Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

Asante.vipi unataka bando? Kazi unayofanya I really appreciate
Anahitaji support aweze kutoa vitabu, alitoa tangazo la harambee na akaomba mwenye chochote amuwezeshe!

Kweli kazi yake ni njema sana, tumsupport!
 
Tgpesa-0675191162
Mpesa-0745373585
Halpesa-0628969272

Na mie ngoja nitume naona napiga domo tu hapa!
Asante kesho nitatuma. Kutuwekea vitu bure tu na sisi tunajisomea tu ni shukran kwa kweli.kesho nitatuma
 
Safi sana ibra kitu kinasonga na utamu wake
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 026

Aliwajua wanausalama na kuwatambua. Hata wangekuwa umbali gani haikuwa shida kwake kuwafahamu. Akaendelea kuwaangalia huku akiondoka pole pole kutoka eneo lile. Utimamu wa akili bado ulimpa uhuru na uwezo wa kutenda kile ambacho alipaswa kufanya kwa wakati ule. Alijua uwezo wa wanausalama wa Tanzania. Aliutambua weledi wao. Kwahiyo alitakiwa kuwa makini kwa kila hatua. Bado alikuwa akiwaona watu wakiongezeka katika eneo husika kutokana na kumulikwa na taa za magari. Kuna ambao walikuwa wakiyumba kama walevi, wengine walikuwa wamevaa mavazi chakavu wakionekana kuokota vitu chini. Hicho ndio kitu ambacho alikitaka masimba. Alitaka kuhakikisha ni kweli alikuwa akitafutwa? Kuipiga simu akiwa pale alitambua angegundua chochote kama ni kweli namba ile ilitumiwa na watu wa usalama. Hilo likafanikiwa, hata wale walevi na omba omba waliokuwa pale ilikuwa ni mbinu ya wanausalama. Akaendelea kutizama kila kilichokuwa kikiendelea. Purukushani ilikuwa kubwa sana, purukushani ya watu na hata magari yaliokuwa yakipita huku na kule. Wana usalama wengi walikuwa wakipanda kwenye mabasi ya mwendokasi, wengine walikuwa madirishani wakichungulia kwa ndani. Ni hapo alipoiona gari aina nissan patrol ikitembezwa taratibu. Haikuwa gari ngeni machoni mwake, ilikuwa gari anayoifahamu vizuri tu. Ilikuwa gari ambayo ilitumiwa mara nyingi na watu tofauti wa idara. Hii ilikuwa gari iliyotumiwa mara nyingi na kitengo kimoja ambacho kipo ndani ya Idara. Kitengo ambacho hujulikana kama black mambaz. Macho yake yakazidi kuitizama gari ile. Wakati ikielekea katikati ya jiji, masimba naye alisimamisha pikipiki, akamuomba aifiatilie gari iliyombele yao kwa siri. Dereva yule hakubisha, taratibu akaanza kuifuatilia gari ile ambayo sasa ilikuwa ikielekea maeneo ya posta mpya. Muda wote masimba alikuwa akiitizama ile gari. Alitaka kujua ni wapi inapoelekea. Akamwambia dereva aache magari manne yatangulie mbele yao ili kutokuwagutusha watu waliokwenye gari. Dereva wa pikipiki akatiii. Akaendesha huku akiwa makini na kila kitu. Punde wakaiona gari ikiingia barabata ya Allhasan Mwinyi. Magari ya mbele yao nayo yakaelekea huko. Wakaendelea kuifuatilia ile gari. Baadaa ya kupita daraja la salenda ile gari ikaacha barabara Ally Hassan Mwinyi ikaingia barabara ya kinondoni. Hapo dereva akageuka kumuangalia masimba. Masimba akampa ishara ya kuendelea kuifuatilia kwa nyuma. Baada ya kuifuatilia kwa muda wakaiona gari ile ikisimama maeneo ya kinondoni Manyanyq. Masimba akamwambia dereva yule aipite ile gari pasipo kuonyesha wasiwasi wowote. Baada ya kuipita ile gari na kutembea mbele kidogo. Masimba akamwambia asimame hapa, akachomoa noti tatu za Elfu kumi na kumkabidhi yule dereva. Baada ya kumkabidhi aliondoka taratibu kurudi nyuma pale ilipoegesha gari waliokuwa wakiifiatilia. Alitembea