NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 026
Aliwajua wanausalama na kuwatambua. Hata wangekuwa umbali gani haikuwa shida kwake kuwafahamu. Akaendelea kuwaangalia huku akiondoka pole pole kutoka eneo lile. Utimamu wa akili bado ulimpa uhuru na uwezo wa kutenda kile ambacho alipaswa kufanya kwa wakati ule. Alijua uwezo wa wanausalama wa Tanzania. Aliutambua weledi wao. Kwahiyo alitakiwa kuwa makini kwa kila hatua. Bado alikuwa akiwaona watu wakiongezeka katika eneo husika kutokana na kumulikwa na taa za magari. Kuna ambao walikuwa wakiyumba kama walevi, wengine walikuwa wamevaa mavazi chakavu wakionekana kuokota vitu chini. Hicho ndio kitu ambacho alikitaka masimba. Alitaka kuhakikisha ni kweli alikuwa akitafutwa? Kuipiga simu akiwa pale alitambua angegundua chochote kama ni kweli namba ile ilitumiwa na watu wa usalama. Hilo likafanikiwa, hata wale walevi na omba omba waliokuwa pale ilikuwa ni mbinu ya wanausalama. Akaendelea kutizama kila kilichokuwa kikiendelea. Purukushani ilikuwa kubwa sana, purukushani ya watu na hata magari yaliokuwa yakipita huku na kule. Wana usalama wengi walikuwa wakipanda kwenye mabasi ya mwendokasi, wengine walikuwa madirishani wakichungulia kwa ndani. Ni hapo alipoiona gari aina nissan patrol ikitembezwa taratibu. Haikuwa gari ngeni machoni mwake, ilikuwa gari anayoifahamu vizuri tu. Ilikuwa gari ambayo ilitumiwa mara nyingi na watu tofauti wa idara. Hii ilikuwa gari iliyotumiwa mara nyingi na kitengo kimoja ambacho kipo ndani ya Idara. Kitengo ambacho hujulikana kama black mambaz. Macho yake yakazidi kuitizama gari ile. Wakati ikielekea katikati ya jiji, masimba naye alisimamisha pikipiki, akamuomba aifiatilie gari iliyombele yao kwa siri. Dereva yule hakubisha, taratibu akaanza kuifuatilia gari ile ambayo sasa ilikuwa ikielekea maeneo ya posta mpya. Muda wote masimba alikuwa akiitizama ile gari. Alitaka kujua ni wapi inapoelekea. Akamwambia dereva aache magari manne yatangulie mbele yao ili kutokuwagutusha watu waliokwenye gari. Dereva wa pikipiki akatiii. Akaendesha huku akiwa makini na kila kitu. Punde wakaiona gari ikiingia barabata ya Allhasan Mwinyi. Magari ya mbele yao nayo yakaelekea huko. Wakaendelea kuifuatilia ile gari. Baadaa ya kupita daraja la salenda ile gari ikaacha barabara Ally Hassan Mwinyi ikaingia barabara ya kinondoni. Hapo dereva akageuka kumuangalia masimba. Masimba akampa ishara ya kuendelea kuifuatilia kwa nyuma. Baada ya kuifuatilia kwa muda wakaiona gari ile ikisimama maeneo ya kinondoni Manyanyq. Masimba akamwambia dereva yule aipite ile gari pasipo kuonyesha wasiwasi wowote. Baada ya kuipita ile gari na kutembea mbele kidogo. Masimba akamwambia asimame hapa, akachomoa noti tatu za Elfu kumi na kumkabidhi yule dereva. Baada ya kumkabidhi aliondoka taratibu kurudi nyuma pale ilipoegesha gari waliokuwa wakiifiatilia. Alitembea kwa umakini mkubwa mpaka jirani kabisa na iliposimama ile gari. Akaangaza macho yake kwa umakini kule gizani. Punde akawaona watu wawili ambao wakikuwa wamesimama kwa kumpa mgongo. Walikuwa wamevaa mabaibui kuficha sura zao, lakini maumbo yao hayakumfanya masimba kupotea. Mbele yake alikuwa akiwatizama Teddy Sambamba na Mwamvita wakiwa wamempa Mgongo. Hapo akaongeza umakini, sasa alikuwa akiwaangalia kwa karibu zaidi. Bado walionekana wakiongea kitu, bado walionekana kulikuwa na mazungumzo yakifanyika. Punde akaiona gari ya kifahari ikisogea taratibu katika eneo lile. Ilikuwa gari ya bei mbaya, gari ambayo thamani yake iliweza kuhudumu kwenye wizara kama tatu za hapa nyumbani. Wakati akiendelea kuiangalia ile gari ikisogea, macho yake yakavutiwa na watu wawili wengine waliongezeka pale. Kitendo bila kuchelewa akawaona watu wale wakimuongoza teddy kuelekea kwenye ile gari ambayo bado ilikuwa ikitembea. Akaliangalia tena lile tukio la teddy kupelekwa kwenye gari. Haukuwa ukokotwaji wa kawaida,haukuwa ukokotwaji wa hiari bali ulikuwa ukokotwaji wa lazima. Kwani kuna wakati teddy alikuwa akigoma lakini alikuwa akilazimishwa kwa mtutu wa bunduki. Kilikuwa kitendo kilichofanyika kwa muda wa nusu dakika na hata alipoifikia gari na mlango kufunguliwa akashuhudia pigo la kitako cha bastola likitua kisogoni kwa Teddy. Hilo likaufanya mwili wake kuingiwa na ganzi, damu kusimama kwa muda huku mwili wake ukitetemeka. "Naam mapenzi yalichukua sehemu yake. Aliumia sana katika kile ambacho kilitendwa kwa Teddy. Licha ya yote aliotendewa na teddy bado alimpenda. Bado alimuhitaji katika kina cha moyo wake. Akaendelea kushangaa na kuduwaa. Teddy alikuwa akiadhibiwa, teddy alikuwa akipelekwa sehemu ambayo si salama kwake. Alitambua kama angemuacha bila kufanya kitu basi asingemuona teddy akiwa hai tena. Hakulikubali hilo na hakuwa tayari. Ilikuwa lazima afanye jambo, jambo la kumuokoa teddy. Lakini hawa waliomchukua ni nani? Na wanampeleka wapi? Haukuwa muda wa kutafuta majibu wala kujiuliza maswali. Muda mfupi alikuwa kwenye tax wakiwa nyuma ya gari iliyombeba teddy, wakiifuatilia kwa nyuma. Muda wote alimhimiza dereva kuongeza kasi na kuhakikisha gari ya mbele haiwapotei. Hilo likafanywa kwa umakini, bado katikati yao waliyaacha magari matatu kama kanuni nyingi za kipelelezi zilivyo. Mpaka wanafika magomeni usalama na gari kuonyesha ishara ya kuingia barabara ya morogoro hata wao wakafanya hivyo. Kufika mbele kidogo eneo la magomeni usalama, wakaiona gari wanayoifuata Ikiingia maeneo ya ukumbi maarufu kwa burudani ya muziki wa mwambao uitwao Travertine Hotel. Baada ya gari ilikukatisha na kuingia kabisa masimba alishuka kwa haraka ni baada ya kulipa ujira wa Dereva, akaongoza kama mtu wa kawaida kuelekea hotelini hapo. Bastola zilikuwa kila upande ndani ya mavazi yake. Hatua tano mbele akakutana na madada poa wanaofanya biashara ya kuuza mili yao katika eneo hilo. Akamuita mmoja na kusimama naye pembeni kama wafanyavyo wanunuzi. Lakini yeye hakumuita hapo kwa sababu ya kutaka huduma, bali alitaka kuutumia kama moja ya kuzuga ili ajue ni wapi twddy anapelekwa. Akasimama na yule binti tena ni baada ya kumpa yule chqngudoa elfu kumi. Macho yake yalikuwa yakitizama kule iliposimama ile gari. Akaushuhudia mlango ukifunguliwa. Kwa kuwa palikuwa karibu sana, alikuwa akishudia kila kitu ambacho kilikuwa kikitendeka.
Baada ya mlango wa gari kufunguliwa wakashuka watu watatu tofauti na wale wa mwanzo. Kati yao mmoja wao alikuwa amebeba kitu kama furushi begani. Baada ya watu wale kushuka wakaongoza moja kwa moja kwenda ndani upande wa hotel. Bado masimba alitulia akichunguza kila kitu. Baada ya watu wale kuingia ndani, huku nyuma mlango wa kati ukafunguliwa tena. Mara hii akashuka mtu mzima ambaye sura yake ilifunikwa kwa kofia ya pama. Baada yq mtu yule kushuka akaonekana akiongozwa na walinzi ambao kwa kuwaangalia tu.. walikuwa ni walinzi wale wa kulinda viongozi wa Kitaifa. Lakini hapa walionekana wakimlinda huyu mtu aliyeshuka kwenye gari. Haikuwa sawa kwa presidential protect unit kuwa katika eneo hili tena kwa mtu ambaye hahusiki na serikali. Hilo likampa wasiwasi wa kutaka kujua zaidi. Teddy kupelekwa ndani, kisha mtu huyu kushuka naye kuelekea huko kilikuwa kitendo kilichomshtua. Hatua ya kwanza aliipiga akimuacha yule changudoa akishangaa. Hatua ya pili, changudoa hakukubali naye akawa anafuata kwa nyuma. Hatua ya tatu alishamfikia masimba na sasa walikuwa wakitembea sambamba wakizipanda ngazi wakiwa kama wa penzi. Kwa kuwa kulikuwa na giza hakuna aliyeweza kumgundua. Baada ya kumaliza ngazi na kutokea mapokezi akashangazwa na watu waliotapakaa. Watu ambao sura zao zilikuwa zikiongea lugha moja. WOTE WALIKUWA MAIFISA USALAMA WA TAIFA.
ITAENDELEA