binadamu”
akawaza akiwa amesimama
mbele ya kioo halafu Yule
mlinzi akamtaka aketi
sofani.Baada ya dakika mbili
akaingia mwanamke mmoja
aliyevaa sketi fupi nyeusi na
shati jeupe akiwa na sinia
lenye chupa ya mvinyo na
glasi akamuwekea Mathew
mezani
“Karibu mvinyo safi”
akasema Yule
mlinzi.Mathew akaitazama
chupa ile ya mvinyo halafu
akatikisa kichwa ishara ya
kukataa kutumia mvinyo
ule.Aliendelea kukaa sofani
mawazo mengi yakizunguka
kichwani kwake na mara
mlango ukafunguliwa
wakaingia watu wanne
“Ahsanteni vijana sasa
mnaweza mkaniacha na
Mathew” akasema mtu
mmoja aliyekuwa amewekwa
kati kati na walinzi wote mle
ndani wakatoka na Yule
jamaa akaenda kuketi sofani
akitazamana na
Mathew.Akaiinua chupa ile
ya mvinyo akaitazama na
kutabasamu
“Mallacan 1946 mvinyo
ghali kabisa
duniani.Nimekuletea mvinyo
huu ishara ya kufungua
mahusiano mapya kati
yetu.Ninaitwa Efraim Dagan
ni mkuu wa idara ya
operesheni za kimataifa
ndani ya Mossad.Kama
hutajali tunaweza kutembea
kidogo?akauliza Efraim na
kuinuka Mathew akasita
kusimama
“Usihofu Mathew,uko
salama.Tafadhali inuke
tutembee kidogo” akasema
Efraim na Mathew akajaribu
kusimama akahisi miguu
haina nguvu.Efraim
akamfuata akamshika
mkono akamsaidia
kusimama wakatoka ndani
ya kile chumba wakaanza
kutembea katika korido
huku walinzi wakiwa nyuma
yao.Mathew alionekana
dhaifu hivyo mwendo
ulikuwa mdogo sana.Ni
Efraim ambaye alikuwa
akiongea lakini Mathew
hakuonekana
kumsikiliza.Waliingia katika
chumba Fulani kilichokuwa
na runinga nane kubwa na
watu kadhaa walikuwa
wanaendelea na kazi katika
kompyuta zao.Efraim
akamuongoza Mathew hadi
katika sofa nzuri wakaketi
wakitazama runinga kubwa
“Mathew Mulumbi kwa
muda wa miaka mitatu
tumekuwa tukihitaji kusikia
kauli yako ukikiri kuhusika
katika uvamizi wa ubalozi
wetu jijini Nairobi ukaua na
kuchukua mateka lakini
umekuwa kiburi na hauko
tayari kufanya
hivyo.Tumekupa kila aina ya
mateso lakini unaonekana u
mvumilivu mno wa mateso
na kwa ajili hiyo basi
umetulazimisha kufanya kile
ambacho hatukuwa
tumekusudia
kukifanya.Naomba nipeleke
Paris” akasema Efraim
akimuelekeza mmoja wa
vijana waliokuwamo ndani
ya kile chumba.Mara katika
runinga zikaanza kuonekana
picha na Mathew akapatwa
na mstuko mkubwa
“Penny !!
Kwa mara ya kwanza
baada ya miaka mitatu
Mathew Mulumbi akafungua
mdomo na kutamka baada ya
kumuona mke wake Peniela
akiwa chumbani na kijana
mmoja mwenye sura
nzuri.Walikuwa wamelala
kitandani wakiwa watupu
kabisa na ilionekana
walikuwa wametoka kufanya
mapenzi.Peniela alionekana
ni mwenye furaha na
walifanyiana utani kwa
kurushiana mito na Yule
kijana
“No this is not true !
akasema Mathew kwa sauti
ndogo na
kunyanyuka.Walinzi
waliokuwa karibu
wakamsogelea.
“Kaa chini Mathew
Mulumbi” akasema Efraim
na walinzi wakamfuata
Mathew wakamkalisha chini.
“Hii si kweli.Hii picha
mmeitengeneza kutaka
kuniumiza.Peniela mke
wangu hawezi akafanya kitu
kama hiki” akasema Mathew
“Hiki si kitu cha
kutengeneza Mathew.Hiki ni
kitu cha kweli.Tazama
saa.Sisi na Patris
tumepishana kwa saa moja
tu.Unachokiona ni kitu
ambacho kinaendelea sasa
hivi katika nyumba yako
iliyoko Paris.Kijana
unayemuona runingani
anaitwa Nahum na kwa sasa
yuko na Peniela mke wako
ambaye anaamini tayari
umekwisha fariki
dunia.Tunao pia watu wetu
ambao wanawafuatilia binti
yako Malaika na mwanao
Patrick.Mathew tunao uwezo
wa ………..” Efraim
hakumaliza alichotaka
kukisema Mathew akapatwa
na nguvu za ajabu akainuka
na kuwasukuma walinzi
akamuendelea Efraimu
akamtandika ngumi nzito
iliyomuangusha sofani mara
Mathew akaanguka chini na
kupoteza fahamu baada ya
kuwekewa mgongoni kifaa
chenye chaji za umeme
alichokuwa amekishika
mmoja wa walinzi.
“Mpelekeni chumbani
mfungeni mikono na
miguu.Mtu hatari sana
huyu” akaelekeza Efraim
aliyekuwa anavuja damu
mdomoni.Mathew
akachukuliwa akapelekwa
katika chumba kingine
kilichokuwa na kitanda
kidogo akafungwa miguu na
mikono kwa pingu maalum
zilizounganishwa katika
kitanda hicho.
“Ana mikono migumu
kama jiwe Yule jamaa lakini
tumempata.Hatimaye baada
ya miaka mitatu leo
ameongea.Ameumizwa na
kile alichokiona na lengo letu
limefanikiwa kwani tulitaka
aumie na sasa atakuwa
tayari kufanya kitu chochote
hata kutueleza kitu chochote
kile kutokana na hasira
alizonazo” akawaza Efraim
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 1: EPISODE 7
Mathew Mulumbi
alirejewa na fahamu baada
ya dakika kumi na tano na
kujikuta akiwa amefungwa
miguu na mikono katika
kitanda akajaribu kujitikisa
lakini hakuweza alikuwa
amefungwa barabara.
“Kile nilichokiona
runingani ni kitu cha kweli
au nilikuwa njozini?
Niliyemshuhudia katika
video ile alikuwa ni Peniela
mke wangu au ni katuni?
Akawaza
“Lakini mwanamke
niliyemshuhudia ni Peniela
mke wangu.Video ile
inaonekana ni video halisi
kabisa na mle chumbani
walimokuwamo kweli ni
chumbani kwangu.Naamini
watu hawa wamenionyesha
video ile kwa ajili ya
kuniumiza baada ya njia zao
zote za mateso
kushindikana.Kwa hili
walilolifanya wamefanikiwa
wameniumiza mno.Peniela
ninampenda mno pamoja na
wanangu” akawaza Mathew
na michrizi ya machozi
ikaonekana machoni
“Peniela..ouh
Pen…………….” Akatolewa
mawazoni Mathew baada ya
mlango kufunguliwa
akaingia Efraim akiwa
ameweka pande la barafu
mahala alipopigwa ngumi na
Mathew.Alikuwa
ameongozana na walinzi
wake.Mathew alipomuona
hasira zikazidi akajaribu
kujitikisa lakini alikuwa
amefungwa barabara.
“Mathew najua umeumia
sana kwa video ile uliyoina
ya mkeo.Tulitaka
tukuonyeshe kile
kinachoendelea huko
nje.Watu wako wote
wanaamini tayari umekufa
ndiyo maana hata mkeo
Peniela ameamua kuwa na
mwanaume mwingine
ambaye ni mtu wetu.Familia
yako iko mikononi mwetu na
tukiamua muda wowote
tunaweza kuifanya kitu
chochote.Mathew hakuna wa
kukuokoa hapa ulipo bali ni
juhudi zako wewe mwenyewe
ndizo zitakuokoa.Chaguo ni
lako kama unataka
kuendelea kukaa hapa au
kuiokoa familia yako.”
akasema Efraim.Mathew
akauma meno kwa hasira na
kuuliza
“Nini mnataka kutoka
kwangu?akauliza Mathew na
Efraim akatabasamu
“Tunataka kuzungumza
nawe.”
Mathew akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Niko tayari kwa
mazungumzo lakini tafadhali
naombeni msiiguse familia
yangu”
“Safi sana.Kama uko
tayari kwa mazungumzo
tutaonana baada ya muda
mfupi” akasema Efraim na
kutoka ndani yakile chumba
“Kwa ajili ya Peniela na
watoto wangu niko tayari
kufanya kitu chochote ili
kuwa nao tena.Hawa jamaa
wanaweza kweli
wakawafanyia kitu kibaya ili
kunilazimisha niwaeleze kile
wanachokitaka.Simlaumu
Peniela kwa kuingia katika
mahusiano na mwanaume
mwingine kwani imepita
miaka mitatu bila kuniona
na anaamini tayari
nimekwisha fariki hivyo
ameamua maisha
yaendelee.Wa kulaumiwa
hapa ni mimi mwenyewe
ambaye kila ninaposema
sitaki tena kazi hizi lakini
ninajikuta nikizifanya bila
kutarajia.Ni mimi ndiye
ninayeiweka familia yangu
njia panda hivi sasa kama
ningeamua kukaa mbali na
hizi kazi haya yote
yasingetokea.Nimekuwa
mtiifu na muaminifu mno
kwa nchi yangu lakini hapa
nilipofika ni mwisho.Ni
muda wa kupambana kwa
ajili ya familia yangu”
akawaza Mathew
“Kuna nyakati najutia
kwa nini nilifahamaiana na
Olivia Themba kwani ni yeye
aliyenifanya nikaingia katika
sakata lile na mwisho wangu
umekuwa hapa.Lakini
sipaswi kujilaumu sana
kwani nilipambana na
kuhakikisha nimemuokoa
Olivia,mtoto wa Rais na wale
wasichana waliokuwa
wametekwa na
magaidi.Katika mapambano
yale ndipo tulibaini kuwa
kuna mtandao mkubwa wa
IS nchini kwetu.Yawezekana
wote sasa hivi wamekwisha
nisahau wakiamini
nimefariki dunia.Kama mke
wangu amekwisha nisahau
hakuna atakayenikumbuka
tena hivi sasa.Hakuna
atakayejaribu hata
kunitafuta.Sina msaada
mwingine kwa hivi sasa
kutoka kwa watu wangu
msaada pekee ni kumuomba
Mungu anionyeshe njia ya
kuweza kutoka hapa
nilipokwama” akaendelea
kuwaza Mathew na mlango
wa chumba alimokuwemo
ukafunguliwa wakaingia
watu watano.Akafunguliwa
mikono na kufungwa pingu
halafu akafunguliwa miguu
na kufungwa pingu yenye
mnyororo mrefu halafu
akavalishwa mfuko mweusi
na kutolewa ndani ya kile
chumba akapelekwa katika
chumba Fulani akakalishwa
katika kiti halafu akavuliwa
ule mfuko kichwani
akajikuta akiwa kati kati ya
chumba huku akitazamana
na watu kumi na tano
waliokuwa katika meza tatu
zilizokuwa mbele ya kile
chumba.Efraim Dagan
alikuwa kati kati yao
akasema
“Mathew Mulumbi
karibu sana.Mbele yako ni
jopo la viongozi na wakuu wa
idara mbali mbali ndani ya
Mossad” akasema Efraim
“Ndugu wajumbe wa
kikao hiki mbele yenu ni
Mathew Mulumbi ambaye
alifanya kazi katika idara ya
ujasusi ya Tanzania,yuko
hapa mbele yetu kwa ajili ya
kujibu maswali kadhaa
ambayo ataulizwa” Efraim
akawaeleza wale watu
alikuwa nao ndani ya kile
chumba halafu akamgeukia
Mathew
“Mathew Mulumbi muda
mfupi uliopita ulinieleza
kwamba uko tayari
kuzungumza
nasi.Tumefurahi kwa uamuzi
wako huo kwani ni miaka
mitatu imepita sasa na
jitihada mbali mbali za
kuipata sauti yako
zilishindikana.Kwa kuanzia
tungependa ulithibitishie
jopo hili lililoko mbele yako
kwamba wewe ndiye
uliyevamia ubalozi wa Israel
jijini Nairobi na kuua watu
wetu akiwemo mkuu wa
Mossad Afrika Mashariki Avi
Abramson kisha kumteka
Edger Kaka aliyekuwa
anahifadhiwa ubalozini
hapo”
Mathew Mulumbi
akageuza shingo akafanya
ishara kuwa anataka maji ya
kunywa.Haraka haraka
chupa ya maji ikaletwa na
kuwekwa mezani.Hakutaka
kutumia glasi akachukua
chupa ile akaigugumia yote
ikamalizika.Akawaangalia
wajumbe wale halafu
akasema
“Naitwa Mathew
Mulumbi ni
mtanzania.Nimewahi
kufanya kazi katika udara ya
ujasusi ya Tanzania”
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Miaka mitatu iliyopita
nilivamia ubalozi wa Israel
jijini Nairobi na katika
operesheni ile watu kadhaa
waliuawa akiwamo Avi
Abramson aliyekuwa mkuu
wa Mossad kwa ukanda wa
Afrika mashariki.”
Akanyamaza kidogo baada
ya minong’ono kusikika
“Miaka mitatu kabla ya
tukio lile kutokea” akasema
na watu wote wakanyamaza
“Kikosi maalum cha
majasusi wa Mossad
waliingia nchini Tanzania
wakafanya operesheni ya
kimya kimya wakaua na
kumteka Edger Kaka na
kwenda kumficha katika
ubalozi wa Israel nchini
Kenya.Nilichokifanya mimi
na wenzangu niliowaongoza
ni kwenda kumkomboa raia
wetu aliyetekwa nyara na
Israel.Nilichokifanya
ulikuwa ni muendelezo wa
kile mlichokianzisha
ninyi.Mnaamini ninyi ni taifa
kubwa lenye nguvu na
mnaweza mkafanya chochote
mnachotaka katika nchi
yoyote ndiyo maana
mkaingia katika ardhi yetu
mkaua na kuchukua mateka
raia wetu.Kama haitoshi
bado mliwatuma majasusi
wengine kuandaa operesheni
nyingine ya kimya kimya
nchini Tanzania ili muweze
kumchukua mateka raia
mwingine lakini majasusi
hao mliowatuma
niliwaua.Niliwaua majasusi
hao ili kuwapa salamu muwe
na heshima.Tanzania ni nchi
huru inayojitawala yenyewe
na hamuwezi kuingia katika
ardhi yake mkafanya kile
mkitakacho.Lile lilikuwa ni
onyo kwamba msithubutu
kukanyaga ardhi ya
Tanzania.” akasema Mathew
ambaye alianza kupandwa
na hasira akawatazama watu
wale mle ndani akaendelea
“Edger Kaka ambaye
mlimteka na kumficha
katika ubalozi wenu Nairobi
ana mahusiano na magaidi
wa kikundi cha IS ambao
wamekuwa wakiendesha
mashambulio katika ardhi
yenu na kwa sasa
wamejitanua zaidi katika
nchi za Afrika.Walijenga
mtandao mkubwa nchini
kwetu wakateka na kuua
watu.Miongoni mwa watu
waliotekwa ni rafiki yangu
Olivia pamoja na mtoto wa
Rais wa wakati huo ambaye
naamini hivi sasa atakuwa
amekwisha maliza muda
wake wa uongozi.IS
waliwateka watu hao
wakishinikiza kuachiwa
huru kwa Edger Kaka
ambaye waliamini
anashikiliwa na serikali ya
Tanzania.Tunao ushahidi wa
kutosha kwamba mliingia
ndani ya ardhi yetu mkaua
na kuteka.Yawezekana
mlifanya hivyo kwa lengo
zuri la kutaka kupata taarifa
za kuhusiana na kikundi cha
IS lakini mlikosea kufanya
jambo hili kimya
kimya.Mlipaswa kuzitaarifu
mamlaka husika nchini
Tanzania juu ya Edger Kaka
na kwa pamoja
mngesaidiana katika
kumdhibiti.Binafsi sijutii
kwa kile nilichokifanya
kwani nilifanya kwa ajili ya
kuirejesha heshima ya nchi
yangu na vile vile
kuwakomboa watu
waliotekwa na sintasita tena
kufanya hivyo kila pale nchi
yangu itakapochezewa na
taifa lolote liwe kubwa au
dogo” akasema Mathew kwa
kujiamini na watu wote mle
ndani walikuwa kimya
wakimsikiliza.
“Katika matukio haya
yote mawili ya ninyi
kumteka Edger na sisi
kuvamia ubalozini kwenu na
kumchukua Edger ,Yote
yamefanyika katika harakati
za kujaribu kupambana na
kikundi cha IS.Adui yetu
hapa sisi na ninyi ni mmoja
ambaye ni IS.Mmenifunga
gerezani kwa miaka mitatu
mkinitesa kila uchao
mkiniadhibu kwa kuvamia
ubalozi wenu huku IS
wakiendelea kushambulia na
kuua watu wenu.Badala ya
kuendelea kunitesa,mimi na
ninyi kwa nini tusikae
pamoja na kuweka mikakati
ya kupamba na adui huyu
mmoja tuliye naye? IS ni
adui wa dunia nzima na si
Israel peke yake hivyo kama
mtakuwa tayari mimi na
ninyi tunaweza kuunganisha
nguvu na kupambana na IS”
akasema Mathew na
minong’ono ikasikika ndani
ya kile chumba.Mathew
akawaacha wajadiliane
halafu baada ya muda
Efraim akasema
“Mathew Mulumbi
umeongea kitu kikubwa sana
na sisi tunakubaliana na
mawazo yako.Tuyaweke
pembeni hayo yote
yaliyotokea na tuufungue
ukurasa mpya sisi na
wewe.Kama ulivyosema sisi
na wewe wote adui yetu ni
mmoja ambaye ni kikundi
cha kigaidi cha
IS.Tulimchukua Edger Kaka
baada ya kubaini kwamba
ana mahusiano na wafadhili
wakuu wa kikundi hicho
ambao ni Habiba Jawad na
Sayid Omar.Kwa miaka
mingi tumekuwa
tukimtafuta Habiba Jawad
na wenzake ambao
wamekuwa wakifadhili
vikundi mbali mbali vya
kigaidi vinavyoendelea
kufanya mauaji katika ardhi
ya Israel.Siku chache
zilizopita yamefanyika
mashambulio ya kigaidi
kutoka kwa IS na kuua watu
zaidi ya thelthini wengi
wakiwa ni watoto na wazee
wasiojiweza.Kumekuwa pia
na mashambulio mengine
madogo madogo ya maroketi
karibu kila siku na watu
wanaendelea kupoteza
maisha.Tunataka kulimaliza
suala hili na kukomesha
mauaji yanaoendelea hapa
nchini.Tunataka kuuondoa
mtandao wote wa kigaidi
unaoendesha mashambulizi
hayo” akasema Efraim na
kunyamaza kidogo
“Kuna mtu mmoja
ambaye tumekuwa
tunamtafuta kwa miaka
mingi bila mafanikio Habiba
Jawad.Tunahisi anafichwa
na serikali ya Saudia ndiyo
maana mpaka leo juhudi zetu
zote za kumsaka zimegonga
mwamba.Tunataka tuungane
sisi na wewe kumsaka na
kumpata Habiba Jawad na
wenzake ambao
wanaendeleza mauaji katika
ardhi ya Israel.IS ni kitisho
si kwa Israel pekee bali ni
hata kwa nchi yenu na dunia
nzima.Tunataka taarifa
ambazo zinaweza kutusaidia
kumpata Habiba Jawad na
wenzake ambao ni wafadhili
wakuu wa kikundi cha IS na
vikundi vingine vya kigaidi”
akasema Efraim na
kunyamaza.Wote
wakayaelekeza macho yao
kwa Mathew.
“Tunaamini unaweza
kuwa na msaada mkubwa
sana katika kutusaidia
kulipiga vita kundi hili
hatari.Habiba Jawad bado
anaendelea kuwa ni mtu
hatari sana kwa dunia kwani
yeye ndiye uti wa mgongo wa
mitandao hii ya
kigaidi.Kama tukifanikiwa
kumuondoa huyu
mwanamama naamini ugaidi
utakoma kama si kupungua
kabisa duniani.Huyu mama
ni tajiri mno na anautumia
utajiri wake katika kufadhili
ugaidi.Kama una chochote
ambacho unadhani kinaweza
kutusaidia kumpata Habiba
tueleze tafadhali na sisi
tutaona namna ya
kukusaidia” akasema
Efraim.Zilipita dakika mbili
Mathew akiwa kimya
akitafakari halafu akasema
“Ninao uwezo wa
kuwasaidia kumpata Habiba
Jawad lakini nataka mimi na
ninyi tuingie makubaliano”
akasema Mathew
“Nini unakihitaji kutoka
kwetu Mathew?akauliza
Efraim
“Nataka kuwa huru”
akasema Mathew na zikapita
sekunde kadhaa za ukimya
halafu Efraim akasema
“Mathew Mulumbi
tunaweza kufikiria ombi lako
endapo taarifa utakazotupa
zinaweza kuwa na msaada
kwetu hivyo kama unazo
taarifa zozote tupe
tuzichambue tuzifanyie kazi
tuone kama zinaweza
kutufaa halafu tutaona
namna ya kukusaidia”
akasema Efraim
“Ngoja niwaambie jambo
ninyi mnaojiita taifa
teule.Hamtafanikiwa katika
vita hii kutokana na viburi
mlivyonavyo kujiona ninyi ni
bora zaidi kuliko
wengine.Hamuonyeshi kama
mna nia ya dhati ya kutaka
kumpata Habiba Jawad na
kukomesha mauaji
yanayoendelea katika ardhi
yenu.Kama mngekuwa na
nia ya dhati ya kumtafuta
Habiba msingejiuliza mara
mbili kuhusu ombi langu la
kutaka kuachiwa huru pale
nitakapowasaidia kumpata
au kumuondoa kabisa
Habiba Jawad na
wenzake.Nawaambia ukweli
kwa sasa Habiba amewabana
kwenye kona na mimi ndiye
pekee ninayeweza kusaidia
kumpata.Ni uamuzi wenu
kama mnataka kumaliza
ugaidi na mauaji katika nchi
yenu kwa kunipa uhuru
wangu au kuendelea
kuniweka hapa na kunitesa
huku mauaji yakiendelea
kila uchao” akasema
Mathew.Efraim akaelekeza
Mathew atolewe nje kwa
dakika kadhaa wakabaki
wao wakijadiliana
“Nimewabana
vizuri.Wana shida na Habiba
Jawad hivyo hawana ujanja
wa kukataa.Lazima
wataniachia huru pale
nitakapokuwa nimefanikisha
kazi yao.Hata mimi
ninamtafuta sana Habiba
Jawad.Huyu kama bado yuko
hai ataendelea kufadhili
makundi mbalimbali ya
magaidi na nina uhakika
mkubwa lazima watarejea
tena Tanzania na
kutengeneza mtandao
wao.Hii ni nafasi nimeipata
ya kuweza kummaliza na
kumaliza kabisa nguvu ya
kikundi cha IS” akawaza
Mathew na mlinzi aliyekuwa
akimlinda akapewa
maelekezo ya kumrejesha
Mathew ndani.
“Mathew tumefanya
majadiliano mafupi
tukiwashirikisha pia viongozi
wetu wa ngazi za juu na
wamekubali ombi lako lakini
endapo utatupa taarifa
zitakazosaidia kumpata
Habiba Jawad.”
“Ninataka uthibitisho wa
barua iliyosainiwa na waziri
mkuu kwa sababu naweza
kuwapa taarifa za
kuwasaidia halafu mkaniua
au kunirejesha gerezani”
akasema Mathew
“Mathew nasikitika
kwamba hicho unachokitaka
hakitawezekana”
“Basi hamna nia ya dhati
ya kuniachia huru mlikuwa
mnanidanganya.Naombeni
mnirejeshe gerezani
nikaendelee kuteseka”
akasema Mathew
“Mathew unaitupa nafasi
pekee ambayo inaweza
kukusaidia.Hakutakuwa na
nafasi nyingine kama hii
uliyoipata”
“Sihitaji nafasi
nyingine.Naombeni
mnirejeshe kule gerezani
mnakonifunga kwenye giza
nikaendelee na maisha ya
kule” akasema Mathew na
kuufumba mdomo wake.Kila
alichoulizwa hakujibu.Efraim
akaelekeza Mathew
arejeshwe katika kile
chumba kizuri.
“Hawana ujanja lazima
watarudi kwangu.Kwa sasa
mimi ndiye tegemeo lao
katika kumpata Habiba
Jawad” akawaza Mathew
wakati akirejeshwa katika
chumba kile kizuri
“Hawanirejeshi tena kule
katika gereza kule
walikonifunga kwa miaka
mitatu hii ni ishara kwamba
wananihitaji.Ninauona
mwanga wa mimi kuondoka
hapa japo njia nitakayopita
inaonekana itakuwa na
mawe na miiba mingi lakini
mwisho wa siku nitafanikiwa
kuondoka hapa na kurudi
nyumbani” akawaza na
kujilaza katika kitanda kile
kikubwa
“Katika maisha yangu
ndani ya kazi hii ya ujasusi
sijwahi kukutana na wakati
mgumu kama huu.Nimepitia
mateso ambayo sijawahi
kupitia lakini nimevumilia
na sikuwahi kuwasaliti
wenzangu nilioshirikiana nao
katika operesheni
ile.Kinachonishangaza
Mossad wanazo taarifa zote
kuhusiana na kila
nilichokifanya.Lazima yupo
mtu ambaye aliwapa taarifa
hizi.Bado akili yangu
inanituma lazima atakuwa ni
mtu wangu wa karibu na
bado jina la Devotha linakuja
kichwani kwangu kila
ninapowaza kuhusu usaliti
huu mkubwa
niliofanyiwa.Kama kweli ni
yeye atakuwa amefanya
jambo baya sana kwani
jambo nililolifanya ni kwa
manufaa ya taifa.Halafu Rais
Dr Evans licha ya kuyaweka
maisha yangu hatarini
kumuokoa mwanae kwa nini
hakufanya juhudi zozote
kunitafuta na kujua mahala
nilipo?Na yeye anaamini
nimefariki dunia?Vipi
kuhusu watu wangu Gosu
Gosu na Austin?Wako
wapi?Nao wanaamini
nimefariki? Dah ! niko
mwenyewe.Sina msaada
wowote.Msaada pekee ni
Mungu wangu ambaye siachi
kumuomba kila siku
aniangazie njia niweze
kutoka katika mateso
haya.Endapo nikifanikiwa
kutoka hapa salama nataka
nitulie na familia yangu.
Peniela tayari ana
mahusiano na mtu mwingine
akiamini tayari nimekufa.I’ll
be back my love.Kwa sababu
yako nitafanya kila
ninaloweza ili kutoka hapa”
akaendelea kuwaza na
kutokana na uchovu
aliokuwa nao taratibu
akaanza kusinzia
Mathew alistuliwa
kutoka katika usingizi mzito
na mtu aliyekuwa akimtikisa
akafumbua macho na
kujikuta akitazamana na
watu saba.
“Mathew Mulumbi amka
tafadhali” akasema Efraim
“Mnanirejesha
gerezani?akauliza Mathew
“Hapana hatukurejeshi
gerezani” akasema Efraim na
kumtaka Mathew waketi
sofani.Akaufungua mkoba
wake na kutoa karatasi
akampa Mathew aisome
“Hiki nini?akauliza
Mathew
“Hiyo ni hati ya
makubaliano iliyosainiwa na
waziri mkuu wa
Israel.Tutakuachia huru pale
utakapotupa taarifa
kuhusiana na Habiba Jawad”
akasema Efraim.Mathew
akaipitia hati ile kwa makini
na kutabasamu
“Mathew hakuna
kupoteza muda tuanze sasa
hivi.Tunahitaji kuzipata
taarifa hizo haraka” akasema
Efraim
“Yuko wapi Edger
kaka?akauliza Mathew
“Wa nini Edger Kaka?
Akauliza Efraim
“Ninahitaji kuzungumza
naye.Hafahamu mahala alipo
Habiba lakini anaweza
akatusaidia kutupa
mawasiliano yake na tukajua
mahala alipo Habiba”
“Kuna tatizo lilitokea
wakati wa kumchukua Edger
Kaka kule Nairobi.Kwa
bahati mbaya usiku ule
Edger alianguka katika jiwe
na kugongesha kichwa
akapoteza fahamu na mpaka
leo hii hajaamka.Kwa mujibu
wa daktari ni kwamba
ubongo wake umekufa na
hataweza kuamka
tena.Kinachomfanya
aonekane kuwa hai mpaka
leo hii ni mashine lakini
kiuhalisia Edger amekwisha
fariki dunia hivyo tupe
taarifa nyingine ambazo
hazitamuhitaji Edger”
akasema Efraim na Mathew
akazama mawazoni kwa
muda kisha akasema
“Sasa naombeni
mnisikilize.Nilitegemea
kupata taarifa kutoka kwa
Edger lakini kwa kuwa
hayupo tena tutafanya vile
nitakavyoelekeza mimi”
akasema Mathew
“Mathew haikuwa rahisi
kuweza kupata sahihi ya
waziri mkuu katika suala hili
hivyo tunachokihitaji ni
taarifa na si vinginevyo”
akasema Efraim
“Mnalo gereza ambalo
mnawahifadhi watu
wanaohusika na makosa ya
ugaidi hapa Israel”
“Ndiyo.Kituo 1391 ndilo
gereza la siri ambako wote
wanaohusika na mitandao ya
kigaidi au mauaji ndani ya
Israel hufungwa” akajibu
Efraim
“Vizuri.Nataka
nipelekwe huko na niwekwe
chumba kimoja na mmoja
kati ya magaidi hatari kabisa
mnaowashikilia katika
gereza hilo kutoka katika
moja ya kikundi cha
wanamgambo wanaoendesha
mapambano dhidi ya Israel”
akasema Mathew na
kumstua Efraim
“Hizo si taarifa
tunazozitafuta” akasema
Efraim
“Nisikilize tafadhali.Huu
ni mpango ambao
utanifikisha kwa Habiba
Jawad.Kwa sasa sina taarifa
zozote kuhusu mahala alipo
kwani nilimtegemea Edger
Kaka lakini kwa kupitia
mpango huu ninaokueleza
ninaamini nitafahamu alipo
au kumfikia Habiba
Jawad.Nitalazimika
kuungana na kufanya kazi
na magaidi ili waweze
kujenga imani kwangu na
wakati huo nikiendelea
kuusoma mtandao wao na
kufahamu alipo Habiba
Jawad”
“Hapana Mathew huu ni
mpango wa hatari sana
ambao siwezi kuruhusu
ukaufanya.Wakifahamu
wewe si mwenzao lazima
watakuua na tutakua
tumerudi nyuma sana”
akasema Efraim
“Nalifahamu hilo Efraim
lakini hakuna njia nyingine
ya kuweza kumpata Habiba
Jawad zaidi ya hii
ninayokueleza.Niwekeni
chumba kimoja na huyo gaidi
nitajenga urafiki naye na
kumfanya aniamini halafu
tutafanya mpango wa
kutoroka hapo gerezani na
huo utakuwa ni mwanzo wa
mimi kushirikiana na
magaidi hao na itakuwa ni
njia ya kuelekea kwa Habiba
Jawad”
“Mathew siwezi kutoa
jibu lolote kuhusiana na
mpango huu kwa
sasa.Nitahitaji kuzungumza
na viongozi wangu wakuu
juu ya mpango huu na wao
watatoa maelekezo” akasema
Efraim na kuondoka
“Nimeamua kufanya
jambo la hatari sana lakini
ndiyo njia pekee ya kuweza
kumfikia au kufahamu
mahala alipo Habiba Jawad
na wale wote wanaofadhili
ugaidi.Kama serikali ya
Saudi wanachangia kumficha
basi njia pekee ya kumfikia
ni kujiunga na magaidi.Ni
maamuzi magumu sana haya
lakini lazima niyafanye ili
niweze kuwa huru.Hakuna
namna nitakavyoweza
kutoka katika mikono ya
Mossad kama sintatumia
njia hii.Pili nahitaji sana
kummaliza Habiba Jawad
ambaye ufadhili wake
unalifanya kundi la kigaidi la
IS kujitanua na kusambaa
sehemu mbali mbali
duniani.Tukifanikiwa
kumuondoa huyu tutakuwa
tumefanikiwa kuupunguza
nguvu ugaidi.Shughuli za
kigaidi zitakosa nguvu baada
ya kukosa fedha” akawaza
Mathew
“Hatari ya mpango huu
kwanza haitakuwa rahisi
kwao kuniamini lazima
nitapitia wakati mgumu sana
hadi waniamini na pili ni
pale watakaponigundua
kwamba ni pandikizi
ninawachunguza.Adhabu
yake ni kifo.Pamoja na hatari
hiyo iliyopo lakini lazima
nitumie njia hii ya kujiunga
na magaidi.Mungu
atasimama nami” akaendelea
kuwaza na haukupita muda
akalala.
PARIS – UFARANSA
“Nimehakikishiwa na
serikali ya Tanzania kwamba
wale wote waliofanya mauaji
haya hakuna atakayebaki
salama.Waliuawa watu
watano siku ya tukio na
wengine bado wanaendelea
kusakwa.Tumeumizwa na
msiba huu mkubwa lakini
ninawaomba tuwe na subira
wakati vyombo vyetu
vikiendelea kulifanyia kazi
suala hili na
ninawahakikishia kwamba
wale wote waliofanya mauaji
haya watapatikana.
Sipati maneno mazuri ya
kumuelezea Lucy Muganza
lakini alikuwa ni mwanamke
shupavu na jasiri mwenye
maono makubwa na zaidi
sana aliyeipenda mno nchi
yake ya Congo”
Haya ni baadhi ya
maneno yaliyokuwamo
katika hotuba ya Rais
Patrice Eyenga wa jamhuri
ya kidemokrasia ya Congo
aliyoitoa katika hotuba yake
wakati wa mazishi ya Lucy
na mumewe Laurent
Muganza waliouawa nchini
Tanzania.Maelfu na maelfu
ya wananchi wa Congo na
wafuasi wa chama cha CDP
walihudhuria mazishi hayo.
Wakati mazishi ya Lucy
na mumewe Laurent
Muganza yakifanyika nchini
Congo,binti yao Theresia
ambaye alinusurika katika
shambulio lile alikuwa nchini
Ufaransa katika hospitali
moja kubwa alikohamishiwa
baada ya kutolewa Tanzania.
Tayari alikwisha fahamu
kuwa wazazi wake walifariki
dunia lakini hakuruhusiwa
kuhudhuria au kutazama
mazishi hayo kutokana na
afya yake kuwa dhaifu.
Katika chumba cha
mikutano ndani ya makazi
ya Rais wa Ufaransa,Rais
Michael Weren alikuwa
katika kikao na jopo la
madaktari kumi na mbili
mabingwa wa upasuaji
wakiongozwa na Dr Alex
McKnees bingwa wa upasuaji
wa plastiki kutoka New York
Marekani.Kilichowakutanish
a hapa ni kujadiliana kuhusu
upasuaji mkubwa
wanaotarajia kuufanya
“Ahsanteni sana kwa
kufika natumai timu nzima
ninayoihitaji kwa ajili ya
kazi yangu
imetimia.Kikubwa
nilichowaitia hapa kuna
upasuaji mkubwa ambao
ninataka muufanye.Kuna
binti ambaye nataka
afanyiwe upasuaji na
kubadili kabisa muonekano
wake” akasema Rais Weren
na kuwasha runinga kubwa
iliyokuwa nyuma yake na
picha za Theresia Muganza
zikaanza kuonekana
“Anaitwa Theresia
Muganza.Ni msomi wa chuo
kikuu.Huyu ni mtoto wa
mabilionea Lucy na Laurent
Muganza ambao waliuawa
nchini Tanzania katika
shambulio siku chache
zilizopita na leo hii
wanazikwa nchini
Congo.Tunaamini watu
waliowaua wazazi wake
wataendelea kumsaka hadi
wahakikishe wamempata na
kumuua kwani lengo lao
lilikuwa ni kuwaua familia
nzima.Ili kumlinda na hatari
hiyo nataka afanyiwe
upasuaji wa kubadili
mwonekano wake.Ninyi ni
mabingwa wa upasuaji huo
mnajua nini cha kufanya
lakini ninachohitaji mimi
baada ya bandeji kuondolewa
mwilini mwake Theresia
anatakiwa awe ni mtu
mpya.Nataka mumtengeneze
awe na uzuri wa kipekee.Awe
ni mwanamke ambaye
ataitikisa dunia kwa uzuri
atakaokuwa nao.Sitaki
kuwafundisha kazi yenu
kwani mnajua kila kitu
lakini kwa ujumla nataka
mnitengenezee malaika
ambaye kila apitapo mtaani
watu wageuze shingo zao
kumtazama.Naamini
mmenielewa” akasema Rais
Weren wakaendelea na
majadiliano na madaktari
wale kisha wakaomba siku
mbili wakalijadili suala lile
na namna watakavyofanya
upasuaji ule mkubwa.
TEL AVIV – ISRAEL
Mathew Mulumbi
alishinda ndani ya chumba
alichohamishiwa akiwa chini
ya ulinzi mkali
sana.Hakuruhusiwa kutoka
au hata kufungua pazia
kuchungulia nje.Muda wote
ndani ya chumba kulikuwa
na walinzi wenye silaha na
alikuwa amefungwa mkono
mmoja kwa pingu
iliyounganishwa na
mnyororo mrefu na
kufungwa katika chuma
kizito.
Saa kumi na moja za
jioni waliingia watu wanne
ndani ya kile chumba
wakamfungua Mathew pingu
na kumvisha mfuko mweusi
kichwani wakamtoa ndani ya
kile chumba wakamuingiza
ndani ya gari na
kuondoka.Mathew hakujua
anapelekwa wapi.Baada ya
dakika ishirini gari lile
likasimama mlango
ukafunguliwa Mathew
akashushwa na kuingizwa
katika lifti baada ya muda
mfupi mlango ukafunguka
wakatoka ndani ya lifti
wakatembea kidogo
wakasimama kwa sekunde
chache mlango ukafunguliwa
wakaingia ndani ya
chumba.Mathew hakuweza
kuona kilichokuwa
kinaendelea.Alikalishwa
katika kiti akafunguliwa
pingu za mikono na mfuko
uliokuwa kichwani
ukatolewa.Alijikuta katika
ofisi nzuri na mbele yake
kulikuwa na watu
watano.Mtu aliyweza
kumtambua katika wale
watano ni Efraim Dagan
ambaye walionana usiku
uliopita.
“Mathew Mulumbi
karibu.Tumekutana tena
mimi na wewe lakini naomba
nikutambulishe wenzangu
ambao niko nao hapa”
akasema Efraim na
kuwatambulisha watu wale
walikuwemo mle ndani na
wa mwisho kutambulishwa
alikuwa ni Moshe Levine
mkurugenzi wa Mossad.
“Kufuatia mazungumzo
yetu ya jana” akaendelea
Efraim
“Tumekuwa na
mazungumzo marefu sana
mimi na wenzangu tangu
asubuhi kujadili wazo
lako.Tumemaliza
majadiliano muda mfupi
uliopita tumeona tukuite
hapa tuje kuzungumza nawe”
akasema Efraim
“Mathew Mulumbi”
akasema Moshe mkurugenzi
wa Mossad
“Efraim alifikisha
kwangu wazo lako jana usiku
na tukalazimika kukutana
kulijadili.Ninataka kujua
kwa nini unataka kufanya
hivi ulivyoshauri kujiunga na
magaidi?akauliza Moshe
“Mkurugenzi kama
nilivyomwambia Efraim
kwamba sisi sote adui yetu ni
mmoja ambaye ni IS.Mambo
yote yaliyotokea na
kupelekea mimi kuwa hapa
ni kwa sababu ya
mapambano dhidi ya
IS.Kikundi hiki ni tishio si
kwa Israel pekee bali hata
nchini kwangu tayari
tumeonja athari za ugaidi
hivyo ninataka kusaidiana
nanyi kulimaliza kundi hili
hatari kama si kulimaliza
nguvu kwa kumuondoa
Habiba Jawad.Nilitegemea
kumtumia Edger Kaka lakini
baada ya kutaarifiwa
kwamba Edger hataweza
kuamka tena ndipo
nilipoamua kutumia mbinu
hii ya kujiunga na
magaidi”akasema Mathew
“Mathew Mulumbi mbinu
hii ni hatari na inaweza
ikakuletea matatizo
makubwa” akasema Moshe
“Nalifahamu hilo
mkurugenzi lakini hatuna
namna nyingine kwa sasa ya
kumfikia Habiba Jawad bali
kwa mbinu hii.Alinieleza
Efraim kwamba mmemtafuta
Habiba kwa miaka mingi bila
mafanikio na kuna hisia
kwamba anafichwa na
serikali ya Saudia hivyo basi
kumpata mtu kama huyu ni
vigumu sana.Ninafahamu
haitakuwa rahisi kuwafanya
magaidi hao waniamini
nitapitia nyakati ngumu
sana lakini nina uhakika
mkubwa kwamba nitafaulu
kujenga imani kwao na
nitafanikiwa kujua mahala
alipo Habiba Jawad.Ikitokea
nikagundulika na kuuawa
nitakuwa nimekufa
nikijaribu lakini nakuahidi
kufanya kila lililo ndani ya
uwezo wangu kuhakikisha
ninakamilisha misheni
yangu” akasema Mathew
“Mathew ninafurahishwa
sana na ujasiri
wako.Unachotaka kukifanya
ni kitu cha hatari mno
ambacho sintaweza
kumruhusu mtu wangu
akakifanya kwani ni
kuhatarisha uhai”
“Mimi si mmoja wa watu
wako hivyo hata ikitokea
nikapoteza maisha hakuna
hasara yoyote
mtakayoipata”akasisitiza
Mathew
“Kwa nini unasisitiza
sana kutaka kutumia mbinu
hii ya kujiunga na
magaidi?akauliza Moshe
“Wakati nikipambana
kuokoa watu aliokuwa
wametekwa na kundi la IS
wakishinikiza kuachiwa kwa
Edger Kaka,niligundua
kwamba tayari walikuwa na
mtandao mkubwa na
walikwisha otesha mizizi
hadi katika ngazi za juu za
uongozi wa nchi yetu kwani
aliyekuwa waziri mkuu wa
wakati ule alikuwa ni mmoja
wa waliokuwa katika
mtandano wao na walikuwa
wanamuandaa aje kuwa
rais.Karibu nusu ya mtandao
mkubwa wa IS uliokuwa
nchini Tanzania tulifanikiwa
kuutambua na kuwakamata
wahusika lakini
sikufanikiwa kufika mwisho
wa sakata lile na kujua
hitimisho lake lakini hatua
kubwa ilikuwa
imepigwa.Mafanikio yale
yalikuwa ya muda tu ili
kulimaliza kabisa tatizo la
ugaidi ni kuukata kabisa
mzizi ambao ni Habiba
Jawad na wenzake
wanaotumia utajiri wao
kufadhili ugaidi.Ninasisitiza
kutaka kutumia mbinu hii ya
hatari kwani kama
tukifanikiwa kumuondoa
Habiba Jawad na wenzake
wafadhili wakuu wa ugaidi
tutakuwa tumesaidia si
Israel pekee bali hata nchi za
Afrika ambako magaidi
wameanza kuotesha mizizi
yao.Jambo lingine ambali
linanilazimu kutaka kutumia
mbinu hii ya kujiunga na
magaidi ninataka kwenda
nyumbani kama nikifanikiwa
kumaliza salama” akasema
Mathew
“Mathew kama
alivyokueleza Efraim
kwamba tunamuhitaji sana
Habiba Jawad.Kwa muda
mrefu tumekuwa tukimsaka
bila mafanikio.Tunaamini
tukifanikiwa kumpata au
kumuua Habiba basi kundi
la IS na vikundi vingine
vinavyofanya mashambulio
ya maroketi na kujitoa
mhanga vitaishiwa nguvu na
kufa kabisa.Kwa hiyo basi
sisi tunataka kushirikiana
nawe kwa kutumia njia hiyo
uliyoipendekeza lakini huu
utakuwa ni mpango wa siri
sana kwani tunaamini hata
hapa Israel Habiba anao
watu wake wanaomsaidia
kwani aliwahi kuingia hapa
Israel bila
kujulikana.Tunataka
tukulinde ili usiweze
kugundulika ndiyo maana
ninasema kwamba
operesheni hiyo
utakayoifanya iwe ya kimya
kimya na tutakaofahamu ni
sisi watu wachache
pekee.Usishangae kusikia
kwamba hata ndani ya
Mossad wapo watu ambao
wanashirikiana na Habiba
Jawad” akasema Moshe na
kumuachia Efraim aendelee
“Tutakuwekea mwilini
kifaa maalum ambacho
kitatuwezesha sisi
kukufuatilia kila mahala
utakapokuwa na kufahamu
kama uko mzima.Kila
mahala utakapokuwa
unakwenda kutakuwa na
kikosi cha majasusi
wakikufuata kwa kutumia
kifaa hicho utakachowekewa
mwilini.Tutakupa kifa
kingine kidogo cha
mawasiliano kitakacho……”
“Hakuna haja” akasema
Mathew na kumkatisha
Efraim
“Hawa jamaa ni watu
waliojipanga
vizuri.Wanazifahamu mbinu
zote za ujasusi.Naamini
watanichunguza na
wakinikuta na kifaa chochote
ambacho kitaniunganisha
mimi na ninyi nitakuwa
nimenunua kifo
change,wataniua.Sihitaji
kwenda nikiwa na kifaa
chochote” akasema Mathew
“Mathew lazima
tufuatilie kila utakachokuwa
unakifanya huko mahala
utakapokuwa
unakwenda.Tunapaswa
kuwa na mawasiliano kati
yetu na wewe.Ni sisi
tunaopaswa kukulinda na
kuhakikisha unakuwa
salama.Hivyo basi lazima
uwe na kifaa ambacho
kitatuwezesha sisi
kukufuatilia” akasema
Moshe
“Sihitaji kifaa
chochote”akasisitiza Mathew
“Tutawasiliana vipi nawe
bila kuwa na kifaa cha
mawasiliano?akauliza Moshe
“Naombeni
mniamini.Ninajua
ninachokwenda
kukifanya.Nitajua namna ya
kuwasiliana nanyi nikiwa
huko.Ninachokitaka kutoka
kwenu ni kuniunganisha na
magaidi halafu
kitakachoendelea huko
nitajua mimi lakini
nawahakikishia kwamba
nitatafuta kila namna ya
kuweza kuwasiliana nanyi
na kuwajulisha kila hatua
nitakayokuwa
ninapiga”akasema Mathew
“Mathew Mulumbi
natamani niseme hapana
lakini kwa vile umesisitiza
basi tutafanya unavyotaka
ingawa matumaini kama
utaweza kumfikia Habiba
Jawad au kufahamu mahali
alipo ni madogo sana.Hata
hivyo ninatoa ruhusa kwa
mpango huu uendelee”
akasema Moshe na Efraim
akasimama akasogea mbele
kulikokuwa na runinga
akaiwasha na katika runinga
akaonekana mtu mmoja
mwenye macho ya kikatili
“Huyu anaitwa Ammar
Al Nazari.Huyu ni kiongozi
wa kikundi kimoja cha
wanamgambo kinachoitwa
Ammar Nazari Brigades
kinachoendesha mapambano
dhidi ya Israel na chenye
mahusiano ya karibu na
IS.Habiba Jawad ni mfadhili
wa kikundi hiki pia.Ammar
Nazari brigades wanahusika
katika kufanya
mashambulizi kadhaa nchini
Israel yaliyoua watu
wengi.Mpaka sasa idadi ya
watu wanaotajwa kuuawa na
mashambulio ya kikundi hiki
inakaribia mia moja ishirini
na nane.Tunataka ujenge
mahusiano na huyu mtu na
kupitia huyu utaweza kupata
taarifa zote kuhusiana na
Habiba Jawad” akasema
Efraim na Mathew
akayaelekeza macho yake
runingani akimtazama Yule
jamaa Ammar Nazari
mwenye macho yaliyojaa
ukatili.
“Ili mpango wetu
ukamilike lazima Ammar
atoke gerezani na utokaji
wenyewe unapaswa kuwa wa
kutumia nguvu yaani
kutoroka” akasema Mathew
“Ammar ni mtu ambaye
tulifanya kazi kubwa
kumtafuta hadi
kumpata.Toka alipokamatwa
kundi lake limefifia na
kukosa nguvu japo bado
wanaendelea na
mashambulizi ila kwa kiasi
kidogo tofauti na wakati ule
kabla
hatujamkamata.Kumuachia
mtu kama huyu ni jambo
linaloumiza sana” akasema
Moshe
“Hakuna ujanja
mkurugenzi lazima mtu
huyu aachiwe kwani kutoka
kwake kutakuwa na faida
kubwa zaidi kuliko
kuendelea kukaa ndani”
akasema Mathew
“Unadhani itachukua
muda gani kwa wewe
kujenga mahusiano na
Ammar?akauliza Efraim
“Simjui mtu
huyu,sijawahi kukutana
naye lakini naamini ndani ya
siku nne au tano nitaweza
kujenga mahusiano
naye.Mpango utakuwa hivi
nitapigwa hadi nipoteze
fahamu kisha nitapelekwa
katika chumba alimo Ammar
na kutupiwa humo.Akiniona
na majeraha niliyonayo
atatamani kujua mimi ni
nani.Nitagoma kuzungumza
naye na nitagoma kula kwa
siku mbili na hali hiyo
lazima itamtisha na ataamua
kutoa taarifa kwa askari wa
gereza nitatolewa ndani ya
kile chumba na kwenda
kutibiwa halafu baadae
nitarejeshwa tena na safari
hii nitakuwa na kisu
kidogo.Naamini huo utakuwa
ni mwanzo wangu mimi na
yeye kuwa marafiki”
akasema Mathew
“Mipango yako Mathew
Mulumbi inaonekana ni
mizuri lakini ya hatari
kubwa sana.Ni vipi kama
Ammar hatanasa katika
mtego wako?akauliza Moshe
“Niamini mkurugenzi
nina uhakika mkubwa
lazima
atanasa.Ninawafahamu
magaidi” akasema Mathew
“Wakati unaendelea
kujenga urafiki na Ammar
sisi tutakuwa tunaandaa
mpango wa wewe kutoroka
na pale utakapotolewa
chumbani kupeleka katika
hospitali ya gereza utaelezwa
kila kitu namna mpango huo
utakavyokuwa.Kitu cha
msingi jitahidi sana
kuhakikisha anakuwa karibu
yako” akasema Efraim
“Nina uhakika
nitafanikiwa.Ninachowasisiti
za katika mpango huo
mtakaouandaa wa kutoroka
hakikisheni uwe ni mpango
unaoonekana kweli
tumetoroka.Ikiwezekana
katika mpango huo Ammar
apigwe risasi sehemu kama
vile kwenye mguu au
mkononi ili aone mpango huo
wa kutoroka ni wa kweli.Vile
vile nitaomba Edger Kaka
asiondolewe katika mashine
zinazomuweka hai kwani
nitamtumia pia katika
kutafuta njia ya kufika kwa
Habiba Jawad”
“Edger Kaka hana
msaada wowote kama
nilivyokueleza.Amekwisha
fariki na kinachomuweka hai
mpaka sasa ni
mashine”akasema Efraim
“Ninalifahamu hilo lakini
ninashauri msiondoe
mashine hizo kwa sasa
yawezekana tukamtumia
pia.Inaweza ikawa ni njia
moja wapo ya kuniweka
karibu zaidi na Habiba
Jawad pale nitakapofanikiwa
kuonana naye” akasema
Mathew na majadiliano
yakaendelea kuhusiana na
mpango ule.
“Mathew tumekuwa na
majadiliano mazuri kuhusu
mpango huu hivyo
kinachofuata sasa ni
utekelezaji.Ninachosisitiza ni
usiri wa mpango
huu.Mtandao wa Habiba ni
mkubwa na nina uhakika
hata ndani ya Mossad anao
watu wake hivyo usiri
unatakiwa sana katika
mpango huu.Mimi na
wenzangu hawa tutaendelea
kufuatilia kwa karibu zaidi
mpango huu lakini hakikisha
siku zote unajitahidi kuwa
salama na kujitahidi kwa
kila namna kufanya
mawasiliano nasi ili tujue
mahala ulipo na kama
utahitaji msaada
wowote.Kumbuka operesheni
hii ni muhimu si kwa Israel
pekee bali hata kwa nchi
yako na dunia kwa
ujumla.Endapo ukiifanikisha
vyema makubaliano yetu
yanabaki vile vile utakuwa
huru lakini usijaribu
kufanya kitu chochote cha
kijinga cha kutaka kutoroka
kwani hautafika mbali kabla
hatujakutia
mikononi.Ninakutakia kila la
heri”akasema Moshe
“Usiwe na hofu kuhusu
mimi kwamba ninaweza
kutoroka.Nimeamua kwa
hiyari yangu kufanya jambo
hili na ninafahamu manufaa
yake ni makubwa kwenu na
kwetu pia” akasema Mathew
na kisha akaongozana na
Efraim kutoka ndani ya ile
ofisi.
PARIS – UFARANSA
Hali ya Theresa muganza
iliendelea vizuri.Ulinzi
ulikuwa mkali sana katika
wodi alimolazwa.
Saa tatu za usiku akiwa
amelala kitandani huku
pembeni yake akiwepo
muuguzi mlango
ukafunguliwa wakaingia
watu wanne na nyuma yao
akatokea mtu ambaye
Theresa alizoea kumuona
katika runinga na taarifa
mbali mbali za habari za
kimataifa,Rais wa Ufaransa
Michael Weren akiwa
ameongozana na
madaktari.Daktari akatoa
maelezo kuhusu maendeleo
mazuri ya mgonjwa na Rais
Weren akawataka watu wote
mle ndani watoke akabaki na
Theresa.Akavuta kiti
akamsogelea Theresa
kitandani ambaye aliinuka
na kukaa.
“Theresa pole sana”
akasema Weren
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais” akajibu
Theresa na Rais Weren
akatabasamu
“Kumbe unanifahamu
mimi ni nani”
“Hakuna asiyekufahamu
wewe ni nani mheshimiwa
Rais” akajibu Theresa
“Vipi unajisikiaje?
“Hali yangu inaendelea
vizuri.Nashukuru sana kwa
kunileta huku na kuokoa
maisha yangu.Ninapata
huduma nzuri sana na sasa
sijambo.Ninapata nafuu
kubwa kila
uchao.Ninakushukuru sana
wewe binafsi mheshimiwa
Rais kwa jitihada zako
kuhakikisha ninahamishiwa
huku na kupatiwa huduma
nzuri.Sina hakika kama
ningeendelea kubaki kule
Afrika kama ningekuwa
ninazungumza nawe muda
huu” akasema Theresa na
kuanza kumwaga
machozi.Rais Weren akatoa
kitambaa na kumpatia afute
machozi
“Pole sana Theresa.Tukio
lile ni baya na la kinyama
sana lakini nakuomba uwe
na ujasiri.Huu si wakati wa
kuendelea kumwaga
machozi.Wazazi wako
wamekufa kishujaa na watu
mashujaa hatuwaenzi kwa
kulia bali kwa kuendelea
yale waliyoyapigania.Mama
yako alikuwa mstari wa
mbele kupigania usawa na
mgawanyo sahihi wa
rasilimali za taifa la Congo
ndiyo maana akaamua
kugombea urais ili
ahakikishe rasilimali
zinawanufaisha watu
wote.Najua bado unaumwa
na sitaki kukuongezea
maumivu lakini lazima
ufahamu kwamba kifo cha
mama yako kinahusiana na
yeye kutaka kuwania urais
wa Congo.Haya ni mauaji ya
kisiasa na si ujambazi kama
inavyodaiwa” akasema Rais
Michael Weren na Theresia
akafuta machozi
“Tumefanya uchunguzi
wa risasi ambazo zilikuwa
katika miili ya marehemu ni
risasi za bunduki za hali ya
juu sana ambazo hutumiwa
na wadunguaji.Bunduki
kama hizo hutumiwa na
vikosi vya majeshi na si
rahisi kwa mtu wa kawaida
kuwa nayo.Kama kweli
majambazi hao kama
inavyodaiwa walikuwa na
hiyo silaha basi walipewa na
serikali ili watekeleze
mpango huo wa
mauaji”akasema Rais
Michael
“Masikini mama yangu
niliwahi kumuonya kuhusu
mpango wake wa kutaka
kugombea urais lakini
akanitaka nisiwe na
hofu.Kwa nini lakini
hakutaka kunisikia na sasa
ameniacha yatima? Akasema
Theresa akiendelea
kumwaga machozi
“Mama yako Lucy
Muganza alikuwa na
malengo makubwa sana
kuhusu Congo na alitaka
kuifikisha mbali
kiuchumi.Mimi binafsi na
baadhi ya maraisi wa nchi
kubwa tulimuunga mkono
baada ya kuyaona mawazo
yake yanahitajika sana kwa
wakati huu.Hivi sasa amani
inayodaiwa iko nchini Congo
ni amani bandia.Wakuu wa
serikali na waliokuwa
viongozi wa waasi
wamewekeana mikataba ya
kupeana utajiri.Wanaendelea
kuinyonya Congo.Ni watu
wachache wanaoendelea
kufaidika na rasilimali za
Congo huku wananchi wengi
wakiendelea kuogelea katika
umasikini mkubwa.Haya
ndiyo mambo ambayo Lucy
Muganza alikuwa
anayapinga kwa nguvu zake
zote hadi akaamua
kugombea urais ili aweze
kuikomesha dhuluma hii
kubwa kwa watu wa Congo
lakini kwa bahati mbaya
hakuyweza kutimiza lengo
lake wakawahi kuondoa uhai
wake” akasema Rais
Michael.Theresa akafuta
machozi na kuuliza
“Serikali ya Congo
wanahusika katika mauaji
ya wazazi wangu?
Rais Michael hakujibu
kwa haraka swali lile
akainuka na kwenda
kutazama mojawapo ya
mashine iliyokuwepo mle
chumbani halafu akarejea
kitini akaketi na kusema
“Hatuna uhakika bado
nani wameshiriki katika
mauaji yale tunaendelea na
uchnguzi lakini kwa namna
yoyote ile itakavyokuwa
lazima serikali ya Congo
itakuwa na mkono wake.Si
serikali ya Congo peke yake
bali tunahisi hata nchi
nyingine za afrika mashariki
kama Tanzania watakuwa
wameshiriki katika mpango
huu wa mauaji ya wazazi
wako”akasema Rais Michael
“Mheshimiwa Rais
ninaomba hawa wote
waliohusika na mauaji ya
wazazi wangu wasakwe na
waadhibiwe vikali.Mauaji ya
namna ila hayakubaliki ni
mauaji ya kinyama mno”
akasema Theresa
“Theresa kama
nilivyokueleza kwamba
tunaendelea na uchunguzi
wa kuwabaini waliofanya
tukio lile lakini naomba
ufahamu kwamba watu
waliotekeleza mauaji yale ni
wataalamu na walijipanga
vyema.Walijua fika Lucy ni
mtu mkubwa na lazima
uchunguzi wa kina
utafanyika baada ya kumuua
hivyo wakajitahidi
kutokuacha kitu chochote
cha kuweza
kuwatambulisha.Uchunguzi
huo unaweza ukachukua
miaka na kuna uwezekano
tusimpate muuaji ni nani
kwani kwa namna tukio lile
lilivyotengenezwa ni mfumo
wa matukio yale ambvayo
yanakosa majibu na hubaki
yakielea.Majambazi
wanaodaiwa kumuua Lucy
wote wameuawa na hakuna
tena mtu wa
kumuhoji.Limebaki ni
fumbo.Kosa kubwa
walilolifanya ni kukosea
kukupiga risasi na
ukanusurika”
“Nimepona kwa huruma
ya Mungu.Kuna wakati
ninaona ni bora ningekufa
mimi na wazazi wangu
wangu wabaki hai waendelee
kuipigania nchi yangu
isiendelee kunyonywa”
akasema Theresa na kuanza
tena kulia
“Usilie Theresa kwani
bado hakijaharibika
kitu.Utakwenda kuifanya
kazi ambayo mama yao
alikusudia kuifanya”
“Siasa?! Akauliza
Theresa kwa mshangao
kidogo
“Theresa jukumu lako
kubwa ni kuvaa viatu vya
mama yako na kuendeleza
kazi aliyoianzisha
kuhakikisha utajiri wa
Congo unawanufaisha watu
masikini” akasema Rais
Weren na kunyamaza
akamtazama Theresa
“Unamaanisha nini
mheshimiwa Rais?akauliza
Theresa akionekana kuwa na
wasi wasi mwingi
“Tunakuandaa kuwa
Rais wa Congo” akasema
Rais Weren na mstuko
mkubwa ukaonekana usoni
kwa Theresa
“Mimi ?! Rais? Theresia
akauliza
“Ndiyo
Theresa.Tunakuandaa ili uje
ushike madaraka ya urais
uendeleze maono ya mama
yako.Usihofu si sasa hivi bali
tutakujenga kwanza na
kukuandaa kushika nafasi
hiyo na muda wako ukifika
basi tutakuingiza
madarakani.Hata mama
yako tulianza kwanza kwa
kumuandaa na alipokuwa
tayari ndipo akatangaza
kuwania urais lakini hawa
watu wamezima ndoto
zake.Nilisema kwamba
walikosea sana kukuacha hai
kwani utakwenda kutimiza
ndoto zote za mama yako”
akasema Rais Weren
“Mheshimiwa Rais sina
hakika kama ninahitaji
nafasi hiyo kubwa.Siipendi
siasa kwani imesababisha
nikabaki yatima wazazi
wangu wote wameuawa kwa
sababu ya chuki za kisiasa”
akasema Theresa
“Usihofu Theresa.Sisi
tupo tutakuongoza na
kukusimamia.Tutakulinda
dhidi ya hatari yoyote”
“Katika kauli zako
unazungumza uwingi.Wewe
na nani mlikuwa nyuma ya
mama yangu?akauliza
Theresa
“Tuko viongozi wa
mataifa kadhaa ambao
tunayapigania maslahi ya
Congo.Tunataka rasilimali za
Congo ziwanufaishe watu
wote wa Congo na si kikundi
cha watu wachache”
“Mheshimiwa Rais
ninashukuru sana kwa
mawazo hayo mazuri juu
yangu lakini nadhani mimi si
mtu sahihi kwa nafasi
hiyo.Watu waliomuua mama
walitaka kuiteketeza familia
yote na mimi nimepona kwa
mkono wa Mungu.Nikisema
nikubali ombi lako sintaweza
kufika mbali kwani hawa
jamaa lazima wataniua
tu.Kama waliweza kuwaua
wazazi wangu hata kama
mlikuwa mmewapa ulinzi
hawatashindwa kuniondoa
na mimi” akasema Theresa
“Usihofu hakuna
atakayejua kama wewe ni
Theresa Muganza”
“Watashindwaje kujua
kama ni mimi?
“Tutakubadili
muonekano wako na
utakuwa mtu mpya kabisa
na jina jipya hakuna
atakayeweza kuhisi wewe ni
Theresa Muganza na hapo
ndipo kazi itakapoanzia”
akasema Rais Weren na
midomo ya Theresa
ikamcheza akionekana
kutaka kuongea kitu lakini
Rais Weren akamtoa
wasiwasi
“Najua taarifa hizi
zimekustua sana lakini
naomba usistuke
Theresa.Tuko pamoja nawe
na tunakuandaa kwa
mipango mikubwa
sana.Nimekuja mwenyewe
kukupa taarifa kwamba
kesho utafanyiwa upasuaji
mkubwa wa kubadili
muonekano wako.Tayari
timu ya madaktari bingwa
kumi na mbili kutoka
sehemu mbali mbali duniani
mabingwa wa upasuaji wa
plastiki wako hapa Paris
wakiandaa upasuaji
huo.Baada ya upasuaji huo
kukamilika utakuwa mtu
mwingine kabisa,Theresia
Muganza atawekwa pembeni
na utaanza na jina
jipya,maisha mapya.Safari
ya kuelekea katika ndoto
kubwa ya mama yako
kuliongoza taifa la Congo
itaanza.Ninachokuomba
usiwe na hofu madaktari
hawa ni mabingwa wa
upasuaji huo na
ninakuhakikishia
watakapokuondoa bandeji
usoni utakuwa ni
malaika,kiumbe mpya
kabisa” akasema Weren na
baada ya maongezi na
Theresa akamuaga na
kuondoka
“Muda si mrefu moto
unakwenda kuwaka Afrika
Mashariki.Naamini
waligundua kitu kuhusu
Lucy kutumika katika
mpango wa kuisambaratisha
Afrika Mashariki ndiyo
maana wakamuua lakini
bado hawajafanya kitu kwani
sisi tunazo mbinu nyingi
zaidi yao na mipango ya
kuisambaratisha Afrika
Mashariki iko pale
pale.Anguko lao linakuja si
muda mrefu sana” akawaza
Rais Weren akiwa garini
baada ya kutoka kuonana na
Theresa.
TEL AVIV - ISRAEL
Mlango mkubwa wa
chuma wa mojawapo ya
chumba ndani ya gereza la
siri wanakofungwa magaidi
na wale wote wenye
kuendesha mashambulizi
dhidi ya Israel,ulifunguliwa
na mtu mmoja aliyeonekana
hana fahamu na aliyeloa
damu mwili mzima
akasukumiwa ndani kisha
mlango ukafungwa.
Ammar Nazari ambaye
ndiye aliyekuwa akilala
ndani ya kile chumba
akastuka sana baada ya
kumuona Yule
mtu.Akamsogelea
akamgeuza na
kumtazama.Uso wake
ulikuwa umevimba na
hakuwa akitazamika kwa
damu iliyokuwa inamvuja.
“Huyu mtu ni nani?Kwa
nini wamekuja kumtupia
humu?akawaza akiendelea
kumtazama vizuri mtu yule.
“Huyu ni
mwafrika.Wamemtoa
wapi?Ni mara chache sana
kumuona mtu mwenye asili
ya Afrika katika gereza
hili.Humu ndani tumejaa
waarabu hasa wapalestina
na wengine ambao
tunaendeleza harakati za
mapambano dhidi ya
dhuluma za Israel.Huyu
amefanya nini hadi akafika
hapa?Ni jambazi?Ameua?
akaendelea kujiuliza Ammar
huku akivua kilemba chake
akakipasua na kuanza
kumfuta damu.
“Huyu jamaa atakuwa
amefanya kosa kubwa
sana.Ameumizwa mno.Mwili
wake wote una
viodonda.Inaonekana
ameteswa sana kisha wakaja
kumtupa humu ndani”
akawaza Ammar na kwenda
kuchukua maji katika
chombo chake cha kuhifadhi
maji ya kunywa akaanza
kumfuta damu Yule mtu
“Huu ni ukatili
usioelekezeka.Hawa watu ni
wakatili mno.Unawezaje
ukamtesa mwanadamu
mwenzako kiasi hiki?Hii
ndiyo sababu inayonifanya
niendelee kuwa na chuki na
hasira dhidi ya watu hawa
na ninaapa kama itatokea
siku moja nikawa huru
nitaendelea kupambana nao
hadi tone la mwisho la damu
yangu.Nitaendelea kuua
waisrael hadi pale
watakaporejesha ardhi yetu
waliyoipora” akawaza
Ammar akiendelea kumfuta
damu.
Katika moja wapo ya
chumba ndani ya lile gereza
Efraim Dagan akiwa na
baadhi ya maafisa wa
Mossad wakiwa na viongozi
wa lile gereza walikuwa
wakitazama kila
kinachoendelea katika
chumba kile cha Ammar
kupitia runinga
iliyunganishwa na kamera ya
siri iliyomo katika chumba
kile.Efraim akachukua simu
na kumpigia Moshe
mkurugenzi mkuu wa
Mossad
“Efraim mambo
yanakwendaje? Akauliza
Moshe Levine
“Mkurugenzi
nimekupigia kukujulisha
kuwa mambo
yameanza.Tayari Mathew
amekwisha ingizwa katika
chumba cha Ammar na hivi
tuongeavyo tunamtazama
kupitia kamera ya siri
iliyomo humo
chumbani.Amestushwa sana
na hali ya Mathew na
anamsaidia kwa kumfuta
damu iliyotapaa mwili
mzima.Inaonekana ana
hamu sana ya kutaka
kumfahamu Mathew ni nani
pale atakapokuwa
amezinduka.Mwanzo
umekuwa mzuri” akasema
Efraim
“Kazi nzuri
sana.Endeleeni kumfuatilia
kwa karibu sana kujua kila
kinachoendelea humo
ndani.Ammar ni mtu mbaya
sana akimgundua kwamba ni
pandikizi atamuua”
“Tuko makini
mkurugenzi kumfuatilia
Mathew na kama
tukigundua kuna jambo
lolote lisilo la kawaida
tutamtoa Mathew haraka
sana lakini mpaka hapa
tunaona kuna mwelekeo
mzuri”
“Kuhusu Mathew
Mulumbi
unamuamini?Haweze
akabadilika na kutoweka?
Akauliza Moshe
“Kuna kila dalili kwamba
hataweza kwenda kinyume
na makubaliano yetu japo
hatuwezi kumuamini
asilimia mia moja kwa
sasa.Tunaendelea kufuatilia
mwenendo wake” akasema
Efraim
“Nashauir pale
atakapokuwa ametolewa
ndani ya chumba hicho
baada ya siku mbili achomwe
sindano ya usingizi na
afungwe kwa siri kifaa
kitakachotuwezesha sisi
kumfuatilia na kujua mahala
alipo.Sina imani naye huyu
mtu anaweza akatoroka”
akasema Moshe na kukata
simu.
Chumbani bado Ammar
aliendelea kumsaidia
Mathew Mulumbi kwa
kumfuta damu halafu
akamlaza katika kitanda
kimoja kwani ndani ya
chumba kile kulikuwa na
vitanda viwili akaendelea
kumpepea kutokana na hali
iliyokuwemo mle ndani ya
chumba kuwa ni joto
.Alikuwa anavuja jasho jingi
usoni
Zilipita dakika arobaini
Mathew akafumbua macho.
“Allahu Akbar ! akasema
Ammar baada ya Mathew
kuzinduka.
“mrhbana,aistarkhaa.sat
akun bikhayr” akasema
Ammar akimtaka Mathew
atulie atakuwa
salama.Akaenda katika
chombo anachohifadhi maji
ya kunywa akatikisa na
kukuta kuna maji kidogo
akamimina katika kikombe
cha bati na kumpatia
Mathew
“ashrb ma'(kunywa maji)
akasema Ammar na
kumsogezea Mathew
kikombe cha maji lakini
Mathew akakipiga kofi kile
kikombe kikaanguka na maji
yakamwagika.Ammar
akamtazama
“sawf tamut huna 'iidha
kunt la tashrib alma'(utakufa
humu kama hutakunywa
maji)akasema Ammar lakini
Mathew hakumjibu
kitu.Ammar akakaa kwenye
kiti cha mbao akimtazama
Mathew.
“min 'ant? madha
faelt?(wewe ni
nani?Umefanya nini?)
akauliza Ammar lakini
Mathew hakumjibu kitu
“laqad qatalat
shakhsana? laqad qatalat
alyahud?(umeua mtu?Umeua
wayahudi?) akauliza Ammar
lakini bado Mathew
hakumjibu alikuwa kimya.
“la takhafuu manya.
asmaa eammar nazaraa. ma
asmaka? min 'ayn
'ant?(Usiniogope.Naitwa
Ammar Nazari.Jina lako
nani?Umetokea wapi?)
akauliza Ammar bado
Mathew hakuweza
kuzungumza
Ammar akafunua bakuli
lililokuwa pembeni ya
chumba akatoka mkate
“aistayqaz wa'akal min
fidlik. tahtaj 'iilaa alttaqat
min ajl albaqa' huna(inuka
ule tafadhali.Unahitaji
nguvu uweze kuishi humu)
akasema Ammar Mathew
hakutaka kumtazama
akafumba macho.
“kayf yumkinuni
masaeiduk? 'ant la turid 'an
takul 'aw tashrub. 'ant turid
'an tamut? (Nikusaidiaje?
Hutaki kula wala
kunywa.Unataka kufa?)
akauliza Ammar
“daeni 'atrikuk alan
lilrraha. sanatahadath
lahqaan(Ngoja nikuache kwa
sasa
upumzike,tutazungumza
baadae” akasema Ammar na
kwenda kujilaza katika
kitanda kingine.
“Mambo mazuri.Nataka
niunganishwe na kila
kinachoendelea ndani ya
chumba kile niwe nikifuatilia
kwa karibu” akasema Efraim
akitaka kuunganishwa
katika simu yake ili aendelee
kufuatilia kila
kinachoendelea katika
chumba kile kisha akatoka
“Umekuwa ni mwanzo
mzuri sana.Kuna kitu ndani
yangu kinanifanya
nimuamini sana huyu
Mathew Mulumbi.Ninakiri
toka nimeingia katika
mambo haya ya ujasusi
sijawahi kukutana na mtu
kama Mathew.Ni mtu wa
ajabu sana.Kwa miaka
mitatu ameweza kuvumilia
mateso na hajatamka hata
neno moja” akawaza Efraim.
- LICHA YA LUCY
MUGANZA KUUAWA
LAKINI BADO
MIPANGO YA
KUISAMBARATISHA
JUMUIYA YA AFRIKA
MASHARIKI IKO PALE
PALE NA SASA
ANAANDALIWA
MWANAE THERESA
KUVAA VIATU VYA
MAMA YAKE
- MATHEW MULUMBI
KATIKA JITIHADA ZA
KUTAKA
KUJIKOMBOA
KUTOKA MIKONO YA
MOSSAD ANAANDAA
MPANGO WA
KUJIUNGA NA
MAGAIDI ILI AWEZE
KUMPATA HABIBA
JAWAD.JE MIPANGO
YAKE
ITAFANIKIWA?MPENZI
MSOMAJI USIACHE
KUFUATILIA SIMULIZI
HII KATIKA SEHEMU
IJAYO….
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 1
DAR ES SALAAM
Saa tatu za asubuhi Rais
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania Dr Fabian Kelelo
alipata ugeni ambao ni balozi
wa umoja wa Ulaya ndugu
Benjamin Hudson ambaye
aliomba kuonana na Rais ili
kuzungumza mambo
muhimu.
