Riwaya: Siri

Riwaya: Siri

SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 2
Jengo la ghorofa sita
lililojengwa mita chache kutoka
bahari ya Hindi limekuwa
likizua maswali mengi kutoka
kwa watu wakitaka kumfahamu
mmiliki wake na wengi
wakitaka kufahamu mmiliki
wake alipataje kibali cha
kujenga jengo sehemu
ile.Mjadala kuhusiana na jengo
lile ambalo kwa muonekano
wake ni kama jengo la hoteli ya
kifahari ulimalizika kimya
kimya na ujenzi wa jengo lile
ukaendelea hadi
lilipomalizika.Kitu ambacho
kiliendelea kuzusha maswali
hata baada ya jengo lile kubwa
na zuri sana kumalizika ni
kutokuonekana shughuli yoyote
ikiendelea zaidi ya watuna
magari kuonekana wakiingia na
kutoka pamoja na uwepo wa
ulinzi mkali.Kitu ambacho
wengi hawakukifahamu kuhusu
jengo lile ni kwamba jengo lile
halikuwa jengo la hoteli au ofisi
bali jengo lile lilikuwa chini ya
idara ya siri ya usalama wa
ndani wa nchi na lilijulikana
kama kitalu 1.
Magari matatu ambayo
mojawapo alikuwemo Mathew
Mulumbi yalifunguliwa geti la
jengo lile yakaingia ndani na
kuvuka geti la pili hadi katika
jengo,lango lingine
likafunguliwa yakaingia chini
katika maegesho.Mathew
akafunguliwa pingu za miguu
akashushwa ndani ya lile gari
akaingizwa ndani ya jengo.Bado
aliendelea
kulindwa.Hawakutaka kumpa
hata nafasi ndogo.Waliingia
ndani ya lifti iliyowashusha
chini umbali wa mita mia
moja.Lango la chumba kimoja
likafunguliwa akaingizwa ndani.
Miguu yake ikafungwa na
minyororo mizito halafu
akasikia lango linafungwa watu
wale wakaondoka.Bado
aliendelea kufunikwa mfuko ule
mweusi kichwani.
“Hapa wamenileta wapi?
Akajiuliza Mathew baada ya
wale jamaa kuondoka na
kumuacha mle ndani peke yake
“Nisipofanya juhudi za
kujiokoa kutoka katika mikono
ya hawa jamaa ninaweza
kujikuta katika matatizo
makubwa.Nikipata hata nafasi
ndogo tu lazima niitumie
kikamilifu.Ili kuifahamu siri
iliyojificha nyuma ya sakata hili
lazima nihakikishe ninatoka
humu na kuwaokoa Olivia na
baba yake” akawaza Mathew
Ndani ya chumba kimoja
watu sita wakiongozwa na
Kaiza walikuwa wanamuangalia
Mathew kupitia kamera
zilizomo ndani ya chumba
alimowekwa.
“Tunatakiwa kuanza
kumtesa taratibu wakati
tunamsubiri Devotha.Tuanze na
baridi” akasema Kaiza
aliyekuwa amevaa suti ya rangi
ya kijivu.
Mabomba ya maji
yaliyokuwamo ndani ya
chumba alimowekwa Mathew
yakafunguka na kuanza
kumwaga maji ya baridi
sana.Mathew aliloa chapa chapa
na kuanza kutetemeka kwa
baridi kali.Baada ya dakika
kadhaa maji yale yakaacha
kutoka na ikatokea baridi kali
sana.Mathew alihisi viungo
vyake vyote vinaganda.
“Imetosha tumpe muda wa
mapumziko” akasema Kaiza na
mashine ile yenye kupeleka
ubaridi ndani ya kile chumba
ikazimwa lakini bado Mathew
aliendelea kutetemeka kwa
baridi kali.
“Atolewe mle apelekwe
chumba cheupe” akasema
Kaiza.Baada ya muda mfupi
lango la chumba kile alimo
Mathew likafunguliwa
wakaingia watu sita watatu kati
yao wakiwa na silaha.Mathew
akatolewa ndani ya kile chumba
akavuliwa ule mfuko mweusi
kichwani akavuliwa mavazi
yake akavishwa mavazi meupe
akatolewa ndani ya kile chumba
akapelekwa katika chumba
chenye weupe mkali.Kila kitu
kilichokuwamo mle ni
cheupe.Akafungwa mikono
katika meza wakamuacha mle
ndani peke yake
“Ninahisi baridi kali
mno.Sijawahi kuhisi baridi ya
namna hii toka kuzaliwa
kwangu.Najua hizi ni mbinu zao
za kunitesa lakini
hawatafanikiwa.Nimepitiam
ateso mengi zaidi ya
haya,wanajisumbua bure”
akawaza Mathew
*****************
Jua lilipochomoza lilimkuta
tayari Devotha Adolph
amekwisha wasili kitalu 2
mahala alikohifadhiwa Olivia na
baba yake Agrey.Bado
wataalamu wa mawasiliano wa
idara yake waliendelea na zoezi
la kuhakikisha mtandao mpya
wa mawasiliano
unakamilika.Devotha
akawasalimu na kuelezwa kile
kilichokuwa kinaendelea
akaelekea ofisini kwake.Mara tu
alipoketi kitini akampigia simu
Kaiza
“Hallo Devotha” akasema
Kaiza baada ya kupokea simu
“Kaiza mnaendeleaje huko?
“Huku tunaendelea vyema
kabisa.Tayari tumeanza kumpa
Mathew mateso
taratibu.Tumeanza na baridi
kali,tayari tumemtoa kwenye
baridi na kumpeleka katika
chumba cheupe.”akajibu Kaiza
“Good.Mmefanya kazi nzuri
sana Kaiza.Huyo ni mtu wa
muhimu sana kwetu”
“Unakuja saa ngapi huku
Devotha?akauliza Kaiza
“Niko hapa kitalu 2 nataka
kuendelea na zoezi la
kumfungua Olivia na vile vile
nitazungumza na baba yake
kama kuna kitu chochote
anakifahamu kuhusu
mwanae.Endeleeni kumpa
mateso Mathew na nikitoka
huku nitakuja huko mara
moja.Kwa sasa hatuna tena
hofu,aliyekuwa anatupa hofu ni
huyo Mathew ambaye tayari
tunaye mikononi mwetu”
akasema Devotha
“Sawa Devotha
tunakusubiri” akasema Kaiza na
Devotha akakata simu
“Leo ninajihisi mwenye
amani sana baada ya Mathew
kukamatwa.Nitaifanya kazi
yangu kwa Amani.Nataka
kubadili namna ya kumuhoji
Olivia.Kutumia nguvu
hakutasaidia kumfungua”
akawaza Devotha akachukua
simu akapiga na kuomba
kuunganishwa na chumba cha
Olivia.Baada ya sekunde chache
akaunganishwa na kamera
zilizopo katika chumba
alimolala Olivia.
Olivia alikuwa amelala
katika chumba kizuri na kitanda
safi.Hakuwa amefungwa pingu
mikononi wala
miguuni.Alionekana mwingi wa
mawaz😵livia akampigia simu
Jasmin na kumtaka afike oisini
kwake haraka
“Jasmin leo tunabadili
mbinu za kumuhoji
Olivia.Hatutaendelea na
taratibu zetu za kutumia
mabavu hivyo nataka
tumuonyeshe kwa sisi si watu
wabaya.Nataka tumfanye
aamue mwenyewe kwa hiyari
yake kufunguka na kushirikiana
nasi.Nataka uende chumbani
alimo mpelekee mavazi
mazuri,hakikisha ameoga na
kisha andaa kifungua kinywa
kwa ajili yangu naye” akasema
Devotha na Jasimn akaenda
kutekeleza maagizo
aliyopewa.Olivia alipelekwa
bafuni kuoga,akatibiwa jeraha
alilochomwa kisu pajani,kisha
akapewa mavazi mazuri ya
kuvaa.Wakati yote haya
yanafanyika Devotha alikuwa
akishuhudia kupitia kamera na
kila kitu kilipokamilika
akaelekea katika chumba cha
chakula ambako kuliandaliwa
kifungua kinywa maalum kwa
ajili yake na Olivia.Akampigia
simu Jasmin na kumtaka
ampeleke Olivia katika chumba
cha chakula.Olivia alistuka na
kupandwa na hasira baada ya
kumkuta Devotha akiwa
amekaa katika chumba kile cha
chakula akitabasamu
“Hallo Olivia” akasema
Devotha.Olivia akasimama na
kumtazama Devotha kwa
hasira.Devotha akasimama na
kuvuta kiti
“Karibu Olivia.Karibu
tupate kifungua kinywa”
akasema Devotha
“I’m not hungry!! Akasema
Olivia na kumgeukia Jasmin
“Take me back to my room”
“Olivia come and join me
here, this is an order!! Akasema
Devotha kwa ukali.Mmoja wa
walinzi waliokuwa nyuma ya
Olivia akamshika mkono na
kumkalisha kitini
“Please madam usifanye
mambo yakawa magumu
kwako.Fanya
utakavyoelekezwa” akasema
yule mlinzi na Olivia akaketi
huku akiendelea kumtazama
Devotha kwa macho yaliyojaa
hasira.Dr Olivia na Devotha
wakanywa chai kimya kimya na
baada ya kumaliza Devotha
akasema
“Olivia let’s take a walk”
Olivia akainuka na
kuongozana na Devotha
wakaenda katika bustani ndogo
kulikokuwa na sehemu nzuri ya
kukaa kupumzika.UKimya wa
dakika mbili ukapita kisha
Devotha akasema
“Unaendeleaje
Olivia?akauliza Devotha lakini
Olivia hakumjibu kitu.
“Olivia I’m sorry for what I
did to you yesterday” akasema
Devotha na Olivia akaonekana
kupandisha hasira zaidi
“You are sorry?akauliza
“With my own two eyes I
watched you shot my father
twice .What kind of a woman
are you?akauliza Olivia kwa
ukali
Devotha akamtazama kwa
muda halafu akasimama
“Niangalie vyema” akasema
“I’m a very sexy
woman.Najifahamu mimi ni
mzuri kukushinda hata wewe
lakini umejiuliza kwa nini
mwanamke mwenye uzuri
kama wangu nikawa
mkatili?Ulichokishuhudia jana
si kitu.Bado haujauona ukatili
wangu.Nilikwambia kwamba
wananiita shetani wa
kike.Unadhani ni kwa nini
nimefikia hapo
nilipofika?akauliza Devotha
lakini Olivia hakujibu kitu.
“Uso wangu umejaa
tabasamu kila wakati lakini si
tabasamu la furaha.Do you
think when I smile I’m
happy?akauliza na kuendelea
kumtazama Olivia ambaye bado
alikuwa kimya
“I’m not happy.I’ve never
been happy in my life.Tabasamu
hili ni uumbaji wa Mungu lakini
ndani mwangu hakuna furaha
hata chembe.Ninapata kila
ninachokihitaji katika maisha
yangu,I have
money,jewels,expensive
cars,houses, but I’m not
happy.Umejiuliza kwa nini?
Akauliza Devotha na kuvuta
pumzi ndefu.Akatoa miwani
aliyoivaa na kuiweka mezani
“Nitazame vizuri macho
yangu” akasema Devotha lakini
Olivia hakusumbuka kuinua
kichwa chake kumtazama
“Olivia nitazame machoni
tafadhali!! Akasema Devotha na
Olivia akainua kichwa
akamtazama Devotha
“Kuna kitu umekigundua?
akauliza Devotha lakini Olivia
akabaki kimya
“Umegundua kitu chochote
kisicho cha kawaida?akauliza
lakini Olivia akaendelea kuwa
kimya
“Kama umeshindwa
kugundua nitakueleza” akasema
Devotha
“Nina jicho moja linalofanya
kazi.Jicho la kushoto ni bandia
na halina kazi
yoyote.Ukinitazama ni vigumu
kuamini kwamba ni natumia
jicho moja” akasema Devotha
na kuvaa miwani yake
“Umewahi kujiuliza kwa
nini kila unaponiona ninakuwa
na glovu mkono wangu wa
kushoto? Unadhani ni urembo?
akauliza Devotha na kuvua
glovu yake aliyovaa mkono wa
kushoto
“Unaona mkono wangu
ulivyo?akauliza.Mkono wa
kushoto wa Devotha ulikuwa na
vidole vitatu pekee.
“Nina vidole vitatu katika
mkono wangu wa
kushoto.Ninavaa hii glovu
ambayo imetengenezwa
maalum ili nionekane nina
vidole timilifu lakini sina vidole
viwili” akasema Devotha na
kuvaa glovu yake halafu
akafungua mkoba na kutoa
albamu la picha akampa Olivia
aangalie
“Tazama hizo ni picha
zangu za zamani” akasema
Devotha.
“Picha zako zitanisaidia
nini? akauliza Olivia
“Fungua tazama” akasema
Devotha na Olivia akafungua
ukurasa wa kwanza wa albamu
lile akazitazama picha mbili
kubwa na sura yake ikaonyesha
mshangao kidogo akaendelea
kufunua kurasa kwa kurasa na
alipomaliza akalifunga lile
albamu
“This is stupid!! Akasema
Olivia na kuiweka mezani ile
albamu
“Umegundua nini
Olivia?akauliza Devotha
“Stop wasting my time
Devotha.Unanipima akili
yangu?akauliza Olivia
“Nieleze umeona nini katika
hizo picha?Devotha
akauliza.Olivia akamtazama
kwa muda halafu akasema
“Nimemuona msichana
ambaye hafanani kabisa na
wewe.Naomba usitake kucheza
na akili yangu Devotha”
akasema Olivia
“Huyo unayemuona katika
hizo picha ni mimi”akasema
Devotha
“Nimekwambia usitake
kuijaribu akili yangu
Devotha.Aliyeko katika picha
hizi na wewe ni watu wawili
tofauti kabisa”akasema Olivia
“Uko sahihi Olivia.Kwa
kutazama picha za kwenye
albamu na kunitazama mimi ni
watu wawili tofauti kabisa
lakini ni mtu mmoja ambaye ni
mimi” akasema Devotha na
kunyamaza kimya kwa sekunde
kadhaa halafu akasema
“Olivia umejiuliza kwa nini
nimekueleza haya yote?akauliza
Devotha.Olivia hakujibu kitu
alikuwa anachezea vidole vyake
“Nisikilize vyema” akasema
Devotha
“Picha hizo ulizoziona ni
wakati nikiwa msichana
mdogo.Wazazi wangu walikuwa
masikini.Hatukuwa na
nyumba,tuliishi katika nyumba
za kupanga.Katika harakati za
kutafuta maisha baba alijikuta
akifika hadi nchini Kenya na
kupata kazi katika shamba
moja kubwa la uzalishaji
maua.Ililazimu familia yetu
kuhamia Kenya kumfuata
baba.Katika sehemu tuliyokuwa
tukiishi nchini Kenya nilipata
rafiki aliyeitwa Halima.Huyu
alikuwa msomali.Wazazi wake
walihama kutoka Somalia na
kuishi Kenya.Familia yao na
yetu tulikuwa na ukaribu
mkubwa.Siku moja wakati
tukitoka shule Halima
aliniambia kwamba baba yake
anamtengenezea chombo
ambacho kitampeleka
peponi.Nilikuwa mdogo bado
lakini katika mafundisho
niliyopewa na walimu wa dini
nilifahamu wanaokwenda
peponi pekee ni wale
waliokufa.Nilimtaka
akanionyeshe chombo hicho
ambacho kitampeleka
peponi.Kabla wazazi wake
hawajarejea kutoka katika
mihangaiko yao ya siku Halima
akanipeleka katika chumba
ambacho baba yake alikuwa
anamtengenezea chombo cha
kumpeleka peponi.Alinionyesha
chombo chenyewe kilichokuwa
juu ya meza.Lilikuwa ni bomu
likitengenezwa la kujitoa
mhanga.Toka nikiwa mdogo
nilipenda sana kutazama filamu
mbalimbali hasa za mapambano
na magaidi na niligundua lile
lilikuwa bomu ,niliogopa sana
nikamdanganya kwamba
ninakwenda kuwaita wazazi
wangu ili waje waone kifaa kile
na mimi wanitengenezee
chombo kama kile cha
kunipeleka peponi ili
ikiwezekana tuende pamoja
mimi na yeye.Nilikimbia
nyumbani nikawachukua
wazazi wangu tukaenda hadi
katika chumba kile cha baba
yake Halima na tukamkuta
tayari Halima amekwisha livaa
lile bomu na akasema anataka
kuwaonyesha wazazi wangu
namna kifaa kile kinavyofanya
kazi.Baba alimsihialivue lakini
Halima akagoma,baba
akamfuata ili amvue lile bomu
lakini alichelewa Halima
alibonyeza kilipuzi na moto
mkubwa ukatokea”
akanyamaza Devotha na
kuinamisha kichwa kwa muda
“I’m sorry sipendi
kulikumbuka tukio lile ni moja
ya tukio linaloniumiza mno
katika maisha yangu.Picha ya
moto ule mkubwa haijawahi
kunitoka katika akili yangu”
akanyamaza tena
“Pole sana” akasema Olivia
akionekana kuguswa na taarifa
ile ya Devotha
“Wazazi wa Halima
walikuwa ni wafuasi wa kikundi
cha Alshabaab cha Somalia na
walikuwa wanajiandaa kufanya
shambulio kwa kumtumia
Halima.Wazazi wangu wote
wawili walipoteza maisha pale
pale.Halima naye alifariki akiwa
angali msichana mdogo.Mimi
sikuwa natazamika,niliharibika
vibaya sana.Serikali ya
Marekani waliamua kunichukua
na kugharamia matibabu
yangu.Nilipelekwa Marekani
kwa matibabu ambako
nilifanyiwa operesheni
thelathini na saba hadi kufikia
hali hii niliyonayo leo ndiyo
maana unaona muonekano
wangu wa sasa na ule wa
kwenye picha ni tofauti.Baada
ya kupona niliendelea na
masomo nchini Marekani na
baadae nikasomea masuala ya
kupambana na
ugaidi.Nilisomeshwa na
kufanya kazi katika idara ya
kupambana na ugaidi ya
Marekani.Nikiwa kule
niliendelea kufuatilia taarifa za
nyumbani Tanzania na nilisikia
kuhusu kuanza kuchomoza kwa
vikundi vyenya viashiria ya
ugaidi nchini
Tanzania.Niliwasiliana na Rais
nikampa wazo la kuanzisha
idara ya siri ya usalama wa
ndani wa nchi.Rais Dr Evans
alikubali wazo langu nikarejea
nchini kuanzisha idara hii na
japo imeanzishwa ndani ya
muda mfupi lakini tayari kazi
tuliyoifanya ni
kubwa.Tumefanikiwa
kufyekelea mbali vile vikundi
vyote vyenye muelekeo wa
kigaidi vilivyoanza kuchomoza
na hadi sasa hujasikia tena
tishio lolote la kuibuka kwa
vikundi vya kigaidi.”akatulia
tena na kumtazama Olivia
“Olivia nimekueleza haya
yote kwa sababu nataka
utambue ni namna gani
ninawachukia magaidi.Ni kwa
sababu yao leo hii maisha yangu
hayako sawa.Maisha yangu
hayana furaha hata chembe.Ni
kwa sababu ya magaidi leo hii
niko peke yangu katika hii
dunia sina baba ,mama wala
ndugu yeyote I’m all
alone.Nimeshuhudia unyama
unaofanywa na magaidi toka
nikiwa mdogo.Asubuhi ya
Jumanne ya 11 September 2011
nilikuwepo jijini New York
wakati kikundi cha kigaidi cha
Alqaeda kiliposhambulia
majengo pacha ya kituo cha
kibiashara cha kimataifa na
kusababisha watu wapatao elfu
tatu kupoteza maisha na maelfu
wengine
kujeruhiwa.Yawezekana
unafahamu kupitia mitandao na
vyombo vingine vya habari
lakini mimi nilikuwepo eneo la
tukio na nilishuhudia unyama
ule kwa macho yangu.Ukiacha
tukio hilo nimeshuhudia
matukio mengine mbali mbali
ya kigaidi yanayofanywa na
vikundi mbali mbali vya kigaidi
duniani hivyo sina huruma hata
kidogo na watu hawa” akasema
Olivia
“Baada ya jitihada za muda
mrefu hatimaye serikali ya
Marekani walifanikiwa kumuua
kiongozi mkuu wa kikundi cha
Alqaeda ambacho kilikuwa
kinaongoza mashambilizi ya
kigaidi na kuua watu wengi
duniani.Kuuawa kwa kiongozi
huyo na wengine kadhaaa
kulilifanya kundi la Alqaeda
likose nguvu na kufifia lakini
kwa sasa limeibuka kundi la IS
ambalo limekuwa likifanya
mashambulio mengi sehemu
mbali mbali duniani na kuua
watu wengi wasio na hatia na
wameapa kuendelea kufanya
mashambulio na kuua watu
hadi pale bendera yao
itakapopepea kutoka mashariki
hadi magharibi mwa
dunia.Nilipogundua kuwa una
mawasiliano na watu walio
katika mtandao wa IS nilistuka
sana na kupata hasira
nyingi.Nilijuliza maswali mengi
kuhusu ukaribu wako na hawa
watu.Kama nilivyokueleza awali
kwamba ninawachukia magaidi
na wewe pia uliingia katika
orodha ya maadui zangu lakini
nikikutazama machoni Olivia
hauonekani kama ni
gaidi.Hauna sifa za kuwa
gaidi.Nataka kufahamu kitu gani
kinaendelea kati yako na hawa
watu wa IS? Olivia wewe u
mwanamke mwenye heshima
kubwa hapa Tanzania kutokana
na shughuli yako unayofanya ya
kuokoa maisha ya watu na hata
kesho ukitaka kugombea urais
watanzania hawatakuwa na
sababu ya kutokukuchagua
kutokana na sifa yako
iliyotukuka.Familia yako pia ina
sifa nzuri lakini haya yote
yanaharibiwa na jambo moja tu
nalo ni ushirika wako na watu
wa kikundi cha kigaid cha
IS.Olivia nataka kuwa rafiki
yako badala ya adui.Nataka
nikusaidie sipendi kukutesa
mtu kama wewe lakini
nitakusaidia pale tu
utakapokuwa tayari kunieleza
ukweli wote kuhusu wewe na
IS.Sipendi kuendelea
kukushikilia hapa
kukutesa,kumtesa baba yako
nataka tulimalize suala hili kwa
amani ili maisha yaendelee”
akasema Devotha na kutulia
akaangalia juu kundi la ndege
lilikuwa linapita.Ulipita ukimya
wa dakika mbili
“Olivia please” akasema
Devotha
“Devotha umejitahidi sana
kunishawishi nikueleze kila kitu
lakini kabla sijakueleza
chochote kuna kitu nakihitaji
kujua kutoka kwako” akasema
Olivia
“Sema Olivia unahitaji
nini?Ninakuahidi chochote
ukitakacho kama kiko ndani ya
uwezo wangu nitakupatia”
akasema Devotha.Olivia
akamtazama na kusema
“Nataka kujua mahala aliko
Edger Kaka.Ukinipa taarifa hizo
na ukanisaidia kumpata
ninakuahidi kukueleza kila kitu
unachokitaka” akasema
Olivia.Devotha akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Olivia my dear,Edger Kaka
hayuko hai.Amekwisha fariki
miaka mitatu iliyopita na
kilichobaki hivi sasa ni mifupa
yake tu.Labda kama unataka
nikupeleke mahala lilipo kaburi
lake” akasema Devotha
“Devotha ninayasoma
mawazo yako,kila
ninapowaeleza kuhusu suala
hili unaamini nina matatizo ya
akili.Naomba nikutoe wasiwasi
kwamba mimi ni mzima sina
tatizo lolote la
kiakili.Ninachokisema nina
uhakika nacho” akasema Olivia
“Olivia kila atakayesikia
suala hili ataamini una matatizo
ya akili kwa sababu Edger
amekwisha fariki na wewe
mwenyewe ndiye uliyetambua
mwili wake hospitali”akasema
Devotha
“Wote tuliaminishwa hivyo
kwamba Edger amekufa lakini
naomba ufahamu Devotha
kwamba mwili ule uliozikwa
haukuwa mwili wa Edger Kaka”
“That’s not true Olivia”
akasema Devotha
“It’s true and I have proof”
“What proof?
“Nimefanya vipimo kwa
kutumia masalia ya mwili ule
ambao wote tunaamini ni wa
Edger na majibu
yamenionyesha kwamba mwili
ule haukuwa wa Edger”
“That’s a lie Olivia.That’s
not true.Edger Kaka is dead”
akasema Devotha
“Sikudanganyi Devotha
ninachokwambia ni ukweli
mtupu.Wote tumeaminishwa
hivyo kwamba Edger alifariki
katika ile ajali lakini ukweli ni
kwamba Edger yuko hai
anashikiliwa sehemu Fulani”
akasema Dr Olivia
“Olivia do you think I can
believe you?akauliza Devotha
“Believe me or not but
that’s the truth Edger is still
alive.Kama unataka nikueleze
yote unayohitaji kuyajua
kuhusu IS nipe taarifa za alipo
Edger” akasema Olivia na
Devotha akaendelea
kumuangalia
“Najua huniamini Devotha
lakini nitakupa maelekezo
ambayo ukiyafuatilia utagundua
hiki ninachokueleza ni kitu cha
kweli.Katika kaburi la Edger
upande wa kulia ukichunguza
vizuri utagundua
kumechimbwa na ukifukua
eneo hilo utakuta kuna tobo
kubwa lililotobolewa katika
ukuta wa kaburi.Mimi ndiye
niliyetoboa tobo hilo kwa ajili
ya kuingia ndani na kuchukua
sampuli za mabaki ya mwili ule
nikaenda kufanya vipimo na
kugundua mwili ule haukuwa
wa Edger Kaka.Kama ukitaka
unaweza ukachukua sampuli za
mwili ule pia na kwenda
kuufanyia uchunguzi na
ninakuhakikishia majibu
utakayoyapata ni kama haya
ninayokwambia kwamba mwili
ule haukuwa wa Edger
Kaka.Devotha kuna siri kubwa
hapa ambayo huifahamu na
kama ukitaka kuifahamu
nisaidie kujua mahala alipo
Edger Kaka.Nakuhakikishia ni
siri kubwa” akasema Olivia
Baada yatafakari ya muda
Devotha akasema
“Olivia natamani sana
nikuamini lakini nafsi yangu
inasita kabisa”
“C’mon Devotha.Unadhani
ningeibuka tu na kudai Edger
yuko hai kama sina uhakika?
Ninao uhakika mkubwa
kwamba yuko hai ndiyo maana
mtoto wa Rais amechomwa
sindano yenye virusi ili
kumshinikiza Rais aweze
kunipa maelezo ya mahala alipo
Edger.Sijakurupuka Devotha”
akasema Olivia
“Kwa nini umemlenga Rais
moja kwa moja katika suala
hili?Kwa nini unataka
kumchafua rais kwa jambo hili
ambalo halina ukweli
wowote?akauliza Devotha
“Rais ninamuita
baba.Amekuwa ni rafiki
mkubwa wa baba yangu toka
wakiwa wadogo lakini jiulize
kwa nini nikatengeneza virusi
ambavyo vinaweza kumuua
mtoto wake Coletha ambaye
ananiita dada?Nimefanya hivi
kwa kuwa ninafahamu rais
anazo taarifa za jambo hili na
nimefanya hivi ili kumshinikiza
anipe taarifa hizo” akasema
Olivia
“Olivia naomba tuachane na
hilo la Edger.Nataka
tuzungumze masuala
mengine.Nataka unieleze
kuhusu mahusiano yako na
IS.Umeonekana ukiwa na Seif
Almuhsin na vile vile umekuwa
na mawasiliano na Sayid
Omar.Nataka kuf…………..”
“Hakuna haja ya kwenda
mbali Devotha.Sintaweza
kukueleza chochote.Kama
nilivyokueleza kuwa
nitazungumza nawe pale
ambapo utanipa taarifa za
mahala alipo Edger Kaka.Kama
hakuna taarifa hizo hakuna
nitakachoweza
kukwambia.Mmekosea sana
kumteka hata baba yangu ili
kunilazimisha niongee lakini
nawahakikishia hata kama
mtatishia kuua familia yangu
nzima mbele yangu
sintafumbua mdomo wangu
kutamka chochote.Muacheni
baba aende zake muendelee
kunishikilia mimi” akasema
Olivia
“One more thing.Fikisha
salamu zangu kwa Rais kwamba
muda unakwenda na asipofanya
juhudi atampoteza
mwanae.Mimi ndiye
niliyetengeneza virusi hivyo
alivyoambukizwa mwanae na
ndiye mwenye uwezo wa
kumtibu.Asisumbuke kutafuta
tiba hospitali kwani atampoteza
mwanae.Anachotakiwa kufanya
ni kunionyesha mahala alipo
Edger na mimi nitamponya
mwanae.Devotha nadhani
hatuna cha kuzungumza zaidi
hapa nirejeshe chumbani
nataka kupumzika mguu
unaniuma” akasema
Olivia.Devotha akawapa ishara
walinzi watatu waliokuwa
karibu akawataka wampeleke
Olivia chumbani wakamfungie
“Natamani sana kumpuuza
Olivia na kuamini ana matatizo
ya akili lakini kuna kitu
kinanilazimisha intake
kumuamini.Japo tunajaribu
kuamini kwamba ana matatizo
ya akili lakini Olivi ani mzima
hana tatizo lolote.Alizungumza
kwanza na Rais akamueleza
jambo hilo la
Edger,nilipozungumza naye
akaendelea kusisitiza kuwa
Edger yuko hai na leo tena
ameendelea kusisitiza na
amekwenda mbali zaidi akadai
anao ushahidi wa kuthibitisha
hicho anachokisema.Nadhani
Olivia hajakurupuka katika
suala hili.Ninachojiuliza kwa
nini amlenge moja kwa moja
Rais Dr Evans? Kuna kitu
anakifahamu kuhusu jambo
hili?akajiuliza Devotha
“Maneno aliyoyatamka
Olivia yamenishawishi
kulitazama suala hili.Ngoja
nitumie muda mfupi kulitazama
suala hili.Nitaanza kwanza
katika makaburi ya Midizini
alikozikwa Edger.Nataka
nikalichunguze hilo kaburi
kama kweli limechimbwa”
akawaza Devotha na kuelekea
katika gari lake akaondoka.Moja
kwa moja alielekea katika
makaburi ya midizini
alikozikwa Edger
Kaka.Alilitafuta kaburi la Edger
akalipata na kuangalia upande
wa kulia mwa kaburi lile kama
alivyoelekezwa na Olivia ni
kweli kulionekana kama
kumetitia kidogo.Akapiga picha
za kutosha halafu akaondoka
“Olivia anaweza kuwa
sahihi.Alisema upande wa kulia
mwa kaburi la Edger
kumechimbwa na hata
ukitazama panaonekana kweli
pamechimbwa japo si hivi
karibuni.Nashawishika kutaka
kulifanyia suala hili uchunguzi
wa kina.Yawezekasna lina
ukweli ndani yake” akawaza
Devotha akiwa garini
“Devotha kuna siri kubwa
hapa ambayo huifahamu na
kama ukitaka kuifahamu
nisaidie kujua mahala alipo
Edger Kaka.Nakuhakikishia ni
siri kubwa” akayakumbuka
maneno ya Olivia
“Msisitizo huu wa Olivia si
wa bure.Hata mimi kuna kitu
nimeanza kukiona katika
maelezo yake.Michezo kama hii
ya kutengeneza vifo ipo na
inafanyika sana katika nchi za
wenzetu zilizoendelea.Kama
suala hili ni la kweli kwa nini
watengeneze kifo cha Edger?Na
kama ni kweli nani waliofanya
jambo hilo? Devotha
akaendelea kujiuliza maswali
“Najiuliza swali lingine
suala hili la Edger lina maslahi
gani kwa Olivia?Kwa nini
alifuatilie namna hii? Je katika
suala hili yuko peke yake au
kuna watu wako nyuma yake?
Kama wapo ni akina nani?
Kweli hapa kuna siri kubwa
kama alivyosema Olivia.Nitajipa
zoezi la kuchunguza ili niupate
ukweli wa jambo hili hata hivyo
bado nitalazimika kumuhoji
zaidi Olivia kuna mengi
ninaweza kuyapata kwake zaidi
ya hili suala la mahusiano yake
na IS.Natakiwa kujenga naye
urafiki badala ya kuwa adui
yake.Hili halitamfurahisha Dr
Evans lakini nitatafuta namna
ya kufanya ili lisiweze kuleta
mgongano.Dr Evans anataka
majibu ya haraka kutoka kwa
Olivia lakini ukimuangalia
Olivia ana mambo mengi
ambayo ili kuyapata hatupaswi
kufanya haraka wala kutumia
nguvu” akawaza Devotha
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 3
Devotha aliwasili kitalu 1
alikopelekwa Mathew Mulumbi
akitokea katika makaburi ya
midizini.Aliingiza gari katika
maegesho chini ya jengo
akashuka na kuelekea
ndani.Juhudi za kuunganisha
mfumo mpya wa mawasiliano
ziliendelea chini ya usimamizi
wa Kaiza.Devotha akamuita
Kaiza ofisi kwake
“Nipe ripoti Kaiza mambo
yanavyokwenda hapa”akasema
Devotha
“Hapa mambo yanakwenda
vizuri.Kama nilivyokueleza
tumefanikiwa kumpata Mathew
Mulumbi yuko hapa.Tumeanza
kumpatia mateso.Tulimuweka
chumba cha baridi na sasa
tumemuweka white room
tukisubiri maelekezo
yako.Kingine kinachoendelea
hivi sasa ni kuunganisha vitalu
vyetu vyote katika mfumo
mpya.Vipi huko utokako
mambo
yamekwendaje?akauliza Kaiza
“Huko mambo ni vile vile
kama yalivyokuwa.Olivia
amegoma kufunguka
kabisa”akasema Devotha
“Devotha nilikushauri jana
kwamba tubadili mbinu za
kumuhoji Olivia.Kwa kutumia
nguvu katu hatutaweza kupata
chochote toka kwake hata kama
tukimuhoji kwa mwaka
mzima.Kama aliweza
kushuhudia baba yake akipigwa
risasi na hakufunguka hakuna
namna tutakayoweza
kumfungua kwa kutumia
nguvu” akasema Kaiza
“Ulikuwa sahihi
Kaiza,matumizi ya nguvu
hayatasaidia.Nimefuata ushauri
wako nikazungumza naye
kirafiki na katika mazungumo
hayo kuna kitu nimekipata”
akasema Devotha
“Umepata kitu gani kutoka
kwa Olivia?akauliza Kaiza
“Jana alipozungumza na
Rais Olivia alizungumza kitu
Fulani ambacho wote tulimuona
kama mtu
aliyechanganyikwa.Alisema
kwamba Edger Kaka ambaye
wote tunafahamu alifariki
katika ajali ya gari miaka mitatu
iliyopita yuko
hai.Nilipozungumza naye pia
akaendelea kusisitiza jambo
hilo na kusisitiza kwamba
Edger kaka yuko hai na akaenda
mbali zaidi akadai kwamba Rais
Dr Evans anafahamu jambo hilo
na ndiyo maana
akamuambukiza mtoto wake
virusi alivyovitengeneza yeye
mwenyewe ili kumshinikiza
Rais ampe taarifa za mahala
aliko Edger Kaka.Leo tena
baada ya kuzungumza naye
amerudia tena jambo hilo
nikamkumbusha kwamba
Edger kaka amekwisha fariki
dunia na hakuna namna ya
kumrejesha akaendelea
kusisitiza kwamba Edger
hajafariki dunia yuko
hai.Akanihakikishia kwamba
ana ushahidi mkubwa kwamba
Edger hajafa.Olivia akadai
alichukua sampuli za mabaki ya
mwili ule uliozikwa katika
kaburi la Edger akaenda
kufanya uchunguzi akabaini
kwamba mwili ule haukuwa wa
Edger Kaka” akasema Devotha.
“Amefanyia uchunguzi
mwili wa Edger? How?akauliza
Kaiza
“Anadai amechukua mabaki
ya mwili uliozikwa katika
kaburi la Edger akaenda
kufanya uchunguzi ndipo
akagundua kwamba mwili ule
haukuwa wa Edger”
“Amewezaje kugundua
kama ule mwili si wa Edger?Ni
mwili wa nani?akauliza Kaiza
“Hakutaka kunieleza kwa
undani jambo hili lakini amekiri
kwamba kuna siri kubwa
ambayo hatuifahamu na kama
ninataka anieleze kila kitu basi
nimsaidie kupata taarifa za
mahala alipo Edger Kaka”
akasema Devotha
“Devotha tujiulize kwa nini
Olivia aibuke sasa na kudai
Edger ambaye wote
tunafahamu amefariki miaka
mitatu iliyopita yuko
hai?Amekuonyesha ushahidi
alio nao kuhusiana na hicho
anachokizungumza?akauliza
Kaiza
“Hajanionyesha ushahidi
wowote lakini kwa kumtazama
tu usoni anaonekana
anamaanisha anachokisema”
“Do you believe
her?akauliza Kaiza
“Simuamini moja kwa moja
lakini kuna kitu ninakiona
katika suala hili” akasema
Devotha
“That woman is a damn
lier! Don’t trust her! Akasema
Kaiza
“Kaiza ukilitazama suala hili
kwa upana utagundua kuna kitu
ndani yake ambacho hatukijui
bad😵livia asingeweza
kulisisitiza jambo hili kama
halina ukweli na isitoshe
amemuelekezea mzigo wote
Rais.Kwa nini awaache watu
zaidi ya milioni hamsini na
ajielekeze kwa mtu mmoja
tu?Hapa lazima kuna jambo
ndiyo maana baada ya
kuachana naye nilikwenda
katika makaburi ya midizini
alikozikwa Edger kaka
kulichunguza.Nimelikagua
kaburi na hizi ndizo picha
nilizozipata” akasema Devotha
na kuzihamishia picha alizopiga
katika kaburi la Edger kwenye
kompyuta yake akamuonyesha
Kaiza.
“Umegundua nini katika
hizo picha Kaiza?akauliza
Devotha
“Sioni chochote katika hizi
picha zaidi ya kaburi la Edger”
“Ukilitazama hili kaburi
kwa makini utagundua kuna
kitu hakiko sawa.Tazama
upande wa kulia wa kaburi
kunaonekana kumetitia kidogo
tofauti na upande wa
kushoto.Kwa mujibu wa Olivia
ni kwamba upande huu wa
kulia wa kaburi la Edger
ulichimbwa ndipo akaweza
kuingia ndani ya kaburi akapata
sampuli za mabaki ya mwili
uliozikwa akaenda kufanya
uchunguzi akagundua mwili ule
haukuwa wa Edger.Ukilitazama
kaburi hili utaona ni kweli
upande huu unaonekana
umewahi kuchimbwa japo si
hivi karibuni lakini
umechimbwa na hii inanipa
uhakika kwamba yawezekana
anachokisema Olivia ni kitu cha
kweli” akasema Devotha
“Bado nafsi yangu inakuwa
nzito sana kukubaliana na hicho
anachokisema Olivia.Edger kaka
amekwisha fariki dunia na
hakuna namna anayoweza
kuwa hai”akasema Kaiza
“Ni vipi kama ni kweli
Edger hajafa?akauliza Devotha
“Haiwezekani
Devotha.Huyu mwanamke
anataka kucheza na akili
zetu.Taarifa zinadai ni yeye
mwenyewe aliyekwenda
hospitali baada ya ajali na
kuutambua mwili wa Edger
iweje leo aibuke na kudai mwili
ule haukuwa wa Edger?akauliza
Kaiza
“Sikiliza Kaiza mambo
kama haya yanatokea sana hasa
katika nchi za wenzetu ambazo
teknolojoa ni kubwa.Watu
wanaghushi vifo vyao na
inaonekana kweli wamekufa
lakini kumbe bado wako
hai.Sishangai hata hili tukio la
Edger likawa kweli ni la
kutengeneza kama anavyodai
Olivia.Haya mambo yapo na
yanafanyika sana ila hapa
kwetu bado ni mageni”akasema
Devotha
“Kwa hiyo umepanga
kufanya nini Devotha kuhusiana
na suala hilo?akauliza Kaiza
“Siwezi kulipuuza.Kuna vitu
vinanipa hamu ya kutaka
kulichunguza hili jambo kwa
undani na kuufahamu ukweli
wake”akajibu Devotha
“Devotha ushauri wangu
tusipoteze muda katika suala
hilo.Yule mwanamke
anashirikiana na magaidi na
hapaswi hata kidogo
kuaminiwa.Jukumu letu ni
kuhakikisha kwa namna yoyote
ile tunamfanya atueleze kila
kitu kuhusu mtandao wao na
mipango yao yote.Hili suala
alilolianzisha la kuhusu Edger
linataka kutupotezea mwelekeo
na kutuvuruga.Ndivyo magaidi
wanavyofanya mambo yao
hutafuta jambo la kuwapoteza
watu muelekeo na wao hupata
mwanya wa kufanya mambo
yao.Tusiwape nafasi hiyo
Devotha”akasema Kaiza
“Kaiza nitafanya uchunguzi
wa jambo hili kuufahamu
ukweli.Olivia hawezi akasisitiza
jambo hili kama halina
ukweli,zaidi ya yote Olivia ana
mambo mengi anayafahamu na
hataweza kutueleza hadi pale
atakapopata taarifa za
kuhusiana na alipo Edger hivyo
lazima uchunguzi ufanyike
katika jambo hili na ukweli
ujulikane” akasema Devotha
“Rais anafahamu kuhusu
hicho unachotaka
kukifanya?akauliza Kaiza
“Rais hafahamu chochote
na hapaswi kujua kama
uchunguzi huu
unafanyika.Olivia amemlenga
yeye moja kwa moja kuwa
anafahamu mahala alipo Edger
hivyo akifahamu kama
tunafanya uchunguzi wa hili
jambo utaibuka mtafaruku
mkubwa”akasema Devotha
“Rais mwenyewe
umezungumza naye ukamuuliza
kama analifahamu hili
jambo?akauliza Kaiza
“Nimezungumza naye
nikamuuliza akakana kabisa
kulifahamu.Olivia hawezi
akamlenga mtu mzito kama
Rais bila kuwa na
sababu.Lazima Dr Evans kuna
kitu anakifahamu hivyo lazima
tuchunguze tuujue ukweli”
akasema Devotha
“Ni vipi kama kweli
anafahamu mahala alipo Edger?
Kaiza akauliza
“Kama kweli anafahamu
suala hili husika atakuwa na la
kutueleza kwa nini alifanya hivi
na wapi alipo Edger.Olivia
ameahidi kunieleza siri kubwa
endapo atapata taarifa za
mahali alipo Edger Kaka hivyo
lazima kufanya juu chini
kulichuguza hili jambo na
kuupata ukweli” akasema
Devotha
“Devotha utanisamehe kwa
hili nitakalolisema lakini
sidhani kama hayo ni maamuzi
mazuri.Sisi tuko chini ya Rais na
kila tufanyalo lazima
tumjulishe.Kufanya uchunguzi
huo kwa siri bila kumjulisha
Rais hauleti picha
nzuri.Akigundua
tunamchunguza tutakuwa
katika matatizo.Hatatuamini
tena.Sikushauri Devotha
tufanye hivyo.Tuachane na hili
jambo na tujielekeze katika
jambo la msingi la kuchunguza
kuhusu Olivia na IS” akasema
Kaiza.Maneno yale ya Kaiza
hayakumfurahisha Devotha
“Kaiza toka lini
ukanifundisha namna ya
kufanya kazi yangu?Naomba
iwe mwanzo na mwisho
kunifundisha kazi.Mimi ndiye
mkubwa hapa na hakuna wa
kuuliza swali kwa chochote
nitakachokifanya.Mimi ndiye
ninayepanga nini kifanyike na
nini kisifanyike na kwa sasa
ninasema kwamba uchunguzi
kuhusu Edger kaka lazima
ufanyike hata kama Rais
anahusika.Umenielewa Kaiza?
Akauliza Devotha
“Ninakuelewa Devotha na
hata siku moja sijawahi
kupingana nawe katika
chochote unachokiamua.Wewe
ni mkubwa wangu na
ninapokea maelekezo yote
kutoka kwako lakini katika hili
nina mashaka makubwa
kwamba kama uchunguzi
ukifanyika na rais akagundua
tunamchunguza tutakuwa
tumejiweka katika matatizo
makubwa” akasema Kaiza
“Haijalishi kama Rais
anahusika au hahusiki katika
suala la Edger lakini lazima
tulichunguze na kuufahamu
ukweli.Kama kweli Edger kaka
yuko hai lazima tujue yuko wapi
ili tuweze kupata taarifa
muhimu kutoka kwa
Olivia.Sitaki tena mjadala katika
suala hili” akasema Devotha na
kusimama akachukua
kompyuta yake ndogo
“One more thing” akasema
Devotha na kumgeukia Kaiza
“Nilichokwambia kinabaki
kati yetu hatakiwi mtu
mwingine yeyote kufahamu”
“Sawa Devotha”
“Good.Ninataka
kuzungumza na Mathew
Mulumbi.Nataka kamera zote
zizimwe”
“Unataka kumuhoji Mathew
nje ya kamera?akauliza Kaiza
“Ndiyo.Nataka kuzungumza
naye nje ya kamera”
“Kwa nini Devotha?akauliza
Kaiza
“Kaiza hii ni mara ya
mwisho nitakuonya kuhusu
kuhoji maelekezo yangu”
“I’m sorry Devotha.It wont
happen again” akasema Kaiza
na Devotha akatoka.Kaiza
akamfuata nyuma hadi katika
chumba maalum kwa ajili ya
kufuatilia kamera zote
akawaelekeza watu
waliokuwemo ndani ya kile
chumba kuzima kamera zote
katika chumba alimo
Mathew.Olivia akaongozana na
watu wanne wakiwa na silaha
kuelekea chini aliko
Mathew.Mlango wa chumba
alimowekwa Mathew
ukafunguliwa na Mathew akiwa
amevishwa mavazi meupe
akaonekana akiwa amekaa
kwenye kiti mikono yake ikiwa
imefungwa katika pingu
zilizokuwa katika meza.
“I need a room” akasema
Devotha na watu wote
wakatoka nje akabaki peke yake
ndani ya kile chumba.Kila kitu
ndani ya kile chumba kilikuwa
cheupe akavuta kiti na
kumsogelea Mathew
“Hallow Mathew Mulumbi”
akasema Devotha.Mathew
akamtazama hakusema
chochote
“Kabla ya yote napenda
nikujulishe kuwa kamera zote
zimezimwa na hakuna hakuna
yeyote anayetazama wala
kusikia mazungumzo
yetu.Nimefanya hivi kwa kuwa
nataka tuzungumze kwa uhuru”
akasema Devotha na ukimya
ukapita
“Naitwa Devotha Adolph”
akaendelea
“Ni mkurugenzi wa idara ya
siri ya usalama wa ndani ya
nchi.Tunashughulika na mtu au
kikundi cha watu wanaojaribu
kuhatarisha usalama wa ndani
wa nchi yetu kwa namna yoyote
ile.Kama jina lake lilivyo idara
yetu inafanya mambo yake kwa
siri kubwa bila
kujulikana.Mfano mdogo tu
kama utakumbuka kwa siku za
karibuni kulikuwa na viashiria
vya kuibuka kwa vikundi vidogo
vidogo vyenye milengo ya
kigaidi hapa nchini lakini sasa
hivi hakuna tetesi zozote za
kuwepo kwa vikundi kama
hivyo tena ni kwa sababu kila
vilipojaribu kuibuka tumekuwa
tunavimaliza kabla havijaleta
madhara yoyote kwa nchi,hilo
ndilo hasa jukumu letu
kuhakikisha nchi inakuwa
salama”akasema Devotha
“Ninyi ndio mliomteka
Olivia Themba?Mathew
akauliza
“Ndiyo ni sisi” akajibu
Devotha
“Kwa nini mlimteka
Olivia?Naye ni hatari kwa
usalama wa nchi?akauliza
Mathew
“Tutazungumza hayo
baadae.Kwa sasa nataka
kufahamu mahusiano yako na
Olivia Themba”
“Mahusiano yetu ni ya
kawaida ya kirafiki”akajibu
Mathew
“Unaweza ukanieleza wewe
na Olivia mna muda gani toka
mmefahamiana?
“Ni miezi kadhaa sasa
sikumbuki mingapi lakini
hatuna muda mrefu sana”
“Mahusiano yenu ni ya
kimapenzi?
“Mwanzo tulianza kama
marafiki wa kawaida lakini
baadae tukajikuta kila mmoja
akimtamani mwenzake”akajibu
Mathew
“Ulimpa namba Fulani
Olivia ukamtaka azipige kila
pale atakapokuwa katika
hatari.Olivia amekwisha tueleza
kila kitu hivyo usishangae
nimefahamuje.Nieleze nini hasa
lilikuwa lengo la kumlinda
Olivia hadi ukamtengenezea
program ile maalum?
“Programu ile ni kwa ajili
ya familia yangu.Mwanangu
aliwahi kutekwa nyara na watu
wasiojulikana wakatishia
kumuua na kudai fedha
nyingi.Baada ya hapo ndipo
nilipotengeneza program ile
kwa ajili ya kunijulisha kama
mmoja wa wanafamilia yangu
yuko katika hatari.Olivia kama
mtu wangu wa karibu
nilimuweka pia katika
programu ile ili nifahamu pindi
anapokuwa katika hatari”
akasema Mathew
“Why Olivia?akauliza
Devotha.Mathew akamtazama
hakujibu kitu
“Mathew unao marafiki
wengi wa karibu lakini kwa nini
Olivia pekee ndiye uliyempa
programu hiyo?
“NI kwa sababu Olivia ni
mtu wangu wa karibu sana,zaidi
ya rafiki na kingine kikubwa
nilihisi usalama wake uko
mashakani ndiyo maana
nikampa programu ile”
“Kitu gani kilikufanya uhisi
usalama wa Olivia uko shakani?
“Baada ya kufahamiana
naye niligundua alikuwa na
tatizo linalomsumbua
nikamtaka anieleze kitu gani
kinamsumbua akaniambia ana
matatizo na watu Fulani ambao
hakutaka kuniweka wazi.Ili
kuhakikisha anakuwa salama
niliamua kumpa namba zile ili
nifahamu kila pale
atakapokuwa katiak
hatari”akajibu Mathew
“Unasema Olivia alikueleza
kuwa ana matatizo na watu
Fulani.Kwa nini hukutaka
kuwafahamu watu
wanaohatarisha usalama wa
mwanamke unayempenda?
“Ni kwa sababu
alinihakikishia nisiwe na wasi
wasi kwani ni suala lililo ndani
ya uwezo wake na anaweza
kulitatua hivyo sikutaka
kuendelea kumghasi anieleze ni
watu gani” akajibu Mathew
“Kwa hisia zako unadhani
watu hao ni akina nani?
“Ninaamini watu aliokuwa
katika matatizo nao ni wale
ambao wamemteka Nyara”
“Unamaanisha sisi?
“Ndiyo.Naamini alikuwa
katika matatizo na ninyi ndiyo
maana mkamteka nyara.Olivia
ninamfahamu vyema,she’s an
angel hana tatizo na mtu.Ni
mwanamke mwenye heshima
zake na hata familia yake ni
watu wanaoheshimika hapa
nchini.Kitendo mlichokifanya ni
uonevu mkubwa sana na
ninaapa lazima nihakikishe
ninamuokoa hata mkimficha
wapi” akasema Mathew na
Devotha akacheka kidogo.
“Mkeo anafahamu
mahusiano yako na
Olivia?akauliza Devotha
“Hayo ni masuala yangu
binafsi hutakiwi kuyajua”
“Mr Mathew Mulumbi
nitakosea nikisema kuna mtu au
watu wamekutuma umlinde
Olivia?akauliza Devotha
“Watu gani wamenituma
nimlinde Olivia?Mathew naye
akauliza
“Wewe ndiye
unayewafahamu.Nataka unitajie
watu hao ni akina nani?akauliza
Devotha.Mathew akamtazama
kwa muda halafu akasema
“Jina lako Devotha
Adolph,right?akauliza Mathew
“Yes I’m Devotha Adolph”
akajibu Devotha
“Devotha,kwa nini unahisi
kuna mtu au watu walionituma
nimlinde Olivia? Ninaonekana
kama mtu ninayeweza kufanya
kazi kwa malipo?Devotha
inaonekana hunifahamu
vyema.Mimi ni bilionea nina
fedha za kutosha na siwezi
kufanya kazi kwa
malipo”akajibu Mathew
“Mathew naamini yupo mtu
au watu waliokupa kazi ya
kumlinda Olivia na kuhakikisha
anakuwa salama na ni hao ndio
waliokupa huo
ubilionea.Ninataka
kuwafahamau watu hao ni
akina nani? Akauliza Devotha
“Narudia tena
kukuhakikishia Devotha hakuna
mtu au watu walinituma
nimlinde Olivia.Ninamlinda
Olivia na nitaendelea kufanya
hivyo dhidi ya wale wote wenye
kuhatarisha usalama
wake.Devotha umeolewa?Una
watoto wangapi?akauliza
Mathew
“Hayo mambo hayakuhusu
Mathew.Nataka kufahamu kwa
nini uchague kuhatarisha
maisha yako kumlinda Olivia na
si mtu mwingine? Wewe una
familia yako kwa nini uamue
kupoteza muda kumlinda mtu
kama Olivia?Akauliza Devotha
Mathew akawa kimya
“Devotha umekwisha
niuliza swali hilo na
nimekujibu tayari”
“Mathew tayari tunafahamu
wewe na Olivia mmekuwa
mnatumiwa na kikundi fulani
cha watu katika kufanikisha
mambo yao hapa nchini.Lengo
letu la kuwashikilia wewe na
Olivia ni kutaka kuwafahamu
watu hao ni akina nani?
Akauliza Devotha
“Bado sijakuelewa
unaposema kuna watu ambao
wanatutumia mimi na Olivia.Ni
akina nani watuhao?Labda
jaribu kutafuta lugha nzuri ya
kuuliza swali lako ili
nikuelewe”akasema Mathew
“Nazungumzia watu
mnaoshirikiana nao ambao
wanawatumia wewe na Olivia
katika kufanikisha mipango yao
hapa nchini.Tukiwafahamu hao
ninakuhakikishia Mathew
hamtakuwa katika hatari
yoyote lakini kama mtaendelea
kuwaficha mtaendelea kujiweka
katika hatari kubwa”
“Devotha kuna kitu
ninakiona katika maelezo yako
lakini hutaki kukiweka wazi
unakizunguka.Kuwa muwazi ili
nielewe unachokitaka” akasema
Mathew
“Mathew Olivia tayari
amekwisha hojiwa na amekiri
kuwa mnatumiwa na kikundi
Fulani kufanikisha mipango yao
hapa nchini.Sasa ni zamu
yako.Ninataka na wewe
unieleze kuhusiana na watu
mnaoshirikiana nao na mipango
yenu hapa nchini.Mathew sitaki
tuanze kutumia nguvu kukutesa
wakati tunaweza kulimaliza hili
suala bila matumizi yoyote ya
nguvu”akasema Devotha
“Kidogo nimeanza
kukuelewa Devotha lakini mimi
na Olivia hatuna watu
tunaoshirikiana nao.Kama
amewaeleza hivyo
amewadanganya.Kwani
amesema tunashirikiana na
akina nani?akauliza Mathew
“Mathew tafadhali
usilifanye suala hili likawa
gumu kwa upande wak😵livia
tayari amekwisha eleza kila kitu
na sasa ni zamu yako.Nieleze
ukweli wote hakuna anayesikia
Zaidi yangu ndiyo maana
kamera zote zilizomo humu
ndani zimezimwa hivyo usihofu
kunieleza ukweli. Nieleze
tafadhali akina nani
mnashirikiana nao?
“Devotha bado jibu langu ni
lile lile kwamba hakuna mtu
ninayeshirikiana naye”
“Nani alikutuma umlinde
Olivia?
“No one” akajibu Mathew
“Mathew tunafahamu
umewahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi na kutokana na
ujuzi wako umekuwa
unatumiwa na watu Fulani
katika kuhakikisha Olivia
anakuwa salama ndiyo maana
ukampa program ile maalum ya
kukujulisha pindi anapokuwa
katika hatari ambayo ilikusaidia
kufahamu mahala alikokuwa
amefichwa baada ya kutekwa
na ukajipanga kwenda
kumuokoa.Nataka kufahamu
nani waliokupa kazi ya
kumlinda Olivia?
Mathew akacheka kidogo
halafu akasema
“Kwa nini unapenda
kurudia rudia maswali ambayo
nimekwisha kujibu?Kama
umeishiwa maswali naomba na
mimi unijibu kwa nini
mmemteka Olivia?Ana
mahusiano gani na usalama wa
nchi?akauliza Mathew
“Mathew naomba tuweke
mzaha pembeni.Nchi iko katika
kitisho kikubwa cha
kutumbukia katika machafuko
makubwa,ni wewe na Olivia
ndio tunaowategemea
kutusaidia katika kuliepusha
hilo lisitokee.Mathew umefanya
mambo mengi makubwa kwa
nchi hii lakini naomba haya yote
mazuri uliyoyafanya
yasiharibiwe na fedha
unazolipwa na IS.Mathew
n……………”
“Umesema IS?akauliza
Mathew na kumkatisha Devotha
“Ndiyo.Mbona unajifanya
kustuka?
“Nimestuka kusikia jina hilo
likitajwa na hasa ulipotamka
kuwa mambo mazuri
niliyoyafanya yasiharibiwe na
fedha ninazolipwa na IS.Una
maanisha nini Devotha?
“Mathew huu ni wakati wa
kuweka wazi kila kitu.Tayari
tunafahamu wewe na Olivia
mnatumiwa na kikundi cha IS
na wanawalipa fedha nyingi
sana ambazo ndizo chanzo cha
utajiri wenu mkubwa.Tunao
ushahidi wa kutosha kuhusu
ninyi kushirikiana na IS hivyo
tuokoe muda nataka
kuufahamu mtandao wenu
wote hapa Tanzania na nini
malengo yenu?
“Devotha hicho
unachonieleza kimenistua
sana.Nani kawapa taarifa kuwa
ninashirikiana na IS? Hiki ni
kikundi cha kigaidi ninawezaje
kushirikiana na magaidi?Kwa
muda mrefu nimekuwa
nikifanya kazi ya kupambana na
magaidi hawa iweje leo
nibadilike na kushirikiana
nao?Kingine utajiri wangu
hautokani na fedha haramu bali
ni utajiri halali kabisa na
nimekuwa tajiri hata kabla ya
kufahamiana na OIivia.Fuatilia
chanzo cha utajiri wangu
utajua.Aliyewapa taarifa kuwa
mimi au Olivia tunashirikiana
na kikundi cha IS
amewadanganya.Hakuna kati
yetu anayeshirikiana na IS”
akasema Mathew
“Mathew hatujakurupuka
.Tunao ushahidi mkubwa wa
jambo hili kwamba wewe na
Olivia mnashirikiana na IS”
akasema Devotha
“Devotha nimekuwa katika
kazi hizi kwa nusu ya umri
wangu nilionao sasa.Nimepitia
mambo mengi na ninazifahamu
mbinu nyingi za magaidi hasa
pale wanapotaka kutekekeleza
mpango wao sehemu Fulani
hutafuta namna ya kuwapoteza
watu ambao wanaona
watakuwa kikwazo kwao.Kama
kuna mpango wowote wa
kufanyika kwa shambulio la
kigaidi hapa nchini basi
mmenasa kwenye mtego wao
na tayari wamewapoteza
mwelekeo kwa kuwaaminisha
kwamba ninashirikiana na
kikundi cha IS”
“Mathew tumefanya
uchunguzi na tumegundua
wewe na Olivia mmekuwa na
mashirikiano na kikundi cha
IS.Nchi iko katika hatari na
binafsi siko tayari kukubali nchi
ikaingia katika hatari.Kazi ya
idara yangu ni kuhakikisha nchi
inakuwa salama na wananchi
wake wanaendelea na shughuli
zao kama kawaida.Nitakutaka
kwa mara ya mwisho unipe
majina ya watu ambao
mnashirikiana nao waliopo
hapa nchini na walio nje ya nchi
kabla sijafikia maamuzi ya
kuufungua ukurasa mpya kati
yangu nawe” akasema Devotha
na kusimama
“Devotha nakuomba ukae
tuzungumze” akasema Mathew
na Devotha aliyekuwa
amesimama akaketi
“Uliniambia kamera zote
zilizopo katika chumba hiki
zimezimwa na hakuna mtu
yeyote anayefuatilia
mazungumzo yetu.Nataka kujua
kwa nini? Huogopi kuwa katika
chumba kimoja na mtu
unayedai ana mashirikiano na
magaidi?
“Wewe ni jasusi
mzoefu,umepitia mambo mengi
unafahamu mbinu zote za
mateso unajua kutunza
siri,sioni sababu ya
kukutesa.Naamini hata ukipewa
mateso ya aina gani hautaweza
kutoa siri ndiyo maana
nikaamua kuja hapa
kuzungumza nawe kirafiki.Kuna
vitu vingi ninaweza kuvipata
kwako kama nikizungumza
nawe ana kwa ana nje ya
kamera na bila kuingiliwa na
mtu yeyote”
“Good.Kwa kuwa
mazungumzo yetu haya ni ya
kirafiki nataka tuzungumze
kweli kama marafiki.Ninataka
kuuliza swali na nitaomba uwe
muwazi kwangu” akasema
Mathew
“Go ahead”
“Ulisema mnao ushahidi wa
kutosha kutuhusisha mimi na
Olivia kushirikiana na kikundi
cha IS.
Yawezekana mmekuwa
mnafuatilia mawasiliano yangu
na mkagundua ninawasiliana na
watu wa IS.Kama ndiyo niambie
bila kunificha kwamba Mathew
umekuwa ukiwasiliana na mtu
Fulani kutoka IS na
mmezungumza mambo
Fulani.Kama mnao ushahidi huo
nieleze tafadhali na sintakataa
kama ni kweli” akasema
Mathew.
“Huu ni mtego.Huyu jamaa
anajiamini sana.Hatuna
ushahidi wowote wa
kumuhusisha na
IS.Nikimtazama haonekani
kama ana mashirikiano
nao.Hapa amenibana ngoja
nimueleze ukweli” akawaza
Devotha
“Mathew naomba nikueleze
ukweli kwamba hatuna
ushahidi wa moja kwa moja wa
kukuhusisha wewe na kikundi
cha IS yawezekana ni kwa kuwa
unafahamu sana namna ya
kujificha lakini mwenzako
Olivia tayari tuna kila ushahidi
kwamba anashirikiana na
kikundi cha IS”
“Olivia anashirikiana na IS?
Kivipi? akauliza Mathew
akionekana kushangaa
“Mstuko huu ni wa kweli au
anaigiza? Akajiuliza Devotha
baada ya kuuona mstuko katika
uso wa Mathew aliposikia Olivia
anashirikiana na IS
“Tulipata taarifa za
kiintelijensia kwamba Olivia
amekutana na Seif Almuhsin
jijini Kinshasa.Seif Almuhsin ni
mmoja kati ya watu muhimu
katika kikundi cha IS na
anatajwa kuwa ndiye
anayeendesha zoezi la usajili wa
vijana wanaojiunga na IS kisha
kupelekwa katika kambi za
mafunzo kuandaliwa kwa
mambo ya kigaidi.Olivia na Seif
walifikia hoteli moja jijini
Kinshasa”akasema Devotha na
kumuonyesha Mathew picha za
Olivia akiwa na Seif Almuhsin
jijini Kinshasa.Mathew
alishangaa sana
“Kitendo cha Olivia
kukutana na Seif Almuhsin jijini
Kinshasa” akaendelea Devotha
“Kilitupa maswali mengi na
tukaanza kumfuatilia kujua
kama ana mahusiano na
magaidi wa IS.Aliporejea
nyumbani kutokea Kinshasa
tulimteka nyara na baada ya
kupekua mawasiliano yake
tukagundua amekuwa na
mawasiliano na mtu anaitwa
Sayid Omar”
“Sayid Omar?Who is he?
Mathew akauliza
“Mathew sipendi
mzaha.Humfahamu Sayid
Omar?akauliza Devotha
“Devotha hizi ni taarifa
mpya kabisa kwangu
ninazisikia kwa mara ya
kwanza toka kwako” akasema
Mathew
“Sayid Omar ni mfanya
biashara mkubwa na anatajwa
kuwa ni mfadhili mkubwa wa
kikundi cha IS.Tumekuta
mawasiliano ya barua pepe kati
yake na Olivia katika kompyuta
ya Olivia”
“Subiri kidogo
Devotha,walikuwa
wanawasiliana kuhusu
nini?akauliza Mathew
“Hatujaweza bado kufasiri
mazungumzo yao kwani
wametumia lugha ya
kiarabu.Kwa bahati mbaya
katika idara yetu tulikuwa na
mtu mmoja tu aliyekuwa na
umahiri katika lugha ya kiarabu
na kwa sasa hayupo hivyo
tumeshindwa kujua ambacho
Olivia na Sayid walikuwa
wanawasiliana hadi hapo
tutakapompata mtu
anayeifahamu vyema lugha
hiyo”akajibu Devotha
“Ninaweza kuyaona
mawasiliano hayo?akauliza
Mathew na Olivia akamtazama
“Nina ifahamu vyema lugha
ya kiarabu.Ninaweza kuyaona
mazungumzo yao nikakusaidia
kujua walikuwa wanaongelea
nini? akasema Mathew
Devotha akaendelea
kumtazama Mathew kwa
makini
“Tafadhali niamini
Devotha.Nionyeshe barua pepe
hizo tujue nini hasa
walichokuwa wanawasiliana”
akasema Mathew.Devotha
akafungua mojawapo ya faili
katika kompyuta yake na
kumuonyesha Mathew ambaye
aliisoma halafu akasema
“Katika barua pepe hii
Sayid Omar anamuuliza Olivia
kuhusiana na maendeleo ya
mpango wa kutengeneza
kirusi.Olivia anamjibu kwamba
anaendelea vizuri na uandaaji
wa kirusi” akasema Mathew
huku mstuko mkubwa
ukionekana usoni pake.
“Una uhakika walikuwa
wanawasiliana kuhusu
kirusi?akauliza Devotha naye
akionekana kushangaa
“Ndivyo inavyosomeka
hapa” akajibu Mathew
Devotha akafungua tena
barua pepe nyingine
akamuonyesha Mathew
akaisoma
“Katika barua pepe
hii,Sayid anamkumbusha Olivia
kua taarifa za mara kwa mara
kuhusu maendeleo ya mradi wa
kutengeneza kirusi.Olivia
anamjibu kwamba anaendelea
vyema na utafiti wake na
amefikia sehemu nzuri.Katika
hii barua pepe nyingine Sayid
anamkumbusha Olivia ajitahidi
kufanya haraka kukamilisha
kirusi kwani muda unakwenda
na operesheni itaanza mara
moja.Olivia anamjibu kwamba
yuko katika hatua za mwisho za
majaribio ya kirusi”
“My God ! Kumbe huu ni
mpango wa IS” akasema
Devotha kwa sauti ndogo
“Devotha unafahamu
chochote kuhusiana na hiki
kinachozungumzwa katika
barua pepe hizi? Una hakika
barua pepe hizi zinatoka kwa
Olivia Themba?akauliza
Mathew.Devotha akamtazama
halafu akasema
“Mathew usiniambie
hulifahamu jambo hili” akasema
Devotha.
“Devotha sikulazimishi
uniamini lakini hii nakwambia
ukweli,hii ni mara ya kwanza
ninalifahamu jambo
hili.Nimekuwa karibu na Olivia
kwa miezi kadhaa sasa lakini
sikuwahi kuhisi kama anaweza
akafanya kitu kama
hiki.Nimestuka sana
Devotha.Naomba tafadhali
unieleze nini hasa
kinachoendelea hapa?akauliza
Mathew lakini Devotha
hakuonekana kumuamini
“Please Devotha tell me
what’s going on.Olivia ni mtu
muhimu sana kwangu hivyo
nataka kujua kama kweli
anashirikiana na magaidi wa
IS.Nataka kujua mipango
wanayoipanga.Tafadhali
Devotha” akaomba Mathew.
“Sawa
nitakueleza.Tulipofahamu kuwa
ana mawasiliano na Sayid Omar
tulitaka atupe maelezo ya kina
kuhusu Sayid na akatupa namba
ambazo alituambia zitatusaidia
kufahamu alipo Sayid Omar na
baada ya kupiga namba zile
ndipo mfumo wetu wote wa
mawasiliano ukajifunga hakuna
kompyuta iliyofanya kazi
tena.Ili kufungua mfumo wetu
ilihitaji namba maalum na
Olivia aligoma kutupa namba
hiyo hadi atakapoona na
Rais.Nilifanya mpango wa
kumkutanisha na Rais
wakazungumza ndipo Olivia
alipomstua Rais kwa
kumwambia eti anamtaka
Edger Kaka”
“Edger Kaka?Mathew
akashangaa
“Edger Kaka aliwahi kuwa
mbunge wa bunge la jamhuri ya
muungano wa Tanzania na
alifariki katika ajali ya gari
miaka mitatu iliyopita” akasema
Devotha
“Wakati suala hili linatokea
nilikuwa nje ya nchi” akasema
Mathew
“Olivia ameibuka na kudai
kuwa Edger Kaka hakufariki
katika ile ajali bali yuko hai”
“Yuko hai?Kivipi?Mathew
akauliza
“Anadai kuwa ni mchezo
ulichezwa lakini Edger hakufa
katika ile ajali”
“Ana uhakika gani kuwa
Edger hajafariki?Mathew
akauliza
“Anadai kuwa amefanya
uchunguzi wake akagundua
kuwa mwili ule uliozikwa
ambao wote tuliamini ni wa
Edger haukuwa mwili wa
Edger.Olivia alimlenga moja
kwa moja Rais Dr Evans kuwa
anafahamu aliko Edger Kaka na
ili kumshinikiza aweze
kumuonyesha mahala alipo
alitengeneza virusi ambavyo
amemuambukiza Coletha mtoto
wa rais na kama Rais
asipotekeleza maagizo ya Olivia
katika muda aliompatia basi
mwanae atapoteza
maisha.Nimestuka baada ya
kugundua kuwa kumbe mpango
huu ameshirikiana na IS
kutokana na ushahidi
tulioupata kutoka katika barua
pepe hizi alizokuwa
anawasiliana na Sayid
Omar.Tuliamini Olivia alikuwa
anatumiwa na wanasiasa
kutaka kumchafua rais na
serikali yake lakini kumbe ni IS
walio nyuma ya mpango huu na
Olivia anatumika tu” akasema
Devotha
“Devotha sasa nimekuelewa
kwa nini mlimteka
Olivia.Ninakuhakikishia sikuwa
nikifahamu chochote kuhusiana
na Olivia kushirikiana na
IS.Nimestushwa mno na hiki
nilichokifahamu.Olivia
alinieleza ana matatizo na watu
Fulani lakini ni tatizo analoweza
kulimaliza.Kwa kuwa ni mtu
wangu wa karibu nikampa
namba zile za programu
maalum ya kuniwezesha mimi
kufahamu mahala alipo kila
pale atakapokuwa amepatwa na
matatizo.Nikiwa mkutanoni
Arusha nikapokea ujumbe
kutoka katika ile namba
niliyompa Olivia.Baada ya
kufuatilia nikagundua kuwa
Olivia alikuwa ametekwa
nyara.Programu ile ilinionyesha
mahala namba ile ilikopigwa
hivyo ikanilazimu kuondoka
Arusha haraka sana kurejea Dar
es salaam kwa ajili ya kwenda
kumuokoa Olivia na nilikua
naendelea na harakati za
kumuokoa hadi pale na mimi
nilipotekwa asubuhi ya leo
kufuatia mtego mlioweka
mkishirikiana na Lucy Themba
mke wa Agrey Themba.Sikuwa
nikifahamu kama Olivia ana siri
kubwa namna hii”akasema
Mathew
“Tulikuchukua kwa vile u
mtu wa karibu na Olivia na
tuliamini mnashirikiana na kazi
yako kubwa ni kuhakikisha
anakuwa salama.Ulifahamu
mahala alikofichwa Olivia baada
ya kutekwa na ukawa mbioni
kwenda kumuokoa na katika
harakati hizo za kumtafuta uliua
watu wetu kumi na tatu kitu
ambacho hakijawahi kutokea
toka idara hii toka
ilipoanzishwa.Kwa gharama
zozote zile ilikuwa lazima
tukupate kwani tayari
ulikwisha kuwa mtu hatari
kwetu na ulikuwa mbioni
kuharibu mipango yetu yote”
akasema Devotha
“Devotha nakuhakikishia
mimi siwezi kuwa na
mahusiano na IS na wala
sikujua kama Olivia ana
mahusiano na watu hao.Kama
ningefahamu ana mahusiano
nao ningekwisha mmaliza
mwenyewe kitambo sana kwani
siwapendi magaidi.Samahani
kwa tukio la jana lakini
nilifanya tukio lile bila kujua
kama wale ni watu wenu,nilijua
ni kikundi cha watu wanaoteka
watu kwa lengo la kujipatia
fedha.Naomba uniamini
Devotha” akasema Mathew
“Mathew hivi tunavyoongea
mtoto wa Rais yuko hospitali na
kuna hatari anaweza akapoteza
maisha endapo Rais
hatamueleza Olivia mahala
alipo Edger
Kaka.Nimezungumza na Olivia
asubuhi hii na ameendelea
kusisitiza kuwa Edger yuko hai
na Rais Dr Evans anafahamu
mahala alipo.Kutokana na
msisitizo huo niliamua
kulifanyia uchunguzi jambo hilo
kuufahamu ukweli wake lakini
baada ya kufahamu kuwa ni
jambo linalowahusisha pia IS
nimeishiwa nguvu ya kuendelea
kulichunguza hili
suala.Nimeanza kuyaamini
maneno ya Rais kuwa huu ni
mpango maalum wa kutaka
kuleta machafuko hapa
nchini.IS wanatambua Edger
alikuwa na watu wengi sana
wanaomuunga mkono hasa
vijana unadhani nini kitatokea
wakisikia kuwa Edger yuko hai
na serikali ndio
wanaomshikilia?Ni wazi
kutatokea machafuko makubwa
na hicho ndicho wanachokitaka
IS ili waweze kujipenyeza na
kufanya mambo yao.Ahsante
sana Mathew kwa kunisaidia
kufahamu mawasiliano ya
Olivia na Sayid.Sina haja ya
kuendelea tena kulichunguza
jambo hili kwani ni moja ya
mipango ya IS kutaka kuleta
machafuko hapa nchini na
hakuna ukweli wowote”
akasema Devotha
“Devotha nisikilize.Kuna
maswali ambayo nimejiuliza
kufuatia maelezo yako.Kwanza
kuna nini kati ya IS na Edger
Kaka?akauliza Mathew
“Mathew huu ni mchezo
unataka kuchezwa na IS.Hakuna
ukweli wowote katika suala
hili.Edger kaka amekwisha
fariki muda mrefu wanataka
kuzua mtafaruku katika jamii na
kuleta machafuko.Wanajua
Edger alikuwa anapendwa na
watu na kifo chake
kiliwahuzunisha wengi hivyo
wakija na taarifa kuwa Edger
yuko hai na anashikiliwa na
serikali moto mkubwa
utawaka” akasema Devotha
“Devotha ninakushauri
endelea kulichunguza hili suala
hadi uufahamu ukweli
wake”akasema Mathew
“Mathew hakuna haja ya
kupoteza nguvu kufanya
uchunguzi wakati tayari ukweli
umekwisha bainika kuwa huu
ni mpango wa IS na lengo lao ni
kutaka kuleta machafuko nchini
na wao kupata mwanya wa
kupenya.Kitu kikubwa kwa sasa
ni kuhakikisha kuwa lengo lao
halifanikiwi na hakuna
machafuko
yatakayotokea”akasema
Devotha
“Devotha ninakushauri
uendelee kulichunguza hili
jambo kwa sababu kuna kitu
ninakiona ndani yake.Hebu
jiulize kuna nini kati ya IS na
Edger Kaka? Kwa nini Olivia
ajiunge na IS katika mpango
huu? Kwa nini IS waibuke sasa
na kudai Edger hajafa? Nini
wanakitafuta hapa nchini je ni
kuleta machafuko kama
unavyodai? Ni wazi kuwa
mashabiki wa Edger wakisikia
kuwa yuko hai na anashikiliwa
na serikali moto mkubwa
utawaka.Je lengo lao ni hilo?
Lakini tunapaswa kujiuliza vile
vile je ni kweli Edger yuko hai?
Kama kweli yuko hai yuko
wapi? Umeniambia kwamba
Olivia amemlenga Rais kuwa
anafahamu mahala alipo Edger
na ndiyo maana akatengeneza
virusi maalum na
kumuambukiza mtoto wake je
ni kweli Rais analifahamu
jambo hili? Hadi utakapoyapatia
majibu maswali hayo ndipo
utafikiria kuachana na suala hili
lakini kwa sasa ni suala
muhimu mno na linatakiwa
kuendelea kuchunguzwa hadi
majibu yake yapatikane”
akasema Mathew
“Mathew hili jambo kweli ni
kubwa kama ulivyosema na
limejaa maswali mengi magumu
kuyapatia
majibu.Nilipozungumza na
Olivia alinieleza kuwa anayo siri
kubwa na kama ninataka
kuifahamu basi nimpatie taarifa
alipo Edger Kaka” akasema
Devotha
“Unaamini anayo siri
hiyo?akauliza Mathew
“Kwa kumtazama machoni
utagundua Olivia anayo siri
kubwa”
“Kama unaamini Olivia
anayo siri kubwa na atakueleza
siri hiyo pale utakapofanikisha
kupata taarifa alipo Edger Kaka
basi endelea na uchunguzi hadi
uhakikishe umeupata ukweli
kama kweli yuko hai au
amekufa”akasema Mathew na
ukimya ukatawala.Mathew
akauvunja ukimya
“Devotha naamini ninyi
ndio mliomteka Agrey Themba
baba yake Olivia.Unaweza
ukaniambia sababu ya
kumteka?
“Mathew hayo ni mambo
ambayo hupaswi kuyafahamu
na ninaomba tafadhali
usiniulize chochote”
“Mlitaka kumtumia ili
kumfanya Olivia aongee kila
kitu,ninazifahamu mbinu
hizi.Mlifanikiwa?akauliza
Mathew
“Mathew shut up!! Akafoka
Devotha
“Devotha I can help
you.Ninaweza kumfungua Olivia
na kumfanya afunguke na
kueleza kila kitu.Tafadhali
kubali nikusaidie katika suala
hili.Kuniweka humu ndani
hakutasaidia chochote mimi
sina mahusiano yoyote na IS
kama
mlivyoaminishwa.Nisaidie
nitoke humu ndani na
ninakuahidi kuupata ukweli wa
suala hili.Nipe nafasi ya
kumuhoji Olivia na ataeleza kila
kitu”
“Mathew japo umejitahidi
sana kunishawishi kuwa
hauhusiki kwa namna yoyote na
Olivia lakini bado haiwezi
kunifanya
nikuamini.Nitaendelea na
uchunguzi wangu wa suala hili
na kuufahamu ukweli na kama
hauhusiki na mtandao wa
IS.Sikuahidi utaachiwa huru
kwa sababu umefanya mauaji
makubwa ya watu wetu kumi
na tatu,umekwisha zifahamu
siri zetu hivyo utaendelea kukaa
sana huku shimoni.Kwa taarifa
yako ni kwamba hapa ulipo ni
mita mia mbili chini ya ardhi
hivyo hautaweza kutoka
kamwe”akasema Devotha
“Devotha tafadhali naomba
uniamini.Ni makosa makubwa
mnayafanya kuniweka humu
ndani wakati nchi iko katika
hatari.IS wana mipango
mikubwa hapa nchini na mtu
kama mimi ninaweza kuwa na
msaada mkubwa kwa nyakati
kama hizi! Akasema Mathew
“Mathew nimekwisha
kueleza kuwa hakuna namna
utakayoweza kutoka
humu.Omba sana Mungu
akusaidie lakini kutoka humu
sahau” akasema Devotha
“Devotha !” akaita Mathew
“Mathew please !” akasema
Devotha kwa ukali
“Devotha hata kama maisha
yangu yataishia ndani ya shimo
hili lakini naomba nisaidie
katika jambo hili.Naomba
unisikilize japo kwa dakika
mbili” Akasema Mathew.
“Nini unataka kuniambia
Mathew? Akauliza Devotha
“Mchunguze Rais”
“Nimchunguze Rais?
“Ndiyo.Kama Olivia
ameelekeza jambo hili kwake
na kudai anafahamu kila kitu
kuhusu Edger basi sehemu ya
kuanzia uchunguzi ni kwa
Rais.Dukua simu yake na
fuatilia mawasiliano yake wiki
moja kabla ya Edger kupata
ajali na wiki moja baada ya
ajali.Angalia amewasiliana na
watu gani na utapata jibu kama
kweli anafahamu kuhusu jambo
hili”
“Mathew huo ni mtihani
mgumu sana.Kudukua simu ya
Rais si kitu kidogo”
“Nafahamu ni jambo zito
lakini ndiyo sehemu pekee ya
kuanzia uchunguzi wa hili
jambo.Kama ukigundua Rais
anafahamu jambo hili itakuwa
rahisi kwako kujua mahala
alipo Edger na kama hajui basi
utakuwa ni mwanzo mzuri pia
wa kutafuta ukweli kupitia
Olivia kwa nini wamemlenga
Rais”
“Mathew ahsante kwa
ushauri huo nitautafakari”
akasema Devotha
“One more thing” akasema
Mathew
“Jambo gani Mathew?
“Ninayo timu yangu ambao
ni watu wenye uwezo
mkubwa.Mmoja anaitwa Papii
Gosu gosu na mwingine anaitwa
Ruby.Hawa wanaweza
wakakusaidia mno katika
uchunguzi wako.Ukihitaji
msaada muda wowote watafute
hao kuanzia saa kumi na mbili
jioni ya leo utawata nyumbani
kwangu watakuwa wamewasili
kutoka nje ya
nchi.Nitakuelekeza nyumbani
kwangu na nitakupa pia namba
ya simu ya nyumbani kwangu
utapiga na kuzungumza nao”
akasema Mathew na kumpatia
Devotha namba za simu za
nyumbani kwake na Devotha
akainuka ili aondoke lakini
akakumbuka kitu
“Mathew ile programu
uliyompa Olivia iliufunga
mfumo wetu wa mawasiliano.Ili
kuufungua kunatakiwa namba
maalum.Hakuna tena ulazima
wa kuendelea kuushikilia
mfumo wetu wakati kila kitu
unakifahamu.Nipe namba za
kuufungua mfumo wetu”
akasema Devotha.Mathew
akampa namba za kuufungua
mfumo ule Devotha
akatabasamu na kuinuka
akaelekea mlangoni akabonyeza
kengele mlango ukafunguliwa
akamkuta Kaiza akiwa na
walinzi wakimsubiri.
“Mpelekeni Mathew
A3”Devotha akawaelekeza
walinzi na kumtaka Kaiza
waondoke
“Devotha why A3?akauliza
Kaiza lakini Devotha hakumjibu
kitu wakaelekea katika lifti
kupanda juu
“Kaiza ofisini kwangu
tafadhali” akasema Devotha
baada ya kushuka katika
lifti.Waliingia katika ofisi ya
Devotha akafunga mlango
“Kaiza nilikuonya awali
kuhoji maamuzi yangu.Kwa nini
kila nikifanya maamuzi yangu
unanihoji?Who is the boss
here?akauliza Devotha
“Wewe ndiye mkubwa
Devotha.Samahani nilistuka
kidogo ulipoelekeza Mathew
apelekwe A3 ambako ni sehemu
maalum kwa ajili ya viongozi.A3
ni sehemu ya starehe sehemu
iliyotengwa maalum kwa ajili ya
watu wakubwa kuhifadhiwa
pale wanapokuwa katika hatari
na mtu kama Mathew ambaye
anashirikiana na IS na ameua
watu wetu kumi na tatu
hakustahili kupewa heshima
hiyo ya kukaa sehemu ya
kustarehe kama yuko nyumbani
kwake.Samahani sana Devotha
kama nimekukwaza kwa
kuuliza lakini nadhani Mathew
hastahili kwenda A3” akasema
Kaiza
“Kaiza mimi ndiye mwenye
maamuzi ya mwisho hapa hivyo
sitaki wewe wala Rais au mtu
mwingine yeyote ahoji
maamuzi yangu,umenisikia?
“Nimekusikia Devotha”
“Good.This is the last
warning.Muite Leon haraka
sana” akasema Devotha na Leon
mtaalamu mkuu wa mifumo
yote ya mawasiliano akaitwa.
“Leon nimepata namba za
kuufungua mfumo wetu wa
zamani” akasema Devotha na
kumpatia namba zile akajaribu
kuifungua kompyuta ya
Devotha ikafunguka na wote
wakatabasamu
“Rudisheni mfumo wa
zamani na huu mpya
mnaoendelea kuushughulia
ukae kama akiba ila wekeni
kinga kubwa katika mfumo
mpya hata ule wa zamani ili
asitokee mtu akafanya kitu
kama hiki walichokifanya
Mathew na Olivia” akasema
Devotha
“Leon tazama pia kama
watu hawa watakuwa
wamepata taarifa zetu zozote”
akasema Kaiza wakati akitoka
na Leon ofisini kwa Devotha
“Mathew hana mahusiano
yoyote na IS.Maelezo aliyonipa
nimeyaamini.Hakumfahamu
Olivia kama ana mahusiano na
kikundi cha IS.Ninamfahamu
mtu anayesema ukweli na sina
mashaka Mathew anasema
kweli.Lengo lake lilikuwa ni
kumlinda Olivia na niliuona
mstuko alioupata baada ya
kusikia kuwa Olivia ana
mahusiano na IS.Hata hivyo
ataendelea kukaa hapa hadi
hapo mambo haya
yatakapokwisha kwani akitoka
atavuruga kila kitu katika
uchunguzi wa suala
hili.Nashukuru amenisaidia
kufahamu suala la Edger Kaka
limetoka kwa
IS.Kinachoniumiza akili yangu
hata kama ni mpango wa IS je ni
kweli Edger yuko hai? Kama
yuko hai yuko wapi? Kama you
hai kwa nini IS waliibue suala
hili?Watafaidika na nini kama
Edger akipatikana? Kwa nini
Rais Dr Evans awe ndiye
mlengwa mkuu katika suala
hili? Hawawezi kuibuka na
kumlenga Rais moja kwa moja
kama hakuna
anachokifahamu.Kuna siri
kubwa iko hapa kama
alivyosema Olivia ambayo
lazima niifahamu na kuipata siri
hiyo lazima kwanza nifahamu
mahala alipo Edger kama kweli
yuko hai” akawaza Devotha na
kuelekeza macho yake dirishani
“Mathew amenipa ushauri
mzuri kama nikitaka
kulichunguza suala hili nianzie
kwa kumchunguza Rais Dr
Evans.Natakiwa kudukua
mawasiliano yake na kujua
amekuwa anawasiliana na nani
hasa katika tarehe zile Edger
alipopata ajali.Nahitaji kumpata
mtu atakayenisaidia kudukua
mawasiliano ya Rais.Hili jambo
kubwa na la siri kwani kama
nikibainika maisha yangu
yatakuwa yameharibika na Rais
hatakuwa na msamaha na mimi
hata hivyo siwezi kuogopa
nitafanya uchunguzi na lazima
nidukue simu ya Rais.Nitahitaji
mtu ambaye ni msiri
atakayeifanya hii kazi” akawaza
Devotha na kuzama mawazoni
halafu akampigia simu Saada
Amiri.
“Madam Director” akasema
Saada baada ya kupokea simu
“Saada naomba uje ofisini
kwangu mara moja”akasema
Devotha.Baada ya dakika
chache Saada akafika
“Saada chukua kompyuta
yako na vifaa vyako vyote
tunaondoka” akasema Devotha
na Saada akaenda kuchukua
vifaa vyake akarejea katika ofisi
ya Devotha wakatoka.
“Tunakwenda wapi madam
Devotha?akauliza Saada
“Kuna kazi Fulani
tunakwenda kuifanya” akasema
Devotha.
“Niko tayari madam
Devotha”akasema Saada na
Devotha akaondoa gari
“Saada wewe ni mtu
ninayekuamini kuliko wote
katika idara yetu.Kuna kazi
ambayo nataka tuifanye lakini
ni kazi ngumu kidogo na
inahitaji ujasiri na usiri
mkubwa” akasema Devotha
“Madam usiwe na hofu na
mimi niko tayari kwa kazi
yoyote ile hata kama ni ya
hatari” akasema Saada
“Tunakwenda ikulu
kudukua simu ya Rais” akasema
Devotha na Saada akaonyesha
mstuko kidogo
“Kudukua simu ya Rais?
“Ndiyo nataka tudukue
simu ya Rais.Wewe ndiye
mdukuzi pekee ninayekuamini”
akasema Devotha
“Madam Devotha unaweza
ukanieleza kwa nini tudukue
simu ya Rais?
“Kuna taarifa Fulani za
muhimu sana ninazitafuta na
hakuna sehemu nyingine ya
kuzipata bali katika simu ya
Rais”
“Nimeingiwa na hofu
kidogo baada ya kusikia
kwamba natakiwa kudukua
simu ya Rais.Hili ni jambo la
hatari sana” akasema Saada
“Usiwe na hofu
Saada.Hautaingia katika hatari
yoyote.Katika jukumu letu la
kulinda usalama wa nchi kuna
nyakati tunajikuta tukilazimika
kufanya mambo ya hatari sana
kama haya lakini lengo ni
kuiweka nchi salama.Are you
ready?akauliza Devotha
“Yes madam I’m ready”
akasema Saada ingawa sura
yake ilionyesha wasi
wasi.Devotha akasimamisha
gari pembeni ya barabara
akashuka upande wa dereva
kumuachia Saada aendeshe
akatoa simu na kumpigia Dr
Evans
“Devotha mambo
yanakwendaje?akauliza Dr
Evans baada ya kupokea simu
“Mheshimiwa Rais
nimekupigia ninahitaji kukuona
kuna suala la dharura nataka
tulijadili” akasema Devotha.
“Devotha suala hilo
haliwezi kusubiri?
“Hapana mheshimiwa Rais
haliwezi kusubiri.Nahitaji
kukuona tuzungumze” akasema
Devotha
“Sawa Devotha njoo
ninakusubiri” akasema Dr
Evans na kukata simu
“Tunakwenda ikulu
kuonana na Rais.Tukifika
nitamtaka tukazungumze naye
katika chumba cha faragha na
wewe ukiwepo na tukiingia
ndani ya chumba hicho wakati
mimi nikizungumza naye wewe
utaendelea na zoezi
lakuunganisha simu yake na
programu ya kuidukua”
akasema Devotha
“Hilo halina tatizo madam
Devotha,progamu ninayotaka
kuitumia kujiunganisha na simu
ya Rais ni ile ya kujiunganisha
na simu ukiwa naye karibu bila
yeye kujua.Haihitaji kuipata
simu yake na
kuingizaprogramu.Swali langu
ni vipi kama Rais hatakuwa na
simu yake wakati ukizungumza
naye?Nivipi kama atakuwa
ameiacha simu yake ofisini au
iko kwa mlinzi wake?akauliza
Saada
“Nimekuwa na ukaribu na
Rais nimekwisha msoma
vyema.Simu yake hupenda
kuiweka katika mfuko wa ndani
wa koti.Hana kawaida ya
kuacha simu yake ofisini au
kumpa mlinzi wake hivyo nina
uhakika mkubwa kwamba hata
tutakapokuwa tunazungumza
naye atakuwa na simu yake”
akasema Devotha
“Madam nitakuomba
tukiingia ndani ya hicho
chumba nawe uzime simu yako
ili niwe na kazi ya kuitafuta
simu moja tu ya Rais”
“Usihofu kuhusu hilo
Saada” akasema Devotha na
Saada akaongeza mwendo wa
gari
“Mpaka sasa sijapata jibu
kwa nini IS waje na mpango
huu wa kudai Edger hajafariki
dunia.Nini hasa wanakilenga
katika mpango wao huu?Ni
kuleta machafuko?Kuichafua
serikali?Nini hasa
wanakitafuta? Akajiuliza
Devotha
“Baada ya kuidukua simu
ya Dr Evans nitaupata ukweli
kama kweli anahusika na jambo
hili au hahusiki.Yeye ndiye
mlengwa namba moja ambaye
wanatumia nguvu
kumlazimisha aonyeshe mahala
alipo Edger.Kama atakuwa
anafahamu chochote kuhusu
suala hili tutafahamu kupitia
mawasiliano yake yake na
nitampa taarifa hizo Olivia ili
anipe siri aliyonayo anayodai ni
kubwa.” akaendelea kuwaza
Devotha
Waliwasili ikulu kwa ajili ya
kuonana na Rais
“Saada we’re here.Get
ready” Devotha akamweleza
Saada walipowasili ikulu
“Wow ! ni pazuri mno.Ni
mara yangu ya kwanza kufika
mahala hapa” akasema Saada
huku akitabasamu
Rais DrEvans alikuwa na
ratiba iliyombana sana siku hii
alikuwa na wageni wengi
aliohitaji kuonana nao na
kazinyingine mbalimbali hivyo
bila kupoteza muda baada ya
akina Devotha kuwasili
wakaelekea moja kwa moja
katikachumba cha mazungumzo
ya faragha
“Devotha mtanisamehe leo
nina muda mfupi sana ratiba
yangu imenibana mno hivyo
naomba twende moja kwa moja
katika kitu kile cha msingi
unachotaka kunieleza” akasema
Dr Evans
“Samahani pia mheshimiwa
Rais kwa ujio huu wa dharura
lakini hatutachukua muda
mrefu” akasema Devotha
“Devotha mambo mengine
si lazima uje kuonana nami
tunaweza kuzungumza kwenye
simu hakuna tatizo lolote.Siyo
kila wakati lazima
tuonane.Halafu watu wanaweza
kuanza kuhisi kuna nini kati
yetu.Idara yako ni ya siri sana
tusiwape watu nafasi ya kuhoji
mambo hadi wakaifahamu.Nini
hasa kikubwa Devotha?akauliza
Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
nilisahau kukutambulisha.Huyu
anaitwa Saada Amir ni mmoja
wa watu wangu ninaowaamini
sana.Ni mara ya kwanza anafika
hapa” akasema Devotha
“Saada karibu
sana”akasema rais
“Ahsante sana mheshimiwa
Rais” akajibu Saada.Akafungua
mkoba wake na kutoa
kompyuta akaiweka mapajani
na kufungua programu ambayo
ilianza kuitafuta simu ya Rais
bila yeye kufahamu.
“Mheshimiwa Rais
kilichonileta hapa nilitaka
tujadiliane kuhusu
AgreyThemba”
“Kuna nini kuhusu Agrey?
Akauliza Dr Evans
“Tulimchukua Agrey kwa
lengo la kusaidia kumfungua
Olivia lakini mpango wetu
unaonekana kushindwa
kufanikiwa.Olivia amegoma
kabisa kufunguka hata baada ya
baba yake kupigwa risasi”
“Unataka
kusemaniniDevotha?
“Nimekuja tujadiliane
hatima ya Agrey
Themba.Binafsi sioni sababu ya
kuendelea kumshikilia na kuzua
taharuki katika jamii” akasema
Devotha
Katika kompyuta ya Saada
ulisikika mlio na ujumbe
ukajitokeza
“New device found”
Kwa wepesi wa aina yake
Saada akaendelea kucheza na
kompyuta yakehalafu akakohoa
kidogo.Devotha akaitambua
ishara ile kuwa tayari zoezi la
kuiunganisha simu ya Rais
lilikamilika.
“Saada tafadhali unaweza
ukamsubiri mkuu wako hapo
nje nataka kuzungumza naye
kwa dakika chache” akasema
DrEvans na Saada akainuka
akaiweka kompyuta yake katika
mkoba akatoka nje.
“Devotha kamwe
usithubutu kuwaza suala la
kumuachia Agrey
Themba.Utakuwa umefanya
kosa kubwa sana kwani
mipango yetu yote
itaharibika.Ataeleza kila kitu
kilichomtokea.Nilikwisha
kueleza kuwa huu ni mwisho
wa Agrey Themba kwani pale
tutakapokuwa hatuna matumizi
naye tutamuua kwa sababu
lazima atafahamu kuwa mimi
niko nyuma ya jambo hili nahii
inaweza kuleta mtafaruku
mkubwa mno hivyo Agrey
tayari ni mfu.Nadhani
umenielewa Devotha” akasema
Dr Evans
“Sawa nimekuelewa Dr
Evans”
“Devotha,mwanangu yuko
hospitali hali yake hairidhishi
hata kidogo ingawa madaktari
wako katika harakati za
kutafuta tiba kutokana na virusi
alivyoambukizwa na Olivia.Nina
hasira sana na Olivia kwa ukatili
mkubwa aliomfanyia
mwanangu.Coletha hana kosa
lolote alilolifanya kwa Olivia
kumtendea hivi.Hicho
anachokisema kuhusu Edger
Kaka ni kitu kigeni kabisa
kwangu na sifahamu
chochote.Alitakiwa anifuate
mimi mwenyewe aniulize
kuhusu jambo hilo kuliko
kuanza kutesa familia yangu
bila kosa.Nataka umfungue
Olivia,nataka aeleze sababu za
kwa nini wametunga uongo huu
mkubwa na kuuelekeza kwangu
akidai kuwa ninafahamau alipo
Edger Kaka.Kama hatakuwa
tayari kufunguka nitaiteketeza
familia yake yote pamoja na
yeye mwenyewe.Sina mzaha
katika hili !! akasema DrEvans
na sekunde kadhaa zikapita za
ukimya
“Devotha nataka
nikikupigia simu jioni ya leo
uwe tayari na taarifa kutoka
kwa Olivia.Umenielewa
Devotha?
“Nimekuelewa mheshimiwa
Rais” akasema Devotha
“Good.Vipi kuhusu
Mathew?Tayari mmeshaanza
kumuhoji?
“Kwa sasa tumeanza
kumtesa kihisia ili kutengeneza
mazingira ya woga.Baadae
tutaanza kumuhoji”
“Vizuri.Hakikisha kila kitu
kinakwenda kama
nilivyokuelekeza
Devotha.Nataka kabla ya siku ya
leo kuisha tuwe tumepata
majibu yote.Kuna lingine
unataka kunieleza? akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais
lililonileta ni hilo tu la Agrey
Themba.Samahani kwa
kukupotezea muda sikutaka
kulizungumza jambo kama hili
simuni.Nitafuata maelekezo
yako”
“Good.Jitahidi kila pale
unapokuwa na tatizo kunipigia
simu kama nitaona kuna
ulazima wa kuonana
nitakujulisha lakini si kila
wakati lazima tuonane”
akasema Dr Evans na kuinuka
wakatoka ndani ya kile chumba
na kumkuta saada akiwa nje
akisubiri.DrEvans akaagana nao
wakaondoka
“Saada natakakujua kama
mpango wetu ulifanikiwa”
akauliza Devotha wakielekea
katika gari
“Kila kitu tayari madam
Devotha.Nilikupa ishara
naamini uliielewa”
“Niliewa ishara
uliyonipa.Nilitaka tu
kujiridhisha kuwa kila kitu
kimekwenda vizuri” akasema
Devotha wakaingia garini na
kuondoka.
“Saada thank you so much
for doing this.Nimesababisha
ukafanya jambo la hatari kubwa
lakini ni kwa ajili ya usalama wa
nchi”
“Usijali madam Devotha.Hii
ni kazi yangu na sijutii
kuifanya” akasema Saada
Kutoka ikulu walielekea
moja kwa moja nyumbani kwa
Devotha
“Madam nyumba yako ni
nzuri sana sikujua kama unaishi
sehemu nzuri kama hii”
akasema Saada
akitabasamu.Devotha
akampeleka katika chumba
chake cha ofisi
“Hii ni ofisi yangu ndogo ya
nyumbani.Utafanyia kazi zako
hapa” akasema Devotha
“Niko tayari kwa kazi
madam.Nielekeze nini hasa
unachokitaka” akasema Saada
akiendelea kubonyeza
kompyuta yake
harakaharaka.Devotha akaingia
mtandaoni kutafuta tarehe
aliyofariki Edger
kaka.Akaandika kijikaratasi na
kumpatia Saada.
“Nataka kujua mawasiliano
ya Rais katika tarehe hizo”
akasema Devotha na Saada
akaanza kazi.Devotha
akamuacha saada akiendelea na
kazi akaenda chumbani kwake
“Dr Evans amedhamiria
kabisa kumuua Agrey
Themba.Hanakosa lolote yule
mzee.Ninawaza namna ya
kumsaidia ili kuokoa maisha
yake.Ngoja kwanza niachane na
mawazo hayo kwa sasa
nijielekeze katika jambo moja tu
kuutafuta ukweli kuhusu Edger
kaka.Leo lazima ukweli
ujulikane kama Edger yuko hai
kama anavyodai Olivia na kama
Rais analifahamu jambo hili”
akawaza na kwenda kusimama
dirishani akatazama nje
“Kitu gani IS wanapanga
kukifanya hapa nchini hadi waje
na mpango kamahuu wa kudai
Edger yuko hai? Kwa nini Edger
Kaka?Wana maslahi gani na
jambo hili?akajiuliza
“Naamini hawawezi
wakapanga jambo kama hili
liwe la kweli au si kweli kama
halina maslahi makubwa
kwao.Nitahakikisha
ninalichunguza jambo hili hadi
niufahamu ukweli wake na
sehemu pekee ya kuanzia ni
kwa kufahamu kama kweli
Edger yuko hai” akawaza
Devotha
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 4
Rais Dr Evans akiwa katika
mazungumzo na wageni
waliofika kumtembelea
akaingia mmoja wa walinzi
wake akamnong’oneza kitu
sikioni.DrEvans akawaomba
radhi wageni wale na
kuwaahidi atawakaribisha siku
nyingine kwa mazungumzo
kuna suala la dharura anahitaji
kulishughulikia.Akaagana nao
wakaondoka
“Nini kimetokea Richard?
Umenistua sana”akauliza
DrEvans
“Kuna kitu kimetokea
mheshimiwa Rais.Naomba
tukazungumze katika chumba
cha siri” akasema Richard na
kumuongoza Rais hadi
katikachumba cha mazungumzo
ya siri ambamo kulikuwa na
watuwawili
“Isaack,Bakari kuna nini
kimetokea?akauliza DrEvans
kwa wasiwasi
“Samahani mheshimiwa
Raiskuna jambo limetokea
tukaona ni vyema ukalifahamu
kwa haraka”akasema Isaack
“Nini kimetokea? Akauliza
DrEvans na mlinzi wake
akamvutia kiti akaketi
“Mheshimiwa Rais simu
yako imeunganishwa na mfumo
maalum ili kuzuia isiingiliwe na
wadukuzi hivyo kuifanya iwe
salama muda wote.Mfumo huo
unaweza kutambua haraka sana
kama kuna mtu anajaribu
kutaka kudukua simu yako,au
ya makamu wa Rais na waziri
mkuu na kutujulisha na sisi
huchukua haua za haraka
kudhibiti jaribio hilo”
akanyamaza kidogo akabonyeza
kompyuta yakena kuendelea
“Muda mfupi uliopita
tumegundua kuna mtu
amefanikiwa kuvuka ukuta
uliowekwa na kuingia katika
simu yako na amekuwa
anafuatilia mawasiliano yako”
Dr Evans akavuta pumzi
ndefu
“Amedukua simu
yangu?Mmefanikiwa
kumtambua mtu huyo ni
nani?Tayari mmemdhibiti?
“Mheshimiwa Rais baada ya
kufuatilia tumegundua mtu
huyo anayedukua simu yako
anafanya kazi zake kutoka
katika nyumba hii ambayo
tumeifuatilia mmiliki wake
anaitwa Devotha Adolph”
Dr Evans alihisi kama kitu
kizito kimegonga kichwa chake
“Umesema Devotha
Adolph?
“Ndiyo mheshimiwa Rais”
“My God!! Akasema Dr
Evans akalegeza tai yake
“Mnaweza kumzuia huyo
mtu asiendelee na kile
anachokifanya?akauliza Dr
Evans
“Ndiyo tunaweza
mheshimiwa Rais lakini
tunahitajikuwa na simu yako
ndiyo maana tumekuita hapa ili
utukabidhi simu yako tuifanyie
kazi” akasema Isaack na kwa
haraka Dr Evans akaitoa simu
yake mfukoni akampatia
“Simu hii hapa.Hakikisha
unamzuia haraka sana mtu
huyo asiendelee kufanya hicho
anachokifanya.Lakini
amewezaje kuvuka ukuta
mliouweka hadi akaingia katika
simu yangu?
“Mheshimiwa Rais huyu
mtu aliyefanya jambo hili
anaonekana ni mdukuzi
mwenye ujuziwa juu sana ndiyo
maana akaweza kuuvuka ukuta
tulioweka na akaingia katika
simu yako”
“Stop them now!! Akasema
Dr Evans hukuakihema haraka
haraka.Isaack na Bakari
wakaanza harakakufanya kazi
ya kuwadhibiti wadukuaji
“Mheshimiwa Rais kuna
maelekezo yoyote unayatoa
kuhusiana na hawa watu
waliojaribu kudukua simu
yako?akauliza Richard
“Nothing for now” akasema
Dr Evan akiwatazama Isaack na
Bakari wakiendelea na zoezi lao
la kuwadhibiti wadukuzi.Zilipita
dakika kadhaa Isaack akasema
“Tayari mheshimiwa
Rais.Tumekwisha wadhibiti
wadukuaji lakini inabidi
tuangalie kwa kina zaidi namna
huyu mdukuaji alivyoweza
kuvuka ukuta uliowekwa na
kuweza kudukuasimu
yako.Tutauangalia mfumo huu
kwa kina zaidi ili tujue wapi
kuna mwanya na kuuimarisha
zaidi na kama tukiona inafaa
tutabadili na kuweka mfumo
mwingine” akasema isaack
“Unaweza kujua kitu gani
hasa walichokuwa
wanakichunguza katika simu
yangu?akauliza Dr Evans
“Tunakwenda kulifanyia
kazi hilo kujua nini hasa
walichokifanya katika katika
simu yako” akasema Isaack
“Isaack ninawashukuru
sana kwa kazi hii kubwa
mliyoifanya.Tafadhali endeleeni
kuwadhibiti watu hawa na wale
wote wanaodiriki kutaka
kufanya kitendo hiki cha
kudukua simu yangu na
vyombo vya mawasiliano vya
viongozi wengine” akasema Dr
Evans
“Tutafanya hivyo
mheshimiwa
Rais.Tutahakikisha hakuna mtu
atakayeweza kufanya hivi
tena.Hawa watuwaliofanya hivi
tunafahamu mahala walipo
kama ungependa wafuatiliwe
na kutiwa nguvuni”akasema
Isaack
“Kwa sasa endeleeni
kulifanyia uchunguzi suala hili
kujua namna walivyoweza
kudukua simu yangu na kama
wamepata msaada wowote
kutoka kwa mtu aliye katika
ofisi yenu.Hayo masuala
mengine niachie nitayafanyia
kazi” akasema Dr Isaack na
kutoka akaeleka ofisini
kwake.Mara tu alipoingia ofisini
akampigia simu Kaiza
“Mheshimiwa Rais”
akasema Kaiza baada ya
kupokea simu
“Kaiza nataka kufahamu
mahala ulipo sasa hivi?
“Kwa sasa niko hapa kitalu
1.Nilisimamia zoezi la
kumkamata Mathew Mulumbi
tukalifanikisha na sasa
tunasubiri maelekezo ya
Devotha”
“Devotha yuko wapi?
“Alitoka hapa hajamueleza
mtu yeyote anaelekea wapi”
“Unadhani amekwenda
nyumbani kwake?
“Sina hakika kama
amekwenda nyumbani kwake
ngoja nijaribu kumtafuta
nifahamu mahala alipo”
“Hapana usifanye
hivyo.Kaiza nataka kufahamu
nini kinachoendelea hapo sasa
hivi?Nieleze ukweli”
“Kinachoendelea kwa sasa
mheshimiwa Rais ni kuwahoji
hawa watu tunaowashikilia”
“Unaweza ukaniambia kwa
nini mpaka sasa Olivia hajaweza
kufunguka?Mmeshindwa
kumfungua ili nitafute watu
wanaoweza kuifanya kazi
hiyo?Nieleze ukweli Kaiza bila
kunificha kuna tatizo
gani?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
hatujashindwa kumfungua
Olivialakini kuna mambo
yanaendelea hapa ambayo
binafsi yananishangaza”
“Nieleze Kaiza ni mambo
gani hayo?Kuwa muwazi
kwangu”
“Mheshimiwa Rais ni
kuhusu mkurugenzi wetu
Devotha.Kuna mambo
amekuwa anayafanya ambayo
binafsi siyaafiki.Leo asubuhi
alifika hapa na akanieleza kuwa
ametoka kuonana na Olivia
akasema kwamba anataka
kulifanyia uchunguzi jambo
aliloambiwa na Olivia
kuhusiana na Edger
Kaka.Anataka kufanya
uchunguzi kujua kama kweli
Edger yuko hai.Nilimzuia
asifanye hivyolakini alinionya
kuwa yeye ndiye mkubwa hapa
na sipaswi kumuingilia katika
maamuzi yake.Baada ya hapo
akataka kuzungumza na
Mathew Mulumbi lakini bila
kamera wala sauti.Tulizima kila
kitu akaenda kuzungumza naye
na alipomaliza kuzungumza
naye akaondoka bila kutuaga
anaelekea wapi.Mheshimwia
Rais mtu kama Mathew ambaye
jana ameua watu wetu kumi na
tatu alistahili mateso makali
lakini imekuwa tofauti,Devotha
ameelekeza Mathew apelekwe
chumba A3 ambako ni sehemu
maalum kwa ajili ya viongozi
wakuu pale wanapokuwa katika
hatari.Nimehojikuhusu Mathew
kupewa hadhi hiyo lakini bado
jibu nililopewa
sikulifurahia.Mheshimiwa Rais
nina uhakika mkubwa kwamba
bado hatujashindwa
kuwafungua Mathew wala
Olivia lakini kwa namna
Devotha anavyoendesha
mambo katu hatutaweza kupata
chochote toka kwao” akasema
Kaiza
“Kaiza ninashukuru sana
kwa kuwa muwazi kwangu.Sasa
naomba unisikilize kwa makini
haya maagizoninayokupa
ambayo nataka yatekelezwe
haraka sana” akasema Dr Evans
“Nakusikiliza mheshimiwa
Rais” akasema Kaiza
“Nataka uende ukamtoe
Olivia kitalu 2 na umpeleke
mahala nitakapokuelekeza ili
akahojiwe huko.Sitaki Devotha
afahamu chochote kuhusu
jambo hili.Ninataka ufanye kila
linalowezekana kuhakikisha
kabla ya jua kuzama leo Olivia
awe amefunguka kila kitu
kuhusu yeye na IS”
“Sawa mheshimiwa Rais
nitafanya kama ulivyoelekeza”
“Unaniahidi kwamba
utafanya kama
nilivyoeleza?Utamfungua
Olivia?
“Mheshimiwa Rais
nakuahidi nitafanya kila
linalowezekana kuhakikisha
Olivia anafunguka”
“Good.Ondoka hapo ulipo
kimya kimya bila kumueleza
mtu yeyote na nitakuelekeza
sehemu ya kumpeleka
Olivia.Jambo lingine kuanzia
sasa Devotha hatakuwa
kiongozi tena badala yake wewe
ndiye utakayeongoza idara
hiyo.Nataka Devotha afungiwe
kilakitu kuanzia simu na
aondolewe katika mtandao
asiweze kupata chochote.Kila
kitu kibadilishwe haraka sana
na mwisho nataka Devotha
akamatwe” akasema Dr Evans
na kukata simu
“Siamini Devotha ameamua
kumuamini Olivia kuhusu suala
la Edger Kaka na ameamua
kufanyauchunguzi kubaini
kama kweli ninafahamu mahala
alipo Edger.Kwa nini
ameshindwa kuniamini
nilipomwambia kwamba
hichoanachokisema Olivia ni
uongo mkubwa na
mimisifahamu
chochote?Ninamuamini sana
Devothana kumtegemea sana
katika mambo mengilakini
nimesikitishwa na kitendo
chake cha kushindwa kuniamini
na badala yake ameanza
kunichunguza.Sina hakika kama
ninaweza kuendelea
kumuamini kwa hili
alilolifanya.Siwezi kufanyakazi
na mtu ambaye
haniamini.Amekosea sana
kufanya hiki alichokifanya”
akawaza Dr Evans
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 5
Saada alitoka ndani ya ofisi
kwa kasi akatazama huku na
huko akimtafuta Devotha
“Madam Devotha !!
akaitakwa nguvu.Alionekana
kuchanganyikiwa
“Madam Devotha ! akaita
tena mara akatokea mtumishi
wa ndani
“Madam Devotha yuko
chumbani kwake
anapumzika”akasema yule
mtumishi
“Naomba umuite
tafadhali.Mwambie namuhitaji
haraka sana” akasema Saada na
kurejea katika ofisi ya
Devotha.Baada ya dakika tatu
Devotha akafika akamkuta
saada akiwa katika hali ya
kuchanganyikiwa
“Saada kuna nini?akauliza
“Madam Devotha !!
akasema Saada
akihangaikakubonyeza
kompyuta yake
“Saada nieleze tafadhali
nini kimetokea?
“Madam tayari
tumejulikana”
“Kivipi?akauliza Devotha
“Wamekata mawasiliano
kati yangu na simu ya
Rais.Nimejaribu kuunganisha
tena lakini haiwezekani tena
kuna ukuta mzito.Madam zoezi
limeishia hapa nashauri
tusiendelee tena,tumejiweka
katika hatari kubwa” akasema
Saada.
“Relax saada.Usiwe na
hofu.Let me handle this”
“Madam Devotha hadi
kufikia hatua ya kukata
mawasiliano kati yangu na simu
ya Rais tayari wanafahamu niko
wapi hivyo yawezekana muda
huu wako njiani wakinifuata
hapa.Madam ….”
“Usihofu Devotha
nilikuahidi kuwa sintakuingiza
katika hatari yoyote.Funga kila
kitu chako tunaondoka”
akasema Devotha na kwenda
chumbani kwake akachukua
funguo ya gari akarejea mle
ofisini
“Kabla hawajakubaini na
kukata mawasiliano tayari
ulikuwa umepata taarifa zozote
kuhusiana na ile kazi
niliyokupatia?akauliza Devotha
“Sikuwa nimefanikiwa bado
kupata namba zile nilikuwa
naendelea na maandalizi.I’m
sorry madam I failed
you”akasema Saada
“Usiwe na hofu Saada.Hata
hivyo tumejaribu” akasema
Devotha wakatoka na kuelekea
garini
“Nimemuweka Saada katika
hatari hata hivyo sikuwa na
namna nyingine ya kufanya
zaidi ya kudukua simu ya Dr
Evans kuutafuta ukweli.Japo
hatujafanikiwa kupata kile
nilichokikusudia lakini
nimejaribu na sasa natakiwa
kumtafutia Saada sehemu
salama ya kujificha kwa muda
wakati nikiweka mambo
sawa.Sehemu pekee ambako
naamini haitakuwa rahisi
kwake kujulikana ni nyumbani
kwa Mathew Mulumbi ambako
ni sehemu ya mwisho kabisa
ambayo mtu yeyote anaweza
akafikiria kwenda kumtafuta
Saada.Atakaa pale kwa muda na
hadi kufikia jioni ya leo
nitakuwa nimepata namna
nzuri zaidi ya kumsaidia Saada”
akawaza Devotha
Alifuata maelekezo
aliyopewa na Mathew akafika
katika geti la nyumba yake
akajitambulisha kwa mlinzi
kwamba ni rafiki wa Mathew
Mulumbi na amewaelekeza
wafike pale wakaruhusiwa
kuingia ndani wakapokewa na
mtumishi wa ndani wa Mathew
aitwaye Theresa
“Sisi ni marafiki zake
Mathew,ametuelekeza tufike
hapa kumsubiri”akajieleza
Devotha
“Karibuni sana.Na ninyi pia
mnatoka nje ya nchi?akauliza
Theresa
“Hapana sisi hatutoki nje ya
nchi.Wanaotoka nje ya nchi ni
wengine” akasema Devotha
wakakaribishwa sebuleni
wakahudumiwa vinywaji
“Saada hapa ulipo ni
sehemu salama na hakuna
yeyote atakayejua kama uko
hapa.Kitu muhimu cha kufanya
zima kabisa vifaa vyako vyote
vya mawasiliano na usiwashe
hadi pale nitakapokujulisha
kupitia simu ya humu
ndani.Usijaribu kuwasiliana na
mtu yeyote yule.Nataka
nikaliweke sawa suala hili na
hadi kufikia jioni ya leo kila kitu
kitakuwa sawa.Umenielewa
Saada?akauliza Devotha
“Nimekuelewa madam
Devotha” akasema Saada
“Good.Mimi ninakwenda
nitafika tena baadae
kukuchukua” akasema Devotha
na kumtaka Theresa
amuandalie Saada chumba cha
kupumzika
“Mtu ninayetakiwa
kuonana naye kwa sasa ni
Olivia.Natakiwa kuzungumza
naye kumueleza kuwa
nimeshindwa kupata uhakika
kama Dr Evans analifahamu
suala la Edger kaka kupitia simu
yake na nitamtaka kama ana
namna nyingine ya kunisaidia
kuthibitisha kuwa Dr Evans
analifahamu suala hili anipatie
ili niweze kumsaidia kumtafuta
Edger” akawaza Devotha na
kuchukua simu akampigia Kaiza
lakini simu yake haikuwa
ikipatikana akaendelea na safari
yake.
Alifika kitalu 2
akafunguliwa geti akaingia
ndani mara tu aliposhuka garini
akamuelekeza mlinzi kumleta
Olivia ofisini kwake akaelezwa
kuwa Kaiza akiwa na wenzake
kwenye magari matatu walifika
pale na kumchukua Olivia
wakaondoka naye bila kueleza
wanaelekea wapi.Taarifa ile
ilimstua sana Devotha akataka
akahakiki kama kweli Olivia
hayupo ndani ya chumba chake
akaamuru mlango ufunguliwe
ili ahakiki kama alichoelezwa ni
kitu cha kweli.Chumba kilikuwa
kitupu.Akachukua simu ili
kumpigia Kaiza lakini akasikia
ujumbe uliomstua kuwa simu
yake ilikuwa imezuiwa kwa
muda
“What’s going on? Kwa nini
simu yangu imezuiliwa?Kwa
nini Olivia akaondolewa bila
mimi kujulishwa?akajiuliza
Devotha.Akazitafuta namba za
Rais akajaribu kupiga lakini jibu
likawa lile lile kuwa simu yake
imezuiliwa.Akatoka kwa haraka
ndani ya kile chumba akaelekea
katika ofisi yake akafungua
kompyuta yake akajaribu
kuingia katika mtandao wa
idara yao lakini namba za siri za
kuingilia katika mfumo zilikuwa
zimebadilika.
“Damn !! akasema na
kupiga meza kwa hasira.Akiwa
ameinamisha kichwa akiwaza
mara mlango wake ukagongwa
wakatokea watu watatu ambao
ni makachero wa idara yake.
“Karibuni” akasema
Devotha na kuwakaribisha watu
wale ofisini kwake.
“Mnasemaje James?akauliza
Devotha huku akipanga mafaili
yake
“Madam Devotha please
come with us”akasema James
“Come with you
where?akauliza Devotha
“Please madam we have
orders to take you” akasema
James.
“Take me where?Nani
kawatuma kwangu?akauliza
Devotha
“Tafadhali madam naomba
uongozane nasi” akaendelea
kusisitiza James
“What if I say no?! akauliza
Devotha
“Madam please usilifanye
jambo hili likawa gumu”
akasema James.Olivia akaushika
mkoba wake na kutaka kuuinua
wale jamaa wote kwa kasi
kubwa wakingiza mikono
katika makoti yao na kutoa
bastora
“Usiguse kitu chochote!!
Devotha akaamriwa
“Easy ! easy gentlemen !!
akasema Devotha
“Kama mmetumwa kuja
kunichukua hakuna haja ya
kutumia nguvu.Siku zote
nimekuwa kiongozi wenu nyote
mnanifahamu vyema.Twendeni
kwa amani huko mlikotumwa
mnipeleke” akasema Devotha
“Come over here slowly
with your hands up !! akasema
James kwa sauti kali.Devotha
akainua mikono juu.Ghafla
Devotha akafanya kitu ambacho
hakuna
aliyekitegemea.Alibonyea chini
ya meza akateleza kwa kasi
kubwa na kumvaa James
akamkata mtama.Kilikuwa ni
kitendo cha ghafla sana
ambacho hawakuwa
wamekitarajia.James alianguka
chini kama furushi kwa kuwa
hakuwa ametegemea kitu kile
kutokea.Wakati wenzake
wakijiuliza kilichotokea
akamtandika James teke kali
katika korodani akatoa mlio
wa maumivu makali akaachia
bastora aliyokuwa ameishika na
kupeleka mikono yake yote
mahala alikopigwa teke.Tayari
Devotha alikwisha waona wale
jamaa namna walivyokaa mle
ndani akachukua chupa moja
kubwa iliyokuwa pembeni na
kumrushia mmoja wao ambaye
aliinama ili kuikwepa na
Devotha akaitumia nafasi hiyo
akageuza jicho lake kama
kinyonga na kumuona jamaa
mwingine akimuelekezea
bastora akajigeuza kama kima
na kumtandika mateke mawili
haraka haraka,alimpiga teke la
mkono bastora ikamponyoka
kisha akamtandika teke kali la
kifua lililompeleka ukutani
kabla hajakaa sawa akamkata
mtama akaanguka chini na
kichwa chake kikagonga meza
akainyakua bastora ya yule
jamaa na kumuelekezea yule
aliyemkosa na chupa
“Weka chini bastora yako
haraka sana!! Akaamuru
Devotha Yule jamaa
akaonekana anasita.Bila ajizi
Devotha akachia risasi mbili
zikapita pembeni ya uso
wake.Jamaa alitetemeka
mikono na bila ubishi akaiweka
chini bastora yake na kuipiga
teke kumuendea Devotha.
“Chukua ule waya wafunge
wenzako!! Akaamuru Devotha
yule jamaa akachukua waya wa
umeme na kuwafunga wenzake
mikono kwa nyuma pamoja na
miguu halafu akamuelekeza
ageukie ukutani na ainue
mikono yake juu.Akafuata
maelekezo aliyopewa na
Devotha akamfunga mikono
kwa waya.
“Nani kawatuma
kwangu?akauliza Devotha lakini
hakujibiwa.Akafungua mkoba
wake na kutoa bastora yenye
kiwambo cha sauti na kumpiga
James risasi katika mguu wake
“Nani kawatuma
kwangu?akauliza Devotha
“Kaiza !! tumepewa
maelekezo na Kaiza !! akalalama
James
“Damn you Kaiza!! Akasema
Devotha akiuma meno kwa
hasira akachukua mkoba wake
akaweka baadhi ya vitu vyake
muhimu akatoka mle
ofisini.Alipotoka nje akawakuta
walinzi watatu
“Na ninyi pia mmetumwa
kwangu?akauliza Devotha
aliyejawa hasira
“Tumesikia mlio wa risasi
tukajiuliza nini kimetokea
humo ndani”akajibu mmoja
wao
“Kaiza akifika hapa
mwambieni ujumbe wake
nimeupata” akasema Devotha
akipiga hatua kuelekea katika
gari lake akaingia na kuondoka.
“Wameniwekea vizingiti
kila mahali.Nahisi tayari Dr
Evans ametambua kuwa ni
mimi niliyekuwa nadukua
mawasiliano yake na akatoa
maelekezo nikamatwe pamoja
na kuondolewa kabisa katika
mifumo yote.Yawezekana vile
vile amepewa taarifa na Kaiza
kuwa ninamfanyia uchunguzi
kwani ni yeye pekee
niliyemueleza jambo hilo.Kaiza
hakukubaliana nami na nina
hakika ni yeye aliyemueleza
Rais kuwa
ninamchunguza.Naanza kuhisi
maelekezo haya ya kufungiwa
simu na mtandao pia yametoka
kwa rais na yawezekana ni
kweli anahusika katika suala
hili la Edger na ndiyo maana
hataki nichunguze jambo
hili.Sasa nimeanza kumuamini
Olivia kuna siri kubwa ambayo
siifahamu.Kikubwa
ninachopaswa kukifanya kwa
sasa ni kuwatafuta Olivia na
baba yake kujua wamepelekwa
wapi” akawaza Devotha
“Hili jambo tayari limekuwa
kubwa.Nahitaji mtu wa
kunisaidia siwezi kupambana
peke yangu.Mtu pekee ambaye
ninamuamini kwa sasa ni Saada
lakini yeye ni mtaalamu wa
kompyuta na hafahamu
chochote kinachohusiana na
mapambano,nahitaji mtu
ambaye anaweza kupambana”
akawaza na kukumbuka kitu
“Mathew aliniambia anao
watu wake ambao anawaamini
na wanaweza
wakanisaidia.Alisema watu hao
wanatokea nje ya nchi.Nadhani
itakuwa vyema nikiwatumia
watu hao wa Mathew katika
kumtafuta Olivia” akaendelea
kuwaza Devotha na kuingiwa na
hofu
“Hili ni wazo zuri la
kuwatumia hao watu wa
Mathew lakini nitalazimika
kuwaeleza ukweli wote kuhusu
Mathew.Naamini watanielewa
na watakubali kushirikiana
nami.Lakini kuna wazo
nimelipata kwa nini
nisisaidiane na hao jamaa
kumuokoa Mathew?
Nimemuhoji mimi mwenyewe
na haonekani kuwa na
muunganiko wowote na
kikundi cha IS.Lengo lake kuu
lilikuwa kumlinda Olivia na
hakuwa akifahamu kama Olivia
ana mahusiano na IS.Hili ni
wazo zuri.Kama nikifanikiwa
kumpata Mathew naamini
kabisa tukiungana tunaweza
tukaupata ukweli wa jambo
hili.Ngoja nikakutane na hao
jamaa zake nizungumze nao na
tuanze haraka mikakati ya
kumuokoa Mathew Mulumbi
kutoka kitalu 1” akawaza
Devotha na kuelekea nyumbani
kwa Mathew
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 6
Geti jeusi lilifunguliwa na
gari tatu nyeusi zikaingia katika
nyumba moja ambayo ilikuwa
na magari mengi
mabovu.Kulikuwepo pia matairi
mengi ya magari yaliyotumika
yamepangwa katika
mafungu.Nyumba hii ilionekana
kama ni gereji ya
magari.Kulikuwa na nyumba ya
wastani ambayo ilikuwa
umechafuka kuta zake na
mafuta ya magari.Hatua chache
kutoka nyumba ile watu watano
walikuwa katika injini ya gari
wakiitengeneza na mara tu
magari yale matatu yalipoingia
wakaacha kazi waliyokuwa
wanaifanya wakaelekea katika
yale magari.Kutoka ndani ya ile
nyumba akatokea jamaa mmoja
aliyevaa koti refu jeupe kama
wavaayo madaktari.Kaiza
akashuka garini akamfuata
wakasalimiana
“Karibuni.Naitwa Dr Alex
ndobe”
“Naitwa Kaiza”
Baada ya kutambulishana
Dr Alex akawatambulisha wale
jamaa waliokuwa
wanatengeneza injini ya gari
halafu mmoja wao akauliza gari
lililombeba mgonjwa.Kaiza
akaelekeza gari ambalo alikuwa
amewekwa Olivia dereva wake
akaombwa aliingize katika
chumba kimoja kilichokuwa na
ukubwa wa kuweza kukaa gari
mbili.Baada ya muda mfupi
sehemu ya sakafu liliposimama
gari lile ikazama chini taratibu
pamoja na lile gari.Kaiza alibaki
anashangaa.DrAlex akamjulisha
kuwa kuna nyumba ya chini
ambayo kila kitu kinafanyika
huko na akamtaka amfuate
wakaingia katika chumba
kingine akaufungua mlango
kwa kadi maalum wakashuka
chini hadi mahala lilipo lile gari
alimo Olivia.Kaiza akaamuru
Olivia ashushwe.Buti la gari
likafunguliwa akashushwa
Olivia akiwa amefunikwa mfuko
mweusi kichwani Dr Alex
akaelekeza aingizwe katika
chumba Fulani kisha
akamchukua Kaiza katika
chumba kidogo kwa ajili ya
maongezi
“Kaiza karibu sana.Mimi na
wewe ni mara yetu ya kwanza
tunakutana.Sitaki kufahamu
mmetokea wapi lakini
nimepewa maelekezo na rais
kuhusu ujio wenu hapa hivyo
karibuni.Hapa ni sehemu ya siri
ambayo hutumika katika kutesa
wale watu ambao ni hatari kwa
nchi na ambao wana taarifa
muhimu
zinazohitajika.Magaidi,majamba
zi sugu hata wale wafanya
biashara wakubwa wa dawa za
kulevya huletwa hapa”akasema
Dr Alex
“Nashukuru pia
kukufahamau Dr Alex.Rais
amenielekeza nije hapa ambapo
ni sehemu sahihi kabisa.Kuna
mtu ambaye ana taarifa nyeti
sana kwa ajili ya usalama wa
nchi na amegoma kufunguka
kutupa taarifa hizo
tunazozihitaji mno.Tumemleta
hapa kwa ajili ya kumfanya
afunguke na atueleze kila kitu”
akasema Kaiza
“Usihofu Kaiza mahala hapa
panaitwa gate of hell.Kama
nilivyokueleza ni sehemu
maalum ambayo huletwa wale
watu ambao ni hatari kwa nchi
ambao wamegoma kufunguka
huko walikokuwa
wanashikiliwa.Hapa ni sehemu
iliyojaa mateso ya kila
aina.Nimekuwa hapa kwa
miaka kumi nikiongoza kikosi
hiki maalum kabisa na vijana
uliowaona hapo nje
wakitengeneza injini ndio
watesaji wakubwa mimi ni
kiongozi wao.Naomba nikupe
siri moja ya hapa Kaiza.Hakuna
aliyewahi kuletwa hapa akatoka
hai ndiyo maana panaitwa ni
geti la kuelekea huko
wanakoenda baada ya
kufa.Wote wanaoletwa hapa
huletwa kuja kuuawa na
kupotea kabisa.Hicho ndicho
kikubwa kinachofanyika hapa
hivyo kama mmemleta mtu
wenu hapa ninakuhakikishia
kwamba atafunguka lakini
hatatoka hai” akasema Dr Alex
“Hakuna tatizo katika hilo
Dr Alex.Kikubwa
ninachokihitaji kutoka kwa
huyu mtu tuliyemleta hapa ni
taarifa alizonazo ambazo ni
muhimu sana kwa usalama wa
nchi” akasema Kaiza
“Vizuri,basi naomba
tusipoteze muda kazi ikaanze
mara moja” akasema Dr Alex
wakatoka na kuingia katika
chumba kimoja chenye
mitambo mingi.
“Hiki ndicho Chumba
ambacho kila kitu hufanyika.Hii
yote unayoiona hapa ni
mitambo ya kutesea watu”
akasema Dr Alex akimuonyesha
Kaiza kitanda ambacho
hutumiwa kutesea watu.
“Watu wangapi
mnawapokea hapa kila mwezi?
Akauliza Kaiza
“Hakuna idadi
maalum.Tunaweza kumaliza
hata miezi mitatu bila kupokea
mtu yeyote” akasema Dr Alex
na Kaiza akaelekeza Olivia
aingizwe katika kile
chumba,akalazwa katika
kitanda maalum
kinachoendeshwa na
kompyuta.Mikono na miguu
yake ikabanwa kwa pingu
maalum.Kiunoni akafungwa
mkanda.Shingoni akawekewa
kifaa Fulani cha kubana shingo
lakini kinachoruhusu hewa
kupita.Baada ya kumaliza
kumuandaa,mfuko uliofungwa
kichwani ukatolewa.Dr Alex
akapatwa na mstuko
mkubwa.Alihisi miguu
ikimtetemeka baada ya
kugundua mtu yule alikuwa ni
Olivia Themba.
“Dr Olivia
Themba?akajiuliza
“Sikujua kama mtu
waliyemleta hapa kutolewa
uhai wake ni huyu.Oh my God!
amefanya nini Olivia hadi
akaingia katika mikono ya hawa
jamaa?akaendelea kujiuliza Dr
Alex.Olivia naye alistuka sana
kumuona Dr Alex.
“Dr Alex?! Anafanya nini
hapa?akajiuliza
“Dr Alex is everything
okay?akauliza Kaiza baada ya
hali ya Dr Alex kubadilika ghafla
alipomuona Olivia na
kushindwa kuuzuia mstuko
wake
“Dr Alex is everything
okay?akauliza tena Kaiza
“I’m okay.Nimestuka kidogo
baadaya kumuona huyu
mrembo.Tumezoea kupokea
watu wenye sura za kutisha za
kikatili.Huyu ni mwanamke wa
pili kuletwa hapa” akasema Dr
Alex na kutoa maelekezo
kadhaa kwa vijana
wake.Mashine kubwa ikaletwa
karibu yake nyaya
zikaunganishwa kutoka katika
mashine ile na kubandikwa
kichwani,kifuani na sehemu
nyingine mbali mbali za mwili
wa Olivia.Dr Alex akamfanyia
ishara Kaiza aweze
kuzungumza na Olivia kabla ya
zoezi la kumtesa kuanza.Kaiza
akamsogelea Olivia na
kumtazama huku sura yake
ikiwa imejikunja kwa hasira
“Olivia kwa jina naitwa
Kaiza,ni mara ya pili ninakutana
nawe.Safari hii tumekutana
katika mazingira magumu zaidi
kwako.Kama unavyoona,humu
ndani kuna mitambo mbali
mbali na yote hii kazi yake ni
moja tu kutesa watu.Ukiingia
ndani ya chumba hiki utapata
mateso ya kila aina na siri moja
ya chumba hiki ni mara chache
sana walioingizwa ndani ya
chumba hiki wametoka
salama.Ni wachache sana wale
waliokubali kutoa ushirikiano
na kueleza kila kitu.Olivia hata
wewe kutoka kwako salama
ndani ya chumba hiki
itategemea na ushirikiano
utakaoutoa lakini kama
hautatoa ushirikiano kwetu this
will be the end of you” akasema
Kaiza akimuangalia Olivia kwa
macho makali
“Chumba hiki kinaitwa gate
of hell kwani ukiingizwa humu
tayari kufuli la geti la kuelekea
huko wanakoenda waliokufa
linakuwa limefunguliwa hivyo
muda wowote geti linaweza
likafunguliwa na ukaingizwa
huko.Ni sehemu ambayo
huletwa watu wajeuri ambao
hawataki kufunguka na kutoa
taarifa muhimu.Hapa ni sehemu
yako ya mwisho na kama
hautakuwa tayari kufunguka
basi utakuwa ni mwisho
wako.Kabla sijafanya chochote
nataka ushuhudie kile ambacho
huwapata wenzako kama wewe
ambao wanakuwa viburi na
kuletwa hapa” akasema Kaiza
na kumfanyia ishara Dr Alex
ambaye alimuelekeza mmoja
wa watu wake awashe runinga
kubwa iliyokuwamo mle
chumbani.
Runingani alionekana mtu
aliyechafuka damu akiwa
amelala juu ya kitanda kile
alichokuwa amelala
Olivia.Kitanda kilikuwa
kimechafuka kwa damu.Uso wa
mtu yule ulifunikwa kitambaa
maalum kiasi cha kutoweza
kumtambua,akatokea Mtu yule
aliyeficha sura yake
akamvalisha kofia ya
chuma.Kofia ile iliunganishwa
na umeme.Mtu mwingine
akaonekana katika sehemu
iliyokuwa na mtambo wenye
kuwaka taa za rangi mbali
mbali.Akabonyeza kitufe
chekundu na yule jamaa
kitandani akaanza
kutetemeka.Alitetemeka sana
na baada ya muda akatulia tuli
tayari alikwisha farik Olivia
akafumba macho hakutaka tena
kutazama.
“Olivia hiyo ni picha moja tu
umeiona.Hivyo ndivyo
wanavyofanywa wale wote
ambao ni hatari kwa usalama
wa nchi wanaoletwa hapa na
kugoma kufunguka.Kwa sasa
wewe pia ni mmoja kati ya watu
hatari kwa usalama wa nchi
hivyo kama hautafunguka
yatakukuta kama yaliyowakuta
hao unaowaona
runingani.Olivia si nia yetu kuua
watu au kuwatesa lakini
inatulazimu kufanya hivyo ili
kuliweka taifa letu
salama.Tunataka raia wa nchi
hii waishi na kufanya kazi zao
bila hofu yoyote ya usalama
wao ndiyo maana sisi tumekula
kiapo cha kufanya kila
linalowezekana kuhakikisha
kuwa nchi inakuwa salama na
tunaondoa kitisho chochote cha
kuhatarisha usalama wa ndani
ya nchi hivyo pale
inapotulazimu kuondoa uhai wa
mtu ambaye tunaamini ni hatari
tunafanya hivyo bila ajizi”
akasema Kaiza
“Olivia wewe u mwanamke
mrembo sana,mwenye elimu na
taaluma kubwa unaheshimika
mno hapa nchini na inaniuma
kukufanyia hivi,lakini
umetulazimisha wewe
mwenyewe tukufanyie
hivi.Bado unayo nafasi ya
kuyamaliza mambo haya kwa
kuamua kufunguka ukweli
ambao utasaidia kuiweka nchi
salama” Kaiza akanyamza tena
halafu akawataka watu wote
mle ndani watoke akabaki yeye
na Olivia pekee,akavuta kiti na
kuketi karibu na Olivia
“Olivia sasa tuko peke
yetu.Nimefanya hivi ili uwe
huru kujieleza.Umekuwa na
mawasiliano na hata kukutana
na baadhi ya watu
wanaosadikiwa kuwa na
mahusiano na kundi la kigaidi la
IS.Ulikwenda Kinshasa
kukutana na Seif Almuhsin
ambaye anafahamika kwa kazi
yake kubwa ya kusajili vijana
ambao hupelekwa katika kambi
za mafunzo za IS ambako
hupatiwa mafunzo ya kigaidi na
kupelekwa sehemu mbali mbali
kupigana.Kama haitoshi
umekuwa vile vile na
mawasiliano na Sayid Omar
ambaye anadaiwa ni mfadhili
mkubwa wa kikundi cha
IS.Nataka kufahamu mahusiano
yako na IS.Tuanzie hapo”
akasema Kaiza.
“Macho ya huyu jamaa
yanaonyesha ukatili mkubwa.Ni
wazi hapa ni sehemu yangu ya
mwisho na kama nisipofanya
juhudi binafsi uhai wangu
unaweza kuondolewa.Natamani
nife niondokane na mateso haya
lakini halitakuwa suluhisho
kwani Edger Kaka yuko
hai,anaweza akapatikana na siri
yake isijulikane hivyo IS
wakaendelea na mipango yao
hapa nchini na yawezekana
akashika hata nafasi ya
urais.Sitaki hilo litokee na ndiyo
maana itanilazimu kuvumilia
mateso yote ili kuhakikisha
kwamba mipango yangu
inatimia.Natakiwa kuhakikisha
kabla ya kufa niwe nimempata
Edger na nikahakikisha
anaondoka hapa nchini kama
tulivyokubaliana na mama yake
Habiba.Endapo atapatikana
nikiwa nimekufa hakuna mtu
yeyote hapa nchini
atakayefahamu siri yake.Yuko
wapi Mathew Mulumbi?Alinipa
namba zile akaniahidi kwamba
mara tu nitakapopiga atajua
mahala nilipo na atatafuta
msaada mbona namba zile
zimepigwa na
hajatokea?Alikuwa
ananidanganya? Hajui kama
nimetekwa?.Tumaini pekee
nimelipata baada ya kumuona
Dr Alex.Nimestuka sana baada
ya kumuona hapa.DrAlex
niliwahi kukutana naye tukiwa
katika mazoezi ya vitendo
katika hospitali moja nchini
Urusi na baadae tukaja
kukutana hapa Tanzania.Hatuna
ukaribu mkubwa lakini ni mtu
ambaye tunafahamiana na
tumekuwa tunakutana mara
kwa mara sehemu mbali
mbali.Amewahi kumleta
mgonjwa wake wakati
ninafanya kazi hospitali kuu ya
moyo nikamsaidia.Nimemuona
machoni namna alivyostuka
aliponiona hakutegemea
kuniona mahala
hapa.Hakuwaeleza hawa jamaa
kama ananifahamu na hii ni
dalili tosha kuwa anataka
kunisaida” akawaza Olivia na
kutolewa mawazoni na kaiza.
“Olivia nimekuachia muda
wa kutafakari sasa ni muda wa
kuanza mazungumzo yetu
tafadhali. Nijibu tafadhali kile
nilichokuuliza.”akasema Kaiza
kwa ukali
“Nimekwisha waambia ni
rais pekee ninayeweza
kuzungumza naye na si
ninyi.Mmenileta hapa kunitesa
hivyo anzeni haraka kunitesa”
akasema Olivia.Kaiza
hakuonekana kufurahishwa na
kauli ile ya Olivia
“Olivia nimekueleza kuwa
hii ni sehemu ya mwisho
itakayoamua hatima ya maisha
yako na yawezekana usitoke hai
ndani ya chumba hiki.Umeona
kile kinachowapata wale
wanaoletwa hapa na
wakaendelea kuwa
kiburi.Nataka ufunguke
mahusiano yako IS”akasema
Kaiza
“Ulisema hili ni geti la
kuingilia kuzimu? Naombeni
msipoteze muda lifungueni geti
hilo nipelekeni huko mnapoteza
muda wenu kunihoji kwani
hamtapata kitu chochote”
akasema Olivia.Kaiza
akamtazama Olivia kwa hasira.
“Huyu ni mwanamke wa
namna gani? Magaidi wale
wamekwisha
muharibu.Wamempa ujasiri
mkubwa na yuko tayari kufa
kuliko kusema chochote.Pamoja
na vitisho vyote hivi bado
anakuwa mgumu kusema
chochote.Nilimuahidi rais
kumfungua Olivia na lazima
nifanye kila kinachowezekana
kuhakikisha Olivia anafunguka
kuhusu mahusiano yake na
IS.Nataka afunguke kila kitu”
akawaza Kaiza na kubonyeza
kengele iliyokuwa ukutani
mlango ukafunguka wakaingia
watu watatu waliojaza miili yao
walikuwa wamevaa fulana
nyeusi zilizowabana.Sura zao
zilionyesha ukatili
mkubwa.Olivia akatetemeka
kwa ndani baada ya kuwaona
“Hata ukiziangalia sura za
hawa jamaa wanaonekana ni
wakatili,ni wauaji lakini silaha
yangu pekee ni kutoonyesha
woga wa aina yoyote.Japo nina
hofu kubwa lakini ninapaswa
kuendelea kushikilia msimamo
wangu na kuendelea
kujiamini.Hata wakinipa mateso
ya namna gani sipaswi
kuonyesha kutetereka”
akawaza Olivia.Kaiza
akamsogelea karibu
“Olivia hawa unaowaona
hapa kazi yao kubwa ni
kufungulia watu geti la
kuelekea kuzimu.Kwa kuwa
umeonyesha kiburi,safari yako
ya kuelekea kuzimu inaanza
sasa hivi lakini bado unayo
nafasi ya kuweza kuzuia hiki
kinachokwenda kutokea.Please
talk to me” akasema Kaiza
“Niko tayari kwenda huko
kuzimu unakosema lakini kabla
hamjanipeleka huko rais
anafahamu hiki mnachotaka
kunifanyia?Mtoto wake
anaumwa yuko
hospitali.Mkiniua mimi,Coletha
mtoto wa rais naye atakufa pia
kwani hakuna anayeweza
kukumtibu zaidi yangu.Kabla
hamjaniua mjulisheni kwanza
mkuu wenu kile mnachotaka
kukifanya lakini mkiniua bila
yeye kufahamu mtakuwa
mmefanya kosa kubwa
sana”akasema Olivia.
“Olivia hii ni nafasi ya
mwisho ninakupa ya
kufunguka”akasema Kaiza
“Nimekwisha waeleza
fanyeni kile mnachotaka
kukifanya lakini nimewapa
tahadhari kuhusu kuniua
muulizeni kwanza mkuu wenu”
akasema Olivia.Kaiza akatoka
na baada ya muda akarejea
akiwa na Dr Alex akampa
maelekezo kuwa kazi ianze
mara moja.Dr Alex akaiwasha
mashine ile ambayo nyaya zake
ziliunganishwa katika mwili wa
Olivia.Wale jamaa watatu
waliojazia miili yao
wakakisogelea kitanda cha
Olivia.
“Charging 75%” akasema
Dr Alex
“Start with 150% “ akasema
Kaiza
“Hapana Kaiza
haiwezekani.Lazima kuanza na
kiwango cha chini.150% ni
kiwango kikubwa sana na
hakifai kwa mwanamke”
“Usimuonee huruma huyu
mwanamke she’s a devil.Anao
uwezo mkubwa sana wa
kuvumilia mateso hata yakiwa
makali kiasi gani.Ameshuhudia
baba yake akipigwa risasi mbili
na hakutetereka!! Akasema
Kaiza
“Pamoja na hayo Kaiza hapa
kuna taratibu zake ambazo
lazima tuzifuate.Tunaanza na
75%” akasema DrAlex.
“Sawa Dr Alex.Lakini nina
uhakika mkubwa sana kiwango
hicho ni kidogo na huyu
mwanamke anaweza
akakihimili” akasema Kaiza
“Usihofu
Kaiza.Tutapandisha kiwango
taratibu” akasema Dr Alex na
Olivia akawekewa kifaa
mdomoni
“Okay do it ! akasema
Kaiza.Dr alex akabonyeza kitufe
Fulani katika ile mashine halafu
akashika kidude chenye rangi
ya kijani akakizungusha.Olivia
akaanza kutetemeka mwili
.Chaji za umeme zilipita mwilini
mwake.Baada ya sekunde
kadhaa Dr Alex akazima ile
mashine.Olivia bado alikuwa
anatetemeka.Kaiza
akamsogelea na kumvua kile
kifaa alichokuwa amewekewa
mdomoni na kumuita
“Olivia!!
Olivia hakuitika alikuwa
anatetemeka mwili
“Olivia unaruhusu
tuendelee au uko tayari
kuongea?akauliza Kaiza.Olivia
hakujibu kitu
“Tuendelee tena.Charge
120” akasema Kaiza na mashine
ikawashwa.Baada ya sekunde
kadhaa Olivia akaanza kutokwa
povu mdomoni.Mashine
ikazimwa haraka zile nyaya
zikaondolewa mwili mwake.Dr
Alex akachukua kifaa cha
kupimia mapigo ya moyo na
kumpima
“Nini kimetokea? Is she
breathing? akauliza Kaiza
“Tuliweka kiwango
kikubwa sana cha chaji.We
nearly killed her” akajibu
daktari na kuchukua sindano
akamchoma Olivia.
“Doctor please don’t let her
die !! akasema Kaiza baada ya
kushuhudia kilichokuwa
kimetokea Olivia.Alipochomwa
sindano ile baada ya muda
mfupi akatulia
“Will she be okay? akauliza
kaiza .Dr Alex akachukua tena
kipimo chake cha mapigo ya
moyo akampima Olivia na
kumgeukia Kaiza
“Yuko salama lakini inabidi
kumpumzisha kwanza kabla ya
kuendelea na zoezi hili”
akasema daktari
“Atapumzika kwa muda
gani?Kaiza akauliza
“Nashauri tumpumzishe
kwa masaa mawili au matatu
kabla ya kuendelea” akasema
Daktari
“Hatuna saa tatu za
kusubiri.Nitaruhusu apumzike
kwa nusu saa halafu tuendelee
na zoezi”
“Hapana Kaiza.Hali ya
Olivia ni mbaya na anatakiwa
apumzishwe kabla ya
kuendelea na mateso
mengine”akasema Dr Alex
“Sikiliza Dr Alex.Huyu
mwanamke anazo taarifa za
muhimu mno ambazo
tunatakiwa kuzipata na
ameletwa hapa ili aweze
kufunguka na si kulala
kitandani.Nataka uhakikishe
anakuwa tayari ndani ya dakika
thelathini.Umenisikia Dr
Alex?akauliza Kaiza kwa
ukali.Dr Alex hakufurahishwa
na kauli ile ya Kaiza
“Mr Kaiza mimi ndiye
daktari na ninachosema mimi
ndicho kinatakiwa
kifuatwe.Zaidi ya yote mimi
ndiye mkubwa wa hapa na kauli
yangu ndiyo ya mwisho!!
Akasema Dr Alex
“Dr Alex usitake mimi na
wewe tufungue ukurasa mpya
wa kuonyeshana nani
mkubwa.Fanya kazi yako na
uhakikishe ndani ya nusu saa
Olivia anakuwa tayari.Fanya
kazi yako vyema ukishindwa
nitakuondoa hapa na kumleta
mtu mwingine ambaye
anaifahamu kazi yake!!
Akasema Kaiza kwa ukali.
“I don’t take orders from
you Kaiza !!akasema Dr Alex
“Imeanza leo.From today
you’ll be taking orders from me
!! akasema Kaiza na Dr Alex
akakunja vidole vyake kwa
hasira akatazamana na Kaiza
“I need a room !! akasema
Dr Alex na wale jamaa wote
wakatoka nje akabaki peke yake
akashusha pumzi.
“Kaiza ni nani hadi anipe
amri? Sijapendezwa na kauli
zake chafu.Nimekuwa katika
chumba hiki kwa zaidi ya miaka
kumi sasa na hajawahi kutokea
mtu yeyote aliyenitamkia
maneno kama aliyonitamkia
Kaiza” akawaza Dr Alex na
kumgeukia Olivia aliyekuwa
amelala kitandani
“Namfahamu sana Dr
Olivia.Mimi na yeye tulikutana
kwa mara ya kwanza nchini
Urusi toka hapo tukawa
marafiki.Japo mimi na yeye
hatuna ukaribu mkubwa sana
lakini ni marafiki na nimewahi
kumpeleka shangazi yangu
katika hospitali ya moyo
alikokuwa anafanya kazi Olivia
kabla ya kuanzisha kituo chake
cha utafiti wa magonjwa na Dr
Olivia alihakikisha
amehudumiwa na
akapona.Amefanyaje hadi
akaingia katika mikono ya hawa
jamaa? Nimesikia anaulizwa
kuhusu mahusiano yake na
kikundi cha IS,msomi kama
huyu anawezaje kushirikiana na
kikundi cha kigaidi cha IS?
Siamini kama hilo
linawezekana.Familia ya Olivia
ni matajiri wakubwa na Olivia
hana sababu ya kujiunga na
kikundi cha kigaidi.Watakuwa
wamemleta mtu ambaye si
sahihi.Olivia hapaswi kuwepo
mahala hapa” akawaza Dr Alex
na kumsogelea Olivia akampima
mapigo ya moyo.
“Mapigo ya moyo
yanakwenda vizuri” akawaza Dr
Alex huku akiweka kile kifaa
cha kupimia mfukoni.Wakati
akijianda kuchukua kifaa
kingine Olivia akafumbua
macho.
“Dr Alex” akaita Olivia kwa
sauti ya kunong’ona.Dr Alex
akastuka halafu akamuinamia
kana kwamba anampima kisha
kwa sauti ndogo akasema
“Fumba macho yako kuna
kamera kila kona humu ndani
wakijua umefumbua macho
watakuja na kuendelea
kukutesa” akasema Dr Alex
huku akijitahidi kumkinga
Olivia
“Dr Alex please help me”
akasema Olivia akiwa
amefumba macho
“Olivia kwa nini uko hapa?
Hawa jamaa wamekutoa
wapi?Hupaswi kuwepo sehemu
kama hii ni sehemu ya hatari
kubwa.Kwa nini umeingia
katika mikonoi ya hawa
jamaa?akauliza Dr Alex
“Ni hadithi ndefu Dr Alex
kama tukijaliwa uhai
nitakueleza lakini kwa sasa
unisaidie kutoka humu.Please
don’t let them kill me” akasema
Olivia
“Olivia ni vigumu sana
kutoka sehemu hii hata hivyo
nitajitahidi kutafuta namna ya
kukusaidia” akasema Dr Alex
“DrAlex naomba mtafute
mtu anaitwa Mathew Mulumbi
muelekeze mahala nilipo yeye
atajua namna ya kuja kuniokoa”
akasema Olivia
“Olivia I can’t do that !
“Dr Alex fikisha ujumbe
kwa Mathew Mulumbi kuwa
niko hapa.Yeye atatafuta namna
ya kuja kuniokoa”
“Olivia hapa ni sehemu ya
siri na hapaswi mtu yeyote
kupafahamu” akasema Dr Alex
“Dr Alex please help
me.Don’t let them kill me”
akasema Olivia
“What have you done
Olivia?akauliza Dr Alex
“Dr Alex something is going
to happen in this country.Ni
mimi pekee ambaye ninaweza
nikazuia jambo hilo lisiweze
kutokea hivyo naomba
unisaidie” akasema Dr Olivia
“Nini kinakwenda kutokea
Olivia?Kwa nini hawa jamaa
wamekuleta hapa? Nimesikia
wanakutuhumu kuwa una
mahusiano na kikundi cha
kigaidi cha IS je ni kweli
unahusiana na kikundi
hicho?akauliza Dr Alex
“Dr Alex sina muda wa
kuelezea lakini naomba
unisaidie kufikisha ujumbe kwa
Mathew Mulumbi ni
mkurugenzi wa kiwanda cha
maziwa cha Masai milk.Mpe
taarifa kuwa niko hapa yeye
atajua namna ya
kunisaidia”akasema Olivia
“Olivia..” Dr Alex akastuka
baada ya mlango kufunguliwa
akaingia Kaiza akiwa na watu
wake wawili.
“How’s she?akauliza Kaiza
“Bado hali yake si nzuri
anahitaji mapumziko” akasema
Dr Alex na kuvuta dawa katika
sindano akamchoma Olivia.
“Dr Alex nimekwambia
ninamuhitaji Olivia ndani ya
nusu saa.Leo lazima afunguke”
“Kaiza na mimi nimekwisha
kueleza kuwa hali ya Olivia si
nzuri anatakiwa kupata
mapumziko ya walau saa moja
au mbili”
“Hatuna muda huo Dr
Alex.Nataka ndani ya nusu saa
awe tayari kuendelea na
mahojiano”akasema Kaiza
Mara ghafla Olivia akaanza
kutetemeka.
“What’s going on? akauliza
Kaiza
“I don’t know.Hali yake
imebadilika ghafla” akasema Dr
Alex.Mashine ya kusoma
mgandamizo wa damu ilikuwa
inatoa mlio na kuonyesha
mgandamizo ni mkubwa kupita
kawaida
“Mgandamizo wa damu
umekuwa mkubwa sana
nahitaji kufanya jitihada za
kuushusha” akasema Dr Alex na
kukimbia nje baada ya dakika
mbili akarejea akiwa na vichupa
kadhaa vya dawa akamchoma
Olivia na baada ya dakika tatu
mashine ile ikaacha kutoa mlio
na mgandamizo ukaanza
kushuka.Kaiza akashusha
pumzi
“Kaiza tafadhali naombeni
mnisikilize.Mimi ni daktari na
nimekuwa hapa kwa miaka
zaidi ya kumi sasa na kila
anayeletwa hapa mimi ndiye
humpima na kujua anahitaji
kiwango gani cha mateso.Kwa
Olivia uwezo wake wa
kustamihili mateso makali
kama haya ya kuchomwa na
umeme ni mdogo ndiyo maana
hali yake imekuwa namna hii na
kama mkilazimisha aendelee
kuteswa atapoteza maisha na
mtapoteza kila kitu
mnachokitaka toka
kwake.Nawaomba mzingatie
ushauri wangu wa kumuacha
apumzike kwa muda
niliowaelekeza” akasema Dr
Alex
Kaiza akamuita pembeni Dr
Alex
“DrAlex samahani kwa
maneno niliyokutamkia awali
lakini ukweli ni kwamba huyu
mwanamke anazo taarifa nyeti
sana kwa ajili ya usalama wa
nchi ambazo tunahitaji kuzipata
kutoka kwake ndiyo maana
tumemleta hapa ambako
tunaamini
atafunguka.Anashirikiana na
kikundi cha kigaidi cha IS na
tunataka kujua ni mambo gani
wanayapanga hapa nchini hivyo
naomba ufanye kila lililo ndani
ya uwezo wako kuhakikisha
anakuwa salama na muda wa
kupumzika upunguzwe ili
tuweze kumuhoji.Naomba
mapumziko yawe ni saa
moja.Tusaidie kwa hilo
tafadhali” akasema Kaiza
“Sawa Kaiza nitajitahidi
lakini naomba heshima iwepo
kati yetu”
“Usihofu kuhusu hilo Dr
Alex” akasema Kaiza
“Sasa mnaweza
mkatoka.Niachieni nafasi
niweze kumuandaa huyu mtu
kwa ajili ya mahojiano”
akasema Dr Alex,Kaiza na watu
wake wakatoka nje
“Kaiza anadai Olivia anazo
taarifa nyeti kwa ajili ya
usalama wa nchi na kwamba
anajihusisha na kikundi cha
kigaid cha IS.Olivia naye anadai
kuna jambo kubwa linakwenda
kutokea hapa nchini na ni yeye
pekee mwenye uwezo wa
kulizuia lisitokee.Nani mkweli
kati yao? Sitaki kujua nani
mkweli ninachohitaji ni
kumsaidia Olivia.Sitaki
kufahamu amefanya nini au
kama taarifa za kuwa
anashirikiana na kikundi cha IS
ni za kweli lakini lazima
nimsaidie kuyaokoa maisha
yake.Nimekuwa nikishuhudia
watu wakiuawa kila
wanapoletwa humu ndani lakini
kwa mara ya kwanza ninahisi
kutaka kumsaidia Olivia
aepukane na kifo.Naamini
ameletwa hapa kimakosa.Olivia
haonekani kama ni mfuasi wa
IS.Familia yao ni watu wenye
uwezo mkubwa na hana
ulazima wowote wa kujiunga na
makundi ya kigaidi” akawaza Dr
Alex akiwa amesimama
pembeni ya kitanda cha Olivia
“Olivia amenitaka nimtafute
Mathew Mulumbi, hili jina si
geni kulisikia.Amesema ni
mkurugenzi wa kiwanda cha
maziwa cha Masai Milk.Anadai
huyu anaweza akamsaidia
akifahamu kama yuko hapa.Hii
ni sehemu ya siri na hatakiwi
mtu mwingine asiyehusika
kufahamu kinachoendelea
ndani ya nyumba hii lakini kwa
mara ya kwanza nitavunja
kanuni kwa ajili ya kumsaidia
Olivia.Siwezi kushuhudia kwa
macho yangu akiuawa”
akawaza na kumtazama tena
Olivia
“Olivia anasema kuna
jambo kubwa linakwenda
kutokea hapa nchini na ni yeye
pekee mwenye uwezo wa
kulizuia.Ni jambo gani
hilo?Nafsi yangu inaniambia
Olivia ana jambo kubwa hivyo
nalazimika kumsaidia.I have to
do something” akawaza Dr Alex
na kutoka mle ndani ya chumba
alimo Olivia ambapo mlangoni
kulikuwa na mlinzi mmoja
mwenye silaha aliyekuja na
Kaiza.Dr Alex akaenda katika
chumba kilichokuwa na runinga
kubwa iliyoonyesha kamera
mbali mbali zilizozunguka lile
jumba akawaona Kaiza na watu
wake aliokuja nao wakiwa
wamekaa katika viti vya
kupumzikia.Haraka haraka
akaingia mtandaoni na
kuitafuta kampuni ya maziwa
ya Masai akapiga simu
ikapokelewa na muhudumu wa
kike,akaomba kuzugumza na
mkurugenzi Mathew
Mulumbi.Alitaarifiwa kuwa
Mkurgenzi hajafika kazini
akapewa namba ya simu ya
mkononi ya Mathew akapiga
lakini haikuwa
ikipatikana.Akapiga tena na
kumjulisha muhudumu kuwa
namba zile hazipatikani
akaomba apatiwe namba
nyingine ili aweze kuzungumza
na Mathew jambo la muhimu
sana akapewa namba ya simu
ya nyumbani kwake ili ajaribu
kuwasiliana na nyumbani kwa
Mathew.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 7
Saada akiwa
amejipumzisha katika moja ya
chumba cha wageni nyumbani
kwa Mathew alisikia mlango
ukigongwa.Akainuka haraka
haraka na kuelekea mlangoni
“Yawezekana Devotha
amekuja” akawaza wakati
akikinyonga kitasa kuufungua
mlango akakutana na mtumishi
wa ndani
“Dada samahani kwa
kukusumbua” akasema yule
mtumishi
“Bila samahani ,karibu”
akasema Saada
“Kuna mtu amepiga simu
anamtafuta kaka
Mathew.Anadai ana jambo la
muhimu sana la kumueleza
amepiga simu kazini kwake
akaambiwa hajafika akapiga
namba zake za simu
hapatikani.Hata mimi nimepiga
namba zake zote za simu
ninazozifahamu lakini
hapatikani.Imenishangaza kwa
kuwa haijawahi kutokea kaka
Mathew akashindwa
kupatikana simuni.Muda wote
simu zake huwa
hewani.Nimekuja kwako nataka
kufahamu mahala
mlikomuacha” akasema yule
mtumishi wa ndani
akimuangalia kwa wasi wasi
“Mathew hapatikani
simuni?akauliza Saada
“Ndiyo hapatikani
simuni.Mlisema mlikuwa naye
na akawaelekeza mje hapa
nyumbani”
“Ndiyo tulikuwa naye na
akatuelekeza tutangulie hapa
nyumbani kwake na yeye
atafuata baadae”
“Kwani ninyi mmetokea
wapi dada?akauliza
Theresa.Kabla Saada hajajibu
kitu,simu yake ikaita akaipokea
akazungumza kwa muda mfupi
halafu akasema
“Nimepigiwa simu kuna
mgeni wa kaka ngoja
nikampokee ninakuja sasa hivi”
akasema na kumuacha Saada
akiwa na hofu kubwa.
“Tumemdanganya huyu
msichana kuhusu Mathew na
sasa ameanza kuwa na
wasiwasi.Hii inaweza kuwa
mbaya kwetu kwani tayari
amekwisha anza kuhoji mahala
aliko Mathew.Devotha yko
wapi?” akawaza Saada na
kwenda kukaa kitandani
“Nimeingia katika matatizo
makubwa.Naamini hivi sasa
nitakuwa ninasakwa kwa
kitendo cha kudukua simu ya
rais.Sikupenda kufanya vile
lakini nisingeweza kukataa
ombi la madam Devotha.Ni mtu
ninayemuheshimu
sana,amenitoa mbali hadi
akanifikisha hapa nilipo
leo.Kikubwa ninachokiona kwa
sasa ni kuondoka hapa nchini
hadi hapo mambo
yatakapotulia.Akija hapa
nitamshauri ili niweze kwenda
nje ya nchi kupumzika kwa
muda hadi hapo mambo
yatakapokaa sawa kwani kama
nikiendelea kukaa hapa nchini
lazima nitakamatwa na
nikikamatwa Devotha naye
atakuwa katika matatizo
makubwa” akaendelea kuwaza
Saada
Katika kibaraza kikubwa
cha kuingilia ndani taksi nyeupe
iliegesha mlango ukafunguliwa
akashuka jamaa mmoja aliyevaa
suruali ya jeanz nyeusi na
fulana nyeupe,shingoni alikuwa
na mkufu mkubwa wa
dhahabu.Macho yake
aliyafunika kwa miwani mizuri
ya jua.
“Theresa ! akasema yule
jamaa baada ya kushuka garini
na kumuona mtumishi wa ndani
wa Mathew akiwa amesimama
kibarazani
“Gosu gosu ! akasema
Theresa akamfuata
wakasalimiana.Dereva wa taksi
akashusha mizigo ya Gosu gosu
na Theresa akaiingiza ndani.
“Pole na safari” akasema
Theresa
“Ahsante.Habari za hapa?
“Hapa kwema
kabisa”akajibu Theresa
Theresa anamfahamu Papii
Gosu gosu kwani amekuwa
akifika hapa mara kwa mara
kutokana na kusimamia
biashara za Mathew zilizopo nje
ya nchi
“Mathew yuko
wapi?akauliza Gosu gosu
“Imekuwa vyema
umefika.Kuna jambo limetokea
hapa muda mfupi kabla
hujawasili”
akasema Theresa
“Kumetokea nini?akauliza
Gosu gosu akionekana kuwa na
hofu kidogo
“Ni kuhusu kaka Mathew”
“Nini kimetokea Theresa?
“Mathew aliondoka hapa
nyumbani asubuhi leo akatoa
maelekezo tuandae vyumba
kwa ajili yako na dada
Ruby.Mchana huu walifika watu
wawili wakadai kuwa
wameelekezwa na Mathew
wafike hapa na
wamsubiri.Baadae mmoja
akaondoka akabaki mmoja
nikamuandalia chumba chumba
cha wageni akaenda
kupumzika.Muda mfupi uliopita
kuna mtu amepiga simu akadai
anataka kuzungumza na
Mathew kama yuko hapa
nyumbani.Anadai amemtafuta
bila mafanikio.Nilishangaa kwa
kuwa kaka Mathew hajawahi
kuzima simu zake.Muda wote
anapatikana hewani.Nini
kimetokea leo hadi simu zake
zote zisipatikane ?” akasema
Theresa
“Theresa unasema toka
Mathew alipoondoka asubuhi
hajarejea hadi mida hii?
akauliza Gosu gosu
“Hajaonekana tena toka
alipoondoka asubuhi.Si
kuonekana tu hata kupiga simu
hajapiga”akajibu Theresa
“Something is not right”
akawaza Gosu gosu
“Huyo mtu aliyepiga simu
amejitambulisha yeye ni nani
?akauliza
“Hakusema yeye ni nani
lakini alionekana kuwa na shida
sana ya kuzungumza na
Mathew.Inaonekana kuna
jambo la muhimu sana alitaka
kumueleza.Aliacha namba zake
za simu ili Mathew ampigie
atakapofika” akasema Theresa
“Huyo mgeni ambaye
anadai ameelekezwa na
Mathew aje hapa umewahi
kumuona?
“Ni mara yangu ya kwanza
kumuona” akajibu Theresa na
simu yake ikaita akaipokea na
kuzungumza kwa sekunde
chache halafu akamgeukia Gosu
gosu
“Nilikueleza kuwa wageni
wale walikuwa wawili na
mmoja wao akaondoka akabaki
moja,nimejulishwa na walinzi
wa getini kuwa yule mwenzake
amerejea”
“Good.Niachie mimi
nitamuhoji ili tujue mahala
aliko Mathew” akasema Gosu
gosu.Wote waliyaelekeza
macho yao nje na muda mfupi
likafika gari jeusi likaegesha
mbele ya nyumba akashuka
mwanamke mmoja mwenye
umbo zuri.
“Ni yule pale” akasema
Theresa wakimtazama
mwanamke yule akishuka
garini
“She’s so pretty !!
akanong’ona gosu gosu
Mwanamke yule akagonga
mlango Theresa akaenda
kuufungua na kumkaribisha
ndani.
“Mpaka sasa sijalifahamu
jina lako” akauliza
“Ninaitwa Theresa.Wewe
unaitwa nani?
“Naitwa Devotha”
“Nafurahi kukufahamu
Theresa.Habari za toka wakati
ule?
“Nzuri kabisa karibu tena
mama Devotha” akasema
Theresa
“Ahsante sana” akasema
Devotha na kuyaelekeza macho
yake kwa Gosu gosu
“Hi”akasema
“Hi”akajibu Gosu gosu
“Mama Devotha huyu ni
rafiki wa kaka anaitwa papii
Gosu gosu.Amefika muda mfupi
uliopita kutoka nje ya nchi”
“Karibu sana Papii..ouh
gosh jina lako refu”
“Papii Gosu gosu” akasema
Gosu gosu
“Gosu gosu.Nafurahi
kukutana nawe.Habari za wapi?
“Nimetokea Dubai” akajibu
Gosu gosu
“Ninaitwa Devotha Adolph
ni rafiki wa Mathew”
“Nafurahi kukufahamu
Devotha” akajibu Gosu gosu
“Mathew hajafika
bado?akauliza Devotha
“Bado hajaonekana” akajibu
Theresa
“Yule msichana wangu
niliyemuacha hapa yuko
wapi?akauliza
“Yuko chumba cha wageni
anapumzika”
“Nipeleke nikaonane naye”
akasema Devotha huku
akiinuka
“Devotha we need to talk!
Akasema Gosu gosu
“Unasemaje Gosu gosu?
“Umenisikia vizuri.We need
to talk.Please follow me !
akasema Gosu gosu na
kuinuka,Devotha akamfuata
wakaelekea katika chumba cha
maongezi
“Devotha mimi si
mzungumzaji mzuri.Maneno
yangu huwa machache
sana.Nataka kufahamu mahala
alipo Mathew”
“Mbona unaonekana kuwa
na hofu gosu gosu?Mathew is
fine”
“Mathew hapatikani simu
zake zote
zimezimwa.Ulimwambia
Theresa kuwa aliwaelekeza
mfike hapa.Where is he?
“Gosu gosu naomba usiwe
na wasiwasi tafadhali.Mathew
ni rafiki yangu.Mimi na yeye
tulikuwa na mazungumzo
Fulani ya kibiashara na yule
msichana niliyenaye anaitwa
Saada.Ni Mtanzania lakini kwa
sasa anaishi nchini
Msumbiji.Mathew alielekeza
nimlete Saada hapa nyumbani
kwake na tumsubiri hadi
atakapofika ili tufanye
mazungumzo.Kwa kuwa
nilikuwa na mizunguko mingine
ya kufanya ilinilazimu
kumuacha Saada hapa na
kuondoka.Kwa nini Mathew
hapatikani simuni?akauliza
Devotha.Gosu gosu akavua
miwani yake na kumtazama
Devotha kwa macho makali
yenye kuogofya.
“Mimi ndiye msimamizi
mkuu wa biashara za Mathew
na kila anachotaka kukifanya
huwa ananishirikisha.Nataka
kufahamu ni biashara gani
wewe na Mathew mnataka
kuifanya na huyo
Saada?akauliza Gosu gosu
“Ni biashara ya madini”
“Madini?akauliza Gosu gosu
na kutoa kicheko kidogo
“Mathew hajawahi kufikiria
kufanya biashara ya madini.Ni
mara ya kwanza ninasikia
kutoka kwako kuwa Mathew
anataka kufanya biashara ya
madini.Mathew ni billionea ana
miradi mingi mikubwa
inayomuingizia fedha nyingi
hajawahi kufikiria kujiingiza
katika biashara hiyo ya madini”
akasema Gosu gosu
“Kweli kabisa mimi na yeye
tunataka kuingia ubia ili
tununue mgodi wa kuchimba
dhahabu” akasema Devotha
“Mathew anao washauri
wake wa biashara na mimi
nikiwa mmoja wao,kila
anachofikiria kukifanya huwa
kinaletwa kwetu
tunakichambua kama kinaweza
kuwa na faida na
tunamshauri.Mathew anaiamini
mno timu yake hiyo ambayo
ndiyo iliyomsaidia sana kwa
biashara zake kukua na kuwa
kubwa.Hajawahi kuleta kwetu
wazo la mradi wa madini”
akasema Gosu gosu.
“Unataka kusema nini Gosu
gosu? Mimi muongo?akauliza
Devotha
“Sijasema hivyo lakini
ninapata ukakasi kidogo
kuamini hicho
unachoniambia.Nataka
nikazungumze na Saada
pia.Devotha mimi ni mtu mbaya
sana naomba usithubutu
kunidanganya.Nikigundua
umenidanganya………” akasema
Gosu gosu
“Gosu Gosu let’s talk”
akasema Devotha wakati Gosu
Gosu akipiga hatua kutoka mle
chumbani
“Please sit down! Akasema
Devotha
“Niambie haraka hicho
unachotaka kuniambia”
akasema Gosu gosu
“I know where Mathew
is”akasema Devotha
“Where is he? akauliza Gosu
Gosu.Tayari sura yake ilikwisha
badilika
“Kabla ya kukueleza
chochote kuhusiana na mahala
alipo Mathew kuna mambo
ambayo nataka uyafahamu”
akasema Devotha
“Go ahead” akasema Gosu
Gosu
“Naitwa Devotha Adolph.Ni
mkurugenzi wa idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi…”
“Devotha ninachotaka
kukifahamu kutoka kwako ni
kitu kimoja tu.Mathew yuko
wapi? Hizo habari za usalama
sijui wa nchi sizihitaji” akasema
Gosu Gosu kwa sauti kali
“Taratibu Gosu Gosu.Ili
ufahamu mahala alipo Mathew
unahitaji kupata maelezo
kwanza.Tafadhali naomba
unisikilize” akasema Devotha
“Idara ninayoiongoza ina
jukumu kubwa la kuhakikisha
inang’amua viashiria vyote vya
kuhatarisha usalama wa nchi na
kuviondoa kabla ya kuleta
madhara” akanyamaza kidogo
kisha akasema
“Tulipata taarifa kuna
mtanzania mmoja amekutana
na mtu kutoka kundi la kikaidi
la IS jijini
Kinshasa.Tulimgundua mtu
huyo ni daktari anaitwa Dr
Olivia Themba.Tulimfuatilia
toka alipokuwa Kinshasa na
aliporejea Dar es salaam
tulimteka lengo likiwa ni
kufahamu mahusiano yake na
kikundi cha IS.Tulipochunguza
mawasiliano yake tuligundua
alikuwa akiwasiliana na mtu
anaitwa Sayid Omar ambaye
anatajwa kuwa mfadhili
mkubwa wa IS.Tulimtaka atupe
maelezo kuhusiana na Sayid
Omar na akatupa namba Fulani
akidai zingetuwezesha
kufahamu alipo Sayid
Omar.Namba zile zilifunga
mtandao wetu wa
mawasiliano.Baadae tuligundua
kwamba namba zile alipewa na
Mathew Mulumbi hivyo
tukaanza kumfuatilia Mathew
pia,tukaweka mtego na leo
asubuhi tulifanikiwa kumpata
Mathew na amehifadhiwa
sehemu Fulani kwa mahojiano”
akasema Devotha
Gosu Gosu akainuka uso
wake ukiwa umejikunja
akakunja ngumu.Devotha tayari
alikwisha msoma Gosu Gosu
naye akasimama.
“Easy Gosu Gosu..Take it
easy..Sit down and let me finish”
akasema Devotha
“Nakupa nafasi ya kumaliza
hicho unachotaka kunieleza na
sentensi ya mwisho nataka
ieleze alipo Mathew” akasema
Gosu Gosu..Wakatazamana kwa
muda Devotha akaendelea
“Olivia alitaka kuonana na
rais.Nikafanya juhudi akaonana
naye wakazungumza na hapo
ndipo jambo jipya likabainika”
akasema Devotha na kumueleza
Gosu Gosu kila kitu kuhusiana
na madai ya Olivia kuwa Edger
kaka yuko hai.
“Baada ya kuona msisitizo
mkubwa aliouweka Olivia
katika suala hili la Edger kaka
niliamua kulipa uzito na
kulichunguza kufahamu ukweli
wake.Olivia alinihakikishia
endapo nitafanikiwa kufahamu
alipo Edger kaka angenieleza
siri kubwa ambayo anaamini
ninahitaji sana
kuifahamu.Nilionana na
Mathew pia nikamuhoji na
akanipa ushirikiano mkubwa
ambao sikuutegemea na..”kabla
hajamaliza sentensi yake Gosu
Gosu akamkatisha
“Where is he?! Akauliza
Gosu Gosu huku akigonga meza
“Gosu Gosu easy ! Let me
finish !
“Devotha hili si suala la
kufanyia mzaha hata
kidogo.Hayo yote unayonieleza
yanapita sikio hili na kutokea
lingine.Ninachohitaji kufahamu
ni kitu kimoja tu Mathew yuko
wapi? Kila unapotoa maelezo
yako na kumtaja Mathew
unazidi kunipandisha hasira!!
Akasema Gosu Gosu kwa ukali
“Tafadhali Gosu Gosu nipe
dakika chache nimalizie kukupa
maelezo yangu” akasema
Devotha
“Go ahead” akasema Gosu
Gosu
“Nimekwambia
nilizungumza na Mathew
akanipa ushirikiano mkubwa na
alinisaidia kuyasoma hata
mawasiliano ya Olivia na Sayid
Omar yaliyoandikwa kwa Lugha
ya kiarabu.Baada ya kumuhoji
niligundua Mathew hahusiki na
chochote kuhusu IS bali lengo
lake lilikuwa ni kumlinda
Olivia.Kwa bahati mbaya
nisingeweza kumtoa mahala
alipo kwa haraka hivyo bado
anaendelea kuwepo mahala
hapo lakini nakuhakikishia
yuko salama kabisa.Alinishauri
niendelee kulichunguza suala
hili la Edger Kaka na akanieleza
anao watu wawili ambao
wanaweza wakanisaidia sana
katika jambo hili wanatoka nje
ya nchi naamini mmoja wao ni
wewe.Alinielekeza niwafuate na
kuwataka mnisaidie katika
kulichunguza hili jambo”
akanyamaza akamtazama Gosu
Gosu halafu akaendelea
“Kitu alichonishauri
nikifanye ni kudukua
mawasiliano ya rais jambo
ambalo nililifanya” “Ulipata
nini kutoka katika simu ya rais?
akauliza Gosu Gosu
“Nothing.Waliwahi
kugundua haraka kuwa simu ya
rais imedukuliwa na
hatukuweza kuendelea
tena.Ikanilazimu kumchukua
Saada ambaye ndiye aliyekuwa
anaifanya kazi hiyo ya udukuzi
na kuja kumficha hapa ambako
ninaamini ni sehemu salama
kwake.Baada ya hapo niliamua
kwenda kuonana na Olivia
kuzungumza naye kwa kina
lakini nilipofika mahala
alipokuwa anahifadhiwa
sikumkuta.Tayari aliondolewa
na kupelekwa mahala
kusikojulikana.Tayari rais
amegundua kuwa ni mimi
niliyedukua mawasiliano yake
hivyo waliniwekea mtego
wanikamate.Kwa bahati nzuri
uwezo wangu ni mkubwa
kuliko watu waliotumwa kuja
kunikamata hivyo
niliwachakaza vibaya na
kuondoka kuja hapa kutafuta
msaada.Gosu Gosu suala hili ni
kubwa na mimi peke yangu
siwezi ninaomba uniamini na
tushirikiane kwa pamoja
kumtafuta Olivia na kuujua
ukweli.Hapa nilipo ninaamini
ninatafutwa na nimewekewa
vizuizi kila kona.Simu yangu
imefungwa na siwezi kuingia
hata katika mtandao
wetu.Nimezuiliwa kila mahali”
akasema Devotha.
“Devotha kama Mathew
alikuelekeza kupata msaada
kutoka kwetu ,basi karibu
sana.Yule ni mkuu wetu ni kaka
yetu na maelekezo yake ni amri
kwetu.Tutashirikiana nawe
lakini kwa sharti moja tu”
“Sharti gani Gosu Gosu?
“Mathew lazima awe wa
kwanza kukombolewa.Tusaidie
tumpate Mathew na kisha
tutakusaidia umpate Olivia”
“Mathew yuko sehemu
salama.Olivia hajulikani
alipo.Nashauri nguvu kubwa
tuielekeze kumtafuta Olivia
kwanza halafu nitawasaidia
kumpata Mathew Mulumbi”
“Mathew first ! akasema
Gosu Gosu
“Fine.Lakin……..”
akanyamaza Devotha baada ya
Theresa mtumishi wa ndani wa
Mathew kuonekana katika
mlango wa kioo
“Karibu Theresa” akasema
Gosu Gosu
“Kaka,yule mtu amepiga
tena anauliza kama
nimefanikiwa kuwasiliana na
Mathew” akasema Theresa
“Naomba simu niwasiliane
naye” akasema Gosu Gpsu
“Nani anayemtafuta
Mathew?akauliza Devotha
“Kuna mtu amepiga simu
anamtafuta Mathew anadai ana
jambo la muhimu sana la
kuzunguma naye.Hii ni mara ya
pili anapiga.Yawezekana ana
jambo la muhimu”akasema
Gosu Gosu
“Wait ! Unamfahamu mtu
huyo?Devotha akauliza
“Hapana simfahamu.Kuna
njia moja tu ya kujua tatizo
lake.Anaonekana hamjui
Mathew nitampigia na kujifanya
mimi ndiye Mathew halafu
tutajua kwa nini anamtafuta
Mathew”akasema Gosu Gosu na
kwa kutumia simu ya nyumbani
kwa Mathew akampigia yule
mtu simu ikapokelewa
“Hallow” akasema jamaa
wa upande wa pili aliyepokea
simu
“Hallow,Mathew Mulumbi
hapa.Ninazungumza na
nani?akauliza Gosu Gosu
“Naitwa Dr
Alex.Nimekutafuta sana.Kuna
jambo nataka tuzungumze la
muhimu”
“Jambo gani Dr Alex?
“Ni kuhusu Olivia”
“Olivia?akauliza Gosu Gosu
na kumtazama Devotha
“Nakusikiliza DrAlex”
akasema Gosu Gosu na mara
akasikia sauti ikiuliza kwa ukali
“Dr Alex unazungumza na
nani?
“Nazungumza na rafiki
yangu!! Akajibu Dr Alex
“Unamueleza nani kuhusu
Olivia?ikauliza sauti ile
kali.Gosu Gosu alisikia kila kitu
kupitia simu yake kwani Dr Alex
hakuwa ameikata
“Nakuuliza unazungumza
na nani? ikauliza sauti ile kwa
ukali
“I can explain
Kaiza”akasema Dr Alex na mara
simu ikakatwa
“Gosu Gosu kuna nini
kuhusu Olivia?” akauliza
Devotha.Gosu Gosu akamueleza
kila kitu alichokisikia
“ My God !! Kaiza alikuwa
msaidizi wangu na ninaamini
yuko na Olivia.Wako wapi
hospitali? Huyo Dr Alex ni nani?
Akauliza Devotha
“Yawezekana Dr Alex
anataka kumsaidia Olivia na
ndiyo maana alikuwa
anamtafuta Mathew.Nadhani
alitaka kumjulisha mahala alipo
ndipo huyo jamaa Kaiza
akaingia”
“Gosu Gosu yawezekana
hali ya Olivia ni mbaya ndiyo
maana amepelekwa
hospitali.Yawezekana
ameteswa sana hali yake
ikabadilika.Tunatakiwa
tukamuokoe Olivia haraka kabla
hajapoteza maisha”akasema
Devotha
“Mathew first! Akasisitiza
Gosu Gosu
“Gosu Gosu nadhani
itakuwa vyema kama tukianza
kushughulikia suala la Olivia.Ni
muhimu sana.Maisha yake yako
hatarini”
“Devotha hakuna kitu
kitakachofanyika bila ya
Mathew kupatikana.Ukitaka
mimi na wewe tuzungumze
lugha moja nionyeshe mahala
alipo Mathew Mulumbi”
akasisitiza Gosu Gosu.Devotha
akavuta pumzi ndefu halafu
akasema
“Mathew yupo mahala
panaitwa Kitalu1.Idara yetu ina
sehemu zake mbali mbali na
zimepewa majina ya vitalu na
kila kitalu kina namba.Mahala
alipo Mathew pamepewa hadhi
ya namba 1 kutokana kuwa
sehemu salama zaidi kuliko zote
tulizonazo.Ni sehemu pekee
ambayo hata kiongozi wa nchi
anaweza akajificha hapo hata
kwa mwaka mzima pale
panapokuwa na kitisho cha
usalama wake.Nataka kufahamu
mko wangapi jumla?akauliza
Devotha
“Niko peke yangu kama
unavyoniona”
“Peke yako?Devotha
akashangaa
“Ndiyo niko peke
yangu.Mathew alikueleza tuko
wawili,mwingine hajawasili
bado anaitwa Ruby nategemea
atawasili jioni ya leo akitokea
Uingereza”akasema GosuGosu
“Hapa kuna tatizo Gosu
Gosu.Kitalu 1 ni sehemu yenye
ulinzi wa kutosha na inahitaji
watu wa kutosha wakiwa na
silaha kama kweli tunataka
kumuokoa Mathew
Mulumbi.Kumefungwa kamera
kila mahali hivyo kila
tutakachokifanya
kitaonekana.Ninahitaji tupate
watu kama kumi hivi” akasema
Devotha
“Hakuna watu kumi.Niko
peke yangu”akasema GosuGosu
na Devotha akaendelea
kumshangaa
“Gosu Gosu tafadhali
tusiweke mzaha katika suala
hili.Tuangalie namna
tutakavyoweza kupata watu wa
kutusaidia katika suala hili”
akasema Devotha
“Devotha mimi peke yangu
ni kikosi kinachojitosheleza”
akasema Gosu Gosu
“Sijakuelewa Gosu Gosu
unamaanisha nini?
“Hakuna haja ya kuwa na
watu kumi au zaidi mimi peke
yangu ninatosha kabisa”
“Gosu Gosu usifanye mzaha
katika mambo muhimu kama
haya.Usalama wa Mathew
Mulumbi na Olivia
unatutegemea sisi kwa sasa
hivyo tunapaswa kuwa na
kikosi cha watu wasiopungua
kumi.Hakuna mahala
tunakoweza kupata watu hata
kwa kuwakodi na kuwalipa?
“Mimi ni
mwanajeshi.Nimekulia msituni
na toka nikiwa mdogo
nimekuwa nikipigana
vita.Ninajiamini mimi peke
yangu ni zaidi ya kikosi”
akasema Gosu Gosu.Devotha
alikosa neno la kusema akabaki
anamtazama.
“Usishangae
Devotha.Nilichokwambia ni kitu
cha kweli kabisa.Hata Mathew
ananifahamu vyema ndiyo
maana alinipigia simu nikiwa
Dubai na kunitaka nifike haraka
Dar es salaam kumsaidia
kumtafuta rafiki yake
aliyetekwa ambaye naamini ni
Olivia”akasema Gosu
Gosu.Wakatazamana kwa
sekunde chache
“Ninachokihitaji kwa sasa
ni kupata silaha..”akasema Gosu
Gosu
“Usihofu kuhusu silaha
utapata kila aina ya silaha
unayoitaka”akasema Devotha
“Good.Kingine ninachohitaji
ni kuipata ramani ya jengo
lilivyo hadi kufika mahala alipo
Mathew naamini unalifahamu
vyema jengo hilo” akasema
Gosu Gosu wakaelekea katika
maktaba ndogo hapo nyumbani
kwa Mathew naDevotha
akaanza kuichora ramani ya
jengo lile ilivyo.Gosu Gosu
akakumbuka kitu
“Ulisema mtu aliyekusaidia
kudukua simu ya rais yuko
hapa?Gosu Gosu akauliza
“Ndiyo anaitwa Saada.Ni
mtaalamu sana wa mambo
hayo”
“Huyo anaweza akawa na
msaada mkubwa kwetu.Ulisema
jengo hilo lina kamera za
ulinzi.Nitahitaji mtu wa
kudukua mtandao wenu ili
kucheza na kamera za ulinzi
zilizomo humo ndani
kutuwezesha kuingia bila
kujulikana.Unadhani Saada
anaweza akaifanya hiyo
kazi?akauliza Gosu Gosu
“Ndiyo anaweza” akasema
Devotha na Saada
akaitwa.Devotha akamueleza
kila kitu wanachotaka
kukifanya.Saada akawasha
kompyuta yake akajaribu
kuingia katika mtandao wa
idara yao lakini hakufanikiwa
“Kuna tatizo” akasema
Saada
“Kuna tatizo gani? akauliza
Devotha
“Namba zangu za siri za
kuingilia katika mtandao wa
idara zimebadilishwa na siwezi
kuingia tena” akasema Saada
“Nilitegemea kitu hicho
kutokea.Wamebadilisha kila
kitu nadhani lengo ni
kunidhibiti mimi.” akasema
Devotha
“Devotha wewe umekuwa
kiongozi wa idara hii naamini
lazima kuna watu ambao ni
watiifu kwako hata kama
litatokea jambo gani.Kuna
yeyote unayeweza kumpigia
akakusaidia kuingia katika
mtandao?akauliza Gosu
Gosu.Devotha akatafakari na
kusema
“Wapo kama watatu hivi
ambao naamini wako tayari
kwenda nami kaburini”
“Good.Tutatumia simu ya
humu ndani kumpigia mmoja
wao na utamuomba akusaidie
ili Saada aweze kuingia katika
mtandao wa idara yenu na
kufuatilia Kamera” akasema
Gosu Gosu na kwenda kuchukua
simu akampatia Devotha
akaziandika namba na kupiga
simu ikaanza kuita baada ya
muda ikapokelewa
“Hallow” ikasema sauti
upande wa pili baada ya
kupokea simu
“Zai tafadhali usistuke wala
kutamka jina langu” akasema
Devotha
“Baba shikamoo.Habari za
huko?akasema Zai huku
akisimama na kutoka mahala
alipokuwa akaenda kujificha
mahala kusiko na watu
“Hallo madam” akasema Zai
kwa sauti ndogo akiwa
amejifungia ndani ya chumba
Fulani
“Zai nina tatizo ninahitaji
msaada wako” akasema
Devotha
“Madam kuna nini?Imekuja
taarifa kwamba kuanzia sasa
nafasi yako imeshikwa na
Kaiza” “Zai kuna tatizo
limetokea nitakueleza siku
nyingine lakini kwa sasa kuna
msaada nahitaji”
“Nikusaidie nini
Madam?akauliza Zai
“Ninataka kuingia katika
mtandao wa idara.Namba zangu
zimebadilishwa nataka
unisaidie kuifungua kadi yangu
ambayo huwa ninaitumia hadi
nyumbani kwangu”
“Madam hilo ni jambo la
hatari sana wanaweza
wakagundua ni mimi
niliyekusaidia nikajiweka katika
matatizo makubwa”
“Usiogope Zai.Siku zote
nimekuwa kinga yako hata pale
ulipoharibu kazi.Naomba na
mimi leo unisaidie hili jambo
dogo.Niunganishe katika
mtandao.Hakuna atakayejua”
akasema Devotha
Zai akafikiri kidogo na
kusema
“Sawa madam naomba
namba yako ya kadi”
Devotha akamtajia namba
za kadi yake,Zai akaenda katika
chumba Fulani kulikokuwa na
kompyuta nyingi akakaa katika
kompyuta moja na kuanza
kuifanya kazi ile baada ya
dakika tano akampigia simu
Devotha
“Madam tayari kadi yako
nimeifungua.Ninaomba itumie
ndani ya saa mbili tu kisha
haitafanya kazi tena.Kama kuna
kitu ambacho unataka
kukifanya basi kifanye ndani ya
muda huo kabla ya muda
niliouweka kumalizika.Namba
za siri utakazotumia kuingia
katika mtandao wetu ni Alpha-
Bravo-660”
“Zai nakushukuru sana”
akasema Devotha na kukata
simu akampatia Saada zile
namba za siri akaingiza
wakafanikiwa kuingia katika
mtandao wa idara ya siri ya
usalama wa nchi.
“Good.Kinachofuata sasa ni
silaha”akasema Gosu Gosu
“Silaha tunazipata
nyumbani kwangu.Ninazo
silaha za kutosha” akasema
Devotha wakaingia katika gari
wakaondoka kuelekea
nyumbani kwa
Devotha.Waliingia haraka
haraka Gosu Gosu akachukua
silaha alizozihitaji kisha
wakaondoka
Kutoka nyumbani kwa
Devotha wakaelekea Lupai
hotel ambayo haiko mbali sana
na kitalu 1.Pale wakachukua
chumba na kumuacha Saada
“Saada utakaa katika
chumba hiki na utaongoza kila
kitu kutokea hapa” akasema
Gosu Gosu na kujaribu kifaa
alichokiweka sikioni kwa ajili ya
mawasiliano halafu akamgeukia
Devotha
“Devotha are you
ready?akauliza Gosu Gosu
“I’m ready” akasema
Devotha wakaingia garini na
kuondoka kuelekea kitalu
1.Devotha alikaa kiti cha mbele
na Gosu Gosu akajificha nyuma
akiwa na silaha.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 8
“Dr Alex nataka unieleze ni
nani uliyekuwa unawasiliana
naye kuhusu Olivia?Kaiza
akamuuliza Dr Alex aliyekuwa
amekestishwa kitini
amefungwa mikono.
“Nina binti yangu anaitwa
Olivia anasoma shule ya
Ukombozi
International,nilipaswa kwenda
kumchukua shuleni lakini
kutokana na kazi iliyopo hapa
sintaweza.Niliyekuwa
nawasiliana naye ni rafiki
yangu nilitaka kumuomba
aende shuleni akamchukue
mwanangu” akasema Dr
Alex.Kaiza akamtazama kwa
makini
Kaiza akachukua simu na
kumtaka DrAlex ampatie namba
za simu za mkuu wa shule
anakosoma mwanae halafu
akampigia simu
“Dr Alex kama
unanidangan….” Akasema Kaiza
na simu aliyopiga ikapokelewa
“Hallow” ikasema sauti ya
mwanamama upande wa pili
“Hallow.Hapo ni Ukombozi
international school?akauliza
Kaiza
“Ndiyo nikusaidie nini
tafadhali?
“Kuna mwanafunzi anaitwa
Olivia Alex anasoma katika
shule yako?
“Ndiyo anasoma katika
shule hii”
“Sawa ahsante sana”
akasema Kaiza na kukata simu
“Umeamini sasa? akauliza
Dr Alex akiwa amekunja sura
kwa hasira
“Samahani Dr Alex nilitaka
kuwa na uhakika,nilistuka
niliposikia ukimjulisha mtu
kuhusu Olivia nikadhani
unamuongelea huyu
mwanamke tuliyenaye ambaye
naye anaitwa Olivia”akasema
Kaiza “Naamini Olivia
atakuwa tayari muda
huu.Tunaweza kuendelea na
zoezi letu”akasema Kaiza
“Sina hakika sana lakini
tunaweza kuendelea” akasema
Dr Alex wakaelekea katika
chumba alimo Dr Olivia.Kaiza
akamsogelea karibu na
kumuita..
“Olivia..!.Olivia ! ..Olivia
hakuinua hata ukope.
“Dr Alex are you sure she’s
okay?akauliza Kaiza.Dr Alex
akachukua kipimo akampima
halafu akamgeukia Kaiza
“Kaiza naomba tuahirishe
zoezi hali ya Olivia si nzuri”
“Dr Alex nimekwisha
kueleza umuhimu wa huyu mtu
hivyo jitahidi kufanya kila
linalowezekana kuhakikisha
anakuwa tayari kuhojiwa”
akasema Kaiza
“Naomba tumpe muda zaidi
apumzike.Mwili wake bado
hauwezi kuhimili mateso
mengine zaidi na kama
mkilazimisha kutaka kumtesa
mtamuua na mtakosa kile
mnachokitafuta kutoka kwake”
akasema Dr Alex.Kaiza
akaitazama saa yake halafu
akasema
“Dr Alex ninaongeza saa
moja pekee.Jitahidi ndani ya
huo muda awe amekuwa tayari
kuhojiwa.Kama ndani ya saa
moja hatakuwa tayari tutafanya
tunavyojua sisi” akasema Kaiza
na kutoka ndani ya kile chumba
akamuacha Dr Alex peke
yake.Jasho lilikuwa linamtoka
“Nilitaka kuharibu kila
kitu.Hawa jamaa hawana imani
na mimi na wananifuatilia.Kuna
kitu wamekwisha
kihisi.Natakiwa kuwa makini
sana” akawaza Dr Alex akifuta
jasho lililokuwa linamtoka
usoni
“Nashukuru nilimpata
Mathew Mulumbi ingawa
sikumueleza chochote
kuhusiana na Olivia hawa jamaa
wakaniwahi lakini naamini
atakuwa amefahamu Olivia
yuko katika matatizo kwani
sikuikata simu makusudi ili
aweze kusikia kila
kilichotokea.Tatizo ni kufahamu
mahala alipo Olivia.Siwezi tena
kuwasiliana naye
kumfahamisha zaidi kwani simu
yangu wameichukua hawa
jamaa.Natakiwa kutafuta
namna nyingine ya kuhakikisha
ninamsaidia Olivia.Nilimchoma
dawa kumfanya awe dhaifu ili
hawa jamaa wasiweze kumtesa
natakiwa kuendelea kutafuta
mwanya wa kumuokoa Olivia
ndani ya saa moja alilotoa
Kaiza” akawaza Dr Alex.
Kaiza alitoka ndani ya kile
chumba akawaita vijana wake
wakaenda kukaa katika chumba
cha kupumzikia
“Simuamini kabisa huyu
DrAlex.Nataka tumuelekezee
macho kila
anachokifanya.Nataka mtu
mmoja akae katika chumba
alimo Olivia ili kufuatilia kila
kinachoendelea.Ninahisi kuna
mchezo unaendelea
hapa”akaelekeza Kaiza na
kuwapanga vijana wake mara
simu yake ikaita akaipokea
“Deo kuna taarifa
gani?akauliza
“Kaiza nimepokea taarifa
kutoka kitalu 2 kuna jambo
limetokea”
“Kumetokea nini?Devotha
amepatikana?akauliza Kaiza
“Hapana mkuu”
“Sasa kumetokea nini?
“Nimejulishwa kuwa wale
makachero niliowaweka kitalu
2 kwa ajili ya kumkamata
Devotha wameshindwa
kuifanya kazi ile na badala yake
wote wamekutwa wamefungwa
katika ofisi ya Devotha”
Kaiza akashusha pumzi
“Watu watatu
wameshindwaje kumkamata
Devotha? Deo nimekuteua uwe
msaidizi wangu kwa muda
hivyo huu ni mtihani wako wa
kwanza,nataka nitakapomaliza
hapa niwe tayari nimepata
taarifa za kukamatwa
Devotha.Sitaki kusikia eti
mmeshindwa kumkamata yule
mwanamke.Tunao watu wengi
wenye uwezo
mkubwa,tengeneza timu nzuri
ya watu ambao unaamini
wataweza kumpata
Devotha.Sitaki hadi machweo
yanaingia Devotha awe bado
hajapatikana.Umenisikia Deo?
“Nimekusikia mkuu”
“Good.Jipange vizuri
kumsaka Devotha.Nimekuteua
uwe msaidizi wangu kwa kuwa
naufahamu uwezo wako hivyo
achana na kila kitu na uelekeze
nguvu katika suala moja tu la
kumtafuta Devotha.Wekeni
mitego kila sehemu kuanzia
nyumbani kwake hadi sehemu
zote anazopenda
kutembelea.Wataarifu walinzi
katika vitalu vyote waimarishe
ulinzi na ikitokea Devotha
akaenda katika kituo chochote
akamatwe mara moja” akasema
Kaiza na kukata simu
“Damn ! Watu watatu
wameshindwaje kumkamata
yule mwanamke? Kwa uzembe
wao sasa Devotha
ameshafahamu anatafutwa na
kuifanya kazi ya kumkamata
iwe ngumu zaidi.” akawaza
Kaiza
“Kwa vyovyote vile lazima
Devotha apatikane.Kama
lisingekuwa hili suala la Olivia
ningemtafuta mimi mwenyewe
na kuhakikisha anapatikana
lakini ninashughulikia suala
muhimu sana na nilimuahidi
rais siku haitakwisha leo kabla
Olivia hajafunguka.Ninazidi
kuchanganyikiwa muda
unavyokimbia na bado sijapata
chochote kutoka kwake.Zoezi
linazidi kuwa gumu kutokana
na hali ya Olivia kutokuwa ya
kuridhisha.Naamini baada ya
saa moja atakuwa amerejea
katika hali yake ya kawaida na
leo ni leo lazima atasema ukweli
wote”akaendelea kuwaza.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 9
Dr Neerav patel daktari
bingwa wa figo akiwa ameshika
faili mkononi alitembea haraka
haraka akaingia ndani ya jengo
kubwa la ghorofa sita ambalo
lina wodi maalum wanazokaa
watu wenye uwezo mikubwa
kifedha na viongozi wa
serikali.Katika jengo hili ndiko
alikokuwa amelazwa Coletha
mtoto wa Rais Dr Evans.Dr
Neerav alikwenda hadi katika
lifti na kubonyeza namba sita
akielekea katika ghorofa ya juu
kabisa alikokuwa amelazwa
Coletha.Alikuwa peke yake
katika lifti akapanda hadi katika
ghorofa ya sita milango ya lifti
ikafunguka akashuka.Mara tu
aliposhuka akakutana na watu
wawili waliovaa suti wakiwa na
vifaa ambavyo walimkagua kila
anayeshuka katika lifti ili
kuthibitsha hana silaha.Dr
Neerav hakukaguliwa
akawaslimu wale wanausalama
akaenda zake.
Katika mfuko wa koti wa
upande wa kulia alipachika kitu
mfano wa nembo Fulani na
hakuna aliyekitilia maanani kitu
kile lakini ile ilikuwa ni kamera
ndogo ya siri yenye uwezo
mkubwa wa kuchukua picha
hata katika mazingira yenye
giza.kamera ile ilikuwa
inaendelea kuchukua picha na
kuzihifadhi. Kulikuwa na
walinzi kadhaa katika njia ya
kuelekea katika chumba
alimolazwa Coletha.Dr Neerav
alikaribia kufika katika chumba
cha mwisho kabisa ambamo
ndimo alimolazwa Coletha.kila
aliyekaribia chumba kile
alizuiliwa na maafisa usalama
na kuhojiwa
anakoelekea.Aliwapita akina
dada wawili waliokuwa
wamesimamishwa wakihojiwa
ambao walijitambulisha ni
marafiki wa Coletha.Dr Neerav
hakusimamishwa akawapita
maafisa wale wa usalama
waliopata wanne akaenda hadi
katika mlango wa chumba
alimolazwa Coletha ambao
ulikuwa wazi akaingia ndani ya
kile chumba na kumkuta
mwanadada mmoja aliyekuwa
amekaa katika sofa akitazama
runinga na katika kitanda alilala
msichana mmoja ambaye hata
bila kuambiwa alionekana ni
mgonjwa
“Karibu daktari” akasema
yule mwanadada aliyekuwa
amekaa sofani aliyeonekana ni
mlinzi wa Coletha
“Ahsante sana anaendeleaje
mgonjwa?akauliza Dr Neerav
“Hali yake inabadilika
badilika lakini daktari anasema
hakuna tatizo” akasema yule
mwanadada.Dr Neerav akaenda
katika kadi iliyokuwa katika
kitanda alicholala Coletha
akaisoma halafu akaaga na
kuondoka moja kwa moja
akaelekea katika lifti akaingia
na kushuka chini
kabisa.Alishuka katika lifti na
kutoka ndani ya lile jengo
akaelekea katika ofisi yake
iliyoko kitengo cha
figo.Akachukua simu yake
akapiga
“Hallow Dr Neerav”
akasema jamaa aliyepokea simu
“Fahad nimemaliza lile
zoezi”
“Good.Vipi ulinzi chini
ukoje?akauliza Fahad
“Nje ya jengo kuna walinzi
wawili waliovaa sare za
kampuni binafsi ya ulinzi
wakiwa karibu na mlango
mkuu wa kuingilia ndani ya
jengo.Kwa ujumla naweza
kusema hakuna ulinzi kwa
upande wa nje”
“Safi sana.Vipi kwa upande
wa ndani? Akauliza Fahad
“Kwa upande wa ndani
wapo walinzi kadhaa kwa
haraka haraka niliowaona ni
kama sita au saba hivi wote
wakiwa wamevalia mavazi yao
yale ya suti”
“Umefanikiwa kumuona
Coletha na kuhakikisha yumo
mle ndani?akauliza Fahad
“Nimeingia hadi katika
chumba alimolazwa
nimefanikiwa kuonana naye”
“Vipi hali yake?
“Hali yake hata kwa
kumtazama tu utagundua ni
mgonjwa.Nilikuwa na kamera
yangu nimechukua picha nyingi
nitazituma kwako ili uzipitie”
“Nashukuru sana Dr
Neerav.Naomba tafadhali
endelea kufuatilia kwa karibu
kama kutakuwa na mabadiliko
yoyote au kama atahamishwa
usiku wa leo tunakuja
kumchukua”
“Ninaendelea kufuatilia
Fahad na kama kutatokea
mabadiliko yoyote
nitakujulisha” akasema Dr
Karim na kukata simu
“Usiku wa leo Tanzania
itatikiswa tena pale
tutakapofanya shambulio katika
hospitali na kumchukua mtoto
wa rais.Naamini kabla ya kufika
asubuhi ya kesho rais atakuwa
ametujulisha mahala aliko
Edger Kaka.Olivia alikosea sana
kuamua kushirikiana na serikali
bila kujua kuwa tayari IS inao
mtandao mkubwa hapa nchini
ambao hakuna anayeufahamu
zaidi ya Edger Kaka.Edger Kaka
alipata mafanikio makubwa na
kujulikana hapa nchini bila
watu kujua kama kuna timu
nyuma yake
inayomnyanyua.Tutaitikisa nchi
hii hadi tumpate Edger”
akawaza Fahad
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 5
EPISODE 10
Devotha aliikaribia
barabara ya kuelekea kitalu 1.
“Saada ninakaribia kuingia
barabara ya kuelekea Kitalu
1.Kila kitu umekiweka
sawa?akauliza Devotha
“Kila kiti kiko sawa
madam.Utakapoingia katika
barabara ya kuelekea kitalu 1
nitazima kamera inayochukua
picha za kila gari linaloekea
katika geti.Hamtaweza
kuonekana hivyo mtaingia
ndani ya jengo kirahisi”
akasema Saada.
Baada ya dakika mbili
Devotha akamwambia Saada
“Ndani ya sekunde ishirini
nitakuwa nimeingia katika
barabara ya kuelekea kitalu1”
Tayari alikwisha washa taa
kuashiria kwamba anakata
kona.Sekunde chache kabla ya
kukata kona Saada akampa
taarifa kuwa tayari kamera
imezimwa na hawataonekana
“Thank you Saada” akasema
Devotha na kukata kona
akaingia katika barabara
inayoelekea katika jengo la
kitalu1.Akaichukua kadi yake
akaipachika katika kifaa Fulani
halafu akamgeukia GosuGosu
“Gosu Gosu kaa tayari.Kazi
inaanza” akasema Devotha
Alilikaribia geti
akakinyoosha kifaa kile
alichopachika kadi yake
akabonyeza namba kadhaa na
geti likajifungua.Gari la Devotha
likaingia ndani na geti
likajifunga taratibu.Kitendo cha
geti kufunguka na gari kuingia
ndani bila walinzi kuliona
katika kamera kiliwastua sana
na kuwafanya watoke ndani ya
nyumba yao kwa kasi wakiwa
na silaha.Devotha
akasimamisha gari baada ya
walinzi kumuelekezea
silaha.Akashusha kioo na
walinzi wote wakastuka
“Mama Devotha!! Walinzi
wake waliokuwa tayari na
silaha zao
wakashangaa.Devotha
hakuwasemesha kitu akavua
miwani yake na kuiweka
pembeni
“Madam tafadhali shuka
garini haraka! Akaamuru
mmoja wa walinzi wale
“Benard ! akaita Devotha
“Madam shuka garini
haraka sana” akasema Benard.
“Get out Devotha” akasema
Gosu Gosu kwa sauti
ndogo.Devotha akafungua
mlango na kushuka garini
“Geukia gari na uinue
mikono juu” akasema Benard
kwa ukali.Mmoja wa walinzi
akamsogelea Devotha kwa
lengo la kumfunga pingu lakini
Gosu Gosu aliyekuwa amejificha
katika kiti cha nyuma alikwisha
jiweka tayari na bastora mbili
mkononi.Walinzi wale
walijielekeza kwa Devotha bila
kuwa na taarifa kama kuna mtu
mwingine ndani ya gari.Kwa
kasi ya ajabu Gosu Gosu
akashusha kioo cha gari na
kuutoa mkono wake wenye
bastora iliyofungwa kiwambo
cha sauti akamlenga Benard
kati kati ya paji la uso
akaanguka chini.Kitendo kile
kilimpa Devotha nafasi
akageuka kwa kasi ya umeme
na kumtandika ngumi mfululizo
yule mlinzi ambaye tayari
alikwisha mfunga pingu mkono
mmoja akaanguka chini.Wakati
Devotha akiendelea kupambana
na yule jamaa Gosu Gosu tayari
alikwisha watanguliza kuzimu
wale walinzi wengine wawili
“Madam naomba msiniue
tafadhali” akasema yule mlinzi
aliyeanguka chini.
Devotha akamuamuru
kuinuka na kuwavuta wenzake
na kuwaficha katika vichaka vya
maua yaliyokuwa katika ukuta
wa kwanza.Devotha akasikia
mlio wa risasi kutoka katika
bastora yenye kiwambo cha
sauti.Akageuka haraka haraka
na kumkuta yule mlinzi akiwa
ameanguka chini akivuja
damu.Gosu Gosu alimpiga risasi
“Hakukuwa na ulazima wa
kumuua,hakuwa na madhara
yoyote”akasema Devotha
“I’m a soldier and any
soldier is trained to kill
enemies.Ndani ya jengo hili kila
mtu ni adui yangu hivyo nitaua
kila nitakayekutana naye hadi
nitakapompata Mathew
Mulumbi” akasema Gosu Gosu
“Hata macho yake
yanaonyesha kweli ni muuaji”
akawaza Devotha akimtazama
Gosu Gosu usoni.
“Saada tumemaliza hapa nje
tunaelekea ndani” akasema
Devotha wakaelekea katika gari
na kulivuka geti la pili ambalo
alilifungua kama alivyofungua
geti la kwanza.Hakukuwa na
mlinzi yeyote katika geti la pili
“Saada tunakwenda katika
maegesho chini ya jengo”
Devotha akamjulisha Saada
“Tayari nimezima kamera
ya eneo la maegesho” akasema
Saada
Devotha aliingiza gari
katika maegesho yaliyokuwa
chini ya lile jengo.Akafungua
mlango na kushuka.Gosu Gosu
akachukua silaha zake
akaziweka kwenye begi na
kubakiwa na bunduki mbili
ndogo alizozishika
mkononi.Devotha alikuwa na
bastora moja.
“Saada tuko maegesho
tunaelekea ghorofani katika
chumba iliko lifti
itakayotushusha chini aliko
Mathew.Zima kamera katika
lifti tunaelekea huko” akasema
Devotha wakiwa katika
mlango.Akapitisha kadi na
mlango ukafunguka.Kulikuwa
kimya kabisa.
“Saada updates
please.Tunakaribia chumba cha
lifti.Kuna walinzi wangapi
unawaona karibu?akauliza
Devotha
“Sioni mlinzi yeyote”
akasema Saada
“Good” akajibu Devotha
Katika chumba kilichokuwa
na runinga kubwa mbili,picha
kutoka katika kamera zote
zilizozunguka eneo lile la kitalu
1 zilionekana.Watu wanne
waliokuwamo ndani ya kile
chumba waliendelea na
shughuli zao kama kawaida
huku wakizungumza na kupata
vitafunwa mara mmoja
aliyekuwa amekaa kiti namba 4
akastuka ghafla baada
kugundua kuna kitu hakiko
sawa katika kamera.
“Guys something is not
right” akasema
“Kuna nini Cosmas?akauliza
mwenzake
“Kuna kitu kimenishangaza
kidogo” akasema Cosmas
“Camera 5 ambayo iko
katika maegesho kubwa
haikuwa ikionyesha picha lakini
sekunde chache zilizopita
imerejea na kuanza kuonyesha
tena picha” akasema Cosmas
“Cosmas is right.Kuna kitu
kweli hakiko sawa.Kamera 7A
ambayo ni ya kwenye lifti pia
haionekani hapa” akasema
mwingine
“What’s
happening?akauliza Cosmas
Haraka haraka kila mmoja
akakaa katika kiti chake
wakaanza kutafuta chanzo cha
tatizo.Baada ya muda Charles
akasema
“Kuna mtu amejiunga na
mtandao wetu na ndiye
anayeziongoza kamera zetu”
akasema Charles aliyegundua
tatizo lile huku akiendelea
kubonyeza kompyuta yake.
“Inaonyesha mtu huyu
hayuko mbali na
hapa.Inanionyesha yupo…oh
wait a second”akasema na
kuendelea kubofya kompyuta
yake
“Mdukuaji yuko
hapa”akasema Charles
“Lupai hotel ?! akauliza
Cosmas kwa mshangao
“Ni nani huyo anayeweza
kufanya hivi? Nini
anakitafuta?akauliza
“Kaiza anatakiwa ajulishwe
haraka jambo hili” akasema
Charles na kuchukua simu
akampigia Kaiza lakini simu
iliita bila kupokelewa
“Kaiza hapokei simu”
akasema
“Tunatakiwa kumtafuta
mtu huyo ni nani na kumtia
nguvuni ili tujue sababu za
kudukua mtandao wetu.Kama
Kaiza hapokei simu tumjulishe
Deo ambaye ndiye msaidizi
wake wa muda.Yeye anaweza
akatuma timu ya watu wakafika
hapo hotelini haraka” akashauri
Cosmas na Charles akampigia
simu Deo
“Hellow Charles” akasema
Deo
“Deo kuna tatizo”
“Tatizo gani Charles?
“Tumegundua kuna mtu
anadukua mtandao
wetu.Amekuwa anacheza na
kamera zetu”
“Mmemfahamu ni nani?
“Bado hatujafahamu ni nani
ila amejiunga na mtandao wetu
kutokea mbali.Tumefuatilia
mahala alipo na kugundua yuko
Lupai hotel ambayo haiko mbali
na hapa”
“Good job
Charles.Endeleeni kumfuatilia
mimi na timu yangu tunaelekea
hapo Lupai kumtafuta huyo
mtu.One more
thing,mmegundua sababu ya
kudukua kamera zetu?
“Bado hatujui tunaendelea
na uchunguzi” akasema Charles
“Endeleeni kufanya
uchunguzi.Yawezekana huu
ukawa ni mchezo wa
Devotha.Jambo kama hilo
haliwezi kufanywa na mtu wa
kutoka nje lazima linafanywa na
mtu wa ndani.Hakikisheni ulinzi
unaimarishwa kila
kona.Mathew Mulumbi
ahamishwe mahala alipo na
apelekwe seli 12B” akaelekeza
Deo na kukata simu.
Devotha na Gosu Gosu
waliingia katika lifti na kuelekea
ghorofa ya tano iliko lifti
itakayowapeleka chini aliko
Mathew Mulumbi
“Guys we have
problem.Kuna watu wanne
ghorofa ya tano wanasubiri
lifti,wana silaha” Saada
akawajulisha akina Devotha
GOSU GOSU NA DEVOTHA
WANAUNGANA KUMUOKOA
MATHEW MULUMBI JE
WATAFANIKIWA?OLIVIA
ATAFANIKIWA
KUKOMBOLEWA? ENDELEA
KUFUATILIA SIMULIZI HII
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 6
EPISODE 1
Devotha akagueka na
kumtazama Gosu Gosu baada ya
kupewa taarifa ile na Saada.
“Don’t panic.Niachie mimi
hiyo kazi,nitawamaliza wote”
Gosu Gosu akamweleza Devotha
“Gosu Gosu nakuomba
jitahidi kujizuia kuua hadi pale
itakapolazimu.Hawa ni watu
wangu nimekuwa nao muda
mrefu kama ndugu hivyo
sipendi kuwaua
hovyo.Sikufurahi ulivyoua wale
walinzi getini” akasema
Devotha
“Kaa nyuma yangu let me
handle this!! akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu
please..”akasisitiza Devotha
lakini Gosu Gosu hakusema
chochote alikuwa amejiweka
tayari kukabiliana na watu
wale.
“Madam Devotha tayari
nimezima kamera ya nj….”
Saada akamtaarifu Devotha
lakini kabla hajamaliza maelezo
yake milango ya lifti ikajifungua
na kwa wepesi wa aina yake
Gosu Gosu akaruka nje na
kuwastua wale jamaa wanne
waliokuwa na silaha wakisubiri
kuingia katika lifti.
“Taratibu wekeni silaha
zenu chini na kila mmoja ainue
mikono juu!! Akaamuru Gosu
Gosu.Wale jamaa walipatwa na
mstuko mkubwa
sana,walimtazama Gosu Gosu
kama wamekutana na dudu la
kutisha.Sura yake alikuwa
ameikunja,macho na sauti yake
vilitosha kuonyesha kuwa
hakuwa na mzaha na angeweza
kutoa roho ya mtu muda
wowote
“Fanyeni
mlivyoamriwa.Wekeni silaha
zenu chini” Devotha akasema
naye akiwa na sura
iliyoonyesha hakuwa na
masihara.Taratibu wale jamaa
watatu waliokuwa na bunduki
kila mmoja akaiweka chini
silaha yake na ghafla kwa kasi
ya aina yake mmoja ambaye
hakuwa na bunduki akachomoa
bastora lakini Gosu Gosu
aliyekuwa na jicho kama la
kinyonga alikiona kitendo kile
akaizinga bunduki yake na
kumchakaza yule jamaa kwa
risasi.Wale jamaa watatu
waliobaki walitetemeka kwa
woga.
Haraka haraka Devotha
akatumia kadi yake akafungua
mlango uliokuwa karibu
akawaamuru wale jamaa
kuingia na kuuingiza pia mwili
wa yule mwenzao aliyeuawa na
GosuGosu.Kwa kutumia waya
wale jamaa wakafungwa miguu
na mikono.Gosu Gosu akakata
mashati yao na kujaza vitambaa
midomoni mwao.
“Tunaelekea wapi baada ya
hapa?akauliza Gosu Gosu
“Kuna sehemu mbili
ambazo tunatakiwa
kudhibiti.Kwanza chumba cha
kamera na pili kuna chumba
kinaitwa control room.Humo
ndimo kuna mifumo yote ya
kuongoza kila kitu ndani ya hili
jengo” akasema Devotha
“Hakuna tatizo nielekeze
njia ya kufika huko”
“Tutaanzia chumba cha
Kamera” akasema Devotha
“Saada tunaelekea katika
chumba cha kamera” Devotha
akamjulisha Saada
“Sawa Madam Devotha
hakuna tatizo lolote mnaweza
kwenda njia zote naona ni
nyeupe” akasema Saada
Gosu Gosu akafungua
mlango akachungulia nje
hakukuwa na mtu yeyote.
“It’s clear ! akasema kisha
akatangulia na Devotha
akamfuata nyuma
Katika chumba cha kamera
zoezi la kumfuatilia mdukuaji
lilikuwa linaendelea.Kamera
ziliendelea kuzimwa na
kuwashwa tena baada ya muda
mfupi wote wakazidi kushangaa
“Nini hasa lengo la huyu
mdukuaji?Kwa nini anazima na
kuwasha kamera zetu?akauliza
Charles
“Guys hapa kuna jambo
linaendelea.Angalieni mtiririko
a namna kamera
zinavyozimwa.Ukifuatilia
utaona imezimwa kwanza
kamera ya maegesho kubwa
chini ya jengo. Ikafuata kamera
7A ambayo ni kamera iliyoko
ndani ya lifti,ikazima tena
kamera 12CC iliyoko katika
korido ghorofa ya tano.Kuna
kitu mnakiona hapa?akauliza
Charles
“Kuna jambo hata mimi
ninaliona hapa.Hizi kamera
haziwezi kuzimwa bila kuwa na
sababu ya msingi.Huyu
mdukuaji anaonekana ni mtu
anayelifahamu jengo hili vyema
na kwa namna anavyozima
kamera zetu inaonekana kuna
jambo analificha
lisionekane.Tunatakiwa
kufahamu anaficha kitu
gani?akauliza Charles
“Jamani tuko kwenye
hatari.Huyu mdukuaji atakuwa
anawaficha wavamizi ndiyo
maana utaona mtiririko wake
wa kuzima kamera ameanza na
ile ya chini kabisa ya jengo.Ili
kujihakikishia kuwa kweli
tumevamiwa chunguza kama
kamera ya getini iliwahi
kuzimwa.Tumeanza kustuka
kuwa kamera zinazimwa katika
kamera ya
maegesho.Yawezekana …….”
akasema Jonathan na kustuliwa
na sauti ya mshangao ya
Charles
“It’s true.Anachokisema
Jonathan ni kitu cha kweli
kabisa.Kamera mbili zilizimwa
kabla ya ile tuliyoanza
kuigundua.Kama alivyosema
Jonathan yawezekana tuko
kwenye hatari.Yawezekana
kweli kuna uvamizi
unafanyika..” akasema Charles
na mara Cosmas akatoa sauti ya
mstuko
“Oh my God !!.
“Nini Cosmas?akauliza
Charles
“Mathew Mulumbi !
Tunamshikilia hapa na
anahisiwa kushirikiana na
mtandao wa IS.Kama kuna
wavamizi ni wazi watakuwa
wamekuja kwa lengo la
kumkomboa yeye tu hakuna
kingine” akasema Cosmas.Wote
mle ndani ya chumba
wakatazamana.Walipatwa na
mstuko.
“Jamani kama ni wavamizi
wamewezaje kupita
getini?Huwezi kuvuka getini
kama si mmoja wetu
,kamahaupo katika mfumo
wetu”akasema Steven
“Fuatilia getini kama kuna
mtu yeyote amepita hapo muda
mfupi uliopita” akasema
Cosmas.Charles akapiga simu
getini lakini
haikupokelewa,akapiga tena
lakini hali ilikuwa ile ile simu
haikupokelewa.
“Simu haipokelewi.Hii
inashangaza sana kwa watu wa
getini kutokupokea simu”
“Jibu ni jepesi tu kwamba
hakuna mtu getini” akasema
Jonathan
“Where are they?akauliza
Steve sauti yake ikionyesha
woga mkubwa
“May be they’re
dea……………….” Kabla Charles
hajamaliza kile alichotaka
kukisema mlango ukafunguka
wakaingia watu
wawili.Alitangulia Devotha na
nyuma yake akafuata Gosu Gosu
aliyekuwa na bunduki mbili
ndogo zilizofungwa kiwambo
cha sauti.Ulikuwa ni mstuko
mkubwa kwa wale watu mle
ndani ambao hawakuutarajia
“Tafadhali kaeni mbali na
kompyuta zenu na kila mmoja
ainue juu mikono yake”
akasema Devotha aliyekuwa na
bastora mkononi.
“Madam Devotha!!
Akasema Charles
“Mmesikia
mlichoambiwa.Kila mmoja
ainue mikono yake juu haraka
sana!! Akasema Gosu Gosu.
Ghafla Charles akarukia
ukutani na kubonyeza kitufe
chekundu ambacho ni kengele
ya kuashiria kuna hatari ndani
ya jengo.Taa nyekundu
iliyokuwa juu ikaanza kuwaka
na mlio wa king’ora
ukasikika.Mkono wa Gosu Gosu
ulikuwa mwepesi sana kabla
Charles hajageuka baada ya
kubonyeza ile kengele tayari
alikwisha izinga bunduki yake
na kumimina risasi.Charles
akaanguka chini.Hakuwa na
uhai tena.Haraka haraka
Devotha akaenda katika kifaa
Fulani chenye namba
akabonyeza namba kadhaa na
ile kengele ya hatari ikatoweka.
“Nawaonya! Yeyote
atakayejifanya mjuaji na kutaka
kufanya kinyume na maelekezo
atapoteza maisha yake kama
Charles.Tafadhali fuateni
maelekezo mnayopewa!
akasema Devotha kwa ukali
“Madam Devotha Please
don’t kill us tutafuata
maelekezo yote.” akasema
Cosmas aliyekuwa
anatetemeka.Haraka haraka
Devotha akakata waya na
kuwafunga wote mikono na
miguu wakawaziba midomo na
kuwafungia katika chumba
kilichokuwa pembeni .
“Gosu Gosu we need to
hurry.Ile Kengele aliyoibonyeza
Charles ni kiashiria kwamba
kuna hatari ndani ya jengo.Kila
ofisi ina kengele hiyo ambayo
ikibonyezwa hupeleka taarifa
katika chumba kinaitwa control
room na taarifa ikifika pale
milango yote katika jengo hili
hujifunga.Taarifa pia hutumwa
kwa kikosi maalum ambacho
hushughulikia masuala ya
dharura pekee.Kikosi hiki
hukaa katika ghorofa ya tatu ya
jengo hili.Mara waipatapo
taarifa hiyo ya hatari hufuatilia
imetoka wapi na kufika hapo
haraka sana kujua tatizo.We
need to get out very quick
kwani hawa jamaa muda
wowote watafika hapa”
akasema Devotha akaenda
katika mlango akapitisha kadi
yake lakini mlango
haukufunguka.
“Tayari milango yote
imekwisha jifunga kama
nilivyokueleza” akasema
Devotha
“Hakuna namna yoyote ya
dharura ya kuweza kuifungua
milango ikitokea hali ya namna
hii?Gosu Gosu akauliza
“Hakuna namna nyingine
hadi kuwasiliana na watu walio
katika control room ndio pekee
wanaweza kufungua milango
inapotokea hali kama hii”
akasema Devotha
“Isiwe taabu Devotha”
akasema Gosu Gosu na kuvua
begi lake akatoa kifaa Fulani na
kukipachika katika mlango
halafu akamtaka Devotha
wasogee mbali kidogo
akakilenga kifaa kile kwa risasi
na ukatokea mlipuko mlango
ule ukasambaratika king’ora
cha hatari kikaanza kulia.
“Hurry let’s go!! Akasema
Devotha
“Hawa jamaa wataendelea
kutufuatilia katika kamera
mahala tunakoenda.We need to
destroy this room” akasema
Gosu Gosu na kutoa bomu dogo
la mkono katika begi
lake,akang’oa kifuniko chake
Devotha akachungulia nje
“It’s clear” akasema
Devotha,Gosu Gosu akasogea
mlangoni wakatoka nje ya kile
chumba halafu akalirusha lile
bomu dogo katika kile chumba
cha kamera likalipuka akawahi
kumkumbatia Devotha
wakaanguka chini.
“Tunakwenda control
room.Kushuka chini mahala
aliko Mathew lazima tushuke
kwa kutumia lifti na kwa sasa
hakuna lifti yoyote inayofanya
kazi hivyo lazima tuingie pale
control ro….” Devotha akastuka
baada ya kuchungulia na
kuwaona watu watatu
wakielekea mbio upande ule
waliokuwepo.Akamfanyia
ishara GosuGosu kuwa watu
watatu wanakuja.Walipokaribia
Gosu Gosu akajitokeza na
kucheza na bunduki zake mbili
wale jamaa wote wakaanguka
chini.Mara ikasikika milio ya
risasi
“Aaaagghh !!! Devotha
akatoa mguno wa maumivu
akaanguka chini.Gosu Gosu
akageuka na kumkuta Devotha
akiwa ameanguka chini akivuja
damu.
“Gosu Gosu take cover !!
Akasema Devotha na kwa
haraka Gosu Gosu akajificha
nyuma ya nguzo huku risasi
zikipiga upande wa pili wa ile
nguzo.Devotha aliyekuwa
amepigwa risasi katika bega la
kushoto akaivuta bastora yake
iliyoanguka sentimeta chache
na kwa kutumia mkono wake
wa kulia akaachia risasi kadhaa
na kuwafanya wale jamaa
waliokuwa wanawashambulia
wajifiche na risasi zikawa
zinarushwa kwa kuviziana,hii
ilimpa Gosu Gosu aliyekuwa
bado amejificha katika nguzo
nafasi ya kuwasoma wale jamaa
namna walivyokaa.Jamaa
mmoja akajitokeza ili aachie
risasi lakini akamkuta tayaro
Gosu Gosu amejiandaa
akamlenga kati kati ya paji la
uso akaanguka na bunduki yake
ikaruka pembeni.Gosu Gosu
akapata nafasi akaruka na
kumuendea
Devotha.Akamkagua alikuwa
amepigwa risasi katika bega la
kushgoto.
“Risasi haijatokeza upande
wa pili bado iko ndani” akasema
Gosu Gosu akavua begi
alilolivaa mgongoni akavua na
fulana yake aliyoivaa na kuweka
mahala alikopigwa risasi
Devotha
“Weka mgandamizo mahala
hapo ili kuzuia damu kutoka
kwa wingi.Tukimaliza zoezi hili
tutaitoa risasi hiyo” akasema
Gosu Gosu
“Thank you Gosu
Gosu.Tunatakiwa kuhakikisha
tunafika control room haraka”
akasema Devotha na Gosu Gosu
akamsaidia kunyanyuka.Mara
tu walipojitokeza katika korido
zikaanza kuvuma risasi.Gosu
Gosu akamkinga Devotha kwa
kuachia risasi mfululizo
wakarejea mahala walipokuwa
wamejificha.
“Sikiliza Devotha hawa
jamaa wamekwisha
jipanga.Hakuna njia nyingine ya
kufika huko control room?
“Hakuna njia nyingine zaidi
ya hii”
“Good” akasema Gosu Gosu
na kufungua begi lake akatoa
kopo akang’oa kifuniko chake
na kulirusha katika
korido.Moshi mzito mweusi
ukaanza kutoka katika lile kopo
na kusambaa.Akatoa lingine na
kulirusha mbele zaidi na baada
ya muda mfupi eneo lote likawa
na moshi mzito kiasi cha
kutoweza kumuona mtu aliyeko
mbele yako.Gosu Gosu alikuwa
amejiandaa akavaa miwani
yenye kifaa maalum ya
kumuwezesha kuona sehemu
zenye giza na katika moshi
mzito.Gosu Gosu akamtaka
Devotha aendelee kukaa pale
pale.Akatembea kwa kunyata
kuelekea upande ule ambako
wale jamaa walikuwa
wamejificha.Alipokaribia
aliwaona jamaa watatu wakiwa
wamejibanza katika uchochoro
uliokuwa na dirisha.Gosu Gosu
hakupoteza muda ndani ya
sekunde chache akawakata
pumzi kwa risasi
mfululizo.Haraka haraka
akamfuata Devotha
“It’s clear.Twende”
akasema Gosu Gosu na
kumuinua Devotha wakaanza
kutembea taratibu hadi
walipokunja kona na kufuata
korido la upande wa kulia kisha
wakafuata korido la kushoto na
hatua chache ikasikika milio ya
risasi Gosu Gosu akamvuta
Devotha pembeni.Kulikuwa na
watu mbele yao
wakiwashambulia.Gosu Gosu
alitumia zaidi ya dakika tano
kupambana na watu wale
wanne akawamaliza kisha
akamuongoza Devotha hadi
katika lile lango ambalo lilikuwa
limefungwa.Akatoa kifaa kama
kile alichokitumia katika
chumba cha kamera
akakipachika mlangoni kisha
akakipiga risasi na lango
likafunguka akarukia ndani
ambako kulikuwa na
mkanyagano mkubwa baada ya
mlipuko ule kutokea mlangoni
kila mtu akikimbia kunusuru
maisha yake.Gosu Gosu akapiga
risasi juu na kutaka watu wote
watulie.Mle ndani kulikuwa na
zaidi ya watu kumi na
tano.Devotha akaingia na
kumuita Zai ambaye ndiye
aliyemsaidia kumuunganisha
tena na mtandao wa idara
akamtaka afungue milango
yote.Zai akakaa kitini na
kubonyeza kompyuta yake
baada ya muda milango yote
ikaanza kufunguka.Devotha
akawataka wale watu kutoa kila
walicho nacho na kutupa chini
halafu akawataka waingie
katika chumba kilichokuwa
pembeni.Akamtaka Zai aufunge
ule mlango kupitia kompyuta
yake ili isiwe rahisi kwa
waliokuwa ndani
kuufungua.Gosu Gosu bado
alikuwa mlangoni tayari
kukabiliana na chochote
ambacho kingejitokeza.Milango
yote ilipofunguka na kila kitu
kurejea kawaida Devotha
akamtaka Zai awafuate
wakatoka ndani ya kile chumba
wakaelekea katika lifti kushuka
chini.Milango ya lifti ikafunguka
wakatoka na Devotha
akawaongoza Gosu Gosu na Zai
kuelekea katika chumba cheupe
“Wakati ninaondoka
Mathew alikuwa huku niliagiza
atolewe apelekwe katika
chumba kingine.Tuanzie huku
kwanza kutazama kama
alihamishwa” akasema
Devotha.Milango yote ilikuwa
wazi wakaelekea katika chumba
cheupe lakini Mathew
hakuwepo
“Watakuwa
wamemuhamisha Mathew
kama nilivyoelekeza.Twendeni
VIP” akasema Devotha
wakatoka ndani ya chumba kile
walipopiga hatua chache milio
ya risasi ikasikika.Gosu Gosu
akamrukia Devotha
akamuangusha chini na
kugeuka kwa kasi ya ajabu
akawaona watu wanne wakiwa
na silaha akamimina risasi
wawili wakaanguka chini
wawili wakakimbia kuelekea
katika lifti.Kabla hawajaingia
mmoja wao akapigwa risasi ya
mguu mwenzake akageuka
akavurumisha risasi halafu
akamvuta yule aliyepigwa risasi
akamungiza ndani ya lifti
akaendelea kuvurumisha risasi
kuwazuia akina Gosu Gosu
kupiga risasi yoyote.Milango ya
lifti ikajifunga na lifti ikapanda
juu.Baada ya wale jamaa wawili
kunusurika na kuondoka,Gosu
Gosu akamuendelea Zai
aliyekuwa amelala chini akivuja
damu akamgeuza lakini Zai
hakuwa na uhai tayari alikwisha
fariki alikuwa amepigwa risasi
nyingi kifuani.
“She’s gone” Gosu Gosu
akamwambia Devotha ambaye
alikosa cha kuongea akabaki
anamtazama Gosu Gosu
“Devotha watu wale tayari
wanafahamu tuko huku chini
hivyo wanapeleka taarifa kwa
wenzao na muda wowote
wanaweza wakaja wengi
tukashindwa kupambana
nao.Tumtafute Mathew haraka
tuondoke eneo hili”akasema
Gosu Gosu
“Nimeumia sana Gosu
Gosu,mimi ndiye nimesababisha
kifo cha Zai.Najuta kwa nini
nilimtumia” akasema Devotha
“Devotha hakuna
tunachoweza kukifanya kwa Zai
tayari amekwisha kufa.Our
priority is Mathew Mulumbi”
akasema Gosu Gosu na
kumfuata Devotha akamuinua
wakaelekea katika sehemu
ambako alielekeza Mathew
apelekwe.Lango la kuingia
katika sehemu ya VIP lilikuwa
wazi wakaingia ndani na
kuingia katika kibao
kimeandikwa A3.Mle ndani
kulikuwa na watu watatu
wenye silaha wakiwa
wamemzunguka Mathew
aliyekuwa amefungwa pingu
mkononi
“Wekeni silaha zenu chini
ni mimi Devotha” akasema
Devotha.Mmoja wao
akauelekezea mtutu wa
bunduki kichwani kwa Mathew.
“Madam Devotha tayari
tunakufahamu wewe ni
nani,tafadhali naomba usimame
hapo hapo usijaribu kunyanyua
hata hatua moja.Taratibu wewe
na mwenzako wekeni silaha
zenu chini !! akasema kwa sauti
kali mmoja wa wale jamaa
“Evans kama kuna kitu
umeambiwa kuhusu mimi
wamekudanganya.Unanifahamu
vizuri mimi nimekuwa kiongozi
wenu mnanifahamu
vizuri.Tafadhali ondokeni hapo
nataka kuzungumza na
Mathew”
“Madam tafadhali fanya
nilivyokuelekeza ama sivyo
Mathew atakufa.Tunajua
ulichokuja kukifanya huku chini
ni kumtorosha.Tunayo maagizo
ya kumlinda Mathew kwa
gharama zozote.Nitahesabu
hadi tatu nataka muweke silaha
zenu chini !! akasema Evans
kwa ukali.
“Okay tunaweka silaha zetu
chini” akasema Devotha na
kuanza kuinama chini taratibu
kuweka bastora yake.Gosu Gosu
aliyekuwa karibu na Devotha
alifanya kitu cha ghafla sana
ambacho wale jamaa
hawakukitegemea,alimsukuma
Devotha akaanguka naye chini
huku akimimina risasi jamaa
wawili wakaanguka,Mathew
aliyekuwa amekaa sofani
alijibinua akaanguka na kiti
kisha akaipiga teke ile bunduki
iliyokuwa imeelekezwa
kichwani kwake,akajibinua
zaidi na kumtandika yule jamaa
teke la shingo akayumba na
kuanguka akamkaba kabali kwa
miguu yake hadi yule jamaa
alipokata pumzi akamuachia.
“Mathew are you okay
brother? Gosu Gosu akamuuliza
Mathew
“Gosu Gosu you are a ghost
! sikutegemea kabisa kukuona
mahala hapa” akasema
Mathew.Hakuamini kabisa
kama angeweza kumuona Gosu
Gosu mahala pale.
“Nafurahi kukukuta ukiwa
mzima Mathew.Tutazungumza
zaidi baadae kwa sasa
tunatakiwa kutafuta namna ya
kuondoka katika hili shimo”
akasema Gosu Gosu huku
akizifungua pingu alizofungwa
Mathew kwa kutumia kifaa
kidogo alichokitoa katika begi
lake
“Gosu Gosu thank you so
much” akasema Mathew
“Don’t thank me.Thank her
! akasema Gosu Gosu
akimuonyeshea Devotha.
Mathew akamfuata Devotha
pale chini alipokuwa
amekaa.Alikuwa amechafuka
damu.Bado aliendelea
kushikilia sehemu alikopigwa
risasi
“Devotha.Pole
sana”akasema Mathew
“Devotha amepigwa risasi
begani katika jitihada za kufika
hapa kukukomboa.Ni zamu yetu
kuhakikisha tunamtoa humu
salama na kumpatia
matibabu.Tayari
amekwishapoteza damu nyingi”
akasema Gosu Gosu
“Devotha we’ll get you out
of here I promise you” akasema
Mathew
“Guys ninahisi nguvu
zinaniishia.Tufanyeni haraka
tutoke humu.Kuna njia ya siri ya
kutoka huku.Hatutaweza kupita
kule juu wako wengi” akasema
Devotha.Mathew akamsaidia
akanyanyuka
“Mathew hawajakuumiza
hawa jamaa?Unaweza
kutembea?Gosu Gosu
akamuuliza Mathew
“Hawakunip amateso
makubwa zaidi ya kuniweka
katika chumba cha
baridi.Shukrani kwa Devotha
kwani yeye ndiye
aliyesababisha nisiteswe.Nina
deni kubwa kwake” akasema
Mathew.Devotha akaelekza
ufunguliwe mlango wa chooni
akaingia,Mathew akamfuata na
Gosu Gosu aliyekuwa kifua wazi
akiwa na bunduki zake mbili
ndogo akawa nyuma
kukabiliana na chochote.Ndani
ya kile choo kulikuwa na
kisanduku mfano wa tanki dogo
la maji limetundikwa
ukutani,Devotha akabonyesa
sehemu Fulani
likafunguka,akakibandua
kifuniko cheupe akakuta kitu
mfano wa simu akabonyeza
namba Fulani na mara ukuta
ukajiachia ikaonekana ngazi ya
kushuka chini.
“C’mon hurry up we need to
leave” akasema
Devotha.Mathew na Gosu Gosu
wakaingia haraka baada ya
kusikika hatua za watu
wakiingia mle
chumbani.Devotha akabonyeza
namba Fulani kwa ndani na ule
ukuta ukajifunga na haikuwa
rahisi kwa mtu kufahamu kama
nyuma ya ukuta ule kulikuwa
na njia.
“Njia hii ni ya siri na
ilitengenezwa maalum kwa ajili
ya kuwatorosha viongozi pale
watakapokuwa na matatizo.Njia
hii inakwenda kutokea karibu
na bahari.Wanaoifahamu njia
hii ni mimi na Ka……” Akasema
Devotha na kutaka kuanguka
Mathew aliyekuwa nyuma yake
akamdaka.
“Davotha..! Devotha !..”
Mathew akamuita lakini
Devotha hakuwa na
nguvu.Mathew akamlaza chini
na kumchunguza.
“She’s still
breathing.Tuharakishe tutoke
humu akapatiwe matibabu
haraka” akasema Mathew
“Mathew ni Devotha pekee
anayeifahamu njia.Tutafanyaje
kutoka huku chini?akauliza
Gosu Gosu
“Papii,it’s just you and I
now.We need to find a
way.Nitambeba Devotha”
akasema Mathew
“No Mathew I’ll do it”
akasema Gosu Gosu na
kumpatia Mathew zile bunduki
na lile begi kisha akambeba
Devotha wakaendelea kufuata
ujia ule ambao Devotha
aliwaeleza unakwenda kutokea
karibu na bahari.
“Mathew ninafahamu
namna ya kutoa risasi kwa nini
tusimtoe Devotha
risasi?akauliza Gosu Gosu
“Hata mimi ninao uwezo wa
kutoa risasi lakini Devotha
tayari amepoteza damu na
kama tukimtoa risasi kienyeji
ataendelea kupoteza damu
nyingi.Tunahitaji kumpeleka
hospitali akaongezewe damu na
kufanyiwa upasuaji kuondoa
risasi.Pili ni muda.Hatuna muda
mrefu wale jamaa wanaweza
wakatukuta hapa” akasema
Mathew
“Mathew are sure she’s
going to make it? Akauliza Gosu
Gosu
“Kama siku yake haijafika
hatapoteza maisha.Keep
moving” akasema Mathew.
Walitembea kwa takribani
dakika kumi na mbili kisha
wakakuta ngazi zinapanda na
baada ya kuzipanda ngazi zile
wakakuta kuna kifaa kama kile
walichokikuta chooni.
“Tumekwama.Huu ni
mlango wa kutokea nje lakini
hatujui namba za kufungulia
tuweze kutoka” akasema Gosu
Gosu
“Hatujakwama.Ninazifaham
u namba za
kufungulia.Nilimuona Devotha
wakati akifungua ule mlango
kule chooni na mimi nina sifa
moja ninapoziona namba hata
kama ni nyingi mara moja
huziweka kichwani” akasema
Mathew na kuzibonyeza namba
zile ambazo Devotha alizitumia
kufungulia mlango kule chooni
na taratibu lango likajifungua
wakatabasamu na kutoka
nje.Ilikuwa ni sehemu yenye
mwanga kandoni mwa bahari
na mlango ule ulitengenezwa
kwa mfano wa mwamba na
haikuwa rahisi kwa mtu kujua
kama katika mwamba ule
kulikuwa na mlango wa
kuingilia katika njia ya chini
kuelekea kwenye jengo la kitalu
1.Jengo lile waliliacha kwa kama
mita mia nne hivi.Dakika mbili
baada ya kutoka ndani ya ile
njia lango likajifunga
“Oh ahsante Mungu
tumetoka salama” akasema
Gosu Gosu
“Gosu Gosu we’re not safe
yet.Tunatakiwa kutafuta namna
ya kuondoka eneo hili,bado
tuko karibu sana na lile jengo la
hawa jamaa” akasema Mathew
“Mathew barabara haiko
mbali na hapa.Tuendelee na
safari.Nitambeba Devotha and
you’ll cover me”akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu hali ya
kiusalama kwa sasa hapa nchini
si nzuri matukio ya utekaji watu
yameshika kasi na watu
wakituona tukiwa katika hali hii
tutajiweka katika matatizo
mengine.Tazama
tulivyochafuka damu.Hatuna
simu wala chombo chochote
cha mawasiliano.Ninachofikiria
nenda katafute gari mimi
nitabaki hapa na Devotha”
akasema Mathew.Bila ubishi
Gosu Gosu akamuachia Mathew
silaha akaondoka kwenda
kutafuta usafiri wa kuondoka
nao.
“Sikutegemea kama
Devotha angeweza kuwageuka
wenzake na kuungana na Gosu
Gosu kuja
kuniokoa.Yawezekana amepima
na akagundua kwamba
walifanya makosa kunikamata
ndiyo maana akaenda
kumtafuta Gosu Gosu
wakashirikiana hadi
wakafanikiwa
kunikomboa.Haikuwa kazi
rahisi kuniokoa” akawaza
Mathew akimtazama Devotha
ambaye hakuwa na fahamu.
“Ee Mungu tafadhali
naomba umponye
Devotha.Amejitolea kuniokoa
kwa kuwa anafahamu umuhimu
wangu katika kuisaidia nchi
yangu dhidi ya hila na mipango
ya magaidi.Ninamuhitaji sana
katika kazi kubwa iliyoko mbele
yetu” Mathew akaomba kimya
kimya
Dakika chache baadae Gosu
Gosu akarejea akikimbia na
kumjulisha kuwa tayari
amepata gari wakasaidiana
kumbeba Devotha wakapanda
mwamba ule hadi juu ambako
Gosu Gosu aliegesha gari
wakamuingiza garini na Gosu
Gosu akaliondoa gari kwa kasi
“Umepata wapi hili
gari?akauliza Mathew
“Mwenye gari yuko kwenye
buti.Usihofu atakuwa huru
baada ya kazi yetu kumalizika.
Tunaelekea wapi?akauliza Gosu
Gosu
“Sehemu pekee ambako
tunaweza kumpeleka kwa sasa
ni kwa Dr Philip.Yule pekee
ndiye ninayemuamini anaweza
akamuhudumia Devotha kwa
siri” akasema Mathew
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 6
EPISODE 2
Deo akiwa na vijana wake
alifika Lupai hotel akampigia
simu Charles lakini simu
haikupokelewa.Akapiga tena
simu ikaita bila
kupokelewa.Akampigia Cosmas
lakini naye vile vile simu yake
ilita bila kupokelewa.
“Kuna nini kinaendelea
mbona hawapokei simu hawa
jamaa?akajiuliza Deo
akaendelea kuwapigia watu
zaidi ya watatu lakini wote simu
zao ziiita bila kupokelewa
“Kitu gani kinaendelea
kitalu 1? Mbona wote
hawapokei simu? akajiuliza Deo
na kuzidi kuingiwa na wasiwasi
akamgeukia mmoja wa watu
wake aliyekuwa naye garini
“Najaribu kuwasiliana na
kitalu 1 lakini hakuna
anayepokea simu.Kitu gani
kinaendelea kule?Tumekuja
hapa kumtafuta mtu
anayedukua kamera zetu na
ambaye kwa mujibu wa Charles
yuko hapa hotel
Lupai.Tutampataje mtu huyo
bila kupata msaada kutoka kwa
watu wetu kitalu 1? akauliza
“Ni vigumu kumpata mtu
huyo bila kupata msaada
kutoka kitalu1.Hoteli hii ni
kubwa ina vyumba vingi na
hatujui mdukuaji huyo yuko
chumba gani” akajibu yule
jamaa
“Nikweli,bila kupata
msaada wa watu wa kitalu 1
hatutaweza kufahamu mahala
alipo.Twendeni kitalu 1 tukajue
kinachoendelea kwa nini watu
wote hawapokei simu” akasema
Deo wakaondoka kuelekea
kitalu 1.
Katika chumba 86 ndani ya
hoteli Lupai ambamo
alikuwemo Saada,mawasiliano
kati yake na Devotha yalikatika.
“Sina kitu cha kufanya
hapa.Devotha hapatikani tena
simuni.Mara ya mwisho
nilichokisikia ni milio ya risasi
na baada ya hapo sijampata
tena Devotha.Nina wasiwasi
yawezekana tayari amekwisha
uawa.Natakiwa kuondoka hapa
haraka sana kabla
sijakutwa.Nina wasiwasi
wanaweza wakafuatilia na
kugundua niko hapa” akawaza
Saada huku akipakia kompyuta
yake katika mkoba akafungua
mlango na kuingia katika lifti
akashuka chini akaelekea zilipo
teksi akaingia katika mojawapo
ya teksi akamuelekeza dereva
ampeleke sehemu Fulani.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 6
EPISODE 3
Deo na timu yake waliwasili
katika geti la kuingilia kitalu 1
na kukuta kuna watu wawili
kutoka katika kikosi cha
dharura.Alistuka kwani si
kawaida kwa kikosi hiki kulinda
geti.Akashuka getini na kuuliza
kilichotokea na akaelezwa kila
kitu kilichokuwa kinaendelea
ndani ya jengo lile.Haraka
haraka akakimbilia ndani na
kukuta kukiwa na taharuki
kubwa.Kitu kikubwa alichotaka
kukifahamu ni kama Mathew
Mulumbi bado yupo.Alihisi
kuishiwa nguvu baada ya
kujulishwa kwamba Devotha
ndiye aliyefanya uvamizi ule na
lengo lake kubwa ni kumuokoa
Mathew Mulumbi.Kulikuwa na
sintofahamu mle ndani namna
akina Devotha walivyoweza
kupotea katika mazingira ya
kutatanisha.Deo akalazimika
kushuka chini ili kuthibitisha
kweli Mathew Mulumbi
ametoweka na kukuta vyumba
vyote vikiwa vitupu Mathew
hayupo.Akampigia simu Kaiza
kumpa taarifa zile
“Deo kuna taarifa
gani?Naomba unieleze haraka
ninajiandaa kuanza kumuhoji
Olivia” akasema Kaiza
“Kaiza kuna jambo
limetokea hapa kitalu 1 si la
kawaida” akasema Deo na
kumsimuliza Kaiza kila kitu
kilichotokea.Kaiza
alichanganyikiwa hakujua
afanye nini
“Devotha ni shetani.Kwa
nini akafanya usaliti mkubwa
namna hii kwa idara ambayo
ameiunda yeye mwenyewe?
Kwa nini amechagua
kumuamini Olivia akaungana na
magaidi na kumsaliti hadi rais
wake? Akajiuliza Kaiza
“Kaiza” akaita Deo baada ya
kuona Kaiza amekuwa kimya
“Deo nini kinachoendelea
hapo kwa sasa?akauliza Kaiza
“Kwa sasa zinaendelea
jitihada za kufahamu mahala
walikojificha akina
Devotha.Inaaminika bado
hawajatoka ndani ya jengo hili
hivyo unaendelea upekuzi wa
kila chumba kuhakikisha
wanapatikana”akasema Deo
“Hamuwezi
kuwapata.Tayari wamekwisha
ondoka” akasema Kaiza
“Kwa mujibu wa watu
waliokuwepo hapa wanadai
akina Devotha hawakufanikiwa
kutoka ndani ya jengo hivyo
wanaamini bado wako humu
ndani”
“Kama wavamizi hao
waliongozwa na Devotha amini
nakwambia tayari wamekwisha
ondoka hawako ndani ya hilo
jengo” akasema Kaiza
“Kaiza hakuna sehemu
wanakoweza kutoka bila
kuonekana nah ii ndiyo
inayotupasua vichwa kwa sasa
.Kama wametoka wamepita
wapi wasionekane?akauliza
Deo
“Deo ninakuja huko sasa
hivi,kama mtafanikiwa
kuwapata kabla sijafika hapo
utanijulisha” akasema Kaiza na
kukata simu akawaita watu
wake
“Nimepewea taarifa kuna
dharura imetokea kitalu
1.Nimetaarifiwa kuna watu
wamevamia kitalu 1 na
wamemtorosha Mathew
Mulumbi ambaye ni mshirika
mkubwa wa Olivia.Ninataka
kwenda huko kuthibitisha kama
hizo taarifa ni za kweli.Mambo
hapa yatasimama hadi hapo
nitakaporejea lakini ninyi
mtabaki mtaendelea kumlinda
Olivia.Elekezeni sana macho
kwa huyu Dr Alex mimi sina
imani naye kabisa” Kaiza akatoa
maelekezo kwa watu wake
halafu akamfuata Dr Alex
“Dr Alex nimepata dharura
kuna sehemu ninahitajika mara
moja.Tutasimamisha zoezi kwa
muda hadi hapo
nitakaporejea.Nataka uutumie
muda huu kuhakikisha Olivia
anaandaliwa kwa ajili ya
mahoijiano ili nitakaporejea
kazi iendelee.Watu wangu wote
wanabaki hapa kuhakikisha
usalama unakuwepo
ninakuonya usijaribu kufanya
jambo lolote la kipuuzi”
akasema Kaiza
“Usiwe na hofu Kaiza.Hii ni
ofisi yangu na niko hapa kwa
zaidi ya miaka kumi.Huna
sababu ya kuwa na hofu na
mimi.Ninaifahamu kazi yangu”
akasema Dr Alex.Kaiza akaingia
katika gari na kuondoka
kuelekea kitalu 1.
“Devotha ndiye aliyempa
rais wazo la kuanzisha idara hii
ya siri ya usalama wa ndani wa
nchi na toka idara hii
ilipoanzishwa amefanya kazi
kubwa na nzuri.Rais
anamuamini mno na idara yetu
sasa inaanza kuwa kubwa na
mipango imeanza ili isambae
kila mkoa hapa
Tanzania.Sifahamu kwa nini
Devotha amechagua kuyaacha
mafanikio haya makubwa na
kuchagua kuisaliti idara
aliyoianzisha yeye
mwenyewe.Kwa nini achague
kumuamini Olivia mtu
anayeshirikiana na magaidi
ambao wanahatarisha usalama
wa nchi?Kwa nini ameamua
kumsaliti rais?Mbaya zaidi
ameshiriki kufanya mauaji ya
watu wake mwenyewe ambao
amefanya nao kazi kama ndugu
zake.Sifahamu ni shetyani gani
amemuingia hadi akafanya haya
aliyoyafanya.Nimepata funzo la
kutomuamini kiumbe anaitwa
mwanadamu.Anaweza
akakusaliti dakika yoyote”
akawaza Kaiza
“Kitendo cha Devotha
kumuamini Olivia na kuamua
kushirikiana naye kumtafuta
Edger Kaka ni wazi ameamua
kushirikiana na magaidi wale
wanaoshirikiana na Olivia
ambao lengo lao kubwa ni
kutaka kuleta vurugu nchini
kwa kuwaaminisha watu kuwa
Edger Kaka ni mzima
anashikiliwa na
serikali.Ameamua kumtorosha
Mathew ambaye naye
anashirikiana na magaidi na
kinachofuata atatafuta
uwezekano wa kumtorosha pia
Olivia.Ameamua kujiunga
upande wa maadui zetu hii
inamfanya awe ni mmoja wa
maadui zetu na adui wa nchi hii
pia.Ninaweka ahadi ya kumsaka
kokote aliko na kumpa stahili
yake kwa usaliti huu mkubwa
alioufanya.Kitu kikubwa kwa
sasa ni kumlinda Olivia kwa
nguvu zote kwani ni mtu pekee
ambaye anaweza akatusaidia
kuutambua na kuusafisha
mtandao huu wa IS hapa
nchini.Nitakaporejea sintajali
litakalotokea lazima nihakikishe
anasema kila kitu kuhusiana na
mtandao wao hapa
nchini”akaendelea kuwaza
Kaiza
Aliwasili Kitalu 1 na
hakuamini macho yake kile
kilichotokea.Aliumia sana
alipowakuta watu wote
waliouawa wakiwa
wamewekwa katika chumba
kimoja
“Huu ni ukatili mkubwa
usiovumilika.Devotha ninaapa
lazima atalipa uovu huu
mkubwa alioufanya!! Akawaza
Kaiza akiitazama miili ile.Kaiza
akaendelea kuzungukia sehemu
nyingine za jengo lile kuangalia
uharibifu uliofanyika halafu
akaenda chini mahala
alikokuwa amehifadhiwa
Mathew.
“Kaiza inashangaza sana
namna Devotha na wenzake
walivyopotea.Hawakufanikiwa
kupanda kule juu lakini
tumebaki tunajiuliza namna
walivyotoweka katika
mazingira ya kutatanisha
mno.Tuliamini labda
wamejificha humu ndani lakini
tumepekua kila mahali
hatujawaona.Wametoweka
kimiujiza” akasema Deo .
“Hapana hakuna muujiza
uliofanyika” akasema Kaiza na
kwenda katika choo kilicho
kwenye chumba cha A3 akakuta
tanki dogo jeupe lililopachikwa
ukutani limefunguliwa
“Damn you Devotha!!
Akasema akilitazama tanki
lile.Akabonyeza namba katika
kifaa kilichokuwamo ndani ya
tanki lile dogo na ukuta
ukajiachia ikaonekana njia
kubwa wote aliokuwa nao
wakabaki wanashangaa.
“Huku ndiko walikopita
Devotha na akina Mathew.Hii ni
njia ya siri ambayo
ilitengenezwa maalum kwa ajili
ya kuwatorosha viongozi
wakuu kama kuna hatari
yoyote.Njia hii inakwenda
kutokea karibu na bahari hivyo
kumuwezesha Rais au kiongozi
yoyote mkubwa kutoroka
kirahisi.Tunaoifahamu siri hii ni
sisi wawili mimi na Devotha
pekee” akasema Kaiza kisha
wakaingia ndani ya njia ile hadi
walipofika mwisho wake
hawakuwakuta akina
Devotha.Kaiza akalifungua
lango wakatokeza nje
hakukuwa na mtu.Wakarejea
kitalu 1 na Kaiza hakuwa na
namna nyingine Zaidi ya
kumjulisha Rais kile
kilichotokea.
“Kaiza nini kinaendelea
hapo?akauliza Dr Evans
baadaya kupokea simu ya Kaiza
“Mheshimiwa rais
nimekupigia kukujulisha kuwa
nimelazimika kuja hapa kitalu 1
kuna tatizo limetokea”
“Tatizo gani limetokea
Kaiza? akauliza Dr Evans
Kaiza akamueleza Dr Evans
kila kitu kilichotokea.
“Hivyo ndivyo ilivyotokea
mheshimiwa rais na kunilazimu
nirejee hapa kitalu 1
kushughulikia hili suala”
akamalizia
“Kaiza sikutegemea kabisa
kusikia kitu kama hicho kutoka
kwako.Nilikupa maelekezo ya
kuhakikisha Devotha
anadhibitiwa na asiweze
kuingia katika mfumo
wetu.Nilitoa maelekezo haya
kwa kufahamu ni mtu hatari
anaufahamu mfumo wa idara
yenu kwa undani na kama
asingedhibitiwa angeweza
kufanya chochote.Mmepuuzia
maelekezo yangu na haya ndiyo
matokeo yake.Amepata
mwanya ameutumia na sasa
anazidi kutupa wakati mgumu
hata wa kumkamata”akasema
Dr Evans kwa ukali
“Tulifanya kama
ulivyoelekeza mheshimiwa rais
na Devotha aifungiwa kila kitu
kuanzia simu yake hata kadi
zake zote ambazo
zingemuwezesha kuingia katika
mfumo wetu”akasema Kaiza
“Kama mlifanya
nilivyowaelekeza amewezaje
kuingia katika mfumo wenu na
akafanya anavyotaka hata
akaingia hadi kitalu 1 mahala
ambako tunaamini ni salama
Zaidi na akafanikiwa
kumtorosha Mathew mtu
ambaye alikuwa muhimu sana
kwetu?
“Mheshimiwa rais tunataka
kufanya uchunguzi kubaini
namna alivyoweza kufanikiwa
kuingia katika mfumo wetu na
akafanikiwa kuingia hapa kitalu
1”akajibu Kaiza
“Kaiza ninachokihitaji
kukisikia kutoka kwako ni kuwa
Mathew na Devotha
wamekamatwa.Hawa ni watu
ambao wataharibu kila kitu
kama tusipowadhibiti.Devotha
amechagua kuungana na watu
wanaoshirikiana na magaidi na
ninaamini malengo yake ni
kumkomboa pia Olivia.Kama
tayari amemtoa Mathew basi
anayefuata ni Olivia.Nataka
kusikia watu hawa
wamekamatwa kabla
hawajaleta madhara
yoyote.Hawa tayari ni maadui
zetu wakubwa.Devotha na
Mathew Muumbi ni watu wenye
mafunzo makubwa na
yawezekana kukawa na ugumu
katika kuwakamata ninatoa
maelekezo kama kutakuwa na
ulazima watakapoonekana
wapigwe risasi na kufa kwani ni
watu hatari sana kwa usalama
wa nchi yetu.Nataka msako wa
kuwatafuta uanze haraka
sana.Kama mkishindwa
niambieni nitumie vyombo
vyangu vingine ingawa sitaki
kushirikisha idara nyingine
katika mambo haya ya
siri”akasema Dr Evans
“Nimekuelewa mheshimiwa
rais na suala hili tunakwenda
kulifanyia kazi”akajibu Kaiza
“Vipi kuhusu
Olivia?Umefikia wapi
kumfungua?Amesema
chochote? akauliza Dr Evans
“Imenilazimu kusimamisha
kila kitu na kuja huku kitalu 1
baada ya tukio hili kutokea
lakini hadi ninaondoka kuja
huku sikuwa nimefanikiwa
kupata chochote kutoka kwa
Olivia hali yake haikuwa nzuri
baada ya kumpitisha katika
mashine ya umeme.Dr Alex
alishauri tumpe muda wa
kupumzika kabla ya kuendelea
tena na mahojiano.Ninakuahidi
mheshimiwa rais kwamba jua
halitazama leo kabla Olivia
hajasema
chochote.Nakuhakikishia
mheshimiwa rais lazima
tutawapata Devotha na
wenzake wote”akasema Kaiza
“Kaiza ninapata wakati
mgumu wa kuyaamini maneno
yenu.Hata Devotha naye
aliniahidi hivyo hivyo lakini
mpaka sasa hakuna chochote
kilichopatikana.Kuna ugumu
gani katika kumfanya Olivia
aongee?Nimewasaidia hata
kumpata baba yake lakini
mmeshindwa kumtumia
kumfanya Olivia afungue
mdomo.Ugumu uko
wapi?akauliza Dr Evans
“Naomba uniamini
mheshimiwa rais kwamba haya
ninayokwambia ni ya kweli
kabisa.Nitakapokupigia simu
lazima nitakuwa na taarifa zote
za kuhusiana na mtandao wa IS
hapa nchini kutoka kwa Olivia”
akasema Kaiza”
“Kaiza tafadhali naomba
ulimalize hili suala.Nina mambo
mengi sana ya kushughulikia na
sitaki kuendelea kupigiwa simu
kuelezwa matatizo badala ya
kuelezwa mafanikio.Endapo
mtashindwa katika hili
sintakuwa na namna nyingine
Zaidi ya kuifunga hii idara
kwani itakuwa imeshindwa
kufanya kazi yake na haitakuwa
na maana tena.Naamini
umenielewa Kaiza”
“Nimekuelewa mheshimiwa
rais tutajitahidi”akajibu Kaiza
“Good.Shughulikia suala
hilo limalizike.Nina mambo
mengi natakiwa
kuyashughulikia nimechoka
kusikia kila wakati matatizo
kutoka kwenu.Nataka ufanisi !!
akasema Dr Evans kwa ukali na
kukata simu
“Rais amekasirika
sana.Devotha amesababisha
Rais asiwe na Imani nasi tena”
akawaza Kaiza.
“Ukiyachunguza maneno ya
rais yawezekana kweli kuna
uzembe umefanyika
hapa.Imewezekanaje Devotha
akafanikiwa kuingia hapa na
kumchukua Mathew
Mulumbi?Zipo kamera za ulinzi
ambazo hata ukirusha sindano
ndogo itaonekana
wameshindwaje kumuona
Devotha wakati akiingia hapa
hadi akaua watu wetu na
kumchukua Mathew? Rais ana
haki ya kuwa mkali.Tunalipwa
vizuri tunaishi maisha mazuri
hivyo lazima tuonyeshe ufanisi
mkubwa katika majukumu
yetu.Rais hana Imani tena nasi
na kazi yangu kubwa ni
kurejesha Imani kwa Rais na
hilo litawezekana kama
tukifanikiwa kuwapata Devotha
na Mathew Mulumbi.Tutaanzia
wapi kuwatafuta watu hawa?
Akajiuliza Kaiza
“Devotha tayari anafahamu
kuwa anatafutwa hivyo
kumpata haitakuwa kazi
nyepesi.Kitu kikubwa kwa sasa
ni kuhakikisha tunamlinda kwa
kila namna Olivia kwani yeye
ndiye njia yetu pekee ya
kutusaidia kuweza kuufahamu
mtandao wake wote na kupitia
kwake tutawapata hata akina
Devotha”akaendelea kuwaza
Kaiza
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 6
EPISODE 4
Devotha alipokelewa katika
hospitali inayomilikiwa na Dr
Philip hali yake haikuwa nzuri
hata kidogo na bila kupoteza
muda akaingizwa katika
chumba cha upasuaji na zoezi la
kuondoa risasi likaanza haraka
likisimamiwa na Dr Philip
ambaye aliwahi kufanya kazi na
Mathew katika idara ya ujasusi
kabla ya kufungua hospitali
yake mwenyewe baada ya
kukopeshwa kiasi kikubwa cha
fedha na Mathew.Wakati
upasuaji ule ukiendelea Mathew
akaomba kuzungumza pembeni
na Dr Philip
“Dr Philip ninamkabidhi
mgonjwa huyu kwako naomba
ufanye kila linalowezekana
kuhakikisha anakuwa
salama.Mimi nitakuja tena
baadae kuangalia maendeleo
yake”akasema Mathew
“Mathew umejingiza
kwenye jambo gani tena? Lini
utaachana na mambo
haya?akauliza Dr Philip
“Dr Philip tutazungumza
baadae kwa kirefu lakini kwa
sasa naomba nguvu kubwa
ielekeze katika kuhakikisa
Devotha anakuwa
salama.Nakuomba sana Dr Pilip
unisaidie katika suala hili”
akasema Mathew
“Mathew usiwe na hofu
kuhusu mgonjwa wako
nitafanya kila lililo ndani ya
uwezo wangu kuhakikisha
anakuwa salama ila nakushauri
ndugu yangu ungeachana na
hizi shughuli.Waachie wengine
na wewe endelea na maisha
yako.Umekwisha fanya mambo
mengi pumzika sasa na jikite
katika biashara” akasema Dr
Philip
“Dr Philip si kwamba
ninazitafuta kazi hizi bali
zinanifuata zenyewe na
ninajikuta siwezi kukataa
kuifanya kwa manufaa
makubwa ya nchi.Jambo lingine
kazi hii tayari iko damuni hivyo
nitaendelea kuifanya kila pale
nitakapolazimika kuifanya”
akasema Mathew na kumuomba
Dr Philip ampatie simu yake
akampigia Jordan dereva wa
kampuni yake akamtaka aende
Tumaini cark parking ghorofa
ya tano amuwekee gari pale
kisha wakaagana na Dr Pilip
wakaondoka pale hospitali.
“Tutaliacha gari hili
Tumaini car parking hatulihitaji
tena” akasema Mathew baada
ya kuondoka hospitali
“Pole sana Mathew”
akasema Gosu Gosu aliyekuwa
katika usukani
“Nashukuru sana Gosu
Gosu.Sikufanya makosa kukuita
uje kwani bila wewe sijui kama
ningetoka mle ndani
salama.Ahsante sana kwa
kuniokoa” akasema Mathew
“Usijali Mathew.Kwa sasa
baada ya kukuokoa tujielekeze
kumtafuta Olivia”
“Tayari umepata habari
zake?Mathew akauliza
“Ndiyo.Devotha amenieleza
kila kitu kilichotokea kwa nini
walimteka Olivia na hadi
walivyokuteka wewe.Alisema
ulimuelekeza kwangu kwa ajili
ya msaada na akanitaka
nimsaidie kumtafuta Olivia
lakini nilikataa na kumwamba
kama anahitaji msaada wangu
kitu cha kwanza ambacho
tunatakiwa kukifanya ni
kukuokoa kwanza
wewe.Hakuwa na kipingamizi
tukaanza taratibu za kufika
mahala ulipokuwa
umeshikiliwa” Gosu Gosu
akamueleza Mathew kila kitu
kilichotokea hadi
walipofanikiwa kumuokoa
“Sikutegemea kabisa kama
Devotha angeweza kuniamini
na kuamua kuwasaliti
wenzake.Alikuja kuzungumza
nami akanihoji maswali mengi
kuhusiana na mahusiano yangu
na Olivia nikamueleza kila kitu
bila kumficha na ndipo
akanieleza mambo yote ya
Olivia kushirikiana na kikundi
cha IS.Mungu amsaidie apone
haraka kwani ana nia ya dhati
ya kutaka kuufahamu ukweli
wa jambo hili linaloendelea”
akasema Mathew
“Simfahamu Olivia lakini
kwa maelezo aliyonipa Devotha
yamenifanya nijiulize maswali
mengi kuhusiana na yeye
kujiunga na kikundi cha kigaidi
cha IS.Ume……”akasema Gosu
Gosu na Mathew akamkatisha.
“Suala hilo hata mimi
limenistua sana
nilipolisikia.Devotha
alinionyesha baadhi ya picha
ambazo zinamuonyesha Olivia
akiwa jijini Kinshasa na mtu
anaitwa Seif Almuhsin ambaye
ni mtu wa IS na kazi yake
kubwa ni kukusanya vijana
ambao hujiunga na kikundi cha
IS kisha kupelekwa katika
kambi zao za mafunzo ya
kigaidi.IS kimekuwa ni kikundi
tishio kwa sasa duniani na
wameanza mikakati ya
kujitanua Zaidi barani
Afrika.Kitendo cha Olivia
kukutana na Seif kinazua
maswali mengi.Kama haitoshi
baada ya kupekua kompyuta
yake amekutwa akiwasiliana na
mtu mwingine anaitwa Sayid
Omar ambaye anatajwa kuwa ni
mfadhili mkubwa wa
IS.Devotha alinipa nisome
baadhi ya barua pepe ambazo
Olivia alikuwa anawasiliana na
Sayid kwa lugha ya
kiarabu.Nilishangaa
sana,sikujua kama Olivia
anaifahamu lugha ya
kiarabu.Katika barua pepe zile
Olivia na Sayid walizungumzia
kuhusiana na utengenezwaji wa
kirusi na kwa mujibu wa
Devotha,Olivia ametengeneza
kirusi ambacho
amemuambukiza mtoto wa rais
na kwa sasa binti huyo wa rais
yuko hospitali hali yake si
nzuri.Olivia amefanya hivi ili
kumshinikiza rais amueleze
mahala alipo Edger Kaka”
“Edger Kaka?!! Gosu Gosu
akashangaa
“Ni nani huyo?
“Edger Kaka aliwahi kuwa
mbunge wa bunge la jamhuri ya
muungano wa
Tanzania.Alifariki katika ajali ya
gari miaka mitatu iliyopita
lakini Olivia ameibukana kudai
kuwa Edger Kaka hajafa yuko
hai” akasema Mathew na Gosu
Gosu akatoa kicheko kidogo
“Kwa nini anadai hivyo?
akauliza
“Hilo ni swali analotakiwa
kulijibu yeye mwenyewe.Kwa
maelezo aliyompa Devotha
anadai ajali ile iliyotokea
ilikuwa ya kutengeneza na hata
mwili uliozikwa haukuwa wa
Edger Kaka.Olivia anadai anao
ushahidi wa kuthibitisha hilo na
amekwenda mbali zaidi kwa
kumnyooshea kidole rais Dr
Evans kwamba anahusika
katika jambo hilo na anafahamu
mahala alipo Edger na ndiyo
maana anamshinikiza
amuonyeshe alipo kwa
kumuambukiza mwanae virusi
na kama rais asipofanya hivyo
basi mwanae anaweza kupoteza
maisha.Mambo kama haya
yanatokea sana katika
ulimwengu wa sasa na
yawezekana hata hili
analolisema Olivia likawa kweli
lakini swali linaloibuka hapa ni
je hili suala lina mahusiano gani
na IS? .Olivia ni kama chambo tu
lakini nyuma yake wapo IS
ambao ameshirikiana nao
katika kutengeneza kirusi hicho
ili kumshinikiza rais aeleze
mahala alipo Edger.Tujiulize IS
wana maslahi gani katika suala
hili?Mwenye kuweza kutupa
majibu ya suala hili ni Olivia
ambaye hatujui mahala alipo
hivyo kazi kubwa iliyoko mbele
yetu ni kuhakikisha tunampata
Olivia Themba.Tayari
tunafahamu anashikiliwa na
idara ya siri ya usalama wa
ndani ya nchi ambayo iko chini
ya rais na hapo hapo
ikumbukwe kwamba Rais ndiye
amenyooshewa kidole na Olivia
kuhusiana na mpango huu wa
kutengeneza kifo cha Edger
Kaka na yawezekana kuna
ukweli ndani yake na Olivia
anaweza akauawa ili jambo hili
liendelee kuwa siri hivyo basi ili
kuupata ukweli wote kuhusu
suala la Edger Kaka,kuhusu IS
lazima tumpate Olivia” akasema
Mathew na kunyamaza kidogo
wakalipita gari lililokuwa mbele
yao halafu akasema Gosu Gosu
akauliza
“Mathew ulikutana vipi na
Olivia?
“Nilikutana na Olivia katika
klabu moja ya usiku tukawa
marafiki.Baadae urafiki wetu
ukawa mkubwa Zaidi nadhani
unanielewa.Ninao uwezo
mkubwa sana wa kumsoma mtu
na toka nilipofahamiana naye
niligundua kuna kitu ananificha
na siku moja baada ya
kumdadisi akanieleza kuwa ana
tatizo na watu fulani ingawa
hakutaka kunieleza ni akina
nani.Sikutaka kuingilia mambo
yake binafsi lakini Kwa kuwa
tayari ni mtu wangu wa karibu
na sikutaka aingie katika hatari
zozote nilimpa namba za ile
programu aliyoitengeneza Ruby
ili atakapopata matatizo nijue
yuko wapi.Nikiwa mkutanoni
Arusha nilipokea ujumbe
kutoka katika namba ile
niliyompa Olivia na taarifa
zikaanza kusambaa mitandaoni
kuwa Olivia ametekwa
nikalazimika kuja Dar es salaam
haraka sana kwani tayari
nilikuwa nafahamu sehemu ya
kuanzia kumtafuta.Nilifika hadi
mahala ambako namba zile
zilipigwa lakini Olivia alikwisha
hamishwa.Nilipokuwa narudi
baada ya kumkosa Olivia
nikapigiwa simu na mama yake
Olivia akanijulisha kuwa mume
wake amepigiwa simu na mtu
ambaye alijifanya ni mimi na
akamdanganya kuwa amempata
Olivia na kumtaka wakutane
mahala.Nilifika mahala hapo
nikalikuta gari la baba yake
Olivia lakini yeye mwenyewe
hakuwemo, tayari alikwisha
tekwa.Nilianza kuhisi kuna mtu
anayeshirikiana na watekaji
ambaye ana ukaribu mkubwa
na familia ya akina Olivia.Usiku
huo huo nikaenda kuonana na
Lucy Themba mama yake Olivia
nikamtaka anieleze kama kuna
mtu yeyote walimwambia
kuhusu mimi kufahamu mahala
alipo Olivia.Lucy alikana kabisa
kumweleza mtu
yeyote.Niliporejea nyumbani
Ruby akanijulisha amegundua
Olivia ametekwa na idara ya
serikali inayojulikana kama
idara ya siri ya usalama wa
ndani ya nchi.Nilijiuliza
maswali kwa nini idara ya
serikali wamteke Olivia na baba
yake?Nilitaka kuufahamu
ukweli ndipo nilipowaomba
wewe na Ruby mje mara moja
kunisaidia katika suala
hili”akasema Mathew
“Usijali Mathew tayari
nimekaribia” akasema Gosu
Gosu.Ukapita kimya mfupi
Mathew akasema
“Mapema alfajiri leo
nilipigiwa simu na Lucy
Themba akanitaka niende
nyumbani kwake kuna jambo
anatakakunieleza.Sikuwa na
wasi wasi wowote nikaenda
kuonana naye.Nilifanya kosa
kutochukua tahadhari kumbe
ulikuwa ni mtego.Nilivamiwa na
kundi la watu wenye silaha
wakanichukua na kunipeleka
mahala pale
mliponikuta.Niliwekwa katika
chumba cha baridi kali halafu
wakanitoa na kunipeleka katika
cumba chenye mwanga mkali
mweupe.Baadae akaja Devotha
akajitambulisha kwangu kama
ndiye mkurugenzi wa idara ile
ya siri ya usalama wa ndani ya
nchi.Devotha alinihoji kuhusu
mahusiano yangu na Olivia
nikamueleza kila kitu bila
kumficha.Alinihoji maswali
mengi akitaka kujua kwa nini
nilimpa Olivia namba zile za
kunijulisha pindi akipata
matatizo.Nilimweleza sababu ya
kumlinda Olivia na bada ya
mazungumzo alitaja kuwa mimi
na Olivia tunatumiwa na IS
kufanikisha mipango yao hapa
Tanzania.Nilistuka na kumtaka
anipe ushahidi wa mimi
kujihusisha na mtandao wa
kigaidi wa IS.Alikiri kwamba
hakuwa na ushahidi wowote wa
mimi kujihusisha na mtandao
huo ila walikuwa na ushahidi
wa kutosha kuhusu Olivia
kujihusisha na mtandao
huo.Alinieleza namna
walivyopata taarifa za Olivia
kuonekana akiwa na watu wa IS
jijini Kinshasa na hadi
walivyomfuatilia na
kumteka.Alinionyesha barua
pepe ambazo Olivia amekuwa
akiwasiliana na mtu anaitwa
Sayid Omar ambaye anatajwa
kuwa mfadhili mkubwa wa
kikundi hicho.Mawasiliano yao
yalikuwa katika lugha ya
kiarabu.Nilisoma barua pepe
zile,Olivia na Sayid walikuwa
wanawasiliana kuhusiana na
maendeeleo ya mradi wa
kutengeneza kirusi ambacho
Devotha aliniambia
walimuambikiza mtoto wa rais
ili kumshinikiza awaeleze
mahala alipo Edger
Kaka.Nilimtaka Devotha
aniachie huru ili niweze
kumsaidia kuutafuta ukweli wa
jambo hili lakini hakuwa tayari
kufanya hivyo ndipo
nikamweleza kama akihitaji
msaada Zaidi awatafute wewe
na Ruby mtamsaidia.Nilimpa
vile vile maelekezo ya kufanya
kwa kumtaka aidukue simu ya
rais ili kufahamu kama rais
analifahamu suala lile la Edger
Kaka kwani yeye ndiye
amekuwa mlengwa
mkubwa.Sikujua tena
kilichoendelea hadi pale
mlipojitokeza na
kuniokoa”akasema Mathew
“Devotha alifanya kama
ulivyomuelekeza” akasema
Gosu Gosu
“Aliidukua simu ya
rais.Kuna dada mmoja anaitwa
Saada ambaye ndiye
aliyemsaidia katika kuidukua
simu ya rais lakini kwa bahati
mbaya hawakuweza kupata kitu
chochote kwani waligundulika
mapema.Nadhani Rais
aligundua kwamba ni Devotha
ndiye aliyedukua simu yake
hivyo akafungiwa kila kitu
kuanzia simu yake,na hakuweza
tena kuingia katika mtandao wa
idara yake.Yeye na Saada baada
ya kuhisi wako katika hatari
walikimbilia nyumbani
kwako.Nilipowasili nilikutana
na Theresa akanijulisha kuwa
kuna mtu alipiga simu pale
nyumbani anakutafuta anadai
ana jambo la muhimu sana la
kukueleza lakini hupatikani
simuni.Theresa alijaribu naye
kukutafuta katika namba zako
zote za simu hukuwa
unapatikana na hii ikampa
wasiwasi.Muda huo huo
Devotha akawasili nikamuhoji
na kumtaka anieleze mahala
ulipo akanieleza kila kitu
kilichotokea na mahala
ulipo.Wakati nikizungumza na
Devotha mtu yule aliyekuwa
anakutafuta simuni akapiga
tena simu ya nyumbani kwako
nikalazimika kuzungumza naye
nikijifanya mimi ni Mathew
nikamuliza anachonikufutia
akasema anazo taarifa kuhusu
Olivia.Kabla ajaeleza chochote
ikasikika sauti ikimuuliza kwa
ukali yule jamaa anazungumza
na nani na simu ikakatwa”
“Alisema anazo taarifa za
Olivia?Mathew akauliza
“Ndiyo.Alitaka kunieleza
kitu Fulani kuhusu Olivia lakini
akazuiwa na mtu baqda ya hapo
simu yake ikakatwa na
haikupatikana tena” akasema
Gosu Gosu
“Kwa namna alivyokuwa
anazungumza unadhani alitaka
kunieleza nini kuhusu Olivia?
Mathew akauliza
“Sina hakika lakini
alichotaka kukueleza
kinahusiana na Olivia.Kwa
taarifa tu ni kwamba Olivia
amehamishwa kutoka mahala
alipokuwa na hata Devotha
mwenyewe hafahamu mahala
alipo” akasema Gosu
Gosu.Mathew akafikiri kidogo
na kusema
“Ninahisi Olivia alimtumia
huyo jamaa kufikisha ujumbe
kwangu lakini akagundulika
kabla hajafikisha ujumbe.Kama
ni kweli Olivia alimtumia huyo
jamaa kutaka kunifikishia
ujumbe na akagundulika basi
kitendo hicho kinamuweka
katika hatari Zaidi.Kikubwa
tunachopaswa kukifanya kwa
sasa ni kutafuta mahala ambako
huyo jamaa alikuwepo wakati
akipiga simu.Kwa bahati mbaya
Ruby bado hajawasili yeye
ndiye mtaalamu sana wa haya
mambo ya mawasiliano”
akasema Mathew
“Tunaye Saada.Anao ujuzi
wa kutosha katika mambo
haya.Ndiye aliyemsaidia
Devotha kudukua simu ya rais
na ndiye aliyetusadia kuingia
pale mahali ulipokuwa
umefungwa kwa kucheza na
kamera.Tulimchukulia chumba
Lupai hotel ili aendelee na zoezi
la kucheza na kamera za jengo
lile tungeweza kumfuata lakini
kwa bahati mbaya Lupai Hoteli
iko karibu sana na lile jengo la
wale jamaa”akasema Gosu Gosu
“Tafuta namba za hoteli
mpigie simu na muelekeze
sehemu ya kukutana anaweza
akatusaidia kufahamu mahala
alipo huyo jamaa aliyekuwa
ananitafuta” akasema Mathew
“Sawa nitafanya hivyo.Vipi
Paul naye anakuja?akauliza
Gosu Gosu
“Hapana Paul
hatakuja.Tutakuwa na Ruby”
akasema Mathew
“Tulikuwa na timu nzuri
sana wakati ule tukiwa kikosi
cha siri”
“Usijali kila kitu kitakwenda
vizuri.Tutampata Olivia na
tutajua kila kitu kuhusu yeye na
kikundi cha IS na kama kuna
mipango yoyote wanayoipanga
hapa nchini tutahakikisha
haifanikiwi” akasema Mathew
na ukimya ukatawala garini
“Bado ninajiuliza maswali
mengi kuhusiana na Olivia na
IS.Kuna nyakati najikuta
nikikataa Olivia hawezi na hana
sababu ya kujihusisha na watu
wa IS lakini upo ushahidi
mkubwa wa jambo hili na kuna
sauti ndani mwangu inaniambia
nilifuatilie hili jambo hadi mzizi
wake na kuufahamu
kweli.Nitahakikisha ninafahamu
kuhusiana na hili suala”
akawaza Mathew na kuivuta
picha ya Olivia kichwani kwake
“She’s an angel.Ana sura
nzuri ya kimalaika.Akicheka
vishimo hutokea katika
mashavu yake.Ana sauti
nyororo kama Wema,ana kila
sifa ya mwanamke
mzuri.Inawezekanaje msichana
mzuri kama huyu akajihusisha
na mtandao wa kigaidi?Ni kwa
ajili ya kujipatia fedha?Sidhani
kama Olivia ana shida na fedha
kwani anatoka katika familia
bora kabisa na yeye mwenyewe
ni msomi mzuri,Olivia ana kila
kitu anachokihitaji katika
maisha yake hana sababu ya
kujiunga na magaidi kwa ajili ya
fedha kitu gani basi
kimempelekea akafanya haya
aliyoyafanya? Jambo hili hata
watu wakilisikia litawapa
ugumu sana kuamini lakini huo
ndio ukweli.Olivia anashirikiana
na magaidi na kwa kushirikiana
na Sayid Omar wametengeneza
kirusi ambacho
wamemuambukiza mtoto wa
Rais ili kumshinikiza
awaonyeshe mahala alipo Edger
Kaka.Huyu Edger Kaka ana nini
hadi IS wamtafute kwa gharama
kiasi hiki?Ana maslahi gani
kwao? Bado mtu mwenye
kuweza kusaidia kupata majibu
ya maswali haya yote anabaki
kuwa ni Olivia pekee” akawaza
Mathew
Walifika Tumaini Car
praking,jengo la ghorofa nane
ambalo ni maalum kwa ajili ya
kuegesha magari.Walipanda
hadi ghorofa ya tano ambako
Mathew alimiuelekeza Jordan
apeleke gari.Alishuka garini
akaenda kulitafuta gari
alilomuelekeza Jordan amletee
akalipata.Milango yake haikuwa
imefungwa na katika droo ya
gari kulikuwa na
funguo.Mathew akaingia na
kuliwasha.Gosu Gosu akafungua
buti la ile gari waliyokuwa
wameitumia akakata Kamba
alizomfunga dereva.
“Kila kitu chako kiko garini
hakuna kilichopotea” akasema
Gosu Gosu na kutoa bunda la
dola za kimarekani akamega
nusu yake na kumrushia yule
jamaa ndani ya buti
“Samahani sana kwa
usumbufu” akasema huku
akimfanyia ishara kuwa afunge
mdomo wake.Akachukua silaha
zao akaelekea katika gari
alimokuwamo Mathew
wakaondoka
“Una hakika yule dereva
hataweza kuwa na
madhara?Mathew akauliza
“Hana
madhara.Nimempooza na kiasi
cha kutosha cha dola” akasema
Gosu Gosu
Mathew ndiye aliyeshika
usukani na safari ikawa ya
kimya kimya hadi walipofika
nje ya nyumba yenye geti jeusi
eneo la Buti mbili.Mathew
akashuka garini akaenda katika
geti akafunua mfuniko wa kasha
Fulani dogo ambalo ndani yake
kulikuwa na vitufe kadhaa vya
namba akabonyeza namba na
geti likafunguka akamtaka Gosu
Gosu aingize gari ndani kisha
akalifunga geti
Ilikuwa ni nyumba ya
wastani iliyokuwa na vyumba
vitatu vya
kulala,sebule,jiko,chumba cha
chakula pamoja na chumba
kingine kidogo kwa ajili ya
maktaba.
“Nani anaishi hapa?
Akauliza Gosu Gosu
“Hii pia ni nyumba
yangu.Nimeinunua kutoka kwa
rafiki yangu na ninaendelea na
ukarabati.Ninapenda wakati
mwingine kuja kupumzika hapa
kuna utulivu
mwingi.Ninawekeza sana katika
majengo kwani thamani yake
haishuki bali inapanda kila
mwaka” akajibu Mathew
“Hongera.Ni nyumba ndogo
lakini nzuri sana” akasema Gosu
Gosu wakaingia ndani
“Kuna vyumba vitatu humu
ndani.Kimoja ni cha kwangu
,kingine atatumia Ruby na
kingine utatumia
wewe.Operesheni yote
itafanyika kutokea hapa”
akasema Mathew na kuingia
katika chumba chake cha kulala
baada ya muda akatoka akiwa
na simu tatu amkapatia moja
Gosu Gosu
“Mimi ni mtu wa tahadhari
muda wote .Sifahamu ni wakati
gani nitakutana na hatari hivyo
basi huwa nina kawaida ya
kuhifadhi vitu muhimu vya
mawasiliano katika baadhi ya
sehemu zangu muhimu.Simu
hiyo utatumia wewe hii
nyingine ataitumia Ruby.Mpigie
yule msichana uliyesema
mlimuacha hotelini
tunamuhitaji tuanze kazi”
akasema Mathew.Gosu Gosu
akajisachi mfukoni alikuwa na
risiti waliyotumia kufanya
malipo akanakili namba za simu
za Lupai Hoteli akapiga na
kuomba kuzungumza na
chumba 86 akaunganishwa
lakini simu ikaita bila
kupokelewa.
“Saada atakuwa amendoka
pale hotelini au yuko katika
matatizo? akawaza Gosu Gosu
na kumfuata Matew chumbani
kwake
“Simu ya chumbani kwa
Saada inaita haipokelewi”
akasema Gosu Gosu
“Usiogope.Tutamsubiri
Ruby si muda mrefu toka sasa
atawasili.Wakati tunamsubiri
kuna mahala nataka twende”
akasema Mathew wakaingia
garini na kuondoka bila
kumueleza Gosu Gosu
wanakoelekea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom