Riwaya: Nitakupata tu

NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 020

Kitu cha Baridi kikagusa kichwani, kisha sauti nzito ikafuatia.. TULIA HIVYO HIVYO. Teddy akatulia kama alivyoamliwa. Akili yake ilitakiwa kufanyakazi zaidi ya uwezo wake. Alitakiwa kufanyakitu ambacho kingemtoa sehemu ile. Akatii na kutulia zaidi na zaidi. Hakutaka kuwa kondoo kufuata kila anachoambiwa. Mikono ilikuwa juu kuonyesha kutii amri. Sauti ikaamrisha tena, safari hii sauti ikimwambia atembee kuelekea kule ilipo nyumba ya Jimmy Lambert bila kugeuka nyuma. Ni kweli teddy hakugeuka, ni kweli teddy aliongoza kuelekea alipoambiwa. Muda wote alitembea akicheza na kivuli cha mtu wa nyuma yake, mtu ambaye alimshikia bastola. Hatua ya kwanza mpaka ya tano zilipotea pasipokufanya kitu, sio kama hakupenda, sio kwanba hakutaka kufanya, alitaka na alitanani sana, lakini bado umbali ulikuwa tatizo, wakati wakiianza hatua ya sita, teddy akakisikia kishindo na ukelele kutoka nyuma yake. Akakumbuka kutakiwa kutokugeuka, hakugeuka.. lakini hatua moja nyingine akagundua kutokukiona kivuli cha mtu ambaye alikuwa nyuma yake. Hilo likamfanya ageuke sasa.. akageuka.. Cha kwanza kukiona ni mwili wa mtu uliolala kuonyesha kuwa haukuwa na uhai. Hilo halikumshangaza sana, alijua Masimba alikuwa nyuma akimlinda. Hilo likampa uhueni na moyo wa kusonga mbele. Alikuwa ameamua Kumuona Jimmy Lambart. Hakuwa na hofu lakini hakutaka kujiamini tena. Muda wote alitembea akiwa makini kwa kila hatua. Alitaka kuzijua mbivu na mbichi. Hakuhofia na wala hakuogopa. Muda mfupi alikuwa nyuma ya uzio wa Jumba la Jimmy. Kwa kuwa alilijua lile jengo kwa undani zaidi, akaamua kuingia kwa kuruka uzio. Muda mfupi alikuwa akitua ndani bila kutoa kishindo. Kutoka hapo akachapuka mpaka pembeni mwa mlango wa kuingilia ndani kabisa. Hapo akatulia kwa muda kusikiliza kama kuna mtu yoyote, lakini bado ukimya ulimpa majibu kuwa hapakuwa na mtu. Akaunyoosha mkono wake mpaka sehemu ya chini ya mlango. Akagusa sehemu na bila kuchelewa mlango ukajifungua. Baada ya mlango kufunguka, akaichomoa bastola yake na kuingia ndani kwa tahadhali kubwa. Mdomo wa bastola ulikuwa umetangulia mbele tayari kwa kufanya kazi. Bado hapakuwa na sauti za kitu chochote ambacho kingemtambulisha uwepo wa watu ndani ya jumba lile. Kimya kilichukua nafasi yake, kimya kilichofanya Teddy aendelee kusogea na kusogea. Akavipita vyumba viwili pasipokusikia chochote kile. Hilo likamfanya aamini kuwa Jimmy hakuwepo hapo ndani. Alimtambua jimmy awapo nyumbani huwa mtu wa kupendelea muziki. Ukimya huo ulimaanisha kwamba hapakuwa na mtu ndani ya jengo hilo. Akaendelea kusonga mbelembele. Mdomo wa bastola ukiendelea kutangulia mbele. Akaukuta ukumbi ambao mara nyingi waliutumia kwa mikutano. Hapo bado macho yake hayakukiona kitu. Bado hakufanikiwa kumuona yoyote. Bado ukimya uliichukua sehemu kubwa. Bado akaivuta subira, bado aliitaka subira tayari kumsubiri, lakini hilo likapotea baada ya kuusikia mngurumo wa gari kutoka nje, kisha kuishia hapo hapo pasipokuendelea. Akaamini kuwa Huyo alikuwa Jimmy, hata sauti ya geti kufunguliwa ilipopenya masikioni mwake, alitambua kuna mtu alikuwa akiingia. Mawazo kuwa Jimmy ndiye yalikuwa asilimia themanini. Akajivuta mpaka karibu na mlango wa kungilia ndani kwa upande wa mbele ya nyumba. Hapo akatulia akiisubiri hatma ya mtu huyo.

Haukupita muda akakiona kitasa kikitingishwa kisha mlango kufunguliwa. Watu watatu wakaingia bila wasiwasi. Lakini Jimmy hakuwa mmoja mmoja wao. Hawa walikuwa wengine, hawa walikuwa wageni kwake. Kwa kuwaangalia walikuwa wageni kabisa. Akaendelea kuwatizama vijana wale. Aliwaangalia katika utulivu mkubwa. Kutokuwepo kwa Jimmy kulimshangaza sana. Haikuwahi kutokea Jimmy kuwatanguliza watu nyumbani kwake bila yeye mwenyewe kuwepo. Aliwatizama watu wale walivyojibweteka pale sebuleni, moyoni akacheka. Alitabasamu na hata kufurahi. Alikuwa na uwezo wa kuwamaliza kwa risasi, alikuwa na uwezo wa kufanya chochote, lakini hakutaka kufanya hivyo. Alihitaji subira, ni subira ambayo ingemkutanisha na Jimmy. Ni kweli, katika muda ule ule akamuona Jimmy akiingia sambamba na mwanamke. Aliwatizama walivyokuwa wakitembea. Alikuwa na uwezo wa kuwapiga risasi kwa urahisi, lakini hakupenda kufanyq hivyo. Wakati Jimmy na mwanamke yule wakitembea kuelekea sebuleni. Jambo jingine la kuustajabisha kama sio kushangaza likatokea. Nyuma ya Jimmy na mwanamke yule, akamuona masimba naye akitokea. Akitokea akitembea kikawaida kana kwamba alikuwa akiingia nyumbani kwake. Hili nalo likimfurahisha, hili nalo likamfanya sasa asitishe kufanya chochote aendelee kumshangaa Masimba. Ilikuwa pichq nzuri iliovutia kuitazama. Hata pale jimmy alipokuwa akijibweteka ndipo nadhani alimuona masimba. Mshtuko alioupata Jimmy baada ya kumuona masimba ndani ya nyumba yake, iliwafanya vijana wake waipeleke mikono yao mifukoni mwao tayari kwa kutoa bastola.

Hakuna aliyeujua wepesi wa masimba, hakuna aliyejua ni muda gani masimba alitumia, lakini wote wakajikuta wakimtizama mwenzao ambaye alikuwa akigalagala chini baada ya kulimwa shaba ya kifua. Hakuna aliyeamini, Jimmy ndio hakuamini kabisa. Macho yake yalimtoka mishipa ya usoni ikaonekana. Midomo miwili ya bastola ilikuwa ikimtizama. Masimba hakuonyesha utani, macho yake yalikuwa yakiwaka na kuwaka. Jimmy akatamani kuongea lakini sauti haikutoka. Mate yalimkauka na maneno hayakutoka kabisa. Alikuwa akimsikia masimba lakini hakuwahi kuonana naye. Leo alikuwa akimuangalia, huku pia midomo miwili ikimtizama.

"Jimmy nadhani kiburi chako cha kuwa karibu na viongozi imekupa mamlaka ya kujipa utawala katika nchi hii. Unaonekana una nguvu kuliko Rais, Makamu wake na Waziri mkuu. Imekupa mamlaka ya kuua watu wasio na hatia kwa sababu ya kufanikisha biashara yako haramu. Asteria anakosa gani hadi kumuua? Uchungu wa taifa lake ndio kisa cha kumuua. Dada wa Asteria na mumewe Godfrey Maboba sambamba na mtoto wao, ni kosa lipi wamefanya? Sasa leo nimekuja na mimi. Nimechoka kutumiwa watu wa Idara ya Usalama wa taifa. Nimechoka kupambana na watu wengine kwa ajili yako. Sasa nataka uniambie ukweli kabla sijaruhus......... kabla hajamalizia maneno yake mlango ukasukumwa kwa nguvu, wakaingia watu watatu na kuanza kuvurumisha risasi pale alipokaa Masimba.. Lakini hazikumkuta, bali zilipita na kutua kwa kichana mwingine, yowe la Uchungu likamtoka. Watu wale wakaendelea kushambulia bila tahadhali. Hawakujua Teddy alikuwepo pale, hawakujua kwamba alikuwa nyuma yao tena na Bastola mbili katika mikono yake, huku vidole vikiwa kwenye trigger tayari kwa Kuruhusu Risasi
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 021

Hawakujua kwamba nyuma yao alikuwepo teddy, tena akiwa na bastola mbili mikononi, vidole viwili vikiwa tayari kwenye trigger kuruhusu risasi. Alikuwa akizihesabu sekunde, hakutaka kufanya kwa haraka sana kukifanya kile alichotaka kukifanya. Sekunde ya kwanza ilipita wakati kidole bado kikiwa kwenye kitufe cha kuruhusu risasi. Hata sekunde ya pili ikapita patupu pasipo kitendo chochote. Lakini sekunde ya tatu haikupita na kwenda bure, bastola ikakohoa mara tatu mfululizo, risasi zikatua na kupenya pale zilipoagizwa, watu watatu walikuwa chini wakivuja damu katika kuonyesha hawakuwa hai. Kilikuwa kitendo mujarabu machoni kwa Teddy, kitendi kilicho mfanya atabasamu. Aliipenda damu, alipenda kuiona ikitoka mwilini kwa mtu na aliihusudu zaidi pale yeye awapo chanzo cha kutoka kwa hiyo damu. Hakutoka pale kwa haraka, bado aliendelea kutizama pale alipoangukia Jimmy. Bado alitaka kuitumbukiza Risasi katika kichwa cha mtu huyu. Licha ya kuangalia sana lakini hakuonekana, hakumuona Jimmy na kibaya zaidi hakumuona Masimba na hatq mmoja kati ya wale watatu walioingia. Sebule ilikuwa kimya, ukimya wa kuonyesha hapakuwa na mtu. Hilo likamfanya auvute muda, hilo likayafanya macho yake yawe makini kwa kila kitu. Bastola mbili bado zilitangulia mbele. Lakini ukimya nao bado uliendelea kutamalaki. Sasa alikuwa ameamua kujitokeza, kujitokeza kuangalia zaidi na zaidi, ikiwezekana aondoke kabisa. Lakini wazo hilo likapingwa na hisia zake, bado hapakuwa na usalama wa yeye kujitokeza. Akaangaza macho yake pembeni kama ataona chochote cha kumsaidia, akakiona kisadolini kidogo ambacho kilionekana kama kimejaa maji. Akainama na kukichukua, baada ya hapo akajaribu kukitupa upande mwingine kama angeweza kugundua chochote, lakini haikuwa hivyo... Bado ukimya uliendelea kuwepo. Hilo likampa uhakika kwamba hapakuwa na watu eneo lile. Akaipiga hatua ya kwanza na ya pili, alipotaka kupiga hatua ya tatu akasikia yowe likitokea nyuma yake. Yowee lililofuatana na mgugumio wa maumivu kutoka kwa mtu. Hakutaka kugeuka kuangalia, kugeuka kwake nyuma kungesaidia kupigwa Risasi iwapo angekuwepo mtu wa kufanya hivyo. Alichokifany yeye ni kuchupa na kuangukia pembeni. Akatulia akiangaza huku na huko. Bado ukimya ulichukua nafasi yake. Hapakuonekana kama kuna tukio kutokana na ukimya. Hapakuonyesha kuwepo kwa mtu. Nani amelifanya tukio lililopita muda mfupi? Masimba! Ndiye mtu pekee wa kulifanya hili, lakini amekalia wapi? Mbona Jimmy haonekani, nani amepigwa risasi nyuma yangu? Amepigwa na Masimba au na mtu gani? Kabla hajalipata jibu bastola ikagota tena kwa mara ya pili kisogoni. Tofauti ya huyu na yule wa mwanzo, huyu hakuongea kitu. Aliendelea kuikandamiza bastola kisogoni. Kabla hajakaa sawa, akashikwa na kugeuzwa kwa nyuma.

Hapo akajikuta akitizamana uso kwa uso na Masimba, Bastola yake ilikuwa bado kichwani kwa teddy. Macho yake yalikuwa yamebadilika kupindukia. Sura yake haikuonyesha utani, sura yake haikuwa na masihara. Teddy akatulia akimuangalia masimba, alitulia akihofu na kuwa na mashaka na mabadiliko yale. Macho ya Masimba hayakuonyesha ule utani. Macho ya masimba yalimaanisha kitu kingine. Akakiona kidole cha Masimba kikishuka kwenye kitufe cha kuruhusu risasi. Akauona uso wa Masimba ukiendelea kubadilika. Hakuonyesha masihara, hakuonyeshq utani, macho yake yalisomeka kifo na sura yake aliongelea mauti. Teddy bado alitulia, bado alikuwa akiiomba toba. Alitulia kuruhusu chochote, haikuwa hivyo wala vile, bali ilikuwa hivi. Bastola ilishushwa kisha bila kuambiwa chochote akamuona masimba akiondoka. Akiondoka huku akiachwa yeye akiwa amesimama. Hakubaki hapo, alikuwa nyuma akimfuata Masimba. Alikuwa nyuma akimfuata mpenzi wake. Hakuwa na wazo tena la kukumbuka uwepo wa Jimmy.

*********
Chumba kilikuwa kimya, kila mmoja alikuwa kimya akimtizama mwenzake kwa utofauti. Wakati teddy akimtizama masimba kwa staili ya nisamehe, masimba alikuwa akimtizama kwa staili ya nautaka ukweli. Uso wake haukuwa na tabasamu, mishipa ya hasira bado ilichukua sehemu kubwa usoni. Sura ya Asteria, Godfrey Maboba sambamba na familia yake, bado zilikuwa usoni mwake. Kumuangalia teddy kulifuatana na kumbukumbu ya mtoto aliyelala mbele ya macho yake akiwa na matundu mawili ya Risasi. Mtoto ambaye hakuwa na hatia, mtoto ambaye hakujua chochote kile aliuawa kwa risasi. Chanzo kikiwa teddy. Ni teddy huyu huyu aliyetaka kumuua kule kigamboni. Kufikia hapo akaanza kutembea kusogea pale aliposimama teddy. Teddy bado hakusogea wala hakurudi nyuma. Alisimama pale pale akimuangalia masimba usoni.

"Kwa nini Umemuua Asteria na familia yake?" Lilikuwa swali, swali ambalo halikutarajiwa na teddy. Sio kutarajiwa kwa kuwa alidhani masimba anajua. Lilikuwa swali ambalo lilimshtua na kumgutusha kupita kiasi. Ni kweli alipewa amri ya kumuua Asteria, lakini hakumuua yeye kwa kuwa alimfahamu Asteria tokea wapo wote Ifakara. Alimfahamu asteria kwa undani zaidi, na hata familia yake aliijua. Ingawa alipokea kweli amri lakini asingeweza kumuua asteria na hata dada yake. "Sikumuua Asteria wala familia ya dada yake. Ni kweli amri ya kuua nilipewa, lakini kabla sijatekeleza hilo wakatumwa watu wengine wakaua ili nionekane mimi ndio nimefanya. Kuhusu familia ya dada yake sikuhusika na chochote kwa kuwa tukio lililotokea mjimwema Kigamboni lilinichanganya baada ya kugundua kuwa gari yetu ndio imelipuliwa na wewe ukiwemo ndani yake. Hilo likanifanya nirudi tena kigamboni kuangalia uwezekano wa kuuona mwili wako lakini sikuuona. Hapo nikatambua kuwa hukuwepo ndipo niliporudi nyumbani kukusubiri. Teddy alimueleza Masimba kila kitu kilichotokea, hata kuvamiwa na walinzi binafsi wa taasisi nyeti. Hakuacha kuongelea usaliti na kukubali kuwa alikuwa tayari kusaliti.

"Nani Yupo nyuma ya mpango wenu wa kutorosha madawa kutoka kwenye mikono ya usalama? Aliuliza Masimva.

"Jimmy Lambert!" Akajibu Teddy

"Ukimtoa Jimmy?

"Yupo mtu mwingine mkubwa sana, lakini mtu huyo anajulikana na watu wawili tu." Akajibu teddy.

"Nani na nani wanamjua?

"Jimmy na suresh. Akajibu teddy
Lilikuwa jibu ambalo halikutegemewa na masimba. Akamuangalia teddy zaidi na zaidi, akihitaji ahakikishiwe kama jibu hilo lina ukweli. Bado teddy alimjibu pasipo na wasiwasi. Alimhakikishia kwamba Suresh alikuwa mmoja kati ya watu wanaomfahamu mmoja ya vigogo waliokuwa nyuma ya mpango huo. Akamuangalia Tena, kisha kwa sauti tofauti akamuuliza. "Unajua kuwa nilikamatwa na kupelekwa makao makuu kabla sijahamishiwa katika nyumba moja ya siri inayomilikiwa na usalama wa TAIFA?

"Mwanzo sikujua, lakini nilipowaona walinzi wale nikajua hili suala limepelekwa mamlaka nyingine. Nilijua utakuwa umeharibu ama njama za kukushurutisha uonyesha ulipo mzigo wa madawa zinaendelea." Akajibu Teddy.

"Upo tayari kuwa na mimi au bado unaitaka pesa?
AKAULIZA MASIMBA HUKU AKIMUANGALIA TEDDY USONI.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom