Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
SAUTI YA MTUTU
(MTAZIKA KILA IKISIKIKA)
Na BAHATI MWAMBA
0758573660,0624155629
Bunduki yangu ilikuwa imeisha risasi na kitu pekee nilichokuwa nakitegemea ni hatua za miguu yangu japo maungio ya magoti yalianza kugoma kunipa ushirikiano.
Mvua kubwa ilikuwa bado inazidi kunyesha,sikuwa mnaona mbele wala sikuwa naona nyuma na mara chache sana nilijikuta nikitamani sana radi ipige tena ili niweze kuona mbele na wale waliokua wakinikimbiza nyuma niweze kuwakwepa.
Kracha,kacha..mlio huu ulizidi kunidhirishia ya kuwa sikuwa japo nimefanikiwa kubakiza risasi hata moja kwenye bunduki yangu niliopenda tangu nifahamu aina za bunduki hii ilikuwa bora kwangu,niliweza kuimudu vyema ilkuwa ni AK 12 bunduki ya kirusi na sio zao la nchi za kisoviet hii ilikuwa imetengenezwa Urusi kwa ubora ulio zaidi yah ii ya AK 47 iliozoeleka kwa wengi.
Nikatazama nyuma tena ila sikufanikiwa kuwaon wale watu walioanza kunikimbiza tangu nilipouvuka mto Iyumbi,mto ulioko karibu kabisa na mpaka wa Kigoma na Burundi na sasa ilikuwa yapata masaa matatu tangu nianze serekasereka ya kukimbizana na watu hawa ambao sikujua dhamira yao kwangu ni nini na kwanini waliamua kupambana na mimi na kila dakika walikuwa wanazidi kunisogelea na hata nilipo jaribu kutengeneza mazingira ya kuwakwepa bado walionesha umahiri wao katika misitu ile yam to Iyumbi.
“wanaujua msitu huu vyema” ndivyo nilivojiambia katika akili yangu na hapo nikapanga kufanya jambo ambalo naamini lingewachanganya na kuwaacha wakiwa hawajui nimeelekea wapi.
Nikasimama na kutumia hisia za mlango wa nane kuhisi umbali wa watu wale hadi kunifikia na hapo nikatuliza kabisa akili yangu,sikutaka kuisikia ile sauti ya matone ya mvua na upepo uliokuwa ukivuma kwa kasi ya ajabu usiku ule.
Kwa mbali nikaisikia sauti ya miguu ya watu zaidi ya ishirini ikikimbia kwa pamoja lakini haikuwa sauti ya miguu ya watu tu kulikuwa naziada ya miguu ya mnyama,ndio ilikuwa ni mnyama na hapo nikatambua watakuwa ni mbwa waliofunzwa na hapo nikapata jibu kwanini walidumu wakati wananikimbiza watu hawa.
Nikainama na kuvua kiatu kimoja na kubaki na soksi iliokuwa imelowa maji chapachapa nikaitupa juu ya mti ulikuwa mbele yangu hatua kadhaa na kweli ikakubali kukaa juu ya tawi moja,nilipokwisha kuhakikisha imekaa kule juu nikavaa kiatu kile kasha nikaanza kulekea kulia kwangu huku mguu mmoja ukiwa upo chini na mmoja nimeuning’iniza juu, na mikono yangu ikifanya kazi ya kuyapangua majani yaliokuwa yamefungamana na kulala chini,bunduki yangu ilikuwa ipo mgongoni ikibembea huku na huko.
Nilipotembea usawa wa mita kadhaa nikaushusha mguu ule kisha nikavua tena mguu mwingine na kutoa soksi nyingine kisha nikavaa na hpo nikaanza tena kutembea kwa kutumia mguu mmoja na kwenda kuitupa ile soksi chini ya majani kisha nikaanza tena kurudi kule nilikovulia soksi ya kwanza.
Sauti ya mbwa kubweka ilikuwa inazidi kunikaribia na hapo nikaliokota begi langu na kuliweka mgongoni huku bunduki yangu nikiihamishia kifuani mwangu kisha nikaanza tena kukimbia kwenda mbele huku nikijaribu kuona kama chenga yangu itakuwa imefanya kazi.
nilienda umbali mrefu huku nikiamini kabisa wale watu waliokuwa wakinikimbiza huku wakinirushia risasi watakuwa wamekosa mwelekeo wangu,lakini mvua ilikuwa bado inazidi kunyesha huku nikijaribu kubashiri muda huo utakuwa saa ngapi nilipojaribu kukadiria nikahisi itakuwa inaelekea saa tano za usiku na mimi sikutaka kutulia sehemu moja ili nipumzike nilihitaji kwenda mbali ili kujihakikishia usalama wangu.
*******
Yalikuwa yamepita masaa kama matatu hivi tangu nipande juu ya mti huu huku nikipumua kwa pumzi za kawaida baada ya kujitahidi kuzua zile pumzi za mchoko ziniathiri katika mwili wangu,usiku nao ulikuwa unazidi kuwa mkubwa na nilikadiria itakuwa inaelekea saaa tisa kasoro hivi na nilikuwa sijapata kitu tumboni na nilisikia tumbo likiunguruma kwa kukosa haki yake.
Nikajitikisa kidogo na nikapata egemeo zuri kisha nikalitoa begi langu mgongoni na nikaliweka karibu ya uso wangu na nikalifungua na hapo mkono wangu ukatoka na vipande vitatu vya mkate,nikalifunga lile begin a kuanza kuvifakamia viapnde vile ndani ya dakika moja tu nikawa nimemaliza kuvitia tumboni,kisha nikajipapasa kiunoni mwangu nahapo nikagusa kibuyu cha maji nilichokuwa nimekifunga kiunoni mwangu,nikanywa maji funda kadhaa lengo likiw ni kuacha mwili wangu huru bila kuupa uzito na hii ni kanuni ya mwanajeshi anapokuwa katika ulingo wa vita.
Nikiwa najaribu kutafakari mwenendo wa maisha yangu nikasikia ule mti ukitikisika,mwanzo nilijua ni ule upepo wa kufukuza mvua ulikuwa ukiyumbisha miti,laini kadri muda ulivyokuwa ukienda nilihisi ule mtikisiko sio wa upepo kuna kitu cha zaidi ya kile nilichokiwaza.
Mwanga mkali wa radi ukamulika na hapo nikapata kuona kile nilichokuwa nakihisi,nilipata kushuhudia macho kama ya paka yaking’aa kwa kunitizama mimi,kisha kukafuatiwa na muungurumo mkali wa kiumbe Yule aliekuwa akinitizama.
Damu yangu ilichemka kutokana na hatari ile na hapo nikaupa mwili wangu utayari wa kukabiliana na mnyama Yule amabae sikumuona ila niliamini ni chui au mnyama wa aina hiyo.
asalaam Kudo
(MTAZIKA KILA IKISIKIKA)
Na BAHATI MWAMBA
0758573660,0624155629
Bunduki yangu ilikuwa imeisha risasi na kitu pekee nilichokuwa nakitegemea ni hatua za miguu yangu japo maungio ya magoti yalianza kugoma kunipa ushirikiano.
Mvua kubwa ilikuwa bado inazidi kunyesha,sikuwa mnaona mbele wala sikuwa naona nyuma na mara chache sana nilijikuta nikitamani sana radi ipige tena ili niweze kuona mbele na wale waliokua wakinikimbiza nyuma niweze kuwakwepa.
Kracha,kacha..mlio huu ulizidi kunidhirishia ya kuwa sikuwa japo nimefanikiwa kubakiza risasi hata moja kwenye bunduki yangu niliopenda tangu nifahamu aina za bunduki hii ilikuwa bora kwangu,niliweza kuimudu vyema ilkuwa ni AK 12 bunduki ya kirusi na sio zao la nchi za kisoviet hii ilikuwa imetengenezwa Urusi kwa ubora ulio zaidi yah ii ya AK 47 iliozoeleka kwa wengi.
Nikatazama nyuma tena ila sikufanikiwa kuwaon wale watu walioanza kunikimbiza tangu nilipouvuka mto Iyumbi,mto ulioko karibu kabisa na mpaka wa Kigoma na Burundi na sasa ilikuwa yapata masaa matatu tangu nianze serekasereka ya kukimbizana na watu hawa ambao sikujua dhamira yao kwangu ni nini na kwanini waliamua kupambana na mimi na kila dakika walikuwa wanazidi kunisogelea na hata nilipo jaribu kutengeneza mazingira ya kuwakwepa bado walionesha umahiri wao katika misitu ile yam to Iyumbi.
“wanaujua msitu huu vyema” ndivyo nilivojiambia katika akili yangu na hapo nikapanga kufanya jambo ambalo naamini lingewachanganya na kuwaacha wakiwa hawajui nimeelekea wapi.
Nikasimama na kutumia hisia za mlango wa nane kuhisi umbali wa watu wale hadi kunifikia na hapo nikatuliza kabisa akili yangu,sikutaka kuisikia ile sauti ya matone ya mvua na upepo uliokuwa ukivuma kwa kasi ya ajabu usiku ule.
Kwa mbali nikaisikia sauti ya miguu ya watu zaidi ya ishirini ikikimbia kwa pamoja lakini haikuwa sauti ya miguu ya watu tu kulikuwa naziada ya miguu ya mnyama,ndio ilikuwa ni mnyama na hapo nikatambua watakuwa ni mbwa waliofunzwa na hapo nikapata jibu kwanini walidumu wakati wananikimbiza watu hawa.
Nikainama na kuvua kiatu kimoja na kubaki na soksi iliokuwa imelowa maji chapachapa nikaitupa juu ya mti ulikuwa mbele yangu hatua kadhaa na kweli ikakubali kukaa juu ya tawi moja,nilipokwisha kuhakikisha imekaa kule juu nikavaa kiatu kile kasha nikaanza kulekea kulia kwangu huku mguu mmoja ukiwa upo chini na mmoja nimeuning’iniza juu, na mikono yangu ikifanya kazi ya kuyapangua majani yaliokuwa yamefungamana na kulala chini,bunduki yangu ilikuwa ipo mgongoni ikibembea huku na huko.
Nilipotembea usawa wa mita kadhaa nikaushusha mguu ule kisha nikavua tena mguu mwingine na kutoa soksi nyingine kisha nikavaa na hpo nikaanza tena kutembea kwa kutumia mguu mmoja na kwenda kuitupa ile soksi chini ya majani kisha nikaanza tena kurudi kule nilikovulia soksi ya kwanza.
Sauti ya mbwa kubweka ilikuwa inazidi kunikaribia na hapo nikaliokota begi langu na kuliweka mgongoni huku bunduki yangu nikiihamishia kifuani mwangu kisha nikaanza tena kukimbia kwenda mbele huku nikijaribu kuona kama chenga yangu itakuwa imefanya kazi.
nilienda umbali mrefu huku nikiamini kabisa wale watu waliokuwa wakinikimbiza huku wakinirushia risasi watakuwa wamekosa mwelekeo wangu,lakini mvua ilikuwa bado inazidi kunyesha huku nikijaribu kubashiri muda huo utakuwa saa ngapi nilipojaribu kukadiria nikahisi itakuwa inaelekea saa tano za usiku na mimi sikutaka kutulia sehemu moja ili nipumzike nilihitaji kwenda mbali ili kujihakikishia usalama wangu.
*******
Yalikuwa yamepita masaa kama matatu hivi tangu nipande juu ya mti huu huku nikipumua kwa pumzi za kawaida baada ya kujitahidi kuzua zile pumzi za mchoko ziniathiri katika mwili wangu,usiku nao ulikuwa unazidi kuwa mkubwa na nilikadiria itakuwa inaelekea saaa tisa kasoro hivi na nilikuwa sijapata kitu tumboni na nilisikia tumbo likiunguruma kwa kukosa haki yake.
Nikajitikisa kidogo na nikapata egemeo zuri kisha nikalitoa begi langu mgongoni na nikaliweka karibu ya uso wangu na nikalifungua na hapo mkono wangu ukatoka na vipande vitatu vya mkate,nikalifunga lile begin a kuanza kuvifakamia viapnde vile ndani ya dakika moja tu nikawa nimemaliza kuvitia tumboni,kisha nikajipapasa kiunoni mwangu nahapo nikagusa kibuyu cha maji nilichokuwa nimekifunga kiunoni mwangu,nikanywa maji funda kadhaa lengo likiw ni kuacha mwili wangu huru bila kuupa uzito na hii ni kanuni ya mwanajeshi anapokuwa katika ulingo wa vita.
Nikiwa najaribu kutafakari mwenendo wa maisha yangu nikasikia ule mti ukitikisika,mwanzo nilijua ni ule upepo wa kufukuza mvua ulikuwa ukiyumbisha miti,laini kadri muda ulivyokuwa ukienda nilihisi ule mtikisiko sio wa upepo kuna kitu cha zaidi ya kile nilichokiwaza.
Mwanga mkali wa radi ukamulika na hapo nikapata kuona kile nilichokuwa nakihisi,nilipata kushuhudia macho kama ya paka yaking’aa kwa kunitizama mimi,kisha kukafuatiwa na muungurumo mkali wa kiumbe Yule aliekuwa akinitizama.
Damu yangu ilichemka kutokana na hatari ile na hapo nikaupa mwili wangu utayari wa kukabiliana na mnyama Yule amabae sikumuona ila niliamini ni chui au mnyama wa aina hiyo.
asalaam Kudo