“Karibu sana
mheshimiwa balozi.Ni furaha
yangu kuonana nawe
leo”akaanzisha maongezi Dr
Fabian
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais kwa
kukubali ombi langu kuja
kuonana nawe”akasema
balozi Benjamin
“Tanzania tuna
mahusiano mazuri na umoja
wa Ulaya hivyo nisingeweza
kukataa ombi la kuonana na
mwakilishi wao hapa
Tanzania”
“Ni kweli mheshimiwa
Rais mahusiano ya Tanzania
na umoja wa Ulaya ni
makubwa na yanakwenda
vizuri hata hivyo nimetumwa
nikuletee salamu za umoja
huo.Kwanza pongezi kwa
maendeleo mazuri na ya
kuridhisha ya kiuchumi
lakini pili ni ombi
nimetumwa niliwasilishe
kwako”
“Ahsante kwa
pongezi.Umoja wa Ulaya
wanaomba kitu
gani?akauliza Dr Evans na
balozi Benjamin akavuta
pumzi ndefu na kusema
“Mheshimiwa Rais hivi
majuzi kumetokea mauaji ya
bilionea Lucy Muganza na
mume wake Laurent
Muganza.Laurent Muganza
alikuwa ni raia wa Ufaransa
mwenye asili ya Congo lakini
vile vile alikuwa ni mmoja
kati ya wafanyakazi wa ngazi
za juu katika makao makuu
ya umoja wa ulaya jijini
Brussels.Nafahamu kwamba
tayari taarifa ya awali ya
mauaji yale imekwisha
tolewa na inatajwa kwamba
chanzo cha mauaji yale
kilikuwa ni
ujambazi.Tunaheshimu
vyombo vya ndani vya
Tanzania lakini umoja wa
Ulaya umenituma
niwasilishe ombi maalum
kwako la kutaka kutuma
timu maalum ya wachunguzi
kuja kufanya uchunguzi wa
mauaji hayo hasa ukizingatia
kwamba Laurent Muganza
alikuwa afisa katika umoja
wa Ulaya.Kwa mujibu wa
maelekezo niliyopewa ni
kwamba timu hiyo itakuwa
na watu nane ambao ni
wabobezi katika mambo ya
uchunguzi” akasema balozi
Benjamin na Dr Fabian
akawa kimya kwa muda
halafu akasema
“Mheshimiwa balozi
sitaki nieleweke vibaya
lakini suala hili la mauaji ya
Lucy Muganza na mumewe
linaendelea kushughulikiwa
na vyombo vya uchunguzi
vya hapa nchini na
watakapokamilisha
uchunguzi wao watatoa
taarifa.Kuruhusu timu
nyingine ya kutoka nje kuja
kufanya uchunguzi wakati
vyombo vya ndani
havijakamilisha uchunguzi
wao kwanza ni kudhalilisha
vyombo vya ndani kwamba
haviwezi kuchunguza
matukio makubwa kama
haya na pili tunawavunja
moyo vijana wetu ambao
hawalali wakitafuta kupata
ukweli wa tukio lile.Ushauri
wangu kwa umoja wa Ulaya
ambao ni wadau wetu wa
maendeleo wasiwe na wasi
wasi na waviamini vyombo
vyetu vya ndani ya nchi na
waviache vifanye uchunguzi
vikikamilisha watatoa
taarifa na kama
hawataridhika na taarifa
hiyo tutaangalia kama
kutakuwa na ulazima wa
kuruhusu wachunguzi
kutoka nje ya nchi lakini kwa
sasa hakuna ulazima wowote
wa kuleta wachunguzi
kutoka nje ya nchi” akasema
Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais ombi
la kutaka kuleta wachunguzi
wa nje si kwamba
hatuviamini vyombo vya
Tanzania bali tunataka
kutanua zaidi wigo wa
uchunguzi.Aliyeuawa ni afisa
mkubwa katika umoja wa
Ulaya na yawezekana
majambazi wale walitumika
tu lakini wahusika wa
mauaji hayo ni wengine
kabisa.Tunataka kuchimba
kiini cha mauaji
yale.Tunahisi zipo njama za
kuwadhuru maafisa wetu
hivyo kupitia uchunguzi huo
utakaofanyika na timu
maalum,itajulikana nani
ambao wanapanga njama
hizo za kudhuru maafisa
wetu”akasema balozi
Benjamin
“Mheshimiwa balozi
pamoja na sababu ulizozitoa
lakini bado sioni ulazima wa
kuruhusu wachunguzi wa
kutoka nje kuja kufanya
uchuguzi wa mauaji
yaliyotokea
Tanzania.Nasema katu
siwezi kuruhusu jambo la
namna hiyo.Tanzania
tunavyo vyombo vya
uchunguzi vyenye watu
wenye uwezo mkubwa wa
kufanya uchunguzi na kwa
ujumla vyombo vyetu
vinafanya kazi nzuri sana
hivyo hakuna sababu ya
kuwa na wasiwasi
wowote.Fikisha salamu
zangu kwa umoja wa Ulaya
kwamba wasiwe na wasiwasi
wasubiri taarifa
itakayoptolewa na vyombo
vyetu na kama
hawataridhika nayo basi
tutaangalia namna nyingine
lakini kwa sasa
hatutaruhusu wachunguzi
wowote kutoka nje ya nchi”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa
Rais,Tanzania ni nchi
ambayo ina heshima kubwa
sana kimataifa.Mauaji haya
ya Laurent na mke wake
Lucy yameistua dunia na
kuzifanya nchi nyingi
zigeuke na kuitazama
Tanzania kutaka kujua
kulikoni mauaji yale
yakatokea hapa katika nchi
iliyojaa amani na
utulivu.Tanzania imepata
doa kutokana natuko lile na
njia pekee ya kulifuta doa
hilo ni kuruhusu wachunguzi
wa kimataifa kufanya
uchunguzi lakini kama
hamtaruhusu timu hiyo
kufanya uchunguzi wake
Tanzania itachafuka
kimataifa jambo ambalo
inaweza kuwa na athari
kubwa hasa
kiuchumi”akasema balozi
Benjamin
“Mheshimiwa balozi
kauli yako inalenga
kuonyesha kwamba
Tanzania inahusika na
mauaji hayo ya Laurent na
mke wake.” Akasema Dr
Fabian
“Hakuna mwenye
ushahidi na hilo mheshimiwa
Rais lakini fahamu kwamba
Tanzania inanyooshewa
kidole kuhusiana na mauaji
hayo na njia pekee ya
kujisafisha na kuondoa doa
ambalo nchi yako imelipata
kwa mauaji yale kutokea
katika ardhi yenu ni
kuruhusu timu ya
wachunguzi wa kimataifa
kufanya uchunguzi
wao.Kama hamtaruhusu
wachunguzi hao itajengeka
hisia kwamba Tanzania kuna
kitu inaficha kisijulikane
kuhusu mauaji yale”
“Mheshimiwa balozi sasa
nimepata picha kamili ya
kwa nini mnataka timu ya
wachunguzi wa kimataifa
waje kufanya
uchunguzi.Tayari mnaamini
kwamba Tanzania ina mkono
wake katika mauaji
yale.Naomba niwatoe
wasiwasi kwamba katu
Tanzania haiwezi kupanga
njama za kumuua Laurent
na mke wake.Subirini
uchunguzi ukamilike na
mtawajua watu wanaohusika
na mauaji hayo lakini
kuihusisha Tanzania ni
kutaka kuipaka matope”
“Mheshimiwa Rais
hakuna mpaka sasa
anayeamini kama Tanzania
inaweza ikahusika katika
mauaji hayo lakini kitendo
cha kugoma kuruhusu
wachunguzi wa kimataifa
kama nilivyosema kinaweza
kuitia doa serikali yako na
kuvuruga mahusiano mazuri
na jumuiya ya Ulaya”
akasema balozi Benjamin na
Dr Fabian akamtazama kwa
muda kisha akauliza
“Kwa nini Laurent
Muganza?Mbona
kumewekwa uzito mkubwa
sana kutaka kufahamu
chanzo cha kifo chake hadi
kutaka kuingilia taratibu
zetu za ndani ya nchi?
akauliza Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
niliweka wazi kwamba kuna
wasi wasi kuna njama za
kuwadhuru maafisa wa
umoja wa Ulaya na tunahisi
mipango hiyo tayari imeanza
hivyo basi tunataka kuanza
kufanya uchunguzi kwa
kuanzia na kifo cha Laurent”
“Nani anataka
kuwadhuru maafisa wa
umoja wa Ulaya?akauliza Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais hayo
ni mambo ya ndani sana ya
kiusalama na hata mimi
siwezi
kufahamu.Ninachokuomba
litafakari ombi hilo la umoja
wa Ulaya na uwaruhusu
wachunguzi wa kimataifa
kuja kufanya uchunguzi wa
jambo hili”
“Balozi Benjamin
nadhani mimi na wewe
tumekwisha maliza
hapa.Jibu langu
halitabadlika.Hatutaruhusu
wachunguzi wowote wa
kimataifa nchini
kwetu.Nifikishie salamu hizo
kwa umoja wa
Ulaya”akasema Dr Fabian na
kutaka kuinuka lakini
Benjamin akamuomba ampe
dakika mbili kuna
kituanataka kumueleza
“Mheshimiwa Rais kabla
sijaondoka kuna jambo
nataka ulifahamu ambalo
ndilo hasa chanzo cha
wasiwasi kuhusu mauaji yale
hadi kutaka kutuma
wachunguzi wa kimataifa”
akasema balozi Benjamin na
kufungua mkoba wake
akatoa mafaili mawili.
“Mheshimiwa Rais hizi ni
taarifa mbili tofauti.Moja ni
taarifa ya awali ya jeshi la
polisi kuhusina na mauaji
yale na nyingine ni taarifa ya
daktari iliyotolewa baada ya
miili ya Lucy na Laurent
kufanyiwa uchunguzi”
akasema balozi Benjamin
“Mheshimiwa rais hizi si
taarifa za siri bali ni taarifa
za wazi kabisa na mtu yeyote
anaweza kuwa nazo.Hii
taarifa ya daktari nimeipata
kutoka kwa ndugu za
marehemu na hii ya jeshi la
polisi iko mtandaoni”
“Kuna nini katika taarifa
hizi?akauliza Dr Fabian
“Mheshimiwa rais katika
taarifa hizi mbili kuna jambo
dogo lakini lenye kuibua
maswali mazito.Taarifa ya
awali ya jeshi la polisi
inaonyesha kwamba
majambazi ambao
wanadaiwa kumuua Lucy na
mumewe pamoja na walinzi
wao,waliuawa wote na
walikutwa wakiwa na silaha
mbali mbali ambazo
zimeorodheshwa hapo
ambazo ni bunduki za vita
aia ya SMG pamoja na
bastora kadhaa.Ripoti ya
jopo la madaktari
walioifanyia miili uchunguzi
inaonyesha kwamba risasi
zilizowaua Laurent na
mkewe Lucy ni kubwa tofauti
na risasi za SMG.Baada ya
kuzifanyia uchunguzi risasi
hizo zimebainika ni za
bunduki aina ya Barret
M82.Mheshimiwa Rais hizi
ni bunduki hatari sana zenye
nguvu na zinazotumiwa na
wadunguaji.Kwa kawaida
bunduki kama hizi
hutumiwa au kumilikiwa na
majeshi au vikosi
maalum.Majambazi
waliouawa hawakuwa na
bunduki hizo.Taarifa
nilizonazo zinanionyesha
kwamba Tanzania mnazo
bunduki za namna hiyo na
mlizinunua kutoka
Marekani.Maswali
yanaanzia hapo mheshimiwa
Rais.Nadhani unakubaliana
nami kwamba suala hili ni
kubwa na linahitaji
uchunguzi mkubwa
pia.Siamini kama Tanzania
inahusika katika suala hili
lakini zitajengeka hisia hizo
pale ambapo utakataa
wachunguzi wa kimataifa
waje kuchunguza suala hili
mheshimiwa Rais” akasema
balozi Benjamin na uso wa
Dr Fabian ukajikunja kwa
hasira.
“Balozi taarifa kama hizo
za silaha tulizo nazo
unazipata wapi?Kwa hilo
balozi umevuka mipaka ya
kazi yako ya uwakilishi wa
jumuiya ya Ulaya na sasa
unaanza kufanya uchunguzi
wa mambo
yasiyokuhusu.Masuala ya
silaha ni masuala nyeti
kabisa ya usalama wa
nchi.Hili sintalifumbia
macho balozi.Lazima umoja
wa Ulaya watueleze kama
walikutuma hapa kuja
kuwawakilisha au kufanya
ujasusi.Ahsante kwa kufika
mheshimiwa balozi” akasema
Dr Fabian akiwa
amekasirika na balozi
Benjamin akasimama
“Mheshimiwa Rais
nakuomba jipe muda
litafakari suala hili na
ufanye maamuzi yenye kufaa
kwa nchi yako.Wachunguzi
hao hawataingilia suala
lolote la nchi yako bali
watachunguza kifo cha raia
wa kigeni hivyo kuwazuia
kufanya uchunguzi ni
mwanzo wa kuibuka kwa
mjadala mpya wenye swali la
kwa nini?Ahsante
mheshimiwa rais
nakushukuru kwa
kunikaribisha na
kunisikiliza.Nategemea
kupata simu yako baada ya
tafakari ya kina” akasema
balozi Benjamin na
kusimama.Dr Fabian
akamuelekeza mmoja wa
wasaidizi wake amsindikize
balozi nje katika gari lake
yeye akaelekea ofisini kwake.
“Mambo yameanza.Sasa
nimeamini kumbe Lucy
Muganza alikuwa mtu
muhimu sana kwao ndiyo
maana wanafanya shinikizo
la kutaka iruhusiwe timu ya
wachunguzi wa kimataifa
kuingia nchini na
kuchunguza.Ni vipi kama
nitaruhusu timu hiyo kuingia
nchini na kuchunguza halafu
wakabaini sisi ndio
tuliomuua Lucy Muganza na
mumewe?Moja kwa moja
nitakuwa nimejivisha
kitanzi.Lakini nisiporuhusu
wachunguzi hao kuingia
nchini lazima watajiuliza
maswali kuna kitu gani
tunakificha? Halafu huyu
balozi amepata wapi taarifa
nyeti kama hizo za sisi
kumiliki bunduki za Barret
M82? Suala hili limeanza
kuchukua sura mpya na
litakuwa kubwa
zaidi.Inaonekana tayari
wamekwisha hisi sisi ndio
tuliomuua Lucy na
wanachokitafuta hivi sasa ni
ushahidi wa kutosha na
ushahidi huo wataupata
endapo watatuma timu yao
hapa nchini.Something must
be done.Hili si suala la
kuachia hivi hivi inaonekana
kuna watu mtandao wa watu
wa ndani pia wanaosaidiana
na umoja wa Ulaya katika
kutafuta ukweli wa hili
jambo.Lazima tuwafahamu
ni akina nani hao na
kuwadhibiti haraka sana”
akawaza Dr Fabian
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 2
Geti la nyumbani kwa
Rais mstaafu Dr Evans
lilifunguliwa na gari
lililobeba shehena ya
matunda likaingia.Yalikuwa
ni matunda kutoka katika
shamba la matunda la Dr
Evans.Watumishi walianza
kupakua matunda yale
yaliyokuwa katika
masanduku na kuyaingiza
ndani katika chumba
maalum cha baridi kwa ajili
ya kuhifadhia mazao ya
shambani yenye kuharibika
haraka kama vile
matunda.Wakati zoezi
likiendelea la kupakua
matunda Dr Evans akatoka
ndani.Siku hii alivaa suruali
ya jeans ya khaki shati jeupe
na kofia ya mzunguko ya
rangi nyeupe.Akalisogelea
lile gari akasalimiana na
wafanyakazi kisha akashika
tunda moja akalitazama na
kutabasamu halafu
akamuagiza mtumishi wake
amuandalie juisi kutoka
katika matunda yale
yaliyotoka shambani siku
ile.Dr Evans akazunguka
zunguka katika makazi yake
akisalimiana na wafanyakazi
na kukagua namna shughuli
zilivyokwenda halafu
akaenda kukaa katika
sehemu ya kupumzikia
pembeni ya bwawa la
kuogelea.
“Maisha ya kustaafu
baada ya kulitumikia taifa ni
mazuri sana.Ninapata kila
kitu
ninachokitaka,ninakwenda
sehemu yoyote ninayoitaka
lakini kuna kitu kimoja tu
ambacho
nimekikosa.Ningekuwa na
mke furaha yangu
ningefurahia zaidi maisha ya
kustaafu.Nimeishi
mwenyewe kwa muda mrefu
toka mama yake Coletha
alipofariki dunia.Kwa nini
nisitafute mwanamke wa
kuishi naye?Naamini siwezi
kukosa mwanamke mtu
mzima mstaafu mwenzangu
na ambaye hana mume ili
niishi naye wakati
huu.Siwezi kuk………………”
DrEvans akatolewa
mawazoni baada ya simu
yake kuita.Akaichukua na
kutazama aliyepiga
akalazimika kuinuka na
kukaa vizuri.Alikuwa ni Rais
Dr Fabian Kelelo.
“Mheshimiwa Rais”
akasema Dr Evans baada ya
kuipokea simu
“Mzee shikamoo”
“Marahaba.Habari yako
Dr Fabian?
“Naendelea vyema mzee
wangu.Habari za hapo
nyumbani?
“Mimi mzima
kabisa.Nina siku mbili tu
nimerejea kutoka Afrika
kusini nilikwenda
kumtembelea binti yangu
anafanya kazi huko”akasema
Dr Evans na mtumishi wake
akamletea juisi akamuwekea
pembeni
“Mzee samahani kwa
kukusumbua.Nina jambo
nahitaji ushauri wako.Najua
ulisema nisikusumbue lakini
sina mwingine ambaye
ninaweza kumkimbilia kwa
suala hili muhimu ” akasema
Dr Fabian
“Una tatizo gani
mheshimiwa Rais? Akauliza
Dr Evans
“Unakumbuka lile suala
la Yule mama Lucy
Muganza?
“Ndiyo.Nakumbuka
aliuawa”akajibu Dr Evans
“Ni kweli aliuawa lakini
kuna tatizo limejitokeza
nahitaji unipe ushauri
nifanye nini” akasema Dr
Fabian na kukaa kimya kwa
muda kisha akasema
“Balozi wa umoja wa
Ulaya ametoka hapa ikulu si
muda mrefu sana ameniletea
taarifa kuwa kufuatia mauaji
yale ya Lucy na
mumewe,umoja wa Ulaya
wanataka kutuma
wachunguzi wao kuja
kuchunguza kujua chanzo
cha mauaji yale”
“Umoja wa
Ulaya?akauliza Dr Evans
“Ndiyo mzee.Umoja wa
Ulaya wanataka kutuma
timu ya wachunguzi wa
kimataifa kuja nchini
kufanya uchunguzi wa
mauaji yale ya Lucy
Muganza na mume wake
Laurent kwa madai kwamba
Laurent alikuwa ni afisa
katika makao makuu ya
umoja wa Ulaya hivyo lazima
umoja huo ujiridhishe sababu
za kuuawa kwake”akasema
Dr Fabian
“Kama umoja wa Ulaya
nao wameingilia kati na
kutaka kufanya
uchunguzi,hii inatoa picha ya
wazi kwamba hawa watu
wawili Lucy na mumewe
walikuwa ni watu muhimu
sana kwao.Ulifanya vyema
kuwaondoa mapema na Dr
Fabian huu ni wakati wako
wa kuonyesha msimamo
mkali kama
Rais.Usiwaruhusu
wachunguzi hao wa umoja
wa ulaya kuingia nchini kwa
namna yoyote ile” akasema
Dr Evans
“Lakini mzee nikisema
niwazuie wachunguzi hao
wasiingie nchini italeta picha
kwamba kuna jambo
ninalificha kuhusu mauaji
hayo” akasema Dr Fabian
“Dr Fabian tatizo lako
unataka uwe mwema na
mzuri kwa kila mtu kitu
ambacho
hakiwezekani.Usifanye
mambo kwa kutaka watu
wakuone mzuri sana bali
fanya jambo kwa maslahi ya
nchi.Huu ni mtego
umewekewa na ukienda
kichwa kichwa
utanasa.Usiwaruhusu
kamwe wachunguzi hao waje
hapa nchini kufanya
uchunguzi.Weka msimamo
kwamba hilo ni suala la
ndani ya nchi na
linashughulikiwa na vyombo
vya ndani.Huhitaji
wachunguzi kutoka
nje.Ukithubutu
kuwakaribisha sebuleni
wataingia hadi chumbani
hivyo nakushauri usiwape
nafasi kabisa katika suala
hilo.Simama na msimamo
mmoja kwamba uchunguzi
utafanywa na vyombo vya
ndani.Umenielwa Dr Fabian?
“Nimekuelewa mzee”
“Good.Unapaswa
kusimama kama Rais
mwenye msimamo mkali
usiyoyumba lakini
ukiwachekea hawa na
ukaonyesha uoga
watakutawala na utafanya
kila wakitakacho
wao.Usitishwe na mtu yeyote
au taifa lolote liwe kubwa au
dogo.Hii ni vita na mpaka
hapa hesabu kwamba vita hii
kwa asilimia kubwa
umeshinda kwani
walimtegemea mno Lucy
Muganza ndiyo maana hivi
sasa wanahaha.Hata hivyo
kuna kitu nataka kujua.Kwa
nini wawe na wasi wasi hadi
watake kutuma watu wao
kuja kuchunguza mauaji
hayo? Kuna kitu wamekiona
au kuna taarifa yoyote
wameipata inayowapa
wasiwasi? Akauliza Dr Evans
“Kuna jambo alinieleza
balozi ambalo mimi nadhani
hata timu niliyowatumia
katika kufanikisha jambo lile
hawakulitilia maanani.Aina
ya risasi zilizokutwa katika
miili ya akina Lucy ni za
bunduki aina ya Barret
M82.Hizi ni bunduki kubwa
na hutumika kwa
udunguaji.Bunduki hizi zipo
katika kikosi cha jeshi cha
operesheni maalum kwani
kuna wadunguaji wako
pale.Majambazi ambao
wanatajwa kuwa walimuua
Lucy walikuwa na bunduki
aina ya SMG na
bastora.Umoja wa Ulaya
wamelibaini hilo na ndiyo
maana wanataka wafanye
uchunguzi.” akasema Dr
Fabian
“Kweli hapo lazima
tukubali kuna kosa
lilifanyika.Ilitakiwa baada ya
kufanya mauaji yale
wafuatilie hadi katika ripoti
ya daktari lakini wao
walipomuua Lucy wakajua
wamemaliza kila kitu.Umoja
wa Ulaya wanayo hoja ya
msingi ya kutaka kuleta
wachunguzi wao lakini jambo
pekee ni kusimama kidete
kukataa hakuna mchunguzi
yeyote kuingia
nchini”akasema Dr Evans
“Kitu kingine
kilichonistua kwa balozi
Benjamin ni kuwa na taarifa
kwamba Tanzania tunazo
bunduki za aina ile
iliyotumika kumuua Lucy na
anafahamu tumezinunua
wapi bunduki hizo”
“Anazo taarifa za silaha
zetu?Amezipata wapi?
Akauliza Dr Evans kwa
mshangao
“Hata mimi nimeshangaa
kama ulivyoshangaa
wewe.Nimefikiria kumtimua
nchini kwa kufanya ujasusi
badala ya kazi iliyomleta”
akasema Dr Fabian kwa
ukali
“Hapana
usimtimue.Huyu ni mtu
anayepaswa kuchunguzwa
sana kujua amepata wapi
taarifa hizo nyeti.Naamini
lazima kuna watu hapa
nchini anashirikiana nao
hadi akafanikiwa kupata
taarifa hizo nyeti.Ukimtimua
nchini utashindwa kujua
anaoshirikiana nao hivyo
nakushauri muache lakini
kuanzia sasa anza
kumchunguza kwa siri
naamini kuna mengi
utayafahamu kutoka
kwake.Kama ameweza
kupata taarifa kwamba
tunazo bundukio aina ya
Barret M82 basi hashindwi
kujua tuna vifaru
vingapi,mizinga mingapi kwa
ujumla huyu mtu
anachokifanya ni ujasusi
lakini mvumilie na
umchunguze kwa siri mno.Ni
mtu hatari sana kwa
taifa”akashauri Dr Evans
“Mzee nakushukuru sana
kwa ushauri wako
nitaufanyia kazi”
“Fabian” akaita Dr Evans
“Naam mzee”
“Samahani nakuita
Fabian kwani hapa nataka
kuzungumza nawe kama
mwanangu na ninaomba
unisikilize vizuri”
“Nakusikiliza mzee”
“Umeingia katika vita ya
kiuchumi.Hii ni vita mbaya
sana kuliko vita ya
silaha.Unatunishiana misuli
na mataifa makubwa yenye
uchumi mkubwa,teknolojia
kubwa na zaidi sana ambayo
tunayahitaji katika ukuaji
wa uchumi wetu lakini kwa
kiasi kikubwa uchumi huo
mkubwa wa mataifa hayo
unategemea sana rasilimali
zetu kama vile madini,mazao
ya kilimo maliasili n.k.Kwa
miaka mingi wamekuwa
wakifaidika kwa kubeba
rasilimali zetu na kitendo
cha kuvuruga mipango yao
ya kutaka kuendelea
kunufaika na rasilimali zetu
kinakufanya uwe ni adui
kwao na kwa kuwa wana
nguvu basi wafanya kila
waliwezalo kuhakikisha
kwamba wanakudhoofisha
au wanakundoa katika
nafasi yako wewe na
wenzako ambao mnasimama
pamoja.Hii ni vita mbaya
lakini kitakachokusaidia ni
uimara wako na kufanya
maamuzi sahihi
yasiyoyumba.Watakutikisa
lakini usikubali
kutikisika.Kutokana na
misimamo yako nchi inaweza
ikayumba lakini wewe kama
kiongozi mkuu simama
imara ipeleke nchi sehemu
salama.Katika vita hii jaribu
kuwa na watu wachache
sana ambao utawaamini
ambao watakusaidia sana
kupambana.Mapambano
yanatatakiwa yawe ni ya siri
kubwa hata viongozi
wenzako wakuu hawapasi
kujua kwani miongoni mwao
wako wasaliti
wakubwa.Ichunge sana
jumuiya ya Afrika mashariki
isivunjike na hasa
kuvunjikia mikononi
mwako.Naamini umenielewa
Dr Fabian” akasema Dr
Evans
“Mzee nimekuelwa vizuri
sana.Ninakushukuru tena
kwa ushauri wako mzuri
ninakuahidi nitaufanyia
kazi” akasema Dr Fabian
akaagana na Dr Evans
“Yule mzee amekuwa na
msaada mkubwa sana
kwangu kila pale
ninapokuwa nimetingwa na
suala zito.Amenipa ushauri
mzuri ambao napaswa
kuuzingatia.Kweli hii ni vita
japo si ya vifaru na mizinga
lakini ni vita ya
uchumi.Nitajitahidi
kusimama imara
kupambana” akawaza na
kuchukua simu akampigia
Austin na kumtaka afike
ikulu jioni ana mazungumzo
naye.
“Austin na wenzake
walifanya kosa dogo ambalo
sasa linakwenda
kutugharimu hata hivyo
bado nitaendelea kumuamini
na kufanya naye kazi nyingi
za siri” akawaza Dr Fabian
PARIS – UFARANSA
Hali ya ubaridi
iliyokuwepo nje ilimfanya
bilionea Peniela aendelee
kulivuta blanketi zito
alilokuwa
amejifunika.Kikubwa
kilichomfanya asitake
kubanduka kitandani licha
ya kwamba tayari imekwisha
gonga saa mbili za asubuhi
ni mtu aliyekuwa pembeni
yake ambaye asubuhi hii
bado alionekana kuzidiwa
sana na usingizi.
“Nahum ! Nahum !
..Peniela akamuita Yule
jamaa aliyekuwa naye
kitandani huku
akimtikisa.Nahum akaitika
kwa sauti iliyojaa uchovu
mwingi.Peniela
akamkumbatia na kumbusu
“Kumekucha haraka
sana leo” akasema Nahum
huku akifikicha macho
“Usiku mzima wa jana
hatujalala.Una pumzi za
ajabu Nahum.Hukutaka
kuniachia kila mzunguko
ulipoisha uliunganisha
mwingine.Sikumbuki hata
nilifika kilele mara ngapi
jana.Wanaume kama wewe
ni nadra sana kupatikana
zama hizi.Nina bahati kwani
hata mum…..” Peniela
akasita na kumtazama
Nahum ambaye alikuwa
anatabasamu
“Mbona
unasita?Unaogopa kumtaja
aliyekuwa mumeo Mathew
Mulumbi? Akauliza Nahum
na Peniela akastuka
“Umemfahamu vipi
Mathew?akauliza na Nahum
akatabasamu
“Kabla ya kukutongoza
nilitafuta kwanza taarifa
zako na kuambiwa kwamba
mumeo alikuwa anaitwa
Mathew Mulumbi na alifariki
nchini Tanzania.Sikutaka
kuwa na mahusiano na mtu
mwenye mume
wake.Nilipopata uhakika
kwamba uko mwenyewe
ndipo nilipoamua kukufuata”
akasema Nahum na Peniela
akawa kimya
“Nini kilimuua Mathew
Mulumbi?akauliza Nahum
“Samahani Nahum huwa
sipendi sana kuzungumzia
suala hilo.Tafadhali naomba
tusiongelee tena habari za
Mathew.Tuko hapa mimi na
wewe tufurahie wakati wetu
huu.Masuala yote ya Mathew
tuyaweke pembeni” akasema
Peniela
“Samahani mpenzi
wangu” akasema Nahum na
kumbusu Peniela
“Naomba dakika mbili
nikawatazame watoto kama
wamekwisha kwenda shule”
akasema Peniela na
kumbusu Nahum halafu
akafunga vizuri nguo yake
na kutoka
Baada ya Peniela kutoka
Nahum akaiwasha simu yake
iliyokuwa imezima,zikaingia
jumbe mbali mbali akazipitia
kwa haraka haraka na kisha
akalitafuta jina la Efraim
akampigia
“Nahum kulikoni
ukazima simu yako kwa
usiku mzima?akauliza
Efraim baada ya kupokea
simu
“Nililazimika kuzima
simu nilikuwa na Peniela
chumbani kwake na huwa
ninachukua tahadhari
kubwa kila ninapokuwa
naye” akajibu Nahum
“Kuanzia sasa
usithubutu kuzima simu”
akasema Efraim
“Nitajitahidi Efraim”
“Vizuri.Nilikuwa
nakutafuta kukujulisha
kwamba misheni
imekamilika na unatakiwa
kuondoka haraka sana huko
Paris kurejea Israel”
akasema Efraim
“Misheni
imekamilika?akauliza
Nahum
“Ndiyo.Ulitumwa huko
kwa ajili ya kazi maalum
ambayo tayari imekamilika
na kitu tulichokuwa
tunakitafuta
tumekipata.Mathew
Mulumbi ameongea hivyo
hakuna tena sababu ya wewe
kuendelea kukaa huko.Rudi
nyumbani haraka sana”
akasema Efraim na ukapita
ukimya
“Nahum unanisikia?
“Ninakusikia Efraim
lakini..”
“Hakuna lakini,rudi
nyumbani haraka sana kazi
uliyotumwa
imekamilika”akasema
Efraim
“Efraim naomba unipe
muda wa wiki mbili ili
nimuandae Peniela kabla
sijatoweka” akasema
“Nahum tayari umeanza
kupenda? akauliza Efraim na
Nahum akawa kimya
alishindwa kujibu
“Nahum hii ni kazi na
hupaswi kuuruhusu moyo
wako kupenda hata siku
moja.Umekutana na
wanawake wengi wazuri na
haujawahi hata mara moja
kutaka kuanguka mapenzini
nakuonya isitokee kwa huyo
mwanamke mweusi.Narudia
tena kukuonya usithubutu
kutaka kumpenda
Peniela.Ukithubutu
kuufungua moyo wako tu
utakufa kabla haujatimiza
lengo lako hivyo nakuonya
chunga sana hicho
unachofikiria
kukifanya.Nakupa siku tatu
kuanzia leo uwe umerejea
nyumbani baada ya siku hizo
tatu akaunti zote zenye fedha
zinazokutambulisha kama
bilionea zitafungwa kadi
zako zote hazitatumika tena
utabaki na hati yako ya
kusafiria tu kwa ajili ya
kurejea nyumbani.Narudia
tena siku tatu kuanzia sasa
uwe nyumbani.Kitu kingine
kwa kuwa misheni
imekamilika tafadhali
usiendelee kutumia fedha
hovyo kwani tunaona namna
unavyotumia fedha kwa fujo”
akasema Efraim na kukata
simu.Nahum alikuwa kama
mtu aliyemwagiwa maji
baridi.Alibaki amekaa
kitandani ameishikilia simu
yake.Alikuwa katika lindi la
mawazo.
“Sikuwahi kuona ugumu
wa kazi hii hapo kabla lakini
leo kwa mara ya kwanza
ninadiriki kuichukia hii
kazi.Nimetengenezwa kwa
ajili ya kazi moja tu ya
kujenga mahusiano na
wanawake wale ambao
tunawahitaji katika misheni
zetu.Nimekutana na
wanawake mbali mbali
masikini,matajiri,wake za
watu,viongozi lakini
sikuwahi hata mara moja
kufikiri kama itatokea siku
moja moyo wangu
utamuangukia mtu ambaye
ninamchunguza.Imenitokea
kwa Peniela.Nakiri sijawahi
kukutana na mwanamke
kama huyu.Sifahamu kama
kuna kitu anatumia
kunivuruga akili yangu
lakini nimechanganyikiwa
kwake.Kwa mara ya kwanza
katika maisha yangu nahisi
kumpenda mwanamke
ambaye ni huyu
Peniela.Nahisi furaha,raha
ya ajabu kila ninapokuwa
naye lakini masharti ya kazi
yangu hayaniruhusu
kupenda na ninatakiwa
ndani ya siku tatu niwe
nimeondoka Paris kurejea
Israel.Nitafanya
nini?akajiuliza.
“Mathew Mulumbi
alikuwa anafaidi
sana.Wanawake kama hawa
ni nadra sana kupatikana
zama hizi.Nitawezaje
kumuacha Peniela? Hapa
ndipo ninabaki njia panda je
niitike wito wa kurudi
nyumbani au niendelee kuwa
na Peniela? Akajiuliza
“Hapana siwezi
kumuacha Peniela.Niko
radhi kuachana na kazi
yangu na kuwa naye.Mathew
Mulumbi hataweza kutoka
tena katika mikono ya
Mossad hivyo sina cha
kuhofia.Ninayo nafasi kubwa
na hata Peniela mwenyewe
ananipenda pia”
Mlango wa chumbani
ukafunguliwa Peniela
akarejea na haraka haraka
Nahum akaificha simu yake
“Nimerejea” akasema
Peniela na kujirusha
kitandani na kumwagia
mabusu Nahum
“Vipi watoto
wanaendeleaje?akauliza
Nahum
“Tayari wamekwenda
shule.Nimekosa kuwasalimu
asubuhi hii”
“Napenda namna
unavyowapenda wanao”
akasema Nahum
“Ni kweli ninawapenda
sana Malaika na
Patrick.Unajua watoto hawa
si wa kuwazaa mimi”
“Siyo wanao?
“Si wanangu wa kuwazaa
lakini baba yao ni
Mathew.Kuna wakati mimi
na yeye tuliwahi
kukwaruzana na kila mmoja
akaenda kuendelea na
maisha yake na huko
alikoenda aliishi na
mwanamke mwingine na
wakazaa watoto wawili kwa
bahati mbaya Yule
mwanamke alifariki na
kumuachia Mathew
watoto.Tulipomaliza tofauti
zetu na kurudiana
niliwachukua na kuanza
kuwalea kama mama
yao.Kwa sasa baada ya baba
yao kufariki mimi nimebaki
ndiye baba yao na mama
yao” akasema Peniela
Nahum akabaki kimya
“Masikini Peniela hajui
kama mume wake yuko hai
anaendelea kupata mateso
makali.Kwa nini tunawatesa
watu namna hii?Kila mtu
tayari anafahamu kuwa
Mathew Mulumbi amefariki
dunia.Hata watoto wake
wanajua baba yao hayup….”
“Nahum ! akaita Peniela
na kumstua Nahum kutoka
katika mawazo
“Mbona umezama katika
mawazo ghafla?akauliza
Peniela
“Kuna kitu
nimekumbuka nitakueleza
siku nyingine.Vipi kuhusu
watoto wako uliozaa na
Mathew wako wapi?
“Mimi na Mathew
tumezaa watoto wawili na
wote wako masomoni
Canada.Unatamani
kuwaona?
“Nina hamu sana ya
kuonana nao.Unadhani
watanikubali?Unadhani
ninaweza kuvaa viatu vya
baba yao? Akauliza
Nahum.Peniela akamtazama
na kutabasamu
“Hakuna atakayeweza
kuvaa viatu vya Mathew.Ni
mwanaume wa pekee kabisa
ambaye mguu wake ni
mkubwa na kila
atakayejaribu kuvaa viatu
vyake vitampwaya.Mathew
atabaki kuwa Mathew”
akasema Peniela
“Kwa kunitazama
unadhani ninaweza kuwa na
asilimia ngapi ya
Mathew?akauliza Nahum na
Peniela akacheka
“Wewe bado mtoto wa
mama,umekulia katika
utajiri hujui kuhangaika
huwezi kuwa hata na
asilimia moja ya
Mathew.Kidogo labda pumzi
ya kitandani lakini hata
hapo bado huwezi kumfikia
Mathew.Yule alikuwa na
mapafu ya farasi.Mwendo
wake si wa kawaida”
akasema Peniela na Nahum
akamrukia
“Kumbe unawapenda
wanaume wenye mapafu ya
farasi basi ngoja nikuonyeshe
kwamba si Mathew pekee
mwenye mapafu ya farasi”
akasema Nahum na kuanza
utundu wake lakini peniela
akamsukuma
“Nahum hatuwezi
kufanya saa hizi tunatakiwa
kwenda katika kikao cha
bodi leo kujadili kuhusiana
na ule mradi wa mvinyo
tunaotaka kuanzisha”
Peniela alipogusia
masuala ya bodi Nahum
akapatwa na mstuko
mkubwa
“Peniela kwa nini
tusiahirishe kikao hicho hadi
siku nyingine?Leo ninataka
nipate muda mwingi wa
kuwa nawe au wewe hupendi
tupate muda wa kutosha wa
kuwa pamoja?Kama ni
miradi tutafanya tu.Wewe ni
bilionea mimi ni bilionea
hivyo hatuna shida na
pesa.Maisha haya ni mafupi
sana kwa kuwa tayari tunazo
pesa basi tujipe muda wa
kutosha wa sisi
kufurahi.Hakuna anayejua
kesho yake.Sitaki itokee
nimekufa halafu huko niliko
nijilaumu kwa nini
sikutumia muda wangu
vizuri na Peniela” akasema
Nahum na Peniela
akatabasamu
“Unataka kikao kifanyike
lini?
“Baada ya siku nne
kutoka sasa”
“Siu nne?
“Ndiyo.Nataka siku hizi
zote niwe nawe tukistarehe
tu.Peniela maisha haya ni
mafupi sana huwezi kujua
nini kinaweza kutokea kesho
hivyo basi tutumie vyema
muda tunaoupata” akasema
Nahum na kumvuta Peniela
akambusu na kuanza utundu
wake haukupita muda kipute
kikaanza.
****************
Jopo la madaktari
bingwa wa upasuaji wa
plastiki lilikamilisha
upasuaji wa kubadili
muonekano wa Theresia
Muganza kwa mafanikio
makubwa.Upasuaji huu
ulifanyika kwa siri kubwa
katika hospitali moja kubwa
ya jeshi na baada ya upasuaji
kukamilika Theresa
alihamishiwa katika jumba
moja kubwa linalomilikiwa
na Rais wa Ufaransa kwa
ajili ya mapumziko.Kwa ajili
ya Theresa jumba hilo
liliwekwa vifaa mbali mbali
vya matibabu ambavyo
vingehitajika wakati wa
kumuuguza na madaktari
waliendelea kukaa karibu na
Theresa kumuhudumia.Kazi
yao haikuwa imekamilika
bado hadi pale ambapo
bandeji alizofungwa katika
sehemu mbali mbali za
mwili wake
zitakapoondolewa ndipo kazi
yao itakapokuwa
imekamilika.
TEL AVIV – ISRAEL
Ni siku ya pili tangu
Mathew Mulumbi aginizwe
katika chumba alimo Ammar
Nazari kiongozi wa kundi la
wanamgambo la Ammar
Nazar Brigades.Toka
ameingia ndani ya chumba
kile Mathew hakufungua
mdomo wake kutamka hata
neno moja.Licha ya kutotaka
kuzungumza Mathew
hakuweka kitu chochote
mdomoni.Hali ile ilimtisha
sana Ammar ambaye
alijitahidi kwa kila namna
kumsaidia Mathew aweze
kula lakini
ilishindikana.Mathew
Mulumbi alianza kutetemeka
mwili ikamlazimu Ammar
kubonyeza kitufe
kilichokuwa karibu na
mlango na mara wakafika
askari sita.
“Kuna nini
humu?akauliza mmoja wa
askari wa gereza
“Huyu mtu ameletwa
humu ndani ni siku ya pili
leo hazungumzi wala hataki
kula chakula wala kunywa
chochote.Hali yake inazidi
kuwa mbaya.Anahitaji
msaada anaweza akapoteza
maisha” akasema
Ammar.Mlango ule mkubwa
ukafunguliwa askari
wakaingia ndani na
kumuinua Mathew Mulumbi
wakambeba wakamtoa mle
ndani mlango ukafungwa
“Ni nani Yule mtu?Ni
mtu wa ajabu sana
Yule.Toka ameletwa humu
ndani hajafungua mdomo
wake kutamka
chochote,hataki kula wala
kunywa.Nini hasa lengo
lake?Anataka
kufa?Anaonekana amekata
tamaa kabisa hasa kutokana
na mateso makali
aliyoyapata.Ameteswa
mno.Ana vidonda kila
sehemu ya mwili
wake.Nahisi kuna jambo
kubwa amelifanya
lililompelekea akateswa kiasi
kile.Hata hivyo anaonekana
ni mtu jasiri sana.Natamani
kumjua zaidi” akawaza
Ammar
Mathew baada ya
kutolewa mle chumbani
akapelekwa moja kwa moja
katika hospitali ya
gereza,hali yake haikuwa
nzuri kutokana na kukosa
nguvu.Haraka haraka
akaanza
kuhudumiwa.Efraim Dagan
alikuwepo pale hospitali
kuhakikisha kila kitu kina
kwenda vizuri kwa mujibu
wa mpango wao.
Baada ya saa tatu
Mathew tayari alikuwa
anajihisi vizuri akatolewa
ndani ya kile chumba
akapelekwa katika ofisi ya
mkuu wa gereza ambako
alimkuta Efraim dagan na
watu wengine watatu
“Hongera Mathew kazi
nzuri sana.Tumefuatilia kwa
makini toka ulipoingia mle
ndani ya kile chumba na
mpaka sasa kila kitu
kimekwenda vizuri” akasema
Efraim
“Nimekuwa nikimsoma
Ammar anaonekana ni mtu
ambaye anataka sana
kunifahamu nimetoka wapi
na nimefanya nini.Amekuwa
akiniuliza maswali kila mara
kuhusu hilo na kubwa zaidi
alichotaka kufahamu ni
kama nimeua
muisrael.Nadhani sintapata
ugumu kujenga naye urafiki”
akasema Mathew
“Tumemaliza awamu ya
kwanza na sasa tunaingia
awamu ya pili ambayo ni
kujenga urafiki na Ammar
halafu kutoroka
gerezani.Mpango wa
kutoroka gerezani
unaadaliwa na kabla ya
kukueleza namna
utakavyotoroka hapa
gerezani na Ammar tunataka
kwanza kujiridhisha kwamba
urafiki madhubuti kati yako
na Amar
umejengeka.Tukijiridhisha
kuwa Ammar yuko tayari
kutoroka gerezani
tutakuwekea kitu Fulani
chini ya sahani ya
chakula.Hakikisha kila
unapopewa chakula
unapitisha mkono chini ya
sahani na utakapokuta kuna
ktu kimebandikwa chini ya
sahani ya chakula ujue
kwamba muda
umefika.Askari atakayepita
kukusanya vyombo
utamvamia na kutaka
kumshambulia lakini askari
wengine watakudhibiti na
kukutoa mle ndani kisha
utaletwa hapa ofisini na
kuelekezwa namna
utakavyoweza kutoroka pale
gerezani” akasema Efraim
“Mpaka hapa tayari
amekwisha onyesha kutaka
kunifahamu na kuwa karibu
nami.Amekuwa mwema
kwangu na ananionea
huruma.Nitakaporejea kazi
itaanza” akasema Mathew
“Kuwa mwangalifu sana
Mathew,Ammar anaweza
akaonekana ni mtu mwema
machoni lakini ni mtu hatari
sana usimuamini
haraka.Jina utakalotumia ni
Abu Al zalawi,raia wa Kenya
mwenye asili ya Misri.Baba
yako aliitwa
Khalid Al Zalawi.Alikuwa ni
mmoja wa viongozi wa kundi
la Abu Hafs al-Masri
Brigades kundi ambalo
linabeba jina la la muasisi
wake ambaye ni Abu Hafs
kutoka nchini Misri
aliyekuwa na mafungamano
ya kindugu na aliyekuwa
kiongozi wa kundi la Alqaeda
Osama Bin Laden baada ya
binti yake kuolewa na mtoto
wa Osama.Baba yako Khalid
aliuawa na majeshi ya Israel
na toka hapo umekuwa
ukiendesha mashambulio
dhidi ya Israel sehemu mbali
mbali duniani.Mama yako
alifariki angali u mdogo na
aliitwa Dalia.Picha yako
itawekwa katika orodha ya
watu wanaotafutwa sana na
Israel na maelezo hayo
niliyokupa ndiyo
yatakayoambatana na picha
yako.Tunaamini watataka
kukufahamu wewe ni
nani,utawapa maelezo hayo
na lazima watataka
kuthibitisha taarifa
utakazowapa hivyo
wakitafuta watakutana na
hayo maelezo kwamba wewe
ni mtu hatari unayetafutwa
na Israel.Makazi yako
yatakuwa ni Nairobi Kenya
na hapa unatakiwa uwe
unazifahamu vyema sehemu
mbali mbali za jiji la Nairobi
kwani wanaweza pia
wakataka kufahamu mahala
unapoishi Nairobi.Nadhani
umenielewa Mathew”
akasema Efraim
“Nimekuelewa
Efraim”akajibu Mathew
“Mathew kwa kukubali
kufanya hivi jina lako
linaingia katika orodha ya
magaidi lakini ni kwa muda
tu hivyo usiwe na wasi wasi
wowote.Baada ya kumaliza
kazi yako tutakuondoa
kutoka katika orodha hiyo”
“Sina tatizo na hilo”
akajibu
Mathew.Wakaendelea
kuelekezana halafu Mathew
akaachwa apumzike.
Alipumzika kwa saa tatu
halafu akarejeshwa ndani ya
kile chumba alimo Ammar
Nazar.Mlango wa chumba
cha Ammar ulipofunguliwa
Mathew akapigwa teke la
mgongo na askari
akaangukia ndani kisha
mlango ukafungwa.Mathew
alijibamiza ukutani na
kuanguka chini.Amar
aliyekuwa kitandani
akainuka haraka na kwenda
kumuinua.
“hal tadhit?(Umeumia?)
akauliza Ammar na
kumsaidia Mathew
kukaa.Alikuwa ameumia
usoni baada ya kujibamiza
ukutani na damu ilikuwa
inamtoka.Ammar akachukua
kitambaa akamsaidia
Mathew kufuta damu usoni.
“aqad yudhik
kathirana(wamekuumiza
sana hawa jamaa) akasema
Ammar akiendelea kumfuta
Mathew damu.
“khudh raha (pumzika)
akasema Ammar
“shukraan
jazilaan(nashukuru)
akasema Mathew na Ammar
akatabasamu
“alhamd lilh.hal tastatie
altahaduth
bialearabia?(Ahsante
Mungu.Unaweza
kuzungumza kiarabu?
“nem fielaan(Ndiyo)
akajibu Mathew na
tabasamu kubwa likajengeka
usoni kwa Ammar
“Vipi hali yako kwa
sasa?akauliza Ammar kwa
kiarabu
“Kwa sasa ninaendelea
vizuri” akajibu Mathew kwa
kiarabu safi
“Hali yako ilinitisha
sana.Kwa nini ulitaka kujiua
kwa kukataa kula?akauliza
Ammar
“Nimekuwa hapa kwa
miaka mitatu nikiteswa kila
uchao na hakukuwa na dalili
zozote za mimi kutoka hapa
ndiyo maana niliona ni bora
nife niepukane na mateso
haya.Tazama mwili wangu
kila sehemu ni vidonda
vitupu” akasema Mathew
“Sikiliza ndugu yangu
mimi nina miaka mitano
nimefungwa hapa katika
gereza hili.Wapo wengine
wana miaka zaidi ya kumi
lakini hata siku moja
hawajakata tamaa.Bado tuna
matumaini kwamba siku
moja tutatoka hapa na
kuendeleza
mapambano.Hatutakata
tamaa kuendelea kupambana
kwa ajili ya ardhi
yetu.Yawezekana sisi
tukaishia njiani na tusiuone
ushindi lakini kwa sababu ya
mapambano yetu ya leo na
kutokukata tamaa watoto wa
watoto wetu wanaweza
wakayaona matunda ya
mapambano yetu pale ardhi
yetu itakapokuwa
imerejeshwa.Gereza hili
limejaa mateso.Tunateswa
mno lakini hakuna ambaye
amewahi kusalimu amri
kwao.Japokuwa sisi tuko
ndani lakini huko nje
naamini mapambano
yanaendelea.Nimekueleza
haya ili kukupa moyo
kwamba usikate tamaa kwa
kile unachokiamini” akasema
Ammar na Mathew akatikisa
kichwa kukubaliana naye
“Kwa nini uko hapa?Kwa
nini wanakutesa namna hii?
Akauliza Ammar
“Naitwa Abu Al
Zarawi.Ni mtoto wa Khalid
Al Zalawi kutokea
Misri.Baba yangu alikuwa ni
kamanda wa ngazi za juu
katika kundi linaloitwa Abu
Hafs al – Masri Brigades
kundi ambalo muasisi wake
ni Mohammed Atef au kwa
jina maarufu Abu Hafs
ambaye alikuwa
mwanachama wa kundi la
Ayman al-Zawahiri’s al-
Jihad.”
“Ninamhamu Ayman al-
Zawahiri mmoja wa viongozi
wakubwa kabisa wa
Alqaeda.Anatajwa ndiye
aliyeratibu mashambulio
mawili ya mabomu katika
balozi za Marekani nchini
Tanzania na Kenya.Kwa sasa
ndiye aliyechukua nafasi ya
Osama Bin Laden baada ya
Marekani kumuua” akasema
Ammar na Mathew
akaendelea
“Baba yangu Khalid al-
Zalawi aliuawa na majeshi
ya Israel na ndipo nilipoapa
kulipiza kisasi kwa kuua
waisrael kokote waliko
duniani.Nilikwenda nchini
Kenya nikiwa la lengo la
kuanzisha kikundi cha
kijihad.Nikiwa Kenya
nilimuua mkuu wa Mosad
Afrika Mashariki alikuwa
anaitwa Avi Abramson.Si
huyo tu bali niliwaua pia
majasusi wengine wawili wa
Mossad na hapo ndipo
nilipoanza kusakwa na Israel
hadi waliponikamata na
kunileta hapa”akasema
Mathew na tabasamu kubwa
likaonekana usoni kwa
Ammar
“Kumbe wewe ni
mwenzetu.Nilijuliza sana
sababu ya wewe kuteswa
namna hii nikahisi kwa
mateso haya unayoyapata
lazima utakuwa umefanya
jambo kubwa na ili upate
mateso makubwa kama haya
lazima uwe umeua
waisrael”akasema Ammar
“Nilimuua mtu wao
muhimu sana na
wameniwinda kwa muda
mrefu hadi wakanikamata”
“Ilikuaje
wakakukamata?akauliza
Ammar
“Kuna rafiki yangu
anaitwa Rashid yeye ni
mfuasi wa IS aliniomba
niungane nao katika
mabadilishano ya mateka na
watanzania ambao walikuwa
wanamshikilia mtu mmoja
aliyeitwa Edger Kaka
ambaye ana mahusiano na
Habiba Jawad” akasema
Mathew na sura ya Ammar
ikaonyesha mstuko
“Habiba Jawad?
“Ndiyo.Unamfahamu?ak
auliza Mathew
“Ndiyo ninamfahamu”
“Basi kuna mtu ambaye
ana mahusiano naye ya
karibu anaitwa Edger Kaka
ambaye alikuwa
anashikiliwa nchini
Tanzania alitakiwa
kufanyiwa mabadilishano na
watu wawili waliokuwa
wametekwa na IS.Tukiwa
katika mabadilishano hayo
ya mateka tulivamiwa na
vikosi vya Israel na
wakaniteka wakanileta
huku.Pamoja nami
alikuwepo pia Edger Kaka
ambaye ana mahusiano na
Habiba Jawad” akasema
Mathew
“Ninafurahi kukufahamu
Abu Zalawi.Mimi ninaitwa
Ammar al-Nazari.Ni kiongozi
wa kundi linaitwa Ammar
Nazari brigades.Lengo la
kundi hili ni kuendeleza
mapambano ya kudai ardhi
yetu inayokaliwa kimabavu
na Israel.Tumekuwa
tukifanya mashambulio
nchini Israel na
tumefanikiwa kuua waisrael
wengi.Pamoja na mimi
kuwepo hapa lakini bado
kundi langu pamoja na
makundi mengine
yanaendelea na mapambano
ya kudai haki yetu na nina
uhakika mkubwa iko siku
hata kama mimi na
wenzangu hatutatoka humu
basi lazima haki yetu
itapatikana” akasema
Ammar
Waliendelea na
mazungumzo halafu Ammar
akauliza
“Huyo mtu ambaye
unadai ana mahusiano na
Habiba Jawad yuko wapi?
“Sifahamu yuko wapi
kwani nilipofumbua macho
nilijikuta sehemu yenye giza
na nimeishi mahala hapo
nikiteswa kwa miaka mitatu
hivyo sifahamu mahala alipo
Edger Kaka.Unadhani
wanaweza kuwa wamemuua?
“Sina hakika kama
wanaweza wakamuua.Israel
wanamtafuta sana Habiba
Jawad lakini bado
hawajafanikiwa kumpata
mpaka leo hii ndiyo maana
wakamteka huyo mtu
mwenye mahusiano na
Habiba”
“Ni nani huyo Habiba
Jawad? Mathew akauliza
“Ni mtu muhimu sana
katika harakati zetu.Ni tajiri
mkubwa sana na ambaye
ndiye anawezesha harakati
nyingi za vikundi mbali
mbali kufanyika.Naweza
kusema yeye ndiye uti wa
mgongo wa vikundi vingi
vinavyoendesha mapambano
dhidi ya udhalimu wa Israel”
akasema Ammar
“Natamani siku moja
ningekutana naye nimueleze
kuhusiana na mtu wake
Edger Kaka.Yawezekana
haujui mahala alipo kwani ni
miaka mitatu imepita sasa
tangu tulipotekwa”
“Habiba si mtu wa
kuonekana kirahisi.Kama
tungekuwa nje ya gereza
ningeweza kukusaidia
ukaonana naye lakini ni
mchakato mrefu hadi
kumfikia”akasema Ammar
na ukimya wa dakika kadhaa
ukapita Mathew akasema
“Ammar mimi sina lengo
la kuendelea kukaa humu
gerezani”
“Umekata tamaa
kuendelea
kupambana?akauliza Ammar
“Hapana sijakata tamaa
lakini siwezi kuendelea
kukaa humu ndani ya gereza
nikiteseka lazima nitafute
namna ya kutoka humu”
akasema Mathew na Ammar
akaangua kicheko
“Abu gereza hili ni moja
ya gereza lenye ulinzi mkali
sana.Hajawahi kutoroka mtu
hapa kutokana na ulinzi
uliopo.Hizo ndoto achana
nazo kwani utakufa kabla
haujatimiza lengo
lako.Endelea kusali
kumuomba Mungu anaweza
akafungua njia na tukatoka
lakini suala la kutoroka
usiliweke kichwani
mwako.Unadhani watu
wangu wangeshindwa kuja
kunikomboa?Lakini
hawawezi kutokana na ulinzi
wa mahala hapa” akasema
Ammar
“Ngoja nikueleze
ukweli.Baada ya kutolewa
kule kwenye giza nililetwa
humu na kwa muda wa siku
mbili sikuweza kuzungumza
nawe chochote pia sikula
wala kunywa.Si kwamba
nilikuwa nimedhamiria kufa
kama ulivyodhani bali ule
ulikuwa ni mpango maalum”
“Mpango
maalum?akauliza Ammar
“Ulikuwa ni mpango
maalum ili niweze kutoka
humu ndani na kupelekwa
hospitali.Kuna mitu nilihitaji
kuonana naye”
“Ulikuwa unahitaji
kuonan na mtu?Kwa
dhumuni gani?akauliza
Ammar huku akijiweka
vizuri
“Ni kwa ajili ya mpango
wangu wa kutoroka”
akasema Mathew
“Abu nakushauri tena
mpango huo wa kutoroka
achana nao utapoteza
maisha bure.Tumuombe
Mungu atatufungulia
milango na siku moja
tutatoka humu”
“Israel wametumia
gharama kubwa kutusaka
hivyo hawawezi kutuacha
huru.Tutafia
humu.Nitajaribu mpango
wangu wa kutoroka na kama
nikifa nitakuwa nimekufa
kishujaa” akasema Mathew
“Abu una familia?
“Wakati ninakamatwa
nilikuwa na mchumba ni
mrembo sana anaitwa Nawal
lakini mpaka sasa hajui
mahala nilipo.Ninampenda
sana na yeye ni moja ya
sababu za mimi kutaka
kutoroka humu gerezani”
“Nawal? Ammar
akashangaa
“Ndiyo.Kwa nini mbona
umestuka?
“Mke wangu mdogo pia
anaitwa Nawal.Imekuwa
bahati wote tuna wapenzi
wenye majina
yanayofanana.Abu kama
kweli unampenda huyo
mchumba wako Nawal
naomba unisikie
tafadhali.Usijaribu
kutoroka.Ukombozi
utakuja.Iko siku tutatoka
humu gerezani na kwenda
kukutana naye tena”
“Ammar tazama
nilivyoteseka.Tazama mwili
wangu wote una
vidonda.Imetosha na sitaki
kuendelea tena.Nataka
kujaribu kutoroka hapa
gerezani.Ninataka
nikaendeleze mapambano
huko nje.Yawezekana siku
moja nikaja kukukomboa
hapa gerezani” akasema
Mathew
“Abu unajiamini vipi
kama kweli utafanikiwa
mpango wako wa
kutoroka?Ammar akauliza
“Sijui kama nitafanikiwa
lakini lazima nijaribu.Siwezi
kukaa humu ndani kusubiri
muujiza.Hakuna muujiza
utakaotokea hapa lazima
nipambane mwenyewe”
akasema Mathew na wote
wakabaki kimya.Ammar
alionekana kuzama
mawazoni.Mathew akapanda
kitandani akajilaza
“Tayari nimerusha
ndoano na anaonekana
kutaka kuisogelea.Atanasa
tu na nitamuondoa
humu.Ameniamini kwa
haraka sana baada ya
kusikia kwamba nimeua
waisrael.Nitakapomtoa
humu huyu ndiye
atakayenipeleka kwa Habiba
Jawad kwani amekiri
mwenyewe kwamba
anamfahamu.Nitakwenda
kuukata uti wa mgongo wa
ugaidi duniani.Wengi
wanawafahamu magaidi
wakubwa kama akina
Osama,Ayman al-Zawahiri
na wengine wengi waliouawa
na walio hai lakini hawajui
watu hawa wanatoa wapi
nguvu na uwezo wa
kuendesha makundi
makubwa ya kigaidi na
kupanga mashambulizi ya
kigaidi.Yote haya
yanawezeshwa na watu
kama akina Habiba ambao
wanatumia utajiri wao
katika kufadhili makundi ya
kigaidi.Haitakuwa kazi
nyepesi lakini Mungu
atanitangulia na
nitafanikisha
kumuondoa.Kikubwa ni huyu
jamaa Ammar lazima anase
katika ndoano yangu.Huyu
ndiye njia ya kunifikisha kwa
Habiba Jawad” akawaza
Mathew.
Ammar alifungua kitabu
alichokuwa nacho akasoma
halafu akainua kichwa
akamtazama Mathew
“Abu ni kweli
umedhamiria kutaka
kutoroka?akauliza Ammar
“Tayari anaelekea
kwenye ndoano” akawaza
Mathew
“Ndiyo Ammar.lazima
nijaribu.Siwezi kuendelea
kukaa humu
ndani.Nimeumizwa sana na
lazima nikalipe kisasi.Hii ni
vita lazima
nipambane.Siogopi
kufa.Tumekwisha poteza
watu wengi katika haya
mapambano wengine ni wa
muhimu sana hivyo siogopi
chochote.Sisi kama viongozi
wa mapambano haya lazima
tuonyeshe njia kwa
tunaowaongoza kwamba
tunapaswa kuendelea
kupambana kwa kile
tunachokitafuta hata kama
ikilazimu kutoa uhai
wetu.Mimi nitaondoka hapa
gerezani kama nikishindwa
nitakufa nikiwa nimejaribu”
akasema Mathew baada ya
sekunde chake Ammar
akauliza
“Umepanga kutoroka
vipi? Akauliza
Ammar.Mathew hakumjibu
“Abu tayari unao mpango
wowote wa kukuwezesha
kutoroka?akauliza tena
“Ammar kwa kuwa wewe
ni mwenzangu ntakueleza
ukweli.Toka nilipoletwa hapa
nilikuwa ninatafuta namna
ya kuweza kutoroka ndipo
nikakutana na daktari moja
anaitwa Abeba anatothea
Ethiopia anafanya kazi
katika hospitali ya
gereza.Nilipelekwa hospitali
nikiwa sijitambui
akanihudumia nikapata
nafuu alinionea huruma sana
na akaahidi kunisaidia
kutoroka.Alisema
ananiandalia mpango wa
kutoroka na utakapokuwa
tayari atanijulisha”
“Anakuandalia mpango
gani? Akauliza Ammar
“Ananiandalia ramani ya
gereza na njia za kupita ili
niweze kufanikiwa
kutoroka.Nilipoletwa hapa
chumbani kwako nilikuwa
natafuta namna ya kuweza
kuonana tena na Abeba nijue
amefikia wapi kuhusu
ramani ile aliyokuwa
ananiandalia ndiyo maana
nikatumia njia ile ya kugoma
kula chakula ili nipelekwe
hospitali na mpango wangu
ulifanikiwa nilionana na
Abeba akanieleza kwamba
ndani ya siku tatu niende
tena hospitali atakuwa
amefanikisha kuipata
ramani hiyo.Nina uhakika
nikiipata na kujua njia za
kupita nitaondoka hapa
gerezani” akasema Mathew
“Huyo Abeba imekuwaje
hadi akaamua kukusaidia
kutoroka?Haogopi
kugundulika? Akauliza
Ammar
“Mimi ndiye
niliyemuomba anisaidie
niweze kutoroka hapa
gerezani.Alinionea huruma
kwa mateso niliyokuwa
nayapata akaahidi kuisaidia”
“Una uhakika
atakusaidia au anakuweka
katika mtego?
“Nina uhakika
atanisaidia”
“Unamuamini vipi?
“Ninao uwezo wa
kumsoma mtu kama ana
maanisha anachokisema au
ananidanganya na kwa
Abeba nina uhakika
anamaanisha anachokisema”
akasema Mathew.Zilipita
dakika tatu za ukimya halafu
Ammar akauliza
“Endapo mpango wako
wa kutoroka utafanikiwa
utakwenda wapi?
“Bado sijajua nitaelekea
wapi lakini nitakapokuwa
nimetoka nje ya gereza
nitajua nielekee wapi.Nina
mpango wa kujiunga na
kikundi kimoja wapo cha
jihad niendeleze mapambano
dhidi ya Israel.Sina mpango
wa kurejea tena Kenya
kwani hawa jamaa
watanifuata kule”akasema
Mathew na kukawa
kimya.Ammar akaendelea
kusoma kitabu chake.
DAR ES SALAAM -
TANZANIA
Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr
Fabian Kelelo alipomaliza
kikao na wageni wake
waliofika kumtembelea
akarejea ofisini kwake na
kumpigia simu Benjamin
Hudson balozi wa umoja wa
ulaya nchini Tanzania
“Mheshimiwa Rais
habari za muda
huu?akauliza Balozi
Benjamini baada ya kupokea
simu
“Habari nzuri
mheshimiwa balozi”
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais kwa
kunipigia simu ninategemea
ni kuhusiana na lile suala
tulilozungumza asubuhi”
“Ni kweli ni kuhusiana
na lile suala.Mheshimiwa
balozi nimekupigia
kukujulisha kwamba
msimamo wangu
haujabadilika bado ni ule ule
kwamba hakuna mchunguzi
yeyote wa kimataifa
atakayeruhusiwa kuingia
nchini kufanya uchunguzi wa
mauaji ya Lucy na Laurent
Muganza.Uchunguzi
utafanywa na vyombo vya
ndani na vitatoa taarifa kwa
hiyo naomba ufikishe ujumbe
huo kwa umoja wa Ulaya”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
ninashukuru kwa majibu
hayo na nitayafikisha
sehemu husika kama
yalivyo”
“Kingine mheshimiwa
balozi nakuomba usithubutu
kuendelea kufanya mambo
yasiyokuhusu.Endapo
utarudia tena kufanya
mambo yaliyo nje ya
majukumu yako
nitakufukuza nchini”
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais na ahsante
sana kwa ushirikiano wako”
akasema balozi Benjamin na
Dr Fabian akakata simu
Dakika ishirini baada ya
kuzungumza na balozi
Benjamin simuni,akaingia
ofisini mkurugenzi wa
mawasiliano ya Rais akiwa
na kompyuta ndogo
“Mheshimiwa Rais kuna
jambo ambalo nadhani
unapaswa kulijua” akasema
na kumuonyesha Rais
ujumbe wa twitter
aliouandika balozi
Benjamin.Katika ujumbe
wake Benjamin aliwaonya
watu wanaotoka nchi za
umoja wa Ulaya kuchukua
tahadhari kubwa wawapo
nchini Tanzania na
kuwataka wale wanaopanga
kuja Tanzania kutafakari
mara mbili
“Mshenzi huyu !!
akasema kwa hasira Dr
Fabian na kugonga meza.
“Si huyu peke yake
aliyefanya hivi bali hata Rais
wa Ufaransa Michael Weren
naye ameandika katika
ukurasa wake” akasema
mkurugenzi Yule wa
mawasiliano wa rais.Rais
Michael yeye aliwaonya raia
wa Ufaransa wanaotembelea
Afrika mashariki akawataka
wawe waangalifu sana
kutokana na hali ya usalama
kutokuwa ya kuridhisha.
“Tunafanya nini kuhusu
kauli hizi mheshimiwa rais?
“Kwa sasa hatufanyi
chochote.Nipe muda kidogo
wa kufikiria nini cha
kufanya” akasema Dr
Fabian na kuegemea kiti
chake
“Dr Evans alikuwa sahihi
kwamba tunaingia vitani na
tayari vita imeanza.Kauli
hizi mbili za balozi wa umoja
wa Ulaya hapa nchini na ya
rais wa Ufaransa zote
zinalenga kuitangazia dunia
kwamba Tanzania si mahala
salama kutembelea wala si
mahala salama
kuwekeza.Idadi ya watalii
itapungua sana na
tutapoteza fedha nyingi za
kigeni,mapato ya nchi
yatapungua kwani utalii
unaingizia nchi fedha nyingi
sana.Kushuka kwa mapato
ya serikali ni chanzo cha
miradi mingi ya maendeleo
kushindwa
kutekelezeka,huduma za
kijamii kuzorota na uchumi
kushuka.Hicho ndicho
wanachokitaka hawa jamaa
kutudidimiza kiuchumi na
tuone kwamba hatuwezi
kupiga hatua bila wao”
akawaza Dr Fabian
“Vita ya uchumi kama
alivyosema Dr Evans ni vita
mbaya sana na kupigana
kwake hakuhitaji mabavu.Ni
akili nyingi inapaswa
kutumika.Kwa sasa
hatutawajibu chochote
kufuatia kauli zao
walizozitoo katika
mitandao.Tutakaa kimya
huku tukijipanga namna
bora ya kuweza kukabiliana
na misuko suko mikubwa
inayokuja mbeleni.Kitu
kikubwa kwa sasa ni
kumfuatilia balozi Benjamin
kufahamu nyendo
zake.Nataka kujua
anashirikiana na akina nani
hapa nchini.Naamini hayuko
peke yake bali kuna watu
anaoshirikiana nao ambao
walimpa taarifa zile za
Tanzania kumiliki aina ya
bunduki za udunguzi ambazo
zinadhaniwa ndizo
zilitumika kuwaua Lucy na
Laurent
Muganza.Namshukuru Dr
Evans kwa kunishauri
vyema kwani bila ushauri
wake hivi sasa tayari
ningekwisha mtimua nchini
Yule balozi.Ngoja niwe
mvumilivu niusome mchezo
huu unakwendaje sitakiwi
kwenda kichwa
kichwa….”akawaza Dr
Fabian
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 3
Saa moja za jioni Austin
January aliwasili ikulu kama
alivyokuwa ametakiwa na
rais.Kabla ya kupata chakula
wakaelekea sehemu ya
mapumziko ambako Rais
alikuwa na mazungumzo na
Austin.
“Austin karibu tena
ikulu.Mahala hapa utafika
mara nyingi sana wakati wa
uongozi wangu na tafadhali
usichoke” akasema Dr Evans
“Siwezi kuchoka
mheshimiwa Rais ni heshima
kubwa kwangu kuwepo
hapa”akajibu Austin
“Austin nilikueleza awali
kwamba wewe utakuwa
msiri wangu na
nitakushirikisha katika
mambo makubwa ya nchi na
ninaamini kwamba yale yote
ambayo mimi nitakuamini
kwayo yatabaki kifuani
kwako na utakwenda nayo
kaburini”
“Mheshimiwa Rais usiwe
na shaka kabisa na
mimi.Nimeapa kutunza siri
utakazonieleza na
ninakuahdi kila
nitakachoona kusikia au
kutenda nitakwenda nacho
kaburini.Si mimi tu bali na
timu nzima ninayoshirikiana
nayo katika kazi mbali mbali
utakazotupa”
“By the way
wanaendeleaje
wenzako?Natamani sana
kukutana nao nitapanga
muda niwaalike tukutane
tufahamiane.Fikisha salamu
zangu nyingi kwao”
“Nitafikisha mheshimiwa
rais”
“Mapema leo asubuhi
alinitembelea balozi wa
umoja wa Ulaya hapa nchini
anaitwa Benjamin
Hudson.Aliniletea ujumbe
kutoka umoja wa Ulaya na
ujumbe huo unanitaka
niwaruhusu wachunguzi wa
kimataifa kuja kufanya
uchunguzi wa vifo vya
Laurent na Lucy
Muganza.Vifo vya watu hawa
wawili vimewastua na
wanahaha hawajui la
kufanya na hii inadhihirsha
wazi kwamba walikuwa ni
watu wao wa muhimu sana
na walikuwa na mipango nao
mikubwa.Lauret Muganza
alikuwa ni mfanyakazi
katika umoja wa Ulaya hivyo
wanatumia kigezo hicho
kulazimisha turuhusu
wachunguzi wa kimataifa
wakidai eti kuna mpango wa
siri wa kuwadhuru maafisa
kutoka umoja wa Ulaya
hivyo wanataka kujua nani
aliyemuua Laurent.Nilikataa
kwamba hatuwezi kuruhusu
wachunguzi wa kimataifa
kwa kuwa suala hilo
linachunguzwa na vyombo
vya ndani.Baada ya
kuonyesha msimamo wangu
wa kutotaka kuwaruhusu
wachunguzi kutoka nje
akanieleza sababu kubwa
inayowafanya watake kuleta
watu wao kuja kufanya
uchunguzi.Akanionyesha
taarifa mbili moja ni taarifa
ya awali ya polisi kuhusiana
na tukio lile na nyingine ni
taarifa ya daktari baada ya
miili kufanyiwa
uchunguzi.Taarifa ya polisi
ilionyesha kwamba tukio lile
lilikuwa ni la kijambazi na
watu kadhaa waliuawa
kuhusiana na tukio hilo
lakini risasi zilizokutwa
katika miili ya marehemu
haziendani na silaha
walizokutwa nao hao
majambazi.Risasi
zilizokutwa katika miili ya
marehemu ni za bunduki za
hali ya juu sana
zinazotumiwa na wadunguaji
ambazo majambazi wale
hawakuwa nazo.Alienda
mbali zaidi na kunieleza
kwamba Tanzania tunamiliki
bunduki za aina hiyo
tulizinunua kutoka
marekani.Nilistuka na
kukasirika kwa balozi huyu
kuanza kufanya mambo
yasiyomuhusu kama
kufuatilia kuhusu silaha
tunazomiliki kama
nchi.Nilitamani kumtimua
nchini lakini nikapata wazo
kwamba yeye peke yake
asingeweza kuipata taarifa
nyeti kama ile lazima kuna
watu anaoshirikiana nao
hapa nchini.Kama
nikimtimua hatutaweza
kuwafahamu watu
wanaoshirikiana
naye.Tulifanya kosa dogo
katika operesheni ile
kwamba baada tu ya
kuwamaliza akina Lucy
hatukuwa na wazo kwamba
miili ile ingefanyiwa
uchunguzi hata hivyo kosa
hilo dogo limetusaidia katika
kufahamu kuwa tuna
wasaliti humu nchini ambao
wamekuwa wakishirikiana
na hawa watu”akasema Dr
Fabian na kunyamaza
akamtazama Austin
“Nakubali mheshimiwa
Rais tulifanya kosa hilo
dogo.Hatukuwa na wazo la
kuendelea kufuatilia zaidi
baada ya kumuua Lucy na
hatukujua kama lingechukua
sura mpya namna
hii.Tusamehe sana
mheshimiwa Rais”
“Usijali Austin.Hata
mimi mwenyewe sikuwa
nikifikiria kitu kama hicho
lakini kwa kuwa lengo kuu
ambalo ni kumuua Lucy
lilitimia hakuna
tatizo.Mchana wa leo
nilimpigia tena simu balozi
nikarudia kumuhakikishia
kwamba hakuna mchunguzi
wa kimataifa
atakayeruhusiwa kuingia
nchini.Muda mfupi baadae
katika ukurasa wake wa
twitter balozi aliandika
ujumbe wa kuwaonya watu
kutoka jumuiya ya Ulaya
wanaotembelea Tanzania
kuwa makini.Si yeye peke
yake bali hata Rais wa
Ufaransa aliandika pia
ujumbe wa twitter akiwataka
raia wa Ufaransa
wanaotembelea Afrika
Mashariki kuwa makini kwa
sababu za kiusalama.Jumbe
hizi mbili zinalenga
kuiaminisha dunia kwamba
Tanzania si mahala salama
kutembelea au hata
kuwekeza.Hii inaweza kuwa
na athari kubwa sana
kiuchumi kwani mapato
yatokanayo na utalii
yatashuka na watu ambao
walitaka kuja kuwekeza
nchini hawatakuja tena”
“Dah ! akasema Austin
“Hii ni vita Austin.Ni
vita ya uchumi.Mataifa haya
makubwa kwa kila namna
yanataka kutudhoofisha
kiuchumi ili tuweze
kuwapigia magoti na
kuwaacha waendelee
kutunyonya.Siko tayari kwa
hilo.Nitaongoza mapambano
haya na nina uhakika
mkubwa tutashinda vita
hii.Hatutashinda kwa
mabomu au vifaru lakini
tutashinda kwa msimamo
wetu.Tunachotakiwa
kufanya kwa sasa kwanza ni
kutambua kuwa tayari tuko
vitani na tunapambana na
mataifa yaliyotuzidi kila
kitu,kiuchumi,kiteknolojia
kijeshi hivyo haitakuwa vita
nyepesi.Kazi ambayo nataka
kuwapa wewe na timu yako
ni kumfuatilia balozi
Benjamin Hudson kila
anachokifanya hapa
nchini.Nataka kujua
anakotoa siri za nchi.Fautilia
mawasiliano yake….”
Akanyamaza baada ya kitu
Fulani kumjia kichwani.
“Mara zote
ninapowasiliana na huyu
balozi hutumia simu ya
mezani ya ofisini kwake au
simu ya mezani ya nyumbani
sifahamu kama ana simu ya
mkononi lakini haya yote ni
sehemu ya kazi yenu ya
kumchunguza.Chunguzeni
kila kitu kuhusu huyu
mtu.Nadhani umenielewa
Austin” akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
nimekuelewa sana na
nimeelewa nini tunatakiwa
kukifanya.Nakutoa wasi
wasi kwamba tutaifanya kazi
hii kwa umakini mkubwa
sana na kujua kila
anachokifanya huyu balozi
na watu wote anaoshirikiana
nao”
“Nafurahi kusikia hivyo
Austin.Hii ni misheni
muhimu sana kwa nchi hivyo
naomba ifanyike kwa
umakini mkubwa
sana.Benjamin anajua
anachokifanya na anafanya
kwa kujiamini sana hivyo
muwe makini mno
mnapomchunguza.Naamini
umeniuelewa vizuri Austin”
“Mheshimiwa Rais
nakutoa tena wasi wasi
kwamba nitalisimamia jambo
hili kwa umakini mkubwa
sana.Itanilazimu kuchukua
likizo ya mwezi mmoja kazini
ili niweze kulishughulikia
suala hili kikamilifu”
“Ahsante Austin
ninakutegemea
sana.Tutakapopata kitu
chochote kutoka katika
uchunguzi huo tutajua nini
kifuate lakini kwa sasa
nguvu kubwa iwekezwe
katika kumfuatilia
Benjamin” akasema Dr
Fabian.
Waliendelea na
mazungumzo kidogo kisha
wakapata chakula na Austin
akaondoka.Alipotoka tu nje
ya ikulu akampigia simu
Gosu Gosu
“Papaa uko wapi?
“Ninaelekea
nyumbani.Leo nimechoka
sana nataka nikapumzike”
“Sawa Papaa ninakuja
hapo nyumbani kwako
nisubiri” akasema Austin
“Rais yuko sahihi
tulifanya kosa kujiamini
kwamba tumemaliza kazi
kumbe tukasahu kama maiti
zile zingeweza kufanyiwa
uchunguzi na kujua ni risasi
za aina gani zilizowaua akina
Lucy.Anyway makosa
madogo madogo kama haya
huwa yanajitokeza kitu cha
muhimu ni kujitahidi kuwa
makini kusitokee tena
makosa yoyote kama
hili.Lakini kwa upande wa
pili kosa tulilolifanya
limemuibua balozi Benjamin
na sasa tunajua
tunapambana na watu wa
aina gani.Kama tungefuatilia
na kuchukua zile risasi
tusingejua kama kuna mtu
ambaye anazo siri za nchi na
hatujui anazipata
wapi.Tutamuonyesha
kwamba Tanzania si nchi ya
mchezo.Wametuzidi kwa kila
kila kitu lakini tutawapa
somo la kujifunza na
hawatathubutu tena
kutuchezea” akawaza Austin
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 4
Baada ya Austin
kuondoka Dr Fabiana
alijihisi mchovu naye
akaelekea chumbani kwake
kujipumzisha.Siku hii
hakutaka hata kutazama
taarifa ya habari.Millen
alimfahamu vyema mumewe
na alijua kuna jambo
linamsumbua hivyo
akamfuata chumbani na
kupanda kitandani akajilaza
pembeni yake akambusu
“Pole sana Fabian.Haya
mambo yatakwisha.Usiumize
mno kichwa chako na
ujipange vizuri namna ya
kukabiliana nao” akasema
Millen
“Tayari unajua
kinachoendelea?akauliza Dr
Fabian
“Ndiyo ninafahamu
kuhusu kauli za balozi
Benjamin na Rais wa
Ufaransa katika mtandao wa
twitter zikiwaonya watu wao
wawe makini wanapokuja
kutembea au kuwekeza
Tanzania kwani hali ya
kiusalama ni mbaya.Hiyo
ndiyo habari kubwa
iliyoviteka vyombo karibu
vyote vya habari
ulimwenguni jioni ya leo”
akasema Millen
“Millen tayari vita
imeanza na hii ni vita ya
kiuchumi.Hii inatajwa kama
vita mbaya na ngumu kuliko
hata vita ya kutumia
silaha.lakini Mungu yuko
nasi na atatupigania
tutashinda”
“Fabian uko sahihi
tutashinda hii vita japo
tutakuwa tumeumizwa sana
kwani kauli zile mbili tu
tayari zina athari kubwa
kiuchumi.Pato litokanalo na
utalii litashuka na mambo
yetu mengi hapa nchini
kushindwa
kufanikiwa”akasema Millen
“Haitaishia hapo Millen
mambo ndiyo kwanza
yameanza na yatakuja mengi
makubwa zaidi ya
hilo.Tutawekewa vikwazo
vya kiuchumi,tutafungiwa
masoko ya bidhaa zetu na
mambo kadha wa kadha ili
mradi kutudhoofisha.Mimi
kama kiongozi wa nchi
ninasema nitapambana
kuhakikisha Tanzania
inasonga mbele na
hatutasalimu amri
kwao.Nitawaeleza wananchi
wangu washikamane
kuipigania nchi yao na umoja
huo ndio utakaotufanya
tushinde vita hii” akasema
Dr Fabian
“Nina wazo Fabian
ambalo linaweza kuwa na
msaada” akasema Millen
“karibu”
“Lengo la kauli zile mbili
zilizotolewa kuhusu usalama
Tanzania ni kuihakikishia
dunia kwamba Tanzania si
salama hivyo watalii na
wawekezaji wasije.Ni vipi
kama ninaweza kuitisha
mkutano mkubwa wa wake
za marais kutoka
ulimwenguni kote na
mkutano huo ukafanyika
hapa Dar es salaam?
“Can you do
that?akauliza Dr Fabian
akainuka na kukaa
“Yes I can.Ninaweza
kuitisha mkutano mkubwa
wa wake za marais duniani
na ukafanyika hapa Dar es
salaam.Ni gharama kubwa
itatumika lakini hii itasaidia
kuuonyesha ulimwengu
kwamba Tanzania ni sehemu
salama kwani wake za
marais watakuja na
kuondoka salama.Kama
mkutano huo ukifanikiwa
itakuwa ni jibu kwa hao
mabeberu kwamba Tanzania
ni nchi salama na amani
imetamalaki”
“Una akili nyingi sana
Millen.Sina cha kumlipa
Mungu kwa kunipa
mwanamke mwenye upeo
mkubwa kama wewe.Sikuwa
na wazo kama hilo.Ni wazo
kubwa na kama likifanikiwa
itakuwa ni ushindi mkubwa
kwetu.Ahsante kwa hilo
Millen” akasema Dr Fabian
“Sambamba na hilo
nashauri kufanyike kampeni
mbali mbali kama vile za
kutokomeza malaria nchini
ili mradi tu kampeni hizo
ziwe kubwa na za kitaifa na
katika uzinduzi wa kampeni
hizo waalikwe wanamuziki
wakubwa wa kimataifa wa
kutoka Marekani na
kwingineko na yafanyike
matamasha makubwa ya
muziki.Wanamuziki wale
wakubwa wanafuatiliwa
duniani kote na kama
akifanya tamasha Tanzania
basi dunia nzima
watafahamu na huu utakuwa
ni ujumbe kwa dunia
kwamba Tanzania ni nchi
salama.Wapo vijana
waliobobea katika masuala
hayo ya burudani unaweza
ukakaa nao mkajadiliana na
kikubwa ni
kuwawezesha.Hakuna haja
ya kutumia nguvu kubwa
kujibizana na hawa jamaa
sisi tutawajibu kwa namna
nyingine kabisa na dunia
itatuelewa”akasema Millen
“Ahsante sana Millen
kwa mawazo hayo makubwa
na mazuri.Tuanze
kuyafanyia kazi.Japo ni
gharama kubwa lakini kama
yakifanikiwa itakuwa ni
faida kubwa sana kwetu”
“Usihofu kuhusu
gharama kwani jambo
tunalolifanya lina manufaa
makubwa kuliko gharama
tutakazotumia.Hata hivyo
gharama zote zitakuwa chini
ya taasisi yangu na tutaanza
kwa kuwatafuta wafadhili
hasa wa
ndani.Nitazungumza na
wafanya biashara wakubwa
ambao watatumia mkutano
huo kutangaza biashara zao
nao watatusaidia kwa kiasi
kikubwa kufanikisha
mkutano huo.Licha ya
kutumika kuitangazia dunia
kwamba Tanzania ni nchi ya
amani lakini pia mkutano
huo utakuwa na manufaa
kiuchumi.Wanawake hao
hawatakuja peke yao
watakuwa wameambatana
na ujumbe mkubwa.Mahoteli
yetu yatajaa
watu,wajasiriamali watauza
bidhaa zao.Tutapanga vile
vile safari ya kwenda katika
mojawapo ya vivutio vyetu
vilivyopo hapa nchini na
tutatumia fursa hiyo
kutangaza pia utalii wetu na
lengo la hao mabeberu
litakwama kwani watalii
wataendelea kumiminika
kila uchao hapa nchini
kwetu” akasema Millen
“Millen sijui
nikushukuruje kwa mawazo
kama haya.Sikuwahi kabisa
mkufikiria kitu kama hicho”
“Usijali mheshimiwa
Rais niko nyuma yako
nitasimama nawe katika vita
hii na tutashinda.Ukiwa na
tatizo lolote tafadhali
niamini” akasema Millen
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 5
Austin alifika nyumbani
kwa Mathew Mulumbi
ambako kwa sasa anaishi
Gosu Gosu.Alimkuta Gosu
Gosu akimsubiri
akamkaribisha kinywaji
“Kwa muonekano huo
lazima utakuwa umetoka
ikulu” akatania Gosu Gosu
na Austin akaangua kicheko
kikubwa
“Hujakosea Papaa.Ni
kweli nimetoka
ikulu.Niliitwa na Rais”
akasema Austin
“Kila utokapo kuonana
na Rais na ukanitafuta
lazima kunakuwa na
tatizo.Kuna nini leo?akauliza
Gosu Gosu.Austin akaenda
katika friji akachukua bia
baridi akanywa funda
kadhaa halafu akasema
“Kuna tatizo
Papaa.Kwanza katika ile
misheni yetu ya hivi majuzi
kuna kosa dogo tulilifanya”
akasema na Gosu Gposu
aliyekuwa ameishika glasi
akitaka kuipeleka mdomoni
akaiweka chini
‘Tulikosea nini? Akauliza
Gosu Gosu akionekana kuwa
na wasi wasi
“Usiwe na wasi wasi
Papaa.Misheni ilikwenda
vyema lakini ni kosa dogo
tulilifanya.Baada ya kumuua
Lucy tulidhani tumemaliza
kazi kumbe tukasau kama
tumeacha risasi katika miili
ya marehemu”
“Jesus ! Gosu Gosu
akastuka
“Miili ya marehemu
ilifanyiwa upasuaji na
kutolewa risasi na baada ya
kuzichunguza wakagundua
kwamba risasi zile ni za
bunduki kubwa za udunguaji
ambazo wale majambazi
tuliowauzia kesi hawakuwa
nazo.Kufuatia sintofahamu
hiyo umoja wa Ulaya
unataka kuleta wachunguzi
wa kimataifa waingie nchini
kulichunguza suala lile
lakini kwa bahati nzuri Rais
ameweka msimamo kwamba
hakuna mchunguzi wa
kimataifa ambaye
ataruhusiwa kuingia nchini
kwani suala lile la mauaji ya
Lucy na mumewe
linachunguzwa na vyombo
vya ndani.Balozi wa umoja
wa Ulaya hapa nchini
anaitwa Benjamin Hudson
alimueleza Rais kwamba
anayo taarifa kwamba
Tanzania tulinunua bunduki
za aina ile kutoka Marekani
hivyo kama hataruhusu
wachunguzi wa kimataifa
kutakuwa na wasi wasi
kwamba kuna kitu Tanzania
tunakificha kuhusiana na
mauaji yale ya Lucy.Kuna
kila dalili kuna kitu
wanakifahamu kuhusu
mauaji yale lakini bado
hawana uhakika wanatafuta
ushahidi ndiyo maana
wanashinikiza kuruhusu
wachunguzi wa
kimataifa.Pamoja na
shinikizo lote alilopewa Rais
lakini bado ameshikilia
msimamo wake kwamba
hakuna mchunguzi yeyote
wa kimataifa
atakayeruhusiwa
nchini.Alasiri ya leo balozi
Benjamin Hudson na Rais wa
Ufaransa kwa nyakati tofauti
wote wameandika ujumbe
katika kurasa zao za twitter
wakiwaonya raia wa
Ufaransa na wale wanaotoka
katika nchi za jumuiya ya
Ulaya kuwa waangalifu
wanapokuwa nchini
Tanzania au kufikiria mara
mbili.Matamko haya
yanalenga kupunguza idadi
ya watalii na wawekezaji
wanaokuja nchini hivyo
kuzorotesha uchumi
wetu.Haya yote yameibuka
baada ya kifo cha Lucy
Muganza na sasa tunapata
picha ya wazi kwamba Lucy
Muganza alikuwa ni mtu
muhimu sana kwao na
walipanga kumtumia katika
mipango yao miovu dhidi ya
nchi zetu.Baada ya njama
zao kushindwa sasa
tumeingia katika vita ya
uchumi nao na baada ya
matamko haya mawili ya leo
tutegemee mambo mengine
makubwa zaidi” akasema
Austin
“Dah ! Kumbe
hatukukosea kumuondoa
Yule mama kwani alikuwa
kibaraka wa mataifa
makubwa” akasema Gosu
Gosu
“Hatukukosea kabisa
kumuondoa lakini sasa
tunaanza kuona athari za
kile
tulichokifanya.Tumeuondoa
mtu muhimu kwa mataifa
makubwa ambayo
yametuzidi kwa kila kitu na
siyo siri tunawategemea
wakubwa hawa katika ukuaji
wa uchumi wetu hivyo basi
tutegemee kukumbana na
misukosuko
mikubwa.Mashambulizi
makubwa hivi sasa
yanaelekezwa moja kwa moja
kwa Rais wetu kwa lengo la
kumdhoofisha na kama
akionekana kuwa imara zaidi
wanaweza wakamuondoa
madarakani kwa njia zozote
zile hata kwa kumuua kwani
uwezo wanao.Tuna kazi
kubwa ya kumsaidia Rais
wetu katika mapambano
haya.Vita hii inapiganwa nje
na hata ndani.Kuna watu
wako humu nchini ambao
wanashirikiana na mabeberu
hao katika kuihujumu nchi
na kumdhoofisha
Rais.Ushahidi wa hilo ni
taarifa ya silaha aliyonayo
balozi Benjamin.Balozi Yule
hawezi kuipata taarifa ile
nyeti kama hakuna mtu au
watu anaoshirikiana
nao.Tujiulize kama balozi
huyo ameweza kujua tunazo
bunduki ngapi aina ya Barret
M82,ni mambo mangapi ya
siri anayafahamu kuhusu
nchi yetu? Nani wanampa
taarifa hizi za siri? Hiyo
ndiyo kazi ambayo rais
anataka
tuifanye.Tumchunguze balozi
Benjamin Hudson na
tufahamu nyendo zake na
anapata wapi taarifa zile za
siri”
“Kweli hii ni vita.Kwa
nini Rais asimtimue nchini?
He’s spying on us ! akafoka
Gosu Gosu
“Angeweza kumtimua
hata usiku huu lakini
kikubwa anachokitaka Rais
ni kufahamu watu
anaoshirikiana nao huyu
balozi wanaompa taarifa
nyeti za nchi.Kama
akimtimua hatutaweza
kuwajua wasaliti hao”
akasema Austin
“Nini hasa Rais anataka
tukifanye katika suala
hili?Gosu Gosu akauliza
“Rais anataka
tumchunguze balozi
Benjamin.Tujue kila
anachokifanya,watu
anaokutana nao na watu
anaowasiliana nao.Kikubwa
hapa ni kujua anashirikiana
na akina nani”akasema
Austin
“It’s a taugh
mission.Kumchunguza mtu
mkubwa kama huyu si kazi
nyepesi.Hapa ndipo
ninapomkumbuka Mathew
Mulumbi.Misheni kama hizi
zilimfaa sana” akasema Gosu
Gosu
“Papaa,Mathew is not
here.It’s just us.Tunaweza
kufanikiwa hata kama
Mathew Mulumbi
hayupo.Mimi nimewahi
kufanya kazi katika idara ya
ujasusi kwa muda mrefu
nina uzoefu mkubwa katika
masuala haya hivyo usihofu.”
“Ninakuamini Austin
lakini siwezi kumsahau
Mathew.Nimekuwa naye
katika misheni
mbalimbali.Tunaanzia wapi
katika misheni hii? akauliza
Gosu Gosu
“Kwa kuanzia ni
nyumbani kwa
balozi.Tunapaswa
kumchunguza kila
anachokifanya nyumbani
kuanzia anapoamka asubuhi
anafanya nini.Tutamfuatilia
anapotoka kila anakoenda na
kuwafahamu watu wote
anaokutana nao na kufanya
nao mazungumzo.Tujue
anazungumza nini nao.Si
kazi nyepesi hii” akasema
Austin
“Ndiyo maana nilisema
awali kwamba ni kazi
nzito.Sisi wawili peke yetu
hatuwezi.Lazima tuongeze
timu yetu iwe kubwa.Tupate
watu ambao watakuwa
wakimfuatilia balozi toka
atakapoondoka nyumbani
kwake na watu hawa lazima
wawe wakibadilika badilika
na hata magari
watakayokuwa wakitumia
lazima yawe yakibadilika.Ni
zoezi pia ambalo litahitaji
fedha”
“Uko sahihi papaa
tunahitaji kuongeza
watu.Kuna watu wangu
watatu wako likizo
nitazungumza nao ili
niwajumuishe katika timu
hii ninawaamini
sana.Kuhusu fedha usijali
tuko vizuri.Rais amenipa
kadi ya akaunti Fulani ya
benki na kunitaka nitoe kiasi
chochote cha fedha
nitakachokihitaji hivyo
hakuna wasiwasi wowote wa
ukosefu wa fedha.Tutaanza
kwa kuingia nyumbani kwa
balozi kisha tutafunga
kamera za siri ambazo
zitatusaidia tuweze
kumfuatilia balozi nyumbani
kwake kila
anachokifanya.Tutasikia
mazunguzo yake yote”
akasema Austin na
kukumbuka kitu
“Nimekumbuka rais
alinieleza kwamba balozi
huyu hana simu ya mkononi
au kama anayo huitumia
kwa siri.Mawasiliano yake
yote hutumia simu ya mezani
ya ofisini na simu ya mezani
ya nyumbani”
“Balozi wa umoja wa
Ulaya ni mtu mkubwa na
haiwezekani akakosa simu
ya mkononi.Anawasiliana
vipi na wenzake pale
anapokuwa mbali na simu ya
mezani ya ofisini kwake au
ya nyumbani?Nimepata
wazo” akasema Gosu Gosu
“Wazo gani
papaa?akauliza Austin
“Ruby anaweza
akatusaidia sana kujua
mawasiliano ya balozi huyo”
“Ruby?
“Ndiyo.Umeshamsahau?
“Hapana siwezi
kumsahau Ruby yule mchawi
wa kompyuta.Uwezo wake
wa kucheza na kompyuta
unashangaza sana.Yuko
wapi hivi sasa?
Mnawasiliana? akauliza
Austin
“Kwa sasa Ruby
anafanya kazi Mamlaka kuu
ya mawasiliano ya
kiintelijensia nchini
Uingereza, GCHQ”
“Anafanya kazi GCHQ?
Akauliza Austin
“Ndiyo anafanya kazi
katika mamlaka hiyo”
“Hawajakosea walioamua
kumuajiri hapo.Anastahili
kabisa kuwepo mahala
hapo.Watu kama wale
walipaswa kuwepo hapa
nchini kuisaidia nchi.Una
mawasiliano naye?
“Ndiyo huwa
ninawasiliana naye mara
kwa mara.Ninataka
atusaidie kutafuta
mawasiliano ya balozi
Benjamin.Lengo ni kutaka
kujua anawasiliana vipi na
ofisi yao kuu ya umoja wa
Ulaya kama hana simu ya
mkononi?akasema Gosu
Gosu
“Fine.Call her.Naamini
atakuwa na msaada kubwa
kwetu kwani kwa mahala
alipo ana uwezo wa
kufahamu mambo mengi ya
Benjamin na umoja wa
Ulaya” akasema Austin na
bila kupoteza muda Gosu
Gosu akampigia simu Ruby
simu ikapokelewa
“Hallow Ruby ! akasema
Gosu Gosu
“Gosu Gosu nilikwisha
kwambia usitumie namba hii
kunipigia wakati niko
kazini.Nitakupigia baada ya
dakika tano” akasema Ruby
na kukata simu
“Amekata simu?akauliza
Austin
“Atapiga baada ya dakika
tano” akajibu Gosu Gosu
Baada ya dakika tano
kama alivyoahidi Ruby
akapiga simu
“Unasemaje Gosu
Gosu?akauliza Ruby
“Samahani sana Ruby
kwa kukupigia katika namba
hii”
“Usijali.Lakini wakati
mwingine nitafute katika
namba yangu ya nyumbani
na kama ukinikosa acha
ujumbe’
“sawa nitafanya hivyo
Ruby”
“Ulikuwa
unasemaje?akauliza Ruby
“Ruby nimekupigia nina
shida.Kwanza kabisa fahamu
kuwa niko na Austin
January”
“Austin?! Akauliza Ruby
“Ndiyo .Niko naye hapa”
“Austin January ni jina
ambalo sitaki kulisikia
kabisa katika maisha
yangu.Aliondoka na
kumuacha Mathew
porini.Sijasahau hilo jambo
hata kidogo.Bora
usingeniambia uko naye
kwani siku yangu tayari
imeharibika”
“samahani sana Ruby
kwa kukuharibia siku.Suala
hilo linatutesa sote lakini
hatuna namna nyingine ya
kufanya zaidi ya kuubali
kwamba tumempoteza
Mathew na maisha
yaendelee”akasema Gosu
Gosu na Ruby akasikika
akivuta pumzi ndefu
“tayari umekata
tamaa?akauliza Ruby
“Hapana Ruby siwezi
kukata tamaa kuhusu
Mathew lakini ni wapi
tutaanzia kumtafuta?
“I’ve never given up on
him.Something is telling me
Mathew is still alive.Bado
nina imani kubwa kwamba
siku moja Mathew atarudi.I
know Mathew than anyone
else and he can’t just die like
that” akasema Ruby na
ukimya ukapita
“I’m sorry Gosu Gosu kila
ninapomkumbuka Mathew
akili huwa inahama
kabisa.Tuyaache
hayo.Ulikuwa
unasemaje?Najua simu hii
haikuwa kwa ajili ya
kunisalimu” akasema Ruby
“Ni kweli Ruby
nimekupigia nina tatizo”
“Sema una tatizo gani?
“We’re in a mission?
“A mission?akauliza
Ruby kwa mshangao
“Ndiyo.It’s a tough
mission”
“Hujaachana na hayo
mambo?Gosu Gosu usishiriki
tena katika hizo misheni
utapotea kama alivyopotea
Mathew.Don’t trust that
Austin” akasema Ruby
“Ruby I’m doing this for
the Nation and for Mathew”
“Nini kinaendelea?Uko
kwenye misheni gani?Ruby
akauliza
“Nadhani ulisikia siku
chache zilizopita mwanamke
mmoja anaitwa Lucy
Muganza na mumewe
Laurent waliuawa hapa
Tanzania”
“Ndiyo
nilisikia.Limekuwa suala
kubwa kwa sasa”akasema
Ruby
“We did it” akasema
Gosu Gosu
“You what?
“We killed them”
“Usinitanie Gosu Gosu”
“Kweli
kabisa.Mwanamke Yule
alikuwa hatari sana kwa
nchi na jumuiya ya Afrika
Mashariki.Alikuwa
anatumiwa na nchi kubwa
kutaka kusambaratisha
jumuiya ya Afrika Mashariki
ndiyo maana
tukamuondoa.Baada ya
mauaji hayo umoja wa ulaya
wametaka kutuma
wachunguzi wa kimataifa
kufanya uchunguzi lakini
Rais amegoma.Balozi wa
umoja wa Ulaya hapa nchini
na rais wa Ufaransa kila
mmoja katika ukurasa wake
wa twitter wameandika
ujumbe wakiwaonya watu
kutoka nchi za umoja wa
ulaya kuchukua tahadhari
au kutokufika kabisa
Tanzania.Kilichonifanya
niombe msaada wako ni
kwamba tunamchunguza
balozi wa umoja wa Ulaya
hapa nchini Benjamin
Hudson.Huyu amekuwa
akishirikiana na baadhi ya
watu hapa nchini na
wamekuwa wakimpa siri za
nchi.Mpaka sasa tayari
anafahamu kuhusu silaha
tulizo nazo.Rais alitaka
kumtimua lakini amesita
kumtimua anataka
tuwafahamu kwanza watu
anaoshirikiana
nao.Ninachotaka utusaidie ni
kufahamu mawasiliano
yake.Katika uchunguzi wetu
tumegundua hana simu ya
mkononi tumejiuliza
anawasiliana vipi na
wenzake? Naomba utusaidie
kwa hilo” akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu sikushauri
uendelee na misheni
hiyo.Umeingia katika
misheni ya hatari sana”
akasema Ruby
“Usihofu Ruby I’ll be
fine”
“Nimekwambia hivyo
kwa sababu ninamfahamu
Benjamin Husdon ni mtu
hatari.Amewahi kufanya
kazi ya ujasusi katika shirika
la ujasusi nchini Ufaransa.Ni
mtu ambaye anafahamu kila
kitu kuhusu ujasusi hivyo si
mtu rahisi kumfuatilia”
“Ruby unanisaidia kwa
hilo nililokuomba
au?akauliza Gosu Gosu
“Nitakupigia baada ya
muda mfupi” akasema Ruby
na kukata simu
Baada ya kusubiri kwa
dakika kumi Ruby akapiga
“Gosu Gosu kama
nilivyokwambia kwamba
huyu mtu amekaa muda
mrefu sana katika ujasusi
hivyo anafahamu kila kitu na
amekuwa akichukua
tahadhari kubwa katika
mawasiliano yake hivyo
mawasiliano yake hutumia
simu ya satelaiti.Hicho
ndicho
nilichokipata.Nitaendelea
kuchimba zaidi kama
nikipata chochote nitakujuza
lakini kuweni makini huyo
mtu mnayemchunguza ni
hatari sana”akasema Ruby
“Ruby ninashukuru sana
kwa taarifa hizo ambazo nina
uhakika mkubwa
zitatusaidia.Naomba kama
ukipata chochote kingine
unachodhani kinaweza
kutusaidia basi tujulishe”
“Sawa Gosu Gosu
nitafanya hivyo” akasema
Ruby na kukata simu
“Ruby anadai kuwa
Benjamin anatumia simu ya
Satelaiti kuwasiliana na ofisi
yao kuu.Inaonekana huyu
jamaa yuko hapa nchini
kimkakati zaidi kwani
anaonekana ni mtu mwenye
kujificha mambo yake na
kuchukua tahadhari
kubwa.Kuna kitu tutakipata
tukiendelea kumchunguza
huyu jamaa”
“Kama anatumia simu ya
satelaiti tunatakiwa kujua
anaitumia saa ngapi na
akiwa wapi.Kesho asubuhi
na mapema nitatuma vijana
wawili waende karibu na
makazi ya balozi huyo kwa
ajili ya kuanza
kumfuatilia.Mara tu
atakapotoka sisi tutakwenda
hapo tukijifanya ni watu wa
kutoka Tanesco tunakwenda
kukagua mita ya umeme na
tutafunga kamera
sebuleni,chumba cha kulala
balozi,na vyumba vingine
tutakavyoona inafaa.Ninao
vijana wawili pale kikosini ni
wataalamu sana wa hayo
mambo watakwenda
kuifanya hiyo kazi.Baada ya
hapo tutafanya mpango wa
kuweka kifaa katika gari
lake ili tuweze kujua kila
mahala anakoenda na
maongezi yote yanayofanyika
katika gari” akasema Austin
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 6
Saa tano na dakika kumi
na nane za usiku Benjamin
Hudson balozi wa umoja wa
Ulaya nchini Tanzania
aliingia katika ofisi yake
ndogo iliyoko nyumbani
akafunga mlango.Pembeni ya
meza kulikuwa na kasiki
dogo akabonyeza namba
kadhaa likafunguka akatoa
ufunguo akafungua droo ya
moja ya kabati lake akatoa
sanduku dogo jeusi
akaliweka mezani
akalifungua.Sanduku lile
kwa kuliangalia waweza
kudhani ni sanduku
linalotumika kubebea
nyaraka mbalimbali za
kiofisi lakini sanduku hili
lilikuwa na matumizi
mengine kabisa.Hii ilikuwa
ni simu maalum ambayo
Benjamin hutumia
kuwasiliana na watu
wake.Akafungua sehemu
Fulani akachomoa eria kama
ya redio akaivuta juu halafu
akachukua kidude kidogo
akakiweka sikioni
akabonyeza sehemu
anakohifadhi namba
akazitafuta namba Fulani
akapiga na simu ikapokelewa
“Mheshimiwa Rais
Michael” akasema Benjamin
akiongea kwa lugha ya
kifaransa baada ya simu
yake kupokelewa.
“Benjamin habari za
Tanzania?akauliza Rais wa
Ufaransa Michael Weren
“Huku salama kabisa
mheshimiwa Rais”
“Benjamin nashukuru
sana kwa kazi nzuri
uliyoifanya.Mpaka sasa tuna
uhakika asilimia kubwa
kwamba Tanzania imefanya
mauaji yale hilo halina
ubishi.Kama wangekuwa
hawajafanya wangeruhusu
wachunguzi lakini
wamegoma kwa vile
wanafahamu fika kwamba
ukweli utajulikana.Kazi
tuliyonayo kwa sasa ni
kutafuta je nani alitoa
maelekezo ya Lucy na
Laurent kuuawa? Na je
Tanzania walifanya mauaji
haya peke yao au kuna watu
walishirikiana nao?Nina
uhakika mkubwa kwamba
lazima suala hili linahusisha
zaidi ya nchi moja.Nina
wasiwasi sana na Patrice
Eyenga lazima atakuwa
anahusika katika suala
hili.Ninahisi hivyo kwani
baada tu ya kukubaliwa
kujiunga na jumuiya ya
Afrika Mashariki ndipo
mauaji yale
yakatokea.Hakuna
mazungumzo yoyote
umeyanasa kuhusu Dr
Fabian na Patrice Eyenga
wakizungumzia mauaji hayo?
Akauliza rais Michael.
“Mheshimiwa
Rais,nimekuwa ninafuatilia
mawasiliano ya Rais Dr
Fabian kila siku lakini
mpaka sasa sijapata
mazungumzo yoyote ya Dr
Fabian akizungumza
chochote na Patrice Eyenga
au hata kuzungumzia suala
lile la mauaji ya Lucy”
akasema Benjamin
“Benjamin tafadhali
hakikisha unalichimba suala
hili kiundani.Rais ana mbinu
njia nyingi za
mawasiliano.Unatakiwa
kupata kila
anachokizungumza.Tunatum
ia fedha nyingi sana katika
jambo hili hivyo tunahitaji
kuona matunda yake”
akasema Rais Michael
“Mheshimiwa
Rais,nimeahidiwa na chanzo
changu cha taarifa kuwa
kesho kutwa nitapata taarifa
nyeti sana na muhimu”
“Chanzo kimesema ni
taarifa gani hiyo?
‘Bado sijaambiwa ni
taarifa gani lakini
nimeambiwa ni nyeti na ya
muhimu sana”
“Sawa Benjamin endelea
kulifanyia kazi hilo
suala.Baada ya kutuma
ujumbe ule twitter Rais
amekupigia simu
akakwambia
chochote?akauliza Rais
Michael
“Hapana hajanipigia
simu.Amekaa
kimya.Nimeambiwa kwamba
ameitisha kikao cha baraza
la mawaziri kesho asubuhi
nadhani ajenda kubwa ya
kikao hicho ni kujadili kile
tulichokiandika katika
kurasa zetu za
twitter”akajibu Benjamin
“Benjamin endelea
kufuatilia kwa karibu sana
hilo suala ni muhimu
sana.Tunahitaji sana kupata
ushahidi wa kumuhusisha
Rais Fabian na mauaji yale
ya Lucy na Laurent.Jambo
lingine nataka
kukufahamisha kwamba
maandalizi ya Theresa
yanakwenda vizuri.Tayari
amekwisha fanyiwa upasuaji
wa kubadili na madaktari
wamenithibitishia kwamba
ulikuwa ni upasuaji wenye
mafanikio makubwa.Kwa
sasa anaendelea
kuhudumiwa na
atakapopona tu ataanza
kupewa mafunzo ya nini
anatakiwa kufanya kisha
atakuja Afrika Mashariki
kituo chake kitakuwa
Tanzania.Misheni yake
kubwa ni kuisambaratisha
afrika Mashariki.Tafadhali
endelea kumuandalia
mazingira mazuri ili
atakapokuja asipate ugumu
kuifanya kazi yake” akasema
Michael
“Mpaka sasa nimekwisha
muandalia mazingira mazuri
na ninaendelea kumuandalia
hivyo atakapokuja
haitamuwia ugumu kuifanya
kazi yake” akasema
Benjamin wakaagana na
kukata simu
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 7
Austin aliwasili katika
makazi ya Gosu Gosu saa
tatu kasoro dakika nane za
asubuhi na kukaribishwa
ndani na mwenyeji
wake.Hakuwa peke yake
alikuwa ameambatana na
watu wawili
“Papaa kutana na
Stanley na Nasibu.Hawa ni
vijana wangu,wataalamu
sana wa masuala ya
elektroniki.Watatusaidia
katika masuala ya Kamera”
akasema Austin na Gosu
Gosu akasalimiana na wale
vijana alioambatana nao
Austin
“Kama nilivyokueleza
simuni kwamba tayari
nimetuma vijana wawili
kuanzia asubuhi kumfuatilia
balozi Benjamin na taarifa
niliyopewa muda mfupi
uliopita kabla sijafika hapa
ni kwamba mke wa balozi
ndiye aliyetangulia kuondoka
nyumbani balozi alifuata
muda mfupi baadae.Hivi
sasa vijana wanaendelea
kumfuatilia na watatupa
taarifa baadae.Kuondoka
kwa balozi Benjamin
kunatuwashia taa ya kijani
kuwa sasa tunaweza kwenda
nyumbani kwake” akasema
Austin
“Tukifika pale
tutajitambulisha kama watu
wa Tanesco tunaopita
nyumba kwa nyumba
kukagua mita za
umeme.Tayari nimekwisha
tengeneza vitambulisho
vyetu vikituonyesha kama
wafanyakazi wa
Tanesco.Nimetaarifiwa kuna
mlinzi mmoja getini hivyo
tutamuonyesha vitambulisho
na kuingia ndani.Nina
uhakika mita hiyo ya umeme
itakuwa nje hivyo basi vijana
wangu wawili wataingia
ndani kujifanya wanakagua
mfumo mzima wa umeme
huku wakifunga kamera za
siri.Ni zoezi ambalo
halitachukua muda mrefu
litakuwa limekamilika”
akasema Austin kila mmoja
akachukua kitambulisho
chake wakaingia garini na
kuondoka.Wakiwa njiani
bado Austin aliendelea
kuwasiliana na vijana
aliowatuma kumfuatilia
Benjamin na wakamjulisha
kwamba balozi tayari
amewasili ofisini kwake na
wako nje wakimsubiri.
Walifika katika makazi
ya balozi Benjamin.Kulikuwa
na askari mmoja mwenye
silaha akilinda.Austin
akashuka garini na
kumsalimia vizuri Yule
askari halafu akamueleza
kwamba wao ni watu wa
kutoka tanesco ambao
wanapita nyumba baada ya
nyumba kukagua mita za
umeme.Walimuonyesha
vitambulisho na askari Yule
akaridhika akapiga simu
ndani akatoa taarifa kwamba
kuna wageni.Mtumishi wa
ndani akatoka na kwenda
kuwapokea.Austin
alijitabulisha kwamba wao ni
maafisa wa kutoka shirika la
umeme tanesco na
wanatembelea nyumba mbali
mbali kukagua
mita.Mfanyakazi Yule wa
ndani wa balozi hakuonyesha
wasi wasi wowote wala
hakutaka kutazama
vitambulisho akawapeleka
moja kwa moja ilipo mita ya
umeme.Austin akiwa na
kifaa cha kupimia umeme
akapima halafu akamgeukia
Yule mfanyakazi akamtaka
akawaonyeshe vijana wake
vifaa vyote vikubwa
vinavyotumia umeme
ndani.Bila kusita mfanyakazi
Yule aliyekuwa amevaa
suruali ya jeans ya bluu na
fulana neykundu
akawazungusha mle ndani
akiwaonyesha vifaa mbali
mbali vinavyotumia umeme
halafu wakatoka nje.Austin
akampa Yule msichana mita
aishike halafu akawataka
Stanley na Nasibu waingie
ndani waanze kuzima kifaa
kimoja kimoja cha umeme.
“Zima friji ! akasema kwa
sauti Austin na Stanley
akaenda kuzima friji.Wakati
zoezi hilo likiendelea Nasibu
alikuwa na kazi moja ya
kufunga kamera za siri
katika vyumba bali
mbali.Kwanza alifunga
sebuleni halafu akafunga
jikoni kisha akafunga
chumba cha mapumziko na
chumba cha mwisho
alichotakiwa kufunga ni
chumba cha kulala balozi
ambacho kilikuwa
kimefungwa kwa
funguo.Mlango wa chumba
kile ulikuwa na kifaa
maalum cha kupiga kelele
kama utafunguliwa endapo
balozi au mke wake
hayupo.Nasibu akachomoa
kifaa Fulani katika begi lake
akakiweka karibu na kifaa
kile cha kutoa ukelele halafu
akachukua vyuma Fulani
vidogo akaufungua ule
mlango akaingia
ndani.Akafunga kamera
mahala ambako si rahisi
kuonekana .Wakati akishuka
akaona kitu Fulani
mezani.Ilikuwa ni kadi ya
mwaliko.Akaisoma
akairudisha mahala pake na
kutoka akaufunga mlango
akachukua kile kifaa chake
chenye usumaku ambacho
kilizuia kelele kutoka katika
kile kifaa kilichowekwa
mlangoni halafu akatoka
nje.Austin alipomuona
akajua kila kitu tayari
akamaliza zoezi la kupima
na kumjulisha Yule
mfanyakazi kwamba hakuna
tatizo lolote wakaaga na
kuondoka.
“Kila kitu tayari
mkuu.Nimefunga kamera
sebuleni,jikoni,chumba cha
mapumziko na chumba cha
kulala balozi” akasema
Nasibu
“Good job guys” akasema
Austin
“Katika chumba cha
kulala balozi kuna kitu
nimekiona”akasema Nasibu
“Umeona nini?
“Nimekuta kuna kadi ya
mwaliko.Balozi amealikwa
katika hafla ya uchangishaji
fedha itakayofanyika kwa
ajili ya mabweni ya kulala
watoto wanaoishimazingira
magumu.Hafla hiyo
itafanyika Zimba hotel siku
ya ijumaa”
“Hizo ni habari njema.Ni
kesho kutwa hivyo
tujipange.Tutamfuata balozi
kila mahala
atakapokwenda.Tutamfuata
kama kivuli anapoamka hadi
anapokwenda kulala”
akasema Austin
Baada ya kutoka
nyumbani kwa balozi
walielekea moja kwa moja
nyumbani kwa Gosu Gosu
ambako ndiko kila kitu
kitafanyika kutokea
hapo.Vijana wale mahiri
Stanley na Nasib walifanya
mambo haraka haraka na
wakaanza kupata picha
kutoka katika kamera
walizozifunga nyumbani kwa
balozi Benjamin.
“Okay guys,ninyi makazi
yenu yatahamia hapa kwa
muda.Kazi yenu kubwa
itakuwa ni kufuatilia kila
kinachofanyika mle
ndani.Hakikisheni
mnafuatilia simu zote
zinazopigwa,watu wote
wanaoingia mle ndani na kila
anachokifanya balozi.
“Tunafanya zoezi hili
kwa muda gani
mkuu?akauliza Nasibu
“Hakuna muda maalum
hadi pale tutakapopata kile
tunachokitafuta” akasema
Austin
“Msijali kila kitu
mtakipata hapa ndani.Kitu
cha msingi ni macho yenu
yasibanduke katika
kompyuta kufuatilia kila
kinachoendelea ndani ya
nyumba ile”
“Yule mfanyakazi
ulikuwa naye nje wakati sisi
tunafanya mambo yetu ndani
una hakika hajahisi
chochote? Akauliza Stanley
“Hapana hajahisi
chochote.Ameamini asilimia
mia moja kwamba sisi ni
watu kutoka tanesco.Hata
Yule askari aliamini hivyo”
akajibu Austin kisha
akamuaga Gosu Gosu
kwamba anakwenda
kufuatilia masuala yake ya
likizo ya dharura.
TEL AVIV – ISRAEL
Inakaribia saa moja za
jioni katika chumba cha
gereza walimo Mathew
Mulumbi na Ammar
Nazari.Ni siku ya tatu toka
Mathew alipoanza
kuzungumza na Ammar na
wa muda huo tayari
walikuwa marafiki
wakubwa.Walizungumza
mambo mengi sana
kuhusiana na harakati zao
na Ammar alikubali kujiunga
na Mathew katika mpango
wake wa kutoroka pale
gerezani na alimtaka
watakapofanikiwa kutoroka
basi akajiunge na kundi lale
la Ammar Nazari Brigades
ombi ambalo Mathew
alilikubali.
Siku hii ndiyo ambayo
ilipangwa Mathew akapewe
maelekezo yote kuhusu
namna watakavyotoroka pale
gerezani.Ammar aliamini
alivyoambiwa na Mathew
kwamba kuna mwanamke
anayeitwa Abeba raia wa
Ethiopia ndiye anayemsaidia
kutoroka kwa kumpa ramani
ya gereza.Jioni ya siku hiyo
waliandaa mpango ambao
ungemfanya Mathew aweze
kutolewa mle chumbani na
kupelekwa hospitalini
“Muda unakaribia
Ammar.Tafadhali tufanye
kama vile
tulivyokubaliana.Kwa namna
yoyote ile leo hii lazima
nitoke humu nikaonane na
Abeba kwani aliniahidi leo
hii tayari atakuwa amepata
ramani ya gereza
itakayoniwezesha kutoroka”
akasema Mathew
“Usijali Abu kila kitu
kitakwenda kama
tulivyokubaliana” akajibu
Ammar
Saa moja na nusu za jioni
wapishi wakiwa na torori
kubwa la chakula walikuwa
wakipita chumba hadi
chumba kugawa chakula
wakiwa wameongozana na
askari wa gereza.Mlango wa
akina Mathew ukafunguliwa
akaingia mpishi kuwapa
chakula.Mathew akaishika
sahani ile ya chakula
akakitazama na kuirusha ile
sahani
“Nimechoka kula aina
moja ya chakula kila
siku.Sisi pia ni binadamu
kama ninyi !! akasema kwa
ukali
“Tafadhali kuwa na
adabu kwa chakula
unachopewa.Unadhani
imewachukua muda gani
kwa wapishi kuandaa
chakula hiki?Siku nyingine
ukirudia kitendo kama hicho
nitakuadhibu vikali”
akasema kwa ukali Ammar
“Unasemaje ?! akauliza
Mathew na kumsogelea
Ammar akamvuta kilemba
chake Ammar akakasirika na
kumtandika ngumi nzito
Mathew akaanguka chini
lakini akawahi kuinuka
akamfuata Ammar na
kumuangusha chini Ammar
akachukua uma ya kulia
chakula akamchoma nayo
mkononi damu zikaanza
kumtoka askari wakaingia
na kuwaamua
“Samahani ndugu zangu
nilikuwa namfunza adabu
huyu mwenzangu kwa kosa
la kudharau
chakula.Mpelekeni akatibiwe
jeraha lake” akasema Ammar
na Mathew akatolewa mle
ndani na kupelekwa hospitali
akatibiwa jeraha lile kisha
akatolewa na kupelekwa
katika ofisi ya mkuu wa
gereza alikomkuta Efraim
Dagan na maafisa wengine
wa gereza na wa Mossad
wakimsubiri.
“Mathew Mulumbi
karibu tena.Kwanza pole
kwa maumivu lakini vile vile
hongera kwa kazi
nzuri.Tumekuwa
tunakufuatilia kila
unachokifanya mle ndani na
tunafurahi kwa kuwa
umefanikiwa kumshawishi
Ammar hadi akakuamini”
akasema Efraim Dagan
“Haikuwa kazi nyepesi
lakini nashukuru
ameniamini na yuko upande
wangu” akasema Mathew
“Baada ya hatua ile
kukamilika sasa
kinachofuata ni mpango wa
kutoroka gerezani.Tayari
tumekwisha andaa mpango
huo” akasema Efraim Dagan
na kumpa nafasi mmoja wa
maafisa wa gereza
kuendelea.Wote wakaelekeza
macho yao katika runinga
kubwa iliyokuwa mbele
ikawashwa na ramani
ikaonekana
“Hii ni ramani ya gereza
lote.Hapa kwenye mduara
mwekundu ndipo chumba
mlimo wewe na
Ammar.Mpango
tulioutengeneza utakuwa
hivi.Siku ya kutoroka
utajifanya umepoteza
fahamu ghafla na Ammar
atabonyeza kengele ya
dharura na watafika askari
wawili haraka kujua
kumetokea nini.Atawaeleza
kwamba umeanguka na
kupoteza fahamu kisha
mmoja wa askari hao
atakusogelea kujua nini
kimekutokea na hapo ndipo
utakapokurupuka kama
Mamba na kumrukia na
wakati huo huo Ammar
atamdhibiti askari
mwingine.Hakikisha askari
hao hamuwaui bali
wapotezeni fahamu
tu.Mtachukua mavazi yao
pamoja na redio ya
mawasiliano kisha
mtaondoka kwa kufuata
ramani tutakayokupa.Baada
ya dakika tano kitalia
king’ora cha hatari kuashiria
kwamba kuna wafungwa
wanatoroka na ninyi
mtakuwa na redio ya
mawasiliano kutoka kwa
wale askari na mtakuwa
mkisikiliza kila
kinachoendelea.Mkifika hapa
geti kumi na moja tutaweka
askari mdunguaji ambaye
atamdungua Ammar kwa
risasi ya mguu na wewe
utaachia risasi kadhaa kama
vile unamlenga askari huyo
kisha utambeba
Ammar.Mtapita katika
mfereji huu wa maji machafu
utakaowatoa nje ya gereza
ambako tutakuwa
tumewaondoa askari
wanaolinda upande huo na
kuwataka waingie ndani ili
kusaidia kuwatafuta
wafungwa
waliotoroka.Mfereji huu ni
mrefu na unakwenda
kuungana na mfumo
mwingine wa maji taka toka
sehemu nyingine za jiji lakini
kabla ya kufika sehemu
ambapo mfereji huu
unaungana na mifereji
mingine mtakuta kuna ngazi
ya kupanda na juu kuna
mfuniko mtatoka nje na hapo
tayari mtakuwa mko nje ya
gereza.Baada ya kutoka nje
mtafuata barabara kuelekea
Kaskazini na kwa dakika
kama saba hivi mtakuta
daraja mtajificha chini ya
daraja kisha atakuja Dr
Abeba atamulika tochi na
kuzima mara tatu
utamtambua kisha
atawapeleka sehemu ambako
Ammar atapatiwa matibabu
na kutoka hapo atawasaidia
kuondoka Israel” akasema
Yule afisa wa gereza
“Mathew unasemaje
kuhusu mpango huo?
Akauiza Efraim
“Ni mpango mzuri lakini
kuna maboresho nataka
yafanyike.Kwa namna
mpango ulivyo tutatoka bila
kutumia nguvu nyingi na
itaonekana ni rahisi
kutoroka.Gereza hili lina sifa
ya ulinzi mkali hivyo basi
lazima ionekane tumetoka
ndani ya gereza kwa bahati”
akasema Mathew na kutoa
maelekezo kadhaa ya
kuboresha mpango ule kisha
akapewa karatasi yenye
ramani ya gereza ikionyesha
njia watakazopita kisha
akarudishwa katika chumba
chake
“Mambo yamekwendaje?
Akauliza Ammar akiwa na
shauku kubwa ya kutaka
kujua namna mambo
yalivyokwenda
“Mambo yamekwenda
vizuri.Nimefanikiwa kuipata
ramani” akasema Mathew na
kutoa karatasi katika nguo
yake ya ndani akaikunjua
ilikuwa ni ramani ya
gereza.Ammar akashindwa
kulizuia tabasamu katika
uso wake baada ya kuiona
ramani ile.Hakuamini kama
kile alichokuwa anakiona ni
kitu cha kweli.
“Ninaona haya kama
maajabu.Sikuitegemea hata
siku moja kama ningeweza
kuikamata ramani ya gereza
hili.Hii itatusaidia sana
tutakapotoka hapa kuandaa
kuja kuvamia na
kuwawachukua watu wetu
waliofungwa hapa” akasema
Ammar na Mathew akaanza
kumuelekeza namna mpango
wote utakavyokuwa na njia
watakazopita.
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Ni siku ya ijumaa ikiwa
ni siku ya tatu toka akina
Austin walipoanza
kumfuatilia balozi Benjamin
Hudson.Kwa muda wa siku
zote tatu Stanley na Nasibu
hawakubandua macho katika
kompyuta wakifuatilia kila
kinachofanyika nyumbani
kwa balozi Benjamin lakini
kwa muda wote huo wa siku
tatu hawakuwa wamepata
kitu chochote cha
muhimu.Timu iliyokuwa
inamfuatilia balozi Benjamin
kila aendako nao walifanya
kazi yao kwa umakini
mkubwa na kupata picha ya
kila aliyezungumza na balozi
Benjamin.Ubao uliokuwemo
katika ofisi yao ulikuwa na
picha za watu mbali bali
ambao Benjamin alikutana
nao katika siku hizo tatu na
wote walifanyiwa uchunguzi
lakini bado hawakuwa
wamepata mtu ambaye
walimuhisi anaweza kuwa
anashirikiana na balozi
Benjamin na kumpa siri
mbali mbali.
Austin January akiwa
amevalia suti nyeusi jioni hii
alikuwa ameegemea meza
akitazama picha za watu
kadhaa waliofanya
mazungumzo na Benjamin
“This dude is very clever”
akasema Austin
“Anajua sana kuficha
mambo yake.Karibu watu
wote hawa aliokutana nao ni
watu wa kawaida
sana.Katika siku hizi zote
tatu hatujamuona na simu
yoyote ya
mkononi.Tumekuwa
tukifuatilia simu zote
zinazopigwa nyumbani
kwake lakini hakuna simu
yoyote tuliyoitilia
shaka.Anafanyaje
mawasiliano yake? akauliza
Austin
“Kuna kitu kimoja
ambacho mimi na wenzangu
tumekiona na
tukajiuliza.Kila ifikapo saa
tano usiku Benjamin hutoka
chumbani kwake”akasema
Stanley
“Huelekea wapi? Austin
akauliza
“Hatujajua huelekea
wapi kwani kamera
tumeweka chumbani
kwake,sebuleni,jikoni na
katika chumba cha
mapumziko”
“Tulipaswa kuweka
kamera kila sehemu ili tujue
kila kinachofanyika mle
ndani.kama anatoka kila saa
tano usiku lazima kuna
mahala huwa anakwenda”
akasema Austin
“Kwa hiyo tunafanya nini
kuhusu hilo?akauliza Gosu
Gosu
“Lazima tutafute namna
ya kurudi tena mle ndani
kufunga kamera nyingine
sehemu mbali mbali kujua
usiku huo akitoka Benjamin
huenda wapi.Kwa sasa
tujielekeze katika tukio la
usiku wa leo ambapo
Benjamin amealikwa katika
hafla ya uchangiaji fedha
kwa ajili ya mabweni ya
watoto waishio katika
mazingira
magumu.Mimi,GosuGosu,na
Nasibu wote tutakuwemo
ndani ya ukumbi huo.Macho
yetu wote tutayaelekeza kwa
mtu mmoja tu Benjamin
Hudson.Wote tutakuwa
tumevaa kamera ambazo
zitamuwezesha Stanley
atakayekuwa amebaki
nyumbani kupata picha za
kila kinachoendelea mle
ndani ya
ukumbi.Tuhakikishe
tunapata picha ya kila
anayezungumza na
Benj……” akanyamaza
Austin baada ya simu yake
kuita.Walikuwa ni vijana
wanaomfuatilia Benjamin
“Hallow” akasema
Mathew baada ya kuipokea
simu
“Mkuu,huyu jamaa
ametoka na ndani ya gari
yuko yeye na mke wake”
“Nadhani wanaelekea
katika hafla waliyoalikwa
jioni hii ya leo.Endeleeni
kumfuatilia na sisi
tunaelekea ukumbini”
akasema Austin na kukata
simu.
“Tayari balozi Benjamin
anaelekea
ukumbini.Tusipoteze muda
tuelekee huko” akasema
Austin.Ni Stanley pekee
aliyebaki pale nyumbani
wengine wote wakaingia
katika magari na
kuondoka.Austin alikuwa na
Nasib Gosu Gosu alikuwa
peke yake.
Zimba hoteli usiku huu
iling’aa kwa mataa ya rangi
mbali mbali yaliyozunguka
hoteli hii ya hadhi ya nyota
tano.Usiku huu mahala hapa
kulikuwa na hafla ya
kuchangisha fedha kwa ajili
ya kuwasaidia watoto
waishio katika mazingira
magumu wa kituo cha
kulelea watoto cha Mama wa
Afrika.Watu wengi
walialikwa kuhudhuria hafla
hiyo ya kuchangisha fedha
kwa ajili ya kujenga
mabweni ya watoto hao
waishio katika mazingra
magumu.Katika sehemu ya
kuegesha magari kulikuwa
na watu watatu wakiongoza
magari kwani usiku huu
kulikuwa na magari mengi
ya watu waliofika katika
hoteli hii kuhudhuria hafla
hiyo.Akina Austin waliwahi
kufika kabla ya balozi
hajafika.Hawakuwa na kadi
za mwaliko kwani kadi
zilitolewa kwa watu maalum
tu lakini kwa wengine ambao
waliguswa na kutaka
kuchangia walikaribishwa
pia hivyo akina Austin
walikuwa katika kundi hili
wakaingia ndani ya
ukumbi.Watu walikuwa
wengi na bado waliendelea
kuingia ukumbini.Nasib
alipanda sehemu ya juu,Gosu
Gosu na Austin kila mmoja
akachukua sehemu yake.
Wakiwa mle ukumbini
Austin akapigiwa simu na
vijana wake kwamba balozi
Benjamini tayari amefika
hapo ukumbini na ameshuka
garini yeye na mkewe
wanaelekea ukumbini.Austin
akawatumia ujumbe Gosu
Gosu na Nasibu kuwajulisha
kwamba muda wowote balozi
Benjamin ataingia ukumbini
hivyo wajiandae.
Balozi Benjamin akiwa
ameongoza na mkewe na
watu wawili walioonekana ni
walinzi wake,wakaingia
ndani ya ukumbi.Toka
alipoingia ukumbini macho
ya Nasibu yalimng’aza na
kuelekeza kamera
kumfuatilia.Alipokewa na
mtu maalum aliyewekwa
kwa ajili ya kupokea
wageni.Alielekezwa kukaa
katika meza ya tatu kutoka
meza ya mbele.Kulikuwa na
watu wengine watatu katika
meza hiyo
wakasalimiana.Wakati
wakiendelea na
mazungumzo,Austin
akainuka kama vile
anakwenda maliwato lakini
aliporejea hakwenda tena
kukaa katika meza ile
aliyokuwa amekaa badala
yake akaenda kukaa karibu
na meza ya balozi huku
macho yae akiyageuza kama
kinyonga kutazama kila
kinachoendelea katika meza
ile aliyokaa balozi.Wote
walikuwa wamevaa kamera
za siri ambazo zote
walizielekeza kwa balozi.
Muongoza shughuli
aliposhika kipaza sauti na
kutangaza kwamba muda si
mrefu shughuli
itaanza,Benjamin
akaitazama saa yake ya
mkononi halafu akainuka na
kutembea kama vile
anaelekea maliwato Gosu
Gosu naye akasimama
akaelekea huko.Nasibu naye
akashuka ghorofani na
kumfuata Gosu
Gosu.Benjamin aliingia
maliwato baada ya dakika
mbili akatoka lakini
hakurejea ukumbini
akachepuka na kufuata
korido akaelekea
baa.Akaenda kaunta na
kununua chupa ya bia.Gosu
Gosu akabaki nyuma
akamuacha Austin aingie
mle baa.Balozi Benjamin
akamimina bia ile katika
glasi akanywa huku
akiangaza huku na kule
halafu akalipa na kumuachia
muhudumu chenji akatoka
mle baa na kuelekea katika
lifti.Wakati akisubiri lifti
iliyokuwa juu Nasibu naye
akafika akaungana naye
kusubiri lifti.Baada ya muda
mfupi milango ya lifti
ikafunguka wakaingia
walikuwa jumla watu
sita.Balozi akaomba
abonyezewe namba sita
akimaanisha anakwenda
ghorofa ya sita.Nasibu
akawaandikia ujumbe akina
Gosu Gosu kwamba balozi
anaelekea ghorofa ya
sita.Haraka haraka Gosu
Gosu aliyefika katika eneo
lile la lifti akaingia katika
lifti ya pembeni ambayo
haikuwa na mtu na
kubonyeza ghorofa ya sita
lifti ikaondoka.
Milango ya lifti
ikafunguka ghorofa ya sita
lakini balozi hakushuka
badala yake akaingia
mwanamke Fulani aliyekuwa
amevaa suruali ya jeans ya
bluu na fulana nyeupe
iliyombana na viatu virefu
vya bluu.Mwanamke Yule
alimsogelea zaidi balozi
ambaye alikuwa karibu na
Nasib.Hakuna aliyemjali
akachomoa mfukoni bahasha
ya khaki na kumuwekea
balozi kwenye
koti.Mwanamke Yule
alishuka ghorofa ya nane
Nasibu naye
akashuka.Baada ya kushuka
mwanamke Yule akaanza
kushuka ngazi kwa
miguu.Nasibu akajibanza
mahala na kupiga simu kwa
Austin
“Kuna mwanamke
amepanda lifti ghorofa ya
sita na akamuwekea balozi
bahasha ya khaki kwa
uficho.Mwanamke huyo
ameshukia ghorofa ya nane
na anashuka kwa kutumia
ngazi za kawaida.Amevaa
suruali ya jeans ya
bluu,fulana nyeupe ya
kumbana na viatu vya bluu
ana mkoba mweupe”
“Kazi nzuri sana Nasib
shuka taratibu rejea chini
uendelee kumfuatilia balozi”
akasema Austin halafu
akampigia simu Gosu Gosu
aliyekuwa ghorofa ya sita
akamjulisha amfuatilie
mwanamke Yule anayeshuka
ngazi.
Milango ya lifti
ilifunguka na balozi
Benjamin akatoka na
kuelekea baa akasimama
kaunta akaangaza angaza
kama vile anamtafuta mtu
halafu akaondoka akaelekea
ukumbini.
“Anarejea ukumbini”
Nasibu akamjulisha Austin.
Balozi aliingia ukumbini
na kukuta tayari hafla
imeanza akaenda kuketi
katika meza yake.
Gosu Gosu aliendelea
kumfuatilia taratibu
mwanamke Yule akapita baa
halafu akatoka nje na moja
kwa moja akaelekea katika
maegesho.Gosu Gosu naye
akaelekea katika
maegesho.Mwanamke Yule
akaingia katika gari la
kifahari aina ya range rover
e vogue rangi nyekundu
akaliwasha na kuondoka
Gosu Gosu naye akawasha
gari lake na kuanza
kumfuatilia
“Ameondoka hapa
hotelini.Ninamfuatilia
kumfahamu ni nani” Gosu
Gosu akamwambia Austin
“Sawa Gosu Gosu
endelea kumfuatilia sisi
tunaendelea kumfuatilia
balozi tayari amerejea
ukumbini.Tunahitaji kujua
bahasha aliyopewa ina nini?
Naamini ina kitu kikubwa
hadi akaenda kumpa
kiuficho namna hiyo.Ruby
alikuwa sahihi huyu jamaa
ni mtu anayechukua
tahadhari kubwa sana katika
mambo yake.Tafadhali
hakikisha unapata majibu
mwanamke huyo ni nani na
amempa nini balozi.Kama
utahitaji msaada nijulishe
haraka sana” akasema
Austin
Baada ya kutoka Zimba
hoteli mwanamke Yule
akaenda hadi Dar es salaam
supermarket.Gosu Gosu naye
akaenda hapo akaegesha gari
na kumuachia mlinzi shilingi
elfu kumi amlindie lile gari
atakuja kulichukua baadae
akamfuata dereva wa boda
boda akamtaka waelekee
sehemu fulani lakini
akamtaka wasubiri kuna
gari wanalifuata.Dakika
kama kumi baadae gari la
Yule mwanamke likatoka na
Gosu Gosu akamuelekeza
Yule dereva wa boda boda
walifuate.
Mwanamke Yule aliingia
katika jumba moja kubwa la
ghorofa moja lililokuwa na
geti lenye nakshi za
kuvutia.Gosu Gosu na Yule
dereva wakalipita jumba lile
na kwenda mbele kidogo
kisha Gosu Gosu akamlipa
Yule dereva kiasi cha pesa
alichohitaji akaondoka
zake.Gosu Gosu akaanza
kurejea taratibu katika
jumba lile.Ni mtaa uliokuwa
na majumba mazuri na kwa
muda ule hakukuwa na watu
wengi barabarani.Kulikuwa
na taa kubwa getini iliyotoa
mwangaza mkubwa.Gosu
Gosu akaenda kuegemea
nguzo ya umeme akatazama
pande zote halafu akachomoa
bastora yake yenye kiwambo
cha sauti akailenga ile taa
ikapasuka.Eneo lile likawa
na mwanga hafifu sana
halafu akatulia pale kwa
muda akiangaza pande zote
kama kuna mtu.Zilipita piki
piki mbili na magari matatu
halafu akavuka barabara na
kwenda katika geti akajaribu
kuusukuma mlango mdogo
wa geti ulikuwa umefungwa
kwa ndani haraka haraka
akavua viatu na kurudi
nyuma hatua kadhaa halafu
akatoka mbio na kuruka
akashika kingo za juu za
geti akapanda na
kuchungulia ndani.Aliliona
gari la Yule dada likiwa
limeegeshwa mbele ya
nyuma akajirusha ndani na
kutua bila kelele.Akaangaza
angaza mara akasikia
muungurumo wa mbwa
mkubwa aliyemsogelea
kimya kimya kwa wepesi wa
aina yake Gosu Gosu
akaizinga bastora yake na
mbwa Yule akaanguka chini
kimya kimya.Akamvuta na
kumtupa pembeni kwenye
maua akatembea taratibu
hadi katika kibaraza
akachungulia ndani sebuleni
akamuona mwanamke
mmoja amekaa sebuleni
akitazama filamu.Yule
mwanamke aliyempa
bahasha balozi
hakuwepo.Akazunguka kwa
nyuma akajaribu
kuusukuma mlango ulikuwa
wazi akaingia ndani
akatokea jikoni hakukuwa
na mtu akatokea sehemu ya
kulia chakula akasikia hatua
za mtu akajibanza pembeni
katik anguzo kwa bahati
mbaya akagonga glasi
ikaanguka na kuvunjika.
“Dada ? akaita Yule
msichana aliyekuwa akipita
akitokea sebuleni lakini
alipoona kimya akaamua
kuingia katika chumba cha
chakula kuangalia kwa nini
glasi ile imevunjika.Mara tu
alipoingia akajikuta
akitazamana na mtu mwenye
bastora
“Mamaaaa ! akapiga
kelele
“Shhhh !! usipige kelele
nitakufumua kichwa kwa
risasi ! akasema Gosu
Gosu.Yule msichana alikuwa
anatetemeka mwili kwa
woga
“Dada yako yuko
wapi?akauliza Gosu Gosu
“Yuko chumbani
kwake”akajibu Yule
msichana akitetemeka
“Nipeleke chumbani
kwake haraka sana”
akasema Gosu Gosu na mara
ikasikika sauti ikiita
“Nancy !
“Nancy !
“Dada ananiita” akasema
Yule msichana
“Itika” akasema Gosu
Gosu na Yule msichana
akaitika
“Nimesikia unapiga
kelele kuna nini
huko?akauliza
“Hakuna kitu dada”
akasema Nancy
“Kamuangalie mtoto
kama amelala” akasema Yule
dada kule juu
“Nipeleke katika chumba
alimo mtoto” akasema Gosu
Gosu na Yule msichana
Nancy akampeleka katika
chumba alimo mtoto mdogo
wa kike mwenye umri wa
kama miaka mitano.
“Anaitwa nani huyu
mtoto?akauliza Gosu Gosu
‘Anaitwa Teddy” akajibu
Yule Nancy na Gosu Gosu
akampa pigo kichwani
akaanguka chini na kupoteza
fahamu akamuinua Yule
mtoto aliyekuwa usingizini
akambeba na kuelekea
ghorofani kilipo chumba cha
Yule dada.Akagonga mlango
“Nancy ! akaita yule dada
mle chumbani na Gosu Gosu
akagonga kwa mara ya pili
na mlango
ukafunguliwa.Yule dada
hakuamini alipojikuta
akitazama na Gosu Gosu
aliyekuwa na bastora huku
akiwa amembeba mwanae.
“Who are you? Akauliza
Yule dada ambaye mstuko
alioupata ulikuwa mkubwa
“Sit down ! akasema
Gosu Gosu na Yule dada
akatii na kukaa
kitandani.Gosu Gosu
akaichukua bastora
iliyokuwa mezani ya Yule
dada akaifutika kiunoni
akamtazama Yule dada
ambaye midomo ilikuwa
inamtetemeka
“Wewe ni nani?Unataka
nini?Tafadhali naom……”
akasem Yule dada lakini
Gosu Gosu akamnyamazisha
“Quiety !
“Nina muda mfupi sana
hapa nataka unijibu maswali
nitakayokuuliza kiufasaha
na kama utathubutu kuleta
jeuri au kujaribu kutaka
kufanya ujinga wowote
nitakuua wewe na
mwanao.Umenielewa?akauli
za
“Nimekuelewa.Tafadhali
naomba usimdhuru
mwanangu.Unataka nini?
Pesa? Akauliza Yule
mwanadada
“Jina lako nani?
“Naitwa Rahel”
“Rahel unafanya kazi
wapi?
“Mimi ni mfanya
biashara wa vipodozi”
“Are you sure?
“Ndiyo mimi ni mfanya
biashara”
“Usiku huu ulikutana na
balozi wa umoja wa ulaya
katika hoteli ya Zimba una
mahusiano naye yapi?
“Balozi wa
Ulaya?akauliza Rahel
“Ndiyo”
“Simfahamu wala sijafika
Zimba hoteli usiku
huu.Nilipotoka kwenye
biashara zangu nimekuja
moja kwa moja
nyumbani.Utakuwa
umenifananisha”
“Nilikwambia nina muda
mfupi sana hapa.Nakupa
nafasi ya mwisho unieleze
una mahusiano gani na
balozi wa Ulaya hapa nchini
bwana Benjamini
Hudson?akasema Gosu
Gosu.Huku machozi
yakimtoka Rahel akajibu
“Naomba uniamini kaka
yangu sina mahusiano yoyote
na huyo balozi wala simjui ni
nani”
“Nilikutaka uwe mkweli
kwangu,kwa kuwa umekuwa
muongo nitaanza kumpiga
risasi moja moja mwanao
hadi utakapokuwa tayari
kunieleza ukweli” akasema
Gosu Gosu na kumuelekezea
yule mtoto bastora mguuni
“Nitahesabu mpaka tatu
kama hautakuwa tayari
nitaufumua mguu wake kwa
risasi” akasema Gosu Gosu
“Tafadhali kaka yangu
nakuomba sana usimuumize
mwanangu.Unamuonea bure
mimi simfaham…….”
“Tatu ! akasema Gosu
Gosu kwa ukali
“Kaka nakuomba ..”
akasema Rahel huku akitaka
kuinuka
“Usiinuke hapo
nitakuchakaza kwa
risasi.Mbili ! akasema kwa
ukali
“M….”
Kabla Gosu Gosu
hajamaliza kutamka mlango
ukapigwa teke zito na bomu
dogo la kurusha kwa mkono
likatupiwa mle ndani
“Oh my God ! akasema
Gosu Gosu.Rahel macho
yakamtoka pima.Picha ya
Mathew Mulumbi akidaka
bomu na kulirusha nje
walipokuwa katika misheni
ya kuwakomboa watoto
waliotekwa na magaidi
ikapita haraka haraka
kichwani kwake
“Mathew Mulumbi
aliwahi kudaka bomu na
kulitupa nje” akawaza na
kufanya kitendo ambacho
Rahel hakuwa
amekitarajia.Gosu Gosu
alimrusha Teddy kitandani
huku akimrushia Rahel
bastora ambaye aliidaka
kiufundi sana akaanguka
chini na kumimina risasi
mlangoni .Gosu Gosu aliruka
akalishika lile bomu na
kulirusha katika dirisha
lililokuwa wazi bomu lile
likaenda kutua ndani ya
bwawa la kuogelea.Alikuwa
anatweta.Hakuamini kama
walikuwa
wamenurusika.Akainuka na
kuelekeza macho yake
mlangoni watu wawili
walikuwa wameanguka
wakivuja damu.Ilikuwa kazi
ya Rahel.Aliwachakaza watu
wale kwa risasi kutoka
katika bastora aliyopewa na
Gosu Gosu
Gosu.Akawasogelea watu
wale akawachunguza
walikuwa
wamekufa.Akamgeukia
Rahel aliyekuwa amejibanza
pembeni ya meza ya vipodozi
alikuwa anatetemeka
“Are you okay?akauliza.
“I’m..I’m … fine” akajibu
kwa kitetemeshi.
“Good job Rahel”
akasema Gosu Gosu
“Thank you.Umeokoa
maisha yangu na ya
mwanangu” akasema Rahel
na kwenda kumkumbatia
mwanae aliyekuwa kitandani
akilia.Gosu Gosu akamtaka
asitoke mle chumbani
akashuka chini kwenda
kuangalia kama kuna watu
wengine lakini hakukuwa na
mtu akarejea chumbani kwa
Rahel
“Unawafahamu watu
hawa?akauliza Gosu Gosu
“Hapana siwajui”akajibu
“Okay we need to get out
of here immediately.Hapa
tayari ni sehemu hatarishi
kwenu.Zima kompyuta na
simu zako zote”akasema
Gosu Gosu na Rahel
akafungua zimu zake mbili
akatoa laini zake
“Unatupeleka wapi?
“Sehemu salama”
akasema Gosu Gosu na
kumtaka Rahel akusanye
kila kitu chake cha muhimu
akaweka katika sanduku
dogo wakatoka mle chumbani
akaenda katika chumba cha
chakula akambeba Yule
msichana ambaye mpaka
sasa bado hakuwa na fahamu
akamuingiza garini.Akarudi
tena ndani na kuibeba miili
ya wale jamaa waliouawa
akaipakia garini na
kuifunika na turubai
“Hao unawapeleka
wapi?akauliza Rahel kwa
wasiwasi
“Miili hii haipaswi
kuendelea kukaa mle ndani
mwako ninakwenda
kuitupa.Polisi hawatakiwi
wajue kuhusiana na tukio
hili” akasema Gosu Gosu
akiwa katika usukani.Bado
Rahel alikuwa amemkubatia
mwanae aliyekuwa
anatetemeka.Alichokishuhud
ia usiku ule kilimstua
sana.Safari ilikuwa ya kimya
kimya wakielekea nje kidogo
ya jiji hadi walipokuta
vichaka Fulani Gosu Gposu
akazima gari na kushusha
miili ya wale jamaa akaitupa
vichakani kisha wakaanza
safari ya kurejea jijini.
“Who are you?akauliza
Rahel
“You’ll soon know who I
am” akajibu Gosu Gosu
“Tafuta sehemu salama
tuliache hili gari hatupaswi
kuendelea kulitumia”
akasema Rahel
“Kwa nini Rajel?
“Kwa sababu
wanatufuatilia.Wanajua hivi
sasa tuko wapi” akasema
Rahel na Gosu Gosu
akamtazama
“Akina nani
wanatufuatilia?
“Do as I say ugly man !
akasema Rahel kwa ukali
“Fine”
Gosu Gosu akaiingiza
gari ile katika baa moja
wakashuka wakashuka
halafu wakachukua taksi
hadi Dar es salaam
supermarket ambako Gosu
Gosu aliacha gari lake
wakaingia garini na
kuondoka
“Huyu mwanamke
anaonekana ana mambo
makubwa sana.Alisema
hawajui watu wale waliokuja
kumuua na sasa anasema
kwamba tunafuatiliwa.Kuna
jambo analifahamu nidyo
maana akataka kuuawa”
akawaza Gosu Gosu
Walipokaribia kufika
katika makazi ya Gosu Gosu
ndipo alipokumbuka kutaka
kuwasiliana na wenzake
akina Austin lakini kumbe
simu yake ilikuwa imepata
hitilafu katika ule mshike
mshike na
ikazimika.Alipofika katika
makazi yake akawakaribisha
ndani Rahel na mwanae
pamoja na Nancy yule
msichana aliyekuwa
amepoteza fahamu ambaye
tayari alikwisha rejewa na
fahamu.Bila kupoteza muda
akamuelekeza mtumishi wa
ndani awaandalie wageni
wale chumba cha wageni na
baada ya muda mfupi
chumba kikawa tayari Rahel
akaenda kumlaza mwanae
na Yule mdogo wake.Wakati
Rahel akimbembeleza
mwanae alale Gosu Gosu
akabadili simu na kumpigia
Austin akamjulisha kila
kilichoendelea.
“Pole sana
Papaa.Niliingiwa na
wasiwasi mkubwa baada ya
simu yako kutopatikana kila
nilipojaribu kupiga”akasema
Austin
“Hata mimi mwenyewe
sikuwa nakumbuka kabisa
kuhusu simu hadi nilipofika
nyumbani.Austin I saw death
today” akasema Gosu Gosu
“Pole sana
Papaa.Umefanya kazi kubwa
sana hadi ukafanikiwa
kumpata huyo mwanamke
ambaye naamini atakuwa na
msaada mkubwa kwetu.Kwa
sasa mpe muda apumzike ila
usimruhusu kufanya
mawasiliano na mtu yeyote
Yule na kila kitu chake
kizimwe kwani wanaweza
wakamfuatilia wakajua
mahala alipo.Mimi
nitawaachia vijana
waendelee kumfuatilia balozi
ninakuja hapo nyumbani
sasa hivi kuungana nawe
tumuhoji huyo
mwanamke.Kuna mambo
mengi ambayo tunahitaji
kuyafahamu kutoka kwake”
akasema Austin
Alipomaliza kuzungumza
na Austin Gosu Gosu
akachukua bia baridi katika
friji akaigugumia yote halafu
akasimama akiwa
ameegemea friji.
“Haikuwa siku yangu ya
kufa leo lakini tayari
nilikwisha chungulia
kaburi.Kama nisingepata
ujasiri wa kuliokota bomu
lile na kulirusha nje mimi na
wote mle ndani tungekwisha
kufa.Namshukuru Mathew
kwa kunipa ujasiri kwani
naye pia aliwahi kudaka
bomu akalirusha nje
akatuokoa wote na leo
nimefanya kama alivyofanya
yeye.” Akawaza na kuvuta
pumzi ndefu sana na
kuelekea katika chumba cha
wageni waliko akina Rahel
akagonga kidogo halafu
akaruhusiwa kuingia
akausukuma mlango
akaingia ndani.Rahel
alikuwa amekaa kitandani
mwanae Teddy na Yule
msichana Nancy walikuwa
wamelala
“Wanaendeleaje?akauliza
Gosu Gosu
“Nashukuru wamepata
usingizi lakini mstuko
walioupata ni
mkubwa”akasema Rahel
“You need something to
drink?Wine,beer or whisky?
Akauliza Gosu Gosu
“No thank you”akajibu
Rahel
“Rahel kama hutajali
naomba tuzungumze
tafadhali” akasema Gosu
Gosu na Rahel akainuka pale
kitandani wakaelekea
sebuleni.Gosu Gosu
akafungua friji akatoa chupa
ya maji ya kunywa
akamminia Rahel katika
glasi akampa yeye
akachukua chupa ya bia
“Rahel hapa ulipo ni
sehemu salama hakuna
anayeweza kukufuata hapa
hivyo jisikioe amani.Baada
ya yote yaliyotokea nadhani
sasa ni wakati muafaka wa
kuzungumza.Niliweka
hatarini maisha yangu
kukuokoa wewe na mwanao
hivyo ninahitaji kuufahamu
ukweli.Nataka unieleze
ukweli bila kunificha na
mimi nitakusaidia lakini
kama ukiamua
kunidanganya utakuwa
unajidanganya wewe
mwenyewe kwani watu wale
ambao walikufuata kukuua
hawatachoka wataendelea
kukutafuta usiku na mchana
hadi watakapohakikisha
wamekumaliza.Nataka
kufahamu wewe ni
nani?Unafanya kazi wapi na
nani unashirikiana naye na
kwa nini watu wale walikuja
kutaka kukuua?akauliza
Gosu Gosu.Rahel akainama
akafuta machozi halafu
akamtazama Gosu Gosu
“Nilikudanganya.Jina
langu si Rahel.Naitwa
Agatha”akanyamza kidogo
halafu akaendelea
“Kabla sijakueleza
chochote nataka
unihakikishie usalama
wangu na familia
yangu.Hawatachoka
kunitafuta hadi pale
watakapohakikisha
nimeuawa.I was so stupid to
believe them” akasema
Agatha
“Agatha nimekuokoa
kutoka kwa wale watu usiku
wa leo na nitaendelea
kukulinda.Nakuahidi wewe
na familia yako mtakuwa
salama”
“You don’t know what
you’re talking about Gosu
Gosu.The people I’m talking
about they’re dangerous than
you think.I know their
secrets so they must find and
kill me” akasema Agatha
“Agatha nakutoa hofu
kwamba utakuwa
salama.Mimi na wenzangu
tutakulinda na kuhakikisha
unakuwa salama.Niambie ni
akina nani hao watu?
“This place is not safe for
me why don’t you
understand?akauliza Agatha
kwa ukali
“Find me somewhere safe
and I’ll tell you everything I
know” akasema Agatha
“Agatha tafadhali
naomba unisikilize.This
place is very safe for you and
for your family.Hakuna
anayejua uko hapa na
hakuna atakayejua kama
uko hapa.Ninaibeba
dhamana ya usalama wako
wewe na familia
yako.Naomba uniamini
tafadhali.Mimi ndiye peekee
unayeweza ukaniamini kwa
maisha yako kwa wakati
hii.Me and my friends we’ll
keep you guys safe I give you
my word” akasema Gosu
Gosu.Rahel akamtazama
kwa muda halafu akasema
“I work for SNSA”
“SNSA? What’s
that?akauliza Gosu Gosu
“Secret Nation security
Agency.Idara ya siri ya
usalama wa nchi
inayojishughulisha na
usalama wa ndani wa nchi”
akasema Agatha na picha ya
Devotha ikapita kwa haraka
katika akili ya Gosu Gosu
“Idara ya siri? Akauliza
“Ndiyo.Hii ni idara
inayofanya kazi zake kwa siri
kubwa hapa nchini na ni
watu wachache sana ambao
wanafahamu uwepo
wake.Mimi nilikuwa katika
kitengo cha udukuzi.Kuna
mambo mengi ambayo
yanafanywa na kitengo hiki
ambayo watu
hawayafahamu.Kila siku
maelfu ya simu zinadukuliwa
tunasikiliza mawasiliano yao
bila wao kujua.Tumekwisha
ingia katika mitandao yote
ya simu iliyopo hapa nchini
na tunao uwezo wa kufuatilia
kila simu tunayoitaka bila ya
wao kujua.Tunaweza
kuwasha mikrofoni ya simu
bila mtu kujua hata kama
simu yake ikiwa imezimwa
na kumfuatilia.Mtu yeyote
tunayemtilia shaka tunao
uwezo wa kumfuatilia ”
akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Nilipewa kazi ya
maalum ya kudukua
mawasiliano yote ya Rais
kujua anawasiliana na nani
na wanawasiliana kuhusu
nini.Hukusanya mawasiliano
ya Rais kwa siku nzima na
kuyaweka katika faili
maalum ambalo mwenye
uwezo wa kulifungua
ukiacha mimi ni Tamar.Kila
jioni ninapowasilisha taarifa
ya siku Tamar hunipatia
shilingi milioni moja na nusu
kama malipo ya kazi
niliyoifanya na hii ni nje ya
mshahara ndiyo maana
sikuacha kuifanya kazi hii
kwani ilikuwa na malipo
mazuri”
“Pesa hizo nyingi Tamar
alizipata wapi? Na kwa nini
akulipe kiasi hicho kikubwa
cha fedha kwa kazi ambayo
ungeweza kuifanya kama
sehemu ya kazi yako ya
siku?akauliza Gosu Gosu
“Alinilipa fedha nyingi ili
kunifanya kwanza nitunze
siri na pili nipate moyo wa
kuendelea kuifanya ile kazi
kwa kujua kwamba ina
malipo mazuri.Kuhusu
anakotoa fedha sikuhitaji
kujua lakini ninachofahamu
Tamar ni tajiri.Anamiliki
magari ya kifahari sana”
akajibu Agatha
“Ulifahamu rekodi zile
anazipeleka wapi
ukishazihifadhi? Gosu Gosu
akauliza
“Hapana sikujua
anazipeleka wapi na
nilitamani sana kufahamu
lakini kutokana na malipo
makubwa aliyokuwa
akinilipa sikutaka
kufuatilia”akajibu Agatha
“Usiku wa leo umempa
balozi Benjamin bahasha ya
khaki ilikuwa na kitu gani
ndani yake?akauliza Gosu
Gosu
“Kama nilivyokueleza
kwamba kazi yangu mimi
ilikuwa ni kukusanya rekodi
zote za mawasiliano ya Rais
na kuzihifadhi katika faili
maalum na baada ya hapo
kazi yangu huwa imekwisha
ninachukua fedha zangu na
kurudi nyumbani.Siku
chache zilizopita nilinasa
mawasiliano ya Rais Dr
Fabian na Rais wa Congo
Patrice Eyenga.Ilikuwa ni
muda mchache baada ya
Yule mwanamama tajiri
Lucy Muganza na mumewe
kuuawa jijini Dar es
salaam.Katika mazungumzo
yao Dr Fabian alimjulisha
Rais Patrice kwamba kazi
imekamilika na Lucy
Muganza tayari
ameuawa,Congo na Afrika
Mashariki watakuwa na
amani.Nilistuka sana baada
ya kunasa mazungumzo hayo
na sikuyaweka katika orodha
ya mawasiliano niliyompa
Tamar.Nilinasa tena
mazungumzo mengine Dr
Fabian akimjulisha Rais
Patrice Eyenga kwamba
kulifanyika makosa madogo
katika operesheni ya
kumuua Lucy Muganza na
umoja wa Ulaya umekwisha
anza kuwa na wasi wasi
kwamba ni serikali yake
ndiyo waliotekeleza mauaji
yale na wametaka
wachunguzi wa kimataifa
waingie nchini kuja
kuchunguza kuhusu mauaji
hayo.Rais Patrice alimpa
pole Dr Fabian kwa
kumsababishia yeye na nchi
yake matatizo yale makubwa
lakini Dr Fabian
alimuhakikishia kwamba
suala lile watalimaliza asiwe
na wasi wasi.Niliingiwa na
hofu ya kumuonyesha Tamar
maongezi hayo kati ya Rais
wetu na Patrice Eyenga na
hivyo nikayaficha.Kutokana
na kufanya kazi mfululizo
bila kupumzika,Tamar
alinipa mapumziko ya siku
tatu kuanzia jana lakini leo
aliniita na kunipa maelekezo
ya kwenda Zimba hotel
kukutana na balozi wa umoja
wa Ulaya hapa nchini bwana
Benjamin Hudson.Alinipa
maelekezo yote ya namna
nitakavyoweza kukutana
naye na kumpatia bahasha
ile”
‘Benjamin hakuwa na
simu ya mkononi uliwezaje
kufanya mawasiliano naye
hadi mkakutana katika lifti?
“Benjamin anatumia saa
yake ya mkononi katika
kuwasiliana.Ana saa
maalum inayotumika kama
simu hivyo ukimpigia katika
namba yake,huonyesha
katika saa na kisha
hubonyeza kidude katika saa
yake na sikioni huwa
ameweka kifaa maalum
kidogo sana cha kusikilizia
maongezi.Hivyo ndivyo
hufanya mawasiliano
yake.Niliyajua haya yote
kutoka kwa Tamar” akajibu
Agatha
“Endelea” akasema Gosu
Gosu
“Nikiwa njiani nilipata
hamu ya kujua kuna nini
ndani ya ile bahasha
nikasimamisha gari na
kuifungua nikakuta kuna
flashi ya kuhifadhia
kumbukumbu nikaichomeka
katika kompyuta yangu
nikakuta kuna rekodi za yale
mazungumzo ya Rais Dr
Fabian na Rais Patrice
Eyenga ambayo sikutaka
kumpa Tamar.Inaonekana
kuna kitu alikigundua ndiyo
maana akanipa siku tatu za
kupumzika na wakati nikiwa
mapumzikoni akapitia upya
rekodi zote za Rais na
kugundua kuna baadhi ya
rekodi nilizificha.Hapo ndipo
nilipogundua kuwa rekodi
zile huwa anampatia
Benjamin lakini sikujua nini
hasa lengo la kufanya vile”
akasema Agatha.
“Pole sana
Agatha.Ahsante kwa kuwa
mkweli lakini nataka
kufahamu kwa nini
hukutaka kumuonyesha
Tamar rekodi hizo za
mazungumzo ya Rais Dr
Fabian na Patrice
Eyenga?Gosu Gosu akauliza
“Niliponasa mazungumzo
yale nikajua Rais wetu
pamoja na Patrice wote
wawili wanahusika katika
mauaji yale ya Lucy
Muganza hivyo sikutaka
jambo hilo lijulikane ndiyo
maana nikayaficha.Kabla ya
kuingia SNSA nilikuwa
nafanya kazi ikulu na Rais
aliyepita Dr Evans ndiye
aliyenipeleka SNSA kwa ajili
ya kumpa taarifa zote
zinazoendelea pale.Baada ya
kuja Rais mpya Dr Fabian
bado nimeendelea kubaki
pale pale.Nikiwa nafanya
kazi ikulu nilikula kiapo cha
kulinda siri hivyo nilijihisi
hatia kubwa sana kufanya
kile nilichokuwa nakifanya
kudukua mawasiliano ya
Rais lakini sikuweza kukataa
kwani yalikuwa ni maagizo
ya wakubwa wangu”
“Good job
Agatha.Unadhani…oh my
God ! Gosu Gosu akashindwa
kuendelea na kushika
kichwa.
“Suala hili limekuwa
kubwa.Idara nyeti ya serikali
tayari imekwisha ingiliwa”
akawaza Gosu Gosu
“Nataka uniambie
kuhusu Tamar ?Who is she?
Akauliza Gosu Gosu
“Ndiye kiongozi wa SNSA
kwa sasa”
“Kuna mtu anaitwa
Kaiza.Do you know him?
“Kaiza?
“Ndiyo.Unamfahamu?
“Kaiza is dead.Alifariki
mwaka jana.Alikutwa
amefariki katika chumba cha
hoteli nchini Afrika
kusini”akasema Agatha
“Baada ya Kaiza kufariki
dunia ndipo alipoletwa
Tamar kuchukua nafasi
yake.Umemfahamuje Kaiza?
“He was a friend of mine”
“Unafahamu kuhusu
idara hii ya siri?akauliza
Agatha
“Ndiyo ninaifahamu
kidogo.Aliwahi kunieleza
Kaiza” akasema Gosu Gosu
“Who are you?akauliza
Agatha
“Naitwa Gosu Gosu.Mimi
na kikosi cha rafiki zangu
tulipata taarifa kwamba
Lucy Muganza anakuja
Tanzania.Mwanamke Yule
tajiri alikuwa anatumiwa na
mataifa makubwa ya nje
kwanza kwa ajili ya kutaka
kuisambaratisha jumuiya ya
Afrika mashariki na pili
kuleta machafuko nchini
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo ili mabeberu hao
wanaomtumia waweze
kupata nafasi ya kuendelea
kuchota rasilimali.Mimi na
wenzangu ndiyo tuliofanya
tukio lile.We killed her.”
Akasema Gosu Gosu na
Agatha akamtazama kwa
mshangao.
“Najua nimekustua
Agatha lakini ni kweli mimi
na wenzangu ndiyo
tuliomuua Lucy
Muganza.Mwanamke Yule
alikuwa hatari sana kwa
nchi yetu na jumuiya ya
afrika Mashariki.Kuna
mpango mkubwa
unaandaliwa na nchi kubwa
kwa ajili ya kusambaratisha
jumuiya ya Afrika
Mashariki.Mpango
unaandaliwa pia kwa ajili ya
kuiondoa madarakani
serikali ya jamhuri ya
kidemokrasi ya Congo na
Lucy Muganza ndiye
aliyekuwa ameandaliwa kwa
ajili ya kushika nafasi ya
Rais wa Congo.Baada ya
kugundua mpango huo
ikatulazimu kumuondoa na
kitendo hicho kimeleta
mtafaruku mkubwa
sana.Kuna vita kubwa ya
chini chini inaendelea hivi
sasa baada ya Lucy Muganza
kuuawa.Umoja wa Ulaya
wanataka wachunguzi wa
kimataifa waweze kuingia
nchini kufanya uchunguzi wa
kifo hicho.Kikubwa
wanachokitafuta hapa ni
ushahidi wa kumuhusisha
Rais wetu na mauaji
hayo.Ulifanya jambo la
kizalendo sana kutowapa
rekodi za mazungumzo kati
ya Rais wetu na Rais Patrice
Eyenga.Naamini walikuwa
wanazitafuta sana taarifa
hizo lakini tumechelewa
kwani tayari wamekwisha
zipata kupitia flashi ile
uliyompa balozi Benjamin
usiku huu”akasema Gosu
Gosu
“Hapana bado
hawajazipata.Nilipogundua
kilichomo ndani yake nilifuta
rekodi zile na kupandikiza
kirusi katika ile flashi
nadhani baada ya kugundua
nilichokifanya ndipo
walipoanza kunitafuta
waniue”akasema Agatha
“Ulifahamu fika kwamba
wangegundua ulichokifanya
lakini bado ukafanya.Kwa
nini?Ulijiamini nini?
Akauliza Gosu Gosu
“I have money.Lot’s of
money hivyo nilikuwa
nimejiandaa kesho niondoke
zangu nchini.Tayari nilikuwa
na tiketi za ndege kwa ajili
ya kuelekea nchini China”
“Agatha unadhani Tamar
kiongozi wako anashirikiana
na balozi Benjamin kwa ajili
ya fedha au kuna jambo
lingine?
“I think it’s more than
money.Baada ya kunielezea
kile kinachoendelea hivi sasa
hapa nchini nimeanza
kupata picha kamili kuhusu
Tamar.There’s must be
something bigger than
money.Ili kujua
kinachoendelea kati yao
lazima kwanza
mumchunguze
Tamar”akasema Agatha.
“One more thing”
akasema Agatha na kutulia
kidogo
“Sikumpa balozi
Benjamin ile flashi
niiyotumwa nimpelekee
lakini haina maana kwamba
hataweza kupata zile rekodi
kwa kuwa bado zipo katika
hifadhi za SNSA.Ili
kujihakikishia kwamba Rais
yuko salama katika hili
tunapaswa kuharibu mfumo
mzima wa kuhifadhi
kumbukumbu za SNSA na
vile vile……….” Akanyamaza
kidogo
“Endelea Agatha
“Kuipata kompyuta ya
Tamar.Kila jioni huhifadhi
rekodi zote nilizozipata kwa
siku katika faili maalum
ambalo tunaoweza
kulifungua ni mimi na
Tamar pekee na faili hilo
limeunganishwa na
compyuta ya Tamar na
anaweza akalifungua hata
akiwa mbali na ofisi yake”
akasema Agatha na
kunyamaza baada ya Austin
kuingia mle ndani.Agatha
akaonyesha woga kidogo
“Agatha huyu anaitwa
Austin January ni mkuu wa
kikosi cha jeshi cha
operesheni maalum na ndiye
kiongozi wangu.Mimi na yeye
tunashirikiana katika yale
niliyokueleza na huyu ndiye
kiongozi wangu” Gosu Gosu
akafanya utambulisho na
kisha akamueleza Austin
yale yote aliyoelezwa na
Agatha.
“Dah ! Pole sana Agatha
na hongera pia kwa ujasiri
mkubwa uliouonyesha.Hapa
ulipo uko sehemu salama
kabisa na mimi na wenzangu
tunakuahidi kukulinda kwa
kila namna
tunavyoweza.Ahsante sana
kwa kutupa taarifa hii
muhimu.Kwa sasa kitu
ambacho tunatakiwa
kukifanya kwa haraka ni
kuharibu hilo faili ambalo
umekuwa ukihifadhi rekodi
zote za mazungumzo ya simu
ya Rais”akasema Austin
“Ili kuharibu faili hilo
ninapaswa kuharibu mfumo
wote wa SNSA.Ninaweza
kupandikiza kirusi katika
mfumo huo na kuuharibu
lakini nina hofu yawezekana
hadi sasa tayari nitakuwa
nimekwisha ondolewa katika
mfumo na sintakuwa na
uwezo wa kuingia na
kufanya chochote.We need
someone from inside”
akasema Agatha
“Kuna mtu yeyote
unayemuamini anayeweza
kukusaidia bila kuhatarisha
maisha yako? Akauliza
Austin.Agatha akafikiri
kidogo na kusema
“Kuna kijana mmoja
anaitwa Samson.Huyu
nimekuwa nikimsaidia na
kumfundisha mambo
mengi.Anaweza akanisaidia”
“Good.You can call him”
akasema Austin na kumpatia
simu yake akapiga
“Hallow ! ikasema sauti
ya kiume upande wa pili
“Hallo Sam it’s me
Agatha.Where are
you?akauliza Agatha
“Niko barabarani
ninaelekea nyumbani.Agatha
nini kimetokea leo?Ujumbe
umesambazwa kwamba
kuanzia sasa wewe ni mtu
hatari sana kwa idara na
yeyopte atakayekuona au
kujua mahala ulipo atoe
taarifa haraka
sana.Umefanya nini?
“Samson sina muda wa
kueleza kwa sasa ila kuna
jambo kubwa linaloendelea
hapo katika idara
yetu.Nitakueleza siku
nyingine,kwa sasa
nimekupigia nahitaji msaada
wako” akasema Agatha
“What do you
need?akauliza Samson
“I need access to our
system”
“What?Are you Crazy
Agatha? How can you access
the system? Tayari
umekwisha ondolewa katika
mfumo nakushauri tafadhali
huko uliko endelea kujificha
kwani ukijaribu kufanya
chochote watajua mahala
ulipo”
“Sikiliza Samson.Nataka
unisaidie niingie katika
mfumo kwa kupitia akaunti
yako.Kuna mambo nataka
niyafanye ambayo kama
nisipoyafanya yataniletea
matatizo makubwa.Samson
ni wewe pekee
ninayekutegemea kwa sasa
unisaidie katika
hili.Nimekuwa msaada
kwako kwa muda mrefu sasa
ni wakati wako
kunisaidia.Please Samson I
need help” akasema
Agatha.Zilipita sekunde
kadhaa Samson akasema
“Agatha unaniweka
katika hatari kubwa.Hata
hivi nnavyozungumza nawe
ni hatari kubwa kwani
wanaweza wakajua”
“Samson please.Help me”
akasema Agatha
“What do you want me to
do?
“I need you to go back
there to the server room and
I’ll direct you what to do”
akasema Agatha
“Sawa Agatha naomba
unipe dakika kumi nirejee
ofisini nitakupigia
nikishafika”
“Ahsante sana Sam and
I’m so sorry for this.Sina mtu
mwingine wa kumkimbilia
zaidi yako” akasema Agatha
“Usijali Agatha”
“Sam jambo lingine
naomba usilitaje jina langu
utakapokuwa unazungumza
na mimi ili watu
wasijue.Sitaki kukuweka
katika matatizo”
“I’m already in touble
anyway” akasema Samson na
kukata simu kisha Agatha
akaelekea chumbani
kuchukua kompyuta yake
Baada ya muda mfupi
Agatha akarejea akiwa na
kompyuta yake akaiwasha
akajaribu kuingia katika
mfumo wa SNSA lakini
namba alizoingiza hazikuwa
sahihi
“Nilijua tu tayari
nimekwisha fungiwa”
akasema Agatha
“Agatha wakati
tunamsubiri Samson afike
ofisini nataka kumfahamu
vizuri huyu Tamar.Umekuwa
naye karibu hadi akakuamini
kufanya kazi ya hatari kama
hii ya kudukua mawasiliano
ya Rais.Nataka kumfahamu
ni mtu wa aina gani?Austin
akauliza
“Ni kweli nimekuwa na
ukaribu na Tamar na
hakuona mtu mwingine wa
kumpa kazi ile zaidi yangu
na nimeifanya kwa uaminifu
mkubwa kuhusu Tamar ni
mtu msiri sana.Ni mtu
mwenye kuchukua tahadhari
kubwa kila wakati.Hapendi
mambo yake binafsi
yajulikane.Anaishi peke yake
na mfanyakazi wake
hajawahi kuzungumzia
chochote kuhusu kuwa na
familia…” akanyamaza
Agatha baada ya simu ya
Austin kuita
“Samson” akasema
Austin na kumpatia simu
Agatha
“Hello Sam” akasema
Agatha
“Tayari nimefika.Nipe
maelekezo unayotaka”
akasema Samson kwa sauti
ndogo
“Good.Nataka unipe
namba za kufungulia akaunti
yako” akasema Agatha na
Samson akampa namba zake
Agatha akaifungua akaunti
ya Samson halafu akaenda
hadi katika faili lile
anakohifadhi rekodi zote za
Rais akajaribu kulifuta
lakini Samson hakuwa na
uwezo wa kulifuta faili lile
ambalo waliokuwa na uwezo
wa kuingia na kulifuta ni
Agatha na Tamar pekee
“Nimejaribu kuingia
katika mfumo kwa kutumia
akaunti ya Samson lakini
imeshindikana kulifuta
faili.Only one option left.To
destroy the whole system”
akasema Agatha
“Do it”akasema Austin
na Agatha akapandikiza
kirusi katika mfumo wao na
mara tu Samson
alipoufungua ujumbe wenye
kirusi kile kikaanza
kusambaa kwa haraka
katika mfumo na ndani ya
muda mfupi mfumo wote
ukasambaa kirusi na kuanza
kuleta mauza uza.
“Done” akasema Agatha
na kuifunga akaunti ya
Samson na
“Samson nakushukuru
sana kwa msaada
wao.Nitakutafuta nikueleze
nini kilichonitokea”
“What have you done?
akauliza Samson
“Get out of there now
Samson” akasema Agatha na
kukata simu
“Nimemaliza.Mfumo
wote umeharibika
kinachofuata ni kuitafuta
kompyuta ya Tamar ambayo
lazima itakuwa na hifadhi ya
zile rekodi” akasema Agatha
“This is another
mission.Hakuna kulala usiku
huu wa leo lazima
tuhakikishe kwa namna
yoyote ile tuanipata
kompyuta ya Tam……….”
akasema Austin na
kunyamaza baada ya Stanley
kutokea alikuwa anahema
kwa kasi
“Stanley kuna
nini?akauliza Gosu Gosu
“Limetokea shambulio
katika ukumbi walimo akina
Nasib.Nikiwa nafuatilia
kilichokuwa kinaendelea
ukumbini mle kupitai
kamera ya Nasb waliingia
watu wapatao sita wakiwa
wamefunika nyuso zao na
kuanza kumimina risasi
hovyo.Sijaweza tena kupata
pich a nyingie kwani
mawasiliano na Nasibu
yamekatika” akasema
Stanley na Austin
akachukua simu na kupiga
namba ya Nasib simu
ikaanza kuita lakini
haiupokelewa.Akapiga tena
lakini haikupokelewa.Wote
wakabaki wamesimama
wakitazamana.
“We need to go back
there” akasema Austin
“Austin mahala pale ni
hatari sana kwa sasa” `
“I have my men in there.I
need to g………..” Austin
akanyamaza baada ya simu
yake kuita alikuwa ni
Nasib.Austin akaipokea
haraka haraka
“Nasibu mambo
yanakwendaje huko?
“Mkuu …” akasema
Nasibu akihema kwa nguvu.
“Nasibu nini kimetokea
hapo?akauliza Austin
“Something happened
here”
“Nini kimetokea?Nieleze
tafadhali”
“balozi Benjamin
ameuawa”
“What?Austin akastuka
“Balozi Benjamin
ameuawa”
Austin akashusha pumzi
na kuuliza
“Nasib tafadhali naomba
unieleze kama taarifa hizo ni
za kweli”
“Kweli kabisa
mkuu.Balozi Benjamin
amefariki.Ameuawa muda
mfupi uliopita”
“Kauawa?Nani
kamuua?akauliza Austin
“Wakati sherehe
zikiendelea waliingia watu
sita wakiwa na silaha huku
wakiwa wamefunika nyuso
zao wasionekane.Walianza
kumiminia watu risasi hovyo
hovyo na kuwaua.Balozi
Benjamin alikuwa mmoja wa
watu waliopigwa risasi kwa
haraka sana baada ya watu
wale kuingia ukumbini na
akafariki pale pale.Mimi
nilikuwa sehemu ya juu
hivyo niliweza kuona
kilichokuwa kinaendelea
upande wa chini.Nilimuona
jamaa mmoja akimfuata
balozi na kuanza
kummiminia risasi ili
kuhakikisha amekufa kabisa
halafu akamvua saa ya
mkononi,akamsachi mfukoni
na kuchukua vitu
fulani.Inaonekana
waliyekuwa wamemlenga ni
balozi Benjamin kwani baada
tu ya kuhakikisha amekufa
wakaondoka zao”
“Wewe na vijana wengine
wote mko salama?
“Wote tuko salama
kabisa mkuu.Mimi nilikuwa
upande wa juu nikajificha
katika nguzo huku
nikishuhudia kilichokuwa
kinaendelea upande wa
chini.watu wengi wameuawa
hapa lilikuwa ni tukio la
kinyama sana.Wenzangu
waliokuwa upande wa nje
wanasema kwamba watu
wale waliondoka kwa
kutumia magari mawili
ambayo hayakuwa na namba
huu wakipiga risasi
hovyo.Tukio hilo limetokea
haraka sana na hatukuweza
kufanya chochote”
“Poleni sana
Nasib.Hakuna mnachoweza
kufanya hapo kwa
sasa.Rudini hapa nyumbani
tujipange”akasema Austin na
kukata simu
“Balozi Benjamin
ameuawa”akasema Austin
“Mungu wangu !
akasema Agatha
“Kwa mujibu wa Nasib
kuna watu sita waliokuwa na
silaha wameingia ukumbini
nak uanza kuwafyatulia
watu risasi hovyo na balozi
alikuwa mmoja wa watu wa
mwanzo kushambuliwa kwa
risasi.Kuonyesha kwamba
balozi ndiye aliyekuwa
amelengwa mmoja wa
washambuliaji alimfuata na
kummiminia risasi
kuhakikisha wanamuua
kabisa”akasema Austin
“Haya lazma ni mauaji
ya kupangwa na
ninakubaliana na Austin
kwamba aliyekuwa mlengwa
hapa ni balozi
Benjamin.Nani anaweza
kuwa amefanya mauaji
haya?akauliza Gosu Gosu
“Ni vigumu kwa sasa
kujua nani aliyepanga
mauaji haya lakini sababu
kuu ilikuwa ni kumuua
balozi Benjamin”
“Wameturudisha nyuma
sana.Tayari tulikwisha anza
kupata mwangaza lakini kifo
cha Benjamin kimeuzima
mwangaza ule”akasema
Gosu Gosu
“Natakiwa kumpigia
simu Rais kumjulisha
kuhusu jambo hili” akasema
Austin na kumpigia simu Dr
Fabian
“Austin habari za usiku
huu?
“Habari si nzuri sana
mheshimiwa Rais.Kuna
tukio limetokea usiku huu
muda mfupi uliopita.Balozi
Benjamin ameuawa akiwa
katika hafla ya uchangiaji
ujenzi wa mabweni ya watoto
waishio katika mazingira
magumu”
“Ameuawa? Dr Fabian
akashangaa
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Balozi Benjamin
ameuawa.Ukumbi ulivamiwa
na watu wasiojulikana
waliofunika nyuso zao
wakaanza kumimina risasi
ukumbini na kuua watu
hovyo.Balozi Benjamin na
mke wake wameuawa na
inaonekana wao walikuwa
walengwa wakuu wa
shambulio kwani baada ya
kuhakikisha wamefariki
dunia wauaji hao
wakaondoka zao”akasema
Austin ukapita ukimya mfupi
“Mheshimiwa Rais”
akaita Austin
“Austin nimestushwa
sana na taarifa hizo.Wewe
ndiye wa kwanza
kunijulisha.Nitawasiliana na
vyombo vya ulinzi kupata
taarifa kamili ya nini
kimetokea hapo na watu
wangapi wameuawa.Kuna
chochote mlichokuwa
mmekipata kabla ya balozi
kuuawa?akauliza Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais,kuna
jambo tulikuwa tumelipata
na tunaendelea kulifuatilia
tutakapolikamilisha nitakuja
kukufahamisha” akasema
Austin
“Austin hakikisha
mnawajua nani waliomuua
balozi Benjamin kwani suala
hili linaonekana ni kubwa
zaidi ya tunavyodhani”
akasema Dr Fabian
“Sawa mheshimiwa
tutafanya hivyo” akajibu
Austin na Dr Fabian akakata
simu Austin akamgeukia
Gosu Gosu
“Rais anataka tuwapate
waliomuua balozi
Benjamin.Sehemu pekee ya
kuanzia uchunguzi wetu
kuwafahamu waliomuua
Benjamini ni kwa
Tamar.Nina uhakika kubwa
anaweza kuwa na mahusiano
na mauaji hayo”akasema
Austin
“Kwa nini Tamar ahusike
katika kumuua balozi
Benjamin ambaye ni
mshirika wake mkubwa?Kwa
maelezo ya Agatha picha
tunayoipata ni kwamba
rekodi zile alizokuwa
anazikusanya Tamar
alikuwa anazipeleka kwa
balozi Benjamin na nina
uhakika kwamba fedha
alizokuwa akilipwa Agatha
zilitoka kwa
Benjamin.Tamar naye lazima
alikuwa akipata fedha nyingi
sana kwa ajili ya kazi
hiyo.Kama alikuwa
akifaidika wa kudukua
mawasiliano ya Rais kwa
nini ashiriki kumuua mtu
aliyekuwa anamuuzia taarifa
hizo? Akauliza Gosu Gosu
“Hata mimi napata
shaka kama Tamar anaweza
kuhusika na mauji hayo
lakini tukirejea katika
taarifa ya Nasib ni kwamba
watu wale walipoingia tu
Benjamin alikuwa ni mtu wa
mwanzo kulengwa risasi na
kuonyesha kwamba
walimlenga yeye mmoja wa
wauaji alimfuata
akamuongeza risasi na kisha
akamvua saa ya mkononi
halafu akampekua na
kuchukua kila kitu
alichokuwa nacho na hii ina
maanisha kwamba ile flashi
aliyopewa na Agatha
wameichukua hawa
wauaji.Kwa picha hii
inaonyesha wazi kwamba
wauaji walifahamu fika
kwamba balozi Benjamin
anatumia saa ya mkononi
katika kuwasiliana pili
walifahamu kuhusu flashi
aliyopewa na
Agatha.Aliyepanga mauaji
haya ni mtu ambaye
anamfahamu vizuri sana
Benjamin Hudson na katika
watu ambao lazima
tuwachunguze Tamar ni
mmoja wao” akasema Austin
na kunyamaza baada ya
simu yake kuita alikuwa ni
Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais”
akasema Austin
“Austin nimepata taarifa
sasa hivi kwamba nyumba ya
balozi Benjamin inawaka
moto hivi sasa.Unadhani
moto huo unaambatana na
tukio la kuuawa kwake?
“Nahisi hivyo
mheshimiwa rais kwani
muda wa kutokea kwa
matukio haya mawili
umekaribiana
sana.Nalazimika kuamini
kwamba waliomuua
Benjamin ni hao waliochoma
nyumba yake”
“Mpaka sasa kuna lolote
mmekwisha lipata kuhusu
mauaji hayo?akauliza Dr
Fabian
“Mpaka sasa bado
hatuna fununu zozote lakini
tunajipanga kuanza
uchunguzi wetu” akasema
Austin
“Taarifa niliyoipata
kutoka kwa mkuu wa jeshi la
polisi ambaye yuko eneo la
tukio ni kwamba mpaka sasa
watu hamsini na sita
wamefariki dunia na
wengine wamekimbizwa
hospitali na kuna uwezekano
idadi ya vifo
ikaongezeka.Tafadhali
fanyeni juu chini kuweza
kujua aliyemuua balozi
Benjamin” akasema Dr
Fabian akakata simu
“Nyumba ya balozi
Benjamin inawaka moto
ndiyo taarifa aliyonipa Rais”
akasema Austin
“Dah ! akasema Gosu
Gosu.Taarifa ile
ilimshangaza sana
“Hata mimi nalazimika
kuamini kwamba
walioichoma nyumba ya
Benjamin ni wale wale
waliomuua.Swali
ninalojiuliza kama kumuua
tu haikutosha kwa nini
wakaenda kuichoma nyumba
yake kuna nini hapa
wanakificha?akauliza Gosu
Gosu
“Swali hilo ndilo
tunatakiwa kulitafutia
majibu.Agatha tuelekeze
tafadhali nyumbani kwa
Tamar.Suala hili haliwezi
kusubiri.Tunaanza
kumfuatilia usiku huu huu”
akasema Austin
PARIS – UFARANSA
Milio ya wadudu ndiyo
iliyotawala usiku huu katika
sehemu tulivu kuzunguka
ziwa dogo ambako Peniela na
mpenzi wake Nahum
walikwenda
kupumzika.Angani kulikuwa
na mbalamwezi kali
ikimulika na wapenzi hawa
walikuwa wamekaa nje
katika kibaraza huku moto
wa kuni ukiwaka mbele
yao.Walinzi wa Peniela
walikuwa wamejipanga
mbali kidogo kuwapa
wapenzi hawa nafasi ya
kuwa peke yao.
“Peniela kwa muda huu
mfupi niliokutana nawe
ninakiri kwamba nimeishi
maisha yangu yote hata
nikifa leo sina wasi
wasi.Nimeipata ile furaha
yote ya maisha yangu
niliyoihitaji” akasema
Nahum
“Nahum mpenzi una nini
leo?Kutwa nzima ya leo
umekuwa ukizungumzia
masuala ya kufa”akasema
Peniela
Nahum akatabasamu na
kuuchukua mkono wa
Peniela akambusu kiganjani.
“Maisha haya ni mafupi
sana Peniela.Ukipata nafasi
ya kufurahi itumie
kikamilifu kwani huwezi
kujua nini kinafuata mbele
yako.Kifo kimetuzunguka
kila mahali” akasema
Nahum
“Nahum sitaki kusikia
ukizungumzia habari ya kifo
tena.Tumekuja hapa
kufurahi na si
kuhuzunika.Kifo kipo na sote
tutakufa hivyo tusiongelee
masuala hayo kwa sasa”
akasema Peniela
“Sawa malaika
wangu,lakini naomba
ufahamu wewe ni
mwanamke wa pekee kabisa
ambaye sijawahi kukutana
naye katika maisha
yangu.Naomba nikiri jambo
moja kwako”
“Nakusikiliza” akasema
Peniela huku akitabasamu
“Kwa muda mrefu
nimekuwa mchezeaji tu
wanawake na sikuwahi
kupenda.Nimekutana na
wanawake wengi na ……..”
Nahum akanyamaza baada
ya mmoja wa walinzi wao
kutokea akikimbia
“Ingieni ndani
harak……..” Hakumaliza
alichokuwa anawaeleza
akina Peniela
akapigwa risasi ya mgongo
akaanguka chini.Kwa kasi ya
aina yake Nahum akaruka
kutoka mahala alipokuwa
amekaa akamrukia Peniela
wakaanguka chini ya kiti.
“Peniela nisikilize.Watu
hawa wananitafuta mimi
wamekuja kuniua hivyo
kama nikifa nakuomba
umtafute Mathew
Mulumbi.Yuko hai”
“Nahum !! akasema
Peniela
“Nisikilize
Peniela.Mathew Mulumbi
yuko hai.Tafadhali mtafute”
akasema Nahum na
kusimama akitaka kukimbia
akapigwa risasi tatu na
kuanguka chini akafa pale
pale.
Peniela mwili
ulimtetemeka alikosa nguvu
akabaki amejificha chini ya
kiti.Baada ya dakika tano
kupita akasikia sauti
ikimuita
“Mama Peniela ! Mama
Peniela ! ilikuwa ni sauti ya
mmoja wa walinzi
wake.Peniela hakuweza
kufungua mdomo wake
kuitika.Walinzi wale
walikuwa na tochi
wakamulika eneo lile ambalo
liikuwa giza baada ya taa
kupasuliwa wakamuona
Peniela akiwa amejificha
chini ya kiti.Hatua chache
mbele yake alilala Nahum
akiwa hana uhai.Mmoja wa
walinzi wale akamfunika
Peniela koti kisha
wakamuinua na kumpeleka
katika gari wakaondoka kwa
kasi eneo lile wakipishana na
magari ya askari
waliojulishwa kuhusu
kutokea kwa mauaji yale.
“Nini kimetokea?Nani
kafanya mauaji yale?Peniela
akawauliza walinzi wake
“Mpaka sasa hatujui nani
kafanya mauaji yale lakini
nilichokishuhudia mimi ni
watu waliovaa makoti
marefu na kufunika nyuso
zao wakiwa na bunduki za
kulenga masafa marefu
wakitoweka katika
msitu.Usihofu mama
tutachunguza na tutajua ni
nani waliofanya tukio lile”
akasema mmoja wa walinzi
“Hivi ni kweli Nahum
amekufa au niko
ndotoni?akajiuliza Peniela na
kuendelea kumwaga machozi
,akakumbuka namna
alivyomuona Nahum
akipepesuka huku
akichakazwa risasi
“Huu ni mkosi gani
unanikuta mimi?Kila
mwanaume ambaye
ninakutana naye na moyo
wangu ukampenda
hadumu.Mathew alipotea na
sasa Nahum”akawaza na
kuendelea kulia
TEL AVIV – ISRAEL
Simu ya Efraim Dagan
aliyekuwa na maafisa
wengine wa Mossad pamoja
na maafisa wa gereza ambalo
Mathew Mulumbi
alifungwa,ikaita akatoika nje
na kuipokea
“Hallow” akasema
Efraim
“Mkuu tumeimaliza
kazi.Nahum tayari amekufa”
“Kazi nzuri sana.Mna
hakika hakutakuwa na tatizo
lolote?
“Tumemuondoa
kiumakini sana hakutakuwa
na tatizo lolote hata hivyo
tulilazimika kuwaua pia
walinzi wachache wa Peniela
ndipo tukaweza kumfikia
Nahum”
“Ahsanteni sana kwa
kazi hii nzuri” akasema
Efraim na kukata simu
“Nahum alikuwa ni
mmoja wa watu wetu wa
muhimu sana lakini
alichagua mapenzi akasahau
kazi na hivyo kuhatarisha
maisha yake mwenyewe na
ya shirika.Amekipata
alichokihitaji” akawaza
Efraim na kurejea ndani
walikuwa wanaendelea
kufuatilia kile
kinachoendelea chumbani
alimo Mathew Mulumbi na
Ammar Nazari
“Ammar muda
umewadia.Nataka kupata
tena uhakika kutoka kwako
kama uko tayari kuendelea
na mpango wetu wa
kutoroka” akasema
Mathew.Ammar akawaza
kidogo halafu akasema
“Tuendelee na mpango
wetu Abu.Ninataka
kuondoka humu ndani”
akasema Ammar
“Safi sana.Kila kitu
kitakwenda kama
tulivyopanga” akasema
Mathew na Ammar akatikisa
kichwa kukubaliana naye
halafu Mathew akalala
sakafuni kama mtu
aliyepoteza fahamu.Ammar
akasogea karibu na mlango
akanyoosha mkono na
kubonyeza kitufe cha kengele
ya dharura.
“Mambo yameanza”
akasema Efraim akiwa
katika ofisi ya mkuu wa
gereza.
Askari wawili wa gereza
walifika katika mlango wa
chumba cha akina Mathew
na kuuliza kuna nini,Ammar
akawajulisha kwamba
mwenzake Abu ambaye ni
Mathew ameanguka ghafla
na kupoteza fahamu.Mlango
ukafunguliwa na askari wale
wakaingia ndani,Ammar
akatakiwa kusogea kwenye
kona wakati askari mmoja
akienda kumtazama
Mathew.Akammulika tochi
machoni halafu akapiga
magoti ili aweze kumtazama
vizuri mara kwa kasi ya
ajabu akajikuta amedakwa
shingo yake akageuzwa na
kuangushwa chini akataka
kuinuka lakini akapigwa
ngumi nzito akalala
sakafuni.Lilikuwa ni tukio
lililotokea kwa kufumba na
kufumbua.Mara tu Mathew
alipomvamia askari Yule
aliyekuwa
anamuangalia,askari
aliyekuwa na Ammar
akageuka kutazama nini
kimetokea ndipo Ammar
akamrukia kama Simba
anayerukia windo akampiga
kichwa kizito akaanguka
chini halafu akaiokoa
bunduki akampiga na kitako
kichwani akamuinua na
akamkaba na kumvunja
shingo kisha akamtupa chini
“Nimeingia kwenye
ulimwengu wa makatili”
akawaza Mathew.Ammar
akachukua mto akaukunja
halafu akachukua bastora ya
Yule askari aliyekuwa
amedhibitiwa na Mathew
akamuwekea kichwani
akaachia risasi na
kumfumua kichwa.
“Tulipanga kutokuua
askari lakini huyu jamaa
ameamua kuua.Nikimzuia
anaweza akaingiwa na
mashaka” akawaza Mathew
na haraka haraka
wakawavua sare wale askari
wakavaa na kuchukua redio
ya mawasiliano pamoja na
kadi ya kufungulia
milango.Wakawaficha askari
wale chini ya kitanda
“Uko tayari?akauliza
Mathew
“Niko tayari” akajibu
Ammar.Mathew akachukua
ramani ile ya gereza
wakaipitia kisha wakatoka
kwa tahadhari wakafunga
mlango.
“Tulikubaliana kutokuua
askari.Mbona wameua askari
wangu?akafoka mkuu wa
gereza.
“Kama Mathew
angemzuia Ammar kutokuua
wale askari angeweza
kuingiwa na wasi wasi ndiyo
maana akaamua kumuacha
awaue”akajibu Efraim
Mathew na Ammar
wakifuata ramani ile
waliyopewa walipita korido
la kwanza halafu wakatokea
katika ngazi wakapanda na
kutokea katika korido la
pili.Kwa mbele wakawaona
askari wakajibanza
wakasubiri askari wale
wapite halafu wakatembea
haraka haraka wakakuta
kuna njia mbili wakafuata
njia ya kushoto wakaifuata
njia ile na mara tu
walipolifikia geti la kwanza
king’ora cha hatari
kikalia.Askari wakaanza
kukimbia kwenda kujua nini
kimetokea.Walipitisha kadi
katika geti lile la kwanza
likafunguka wakavuka na
kukimbia hadi katika ujia
ambao walikuta askari
watatu wakikikimbia
,Ammar akawamiminia
risasi.Mathew akaitazama
ramani akakuta lazima
waruke ukuta kuingia
upande wa pili haraka
haraka akamtaka Ammar
kuinama akapanda juu ya
mgongo na kushika kingo za
ukuta kisha akamvuta
Ammar naye akapanda
wakajirusha upande wa
pili.Walikwaruzwa na
seng’enge zilizokuwa juu ya
ukuta.Mathew akainuka na
kumtaka Ammar waendelee
baada ya kusikia katika
redio kwamba wafungwa
waliotoroka wamevaa sare za
askari.Mathew akiwa
ametangulia mbele mara
ghafla wakamulikwa na tochi
zenye mwanga mkali na
kutakiwa kusimama.Kwa
kasi ya aina yake Mathew
aliyekuwa ametangulia
mbele akajitupa chini na
Ammar akamimina risasi
askari watatu wakaanguka
chini kisha wakakimbia
kuelekea katika geti la
pili.Wakati Mathew
akijandaa kufungua geti lile
mara Ammar akatoa mguno
wa maumivu alikuwa
amepigwa risasi ya mguu
akaangua chini.
“Nimepigwa risasi ya
mguu !! akalalama
Ammar.Mathew akageuka
na kumimina risasi halafu
akamfuata Ammar
akamuinua na kumtaka
ajitahidi wamekaribia.
“Ammar jitahidi utembee
tunakaribia sana kufika
katika ule mfereji mkubw..”
akasema Mathew na risasi
zikaanza kuvuma akamkinga
Ammar na kuanza kumimina
risasi halafu akamuinua na
kuvuka geti mara Ammar
akapigwa tena risasi
nyingine ya mguu
ikamlazimu Mathew
kumuinua na kumuweka
begani
“Naona mambo yanaanza
kuwa magumu.Mpango
ulikuwa apigwe risasi moja
lakini amepigwa
mbili.Yawezekana kuna
askari ambao hawajui
kuhusu huu mpango wa
kutoroka.Kinachofuata kwa
sasa ni kuwafagia tu kila
atakayetukaribia kwani
tukifanya mchezo wanaweza
wakatumaliza hawa.”
Akawaza Mathew na mara
taa zikazima.Hii ilikuwa ni
ishara kwamba wanakaribia
kufika katika mfereji
mkubwa wa maji taka.Katika
mfuniko wa kuingilia katika
mfereji wa maji taka
kulikuwa kimya lakini
Mathew akageuka na
kumimina risasi kwa nyuma
kana kwamba kuna watu
walikuwa wanawafuatilia
halafu akamuweka chini
Ammar akalifungua geti
akambeba Ammar hadi
katika mfuniko.Akachana
shati lake na kumfunga
Ammar pajani halafu
akautafuta mfuniko
akauona.Ulikuwa ni mfuniko
mkubwa wa zege akajitahidi
kuusogeza pembeni
akashindwa
“Natakiwa kujitahidi
vinginevyo wakitukuta hapa
watatuua” akawaza Mathew
na kukusanya nguvu
akausukuma mfuniko ule
ukasogea akajitahidi tena
ukasogea zaidi akamulika
ndani na kuziona ngazi za
kushukia chini.Haraka
haraka akamfuata Ammar
akamsogeza pale kwenye
shimo na kuanza kumshusha
chini taratibu kisha
wakaanza kutembea katika
maji yaliyokuwa na
harufu.Baada ya dakika
kumi na moja wakazikuta
ngazi ambazo kwa mujibu wa
maelekezo aliyopewa
Mathew zinatokea
barabarani Mathew
akapanda na kuusukuma
mfuniko wa chuma
akachungulia nje ni kweli
walikuwa
barabarani.Akampandisha
Ammar na kuufunika
mfuniko ule wa chuma
akamtegemeza wakavuka
barabara wakaanza
kutembea hadi walipokuta
daraja wakaingia kwa chini
wakajificha
“Tuko nje ya gereza
sasa” akasema Mathew
“Ahsante sana Abu.Bado
naona kama ni ndoto”akajibu
Ammar akihisi maumivu
makubwa
“Si ndoto ni kweli kabisa
tuko nje ya
gereza.Kinachotakiwa sasa
ni kutafuta namna ili uweze
kupata matibabu kwanza
kuondoa risasi ambazo
umepigwa na pili
kuongezewa damu.Dr Abeba
atafika kutupeleka sehemu
salama”
“Unamuamini huyo
Abeba?akauliza Ammar
“Ndiye aliyetusaidia
tukafika hapa na ndiye
atakayetusaidia tuweze
kuondoka hapa Israel
salama” akasema Mathew na
magari kadhaa yakapita pale
juu ya daraja.
“Tutafute namna
nyingine ya kujiokoa huyo
mtu wako hawezi kuja
tena.Ninazidi kupoteza damu
nitakufa”akasema Ammar
akiwa katika maumivu
baada ya kusubiri kwa muda
bila Abeba kutokea
“Vuta subira
atakuja.Ninamtegemea yeye
kwa kila kitu” akasema
Mathew na kuendelea
kusubiri
Baada ya dakika kadhaa
likapita gari moja na kwenda
kusimama mbele kidogo ya
daraja halafu mlango
ukafunguliwa.Tochi
ikawashwa na kuzimwa
mara tatu kisha Mathew
akajitokeza.Alikuwa ni
Abeba.Wakasaidiana
kumbeba Amar
wakamungiza katika gari na
kuondoka
“Nashukuru sana Abeba
kwa msaada huu
mkubwa.Nadhani hii ni mara
ya kwanza watu
wanafanikiwa kutoroka
katika gereza lile” akasema
Ammar lakini Abeba
hakujibu kitu.Aliendesha
gari hadi nje kidogo ya mji
wakaingia katika shamba la
matunda kulikuwa na
nyumba wakaingia ndani na
bila kupoteza muda Abeba
akaanza kumshughulikia
Ammar.Wakafanikiwa kutoa
risasi mbili katika mguu
wake na kumuongezea damu
kwani Abeba alikuwa
amekwenda na akiba ya
damu.
Baada ya kumuhudumia
Ammar ikafuata zamu ya
Mathew akamganga
majeraha mbalimbali
aliyoyapata wakati akiwa
mle gerezani.
“Mnatakiwa kabla ya
mapambazuo muwe
mmeondoka hapa Israel
kwani picha zenu
zitasambazwa kila mahali
kwamba ni wahalifu na
mnatafutwa.Wapi mnaelekea
ili niwapeleke?akauliza
Abeba na Mathew
akamtazama Ammar
aliyekuwa amelala kitandani
“Naomba unisaidie simu
tafadhali” akasema Ammar
na Abeba akampa simu
Ammar akaandika namba na
kupiga.Simu ilipopokelewa
akazungumza na mtu na
kumpa maelekezo kadhaa
halafu akamuelekeza Abeba
sehemu ya kuwapeleka.
Chupa ya damu
ilipomalizika wakaingia
garini na safari ikaanza
kuelekea Ramallah huku
Ammar akimuelekeza Abeba
njia ya kupita kukwepa
vizuizi vya wanajeshi.Safari
ilikuwa ya kimya kimya na
baada ya mwendo wa saa
moja wakasimamishwa na
kundi la watu wenye
silaha.Mathew akaiweka
sawa bunduki yake lakini
Ammar akamzuia
“Hawa ni watu wangu
niliwaelekeza niwakute
hapa” akasema Ammar na
kumshukuru Abeba kwa
msaada mkubwa
aliowasaidia.Kundi lile la
watu wenye silaha
wakalisogelea gari lile na
Ammar akafungua mlango
akashuka.Watu wake
walipomuona wakambeba
huku wakishangilia na
kupiga risasi juu
“Be safe” Abeba
akamwambia Mathew
“Go now.This place is too
dangerous” akasema Mathew
na Abeba akageuza gari
akaondoka zake.Mathew
akabaki amesimama.Ammar
akapelekwa katika gari kisha
akaagiza Mathew aletwe
katika gari alimo na msafara
wa magari ukaondoka
eneolile huku watu
wakishangilia na kupiga
risasi juu
“Abu nashukuru sana
rafiki yangu.Bado sijaamini
kama niko nje ya gereza
lile.Siamini kama leo
ninakwenda nyumbani
kwangu.Sina namna nzuri ya
kukushukuru kwa msaada
huu mkubwa.Karibu sana
katika himaya
yangu.Eneolote hili ni la
kwangu” akasema Ammar
Abeba baada ya
kuwaacha akina Mathew
akasimamisha gari na
kusubiri huku akiwatazama
kupitia kiona mbali maalum
chenye uwezo wa kuona
kwenye giza akaona Mathew
akiingizwa katika gari alimo
Ammar na msafara wa
magari ukaondoka
akachukua simu na
kumpigia Efraim
“Mathew na Ammar
tayari wamekutana na
wanamgambo wa Ammar
Nazari Brigades
wamewachukua na
wameondoka”
“Kazi nzuri Abeba.Sasa
unaweza
ukarudi.Tumuombee Mungu
aweze kufanikisha mpango
wetu.Kwa namna
ulivyomuona Ammar
anawasi wasi wowote kuhusu
Mathew?
“Hana wasi wasi
wowote.Furaha yake
haielezeki”
“Safi sana.Hii ni bahati
nasibu tumecheza tuendelee
kusubiri” akasema Efraim
 
SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 2: EPISODE 8
Katika makazi ya
Ammar Nazari sherehe
kubwa ilikuwa
inaendelea.wafuasi wake
walikuwa wakicheza ngoma
na kufurahi.Msafara wa
magari uliwasili na furaha
ikazidi.Ammar akashushwa
garini na kuingizwa ndani
akasalimiana na mke wake
na watoto.
“Abu kutanana familia
yangu.Nina watoto tisa na
wake wawili” akasema
Ammar na kumtambulisha
Mathew kwa wake zake na
watoto.
“Huyu anaitwa Abu Al
zalawi ni mwenzetu katika
mapambano dhidi ya Israel
na ndiye aliyefanikisha mimi
kuwepo hapa leo.Ni mtu
muhimu sana kwangu na
nina deni kubwa kwake”
akasema Ammar na
kuelekezwa Mathew apewe
chumba maalum katika
makazi yake na ahudumiwe
kwa kila kitu.Mke mdogo wa
Ammar akamchukua
Mathew na kumpeleka
katika chumba cha wageni
muhimu katika jumbe lile la
Ammar
“Karibu jisikie
nyumbani.Naitwa Nawal.Ni
mke mdogo wa Ammar”
akasema Nawal na kumtaka
Mathew akaoge.
“Mathew Mulumbi
karibu katika ulimwengu wa
magaidi.Mpaka hapa
naamini Ammar ameniamini
vya kutosha kwani
nimefanikiwa leo hii
amewasili nyumbani
kwake.Uhakika wa kumpata
Habiba Jawad ni mkubwa
sana” akawaza Mathew
akiwa bafuni akajitazama
katika kioo
“Ninatisha.I look like
hell.Hata Peniela
akinitazama leo anaweza
akanipotea.Tazama mwili
wangu ulivyokuwa na
makovu na vidonda kila
mahali.Sijawahi pitia kipindi
kigumu katika maisha yangu
na katika kazi yangu ya
ujasusi hadi sasa.Nimeteseka
mno na kama nikifanikiwa
kutoka salama katika sakata
hili sintajishughulisha tena
na mambo haya.It’s
over.Nataka nitulie na
familia yangu” Mathew
alipokumbuka familia yake
akajikuta akipandwa na
hasira za ghafla.
“Peniela anaamni tayari
nimekwisha fariki na
ameamua kuendelea na
maisha yake akaanzisha
mahusiano na na Yule mtu
wa Mossad.Inaniuma sana
kwa mke wangu
ninayempenda kuchezewa
kiasi hiki.Mossad
wanamtumia kwa ajili ya
kunitaka nifanye
wakitakacho.Siwezi
kumlaumu sana kwani haya
yote nimeyataka mimi
mwenyewe.Lakini naapa
kama nikifanikiwa kutoka
salama na kumkuta Yule
jamaa anaendelea na
mahusiano na Peniela
nitamnyonga kwa mikono
yangu nimalize hasira zangu
zote nilizonazo” akawaza
Mathew na kuoga maji
alipotoka akakuta kuna nguo
zimewekwa kitandani
akavaa halafu akakaa
kitandani
“Najaribu kuwaza ni vipi
kama wakigundua mimi
nimetumwa na
Mossad?Hakutakuwa na
kingine zaidi ya
kuuawa.Natakiwa kuwa
makini sana kuhakikisha
sifanyi kosa hata dogo kwani
kosa dogo sana linaweza
kuniletea matatizo
makubwa”
Mlango ukagongwa
akaenda kuufungua
akakutana na Nawal
akamkaribisha seheu ya
chakula ambako alikuwepo
Ammar na watu wengine
watano waliokuwa na ndevu
nyingi.Wale jamaa
walimuangalia Mathew kwa
makini sana akawasalimu
halafu akaketi katika mkeka
pamoja nao.Ammar
akamtambulisha Mathew
kwa wale jamaa ambao ni
viongozi wa juu wa kundi la
Ammar Nazari Brigades
“Ndugu zangu viongozi
wenzangu huyu anaitwa Abu
Al Zalawi ni raia wa Kenya
lakini mwenye asili ya
Misri.Amekuwa akiendesha
mapambano dhidi ya
waisrael nchini Kenya na
amefanikiwa kumuua mkuu
wa Mossad Afrika mashariki
aliitwa ..” akasema Ammar
na kumtazama Mathew
“Aliitwa Avi Abramson”
akasema Mathew.
“Vile vile aliua watu
wengine wawili wa Mossad
hadi alipokamatwa na
kuletwa katika gereza
nililokuwa nimefungwa.Kwa
bahati nzuri mimi nay eye
tulielewana na kuwa
marafiki na yeye ndiye
aliyefanikisha mimi kuwepo
hapa muda huu.Yeye ndiye
aliyenisaidia hadi
kunifikisha hapa.Nilipigwa
risasi na kushindwa
kutembea angeweza
kuniacha na kuendelea
kutoroka lakini hakuniacha
alinibeba na kuhakikisha
tunatoka wote
gerezani.Ndugu zangu huyu
ni mgeni muhimu sana
kwetu na tuna deni kubwa
kwake.Baada ya kutoka
gerezani hatarejea tena chini
kwake kwani tayari taarifa
za kutoroka kwake zitakuwa
zimesambaa hivyo atabaki
hapa ataungana na sisi
katika mapambano” akasema
Ammar na watu wale
wakamkaribisha Mathew
kwa furaha.Baada ya kupata
chakula Ammar akaelekeza
Mathew apelekwe
akapumzike
Baada ya Mathew
kuondoka Ammar akawa na
kikao kizito na wasaidizi
wake wakampa kwa
muhtasari yale yote
yaliyofanyika wakati akiwa
gerezani akawapongeza kwa
kuendeleza mapambano hata
wakati akiwa
amefungwa.Baada ya
maongezi marefu
yaliyochukua saa tatu Habib
msaidizi mkuu wa Ammar
akasema
“Ammar sote
tunashukuru sana kwamba
umerejea salama kutoka
gerezani.Lakini kuna kitu
kinanipa wasiwasi sana”
“Nini kinakupa wasi
wasi?
“Huyu jamaa uliyekuja
naye.Una uhakika gani kweli
ni mpiganaji?Hudhani
kwamba anaweza kuwa ni
pandikizi la waisrael
wakitaka kutuchuguza na
kupata taarifa zetu?akauliza
Habib
“Msiwe na wasi wasi
ndugu zangu.Abu Zalawi ni
mtu mzuri na si
pandikizi.Haikuwa rahisi
kwangu kumuamini lakini
baada ya kumchunguza
nikamuamini ni
mwenzetu.Ameteswa kwa
miaka mitatu na hata
mngebahatika kumona
mgongo wake wote umejaa
vidonda.Msiwe na shaka
naye hata kidogo” akasema
Ammar
“Ammar wewe ni
kiongozi wetu na hata siku
oja hatuwezi kukupinga kwa
kila ukisemacho lakini
binafsi bado nina mashaka
na huyu mtu.Kama
mtakubaliana name kabla ya
kumuingiza katika jeshi letu
tumchunguze na kumjua ni
nani na tumpime kwa kumpa
jaribio kama kweli anaweza
kuwa ni muaminifu kwetu”
akasema Habib na ukimya
ukatawala mle chumba
baada ya muda Ammar
akauliza
“Kwa nini mnakuwa na
wasi wasi kuhu huu
mtu?Kwa mambo
aliyonifabnyia hatustahili
hata kumchunguza kwani ni
mtu safi na hana tatizo.Huyu
ni mwenzetu anastahili
heshima kubwa” akasema
Ammar akionekana
kukereka na maneno yale ya
Habib
“Ammar utanisamehe
kama maneno yale
yalionyesha utovu wa
nidhamu lakini ni kanuni ya
jeshi letu kabla ya
kumuingiza mtu yeyote
lazima kwanza tumchunguze
na tujiridhishe kama kweli ni
mtu safi na anaweza
akatufaa.Hata huyu pia
lazima tumchunguze tumjue
ni nani na katokea
wapi.Naomba unipe ruhusa
nimchunguze huu mtu na
kama nikikuta kuna chembe
ya kasoro basi nitakupa
taarifa”
“Sawa hakuna tatizo
fanya hivyo” akasema ammar
na kikao kikaishia hapo
kwani hakuonyesha
kufurahishwa na kitendo kile
cha kutaka kumchunguza
Mathew
Habib hakutaka kusubiri
hadi asubuhi akawachukua
vijana wawili wakiwa na
kifaa Fulani wakaenda
katika chumba cha Mathew
wakagonga akaamka na
kufungua mlango wakaingia
ndani.
“Abu Zalawi
unajisikiaje?akauliza Habib
“Ninajisikia maumivu
mwili mzima” akasema
Mathew
“Pole sana.Mimi naitwa
Habib ni kamanda mkuu wa
vikosi vyote vya Ammar
Nazari Brigades.Ammar
amenipa maelekezo ya
kukujumuisha katika jeshi
letu hivyo basi kabla ya
kukuingiza rasmi jeshini
kuna mchakato ambao
lazima uupitie” akasema
Habib na kuwapa ishara
wale vijana aliokuwa nao
wafaye ukaguzi.Kifaa kile
walichokuwa nacho
kikawashwa na kuanza
kupitishwa katika mwili wa
Mathew lakini hawakukuta
kuna kitu chochote ambacho
Mathew alikuwa
amepandikizwa mwilini ili
kuwajulisha Mossad mahala
alipo.Habib akaagiza
warudie tena lakini
hakukuwa na kitu
chochote.Akaelekeza nguo
zote alizokuja nazo Mathew
zichunguzwe lakini
hakukuwa na kifaa chochote
“Uko safi sasa tunaomba
tuongozane”akasema Habib
na Mathew akainuka
akaongozana na wale jamaa
“Nilijua mambo kama
haya yanaweza kutokea
ndiyo maana nilikataa
kufungwa kifaa chochote cha
kuwajulisha Mossad mahala
nilipo.Kama ningekuwa na
kifaa kile hivi sasa
yangekuwa ni mambo
mengine.” Akawaza Mathew
Waliingia katika chumba
kimoja kikubwa chenye
mitambona vifaa vingi vya
mawasilano
“Watu hawa
wameendelea sana.Ofisi hii
ni kubwa utadhani ofisiya
Mossad” akawaza Mathew na
kuingizwa katika chumba
kidogo chenye meza na viti
viwili.Akakaa mle na baada
ya muda akaingia kijana
mmoja aliyevaa kanzu ya
rangi ya kijivu.Alikuwa
amevaa miwani na hakuwa
na ndevu nyingi kama
wenzake.Mkononi alikuwa
na faili akaliweka mezani.
Habib na wenzake
walikuwa wanafuatilia
mahojiano yale ya Mathew
na Yule kijana kupitia
runinga kubwa katika
chumba kingine
“Naitwa
Mustapha.Nimekuja hapa
nataka kuchukua taarifa
zako hivyo naomba unipe
taarifa za kweli ili tuweze
kukufahamu na kukuingiza
katika mfumo wetu”akasema
Mustapha.
“Nafurahi kukufahamu
Mustapha.Natumai
tutafanya kazi
pamoja”akajibu Mathew
huku akitabasamu
“Nataka kufahamu jina
lako nani?akauliza Mustapha
“Naitwa Abu Al Zalawi”
“Unaweza ukatupa
historia yako kwa ufupi
umetokea wapi hadi ukafika
hapa?akauliza Mustapha
“Kama nilivyosema
naitwa Abu Al zalawi,raia wa
Kenya mwenye asili ya
Misri.Baba yangu aliitwa
Khalid Al Zalawi.Alikuwa ni
mmoja wa viongozi wa kundi
la Abu Hafs al-Masri
Brigades.Baba yangu Khalid
aliuawa na majeshi ya Israel
na hapo ndipo nilipoapa
kuendeleza mapambano na
Israel.Mama yangu alitokea
Kenya hivyo haikuwa kazi
kwangu kupata uraia wa
Kenya.Nikiwa Kenya
nilimuua Avi Abramson
mkuu wa Mossad Afrika
Mashariki pamoja na
majasusi wengine wawili
ndipo nilipoanza kutafutwa
na serikali ya Israel”
Wakati Mathew
akimuelezea Mustapha
historia yake katika chumba
kile walichokuwemo akina
Habib vijana walikuwa na
kasi ya aina yake na mara tu
alipotaja jina lake
wakalitafuta na sura na
picha yake vikaonekana
Runingani.Abu Zalawi
alikuwa ni mmoja wa watu
waliokuwa wanatafutwa
sana na serikali ya Israel.
“Anachokisema ndicho
kilichoandikwa na Israel”
akawaza Habib
Mathew aliulizwa
maswali mengi kuhusu
maisha yake na hadi namna
walivyofanikisha kutoroka.
“Majibu yake
yanaridhisha kabisa na
yanashawishi kumuamini
lakini bado nafsi yangu
inakuwa nzito kumuamini
moja kwa moja.lazima nimpe
mtihani kesho” akawaza
Habib na kumrejesha
Mathew chumbani kwake.
“Nashukuru Mossad
wameweza kufanya kama
walivyoelekeza.Taarifa zote
nilizowapa ziko mtandaoni
na wameridhika mimi ni Abu
Zalawi lakini huyujamaa
Habib bado haonyeshi
kunikubali.Amesema
tutaonana asubuhi.Sijui
anataka afanye nini tena”
akawaza Mathew na kujilaza
kitandani alikuwa amechoka
sana
Saa kumi na mbili za
asubuhi mlango wa chumba
alimolala Mathew
ukagongwa akaingia Habib.
“Abu kumekucha kazi
inaanza.Sisi hatuna muda
wa kupumzika” akasema
Habib na Mathew bila hata
kunawa uso akatoka
wakaingia katika gari na
kuondoka.Ulikuwa ni
mwendo mrefu hadi ilipofika
saa nne za asubuhi
wakasimamisha gari sehemu
na Habib akasema
“Abu wewe ni mtu
shujaa.Tunakushukuru sana
kwa kumuokoa mkuu wetu
na kuamua kuungana nasi
katika mapambano dhidi ya
waisrael.Jana ulinieleza
hasira ulizo nazo kuhusu
Israel na uliapa kulipiza
kisasi kwa kitendo cha
kumuua baba yako.Kilometa
chache kutoka hapa kuna
soko kubwa la samaki na
watu wengi kutoka upande
wa Israel huja kununua
samaki.Ulinieleza kwamba
umeteswa kwa miaka zaidi
ya mitatu gerezani.Ni wakati
wa kulipa
kisasi.Tunakwenda kuondoa
maisha ya waisrael” akasema
Habib na kufungua sanduku
lililokuwa nyuma
likaonekana bomu kubwa.
“Jesus Christ ! akawaza
Mathew baada ya kuliona
bomu lile.
“Abuu nadhani mpaka
hapa umekwisha fahamu
ninachokimaanisha”
“Nimekuelewa Habib”
akasema Mathew huku
akijitahidi kutokuonyesha
woga wowote.
Walikwenda hadi katika
soko kubwa la
samaki.Magari kadhaa
yalikuwa yamejipanga
yakiuza samaki wabichi.Gari
walilopanda akina Mathew
likapenya na kuingia kati
kati ya magari yale ya kuuza
samaki.
“Abu tumefika.Muda
utakapowadia utabonyeza
kitufe hiki bomu litalipuka
na damu ya waisrael
itamwagika.Wewe ni
mpambanaji nadhani
unafahamu thamani ya hiki
unachokwenda kukifanya”
“Ninafahamu Habib”
akasema Mathew.Habib
akamfanyia dua halafu
akabonyeza saa iliyokuwa
mbele halafu akashuka
akafungua mlango.
“Mathew dunia
itakukumbuka kwa ushujaa
huu wa leo na sote
tutakutana ahera” akasema
Habib na kushuka garini
akamuacha Mathew
“Nimenusurika mara
nyingi kupoteza maisha hadi
watu wananiambia nina
maisha marefu kama paka
lakini leo hii nadhani maisha
yangu yamefika
ukingoni.Hakuna namna
nitakavyoweza kupona.Bomu
litalipuka na kuua watu
wengi na mimi
nikiwemo.Najuta
kilichonileta huku.Bora
ningebaki gerezani Israel
kuliko kuja kufa kigaidi
huku nikiua watu wengine
wasio na hatia” akawaza
Mathew huku uso wake
ukiwa umeloa jasho
akitazama sekunde
zinavyozidi kukimbia kwa
kasi
“Mathew Mulumbi leo
ninakufa kifo cha kijinga
sana.Ile sifa yangu yote ya
mtu shujaa lakini leo
inafutika na kufa kama
gaidi.Nadhani muda huu
uliobaki wa dakika mbili
niutumie kwa maombi”
akawaza Mathew na
kufumba macho
“Ee Mungu ni wewe
pekee mwenye kuona hadi
ndani ya mioyo yetu na kujua
dhamira zetu nadhani
unanitazama hivi sasa
dhamira yangu si kuua watu
wako wasio na
hatia.Nimefika hapa
kutokana na mapenzi
makubwa niliyo nayo kwa
nchi yangu na lengo langu ni
kuhakikisha ninapambana
na magaidi hawa wasio na
huruma hata chembe lakini
nimejikuta mikononi mwao
na wananilazimisha kujiua
na mimi kuua
wengine.Nimekukosea
mambo mengi ee Mungu
wangu naomba unisameheme
yale yote niliyokukosea
makubwa na madogo.Mungu
wangu,Musa aliwaondoa
waisrael utumwani Misri
lakini hakuweza kufika nchi
ya ahadi,ninaomba baada
yangu umuinue mtu
mwingine aweze kuiendeleza
hapa nilipofika na
kuutokomeza kabisa
ugaidiNinakufa nikiwa na
mapenzi makubwa na nchi
yangu Tanzania na ndilo
neno langu la mwisho
kulitamka.Nakupenda
Tanzania” akafumbua macho
na kutazama saa zilibaki
sekunde tano.
“It’s time” akawaza na
kutazama nje halafu
akatazama saa sekunde
zilibadilika tatu ,mbili moja
“Allahu akbar ! akasema
Mathew na kubonyeza kitufe
alichoelekezwa
MPENZI MSOMAJI
USIACHE KUFUATILIA
SIMULIZI HIIKATIKA
SEHEMU IJAYO……..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom