Riwaya: Nitakupata tu

Riwaya: Nitakupata tu

Duuh ngoma nzito hii masimba na yeye anachanganya kazi na mapenzi ona sasa.demu wa kipere kwenye hela hakamatiki.
 
Ila mm nimependa veronica kuwa hupande wa masimba maana tayari tedy hayuko salama maana yuko mikononi kwa veronica yaani imechanganya vzr sana
 
Sasa hivi Teddy auwawe tu,Japo masimba hawezi kufanya hivyo,ila asaidiwe na wenzake kumpa tiketi Teddy wake.
 
Hiyo so kwel kwan ni mawazo ya ibra87 ila namshauri ibra bora huyo teddy amfutee tuu,,,sema apana stry ndoinakuw vyeme acha we msaliti hivohivo
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 081

"Kama Sio Veronica ningeshakuwa maiti? Veronica huyu aliyemteka Teddy Nje tu ya kibanda hiki? Mbona kama naona unaongekea kitu kigumu sana Mzee?.. Akauliza Masimba haku akionyesha kutokukubaliana na Maneno ya Mzee Raymond. Veronica amuokoe yeye? Teddy awe pandikizi la CIA? Imekuwaje Veronica akapewa jukumu la kumlinda yeye wakati huo huo inasemekana yupo na Teddy mahala fulani? Bado hakutaka kuamini na hata akili yake haikutaka kuamini kile ambacho alitaka kuamini. Bado alijiona katika kizungumkuti katika Suala hilo. Ni katika kuwaza hilo akawakumbuka wanawe. Akamkumbuka Yaser na France. Mara ya mwisho alikumbuka kutoa maagizo kwa watoto wake kuondokewa sehemu ambayo walihafadhiwa hapo mwanzo. Lakini Muda huu alikuwa akipata taarifa kuwa Chief Amepelekwa mafichoni. Je wako wapi watoto wake? Swali hilo likamfanya ainue macho kumtizama mzee Raymond tena. Alihitaji kujua kila kitu ambacho hakuwa akikijua. "Mzee naomba kujua kila kitu ambacho sikuwa na kijua kuhusu ofisi hii kujua haya yote. Pia wanangu walihifadhiwa eneo fulani na hata mara ya mwisho kuwasiliana na Chifu nilimwambia kuhusu hilo. Nitahiraji kujua pale walipo kwa sasa." Aliongea Masimba akimuangalia mzee huyu. "Mr Masimba najua wewe ni mpelelezi wa kiwango cha juu sana kuwahi kumuona. Lakini kiwango chako kinashushwa na mapenzi uliyonayo kwa mwanamke huyu. Mwanamke huyu ndiye amekushusha kutoka pale ulipokuwa kipindi kile ulipokuwa Russia na Hata Syria. Ofisi ilikusifu sana pale ulipoanza kuhisi ushirika wa Teddy katika masuala haya ya usaliti. Mara nyingi ulikuwa ukiapa kumuua lakini hukufanya hivyo. Na hata pale bastola yake ilipomuua mama yako na Baadae kumuua Dee Plus wewe ulijua muuaji alikuwa Mwamvita. Lakini kiuhalisia Aliyemuua Mama yako Alikuwa ni Teddy. Pale alipowashambulia wanao na mama kutaka kwenda kumvaa , ndipo hapo alipofyatua risasi ambazo zilimmaliza mama yako. Ukitaka kugundua hilo kumbuka umbali ambao alikuwepo nwamvita na ugumu wake katika kuifyatua risasi. Teddy ndiye aliyefanya hayo. Hata kifo cha Dee plus yeye ndiye aliyemuua ingawa baadae alikuja kwenu kukuomba msamaha lakini ilikuwa Geresha tu. Nia kubwa na Amri ambayo ilitoka Makao makuu ya CIA ni kuuliwa kwako wewe. Na hilo lilitakiwa kutekelezwa na Jimmy ambaye ni Mmoja wa kati ya Majasusi wa NSA (national security Agency). Lakini Jimmy akawa anasita kutoka na Amri ya Kiongozi wa Nchi kuwa kukuua wewe mapema kutatibua Hali ya usalama nchini. Hivyo wakawa wanakuacha ili uendelee kumuamini Teddy na Mwisho wa Siku Wakuue. Ushiriki wa Waziri Mkuu na Kiongozi wa Nchi katika suala hili ulianza pale Nchi Yenu ilipotaka kuingia mkataba na Nchi Ya Urusi. Rais alikataa kutokana na kuwajua warusi walivyo katika masuala ya Kiusalama. Na baada ya Marekani kuligundua hilo ndio wao wakaingia kwa gia ya msaada na kuisaidia Tanzania Kijeshi, ki uchumi na Hata Katika Masuala mengine.

Kuhusu Ofisi hii kuyajua hayo, kumbuka Ofisi Hii inafanya kazi kwa karibu na Viongozi wakuu wa Ulinzi na Usalama. Mtu wa kwanza kuniomba Msaada wa kutafuta mtu wa kukulinda alikuwa ni Meja Jenerali chomboko. Yeye ndiye wa kwanza kunieleza hili suala katika usiri mkubwa tulipokuta Geneva Uswis Katika mkutano wa Kiroho baada ya Papa Francis Kudhuru katika Nchi hiyo. Hapo ndipo Meja jenerali aliponieleza hili na kuniambia upo katika Hatari ya kuuawa kwa Amri ya Cia na Kiongozi wa nchi. Ni hapo nilipomtafuta Veronica ambaye kipindi Hicho alikuwa ni Mwanakikundi wa Kundi letu la Mafia." Yapo mengi sana lakini kwa Uchache ni Hayo. Kifo cha Jenerali Chomboko Unataka kupewa wewe ili iwe rahisi kukupoteza. Kitendo cha wewe kutoka Ikulu na Kukutana na Jimmy nyuma ya Benki Kuu ya Tanzania, ilikuwa ni Mmoja ya Mkakati wa kukuua baada ya kuamua kuachana na Kazi yako. Hivyo tambua unawindwa, Tambua huna kinga tena ya kukuzuia wewe kuuawa. Itabidi ujilinde na uitumie bastola na Usiruhusu alichonacho Teddy Kifike kule anapotaka kukifikisha."alimaliza kuongea Mzee raymond Huku akimuacha masimba katika kizingiti Chenye giza. Giza totoro ambalo halikuutoa hata theruthi ya Mwanga. Teddy ndiye aliyemuua mama yake, Teddy ndiye aliyemuua Dee plus. Kumbukumbu yake ikarudi nyuma tena. Siku ya kuuawa kwa mama yake. Watoto wake walipotaka kwenda kumkumbatia Teddy huku wakimuita Mama Yao. Shambulio lake kwao na kukurupuka kwa Mama yake. Kufika hapo akafumba macho, ni kweli Risasi Haikutoka kwenye Bastola ya Mwamvita. Teddy Ndiye aliyeifyatua risasi kweli. Kuligundua hilo kulimfanya Masimba Asimame akitweta. "NITAKUPATA TU TEDDY NA NITAKUUA." Aliongea huku akiruhusu machozi kutoka. Mambo mengi aliyoelezwa na Mzee huyu vilimuonyesha ni Jinsi gani Marais wa nchi za Kiafrika wanavyokuwa vibaraka wa nchi za magharibi. Rais kusaini mikataba ya kinyonyaji na hata kukubali wananchi wake kudhurika ni kitu ambacho hakikubariki. "Naingia kazini Rasmi, naingia katika vita hii nikiwa sio masimba wa Idara ya Usalama wa Taifa. Bali masimba mzalendo na mpenda nchi yake. Najua naweza kupoteza Maisha yangu lakini lazima nilifanye hili katika Usiku Huu. Lazima nilizuie hili. Najua watoto wangu wako hapa lakini Waambie nitarudi nikiwa Hai na kama nitakufa, waambie nimekufa kwa Ajili ya Damu ya bibi yao na pili Taifa langu la Tanzania." Baada ya kuongea hayo Masimba akatoweka pale ndani akimuacha mzee Raymond Akitingisha kichwa. Alitingisha kichwa kwa kumuonea huruma na alitingisha kichwa kwa kuwa alitamani kumrudisha Masimba katika utimamu wake. Lakini ni wakati huo akiliwaza hilo akamuona Masimba Akirudi tena hapo ndani. "Nipe uelekeo wapi alipo Veronica kwa sasa. Hii ni kazi yangu nitaibeba mwenyewe."aliongea masimba macho yake yakionyesha kuzamilia alichookiongea. "Wapo maeneo ya Msasani karibu na Ubalozi wa Marekani. Taarifa nilioipata muda huu ni kwamba kuna vijana wa usalama wameuawa walipokuwa wanajaribu kumfuatilia Teddy. Lakini bado hajapotea kwenye macho ya Veronica. Ingawa Teddy hayupo peke yake.". Akajibu Mr Raymond. Masimba akatoweka Tena.

******

"Haiwezekani kuna mtu atakuwa amelivujisha hili. Nina uhakika Masimba hakuwa amemuona Isabella Ndani ya Daladala. Ile ajali inaonyesha kuna watu wanatembea na sisi." Alifoka Teddy akiwa pembeni ya kiti ndani ya gani aina ya Toyota Rav 4. "Hata mimi nimeweza kuhisi hilo. Kwani wakati tunamfuatilia hatukumuona mtu yoyote. Sasa Najiuliza Nani ambaye ameitengeneza Ajali ile iliyomuua Isabella?"" Akajibu dada mmoja ambaye alikuwa mmoja kati ya wale watatu ambao walikuwepo pale alipokuwa Masimba Akichagua viatu. "Basi nishapata majibu, kuna watu wanatufuatilia. Jaribu kumpigia simu Jimmy mueleze Hili. Pia mwambie anaowatuma wawe ni watu wanaomjua Masimba. Nahisi yupo nyuma ya Suala hili na pia nahisi ile ajali imemshtua." Aliongea Teddy safari hii akiwa makini kuangalia kupitia kioo cha pembeni. Roho yake ilikuwa imeshageuka huku mapenzi juu ya Masimba ya kiyeyuka mithiri ya barafu juani. Alikuwa akiiangalia pesa kana kwamba hakuwahi kuishika. Muda wote alikuwa akiitizama betri ndogo ambayo alikuwa nayo katika sehemu fulani ya siri. Muda wote alikuwa akiwasubiri Wenzake kwa Ajili ya kuianza safari kuelekea Ikulu. Safari ambayo ilikuwa ni ya mwisho kwake kuwepo hapa nchini. Alitaka kupotea na kutoonekana tena. Ili kutotaka kufuatiliwa alikuwa ametamani kumuua masimba kisha watoto harafu yeye kupotea. Alijua mpaka muda ule masimba alikuwa Ameshajua Huyu ni Mtu wa aina gani. Ni wakati akiliwaza hilo akamuona mtu mmoja akitembea pembezoni mwa barabara. Kwa kumuangalia mtu huyu angemfananisha kabisa na Lundo la Vijana Walioharibika kutokana na Matumizi ya madawa ya kulevya. Lakini huyu hakuwa mmoja kati yao, alimtambua na kumjua kuwa alikuwa kijana wao. Alikuwa mmoja ya makachero wa siri waliojipenyeza na kuishi maisha ya pamoja na Raia wa Tanzania. Alikijua Kiswahili na alikizungumza kuliko hata Mtanzania mwenyewe. Kijana yule aliyekuja na kidumu kidogo cha Maji sambamba na kitambaa mkononi. Alitembea mpaka pembezoni mwa kioo Cha Gari. Akainama kama anafuta vioo vya gari ile. Baada ya muda Teddy akaonekana kutoa pesa na kumpa kijana yule kisha kuondoka. Baada ya kijana yule kuondoka gari ikachepuka kushoto na kushika barabara Kuelekea msasani huku akiamini kuwa walikuwa salama.

*******

Baada ya kuondoka pale nyuma ya kanisa kwa Mr Raymond. Masimba aliamua kuingia kazini akiamini kuwa Teddy alikuwa ni Adui namba moja kwake. Alitambua hili baada ya kufumbuliwa juu ya aliemuua mama yake na hata ndugu yake kipenzi dee plus. Alitaka kumuua Teddy kwanza kabla ya kwenda kwenye mamlaka za Juu. Safari yake Ya kwanza iliishia mpaka kinondoni Manyanya katika nyumba ambayo alikuwa akiishi. Aliingia kwa Usiri mkubwa mpaka ndani ya Nyumba. Akaongoza mpaka sehemu fulani alipokuwa akihifadhi Vitu vyake kwa Siri. Baada ya Kuingia Hapo macho yake yalitua ukutani kwenye hazina yake ya Silaha. Macho yake yakatua Juu ya bastola mbili Ruger Sr na Armalite Ar 24. Akazichukua na kuziweka Sehemu husika. Akachukua na magazine kadhaa za Risasi pia akaweka sehemu Husika. Baada ya kumaliza hilo akaamua kutoka hapo kuelekea msasani. Muda wote huo bado hakuwa amefanya mawasiliano na Veronica. Aliondoka hapo kwa kupita njia zake za kificho. Dakika sita baadae alikuwa maeneo ya Namanga. Muda wote macho yake yalikuwa yakitembea nje kuangalia kama angeweza kumuona mtu yoyote. Aliiendesha gari taratibu akihakikisha hapitwi na kitu chochote kile. Wakati akikipita kituo Cha Mbuyuni, akaliona gari limesimamishwa pembeni mwa barabara. Mwanamke na mwanaume walikuwa wameliegemea gari wakifanya uasherati wao. Mara ya kwanza alipoliona alitaka kupuuza. Lakini alipotizama ukaaji na vitendo vya watu wale, akaiona Namna, namna ambayo ilimwambia wale walikuwa watu wake. Watu ambao wako upande fulani ama upande wake yeye. Wakati analifikiria Hilo akayaona magari mawili mengone yakipita kwa kasi. Magari hayo yakafuatiwa na gari nyingine ambayo hii haikuwa katika mwendo wa kasi. Masimba akaisimamisha gari aliyokuwa akiendesha kisha akainama kuchungulia kwenye matairi lengo likiwa ni kuangalia kile kinachoendelea pale. Bado watu wale wawili walikuwa pale wakidendeka pasipokuwepo kwa wasiwasi. Haikupita muda akawaona watu wale wakiingia kwenye gari yao na muda ule ule gari ikaondoshwa kuelekea mahala ambapo ni tofauti na kule zilikoelekea zile gari tatu. Masimba bado alikuwa ametulia. Alihisi kuwepo kwa mchezo wa hatari
 
Masimba sasa ameamua kutupa kitumbua baada ya kuona kimedondokea mchangani ahsante mkuu ibra87
 
Mi ntakufa mwaka huu, sojui asingekua IBRAH ningekuwajr?? Ibrah shukrani za dhati kwako mkuu
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 082

Akauhisi Mchezo, mchezo wa Hatari ambao unachezwa hapo. Ni wakati akilifikiria hilo likatokea Jingine. Likatokea hili ambalo hakulitegemea. Gari aliyokuja kwa mwendo wa kasi akidhani ni ya watu baki, haikuwa Hivyo, haikuwa hivyo kwa kuwa muda ule ule vioo vya magari yale vilishushwa kisha risasi zikaanza kuvulumishwa kuelekea pale pale alipokuwa amesimama Masimba. Hakuwa mzito katika kuling'amua hilo. Muda mfupi baadae masimba alikuwa angani akizikwepa Risasi. Alikuwa katika namna ambayo ilikuwa ikitia burudani Hata kwa watu wenyewe waliokuwa wakimshambulia Masimba. Alikuwa akiruka Hapa na kuruka pale. Alikuwa akiingia hapa na kutokea pale katika Ustadi wa kipekee. Katika ustadi ambao uliyonyesha kwamba hakuwa mtu wa utani. Alipokuja kutua alijikuta akiwa nyuma ya kichaka kilichopo pembezoni mwa Barabarani. Bastola ilikuwa mkononi tayari kwa kufanya kile kilichombele yake. Lakini Eneo lote lilikuwa kimya kanakwamba hapakuwa pametokea kitu chochote katika eneo hilo. Bado alikuwa ametulia akitizama. Taratibu akaanza kuburuzika kwa tumbo akiondoka hapo akielekea Sehemu Nyingine. Alitembea kwa tumbo mpaka alipofikia sehemu ambayo kulikuwa na Ukuta kwa Upande mmoja. Kufikia hapo akatulia Tena safari hii akiamua kutizama kule alipotoka. Ukimya. Ukimya ndio kitu ambacho kilitawala katika Eneo lote. Eneo ambalo muda mfupi Uliopita lilikuwa katika sekeseke la milindimo ya Risasi. Hilo halikumpa Masimba tumaini la kuinuka. Alichokifanya ni kuendelea kutizama alipotoka. Macho yake yalikuwa yakihitaji kulifanya giza, ligeuke kuwa mchana wa mwanga. Ni wakati huo alipouona umeme Ukizimwa maeneo yote na Kulifanya giza kutamalaki. Masimba akajua kinachotaka kufanywa. Sekunde hii alikuwa yupo chini akitizama Alipotoka, lakini sekunde aliyofuata Alikuwa ameparamia ukuta na kuangukia Upande wa Pili. Bado hapa kuonesha kuwepo kwa watu, bado giza lilitawala kila upande kuonyesha kuwa hapakuwepo na uwezekano wa kukosekana kwa wakora. Hazikupita Dakika mbili tokea kuzimwa kwa umeme, milio ya Risasi Ikatawala. Milio ambayo ilimuacha Masimba katika sintofahamu ya nini na nani wanapambana. Suala kuwa Veronica Alikuwa Yeye Halikuwa katika kichwa Chake, hakuliwaza kwa kuwa alijua Vero Asingeweza kukubali kumuacha Teddy. Sasa Huyu ni nani? Hilo ndilo ambalo aliliwaza. Bado milio ilikuwa Ikisikika kwa Ukaribu. Masimba akauona kuwa ulikuwa muda wa kusaidia mapambano. Swali lililokisumbua kichwa chake Je ni nani ambao walikuwa wakipambana. Je hata kama atapambana, je atajua wanaomsaidia wako upande Gani? Kuwaza huko kukamfanya Atulie. "Masimba sogea huku, ilikuwa ni sauti iliyomuita katikati ya milindimo ya Risasi. Tena hii ilikuwa sauti ya kike. Sauti ya mtu aliyemfahamu. Hii ilikuwa sauti Ya Veronica. Sauti ambayo ilimzindua na kujua kule anapotakiwa kukifanya. Hakuelekea upande ulipotokea sauti ya Vero, bali alielekea upande Tofauti. Upande ambao ulikuwa Tofauti. Akainuka na kuanza kutembea Taratibu kabisa. Akafanikiwa kukifikiwa kiwambaza cha nyumba ambayo ilikuwa mwishoni kabisa mwa Ukuta ule. Kufikia hapo Masikio yake yakanasa mchakato, mchakato wa miguu ya watu zaidi ya mmoja. Akatega Masikio yake zaidi ya Zaidi. Bado michakato ya miguu akaisikia ikizidi kusogea. Akauinua mkono wake wenye Bastola tayari kwa kuachia Risasi. Alikuwa makini kwa kuwa alijua anapambana na Oda kutoka mamlaka za Juu. Alitakiwa kuwa makini zaidi na Zaidi. Wakati akiwa hapo akawaona watu wawili wenye sub machine Gun Mikononi wakitokea kwa mbele yake. Inavyoonekana watu wale hawakuwa wamemuona Masimba. Masimba akawasubiri wasogee kwa kuwa hakutaka kuitumia Bunduki Kuua Watu wale, alitaka kuitumia mikono yake pekee. Akawasubiri waendelee kusogea. Hatua mbili kabla ya kumfikia Masimba akajitokeza mbele yao. Kwa kuwa hawakuwa wamejiandaa na kitu hicho, watu wale wakashikwa na Mfadhaiko ambao uliwapotezea sekunde kadhaa za kushangaa. Ni muda huo ambao aliutumia masimba kuwapa mapigo yaliyowaacha watu hawa wakianguka chini. Hakusubiri wainuke, hajusubiri wafanye chochote. Mlio mdogo mfano wa chafya ya binadamu kutoka kwenye bastola yake ilitosha kuruhusu Risasi zilizowapata watu wale na kuwaulia mbali.

Baada ya kuhakikisha watu wale wamekufa, hakutaka kuchelewa. Aliondoka hapo kwa kuuparamia ukuta kisha kuangukia Nje Tena. Baada ya kutua chini akatembea taratibu huku akikutana na miili ya Askari ikiwa chini ikivuja Damu. Akatambua hii ilikuwa kazi ya Veronica. Ilikuwa kazi ambayo ilionyesha ujuzi na Utaalam wa Veronica. Ilimuonyesha ni kiasi gani Veronica alikuwa Hatari. Akatembea na kutokea barabarani. Alipotokea tu barabarani, gari moja ikaja kusimama mbele yake. Kabla hajakaa sawa mlango ukafunguliwa na Kutakiwa kuingia ndani ya gari. Masimba akasita kwanza, lakini Baada ya kumuona Veronica Yupo ndani ya Gari, naye akaingia. "Teddy Yuko wapi? Lilikuwa swali la kwanza baada ya Masimba kutulia. "Amepewa hifadhi Kwenye Ubalozi wa Marekani. Nadhani kuna mpango unataka kufanyika kumuwezesha kumfikisha Ikulu." Akajibu Veronica Huku Akimuangalia Masimba. "Mbona uko hapa, nani atamuona atakapotolewa. Ukizingatia kuna Handaki limechimbwa Chini kwa Chini Mpaka Baharini?" Akauliza Masimba akionyesha Umakini wa Hali ya Juu. Kila kitu kipo kwenye utaratibu. Hataweza kuondoka hapo pasipo sisi kujua." Akajibu Veronica Akionyesha kutokuwa na wasiwasi kabisa. Lilikuwa jibu ambalo lilimfanya Masimba ageuke na kumtizama Veronica. Macho yake yenye maswali yalikuwa yakimuangalia mwanamke huyu katika aina fulani ambayo hata Veronica mwenyewe Aliitambua. "Unamjua Teddy Vizuri? Unakijua kile kichwa? Nipe majibu ya kuniridhisha. Usiongee Juu juu Veronica." Alisema huku akiendelea kumuangalia. Vero hakujibu bali alichomoa kidude fulani ambacho kilikuwa na ukubwa kama wa Simu. Akakiwasha na kumpa Masimba akiangalie Kwa Umakini. Macho ya masimba yalikuwa yakiliangalia jengo la Ubalozi Wa Marekani kupitia Kile kitu mfano wa Simu. Alikuwa akiangalia pande zote mpaka ndani ya Ubalozi. Kilikuwa kitu kilichomfanya Masimba amtizame Tena Veronica. Moyoni kwake alikubali kwamba ni kweli mtu huyu alikuwa ni Hatari. "Aiseee!! Nimeamini hiki unachokitenda. Hakika Ulijiandaa vya kutosha kutokana na Hali hii." Aliongea Masimba akikirudisha kile kidude mikononi kwa Veronica. "Una mpanga gani kwa Muda huu ambao tunamtega mtu wetu? Akauliza Veronica akimuuliza Masimba. "Usiku huu nataka niutumie kujua pale alipo Mkurugenzi Wa Idara ya Ujasusi. Nikitoka hapo nataka nikamalizane na Jimmy Lambert kabla ya kummaliza huyu Teddy." Akajibu huku akitizama kwa nje. "Unaijua Sehemu iitwayo Buzuruga ndani ya Jiji la Mwanza? Akauliza Veronica. "Napafahamu sana, nilishafika mara nyingi kila nilipokuwa na kwenda kuwahifadhi watu hapo." Akajibu Masimba. "Basi Chief inasemekana Yupo huko, na Ameshushwa Jioni Hii Kwa Usafiri wa Helkopta." Akajibu Veronica. Wakati akiongea na Masimba, kile kitu mfano wa Simu kikatoa Mlio. Veronica akakitoa haraka kisha kukiwasha. Macho yao yakawaona watu zaidi ya Sita wakiingia Mle ndani. Muonekano wa watu wale haukufichika machoni kwao. Walikuwa wana Usalama tena Wale Walinzi Binafsi Wa Rais. "Kazi imeanza, naona Rais ametuma Walinzi binafsi kwenda kumchukua Teddy." Akasema veronica Huku akimuonyesha masimba. "Tunatakiwa kufanya Jambo. Walinzi hawa ni wale wenye nafunzo ya Hali ya Juu. Na hawawezi kwenda sehemu bila uwepo wa Rais mwenyewe. Ninachoamini Rais yupo hapo na atakuwa katika Mazungumzo na Teddy. Hembu tusogee kuelekea maeneo hayo." Aliongea Masimba huku akiwaaangalia Vizuri Walinzi wale.

*******

Ulikuwa Ujio wa Siri kufanywa na Rais wa Nchi katika Ubalozi wa marekani. Ziara hiyo siri ilifanyika pasipo kujulikana popote. Na pia imefanywa baada ya mazungumzo ya Rais Wa marekani na Rais Wa nchi hii. Mkakati uliokuwepo ilikuwa ni lazima Biashara iendelee ili waendelee kupata pesa bila kujali Athari ambazo zilikuwa zinawapata Wananchi. Msaada wa mamilioni ya shilingi anayopewa sambamba na mikopo ilisababisha kiongozi wa nchi akubali kila mpango unapangwa na serikali ya marekani. Ni usiku huo baada ya mazungumzo na Rais Wa Marekani. Ndipo Rais alipoamua kuifanya Ziara ya Kuja hapo ubalozini kwa kutumia Njia maalum ambayo ilipita chini ya Ardhi nia ni kuja kuonana na Teddy. Sio rais wala wasaidizi wake waliotambua kuwa teddy alikuwa ni wakala maalum wa CIA. Hakuna aliyejua kuwa Teddy alikuwa ni special Agent wa CIA. Walimchukulia Teddy kama mwenzao. Walichukulia kile anachokifanya kinatokana na kile ambacho ameahidi Rais. Hawakujua katika pesa ambayo rais ameahidi itarudi katika mikono ya Serikali ya Marekani. Ulinzi ulitisha kila upande. Chumba alichokuwa amewekwa Teddy kilikuwa kikilindwa na mitambo maalum ambayo ilikuwa na uwezo wa kutokuruhusu Makombora ya Aina yoyote kuingia na hata kulipua. Rais alitembea akiongozwa na Makomandoo maalum ambao ndio waliokuwa Walinzi Binafsi wa Ubalozi. Sambamba na walinzi Binafsi wa Rais. Kila mmoja alikuwa ni mwenye Tabasamu. Kila mmoja sura yake ilikuwa ikionyesha furaha. Mavazi ambayo alivaa Rais Kwa siku Hiyo yaliupoteza muonekano wake. Hakuweza kugundulika kuwa ni yeye. Hata ule mtambo maalum Haukuweza Kumtambua Rais, ingawa Masimba alijua kuwa kuwepo kwa kikosi kile hata Rais hakuwa Mbali. Ilikuwa ni lazima wa hakikishe kwa njia yoyote ile Wanazuia Kitu hicho kutua mikononi mwa kiongozi. Ilikuwa ni lazima wauvamie Ubalozi wa Marekani na Kuufanya mashambulizi. Lakini swali lilikuwa Je Watafanikiwa? Hilo likabaki kuwa swali lililomtoa Masimba ndani ya gari. Alihitaji kufika Ndani Ya Ofisi Za Ubalozi na alihitaji kumzuia Teddy na pia alihitaji kuipata betri maalum yenye kuzalisha kemikali ambazo hutengenezwa kwa kuongezwa kwenye Madawa na kuyafanya madawa kuwa na Thamani kubwa. Ilikuwa ni lazima azuie hilo katika Aina yoyote na kwa Njia Yoyote. Hata kama alikuwa ni kufa yeye Hakujali hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom