NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 084
Teddy alikuwa kwenye ulinzi wa hali ya juu. Ulinzi ambao uliongozwa na makomandoo sambamba na majasusi wa CIA. Lakini licha ya hilo, kilichomburudisha Zaidi ni Kule kumuona Veronica. Veronica aliyekuwa naye muda mfupi uliopita. Alikuwa katika msafara ule tena akiwa katika sare na mavazi maalum wanayovaa walinzi Wa Jengo hili la ubalozi wa Marekani. Amefikaje ndani na kuwa mmoja kati yao? Ni swali lililomsisimua Masinba, sio kumsisimua kwa woga ama burudani. Bali mwili ulimsisimka kwa utembeaji ule wa Majasusi wale. Walikuwa wakitembea kanakwamba wapo katika Ardhi ya Marekani. Licha ya kuinyonya nchi yenye rasilimali nyingi sana, pia waliimfanya Nchi hii kama shamba la kuchuma mali na kutokomea nazo. Akauvuta Muda naye akitaka kujua kule wanapoelekea. Hata walipompita pale ambapo alikuwa amejificha, bado Masimba alitulia akiwatizama. Alikuwa na Uwezo wa Kumtwanga Teddy Risasi, lakini Hakutaka iwe hivyo. Alitaka kumuonyesha Teddy kuwa anauwezo kuliko hata yeye. Alitaka kumuonyesha kuwa alikuwa akiifuatilia na kuipigania Tanzania. Akaruhusu Teddy na walinzi wake wampite. Akatembea nao kwa nyuma kila pale walipotembea. Alitaka kuwatizama ni wapi walipokuwa wakielekea. Alitaka kujua ni wapi Teddy ameuhifadhi betri ile. Majasusi wakimarekani wakazidi kutembea wakiingia Ndani Zaidi. Bado Veronica alikuwa nyuma na Hata Masimba hakuwa mbali na watu hawa. Tanzania yake ilikuwa katika moyo wake. Hakutaka kujua wapi alipokuwa rais. Alichotaka kufanya ni kukipata kile ambacho kilisababisha Teddy kuwa msaliti. Muda mfupi watu wale wakatokea katika barabara fulani ya vumbi. Hapo walikutana na msululu wa magari yapatayo matano. Yalikiwa magari yasio na namba. Yalionekana kuwa magari mapya. Baada ya Teddy na majasusi wale kuyafikia magari yale, milango ikafunguliwa katika aina fulani ya Uharaka. Teddy akatakiwa kuingia ndani ya Gari. Wakati Huku wakilifanya hilo kwa Teddy, tayari bastola ya Masimba ilikuwa mkononi. Tayari alikuwa tayari kulizuia hilo. Muda mfupi baadae alikuwa ameiruhusu Bastola kutoa Risasi. Risasi ambayo ilikwenda kutua katikati ya kifua kwa jasusi mmoja wa kimarekani. Akapiga yowe kubwa huku akitupwa angani mithiri ya furushi. Ilikuwa risasi iliyopenya katika kifua cha Jasusi yule. Risasi ikamtupa angani huku yowee kubwa likifuatia. Majasusi wengi wa kimarekano wakacharuka. Kila mmoja alikuwa akichupa na kuangukia mahala pengine. Kilikuwa kitendo kilichofanywa katika muda mfupi ambao ulimacha Teddy akiwa amesimama tena akiwa katika mzubao. Kulikuwa na uwezekano wa kumshuti. Lakini muda mfupi Komandoo mmoja wa kimarekani akampitia kwa kumbo mpaka chini. Kila kitu kilichokuwa kikitokea Masimba alikuwa pembeni akitizama. Kutokumuona Vero katika viunga vile, hakukumpa shaka. Hakukumpa shaka kwa kuwa alijua na kutambua kinachotokea. Hata yeye alikuwa akihama hapa akienda kusimama sehemu nyingine. Sehemu ambayo ilikuwa na giza totoro tofauti na kule alipotoka. Ukimya ulikuwa umechukua sehemu kubwa sana. Hapakuonekana uwepo wa watu. Hapakuonekana ni sehemu ambayo ilikuwa na Rabsha. Masimba akatulia akiendelea kutizama mbele. Kutizama kama angemuona Veronica. Komandoo yule aliyemkumba Teddy hakuinuka katika wakati ule. Alijua nini ambacho kinaendelea Hapo. Alijua watu wale walikuwa wakipotea katika namna fulani. Ni wakati huo akikiangalia hicho, ndipo hapo akakiona kile ambacho alitaka kukiona hapo mwanzo. Veronica Tayari alianza kugawa tiketi katika aina ile ile ambayo ilitakiwa. Miili ya watu kadhaa ilikuwa imetambarajika chini kuonyesha kuwa Vero alikuwa akiua watu taratibu. Ulikuwa uuaji ambao ulimfanya Masimba aamini kuwa huyu alikuwa Mafia kweli. Hilo likampa nguvu ya kuinuka na kuanza kusonga kuelekea kule kule. Kuelekea pale walipolala watu wale walioonyesha hawakuwa na Uhai. Hatua ya kwanza ikamuacha ikiivuka barabara, hatua ya pili alishaivuka barabara. Hatua ya tatu alijikuta akiisalimia Ardhi baada ya kujikuta akiisalimia Ardhi. Wakati akitaka kujitayarisha kuinuka akakutana na kitu kizito ambacho kilitua kisogoni na kumfanya Arudi chini. Giza likaanza kuyagubika macho yake. Akataka kujaribu kupambana na Giza. Hakuweza, hakuweza kwa kuwa alihisi kitu kingine kikitua kichwani. Hakupata nguvu na Uwezo Tena wa kufumbua macho yake. Alijikuta akizidiwa na giza. Akatulia kana kwamba Alikuwa Maiti.
********
Moscow Russia.
Mkurugenzi wa Shirika la Kijasusi la Urusi (KGB) Bwana Vandelov Pashovic. Alikuwa Ofisini kwake akiwa ametulia akiangalia hiki na kile upenuni mwa Ofisi ile ambayo ilikuwa katikati mwa jiji la Moscow. Alikuwa akiangalia hiki akiwaza kuhusu taarifa aliyoipata muda mfupi uliyopita kutoka africa, kuwa Kuwa shirika la Kijasusi la Marekani lilikuwa limeiuzia Nchini Ya Tanzania Mtambo maalum wa kutengeneza Kemikali hatari zinazotumika kuchanganywa na madawa ya kulevya. Mara ya kwanza baada ya kupewa taarifa hiyo alitaka kuipuuza. Lakini badala ya kuifuatilia hiyo taarifa na kuupata ukweli kuhusu hilo. Akajikuta akihitaji kulichunguza Hilo suala. Alihitaji kuujua huo Mtambo, alihitaji kuuondoa huo mtambo mikononi mwa Serikali ya Tanzania. Baada ya kutafakari kwa Kina akaona awasiliane na Vijana wake ambao walikuwa Nchini Rwanda kwa . maalum ya Umoja wa Mataifa. Aliwataka Vijana Hao waingie katika nchi ya Tanzania ili kuchunguza taarifa hizo na wampe Majibu katika Masaa sabini na mbili. Ni kweli vijana hao watatu wakaingia Nchini Tanzania kama Watafiti wa Masuala Ya Ufaidikaji wa Rasilimali kwa Watanzia Wenyewe. Walipoingia katika nchi ya Tanzania Cha kwanza Walichokifanya ni kuonana na Mtu Mmoja Aitwaye Mr Raymond ambaye alikuwa ni Mshirika wa karibu wa Genge la Mafia Katika nchi ya Italy. Ni mtu huyu ambaye aliletwa na Kanisa katoriki kama msimamizi mkuu wa madhehebu hayo katika Afrika. Msukumo wa kuonana na Mtu huyu, ulitokana na Taarifa ambayo waliipata baada tu ya kuingia Chini Tanzania kuwa kuna mzee mmoja anaweza kuwasaidia katika Hilo. Ni usiku huo ambao Vijana wale walifika pale, ndio usiku ambao Walikutana na Veronica. Kukutana kwao hapo ni baada ya Veronica kuitwa na Mr Raymond kukifuatilia kile kile ambacho vijana hawa watatu walitaka kuijua Taarifa yake. Baada ya vijana hawa tatu kufika katika makazi ya Mzee Huyu ambaye alipachikwa cheo cha Usimamizi wa makanisa ukanda wote wa Africa ya Mashariki. Ndipo walipokutana na Veronica Senka Ambaye naye alitumwa na Genge la mafia kuufuatilia mtambo huo ambao kwa upande wa Kundi la Mafia waliihitaji betri pekee ambayo ndio husukuma Mtambo huo. Baada ya vijana wale kufika na kufanya mazungumzo ya kina na Mzee Raymond kisha kugundua kuwa wapo katika kufuatilia kitu kimoja. Wakatuma Taarifa hiyo kwenye Ofisi za KGB Jijini Moscow. Baada ya Taarifa Hiyo kutua mezani kwa mkurugenzi wa KGB. Mazungumzo ya kina yajafanyika kwa pande mbili. Upande wa Mafia pamoja na Shirika la Kijasusi la Urusi. Baada ya mazungumzo ambayo yalichukua Takribani siku sita makubaliano yalifikiwa kwa Shirika la kijasusi la Urusi kukubaliana na Kundi la Mafia kuangalia Namna ya Kuipata hiyo betri kisha watajua nini cha kufanya. Baada ya makubaliano Hayo Kufikiwa. Veronica ndipo alipopewa Jukumu la kuipata Hiyo Betri Kutoka mikononi mwa Serikali ya Tanzania. Jukumu ambalo alitakiwa kulifanya akiwa na Special Agent's wa KGB. Kazi ya kufuatilia ikaanza kwa Watu hawa kuanza kujiingiza ndani ya Serikali. Ni katika ukaribu huo wakaweza kuunda ukaribu na Serikali hasa kwa Waziri. Ni katika ukaribu huo ndipo walipoambiwa Betri Hiyo ipo mikononi kwa watu wawili ambao waliheshimika katika jamii yote ya Kitanzania. Wakati hilo likiendelea likatokea Suala la kupotea Kwa mzigo wa Mamilioni ya Shilingi. Mzigo ambao ulichukuliwa katika mazingira ambayo special Agent's wa KGB pamoja na Veronica walikuwa nyuma ya Hilo. Nikatika hilo kuliko ibua mzozo kati ya Washirika wa mzigo huo. Ni mzozo huo uliomuibua Masimba, ni mzozo huo ambao ulichukua maisha ya Asteria P Paulo ambaye alikuwa akiujua ukweli. Wakati Special Agent's walipomuua Asteria Walikuwa wakipata maagizo kutoka kwa Teddy na Hata Veronica. Kwahiyo Veronica na Teddy ni watu ambao wanafahamiana lakini pia ni watu ambao walikuwa wakiwakilisha mashirika tofauti. Wakati Teddy akiwa ni Afisa Usalama wa Shirika la kijasusi la Tanzania (Tiss) pia alikuwa ni Special Agent wa Shirika la kijasusi la Marekani CIA (Central Intelligence Agency ). Pia Veronica Alikuwa ni Special Agent wa Mafia, na Vile vile alikuwa akiwakilisha shirika la Kijasusi la Urusi (KGB) (KOMITET GOSUDARSTVENNOE BEZOPASNOSTI) AMBALO kwa kiingereza lilijulikana kama (committee for state Security, foreign intelligence and Domestic security Agency of the Soviet Union ). Licha ya kufahamiana Huko na kuifanya kazi kwa pamoja. Teddy na Veronica Kila mmoja alikuwa akitumiwa na Mtu ambaye yupo nyuma. Wakati Teddy akitumiwa na Viongozi Wakuu wa Nchi. Veronica yeye alikuwa akitumiwa na Mzee Raymond wa Kundi la Mafia. Waliifanya kazi ya kufuatilia Mtambo Hasa Wakiitaka Betri ya ule mtambo. Wakati wao wakiendelea ndipo hapo Masimba alipoibuka na kuanza kulifuatilia hilo suala. Kitendo cha masimba kuanza kulifuatilia lile suala kukaleta Ugumu katika kufanikisha uzalishaji wa Kemikali hizo kitendo ambacho kilisababisha rais Amruhusu Teddy kumuua Masimba. Wakati mpango wa kumuua Masimba ukiendelea kusukwa kwa umakini ndipo ulipotokea Mzigo wa Madawa kupotea nyumbani kwa Jimmy. Kabla suala la Mzigo halijapoa ndipo yalipotokea Mauaji Ya Waziri. Mauaji Ambayo yalifanyika baada ya Waziri mkuu kumteka teddy, kisha kutaka kwenda kumuingilia kimwili. Mauaji ya waziri mkuu ndiyo yalimfanya Rais Aamue kuitoa Betri ile Kisha Kuikabidhi kwa Watu Wawili ambao walikuwa Maarufu Sana Katika Jamii kutokana na Ucha Mungu Wao. Betri ilikuwa mikono mwa Askofu Ibrahim Lexandre Rengima sambamba na Sheikh mkuu Wa Mkoa Dk Ramadhani Chilemba. Hili suala alilifanya Rais Kwa Siri akimshirikisha meja Jenerali Chomboko. Licha ya kulifanya hili kwa Siri, lakini Veronica na Teddy waliinusa fununu ya hilo. Na siku ambayo alipewa maagizo na Masimba kwenda kumuua Askofu na kukuta ameshauawa. Alitambua veronica ndiye aliyeyafanya mauaji yale. Licha ya kumuwahi Baba askofu lakini hawakuipata bahasha kwa kuwa Baba Askofu Hakuwa tayari kuitoa kwa kuwa alitaka imfikie Masimba. Kwahiyo Veronica na Teddy walikuwa ni watu wawili wanaofanya kazi pamoja lakini kila mmoja akiwakilisha upande Mwingine. Baada Ya Veronica kugundua masimba anauwezekano wa kuipata Ile betri ndipo hapo likipoundwa Tukio fake ili kumuaminisha masimba kuwa Veronica Alikuwa mtu sahihi Kwake. Ndio maana aliipata hamu ya kwenda pale Kanisani kuonana na mzee Raymond Bila kujua kuwa watu hawa hawakuwa upande wake.
*********
Alifumbua macho taaratibu kama mtu aliyekuwa akitoka kwenye usingizi. Maumivu nyuma ya kichwa chake yalimkumbusha kitu kilichotokea Mpaka yeye kufika Hapo Ndani. Akataka kuupeleka mkono wake kisogoni, lakini alipojaribu kufanya hivyo akajikuta hawezi kwa kuwa mikono yake ilikuwa imefungwa pingu. Akaendelea kuangaza huku na huko kama angeweza kuona kitu. Lakini Giza totoro ndani ya Chumba kile, halikumpa uwezo macho yake kuona Chochote. Akatulia akimuwaza Veronica. Alitambua kama Veronica ameliona tukio la kutekwa kwake, basi atafanya lolote kumuokoa. Hakujua kwamba hata Veronica Hakuwa Rafiki kwake.