kwa umakini mkubwa mpaka jirani kabisa na iliposimama ile gari. Akaangaza macho yake kwa umakini kule gizani. Punde akawaona watu wawili ambao wakikuwa wamesimama kwa kumpa mgongo. Walikuwa wamevaa mabaibui kuficha sura zao, lakini maumbo yao hayakumfanya masimba kupotea. Mbele yake alikuwa akiwatizama Teddy Sambamba na Mwamvita wakiwa wamempa Mgongo. Hapo akaongeza umakini, sasa alikuwa akiwaangalia kwa karibu zaidi. Bado walionekana wakiongea kitu, bado walionekana kulikuwa na mazungumzo yakifanyika. Punde akaiona gari ya kifahari ikisogea taratibu katika eneo lile. Ilikuwa gari ya bei mbaya, gari ambayo thamani yake iliweza kuhudumu kwenye wizara kama tatu za hapa nyumbani. Wakati akiendelea kuiangalia ile gari ikisogea, macho yake yakavutiwa na watu wawili wengine waliongezeka pale. Kitendo bila kuchelewa akawaona watu wale wakimuongoza teddy kuelekea kwenye ile gari ambayo bado ilikuwa ikitembea. Akaliangalia tena lile tukio la teddy kupelekwa kwenye gari. Haukuwa ukokotwaji wa kawaida,haukuwa ukokotwaji wa hiari bali ulikuwa ukokotwaji wa lazima. Kwani kuna wakati teddy alikuwa akigoma lakini alikuwa akilazimishwa kwa mtutu wa bunduki. Kilikuwa kitendo kilichofanyika kwa muda wa nusu dakika na hata alipoifikia gari na mlango kufunguliwa akashuhudia pigo la kitako cha bastola likitua kisogoni kwa Teddy. Hilo likaufanya mwili wake kuingiwa na ganzi, damu kusimama kwa muda huku mwili wake ukitetemeka. "Naam mapenzi yalichukua sehemu yake. Aliumia sana katika kile ambacho kilitendwa kwa Teddy. Licha ya yote aliotendewa na teddy bado alimpenda. Bado alimuhitaji katika kina cha moyo wake. Akaendelea kushangaa na kuduwaa. Teddy alikuwa akiadhibiwa, teddy alikuwa akipelekwa sehemu ambayo si salama kwake. Alitambua kama angemuacha bila kufanya kitu basi asingemuona teddy akiwa hai tena. Hakulikubali hilo na hakuwa tayari. Ilikuwa lazima afanye jambo, jambo la kumuokoa teddy. Lakini hawa waliomchukua ni nani? Na wanampeleka wapi? Haukuwa muda wa kutafuta majibu wala kujiuliza maswali. Muda mfupi alikuwa kwenye tax wakiwa nyuma ya gari iliyombeba teddy, wakiifuatilia kwa nyuma. Muda wote alimhimiza dereva kuongeza kasi na kuhakikisha gari ya mbele haiwapotei. Hilo likafanywa kwa umakini, bado katikati yao waliyaacha magari matatu kama kanuni nyingi za kipelelezi zilivyo. Mpaka wanafika magomeni usalama na gari kuonyesha ishara ya kuingia barabara ya morogoro hata wao wakafanya hivyo. Kufika mbele kidogo eneo la magomeni usalama, wakaiona gari wanayoifuata Ikiingia maeneo ya ukumbi maarufu kwa burudani ya muziki wa mwambao uitwao Travertine Hotel. Baada ya gari ilikukatisha na kuingia kabisa masimba alishuka kwa haraka ni baada ya kulipa ujira wa Dereva, akaongoza kama mtu wa kawaida kuelekea hotelini hapo. Bastola zilikuwa kila upande ndani ya mavazi yake. Hatua tano mbele akakutana na madada poa wanaofanya biashara ya kuuza mili yao katika eneo hilo. Akamuita mmoja na kusimama naye pembeni kama wafanyavyo wanunuzi. Lakini yeye hakumuita hapo kwa sababu ya kutaka huduma, bali alitaka kuutumia kama moja ya kuzuga ili ajue ni wapi twddy anapelekwa. Akasimama na yule binti tena ni baada ya kumpa yule chqngudoa elfu kumi. Macho yake yalikuwa yakitizama kule iliposimama ile gari. Akaushuhudia mlango ukifunguliwa. Kwa kuwa palikuwa karibu sana, alikuwa akishudia kila kitu ambacho kilikuwa kikitendeka.

Baada ya mlango wa gari kufunguliwa wakashuka watu watatu tofauti na wale wa mwanzo. Kati yao mmoja wao alikuwa amebeba kitu kama furushi begani. Baada ya watu wale kushuka wakaongoza moja kwa moja kwenda ndani upande wa hotel. Bado masimba alitulia akichunguza kila kitu. Baada ya watu wale kuingia ndani, huku nyuma mlango wa kati ukafunguliwa tena. Mara hii akashuka mtu mzima ambaye sura yake ilifunikwa kwa kofia ya pama. Baada yq mtu yule kushuka akaonekana akiongozwa na walinzi ambao kwa kuwaangalia tu.. walikuwa ni walinzi wale wa kulinda viongozi wa Kitaifa. Lakini hapa walionekana wakimlinda huyu mtu aliyeshuka kwenye gari. Haikuwa sawa kwa presidential protect unit kuwa katika eneo hili tena kwa mtu ambaye hahusiki na serikali. Hilo likampa wasiwasi wa kutaka kujua zaidi. Teddy kupelekwa ndani, kisha mtu huyu kushuka naye kuelekea huko kilikuwa kitendo kilichomshtua. Hatua ya kwanza aliipiga akimuacha yule changudoa akishangaa. Hatua ya pili, changudoa hakukubali naye akawa anafuata kwa nyuma. Hatua ya tatu alishamfikia masimba na sasa walikuwa wakitembea sambamba wakizipanda ngazi wakiwa kama wa penzi. Kwa kuwa kulikuwa na giza hakuna aliyeweza kumgundua. Baada ya kumaliza ngazi na kutokea mapokezi akashangazwa na watu waliotapakaa. Watu ambao sura zao zilikuwa zikiongea lugha moja. WOTE WALIKUWA MAIFISA USALAMA WA TAIFA.
ITAENDELEA
 
Thaks sana kwa hatua hizi za kusonga mbele
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 027

Watu waliokuwa wakiongea lugha moja, watu ambao kwa kuwaangalia wangekujulisha wao ni kina nani. Masimba bado akilimshikilia changudoa wake. Mwili na mikono vikiwa kwenye utayari. Hata yeye macho yake yalikuwa yakiwatizama. Sasa alikuwa akienda mapokezi na changudoa wake. Changudoa aliemuokota nje na kumfanya kama chambo cha kumuingiza hapo hotelini. Kufika mapokezi hakuongea chochote zaidi ya kuchomoa bulungutu la pesa na kuliweka juu ya meza ya mapokezi. Mhudumu alitmhamaki kutokana na wingi wa pesa zilizowekwa mezani. Hata changudoa naye alikuwa katika hamaniko, hamaniko lililozaa sononeko la moyoni. Alikuwa akiitafuta pesa kwa kuuza utu wake, lakini leo hii amakutana na mtu anayeitumia pesa kwa fujo. Wote wakabaki wameduwaa wakiisubiria kauli ya masimba. Kauli kuhusu matumizi ya pesa ile. "Nataka kujua watu waliobeba mzigo wamekwenda chumba namba ngapi. " ilikuwa sauti iliopenya masikioni mwa watu hawa wawili, mhudumu na changudoa. Hawakujibu wala kupata jibu kwa wakati ule. Huyu ni nani? Na kwa nini anataka kujua? Yalikuwa maswali ambayo hayakupata majibu kwa wakati ule. "Fanya hivyo uchukue pesa kama hutaki hii hapa itakuwa zawadi yak0." Alinong'ona safari hii sura yake ikiwa haina masihara. Wasichana wote waliduwaa. Hawakuduwaa kwa kutokujua cha kufanya, bali waliduwaa baada ya kuuona mdomo wa bastola ukichungulia. Binti akatii bila kuonyesha wasiwasi. Akainuka na kuwapa ishara wafuatane. Ishara ambayo haikuonekana popote. Bado changudoa alikuwa mkono wake wa kushoto. Walitembea kwa hatua za umakini huku macho yake yakitambazwa kila sehemu kwa utulivu. Wakawapita wanausalama na kuanza kuipanda ngazi kuelekea juu. Hatua tano baada ya kutokea kwenye korido wakauona mlango wa mbele ukifunguliwa. Watu wawili aliowafahamu walikuwa wakitoka hapo. Alikuwa Jimmy sambamba na mtu mwingine mwenye asili ya kihindi. Masimba akainama kisha kuonekana akimbusu changudoa yule.alifanya kitendo kile mpaka pale walipopishana na watu wale ndio wakaacha. Hapa akaukuta uhuru, hapakuwa na wanausalama na hapakuwa na mtu mwingine. Ishara ikafuata kutoka kwa mhudumu yule. Ishara ya kuwaonyesha kwamba hapa ndio sehemu yenyewe. Akaimpa ishara ya mwanamke yule kuugonga mlango. Muda wote yeye alikuwa ameikamata bastola akitizama nyuma. Mhudumu akaugonga mlango kwa mara ya kwanza, kukapita kimya, mara ya pili bado hapakuwa na mtu wa kujibu. Wakati mhudumu yule akigeuka amuulize masimba cha kufanya,. Mlango ukafunguliwa kisha mtu kuchungilia. Kilikuwa kitendo cha nusu dakika kufanywa na Masimba. Kwani wakati dakika inatimia masimba Alikuwa ndani huku mtu yule aliyechungulia akivuja damu. Macho yake yalishatambaa kila upande mle chumbani na kukinasa kitu kilichompandisha Hasira. Teddy alikuwa juu ya kitanda akiwa na nguo ya ndani tu, huku fahamu zikiwa bado zimempotea. Hakushughulika sana na teddy. Bastola yake ilikuwa ikimuangalia mtu yule. Hata alipomuangalia mtu yule na macho yao kuonana hakuamini. Hakuamuni mtu aliyekuwa akitizamana naye. Hakuamini kumuona mtu huyu akiwa chumbani na Teddy. Alikuwa kiongozi mzito wa serikali. Kiongozi wa ngazi za juu kabisa katika nchi husika. Mtu mwenye jina kubwa katika jamii na katika nyanja za kimataifa. Alimuangalia kisha kumuangalia teddy pale kitandani. Haukupita muda sauti ya chafya ikasikika ndani ya chumba kile. Damu ikaruka na kusambaa chumba kizima. Yule changudoa hakutegemea kuliona lile tukio kufanywa na mtu huyu aliyemchukulia kama mteja. Akataka kupiga kelele lakini alipouona mdomo wa bastola unamtizama, akanyamaza akibaki anatetemeka. Macho yake yalikuwa yakiutizama mwili wa kiongozi wa nchi ukiwa umalala katikati ya dimbwi la damu. Masimba akaufunga mlango kwa ndani kisha kumvuta mwanamke yule.

"Sikiliza naomba unisikilize kwa makini. Ukileta ukaidi kilichompata huyo mtu hapo hata wewe kitakupata. Nataka tuondoke humu ndani tukiwa na huyu dada kwa kupitia mlango wa dharura wa hoteli hii. Sasa chukua hii bastola, mimi nitambeba huyu mwanamke, wewe utakuja nyuma yangu ukinilinda. Yoyote ambaye atajitokeza piga risasi. Umenielewa?

Changudoa yule akajibu kwa kutingisha kichwa. Akachukua mavazi ya Teddy na kumvisha. Muda mfupi walikuwa Nje ya chumba kile wakielekea nyuma ya hoteli kwenye mlango wa dharura. Kilikuwa kitendo kilichotendeka kwa muda mfupi sana. Kitendo ambacho hakikuchukua hata dakika mbili. Wakatembea kwa uhuru bila kukutana na chochote. Mpaka wanatokea nje hawakuonekana na mtu yoyote. Baada ya kufika nje wakaivuka barabara kama wanaelekea magomeni mapima. Hatua kadhaa mbele wakaiona tax mbele yao, wakaisimamisha, kisha kumuomba jamaa awapeleke kimara mwisho. Dereva akawasha gari na safari ya kimara kuanza. Baada ya kutembea mpaka magomeni mwembe chai, masimba akachomoa burungutu la pesa na kumpa yule changudoa.

"Shuka hapa nitakutafuta, lakini nakuomba ufumbe mdomo wako." Akanong'ona masimba huku akimpa kile kitita. Binti akakipokea huku akionyesha wasiwasi. Hiyo haikuwa dalili nzuri kwa masimba. Baada ya kushuka na kuondoka masimba akamuomba dereva ashuke amfuatie msichana yule kwani kuna kitu ambacho alisahau kumwambia. Dereva hakuwa na hiyana, akaipaki gari pembeni mwa barabara. Masimba akashuka na kuanza kumfuatilia mwanamke yule bila mwenyewe kujua kama anafuatiliwa. Ilimchukua masimba dakika tano kuifahamu nyumba ambayo anaishi msichana yule. Baada ya kuigundua nyumba ile akarudi kwenye gari.

*******

Siku zote kazi ya kijasusi huwaga hazitakiwi kuacha ushahidi nyuma. Kifo cha kiongozi yule wa nchi alijua kitaibua mambo mengi sana. Alijua msako utakuwa mkali na hoteli nzima lazima ipekuliwe. Alitambua wahudumu na hata baadhi ya wapangaji watatiwa kashkash kutokana na hilo. Ni katika kashkash hizo nipo watakapo mpata mhudumu ambaye alikuwa zamu katika siku hiyo. Alitambua akipatikana mwanamke yule basi na hata yule changudoa angepatikana. Hapo kila kitu kingewekwa wazi na angejulikana kwamba ni yeye aliyetengeneza mauaji hayo. Baada ya kuwaza sana akaona hakuna njia nyingine zaidi ya kuwafuta watu hawa wawili kwenye ulimwengu. Ilikuwa ni lazima mhudumu auawe na ilikuwa bora zaidi kwa changudoa yule kuondolewa uhai ili kuufuta ushahidi. Hilo hakutaka kulifanya yeye, hili aliamua kumpa rafiki yake. Akachomoa simu yake na kubonyeza namba kadhaaa. Akaipeleka simu sikioni. Baada ya muda simu ikapokelewa.

"Don." Ilisikika sauti kutoka upande wa pili.

"Dee plus kuna watu wawili nahitaji uwasafirishe kuzimu usiku huu kabla ya jua la asubuhi." Alinong'ona Masimba.

"Nipe ramani, nina hamu sana ya kupambana." Alijibu Dee plus.

Muda mfupi alikuwa akipewa maelezo yote ya kufuata kufanikisha safari za watu hao.

"Nimekuelewa Don, nimeshachukua tiketi zao nawapelekea muda sio mrefu." Akajibu De plus. Masimba akakata simu kisha kugeuka na kumtizama teddy pale kitandani. Alikuwa akimpenda sana teddy. Akajisogeza na kujilaza pembeni yake.

******
Ilikuwa yapata saa kumi na mbili za asubuhi, wananchi wengi wakiwa bado vitandani.. Kila mmoja alishtushwa na wimbo wa Taifa kupigwa asubuhi ile. Hakikuwa kitu kiliozoeleka kwa watu. Punde ikasikika sauti ya kiongozi wa nchi akitangaza kitu ambacho kilimshtua kila mtu.

"Ndugu wanachi, nasikitika kutangaza kifo cha Waziri wenu mkuu kilichotokea usiku wa jana. Nawaomba wote muwe kwenye utulivu katika kipindi hiki kigumu. Mambo mengine mtaendelea kupewa kadili muda utakavyo kwenda."... ilikuwa taarifa iliomsha watu, watu wakaanza kukaa vikundi vikundi wakiongea hili na lile. Kila mmoja akionyesha kuguswa na kifo cha kiongozi huyu wa nchi. Wakati watu wakiendelea kuhuzunika, upande mwingine, wanausalama walikuwa wakihaha kila sehemu kutafuta chochote cha kuwasaidia lakini haikuwa hivyo. Hawakupata chochote. Ni wakati huo walipopqta taarifa kuwa kuna changudoa mmoja alionekana akiwa na mwanaume ambaye anahisiwa kufanya mauaji hayo.

ENDELEENI KUNICHANGIA KUPITIA 0745373585 M PESA

0675191162 TIGO PESA. ILI NIFANIKISHE LENGO LANGU LA KUTOA VITABU. HIKI MNACHOKISIFIA HAPA KIMEUCHUKUA MUDA WANGU SANA. JITOLEE KUNI SAIDIA KUTIMIZA NDOTO HIZO.
 
Asante Ibra, unajua mi ni mchangiaji ilani Leo nipo alosto mbaya. Usikawie kurudi. Pia amini tu za kitabu utapata. Usikawie sana kurudi tena.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom