SEHEMU YA 12
Nikaipiga teke kurunzi ile na ikadondoka mbali na kisha nikaweka mikono yangu chini na kubetua miguu yangu na kusimama wima,na wakati huohuo masikio yangu yakaunasa usauti mdogo wa kukokiwa silaha ya uzi micro na bila kujiuliza nikajinyonga na kurusha ngumi matata kwa mtu yule alieikoki silaha ile na ikampata sikioni na kudondoka chini huku akitoa mlio wa maumivu na hapo nikanasa tena sauti ya hatua za mtu akija kwa kasi nyuma yangu na hapo nikageuka kwa kasi na kuachia teke msawazo yaani teke linalopigwa kimo cha pembe za ng’ombe na kupata yule mtu kifuani na kumtupa nyuma huku mikono yangu ikiwa tayari imenasa shingo ya mtu na kuivunja.
Waliobaki kama wane hivi wakaanza kukimbia huku wakipiga makelele ya woga na mimi ikabidi nitulie kwanza na kutazama eneo nililopo na kuona pembeni yangu kuna shimo refu lililochimbwa kama yale mashimo ya migodini na hpo nikajua nipo migodini na nilipotazma upande mwingine nikaona kuna matuyrubai na taa zikiwaka huku kukiwa na makelele mengi upande huo na hapo nikatazama chini nikamwona mwanajeshi mmoja amelala chini na bunduki yake akigalagala nikamfuata na kumtandika teke la mbavu na nikamsikia akikohoa nakutema kitu nikajua ni damu hiyo.
Nikamtazma mwingine tena alikuwa katulia kimya chini kama mfu huyu ni yule niliekuwa nimempiga teke msawazo na nilipomkazia macho nikaona anakimo na mwili kama mimi sikuchelea kumvua mavazi yake na kuyatia mwilini kwangu pamoja na viatu vyake vya kutoka kampuni ya didasi,navyo nikaviyia mguuni na kuutikisa kidogo mguu wangu nikatambua havinitoshi viatu vile.
Pale nilipokuwa kulikuwa na kimlima kidogo na hivyo ikanilazimu kushuka bondeni kulikokuwa na makele ya watu huku nikikutana na mashimo mengi yaliochimbwa na kuachwa na hapo akili yangu ikatambua kabisa nilkitaka kutolewa kafara na watu wale wapuuzi.
Sikutaka maumivu yautawale mwili wangu hivyo nikajikaza na kuanza safari ya kuelekea kule kunakosikika kelele nyingi za watu na umeme ukiwaka vyema.
Nilianza kuyakaribia makazi yale na hapo nikapokelewa na sauti za muziki wa kilevilevi kutoka kwa wasanii wa pale Burundi,mitaa ile ya machimboni ilikuwa imechangamka kweli huku walevi wakiwa ni wengi kuliko waliosafi kiakili.
Kadri nilivyozidi kusogea ndivyo nilivyozidi kujionea mambo ya ajabu eneo lile kuna watu walikuwa wakijamiaana hadharani huku kitu pekee kilichowasitiri ni vijumba vya maturubai,miguno ilisikika huku na huko na baadhi ya watu wanavuta bangi hadharani kabisa yaani ilimradi kila mtu alifanya kile alichojisikia.
Macho yangu yakavutiwa na watu wawili waliokuwa wamegandiana kwenye kichochoro kimoja hivi,kilichonivutia ni yule mwanume aliekuwa amemwinamisha mwanamke mmoja wakingonoka,kilichonivutia kwake ni mavazi yake,alikuwa amevaa koti refu lililomfunika kichwani na nilihitaji lile koti.
Niliwafuata wale watu huku mwanamke akiwa wa kwanza kuniona na kujichomoa kwa mwanaume wake huku mwanaume akitoa tusi kubwa kulaani kitendo kile lakini mwanamke wake akamnyooshea kidole kuja nilipo yule bwana huku akiongozwa na pombe akanifuata kwa gadhabu za kukatishiwa uroda wake na mimi sikutaka kumkawiza nilikuwa nimejiandaa kumpa ngumi nzito.
Aliponifikia kweli sikutaka kumkawiza nikampiga ngumi katikati ya kifua katika uzito wa kumfanya asife ila asinyanyuke kwa muda huo na kweli kaenda chini na alivyotaka kunyanyuka akashndwa na nilipotazama pale alipokuwa yule mwanamke hakuwepo tena.
******
Nikiwa tayari nina lile koti refu nakisu kirefu nilichokikuta kwa yule bwana mfanya sodoma,nikaingia kwenye bar ya makuti iliokuwa ikitoa mziki mnene na makele ya watu na nilivyoingia hakuna ailienitilia shaka yoyote maana niliingia huku nikiwa nimeigiza kulewa hivi na nikawa nikiwapita watu walikuwa wamebambiana,huku wengine wakipepesuka huku na huko lakini cha ajabu hakuna alieangusha chupa ya pombe.Nikawapita kwa tabu huku nikiwapiga vikumbo watu kadhaa na kuelekea ilipo kaunta.
Nilipofika nikamkuta mhudumu wa kule kaunta kiwa bize kuhudumia watu na huku wengine wakiingia kule aliko wanachukua pombe na kulipa kisha wanendelea kuburudika na mimi niakingia kule kaunta lakini nilipofika nikaufunga ule mlango wa kaunta na nikamgusa yule dada wa pale kaunta makalio yake akaruka juu huku akigeuka na kucheka lakini alichokutana nacho ikabidi aanze kutetemeka na nikamwekea kidole kimoja mdomoni kama ishara ya kumwashiria haruhusiwi kupiga kelele nae akatii.
Watu waliendelea kupiga kelele lakini mimi nilikuwa nimedhibiti muuzaji yule na tayari alikuwa ameanza kunihesabia pesa aliokuwa ameuza.
Alinipa pesa sawa na tsh.laki mbili hivi ambayo ni sawa na faranga miamoja na sabini elfu.Alipokwisha kunipa nikaanza kutoka mule ndani huku sasa nikipiga hesabu za kuchomoka mule baani haraka kabla mabo hayajaharibilka.
Wakati nimeshajichanganya na walevi yule dada akaanza kupiga makele lakini kelele zake zilimezwa na muziki mkubwa na kelele za waponda raha wale.
Nilifanikiwa kutoka hadi nje kabisa ya ukumbi ule na huko nikalitupa koti lile na nikabaki na kisu kile kirefu nilichokitia kwene pindo la nguo nilizozivaa na kisha nikachukua kofia niliokuwa nimepora kichwani mwa mlevi mmoja wakati natoka mle ndani ya ukumbi ule wa anasa.
Safari yangu ilikuwa ni kujaribu kutafuta uelekeo wa kule kituo cha polisi ambako niliamini nikifika huko basi uelekeo wangu wa kumtafuta mzee Niyonzima ungerudi kidogo kichwni pangu.
Nikazidi kupishana na watu kadhaa wakiwa katika harakati walizozijua wao usiku ule,nikazidi kwenda mbele kwa kufuata barabara iliokuwa ikiingia mgodini mle,sasa mimi nilikuwa naifuata kwa kutoka yaani kwa kuelekea kule inakotokea barabara ile.
Kwa mbele niliona kibao kikiwa pembeni mwa barabara ile na hapo tabsamu jepesi likajijenga usoni pangu nikajikuta nakimbia ili kukifikia maana niliamini kitakuwa na jina la mgodi ule mdogo.
“WELCOME CAMP DE BUKAMBO” kibao kile kiliandikwa vile na hapo nikajaribu kuvuta kumbukumbu za ramani yangu ililokuwa kwenye begi ambalo sijui hadi wakati huo litakuwa wapi.
Kumbukumbu zangu zilinionesha kutoka hapo Bukambo hadi kule Salimbe kulikuwa na mwendo wa kama kilomita 9,lakini eneo ninalolitafuta nilo hilo Bukambo hivyo sikuwa nahaja ya kurudi kule ilihitajika nitafute makazi ya Mzee Niyonzima ndani ya Bukambo.
Ijapokuwa hapo nilipokuwa hapakuonesha kuwa na makazi ya watu lakini niliamini kabisa ndani ya eneo lile kulikuwa na makazi karibu maana nilitoka mbali kuja kulitafuta eneo hilo la Bukambo,hivyo nikafanya shauri la kurudi kule vilabuni ili nipate kuutega usiku na pakikucha basi nijue pa kuanzia.
*********
Katika pitapita zangu usiku ule nikafanikiwa kuona sehemu palipokuwa pameandikwa GEUST.Na nilipoingia kweli kulikuwa vyumba na chumba kilikuwa ni faranga 850,nikapewa chumba na kwenda kujipimzisha.
Huko chumbani nilijuta kulipia yaani mara mia ningelala nje kuliko pale ndani,kitanda kilikuwa kina chaga za miti huku godoro likiwa ni la pamba na limechakaa sana,lakini kulikuwa na kero ya kutoka vyumba vya jirani ambapo watu walikuwa wakifanya ngono na kupiga makele kwa sauti ya juu,ama hakika migodini ni sehemu zilizolaaniwa si kwa sodoma ile.
ASALAAM KUDO
0758573660
0658564341for whatsap